Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Ampiga Risasi Baba Mkwe Wake Kanisani Kwa Kumuachanisha na Mkewe

$
0
0

Chanzo cha mwandishi wa habari wa kujitegemea, Elias Mhegera kumpiga risasi baba mkwe wake kanisasni juzi ni hisia kuwa mzazi wa mwanamke huyo ndiye chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yao miaka 10 iliyopita. Mhegera ambaye kwa sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi tangu juzi amekuwa katika mvutano na mke wake ambaye waliachana miaka 10 iliyopita.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni amethibitisha kutokea kwa tukio hilo juzi majira ya saa1:30 asubuhi katika Parokia ya Bikira Maria, Kibangu na kueleza kuwa chanzo ni ugomvi wa kifamilia.

“Adrian Mpande alijeruhiwa bega la kushoto na mtu anayedaiwa kuwa ni mkwe wake. Uchunguzi wa awali umebainisha kuwa sababu ni mambo ya kifamilia,” alisema Kamanda Kaganda na kuongeza: “Tunaendelea na uchunguzi na kukiwa na umuhimu tutawaeleza kwa uwazi.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa Mzee Mpande alipigwa risasi mbili wakati akijiandaa kuingia kanisani kwa ibada juzi Jumapili.

Nipashe

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA..Anatibu Magonjwa Mbali Mbali, Kusoma Nyota na Mengine

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote


..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14.

Na Mengi zaidiWhatsapp/Calls +255 710 279 458
+255 710 279 458

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Tundu Lissu Amvuruga JPM.....Magazeti ya Leo Jumatano

$
0
0


Tundu Lissu Amvuruga JPM.....Magazeti ya Leo  Jumatano

Uteuzi wa JPM Wawachanganya Wapinzani....Wengine Wadai ni Kukubali Alichokikataa Hadharani

$
0
0
Kauli ya Rais John Magufuli kuwa ataendelea kuteua wapinzani wenye akili na kuacha vilaza imewachanganya wapinzani, kutojua Rais anafanya siasa ya aina gani.

Rais Magufuli amezungumzia kuendelea kuwateua wapinzani akiwa anahutubia wananchi wa Mkoa wa Tabora katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi baada ya kuzindua miradi ya barabara yenye thamani ya Sh 457.256.

Kauli hiyo inachukuliwa kama mwendelezo wa uteuzi unaofanywa na Rais Magufuli ambapo tayari amemteua muasisi na mshauri wa chama cha ACT Wazalendo, Profesa Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji na aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Anna Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Akizungumzia kauli ya Rais na uteuzi anaofanya kwa wapinzani Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui amesema kinachofanyika ni kukubali alichokikataa hadharani.

Amesema Rais Magufuli aliwahi kufanya mkutano Pemba na kusema kuwa hawezi kamwe katika Serikali yake kuteua wapinzani, “Inaonyesha wazi aliowateua siyo wapinzani kama ambavyo alisema hawezi kuwateua.”

Mwenyekiti wa NCCR – Mageuzi, James Mbatia amesema hayo yote yanatokana na baadhi ya wapinzani kusahau misingi na mifumo ya uwapo wa vyama vyao.

 “Hizi zote ni kelele, hakutakuwa na upinzani wa kweli, siasa za kweli kama hakutakuwa na meza ya majadiliano ili kupata muafaka.

“Atawateua, watafanya wanachoelekezwa na hiyo haitasaidia kwa sababu haitaleta msukumo wa kusonga mbele, hakuna hekima bila ufahamu, ufahamu unatokana na kupata mawazo kinzani badala ya kuyapinga,” amesema kwa kifupi Mbatia.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wakizungumzia kauli ya Rais Magufuli wameeleza kuwateua wapinzani ni kubadili dhana nzima ya vyama hivyo.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Richard Mbunda amesema uteuzi umebadili dhana nzima ya upinzani kama ulivyowaziba mdomo wabunge wa CCM.

