Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

KUTANA na Tabibu wa Tiba za Asili Maalim Issa Najimu Mwenye Uwezo wa Kutibu Magonjwa.... Tiba Asilia

$
0
0
KUTANA NA TABIBU MWENYE KUBRI KUTOKA KWA ALAH MAALIM ISSA NAJIMU.
NI SHARIFU MWENYE UWEZO WA KUBAINI TATIZO LAKO PUNDE TU UNAPO MFANYIA MAWASILIANO KUPITIA WASAA NA SIKU KWA MAWASILIANO:-
MAALIM ISSA NAJIMU KUTOKA MKOA WA TANGA MWAMBONI MAGOFU KATA YA NGUVU MALI NCHINI TANZANIA,

NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA
QUR-AN, DAWA ZA ASILI PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.

ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE / MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-


ULIJALI (NGUVU ZA KIUME)
MIGUU KUWAKA MOTO
KUTAFSIRI NDOTO
MFARAKANO WA WANANDOA
MFARAKANO KAZINI
KUPANDSHWA CHEO
KUTOA PETE YA BAHATI
ANAO UWEZO WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUBASHIRI
KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA
KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU
MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA.
ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE.
ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA KWA NJIA YA MSUKULE
ANAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA PYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAIDI YALIYO KUWA SUGU


PIGA SIMU-
 Mobile; 0717 70 32 41. 
 WhatsApp 06226 535419.

TUTEGEMEE Kuiona Orijino Komedi Tena? Hali ya Vengu Nayo vipi?

$
0
0
Kwako ambaye unawafuatilia mabingwa wa kuchekesha wanaoishikilia rekodi ya Wachekeshaji waliotazamwa sana kwenye TV Tanzania Orijino Komedi ambao hawajaonekana kwenye TV kwa muda mrefu sasa na ungependa kusikia chochote.

Ayo TV na millardayo.com zimepiga stori na mmoja wa wachekeshaji wa kundi hilo Joti kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo show ya Orijino Komedi na moja ya maswali aliyojibu ni kuhusu kama itarudi huku pia akituambia hali ya Vengu ambaye ni mgonjwa kwa muda mrefu sasa.

”Mpango upo kwa sababu wakati tunafanya hii kazi hakuna mtu ambaye alijua kama komedi ingeweza kuja. Hata sisi pia tuna time kwamba tumefanya kazi muda mrefu sana zaidi ya miaka 10, hivyo namna ya kupumzika tunapanga sisi.


“Tunajua mashabiki, tunajua watu wanaotutazama kila siku wanataka wafurahi lakini sisi tunaofanya hiyo kazi ni binadamu pia tunahitaji kupumzika, kuishi na familia, kutengeneza maisha, kutulia kwanza akili zetu kutafuta vitu vingine zaidi.” – Joti.


“Ni kweli…ana nafuu kwa sababu kwa sisi tunaomjua, kumuona na kuishi naye tunajua nafuu yake ikoje. Kwa mtu mwingine anaweza kusema hana nafuu lakini sisi tunasema ana nafuu.” – Joti.

PLAY kwenye hii VIDEO ili kujua kila kitu kuhusu Show hiyo iliyokuwa inaundwa na wachekeshaji Masanja Mkandamizaji; Joti, Wakuvanga, MackReggan aka Shemeji, Mpoki  na Vengu ambaye amekuwa akiugua kwa muda mrefu.

MWANAMKE Ukiwa na Tabia Hizi 7, Lazima Mwanaume Akukimbie

$
0
0
1. CHOKOCHOKO
Wanaume wengi huwa hawapendi chokochoko. Hawapendi mwanamke ambaye yeye kila wakati ni kuanzisha chokochoko ambazo zinazalisha ugomvi. Wanaume wengi hawapendi mabishano. Hawapendi ugomvi hivyo mwanamke anapokuwa hodari wa kuleta chokochoko, huepukwa.

Ni vyema basi mwanamke akachunga kauli. Akawa si mtu wa kuchimbachimba vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Asiwe na kisirani. Kinywa chake kitawaliwe na maneno matamu, yatakayomtia moyo mpenzi wake, yatakayomfariji na yatakayomfanya apende kuzungumza naye.

Mara nyingi mwanaume akiona mke au mpenziwe ni mtu wa kupenda chokochoko, mara nyingi humuepuka. Anajitahidi kadiri ya uwezo wake kukaa naye mbali. Ataona ni bora achelewe kurudi nyumbani akakutane na marafiki baa, wapige stori ili muda uende na akirudi nyumbani asiwe na muda wa kuzungumza na mwenzi wake, yeye ni kula na kulala.

2. KUTORIDHIKA
Wanaume wengi wanachukia kuwa na wanawake wasioridhika. Baadhi ya wanawake hata uwape nini huwa hawaridhiki. Wanawasumbua wapenzi wao kwamba hawawatimizii mahitaji. Mwanaume anajitoa kumpa zawadi mpenzi wake, haridhiki tu.

Anaanza kuikosoa. Anasema haifanani na yeye, eti si ya hadhi yake. Akipewa fedha anasema hazitoshi. Kila siku ni malalamiko. Hampi nafasi mpenzi wake ya kufurahia uhusiano wao.  Anamfanya kila anapokutana naye awaze atapigwa mzinga.

Bahati mbaya sasa kila atakachopewa haridhiki. Anatamani kikubwa zaidi. Wanaume wengi siku hizi wanaichukia tabia hiyo. Hawapendi kuwa na mwanamke ambaye haridhiki na kile kidogo walichojaliwa. Wanaume wengi wakiona hivyo huwa wanaanza kumuepuka mwanamke wa ‘sampuli’ hiyo.

Kwake kunakuwa hakuna jema. Badala ya kumshauri mpenzi wake mbinu za kujikwamua kiuchumi yeye ni lawama tu. Kila siku analalamika kwamba wanaume wengine wanawapa wapenzi wao mahitaji muhimu lakini wa kwake hamtimizii.

Mwanaume akiona kila analofanya kwa mpenzi au mkewe haridhiki, hatoi shukurani ni rahisi kupunguza mapenzi kwa mtu wake. Taratibu anaanza kujitoa na hata kuhamishia mapenzi kwa mtu mwingine ambaye atakuwa anaridhika kwa kidogo anachopewa. Ni muhimu kuridhika.

3. KULINGANISHA
Hii nayo ni tabia isiyopendwa na wanaume wengi. Wanaume wanapenda kuishi maisha yao. Wanapenda kuheshimiwa na wapenzi wao. Wanapenda kumsikia mwanamke akisema; ‘hakuna mwanaume mwingine wa kufanana na wewe.’

