Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Usher Raymond Atembelea Mbuga ya Serengeti

$
0
0
Msanii wa Marekani Usher Raymond yuko ziarani nchini Tanzania akitembelea eneo la uhifadhi wa wanyama pori la Serengti National Park.

Bwana Raymond alichapisha baadhi ya picha akiwa na familia yake katika akaunti yake ya Twitter.
Alielezea hali ilivyo katika eneo hilo kama ya kufurahisha .

Ripoti za Usher Raymond kuzuru Tanzania zilisambaa kwa haraka nchini humo.

Watu wengine maarufu akiwemo mchezaji wa zamani wa Manchester United na Real Madrid David Becham, aliyekuwa mchezaji wa Liverpool Mamadou Sakho, mchezaji wa Everton Morgan

Schneiderlin ni miongoni mwa wale waliozuri katika sehemu mbali mbali za kitalii nchini humo mwaka huu.

Vivutio vya kitalii nchini Tanzania kama vile mbunga ya uhifadhi wa wanyama pori ya Serengeti na mlima Kilimanjaro ni vivutio vinavyoongoza kwa utalii ambapo watu wengi maarufu wametembela.

Wabunge Wazichapa Kavu Kavu Bila Gloves

$
0
0
WABUNGE wa Taiwan leo walichapana makonde, wakarushiana viti na mabaluni ya maji baada ya kutofautiana kuhusu mradi mmoja wa miundombinu. Tukio hilo ni mwendelezo wa matukio yaliyoanza jana ambapo katika kubishana, wabunge hao walikwidana mashati na kuchapana wakati wa kupitia bajeti ya mradi huo.

Mpango huo ni moja ya miradi mikubwa iliyopendekezwa na Rais Tsai Ing-wen ambayo inajumuisha ujenzi wa reli za kutoa huduma ndogondogo, hatua za kuthibiti mafuriko na mazingira yanayosababishwa na viwanda.

Hata hivyo, chama cha upinzani cha Kuomintang kinapinga mradi huo kikisema unapendelea miji na wilaya ambazo zinaunga mkono chama cha Democratic Progressive (DPP) ambako kina uhakika wa kuungwa mkono katika uchaguzi wa mikoa mwaka kesho. Isitoshe, wapinzani wanapinga kiasi kikubwa mno cha Dola bilioni 13.8 ambazo zitatumika katika mradi huo.

Waziri Mkuu Lin Chuan alishindwa kutoa ripoti ya bajeti hiyo Alhamisi baada kutupiwa baluni la maji na kumfanya aondoke bungeni ambalo liliahirishwa. Leo, Lin aliingia tena bungeni lakini akiwa bado hajasema chochote vurugu ziliibuka.

Wapinzani waliinua viti juu na kulizunguka jukwaa la kutolea hotuba huku wakishikana mashati na mahasimu wenzao na hivyo kumfanya Lin ashindwe kusema chochote ambapo mabaluni ya maji yalikuwa yakitupwa kuelekea eneo hilo.

Diwani Chadema Mikononi Mwa Takururu Kwa Rushwa.....

$
0
0
Diwani Kata ya Msigani, Ubungo, Israel Mushi ( 48 ) na Mrasimu ramani wa Manispaa ya Ubungo, Francis Mwanjela Peter ( 28 ) wamekamatwa na Tasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU),wilaya ya Kinondoni kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa  Sh.5,000,000/=.

kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa  TAKUKURU wilaya ya  Kinondoni Teddy Mjangira, amesema kuwa Watuhumiwa walikamatwa Julai 12, 2017 baada ya kupokea kiasi hicho cha fedha toka kwa mwananchi ambaye jina lake limehifadhiwa na ambaye mbali na kutoa kiasi hicho cha pesa alitakiwa  na watuhumiwa kuwapa  rushwa ya Sh.10,000,000/=

Inadawaiwa Watuhumiwa walishawishi na kupokea rushwa ili waweze kutoa ushawishi kwa wajumbe wa kamati ya mipango miji  inashughulikia maombi ya kubadilisha michoro, kubadilisha matumizi ya kiwanja na kupitisha kibali cha ujenzi katika Manispaa ya Ubungo.

Uchunguzi wa tuhuma unaendelea na Watuhumiwa ambao wanatuhumiwa kutenda makosa kinyume na kifungu namba 15 cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007 wamepewa dhamana.

