Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Beka Flavour Amtupia Dongo Kiana Mwimbaji Aslay...Adai Hamuogopi......

$
0
0
Beka Flavour Amtupia Dongo Kiana Mwimbaji Aslay...Adai Hamuogopi......
Mwanamuziki anayefanya vizuri na ngoma yake ya 'Nibebe', Beka Flavour amefunguka na kusema Aslay siyo msanii mkubwa wa kumuangalia wakati anafanya kazi zake na badala yake Alikiba ndiye kioo chake kwa Tanzania.


Beka amelazimika kusema hayo baada ya kuwepo minong'ono kuwa huenda anamuogopa msanii huyo ambaye zamani walikuwa wakifanya kazi pamoja kama kundi la 'Yamoto Band' kabla ya kila msanii kuanza kusimama mwenyewe.

"Mimi natoa nyimbo zangu kulingana na jinsi ambavyo nimepanga ratiba yangu na uongozi wangu. Sijashindwa kuachia wimbo eti kwa sababu Aslay katoa ngoma mpya ila matatizo niliyopata ya kupelekwa polisi ndiyo yaliyonifanya nisogeze vitu mbele," Beka alifunguka mbele ya kamera za eNewz
Beka aliongeza kuwa "Aslay siyo msanii mkubwa kusema kwamba mimi nimuogope au nimfikirie. Hapa nchini msanii mkubwa ni Alikiba na ndo kama kioo najitazama lakini siyo Aslay. Mimi natazama wasanii wakubwa nje ya nchi lakini siyo ndugu yangu".

Pamoja na hayo Beka amedai hataweza kumvumilia tena msanii huyo ambaye amefululiza kutoa nyimbo nyingi hivi karibuni endapo ataachia tena kazi mpya.

"Nimepanga kuachia wimbo mpya wiki mbili zijazo lakini kama Aslay akiachia tena kazi mpya sitaweza kumvumilia na mimi nitaachia mashine ili zipambane mbele kwa mbele maana mimi nimeshapanga ratiba zangu na siwezi kuzivunja," aliongeza.


Mtoto Mwenye Jinsia Mbili ya Kike na Kiume Amtoa Mama yake Machozi...Madaktari Wafunguka

$
0
0
Mtoto Mwenye Jinsia Mbili ya Kike na Kiume Amtoa Mama yake Machozi...Madaktari Wafunguka
MSICHANA wa miaka 19, Elizabeth Chengula anaelezea anavyoishi maisha ya shida ambayo ni pamoja na kupata mtoto mwenye tatizo la utata wa jinsi yake huku madaktari wakifafanua tatizo hilo kitaalamu.

Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Chengula alisema Agosti mwaka jana alijifungua mtoto ambaye aliambiwa katika Zahanati ya Ifisi iliyoko Mbalizi Mbeya Vijijini kuwa mtoto huyo ni wa kiume, lakini siku zinavyozidi kwenda hajui ni wa jinsi gani baada ya maumbile yake ya siri kuwa hayaeleweki ni ya kike au ya kiume. Chengula alisema alipompeleka hospitali huko Mbeya aliambiwa kuwa tatizo hilo ni mpaka ampeleke Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), lakini kutokana na hali yake ya maisha kuwa duni, hakuwa na uwezo wa kufika Dar es Salaam iliko hospitali hiyo.

“Hali hii ilinichanganya sana nikaenda kuomba msaada Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, walinisaidia nikachangiwa pesa kwenye ofisi yao ikapatikana laki mbili na orobaini, nikapewa kwa ajili ya safari pamoja na barua ya rufaa, hata hivyo pesa hizo ziliibiwa zote pamoja na begi langu nikiwa safarini kuja Dar es Salaam,” alieleza msichana huyo. Akielezea maisha yake, alisema mama yake ni mlemavu wa mikono na miguu ambaye hawezi kujishughulisha na kitu chochote na yeye na mama yake wanaishi kwa ndugu yao ambaye anafanya vibarua vya kubeba mizigo ya watu sokoni Mbalizi.

“Maisha yangu ni ya shida sijui nitapataje msaada wa mtoto huyu ambaye nimeambiwa Muhimbili anatakiwa kufanyiwa vipimo na baadaye kufanyiwa upasuaji na mimi sina mtu yeyote wa kunisaidia,” alisema Chengula kwa masikitiko. Aliongeza kuwa pamoja na kwamba hana uwezo wa kumsaidia mtoto wake, lakini anaamini atapata msaada mtoto wake aweze kuwa kama watoto wengine ingawa baba wa mtoto huyo alimkimbia baada ya kuambiwa mtoto ana tatizo.

