Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Mwalimu afumwa akifanya mapenzi na mwanafunzi

$
0
0

Mwalimu Abasi Hussein wa shule ya msingi Mwabomba iliyopo tarafa ya Ngula wilayani Kwimba mkoani Mwanza anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kukutwa darasani akifanya mapenzi na mwanafunzi wa kidato cha nne mwenye umri wa miaka 17.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo mkoani humo na kusema mpaka sasa mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 27 anashikiliwa na jeshi la polisi muda wowote upelelezi ukikamilika mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.

"Babu wa mwanafunzi alipoona mjukuu wake amechelewa kurudi nyumbani alianza kufanya msako alikwenda kwenye shule ya sekondari lakini hakumuona ikabidi aendelee kumtafuta mjukuu wake, ilipofika kwenye muda wa saa sita na kitu alikwenda kwenye shule ya msingi ya Mabomba katika moja ya darasa wakakuta huyo mwanafunzi wa kike akifanya mapenzi na mwalimu mwalimu wa shule hiyo ya msingi ya Mwabomba" alisema RPC Msangi

Msangi aliendelea kuelezea jinsi babu alivyoweza kuwakamata watu hao

"Yule babu alikuwa ameongozana na watu wengine hivyo walipowaona waliwakamata wakaita na watu wengine, baadaye taarifa zilifika kituo cha polisi na polisi walikwenda na kuwakuta watuhumiwa hao kwenye lile darasa hivyo wakawachukua na kuwafikisha kituoni, hivyo mtuhumiwa yupo kituo cha polisi tunaendelea na mahojiano na taratibu nyingine za kiupelelezi zinaendelea ili tuweze kukamilisha upelelezi tuweze kumfikisha mahakamani kujibu tuhuma hizo" alisisitiza Msangi

Mbali na hilo Kamanda Msangi ametoa onyo kwa watu wanaojihusisha na mapenzi na watoto chini ya miaka 17 na kusema huenda awe amekubali mwenyewe hilo ni kosa la ubakaji hivyo amewataka kuacha na kusema kufanya vitendo hivyo ni sawa na kuhitaji kwenda jela miaka 30.

KAMPENI "Magufuli Baki" Yaanzishwa, Mikutano Kufanyika Nchi Nzima

$
0
0

Rais John Pombe Magufuli ameendelea kupongezwa na wananchi pamoja na Taasisi za kiraia mbalimbali kutokana na misimamo yake na kazi kubwa anayoifanya ya kupigania rasilimali za nchi, kwa masilahi ya wanyonge na masikini. 

Pongezi hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti leo, Julai 17, 2017 jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Masjid Ridhwaa, Alhaj Suleiman Seif Nassor na aliyekuwa mgombea wa CCM wa Ubunge Jimbo la Sengerema kupitia kura ya maoni, Laurence Mabawa.

Wakati akizungumza na wanahabari, Alhaj Nassor amesema bodi hiyo imemamua kumpongea Dkt. Magufuli kutokana na kazi nzuri anayofanya tangu alipoingia madarakani.

Kwa upande wake Mabawa, amesema licha ya kumpongeza Rais Magufuli, ameandaa kampeni kabambe inayojulikana kama ‘Magufuli Baki’ inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni kwenye mikoa yote nchini, ambapo kupitia mikutano wananchi wenye nia njema watamuomba rais abaki katika msimamo wake wa kuwatetea wanyonge na masikini. 

“Kampeni ya Magufuli Baki itahusisha mikoa yote ya Tanzania kwa kuwafikia wananchi wakiwemo wanafunzi wa sekondari kwa kufanya mikutano yenye nia njma ya kumwomba Rais abaki kwenye msimamo wake, kampeni hii itawapa fursa wananchi kutoa maoni yao kuhusu utendaji kazi wake iwe kwa kupongeza au kukosoa,” amesema.

Katika hatua nyingine, Mabawa amelaani baadhi ya wanasiasa na wananchi wanaotoa lugha za maudhi na kejeli kwa watu wanaojitokeza hadharani kumpongeza Rais Magufuli na serikali yake.

“Niombe TCRA kuwachukulia hatua kali wote wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuwatolea maneno ya kejeli na kuudhi watu wanaojitokeza kumpongeza Rais,” amesema.

Na Regina Mkonde 

MBUNGE Goodluck Mlinga Azidi Kutetea Diamond Kuchongewa Sanamu la Heshima Aliyoipa Tanzania

$
0
0

Mbunge wa Jimbo la Ulanga, Mh #GoodluckMlinga amezidi kutetea hoja yake ya kuwa wasanii waliofanya vizuri na kuiwakilisha nchi nje vizuri, kupewa heshima kama kujengewa sanamu na baadhi ya mitaa na barabara kupewa majina yao.
.
.
Kipindi cha nyuma Mbunge huyo alisimama Bungeni na kusema kwa namna msanii #DiamondPlatnumz anavyoiwakilisha nchi vizuri kimataifa anastahili kujengewa sanamu, na kupendekeza ikibidi sanamu la askari posta Dar es Salaam liondolewe na kuweka hilo la #Diamond.
.
.
#GoodLuck👉“Na sikumtaja Diamond pekee, niliwataja wasanii wengi kama wakina Mr Nice ambao wameiwakilisha Tanzania sana nje lakini mpaka leo hii wamepotea hawana alama, inakuwa hawawezi kuwahamasisha wasanii wengine, lakini tunapoweka alama kila msanii anapofanya vizuri tunahamasisha wengine na ndiyo utaratibu katika nchi za wenzetu,” ameiambia Habari Xtra ya Times Fm
.
.
Na kuongeza👉“Kuna mchezaji mmoja wa mpira alitoka Kenya (Victor Wanyama) kuja Tanzania siku ya pili alipewa mtaa, sasa vile vitu ndio tunatakiwa tuvifanye kwa wasanii wetu wanaoibeba nchi. Sasa wewe fikiri mtu katoka nje ambaye anawakilisha nchi nyingine tunampa mtaa, lakini kwetu ni msanii gani alishawahi kuacha alama hata akapewa Barabara, hakuna!!!,” .
.
.
JE UNAMUUNGA MKONO MBUNGE HUYU AU UNAMPINGA??