Mwanaume anapenda kuhakikishiwa kwamba hakuna mwanaume mwingine kama yeye. Yeye ndiye mzuri au bora kuliko wanaume wengine hivyo mwanamke anapoanza kuonesha tabia za kumlimnganisha na mwanaume mwingine linakuwa tatizo kubwa.

Mwanaume anakasirika. Anaona ni rahisi mwanamke wake kumtamani mtu mwingine baki kuliko yeye. Sifa anazozitoa kwa mwanaume mwingine ni nzuri hivyo zinamvutia. Kama zinamvutia siku yoyote anaweza kushawishika kumfuata yule anayemvutia.

Wanawake wanapaswa kuwa makini katika eneo hilo. Hata kama umeona kuna kitu kizuri kimekuvutia kutoka kwa mwanaume mwingine, kamwe usije kumwambia mwenzi wako. Baki nalo moyoni. Jipe moyo kwamba mwanaume uliyenaye ndiye bora kuliko wanaume wote duniani.

4. KUWA TEGEMEZI
Wakati mwingine hata kama huna kitu lakini mwanamke unashauriwa kutojionesha huna kitu. Jioneshe kwamba una kitu hata kama huna. Wanaume wa sasa hawapendi kuwa na mwanamke ambaye kila kitu anategemea kutoka kwa mwanaume.

Hata kama huna kazi lakini ni vyema basi mwanamke akajaribu kufanya biashara ndogondogo ambazo zitampunguzia mwanaume wake makali ya kuombwa fedha kila wakati. Wanaume wanapenda kuwapa wapenzi wao fedha lakini inapozidi kipimo inageuka kuwa kero.

Yani kuanzia mahitaji ya kila siku, saluni, mavazi, ada ya watoto na mengine mengi mwanamke anamtegemea mwanaume. Yeye hataki kujishughulisha hata kidogo. Anataka aletewe, kazi yake kubwa ni kulea familia nyumbani.

Mwanaume akigundua mwanamke ni tegemezi mkiwa katika hatua za mwanzoni, ni rahisi kumkimbia mwanamke na kwenda kwa mwanamke ambaye angalau atakuwa hamtegemei kwa kila kitu. Mwanamke anayejiongeza hata kwa kutoa wazo la kuanzishiwa biashara ambayo itamfanya asiwe tegemezi.

5. KUTOKUA MUELEWA
Mwanaume anapenda mwanamke muelewa. Hapendi mwanamke mbishi. Anatamani kuwa na mwanamke ambaye akimueleza kitu, anajiongeza na kufanya zaidi ya pale mwanaume alipofikiria. Mwanaume anapenda mwanamke atakayeanzisha wazo la kimaendeleo na kumshirikisha mpenzi wake ili walifanye.

Wanaume wanapenda wanawake wanaowaelewa. Kama mwanamke anakuwa si wa kumuelewa mpenzi wake, kumsaidia basi mara nyingi mwanaume humkimbia.

6. KUJITAPA KWA KUWA NACHO
Hakuna mwanaume anayependa kutawaliwa. Wanawake wenye fedha mara nyingi wanakuwa na tabia ya kutaka kuwatawala wanaume. Anataka mwanaume afanye kile ambacho yeye anataka. Fedha zinamvimbisha kichwa na kuona kwamba anaweza kuwa na mamlaka ya kumuamrisha mumewe.

Anatumia fedha zake kama fimbo ya kumchapia mpenzi wake. Ni vigumu sana wanaume kumvumilia mwanamke wa aina hiyo, mara nyingi wanajiepusha naye. Kwa kutumia fedha zake anaweza kupata mwanaume mwingine lakini pia watashindwana katika suala la kumtawala.

7. KUWA BIZE SANA
Wanaume wengi hawapendi mwanamke tegemezi lakini pia wanaume haohao wanachukia mwanamke akiwa bize sana na kazi zake. Mwanaume hapendi kuona mwenzi wake anakuwa bize na kazi au biashara zake kiasi ambacho kitamfanya hata akose muda na mwenzi wake.

Unachotakiwa kufanya hapo mwanamke ni kujigawa. Hakikisha unakuwa bize na kazi lakini si ya kupitiliza maana itamfanya mwanaume akose muda wa kuwa na wewe pale anapokuhitaji, badala yake anaweza kwenda kwa mwanamke mwingine ambaye hayupo bize.

HATIMAYE..Miss Tanzania Mwaka 2001, Happiness Millen Magese Apata Mtoto

$
0
0
Miss Tanzania mwaka 2001, Happiness Millen Magese ambaye anafanya kazi ya uwanamitindo amebahatika kupata mtoto wake wa kwanza Julai 13 mwaka huu.


Millen akiwa na Kairo Hospitalini

Mrembo huyo ambaye alijitangaza hadharani kuwa na tataizo la Endometriosis, tatizo ambalo huwakuta wanawake wengi pindi wanapoingia hedhi, ameweza kupata mtoto wa kiume aitwaye Kairo hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Instgram alivyopost.

May you bring Hope ,faith and Miracles to millions women out there who wishes to hold their children just the way I wished to hold you.
May you grow to change the world and be there for others .
May you believe in God and own his miracles .
As much as life can be tough ,may you learn to be patient, work hard and knowing that ,everything always happens for a reason and every human being has their own path and plans from God for them.
Don’t ever loose hope .
And no matter what happens in your life remember,you have our God Almighty and I will be here always .

Father I thank you for making me A Woman and Finally A mother .
Father I thank you for bringing my dad back What a gift .jina Lako Lihimidiwe 🙏🙏🙏
I love you my Son ❤️ And to you godmother @funminewyork . I believed you had a good heart you have been with me for 13 years but Gosh what you have done through out my pregnancy journey is unexplainable. God bless you sis I can’t say more . 😢😢🙏🙏🙏
Prince Kairo Michael Magese was born
Time :6 .58 am
Weight :9 pounds 2 oz
Date :July 13 th 2017 . You’re my Victorious just like the meaning of your name “Kairo”
Glory to God . Dansaki . Asante Mungu Many thanks to Dr Seckin @endofound , Dr Lobo,Dr Gyamfi and the whole team from Columbia Doctors . Many thanks to all my friends and family oooh you guys tried @theojinika @lebogangm @samanthajansen @jimi_mugul .Special thanks to all Endometriosis groups World wide for all you do . We will raise awareness till we find Cure 💪🏽.And to you all my supporters thank you , Don’t stop supporting us. I believe A cure for Endometriosis is almost here . Support Us👊🏽🙏🙏 To Everyone don’t you ever forget ,If you knew who walked beside you, at all times, on the path that u have chose, you could never experience fear or doubt again,Have Faith 💪🏽Stand on Your Faith 💪🏽Change Your Story 💪🏽You Can Do It💪🏽
Millen Magese 💛 #PrinceKairo👑

Millen alijitangaza miaka kadhaa nyuma kuwa anatatazo la Endometriosis, kupelekea kuanzisha taasisi yake inayotoa elimu juu ya ugonjwa huo, mwaka 2015 alipata tuzo ya BET International Global Good Awards kwa mchango wake wa kutoa elimu kuhusu swala hilo.