Amesema wabunge wa CCM hawawezi kuikosoa Serikali kwa kuamini kuwa hawatapata nafasi za uteuzi kama uwaziri na unaibu, wapinzani pia wameingia kwenye mkumbo huo na matokeo yake watapotea.

“Nafasi za uteuzi wa kisiasa dunia nzima unachukuliwa kama ajira, hivyo ni ngumu kumkemea aliyekuajiri, wapinzani kupenda, kukubali kuteuliwa wanajiua bila kufahamu,”amesema Mbunda.



‘Tanzania Haina Uwezo Kudhibiti Uhalifu’

$
0
0
By Aurea Simtowe
Tanzania haina uwezo wa kudhibiti uhalifu wa kimtandao kutokana na mitandao inayotumika kumilikiwa na watu wa Magharibi.

Kauli hiyo imetolewa jana katika mkutano uliowakutanisha viongozi wa Serikali kutoka Tanzania na China na wawakilishi wa vyombo vya habari jana.

Mkutano huo ulikuwa ukidhibiti matumizi mabaya ya mtandao yanayoweza kuleta madhara katika vyombo vya habari.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani amesema sheria ya udukuzi wa kimtandao inayotumika nchini haina uwezo wa kuwawajibisha watu wanaotumia vibaya mtandao kutokana na tofauti za tamaduni.

“Sasa tuna watu wanaodhibiti wahalifu wa kimtandao, lakini wanapata wakati mgumu kuthibitisha ushahidi kupitia mitandao ya kijamii kwa sababu mingi inatoka Marekani na kusimamiwa na sheria za nchi hiyo,” amesema Ngonyani.

Balozi wa China nchini, Lu Youqing amesema Tanzania ni moja kati ya nchi barani Afrika ambayo matumizi ya kimtandao yanakua kwa kasi, hivyo ni lazima kuwe na udhibiti wa watumiaji wabaya.

“Kupitia takwimu za TCRA (Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania) zinaonyesha kuna ongezeko la mara 13.7 kwa watumiaji wa simu ndani ya miaka 10 kutoka milioni 2.9 mwaka 2005 hadi kufikia watu milioni 39.8 mwaka 2015, huku watumiaji wa tovuti wakifikia milioni 17.26 mwaka 2015 kutoka milioni 1.01 mwaka 2005,” amesema  Balozi Youqing.

Mwananchi

Mwanamke Aliyekeketwa Je Huwa Anaridhika Kimapenzi?

$
0
0
Nataka kujua hawa dada zetu waliokeketwa wakiwa wadogo hawajitambui kipindi hicho je wanakabilianaje na swala la kuridhishwa kimapenzi.

Maana huwa nasikia ni wagumu sana kukojozwa kabisa sasa je wanaridhika? au bora liende na je wanakabilianaje na hili swala maana nasikia bado baadhi ya mikoa na makabila wanakeketwa kama wakurya, wanyaturu, warangi, wagogo, wanyakyusa nk.

Ingetakiwa watu maarufu wenye ushawishi pia wapigie vita huu ukeketaji kama kina wema maana nae ni si ni mnyaturu?

Shilole Kiuno Afungukia Kiacha Mziki Kisa Umama Ntilie......

$
0
0
Shilole Kiuno Afungukia Kiacha Mziki Kisa Umama Ntilie......
MWANAM-UZIKI wa miondoko ya mduara, Zuwema Mohammed ‘Shilole’ ameweka wazi kuwa huenda akaukacha muziki siku za usoni kutokana na kunogewa na biashara yake ya kuuza chakula katika mgahawa wake.

Akizungumza na Risasi Vibes, Shilole alisema anaona biashara yake hiyo inampa faida nyingi kuliko uigizaji na hata muziki anaofanya, hivyo kutokana na maisha magumu ni bora kufanya kitu kinachomu-ingizia kipato.

