Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Everton Wamefurahia Ukarimu wa Watanzani – Rooney

$
0
0
Timu ya Soka ya Everton inayoshiriki ligi kuu nchini Uiungereza imemaliza ziara yake ya siku mbili nchini Tanzania na kueleza kufurahishwa na namna Watanzania walivyoipokea timu hiyo.

Wayne Rooney (wa tatu kushoto) akiwa na wachezaji wenzake walipokuwa Jijini Dar es Salaam ambapo timu ya Everton ilicheza na timu ya Gor Mahia katika mchezo wa kirafiki ulichezwa katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

Timu ya Everton iliwasili Tanzania siku ya Jumatano wiki hii ambapo juzi ilicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Gor Mahia kutoka Kenya.

“Nimepata uzoefu mpya kwangu kuja hapa (Tanzania) na nina tumaini sasa Makamu wa Rais atakuwa akiishabikia Everton”, alieleza Wayne Rooney kupitia tovuti ya timu hiyo.

Pia katika akaunti yake ya mtandao wa tweeter, Rooney aliwashukuru mashabikji wa Tanzania kwa kuiunga mkono Everton katika mchezo wao wa kirafiki dhidi ya timu ya Gor Mahia kutoka Kenya.

“Great start to the pre-season. Special thanks to the fans supporting us in Tanzania”, aliandika Rooney akitoa shukrani za pekee kwa Mashabiki wa Tanzania.

Kwa upande wa Kocha wa timu hiyo, Ronald Koeman alielezea kufarahia ziara ya kuja Tanzania na zaidi ni kutokana na hali ya urafiki iliyooneshwa na mashabiki wa soka nchini.



Rooney pia aliungana na wachezaji wengine kama Morgan Schneiderlin, Jonjoe Kenny na Kevin Mirallas wa timu hiyo walipata fursa ya kujifunza tamaduni za kimsai, kujifunza kupika chakula cha asili, kutembelea shule yenye wanafunzi wenye mahitaji maalum na pia kufanya mazoezi na timu ya vijana wenye ulemavu wa ngozi (Albino United).

Timu ya soka ya Everton ilifanya ziara nchni Tanzania ambapo ilicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa Mgeni Rasmi, Marais wastaafu, Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Shule 10 Bora Matokeo Kidato cha 6

$
0
0
Matokeo ya kidato cha sita kwa mwaka 2017 yametoka leo Jumamosi, Julai 15 huku shule ya Wasichana ya Feza Girls ikiibuka kinara kwa watahiniwa wake 67 kufaulu kwa kupata daraja la kwanza na la pili.

Shule nyingine zilizoibuka kidedea katika matokeo hayo ni Marian Boys, iliyoshika nafasi ya pili, Kisimiri (Arusha) imeshika nafasi ya tatu na Ahmes (Pwani) imeshika nafasi ya nne.

 Shule nyingine  ni  Marian  Girls (Pwani) iliyoshika nafasi ya tano, Mzumbe (Morogoro) nafasi ya sita, St Marry Mazinde Juu (Tanga) nafasi ya saba, Tabora Boys (Tabora) nafasi ya nane, Feza BOYS (Dar es Salaam) nafasi ya tisa na Kibaha ya Pwani iliyoshika namba kumi.

Breaking News: Matokea Kidato cha 6 Mwaka 2017 Yametoka.....Bofya hapa kuyatazama

USAJILI: Msuva aipatia Yanga Mamilioni ya fedha

$
0
0
Mchezaji wa klabu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania, Simon Msuva sasa yupo tayari kwenda kuanza maisha mapya ya soka la kulipwa nje ya Tanzania na hii ikiwa ni mara yake ya kwanza.

 

Kiungo huyo muhimu wa Yanga SC anakwenda nchini Morocco kujiunga na timu ambayo imeridhia kuwalipa wana jangwani hao kiasi cha dola 80,000 (Sh milioni 177) kwa kandarasi ya miaka mitatu.


Kupatikana kwa fedha hizo kutaifanya klabu hiyo kufanya usajili wa uhakika ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu Tanzania Bara na mashindano ya kimataifa.

Klabu hiyo iliyoshika nafasi ya pili msimu uliopita, imekubali kumlipa Msuva mshahara wa dola 4,000 (takribani Sh milioni 9).

Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa, Msuva ameamua kujiunga na Klabu ya Difaa al Jadida ya Morocco ambayo imekuwa ikimuwania kwa takribani miezi mitatu sasa.

Haya Hapa Matokeo ya Taifa Stars na Rwanda Uwanja wa CCM Kirumba....

$
0
0
Timu ya taifa ya Tanzania ‘Tsifa Stars’ imeshindwa kupata ushindi kwenye mechi yake ya kwanza ya kufuzu fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) itakayofanyika Kenya mwaka 2018.

Stars ilijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kutanguliwa kufungwa goli la mapema dakika ya 17 kipindi cha kwanza na Dominique Nshuti.