“Baba wa mtoto alisema hamtaki mtoto na nisimpe jina lake mtoto huyu ni mkosi hataki kujihusisha naye, nahangaika peke yangu nikipata watu wa kunisaidia nitashukuru kwa sababu mimi naamini sio mkosi na atapona,” alieleza msichana huyo. Aidha, alisema katika kipindi chote hicho amemlea mtoto wake kama wa kiume na alimpa jina la kiume ingawa hajui jinsi yake.

“Kipindi chote hicho mimi namlea kama mtoto wa kiume kwa mavazi na jina nimempa la kiume, sasa nikiambiwa ni wa kike sijui nitaenda kuwaambia nini watu kule nyumbani, nadhani nitahama kabisa na sijui nitaenda wapi maana hawatanielewa,” alibainisha. Watoto kuzaliwa na jinsi mbili au isiyoeleweka Daktari Bingwa wa Upasuaji kwa Watoto, Zaituni Dkhary akizungumzia tatizo hilo, alisema mzazi yeyote anaweza kupata mtoto wa namna hii na kwamba tatizo hilo sio mkosi.

Dk Dkhary alisema wazazi mwanzoni huwa wanachanganyikiwa kwa sababu hawajui kama wataweza kuwa kawaida yaani wa jinsi moja walivyo watu wengine au la, lakini tatizo hilo lina ufumbuzi. “Na hakuna kesi yoyote ambayo tumeipata mzazi kurudi kulalamika kwamba kuna hali tofauti imetokea baada ya kuwasaidia, hapa Muhimbili tunawafanyia upasuaji vizuri kabisa kuwarekebishia maumbile na wanakuwa sawa kabisa,” alieleza Dk Dkhary.

Alisema madaktari wanaofanya upasuaji huo ni madaktari bingwa wa upasuaji wa watoto (Pediatric Surgeon) au madaktari bingwa wa upasuaj wa njia ya mkojo (Urologist Surgeon) na kama kuna kesi ngumu wanaweza kusaidiana lakini upasuaji huo ni wa kawaida kabisa. Daktari huyo alisema watoto ambao wanazaliwa wakiwa na maumbile hayo ni vigumu kuelewa jinsia yake kwa kumtazama kwa macho katika sehemu zake za siri kwani wanakuwa na viungo vya jinsia ya kike na pia ya kiume.

“Watoto hawa kwa mzazi hata mzalishaji inakuwa ni vigumu kutambua kwa kuangalia kwa sababu ukimuangalia mtoto sehemu zake za siri anakuwa na kiungo cha kiume na pia maumbile ya kike na kwa chini anakuwa na tundu la kukojolea,” alieleza. Anasema katika hospitali hiyo wanapokea watoto waliozaliwa katika hali hiyo wengi ambapo karibu kila wiki wanawafanyia upasuaji wa kurekebisha maumbile baada ya kuwafanyia vipimo mbalimbali na kubaini jinsi yake.

“Kama ni mtoto wa kike utamfanya awe wa kike kwa kurekebisha maumbile yake, na kama ni wa kiume hivyo hivyo, na ni lazima kufanya vipimo kadhaa kwanza ili kuhakikisha jinsi ya mtoto,” alisema na kuongeza kuwa hakuna sababu maalumu inayoweza kusababisha kupata mtoto mwenye tatizo hilo.

Alitaja vipimo hivyo kuwa ni pamoja na vya damu kujua vinasaba vya mtoto na pia kuchukua kijinyama kwenye mdomo wa mtoto kupima baada ya kuiotesha pamoja na kipimo cha MRI kuona viungo vya ndani vya mtoto ni vya jinsi gani.

VIDEO: Alichozungumza Mke wa Tundu Lissu Baada Mume wake Kukosa Dhamana

$
0
0
 VIDEO: Alichozungumza Mke wa Tundu Lissu Baada Mume wake Kukosa Dhamana
Leo July 24,2017 Rais wa TLS na mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amefikishwa ktk Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa kosa moja la kutoa lugha ya uchochezi.

Hata hivyo, Lissu amerudishwa baada ya kukosa dhamana kutokana na pingamizi lililowasilishwa na upande wa mashtaka. Kesi imeahirishwa hadi July 27, 2017 kwa ajili ya Hakimu Mashauri kutoa uamuzi kama Lissu apate dhamana au la. Nje ya mahakama hiyo, Mke wa Lissu Alicia Magabe amezungumza haya…….

