Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live

Barakah The Prince Akimbia ‘Kichambo’ cha Team Kiba

$
0
0

Msanii wa muziki, Barakah The Prince ameendelea kukosa uhuru wa kifanya kile anachokitaka kupitia mtandao wa Instagram kwa madai ya kuogopa kishambo kutoka kwa Team Kiba mtandaoni.


Muimbaji huyo ambaye wiki hii ametangaza kuachana na label ya RockStar4000 iliyokuwa inasimamiwa muziki wake, ameonekana kukosa amani mitandaoni kutoka na kauli ambazo amekuwa akizitoa juu ya msanii Alikiba ambaye ni mmoja kati ya Wakurugenzi wa RockStar4000.

Barakah ambaye anamiliki label ya Bana Music Entertainment, ameamua kufunga sehemu za kukomenti katika mtandao wa Instagram baada ya mashabiki ambao wanaonekana kuwa wa Team Kiba kutopendezwa na kauli za muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo, Acha Niende.

Muimbaji huyo alidai amechana na label hiyo baada ya kuona kuna mambo kadhaa yameshindwa kwenda sawa huku akishindwa kuyaweka wazi.

RockStar4000 bado hawajatoa kauli yoyote juu ya kauli ya muimbaji huyo.

Muimbaji huyo mpaka sasa ana rekodi mbaya ya kukorofishana na label kadhaa ikiwemo ya Tetemesha Entertainment ambayo ilimtambulisha kwenye muziki.

Je Dada Unahitaji Kuwa Mrembo na Mkaka Kuwa Mtanashati na Rijali.....Waona Hawa Black Beauty

$
0
0

BLACK BEAUTY COMPANY
je Dada unahitaji kuwa Mrembo na ule muonekano bomba wa kisuperstar👌🔥,kaka unahitaji kuwa mtanashati na mvuto zaidi wa KIUME?fika black beauty company utatimiza ndoto zako,hawakosei hata siku moja kwa products original na zenye matokeo yaharaka sana,bila madhara,ni kampuni yenye uzoefu wa hali ya juu sana🔥
1)kuongeza hips,makalio,mapaja@150000
(b)kuongeza hips,makalio,mapaja na miguu@200000/=
2)kuongeza miguu ,kuondoa vigimbi@120000/=
3)kuwa mweupe mwili mzima (Rangi moja)@150000/=
4)Kupungua mwili mzima@150000/=
5)kupunguza tumbo@100000/=
6)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
7)kukuza nywele@100000/=
8)kuondoa michirizi @100000
9)kuondoa madoa,mabaka na chunusi sugu@100000/=
10)kuongeza uume na nguvu za kiume@150000/=
Dawa zetu niuhakika sana100%na utaletewa popote ulipo,mikoani tunatuma,nje ya nchi tunatuma DHL,ofic zetu zipo kariakoo msimbazi police,🔥

karibuni kwa mawasiliano zaidi WhatsApp+255657778924,au call0743534406

au unaweza kutufollow
👇👇👇👇👇👇
@black_beauty_company
@black_beauty_company
@black_beauty_company

Staa wa filamu za Home Alone afariki dunia

$
0
0

California, Marekani. Mwigizaji John Heard aliyejizolea umaarufu kwa kuigiza kama baba katika filamu za Home Alone, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 72.

Mwili wake aligundulika na mhudumu wa hoteli aliyofikuwa amefikia kwa ajili ya mapumziko baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo wa mgongo jijini California, Marekani.

Heard alikuwa akiigiza kama Peter McCallister katika filamu za Home Alone akiwa baba wa Macaulay Culkin maarufu Kelvin.

Ameigiza katika filamu mbili kati ya hizo ambazo ni  Home Alone na Home Alone 2: Lost in New York

Mbwana Samatta na Rooney Ngoma Droo....

$
0
0

Mtanzania Mbwana Samatta alipata nafasi ya kuiongoza safu ya ushambuliaji ya timu yake ya KRC Genk ya Ubelgiji katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Everton FC inayodhaminiwa na kampuni ya michezo ya kubashiri ya SportPesa.

Mchezo wa Everton dhidi ya KRC Genk uliyochezwa nchini Ubelgiji katika uwanja wa Luminus Arena, umempa nafasi nahodha wa Tanzania Mbwana Samatta kuonesha uwezo wake dhidi ya Everton ambayo ni miongoni mwa vilabu saba England ambavyo havijawahi kushuka daraja toka kuanzishwa kwa mfumo wa Ligi Kuu England 1992.

Mbwana Samatta ambaye ndio mshambuliaji tegemeo wa KRC Genk baada ya kuumia kwa mgiriki Nikolaos Karelis aliifungia KRC Genk goli la kusawazisha dakika ya 55, hiyo ni baada ya Wayne Rooney kuifungia Everton goli la kwanza dakika ya 45 kwa kutumia vyema assist ya Sandro Ramirez.