“Huku kwa mama ntilie naona kunanilipa zaidi ya sehemu nyingine ambazo nipo, sasa ni bora kufanya kitu ambacho kina kuingizia kipato kuliko kung’ang’ania sehemu ambayo haikulipi au inakulipa kidogo tena kwa kusubiri,” alisema Shilole.
 Stori: Imelda Mtema

Simanzi....Mjomba Adaiwa Kumbaka, Kumnyonga Mpwa Wake.......

$
0
0

 SIMANZI! Mtoto Nora Jimmy (11), mkazi wa Sinza Mapambano jijini Dar aliyekuwa akisoma darasa la sita Shule ya Msingi Atlas, amedaiwa kufanyiwa kitendo cha kikatili cha kubakwa kisha kunyongwa mpaka kufa na mjomba wake aitwaye John Msigala.

MSIKIE MAMA MZAZI

Akizungumza kwa simanzi kubwa jana, mama wa mtoto huyo, Agness Msigala alisema kuwa siku ya tukio juzi saa 10 jioni yeye hakuwepo nyumbani bali alimuacha mtoto wake huyo na wadogo zake watatu ambao wawili ni wa kiume.

Aliongeza kuwa alipotoka kazini alipita kwenda kumuona mgonjwa ambaye ni mama wa rafiki yake lakini alipokuwa anarudi nyumbani, njiani alipigiwa simu na jirani yake na kumueleza kuwa Nora, ameanguka wamempeleka Hospitali ya Palestina hivyo kabla ya kwenda nyumbani apitie hapo.

“ Nilipopigiwa simu hiyo nilishtuka sana na kuanza safari ya kwenda Palestina huku nikiwa na hofu kwa sababu mwanangu nilipoondoka jana yake kwenda kwa baba yake kisha nikaamkia huko kwenda kazini alikuwa yuko vizuri tu.


 “Baada ya kufika hospitali nilikutana na jirani yangu pamoja na manesi ambao walijaribu sana kunituliza huku wakinipa moyo wakiniambia kuwa inabidi nijikaze kwani mtoto wangu tayari ameshafariki dunia.

“Nilichanganyikiwa na nikaomba nikahakikishe, niliruhusiwa na nilipomchunguza vizuri niliona amefanyiwa kitendo cha ubakaji na pia shingoni kuna alama ya kamba…,” alisema mama huyo huku akitokwa machozi, ilielezwa kuwa muda mfupi uliopita alizimia.

BABA ANENA

Naye baba mzazi wa mtoto huyo, Jimmy Mariale, alisema kuwa ameumizwa na kifo cha mtoto wake huyo kwa kuwa ndiyo wa pekee na atahakikisha sheria inafuata mkono wake na kama shemeji yake ndiye aliyefanya ukatili huo atahakikisha haki inatendeka.

“Nimeumia mno mtoto wangu ndiye wa pekee sina mwingine kitendo alichofanyiwa ni cha kinyama na kinaumiza mno lakini nitahakikisha sheria inachukua mkondo wake,” alisema baba huyo.



WASIKIE MAJIRANI

Gazeti hili lilizungumza na mmoja wa majirani aliyejitambulisha kwa jina moja la Chacha aliyekuwa eneo la tukio ambaye alisema kuwa akiwa anajiandaa kutoka kwenda kwenye shughuli zake aliona majirani wengi wakiwa nje ya nyumba hiyo huku mwili wa Nora ukiwa umelala chini wakijishauri kuupeleka hospitali.

Alipohoji kulikoni aliambiwa kuwa amekutwa amenyongwa pembezoni mwa banda lao la kuku na hata alipoenda kuchunguza sehemu ambayo amekutwa amenyongwa pia aliona panatatanisha.

“Mpaka sasa hivi mimi siamini ni kitu gani kimetokea jamani maana sehemu ambayo inadaiwa ndipo aliponyongwa ni fupi mno maana miguu inaweza kugusa chini. Inashangaza sana,” alisema jirani huyo.