Nigeria: Mwanamke Ajitoa Muhanga na Kuua 8

$
0
0

Mwanamke mmoja nchini Nigeria ameripotiwa kujitoa mhanga kwa kujilipua msikitini kaskazini mwa nchi hiyo.

Ripoti zinaonyesha kuwa watu nane wamefariki huku 18 wakiwa wamejeruhiwa vibaya baada ya mlipuko huo kutokea wakati mwanamke huyo akilazimisha kuingia katika msikiti huo.

Jenerali wa polisi mjini humo amesema kuwa mwanamke huyo amesababisha vifo vya watu wanane mjini Maiduguri.

Maiti na majeruhi zimefikishwa katika hospitali ya taifa.

Hapo awali mlipuko mwingine ulitokea Molai amabapo aliyejitoa mhanaga ndiye aliyepoteza maisha peke yake.

Hata hivyo mpaka sasa hakuna kundi lolote la kigaidi lililotangaza kufanya mashambulizi hayo.Bokoharamu wamekuwa wakifanya mashambulizi kama hayo siku za nyuma.

Hii Inakuhusu Wewe Usiku wa Leo.."Kimbia Mbio zako Binafsi na Watakie Wengine Kila la Kheri"

$
0
0

Leo asubuhi Nilikuwa nafanya mazoezi ya kukimbia, ilikuwa ni asubuhi ya saa kumi na mbili, na ni barabara ambayo sijawahi kufanya joging.

Wakati nikiendelea kukimbia kwa mbele kama nusu Kilometa hivi nikamuona mtu mwingine nae akikimbia. Bila shaka alikua akikimbia taratibu kuliko mimi. Hapo hapo nikajiambia nikimbie mpaka nimfikie na kumpita. Nilikimbia kwa kasi ilimradi tu nimfikie na kumpita.
Baada ya dakika chache nikawa nimebakiwa na kama mita 100 hivi nimfikie, mara akachepuka kushoto mwa barabara. Nikajiambia kuwa nia yangu nataka nimpite hivyo alivochepuka na mimi nikamuungia na kuendelea kumfuata.

Nikiwa nimekaribia kumfikia nikazidisha speed kama Usain Bolt amefikia utepe wa mwisho wa mashindano ya olimpic. Moyoni mwangu nikafarijika sana kumpita, na nilifurahi mno, nisijue kuwa mwenzangu hata hakuwa na wazo kuwa tulikuwa tukishindana. Hili lilikuwa wazo langu binafsi.

Baada ya kumpita na kwenda umbali mrefu kidogo mara nikahisi kama nimepotea na sijui ni wapi ninaelekea. Kuangalia saa ilikuwa ni saa moja na dakika 45 na saa moja kamili nilikuwa na appointment muhimu sana ya pesa. Hivyo ikanibidi kuanza kurudi nilikotoka.
Nikiwa nimepoteza muda na mpaka nafika nyumbani hakukuwa na appointment tena maana nilipoteza muda mwingi. Hivyo na pesa nikaikosa pia.

Haya ndio yanatokea katika maisha yetu ya kila siku pale tunapoweka mashindano na wafanyakazi wenzetu, majirani zetu, marafiki, na familia ili tuwaonyeshe kuwa tuna mafanikio au wa muhimu kuliko wao? Tunatumia nguvu nyingi pamoja na muda mwingi kuwafukuzia na imefika hatua mpaka tukasahau njia zetu.

Tumejisahau kuwa kila mmoja ana mwisho wake wa tofauti. Tatizo la mashindano yasiyo na tija ni kuwa huwa hayana mwisho.
Katika Maisha lazima kutakuwa mtu ambaye yupo juu au mbele yako hata ufanyeje.
Lazima atakuwepo mtu ambaye ana hela kuzidi zako, lazima atakuwepo mtu ambaye ana elimu kukuzidi wewe pamoja na ukoo wenu wote, lazima atakuwepo mtu ambae ana kazi nzuri kuzidi yako, gari zuri kuzidi lako, pesa nyingi Bank kuzidi zako, mke mzuri kuzidi wako, mume mzuri kuzidi wako, watoto wenye tabia nzuri kuzidi wako na kadhalika.

Hata ufanyeje hauwezi kuwa juu au mbele kuliko wote. Lakini kumbuka unaweza kuwa bora sana (the best) kama utaamua kuwa wewe kama wewe. Watu wengine imefika hatua wamekosa hadi raha kwa kuwa wamekua wakiangalia sana majirani zao jinsi wanavyoishi, wanavyokula, magari wanayoendesha, utajiri wao n.k. Shukuru Mungu alichokupa, fanya kazi kwa bidii ukiangalia ni nini mahitaji yako, usinunue kitu ilimradi tu kwa kuwa jirani yako au rafiki yako anacho, kwa kuwa itafika wakati itakibidi uuze vitu ambavyo ni vya muhimu.
Ishi maisha ya furaha, vaa vizuri kula vizuri. Relax hakuna mashindano katika hatima ya mtu.
Alichokupangia Mungu utakipata tu. Hata kicheleweshwe vipi utakipata tu. Vuta subira huku ukijibidiisha.
Kimbia mbio zako binafsi na watakie wengine kila la kheri!