Mkuu wa TAKUKURU (M) Kinondoni Bi.T. MNJAGIRA anawaasa Viongozi wote wa Umma, Wanasiasa na Watumishi wote wa Serikali, kuheshimu nyadhifa zao na kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria bila kujihusisha na vitendo vya Rushwa. Pia, anatoa wito kwa  Wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU kwa kuwafichua wale wote wanaojihusisha na  vitendo vya rushwa ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria, Kwa kufanya hivyo, tutakuwa tumezuia vitendo hivyo visiendelee kujitokeza katika Jami

TRA Arusha Yafungia Vituo 54 vya Mafuta .

$
0
0
Mamlaka ya mapato Tanzania ,Mkoa wa Arusha TRA ,imevifungia vituo zaidi ya 50 vya mafuta kwa kosa la kutoa Huduma ya kuuza mafuta bila kuwa na mashine za kielitroniki(efd's)zinazotoa risiti kwa mteja.

Meneja wa TRA Mkoani hapa ,Mbaruku Apili alisema zoezi hilo ni endelevu na linakusudia kuimarisha mapato ya serikali ,qmbapo amewahimiza wamiliki wa vituo hivyo kufunga mashine za kutoa risiti ambapo mashine moja inathamani ya shilingi milioni 7

By Jembejembe/JF

Ilipofikia Kesi ya Kina Rugemalira wa ESCROW

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imeahirisha kesi inayowakabili mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder  Singh Sethi na  mfanyabiashara James Rugemalira wanaokabiliwa na mashtaka 12, yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha serikali hasara.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 22, mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya wakili wa serikali, Leornad Swai, kueleza kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Mawakili wanaomtetea mfanyabiashara Harbinder Singh Sethi wameiomba Mahakama imruhusu mteja wao akatibiwe nje ya nchi, kutokana na kuwa na uvimbe na Baloon tumboni hali inayomsababishia maumivu makali na kumnyima usingizi kwa wiki ya nne sasa, ombi ambalo limekataliwa na Mahakama na kuagiza atibiwe Muhimbili.

Ulinzi Aliyoingia nao Wayne Rooney Uwanja wa Taifa leo

$
0
0
Baada ya kikosi cha Everton cha England kuwasili Tanzania asubuhi ya July 12, jioni walifanya mazoezi yao ya mwisho kabla ya kucheza dhidi ya Gor Mahia Alhamisi ya July 13 2017 katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Miongoni mwa mastaa wa Everton waliyowasili katika mazoezi alikuwa ni Morgan Scheiderlin na Wayne Rooney ambaye yeye alionekana kuwekewa ulinzi zaidi wa pekee yake wakati akielekea katika vyumba vya kubadilishia nguo kabla ya kuanza mazoezi.

Rooney ambaye katika kikosi cha Everton ndio mchezaji mwenye jina kubwa kuliko wote, aliingia na walinzi watatu wakiwa wanamlinda ili asipate ghasia yoyote, Rooney amejiunga na Everton msimu huu akitokea Man United lakini ni nahodha pia wa timu ya taifa ya England.


Sumaye:Hatutanyamaza Hata Kidogo

$
0
0

Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani na Mjumbe wa Halmashauri  Kuu Chadema, Frederick Sumaye amesema kuwa licha ya kukatazwa wasizungumze masuala ya kisiasa, lakini hawatanyamaza.

Akizungumza na vyombo vya habari leo, Sumaye amesema kuwa wataendelea kufanya kazi kwa niaba ya wananchi ambao wana imani nao.
Amesema nchi  kwa sasa inakazana kujenga mfumo wa demokrasia kandamizi ambayo kwa kiasi kikubwa inarudisha nyuma maendeleo.

“Viongozi wa upinzani wamekuwa wakikamatwa, wanawekwa rumande, wanatishwa lengo ni kudhoofisha upinzani,” amesema Sumaye.
Amesema licha ya juhudi hizo za kuwarubuni baadhi ya viongozi wakiwamo madiwani wachache, hawatadhoofika na wataendelea kufanya kazi.

Sumaye amesema kwamba  wanataka kujenga upinzani  wa kweli wenye lengo la kusaidia wananchi.
Amesema katika kulihakikisha hilo hadi kufikia mwaka 2018 hakutakuwa na kijiji, mtaa utakaokuwa hauna tawi la Chadema.

Jack Wolper Sarakasi za Mapenzi Zinakuharibia........

$
0
0
MIONGONI mwa mambo ambayo napenda kuyafanya nje ya kazi yangu ya uandishi, ni kutazama filamu. Kwenye eneo hili ninao uzalendo wa kuringia kwani nimejikita sana kuangalia sinema za hapa Bongo, ingawa zipo nyakati huwa najikuta nikinogewa na uigizaji wa wasanii wa nje, kutegemeana na aina ya filamu na maudhui yake.