’Kwa kweli sikutarajia maamuzi kuhusiana na kesi yake, ameshawekwa mahabusu mara nyingi sana namjua yuko imara sana– Alicia, Mke wa Tundu Lissu

Hii hapa chini ni video ya Mke wa Tundu Lissu akiongea

Wanaotaka Mh. JPM Aongezewe Muda Wana Hoja, isipokuwa Kuna Sehemu Hawafiki

$
0
0
Wanaotaka Mh. JPM Aongezewe Muda Wana Hoja, isipokuwa Kuna Sehemu Hawafiki
Nikiri tu kwamba nami ni mmoja wa watu ambao naiona dhamira ya dhati ya Mh. Rais wa awamu ya tano katika kulisaidia taifa letu. Kutokana na kauli zake na matendo yake ni wazi Mh. ana kiu ya kuona mabadiliko ya haraka kwa nchi yetu. Mh. anatamani kuona kila mtu anatembea kwenye nyayo zake ili kuifikia kwa haraka dhamira yake njema. (Ingawa kuwa na dhamira njema pia kunategemea sana njia bora za kuifikia dhamira hiyo)

Kitu nachokiona, kuanzia mh. mwenyewe mpaka wafuasi wake yaani sisi tunaoamini katika dhamira yake njema, tunaona kabisa kwa muda wa kikatiba uliopo ni ngumu kuifikia dhamira njema aliyo nayo mh. Na hapo ndipo tatizo linapoanzia. (

Kutokana na athari za kuona muda ni mdogo, mh. amekuwa akitaka mambo mengi yabadilike kwa haraka kitu ambacho ni ngumu kutokea, matokeo yake ndipo watu wanaona kama mh. anakurupuka kumbe la hasha ni kule kutaka kukimbizana na muda tu.

Kwa upande wa wafuasi nao wameshindwa kabisa kuamini kwamba baada ya muda huu mfupi kuisha atatokea mtu mwingine atakayekuwa na dhamira ya dhati kama ya Mh. JPM. Wengi nikiwepo na mimi tuna wasi wasi pengine mtu ajaye anaweza akaturudisha kule kule tulipotoka, ndipo sasa wanapoona suluisho pekee ni kumuongea muda Mh. JPM (Hapo ndipo tunapoachana na wenzangu walio wengi)

Angalau juzi nimemsikia Mh. Kule Kigoma akitamka kwamba yeye anataka amtengenezee Rais anayemfuata njia ya kuongoza vizuri. Tena akajifananisha na Yohana wa katika Biblia aliyemtayarishia mapito Yesu/Issa bin Mariam. Kumbe Mheshimiwa ana mpango hata wa kutaka kuongezewa muda. Kwa maelezo hayo ina maana wale wanaotaka mh. aongezewe muda wana hoja lakini kuna sehemu moja tu ambayo hawafiki; Tumeshuhudia huko nyuma wakuu wa nchi wakibadilisha badilisha mambo mengi kulingana na wanavyoona inafaa. Mengine yalileta manufaa, na mengine ndio yametufikisha kwenye matatizo haya tuliyo nayo leo.

Sehemu pekee ambayo wenzangu hawataki kufika ni kwenye marekebisho ya katiba. Baba yetu Magufuli chonde chonde tuachie katiba mpya baba. Na katiba hiyo si nyingine ni ile ya Mh. Warioba. Kwa kutupa/kutuachia katiba safi, si tu itakupa heshima na kudhihirisha wazi dhamira yako njema, bali itafanya hata anayekufuatia kutokuturudisha kule kule tulipotoka. Lakini pia itatupa meno meno na sisi kuwashughulikia wawakilishi wetu wa hovyo. Kwa katiba ile hata hawa wawakilishi wanaosadikikika kuwa wachochezi, tutawaondoa wenyewe maana tutakuwa tumepewa meno ya kuwaondoa.

Nakaribisha majadiliano yenye afya.

By Dmketo

Breaking News: Majina ya Vyuo 19 Vilivyozuiwa Kuandikisha Wanafanzi Mwaka 2017/18

$
0
0
Breaking News: Majina ya Vyuo 19 Vilivyozuiwa Kuandikisha Wanafanzi Mwaka 2017/18
Breaking News: Majina ya Vyuo 19 Vilivyozuiwa Kuandikisha Wanafanzi Mwaka 2017/18

Rais Kikwete Akosoa Wanaozuia Watu Kwenda Kutibiwa Nje ya Nchi.......!!!