Dakika ya 34 Himid Mao Mkami akaisawazishia Stars kwa mkwaju wa penati kufuatia beki wa Rwanda kuushika mpira kwenye penati box wakati akiwa kwenye harakati za kuokoa hatari golini kwao.

Baada Stars kusawazisha bao, wachezaji wa Rwanda mara kadhaa walikua wakitumia mbinu ya kujiangusha ili kupoteza muda. Golikipa wa Rwanda Marcel Nzarora alikua kiongozi kaika zoezi la kuchelewesha muda hadi kupelekea kuoneshwa kadi ya njano.

Kocha wa Stars Salum Mayanga alilazimika kufanya mabadiliko kipindi cha kwanza baada ya beki wake wa kuli Shomari Kapombe kushindwa kuendelea na mchezo baada ya kuumia na kulazimika kupumzishwa. Boniface Maganga aliingia kuchukua nafasi ya Kapombe.

Wakati dakika zikiwa zimekaribia kumalizika, Mayanga alimpumzisha John Bocco na nafasi yake ikachukuliwa na Stamili Mbonde.

Stars itarudiana tena na Rwanda Julai 23, 2017 katika mchezo ambao utaamua ni timu gani itasonga mbele baada ya matokeo ya mwisho ya mchezo huo.

Ruvuma: Mashinji (Katibu Mkuu wa CHADEMA) na Wabunge Wawili, Washikiliwa na Polisi

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Dkt. Vincent Mashinji, Mbunge wa Jimbo la Ndanda Cecil Mwambe ambaye pia ni Mkiti wa Chama Kanda ya Kusini pamoja na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Zubeda Sakuru wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani Mbamba Bay. Wamepelekwa kituoni kuhojiwa ambapo Katibu Mkuu Dkt. Mashinji ametakiwa kueleza kwanini yuko Mbamba Bay na aeleze amekwenda kufanya nini.

Polisi wamemkamata Katibu Mkuu Dkt. Mashinji, Mbunge Mwambe na Mbunge Zubeda baada ya kuvamia kikao cha ndani kilichokuwa kikiendelea mjini hapo ikiwa ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu Dkt. Mashinji kukagua shughuli za chama katika majimbo ya kanda hiyo iliyoanza leo.

Tutaendelea kuwajuza.

*Makene*

Source:Jamii Forums

Channel Ten Lawamani kwa Kumuonyesha Paul Makonda

$
0
0
Channel Ten Lawamani kwa Kumuonyesha Paul Makonda
 Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limesema uamuzi wa pamoja wa kutotangazwa kwa habari zozote zinazomhusu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam bado haujatenguliwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Katibu wa TEF, Neville Meena, amesema licha ya mkuu huyo wa mkoa kutangazwa mara kadhaa na vyombo vya habari, msimamo wa wahariri nchini kutotangaza habari zake bado haujatenguliwa.

Amesema vyombo vya habari vinavyomtangaza Mkuu huyo wa Mkoa kama vile Star TV and Channel ten, vinafanya hivyo kwa kukiuka msimamo wa pamoja ambao ulifikiwa na wahariri, wakiwamo wa vituo hivyo.

“Tunafahamu kuwa Mkuu wa Mkoa huyo ametangazwa zaidi ya mara moja katika kituo cha Channel Ten, mara moja katika tukio la msiba lililorushwa na kituo cha Radio cha  EFM,” amesema Meena.

Amesema TEF haishangazwi na hatua hizo kwa sababu imekuwa ni msimamo wa vyombo vinavyomilikiwa na kampuni ya Sahara media (Star TV na Redio Free Afrika), ingawa wanachokifanya kikapingana na makubaliano ya ushirikiano wa kitaaluma (Professional Solidarity). Amesma uongozi wa TEF unalifanyia kazi suala hilo.

Amesema wameshaanza kuwasiliana na taasisi husika na baada ya hapo itatolewa taarifa rasmi kuhusu matokeo ya mchakato huo.

Meena amewakumbusha wahariri na waandishi wa habari kwamba makubaliano yaliyofikiwa kuhusu suala hili yako palepale hadi uamuzi mwingine utakapotanaghzwa.

“Tunaomba tuendelee kushirikiana katika kulinda uhuru wa taaluma yetu… hatufanyi hivi kwa kumchikia mtu, bali kulinda taaluma,” amesisitiza.

Amesema mtu ambaye amefungiwa kutokutangazwa habari zake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na siyo habari za Mkoa wa Dar es Salaam kama baadhi ya watu wanavyosema.