SHARE na Marafiki zako kama Unakubaliana nami

*Your Dream Our Plan*

Kutana na Tabibu wa Tiba za Asili Maalim Issa Najimu Mwenye Uwezo wa Kutibu Magonjwa...

$
0
0
KUTANA NA TABIBU MWENYE KUBRI KUTOKA KWA ALAH MAALIM ISSA NAJIMU.
NI SHARIFU MWENYE UWEZO WA KUBAINI TATIZO LAKO PUNDE TU UNAPO MFANYIA MAWASILIANO KUPITIA WASAA NA SIKU KWA MAWASILIANO:-
MAALIM ISSA NAJIMU KUTOKA MKOA WA TANGA MWAMBONI MAGOFU KATA YA NGUVU MALI NCHINI TANZANIA,

NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA
QUR-AN, DAWA ZA ASILI PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.

ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE / MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-

 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME)
 MIGUU KUWAKA MOTO
 KUTAFSIRI NDOTO
 MFARAKANO WA WANANDOA
 MFARAKANO KAZINI
 KUPANDSHWA CHEO
 KUTOA PETE YA BAHATI
 ANAO UWEZO WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUBASHIRI
 KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA
 KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU
/MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA.
 ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA
KUMUOA AU KUWA NAYE.
 ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA KWA NJIA YA MSUKULE
 ANAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA PYA NDANI SIKU 7 TU.
 MENGINEYO MENGI ZAIDI YALIYO KUWA SUGU

PIGA SIMU-
 Mobile; 0717 70 32 41.
 WhatsApp 06226 535419.

EDWARD Lowassa Aweka Wazi Mikakati yake ya Urais Mwaka 2020

$
0
0
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Lowassa amesema kuwa licha ya kuwa upinzani nchini Tanzania unakumbwa na changamoto nyingi, lakini atagombea tena urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Lowassa amesema kuwa atagombea tena na kwa mapenzi ya Mungu anaamini kuwa atashinda na kuingia Ikulu kwa mikono safi.

Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa Nation Media Group (NMG) jijini Nairobi, Kenya.

“Kwa mapenzi ya Mungu nitajaribu tena mwaka 2020 na nitapita kwa mikono safi,”  alisema Lowassa.

Kwa mwaka 2015, Lowassa aligombea urais kwa tiketi ya CHADEMA akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), alipata kura  6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote halali.

Lowassa alishindwa na Rais Magufuli ambaye alikuwa akipeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) aliyejizolea kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46.

Katika uchaguzi huo uliopita Lowassa aliukosoa na kusema kuwa aliibiwa kura zake. Aidha, alifafanua kuwa, licha ya kuwa uchaguzi huo haukuwa huru na wa haki, bado anamtambua John Pombe Magufuli kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Hata kama Dk Magufuli alichaguliwa katika mfumo usioaminika wa uchaguzi, bado tunamheshimu kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Utendaji wa Rais Magufuli utaamuliwa na watu utakapofika mwisho wa muhula huu mwaka 2020. Bora niwe makini katika hili nisije nikanukuliwa vibaya nikaingia kwenye matatizo nitakaporudi nyumbani,” alisema Lowassa

Kuhusu kuzuiwa kwa mikutano na maandamano ya kisiasa, Lowassa alisema kuwa watakwenda mahakamani kuishtaki serikali kufuatia zuio hilo kwani ni kinyume na sheria. Alisema kuwa, watu zaidi ya milioni 6 walimpigia kura, lakini kitu cha ajabu haruhusiwi hata kwenda kuwashukuru.

“Nilipata kura milioni sita na siwezi kufanya mikutano hata ya kuwashukuru watu kwa kunipigia kura. Hiyo si tu kinyume cha demokrasia, bali si haki.”

Lowassa alikwenda Kenya kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa Waziri wa Usalama, Jenerali Joseph Nkaiser aliyefariki hivi karibuni.

Mbali na siasa za Tanzania, Lowassa aliwasihi wa Kenya kufanya uchaguzi kwa amani na kuepuka vurugu kama za mwaka 2007 ambazo zilipelekea zaidi ya watu 1000 kufariki dunia, huku maelfu wakijeruhiwa pamoja na mali na miundombinu kuharibiwa vibaya.

MSEMAJI wa SIMBA Haji Manara Aponea Tundu la Sindano...Aachiwa Huru

$
0
0
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imefuta adhabu dhidi ya wanafamilia wanne waliofungiwa kushiriki masuala la soka kwa mwaka mmoja.


Wanafamilia hao ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Rukwa, James Mwakwinya; Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Rukwa (RUREFA), Blassy Kiondo; Kaimu Katibu wake, Ayoub Nyaulingo pamoja na Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara.

Haji Manara alitiwa hatiani Aprili 23, mwaka huu kwa makosa ya lugha chafu na za chuki kwa viongozi wa TFF na kupotosha umma dhidi ya kadi njano ya mchezaji Mohammed Fakhi wa Kagera Sugar ambako alifungiwa kushiriki masuala ya mpira kwa mwaka mmoja na faini ya Sh milioni tisa.

