Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Watangazaji wa Radio Citizen na Citizen TV za Nchini Kenya Wapata Ajali ya Ndege

$
0
0
Watangazaji wa Radio Citizen na Citizen TV za nchini Kenya, wamenusurika kufa baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kuelekea Karbanet, kupata ajali katika eneo la Kibra jijini Nairobi.

Taarifa kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Usalama wa Ndege za Polisi, Rodgers Mbithi zinaeleza kwamba ndege hiyo ilianguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Wilson, ikiwa na wanahabari watatu waliokuwa wakielekea kwenye mkutano wa NASA, ndipo ajali hiyo ilipotokea.

Ndege hiyo, CESNA 206 ilikuwa imewabeba watangazaji wa Citizen TV ambao ni; Sam Ogina, Cameraman Mauritius Oduor na Joseph Njane wa Radio Citizen.

Majeruhi wote wanaendelea kupatiwa matibabu hospitalini.

Jack Wolper Akwaa Skendo ya Kupora Mume wa Mtu....

$
0
0
SAKATA la staa wa Bongo Muvi, Jacqueline Wolper kudaiwa kupora mume wa mtu aliyefahamika kwa jina moja la Brown, mwenyewe amecharuka kwa kutamka kwamba kama kuna mtu anasema huyo ni mumewe basi ajitokeze hadharani kuliko kusemamitandaoni.

Akizungumza na Amani, Wolper alisema wakati hayupo na Brown, hakuna mtu aliyeibuka na kusema huyo ni mumewe, lakini tangu aanzishe naye uhusiano, miruzi imekuwa mingi ya wanawake kuibuka kila kukicha wakidai mume wao.

“Kinachonishangaza ni kitendo cha mimi kuwa naye tu ndiyo watu wanaanza kuibuka na kusema eti ana mke, duh!

“Mbona kipindi siko naye, hakuna mwanamke ambaye alikuwa anasema ni mumewe. Sasa basi kama kuna mwanamke ambaye anadai ni mumewe ajitokeza hadharani.
 
“Nilichogundua baadhi ya wanaoibuka ni wale ambao waliwahi kuwa naye kitambo, sasa nasema hivi, huyo anayesema ni mume wake basi ajitokeze,” alisema Wolper.

Amani lilimsaka pia mwanaume huyo ambaye anadaiwa ku-date na Wolper, Brown ambaye baada ya kusomewa madai yake alisema hana mwanamke mwingine ambaye yuko naye kwenye uhusiano zaidi ya Wolper na kudai mwanamke aliyeibuka ni exwake.

“Sina mwanamke mwingine niliyenaye kwenye uhusiano zaidi ya huyo unayemjua, ninachojua ni kwamba mwanamke aliyeibuka na kudai mimi ni mumewe huyo ni ex wangu ambaye tuliachana kitambo sana hata wakati sijawa na uhusiano na mwanamke niliyenaye sasa.

“Kitu cha kujiuliza, alikuwa wapi siku zote jamani kama siyo kuniharibia?” alihoji Brown.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa leo

$
0
0

JE Dada Unahitaji Kuwa Mrembo na Muonekano Bomba na Kaka Kuwa na Mvuto wa Kiume...Waone Hawa....

$
0
0
BLACK BEAUTY COMPANY
JE Dada unahitaji kuwa Mrembo na ule muonekano bomba wa kisuperstar👌🔥,kaka unahitaji kuwa mtanashati na mvuto zaidi wa KIUME?fika black beauty company utatimiza ndoto zako,hawakosei hata siku moja kwa products original na zenye matokeo yaharaka sana,bila madhara,ni kampuni yenye uzoefu wa hali ya juu sana🔥
1)kuongeza hips,makalio,mapaja@150000
(b)kuongeza hips,makalio,mapaja na miguu@200000/=
2)kuongeza miguu ,kuondoa vigimbi@120000/=
3)kuwa mweupe mwili mzima (Rangi moja)@150000/=
4)Kupungua mwili mzima@150000/=
5)kupunguza tumbo@100000/=
6)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
7)kukuza nywele@100000/=
8)kuondoa michirizi @100000
9)kuondoa madoa,mabaka na chunusi sugu@100000/=
10)kuongeza uume na nguvu za kiume@150000/=
Dawa zetu niuhakika sana100%na utaletewa popote ulipo,mikoani tunatuma,nje ya nchi tunatuma DHL,ofic zetu zipo kariakoo msimbazi police,🔥karibuni kwa mawasiliano zaidi

