Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Wampigisha Kwata Waziri wa Afya

$
0
0
Wabunge wanawake bila kujali itikadi za vyama juzi usiku waliungana kuibana Serikali wakishinikiza iongeze fedha za Bajeti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya mwaka 2014/15 ili kukabiliana na vifo vya kina mama na watoto.

Kibano hicho kilianza mapema asubuhi lakini moto zaidi uliwaka jioni wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha bajeti hiyo iliyotengewa Sh622 bilioni, ikiwa ni pungufu ya Sh131 bilioni ya bajeti ya wizara hiyo mwaka 2013/14 ambayo ilitengewa Sh753 bilioni. Wabunge wanawake 10 na wanaume wawili walichangia ikiwamo kutoa shilingi.

Kambi ya Upinzani ilianza kuibana Serikali ikisema imeweka rehani wananchi wake kutokana na kitendo chake cha kuchangia kiasi kidogo cha fedha za maendeleo za wizara hiyo.

Akiwasilisha taarifa ya kambi, Waziri Kivuli wa Afya, Dk Anthony Mbassa alisema Bajeti ya Sh622 bilioni na fedha za maendeleo ni Sh305 bilioni ambazo kati ya hizo, Serikali itatoa Sh54 bilioni tu, wakati washirika wa maendeleo watatoa Sh251 bilioni.

“Hii inaonyesha wazi kuwa Serikali imeendelea kuweka rehani wananchi wake kutokana na bajeti kuendelea kuwa tegemezi kwa wahisani,” alisema.

Kibano cha wanawake

Licha ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), William Lukuvi, Waziri wa Afya, Dk Seif Rashid na Naibu Mawaziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na Adam Malima kutoa ufafanuzi, walishindwa kuwashawishi wabunge hao waliokuwa wakililia nyongeza ya bajeti.

Hoja hiyo, iliibuliwa na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Cecilia Paresso baada ya kuondoa shilingi akiitaka Serikali itoe majibu ya sababu za kutoa Sh387 bilioni pekee kati ya Sh753 bilioni za bajeti ya mwaka 2013/14, jambo ambalo limekwamisha utendaji kazi wa wizara hiyo, ikiwa ni pamoja ya kushindwa kutekeleza Azimio la Abuja kuwa kila nchi itenge asilimia 15 ya bajeti kuu kwa ajili ya Wizara ya Afya ili kunusuru vifo vya kina mama na watoto.

Baada ya kauli hiyo wabunge kadhaa walisimama na kuunga mkono hoja hiyo licha ya Mwigulu kulieleza Bunge kuwa Serikali imepanga kuongeza kiasi cha fedha kilichobaki kabla ya Juni 31, mwaka huu.

Hoja hiyo ilifafanuliwa na Malima ambaye alisema Serikali imetoa Sh12 bilioni na kwamba tayari fedha hizo zimeshaingizwa katika akaunti ya Wizara ya Fedha kwa ajili ya kulipia deni la Bohari Kuu ya Dawa (MSD), ambalo ni Sh89 bilioni na deni la matibabu nje ya nchi ambalo ni Sh21 bilioni.

“Kwa nini Bunge lilipitisha Sh753 bilioni wakati likijua wazi kuwa haziwezi kupatikana, Watanzania watapataje huduma za afya?” alihoji Paresso.

Jaji Werema alijibu akisema Azimio la Abuja ni la hiari na hata kama nchi husika ikishindwa kulitekeleza haitapata adhabu yoyote, huku akisisitiza kuwa Serikali haikupata fedha za kufikia malengo ya azimio hilo na kuahidi kuwa kiwango cha fedha kilichobaki kitaongezwa kabla ya mwisho wa mwezi huu.

Unamkumbuka yule Trafic wa Kenya Alievaa Sketi Fupi? Kaja na hii Tena.