WENZAKE WAANGUA KILIO

Baadhi wanafunzi wenzake wa Shule ya Atlas waliompitia mwenzao jana wakiwa kwenye basi la shule waliangua kilio walipokuta mwenzao ameshafariki dunia baada ya kukuta kundi la watu nyumbani hapo, jambo lililozidisha simanzi mtaani hapo.

“Huyu marehemu alikuwa na kawaida ya kuwagongea milango wenzake ili wawahi kupanda basi, hivyo leo hakufanya hivyo na ndiyo maana umewaona wenzake wamemlilia sana,” alisema jirani mwingine.

MJOMBA ASIMULIA

Mmoja wa mjomba wa marehemu, aliyejitambulisha pia kwa jina la John (ni mtoto wa baba mkubwa na mdogo na mtuhumiwa) ambaye yeye hakuwepo nyumbani hapo tangu asubuhi alisema kuwa kamba ambayo imekutwa shingoni mwa Nora, yeye aliifunga siku tatu za nyuma nyumbani hapo kwa ajili ya kumnyongea paka aliyekuwa akisumbua usiku.

Mtuhumiwa anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Kijitonyama (Mabatini) ambapo afisa mmoja kituoni hapo amethibitisha kukamatwa kwa kijana huyo.

GPL

Markson Beauty Wanakuletea Dawa ya Upungufu wa Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo...

$
0
0

JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUFIKA KILELENI HARAKA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?
Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k.
Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/=


BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-


@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

WELCOME ALL

VIONGOZI na Wafuasi 51 wa Chadema Wanaosota Selo Hatma yao Kujulikana Leo.....

$
0
0
VIONGOZI na wafuasi 51 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao wameendelea kusota kwa siku 18 kwenye Gereza la Biharamulo mkoani Kagera kutokana na kunyimwa dhamana na Mahakama ya Wilaya ya Chato, hatma yao ikajulikana leo.

Ni baada ya mahakama hiyo kupokea hoja za upande wa mashtaka na utetezi ambao unaiomba mahakama kuondoa zuio la kutopewa dhamana ambalo liliwekwa na Mwendesha Mashtaka, Semen Nzigo.

Viongozi na wafuasi hao walikamatwa na Jeshi la Polisi wilayani hapa Julai 7, mwaka huu wakiwa kwenye kikao cha ndani kilichowahusisha viongozi wa Chadema mkoa, wilaya na Kata ya Muganza, ambapo walifunguliwa mashtaka ya kufanya mkusanyiko bila kuwa na kibali.

Baada ya pande hizo kuwasilisha hoja zao juzi, Hakimu wa Mahakama hiyo, Jovith Kato, alisema atatoa uamuzi wa mapingamizi hayo kesho, iwapo washtakiwa wapewe dhamana au waendelee kubaki mahabusu.

Wakizungumza nje ya mahakama, mawakili wa upande utetezi, John Edwar na Siwale Isambi, walisema wanatarajia mahakama itatenda haki kwa kuwapa dhamana kabla ya kesi ya msingi haijasikilizwa.

“Tunashukuru, mahakama imesema itatoa uamuzi wake keshokutwa (leo) iwapo wateja wetu wapewe dhamana au la...ila ni matumaini yetu makubwa kuwa zuio la upande wa mashtaka litaondolewa,” alisema Edward.

Baadhi ya viongozi walioko gerezani ni Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Geita, Phabian Mahenge, Katibu wa Chadema mkoa huo, Sudy Tuganyala, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee mkoa, Vitus Makoye na Mwenyekiti wa Bavicha mkoa huo, Neema Chozaile.

Wengine ni Katibu wa Wilaya ya Chato, Mange Ludomya, Kaimu Mwenyekiti Wilaya ya Chato, Uhuru Selemani, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa wilaya hiyo, Meshark Tulasheshe na Katibu Mwenezi Kata ya Muganza, Marko Maduka.

Hata hivyo, wakati mahakama hiyo ikitoa tarehe ya uamuzi wa pingamizi hilo, washtakiwa wote hawakuwapo mahakamani.