Kwa mantiki hiyo, wapo wasanii wachache hapa Bongo ambao nawakubali kwa uwezo wao wanapokuwa wakikamua kazi mbele ya kamera, miongoni mwao ni pamoja na mdogo wangu, Jacqueline Wolper.


Aliingia kwenye game la Bongo Movie, tayari kabati langu la stoo likiwa limejaa filamu nyingi za Kitanzania nilizokwisha kutazama,  naye akafanya yake na kunishawishi kumkubali.

Kwa jinsi alivyo kikazi, Jack anajua kucheza na akili za watazamaji wenye macho ya uchambuzi na upembuzi wa mambo kama mimi. Pia msanii huyu ni kati ya wanawake wachache sana waigizaji wetu wenyekupambana na maisha kwa kiwango kikubwa, anayo kiu kubwa sana ya mafanikio na ndiyo maana amekuwa akiruka huku na kule kusaka noti kwa kutoka jasho halali.
Pamoja na hayo, lipo jambo moja ambalo mdogo wangu asipolitazama kwa jicho la ziada, linaweza kumuondolea kabisa sifa yake ya upambanaji wa maisha kama msanii na mjasiriamali. Ni upande wa pili wa maisha yake, yaani mapenzi. Eneo hili Jack amekuwa na sarakasi nyingi sana ambazo zimenifanya leo nifikirie kumpa ushauri kupitia hapa kwani muda wangu wa kukutana naye kama nilivyosema hapo juu, ni mdogo na ni wa kubahatisha mno.


Mlolongo wa maisha yake ya mahusiano umejaa dosari za namna ambayo hailingani kabisa na hadhi na nafasi aliyonayo katika jamii pamoja na umri kwa jumla. Nimewahi kufanya mahojiano fulani na Jack ambapo alinibainishia umri wake halisi, ni kweli bado ni binti mdogo sana, tofauti kabisa na namna ambavyo watu wengi wanamfikiria, lakini lazima ajue kuwa kila siku usomaji wa kalenda unabadilika.

Amekuwa mtu wa kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, tena mara nyingi na vijana wadogo kabisa anaowaacha mbali kiumri na kuishia kuumizwa kwa kuachwa hivyo kuongeza orodha na idadi isiyokuwa na maana katika historia ya maisha yajayo.

Niseme tu kuwa, Jack una sifa nyingi nzuri mno, lakini tatizo ni nini linalokufanya ushindwe kuwa na utulivu kwenye anga la mapenzi? Kama ni urembo unao? Jina maarufu unalo na kwa upande wa pesa sina shaka juu ya hilo kutokana na mambo ninayoyaona ukiyafanya kwa juhudi za mikono yako, tatizo lako ni nini mdogo wangu? Hebu kaa chini ujiulize mara mbilimbili. Muda haukusubiri kwa chochote.

Hayo mambo ya sijui umeiba mume wa mtu, mara umepora mpenzi na mchumba wa mwanamke fulani, yanaharibu mno mustakabali wa maisha yako yajayo, kwani historia inayo
tabia ya kudumu milele hata kama mhusika ataondoka chini ya jua. Au una shida gani kwenye eneo hilo la mapenzi? Uliwahi kufanya mahojiano na mmoja wa waandishi wetu, ukamwambia wanaume wote uliowahi kuwa nao kwenye mahusiano hawana matatizo, ila wewe ndiye ‘mshenzi’ na kwamba huabudu mapenzi hivyo ukimchoka mtu unamuonesha njia na hujawahi kuachwa! Sasa mambo gani hayo?

Yaani kweli uzuri wote wa sura ulionao nao, ujuzi wa kazi na upambanaji wa kimaisha ulionao, kumbe ndani si chochote? Sitaki kuamini kama na wewe una ule uzuri wa mkakasi kumbe ndani ni kipande cha mti. Ni wakati wako sasa kubadilika na kuwa Wolper mpya, kutulia na mwanaume unayeendana naye, kufunga naye ndoa na kisha kutengeneza familia na kuyaacha maisha yasonge kwa heshima zake.