JE Dada Unahitaji Kuwa Mrembo na Mkaka Kuwa Mtanashati na Rijali.....Waona Hawa Black Beauty

$
0
0
BLACK BEAUTY COMPANY
je Dada unahitaji kuwa Mrembo na ule muonekano bomba wa kisuperstar👌🔥,kaka unahitaji kuwa mtanashati na mvuto zaidi wa KIUME?fika black beauty company utatimiza ndoto zako,hawakosei hata siku moja kwa products original na zenye matokeo yaharaka sana,bila madhara,ni kampuni yenye uzoefu wa hali ya juu sana🔥
1)kuongeza hips,makalio,mapaja@150000
(b)kuongeza hips,makalio,mapaja na miguu@200000/=
2)kuongeza miguu ,kuondoa vigimbi@120000/=
3)kuwa mweupe mwili mzima (Rangi moja)@150000/=
4)Kupungua mwili mzima@150000/=
5)kupunguza tumbo@100000/=
6)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
7)kukuza nywele@100000/=
8)kuondoa michirizi @100000
9)kuondoa madoa,mabaka na chunusi sugu@100000/=
10)kuongeza uume na nguvu za kiume@150000/=
Dawa zetu niuhakika sana100%na utaletewa popote ulipo,mikoani tunatuma,nje ya nchi tunatuma DHL,ofic zetu zipo kariakoo msimbazi police,🔥

karibuni kwa mawasiliano zaidi WhatsApp+255657778924,au call0743534406

au unaweza kutufollow
👇👇👇👇👇👇
@black_beauty_company
@black_beauty_company
@black_beauty_company

Haya Hapa Mahojiano ya HAMISA Mobeto Kuhusu Mtoto wa Diamond......

$
0
0
Tangu ilipoachiwa video ya ‘Salome’ ya mkali wa Bongofleva Diamond Platumz akishirikiana na Rayvanny, kulianza maneno kuwa Diamond anatoka kimapenzi na mwanamitindo Hamisa Mobeto.

Hamisa alikuwa mmoja wa warembo walioonekana kwenye video hiyo. Wiki kadhaa mbele, Hamisa alionekana kuwa na ujauzito na hapo ndipo maneno yalipozidi kwenda mbali zaidi kwamba mhusika wa mimba hiyo ni mwanamuziki Diamond.

Yafuatayo ni mazungumzo kati ya muandishi wa habari na bibie Hamisa Mobeto kuhusu suala hilo:

Hamisa alisema kuwa ni kweli amesekia maneno mengi kuhusu mimba yake akihusishwa mwanamuziki Diamond kama inavyosemwa.

“Huu uvumi unataka niweke wazi maisha yangu. Hilo halitajitokeza kwangu kwani mtu akishaumwa na nyoka akimuona mjusi anamuogopa. Baba wa mtoto wangu mtarajiwa namjua mimi na familia yangu. Nadhani inatosha.

“Sidhani kama ni lazima nimtaje kwenye media (vyombo vya habari) lakini wale wanaosema ni Diamond tafadhali sana, siye. Baba wa mtoto wangu yupo na sio matangazo ya biashara kila mtu majue mpenzi wangu.

“Hao wanaotutukana mbona maisha yao wameyaweka siri, au mimi tu ndiyo nijianike? Siwezi kufanya hivyo, najua nachokonolewa ili niseme lakini sitasema,” amesema Hamisa.

Amesema kuwa kwa sasa yeye ni mtu mpya na kwamba mashabiki wake watamjua kwa kazi zake na siyo maisha yake binafsi kwa sababu ameshajua madhara ya maisha yake hadharani.

“Maisha yangu binafsi yatabaki kuwa yangu mimi mwenyewe ila ya kibiashara yatajulikana na kila mtu. Mimi kwa sasa sihitaji sifa za kijinga, nahitaji mashabiki zangu wafahamu nafanya nini katika jamii na wanishabikie hivyo, sio kwa maisha yangu binafsi,” amesema.

“Kuruhusu ushabiki katika maisha yako binafsi hasa ya mapenzi ni kujijengea uadui na marafiki wa uongo ambao wengi wao wanakuja kinafiki na kujifanya wanakufahamu kiundani au mpenzi wako kumbe ni waongo. Wanataka kuwavuruga na wakifanikiwa hutawaona,” alisema.

HT @ MTANZANIA

UKWELI Mchungu...Bongo Tatizo sio Elimu zetu Tatizo ni sisi Kushindwa Kuwaza nje ya Box

$
0
0
Mpaka sasa nazani hatujaelewa kwa nini Wakina Bil wali Drop Chuo.

Wakina Mark Zuckerberg.

Hawa jamaa na wengine wengi wao tiyari wakiwa vyuoni walisha anza kuwaza nje ya wanavyo fundishwa.

Wenzetu akisha anza kuwaza nje ya anacho fundishwa Haraka haraka husepa ili asipoteze muda yaani Walimu wanafundisha kuelekea Kusini wao wanawaza kuelejea Kaskazini.

KIBONGOBONGO SASA

Sosi tunaamini kwamba ukisomea Udakitari basi piga ua galagaza unapaswa kwenda kuwa Dakitari.

Ukisomea IT basi lazima uwe na laptop yao na ofisi.

Ukisomea Animal sayansi basi unapaswa kuwa kwenye mifugo.

Ukisomea Procurement lazima uwe kwenye Mastoo kama afisa Ugavi.

