Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Tazama Video Jinsi Joti Alivyozua Valangati la Da Kiboga Ndani ya Bar.......

0
0
Tazama Hapa Chini Video Jinsi Joti Alivyozua Valangati la Da Kiboga Ndani ya Bar.......


Aliyeimba Nitarejea na Diamond Sasa Amekuwa Teja wa Gongo...

0
0
Alikuwa akihojiwa na kipindi cha shilawadu na kukiri sasa amekuwa teja wa gongo akiwa hapo studio na mama yake
Mama yake amesema anampa tabu kwa kuwa ameshindwa kulea mtoto wake na afya yake imedhoofu
Anaomba asaidiwe: Tazama Video:

Usiseme Haiwezekani Sema tu Aliumba Dunia na Maajabu yake...Tazama Huyu

0
0

Bwana Urio hana mikono wala miguu ila amebahatika sana kuwa na vipaji lukuki. Moja ya kazi anazofanya ni kuchora ramani za nyumba.

Bwana Urio alioa mke wa kwanza ambaye alibahatika kupata watoto nae bahati mbaya watoto na mama walifariki ila mwaka jana ameoa tena mpaka sasa bado yuko na mke wake na ana wivu sana na mke wake na anasema anampa style zote za mapenzi kitandani kumridhisha mkewe asichepuke nje.

Bwana Urio anaweza kuimba, anaweza kuchekesha,anaweza kuigiza etc hivi vyote ni vipaji amezaliwa navyo.

Kati ya vitu ambavyo hawezi ni kuomba omba.

Kilichonishangaza zaidi yeye kama mwanaume wa nyumba ana fight kwa sababu ya familia yake ana fight kwa sababu ya mama yake aliye Arusha ana fight kwa ajili ya ndugu zake wengine. Kubwa kuliko amejenga nyumba yake ambayo anaishi na mke wake kifupi tu yeye ni baba mwenyenyumba.

Kutokuwa na mikono haimzuii kutokuwa na simu wala kutuma sms wala kupiga simu kuna uwezo Mungu ameweka kwake kupitia kamkono kadogo ka upande wa kulia. Amesema akikukaba hapo mpaka uite breakdown ndo itakutoa.

Kati ya vitu nina amini tukifika Mbinguni vitakuwepo ni Fimbo za kwenye makalio. Kuna wengi sana tutachapwa malaika fimbo za kutosha kwa sababu tutaanza kusema "Unajua Mungu mimi sikufikia ndoto zangu sababu baba alikufa, sikufanya sababu nilikuwa mfupi, sikufanya hivi kwa sababu kadha wa kadha" ukimaliza kuhadithia Mungu atakuletea akina Urio kama 9 hv ambao hawakuwa na mikono wala miguu ambao wali fight wali fight wakatimiza ndoto zao.

Siku utakayofukuzwa kazi utashangaa kuwa unaweza kuishi bila hiyo kazi, siku utakayoanza kutumia kipaji chako utashangaa kuwa unaweza ishi bila Digrii yako, siku Utakayoanza tumia Ubunifu Kutumia Taaluma yako utagundua kuwa unaweza kuishi bila kutegemea kupandishwa cheo, mengi unayodhani huyawezi ni kwa sababu tu una njiHujui...Mungua mbadala.

Usiseme haiwezekani sema tu aliumba Dunia na Maajabu yake... Wote tuseme AMEN

NOMA...Mwanasiasa Atupiwa Mayai Viza Brazil

0
0
Mwanasiasa mmoja nchini Brazil amewakashifu waandamanaji wa mrengo wa kushoto kwa kuwadhulumu wageni wakati wa harusi yake kufuati familia yake kumuunga mkono Rias Michel Temer.

Maria Victoria Barros, 25, ni mbunge huko Panara na bintiye waziri wa afya nchini Brazil
Mamia ya waandamanaji walikusanyika nje ya kanisa ambapo sherehe zilikuwa zikifanyika siku ya Ijumaa jioni.

Waandamanaji hao walirusha mayai na mwanasiasa huyo akalamizimika kuondoka akitumia gari lisilopenya risasi

Sherehe hiyo ilihuduriwa na wanasiasa wa nchi hiyo, akiwemo babake Ricardo Barros na mamake Cida Barghetti naibu gavana wa Parana.

Takriban wabunge 30 wa nchi hiyo waliakikwa kusafiri kutoka mji mkuu Brasilia kuhudhuria harusi kwenye mji mkuu wa jimbo la Parana Curitiba.