$
0
0
Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete jana aliibuka na kutolea utetezi kufuatia Benki ya Dunia (WB) kukosoa serikali za nchi za Afrika Mashariki namna zinavyoshughulikia maendeleo ya sekta ya afya, na jinsi viongozi walivyoshindwa kuboresha huduma hiyo muhimu kwa jamii, huku wao wakisafiri kwenda nje kutibiwa.

Akizungumza katika ufunguzi wa watoa huduma za afya, wamiliki wa vituo vya afya na wataalamu wa afya kutoka nchi za Afrika Mashariki na nje ya Afrika, Rais Kikwete alisema kuwa, kusimama kwenye majukwaa na kusema kuwa, watu kwenda kutibiwa nje ya nchi ni kupoteza fedha, jambo hilo si sahihi.

Alisema, serikali za Afrika Mashariki zimekuwa zikijitahidi sana kuhakikisha zinaboresha sekta za afya, lakini akatahadharisha kwamba, maendeleo ya kiwango cha juu kama nchi zilizoendelea hayawezi kupatikana kwa usiku mmoja.

Akieleza sababu kubwa inayopelekea watu kwenda kutibiwa nje ya nchi, Rais Kikwete alisema ni kutokana na upungufu wa wataalamu katika nchi hizo. Akitolea mfano Tanzania ambapo kuna wataalamu watatu wa upasuaji wa mishipa ya fahamu ambapo kwa kawaida hawawezi kuwahudumia wananchi ambao ni milioni 50.

Rais Kikwete aliisihi Benki ya Duania (WB) kutumia suala hilo kama changamoto kwa kuziwezesha nchi za Afrika Mashariki kuboresha sekta ya afya badala ya kutoa lawama kwamba serikali hazifanyi jitihada jambo ambalo si sahihi. Wananchi wanalalamika, sasa na wewe (mwakiliashi wa WB) hautakiwi kuwa katika nafasi ya kulalamika bali kuhakikisha fedha za kuboresha sekta ya afya zinaletwa, alisema Rais Kikwete.

Akizungumza kabla ya Rais Kikwete, mwakilishi wa WB, Khama Rogo alionyesha kushangazwa na wananchi wa nchi hizo kupoteza maisha kutokana na magonjwa kama vile, malaria, kutapika, kuharisha huku viongozi wa nchi hizo wakienda kutibiwa nje ya nchi.

Rogo alisema mara nyingi huwa anasikia viongozi wa Afrika wamekwenda kupatiwa matibabu nje ya nchi jambo ambalo yeye linamkera kwani anaona badala ya wao kuimarisha miundombinu ya ndani wanapoteza fedha nyingi kwenda kutibiwa nje ya nchi. Katika hali ya masikitiko, alisema, mara nyingi anaposikia suala la afya kutoka nchi za Afrika, ni mtu amefariki.

Mkutano huo uliohudhuriwa na nchi 12 pia ulituma ujumbe wa wahudumu katika sekta ya afya, kutoa huduma sahihi na kwa wakati ili kuweza kupunguza vifo vinavyoepukika.

Mke wa Mshikaji Wangu Aniduwaza!!

$
0
0

Jana nimeduwazwa sana baada ya mke wa rafiki yangu kunitamkia wazi kuwa ananipenda na anataka kutoka na mimi.
Tangu nifahamiane naye miaka takribani mitano sasa tumekuwa tukiheshimiana naye sana kama mashemeji. mwaka huu akaniambia kuwa mumewe ameanza kubadilika kwa kuzidisha ulevi, kuchelewa kurudi nyumbani na wakati mwingine kulala nje na pia alizifuma meseji za mapenzi kwenye simu ya mumewe kutoka kwa mtu aliyemsave kwa jina la kiume, hivyo nimsaidie kumshauri ili abadilke ila akanionya nisimwambie kama ni yeye ndiye kaniambia.

Nilimtia moyo kuhusu hali hiyo na kumwomba awe mvumilivu na asichoke kuongea na mumewe kuhusu hali hiyo ili abadilike. Binafsi nilipata wakati mgumu wa namna gani nitamshauri jamaa bila kumtajia makosa yake na wapi nimeyapata hivyo nikashindwa hiyo kazi.