HATUELEWI HAYA

Dakitari wa Binadamu anaweza maliza na kaanzisha kampuni yake ya Usafiri wa mabasi ila katika usafiri wa mabasi mbele ya safari akaamua kuja kivingine na mabasi ya kubebea wagonjwa pekee yaani mabasi yenye vitanda.
Atatumia sehemu ndogo alio fundishwa hasa kwenye kusafirisha wagonjwa.

Kwamba IT anaweza kuuza karanga lakini kwenye kuuza akaona Adevelop Program au njia ya yeye kuuza karanga kwa utofauti kabisa.

Kwamba Animal Sayansi anaweza baada ya kuhitimu akafungua Microfinance yake ya kutoa mikopo lakini yeye kwa sababu alisomea Nutrion ya Mifugo ili kutatua changamoto za mifugo akawa anatoa mikopo kwa wafugaji wa mifugo pekee ili wanunue vyakula vya mifugo. anafanya hivyo kwa sababu anajua fika mambo ya nutrion na shida wanayo pata Mifugo.

Kwamba Dakitari wa Binadamu baada ya kuhitimu anaweza kwenda kuwekeza kwenye kilimo na ufugaji na kwenye kilimo akalima mazao pia ya kuweza kuwasaidia wagonjwa na akawa anawauzia sana wagonjwa na kwa sababu ana Idea za nutrition ya binadamu..

Hapo ndo kukariri kunapo chukua nafasi kubwa sana ye Elimu zetu.

KUFIKIRI TOFAUTI NI DHAMBI KUBWA MNO KWA SISI WASOMI

By Chasha Poultry Farm

HUYU Ndiye mh. Freeman Mbowe Kiongozi wa Chama cha Upinzani (CHADEMA) Nchini Tanzania Ninayemkubali

$
0
0
(1) Aliipasua CCM vipande vipande mwaka 2015 kwa kumfanya Lowasa kuwa Mgombea kiti cha Urais na kuufanya uchaguzi kuwa mgumu ktk historia ya nchi ya Tanzania Tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya Kisiasa mwaka 1992.

Wafuasi wa CCM mamilioni waliamia CHADEMA na kwa tafiti za awali tu zinaonyesha bado wana hali ya kuja kumpigia kura za kutosha Lowassa mwaka 2020 na inaonyesha wengine watazidi kuiunga mkono CHADEMA maelfu ya wasomi Kutokana na kuitazama nchi kwa jicho la Tatu.

(2) Ndiye aliyekilinda Chama Cha Demokrasia Maendeleo(CHADEMA) kuwa chama Tishio kwa Chama Tawala (CCM). Vyama vingi vya upinzani Barani Afrika viliingiziwa vibaraka wa kisiasa na kuviharibu lakini si kwa CHADEMA ,,,mamluki na vibaraka huhama wenyewe au huumbuka kabla ya njama zao kutekelezeka na hatimaye kutimuliwa mapema .

(3) Ndiye kiongozi ambaye hanunuliki ,,hawezi kuwa kibaraka ndani ya mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania.Wanasiasa wengi wa Afrika hususani wa upinzani ni wanafiki na wasaliti huweza kununulika na vyama Tawala lakini si kwa nguli huyu wa siasa nchini Tanzania.

(4) Ndiye kiongozi anayetafutiwa kashifa ili akose credits za kuongoza CHADEMA na Taifa lakini imeshindikana. Mkumbuke kashfa za madawa ya kulevya . Ile kashifa ipo wapi ? Ikumbuke iliibua taharuki kubwa lakini sijaisikia tena.ILIPOTEA kama upepo .

(5) Ndiye kiongozi aliyewaandaa viongozi wengi wajao watakaopambana na Dhuluma na maonevu ndani ya Nchi mpaka nje ya mipaka ya Nchi .
Nikiwa kwenye Taasisi za Elimu ya juu mbalimbali nilishuhudia vijana wakipokea kweli zake kisiasa na kuwa wakakamavu wa hoja kupitia mikutano yake ya Kisiasa hususani anapofanya mikutano ya waandishi wa habari(Press conference ) kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa na anapozungumza bungeni .

Kweli zake zimefanya wasomi wengi kufanya CHADEMA kuwa jukwaa halisi na la kuaminiwa ktk kuyazungumzia masuala ya Kitaifa hususani yanayolenga kuliondoa Taifa lilipokwamia mfano Kuwaletea wananchi wa Tanzania Maendeleo na kupigania haki zao dhidi wale wote wakandamizaji wa haki .

Kama mnasema Rais Magufuli ni mpigania haki za watanzania mnapaswa kujua kabla hajawepo Magufuli basi CHADEMA ulikuwepo na ndio imeibua kashifa zote za Mafisadi na wala Rushwa Serikalini bila kusahau Biashara ya madawa ya kulevya .

CHADEMA ikishirikiana na CUF ,NCCR mageuzi na wadau wa kupambana na Ufisadi iliibua kashifa za Mabehewa na vichwa vya Treni vibovu ,kashifa ya RADAR,MEREMETA ,ESCROW n.k .Kashifa zote Zilisimamiwa na kujadiliwa vilivyo chini ya Captain Mbowe akiwa kiongozi mkuu wa vyama vya upinzani Bungeni.