$
0
0


Yule trafiki wakike wa Kenya ambae kwa sasa Wakenya wengi wanamuita Koplo Linda Okelo ameingia tena kwenye headlines huko huko Kenya na kwa sasa ameamua kwenda mahakamani kupinga hatua ya kamati ya kinidhamu iliyowekwa.
Hatua hiyo ni ya kuchunguza madai ya kuvaa sketi fupi ambayo imesemwa kuwa ilikua nje ya maadili ya kazi na sheria za Jeshi hilo la Polisi la nchini Kenya.
Kupitia kwa wakili wake Tom ojienda Koplo Lindah amesema kwamba hakufanya kosa lolote kuvaa sketi hiyo hadi kulazimika kuundwa kamati ya kumchunguza na kutoa maelekezo ya adhabu anayostahili.
Lindah amesema kwamba asubuhi ya April  26 alifanya mkutana na OCPD wa kituo cha kiambu ili kuelekezwa,ingawa mkuu huyo wa polisi hakusema lolote kuhusiana na mavazi aliyovaa.
Ingawa May 2 Lindah alichukuliwa hatua za kinidhamukwa kosa la kuvaa mavazi yaliyombana kulingana na sheria za huduma za polisi-alivyo kuwa amevalia sketi fupi iliyombana saa saba mchana nje ya tawi la benki ya KCB lililopo kiambu.
Linda amedai kwamba sketi iliyo zua utata alikabidhiwa na afisa anaye shughulika na sare za polisi mwaka 2003 na amekua akivaa kila siku na mabosi wake hawakuwahi kulalamika kabla ya tarehe 26 Aprili.
Wakili wake Ojienda amesema kwamba wakati wa kikao cha kamati hiyo may 7 na may 9 Bii Okelo alichukuliwa hatua kimakosa kwani hakukua na sababu za kumuhukumu kulingana na mavazi yake,kesi yake itatajwa june 12 mwaka huu.

Audio: Mtoto wa Marehemu George Tyson 'Sonia' Atoa Ujumbe Mzito wa Majonzi Kumuaga Baba Yake

$
0
0
Jana simanzi ma majonzi vilitawala katika viwanja vya Leaders Club wakati mamia ya watu walipokuwa wakiaga mwili wa muongozaji wa filamu na vipindi vya televisheni, George Tyson aliyefariki katika ajali ya gari.

Moja kati ya matukio yaliyowatoa machozi mamia ya watu waliohudhuria katika tukio la kumuaga Tyson, ni pale mtoto wake wa kike aitwae Sonia alipokuwa akitoa neno/ujumbe wa kumuaga baba yake.

Sonia aliongea kwa majonzi maneno yaliyosababisha watu wengi watokwe machozi.

“You were kind na rafiki yangu kipenzi. Ulikuwa mtu ambaye ni rahisi kuongea nae na kunielewa. Daima ulikuwa unanitunza na kunidekeza. Na mara ya mwisho kuonana na wewe wiki iliyopita ulinambia ni jinsi gani nimekufanya uwe pride na mimi. And moreover I sing…I take a breath away. Na ninakuahidi, sitaacha kuimba kwa ajili yako. Nataka ufahamu kwamba nitakupenda milele. I will always Love You dad. Rest In Peace.”

Sonia ni mtoto wa marehemu aliyempata na muigizaji Monalisa ambaye pia ni mtangazaji wa 100.5 Times Fm.

Misikilize hapa:

Mke wa Mtu Ajeruhiwa Baada ya Kumfumania Mume Wake Akibinjuka na House Girl

$
0
0
Stori: issa mnally via GPL
UBABE! Tofauti na inavyoaminika na wengi kuwa mfumaniwaji huwa mpole, kibao kimebadilika, mfanyakazi wa ndani aliyejulikana kwa jina la Niachie amegeuka mbogo na kumchoma bisibisi bosi wake, Amina ‘Mama Zai’ aliyemfumania akiwa na mumewe aitwaye Amri.

Tukio hilo lilitokea juzikati maeneo ya Mbagala jijini Dar ambako mama Zai alimwekea mtego mfanyakazi wake huyo wa ndani baada ya kubaini kuwa alikuwa akitembea na mumewe wakati yeye akiwa kazini.

ISHU ILIVYOANZA
Akizungumza na paparazi wa kitengo maalum cha kufichua maovu (OFM) siku mbili kabla ya tukio, mama Zai alidai kuwa mumewe ana kawaida ya kufanya mapenzi na mfanyakazi wao wa ndani wakati yeye akiwa kazini hivyo akaandaa mtego ili kukomesha tabia hiyo.

KUMBE NI NESI
Mama Zai alizidi kumwaga data kuwa, yeye ni nesi katika hospitali moja ya mtu binafsi iliyoko Jangwani jijini Dar hivyo akiwa zamu ya usiku, mumewe hutumia mwanya huo kubanjuka na hausigeli.