WASILIANA NASI

WhatsApp+255657778924,au call0743534406 



Au unaweza kutufollow INSTAGRAM
👇👇👇👇👇👇
@black_beauty_company

Download App ya UDAKU SPECIAL Bure Kutoka Play Store...Bonyeza Hapa ...Usipitwe

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Wahenga wa Escrow Wazidi Kuibuka..."Kashfa ya Escrow ni kubwa Kuliko Kitendo Cha Kurejesha Pato la Uhalifu"

$
0
0
SIKU moja baada ya Tundu Lissu na David Kafulila kutaka watu wote waliopata mgawo wa fedha za akaunti ya Tegeta Escrow miaka mitatu iliyopita wakamatwe na kushtakiwa mahakamani.

'mhenga' mwingine aliyekuwa mstari wa mbele kufichua kashfa hiyo, Zitto Kabwe, amefunguka na kusema mazito kuhusu sakata hilo.

Baada ya William Ngeleja kutangaza Jumatatu kurejesha kwa Mamlaka ya Mapato (TRA) mgawo wake wa Sh. milioni 40.4 zinazodaiwa kuwa zao la kashfa ya uchotwaji wa mabilioni ya akaunti ya Tegeta Escrow, Rais wa Chama cha Wanasheria (TLS), Lissu alisema juzi kuwa Mbunge wa Sengerema (CCM) huyo na watu wote waliopata mgawo huo wanatakiwa kukamatwa na kushtakiwa kwa kuwa ameuthibitishia umma kuwa ni mla rushwa.

Kauli hiyo ya Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), iliungwa mkono na Kafulila ambaye ndiye aliyeibua kashfa hiyo bungeni, kipindi hicho akiwa Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR Mageuzi).

Alipotafutwa na Nipashe jana kuzungumzia suala hilo, Zitto alisema sakata la akaunti ya Tegeta Escrow ni kubwa zaidi ya kurejeshwa kwa fedha hizo.

Zitto (40), ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia chama hicho, aliitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhakikisha inafuatilia kila senti iliyotoka kwenye akaunti ya Tegeta Escrow na ilikopelekwa.

Alisema wahusika wote, walioiba na waliowasaidia wezi ni lazima wakamatwe, huku akieleza kuwa mitambo ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL) bado iko chini ya kampuni hiyo licha ya Bunge kuazimia itaifishwe.

Kutokana na mazingira hayo ya mitambo kuwa bado chini ya IPTL, nchi bado inalipa mabilioni ya Shilingi kwa kampuni hiyo, alisema zaidi.

"Kashfa ya Escrow ni kubwa kuliko kitendo cha kurejesha pato la uhalifu. Takukuru ni lazima ifuatilie kila senti iliyoibwa kutoka Tegeta Escrow mpaka ilipoishia," alisema na kueleza zaidi: "Baada ya hapo, washtakiwe wote, wale walioiba na wale waliosaidia wezi.

Mitambo bado ipo mikononi mwa IPTL, bado tunalipa mabilioni ya shilingi kama tozo ya uwekezaji. Hilo ndilo jambo kubwa tunalopaswa kulizungumzia." Mbali na Zitto, Kafulila na Lissu, wabunge wengine waliokuwa mstari wa mbele kulisimamia sakata hilo bungeni mwaka 2014 ni marehemu Deo Filikunjombe, aliyekuwa Mbunge wa Ludewa (CCM) na Kangi Lugola, Mbunge wa Mwibara (CCM).

Katika ripoti yake iliyowasilishwa kwenye Kikao cha 18 cha Bunge la 10, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ilianika majina ya maofisa wa serikali, wabunge na viongozi wa dini waliopata mgawo wa fedha.

Watu hao walipewa fedha hizo na Mkurugenzi wa VIP Engineering na mmiliki mwenza kwa kampuni ya IPTL, James Rugemalira.

Mkurugenzi huyo na Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya Power African Power (T) Limited (PAP), Habinder Sethi Sigh wako mahabusu kwenye Gereza la Keko jijini baada ya kukosa dhamana walipofikishwa mahakamani na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wiki iliyopita na kusomewa mashtaka 12, yakiwamo ya uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na kuisababishia serikali hasara ya dola za Marekani milioni 22.1 na Sh. bilioni 309.4.

