Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live

Zitto Kabwe kusomesha wanafunzi 541 bure

0
0

Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya Chama Cha ACT Wazalendo, Mhe Zitto Kabwe amefunguka na kusema katika mwaka wa masomo 2017/2018 manispaa ya Kigoma Ujiji ambayo ipo chini ya chama chake inawasomesha bure jumla ya wanafunzi 541 wa kidato cha tano na cha sita katika shule mbalimbali.

Zitto Kabwe amesema hayo alipozungumza na EATV na kudai kuwa Manispaa ya Kigoma Ujiji imeamua kuwa mfano, kwani ni Manispaa ya kwanza Tanzania kusomesha wanafunzi wake wote wanaomaliza kidato cha nne katika shule zilizopo ndani ya manispaa hiyo na kuwalipia ada katika Elimu ya Juu ya Sekondari
"Tunasomesha bure wanafunzi waliomaliza kidato cha nne katika shule zilizopo ndani ya manispaa yetu ambao wanakwenda popote pale ambapo wanapangiwa kwenda kusoma, mpaka sasa tunasomesha wanafunzi 541, wanafunzi 254 wapo kidato cha tano  na wanafunzi wengine 287 wapo kidato cha sita katika shule mbalimbali, hawa wote wametoka katika shule za manispaa yetu" alisema Zitto Kabwe

Aidha Zitto Kabwe amesema Manispaa ya Kigoma Ujiji ina mpango wa kuongeza wanasayansi walio wengi hivyo sasa imeamua kujenga shule nyingine ya kidato cha tano na sita ambayo itakuwa ni maalum kwa wanafunzi wanaosoma masomo ya Sayansi tu.

"Wakati tunachaguliwa hapa Kigoma shule ya sekondari ya masomo ya juu ilikuwa Kigoma sekondari tu lakini chini ya miaka miwili ambayo tumecahguliwa tayari tumeongeza shule mbili za masomo ya juu yaani kidato cha tano na sita. Sasa hivi tumeamua kuongeza shule nyingine moja ya kidato cha tano na sita ambayo itakuwa ni ya masomo ya sayansi peke yake, tumeamua kufanya hivi sababu tunahitaji wana sayansi zaidi katika mji wetu, tunahitaji vijana wetu wasome sanyansi zaidi" alisisitiza Zitto Kabwe

Manispaa ya Kigoma Ujiji imekuwa manispaa ya kwanza nchini Tanzania kutoa elimu bure kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita ambao wametoka katika shule zilizopo ndani ya manispaa hiyo na kwenda shule zingine mbalimbali nchini.

Pata Tiba za Asili Toka Kwa Chief Sultan Makata...Anayetibu Kwa Kutumia Nyota na Dua ....

0
0

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH CHIEF SULTAN MAKATA Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika 
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote 


..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza. 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi. 
Chief Sultan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako.. 
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14.

Na Mengi zaidiWhatsapp/Calls +255 710 279 458 
+255 710 279 458 

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Job Ndugai Apata Shavu Umoja Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika...

0
0

Ofisi ya Bunge inapenda kuuarifu umma kuwa Spika wa Bunge Mhe. Job Yustino Ndugai (Mb),amechaguliwa kuwa Mwenyekiti  wa Maspika na Viongozi wa Bunge katika Umoja Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika. 


Uchaguzi huo umefanyika  katika Mkutano wa Maspika wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Barani Afrika uliomalizika jana Mjini Abuja.


Kwa wadhifa huo, Mhe Ndugai ataongoza Maspika wenzake toka Mabunge na Mabaraza ya kutunga Sheria  63 yaliyoko katika nchi 18 za Jumuiya ya Madola kwenye Bara la Afrika. 


Wadhifa huo ni wa miaka miwili kuanzia sasa hadi mwaka 2019 kutakapofanyika uchaguzi mwingine.


Nchi wanachama wa Umoja wa Mabunge Barani Afrika ni pamoja na Afrika  ya Kusini, Botwana, Cameroon ,Ghana, Kenya, Lesotho,   Msumbiji, Mauritius, Malawi, Nigeria, Namibia, Rwanda, Seychelles, Sierra Leone, Swaziland, Tanzania, Uganda na Zambia.


Akizungumzia uchaguzi huo,  Mhe Ndugai amesema "Kwa hakika nawashukuru Maspika wenzangu kwa kunipa dhamana hii ya kuwa Mwenyekiti wao, ni heshima kwangu binafsi lakini zaidi Kwa Tanzania. Ni matumaini yangu kwamba Bunge letu litaendelea kung'ara kitaifa na kimataifa tukiwa Bunge moja lenye Upendo na mshikamano".


Huu ni wadhifa wa nne kwa Mhe. Ndugai katika masuala ya Bunge kwenye medani ya Kimataifa. Amewahi kuwa Mwakilishi wa Nchi za Afrika Mashariki katika Kamati ya Utendaji ya Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Duniani mwaka 2008-2011, Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii ya Umoja wa Mabunge ya Afrika, Pacific na Carribbean na Jumuiya ya Ulaya  mwaka 2011-2014 na Rais wa Baraza la Mabunge ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC – PF)


Imetolewa na:

Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano

Ofisi ya Bunge

DODOMA

Mwanaume Ukiwa Unafanya Haya Usilalamike Mkeo/Mpenzi Akichepuka

0
0

Ikifikia mke kukusaliti kwanza unahitaji kujiuliza kuna tatizo gani mpaka akafikia kukusaliti? Mwanamke anaekupenda sio rahisi kumsaliti ampendae hata akitongozwa na Sharobaro, Mzee Yussuf, Diamond hata Reginal Mengi.