Mke wa jamaa akaanza kunipigia simu usiku kulalamika kila mumewe anapochelewa kurudi na wakati mwingine akinipigia alfajiri kuniambia kuwa mumewe hajarudi hadi muda huo. Niliendelea kumtia moyo ingawa mambo hayo yalikuwa ni ya kweli.

Cha ajabu kuanzia wiki jana amekuwa akinitumia meseji za mapenzi, nikajua ni hizi meseji ambazo watu hutumiana hivyo sikujali sana hadi pale aliponiandikia akiniambia kuwa yuko serious anataka kutoka na mimi. Sikuamini nikampigia simu kusikia sauti yake kama ni yeye kweli, ndipo aliponithibitishia kuwa yuko serious na atatunza siri na kunitunzia heshima yangu kwa jamaa kwani tayari moyo wake umeangukia kwangu.

Sikuweza kumjibu kitu kwa namna nilivyopatwa na mshangao. hadi sasa anaendelea kunibembeleza na kunipa mbinu nyingi za kutimiza lengo lake bila kujulikana na watu.

Binafsi sina lengo la kumsaliti mshikaji wangu ila nimelileta kwenu ili mnishauri nimjibu vipi huyu mwanamke ili heshima yangu kwa familia hii iendelee kuwapo na pia kusitokee chuki yoyote kutokana na kadhia hii itakayopelekea urafiki wangu na familia hii kuyumba au kupotea.

SIKILIZA Wimbo Mpya wa Rosa Ree & Navy Kenzo – Mchaga Mchaga

$
0
0
Female Rapper ambaye anatisha kwa sasa Bongo, Rose Ree kutoka label ya The Industry ameachia ngoma mpya ‘Mchaga’ ambayo amewashirikisha Navy Kenzo, prodyuza wa ngoma hii ni Nahreel. Hii inakuwa kolabo ya pili kwa Rosa Ree baada ya remix ya ngoma ya One Time aliyompa shavu Khaligraph Jones kutoka nchini Kenya.

VIDEO:

Mwanamke Mzuri wa Sura, Umbo Zuri and Classic lakini Chini Anatoa Harufu..

$
0
0
Kwa muonekano wa nje ni msichana mzuri sana mwenye kila sifa ya urembo, msafi anajua kuongea mpaka unamtamani awe zaidi ya rafiki mpenzi na kadhalika blah blah. nimeamua niseme manake nimekaa nalo nimeona niwaambie tu wadada labda itakuwa ushauri kwenu na manufaa kwenu mtajirekebisha. pia anaonekana she is hard to get, unamchombezea unafanikiwa kila kitu na siku ambayo ni zaidi ya mara moja kuja getho na kidume unajisemea ndio wakati muafaka wa kumchinja mnyama.

mnaanza kidogo kidogo taraatibu, romance, kisha kuchojoana kidogo kidogo, mnamalizana chojoa zote inabaki ile tu inayofunika ikulu . ile ya ikulu kuanza tu kuichojoa ndio hapo ninapoanza kusikia harufu ya "panya kafwa" . kama vile siamini kutokana na uzuri wa mtoto, kisha mtu mzima ili kuhakikisha ni kweli harufu inatokea wapi najisogeza kichwa na pua karibu na kitovu kisha nashuka taratibu karibu na "ikulu", agkhaaa mama pua zangu "ni kweli panya kafwaa" na kafia kwenye "shimo la ikulu".

pamoja na harufu yote kali siwezi muacha mtoto ngoja nimuonje kiduchu ili tu anione kidume moyoni najisemea. chomeka na kuanza piga mzigo na hapo stimu zimehama nataka tu mtoto nione amejilegeza kama mara 2 au 3 , kisha ndio nichomoke zangu kutoka shimo la panya. mtoto akajilegeza mara 2 na kisha ya 3, nami nikamaliza mambo yangu. hapo kichwa kinaniuma manake najua nikichomoa tu na hiyoo harufu iliyopikwa humo itakavyotoka, nitahitaji air fresh za kutosha baadaye!!

nachomoka zangu na huku pua nimezibana sababu harufu ya "panya kafwa" imezidi, nakimbilia bafuni nikajitoe maharufu ya mzoga wa panya!! cha kushangaza yule mtoto sijui haisikii harufu au ameizoea anahisi ni kawaida sielewi!! natoka bafuni na kumwambia na yeye aende akjiswafi, wakati yupo bafuni ninakakumbuka kale kademu kangu amabacho ni cha kawaida sana, washikaji wanachoniambia sina hadhi nacho, nje ana uzuri wa kawaida sana, japo ndani ni mzuri kupita kiasi ni mtamu wa ajabu na msafi mpaka baasi, nahisi utamu wake unasababishwa na usafi wake....!!!