Nguvu Kuu 7 Alizonazo Mwanamke

$
0
0
Nguvu kuu 7 alizonazo mwanamke

1. Uwezo wa kuona na kugundua ya mbeleni (anawezakuona kisichosemwa au kitakachokuja).               Anatumia mlango wa sita wa fahamu unaoitwa EPS
2. Ananguvu ktk kinywa chake kuliko nguvu za mwili kwa mwanaume. Athari za kutotumia kinywa       chake vema ni kubwa zaidi.
3. Nguvu na uwezo wa kuendeleza uumbaji
4. Nguvu ya ushawishi
5. Nguvu na uwezo wa kustahimili. Kuvumilia. Kubeba mazito.
6. Nguvu na uwezo wa kujadili bei (bargaining power)
7. Uwezo wa kuwaathiri watoto (positively or negatively)

ILI NGUVU HII ITENDE KAZI
1. Tumia vema kinywa chako
2. Tumia vema ushawishi wako
3. Jitambue

Video: Mayweather Amchapa Mpinzani wake Kwa Noti Kabla ya Pambano lao

$
0
0
Homa ya pambano la masumbwi baina ya mfalme wa uzito wa welter, Floyd Mayweather dhidi ya Conor McGregor inazidi kupamba moto mara baada ya bondia huyo wa Marekani usiku wa jana kumwagia noti za dola za Kimarekani mpinzani wake mara baada ya kukutana katika mkutano wao na waandishi wa habari.



Mayweather ambaye alistaafu masumbwi mwaka 2015 akiwa na rekodi ya kutopoteza pambano hata moja kati ya michezo 49 aliyowahi kucheza anatarajia kukutana na McGregor ulingoni huko Las Vegas Agosti 26, mwaka huu.

Baada ya Kuvuja Kwa Picha za Uchi....Blac Chyna Aamua Kurudi Kwenye Kazi yake ya zamani

$
0
0
Blac Chyna ameamua kutafuta mkwanja zaidi na kuweka pembeni ugomvi uliopo kati yake na ex wake, Rob Kardashian.


Kwa mujibu wa TMZ, umeripoti kuwa mrembo huyo ameamua kurudi kwenye kazi zake za mwanzoni alizokuwa akizifanya kwa kutangaza katika klabu za usiku nchini Marekani.

Chyna anatarajiwa kuanza kuonekana kwa mara ya kwanza kwenye kazi yake hiyo ya katika klabu ya Medusa Lounge, mjini Atlanta Jumamosi hii.


Wakati huo huo siku ya Jumatatu ya Julai 17, video vixen huyo atakuwepo katika klabu ya Ace of Diamonds iliyopo West Hollywood ambapo anadaiwa kupokea kiasi cha dola 10,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 22 kwa fedha za kitanzania.

Hajawahi Kujamiiana, na Bado Ananibania Mpaka Sasa

$
0
0
Habari Wadau... Nina mpenzi wangu, nampenda saana, we have been dating for 1 year and 9 months now. Hatujawahi ku-doo. At the early stages of our relationship, i once cheated, na nlimuumiza sana, lkn nilikiri makosa, na akanisamehe, and we trust each other once again, na tunaendelea vzri sana kwakweli, mapenzi yapo vizuri.

The issue is, she is a virgin,ive proved it, coz sometimes tunakua faragha pamoja, we kiss and romance, bt we dont do it,, lakini kila nikimuomba, ananiambia she is not ready, she told me to wait for another year, i am ready to wait bcause of the love i have for her, lkn maswali hayaishi kichwani mwangu, je, nikiendelea kungoja, mpaka muda huo, which will b almost three years, will it b not too long? Hatakuja kunidharau na kuniacha njia panda? Will she keep on loving me? Am i doing the right thing kungoja,?? Samtymz nakua na hamu and i dont want to cheat on her,, na maswali mengine mengi,, nishaurini wadau? Am i going in the ryt track? Should i wait?? Au nimuombeje akubali na ajue kua kwa muda wote niliokua nae, kama ningekua nahitaji ngono tu, ningeshamuacha, im rreally into her, na akiendelea kua na tabia njema, Mungu akipenda tutaoana,kwasababu sijaona baya lolote kwake,, ushauri wadau. Shukrani sana

Aibu Kubwa:Nitaiweka Wapi Sura Yangu?