Ikitokea mkeo kakusaliti kuna kitu nyuma ya pazia lako, ingawa wengi wetu tunasema hela na Gari vinawalainisha wanawake. Wengi waliosalitiwa basi hizi ndio kasoro zao:-

1 Kaowa mwanamke wa mtu (mwanamke alikuwa na mpenzi wake lakini jamaa kaingia wakati mwanamke anatamani ndoa)

2 Alikuwa na hela sasa kafulia hana kitu au alijifanya alikuwa na hela lakini baada ya kuowa mke anagutuka mume mchovu.

3 Humtoshelezi kwenye tendo la ndoa( humkojozi) kama umeowa mke ameshawahi kufikishwa kilima cha kilimanjaro pole yako fanya maujuzi umpeleke kilima cha Everest.

4 Ubahili hapa wengi wa wanaume ndio hupigiwa sana wake zao, mke anahitaji matumizi yake binafsi sio kula na kulala tu au kumnunulia madira na chocolate za kichina. kuna matozi wanahonga mpaka malaki na milioni halafu unawacha hela ya ugali unapikiwa pilau ukimaliza kula unakwenda kulala, bwege kama wewe lazima uchapiwe dadeki zako.

5 Huna muda wa maongezi na mkeo hujui hata nini anapenda,nini leo kimemkuta,wala huna future plan kwenye familia wewe ukali,mpira,vijiwe,kazi na marafiki tuu wakati rafiki yako wa kweli(mkeo) huna muda wa maongezi nae.

6 Kuwaachia marafiki kuzoweana sana na shemegi yao, sio kama vibaya kutaniana na shemegi yao lakini kuna mataani mengine hupitiliza. utakuta mpaka baadhi ya rafiki wanampigia simu shemegi yao wanaongea kwa masaa na vicheke kibao.

7 Kujifanya mkali kila wakati wewe uso umeukunja kama ngozi za pumb..u hujulikani kijana au mzee hujulikani leo umefurahi au umenuna. Tokea umuowe mkeo hujawahi kumtania hata siku moja.

8 Kuchepuka kuna baadhi ya wanaume walioowa nishawahi kuwauliza kwanini wanachepuka jibu lao kubwa wanasema hawajui. HUbaki kumalizia kusema eti hawa wanawake watakuwa na sumaku

Kuna baadhi ya mambo husababisha sisi wenyewe wake zetu kufikia kuchukua uamuzi wa kutusaliti, Kama ukali unafanya kazi mbona simba na ukali wake lakini kazungukwa na mabebez kibao

PROF Lipumba Kikaangoni...Kisa Kuwafuta Wabunge Uanachama......

0
0
Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Prof. Lipumba kuwavua uanachama Wabunge wanane wa Viti Maalum kisha Spika Ndugai kuridhia uamuzi huo, jana July 27, 2017 Wabunge hao wamefungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Wabunge hao wamefungua kesi hiyo iliyopewa namba 143/2017 kupitia Wakili wao Peter Kibatala lakini hata hivyo bado haijapangiwa Jaji huku Wabunge hao wakidai hawajapewa muda wa kujitetea.

Mbali na kufungua kesi katika Mahakama Kuu Tanzania, pia wamekata rufaa ndani ya Chama chao kupinga utekelezaji huo na kuiomba Mahakama isitishe utekelezaji wa uamuzi wa kufukuzwa Uanachama wao.

PENZI ni Kikohozi...Nisha Amuonyesha Mpenzi wake Mpya

0
0
MSANII wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amebadili jina lake na kujiita Nisha Minhal Azad huku kisa kikidaiwa kuwa amefanya hivyo baada ya kuingia katika uhusiano wa kimapenzi na ‘Serengeti Boy’ anayetumia jina hilo.

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na msanii huyo, Nisha amekuwa karibu na ‘Serengeti Boy’ huyo ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva na kwamba ameamua kuanika kabisa uhusiano huo bila kificho.

“Nisha amepata tulizo baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kuwa na mwanaume. Huyo mpenzi wake wa sasa ni msanii wa Bongo Fleva anajulikana kwa jina la Minu, yaani Nisha humuelezi chochote juu ya dogo huyo na wanaongozana mara kwa mara,” kilidai chanzo na kuongeza;


“Kwa sasa ameamua kuanika ukweli huo kila kona, kwenye mitandao ya kijamii amebadilisha mpaka jina lake na kujiita Nisha Minhal Azad. Hivi karibuni aliweka picha katika Insta yake akiwa naye katika pozi la mahaba na kuandika; ‘kuna tofauti kubwa kati ya Serengeti na Ngorongoro.’

Baada ya kunasa madai hayo, Ijumaa lilimtafuta Nisha na kumuuliza ukweli juu ya kinachoonekana na kuongelewa, alipopatikana alikiri kubadili jina na kuwa katika uhusiano na Serengeti Boy huyo;
“Ni kweli nipo katika uhusiano na huyo mtu, mengine siwezi kuyaanika ila kifupi ni hivyo.”