na ukweli ni kwamba ninaishuhudia hiii zaidi kwa wale mademu ambao nje ni wasaafi na wazuri ajabu hata huwadhanii kama ndani wanaweza kuwa wameficha "panya aliyekufa"!!!

ushauri wabure kwa wadada mkiwa wasafi nje, wekeni na mazingira ya ndani yawe safi zaidi, mimi siamini mtu kama unanuka eti hujijui..!! utashangaa unaachwa bila sababu pamoja na uzuri wako!!

By Mdau

Mrembo Huddah Afanikiwa Kumnasa Wizkid Katika Himaya yake.....

$
0
0
Baada ya kutamka kupitia mtandao wa Snapchat kuwa anampenda na anatamani kuzaa na mwanamuziki Wizkid, mrembo Huddah amesherekea ushindi wa kumnasa tena mkali huyo siku ya Jumamosi.



Wizkid ambaye kwa sasa ameachia mixtape yake Sounds from the other side ‘SFTOS’ aliweza kuangusha bonge la show licha ya kuwa na mvua kubwa ndipo walipokutana wawili hao.

Kwa mujibu wa mtandao wa Snapchat ya mrembo huyo ameandika “Everything was a mess last night! But i had fun.Great laughing out loud with Daddy yo! Gang! Gang! foevaa!.”

Rais Magufuli Afunguka "Ukiona Mtu Anapiga Kelele Wananchi Wake Waendelee Kuwa Masikini Ujue Amemeza Kitu Ndani"

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaania, Dkt John Pombe Magufuli amezungumza mambo mbalimbali akiwa ziara mkoani Singida na leo amezindua barabara ya Manyoni – Itigi – Chaya yenye urefu wa KM 89.3.



Tazama nukuu zake hapa:

-Kabla sijaongea chochote naomba tuwaombee Mashujaa wetu walioitetea nchi yetu. Naomba tuiname tuwaombee

-Watanzania naomba tuwe tunakumbuka mahali tulipo toka, mahali tulipo na mahali tunapoelekea

-Tanzania ninayoipenda ni Tanzania yenye umoja, Tanzania yenye upendo, Tanzania inayomtanguliza mbele Mungu

-Tunataka tuwe na umeme wa uhakika ili tuweza kuwa na Tanzania ya viwanda tunayoitaka

-Wakati wa kukaa kwenye magenge na kushinda kwenye pool kukaa kupiga stori kwamba tutaletewa chakula cha bure, hakuna.

-Utajiri hautakuja kwa wavivu, lazima niwaeleze ukweli. Niwaombe wana Itigi wakati wa kukaa kwenye magenge umepita

-Mimi ndiye Rais, hakuna anaejua siri za Serikali kama Rais. Leo mmepata Rais anaewaambia ukweli
Kosea hata kuoa, utatoa hata talaka ila usije ukakosea kuchagua

-Ukiona mtu anapiga kelele wananchi wake waendelee kuwa masikini ujue amemeza kitu ndani

-Kazi ya kutumbua ni ngumu unaweza ukajikata, unaweza ukarukiwa na usaa . Inadepend hilo jibu limekaa sehemu gani

-Na leo watoto wote wanakalia madawati awe wa Chadema awe wa Tundu Lissu anakaa

-Ni mataifa machache duniani yanayosomesha watu wake bure, hata Ulaya hawafanyi hivyo ndugu zangu

-Ndege ya abiria 262 yenye uwezo wa kusafiri moja kwa moja kutoka Marekani inakuja mwakani

-Waliojenga kwenye hifadhi ya reli waanze kujiandaa kisaikolojia, wanaweza kuanza kubomoa taratibu nyumba zao

-Ma-DC na Ma-RC, sitoi chakula kama kwako kuna njaa, wilaya ikiwa na njaa wewe DC hufai kuwa DC, na wewe RC hufai

-Nataka Tanzania iwe kama Ulaya. Tutafika tu lakini tutabanana

– TanRoadS ni ya 3 kwa uchapaji kazi Afrika

-Suala la ubinafsishaji mimi silipendi kabisa, siwezi nikawalaumu waliofanya hivyo, lakini kuacha kusema siwezi

-Nikiondoka mimi hakuna atakayekuwa kama mimi, nasafisha njia ya Rais atakayekuja

Taarifa ya Wabunge wa CUF Kufukuzwa na Pro.Ibrahim Lipumba Yafika Kwa Spika Wabunge....Afunguka Haya

$
0
0
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amesema amepokea taarifa kutoka kwa Mhe. Ibrahim Lipumba Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha wananchi CUF, Ibrahim Lipumba ya kuwafukuza wabunge na 8 na Madiwani wawili.Baada ya kuitafakari barua hiyo Spika amesema atoa maamuzi.