$
0
0
Kumbe ile kauli ya wahenga ya kwamba "Zamwizi ni arobani" kumbe ni kweli. Ona huyu binti anavyo nitia haibu na nisijue niwapi nitaiwka sura yangu? Hii ilitokea baada ya mimi kupata likizo ya mwezi m-moja hapa kazini kwangu, ndipo nikaamua kumtembelea dada yangu aliyeolewa Arusha. Ndani ya nyumba nilikutana na Beki 3 (mfanya kazi) marayakwanza tulikutana chooni hii nibaada ya yeye kuni kuta nikiwa uchi chooni (naoga) ndipo nilipo mkamata mkono na kumuuliza kipi kilicho mfanya aingie wakati kaniona mimi nakwenda kuoga? Jibu lake lilikua "samahani"huku akiwa na mapepe. Ndipo nilipo mkamata mkono na kumtuliza huku nikiwa uchi wa mnyama. Kwakuwa ilikuwa ni usiku wa mananane (watu wote wame lala) mtoto (beki3)alitulia kama anasubili kunyolewa. Sikuhiyo nilijipigia la jogoo (goli moja) huko choon. Siku zilivyo endelea mtoto alizoea kale kamchezo. Japo alikua na miaka 15 lakini mtoto alionekana kamchezo anakijua (fundi) ilifikia wakati mtoto alikua akini fuata chumbani nilipo lala, na kuendela na kumuudhi mungu (kufanya zinaa). Bada ya mwezi na likzo yangu kuisha nilirejea nyumbani (Dar). Sasa ni miezi mitano (5) ninapata habari yule binti ana mimba na mtu pekee aliye mtaja ni mimi. Hapa nilipo nime lowa jasho sijui mkewangu akijua itakuaje? Sijui dada yangu yuko kwenye hali gani? sijui nitaiweka wapi sura yangu?

Wagombea CCM Kibiti Washindwa Kuchukua Fomu....Kisa....

$
0
0

Wakati hali ya wasiwasi ikizidi kushamiri kwa wakazi wa wilaya za Kibiti na Rufiji juu ya usalama wa maisha yao kutokana na kuendelea kwa matukio ya mauaji, hofu hiyo bado imetanda miongoni mwa wanachama wa CCM wanaohofia kuchukua fomu za kuwania uongozi ngazi ya matawi na shina.


Akizungumza na gazeti la Mwananchi kwa njia ya simu, Katibu wa Siasa na Uenezi wa chama hicho katika wilaya hizo, Mussa Mnyeresa amesema sababu za wanachama kususa kuchukua fomu hizo hasa ngazi za tawi, shina na  nafasi nyingine ni mfululizo wa matukio ya mauaji yanayoendelea katika wilaya hizi.


Amesema katika wilaya ya Kibiti, kata za Mjawa, Ruaruke na Mchukwi yanaongoza kwa wanachama wa chama hicho kutochukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.


Aidha amesema katika wilaya ya Rufiji uchukuaji fomu za nafasi za uongozi Tarafa ya Ikwiriri yenye Kata tatu za Umwe, Mgomba na Ikwiriri napo zoezi la uchukuaji fomu wa nafasi hizo si la kuridhisha.


Mnyeresa amesema hadi sasa kasi ya uchukuaji fomu hizo katika kata hizo bado ipo chini huku viongozi wa chama hicho wakiendelea kuwahamasisha wanachama wa chama hicho wachukue fomu.


Amesema uongozi wa chama hicho ngazi ya wilaya hizo ambazo awali ilikuwa ni wilaya moja tayari umepeleka taarifa za wanachama kwenye baadhi ya maeneo kutochukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali wakihofia usalama wao.


Akizungumza juu ya wanachama kuchukua fomu za uongozi Ngazi ya Tawi na Shina katika wilaya ya Kibiti, Katibu wa chama hicho wilayani hapa, Zena Mgaya amesema hali ya uchukuaji fomu kwenye ngazi hizo hairidhishi.


Zena alisema katika ngazi za uongozi za kata na wilaya hali inaridhisha na wanachama wamehamasika kuchukua fomu hizo.


Amesema hadi sasa kati ya kata 16 zinazounda wilaya ya Kibiti, tayari wamepokea fomu za kata 10 za wagombea wa nafasi za tawi na shina.


Amesema kwa upande wa nafasi za uongozi wa ngazi za kata na wilaya, bado wanachama wanaendelea kuchukua fomu na kuzijaza.


Zena amesema pamoja na kuwepo hofu ya mauaji kwa wananchi na wanachama wa chama hicho, bado mwitikio ni mzuri zaidi kwenye nafasi za kata na wilaya.


Akizungumzia wanachama wa chama hicho kutochukua fomu hasa za ngazi ya tawi, mmoja wa wanachama wa chama hicho, ambaye pia ni Diwani Kata ya Mtawanya, Malela Tokha amesema ni vyema uongozi wa chama hicho ngazi ya taifa ukayafanyia kazi maombi ya wanachama wa chama hicho waliyoomba uchaguzi huo usogezwe mbele.


Amesema hali hiyo itaepusha chama hicho kupata viongozi wasiokuwa na sifa na uwezo na kuzidi kukidhoofisha chama kwa kuwa wakati huu wanachama wenye uwezo wengi wao wanaogopa kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi.

