Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

MREMBO Gigy Money Akiri Kumnyatia/kummendea Kimapenzi Diamond Platnumz....Afunguka Kila Kitu Hapa

0
0
Kupitia Uheard leo July 18, 2017 imemfikia hii mtangazaji Soudy Brown kuhusu Gigy Money kudaiwa kumtaka boss wa WCB, Diamond Platnumz baada ya video na Picha zao wakiwa pamoja zikionekana kwenye mitandao ya kijamii kwa kasi.

Soudy amemtafuta Gigy Money ambaye amedai kuwa watu wasubiri kwanza hayupo tayari kutoa siri kwani ni ya mtu mmoja huku akisema kumpenda mtu nikawaida na yeye yupo serious…

“Mimi nipo serious kabisa kawaida kumpenda mtu akikubali kuwa mateka anatekwa kwani shilingi ngapi..? najua anafamilia kabisa kawaida tu mahusiano yake nt ayaharibu vipi mbona yanaonekana kama yameshaharibika?


“Wangapi wanaonekana kama washapita tu, yeye mwenyewe mbona yupo tayari sema ntakuwa kama nakupa exclusive tulieni siri ya mtu mmoja nikikupa wewe kuna siri” – Gigy Money
Sikiliza Hapa Chini:

VIDEO: Taarifa Mpya Kuhusu Watoto Majeruhi wa Ajali Arusha

0
0
Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ambaye anaratibu mchakato mzima wa matibabu ya Watoto watatu Nchini Marekani, waliojeruhiwa katika ajali ya Basi la Shule ya Lucky Vincent ya Arusha iliyoua wanafunzi 32, kwa kushirikiana na Serikali ya Mkoa huo amesema hali za watoto hao zimeimarika na kwamba Wanatarajiwa kurejea nchini Tarehe 18/8/2017 siku ya Ijumaa majira ya saa tatu Asubuhi katika Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Kuhusu kama watoto hao mpaka sasa watakuwa wameelezwa chcochote kuhusu ajali iliyowakuta, Nyalandu amelijibu swali hilo

KIMENUKA...Kuanzia Sasa Wanaotoa Siri za Serikali Mtandaoni Kutupwa Jela

0
0
SERIKALI imetoa onyo kwa watumishi wa umma wanaotoa siri za serikali na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii kuwa watachukuliwa hatua za kisheria.

Onyo hilo lilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki (pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa watumishi wa umma wa Manispaa ya Ubungo.

Kairuki alisema mtumishi wa umma atayejihusisha na usambazaji wa taarifa za serikali, atachukuliwa hatua za kisheria ikiwamo kufikishwa mahakamani na kupewa kifungo cha miaka 20 jela. Alisema serikali ina utaratibu wake wa kutoa taarifa kwa umma ikiwa ni pamoja na kupitia machapisho yake kwa jamii.

SOMA Nafasi za Kazi Mpya Zilizotangazwa Leo

0
0

Kutana na Tabibu wa Tiba za Asili Maalim Issa Najimu Mwenye Uwezo wa Kutibu Magonjwa....

0
0
KUTANA NA TABIBU MWENYE KUBRI KUTOKA KWA ALAH MAALIM ISSA NAJIMU.
NI SHARIFU MWENYE UWEZO WA KUBAINI TATIZO LAKO PUNDE TU UNAPO MFANYIA MAWASILIANO KUPITIA WASAA NA SIKU KWA MAWASILIANO:-
MAALIM ISSA NAJIMU KUTOKA MKOA WA TANGA MWAMBONI MAGOFU KATA YA NGUVU MALI NCHINI TANZANIA,

NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA
QUR-AN, DAWA ZA ASILI PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.

ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE / MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-


  • ULIJALI (NGUVU ZA KIUME) 
  • MIGUU KUWAKA MOTO 
  • KUTAFSIRI NDOTO 
  • MFARAKANO WA WANANDOA 
  • MFARAKANO KAZINI 
  • KUPANDSHWA CHEO 
  • KUTOA PETE YA BAHATI 
  • ANAO UWEZO WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUBASHIRI 
  • KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA 
  • KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU 
  • MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA. 
  • ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE. 
  • ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA KWA NJIA YA MSUKULE 
  • ANAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA PYA NDANI SIKU 7 TU. 
  • MENGINEYO MENGI ZAIDI YALIYO KUWA SUGU


PIGA SIMU-
 Mobile; 0717 70 32 41. 
 WhatsApp 06226 535419.

MDAU Amshukia Tundu Lissu Kwa Kauli yake Kuwa RAIS Anaongoza Nchi Kwa Upendeleo wa Kifamilia, Kikabila, na Kikanda!!

0
0
Honestly speaking, I real appreciate Ngosha's administration by 100% irrespective to his weakness he has. Additionally, regardless of my little knowledge I have about politics, politicians, and with the support from the preceding governments after that of the founding father of this nation, the late Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, now, I can see a green light coming again for this country under Magufuli's era.

While some people, more specifically the opposition leaders still ignore Magufuli administration plans and efforts on creating a new bright, and strong Tanzania economically, it is now a time for other Tanzanians to support and encourage our president to keep it up, and of course, we will, regardless of what other say. Moreover, the situation which we reached as a nation, it was obvious that we wanted Magufuli's approach to move this country a step ahead. Furthermore, in order to reach our national economic strategic ambition of 2025, we wanted a creative, strong and practically-oriented leadership style, that set the plans and start implementing them rather than that which end by politicizing them only, of which Magufuli leadership style deserve those credits.