Kutana na Mtabibu wa Tiba Asili...Unasumbuliwa na Mapenzi na Hela Hazikai...Jibu Lipo Hapa

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shalifu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Shalifu Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Maalim Shalifu Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..

Mengi zaidi +255 629793352 au 0679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

JPM amefunika Nyayo za Nyerere - Professa Norman Sigalla

$
0
0

Mbunge wa Makete Prof. Norman Sigalla amemsifu Rais wa Awamu ya tano kuwa amefuata nyayo za Mwalimu Nyerere kutoka na matendo yake yatanabaishwa kwenye hutuba za Baba Taifa

"Mambo mengi yaliyozungumzwa kwenye hotuba za Mwalimu Nyerere ndiyo yanayoonekana kwa Rais Magufuli"

Hayo ameyasema leo kwenye ziara ya rais Magufuli Mkoani Singida

Professa Sigalla ameongeza kuwa Vyama vyetu tuviweke pembeni wote tumuunge mkono Rais

Hatimaye Mwanamuziki Linah Sanga Ajifungua Mtoto huyu

$
0
0
Hatimaye Mwanamuziki Linah Sanga Ajifungua Mtoto huyu
Neema ya Mtoto yamshukia Msanii wa kike wa Bongo Flava Lina Sanga Mapema leo hii kwa Kujifungua Mtoto wa kike.

Lina  mwenye KIbao chenye kubamba cha Jipe Raha amejifunga salama

Aliyemuita David Kafulila Tumbili Aibuka

$
0
0
Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Jaji Fredrick Werema ameibuka na kueleza juu ya kauli yake ya  kumuita 'Tumbili' Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David Kafulila

ni siku chache Tangu Rais John Magufuli kuwaeleza kwamba waliomuita Mbunge huyo Tumbili wao ndio watakao kuwa matumbili

walema amempongeza Kafulila kwa ujasiri wa kutete Maslahi ya Umma na kwamba alionyesha uzalendo wa hali ya juu unaopawsa kuigwa.

Walema ameeleza kuwa watu hawakuelewa alichomaanisha na kwamba alieleza kuwa" tumbili haamui mambo ya msituni, na huo ni msemo wa kawaida tu"

Magufuli Amtolea Uvivu Lissu

$
0
0

Rais John Magufuli amesema kuwa Serikali imetatua Changamoto mbalimbali pamoja na Madawati  kwenye Jimbo la Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

"Tumetatua changamoto ya madawati...sasa hivi hata watoto wa TunduLissu wanakaa"

Magufuli amesema kuwa kuna "Wengine mmewachagua lakini wanaongelea ya Dar es Salaam tu...Kosea kuoa unaweza kutoa talaka, lakini usikosee kuchagua"

Chemical Afafanua Kubadilisha Muonekano wake

$
0
0
Rapa wa kike anayefanya vizuri na ngoma ya 'Queen Of Dar es salaam', Chemical ameweka wazi sababu ya kukubali kubadili muonekano kwenye video mpya ya Msami 'So Fine' iliyotoka hivi karibuni ni kutaka kujiona yeye mwenyewe kwenye muonekana mpya.

Akifanya mahojiano na EATV Website, Chemical amesema baada ya Msami kumuelekeza kwamba anamuhitaji Chemical wa aina gani ilimfanya awe mpole hata wakati wa kufanyiwa 'Make up' ili kipatikane kitu ambacho kilidhamiriwa ingawa siyo mashabiki zake wote waliofurahi kumuona katika muonekano wa aina hiyo.

"I was so excited like Ok na mimi nataka kujiona nitakuaje kwa hiyo kuanzia make up mpaka mavazi hakuna mahali niliongea niliambiwa vaa hivi nikakubali na kila kitu alikuwa ni Msami.  Kwa hhiyo watu wasiseme kwa Chemical hawezi kuwa hivi au kuvaa hivi nataka tu wajue kwamba naweza kuwa mtu yoyote ambaye nataka kuwa" amesema.