(6) Ndiye aliyefanya kila mtanzania kwa asilimia kubwa kuwa Mwanasiasa na mwanaharakati na kuweza kupaza sauti dhidi ya wala rushwa na mafisadi .CCM kiujumla wanaweza kukataa lakini kuna wafuasi wengi wa CCM wamejifunzia kwa Mbowe ujasiri wa kusema ukweli juu ya Ufisadi na wizi wa fedha za Umma ulikuwa unaendelea Serikalini mfano masuala ya ESCROW, RICHMOND, Kashifa ya RADAR, Mishahara hewa,Wafanyakazi Hewa,Usafirishaji wa wanyama Hai nje ya Nchi n.k

(7) Ndiye kiongozi mvumilivu kisiasa Barani Afrika.Mara nyingi kauli zake zimeleta Mshikamano wa kitaifa badala ya kuleta matengano ya kitaifa. Hatakama kaonewa kajitahidi kuwa mwenye Hekima na Busara ktk kutetea haki zake .

(8) Ni mtu anayeitazama Tanzania kwanza badala ya CHADEMA. Ni mtu anayetazama watanzania kwanza kabla ya CHADEMA. Ni mtu wa mikakati kuliko maneno. Ni Simba wa mikakati ya kisiasa na kuthibitisha hilo Mtaona 2019-2020 mwaka 2015 mlishuhudia .

Mh.Freeman Mbowe kwa mwenye Akili Timamu hawezimpuuza hata Mara moja hususani ktk kuleta mageuzi MAKUBWA ya kiuchumi ,Kisiasa na kijamii . Kwa jamii ya kistaarabu na watu wasio na upendeleo Mbowe hapaswi kupuuzwa. Yote Niliyotaja HAPO juu Yana umuhimu mkubwa sana kwa Taifa letu.

Lakini nitaeleza umuhimu wa matukio au mambo mawili kwa kuwa mengine tajwa yamejieleza kiundani . Umuhimu nitakaoeleza ni wa matukio mawili ambayo ni kitendo cha kuigawa CCM vipandevipande na kitendo cha Mbowe kuilinda CHADEMA isiingiliwe na CCM . Twende pamoja ktk kuelezea umuhimu wa matukio hayo mawili,,,,,,,

(1) Kitendo cha Mbowe kuigawa CCM vipandevipande kwa kukubali Lowassa atumie jukwaa la kisiasa la CHADEMA kuwa mgombea Urais mwaka 2015 kuliifanya CCM ianze kujikagua na kuanza kujibadilisha mienendo yake kupitia baadhi ya viongozi wake na watendaji wa serikali Kuifanya nchi ya Tanzania kuwa shamba la bibi.

CCM ilijisahau sana HAPO hapana ubishi ,,,CCM iliamini Kuwa watatawala milele bila shaka 2015 waliamini sasa kwamba IPO siku watang'oka wakiendekeza mambo ambayo wananchi wa Tanzania hawayataki .Nakumbuka mwaka 2014 katibu mkuu wa CCM mh.Abuldulhaman Kinana aliwahi sema kuna mawaziri mizigo ktk Serikali ya awamu ya nne ,,,

sasa mawaziri hao hawa kuwa ni mizigo kwa maana ya vifurushi no walikuwa na kashifa nyingi za Ufisadi na wizi wa fedha za walipakodi masikini wa nchi hiii na kuna mawaziri wengine walisaini mikataba isiyo na tija kwa Taifa bila shaka walisaini kwa faida zao wao wenyewe.

(2)Kitendo cha MBOWE kuilinda CHADEMA isiigiliwe na CCM kama chama Tawala kumekifanya chama cha CHADEMA kuwa kioo cha kujitazamia kwa CCM na Serikali yake kwa miaka takribani 25 ya mfumo wa vyama vingi nchini tokea mwaka 1992 ,,,kwa maana ya kwamba ili CCM ijue imekosea au imepatia lazima itumie CHADEMA kama kioo chake cha kujitazamia ,,,,,na ndio kazi kubwa ya chama cha upinzani chochote chenye nguvu ktk nchi ya kidemokrasia.

Kauli ya Rais Magufuli ya hivi karibuni kwamba "Ukiona adui yako anakushangilia sana na kukusifu ujue umekosea na ukiona anakushambulia sana ujue umepatia''' inaonyesha wazi kuwa CHADEMA ni kioo kwa CCM na CCM inapaswa kuheshimu kioo hiki cha heshima Siyo kukiharibu .

Kioo cha kujitazamia ukikiharibu kuna wakati unaweza ukaenda nje ukadhani USO wako upo vizuri kumbe umebabuka ukatia aibu kwa watu nje.Kukipoteza chama cha CHADEMA ni faida kwa CCM na hasara kwa kitaifa kwani litakuwa likitembea gizani bila kujua nini kinaendelea ndani ya Serikali.

Daima nitasema kweli ,,Unafiki nitauweka kando kwa kuwa yapo maisha baada ya haya Duniani.

#CHADEMA #haiwezi #potea kwa kuondoka kwa Madiwani wenye njaa.