Mbali na Ngeleja, watu wengine waliopata mgawo huo ni ofisa katika Ofisi ya Rais wakati huo, Shabani Ngurumo aliyepewa Sh. milioni 80, aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu, Eudes Ruhangisa Sh. milioni 404.25 na aliyekuwa mjumbe wa Bodi ya Shirika la Ugavi wa Umeme (Tanesco), Dk. Enos Bukuku Sh. milioni 161.7.

Katika ripoti hiyo Waziri wa Nishati na Madini wa serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, Mbunge wa zamani wa Sumbawanga Mjini, Paul Kimiti, aliyekuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), Emmanuel Ole Naiko na aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu, Aloisius Mujulizi walitajwa kupatiwa Sh. milioni 40.4 kila mmoja.

Wengine ni Ofisa wa TRA, Lucy Apollo Sh. milioni 80.8, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mkuu wa Mamlaka ya Usajili wa Vizazi na Vifo (Rita), Philip Saliboko milioni 40.2, maaskofu Methodius Kilaini Sh. milioni 80.9 na Eusebius Nzingirwa 40.4, Padri Alphonce Twimannye Sh. milioni 40.4, maofisa wa Rita Placidus Luoga Sh. milioni 121.2 na Theophil Rugozobwa Sh. milioni 323.4.

Huyu Hapa Mwanaume wa Shoka....Ana Watoto 100 na Wake 12, Bado Anataka Kuongeza (+Video)

$
0
0
Mzeze mwenye umri wa miaka 80, Kofi Asilenu raia wa Ghana ambaye ana watoto 100 amedai bado anahitaji kuongeza watoto wawili katika familia yake.


Asilenu ana wake 12 na anaishi na familia yake katika kijiji cha Amankrom kilicho umbali wa kilomita 45 kutoka mji mkuu wa nchii hiyo, Acca. Familia yake ni thuluthi moja ya watu 600 katika kijiji anachoishi.

Sababu ya yeye kutaka kuendelea kuzaa ameeleza kuwa anahitaji familia kubwa kwa sababu hapo awali hakuwa na ndugu, “sina kaka wala shangazi, ndio sababu niliamua kuwa na watoto wengi ili nipate maziko mazuri nikifa,” alisema Asilenu.

Mjue zaidi Kofi Asilenu kupitia hii video:

EXCLUSIVE: Majibu ya Tundu Lissu Kuhusu Kumfuta Uwanachama wa TLS Waziri Mwakyembe

$
0
0
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, TLS Tundu Lissu amezungumza na kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa za ukimya wake baada ya kuchaguliwa kuwa Rais wa TLS ambapo mbali na hayo amezungumzia pia mchakato wa Katiba mpya na majukumu ya Rais wa TLS.

Kwenye EXCLUSIVE interview na Ayo TV na millardayo.com Tundu Lissu amefunguka pia kuhusu issue ya kumfutia usajili Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe pamoja na utawala wa sheria nchini Tanzania.


Tazama Video:


"Alichokifanya Ngeleja Kurudisha Fedha za ESCROW ni Udhaifu Mkubwa" - Mwanasheria Mziray

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alitangaza hivi karibuni kurudisha Tsh. mil 40.4 alizopewa na mfanyabiashara James Rugemarila ambaye anahusishwa na tuhuma za ESCROW na kuibua mijadala katika jamii.

Hatua ya Ngeleja kurudisha fedha hizo imeibua mijadala mbalimbali katika jamii ambapo watu mbalimbali waikiwemo Wanasheria wamekuwa wakiizungumzia issue hiyo ambayo tayari baadhi ya wahusika wamefikishwa Mahakamani akiwemo Rugemarila na kusomewa mashtaka.

Miongoni mwa wanasheria hao ni Hashimu Mziray ambaye anasema alichokifanya Ngeleja ni udhaifu na anatakiwa kuomba radhi, kwani fedha hizo alizichukua muda mrefu na huenda alizifanyia uzalishaji ambapo kisheria halijakaa sawa.


Sipati Hamu Wala Kusikia Raha Wakati wa Kufanya Mapenzi...Natamani na Mimi Nifike Kileleni?