Picha katika mtandao wa You Tube zinaonyesha walinzi walifungua miavuli kuwakinga binti na bwana harusi walipokuwa wakiondoka kanisani.

UGOMVI wa CUF na CHADEMA Hauwezi Kumwacha Mtu Salama..Chama Kingine Chaingilia Kati

0
0
CHAMA Cha ADC kimekitaka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Kutoingilia Mgogoro ulikuwepo Ndani ya Chama cha Wananchi CUF.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Katibu Mkuu wa Chama Hicho Doyo Hassan katika Maandalizi ya kuazimisha Miaka mitano ya kuzaliwa kwa Chama hicho.

Doyo amesema kuwa Chadema kuingilia Mgororo wa CUF kunaweza kuhatarisha amani ya nchi.

"Tumeshuhudia Migogoro mingi ya vyama vya siasa lakini hatujaona kingene kikiingilia Mgogoro wa Chama kingine".

Hata hivyo Doyo ameitaka serikali iviache vyama vya siasa nchini vifanye shughuli zao.

Maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama hicho yatafanyika Tarehe 22 Agosti Mwaka Huu ambapo chama hicho kitakuwa na ziara kwenye asasi za Kiraia, kuwatembea Waginjwa, Wafungwa, Vyuo vikuu na Kutembea Nyerere Foundation ,N.K  na Mwisho kuhitimisha kwenye Ofisi za chama hicho Buguruni Jijini Dar es Salaam.

JE Wewe ni Mpenzi wa Kuvaa Mitumba? Basi Hili Hapa Linakuhusu

0
0
Waziri Kassim Majaliwa amesema safari ya Watanzania kuachana na nguo za mitumba imewadia kutokana na uwepo wa viwanda vya kutengeneza nguo nchini.

Waziri Mkuu alisema hayo jana wakati alipotembelea kiwanda cha nyuzi cha Namera kilichoko Gongo la Mboto na kiwanda cha nguo cha Nida kilichopo Ubungo Dar es Salaam ambapo alidai viwanda vya kutengeneza nguo nchini ni ushahidi tosha kwamba nchi iko njiani kuondokana na matumizi ya nguo za mitumba kwa kuwa nguo nyingi zitakuwa zinatengenezwa nchini, hivyo kupatikana kwa bei nafuu.

Mbali na hilo Waziri Mkuu aliwapa matumaini wakulima wa pamba na kusema hawana sababu ya kwenda kuuza nje ya nchi na badala yake wauze pamba hiyo katika viwanda vya ndani ili vizalishe nguo za kutosha zitakazouzwa nchini kwa gharama nafuu.

“Pamba yote inaweza kuchakatwa nchini, hivyo hakuna haja ya kuiuza nje ya nchi. Natoa wito kwa wakulima wetu wa pamba walime mazao ya kutosha kwa sababu soko la uhakika lipo na hii ndio safari ya mwisho ya mitumba Tanzania" alisema Waziri Mkuu

Mbali na hilo Waziri Mkuu alitoa wito kwa wamiliki wa viwanda vyote nchini kuhakikisha wanatoa kipaumbele cha ajira kwa wananchi waishio katika maeneo ya karibu na viwanda hivyo sambamba na kulipa kodi kwa wakati na kwa viwango sahihi.

Kwa mujibu wa Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alisema kuwa Tanzania imeazimia kufikia mwaka 2018 kuachana na biashara ya kuingiza nguo za mitumba kutoka nje, makubaliano ambayo yalifikiwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

MBWANA Samatta Awapiga Chenga za Mauzi Mabeki wa Ajax na Kutupia Bao....

0
0

Mshambuliaji wa KRC Genk, Mtanzania, Mbwana Samatta akiwatoka wachezaji wa Ajax katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na msimu jana Uwanja wa mazoezi wa The Ajax Future timu hizo zikitoka sare ya 3-3.


Mbwana Samatta alifunga bao moja jana katika sare hiyo

RAIS Kagame Ajitabiria Ushindi Uchaguzi ujao....

0
0

Rais wa Rwanda Paul Kagame tayari anadai kuwa mshindi katika uchaguzi ujao wa Rais utakaofanyika tarahe nne mwezi ujao.

Kagame amewaambia wafuasi wake katika mkutano wa kwanza wa kuanza rasmi kwa kampeni nchini humo kuwa matokeo ya uchaguzi tayari yalijulikana mnamo mwaka 2015 wakati Wanyarwanda waliposhiriki katika kura ya maoni ili bunge kuifanyia katiba mageuzi ya kumruhusu kugombea muhula mwingine.