“Kumfungia Mkuu wa Mkoa haimaanishi kuwa habari zote za mkoa wa Dar es Salaam zisizomhusisha mkuu huyo wa mkoa nazo zimefungiwa. Zitaendelea kutangazwa na kuandikwa kama kawaida,” amefafanua na kuongeza:

“Siyo kweli kwamba kutotangazwa kwa taarifa zinazomhusu Mkuu wa Mkoa ni kutotangazwa kwa habari za Mkoa. Huu ni upotoshaji unaofanywa kwa lengo la kuficha uovu ambao mhusika aliufanya kwa kuvamia chombo cha habari usiku akiwa na silaha.”



Nisha Ampiga Wolper Dongo Kuhusu Serengeti Boy Wake......

$
0
0
Alichokiandika Nisha.

STAA kutoka kiwanda cha filamu Bongo, Salma Jabu almaarufu Nisha Bebe staa, amesema hawezi kutoka na vijana wenye umri mdogo kumzidi (Serengeti Boy) kwa kile alichosema Serengeti ameiachia mbuga.

Walichokijibu mashabiki.

Nisha ambaye yupo kimya kidogo katika muvi kwa vile yuko bize na biashara zake za nguo, alitoa kauli hiyo kupitia mtandao wake wa Instagram bila kumtaja mtu, lakini baadhi ya mashabiki wakatoa maoni yao na kusema hilo ni dongo kwa msanii mwenzake wa Bongo Movie, Jacqueline Wolper ambaye kwa sasa anakula maisha na ‘dogo’ anayejulikana kwa jina la Brown ambaye pia ni mwanamitindo.




Bado haijafahamika na Nisha hajawa wazi kwamba dongo lae amemlenga nani kutupia maneno hayo aliyoyatoa.

Maaskofu Kanisa la Anglikana Wamkataa Askofu Kwangu....

$
0
0
Maaskofu wa Kanisa la Anglikana Jimbo la Tanzania waliokutana kwenye kikao cha Baraza la Maaskofu, wamemkataa Askofu wa Dayosis ya Victoria Nyanza, Boniface Kwangu na kumtaka ajiuzulu kazi hiyo mara moja

Mkutano huo uliofanyika wiki jana mkoani Dodoma chini ya uongozi wa Askofu Mkuu wa Jimbo, Jacob Erasto Chimeledya, ulifikia uamuzi huo baada ya kuwepo kwa mgogoro wa uongozi wa muda mrefu katika dayosis hiyo iliyoko mkoani Mwanza.

Askofu Mkuu, Chimeledya amesema kwamba baraza hilo limefikis uamuzi huo baada ya kulazimika kupiga kura ili kufikia azimio ambapo maaskofu 25 waliunga mkono na maaskofu 3 kupinga.

"Baada ya matokeo hayo ya kura, baraza limenipatia jukumu la kusimamia utekelezaji wa azimio hilo kwa kuandaa ratiba ya kuachia madaraka kwa amani" alithibitisha Askofu Chimeledya.

Apoulizwa kuhusu azimio hilo la maaskofu wenzake, Askofu Kwangu wa DVN alikiri kuwepo kwa azimio hilo lakini akadai kuwa uamuzi wa kujiuzulu atauchukua endapo ataona unafaa. "Mgogoro wenyewe sio mkubwa kihivyo ila nitaangalia na kuamua, sidhani kama kunasababu ya mimi kujiuzulu" alisema Kwangu na kuongeza kuwa wanaompinga ni wakristo wachache pamoja na baadhi ya wachungaji.

Akithibitisha kuwepo kwa azimio hilo, Askofu wa dayosis ya Ruvuma, R. Haule, amesema kuwa mgogoro huo wa DVN unalichafua kanisa la Tanzania na hivyo wamemtaka Kwangu ajiuzulu.
"Tumepiga kura na maamuzi yanamtaka ajiuzulu kwa amani na heshima ili jina la Mungu litukuzwe" alisema Askofu Haule.

Mgogoro huo ambao umelidhoofisha kanisa la DVN limeshika kasi katika siku za karibuni ambapo waumini wa kanisa hilo walimpiga marufuku Askofu huyo kuabudu kwenye kanisa kuu (cathedral) na makanisa mengine kwenye parishi 40 kati ya 47 na pia kumnyang'anya gari moja aina ya Suzuki Vitara.

Kama Wewe Mwanaume Una Tatizo La Kufika Kileleni Haraka Kabla Mpenzi Wako Hajaridhika Soma Hapa

$
0
0
Pre mature ejaculation ni nini?
Hii ni hali ambayo mwanaume anatoa mbegu mapema sana kipindi cha tendo la ndoa na mara nyingi huambatana na kushindwa kumridhisha mpenzi wake.