DIAMOND, Rayvanny, Tudd Thomas, Darassa Waongoza Kutajwa Tuzo za Afrimma 2017

$
0
0
Rayvanny ametajwa katika vipengele vitatu wakati Darassa na Tuddy Thomas wakitajwa kwenye vipengele viwili. Wengine walitajwa ni Alikiba, Lady Jaydee, Vanessa Mdee, Yamoto Band, Dj D-Ommy, Dayna Nyange na Mose Iyobo.

Tuzo hizo zitafanyika October 8 ya mwaka huu mjini Texas. Hii ni orodha kamili ya vipengele hivyo.

Best Male West Africa

Wizkid – Nigeria
Falz – Nigeria
Serge Beynaud – Ivory Coast
Mr Eazi – Nigeria
Toofan – Togo
Moh Dediouf – Senegal
Davido – Nigeria
Stonebwoy – Ghana
Tekno – Nigeria
Kedejevara DJ (Ivory Coast)

Best Female West Africa

Tiwa Savage – Nigeria
Yemi Alade – Nigeria
Efya – Ghana
Adiouza – Senegal
Becca – Ghana
Josey – Ivory Coast
Mz Vee – Ghana
Simi – Nigeria

Best Male East Africa

Eddy Kenzo – Uganda
Diamond Platnumz – Tanzania
Jacky Gosee – Ethiopia
Ali Kiba – Tanzania
Navio – Uganda
Bebe Cool – Uganda
Sauti Sol – Kenya
Dynamq – South Sudan
Nyashinski – Kenya
Darassa – Tanzania

Best Female East Africa

Victoria Kimani – Kenya
Vanessa Mdee – Tanzania
Ester Aweke – Ethiopia
Avril – (Kenya)
Lady Jaydee (Tanzania)
Knowles Butera – Rwanda
Irene Ntale – Uganda
Akothee – Kenya
Dayna Nyange – Tanzania

Best Male Central Africa

Fally Ipupa – Congo
Magasco – Cameroon
Ferre Golla – DRC
C4 Pedro – Angola
Stanley Enow – Cameroon
Anselmo Ralph – Angola
Maitre Gims – (Congo)
Werrason – DRC

Best Female Central Africa

Laurette La Perle – Congo
Betty Akna – Equitorial Guinea
Syssi Mananga – Cameroon
Ary – Angola
Rennis – Cameroon
Arielle T – Gabon
Nsoki – angola

Best Male Southern Africa

Donald – South Africa
Black Coffee – South Africa
The Dogg – Namibia
Jah Prayza – Zimbabwe
Nasty C – South Africa
Emtee – South Africa
Roberto – Zambia
Casper Nyomvest – South Africa
Aka – South Africa

Best Female Southern Africa

Babes Wodumo – South Africa
Miss Lira – South Africa
Ice Queen Cleo – Zambia
Lizha James – Mozambique
Pah Chihera – Zimbabwe
Sally Boss Madam – Namibia
Zahara – South Africa
Chikune – Namibia
Bucie – South Africa

Best Male North Africa

Amr Diab – Egypt
Tamer Hosny – Egypt
Chawki – Morocco
Ahmed Soultan – Morocco
Douzi – Morocco
Ayman Alatar – Morocco
Khaled – Algeria
Saber Rebai – Tunisia

Best Female North Africa

Samira Said – Morrocco
Ibtissam Tiskat – Morocco
Angham – Egypt
Sandy – Egypt
Amal Maher – Egypt
Latifa – Tunisia
Amani Swissi – Tunisia
Sarah Ayoub – Morocco

Best African Group

Sauti Sol – Kenya
Radio & Weasel – Uganda
Toofan – Togo
Bracket – Nigeria
Mi Casa – South Africa
R2bee’s – Ghana
Bana C4 – Congo
Yamoto Band – Tanzania
Forca Suprema- Angola

Crossing Boundaries With Music Award

C4 Pedro (Angola)
Wizkid (Nigeria)
Young Paris – (Congo)
French Montana- Morocco
MHD – Senegal
Ayo Jay – Nigeria
King Kanja – (Kenya)
Wale (Nigeria)
Jidenna (Nigeria)
Maleek Berry (Nigeria)

Best Gospel

Frank Edwards – Nigeria
Uche Agu – Nigeria
Willy Paul – Kenya
SP Koffi Sarpong – Ghana
Icha Kavons – Congo
Ntokozo Mbambo – South Africa
Nathaniel Bassey – Nigeria
Sonnie Badu – Ghana

Best Newcomer

Dremo – Nigeria
Medikal – Ghana
Ray Vanny – Tanzania
Preto Show- Angola
Maleek Berry – Nigeria
Mr Leo – Cameroon
Nathi – South Africa
Julz – Ghana
Niniola – Nigeria
Zani Challe – Malawi

Artist of The Year

Flavour (Nigeria)
Diamond Platnumz ( Tanzania)
Fally Ipupa- Congo
Wizkid (Nigeria)
Cassper Nyovest (South Africa)
Davido – (Nigeria)
Eddy Kenzo – Uganda
Tekno – Nigeria
Mr Eazi – Nigeria
C4 Pedro – Angola

Dancehall Act of the Year

Timaya – Nigeria
Stonebwoy – Ghana
Jah Prayza – Zimbabwe
Burna Boy – Nigeria
Samini – Ghana
Patoranking – Nigeria
Shatta Wale – Ghana
Buffalo Souljah- Zimbabwe

Best Video Director

Daps – Nigeria
Justin Campos – South Africa
Sesan – Nigeria
Clarence Peters – Nigeria
Patrick Elis – Nigeria
Shammack – Cameroon
Enos Olik – Kenya
Savy Filmz – Uganda
Avalon Okpe- Nigeria
Godfather- South Africa