“Ananivizia nikitoka tu na akijua nimeshafika mbali, anaingia chumbani kwa hausigeli na kuvunja naye amri ya sita,” alidai mama huyo.

MTEGO WANASA
Mama huyo alisema ili kufanikisha zoezi la kumnasa mumewe, alijifanya anakwenda zamu ya usiku kisha akajifungia stoo ili aweze kufanya fumanizi matata.

Kama kawa, OFM ilitia timu nyumbani kwa mama huyo ikiwa kamili na zana zake, ikakita kambi katika baa moja iliyo jirani na nyumba hiyo na ilipofika saa tano usiku, ishu ikatiki, baba Zai aliingia katika chumba cha mfanyakazi huyo kwa lengo la ‘kuharibu’.

'MISS IN ACTION’
Wakati makamanda wa OFM wakiwa ‘wanaseti’ kamera zao huku wakisubiri polisi na mwenyekiti wa serikali za mtaa wafike eneo hilo, mama Zai alivamia chumba hicho (alihofia baba atamaliza mchezo) na purukushani ya nguvu ikaanza.

Katika harakati za kujinasua katika kipigo cha bosi wake, hausigeli huyo aliokota bisibisi na kumchoma mama mwenye nyumba shingoni kisha kutimua mbio huku mume naye akiingia mitini.

Hermy B Afunguka Kuhusu Mtu Aliyemkosanisha na Wasanii wa B’Hits

$
0
0
Producer na CEO wa B’Hits Hermy B ameamua kufunguka ya moyoni kuhusiana na mtu wa karibu yake anayeamini kuwa ndiye aliyemkosanisha na wasanii wa B’Hits ambao kwa sasa hawako naye tena. Kupitia Twitter, Hermy amesema B’Hits ilivunjwa kutokana na maneno ya watu.

Leo natoa ya moyoni,Group ya Bhitz ilivunjwa kutokana na majungu na maneno ya watu ambao wengine ni marafiki zangu wa karibu sana na nawajua

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Na ushahidi wa nani amehusika kwenye kututenganisha tunao…hibi nimewakosea nini jamani…hiki kipaji tumepewa na mungu na ni kwa nia nzuri

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Wengi weni hamjui but maugomvi yote yale yametengenezwa na inauma kugundua kuwa nina marafiki ambao ni wanafki na hawanitakii mema.

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Siku Pancho joined Bhitz,mmoja wa rafiki wanafki akamfata na kumueleza kuwa aache kazi bhitz…leo hii pancho ndo bhitz…huo ni urafiki au?

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Vita ya ay na mwanaFA ilitengenezwa na mtu wote mnamjua..hivi kweli mimi ni wa kudai mamilioni kwa watu ambao tumeanzia kwenye shida pamoja?

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Kuna vingi jamii imepotoshwa kuhusu utendaji wetu na mengine…hamjui mengi coz tumekaa kimya…but ipo siku ntafunguka na kutaja majina

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Imajin mpaka nyimbo za bhitz hazipigwi kwenye baadhi ya radio but kwenye radio yangu nawapa full rotation bila kubana..hii ni haki?wanajijua

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Ipo siku wote tutarudi studio & do wat we do best,sitoacha kutoa nyimbo coz jamii lazima itambue uwezo wao,Bhitz and that team was the BOMB

— Hermy B (@HermyB1) June 4, 2014

Kwa Mnao Kuza Makalio Kwa Dawa za Kichina na Kienyeji hii Inawahusu

$
0
0
Kwa wale wadada wanaotumia dawa za uongeza makalio ziwe za Kichina ama za Kienyeji  wakiamini kuwa ndio wataonekana wazuri na kuwavutia wanaume, au haujatumia ila unafikiria kutumia siku moja,angalia hapa alafu utapata jibu utumie au ubaki na maumbile yako ya halisi, Huyo Mdada Amekuwa hivyo baada ya kutumia dawa hizo kwa muda mrefu na kupata hayo madhara kama unavyoona pichani

Hii Kali Sana eti CNN, BBC na AL Jazeera Wanajua Kuwa Raila Odinga Ndio Raisi wa Kenya

$
0
0
Former Prime Minister Raila Odinga told a mammoth crowd of his supporters in Eastleigh that many foreign media houses view him as the legitimate President of Kenya.