RC Gambo ameonya shule kugeuzwa kuwa matawi ya siasa

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa ARUSHA,MRISHO GAMBO,ameonya shule kutogeuzwa kuwa matawi ya siasa na walimu wakuu kuacha kuruhusu hali hiyo na iwapo watabainika kukiuka agizo hilo watachukuliwa hatua za kisheria.


Gambo anatoa onyo hilo wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa wakuu wa shule za sekondari ARUSHA-TAHOSA-na kutoa angalizo kuwa shule ni eneo kwa ajili ya kutoa elimu kwa wanafunzi na si kitovu cha siasa.


Amesema kuna tabia imeanza kuibuka ya baadhi ya shule kugeuzwa vijiwe vya siasa na kuyataka mashirika yasiyo ya kiserikali endapo yanalengo la kusadia wanafunzi wanaopata mimba mashuleni ni vyema wakaweka mawakili wakuwaadhibu watu wanaowapa ujauzito wanafunzi.


Wakuu hao wa shule wametaja kuwa mkutano huo kuwa ni mojawapo ya jitihada mbalimbali wanazozifanya kuboresha elimu katika shule za sekondari mkoani ARUSHA.

Kwa Hii Serikali ya JPM Tutanyooka tu...SUMATRA yafungia Meli Mbili

$
0
0
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) mkoani Mwanza imesimamisha usafiri wa meli mbili zinazotoa huduma ya usafiri wa abiria kati ya jiji la Mwanza na baadhi ya visiwa vilivyopo ndani ya ziwa Victoria kutokana na ubovu wa meli.

Mbali na hilo (SUMATRA) imeagiza wamiliki wa meli zingine tatu ikiwemo Mv Clarias inayomilikiwa na serikali kufanya matengenezo ya meli zao kwa haraka iwezekanavyo ili kuendelea kutoa huduma ya usafiri ulio salama kwa abiria na mali zao.  

Waziri Mwakyembe Azishukia Simba na Yanga...."Hawako Series"

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amezishukia klabu za Simba na Yanga na kuzitupia lawama kuwa zimekosa nafasi muhimu ya kucheza na timu kubwa ya Everton ambayo jana imeshuka dimbani na klabu ya Gor Mahia

Katika mchezo wa jana ambao Everton waliweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya klabu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya katika mchezo wa kirafiki umempelekea Waziri Mwakyembe kutoa yake ya moyoni kwa klabu za Tanzania.

"Kwanza nafikiri hili liwe fundisho kwa klabu zetu za nyumbani mimi nina uhakika wanaweza kunisahihisha tulipowaambia kutakuwa na mashindano na timu ya Everton hapa kwa timu itakayoshinda sidhani kama walituamini, sababu timu walizokuwa wanaleta mlikuwa mnaziona wachezaji wale mahiri wengi walikuwa hawapo, mimi nilisikitika sana na niwe mkweli nilitamani sana timu ya Tanzania ndiyo icheze na Everton katika mchezo ule kwenye uwanja wetu ambao tumeuhangaikia sana kuweka nyasi mpya za muda" alisema Mwakyembe 

Mbali na hilo Waziri Mwakyembe alitoa wito kwa klabu za Tanzania
"Jamani pale tunapowaambia kuna mashindano tuchukulie jambo hilo umuhimu, maana ujio wa Everton unafaidia kubwa tatu kwa taifa letu na Afrika Mashariki kiujumla moja ni kwa timu yenyewe ambayo imecheza nayo Gor Mahia pamoja na kufungwa lakini waliibuka mashujaa, kwa sababu wamepata uzoefu wa kimataifa na wameonekana dunia nzima, hivyo vijana wa Gor Mahia waliocheza vizuri kesho na kesho kutwa watatafutwa na watu wanaotafuta wachezaji, lakini pia imefunguka njia kwa dunia kwamba Tanzania ni nchi inayopenda michezo lakini imeonyesha kuwa tuna viwanja vya kimataifa hapa. Faida nyingine ni utalii imefungua njia kwamba Tanzania tuna vivutio vingi vya utalii" alisema Mwakyembe

Mbali na hilo Mwakyembe alisema kuwa timu ya Gor Mahia kucheza na Everton imewajengea kujiamini kwamba hakuna timu wanaweza kukutana nayo Afrika Mashariki ikawasumbua, na kudai kutokana na hali hiyo saizi timu yoyote itakayokutana na Gor Mahia itafungwa tu.