Best Dj Africa

Dj Spinall – Nigeria
Dj Joe MFalme – Kenya
Dj Black Coffee – South Africa
Dj Exclusive – Nigeria
Dj Kalonje – Kenya
Dj D-Ommy – Tanzania
Dj Paulo Paulo Alves – Angola
Dj Crème Delacreme – Kenya
DJ Nyce- Ghana

Best African Dj USA

Dj Tunez – Nigeria
Dj Wangura – Ethiopia
Dj FreshyK – Nigeria
Dj Deemoney – Nigeria
Dj Silent Killa – Carribeans
Dj Akua – Ghana
Dj Fully Focus -Kenya
Dj Rell – Sierra Leone
Dj Poison Ivy – Kenya
Dj Mike Kiss – Carribeans

AFRIMMA Video of The Year

Toofan – Terre (Togo)
Davido – If (Nigeria)
Wizkid – Come Closer (Nigeria)
Runtown – Mad Over You (Nigeria)
Casper Nyovest – Tito Mboweni (South AFrica)
Emtee ft Nasty C – Winning (South Africa)
Diamond Platnumz ft Ray Vanny – Salome (Tanzania)
Victoria Kimani ft Donald – Fade Away (Kenya/South Africa)
Fally Ipupa – Eloko Iyo (Congo)
C4 Pedro ft Sauti Sol – Love again (Angola/Kenya)

Music Producer of The Year

Dj Breezy – Nigeria
Masterkraft – Nigeria
Dr Fizol – Uganda
Julz – Ghana
Visita – Kenya
Tweezy – South Africa
Tud Thomas – Tanzania
Krissbeatz – Nigeria
Del B – Nigeria
Sidikiba Diabate – Mali

Best African Dancer

Kaffy Dancequeen – Nigeria
Korra Obidi – Nigeria
Nabile Danser – South Africa
Sherri Silver – Rwanda
La Petite Zota – Ivory Coast
Manuel Canza Laurenzo – Angola
Moses Iyobo – Tanzania
Brenda Derry – Cameroon
Ghetto Triplet Kids (Uganda)
Eddy Wizzy Dances (Uganda)

Best Rap Act

Phyno – Nigeria
Olamide – Nigeria
Aka – South Africa
Sarkodie – Ghana
Casper Nyovest – South Africa
King Kaka Sungura – Kenya
Octopizzo – Kenya
Prodigio – Angola
Falz – Nigeria

Best Collaboration

Wizkid ft Chris Brown- African Bad girl (Nigeria/USA)
Diamond Platnumz ft NeYo – Marry you (Tanzania/USA)
Babe Wodumo ft Mampinsta – Wololo (South Africa)
Ycee ft Maleek Berry – Juice (Nigeria)
Runtown ft Sarkodie – Painkiller (Nigeria/Ghana)
Davido ft Nasty C – Coolest Kid in Africa (Nigeria/South Africa)
Edy Kenzo ft Alaine – Addicted (Uganda/Jamaica)
C4 Pedro ft Sautisol- Love again (Angola/Kenya)
Darasa ft Ben Pol- muziki (Tanzania)
Fally Ipupa ft Booba- Kinane (Congo)

Song of The Year

Runtown – Mad over you (Nigeria)
Davido – If (Nigeria )
Diamond Platnumz ft Rayvanny – Salome (Tanzania)
Babe Wodumo ft Mampintsha – Wololo (South Africa )
Wizkid – Come Closer (Nigeria)
Caspper Nyovest – Tito Mboweni (South Africa)
Fally Ipupa – Eloko Iyo (Congo)
Toofan – Terre (Togo)
Darasa ft Ben Pol – Muziki (Tanzania)
MHD- Bravo (Guinea Conakry)

Best Lusophone

C4Pedro- Angola
Nsoki – Angola
Ary- Angola
Yola Semedo- Angola
Yasmine (Guinea)
Calema (Sao Tome)
Anselmo Ralph- Angola
Nelson Freitas- Cape Verde
Mr Bow- Mozambique
Djodje- Cape Verde

Best Francophone

Sidikiba Diabate – Mali
Moh Dediouf – Guinea Conakry
Dj Arafat – Ivory Coast
Toofan – Togo
Hiro- Congo
Fally Ipupa – Congo
Maitre Gims – (Congo)
Adiouza – Senegal
Daphne – Cameroon
Serge Beynaud – Ivory Coast

Best Sound Engineer

MixMonster- Nigeria
Suka sounds- Nigeria
Ogopa Brothers- Kenya
Tud Thomas- Tanzania
Sheyman- Nigeria
Kaywa- Ghana
Twizzy – South Africa
Bebe Philip – Ivory Coast

SHETTA Amchana Diamond Kiaina Kuhusu Kutoa Nyimbo Mfululizo.....

$
0
0
Msanii wa Bongo Flava, Shetta amesema haamini kutoa nyimbo nyingi kwa wakati mmoja ni sababu ya kufanya vizuri.



Shetta ambaye amekaa kipindi kirefu bila kutoa ngoma, ameiambia EA Radio kuwa yeye anaamini katika kujipanga zaidi na kutoa ngoma kali.

“Mimi siamini kwenye kutoa nyimbo nyingi ndio ku-trend, nafikiri kujipanga kwangu ndio huwa kuna sababisha kukaa muda mrefu bila kutoa wimbo, ningekuwa naweza kujipanga haraka ningeweza kutoa madude haraka lakini so far so good ngoja tutaibadilisha, ngoja tuone system yetu tufaifanyaje,” amesema Shetta.

Ameongeza kuwa, “naamini ukitoa kazi ambayo umejipanga nayo watu wanaweza wakaenyoy mwaka mzima au miaka miwili, kukaa kimya haijawahi kunihadhiri kwa chochote sana sana watu wananimisi lakini ninapokuja watu wanakuwa wananipokea, so am happy katika kitu ninachokifanya,” amesisitiza.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa leo

$
0
0

FAIZA Ally Amfungukia Baba Kijacho wake

$
0
0
Mrembo kunako Bongo Muvi ambaye pia ni mzazi mwenzie na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Faiza Ally amefunguka kuwa kati ya vitu ambavyo havipendi katika ujauzito wake huu ni kumuanika baba kijacho wake.

Akipiga stori na Star Mix, Faiza alisema kuwa, anafurahi kuwa mama mtarajiwa wa mtoto wake pili lakini linapokuja suala la kupiga naye picha ama kumuanika baba kijacho wake mitandaoni kama wafanyavyo wasanii wengine kwake halina nafasi.