Tatizo hili limekua likiwapata wanaume wengi na kujisikia aibu mbele za wenzi wao pale wanaposhindwa kuendelea kabisa baada  ya hali hii kutokea.
Kimsingi  mwanaume anatakiwa achukue dakika nne mpaka nane kabla ya kutoa mbegu za kwanza lakini watafiti wanasema tatizo hili hugundukiwa mtu anapotoa mbegu ndani ya dakika moja au kabla ya dakika moja.
Tatizo hili huweza kutokea mara tu baada ya kubalehe,{primary pre mature ejaculation} mda mrefu baada ya kubalehe{secondary PE} au kutokana na aina ya mwanamke uliompata.{situational PE}

Chanzo ni nini?
Tatizo hili halina sababu za kitaalamu zilizofanyiwa utafiti zikakakubalika ila wanasayansi wanaamini sababu zifuatazo zinaweza kua chanzo kikuu cha tatizo hilo.

kupiga punyeto au kujichua; mara nyingi watu wanaopiga punyeto hua wanafanya haraka kwa kujificha ili wasikutwe na mtu. tabiaile ya kulazimisha mbegu zitoke haraka huweza kuleta tatizo hili.

kukaa muda mrefu bila kushiriki tendo la ndoa; kukaa mda mrefu sana bila kushiriki tendo la ndoa husababisha mkusanyiko mkubwa wa mbegu za kiume ambazo zinaleta msisimko mkubwa na ukichelewa sana kushiriki tendo la ndoa zitatoka kwenye ndoto nyevu. kawaida mwanaume anatakiwa ashiriki tendo angalau mara nne kwa wiki.

kuwa na wasiwasi wakati wa tendo la ndoa; mtu akiwa na historia ya kupata  hali hii kabla, hua hajiamini na kua na wasiwasi kwamba litatokea tena na matokeo yake hulipata kweli.

madhara ya dawa zinazofanya kazi kwenye mishipa ya fahamu; baadhi ya dawa za usingizi, mawazo na zingine zinazofanya kazi kwenye mishipa ya fahamu huleta tatizo hili mfano amitriptyline.

kurithi; baadhi ya koo au familia fulani hurithi vimelea vya kua na ugonjwa huu kwa vizazi mbalimbali vya familia husika.

Magonjwa ya mfumo wa uzazi wa mwanaume mfano prostatitis.


Diagnosis{ kuutambua ugonjwa]
Mwanaume yeyote ambaye anatoa mbegu chini ya dakika moja au mbili ni muhanga wa hili tatizo na anatakiwa apewe matibabu.
 

Matibabu

Matibabu ya ugonjwa huu yamegawanyika sehemu kuu mbili kulingana na ukali wa tatizo husika.
Non pharmacological treatment{matibabu yasiyo hitaji dawa}:  matibabu haya hupewa watu ambao wanahimili mpaka dakika tatu bila kutoa mbegu.
Pharmacological treatment{matibabu yanayohusu dawa}: matibabu haya hupewa watu ambao hutoa mbegu ndani ya dakika moja baada ya kuanza kushiriki tendo la ndoa, watu hawa hushauriwa kutumia na mbinu zote mbili za matibabu.


Yafuatayo ni matibabu yasiyohitaji dawa.

Tumia condom:

Condom ni moja ya tiba nzuri ya tatizo hili kwani hufanya kazi kwa kupunguza hisia kali za mapenzi mtu anazozipata pale ambapo hatumii condom.
Kandamiza perineum kwa kidole:Perineum ni eneo kati ya mkundu na korodani, ile sehemu ikikandamizwa na kidole huweza kuzuia kukojoa haraka wakati wa tendo la ndoa.
Punguza wasiwasi: hebu lifikirie tendo hili kama njia ya kujifurahisha sio njia pekee ya kutafuta kutoa mbegu,  hii itakusaidia kuondoa mawazo ya kutafuta mbegu na kuchelewa kumaliza.
Fanya taratibu: picha za ngono zinadanganya sana watu kwamba kulala na mwanamke lazima ufanye kwa haraka haraka kama mbwa. HAPANA; ukifanya taratibu ndio njia nzuri ya kumfikisha mwenzako na wewe kuchelewa kufika kileleni.

Badilisha style:

ile style ya zamani ya kumlalia mwanamke kwa juu{missionary position} inaleta msuguano mkubwa kwenye kichwa cha uuume hivyo itakufanya ufike haraka sana.
Tumia style ya wewe mwanaume kutangulia chini afu mwanamke juu au kulala kwa upande wote mnaangalia upande mmoja hii itakusaidia sana kuchelewa

Toa mawazo kwamba unafanya ngono: hebu jaribu kufikiria mambo mengine ya kikazi au masomo wakati unafanya tendo hilo, hii itakupunguzia hisia kali za mapenzi na kuchelewa kufika.

Fanya na kuacha: hii ni ile hali ya kuzuia msuguano pale unapoona unakaribia kutoa mbegu kwa kama sekundi 30 kisha unaanza upya. Hakikisha haufiki “point of no return”. pointi ambayo huwezi kujizuia tena kumaliza.

Kandamiza sehemu ya shingo la uume: hii sehemu ya shingo ya uume kwa chini ambayo ukiibana itakusaidia kuanza upya tena kihisia. Nimetumia shingo la uume kwasababu najua uume hauna mabega.