As I'm enjoying to see what I wanted to be done in Tanzania, much is needed to support our president on moving this country ahead. Normally, a good and wise human character, appreciate nice stuffs those that are done by a leader, and provide constructive critics without, tamper, haterate, despising, disrespect etc on some issues seems to be not correct, of which Ubuntu has to be applied on them. Besides, being an opposition leader, does not mean that you opposite each and every what the ruling government do. On top of that you as a leader, you can oppose each and everything, but we, as the mere citizens, we truly see, and we know, what our innermost heart tell us about our President Maguli's ambitions to this country.

It is my time now to ask politicians of this country, and more specifically opposition leader, of whom Tundu Lisu is my prime target, and I have some few questions here:

1) will you teach us to see what Magufuli administration is doing?; 

2) do you think that we do not know where we came from, where are we now, and where are we heading?; 

3) do you think that we do not know where did you mess up, after all your efforts you devoted on building your political part, and the you fallen in a graving trap in 2015, because of greedy of securing Magogoni by shortcut? Now you see, the way you messed up, we had a trust in you, but you ended by lying us; 

4) Why are you denying yourself? what you wanted to be done in this country, such as curbing corruption, we have now and we are still seeing Ngosha's success on this, can you ignore this achievement?, 

and 5) why are you now coming with simple, and lower-minded arguments against our president? I can see now you are talking about tribalism, religious sentiments, ukanda, and dictatorship, this click in my mind and tell me that no more ufisadi in this country as you used to see. No matter which tribal, religion, and zone background any leader is coming from, for me if he or she is qualified for serving this nation, let them do their best in bringing development in this nation.

Sometimes, professionalism is blinded by politics, and this what is happening with Tundu Lisu. Matokeo ya kukosa nini wasimamie kwa sasa kama chama, maana ajenda kuu waliizika 2015, saizi imebaki kuvizia tu. Na haya ndiyo matokeo ya kutaka kuingia ikulu kwa shortcut unaacha misimamo au misingi yenu kama chama, mlioijenga kwa miongo mingi. Watu wanapo mess up, wanakuja na simple justification za siasa hazina adui wa kudumu au rafika wa kudumu, lakini implication zake ni kubwa sana. This is what they are reaping now. Unajua sisi wa tz ni waongeaji sana, bila vitendo, now we have a man who speak and do it practically, what else do we what?. Jamaa hawa hawa, walimtukana sana JK kuwa ni dhaifu, TZ kuna ombwe la Uongozi, rushwa zilizokithiri, and I agree with them, but now, Ngosha has curbed all these malicious stamping blocks in our development.

Finally, may God almighty be with our president Dr John Joseph Pombe Magufuli in all his every steps to move this country ahead, give him wisdom strength to lead this nation.

God Bless Africa, Tanzania, and our president Dr John Joseph Pombe Magufuli.

Best,
A mere citizen with no any post in government, but I will keep on supporting and advising him in his plans and effort on leading this nation .


By Keju/JF

TANZIA...Jaji Ambaye Rais Magufuli Aliridhia Ombi Lake la Kujiuzulu Afariki Dunia

0
0

Aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ambaye amejiuzulu  hivi karibuni, Upendo Msuya amefariki leo Julai 19 baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa kiharusi.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu, mjomba wa marehemu, Niva Mbaga amesema kwamba marehemu amefariki akiwa Hospitali ya Kairuki alipokuwa amelazwa.

Amesema kwamba shughuli za mazishi zinafanyika nyumbani kwa marehemu Tegeta jijini Dar es Salaam.

“Amesumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kiharusi hivyo akawa anapelekwa hospitali na kurudi nyumbani zaidi ya miezi mitatu sasa na leo hii amefariki dunia’’ amesema Mbaga

Amesema marehemu ameacha watoto wanne.

KIMENUKA..Mchungaji Mwingira Ashtakiwa Kwa Kudaiwa Kuzini na Kuzaa na Mke wa Raia wa Marekani

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeombwa kumwamuru Mchungaji Josephat Mwingira akapime kipimo cha kubaini vinasaba (DNA) ili kujua baba halali wa mtoto anayedaiwa kuzaa na Dk. Phillis Nyimbi ambaye ni mke wa Dk. William Morris.

Maombi hayo yamewasilishwa mahakamani hapo, Dar es salaam jana na Dk. Morris kupitia wakili wake, Respicius Ishengoma.

Dk. Morris ambaye ni raia wa Marekani, alifungua kesi katika mahakama hiyo akimtuhumu Mchungaji Mwingira kuzini na kuzaa na mke wake Dk. Nyimbi.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakili Ishengoma aliwasilisha maombi hayo akitaka mteja wake, Dk. Morris na mkewe Dk. Nyimbi, Mchungaji Mwingira na mtoto aliyezaliwa, wakapime kipimo hicho ili kujua baba halali wa mtoto huyo mwenye umri miaka tisa sasa.

Katika maombi hayo namba 113/2017, Dk. Morris anaomba mahakama itoe amri wahusika wote wakapime DNA.