“Kwanza nalipenda tumbo langu likiwa imejaa (ujauzito) lakini pia hakuna kitu ninachokiogopa kwa sasa kama kumuanika baba kijacho wangu ambaye yupo nje ya nchi kwa sasa naogopa wasije mkwapua bure, hayo mambo sijui ya kuuza sura naawaachia hao wasanii wengine,” alisema Faiza ambaye mtoto wake wa kwanza amezaa na Sugu.

Kisa cha Vijana Sita wa Africa Waliopotea Katika Mazingira ya kutatanisha Marekani

$
0
0
Vijana sita wa Burundi waliokuwa wakishiriki katika mashindano ya roboti nchini Marekani wameripotiwa kutoweka, polisi wanasema.

Wavulana wanne na wasichana 2 walio kati ya umri wa miaka 16 na 18 walipotea wakati wa mashindano hayo ya kwanza duniani yaliofanyika Washington DC.

Idara ya polisi mjini humo imesema kuwa mara ya mwisho vijana hao kuonekana ilikuwa siku ya Jumanne wakati wa makamilisho ya michezo hiyo.

Ripoti zinasema kuwa vijana wawili kati yao tayari wamevuka mpaka na kuingia Canada lakini ripoti hiyo haijathibitishwa na polisi.

Siku ya Alhamisi, idara ya polisi mjini humo ilibandika picha za sura za vijana hao sita waliopotea katika mtandao wao wa Twitter, wakiwataka raia kuwasiliana nao iwapo watakuwa na habari yoyote kuwahusu.


Vijana sita wa Burundi waliotoweka katika mashindano ya roboti nchini Marekani


Vijana hao wanatambulika kuwa Don Ingabire, Kevin Sambukiza, Nice Munezero, Audry Mwamikazi, Richard Irakoze na Aristide Irambona.

Waandalizi wa mashindano hayo wanasema kuwa waliwaeleza polisi baada ya msimamizi wa timu hiyo ya Burundi kushindwa kuwapata vijana hao.

Katika taarifa , msemaji wa mashindano hayo Jose Escotto alisema, ripoti kamili imewasilishwa kwa polisi ambao wanachunguza kisa hicho, kulingana na gazeti la The Washington Post.

Mashindano hayo ya siku 3 yalihudhuriwa na timu 150 zilizokuwa zikishindana.
Mashindano hayo yanalenga kuwashawishi vijana kukuza vipaji vyao katika masomo ya sayansi, technolojia, uhandisi na hesabu.

SAID Aliyetobolewa Macho na Scorpion Amgeuzia Kibao Mkewe

$
0
0
Songombingo la ndoa ya jamaa aliyetobolewa macho na Scorpion, Said Mrisho na mkewe Stara Sudi ‘Mama D’ juzikati lilichukua sura mpya baada ya Said kumgeuzia kibao mkewe na kusema watoto mapacha waliozaliwa na mwanamke huyo anahisi siyo damu yake.

Awali akizungumza na kituo kimoja cha redio jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita, Mama D alisema kuwa mumewe huyo aliwahi kukana mimba ya watoto hao lakini Said aliyekuwepo redioni hapo alikanusha na kusema kuwa, jamii ijue kuwa watoto ni wake hivyo akampa mkewe matumaini mapya.

Hata hivyo, Jumanne iliyopita Ijumaa liliibuka nyumbani kwa Said, Vingunguti jijini Dar anakoishi na yule mkewe Mwarabu na katika maelezo yake akasema, kauli yake kutoka moyoni ni kwamba anahisi wale watoto mapacha siyo wake.

“Jamani iko hivi, kabla sijapata ulemavu nilikuwa na miezi kama mitatu sijakutana na mke wangu, baada ya kupata matatizo nikawa na miezi mingine mitatu bila kukutana kimwili, baada ya kuishi kwa siku nyingi bila kukutana, siku tulipokutana tu wiki chache baadaye akaniambia ana mimba ya miezi minne!

“Ndiyo maana nasema nina wasiwasi na hawa watoto mapacha si wanangu. Haya yote sikutaka kuyasema tangu mwanzo kwa kuwa sikutaka mvutano na mwanamke huyo, wala sikuona kama ni vema kusema maovu yake mengi,” alisema Said.

Baada ya maelezo hayo, paparazi wetu alimvutia waya Mama D ambapo baada ya kumwagiwa maelezo ya Said alitokwa na povu ‘si la nchi hii’ huku akimuomba Mungu ampe mabalaa mzazi mwenzake huyo.

“Mungu amlaani maisha yake yote na niseme tu, natamani apate balaa kubwa kuliko hilo alilonalo, naona ulemavu umemfanya akili yake ishindwe kufikiri sawasawa.

“Ambacho naweza kusema ni kwamba, kama ana wasiwasi na hawa watoto anaweza kwenda kupima DNA akikuta watoto si wake, ruksa aniache nao, nitawalea peke yangu na kama vipimo vitaonyesha watoto ni wake naapa kwa jina la Mungu naenda kumtelekezea vichanga hivi mlangoni kwake awalee mwenyewe,” alisema mama D.

NAMPENDA Rafiki Yangu Mpaka Naogopa

$
0
0
Mimi ni Msichana wa miaka 19 Nilipoingia 4m 5 nimesoma shule ya girls only...nilimpenda rafiki yangu mmoja sanaaaa kuliko wote...nilimpa zawadi nyingi hata wakati wa likizo nilikuwa namtembelea kwao..nilimpenda sana...kila tukigombana tunasameheana.

Juzi aliniboa kidogo nikamtumia meseji za hasira za kwamba simpendi tena, ila badaae hasira zilipoisha nikajikuta nalia sana kumpoteza rafiki yangu nilimuomba msamaha ila hakunijibu sababu meseji nilizomtumia zilikuwa mbaya sana.Nimemuomba msamaha ila hajanijibu..Bado nampenda sana yaaani hata boyfriend wangu simpendi kama navyompenda huyu rafiki yangu japo si wapenzi ila namfeel sana yaaani sometimes natamani nimkiss japo ni msichana mwenzangu ...

Naogopa jamani nishaurini ama ndio hizi wanazosema dalili za Usagaji

By Kurwa

MREMBO Kidoa Adai Bila Cheni ya Kiuno Hajatimia......