Viongozi wa RUREFA walifungiwa kwa mwaka mmoja na faini ya Sh. milioni mbili kwa kila mmoja kwa makosa ya kukiuka maagizo ya viongozi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliyotaka wasitishe mchakato wa uchaguzi mkoa kwa kuwa kulikuwa na rufaa iliyokatwa TFF.

Akizungumza na Wanahabari leo Julai 17, 2017 Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya TFF, Tarimba Abbas, alisema viongozi hao wamesamehewa adhabu zao kwa kuwa waliomba kupitiwa upya kwa mashauri yao na kamati imeona ni bora kuwaachia huru ili kuendeleza masuala ya soka.

“Wapo wengi waliofungiwa wengine maisha na wengine adhabu fupi, msamaha huu ni kwa wale ambao wameomba tu kupitiwa upya kwa adhabu zao, pia milango ipo wazi kwa wengine ambao wanataka kupitiwa kwa mashauri yao, lakini si kwa wale waliopanga matokeo uwanjani,” alisema Tarimba.

Kadhalika, Tarimba aliwaomba viongozi wa TFF kuandaa semina ya Maofisa Habari na Viongozi wa Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ili kuepuka maneno machafu ambayo yanasababisha wao kufungiwa.

“Inaonekana viongozi na Maofisa Habari hawana maneno mazuri ya kuongea na wadau wa soka na ndio maana matatizo ya kufungiwa yanajitokeza mara kwa mara, naamini wakipata semina hiyo itawasaidia kujirekebisha na kupunguza kesi kama hizo,” alisema Tarimba.

Kwa niaba ya TFF, Ofisa Habari wa Shirikisho, Alfred Lucas, wameyapokea mapendekezo hayo kutoka kwa Tarimba na kwamba tutafanyia kazi ili kurekebisha makosa hayo kwa manufaa ya soka la Tanzania.

JESHI la Polisi Laanza Msako wa Wezi wa vifaa vya Magari

$
0
0
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam, LJ Mkondya amesema Jumatatu hii jeshi la polisi limeanzisha operesheni ya kuwakamata wezi wa vifaa vya magari.

RAYVANNY: Fahyma Hawezi Kuchukia, Ni Baada ya Video na Gigy Kusambaa Wakiwa Pozi Tata

$
0
0
Baada ya video yake yenye utata na video vixen Gigy Money kusambaa, msanii wa Bongo Flava Rayvanny amesema Baby Mama wake ‘Fahyma’ hawezi kuchukia.



Mshindi huyo wa tuzo ya BET 2017 akiwa chini ya label ya WCB, ameiambia Times Fm kuwa yeye na mpenzi wake hawachungani, hivyo jambo hilo alilichukulia kawaida.

“Hawezi kuchukia, halafu pia mimi sichungwi am live my life, president of own life, so nobody anaweza akaingilia akasema usifanye hiki, so Fahyma hana noma sometimes anaweza akafanya vitu vyake mimi simuingilii,” amesema Rayvanny.

Kuhusu ukaribu wake na Gigy Money, Rayvanny amesema, “It’s just a joke, Gigy ni mshikaji wangu na ni wa Mbeya pia, namjua before hajanza mbwembwe zake na ni mtu ambaye yupo happy muda wote mimi naona anaenjoy maisha yake”. Rayvanny na Fahyma amejawali mtoto mmoja wa kiume aitwae Jaydan.

ESCROW: Waliochota Kwenye Masandarusi Watajwa, Gari Lililotumika Kubeba ni la Ikulu

$
0
0
ESCROW: Waliochota Kwenye Masandarusi Watajwa, Gari Lililotumika Kubeba ni la Ikulu

VIDEO: Tundu Lissu Ataka Rais Magufuli Asusiwe Kila Mahali na Mataifa Mengine Duniani

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki amefanya mkutano na waandishi wa habari akimtuhumu Magufuli kwa mambo mengi na kutaka asusiwe kila mahali.

Amesema mataifa ya nje yanayompa hela Magufuli yamsusie Magufuli na kutompa pesa za kuikandamiza Tanzania. Kujenga uwanja wa ndege Chato ni kama Mobutu Seseseko alivyojenga kijijini kwao.

Amesema Mwinyi na wengine wanaotaka Magufuli aongoze miaka zaidi ya 10 wanataka Magufuli awe kama rafiki zake Nkurunziza, Kagame na Joseph Kabila na kuita huo ni ujinga. Wanaoshangilia Bombardier hawajui zimenunuliwaje na Magufuli anaendesha nchi kwa misingi ya kikabila na Kifamilia, akimtolea mfano Dotto James Katibu Mkuu wizara ya fedha na Naibu wake ni watoto wa dada alikuwa afisa ngazi za chini wa TANROADS miaka 2 iliyopita na wanaambiana mjomba tununue ndege, tujenge uwanja wa ndege nyumbani na hela zinatoka.

Mmoja wa wanasheria wa wizara mmoja Medad Kalemani na Naibu Waziri nishati na madini hakufukuzwa kwenye skendo ya madini iliyomuondoa Muhongo. Kuingilia uhuru wa mahakama. Anawaambia majaji kwenye mikutano ya hadhara namna ya kutoa hukumu.