Baada ya kuwasilisha maombi hayo, mahakama imeyapokea na kutoa siku 14 kwa Mwingira kuyajibu kisha usikilizwaji uanze na kutolewa uamuzi. Mwingira atajibu Agosti 2,mwaka huu.

Katika kesi ya msingi namba 306/2013, Dk. Morris amewashtaki Mwingira na Dk. Nyimbi, na anadai alipwe fidia ya Sh bilioni 7.5 kwa mchungaji huyo kuzini na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mkewe.

Chanzo: Mtanzania

Mghwira: Lowassa Kuhamia Chadema Ufisadi wa Kisiasa

0
0
Moto wa Uchaguzi Mkuu wa 2015 ulishazimika lakini kuna kila dalili kwamba majivu yake bado hayajapoa na moja ya dalili za kuwapo kwa hali ya uvuguvugu ni kauli ya hivi karibuni ya Anna Mghwira dhidi ya Edward Lowassa kwamba njia aliyotumia kugombea urais ilikuwa ni aina nyingine ya ufisadi.

Katika uchaguzi huo, Mghwira ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, alikuwa mwanamke pekee aliyegombea urais na kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), alishika nafasi ya tatu nyuma ya Lowassa akipata kura 98,763 sawa na asilimia 0.65 ya kura zote.

Lowassa,  aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika Serikali ya Awamu ya Nne, katika uchaguzi huo aliwania kiti hicho kupitia Chadema akiungwa mkono na vyama vilivyoungana chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa)na alipata kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote. Dk John Magufuli aliibuka mshindi kwa kupata kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46.

Juni 3, Mghwira aliteuliwa na Rais Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro wakati huo akiwa mwenyekiti wa ACT –Wazalendo na muda mfupi baadaye chama hicho kikamuondoa katika nafasi hiyo kutokana na uteuzi huo.

Katika mahojiano maalumu na gazeti hili wiki hii, Mghwira alisema njia aliyoitumia Lowassa kugombea urais ilikuwa ni aina nyingine ya ufisadi wa kisiasa kwa kuwa hakupitishwa na chombo chochote ndani ya chama chake.

Alidai kuwa hata katika kampeni, Ukawa haukuzungumzia ajenda ya ufisadi baada ya waziri mkuu huyo wa zamani kujiunga Chadema.

“Kwenye kampeni 2015 chama kikuu cha upinzani (Chadema) hakikuwa kinazungumzia tena ufisadi labda kwa hofu kwamba mshutumiwa mmojawapo wa ufisadi ndio alikuwa mgombea wao. Kwa bahati mbaya ni wao walioibua tuhuma hizo za ufisadi. Lakini kuondoka Dk Slaa (Wilbroad aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema) nako kulileta tatizo ambalo watu hawakutaka kulifuatilia.

“Ni tatizo watu walitakiwa kuuliza alikuwa (Dk Slaa) na sababu ya msingi ya kuondoka? Ameondoka kwa nini? Anaenda wapi na anaenda kufanya nini. Ilikuwa ni ajabu kwamba kiongozi ambaye unataka uje kuwa mfano wa demokrasia, unaingia kugombea nafasi kubwa kama hiyo ya urais bila kuchaguliwa na chombo chochote cha chama,” alisema.

Mghwira aliendelea kujiuliza maswali kuhusu hatua hiyo ya Lowassa, “Umeingiaje? Inatokeaje?” Kisha alihitimisha, “Hiyo ni aina nyingine tena ya ufisadi wa kisiasa. Lowassa kama anataka kujisafisha vizuri kisiasa aangalie sana angeweza kufika mbali kama angetumia njia sahihi.”

Mghwira ambaye ni kiongozi wa kwanza wa upinzani kushika wadhifa wa ukuu wa mkoa tangu kurejea kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992, alisema, “Njia iliyotumiwa na Chadema si tu kwamba inarudisha nyuma siasa zetu lakini haikutoa picha nzuri ya uwepo wa demokrasia ndani ya upinzani. Hili lilikuwa doa kubwa kwa Mzee Lowassa.”

Uteuzi wa Lowassa kugombea urais kupitia Ukawa ulishuhudia Dk Slaa aliyetajwa sana wakati huo kuwa mgombea wa nafasi hiyo , akijiuzulu siasa na kwenda kuishi nje ya nchi.

Mbali na Dk Slaa, aliyekuwa mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba naye aliamua kuikimbia CUF aliyokuwa mwenyekiti wake kabla ya kurejea baadaye na kutambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa jambo lililozua mgogoro mkubwa ndani ya chama hicho hadi sasa.

Alikerwa kuvuliwa uenyekiti

Katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Shanty Town mjini Moshi, Mghwira alikumbuka karaha aliyoipata baada ya furaha ya kuaminiwa na Rais na kupewa wadhifa huo.

Alisema kama si ubabaishaji wa kisiasa Tanzania, asingeondolewa kwenye uenyekiti wa ACT-Wazalendo.

“Changamoto niliyokutana nayo ACT-Wazalendo kama mwenyekiti ni kukosa wigo sahihi wa kisiasa kwa sababu kama tungekuwa tunafanya siasa sahihi, nisingeondolewa uenyekiti,” alisema.