Nisha kwa nyakati tofauti aliwahi kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elbariki ‘Nay wa Mitego’ pamoja na Baraka Andrew ‘Barakah The Prince’.

KISHINDO Kingine Makinikia Chaiva...Vigogo wa Kampuni ya Barrick Gold Watua Nchini,,,

0
0
KISHINDO kingine kuhusiana na sakata la usafirishaji wa mchanga wa madini (makinikia) kwenda ughaibuni kimeiva baada ya kuwapo kwa taarifa za ujio wa vigogo wa kampuni ya Barrick Gold nchini ili kuanza tena mazungumzo mazito na serikali.

Hivi karibuni, Serikali ilitangaza kuzuia usafirishaji makinikia kwenda ughaibuni na pia Mamlaka ya Mapato (TRA) kuwataka Barrick, ambao humiliki hisa nyingi za kampuni ya Acacia Mining, kulipa kodi na adhabu inayofikia jumla ya dola za Marekani bilioni 190, sawa na zaidi ya Sh. trilioni 400.

Kodi hiyo ni matokeo ya taarifa zisizokuwa sahihi kuhusiana na madini yaliyochimbwa kuanzia mwaka 2000 -- kiasi ambacho kilibainishwa na ripoti za kamati mbili teule za Rais kuchunguza makontena 277 ya makinikia yaliyozuiliwa kwenye bandari ya Dar es Salaam.

Taarifa ambazo Nipashe ilizipata jana na kuthibitishwa na Barrick na Acacia, ni kwamba viongozi wa juu wa Barrick wanatarajiwa kutua nchini wiki ijayo ili kuendelea na mazungumzo na serikali kwa nia ya kufikia mwafaka juu ya suala hilo.

Nipashe inatambua kuwa ikiwa ujio huo wa Barrick utafanyika wiki ijayo, itakuwa ni siku chache baada ya Rais John Magufuli kutangaza wazi akiwa katika ziara zake mkoani Kigoma kuwa anaweza kutaifisha migodi yote ya wawekezaji hao na kuwapa Watanzania ikiwa watachelewa kufanya mazungumzo kwa lengo la kulipa mapato ya serikali yaliyopotea katika kipindi chote tangu waanze shughuli zao nchini.

“Kwa sasa tumewaita wafanye mazungumzo wamekubali, lakini wakichelewa nitafunga migodi yote, ni mara kumi migodi hii tukaigawa kwa Watanzania wachimbe wao wauze tupate kodi kuliko hawa wawekezaji ambao hawalipi kodi,” alisema Rais Magufuli.

Akizungumzia ujio huo wa vigogo wa Barrick nchini, mmoja wa maofisa wa Acacia aliiambia Nipashe jana kuwa hawashiriki moja kwa moja kwenye mazungumzo hayo, lakini chochote kitakachoamriwa watakiridhia.

Aidha, katika ripoti ya mapato ya robo mwaka ya Barrick iliyopo kwenye tovuti yao, imeelezwa kuwa wataendelea na mazungumzo na Serikali ya Tanzania kuanzia wiki ijayo kuhusu makinikia yaliyozuiliwa kusafirishwa nje na mambo mengine yanayohusu utendaji wa kampuni hiyo nchini.

Mbali ya hilo, kampuni hiyo ilielezea mwenendo wa biashara kwa kipindi kilichomalizika Juni 30 mwaka huu kuwa ni mzuri, licha ya kuongezeka kwa gharama za uchimbaji dhahabu kwa asilimia 10.

Makubaliano ya kufanyika kwa mazungumzo kati ya Barrick na Serikali yalitokana na kikao kilichofanyika Juni 14, mwaka huu Ikulu jijini Dar es Salaam, kati ya Rais Magufuli na Mwenyekiti wa Barrick, Prof. John Thornton.

Katika mazungumzo hayo, Prof. Thornton alisema kampuni yake iko tayari kufanya mazungumzo na Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza.

Mazungumzo hayo yalifanyika zikiwa zimepita siku tatu baada ya Rais Magufuli kukabidhiwa ripoti ya pili ya mchanga wa madini na kamati ya pili aliyoiunda kuchunguza suala hilo.

Alipoulizwa kuhusu ujio wa viongozi wa Barrick, Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka, alijibu kuwa suala hilo haliratibiwi na wao.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, ambaye alisema atafutwe Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani ili azungumzie ujio huo mwingine wa viongozi wa Barrick.

Hata hivyo, jitihada za gazeti hili kumpata Dk. Kalemani zilishindikana jana baada ya kukosekana kupitia simu yake ya mkononi.

Source: Nipashe

TCU Yawatoa Hofu Wanafunzi Wanaotarajia Kujiunga Vyuoni Mwaka Huu

0
0
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imesema kuwa haitegemei kufutiwa udahili kwa wanafunzi kwa baadhi ya vyuo, kutawakosesha baadhi ya wanafunzi watarajiwa nafasi au kozi walizodhamiria kwenda kuzisoma.

Akizungumza kwenye Viwanja vya Maonesho, Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari Mwandamizi, Edward Mkaku alisema TCU haitahusika na wanafunzi ambao watakosa vyuo kwa sababu kwa sasa wameratibu udahili na hivyo ni jukumu la mwanafunzi kutafuta chuo kulingana na ufaulu alionao.