Sasa ni mwezi wa 8 mahakama ya Tanzania haina Jaji mkuu ina Kaimu jaji mkuu na hii haijawahi kutokea Magufuli anajiona yeye ndio dola kwenye karne ya 21. Majaji wa mahakama kuu 4 kujiuzulu ndani ya miezi 3 haijawahi kutokea na sababu wala maelezo hayatolewi japo kuna baadhi yao walihusika na Escrow ila haijatolewa sababu

Kama majaji wanalazimishwa kujiuzulu bila maelezo nani yupo salama?
Vyombo vya habari vinavamiwa kwa bunduki na hakuna hatua inayochukuliwa
Tunaposema udikteta ndio huu. Kazi ya kupinga udikteta sio ya CHADEMA tu, ni vyombo vya habari, wafanyakazi wa serikali viongozi wa dini. Kutumia vibaya fedha na rasilimali za taifa.
Source:Jamii Forums

NAFASI za Kazi Zilizotangazwa Leo....

WILL Smith Ndani ya Filamu Mpya ya ‘Aladdin’

$
0
0
Muigizaji kutoka Hollwood – Marekani, Will Smith anatarajiwa kuonekana katika filamu mpya ya ‘Aladdin’ kama Genie.

Filamu hiyo inayotayarishwa chini ya kampuni ya Disney, huku ikitarajiwa kuwakutanisha watu kama Mena Massoud na Naomi Scott ambaye ataigiza kama Princess Jasmine.

Script za ‘Aladdin’ zimeandika na John August na muongozaji wa filamu hiyo ni Guy Richie, Filamu ya ‘Aladdin’ ni moja ya filamu kubwa zaidi tangu mwaka 1992, na imewahi kushinda tuzo ya Academy Awards.

WATU 200 Wakamatwa Kwa Tuhuma za Dawa za Kulevya, Unyang’anyi

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar ES salaam limeendelea kufanya misako na operesheni kali ambapo kuanzia 10/7/2017 mpaka tarde 16/7/2017 limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 200 kwa makosa mbalimbali ya uhalifu.



EBITOKE : Ben Pol Ananipenda Kama Nilivyo

$
0
0
Msanii wa vichekesho Anastazia Kisaveli alimaarufu kama Ebitoke ameweka wazi jambo ambalo anavutiwa zaidi na Ben Pol na kusema ni vile msanii huyo alivyompenda na kumkubali jinsi alivyo.

Ebitoke ambaye inadaiwa anatoka kimapenzi na Ben Pol amesema hayo kupitia kipindi cha Weekend Breakfast cha East Africa Radio kinachoruka kila Jumamosi na kudai Ben Pol hakumtenga wala kumdharau kutokana na kazi yake hiyo bali alimkubali na kumuhakikishia kumpa support katika kazi yake hiyo ili afanikiwe zaidi na zaidi.

"Kuna watu wananitisha kweli wanakuja 'DM' wengine wananitukana, wengine hivi wewe Ebitoke unaweza kuwa na Ben Pol? Hivi mimi wananionaje hawa watu wasinichukulie poa poa.

"Tunachotarajia sasa Ben Pol kwanza lazima anipe 'support' kwa kila kitu nachokifanya na mimi lazima nihakikishe natimiza malengo yangu kwa sababu amesema atanisapoti kuanzia kazi yangu nayofanya mpaka mbeleni kwa hiyo huyo ni mwanaume wa kweli kwangu, ambaye amekubali kazi yangu nayofanya, amenikubali jinsi nilivyo hajanibagua nimefurahi sana aliposema kuwa lazima anipe nguvu kutumiza malengo yangu" alisema Ebitoke

Mbali na hilo Ebitoke anasema kuna mambo mengi yeye na Ben Pol wameyapanga na anaamini kuwa yatatimia mbele ya safari katika maisha yao ya kila siku, ila anasema kaka zake yeye walimjia juu kuona hizo stori za mahusiano na Ben Pol lakini baadaye walielewa kuwa anachofanya ni kutafuta maisha hivyo ilibidi wamuache na kazi yake hiyo ya uigizaji na kuendelea kumpa 'Support'

R Kelly Yamkuta Makubwa 'Atuhumiwa Kwa Kuwanyanyasa Kingono Wanawake

$
0
0

Mwanamuziki wa mtindo wa R&B R Kelly amekana madai kwamba anawazuia wanawake kadhaa katika dhehebu lake analotumia kuwanyanyasa.

Wakili wa mwanamuziki huyo alisema kuwa atatumia kila njia kuhakikisha kuwa wale wanaomtuhumu anawakabili kisheria ili kusafisha jina lake.

Ripoti ya BUzzFeed imemtuhumu mwanamuziki huyo kwa kuwabadili kimawazo wanawake walio karibu naye kwa lengo la kuimarisha usanii wao wa muziki.

Kelly tayari amewahi kukabiliwa na tuhuma za dhulma za kingono lakini hakupatikana na hatia.
Amekana kufanya makosa yoyote.

Ripoti hiyo iliowanukuu wazazi watatu inasema kuwa hawajawasiliana na wanao kwa miezi kadhaa ,na kwamba wanawake hao wote wakiwa na umri wa zaidi ya miaka 18 walikuwa wakidhibitiwa na msanii huyo.

Udhibiti huo unashirikisha chakula wanachokula na nguo wanazovaa ,wakati gani wa kuoga na kulala mbali na kufanya tendo la ngono yote hayo yakirekodiwa na msanii huyo.

Wanachama watatu walio karibu na mwanamuziki huyo pia walihojiwa na kusema kuwa wanawake sita wanaishi katika nyumba zinazosimamiwa na msanii huyo.