$
0
0

Poleni na kazi, mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 25, na nimechumbiwa. Tatizo langu ni kwamba sijawahi kujisikia hamu ya kufanya mapenzi na wala huwa sitamani kufanya ngono, lakini huwa napenda kufanya mapenzi japokuwa hamu haipo kabisa na hivyo huwa naumia kwani kufanya mapenzi bila ya kuridhika na wala kusikia raha ni kazi

Wakati mwingine huwa najutia kitendo nilichokifanya yaani najuta kufanya mpenzi, Nifanyeje ili na mimi niweze kufika kileleni kwani wasichana wengine wanasema wanasikia raha sana...Naomba mawazo yenu...
My e-mail...Rachel2020@gmail.com

Mambo Manne Aliyosema Barakah The Prince Kuhusu Mpenzi wake Naj

$
0
0
Msanii wa Bongo Flava, Barakah The Prince amefunguka mambo manne kuhusu mpenzi wake, Naj.


Kupitia 5 Selekt ya EATV, Baraka amesema kwanza ieleweke kuwa Naj ni mchumba wake na si mke, kwani mke ni neno zito na maana yake tayari mmefunga ndoa.

Jambo la pili ni kuhusu picha aliyowahi kuposti instagram kuhashiria Naj ni mjamzito, Barakah amefafanua kuwa, “kwanza kabisa picha niliyoiposti ilionesha Naj kanenepa, si maana kwamba alikuwa na mimba.

Ameongeza kuwa, “maana ya kuandika caption thanks God sio maana kwamba ana mimba, ujue hata mpenzi wako mwili wake ukibadilika unashukuru”.

Kitu kingine kuhusu Naj, amedai kwa siku huwa anachati nae mara kibao, “suala la kuchati na Naj ni mara nyingi sana, hapa hata dakika tatu nyuma nimetoka kumtumia message, nawasiliana nae mara kwa mara”.

Jambo la nne Barakah ameeleza siku anapewa tetesi kuwa Naj yupo sehemu fulani anachepuka, ni kitu ambacho hawezi kukiamini kwanza, na pengine itakuwa ni siku ya wajinga duniani.

Waliofukuzwa Kazi NSSF (12), Nane Kati yao Kupandishwa Mahakamani Muda Wowote Kuanzia Sasa

$
0
0
Wale "miungu mtu" waliokuwa pale NSSF enzi za Dr. Dau sasa wamekufuzwa kazi rasmi, na tayari wengine muda wowote watapandishwa mahakamani kwa sababu mbalimbali zikiwemo matumizi mabaya ya madaraka, ubadhirifu, forgery, uwizi katika ardhi nk...

NSSF kuna watu walijipachika "umungu". Viashiria vya udini ulitamalaki, upendeleo ulitamalaki, undugu ulitamalaki. Watu tukapiga kelele kwa miaka 10 hatukusikika, leo kaka Mwana aliyeletwa na Mungu kukumboa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ananyosha viongozi uchwara kama hao waliokuwa NSSF..

Safi sana wizara ya utumishi

By Pagan Amum

Said Aliyetolewa Macho na Scorpion Afunguka Mazito...Adai Mkewe Anamsaliti na Mlevi

$
0
0

SAID ANAFUNGUKA MAZITO. "Mke wangu amenifanyia vitu vingi vya ajabu anapigiwa simu na wanaume na hao wanaume wananitukana nilimweleza baba yake akaniambia nimpe talaka au nimuoe mwanamke mwingine, amekuwa mlevi anaweza hata kumuingiza mwanaume mwingine chumbani kwangu kwa sababu sioni kwakweli nilishindwa kuvumilia hasa kutokana na hali yangu." #SaidMrisho #Live #LeoTena

Masamaki wa TRA Aachiwa Huru

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru Kamshna wa zamani wa Mamalaka ya Mapato Tanzania (TRA),  Tiagi Masamaki na wenzake watano.

watuhumiwa hao walikuwa washtakiwa kwa tuhuma za uhujumu uchumi ambapo waliidaiwa kuisababishia Hasara Serikali  Shilingi Bilion 12.7.


Mbali na Masamaki washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo  iliyotokana na sakata la makontena 329 ni Meneja Kitengo cha Huduma za Ushuru  TRA, Habib Mponezya  (45) na Meneja Msimamizi na Ufuatiliaji wa Forodha, Burton  Mponezya (51).