Tumia kilevi: unywaji wa pombe mfano bia mbili kwa siku kwa wanaume pombe hupunguza kidogo nguvu ya mishipa ya fahamu na kufanya mtu aliyekunywa kuchelewa sana kufika kileleni, [watu wanaokunywa pombe lazima mtakubaliana na hili] hivyo unaweza kunywa bia, wine au whisky nusu saa kabla ya tendo na kuondoa shida hii.

·    
Matibabu ya kutumia dawa.
hizi hupewa iwapo tatizo lako ni kubwa sana na hizo njia hapo juu zimeshindikana...
1. Serotonin reuptake inhibitors mfano paroxetine na  clomipramine zimefanya kazi nzuri ya kuzuia kufika kileleni haraka..... humezwa saa moja kabla ya tendo la ndoa.[dawa hizi hazipatikani ndani ya nchi hivyo tunaagiza nje, ukihitaji wasiliana nasi kwa namba hapo chini]

2. Anesthetic creams: hii hupakwa kwenye kichwa cha uume saa moja kabla ya tendo la ndoa kuzuia msisimuko na kufanya mwanaume achelewe kufika kileleni wakati wa tendo.[dawa hizi hazipatikani ndani ya nchi hivyo tunaagiza nje kama ukihitaji wasiliana nasi kwa namba hapo chini]

Hiki Ndicho Kinachoitwa Kichaa Cha Mapenzi

$
0
0
Kabla mtu hajaoa au kuolewa , huamini kabisa kwamba, kabla hajafanya mapenzi au tendo la ndoa na mtu anayemwita mpenzi wake, bado hawezi kudai kwamba, huyo mtu ni mpenzi wake na kwajibika kwake kama mpenzi.

Vijana wengi huamini kwamba, baada ya kukutana kimwili, ndipo wanaweza kudai kwamba, hao ni wapenzi wao na kwamba kukutana kimwili, ndiyo mapenzi au kupenda kwenyewe.

Inapotokea wanapokutana huvutiwa na tendo la ndoa, huamini kabisa kwamba, uhusiano nao utakuwa mzuri. Kwao, tendo la ndoa ndio kipimo cha uimara wa uhusiano wao.


Baada ya kufanya mapenzi, wapenzi hao huamini kwamba, sasa wanaweza kujitolea kwenye uhusiano huo na kwamba, wanaweza kuwa na nguvu nao kwa asilimia kubwa.

Suala hili, kuna wataalamu huliita mtego wa kimapenzi. Huitwa hivyo, kwa sababu huwafanya wapenzi kutokuangalia sifa nyingine na badala yake kuweka nguvu kwenye mwili, yaani tendo la ndoa.

Upofu hutokea kutokana na kuzalishwa kwa kemikali nyigi mwilini, zenye kumfanya mtu asiweze kujiuliza kuhusu maeneo mengine ya kimasha ya binadamu, zaidi  ya mwili.

Kinachotokea ni mwili kuvutwa na wale tunaowapenda kwa kuzalisha homoni inayofahamika kama ‘phenylethylamine’ au PEA kwa kifupi.

Kemikali au homoni hii pamoja na nyingine kama vile ‘depomine’ na ‘norepinephrine’ (ambazo huchochea hali za kimwili) na ‘ testosterone’(ambayo huongeza hamu ya kujaamiana), huzalishwa mara baada ya kukutana kimwili.

Baada ya kuzaliswa kwa homoni hizi, akili ya mtu huona mwili tu, yaani mapenzi na siyo sifa nyingine. Hapa ndipo ambapo, mtu hujikuta hawezi kujizuia tena kukutana kimwili na mpenzi wake, mara baada ya kukutana naye mara ya moja.

Baada ya kufanya mapenzi na kufikia kileleni, huzalishwa homoni iitwayo ‘oxytocin’ (ambayo huhusika na mihemiko), homoni hii humfanya mtu kujikuta anapenda kuwa karibu na kujifungamanisha na mtu aliyefanya naye mapenzi. Tunaweza kusema, ukaribu kwa wapenzi wawili huongezeka na unakuwa ni ukaribu wa mwili zaidi.

Kuzalishwa kwa homoni hizi, ni jambo ambalo mtu hawezi kulizuia na huwa linakuja kwa nguvu sana, kiasi kwamba, mtu kuwa kama amepoteza ufahamu wa maeneo mengineyo ya kimaisha isipokuwa mapenzi tu.

Homoni hizi humfanya mtu kuwa na hisia za kuvutiwa na mwingine, uchangamfu, ukaribu, kuvutiwa na hisia za ukamilifu zaidi. Wale waliowahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kabla ya ndoa au wale waliowahi au wanaotoka nje ya ndoa zao kwa kuvutwa kimwili na wapenzi wengine, wanajua inavyokuwa.