Speaking after visiting Eastleigh Estate on Thursday, Raila said many media stations around the world usually call him when there is a problem facing Kenyans.

He cited the recent concentration of Somalis and Muslims at Kasarani, saying BBC, Aljazeera and CNN called him asking him what is happening in Kenya.

Raila also said during the Westgate Shopping Mall terror attack last year, over 50 foreign media stations called him asking him the details of the attackers.

He said it is only a group of few Kenyans who don’t know that he is the “legitimate President of Kenya” because he has won two consecutive  elections only to be rigged out by Kibaki’s and Jubilee’s administration consecutively.

Paparazi Wamnasa Lupita Nyong'o Ndani ya Nguo za Kuogelea na Shanga Kiunoni (Photos)

$
0
0




Akiwa Mapumzikoni , Paparazi Bila ya Ajizi walifanikiwa kumfotoa Mwanadada Lupita Nyong'o akiwa Beach akifurahia maisha bila yeye kuwa na Habari hata kidogo ....
Mmhh Any Comment?

Ukamataji Wanaodai Kutibu Ukimwi Ufanywe kwa Vitendo

$
0
0
MATANGAZO ya watu mbalimbali kuibuka na kudai kutibu magonjwa mbalimbali yamekuwa yakiongezeka kadri siku zinavyosonga mbele kwa kubandikwa mitaani pamoja na kutangazwa sehemu mbalimbali.

Suala hili, limezidi kushika kasi kutokana na ukweli kuwa kwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza kama kisukari, presha, magonjwa ya figo pamoja na mengineyo.

Vyombo vya habari vimekuwa na mchango mkubwa katika kuwatangaza watu hawa bila kutambua iwapo dawa hizo zimethibitishwa au hapana jambo ambalo ni hatari kwa afya za wananchi.

Watu hawa wamekuwa wakitumia mianya ya magonjwa hayo ukiwemo Ukimwi kwa kujipatia fedha mbalimbali kwa kulipia matangazo hayo katika vyombo vya habari na kutangazwa jambo linalofanya watu kuamini kuwa iwapo limetangazwa ni wazi limepitishwa kutibu magonjwa mbalimbali.

Hivyo, ni vema Wizara ya Afya ambayo imetangaza bungeni kuviagiza vyombo vya dola, kukamata waganga wa jadi, wanaojitangaza kutibu magonjwa ya Ukimwi, kisukari na shinikizo la damu.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid aliwasihi wataalamu wa tiba asili na tiba mbadala, kuacha mara moja, kujitangaza kuwa na uwezo wa kutoa tiba dhidi ya ugonjwa wowote ule ambao uwezo huo haujathibitishwa kitaalamu.

Alisema hilo ni kosa kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha tiba asili na tiba mbadala, na kutaka matangazo hayo yaondolewe mara moja.

Utata wa suala hili, linakuja ni jinsi gani wananchi wanaweza kutambua tiba iliyoidhinishwa kitaalamu na ambayo haijaidhinishwa ili vituo vya redio viweze kutangaza ambazo zimeidhinishwa.

Kutokana na changamoto hiyo, bado wizara husika ina kazi katika kusaidia kutoa elimu stahili kwa wananchi juu ya dawa hizo kwani wote tunaamini mtu anapokuwa akisumbuliwa na magonjwa anahangaika kupata tiba.

Ni vema wizara kwa kutumia wataalamu wake kuwa na kitambulisho maalumu kwa vyombo vya habari kutangaza matangazo ya dawa husika ili wanapotaka kutangaza kuhakikisha yameidhinishwa na Serikali.

Pia ni vema, suala hilo la kuwakamata waganga hawa wanaojitangaza kufanyika kwa vitendo kwani kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia kauli hizo lakini bado matangazo mitaani ya kwenye vyombo vya habari yakiendelea.

Kuendelea kwa wizara kutoa matamko bila kutumia vitendo ni sawa na kazi bure kwani watu hao wamekuwa wakiongezeka kwa muda kadhaa na kuwachanganya wananchi jambo ambalo wanafanya kwa uwazi hivyo ni rahisi kuwachukulia hatua.