“Hatutarajii mwanafunzi kukosa chuo, na pia kufutiwa udahili kwa baadhi ya vyuo siyo sababu ya wanafunzi kukosa nafasi kwenye vile vyuo vilivyopo,” alisema.

UNAWEZA Kuwadanganya Watu Wachache Muda Wote, Lakini Huwezi Kuwadanganya Watu Wote Muda Wote...

0
0
“Unaweza Kuwadanganya Watu Wachache Muda Wote, Lakini Huwezi Kuwadanganya Watu Wote Muda Wote”

Mh Tundu Lissu aliyekuwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma ya uchochezi aliachiwa tarehe 27 Julai 2017 baada ya kupata dhamana. Mh Tundu Lissu alipata nafasi ya kuongea na vyombo vya habari na alieleza mambo kama manne. Kwa haki hiyo hiyo ya kikatiba anayoidai Mh Tundu Lissu nimeona na mimi ni vyema nitoe maoni nyangu kuhusu aliyoyaeleza au aliyodai.

Kwanza kabisa Mh Lissu amedai kwamba siyo kosa kuikosoa serikali na siyo kosa kueleza uovu wa serikali iliko madarakani na siyo kosa kuikemea serikali iliyopo madarakani. Pia ameeleza kwamba vyama vya upinzani vina haki ya kuwakosoa, kuwasema na kuwakemea watawala kwa sababu ipo sheria ya Vyama vingi inayotoa haki hiyo.

Ni kweli Nchi yetu ilikubali mfumo wa vyama vingi vya siasa na ipo sheria ya Vyama vingi vya siasa inayoeleza pamoja na mambo mengine haki ya kuikosoa serikali na haki ya kufanya mikutano ya siasa na maandamano.

Nimefuatilia kwa muda sasa hotuba za Mh Tundu Lissu bungeni na kwenye mikutano ya hadhara na anapoongea na vyombo vya habari. Mh Tundu Lissu haikosoi serikali bali anatukana au anatumia lugha ya kuudhi kwa viongozi wa nchi au wa vyama vingine. Mh Tundu Lissu anatumia lugha ya jeuri na kutakabari na majivuno anapotoa maoni au ushauri wake.

Lengo la kuruhusu vyama vingi vya siasa ni kupanua wigo wa majadiliano ili kuruhusu maoni au ushauri kutoka kwenye vya siasa vyenye mitazamo tofauti, kwani Papa pamoja na mkulima ni bora kuliko Papa pekee. Kuna sheria ya vyama vingi vya siasa lakini pia ipo sheria ya maadili ya viongozi na pia kama Taifa tuna utamaduni wetu.

Mh Tundu Lissu anataka watanzania waamini kwamba anaonewa kwa sababu yeye anaikosoa serikali na anaeleza uovu wa watawala tu kama sheria ya vyama vya siasa inavyotaka. Mh Lissu anadaganya. Mh Lissu anatumia lugha ya kuudhi na anatukana serikali. Mfano hata Polisi hawaheshimu. Mh Lissu alisema ameambiwa na Lipolisi moja tena likubwa kwamba Lowassa atapelekwa mahakamani. Hiyo ni dharau kwa Polisi. Mh Lissu analidharau Jeshi la Polisi, anamdharau Mh Rais ambaye anaridhaa ya watanzania. Mh Tundu Lissu anasema hatanyamaza kwa sababu nchi inaangamia. Mh Tundu Lissu anataka kuwadanganya watanzania.

Je hatua anazuchukua Mh Rais JPM kupigania rasilimali za nchi ili ziwanufaishe watanzania zinaliangamiza Taifa ?
Je hatua alizochukua Mh Rais JPM dhidi ya mafisadi wa Escrow, mafisadi Bandarini zinaliangamiza Taifa ?
Je Hatua anazochukua Rais dhidi wa wabadhirifu wa mali ya umma na wazembe na wale wanaojinufa kutokana na madaraka waliyonayo zinaliangamiza Taifa ?
Je hatua alizochukua Mh Rais JPM kwenye elimu na hatua za kuhakikisha fedha zinatumika kama ilivyopangwa zinaliangamiza Taifa ?
Je hatua alizochukua Mh Rais JPM kutetea wanyonge na maskini ni uovu ?
Je hasira na ghazabu anazozionyesha Mh Tundu Lissu mpaka amwite Mh Rais ni dikteta uchwara zimesababishwa na kutoandamana tu ?
Mh Tundu Lissu amedai kwamba Mh Rais anawagandamiza watanzania ili aendeshe nchi anavyotaka. Huu ni udanganyifu mwingine. Wakati wa kampeni , CCM na vyama vingine vya siasa vilikuwa vinanadi ilani zake za uchaguzi. Watanzania wengi wakaipenda ilani ya CCM na wakamchagua JPM kuwa Rais. JPM anaongoza serikali inayotekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM haendeshi nchi kama anavyotaka.
Mh Tundu Lissu amesema hatanyamaza kwa sababu anapigania haki. Je haki ya kufanya mikutano ya hadhara na maandamano ?
Lakini pia Mh Lissu atambue yupo Amiri Jeshi Mkuu aliye na dhamana ya kuhakikisha nchi yetu ina amani. Na Amiri Jeshi Mkuu anatambulika na Katiba pia. Hivyo, Vyama vya siasa vitakapotoa taarifa Polisi ya kutaka kufanya mikutano au maandamano. Jeshi la Polisi linaloongozwa na Amiri Jeshi Mkuu ambae ni Rais likiona si vyema mikutano isifanyike au maandamano yasifanyike litatoa taarifa kueleza kuzuia maandamano au mikutano. Maana yake hapa ni kwamba kila mtu anatimiza wajibu wake kikatiba. Anayetaka mikutano na maandamano na anayehakikisha amani ya watanzania. Mazingira ya maelewano yanahitajika na wala siyo ugonvi. Mh Lissu pia anatakiwa aliheshimu Jeshi la Polisi na Amiri Jeshi Mkuu. Huwezi ukamtukana Amiri Jeshi Mkuu halafu unapeleka taarifa kwa Amiri Jeshi Mkuu huyo huyo uliyemwita Dikteta akuruhusu ufanye shughuli zako na akulinde ili ufanye shughuli zako kwa amani. Papa na mkulima ni bora kuliko Papa pekee. Mh Lissu alitendee haki Jeshi la Polisi pia.