Kagame amesema wapinzani wake hawawezi kubadilisha mapenzi ya wananchi kuwa yeye ndiye chaguo lao.

Paul Kagame licha ya kuwa anasifiwa kwa kuleta uthabiti katika taifa hilo la takriban watu milioni 12, anashutumiwa na mashirika ya kutetea haki za binadamu kwa kutumia mkono wa chuma kuliongoza taifa na kuwakandamiza wapinzani.

Kitendo cha Heshima na Kishujaa Kilichofanywa na huyu Mwanajeshi wa USA wa Kwetu TZ Wangekiweza?

0
0
Mwanadada mmoja wa Kimarekani aitwae Erin Hester aliyekuwa ndani ya Gari lake aliweza kumuona Mwanajeshi mmoja akifanya Kitendo ambacho ni adimu na nadra sana kukiona kwa Wanajeshi pale ambapo Mwanajeshi huyo aliweza kuonyesha kwamba kweli ' Uanajeshi ' ni zaidi ya ' Nidhamu ' ya kawaida ambayo unaweza kuikuta kwa Raia mwingine yoyote baada ya kuamua kushuka ghafla katika Gari lake tena katika ' Mataa ' huku Mvua kubwa sana ' ikinyesha ' na kuipigia ' Salute ' Gari ambayo ilikuwa imebeba ' Jeneza ' inakwenda ' Kuzika ' huku Yeye akiwa ameloana ' chapachapa '.

Na kilichowashangaza wengi ni kwamba hilo Gari lililobeba ' Jeneza ' lilikuwa ni la Raia tu halafu hata huyo ' Marehemu ' mwenyewe alikuwa hajulikani na huyu ' Askari ' mpiga ' Salute ' wala Ndugu wa ' Marehemu ' nao alikuwa hawajui kitu ambacho kiliwavutia ' Wamarekani ' wengi huko katika mji wa Kentucky na hatimaye kummiminia ' Kongole / Pongezi ' nyingi mno huyu Mwanajeshi / Mjeda.

Swali ni dogo tu je hii nidhamu ' iliyotukuka ' kutoka kwa huyu ' Afande ' wa Kimarekani tunaweza pia ' kuibahatisha ' siku moja kuiona kwa ' Wajeda ' wa Kitanzania hasa hasa katika matukio muhimu ya Gari zilizobeba ' Majeneza ' ya Raia huku ' Bogi / Mvua ' kubwa inanyesha?

Shikamooni ' Maafande / Wajeda ' wote nchini Tanzania hata wale mliopo sasa Sudan na Congo DR.

Endapo utapenda kupata ' uhondo ' kamili wa hii ' Kitu ' ya huyu ' Afande ' wa Kimarekani basi bonyeza hapa chini:


By GENTAMYCINE

NAFUMANIWA na Wanawake Tofauti Kila Siku - Peter Msechu

0
0
Msechu alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha 5 Selekt ambapo alidai licha ya kuwa na mwili mkubwa lakini mwili huo haumsumbui wala kumpa tatizo lolote kama baadhi ya watu wengine wanavyodhani na kusema amekuwa akiupigisha sana mazoezi ndiyo maana yuko fiti.

"Wakati Timbulo anasema mshumaa mambo ya kuachwa mimi na Yakawa yaani na wanawake wengi, mimi nafumaniwa kila siku kwa hiyo mimi na nguvu ya kujitahidi kwenda na mwili wangu huu, mimi nafanya sana mazoezi watu wengine ooh Msechu sijui mnene, mimi wanawake mtaani wanaongozana nasingiziwa kila kukicha watoto eti watoto wangu, kwa hiyo msinichukulie poa niko vizuri kila idara" alisema Msechu

Mbali na hilo Msechu anasema wimbo wake mpya na video yake imempa madeni makubwa kwani pesa zote amekwenda kufanyia video hiyo na kuwataka watu wasiishie tu kutumiana wimbo huo kwenye mitandao bali waangalie kwenye account zake 'You Tube' na kununua wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ambako ameuweka ila kumsaidia kupata fedha za kulipa madeni hayo.

TUHUMA za Pole Pole Kuwanunua Viongozi wa Chadema, Mwenyewe Adai Bado Orodha ni Ndefu Kwa Wanaotaka Kuhamia CCM

0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Humphrey Polepole amesema anayo orodha ndefu ya viongozi wa upinzani wanaotaka kuhamia CCM.