Mghwira alisema, “Naapishwa tu kuwa RC (mkuu wa mkoa) kesho yake naondolewa tena tukiwa tumepanga kukutana kwenye kikao na mpaka leo hatujawahi kukutana.

“Nimesoma kwenye magazeti kuwa mrithi wa Mghwira kutembelea mikoa saba, yaani na mrithi ameshapatikana. Hizo si siasa, huo ni ubabaishaji. Ubabaishaji wa kisiasa Tanzania ni tatizo,” alisema.

Aliongeza, “Sisi kina mama tukisimama imara tunaweza kuondoa dhana hii ya siasa za ubabaishaji. Ni siasa za kipuuzi kabisa. Mmekubaliana mkutane muongee, hamuongei wenzako wanakaa pembeni. Umechaguliwa na mkutano mkuu unaondolewa na kamati ndogo. Watu 370 karibu 400 hivi walikuchagua, siku ya kuondolewa unaondolewa na watu watatu au wawili au mmoja. Hiyo si siasa ni dalili tosha kuwa hakuna siasa.”

Alisema mbaya zaidi ni kuwa watu wanaokuondoa hawakutumwa na mkutano mkuu, wala hawakukaimishwa na kamati kuu.

Hakuna upinzani nchini

Baada ya kujumuisha yote hayo na hasa alivyotimuliwa kwenye uongozi, mkuu huyo wa mkoa akawa na jibu moja kuhusu siasa za upinzani, “Hakuna siasa za upinzani, bali zilizopo ni za kurudishana nyuma maendeleo.

“Siasa ni kitu kizuri kwa maana ya ile mijadala, kubadilishana mawazo na kuzungumzia masuala ya itikadi, mipango ya kijamii... hakuna hiki kitu Tanzania.”

Badala yake alisema, “Tumeweka siasa kama ni uhasama kati ya chama tawala kilichoshinda kihalali na vyama hivi vingine. Kila siku watu wanatafuta makosa ya wenzao (Serikali) hata kama inafanya vizuri. Hiyo sio siasa.

“Vyama vya upinzani hapa hatuendeshi siasa. Awali, chama chochote kitakachoibuka na siasa inayoeleweka kinaweza kutawala nchi hii kwa miaka 100 ilimradi tu kitoke na siasa inayoeleweka.”

Mghwira alisema, “Vikitokea vyama vitatu vinaendesha siasa inayoeleweka tunakuwa mahali pazuri zaidi. Kwa maana kwamba wale wakiongea jambo lao, hata kama hawatawali, mtawala asikie na kuthamini.

“Sisi hapa Tanzania kuna aina ya siasa za kudidimizana. Kwa sisi wanawake wanaharakati tunaziita PhD (pool her down). Unavutwa tu chini hutakiwi kukua. Nchi haiwezi kwenda kwa staili hii.”

Alisisitiza, “Kuna watu wanafikiri kwamba ili kitu kiwe sahihi ni lazima wao wakifanye (upinzani) lakini kikifanywa na watu wengine hakiko sahihi. Hiyo ni kutokuwa mwanasiasa. Kuwa mwanasiasa si kugombana ni kuwa na uwezo wa kujenga hoja, kuitetea na kuisimamia. Mwenzako akija na hoja kubwa zaidi kubali.”

Changamoto za ugombea urais

Mghwira alisema wakati akigombea urais alikumbana na changamoto mbili, moja ikiwa ni ya nchi na nyingine ni ya yeye kutojiandaa kugombea.

“Changamoto zangu binafsi sizijali sana kwa sababu sikuwa nimejiandaa kugombea urais. Ingawa sikushinda urais, lakini nilishinda hatua ya kushiriki kwenye kampeni. Nilishinda ndiyo maana hata Rais Magufuli ameona na akaniteua kuwa RC. Kushinda kwenye kampeni ni kushiriki na kutoka ukiwa umewaachia watu kitu.

“Nafikiri nimeacha hicho kitu. Kila mtu ana ushindi wa viwango vyake. Yeye (Rais Magufuli) alishinda ushindi halisi wa kura na nafasi lakini hajanyima nafasi, amegawa,” alisema na kuongeza kuwa kinachobaki ni kushirikiana ili kuijenga nchi.

“Kuna watu wanasema nilishindwa, sikushindwa kwa sababu sikuenda kushinda, bali nilienda kushiriki. Uchaguzi unashiriki kwanza, ukishashiriki wananchi ndio wanaamua nani ni mshindi.

“Kura zikishahesabiwa na akapatikana mshindi, mnarudi kuijenga nchi. Kuna wapinzani wa Magufuli ndani ya chama chake, nao wamo kwenye Serikali na tuko nao pamoja. Hao ni wabaya zaidi kuliko mimi kwa sababu mimi namkubali kwa asilimia 100 wao wanamkubali sehemu kwa sababu wanatoka chama kimoja. Wanajua mambo yao ndani ya chama yalikuwaje,” alisema.

Alisema wanaotoka upinzani wanaweza kuwa na ufanisi mzuri na uhusiano mzuri zaidi wa kikazi na Rais kwa sababu hawana masilahi ya kisiasa.