Iwapo watavunja sheria, wanasema wanawake hao huadhibiwa kwa kupigwa mbali na kutukanwa na msanii huyo kulingana na ripoti hiyo.

Baadhi ya wazazi wao wameripoti wasiwasi kwa polisi, lakini wanawake hao wanasema kuwa wamekubali kuishi katika nyumba hizo.

Wakili wa msanii huyo Linda Mesch alisema: Robert Kelly ameshangazwa na kukerwa kuhusu madai hayo mapya anayodai kutekeleza.

TRA Yamkana Ngeleja Mchana Kweupe Sakata la fedha za Escrow

$
0
0

Waziri wa Nishati na Madini wa zamani Ngeleja ni mmoja kati ya watu waliopokea mgawo wa fedha zinazodaiwa kuwa zao la kashfa ya Tegeta Escrow, lakini akatangaza kuzirejesha kwa TRA Jumatatu iliyopita.

Februari 2014, Ngeleja ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Sengerema (CCM) aligaiwa Sh. milioni 40.4 na mfanyabiashara maarufu James Rugemalira ambaye mwanzoni mwa mwezi alifikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka 12, yakiwamo ya kughushi na utakatishaji fedha.

Hata hivyo, wakati Ngeleja akithibitisha kwa risiti mbele ya waandishi wa habari kuziingiza fedha hizo katika akaunti ya TRA, mamlaka hiyo imesema haizitambui. TRA imesema haina mpango wowote wa kufuatilia fedha hizo kwa sababu shughuli yake ni kukusanya kodi.

Akizungumza na Nipashe mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma wa TRA, Richard Kayombo alisema mamlaka hiyo inahusika na kuhakikisha serikali inakusanya kodi stahiki na siyo urejeshaji wa fedha za kashfa kama Escrow.

Kayombo alitoa ufafanuzi huo wakati alipoulizwa na Nipashe juu ya utaratibu rasmi uliopo wa urejeshaji wa fedha hizo endapo wanufaika zaidi wa mgawo wa Rugemalira watataka kufuata nyayo za Ngeleja.

Akifafanua zaidi juu ya suala hilo, Kayombo alisema TRA haihusiki na fedha zilizochotwa kwenye akaunti ya Tegeta Escrow kwa kuwa hazikuwa mali yake.

Aidha, Kayombo alisema TRA haiwezi kuzizungumzia fedha hizo kwa kuwa hazijawahi kuwa mali yake na kuelekeza watafutwe wenye fedha hizo kwa ufafanuzi zaidi.

“Fedha za Escrow zinaihusu vipi TRA? Tunawezaje kukaa na kuzungumzia fedha ambazo si zetu?” Alisema Kayombo. “Mimi nashauri watafutwe wenyewe wazungumze kama wanataka kurejesha… siyo sisi.”

Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu aliiambia Nipashe wiki iliyopita kuwa uamuzi wa Ngeleja kupeleka fedha za hizo TRA unazua maswali zaidi kwa kuwa alipewa na Rugemarila, na viongozi wa awamu ya nne ya serikali walisema siyo za umma bali mtu binafsi.

Lakini akizungumza jijini Jumatatu iliyopita Ngeleja alisema amerejesha mgawo huo kwa TRA kwa kuwa pamoja na sababu nyingine, ili kujiweka kando na kashfa.

Alisema aliyetoa mgawo huo ameshakamatwa na Takukuru na ana kesi inayoendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Huku akionyesha stakabadhi ya malipo ya Benki ya CRDB tawi la Tower, Ngeleja alisema pia “nimeamua kurejesha fedha hizi hata kama aliyenipa msaada bado ni mtuhumiwa, kwa vile hajathibitika kupatikana na hatia, kwa sababu sitaki kuwa sehemu ya kashfa au tuhuma hizo.”

“Nimesononeshwa na kufadhaika sana kuona kuwa msaada niliopewa sasa unahusishwa na tuhuma.”

Alisema alipokea mgawo huo Februari 12, 2014 na Januari 15, 2015 alilipa kodi kwa TRA kiasi cha Sh. 13,138,125 ikiwa ni sawa na asilimia 30 ya msaada huo aliopewa.

Hakusema ni kwa nini ulipita muda mrefu kati ya kupokea na malipo ya kodi.

Baada ya Ngeleja kurejesha fedha hizo palikuwa na wito kutoka kwa wanasiasa na wanaharakati waliotaka wote waliopata mgawo huo kurejesha fedha hizo kwa TRA kama alivyofanya waziri huyo wa zamani.

MASHTAKA 12
Rugemalira na mwenzake, mmiliki wa Kampuni ya Pan African Power (PAP), Harbinder Singh Sethi walisomewa mashtaka 12 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Julai 3.

Mashtaka hayo ni pamoja na ya kugushi, utakatishaji fedha na kusababisha hasara ya dola zaMarekani milioni 22.1 na Sh. bilioni 309.4 kwa serikali.

Novemba 26, 2014, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliwasilisha mjini Dodoma ripoti ya uchunguzi wa kashfa Tegeta Escrow ambapo ilisema Sh. bilioni 306 zilichotwa kutoka Benki Kuu kinyume cha sheria.

Mwenyekiti wa kamati hiyo wakati huo, Zitto Kabwe alisoma ripoti na kulithibitishia Bunge kwamba viongozi na wafanyakazi wa Serikali, wafanyabiashara, viongozi na taasisi za dini, mabenki na watu binafsi walihusika katika ufisadi.