Msimamizi Mkuu Kitengo cha Ushuru wa Forodha  ICD Azam, Eliachi  Mrema (31),  Mchambuzi  Mwandamizi  wa Masuala ya Biashara  TRA,  Hamis Omary (48), Meneja wa Oparesheni  za Usalama na Ulinzi  ICD, Raymond Adolf Louis (39) na Meneja wa Azam ICD, Ashrafu Khan (59) na Haroun Mpande (28) wa kitengo cha Mawasiliano ya Kompyuta ICT TRA.

Kwa pamoja wanadaiwa kuwa kati ya Juni Mosi na Novemba 17, 2015 walikula njama kwa kuidanganya serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu Sh 12.7 bilioni.

Washtakiwa hao, wanadaiwa ku danganya kuwa Makontena 329 yaliyokuwepo katika Bandari Kavu ya Azam (AICD) yalitolewa baada ya kodi zote kufanyika wakati wakijua si kweli.

Habari zaidi punde endelea Kufuatilia Muungwana Blog

Star TV na Radio Free Africa zafungiwa

$
0
0

Mwanza. Ofisi za Kampuni ya Sahara Media Group inayomiliki kituo cha televisheni cha Star na cha redio cha Radio Free Africa (RFA) zimefungwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa deni la Sh4.5 bilioni.

Ofisi hizo zimefungwa leo Alhamisi (Julai 13) na wakala wa TRA, Kampuni ya Sukah Auction Mart and Court Brokers ya jijini Mwanza.

Meneja utumishi na utawala wa Sahara Media Group, Raphael Shilatu amesema ni kweli wana malimbikizo ya madeni yanayotokana na kuhama kutoka mfumo wa analogia kwenda digitali.

Haiwezekani... Nataka Kupima DNA Nimestuka!! Wanangu Hawajafanana na Mimi

$
0
0
Mwenzenu jamani nahisi nmechakachuliwa,nina mke wangu tumezaa watoto wawili mmoja yuko na miaka mitano na wa pili miwili,kati yetu mimi na mke wangu nahisi kuna kitu kinaendelea na nimefanya uchunguzi wa kina na kuishia kwa majibu ambayo hayaniingii aklini na pili vilevile hawa watoto wanafanana exactly na watu ninao wahisi

Nkijaribu kurudisha hisia nyuma naona matukio yanafanana na mke wangu pia alikuwa amejipatia ujauzito kwenye mazingira ya kutatanisha,Huyu wa kwanza anafanana sana na boyfriend wake wa zamani ambaye mimi namjua!kipindi yuko mjamzito nilishawahi kumfuma na meseji kibao za mahapa na njemba hilo!

Huyu wa pili anafanana sana na Babu mmoja hapa mtaani kwetu anashona viatu
Huyu mara nyingi nmeshawahi kumkuta home anajisingizie kuja kuchukua viatu,mbaya zaidi hata huyu mtoto huyu mwwanamke anajitahidi sana kumjengea mazoea nae

Sasa naombeni ushauri jamani mimi nifanye nini?

Kamanda Mkuu Usalama Barabarani Ang’olewa

$
0
0

Katika taarifa hiyo, inaelezwa kuwa Mpinga ameng’olewa baada ya kubadilishwa kituo chake cha kazi, akipangiwa katika eneo lingine, ikiwa ni mwendelezo wa mabadiliko ndani ya jeshi la polisi.

Habari za ndani ambazo Nipashe ilizipata kutoka kwa chanzo chake cha uhakika zilidai kuwa Kamanda Mpinga amebadilishwa kituo chake cha kazi kwa kupelekwa Mbeya kuwa Kamanda wa Polisi wa mkoa huo huku nafasi yake ikichukuliwa na aliyekuwa Ofisa Mnadhimu wa kikosi cha Usalama Barabarani, Fortunatus Musilimu.

Taarifa zaidi zilieleza kuwa Kamanda wa Mkoa wa Mbeya,Dhahiri Kidavashari, amerudishwa makao makuu  ya jeshi.

Hata hivyo, hadi kufikia jana jioni, Nipashe haikufanikiwa kupata taarifa rasmi za jeshi hilo kuelezea mabadiliko hayo.

Awali, alipoulizwa juu ya taarifa hiyo, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Barnabas Mwakalukwa, alisema hawezi kusema taarifa hizo ni za kweli au uongo kwa kuwa hazijamfikia, na kwamba akijulishwa atazitoa bila shida.