“Sina masilahi ya kisiasa CCM ila ACT-Wazalendo. Kama nina masilahi ya kisiasa kwenye chama changu hicho hakimdhuru yeye wala hakiharibu kazi yangu huku kwa sababu mimi na yeye tunahusiana kikazi tu,” alisisitiza.

ACT-Wazalendo ni CCM B?

Alipoulizwa kuhusu dhana iliyoanza kujengeka kuwa huenda ACT-Wazalendo ni tawi la CCM na ndiyo maana Rais ameteua wanachama wake wawili kushika nyadhifa kubwa serikalini alisema hilo si kweli.

Alisema katika kuunda Serikali ya mseto, ukitaka kwenda vizuri huchukui sana wale watu mnaopingana mno kwa kuwa mtapingana tu kila siku.

“Lazima uchukue watu ambao mnaendana katika utendaji kazi. Hata ACT-Wazalendo sidhani ana maanisha atachukua kila mtu...”

Mbali na Mghwira, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa mshauri wa chama hicho, Profesa Kitilla Mkumbo kuwa katibu mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Uteuzi ambao uliibua mijadala katika mitandao ya kijamii baadhi wakipongeza na wengine wakishutumu, huku baadhi ya wana-CCM wakinuna.


Install App Namba Moja Tanzania Kwa Habari za Udaku na Mengine.....Udaku Special App

0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

GOOD News..Mtandao Waitangaza Tanzania Nchi Bora Kwa Utalii Afrika

0
0
Wakati idadi ya watu maarufu kutoka nje ya nchi wanaokuja kutazama vivutio vya utalii nchini ikiongezeka, mtandao wa   kimataifa wa kibiashara umeitangaza Tanzania kuwa nchi ya kwanza Afrika inayowavutia zaidi watalii.

Mtandao huo, SafariBookings.com ulifanya uchambuzi kwa kuchukua maoni ya watalii zaidi ya 2,500 waliotembelea nchi za Afrika na idadi kubwa waliitaja Tanzania kuwa bora kuliko nchi nyingine.

Hii ni mara ya pili kwa mtandao huo wa Marekani  kuitaja Tanzania kama nchi ya kwanza inayowavutia zaidi watalii. Mara ya kwanza ilikuwa 2013.

Sifa kubwa iliyoipa hadhi ya juu Tanzania ni kuwa na eneo kubwa lenye wanyamapori na misitu. Nchi nyingine zilizoshika nafasi ya juu ni Zambia na Kenya.

 Wakati mtandao huo ukiitaja Tanzania kuwa eneo bora la utalii, watu maarufu kutoka mataifa makubwa duniani wameendelea kumiminika nchini wakitembelea  hifadhi za Taifa na vivutio vingine.

 Miongoni mwa watu maarufu waliotembelea vivutio hivyo ni pamoja na mwanamuziki wa Marekani, Usher Raymond na mcheza soka maarufu David Beckham aliyewahi kuchezea timu ya Taifa ya England na timu za Manchester United na Real Madrid.

Mara baada ya kutembelea vivutio hivyo, Usher aliweka picha za ‘matanuzi’ aliyopata akiwa Tanzania, katika mitandao yake ya kijamii ya Twitter na Instagram.

Usher alikuwa ameongozana na familia yake wakiwamo watoto wake wawili wa kiume katika Hifadhi ya Serengeti.

“Safari hii imekuwa ya maajabu, tumefurahi sana kuona uzuri wa mbuga hii nikiwa na familia yangu,” ameandika katika ukurasa wake wa Twitter.

Si hao tu, watu wengine maarufu waliofika ni mcheza filamu wa Marekani, Will Smith na familia yake na mchezaji wa zamani wa timu ya Liverpool, Mamadou Sakho.

Pia, mchezaji wa Everton Morgan Schneiderlin alitembelea vivutio hivyo hivi karibuni akiwa fungate.

Wiki hii, msanii maarufu wa filamu za Bolywood, India, Sanjay Dutt naye aliwasili kwa ajili ya kutembelea vivutio hivyo.

Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) limesema kazi kubwa inayofanywa na shirika hilo kutangaza vivutio vya utalii duniani ndiyo iliyozaa matunda hayo.

Msemaji wa Tanapa, Paschal Shelutete alisema lengo lao ni kufikia watalii milioni tatu ifikapo mwaka 2020. Alisisitiza kwamba Tanapa inatathmini namna ya kuwatumia watu mashuhuri wanaotembelea nchini kujitangaza zaidi kimataifa ili kufikia lengo hilo.

Alipoulizwa namna wanavyoitumia fursa ya watu hao mashuhuri kutembelea nchi, Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Phillip Chitaunga alisema,  “Hili ni jambo ambalo kwetu tunalichukulia kwa mapana yake kwa sasa.”

Akizungumzia vivutio vilivyopo nchini, mwandishi wa habari za usafiri na utalii wa Marekani, Tim Bewer alisema, “Tanzania ina Mbuga nyingi nzuri kama Serengeti na Ngorongoro, wanyama watano bora, simba wapandao miti, kikubwa ni ubora wa hifadhi hizo ambazo zimetumia robo tatu ya ardhi yake kuhifadhi wanyamapori.”