Polepole amesema hayo leo huku akibainisha kuwa orodha hiyo inahusisha wenyeviti, madiwani na wabunge lakini siku nyingi tu alikuwa amewakatalia kuwapokea.

Hata hivyo Polepole amesema kwamba kutokana na kutuhumiwa kuwanunua sasa anafanya kweli, atawachukua mmoja mmoja.

Polepole amesema amemua kuchukua uamuzi huo baada ya Chadema kuonyesha utovu wa nidhamu kwa kudai kuwa madiwani wanaokihama chama hicho wamehongwa na CCM.

“Sasa tutaanza kumchomoa mmoja baada ya mwingine na kwa kutekeleza hilo wiki hii watampokea kiongozi mkubwa wa chama hicho,’’anasema Polepole.

Amebainisha kuwa kama chama kinakuwa na viongozi wanaoweza kuhongwa na wakahongeka basi  chama hicho kitakuwa ni cha hovyo
"Madiwani wamesema wanamuunga mkono John Magufuli, wametoka wenyewe wameanza kusema CCM imewanunua, sasa kwa vile wameanza utovu wa nidhamu nitaanza kumtoa mmoja baada ya mwingine,’’anasema.

Polepople anaongeza kwamba: “Nilikua nakataa kuwapokea ila nina orodha kubwa wapo wenyeviti, wabunge kibao kama vile watu wanaojisaliji kodi ya majengo TRA," amesema.

"Unajua wanasema wanaisoma namba, nawahakikishia baada ya miaka mitano kwa spidi hii iliyoanza nayo CCM namba inayoonekana wakati huu itakuwa haisomeki kabisa, nitafanya shoo ndogo tu kuwachomoa viongozi hao sipendi kwenda kuwachukua wengi sababu nitaonekana kama nawahujumu vile na pia ili upinzani usikose watu angalau wa kuzungumza nao,"amesema

JE Unatamani Kua na Mume Kama Huyu?

0
0
Kwa kawaida kina dada wengi wanajisikia kumpata mume aliobora

Kwa akina dada jeee unafurahia kumpata mtu wa aina hiii au unachukia?

Na jeee wanaume munafurahia hii hali ya kuwasaidia familia zenu au kwenu ni ubwege?

"HII Sasa ni Zaidi ya Hatari"....Be careful

0
0
Ilikuwa yapata mida ya saa kumi na mbili natoka ofisin nimebeba bag langu la laptop....ofsn kwetu ni karibu na chuo fulan cha uhasibu nikawa natembea miguu kwan sijabahatika kupata usafiri....

 Wakati natafakari nikifika nipike nn kwan bado niko "bachelor", njian nikakutana na binti mrembo sana tena sana akawa anatembea anaelekea maeneo ya chuo...

    Bhana eeeh c unajua mtu ukiwa katika harakati za kutafuta mchumba unatupa huku na huku, nikaamua nimpe hi then nikaomba namba ili tuwe tunawasiliana....

    Baada ya muda mawasiliano yalikuwa makubwa sana tena sana akawa anakuja hadi ofsn kwangu......

    Kilichofanya nilete hii mada hapa ndan ni siku huyu binti alipokuja ndan kwangu.....

    Ili ajionyeshe kuwa yeye ni salama i mean kashapima akaja na cheti cha angaza akiwa amekipiga picha kikiwa kwenye cm yake.....hilo suala linitia hofu kidogo kwan sikuamini kama ni kwel au danganya toto...

    Siku hyo alidai anataman kuwa na mm kimapenz...., nashukuru nimepewa uwezo wa kuvumilia nilimkatalia nikamwambia nashukuru yy kapima bt hapaswi kuniamni mm nikamuomba asbh yake tukapime ili wote tuwe na uhakika tufaidi penz letu kwa raha....

    Huwezi amin asbh nikachukua tax nikambeba ili tukapime, tulipofika sehemu husika nikaomba nikamuone doctor then nitamuita......eeeeeeeeeh niliporudi sikumkuta na simu yangu hakupokea tena na sijawah kumuona tena....

    Vijana tuwen makini hii ni zaidi ya hatari kama watu wamefikia kuforge vyeti vya angaza...????

SABABU za Waziri Lukuvi kukesha Ofisini Kwake

0
0

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi usiku wa kuamkia jana alitumia takribani saa 20 kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa tisa usiku kusikiliza wananchi 189 wenye matatizo ya kero za ardhi ofisini kwake.