$
0
0
MUIGIZAJI ambaye pia ni Mshindi wa Shindano la Ijumaa Sexiest Girl 2015, Asha Salum ‘Kidoa’ amesema katika mwili wake atavaa vyote lakini bila kuwa na cheni kiunoni hujiona hajatimia.
Akizungumza na Star Mix, Kidoa ambaye kwa sasa anaigiza Tamthiliya ya Huba alisema kuwa, iliwahi kumtokea siku moja akasahau kuvaa cheni kiunoni, alijihisi hana amani na muda wote alijiona mtu wa aibu.

“Kiukweli yaani kwenye mtoko wowote bila kuvaa cheni kiunoni sijui najionaje? Najiona kama sijatimia vile. Napenda sana kuvaa cheni, imekuwa kama ugonjwa kwangu,” alisema Kidoa.

HALI ya Mchekeshaji Mzee Majuto sio Nzuri...Anaitaji Maombi yako

$
0
0
MWEZI Mei, mwaka huu, gazeti ndugu la hili, Ijumaa Wikienda liliripoti habari mbaya juu ya lejendari wa vichekesho Bongo, Amri Athman ‘Mzee Majuto’ kuwa katika hali mbaya kiafya, lakini kwa hali yake ilivyo kwa sasa anahitaji dua za Watanzania.

AFANYIWA UPASUAJI
Habari mbaya zilizolifikia Amani, mapema wiki hii zilieleza kuwa, Mzee Majuto yu kitandani kwa mara nyingine kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa uliosababisha afanyiwe upasuaji.
Chanzo makini kililieleza Amani kuwa, Mzee Majuto ambaye amezaliwa mwaka 1948, alilazwa kwa siku tano hospitalini huko mkoani Tanga akisumbuliwa na ugonjwa wa hernia (ngiri) ambapo ililazimu afanyiwe upasuaji ili kumsaidia kwenye tatizo lake hilo la muda mrefu.

Chanzo hicho kilieleza kuwa, kufuatia tatizo hilo, Mzee Majuto amekuwa akitumia dawa za hospitalini na zile za kienyeji, lakini hakuna unafuu wowote anaoupata.
“Kuna kipindi alilazwa hapo katikati, alipopata nafuu aliruhusiwa lakini wiki iliyopita alibanwa sana na unajua yule mzee alikuwa anaogopa kufanyiwa operesheni ila kutokana na afya yake imebidi akubali tu,” kilisema chanzo chetu hicho na kuongeza:
“Kimsingi Mzee Majuto anahitaji dua za mashabiki wake na Watanzania kwa jumla.”



MKE WA MZEE MAJUTO AFUNGUKA
Baada ya kupata habari hizo, Amani lilimtafuta msanii huyo kwa njia ya simu yake ya kiganjani ambapo ilipokelewa na mkewe, Aisha Yusuf ambaye alithibitisha mumewe kuumwa.

Mama Majuto alisema kuwa, hadi wakati anazungumza na gazeti hili alikuwa yupo na mumewe katika Hospitali ya Tanga Central Health Centre (TCHC) ambako alilazwa kwa siku tano na kufanyiwa upasuaji.

“Ni kweli Mzee Majuto anaumwa ndiyo maana nimepokea simu yake, nipo naye hapa hospitalini, anasumbuliwa na ugonjwa wa hernia ambao umeibuka na kumuanza tena.
“Tunamshukuru Mungu kwa sasa anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji hivyo Watanzania na mashabiki wake waendelee kumuombea na Mungu akipenda hivi karibuni tu atarudi mzigoni, watarajie mambo mazuri kutoka kwake,” alisema mama Majuto.

Amani lilipoomba kuzungumza na Mzee Majuto mwenyewe, mkewe alisema alikuwa usingizini kwani alitakiwa apumzike baada ya upasuaji.
“Nitamfikishia pole lakini haruhusiwi kuzungumza, anatakiwa kupumzika,” alisema mama huyo na kuongeza:
“Hata hivyo, tumeambiwa tutaruhusiwa kutoka hapa hospitalini muda wowote.”

MASHABIKI WAMMISS
Wakiongea na gazeti hili, baadhi ya mashabiki wa staa huyo walisema kuwa, wamemmiss sana kwenye fani yake ya uigizaji na kumuomba Mungu afanye miujiza na amrejeshee afya yake.
“Kwa kweli tumemmiss sana, tunaamini atapona na kurejea kwenye hali yake ya kawaida,” alisema mmoja wa mashabiki aliyejitambulisha kwa jina la Said Juma.

UGONJWA WA HERNIA
Hernia au ngiri ni aina ya ugonjwa ambao humpata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikilia au kubeba viungo (organs) fulani kupoteza uimara au kuwa na uwazi (opening) hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiliwa ipasavyo.

Miongoni mwa vitu vinavyoweza kumsababisha mtu kupata hernia ni pamoja na kuwa na uzito mkubwa au kuongezeka uzito kwa ghafla, kazi ya kubeba au kunyanyua vitu vizito, tatizo la kukohoa au kupiga chafya kwa muda mrefu, ujauzito au matatizo yanayojitokeza kwa mwanamke wakati wa kujifungua.
Pia kuharisha au kuvimbiwa (constipation). Vitu hivyo humfanya mtu apate hernia ambayo husababisha afanyiwe upasuaji ili kumaliza tatizo hilo.

Stori: GLADNESS MALLYA, DAR

Install App Namba Moja Tanzania Kwa Habari za Udaku na Mengine.....Udaku Special App

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Je Dada Unahitaji Kuwa Mrembo na Kaka Kuwa Mtanashati na Kupendeza? Waone Hawa

$
0
0
BLACK BEAUTY COMPANY
Je Dada unahitaji kuwa Mrembo na ule muonekano bomba wa kisuperstar👌🔥,kaka unahitaji kuwa mtanashati na mvuto zaidi wa KIUME?fika black beauty company utatimiza ndoto zako,hawakosei hata siku moja kwa products original na zenye matokeo yaharaka sana,bila madhara,ni kampuni yenye uzoefu wa hali ya juu sana🔥
1)kuongeza hips,makalio,mapaja@150000
(b)kuongeza hips,makalio,mapaja na miguu@200000/=
2)kuongeza miguu ,kuondoa vigimbi@120000/=
3)kuwa mweupe mwili mzima (Rangi moja)@150000/=
4)Kupungua mwili mzima@150000/=
5)kupunguza tumbo@100000/=
6)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
7)kukuza nywele@100000/=
8)kuondoa michirizi @100000
9)kuondoa madoa,mabaka na chunusi sugu@100000/=
10)kuongeza uume na nguvu za kiume@150000/=
Dawa zetu niuhakika sana100%na utaletewa popote ulipo,mikoani tunatuma,nje ya nchi tunatuma DHL,ofic zetu zipo kariakoo msimbazi police,🔥karibuni kwa mawasiliano zaidi

WhatsApp+255657778924,au call0743534406 

au unaweza kutufollow

👇👇👇👇👇👇
@black_beauty_company

MWANAMKE wa Kibantu: Kama Una Wowowo, Usipoolewa Huo ni Uzembe Wako!!