Pia, mtaalamu wa masuala ya safari na utalii na raia wa Uingereza, Phillip Biggs amekaririwa na jarida mtandao la Huffpost akisema, “Hakuna majadiliano, hakuna nchi ya Afrika, kusema ukweli, yenye wanyama wakubwa katika eneo kubwa kama Tanzania.”

SERIKALI ya Nigeria Yaingia Katika Mgogoro Mkubwa na Wasanii...Yaamuru Mr Peter Okoye wa P Square Akamatwe Haraka

0
0
Serikali ya Nigeria imeagiza police kumkamata Peter Okoye "P-Square" baada ya kuwakoromea na kuwafumua viongozi wa serikali Kwa kuwaita "mad and stupid" baada ya serikali kutoa azimio la kupiga marufuku wasanii wote wa Filamu na muziki kushuti kazi zao nje ya Nigeria

Uamuzi ambao umepingwa vikali na asilimia 99% ya wasanii wa nchi hiyo kwa kusema iweje wao wapiganie tasnia hizo kwa shida kubwa kwa miaka mingi bila support ya serikali na Sasa serikali hiyo hiyo inakuja kibabe kupitisha Sheria zisizo rafiki bila hata kuwashirikisha wasanii wenyewe
Sehemu ya andiko la serikali ya Nigeria ikionyesha ubabe flani inasema.....
"We urge the security agencies in the country to arrest Mr Peter Okoye for disrespecting our government and bringing it to a disrepute. If you cannot produce in Nigeria and hire Nigerians, then leave the industry. We must export Nigerian culture to the outside world through our music and videos" .

RAY C Atangaza Kuhitaji Mpenzi Mwenye Miaka 60

0
0

Msanii Ray C amesema  sasa hana muda tena wa kuhangaika na vijana katika mapenzi na kudai anatafuta mzee wa miaka 60 atulie naye.

Ray C amesema hayo jana kupitia kipindi cha NIRVANA wakati akihojiwa na Deogratius Kithama na kusema sasa anatafuta mzee kuanzia miaka 60 ndiyo anaweza kuwa naye kwenye mahusiano na kusema muda wa kucheza na vijana kwake umeshapita.

"Nimeshakuwa sana katika mahusiano na vijana naona hakuna jipya sasa nimeamua kutoka huko na kutafuta mtu mzima angalau miaka hamsini hivi, tena hata huyo naona bado kijana bora awe na miaka sitini hivi nitulie naye, hawa vijana wameshanichosha mimi" alisema Ray C

Mbali na hilo Ray C alizungumzia juu ya jaribio lake la miaka ya nyuma kutaka kubadili kifua chake na kusema ni kweli alitaka kufanya hivyo kwani anaamini kila binadamu kuna kitu anaweza kutaka kukifanya vile ambavyo yeye anapenda kiwe, japo jambo hilo hakuweza kulifanya.

RAIS Magufuli Ametupunguzia Kazi 2020: UVCCM

0
0

Umoja  wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umesema kuwa kazi kubwa inayofanywa kwa sasa na Rais Dk. John Magufuli, imeipunguzia kazi CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Kwamba Watanzania wamekuwa wakivutiwa na utendaji kazi wa kiongozi huyo wa nchi ikiwamo kusimamia rasilimali za nchi.

Kauli hiyo imetolewa jana wilayani Uvinza mkoani hapa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka, alipokuwa akizungumza na wana-CCM kwenye mkutano wa ndani uliofanyika katika kata za Kazuramimba na Nguruka.

Alisema kwa sasa njia imekuwa nyeupe kuelekea mwaka 2020 kwani kazi kubwa inayofanywa na Rais Magufuli ni kielelezo tosha kwa kiongozi huyo kuwa anastahili kupewa nchi na kuongoza kwa awamu ya pili.

Shaka aliwataka wanachama wa CCM kutobweteka na uhakika huo na badala yake wajitume kwa bidii, kufanya kazi ya kisiasa kisayansi na kizalendo kama njia ya kuwatumikia Watanzania wote.

“Utendaji wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli katika kipindi kifupi, kwa hakika umewakosha Watanzania pamoja na kuitikisa dunia na kwa sasa wanyonge nao wanajiona wana thamani na hadhi katika nchi yao.

“Dk. Magufuli ametupunguzia hekaheka na kazi nzito ya kusaka kura za ushindi wa mwaka 2020, hata viongozi na wanachama wa CCM tusibweteke na kujiamini, wajibu wetu ni kufanya kazi na kuwatumikia wananchi,” alisema.

Aidha Shaka alivichambua vyama vya upinzani na kusema vingine ni mabaki ya ukoloni mamboleo katika ardhi ya Tanzania.

Alisema vyama hivyo vimekuwa vikiongozwa na wanasiasa uchwara waliojitahidi kwa miaka mingi kuvipinga vyama vya TANU, ASP na Serikali baada ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 na Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Shaka alisema kwa sasa upinzani uliokuwapo nchini hauna lolote zaidi ya kupoteza muda kutokana na vyama hivyo kurithi sera na mipango ileile ya wakoloni na Sultan kwa kuwagawa wananchi.