Kwa taarifa zilizothibitishwa na Ofisa Habari wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Hassan Mabuye amesema Waziri Lukuvi alifanya hivyo baada ya wananchi wenye kero kugoma kutoka ofisini kwake wakitaka hadi kero zao zisikilizwe.


“Wananchi wengi wenye matatizo na kero za ardhi kutoka maeneo ya Bagamoyo, Kibaha, Mkuranga, Kibiti na Dar es Salaam kwa ujumla wametumia fursa hii ya kipekee ya kuonana na waziri mwenye dhamana ya ardhi na kumuelezea kero zao na hatimaye kupatiwa ufumbuzi papo hapo,” amesema Mabuye kwenye mahojiano yake na Gazeti la Habari Leo.


Hata hivyo Mabuye amesema Wananchi hao wamesifu utendaji kazi wa Waziri Lukuvi hususani kwa hatua ya kukutana nao ana kwa ana na kutatua kero zao za ardhi ambazo ni za muda mrefu huku akisema haijawahi kutokea hata siku moja Waziri kukesha ofisini.


Mwanzoni mwezi Juni 2017, Waziri Lukuvi alitoa tangazo la kuwataka wakazi wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, ambao wangependa kumuona, wafike katika ofisi yake ya Kanda ya Dar es Salaam iliyopo ghorofa ya pili, jengo la Wizara ya Ardhi – Magogoni, Kivukoni ili kujiandikisha majina yao, anuani na namba zao za simu.

Ajinyonga kwa kushindwa kurejesha mkopo

0
0

Mkazi mmoja wa mtaa wa Tambukareli, Manispaa ya Shinyanga, Sarah Bundala (55) amekutwa amejinyonga chumbani kwake baada ya kushindwa kufanya marejesho ya mkopo aliokuwa amemdhamini rafiki yake aliyetoroka na pesa, ingawa haijafahamika ni kiasi gani.

Akithibitisha taarifa hizo Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Jumanne Muliro amesema tukio hilo limetokea juzi (Ijumaa Tar 14 Julai) majira ya saa 10:00 jioni.

Kamanda Muliro amesema kabla ya kujinyonga, mama huyo alikuwa na rafiki yake wakihangaika pamoja kutafuta pesa ili apate za kupeleka kwenye marejesho ya mkopo ambao alikuwa amemdhamini rafiki yake aliyetoroka kusikojulikana.

Akielezea tukio hilo, rafiki wa karibu na marehemu, Mariamu Mugaya amesema majira ya saa 8:00 mchana alimwita ili amsindikize kutafuta pesa za kurudisha mkopo, lakini walizunguka bila mafanikio, ndipo akamshauri ampigie simu mumewe amsaidie kiasi hicho cha pesa anachohitaji, lakini akagoma kufanya hivyo.

Baada ya kushauriana mahala pa kupata pesa, lakini wakazikosa, marehemu alimwambia aenda nyumbani, ili yeye akalale kwanza na ikifika majira ya saa 10:00 jioni arudi kumuona na kwamba hata watu wakimuuliza yuko wapi, awaambie amelala nyumbani kwake asiwafiche. Lakini ilipofika muda huo, akapokea taarifa ya kujinyonga kwa rafiki yake.

Chanzo : HabariLeo

DIVA afunguka kuhusu ujauzito wake

0
0

Ni kweli mtangazaji wa kipindi cha Ala Za Roho, Diva The Bawse ni mjamzito? Hilo ndio swali ambalo wengi wamekuwa wakijiuliza tangu Jumamosi hii kutokana na picha ya Ultra Sound iliyokuwa ikisambaa mitandaoni.


Akiongea na Bongo5, mrembo huyo alikataa kuwa si mjamzito na picha inaonekana mitandaoni ni yake kweli ambayo alienda hospitali kuangalia kama ana uvimbe tumboni kutokana na operesheni aliyofanyiwa mwaka juzi.

“Ile ultra sound ni yangu, nilienda check kama nina uvimbe tumboni maana had surgery ya mwaka juzi nikakuta hamna uvimbe and nikasema it catches my soul maana i was worried, sijaandika Im pregnant,” amesema Diva.

“Siwezi kusema I’m a pregnant, i keep it to myself sababu sio vizuri kutangaza hayo mambo mapema mapema, anything can happen lakini nina uwezo wa kuzaa watoto mwisho wa 5,” ameongeza.

Jamani Mwenzenu Demu Wangu ni Mjeuri, Anakiburi na Mkaidi Sana Nimfanyeje?