Mbali na majibu hayo, Mwakalukwa alimtaka mwandishi amuulize Mpinga mwenyewe ambaye pia ni msemaji.

“Sasa nikuambie kitu, taarifa kama hizo unamuuliza anayehama, yaani Mpinga… maana na yeye ni msemaji.

Halafu kama anahamishwa, yupo ambaye atachukua nafasi yake atakuambia. Mimi ninasemea Jeshi zima hivyo kama amehama na namba zake mnazo, muulizeni,” alisema Mwakalukwa.

Aidha, Mwakalukwa aliongeza: “ Lakini huenda akawa bado … mmesikia fununu tuu. Msifanye kama wale wa social media. Kama umepata hizo fununu, si usubiri mamlaka iseme na uzuri wake tumeruhusu wasemaji ni makamanda wa mikoa na makamanda wa vikosi. Hivyo anaweza kukujibu vizuri,”

 Mwandishi alipumuuliza Kamanda Mpinga juu ya kuwapo kwa taarifa za yeye kuhamishiwa Mbeya, alisema: “Mimi natokea safari Dodoma kikazi. Kwa hiyo nitatoa taarifa rasmi leo. Na mimi nimesikia kuna uhamisho ila sijajua nimepangiwa wapi.”

Source: Nipashe

John Mnyika Amshukia JPM Kuhusu Waziri wa Nishati na Madini

$
0
0

Mbunge wa Kibamba(Chadema) John Mnyika, ameandika katika ukurasa wake wa twitter akimtaka Rais John Magufuli ateue Waziri wa Nishati na Madini.


“Mheshimwia Rais, lini utateua Waziri wa Nishati na Madini,” ameandika jana Mnyika


Mei mwaka huu, Rais Magufuli alitengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo mara baada ya kupokea ripoti ya kamati ya kwanza iliyochunguza makontena 277 yenye mchanga wa madini yaliyozuiwa bandarini.


Tangu wakati huo, hakuna aliyeteuliwa kushika nafasi ya Profesa Muhongo, ingawa Naibu Waziri Dk Medard Kalemani anaendelea na kazi.

JE Una Tatizo la Nguvu za Kiume , kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr.

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0767447444 na 0714335378

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

Yanga Yapata Kigugumizi Baada ya Kocha Kuwakimbia......

$
0
0
Katibu Mkuu wa klabu ya Mabingwa Ligi Kuu Tanzania Bara Young Africans, Charles Boniface Mkwasa amepatwa na kigumuzi kwa kushindwa kuzungumzia sakata la kuondoka kwa msaidizi Juma Mwambusi na kudai suala hilo lipo katika uongozi linashughulikiwa.

Mkwasa ameeleza hayo baada ya kuwepo tetesi kuwa mkataba Mwambusi umefikia tamati tangu tarehe 30, Juni mwaka huu kuitumikia klabu hiyo.

"Suala la Mwambusi lipo kwenye uongozi linafanyiwa kazi lakini kama mwenyewe amezungumza hilo anaondoka basi ameongea yeye mwenyewe lakini mimi najua suala lipo katika uongozi na siwezi lisemea mpaka litakapofanyiwa kazi", amesema Mkwasa.

Katika hatua nyingine, Mwambusi amenukuliwa akisema anaondoka katika timu hiyo kwa kuwa kuna mambo mengine binafsi amepanga kuyafanya.

“Mkataba wangu umeisha tangu Juni 30, naushukuru uongozi na wana Yanga wote, kwa misimu miwili tumefanya kwa mafanikio… Naondoka kwa roho safi… Msimu wa kwanza tumechukua makombe mawili, msimu wa pili nimefanya kazi na makocha wawili na tumefanikiwa kuchukua ubingwa ….Sitakuwa kwenye mpira, nitakuwa kwenye mambo binafsi, nahitaji kupumzika, ila msimu unaofuata ikiwezekana tunaweza kuonana tena,”amesema Mwambusi
Kocha huyo ambaye amedumu Yanga kwa misimu miwili akitokea Mbeya City, amewataka wana Yanga wote kuendelea kushirikiana ili kuongeza mafanikio zaidi.

Kwa upande mwingine, Mwambusi ametaja deni kubwa ambalo timu hiyo inalo ni kutwaa kombe la mabingwa barani Afrika, kwa kuwa ubingwa wa Tanzania hadi sasa siyo kitu kigeni tena kwao.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images