Ripoti ya PAC ilianika orodha ya waliopata mgawo huo kuwa mbali na Ngeleja ni aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa zamani, Andrew Chenge ambao kila mmoja alipata Sh. bilioni 1.6.

Wengine ni ofisa katika Ofisi ya Rais wakati huo, Shabani Ngurumo aliyepewa Sh. milioni 80, Jaji wa Mahakama Kuu, Eudes Ruhangisa alipata Sh. milioni 404.25 na aliyekuwa mjumbe wa Bodi ya Shirika la Ugavi wa Umeme (Tanesco), Dk. Enos Bukuku, aliyepewa Sh. milioni 161.7.

Katika ripoti hiyo Waziri wa Nishati na Madini wa serikali ya awamu ya tatu, Daniel Yona, Mbunge wa zamani wa Sumbawanga Mjini, Paul Kimiti, aliyekuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), Emmanuel Ole Naiko na Jaji wa zamani wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Aloisius Mujulizi walitajwa kupatiwa Sh. milioni 40.4 kila mmoja.

Wengine ni ofisa wa TRA, Lucy Apollo Sh. milioni 80.8, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usajili wa Vizazi na Vifo (Rita), Philip Saliboko Sh. milioni 40.2, maaskofu Methodius Kilaini Sh. milioni 80.9 na Eusebius Nzingirwa Sh. milioni 40.4, Padri Alphonce Twimannye Sh. milioni 40.4, maofisa wa Rita Placidus Luoga Sh. milioni 121.2 na Theophil Rugozobwa Sh. milioni 323.4.

BAJETI WIZARA
Mgawo waliopata wabunge, maofisa wa serikali na viongozi wa dini kutoka kwa Rugemalira unatosha bajeti ya mwaka mzima ya miradi ya maendeleo ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Nipashe imegundua.

Katika miaka mitatu iliyopita ya bajeti (2014/15, 2015/16 na 2016/17), wizara hiyo ambayo kwa sasa iko chini ya Waziri Dk. Harrison Mwakyembe, ilitengewa bajeti ya Sh. bilioni tatu kila mwaka, ikiongoza wizara zote 18 kwa kuwa na bajeti ndogo zaidi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati wizara hiyo ikiambulia Sh. bilioni moja (theluthi ya bajeti yake ya maendeleo) hadi inapofika robo tatu ya mwaka wa bajeti katika miaka hiyo mitatu, imebainika Sh. bilioni 4.77 zinazodaiwa zao la kashfa ya uchotwaji wa fedha kwenye akaunti ya Tegeta Escrow walizopatiwa waheshimiwa hao zingetosha kugharamia kikamilifu miradi ya maendeleo ya wizara hiyo kwa mwaka mzima na ‘chenji’
ya Sh. bilioni 1.7 ikabaki.

Katika mwaka uliopita wa fedha, kwa mfano, kati ya Sh. bilioni tatu zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wizara hiyo, ni Sh. bilioni 1.19 tu (asilimia 40) ndizo zilizokuwa zimetolewa hadi Aprili 30, mwaka huu kwa mujibu wa Dk. Mwakyembe.

Chanzo: Nipashe

Hii kali, anayedaiwa kufariki na kuzikwa aibuka msibani

$
0
0

TAHARUKI imeibuka msibani baada ya kijana aliyedaiwa kufariki dunia na kuzikwa, Seif Ramadhan (33), kuibuka wakati ndugu na jamaa zake walipokuwa wakiomboleza msiba wake.

Tukio hilo lilitokea juzi katika Mtaa wa Relini, Kata ya Kizota, Manispaa ya Dodoma.

Akisimulia tukio hilo, mjomba wa Seif aliyejitambulisha kwa jina la Idd Salum, alisema walipokea taarifa ya kifo Jumanne ya wiki iliyopita kutoka kwa rafiki yake aitwaye Seleman Kipusa, maarufu kwa jina la Babeshi, mkazi wa Mtaa wa Kizota.

Alisema kwamba Kipusa alipata taarifa za kifo hicho kutoka kwa rafiki zake Seif waliopo mkoani Morogoro ambako alikuwa akiishi.

“Tulipopata taarifa hizo, tulikubaliana na dada yangu ambaye ni mama wa Seif aitwaye Sarah Michael na kukubaliana mimi niende Morogoro pamoja na rafiki yake aitwaye Mohammed Hamisi ili tukauchukue mwili.

“Tulipofika Morogoro, tulikwenda Kituo Kikuu cha Polisi Morogoro kwa sababu wakati tuko Dodoma, tuliambiwa mwili wa ndugu yetu uliokotwa Stendi ya Msamvu, baada ya kuuawa kwa kipigo.

“Polisi walitwambia twende Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kuangalia miili ya marehemu iliyohifadhiwa huko ambapo tuliukuta mwili wa marehemu ndugu yetu.

“Nilipofunua ule mwili, cha kwanza nilichoangalia ni kovu la kichwani kwani Seif ana kovu na nilipolikuta, nikaangalia urembo aliokuwa ameuweka mkononi, nao nikaukuta na nilipoangalia miguu na mikono, mimi na mwenzangu tukaamini ni mwili wa ndugu yetu.

“Kwa hiyo, niliamua kumpigia simu dada yangu nikamwambia ni kweli mwanae amefariki, hivyo nikamtaka atume fedha za kusafirisha mwili baada ya kuwa tumeufanyia usafi,” alisema Salum.

Kwa upande wake, Sarah, alisema Seif ni mtoto wake wa tano kati ya watoto watano aliozaa.