Kwani ikiwa wanatumia vyombo vya habari wanaelekeza mpaka mahali wanapotolea huduma hizo na hata katika matangazo wanayobandika barabarani pia wanajielekeza walipo sasa jambo la kushangaza ni nini kinachokwamisha katika kuwakamata?

Pia, ninashauri kuwa katika kukabiliana na watu hawa hatari kwa afya za Watanzania kwani kwa kuwadanganya kutibu magonjwa mbalimbali hufanya wagonjwa kuacha kutumia dawa stahili ni vema elimu ikatolewa kwa nguvu zote.

Pia Wizara ingeshirikiana na manispaa zote za miji kuhakikisha wanaondoa matangazo yote yaliyobandikwa mitaani na kisha kuwachukulia hatua watu hao kwa kuwalipa vijana watakaowekwa kuangalia mabango hayo na kuyaondoa.

Jeshi la Polisi Linadaiwa Kuvamia Nyumbani kwa Lwakatare na Kuwakamata

$
0
0
Taarifa ya awali...

Katika hali ile ile ya mwendelezo wa kutumikia maelekezo na maslahi ya CCM dhidi ya wapinzani wa kisiasa wa chama hicho, Jeshi la Polisi usiku huu limevamia nyumbani kwa Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA, Wilfred Lwakatare na kumkamata housegirl wake.

Kama hiyo haitoshi, jeshi hilo la polisi limewakamata wafanyakazi wengine wawili (house boys) wa Lwakatare. Hadi muda mfupi uliopita vijana hao wawili, walikuwa wako Kituo cha Polisi Mbezi huku msichana wa kazi wakizunguka naye kwenye gari la patrol bila kumfikisha kituoni.

Jeshi hilo la polisi kupitia kituo hicho cha Mbezi lilikuwa linawatisha kila mtu anayekwenda hapo kituoni kuulizia sababu za vijana hao kukamatwa, lakini hatimaye mmoja wa watu walioko kituoni hapo ametonya kuwa polisi wanasema mmoja wa vijana hao kesi yake iko Arusha!

Kijana anayetaka kubambikiwa kesi huko Arusha ni mwanagenzi kabisa mjini. Hata ukimwambia aende Chalinze au Wami hawezi kupajua. 

Hatimaye mbinu za CCM kupitia jeshi la polisi ya kutaka kukichafua CHADEMA au viongozi wake kwa kutumia kes za kubambikia ugaidi imerejea tena...

Tutawaletea taarifa kamili...
JF

Hatupendi Kuwa na Historia Mbaya kuwa na Wanaume weng ila Inabidi

$
0
0
Mwanaume wa kwanza, nilikutana nae kidato cha tano lakini baada ya matokeo kidato cha sita aliniacha eti kwa sababu mimi nimefauru hivyo chuo lazima nitamsaliti nilimsihi sana kwa sababu niliamini,kuna maisha zaidi ya elimu but ugomvi kila siku nikaamua kuachana nae japo tulipendana sana.

Mwanaume wa pili huyu alinipenda sana lakini kumbe alikuwa na mtu mwingine before ambae ni rafiki yangu nae hakutambua kuwa mimi na yule dada ni marafiki. 

Lakin baada ya kungundua alinambia anamuacha coz ni kweli alinipenda nikamweleza mimi namuacha coz sipendi zaidi, aendelee na rafiki yangu na nilimuacha.

Mwaume wa tatu huyu nilianza nae nikiwa second year first semister, kijana ni mchaga jamani wachaga wanapenda asikwambie mtu nilienjoy aisee huyu kaka, kaka alipenda mpaka kasahau kusoma na course yake ni ngumu kisa kakolea mapenzini akadisco mwaka wa 3.

Kaenda kitaa na bado alinipenda zaidi kumbe huyu kaka nae ni yatima hivyo alikuwa anasomeshwa na mdada ili baadae waoane kaka kakutana na mimi kasahau fadhila za yule dada.

ATM ya mdada mimi niliishi nayo na kuchukua pesa nitakavyo bila kujua ni ya mwanamke jamani huruma. Kijana kafeli kaenda kwa mdada wake lakini bado anawasiliana na mimi.

Siku ya siku mdada kanitafuta analia vibaya mno jamaa kamwambia hampendi ananipenda mimi kwa kweli niliona machozi ya yule dada yananiletea mkosi, nilimwacha japo mpaka sasa ananipenda sikuweza kuendelea nae sitaki ni muongo.