$
0
0
Wanawake waliofungashiwa ni highly marketable securities katika soko... Ops, nimetumia lugha ya ki Finance.
Highly marketable securities ni zile hisa za makampuni makubwa Duniani, Marekani wanaita top 500 fortune companies kama vile Apple, General electric and the like... Ambazo zinauzika kwa upesi sana katika soko la hisa...

Kwa mwanaume rijali anayetafuta mchumba, wakisimama wanawake kumi mmja kawa na wowowo, hata kama ana sura mbaya, lazima awe chaguo la wengi.

Sasa kama wewe mwanamke wa kibantu umefungashiwa na Mola wako alafu bado unahangaika kupata bwana, ujue una very serious problems ambazo zinawafanya watu washindwe kukaa na wewe. Otherwise, tiketi yako ya kuolewa iko wazi kama jua lilivyo angani...

JESHI la Polisi Dar Latoa Siku 7 Majambazi Wajisalimishe

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limetoa siku saba kwa majambazi wote waliowahi kutumikia vifungo na kuachiwa kwa kumaliza vifungo au rufaa, wajisalimishe kwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu.

Kauli hiyo ilitolewa jijini hapa na Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Lucas Mkondya wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Mkondya alisema lengo la kuwaita majambazi hao ni kutaka kupanga utaratibu mzuri ili waone kama baada ya vifungo vyao, wamebadilika na wanajihusisha na shughuli gani kwa sababu walikuwa ni majambazi sugu na walifanya matukio.

“Kuanzia leo (jana) nataka wajisalimishe, wasipojisalimisha wanajua jinsi tunavyowatafuta kwa sababu ni jambazi hatumtafuti kwa kucheka tunamtafuta kwa silaha lengo la kuhakikisha hatusikii milio ya bunduki ikipigwa Dar es Salaam,” alisema Mkondya.

Aidha, Mkondya aliwataka wenyeviti wa serikali za mitaa, kutoa taarifa kama kuna majambazi katika maeneo yao ambao wamechiwa ili polisi wawafuatilie kikamilifu. Katika tukio jingine, jeshi hilo limewakamata watuhumiwa 44 wa wizi wa vifaa vya magari pamoja na vifaa hivyo vya magari.

Alisema watuhumiwa hao walikamatwa kutokana na operesheni maalumu, ambayo inalenga kuwakamata wezi wa vifaa mbalimbali vya magari, ikiwa ni pamoja na wanunuzi wa vifaa hivyo katika sehemu mbalimbali za jiji hili.

Aliongeza kuwa operesheni hiyo iliyoanza Julai 18, mwaka huu na katika operesheni hiyo ambayo endelevu, watuhumiwa hao walikamatwa na baada ya kupekuliwa katika maduka yao walikutwa na vifaa mbalimbali vya magari.

Katika mahojiano na watuhumiwa wote waliokamatwa, wapo walioshindwa kuvitolea maelezo vifaa hivyo ni namna gani na wapi vifaa hivyo wamevipata huku baadhi ya vifaa vikionesha kuwa vimefunguliwa kutoka kwenye magari mengine kwani vimekutwa na namba za magari.

“Watuhumiwa wote bado wanaendelea na mahojiano na uchunguzi bado unaendelea ili kubaini mtandao wote unaojihusisha na wizi huo wa vifaa vya magari ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani kwa hatua zaidi,” alisema Kaimu Kamanda.

Aidha, jeshi hilo linawashukuru wananchi kwa kutoa taarifa na kuwataka wafanyabiashara wa vifaa vya magari kufuata sheria zinazowawezesha kufanya biashara hiyo kihalali.

Wakati huo huo, jeshi hilo limekamata bastola moja aina ya Browning Patent ikiwa na risasi tisa baada ya majibizano ya risasi kati ya askari polisi na jambazi mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Adam, ambaye alifariki dunia katika majibizano hayo.

Alisema tukio hilo ni la Julai 19, mwaka huu maeneo ya Ubungo Mawasiliano, ambako awali jambazi huyo na wenzake ambao wanaendelea kutafutwa, walishiriki katika tukio la mauaji lililotokea maeneo ya Kinondoni Block 41 ambako mtu mmoja aliuawa kwa kupigwa risasi.

Baada ya jambazi huyo kuuawa, alipekuliwa na kukutwa na silaha hiyo Browning, na pia alikutwa na sare za kampuni ya ulinzi zisizokuwa na nembo na zenye rangi ya buluu bahari, fulana moja idhaniwayo ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na boti za kijeshi jozi moja, kamba ya mkonge, plasta, bisibisi na maski za mdomo.

Aidha, alisema sare za ulinzi alizokutwa nazo jambazi huyo ndizo zilizoonekana kuvaliwa siku ya tukio la Kinondoni, huku mtuhumiwa aliyekamatwa awali akikutwa na vibao vya namba za magari zenye namba za usajili STK 4704 na T. 503 APG, vocha za Vodacom za Sh 5,000 pisi 10, tabuleti aina Samsung, pasipoti mbili zenye majina ya Salum Malulu na Jeremiah Malulu zenye picha ya mtu mmoja, kitambulisho kinachodhaniwa ni cha Usalama wa Taifa na mihuri minne.

Alieleza kuwa uchunguzi unaendelea ili kuwapata washiriki wote wa tukio hilo la mauaji ili wachukuliwe hatua za kisheria.

MTOTO: Jaji Msuya Alikata Kauli Tangu Oktoba Mwaka Jana

$
0
0
Mtoto wa aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu, marehemu Upendo Msuya amesema, kujiuzulu kwa mama yake kulitokana na kuugua kwa muda mrefu kulikosababisha akate kauli tangu Oktoba mwaka jana.

Masha Msuya, mtoto wa pili wa Jaji Msuya, alisema hali ya mama yake ilizidi kuwa mbaya mara baada ya kurudi kutoka India alikokuwa akitibiwa Oktoba mwaka jana.

Jaji huyo alifariki dunia usiku wa kuamkia juzi katika Hospitali ya Kairuki baada ya kuugua kwa muda mrefu.