Ningependa watanzania wajiulize Je Mh Lissu anapigania haki ya kutoa maoni na kukemea maovu ndani ya Chadema ? Kwa sababu uovu ni uovu tu. Wengi wanafahamu kuna watu wananyimwa haki ya kukosoa ndani ya Chadema. Mfano, Mh Zitto alipoonekana kutofautiana na uongozi ndani ya Chadema aliitwa msaliti na alikiiona cha mtema kuni. Kafulila pia. Mbona Mh Lissu hajamwita kiongozi yoyote ndani ya Chadema dikteta uchwara ? Mbona Mh Lissu hajapiga kelele juu ya ukabila na kanda ndani ya Chadema ?. Mh Lissu anadai anapigania demokrasia ambayo imeminywa na serikali ya CCM. Iko wapi demokrasia pana ndani ya Chadema wakati uteuzi wa wagombea ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki ulidhihirisha pasipo shaka kwamba kulikuwa na udikteta uliopitiliza ? Je Mh Lissu alikemea kuminywa kwa demokrasia wakati wa mchakato ? Je mchakato wa uteuzi wa mgombea urais wa Chadema wa mwaka 2015 ulikuwa wa kidemokrasia ? Gia ilipobadilishwa angani Je Mh Lissu alikemea hilo ? Mh Lissu anadaganya kwamba anapigania haki, siyo kweli Mh Lissu anapigania maslahi yake au kuna watu wanaomtumia.

Wahenga walisema, urais haubadilishi tabia ya mtu bali huidhihirisha. Ni kweli. Mh JPM Rais wa Tanzania amekuwa waziri kwa miaka 20. Watanzania hawakumjua kama ana tabia ambayo kwa sasa inaonekana wazi. Mh JPM amekuwa Rais na sasa ana miaka 2 na tabia yake imeanza kudhihirika. Mh JPM amejulikana si Tanzania pekee bali Afrika Mashariki na Dniani kote. Tabia kuu ya Mh JPM iliyodhihirika wazi ni tabia ya kupenda kutetea watu maskini na kuchukia ufisadi na aina yoyote ya dhuluma. Ni tabia yake ambayo ameiishi na siyo ya kuiga. Miaka 20 iliyopita watanzania hawakuijua tabia hii ya Mh JPM.

Mh Lissu nimemfahamu kuanzia miaka ya 90 akiwa mwanasheria wa LEAT. Wakati huo Mh Lissu hakuwa na lugha hii inayoonekana leo. Lissu alipokuwa Mbunge tabia yake iliaanza kudhhirika. Mtakumbuka hoja zake Mh Lissu kuhusu Muungano. Hivi karibuni Mh Lissu amekuwa Rais wa Shirika la wanasheria Tanzania. Mh Lissu tabia yake kwa sasa iko wazi kwa kila mtanzania. Hamweshimu Rais, Jeshi la Polisi na amesema anakamatwa kwa kuwa ana aklili za kutosha. Anadaganya. Tabia yake iko dhahiri. Mh Lissu ni jeuri na mbishi na anaona yeye tu yuko sahihi na hawezi kunyenyekea. Lakini ni kanuni ya dunia hii kwamba huwezi ukawa kiongozi bila kukubali kuongozwa kwanza. Mh Lissu anawadanganya watanzania kwamba anapigania demokrasia na haki, lakini muda utafika watanzania wengi watatambua kwamba anapigania maslahi yake na kikundi cha watu.

Huwezi ukawadanganya watu wote wakati wote, lakini unaweza kuwadanganya watu watu wote kwa muda

By Fred Mpendazoe

VIDEO:Maalim Seif Atangaza Msimamo Wake Baada ya Wabunge 8 Kufukuzwa....!!

0
0

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad amesema kuwa ameshangazwa na kuvuliwa ubunge kwa waliokuwa wabunge wanane wa chama hicho na kusema kwamba, njama hizo ni kulenga kuidhoofisha CUF pamoja na UKAWA kwa ujumla.