CHINA Kubaini Watukanaji WhatsApp, Facebook Bongo

$
0
0
WATU wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii kama WhatsApp na Facebook, huenda wakaanza kubainika kirahisi katika siku za karibuni na kufikishwa mbele ya vyombo vya dola kwa msaada wa China, imeelezwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani, alisema watu wanaotumia lugha za matusi, kutuma picha zisizokuwa na maadili katika mitandao ya kijamii watabainika kwa urahisi kwa kutumia mfumo wa China.

Ngonyani alisema China imefanikiwa kudhibiti suala hilo kwani kitu kibaya kinapoingizwa nchini mwao kupitia mtandao, hukizuia kabla hakijaleta madhara kwa jamii.

Sheria ya Makosa ya Mtandao ilipitishwa na Bunge Aprili Mosi, 2015 lakini ujio wa sheria hiyo haujaleta matokeo chanya kwa kuwa kumekuwa na matukio ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ikiwemo Instagram pia.

Sheria hiyo ambayo tayari imeshaanza kutekelezwa ilipelekwa bungeni kwa hati ya dharura.

Ngonyani aliyekuwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa vyombo vya habari na matumizi ya mtandao uliofanyika jijini Dar es Salaam, alisema kuna idadi kubwa ya wananchi wanaotumia mitandao ya kijamii.

"Lakini baadhi yao huitumia kwa kuwatukana watu na hata kuweka vitu visivyotakiwa kwa maadili ya Kitanzania," alisema.

"Kama mtu amekutumia ujumbe mbaya, tunataka tuwe na uwezo wa kumkamata na kumchukulia hatua.

"Au (mtu) amekutumia barua pepe, au ametuma picha mbaya kwenye WhatsApp, wenzetu China wameweza kuwanasa kwa urahisi.

"Sasa na sisi tunataka kujifunza hilo ili tuanze kuwabaini."

Ngonyani alisema mgeni yoyote anayeingia China hawezi kutumia mtandao wowote wa kijamii isipokuwa wa Kichina, tofauti na hapa nchini ambako mgeni anaweza kutumia mitandao ya nje.

AANDAA MFUMO
Mhandisi Ngonyani alisema serikali inaandaa mfumo huo wa kuwabaini moja kwa moja watumiaji wabaya wa mitandao na kwamba pindi utakapokamilika utapelekwa katika Baraza la Mawaziri; kisha kupelekwa bungeni na kupitishwa kuwa sheria.

"Mfumo huo ukikamilika tutaweza kujua ujumbe huu umetoka kwa nani, kwa sababu kwa sasa hivi mtu anaweza kutumia simu ya mtu mwingine kutuma ujumbe mbaya," alisema zaidi.

"Sasa ni lazima tutafute teknolojia mpya ambayo hata mtu akitumia simu (namba) ya mtu na kuitumia vibaya tunamkamata.

"Kule (ujumbe) ulikotoka lazima ujulikane."

Alisema kwa sasa serikali imefikia hatua nzuri ya udhibiti wa wezi wa fedha wa mitandao lakini bado inatatizwa na mitandao ya kimajii kutoka nje ya nchi. WhatsApp, Facebook na Instagram yote ina kanzidata Marekani.

Pamekuwa na hukumu zinazotokana na Sheria ya Makosa ya Mtandao hata hivyo.

Isaack Emily wa Arusha alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu au kulipa faini ya Sh. milioni saba na Mahakama ya Hakimu Mkazi

Arusha katikati ya mwaka 2016, baada ya kumuona na hatia ya kumtukana Rais John Magufuli kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Aidha, Februari 21, mwaka huu wanafunzi wanne wa Chuo Kikuu cha Kampala (KIU) kampasi ya Dar es Salaam, walifikishwa katika

Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shitaka la kusambaza picha za kumkashifu Rais Magufuli kupitia mtandao wa kijamii wa WhatsApp.

Washitakiwa hao ni Amenitha Kongo (19), Maria Tweve (20), Agnes Gabriel(21) na Anne Mwansasu(21).