Walahi Sikutegemea Kama Baraka The Prince Kuja Kuwa Mpenzi Wangu, Najma Afunguka Makubwa

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva Najma ambaye ni mchumba wa Baraka The Prince amefunguka na kusema hakutegemea kuwa katika mahusiano na Baraka The Prince lakini alijikuta tu ameingia kwenye mahusiano na msanii huyo.

Msanii Baraka The Prince akiwa na mpenzi wake Najma
Najma alisema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema awali hakutegemea kama angekuwa katika mahusiano na msanii huyo.
"Kiukweli kabisa mimi wala sikutegemea kuwa na Baraka The Prince sema imetokea, nashukuru Mungu tunapendana saizi yeye ndiye ananichagulia hata nguo za kuvaa akiona sijapendeza ananiambia hata kama kitu mimi nimependa yeye asipopenda nabadili, kwa hiyo tunapenda sana" alisema Najma 

Kwa upande wake Baraka The Prince alisema kuwa ni mapenzi ni moyo wa mtu wala si kabila au ushamba ni vile watu wawili mnavyopenda na kukubaliana na ndiyo kitu kilichotokea kati yao.
"Unajua mimi ni Msukuma na natoka Mwanza lakini nikwambie kitu mapenzi siyo kabila wala sehemu unayotoka, maana unaweza kuwa unatoka mkoani lakini ukawa mjanja na wapo wengine wanatoka mjini lakini washamba, kwa hiyo mimi na Naj tunapendana na tumekubaliana na ndiyo maana unaona tuko pamoja mpaka sasa" alisema Baraka The Prince.

JE Wajua Faida za Kunywa Chai ya Kahawa Katika Mwili Wako?

$
0
0
Ukikunywa vikombe vitatu vya kahawa kwa siku unaweza kuishi miaka mingi, kwa mujibu wa utafiti uliofanyiwa karibu watu nusu milioni kutoka nchi 10 za Ulaya.

Utafiti huo uliochapishwa kwenye jarida na Annals of Internal Medicine, unasema kuwa unywaji wa kahawa unaweza kuongeza maisha ya mtu.

Lakini wataalamau wanasema kuwa ni vigumu kusema kuwa ikiwa ni unywaji kahawa unachangia watu kuishi miaka mingi au ni maisha ya kiafya wanayoishi wanywaji kahawa.

Watafiti kutoka shirika la Agency for Research on Cancer and Imperial College London, wanasema wamegundua kuwa unywaji wa kahawa nyingi unahusiana na hatari kidogo ya kufariki hasa kutokana na magonjwa ya moyo.

Waliafikia uamuzi baada ya kuchunguza takwimu kutoka kwa watu walio na umri wa zaidi ya miaka 35 kutoka nchi 10 za Ulaya.

Waliawauliza watu wakati wakianza utafiti kuhusu kiasi cha kahawa walikuwa wakinywa kisha wakaangali vifo vilivyotokea katika kipindi cha miaka 16.


Lakini cha kuvunja moyo kwa wanywaji wa kahawa, ni kuwa ugunduzi huu haueleweki vyema.

Kwa mfano haukuonyesha ni kipato cha kiwango gani wanywaji pombe hupata ikilinganishwa na wale wasiokunywa kahawa.

Huenda ikawa labda watu walio na uwezo wa kununu vikombe vitatu vya kahawa kila siku wana pesa zaidi, na kwa njia moja au nyingine huwasaidia kulinda afya zao.

Hizi Hapa Namna za Kuishi na Mpenzi au Mke Anayependa Kuchuna Fedha....

$
0
0
Hizi Hapa Namna za Kuishi na Mpenzi au Mke Anayependa Kuchuna Fedha....
HAPA tunazungumza kuhusu mapenzi kama kawaida yetu. Leo nimekuja na mada ambayo naamini itawagusa wengi. Marafiki zangu, kusaidia katika mapenzi ni jambo zuri tena lenye mantiki sana.
Suala la kusaidiana si la upande mmoja. Linaweza kuwa kwa wote, kwa mwanaume au mwanamke. Ni kati ya nguzo muhimu katika mapenzi, lakini kwa bahati mbaya kuna wale ambao
wamekuwa na tabia ya kupenda sana fedha!

Unajua wenzi wanajuana kulingana na wanavyoishi, hivyo ni rahisi sana kumgundua mwenzako kama anapenda sana fedha au ni kweli ana tatizo linalohitaji msaada wako. Hii ni kasoro, lakini haimaanishi kwamba ndiyo sababu ya kuachana.