Maalim Seif aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na mwandishi wa Azam Tv ambapo alisema ameitisha kikao cha Baraza Kuu la Uongozi cha dharura ili kuweza kujadili hali ya chama hicho kwa sasa.

Aidha, Maalim Seif alisema ameshangazwa na uamuzi wa Spika wa Bunge kuwavua ubunge wabunge hao wa viti maalum, akisema kuwa jambo hilo limefanyika kwa haraka sana.

Spika alipokea taarifa ya Lipumba na kusema anashughulikia, lakini siku moja baadae aliwavua ubunge wabunge wetu akisema amejiridhidha kwamba taratibu za chama zimefuatwa. Spika amejiridhisha vipi kwa haraka namna hiyo tena akiwa nje ya nchi? alihoji Maalim Seif.

Kuhusu kikao hicho alichosema kitafanyika kesho (leo), alieleza kwamba maamuzi yatakayotolewa hapo ndiyo watakayoyasimamia kwani hilo ndilo baraza halali na hata Lipumba na Msajili wa Vyama vya Siasa wanalitambua hilo, alisema Seif.

BREAKING News: Wasira Aangukia Pua Tena...Rufaa Yatupiliwa Mbali

0
0
Mahakama ya Rufani imetupia mbali rufaa iliyokatwa na wapiga kura 4 wa Jimbo la Bunda Mjini kupinga ushindi wa Mbunge, Esther Bulaya.

MWIMBAJI Lulu Diva Adaiwa Kutoka Kimapenzi na Mwimbaji Jaguar wa Kenya....!!

0
0
BAADA ya kuweka hadharani kuwa amepata meneja mpya katika za muziki, msanii wa Bongo Fleva, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ anadaiwa kutoka kimapenzi na meneja huyo ambaye pia ni mwanamuziki kutoka Kenya, Jaguar.
Kwa mujibu wa chanzo, hivi sasa mrembo huyo amejiweka kwa Jaguar na hivi karibuni alipewa kipondo na bwana’ke wa zamani baana ya kubaini uhusiano huo.


“Safari zake Kenya zimekuwa haziishi, wenyewe wanadai wapo kikazi lakini mhh si kwa mapozi ya kimahaba wanayoonesha,” kilibonyeza chanzo na kuahidi kuwabofya picha akiwaona tena.
Baada ya kunasa madai hayo, Star Mix lilimtafuta Lulu na alipopatikana alisema;
“Ni uzushi kama unavyojua Wabongo, Jaguar ni meneja wangu tu ambaye ananisaidia katika kunisimamia katika muziki na si vinginevyo.”

Na Imelda Mtema 

MTEJA Amuua Mganga wa Kienyeji Baada ya Kushindwa Kumtibu...!!

0
0
Mganga wa jadi, Revocatus Kanjalanga (65) katika Wilaya ya Nkasi mkoani Ruvuma ameuawa kikatili kwa kuchomwa na mkuki mgongoni na mtu asiyefahamika ambaye anadaiwa kuwa ni mteja wake wa muda mrefu.

Ilielezwa kuwa wateja wa mganga huyo walikuwa wakimlalamika kuwa kwa kipindi kirefu mganga huyo amekuwa akiwatibu kwa kuwatoza fedha nyingi za malipo ya matibabu lakini wamekuwa hawaponi kupitia uganga wake.

Mtoto wa mganga huyo aliwaambia waandishi kuwa baba yake aliuawa juzi saa 1:30 asubuhi kwa kupigwa mkuki mgongoni akiwa anatembea mitaani katika kitongoji cha Chawe kilichopo katika Mji wa Namanyere wilayani Nkasi.

Alisema kuwa kwa muda mrefu watu ambao walikuwa wanatibiwa na baba yake walikuwa wakilalamika kutozwa fedha nyingi pamoja na mifugo lakini hawaponi, hali iliyosababisha kuanza kumuona kama tapeli.

Alisema watu hao walikuwa wanalalamikia kutofanikiwa matatizo yao ya kiafya, kutafuta mali pamoja na mazindiko.

“Pengine malalamiko hayo ndiyo yaliyosababisha mtuhumiwa aamue kumuua kwa kumchoma mkuki mgongoni, na aliyefanya hilo hajapatikana na mpaka sasa anatafutwa,” alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anasakwa.

TUNDU Lissu Afunguka Baada ya Kutoka Rumande

0
0
Tundu Lissu anasema baada ya kukamatwa na jeshi na polisi alizungushwa sana polisi na mwisho wa siku walimpeleka sehemu katika kituo cha afya ili apimwe mkojo lakini anadai alikata kupimwa mkojo kwani alikuwa anatuhumiwa kwa kosa la uchochezi  lisilo husiana na kipimo cha mkojo.
"Nilizungushwa sana siku ile lakini mwisho wa siku nikapelekwa maeneo ya Ocean Road hospitali ya kansa nikaambiwa Mhe. tunahitaji tukupime mkojo wako, nikamwambia nyie askari mimi nimeshtakiwa kwa uchochezi hivyo kupima mkojo unathibitishaje uchochezi kwa kupima mkojo. Wakasema sisi kuna vitu tunavitafuta, nikawaambia kama kuna vitu mnatafuta wakanishtaki kwanza kwa hilo kosa  ili sasa muende kwa hakimu mkamwambie kuwa mnawasiwasi na mimi kuna vitu mnavitafuta mnaweza kuvipata kwenye mkojo wangu, ila kama hajampata 'order' ya hakimu kwangu mkojo hamjapata" alisema Tundu Lissu 

Aidha Mhe Tundu Lissu anasema kuwa walikuwa wanafanya hivyo ili wapate vitu vya kuandikwa kwenye vyombo vya habari kwamba amepimwa mkojo ili waone kama kuna dalili za madawa ya kulevya na kusema ingewezekana Polisi wakasema kuwa yeye anaongea maneno mabaya kwa kuwa anatumia dawa ya kulevya.