0
0
Wana Udaku naombeni msaada kwa huyu mdada sijui ata nini nimfanyie anakiburi na mjeuri ajabu akiambiwa tofauti na alivyotegemea ananuna wenda ata asiongee ama kama tunaongea kwa simu anakata na hapokei simu, nikimwambia nitamwacha analia na kulalamika eti nimepata mtu mwingine na ndiyo maana nimeamua kumwachaa,,,, kiukweli mimi ni mwaminifu ila sasa anaifanya niamini msemo ambao mwalimu wangu aliniambia nikiwa form two kwamba kuwa na demu mmoja unatafuta uginjwa wa moyo....kiukweli namppenda san na ndiyo maana sijaribu ata kumchiti ila sasa natamani ata ajikoze mdada mwenye kuhitaji mume tuendelee maana sasa inatosha naumia kiukweli acheni masihara kwa mapenzi yanauma kuliko kuchapwa mboko sure....msaada ata kama kuna mdada ambaye yupo siriasi naomba aje tujenge mahusiano ya kweli mimi naweza kumilikiwa bila ata kusumbua love you wanajamiii mnanielimisha mengi sana!

Waziri Ampa Joto na Kashikashi Mkandarasi wa Barabara, Apewe Miezi Kumi tu Lazivyo...

0
0

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amempa muda wa miezi kumi Mkandarasi wa Kampuni ya CICO anayejenga barabara ya Tabora-Sikonge yenye urefu wa KM 30 kwa kiwango cha lami kukamilisha kazi hiyo.


Prof. Mbarawa ameyasema hayo mkoani Tabora mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo na kuelezea kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wake.


“Nakupa miezi kumi tangu sasa hadi mwezi Mei mwakani uwe umeikabidhi Serikali barabara hii”, amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa ukamilishaji wa barabara hiyo uendane na viwango na ubora vinavyoendana na thamani ya fedha waliyopewa ili barabara hiyo iweze kudumu kwa muda uliopangwa.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mwalimu Queen Mlozi, amemshukuru Waziri Prof. Mbarawa kwa kuufuatilia kwa karibu mradi huo ambao utachochea kasi ya maendeleo mkoani humo.

Mgogoro Kanisa la Anglikana Bado Kitendawili...Sasa Waamua Kugusa Katiba

0
0

Kanisa Anglikana Tanzania linakusudia kufanya mabadiliko ya katiba yake ili kuruhusu kanisa kufanya uwekezaji.


Akizungumza wakati wa ibada iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Albano jijini Dar es Salaam leo, Askofu Mkuu wa kanisa hilo nchini, Dk Jacob Chimeledya amesema lengo la mabadiliko hayo ni kulifanya kanisa kugusa maisha ya watu.


Dk Chimeledya amesema kanisa hilo linaunga mkono jitihada za Rais John Magufuli za kuwainua watu wa chini na kwamba, jambo hilo haliwezi kufanikiwa kama injili haitawafikia.


"Nguvu ya kanisa lazima iguse maisha ya watu wa chini. Tutafanya mabadiliko ya katiba ili kuruhusu uwekezaji ambao tulishaanza kuufanya," amesema Dk Chimeledya.


Askofu Chimeledya amewataka mapadri wa kanisa hilo kufanya jitihada za kuanzisha parokia zingine katika maeneo yao kwa sababu Dayosisi ya Dar es Salaam ina parokia chache ambazo hazifiki 100.

Huwezi Amini..Haki za Binadamu Wadai Taifa liko Katika Kipindi Kigumu

0
0

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) umesema Taifa linapitia kipindi kigumu cha kuminywa kwa haki za binadamu.


Akizungumza leo Jumapili, Julai 16, Mratibu  wa Kitaifa wa mtandao huo, Onesmo Olengurumwa amesema tangu kuanza kwa mwaka huu kuna matukio makubwa 20 ambayo yanaminya haki za binadamu.


Amesema wakuu wa mikoa na wilaya wanakamata watu na kuwaweka mahabusu bila ya makosa.


Olengurumwa amesema hivi sasa mtu akitoa maoni anakamatwa na kufunguliwa mashtaka kitendo ambacho ni uonevu.


Amesema kufanya mikutano ambayo ni haki ya kisiasa inakatazwa bila ya kutolewa sababu za msingi.


Mratibu huyo amesema mtandao unaangalia namna ya kuchukua hatua za kisheria kuhusu uvunjaji wa haki za binadamu unaofanywa na Serikali.


   
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images