RAPA Chemical Aachana na Utomboy na Sasa Kawa Beyonce

0
0
Mwana dada chemical asiyekuwa na mpinzani kunako ulingo wa hip hop kwa upande wa kina dada tanzania ameamuwa kutoka kwenye utomboy na sasa amekuwa na muonekano wa beyonce. Inasemekana baada ya msanii mwenzake "stereo" ambaye anahit na wimbo wake wa "mpe habari" kumtoa bikra aliyokuwa akidai kuwa nayo sasa amebadilika kabisa kimuonekano. Kweli dudu haijamuwacha mwanadada chemical salama!

50 Cent Atamba Kumfunika Jay Z Mwishoni mwa Mwaka na Albam Mpya

0
0
Baada ya kuikosoa vikali albam ya Jay Z ‘4:44’, 50 Cent ametangaza kuonesha mfano kwa vitendo kwa kuachia albam mpya mwishoni mwa mwaka huu akitamba kuwa itaipiku ya Jigga.

Kiongozi huyo wa G-Unit ambaye hajaachia albam rasmi tangu mwaka 2014 alipoachia ‘Animal Ambition’, amedai kuwa albam hiyo itakuwa na ladha bora zaidi na inayowapa shangwe mashabiki tofauti ya 4:44 ambayo alidai ina lugha ya kisomi na kwamba ni muziki wa kwenye uwanja wa golf.

Wakati 50 Cent anaichana 4:44, Jigga ameendelea kuweka rekodi kubwa na albam hiyo akifika mauzo ya ‘Platinum’ ndani ya wiki chache.

“Nina albam ambayo nilikuwa nasubiri kuiachia,” 50 alifunguka kwenye kipindi cha Access Hollywood Live.

“Itatoka mwishoni mwa mwaka huu. Haitakuwa ‘smart’ kama ya Jay Z. Nataka kufanya muziki ambao watu wakiusikiliza wanapata shangwe. Huwezi kuupata haraka hadi ukae chini uchambue,” alitamba.

Ingawa 50 Cent hakuweka wazi jina la albam hiyo, huenda ikawa ni ‘Street Kings Immortal’ (SKI), jina la mradi aliowahi kuupigia debe tangu mwaka 2012.

Mwaka jana Fiddy aliwahi kusema kwenye moja kati ya mahojiano yake kuwa hawezi kufanya mradi mwingine kabla hajaachia SKI.

JIBU la Aika (Navy Kenzo) kuhusu Jux na Vanessa Mdee kuachana

0
0
Msanii wa Bongo Flava kutoka kundi la Navy Kenzo, Aika amepata kigugumizi kuzungumzia taarifa za Jux na Vanessa Mdee kuachana.


Muimbaji huyu ambaye amekuwa rafiki wa karibu wa couple hiyo, alipoulizwa na 5 Sekt ya EATV alijibu, “sidhani kama hilo ni swali ambalo naweza kulijibu, wale ni wapenzi wana-relationship yao, mimi hainihusu kabisa ila naheshimu maamuzi yao,” amesema Aika.

Katika hatua nyingine Aika ametoboa siri ya uhusiano wake na Nahreel kudumu kwa muda mrefu, “sisi tuko real ikitokea kitu kwa siku moja ikavuma inakuwa ndio hivyo lakini tunajua jinsi ya kutatua matatizo yetu, tunajua jinsi ya kutulizana ikitokea tatizo, tunajua jinsi ya kuongea na kuhakikisha vitu kama watu wazima vinaishia ndani ya nyumba,” amemaliza kwa kusema.

LULU Michael Afunguka ya Moyoni Kuhusu Dr. Cheni

0
0

Mwigizaji staa wa Tanzania Elizabeth Michael maarufu Lulu leo July 19 ametumia Instagram yake kumuandikia salamu za upendo na shukrani Mwigizaji wa siku nyingi Dr.Cheni ambae leo ni kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa.

Lulu aliandika “Happy Birthday Baba…! Asante Kwa Kuwa Baba Mlezi Kwa Miaka Yote Tangu Uliponijua…..Asante Kwa Kuwa Mtu Wa Kwanza Uliyekiona Na Kukiamini Kipaji Changu Na Kuhakikisha Hakiishii Kwenye Macho yako Tu….Ninaweza Kusema Mpaka Hapa Nilipofika Kuna Mchango Wako Mkubwa sana…Mbali Na Wakati Wa Furaha Hujawahi Kuniacha Wala Kunikana Katika Shida Na Hata Aibu Zangu…..Sidhani Kama Kuna Kitu Naweza Kukulipa Wewe na Familia Yako Zaidi ya Kumuomba Mungu Aendelee Kuwatunza❤️Unapoongeza Mwaka Mwingine Mungu wangu Ninayemuamini Akakuongeze Katika Kila Eneo…..Afya,Uzima,Maarifa,Uchumi na Akakutane Na Haja Zoooote Za Moyo Wako. @drchenitz @drchenitz @drchenitz”

MKURUGENZI wa Star TV Aburuzwa Mahakamani

0
0

ANTONY Diallo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sahara Media Group (SMG), inayomiliki kituo cha televisheni Star TV, Redio Free Africa (RFA) na Kiss FM anatarajiwa kupandishwa kizimbani kwa kushindwa kulipa wafanyakazi mishahara

Diallo atafikishwa katika Mahakama Kuu kanda ya Mwanza kwa kushindwa kuwalipa mishahara wafanyakazi wake 20 kiasi cha zaidi ya Sh. 100 milioni ikiwa ni malimbikizo ya kipindi cha miezi 16 sawa na mwaka mmoja na nusu.