Tundu Lissu aliendelea kulituhumu jeshi la Polisi kuwa wapo baadhi ya polisi wanatengeneza sana kesi na kuwabambikia watu kesi na kutengeneza ushahidi wa uongo
Hata hivyo Tundu Lissu amesema kuwa yeye mwenyewe hapendi kulala rumande na kuacha sehemu nzuri ya kulala yeye na familia yake, anadai kuwa hapendi kukamatwa na polisi wala kulala rumande wala magereza lakini kwenye masuala ya msingi yupo tayari kwa lolote lile.

Mke wa Mugabe Amtaka Mumewe Kumtangaza Mrithi

0
0

Rais wa Zimabwe ametakiwa na mkewe kumtaja ''mrithi'' wake ili kupunguza migawanyiko kuhusu mtu atakayemrithi.


''Rais hafai kuwa mwoga kumchagua mrithi wake na neno alke litakuwa la mwisho'',alisema bi Grace Mugabe.


Bwana Mugabe ndio kiongozi mzee zaidi na chama chake cha ZANU PF kimemchagua kuwania urais kwa mara nyengine mwaka ujao.


Lakini makundi pinzani yamekuwa yakiwania urais ili kuimarisha uwezo wao huku kukiwa na wasiwasi kuhusu hali yake ya kiafya.

Msukuma nurusa amchape makonde Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji

0
0

MBUNGE wa jimbo la Geita Vijijini na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita,Joseph Kasheku Musukuma nurusa amchape makonde hadharani Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Ihumilo kata ya Nkome Wilayani humo Thomas Halila, muda mfupi baada ya Mbunge huyo kuongoza mamia ya wananchi wa kijiji hicho kungíoa vigingi vilivyowekwa kwenye mipaka ya eneo la Serikali ya kijiji hicho linalodaiwa limeuzwa kinyemela Tsh. Million sita (600,000.),na mwenyekiti Halila, wakishirikiana na mtendaji wa kijiji hicho Charles Mbilingi kwa kutumia Muhtasari wa majina na saini hewa za wakazi wa kijiji hicho.

Hatua ya Mbunge huyo kuongoza,mamia ya wananchi wa kijiji hicho kisha kungíoa vingingi kwenye eneo hilo lenye ukubwa wa hekali moja na nusu ilikuja baada ya malalamiko ya wananchi hao kudai kutoshirikishwa na kwamba majina yaliyomo kwenye muhtasari wa kikao hicho na hata saini ni za kughushi hali iliyomlazimu Mbunge huyo kusoma jina moja baada ya jingine ili kubaini janja nyani iliyofanywa na mwenyekiti pamoja na mtendaji huyo.

Ambapo iligundulika,mhtasari uliotumika kuuza eneo hilo ni wa kughushi kutokana na wananchi hao kukana kushiriki kikao hicho kilichoketi 15/07/2017 kubariki uuzwaji wa eneo hilo mbali na majina yao kusomwa hadharani,huku diwani wa kata hiyo Masumbuko Sembe akigeuka mbogo baada ya jina lake kuwa miongoni mwa yaliyosomwa na Mbunge wao.

Kufuatia udanganyifu huo, Mbunge huyo akalazimika kuongoza wananchi kwenda kungíoa vingingi vilivyowekwa kwenye mipaka ya eneo hilo lililouzwa kwa mtu ambaye hakufahamika kwa majina wala makazi yake,sambamba na kumwagiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo Deus Seif kuondoka na mtendaji huyo.

Okoa Ndoa yako sasa..Ongeza Maumbile, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa Hata kwa wenye Kisukari

0
0

OKOA NDOA YAKO SASA. ONGEZA MAUMBILE, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA HATA KWA WENYE KISUKARI.
Tatizo la maumbile madogo, nguvu za kiume na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limekuwa likiwasumbua wengi na kusababisha kushindwa kujiamini ktk tendo hivyo kusababisha ndoa nyingi kuvunjika pamoja na mahusiano. Upungufu wa nguvu na hamu ya tendo husababisha mambo kama:-
(a)Uume kulegea wakati wa tendo
(b)Kukosa hamu ya tendo la ndoa
(C)Kuwahi kufika kileleni
(D)Uume kuchelewa kusimama baada ya round ya kwanza.
(E)Kuchoka sana baada ya round moja n.k
@Markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo kwa kutumia bidhaa zilizotengenezwa kwa mimea na matunda zisizo na kemikali wala madhara na kuthibitishwa kiafya.
PATA 👇👇👇👇
🍉🌿🍅🍒🍍🍓🍉🍎
1.HANDSOME UP ni kifaa chenye uwezo wa 99 % kuongeza uume (size unayohitaji) na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo hata mara 3 @130,000/=
Kwa Bidhaa hizi na nyingine kama:-
5.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi @150,000/=
7.Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) @200,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @130,000/=
9.Kuwa mweupe na soft mwili mzima bila kuacha sugu 120,000/=
10.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
11.Kupunguza au kuongeza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @120,000/=
Wasiliana nasi kwa (+255)
0767447444 au 0714335378.
NB: Matokeo ni uhakika na garantii na upate risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii.
Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