Lakini homoni hizi, hatimaye huanza kupungua na mtu huanza kuhisi kwamba alikosea. Huoni tena na huhisi kama ilivyokuwa awali. Sasa haoni kuwa mpenzi wake ni mzuri au anafaa kama iivyokuwa awali. Kwa sababu, homoni zile zimeshuka sana, mwili unakuwa hauna maana tena.

Kwa bahati mbaya  kile kilichokuwa kinaitwa upendo, kilikuwa kimefungiwa kwenye mwili na homoni hizo ambazo kwa sasa hazipo. Hivyo, wapenzi hawana kingine cha kushika ambacho, wataweza kukiita mapenzi.

Unajua sasa ni kwa nini, tangu kale kabisa suala la wachumba kukutana kimwili kabla ya ndoa lilikuwa likipingwa sana? ni kwamba, watu wanapokutana kimwili, uwezo wa kukaguana tabia unakuwa umefungwa kutokana na kufumuka kwa homoni hizi, ambazo hubadili hali ya mtu na hisia zake kwa ujumla.

Kwa nini unadhani watu, hasa wanaume wakishaanza mapenzi ya kimwili na mtu mpya, yaani nyumba ndogo au yeyote, inakuwa rahisi sana kwao kujisahau na kukamatwa? Sababu ni hiyo hiyo, kwamba, uzalishwaji wa homoni hizi huwa ni mkubwa kiasi cha mtu kuamini kwamba, hakuna kingine chene kufurahisha na kuliwaza kama uhusiano huo.

Kumbuka, watu wawili wanapovutana, kwa maneno mengine tunasema kuna kemia kati yao. Hii ina maana kwamba, huwa kuna mabadiliko ya badhi ya homoni kama nilivyosema. Lakini,

wanapokutana, homoni hizi huwa nyingi kiasi cha kufanya upofu wa muda. Unaweza kuwa upofu wa mwezi, mwaka au miaka.

Upofu huu unapmalizika, uhusianao huwa ni wa vurugu tupu, kwa sababu kama nilivyosema awali, hqakuna mahali pengine pa kushika  siyo tabia, mienenfo waa haiba.

Upofu huu unapomalizika, uhusiano huwa ni wa vurugu tupu, kwa sababu kama nilivyosema awali, hakuna mahali pengine pa kushika siyo tabia, mienendo wala haiba.

Inashauriwa kwamba, mtu anapovutiwa na mwingine au watu wanapovutana ni vema wakawa wangalifu sana. kwanza, wajue kwamba, uhusino ambao msingi wake ni miili tu, yaani tendo la ndoa haudumu, kwani homoni zitokanazo na kukutana watu kimwili, hazina maisha, huwa zinaisha haraka.

Lakini pia inashauriwa kwamba, mtu anapoingia kwenye mapenzi ajaribu kushariana au kuukagua moyo wake, akili pamoja na hisia zake. Kuacha tu mabadiliko ya hali ya mwili yakatawala ni kutafuta maumivu.

Hebu jiulize, ni kwa nini mapenzi yanapoanza kwa moto sana, huzimika haraka  au kwa kishindo sana? ni kwa sababu yanajengwa kwenye msingi usioaminika, yaani katika mihemiko na kimapenzi. Penzi linalokua polepole ndilo lenye kushika, kwani halina msingi wa mwili.

Kutana na Maalim Fadhil Rashid Kutoka Komoro ni Mtaalam wa Tiba za Asili......

$
0
0
KUTANA NA MAALIM FADHIL RASHID KUTOKA KOMORO NI MTAALAM WA TIBA ZA ASILI

UNASHIDA NA MCHUMBA UNATATIZO PESA HAIKAI KURUDISHA MUME AU MKE KWA MUDA MFUPI MVUTO WA MAPENZI

MVUTO WA BIASHARA KUMSHIKA MUME AU MKE ASIKUSUMBUE

DAWA YA ( LIMBWATA )KUMTAWALA MPENZI WAKO KWA SABABU MAALUM KUSAFISHA NYOTA ILI UWE NA MUONEKANO

NA PIA ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA MASHARTI

NA KUMILIKI MALI DAWA YA KUONGEZA UUME SAIZ UIPENDAYO

DAWA YA NGUVU ZA KIUME INAPATIKANA PIA ANAYO DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEP KUA NA UMBO BOMBA UMEIBIWA AU KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALI YAKO NDANI YA MASAA 24 ANAFUNGA KESI NA KUPATA HAKI YAKO DAWA YA MVUTO WA BIASHARA KUUZA MALI YAKO KWA HARAKA KUZUIA CHUMA ULETE

NA KUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHA KUTESEKA ACHA KUHANGAIKA MAALIM FADHIL RASHID

YUPO TANZANIA KWA AJIALI YAKO. CALL...+255719362806/
+255763276239/

WhatsApp IMO +255785786436/

JE, Una Tatizo la Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0

JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @220,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @130,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @130,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @130,000/=
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr.
Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no (+255)
0767447444 na 0714335378
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

Ukweli wa Simba Kumnyonyesha Mtoto wa chui Ngorongoro Wajulikana....