Mwanaume wa 4, jamani huyu ni Dk hosipital 1 hapa Dar jamani, kaka sikujua ni mhuni kiasi hiki, ajabu alinipenda mpaka sikuweza kutambua tabia yake.
Kila akisema anataka kujitambulisha home moyo wangu ulisita sana, jamani nilimfumania, nikamwacha.

Sasa kumbe sikujua ameniweka moyon na alinitegemea kuwa mke now ninavyosema alichanganyikiwa mpaka alikosea kumtibu mgonjwa kamletea matatizo alisimamishwa kazi. Ila karudishwa now mimi sikumuhitaji sio mwaminifu angenisumbua sana.

Mwanaume wa tano huyu alikuwa anaishi Marekani kule alienda kimasomo ,kumbe tayari alikwisha oa ila waliachana na mkewe baada ya miaka 3 tena kaoa kwa taratibu za kikanisa, mimi sikujua kabisa, alinipenda sana but ukweli hawezi kuoa tena kwa taratibu za kikanisa ila mtaishi kama wazinifu tu,pia sikumumini sana.


Mwanaume wa sita, jamani before sijampata mwanaume huyu kwanza nilikaa miaka 3 single, nilimuomba mungu sana msamaha na kuvunja mikosi, sasa mimi nilibadilishwa na kuwa mwingine.

Tena roho mtakatifualizidi kukaa ndani yangu na hata sasa, nilipata mume na sasa nimeolewa, mume wangu nampenda na ana hofu ya mungu.

Ushauri, mume bora hutoka kwa mungu , na acha historia yako ya nyuma wala isikuumize wanaume waoaji wapo, tena ukiomba kwa kumaanisha

Pili usivunje amri ya sita wala usiruhusu kujuana na mwanaume kabla ya ndoa nimejifunza mengi sana.

Sabuni Hizi Zinaongoza Kuachanisha Ndoa

$
0
0
Ukienda guest au hoteli yoyote hapa TZ unakuta sabuni hizi za EVA zimewekwa kwenye bafu la choo cha chumba ulichopanga..

Kwa kawaida ni adimu sana kuikuta inatumika nyumbani,hivo nadhani hata watengenezaji wa hizi sabuni wanajua kuwa soko lao kubwa ni nyumba za wageni..

SABUNI HIZI ZINA HARUFU SANA..
Wanawake wanazijua sana harufu za sabuni hizi na ikitokea umerud nyumbani na harufu yake una maswali magumu ya kujibu,.

Inavosemekana baadhi ya ndoa zimevunjika kwasababu ya harufu ya hizi sabuni..

Ni wakati mwafaka wa kampuni inayozitengeneza kuangalia kama kuna umuhimu wa kuweka harufu kali kwenye bidhaa yao hii..

Wasiozijua kwa jina picha hiyo hapo..

Sintah Ampa Pole Capt. Komba Kwa Kuchafuliwa na Picha Fake

$
0
0
"Kwakweli watu wakikuamulia wamekuamulia aisee, picha hizi ni za uzushi na zimetengenezwa wabataka kumchafua Mh Komba, hivi uko chumbani na baby wake wewe uvae khabga yeye awe na shirt badala ya vest kama kweli mko wenyewe kimahaba? Khaa eti na mabusu juu inamaana Mh alikuwa anaona picha zinapigwa na yeye akauchuna?? maana ni picha za kujiandaa haswa 

Pole sana Mh Komba tupo na wewe katika hili kuhakikisha uko salama salmini na haya majitu ya kutengeneza pics fake" Sintah

Hivi Huyu Halima Kimwana ni Nani Kwa Diamond?

$
0
0
Kuna watu wanashangaza kidogo,siyo kwamba tunawafuata majumbani mwao na kugundua tabia zao,kwamba wanakula sana,wachoyo,wachafu au hawapatani na majirani zao,hapana,wanayoyafanya ama kuzungumza,wanatufanya tuwatambue.Lakini tunaishia kuwajua kwa majina na matukio yao.Ukiniuliza babu Tale ni nani,fasta nitakujibu kuwa ni msaidizi wa shughuli za Diamond,Romie Jones nitakuambia ni ndugu yake Diamond,Wema Sepetu,ni usingizi wa Diamond,kwa maana ya mpenzi,lakini ukiniuliza Halima Kimwana ni nani,naweza kulipuuzia swali lako kwa maana sitambui wala kujua ni nani kwa Diamond.