Kwa pamoja walidaiwa kuchapisha picha ambazo zinaonyesha Rais Magufuli akiwa amevaa hijabu kama mwanamke wa Kiislamu na kuzisambaza kwenye mtandao huo wa WhatsApp, huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

UJUMBE Mzuri siku ya Leo Kwa Ajili Yako Utakaokufungua Macho na Moyo...

$
0
0

DARASA HURU

Kijana mmoja wa kiume alikuwa akipita nyumba moja hadi nyingine kulilisha tumbo lake lilokuwa na njaa, mwishowe akaamua kuomba chakula katika nyumba inayofuata. Lakini katika hiyo nyumba alishindwa kutimiza dhamira yake hiyo pale msichana mzuri alipofungua mlango. Hivyo badala ya kuomba chakula, akaomba glass ya maji. Msichana alipomtazama akamuona yule kijana anaonyesha ana njaa, hivyo akamletea glass kubwa iliyo jaa maziwa. Akayanywa taratibu, kisha akamu uliza yule msichana "unanidai kiasi gani kwa ajili ya hiki ulichonipa?""Sikudai chochote. Mama ametufunza tusikubali malipo kwa tendo lolote la fadhila." Yule kijana akamwambia, "kwa hiyo ninakushukuru kutoka moyoni mwangu kote".
Miaka mingi ikapita, yule msichana (sasa ni mwanamke) alipata maradhi mabaya na madaktari wa sehemu ile walijaribu sana kumponesha lakini hawakuweza. Mwishowe wakaamua kumpeleka mjini ambapo madaktari bingwa watamchunguza. Dr Kelly ali itwa, na aliposikia mji yule msichana anapotoka, mwanga wa ajabu ukampata machoni mwake.
Mara moja aliamka akaenda chumbani akipolazwa yule mwanamke. Alimtambua mara moja. Alirudi ofisini kwake akaa mua kufanya kila awezalo kumponyesha yule mwanamke. Baada ya jitihada kubwa, alifanikiwa na yule mwanamke akapona.
Dr Kelly akaiagiza ofisi ya biashara kumletea bill ya mwisho ya yule mwanamke. Aliitazama bill ile, aka andika maneno machache kisha bill ile ikapelekwa chumbani kwa yule msichana. Mwanamke yule akawa anaogopa kuifungua ile bill akihofu itamchukuwa akiba yake yote aliyokuwa ameweka kulipa gharama za pale. Mwishowe alipofungua, akaona maandishi yaliyo andikwa chini yake "imelipwa kamilifu kwa glass ya maziwa"
Machozi yalimtiririka mara moja alipokumbuka. Tendo lolote la fadhila unalolitenda halipotei. Linajirudia. Sio lazima palepale lakini baadae hujitokeza. Nimekuwa mwema kukupa hadithi hii. Nawe kuwa mwema kuwapa wenzio. Ni vyema kuwa mwema. Kila mara kuwa mzuri : itakurejea.

DOWNLOAD Wimbo Mpya wa Rosa Ree Feat NavyKenzo Unaoitwa Mchaga Mchaga

$
0
0
DOWNLOAD Wimbo Mpya wa Rosa Ree Feat NavyKenzo Unaoitwa Mchaga Mchaga:

VIDEO: “Wanaume wa WCB wote Waaminifu” – Babutale

$
0
0
Kutoka Makao Makuu ya WCB kwa Meneja wa mwimbaji staa wa Bongofleva Diamond Platnumz na Tip Top Connection, Babutale leo July 25, 2017 amepost picha yenye maneno yalioandikwa ‘Wanaume wa WCB wote waaminifu’ kupitia ukurasa wake wa Instagram @babutale

Mabilionea 26 Watalii Waliokuja Serengeti kwa Kuvutiwa na Uzuri wa Tanzania

$
0
0
Siku za hivi karibuni headlines za mastaa kadhaa wa Soka, Muziki na Filamu Duniani kutembelea Mbuga za wanyama na vivutio mbalimbali vya Tanzania zilishika kasi licha ya mastaa hao kuingia kwa siri kwa ajili ya mapumziko.