“Mara ya mwisho sisi kuongea na mama vizuri ni mwezi wa 10 mwaka jana na muda wote huo mama alikuwa anawasiliana na sisi kwa kutumia maandishi,” alisema Masha.

Kabla ya kifo chake, Mei mwaka huu Msuya pamoja na Jaji Aloysius Mujulizi waliomba kujiuzulu nyadhifa zao, kitendo ambacho Rais John Magufuli alikiridhia.

Baada ya kujiuzulu taarifa mbalimbali zilizagaa zikidai kuwa Jaji Msuya alijiuzulu kwa sababu ya kutotenda haki katika kesi za dawa za kulevya alizozitolea hukumu.

Hata hivyo, Masha alisema mama yake alikuwa amekata kauli na hicho ndicho kilichokuwa chanzo cha kujiuzulu nafasi hiyo.

Alisema mama yake alisumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu ambalo lilikuwa likijirudia mara kwa mara, hali iliyomsababishia ugonjwa wa kiharusi na kumfanya kutokuwa na uwezo wa kuongea vizuri.

Alisema mwaka huu ndio ulikuwa muda wa mama yake kustaafu na alipewa uhamisho kutoka Tanga kuja Dar es Salaam na ndipo alipowaambia watoto wake kuwa anataka kuandika barua ya kustaafu.

Alisema hiyo ndiyo moja ya sababu ya kujiuzulu kwa mama yake kwa kuwa kwa kazi yake ya ilihitaji kuwa na uwezo wa kuzungumza.

“Tutamkumbuka daima pamoja na kwamba alikuwa hawezi kuongea wala kutembea kutokana na ugonjwa wa kiharusi, lakini alikuwa anasisitiza upendo kwetu kila mara na yote hayo aliyafanya kwa kuandika,” alisema.

Mume wa marehemu, Hilary Msuya alisema kuondoka kwa mkewe ni pigo kwao, kwani afamilia ilikuwa inamtegemea kama mama.

“Kwa mapenzi ya Mungu ametutoka tukiwa bado tunamhitaji,” alisema Msuya.

Msuya alisema viongozi waliofika kutoa pole ni pamoja na Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Kiongozi, Ferdinand Wambali, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi na Jaji Mkuu mstaafu, Barnabas Samatta.

Majaji wengine waliofika kwenye msiba huo ni Richard Mziray, Sekieti Kihio na Pellagia Khaday.

Alisema, ibada ya kuaga mwili wa Jaji Msuya itafanyika Jumamosi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Wazo Hill na mazishi yatafanyika katika makaburi ya Kinondoni.

Jaji Msuya aliteuliwa na Rais mstaafu, Jakaya Kikwete, Mei 28 2008 kushika wadhifa huo akiwa pamoja na majaji wengine kumi na moja.    

MAMBA Atishia Amani Tanga

$
0
0
Wakazi wa Mitaa ya Kange na Mkurumuzi jijini Tanga wamesema maisha yao yapo hatarini kutokana na bwawa lilioibuka baada ya kubomoka bwawa la samaki la kiwanda cha Rhino kuwa na mamba wakubwa.

Wakazi hao wamedai kuwa mwanamke mmoja alinusurika kuliwa na mamba mkubwa ambaye alikuwa amejificha katika kichaka.

Licha ya kufikisha malalamiko yao katika mamlaka husika na
kamati ya maafa ya Wilaya ya Tanga kutembelea, lakini ni miezi mitatu sasa hakuna hatua za kwuadhibiti wanyama hao zilizofanyika.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Maopinduzi (CCM) Kata ya Maweni, Said Bindo (72) amesema hali ilivyo inavyohatarisha usalama wa wakazi wa mtaa huo na kuitaka Serikali kutosubiri maafa yatokee.

“Tatizo hapa ni kwamba ni sababu huku wanaishi watu wa hali ya chini… kama wangekuwa wanaishi vigogo, hili bwawa lisingekuwepo. Kinachohitajika ni kutengeneza daraja litakalokuwa na uwezo wa kupitisha maji kwa wingi ili bwawa likauke,” amesema Kada huyo wa CCM.
Bindo, ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya siasa ya CCM tawi la Kange, amesema ameishi hapo  kwa kipindi cha zaidi ya miaka 50 na haijawahi kutokea hali kama hiyo.

“Sababu zinazotolewa tunaona kama ni visingizio… wanasema eti mara Halmsahuri itakapopata fungu, lakini kwa umri wangu na uzoefu nilionao, tatizo kama hili ni janga ambalo linahitaji kutatuliwa kwa fungu la dharura au kukiamuru kiwanda cha Rhino kujenga daraja kwa sababu ndiyo chanzo,” amesema Bindo.
Issa Shaaban, ambaye nyumba anayoishi inapakana na mto huo alilalamika kuwa jana jioni mke wa kaka yake alikurupshwa na mamba mkubwa lakini alifanikiwa kukimbia na kujiokoa.
Diwani wa kata ya Kange, Joseph Colyvirs, amesema tayari Baraza la Madiwani la Halmashauri ya jiji la Tanga limeshapitisha katika mpango wake wa kujenga makaravati katika mto huo ulioibuka hivi karibuni ili kuruhusu maji yapite.
“Yupo mwekezaji alifanya kazi ya kuzibua pale lakini kutokana na maji kuwa mengi iimeshindikana,” amesema diwani huyo.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Thobias Mwilapwa, amesema taarifa za kuibuka kwa bwawa katika eneo hilo anazo lakini tukio la kuonekana mamba halijamfikia na akaahidi kufanyia kazi haraka iwezekanavyo ili kunusuru maisha wananchi.

JERRY Muro Atoa Maoni yake “Rais wa Tanzania ni Mmoja tu”

$
0
0
Ni maoni ya Mwandishi wa habari ambaye pia amewahi kuwa Msemaji wa Club ya soka ya Yanga Jerry Muro kwenye mtandao wake wa kijamii kuhusu Rais wa Tanzania na wengine wenye vyeo vya Urais.

Jerry Muro ameandika :

“Rais wa Tanzania ni mmoja tu, Hawa wengine 
Rais wa TLS Rumande
Rais wa TFF Rumande
Rais wa Yanga Rumande 
Rais wa Simba Rumande 
Mwingine akijiita *Rais* asubiri moto wake.
#utanikamakweli 
Nchi haiwezi kuwa na utitiri wa marais ikakubalika.
#raiswangu #HapaKaziTu@lemutuz_nation
@paulmakonda @gersonmsigwa“


Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images