Katika mada hii ipo dawa ya namna ya kudumu katika mapenzi motomoto na mwenzi wa aina hii. Imekuwa ni kawaida kumsikia msichana akitamba mbele ya wasichana wenzake kwa kusema: “Mimi nina kibuzi changu bwana kila ninachotaka kinanipa, kinajua kisiponipa nakitosa tu, yaani nakichuna kama sina akili nzuri.”

Umewahi kukutana na maneno ya aina hii? Bila shaka jibu ni ndiyo. Si hivyo tu, wapo wanaume pia ambao ni kero kwa wapenzi wao, yaani wamegeuka wanaume kama mabinti kwa tabia zao za kutegemea kupewa kila kitu na wapenzi wao hata kama wanao uwezo wa kuvipata vitu hivyo kama watajishughulisha.

Ninachotaka kusema leo ni kwamba, mapenzi ya kweli hayana uhusiano wowote na fedha, ukiona mpenzi wako anaweka fedha mbele na ukishindwa kumpatilizia anachokitaka anakasirika, jua penzi lake lina walakini, hakupendi bali anataka kukutumia kisha kukuacha.

Katika mapenzi hatukatai suala la kusaidiana, mpenzi wako akiwa na shida fulani akaomba umsaidie, kama unao uwezo msaidie na kama huna mueleze ukweli kisha muangalie namna nyingine ya kumsaidia.

Itakuwa siyo busara kama utakuwa na tatizo lakini ukaona kwamba ukimweleza mpenzi wako ataona unamchuna. Wapenzi wanaopendana kwa dhati hawachunani bali wanasaidiana na hili ni kwa pande zote mbili.

Kinachokera ni kutoishiwa na matatizo na wakati mwingine unakuta kuchuna kwingine ni kwa mambo ya starehe. Yaani sasa hivi umemuomba mpenzi wako vocha, hajakaa vizuri umemtaka akija akuletee chipsi mayai, baadaye unataka akutoe ‘out’, bila kujali kwamba wakati huo mpenzi wako ana fedha au laah.

Katika mazingira hayo unadhani mpenzi wako atashindwa kukuchoka? Akikuacha kwa sababu hiyo utamlaumu? Kimsingi ukiwa na mpenzi mwenye tabia ya kutaka kukuomba fedha kila wakati tena katika matumizi mengine ambayo siyo ya msingi, mbinu zifuatazo ni muhimu kuzifuata. Twende tukaone.

MWELEZE UKWELI
Kama huna fedha wakati mpenzi wako anakuomba, mueleze wazi kuwa huna na kamwe usijaribu kutoa ahadi ambazo huenda ukashindwa kuzitimiza. Usiwe mtu wa kutoa ahadi za uongo, mara nitakununulia hiki na kile.
Mwanaume hatakiwi afahamike siku ana fedha au hana. Maana kuna wenzangu ambao siku za mishahara wanabadilisha hadi kutembea! Mwanamke akijua hilo naye ataongeza ‘mizinga’ ili afaidi.

JENGENI KUSAIDIANA
Jambo la muhimu ambalo wanaume wengi wanalisahau ni kutokuwafundisha wapenzi wao wajibu wa kutoa. Utakuta kila kitu ananunua yeye, hata nauli ya basi analipa, wakati mpenzi wake ana kazi yake.
Ifike wakati kwa makusudi, mwanaume ampe majukumu ya kufanya mpenzi wake, hiyo itamsaidia mwanamke kujua namna fedha zinavyokuwa hazitoshi na ataweza kubana matumizi.

ACHA UFUJALI
Kuna wanaume wengine tangu wanatongoza wanakuwa ni wafujaji wakubwa wa fedha kwa kutoa ofa na zawadi kibao. Hii inaweza kumjengea imani mpenzi wako kuwa unazo!

Unachotakiwa ni kudhibiti mapema matumizi yako hata kama fedha itakuwepo. Ifahamike kuwa kutoa hakushibishi uhitaji, kadiri unavyotoa ndivyo unavyoongeza mahitaji. Weka maisha yako katikati usijidai tajiri kumbe ni kapuku tu.

BAKI NA HILI
Katika kumalizia niseme tu kwamba, mapenzi si kukomoana, bali kusaidiana. Jenga tabia ya kumsaidia mwenzako ili siku na wewe ukiwa na tatizo akusaidie.

Kitu unachotakiwa kukiepuka ni kuwa tegemezi hadi unakuwa kero. Kumbuka kumpiga mizinga mpenzi wako kila mara kunapunguza mapenzi hivyo epukana na tabia hiyo.
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images