#Kutaka kupoteza #CHADEMA hakutaleta Maendeleo nchini Tanzania Bali ubunifu na utawala bora utaleta Maendeleo nchini.

#CHADEMA haijipotezwa hata wabunge
kununulika waacheni mamluki waende kwao.

#Ukweli haufi ,,uongo hufa.

Mwanahabari Huru

MGODI wa Acacia Waeleza Hasara Waliyopata Baada ya Kuzuiwa Kusafirisha Mchanga

$
0
0
Kampuni ya uchimbaji madini Tanzania, Acacia imetoa mchanganuo wa matokeo ya kuzuiwa kwa usafirishaji wa mchanga wa madini (makinikia) nje ya nchi kwa kipindi cha miezi 6, ambapo inaonyesha kampuni hiyo imepata hasara.

Kwa mujibu wa taaarifa iliyochapishwa katika ukurasa rasmi wa kampuni hiyo janan Julai 21, Acacia ilionyesha kuwa imepata hasara ya Tsh 391.9 bilioni.

Kama ilivyosema awali, kampuni hiyo imezungumzia pia mababdiliko ya sheria ambapo wameeleza kuwa sheria hizo zilizopitishwa na bunge Juni 29 na kuanza kutumika wanaamini zinahitaji kanuni zaidi. Lakini pia wamekubali kuongeza kiwango cha mrahaba pamoja na ada ya ukaguzi wakati wakisafirisha mchanga.

RAIS Magufuli Afunguka...Siogopi Kufungwa.......

$
0
0
RAIS Dkt. John Pombe Magufuli ‘JPM’ amesema yeye kama kiongozi mkuu wa nchi haogopi vitisho vya kufungwa ama kushtakiwa vinavyotajwa na baadhi ya wanasiasa baada ya kuwashughulikia wawekezaji wanaokiuka mikataba na kuhujumu uchumi wa nchi na badala yake ataendelea kuwatetea Watanzania wanyonge ili wapate haki yao.

JPM ameyasema hayo leo wakati akiwahutubia wananchi wa Kigoma katika Uwanja wa Lake Tanganyika mjini humo.

“Hii nchi imejaa mafisadi, wamo wa CCM, Chadema, CUF, ACT, wazungu na wengine hawana chama.

“Siogopi kufungwa, kama mliniteua niwatetee, nitawatetea kwa nguvu zangu zote juu ya majizi, tumeibiwa vya kutosha, madini yetu yanachimbwa yanapelekwa nje na hatupati kitu.
“Wengine wamelipwa pesa ili kupinga tusichukue hatua dhidi ya majizi, nawaambia mimi kama rais nimejitoa kufa na kupona mpaka nihakikishe mali za Watanzania wanyonge haziibiwi na haki yao wanaipata.

“Watambue kwamba sitafungwa badala yao majizi ndiyo yatafungwa. Ilikuwa lazima tubadilishe sheria zetu hatuwezi kuendelea kuibiwa rasilimali zetu,” alisema Rais Magufuli.

JESHI la Polisi Lakana Katu Katu Kuwaandama UKAWA na Chadema.......

$
0
0
Jeshi la Polisi limekanusha madai kwamba linalenga na kutumia nguvu kubwa sana kuvinyamazisha vyama vya upinzani nchini na badala yake limesema kuwa linashughulika na watu wanaovunja Sheria na wakikamatwa wanasingizia kuwa ni kwa sababu ya kuwa kwenye upinzani.

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna Msaidizi wa Polis (ACP) Barnabas Mwakalukwa alisema hayo jana katika mahojiano na alipokuwa akijitambulisha kwa waandishi wa habari.

Amesema kuwa Jeshi la Polisi halina haja ya kumfatilia mtu yeyote mmoja mmoja lakini huwa linaangalia watu wote ambapo baadhi yao wamo wanaovunja Sheria, amani na kufanya makosa mengine.

Alitoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa kuhusu ukamataji unaendelea unaohusisha viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani kama Mbunge wa Kawe – Halima Mdee, ambaye alishikiliwa na Jeshi la Polisi kwa saa 48, Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA wakiwa ni baadhi yao.

Alipoulizwa kuhusu tathmini ya Jeshi hilo juu ya hali ya uhalifu nchini, alisema kwamba matukio ya uhalifu nchini yamepungua sana, hasa kwa yale yanayohusu ujambazi wa kutumia silaha na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi na wazee.

“Kwa sasa changamoto kubwa ni matukio ya ubakaji kwani yanaongezeka kwa kasi na wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari kwa wageni wanaolala majumbani mwao na kwamba wasiwaruhusu kulala kwenye chumba pamoja na watoto wao,” alisema.

Kwa mujibu wa Kamishna Barnabas, matukio ya ubakaji ya aina hiyo yanayohusisha ndugu yanachukua muda mrefu kuripotiwa polisi na hadi muda yanafikishwa polisi, ushahidi unakuwa ushapotea.

HT @ THE CITIZEN

BONGE Movie Hailipi....DUDE Aaamua Kukimbilia Kwenye Kilimo Kwanza

$
0
0
STAA wa filamu za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ ameeleza kuwa kutokana na hali ngumu ya maisha na soko la filamu kuwa gumu amejikuta akiwa kimya na kugeukia kwenye kilimo cha mpunga.