$
0
0
SIKU mbili tu baada ya kusambaa mitandaoni kwa picha ya tukio nadra la mama simba kumnyonyesha maziwa kwa upendo mtoto wa chui kwenye Hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha, hatimaye undani wa jambo hilo umepata ufafanuzi wake.

Juzi, habari iliyoambatana na picha ya tukio hilo, ambalo kwa mara ya kwanza lilirushwa na Shirika la Habari Uingereza (BBC), ilitawala katika mitandao mbalimbali ya kijamii na kuibua mjadala. Mtoto wa chui alionekana akimnyonya maziwa mama Simba ambaye naye, alionyesha ukarimu mkubwa kwa kuketi chini pasi na hofu yoyote.

Picha hiyo ilipigwa na Joop Van Der Linde, mgeni aliyekuwa katika eneo la Ndutu Safari Lodge, Tanzania. Aidha, taarifa zilizorushwa na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, zilieleza kuwa simba huyo mwenye miaka mitano amewekewa mfumo wa ufuatiliaji (GPS) katika shingo yake ili kutambua mwenendo wake.

Katika mahojiano na Nipashe, Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Dk. Fredy Manongi, alisema kitendo cha simba huyo aitwaye Nosikitok kukutwa akimnyonyesha mtoto wa chui siyo kitu cha ajabu kwa wataalamu wa masuala ya wanyama kwa sababu hao (simba na chui), wako kwenye jamii moja.

Akieleza zaidi, Dk. Manongi alisema simba na chui si maadui kwa kuwa wako kwenye ikolojia tofauti na huwa hawadhuriani katika harakati za kusaka milo yao.

Alisema wanyama hao ambao walionekana wakinyonyeshana Jumanne (Julai 11, 2017), wana tofauti katika malisho yao na pia namna ya uwindaji, hiyo ikiwa ni sababu mojawapo kubwa ya kutopigana bali kusaidiana.

Akisimulia kuhusu simba huyo, Manongi alisema alizaa mwishoni mwa Juni mwaka huu, lakini inawezekana watoto wake hawapo kwa sasa.

TABIA ZA SIMBA, CHUITaarifa zaidi za kitaalamu zinaeleza kuwa simba na chui ni wanyama walio katika kundi la mamalia, yaani wanyama wanaonyonyesha na wako katika ukoo wa paka na wana maumbile yanayofanana na paka.

Simba ni miongoni mwa jamii ya paka wakubwa, akiwa ni wa pili kwa ukubwa nyuma ya chui.

Chakula cha simba ni nyama kama ilivyo kwa chui na wote wamekuwa wakiwinda wanyama lakini wao kwa wao hawadhuriani.

Simba hutegemea chakula kwa kuwinda wanyama wadogo na hata wakubwa na wakati akiwa mawindoni, huwinda kwa kunyatia na anapokaribia windo lake ndipo huchomoka kwa kasi. Mara nyingi simba jike ndiye muwindaji mzuri kuliko dume.

Watu 8 Wamefariki Katika Mkasa wa Kukanyagana Kiwanjani Nchini Senegal

$
0
0
Duru kutoka Senegal, zinasema kuwa watu wanane wameuwawa katika kisa cha kukanyagana, baada ya vurumai kutokea wakati wa mchuano wa mechi ya kandanda, kwenye mji mkuu wa nchi hiyo, Dakar.

Shirika rasmi la habari la serikali ya nchi hiyo- (APS), linasema kwamba mashabiki wa timu mbili za soka, walikabiliana baada ya mchuano wa soka uliochezewa katika uwanja wa michezo wa Demba Diop stadium, kumalizika.

Ukuta uliporomoka wakati ambapo idadi kubwa ya watu walipokuwa wakiondoka kwa kasi uwanjani.


Idadi kubwa mno ya watu wamejeruhiwa.

Kisa hicho kilitokea wakati wa fainali ya kuwania kombe la ligi kuu nchini humo, kati ya timu ya soka ya Stade de Mbour na Union Sportive Ouakam.

Mapigano yalianza kati ya mashabiki wa timu hizo mbili hasimu, hatua iliyowachochea maafisa wa polisi kuwarushia vitoa machozi. Hatua hiyo ilisababisha taharuki kubwa miongoni mwa mashabiki ambao walianza kukimbia na kusababisha mkanyangano, na kuporomoka kwa ukuta.

Baadhi ya mashabiki walirusha kila aina ya vifaa yakiwemo mawe.

Picha zinazosambazwa mitandaoni, zinaonesha watu wakikurupuka na kujaribu kupanda juu ya ukuta mfupi, huku wakizungukwa na wingu kubwa wa moshi wa vitoa machozi.