Mahakama hiyo inatarajiwa kusikiliza mashauri 15 yote yakiwa ni ya kudai malimbikizo ya mishahara ambayo yatasikilizwa Julai 21 mwaka huu, ambayo tayari Tume ya Utumishi na Usuluhishi ulimuagiza Diallo kuwalipa lakini hakufanya hivyo.

Julai 13 mwaka huu, kampuni ya Diallo, ilifungwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kushindwa kulipa kodi ya Sh. 4.5 bilioni ambapo tayari wiki moja imekatika na taarifa zinadai hajalipa hata senti moja.

Katika hatua hiyo kampuni ilipewa siku 14 (wiki mbili) kuanzia Julai 13 mwaka huu, iwe imelipa kiasi hicho cha fedha na kama haitafanya hivyo majengo ya kampuni hiyo yanaweza kupigwa mnada ili kufidia deni hilo.

Diallo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza, anadaiwa kiasi hicho cha fedha za malimbikizo ya kodi ya kipindi cha awali huku kipindi cha miaka miwili 2016/17.

Mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo (jina linahifadhiwa) aliueleza Mtandao huu kuwa wamelazimika kumfikisha Mahakama Kuu baada ya kushindwa kutekeleza makubaliano yao, yaliotolewa na Tume ya Utumishi na Usuluhishi (CMA).

Mtoaji taarifa huyo ameeleza kwamba wanataka kuiomba mahakama kuagiza mara moja walipwe fedha zao mara moja na kwamba kama Diallo hana fedha pia Mahakama iangize wauze vitu vyake ili walipwe stahiki zao.

Amesema kuwa, kiongozi huyo ambaye alishawahi kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji na baadae Waziri wa Maliasili na Utalii, amekuwa akiwatishia maisha kitendo kilichowalazimu wakaitafute haki yao mahakamani.

“Yeye amekuwa na dharau na kiburi kwa wafanyakazi wake na watu wengine, ndiyo maana hata kampuni yake ilifungiwa na TRA baada ya kupewa mwaka mmoja awe amelipa madeni yake lakini akafanya kiburi mpaka akafungiwa,” amesema mfanyakazi huyo.

Hata hivyo, alidai kwamba kitendo hicho cha kutolipwa mishahara kilisababisha baadhi ya wafanyakazi kupoteza maisha yao kwa msongo wa mawazo kutokana na kutengemewa na familia zao.

“Wanaolipwa pale mishahara ni wanawake tu, tena wale ambao hawana sifa lakini sisi wenye uwezo wa kufanya kazi hatulipwi mishahara yetu na tukihoji tunaonekana ni wachochezi, hali hii imetuchosha,” amesema.

Pia amedai kumekuwa na udanganyifu mkubwa unaofanywa na mwajiri kwa kutokupeleka michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii PPF/NSSF na hata inayopelekwa imekuwa na taarifa za uongo ambayo michango inayowasilishwa hailingani na mishahara ya wafanyakazi.

Taarifa nyingine kutoka ndani ya kampuni hiyo zinaeleza kwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imempunguzia masharti Diallo, badala ya kulipa deni la Sh. 4.5 bilioni, alipe Sh. Bilioni 2 ili wafunguwe kampuni hiyo lakini na yenyewe ameshindwa kulipa.

Kwa upande wake, Diallo, amekiri kuwepo na wafanyakazi wanaomdai lakini alidai hawazidi wawili huku akishindwa kuweka wazi kiasi wanachomdai.

SIMON Msuva Bye Bye Yanga

0
0

Baada ya tetesi za kuondoka Yanga kuzagaa, hatimaye mshambuliaji wa klabu ya Yanga Simon Msuva amethibitisha taarifa zake za kuondoka na kuelekea nchini Morroco kujiunga na klabu ya Difaa Al Jadida ambayo ni washindi wa pili wa ligi kuu Morroco.

Msuva amesema amefuata taratibu zote ambapo viongozi wote wa pande mbili wameafikiana na kufanya biashara, na anaamini ipo siku atarudi kuitumikia Yanga tena ila mpaka nitimize malengo yangu ya kucheza soka la kulipwa Ulaya.

"Kila kitu kipo tayari nasubiria viza tu itoke, nitaelekea Morocco kujiunga na klabu ya Difaa Al Jadida (washindi wa pili ligi kuu Morocco). . Naondoka Yanga SC , timu iliyonilea na kunipa mafanikio . . Siondoki kwa ubaya ndio maana nimefuata taratibu zote na viongozi wote wa pande mbili wameafikiana na kufanya biashara". Amesema Msuva.

 "Naamini ipo siku nitarudi kuitumikia Yanga tena ila mpaka nitimize malengo yangu ya kucheza soka la kulipwa Ulaya na kuwa miongoni mwa wanasoka waliofanikiwa nchini, baada ya Morocco Mungu akijalia basi itakuwa Ureno lakini hasa hasa ni Spain maana nina uwezo wa kucheza La Liga .

 Ahsante wana Yanga kwa usurious no mlionipa naamini kupitia kipaji changu kuna furaha nimewapa" alisema msuva alipozungumza na EATV.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images