Licha ya baadhi ya mastaa hao kuja kwa siri Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe amekutana na Watalii 26 ambao ni Mabilionea ambao wamewasili nchini kwa ajili ya kutembelea Mbuga ya Serengeti wakidai kuvutiwa na Tanzania kutokana na ubora wa Mbuga za wanyama.

Leo July 25, 2017 Ayo TV na millardayo.com zimezungumza na Waziri Maghembe:
“Wanatembelea nchi nane. Ni Mabilionea, Maraisi wa Makampuni. Kwa hiyo, wana Chama chao wakati wa likizo wanapenda kutembelea nchi kwa pamoja. Wakati huu wanatembelea nchi nane, walitembelea Uingereza, Rwanda na ya tatu Tanzania.

“Wakiondoka hapa wanakwenda Maldives, karibu na India halafu wanakwenda Nepal, Bhutan, Rajasthan. Ni watu ambao wamekuja Tanzania kwa ubora wake, kwa uzuri wake na wamekuja moja kwa moja Serengeti.” – Waziri Maghembe.

“Nikiondoka Hakuna Atakayekuwa Kama Mimi” – Kauli 7 za Rais JPM

$
0
0
Rais Magufuli leo July 25, 2017 ameendelea na ziara yake ambapo alikuwa katika Mkoa wa Singida alikozindua Barabara ya Manyoni – Itigi – Chaya yenye urefu wa km 89.3 ambapo mbali na kufanya uzinduzi huo alipata nafasi ya kuhutubia wananchi.

Nimekusogezea mambo 7 makubwa kati ya mengi aliyozungumza kwenye hotuba yake.

'Pengine nikiondoka mimi hakuna atakayekuwa kama mimi, nasafisha njia ya Rais atakayekuja baada ya mimi' - Rais @MagufuliJP

'Ni lazima niyatapike yote haya, nikikaa nayo nitapata presha bure, ila wale walioyafanya wakumbuke na madhambi yao' - Rais @MagufuliJP

'Suala la ubinafsishaji mimi silipendi kabisa, siwezi nikawalaumu waliofanya hivyo lakini pia siwezi nikaacha kusema' - Rais @MagufuliJP

'Nataka Tanzania hii iwe kama Ulaya na tutafika tu, lakini ili tufike huko ni lazima tutabanana kweli kweli'- Rais @MagufuliJP

'Wananchi waliojenga kwenye hifadhi ya reli waanze kujiandaa kisaikolojia, wanaweza tu kuanza kubomoa taratibu nyumba zao'- Rais @MagufuliJP

'Niliporudishwa wizara ya ujenzi nilimfukuza Chief Executive Officer ndani ya siku 3 kwa sababu ya matumizi mabaya ya fedha' - @MagufuliJP

Wengine mmewachagua lakini wanaongelea ya mambo Dar es salaam tu kosea kuoa unaweza kutoa talaka lakini usikosee kuchagua - Rais @MagufuliJP

Madee na IdrisSultan wachambana Live Instagram, Madee Akumbushia Pesa za Big Brother

$
0
0
Madee na IdrisSultan wachambana Live Instagram, Madee Akumbushia Pesa za Big Brother

Soma Hapa chini majibishano yao:


Je MadeeAli yuko sahihi alivyomjibu Idris Sultan.
Nawe dondoka hapa.