Runinga ya taifa ya nchi hiyo, inasema kuwa, magari ya huduma za dharura na vikosi vya zima moto vilifika maeneo ya tukio hilo.


TANZIA: Waziri Mwakyembe afiwa na mkewe

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe amepatwa na msiba wa kufiwa na mke wake Bi. Linah George Mwakyembe usiku wa kuamkia leo.

Bi. Linah alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Agha Khan alipokuwa akipatiwa matibabu hadi umauti  ulipomkuta.

Unamjua Binti Aliyeongoza Matokeo ya Kidato cha Sita?

$
0
0

Sophia Juma, mwanafunzi wa St Marry’s Mazinde Juu ya Tanga ameibuka kidedea katika matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa leo Jumamosi, Julai 15, akishika namba moja kitaifa.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Charles Msonde imeeleza kuwa nafasi ya pili imeshikwa pia na msichana, Agatha Julius Ninga wa Tabora Girls. Wote walikuwa wakichukua masomo ya mchepuo wa Sayansi (PCB).

Filamu ya ‘Kiumeni’ Aliyoshiriki Idris Sultan Yatikisa Tamasha la ZIFF

$
0
0
Filamu ya ‘Kiumeni’ imeendelea kujizolea sifa kila kukicha.


Filamu hiyo ambayo imewakutanisha wastaa wa Bongo kama Idris Sultan, Ernest Napoleon, Muhogo Mchungu, Antu Mandoza, Rashid Matumla na wengine, imetikisa katika tuzo za tamasha la ZIFF linaloendelea huko visiwani Zanzibar kwa kufanya watu walioshiriki kuiandaa kunyakuwa tuzo mbili tofauti.

Tuzo ambazo zimenyakuliwa kupitia filamu ya ‘Kiumeni’ ni muongozaji bora wa filamu, ambaye ameshinda Nicholas Marwa na muandishi bora wa script, ambaye Daniel Manege ameshinda tuzo hiyo kupitia filamu hiyo hiyo.
Wengine walioshinda tuzo hizo za ZIFF ni Ibrahim Osward aliyeshinda tuzo ya muigizaji bora wa kiume, tuzo ya mpiga picha bora na editor bkra imekwenda kwa Kwetu Studio.

Tuzo ya muigizaji bora wa kike imekwenda kwa Hawa aliyetokea kwenye filamu ya T Junction na tuzo ya filamu bora kutoka Tanzania imekwenda kwa T Junction.

Waziri wa Uganda Apongeza Mabasi ya Mwendokasi Dar

$
0
0
WAZIRI wa Nchi anayeshughulikia Uchukuzi nchini Uganda, Bagiire Aggrey Henry, ameusifu Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) kwa namna unavyosaidia kurahisisha huduma ya usafiri jijini Dar es Salaam.

Pongezi hizo alizitoa juzi baada ya kutembelea na kupanda basi la kuanzia Kivukoni hadi Morocco, akisema mradi huo umesaidia kuondoa msongamano wa magari.

Waziri huyo wa Uganda ambaye aliongozana na ujumbe wa Serikali yake kuja nchini kutembelea na kujifunza kuhusu mradi huo, alisema wana mpango wa kuanzisha mfumo kama huo katika jiji la Kampala.“Tumefurahi kuuona mfumo wenu wa mabasi yaendayo haraka unavyofanya kazi. Nasi tukirudi Uganda tutaenda kutekeleza kile tulichokiona,” alisema Bagiire.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Dk. Leonard Chamuriho, alisema mradi wa BRT umekuwa kivutio kikubwa cha wageni, ndiyo maana viongozi hao kutoka Uganda waliomba kuutembelea.

Dk. Chamuriho alitumia fursa hiyo kuwataka wakazi wa jiji la Dar es Salaam na watumiaji wa usafiri huo kuitunza miundombinu yake ili idumu na kuleta manufaa zaidi kwa Watanzania.

Mkurugenzi wa Uendeshaji na Usimamizi wa Miundombinu kutoka Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Mhandisi John Shau, aliwashukuru wageni hao kutoka Uganda kwa kutembelea mradi huo.

Hivi karibuni Jiji la Dar es Salaam kupitia Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka, lilipata tuzo ya mwaka ya usafirishaji endelevu duniani.

GIGY Money Afanya Balaa Kwenye Studio za Wasafi Classic, Rayvany Alazimishwa Kupewa Papa

$
0
0
WASAFI na Gigy money ni marafiki wa karibu, gigy money alishasema live kuwa anamkubali Diamond Platinumz zaidi ya Alikiba.
hivi karibuni gigy alitembelea studio za wasafi na kupost video ikionyesha akienjoy na wasafi, pia video moja ikimuonyesha akimlazimisha rayvany kurekodi nae selfie video huku rayvany akikataa kwa kusema anafamilia.

Video:

Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images