Siwezi kuacha kujiuliza hivi huyu binti wa mjini  ni nani kwa Diamond?rafiki,dada,shemeji yake,mpambe au nani,Au ndiye kiunganishi chake kwa wale viumbe waliosababisha aitwe sukari ya warembo?yeye ni nani haswa hata afikie hatua ya kumchagulia Diamond mpenzi wa kuwa nae,ni nani hasa hata afikie kumaindi uwepo wa Wema kwenye himaya ya Diamond,kajina kake kamezidi kukaa on ea kwa kipindi kirefu kutokana na uwepo wake karibu na Diamond,ana nguvu sana kwa Diamond,Nilipuuzia kwa muda mrefu sana nikiamini ni mtu wake wa karibu wa kumshikia poda awapo lokesheni ya video zake,au anashikilia simu zake awapo stejini,baadae nikadhani kuwa huenda ni msaidizi wa mambo binafsi ya Diamond.Lakini kufikia hatua ya kumpangia Diamond mwanamke  wa kuwa nae,kidogo hapo nashindwa kuelewa,yeye ni nani kwa Diamond?
Wadau mnaojua uhusiano wa huyu dada hebu mtujuze,ni nani,anafanya shuhuli gani,naamini wote mliosoma gazeti hilo mna kiu ya kujua.

Source:Gazeti la KIU ya jibu toleo no 1275 la tarehe 2-5/6/2014 
Via Sintah Blog

Hivi Ndivyo Fastjet ilivyohakikisha Diamond Anarudi na Tuzo.

$
0
0
Kampuni ya safari za ndege nchini tzee ya Fastjet, imetokea kumpa sapoti mkali wa Afro Pop Dimond Platnumz, kwa kusimamia swala zima la usafiri wa Diamond na kuhakikisha kuwa anafika nchini africa kusini pamoja na wapambe wake aliongozana nao salama, mbali na sapoti hiyo, ile katika kuzidi kuweka msisitizo zaidi mbali na kuhakikisha anatia mguu sauzi, imezidi kutoa promo kupiti matangazo yake ikiwa inamtangangaza mkali huyo anayewania tuzo nyingi hivi sasa ikiwemo hiyo ya Mtv MAMA.

Diamond alizidi kufunguka kupitia akaunti yake ya instagram na kusema haya:

“Asante sana @fastjetofficial kwa kunisafirisha mimi, Familia yangu na team yangu nzima kuelekea kwenye Tuzo za MTV Awards Nchini South Africa.. hakika nyinyi ni Mfano Bora.. Kama Hauna Taarifa bado, Kampuni ya Fast jest sasa imeanzisha huduma mpya ya kutoka Tanzania hadi South Africa…“

Demu wa Young Killer Autafuta U-Super Staa Kwa Nguvu, Sasa Atuonyesha Umbo lake Live(Photos)

$
0
0

Baada ya kugeuza noti za buku 10 kuwa shuka mrembo wa rapper wa ‘Mrs Supastaa’ Young Killer aitwaye Halimaty ameendelea kumake headlines kwa picha zake kwenye mtandao wa Instagram. Na sasa ameamua kuwaonesha followers wake umbo lake lililomfanya apate cheo cha ‘Umrs Supastaa’ 

Hatimaye akaunti ya Twitter ya Diamond yawa Verified.

$
0
0
Diamond Platinumz ambaye kwa sasa yuko Afrika Kusini akijiandaa na shughuli ya utoaji wa tuzo za MTV,leo mtandao wa Twitter umempa umiliki halali wa akaunti yake ya Twitter kwa kuwa Verified.
Diamond Platnumz anaungana na mastar kadhaa wenye  verified kwenye akaunt zao ambao ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete,Ambwene Yesaya ‘Ay’,Flavian Matata.January Makamba na baadhi ya mastaa.

Diamond Kuperform MTV Mama Awards na Davido Kesho…Angalia Baadhi ya Picha za Rehearsal

$
0
0
Siku ya Kesho Diamond Platnumz na Davido watalishambulia jukwaa kutumbuiza nyimbo ya my number one remix . Tayari wameanza maandalizi ya performance hiyo na hizi ni baadhi za picha za maandalizi hayo..