Akipiga stori na Risasi Jumamosi, Dude alisema hivi sasa hali imekuwa ngumu sana hasa kwa upande wa sanaa ya filamu jambo ambalo limemsababisha kuwa kimya na kuamua kwenda kulima mpunga huko mkoani Morogoro huku akiendelea kusubiri soko la filamu angalau libadilike.

“Tumelima mpunga na mke wangu Eva maana maisha ni magumu mno, tunamshukuru Mungu ndiyo tunavuna tumepata magunia kadhaa ambayo yatasaidia kuendesha maisha huku nikipambana na tamthiliya mpaka hapo soko la filamu litakapokuwa vizuri,” alisema Dude.

NYAMA ya Kitimoto Chamharibu Wema Sepetu.....

$
0
0
Siku chache baada ya kubainika kuwa, Miss Tanzania 2006-07 ambaye pia anatisha katika tasnia ya filamu nchini, Wema Isaak Sepetu ni mtumiaji mzuri wa nyama ya Nguruwe ‘Kitimoto’, imeonekana kuwa msosi huo umeanza kumharibu kwa kutokwa na minyama uzembe.

Kwa mujibu wa uchunguzi wetu, kwasasa mrembo huyo ameongozeka unene na kuwa na ‘shavu dodo’ tofauti na ilivyokuwa hapo nyuma kidogo, huku utumiaji wa nyama hiyo ukitajwa kama chanzo.

Akiongea na Mwandishi Wetu, rafiki wa karibu wa msanii huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema kuwa, ulaji wa Kitimoto kwa Wema huenda ukamuathiri kwani kwa muda mfupi ‘figa’ yake imeanza kubadilika.

“Yaani Wema kwa Kitimoto usimpimie kabisa, lakini sasa ulaji wa nyama hiyo umeanza kuuharibu mwili wake kwani katoka minyama uzembe, nimekuwa nikimshauri ale kwa kiasi lakini mwenyewe anaona sio ishu,”alisema shoga huyo wa karibu na Wema.

Katika siku za hivi karibuni, Wema alinaswa akipata nyama ya Kitimoto pamoja na ndizi za kuchoma katika baa moja bubu iliyopo nyuma ya Ukumbi wa Africentre uliopo Ilala jijini Dar es Salaam huku akishushia na kinywaji murua kisicho na kilevi.


Msanii wa filamu ambaye anajulikana zaidi kwa ‘taito’ ya Pacha wa Uwoya, Jacqueline Wolper amepigwa chini kwenye shindano la kusakata muziki, maarufu kama Serebuka.

Za chini chini zinadai kuwa, Pacha wa Uwoya ameburuzwa out ya mashindano hayo yanayosindikizwa hewani na runinga ya TBC1 baada kuwa mtoro kwenye mazoezi.

Aliposakwa kwa simu na kijiwe hiki, Jack hakupatikana hata.

UKWELI Mchungu...Nani Anaweza Kusimama na Kuyapinga Maneno ya Tundu Lissu yote Aliyoyaongea Kuhusu Serikali

$
0
0

Nani anaweza kusimama na kuyapinga maneno ya Tundu Lissu yote aliyoyaongea kuhusu serikali juzi  ?

Hadi sasa wanaojitahidi kuipinga kauli za Lissu juzi hawajamjibu wala kuonyesha uongo wa kauli zake zaidi wanatoa maneno ya kusutana  , msemaji wa serikali hajamjibu kisomi na   Zitto Kabwe nae amaengukia humo humo kujibu kwa kusuta badala ya hoja.

Lissu ajibiwe kwa hoja siyo vijembe.
By PRODA LTD/JF

KUTANA na Tabibu wa Tiba za Asili Maalim Issa Najimu Mwenye Uwezo wa Kutibu Magonjwa.... Tiba Asilia

$
0
0
KUTANA NA TABIBU MWENYE KUBRI KUTOKA KWA ALAH MAALIM ISSA NAJIMU.
NI SHARIFU MWENYE UWEZO WA KUBAINI TATIZO LAKO PUNDE TU UNAPO MFANYIA MAWASILIANO KUPITIA WASAA NA SIKU KWA MAWASILIANO:-
MAALIM ISSA NAJIMU KUTOKA MKOA WA TANGA MWAMBONI MAGOFU KATA YA NGUVU MALI NCHINI TANZANIA,

NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA
QUR-AN, DAWA ZA ASILI PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.

ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE / MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-


ULIJALI (NGUVU ZA KIUME)
MIGUU KUWAKA MOTO
KUTAFSIRI NDOTO
MFARAKANO WA WANANDOA
MFARAKANO KAZINI
KUPANDSHWA CHEO
KUTOA PETE YA BAHATI
ANAO UWEZO WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUBASHIRI
KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA
KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU
MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA.
ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA KUMUOA AU KUWA NAYE.
ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA KWA NJIA YA MSUKULE
ANAO UWEZO WA KUUA KESI SUGU NA PYA NDANI SIKU 7 TU.
MENGINEYO MENGI ZAIDI YALIYO KUWA SUGU


PIGA SIMU-
 Mobile; 0717 70 32 41.
 WhatsApp 06226 535419

MASKINI Tazama Jengo la Ghorofa Saba Ambalo Mmiliki Ameshindwa Kulipa Mkopo Hivyo Kupigwa Mnada

$
0
0
Kampuni ya Udalali ya Yono inatarajia kupiga Mnada Jengo la Abla Complex lenye urefu wa ghorofa saba lililopo Mikocheni Dar es Salaam kutokana na mmiliki wake kushindwa kulipa mkopo anaodaiwa na KCB Bank Limited.