Pamoja na hayo, alisema kabla ya taarifa hizo, mwanae huyo aliondoka nyumbani Dodoma hivi karibuni na kwenda Dar es Salaam kwa kaka yake aitwaye Chilewa William.

“Imepita kama wiki moja hivi aliponiaga kwamba anakwenda kutafuta maisha Dar es Salaam kwa ndugu yake Chilewa.

“Kwa hiyo, mwili wa marehemu ulipoletwa, tuliukagua na kujiridhisha kuwa alikuwa ni mwanangu kwani alikuwa na alama zote ninazozifahamu.

“Jambo la ajabu ni kwamba baada ya mazishi kufanyika Alhamisi wiki iliyopita, nilipokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kwamba ni Seif na yupo Dar es Saalam.

“Nilishtuka, lakini mwishowe nikawaita baadhi ya ndugu zangu na tulimuuliza maswali mengi na alipotujibu, tulibaki tumeshangaa.

“Sasa basi, tulimtumia nauli na kumtaka arudi nyumbani haraka kwani tulikuwa na msiba wake, jambo ambalo alilifanya na kufika juzi usiku,” alisema Sarah.

MAREHEMU ATINGA NYUMBANI

Akisimulia mkasa huo, Seif alisema baada ya kufika Dar es Salaam, hakwenda kwa kaka yake moja kwa moja, bali alianza kuishi mitaani akitafuta namna ya kuanza maisha.

“Nilipofika Dar es Salaam, sikwenda kwa kaka, lakini baada ya maisha kuwa magumu, nilikwenda kwa ndugu yangu huyo, aneo la Kisanga, Wazo.

“Nilipofika kwa kaka, wanaonifahamu walikimbia kwa sababu walidhani mimi ni msukule kwani walijua nimeshafariki.

“Lakini, kuna dada mmoja anaitwa Chiku ni jirani yake kaka, huyo alikuwa mvumilivu kwa sababu alinifuata na kuniambia wana taarifa nimefariki na hata kaka yangu amekwenda kwenye msiba wangu Dodoma.

“Kauli ile ya Chiku ilinitisha sana, nikabaki nashangaa, lakini wakati naongea naye, alikuwa amejaa hofu ingawa nilimwambia asinikimbie kama wenzake,” alisema Seif.

Kutokana na hali hiyo, alisema alimuomba Chiku atumie simu yake kuwasiliana na mama yake Dodoma, jambo ambalo lilimtisha sana mama yake.

“Mama alishtuka, aliniuliza maswali mengi na baadaye akampa siku kaka yangu Chilewa, naye akashangaa, hapo hapo nikagundua ni kweli nimezushiwa kifo.

“Ili waridhike kwamba ni mimi, walinitumia nauli ya Sh. 40,000 ili nisafiri kurudi Dodoma, Jumapili. Nilipofika nyumbani majira ya saa tatu usiku, nilikuta watu wengi sana sijawahi kuona.

“Wengine walikuwa wakinipa pole, wengine walikuwa wakilia na wengine walikuwa wakinishikashika utadhani wameona kitu cha ajabu,” alisema Seif.



DIWANI AZUNGUMZA

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kizota, Jamal Yaled (Chadema), alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kusema limewashtua wananchi wa kata yake.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Relini Kizota, Omary Bangababu (Chadema), alisema tukio hilo ni kati ya matukio yaliyowahi kuwatisha wananchi.

CHID Benz Ampa Makavu Godzilla

$
0
0

Rapa Chid Benz amemtaka Rapa Godzillah kupunguza maneno yasiyo ya msingi kwenye nyimbo zake na badala yake afanye muziki mwepesi utakao burudisha watu na siyo kuandika kizungu kingi kinachompotezea mashabiki.

Chid amesema kwamba Godzillah alikuwa muandishi mzuri wakati anaingia kwenye game lakini kwa sasa amekuwa muandishi anayeandika vitu vingi kupitiliza kitu ambacho kinamfanya aonekane kama mtu asiyejua anataka nini kwenye uandishi wake.

"Godzilla ni muandishi mzuri sana, nyimbo zake alikuwa anajua kipi aandike kipi aache lakini siku hizi amekuwa anaandika kupita kiasi hadi kuonekana kama mtu aliyechanganyikiwa. Namshauri mdogo wangu afanye muziki mwepesi ambao kama ule alioanza nao kwani alijipatia mashabiki wengi. Pia aachane na hayo makundi ya watu wanaoimba kingereza halafu lugha yenyewe hawaijui hii inamuharibia sana", amesema Chid Benz

Vile vile Chid ameongeza kwamba "Godzilla sasa hivi nyimbo zake za zina maneno mengi kiasi kwamba unaweza kuimba halafu ukasahau mwanzo ulikuwa unaimba nini".

Kwa upande wa Wakazi na Billnass, Chid amewataka wasanii hao wapige kazi na kuachana na Godzilla kwani amekuwa mzungumzaji kuliko vitendo.

"Wakazi nawasiliana naye sana, nilimwambia fanya kazi achana na Godzilla anayezungumza maneno 1000 kwa dakika lakini pia Billnass nimemwambia afanye muziki wake tena awe anajisifia ndio atapata mashabiki na kufika mbali sana" Chid aliongeza.

Hivi karibuni kumekuwepo na bifu linalomuhusisha msanii Godzilla pamoja na Wakazi huku msanii Billnass akitajwa kama mtu anayempatia Zilla changamoto katika muziki wake.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images