Huyu ndiye aliyemloga Cristiano Ronaldo asicheze Kombe la Dunia

$
0
0
Mwanzo wa majerahaa ndo huyuAlipo kuwa kwenye mahojiano kwenye kituo cha Radio cha Angel Fm Nana Kwaku Bonsam alisema kuwa yeye ndie kahusika kwa kumroga Christiano Ronaldo ili aweze kuzikosa match kadhaa muhimu za kombe la dunia ikiwemo ile ya timu ya Ghana na Ureno na alifanya hivo kama njia moja wapo yakuivunja nguvu timu ya Ureno.

Alisikika akisema hivi kwa Kingereza: “I know what Cristiano Ronaldo’s injury is about, I’m working on him,” Nana Kwaku Bonsam alisema kwenye kituo cha Radio cha Angel Fm.

Vicky Kamata Afunguka Kuhusu Ndoa yake Baada ya Kudaiwa Kuzuiliwa Kufungwa

$
0
0

Mwanamuziki wa zamani na mbunge Vicky Kamata baada ya ndoa yake kudaiwa kuzuiliwa kufungwa kutokana na kudaiwa mwanaume aliyetaka kufunga naye ndoa ana ndoa nyingine, amefunguka kwa kudai kuwa hizo zilikuwa ni habari za kutungwa na hazikuwa na ukweli wowote.
Vicky ameiambia amplifaya ya Clouds fm jana kuwa maneno mengi ambayo yalikuwa yanazungumzwa kuhusu ndoa yake kutofungwa yalikuwa yametengenezwa na watu.
Kweli ni maradhi kama ambavyo ilitangazwa wakati huo, lakini pamoja na hayo mimi bado nasema mungu alikuwa hajapanga ,alikuwa hajaruhusu kuwa tarehe 24 mwezi wa tano iwe siku wa kufunga ndoa.

“Mimi kama binadamu na mwenzangu tulipanga lakini mungu alipanga vinginevyo , kwaiyo siku zote mapenzi ya mungu huwaga yanatimia siyo mapenzi ya binadamu.

“Ni kweli alishawai kufunga ndoa lakini ninachofahamu mimi ni kwamba waliachana kihalali kabisa kwa divorce ya mahakama ya Kinondoni mwaka 2012 na mimi siyo mtoto mdogo kwamba ninaweza mpaka nikafikia hatua hiyo bila kuwa nimemchunguza huyo mtu.

“Kuhusu swala la kwamba alikuwa na mke wake , mke wake alikwenda kuzuia Kanisani sijui alikuja Bungeni, yale yalikuwa tu ni maneno ambayo yalitengenezwa na baadhi ya watu kwa interest zao ,lakini siyo kwamba nilikuwa nimeingilia ndoa ya mtu hata kidogo, kwa sababu ata huyo mke wa kwanza wa huyo aliyekuwa mchumba wangu aliongea na vyombo vya habari akasema mimi sijaenda Dodoma wala sijaenda kuzuia harusi.

“Kwaiyo maneno yaliyokuwa yamezagaa ,sijui mke wake amezuia yalikuwa ni maneno ya kutengenezwa na watu tu kwa nia zao wenyewe lakini siyo kweli.
“Kuhusu kwamba hajulikani alipo mimi hilo siwezi kumjibia, mimi nafahamu kwamba yupo na anaendelea na shughuli zake kama kawaida, kama ambavyo mimi naendelea na shughuli zangu kama kawaida, tunawasiliana, yani cha kufahamu tu kwamba ndoa haikufungwa basi.

“Hata kama kuna mkono wa binadamu katika jambo hilo mimi naamini mungu ndo mwenye mamlaka na Mungu ndiyo mwenye kupanga mambo, kwaiyo kama Mungu alikuwa anataka hiyo harusi ifugwe ata kama kungekuwa na binadamu mwingine hataki bado ingefungwa…

“Kwaiyo mimi sitaki kuamini sana kwamba kuna waheshimiwa wabunge wenzangu wamechangia kwa kiasi kikubwa kwamba ndoa ile isifungwe, mimi ninaamini ni mapenzi ya Mungu tu yametimizwa kwa staili hiyo” Alisema Vicky

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images