Yono wataendesha Mnada huo August 12, 2017.

TAZAMA VIDEO:

HABARI Mpya Kuhusu Eneka ya Diamond Platnumz Kufanana na Fall ya Davido

$
0
0

Siku chache baada ya mwimbaji wa Bongofleva na kiongozi wa WCB, Diamond Platnumz kuachia video ya wimbo mpya ‘Eneka’ mashabiki na wafuatiliaji wa muziki wa Bongo wanadai kuwa wimbo huo unafanana na wimbo wa mwimbaji staa wa Nigeri Davido unaoitwa ‘Fall’.

Kutokana na stori hizo kushika kasi kwenye mitandao ya kijamii Ayo TV na millardayo.com zimemtafuta producer ambaye alihusika kutenegeneza wimbo huo kutoka WCB, Lizer ambapo amefunguka kutolea ufafanuzi juu ya madai hayo ya Eneka kufanana na Fall.
”Kwanza naweza nikasema hivi huu ni muzuki na muziki pia una style yake inategemea ni muziki wa aina gani unaweza ukafanana. Nimesikia hizo habari kwamba wimbo wa Eneka unafanana na Fall ya Davido lakini naomba kitu kimoja watu waelewe kwamba muziki wa Kimarekani umechanganywa na kiafrika lakini vitakavyobadilika vitabadilika vichache.

“Tusiwe waongo, sisi tunafuata Nigeria wanafanya nini, tusiwe wanafiki kwamba tusiangalie Nigeria wanafanya nini kwa sababu wametutangulia. Kwa hiyo ili tufike kule walikofika wao lazima tupite njia ambazo wanapita wao.
 
“Sioni ajabu kwamba mtu akisema hii imefanana…mi ninachojali ni kwamba watu watapokeaje nyimbo, itapendwa au itafanya vizuri. Hicho ndicho ninachokiangalia zaidi.” – Lizer.

AINA 10 za Waume Ambao Wake zao Wanakereka Kuwa nao

$
0
0
1. Wanaojiona Kama Wafalme (King Husband).
HIi ni aina ya wanaume ambao hutaka kusujudiwa kama wafalme na hupenda kuwafanya wake zao kuwa kama watumwa. Hawafanyi chochote ndani ya nyumba kazi yao ni kutumatuma hata kama mke anaumwa atapaswa kuamka na kupika, wanataka waheshimiwe wao tu na mwanamke akikosea kidogo ni maneno au kipigo. Mwanamke hana kauli ndani na mume akiingia nyumbani ni kama bosi anavyoingia ofisini, wote kimya hakuna hata kuongea.

2. Wanaume Wanaojihisi Bado Hawajaoa (Bachelor Husband).
Hii ni aina ya wanaume ambao hawawashirikishi wake zao kwa chochote. Hufanya mambo kama vile bado hawajaoa, hutumia muda wao mwingi na marafiki zao wakifanya mambo ambayo mke hata hayajui mke anaweza kustukizia tu mume kanunua gari bila kumshirikisha na mume haonyeshi hata kujali kuweza kumshirikisha. Hajali kama ana mke na mda mwingi huutumia akiwa na marafiki kufanya mambo yasiyo na msingi ambayo hayana mnanufaa yoyote katika ndoa yake.

3. Wanaume Wenye Gubu (Acidic Husband).
Hawa hukasirika kila mara tena bila kua na sababu ya misngi, mambo hayaishi, kosa la mwaka juzi anaweza kukukasirikia leo. Wamemuudhi kazini hataki kusemeshwa na mnanuniwa nyinyi, mwanamke akiomba hela ya chakula ni shida ni kununa kutwa nzima, wanahasira na nirahisi kumpiga mke.

4. Mume Wa Kila Mtu (Genarel Husband).
 Hawa wanajifanya wasamaria wema, wanajali kila mwanamke, wanajali marafiki wakike wa mke na wakwao kuliko wanavyowajali wake zao. Mke anaweza kuwa na shida akasema hana hela lakini rafiki akampa. Wana marafiki wengi wakike na mara nyingi huwa hawaachani kabisa na ma X wao, wakiwalalamikia wanawasaidia kuliko hata wanavyowasidia wake zao wakati wakiwa na shida.

5. Wanaume Wanaojifanya Wagumu (Dry Husband).
Hawa wanajifanya wagumu sana, hawana yale mambo ya kimahaba na wao hujua kuwa ndoa ni kuleta chakula tu na kushughulika kitandani. Hakuna kuongea na hawajali hata hisia za mke, mke akiongea kwao wala hawajali wanajifanya ni vidume sana na wanaona mambo kama vizawadi, kupiga simu, kutuma sms, kusema nakupenda, kununua maua ni mambo ya kike, yaani hawaonyeshi juhudi yoyote kuwafurahisha wekea zao.