Pamoja na kuonekana na mabadiliko makubwa katika video hiyo Chemical amedai kuwa hawezi kuwaahidi mashabiki zake kama ataweza kuendelea na muonekano mpya au ule wa zamani kwani yeye ni msani.

"Chemical ni yuleyule kama kutakua na mabadiko yanahitajika kufanywa yatafanyika lakini muonekano wangu wa awali ulinitambulisha na watu walinikubali vile nilivyokuwa. Nilifanya vile pia kujua  watu wanamtaka chemical wa aina gani ingawa mpaka sasa ni 50/ 50 wapo walionikubali lakini wapo walioponda" ameongeza

Hatimaye Jaribio la Kifaa Kinachowalinda Wanawake Dhidi ya HIV Lafaulu

$
0
0
Watafiti nchini Marekani wanasema kuwa jaribio ambalo vijana wa Marekani walitumia mpira wa mviringo kujilinda na virusi vya HIV limefanikiwa.

Utafiti zaidi sasa utafanyiwa vijana barani Afrika.

Wasichana walitumia mviringo wa plastiki uliowekwa dawa za kujilinda na ukimwi , ambao hulibadilishwa kila mwezi baada ya kipindi cha miezi sita.

Ni mojawapo ya mipango ya kutengeza kifaa ambacho wanawake watatumia kujilinda dhidi ya maambukizi ya HIV ili wasiweze kuwategemea wanaume kuvaa mipira ya kondomu.

Wakiripoti ugunduzi huo mpya kuhusu virusi vya HIV mjini Paris, watafiti walisema kuwa wanafurahi kwamba wasichana hao walitumia mvirongo huo na kusema kuwa wameupenda.

Wanawake na wasichana walio na kati ya umri wa miaka 15-24 wanadaiwa kuwa moja kwa tano ya visa vyote vya maambukizi ya HIV duniani.

Takriban wanawake 1000 huambukizwa virusi kila siku katika Afrika ya jangwa la sahara.

Rais Uhuru Aongea na Wafuasi wake 3 Milioni Kwa Facebook

$
0
0

Siku moja kabla ya mdahalo wa wagombea urais, Rais Uhuru Kenyatta ambaye timu yake inasema hatashiriki alijichanganya na mashabiki wake wa Facebook kwa kujibu maswali waliyomuuliza.

Tukio hilo lilikuwa kubwa na lilionyeshwa mubashara kupitia vituo vya televisheni vya KBC na K24 TV.

Akiwa amevalia fulana, mkuu huyo wa nchi alijibu maswali mbalimbali ya wafuasi wake aliyokuwa ametumiwa mapema tena yale ambayo yeye na timu yake walichagua. Maswali hayo yaligusia nyanja za uchumi, rushwa, uchaguzi ujao na maendeleo ya miundombinu.

Katika majibu yake Kenyatta aliwataka mashabiki na wafuasi wake wapatao milioni 3 kuombea amani uchaguzi na kwa unyenyekevu aliomba achaguliwe kwa muhula mwingine wa kuwaongoza Wakenya.

    “Ni lazima tupendane,” alisema moja kwa moja kutoka Ikulu ya Nairobi. “Na ujumbe huu ninaoutoa Jumapili hii wakati wengine wako kanisani, nawasihi muombe: Kwamba tutaishi kwa Neno. Kwamba tunapendana.”

Akitambua kwamba asilimia 51 ya Wakenya 19.6 milioni waliojiandikisha kupiga kura wana umri kati ya miaka 18 na 35, Rais Kenyatta aliyajenga maswali yake na kwa ukweli maswali aliyochagua kuwaridhisha vijana na kwamba Serikali inayoundwa na yeye ndiyo bora kwa ajili yao.

Katika kujibu maswali hayo alielezea maendeleo ya nchi kama vile ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), barabara, usambazaji umeme na matarajio ya kuongeza ajira kwa vijana.

“Tuna mpango wa kujenga mtandao wa reli jijini Nairobi, kupanua reli ya SGR hadi Naivasha na Narok, kisha ipite Kisumu,” alisema kwa watumiaji wa Facebook.

“Hatujachelewa tuko kwa wakati,” alisema na akatetea mapambano dhidi ya ufisadi akisema Serikali yake haitawavumilia kamwe.


Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images