Aliyemuita Mbwa Wake Buhari Aachiliwa Huru Nigeria

0
0

Mashtaka yameondolewa dhidi raia mmoja wa Nigeria aliyemuita mbwa wake Muhammadu Buhari.
Joachim Iroko mfanyibiashara wa sokoni ambaye anajulikana kama Joe Fortemose Chinakwe alikamatwa 2016 akishutumiwa kwa kufanya kitendo ambacho kinaweza kusababisha ghasia.

Jaji mmoja kusini Magharibi mwa jimbo la Ogun alibaini kwamba upande wa mashtaka ulifeli kutoa, Wakosoaji waliwashutumu maafisa wa polisi kwa kukiuka uhuru uliopo.

Wakati huohuo msemaji wa rais Garba Shehu alisema kwamba bwana Buhari amekuwa akicheka kuhusu habari hiyo na kusema kuwa mtu yeyote aliyekuwa akimhusisha na kisa hicho cha mbwa haelewi.

Akizungumza na gazeti la kila siku nchini Nigeria ''The vanguard'' baada ya uamuzi huo ,bwana Iroko alisema kuwa hakupatikana na hatia na kuwashukuru waliozungumza kwa niaba yake.
Wakili wa bwana Iroko alisema kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuwasilisha mashahidi na kwamba mlalamishi pia hakuwepo.

Mtu huyo aliyewasilisha malalamishi yake mnamo mwezi Agosti 2016 aliripotiwa kuwa jirani.
Bwan Iroko alitembea na mbwa wake huku jina Buhari likiwa limeandikwa katika pande zote mbili za mnyama huyo katika eneo ambalo rais Buhari ana wafuasi wengi ,polisi walisema.

Maafisa walisema kuwa walikuwa na waiswasi kwamba hatua hiyo huenda ingewachokoza watu, ijapokuwa alisistiza kuwa alifanya hivyo ili kumpongeza na kwamba watu hawakumuelewa.
Bwana Iroko alisema huwapatia majina mbwa wake baada ya watu mashuhuri walio na mfano bora , na kwamba wengine amewaita Nelson Mandela na Obama.

''Nilimtaja mbwa wangu Buhari , ambaye ni shujaa wangu....Upendo wangu kwa Buhari ulianza wakati alipokuwa mkuu wa jeshi'', Baadaye aliviambia vyombo ya habari kwamba amepokea vitisho kifo kufuatia hatua hiyo.

Mwanariadha, Francis Damian aitoa kimasomaso Tanzania Jumuia ya Madola

0
0

Timu ya taifa ya Tanzania ya mchezo wa riadha ya vijana walio na umri chini ya miaka 17 imerejea kwa kishindo leo baada ya  kutwaa medali ya shaba ya michuano ya sita ya dunia ya vijana ya Jumuia ya Madola (Bahamas 2017 Commonwealth Youth Games) yaliyomalizika hivi  karibuni huko nchini India.

Mwanariadha wa Tanzania, Francis Damian amefanikiwa kushika nafasi ya tatu  katika mashindano hayo na kupata medali ya shaba kwenye mbio hizo kwa upande wa wavulana baada ya kukimbia umbali wa mita 3000 akitumia muda wa 8.37.51 wakipishana kwa sekunde 13.55 na mshindi wa kwanza Mkenya na sekunde 2.36  kwa mshindi wa nafasi ya pili ambaye ni raia wa Canada.

Kwa kutwaa medali hiyo, Damasi Francis ameiwezesha Tanzania kushika nafasi 19 kwenye ushindi wa jumla wa riadha nakufungana na Botswana, Cyprus, pamoja na Afrika Kusini.

Na kufanikiwa kushika nafasi ya 31 kwa ushindi wa jumla wa michezo yote na kufungana na  Nchi za Grenada,Namibia na Rwanda.

Katibu mkuu wa wizara ya Habari , Utamaduni ,Sanaa na Michezo, Elisante Ole Gabriel ameongoza mapokezi ya viongozi na wachezaji hao waliowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Julius k . Nyerere hii leo.

Tundu Lissu Afunguka Baada ya Ester Bulaya Kumgaragaza Tena Wassira Mahakamani...

0
0

From #tundulissutz - Nimetoka mahabusu Segerea jana asubuhi.

Leo Mahakama ya Rufaa ya Tanzania imetupilia mbali rufaa ya wapambe wa Mzee Stephen Wassira dhidi ya mbunge wa Bunda Mjini, Mheshimiwa Esther Bulaya ambae nilikuwa namuwakilisha.

Mahakama ya Rufaa imekataa hoja zote kumi za rufaa zilizowasilishwa na maCCM hao dhidi ya Mheshimiwa Bulaya. .

Mapambano yanaendelea. Hatutanyamazishwa na Dikteta Uchwara.
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live




Latest Images