MWANAMUZIKI Alikiba Aachia Ngoma Mpya.....Isikilize Hapa Kwa Mara ya Kwanza

$
0
0
Aman iwe nanyi wapendwa katika bwana
Yule mkali wa bongo, mkali wa sauti king kiba, kaachia ngoma ambayo haitamwacha mtu salama ngoma inakwendwa kwa jina joho tena

Hii ngoma ni noma mazee naona simba mwaka huu watAkula nyasi kudadadek
LONDON BABY

SIKILIZA HAPA NGOMA YAKE MPYA:

Ajinyonga Baada ya Kugundua Mkewe Anashiriki Mapenzi ya Jinsia Moja

$
0
0
Mwanaume Mmoja Nchi Kenya amejinyonga  hadi kufariki kutokana na kugundua mke wake anashiriki mapenzi ya Jinsia moja (Usagaji).

inadaiwa kuwa Mwanamke huyo alitoroka nyumbani kwake kwenda kwa Mwanamke anayeshiriki naye mapenzi hayo ya Usagaji.

Lile Sakata la Mama Kuibiwa Mtoto Kutua kwa JPM

$
0
0
Lile sakata la mwan­amama Asma Juma (29) aliyedai kujifungua watoto wawili mapacha katika Hospitali ya Temeke Machi mwaka huu, limechukua sura mpya baada ya familia yao kusema italifikisha suala hilo kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli ili kupatiwa suluhisho.

Hatua ya familia hiyo inatoka­na na kutoridhishwa na ripoti iliyotolewa na timu iliyoundwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ambayo ilidai baada ya uchunguzi wa kina, ilibainika kuwa mama huyo al­ijifungua mtoto mmoja, tofauti na madai yake kuwa alikuwa na ujauzito wa mapacha waw­ili.

Akizungumza na Risa­si Mchanganyiko jana, mama huyo alisema yeye na mumewe, hawajakubaliana hata kidogo na ripoti hiyo ili­yotolewa siku chache zilizopi­ta na kwamba msimamo wao upo palepale.

“Ile ripoti iliniumiza mno, ni ngumu kwangu kukubaliana nayo, tumeona bora kwenda kwenye haki za binadamu ili watusaidie swala letu, kwa mujibu wa ripoti hiyo inasema sikuzaa mapacha ila kosa la hospitali lipo kwenye kipimo, si sawa,” alisema.

Naye mumewe, Abubakar Pazi alisema kamwe hawezi kukubaliana na majibu hayo, ndiyo maana ameona uamuzi mzuri ni kwenda haki za bin­adamu ili wasaidiwe na kama haitoshi, atafika hadi ikulu akamuone Rais Magufuli.

“Kitu kilichoniumiza kwenye hiyo ripoti ni kusema mke wangu hakuzaa watoto waw­ili, kwamba hospitali wata­wajibika kwa kukosea kipimo tu, naona si sawa, niliomba ile ripoti baada ya kusomwa nipewe ili na sisi tuwe nayo, lakini tumenyimwa, tunatafuta njia ya kumfikia rais hata kwa kumuandikia barua atusaidie hili suala,” alisema.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Temeke hakupatikana ili kuzungumzia suala hilo, lakini Msaidizi wake, Dk. Emmanuel Salakisha ambaye ndiye mse­maji wake, alisema kwa sasa hawana la kusema kwa vile lil­ishavuka ngazi yao.

“Kilichoonekana kwenye ile ripoti, kipimo kilikosewa kwenye ile hospitali waliy­opima mwanzo, kuhusu hayo mambo ya kwenda haki za binadamu bado hatujapata taarifa, hata hivyo hilo jambo lilishavuka kwenye ngazi yetu, lipo ngazi ya wizara, kama likija huku kwetu tutawapa ushiriki­ano,” alisema.

Sakata la mama huyo lil­ianza Machi mwaka huu baada ya kudai kuwa madaktari katika Hospitali ya Temeke walimuibia mtoto wake mmoja, kwani siku zote za ujauzito wake, aliamini ana watoto mapacha kutokana na vipimo alivyofanyiwa katika hospitali binafsi ya Huruma, iliyopo Mbande.

Baada ya mama huyo kuhoji juu ya tukio hilo, madaktari wa Temeke walimweleza kuwa vipimo alivyofanyiwa awali vi­likosewa, kitu ambacho wame­kuwa wakikipinga kwa muda wote.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images