6. Wanaume Wanaopenda Kutumia Wake Zao (Panadol Husband).
Hawa huwa wanaume pale tu wanapokuwa na shida, wanakuwa na wake wazuri wanaowajali lakini wao wala hawajali. Wanapomhitaji mwanamke, wanapotaka mwanamke awafanyie kitu flani basi huja na maneno mazuri na hata kuleta vizawadi, wanajua udhauifu wa wake zao na huutumia kuwalaghai kuwatimizia mahitaji yao lakini wanapotimiziwa tu basi husahau hata kama wanawake, hawajali tena.

7. Wanaume Ambao Hawataki Kukua (Baby Husband).
 Bado wanatabia za kitoto, hawawezi kufanya maamuzi yao wenyewe mpaka kuuliza kwa ndugu zao, mtu kaoa lakini kila siku humpigia simu Mama yake kuuliza hiki na kile. Yaani wakiongea kitu na mke nilazima aulize ndugu kwanza ndiyo kipitishwa na mke akifanya kosaa kidogo kazi nikulinganisha mke na ndugu zake, mbona flani alifanya hivi, flani anaweza fanya zaidi na mambo kama hayo. Kwakifupi hawawezi kufanya maamuzi na mkewe, ndugu zake hasa Mama yake anakuwa kama shemeu ya ndoa.

8. Mume Mtalii (Visiting Husband).
Hawa wanakuja nyumbani kama wageni vile, mume ataihudumia familia yake kwa kila kitu lakini hawezi kuipa muda wake. Akirudi mke na watoto wamelala ni kugonga na hana sababu za msingi za kuchelewa, hata mwisho wawiki hupenda kutumia na marafiki au ndugu lakini si na mke. Hakuna kitu cha pamoja ambacho anafanya na mkewe au watoto wake, kila akiingia tu anakua na safari ya kutoka yaani hata atoke akakae nnje tu lakini si kukaa na mke au watoto.

9. Wanaume Wanaofuatilia Kila Kitu (Stalking Husband).
Hii ni aina ya wanaume ambao hufuatilia kila kitu, huchunguza kila kitu mwanamke anachofanya na hawampi pumzi. Akienda sehemu atachunguza anaenda na nani na alikutana na nani, huwa na wivu wa ajabu ajabu na kila saa huhisi wake zao ni wasaliti. Kila mtu mwanamke anayeongea naye wa jinsia tofauti huhisi ni mchepuko na hata marafiki wa mke wakike pia huhisi wanamkuwadia, kwakifupi hampi pumzi mwanamke.

10. Mwanaume Mbahili (Miserly Husband).
Huyu anaweza kuwa na hela lakini mbahili ajabu. Akimpa mwanamke hela atafuatilia matumizi yake mpaka senti ya mwisho, anafuatilia mpaka mambo ya jikoni. Sukari ikiisha naataka ajue iliisha ishaje na kila mara huhisi mke anamuibia hela labda akajenge kwao, huwa msumbufu sana na mgumu kutoa hela. Mwanamke akifikiria mchakato wa kuomba hela kwa mume hukata tamaa na wakati mwingine kuamua tu kukaa kimya na matatizo yake.

MUME Wangu Hafiki Kileleni ni Kawaida au Matatizo?

$
0
0
Habari zenu wapendwa, Weekend nilipata mgeni ambae ni ndugu yangu, ameolewa ana miezi 3 tu, lililomleta hasa ni kutafuta ufumbuzi anasema tangia ameolewa Mume wake alifika kileleni siku ya Honey Moon tu wana miezi 3 sasahivi hajawai fika tena lakini akiingia uwanjani anaweza ata kukesha tatizo ni hilo hafiki mwisho, amemuuliza kwanini anasema nayeye hajui kwanini, nimeona niwaletee nyinyi wana JF mabingwa wa TIBA ya kila tatizo, maana mdogo wangu amekosa amani ameshaanza kuona kupata watoto itakuwa ndoto

CCM Yatoa Mpya..Sasa Kutoa Mikopo Kwa Wanafunzi Vyuo Vikuu

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wake, Humphrey Polepole kimetangaza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini ambao wamekosa mikopo ya kuendelea na masomo na wanafunzi ambao ni yatima.

Taarifa iliyotolewa na Polepole inasema kuwa wanafunzi hao wanapswa kufika katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili waweze kusaidiwa shida zao hizo za mikopo, jambo ambalo limepokewa tofauti na baadhi ya watu wakidai kuwa suala la kutoa mikopo kwa wanafunzi ni jukumu la bodi ya mikopo.

Kutokana na mitazamo ya watu kuwa tofauti katika jambo hili, Humphery Polepole aliibuka na kusema kuwa upinzani wa Tanzania ni mtihani mkubwa kwani wanapojaribu kutatua matatizo ya watu wanakujua juu na wasipotatua matatizo pia wanakuja juu.

"Tukikaa kimya kwa shida za watu inakuwa tatizo, tukishughulika na shida za watu inakuwa tatizo kubwa. Huu upinzani mtihani" alisema Polepole
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live




Latest Images