Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104702 articles
Browse latest View live

DIAMOND Awatolea Mapovu Wanaomsakama Zari Kuhusu Msimba wa Mama yake...Awaita Chupi Kunuka...!!

$
0
0


By diamondplatnumz - Kuna vichupi kunuka wanajifanya wanajua sana uchungu wa Misiba ya watu.... Mtoto wa watu katoka katika matatizo mfululizo, anatakiwa apelekwe sehem tulivu apetiwepetiwe apate faraja!...sasa kama nyie hamna mabwana wa kuwafanyia hayo, Msijifanye ni Tamaduni na kulazimisha kila mtu awe kama nyie, eti kutwa nzima ajifungie chumbani kulia... Pambaneni na Mahusiano yenu...! Nina siku 5 za kumpetipeti... leo ndio kwanza Ya kwanza

MAKUBWA...Mwanadada Witness KIBONGE Mwepesi Kaanza Kufata Nyendo za Gigy na Amber Lulu Kupika Picha Tata!!!

$
0
0
Picha hapo chini zinajieleza huyu mwanadada Witnes mwenyewe hupenda kujiita kibonge mwepesi dizaini kama kaanza kuiga mikato ya Gigy money na Amber lulu kupenda kupiga picha huku sehemu kubwa ya mwili wake ikiwa Wazi(nusu uchi)

Weka Comment yako hapo Chini ukimshauri Witness Kibonge

RIHANNA Awachanganya Mashabiki Wake..Muonekano Wake Huu Wawachukiza Wengi..Tetesi za Ujauzito

$
0
0
WANAMUZIKI, Robyn Rihanna Fenty ‘Rihanna’ anadaiwa kuwa mjamzito kutokana na muonekano wake kifuani, usoni, matendo na mavazi.
Kwa mujibu wa mtandao mmoja umedai kuwa, Rihanna anadaiwa kushika ujauzito wa mpenzi wake Bilionea Hassan Jameel ambapo ameongezeka uzito wa pound 50 (kilo 23) tofauti na kawaida.

Julai Julai 25, mwaka huu Rihanna alionesha vazi lake jekundu lililoonekana la hadhi kubwa ambalo lilipendwa na wanamitindo alipokuwa kwenye maonesho huko London ndipo maneno ya kuwa mjamzito yalipoanza kuvuma huku watu wakidai kuwa maziwa yake na uso uliojaa ndiyo unaoonesha kuwa ni mjamzito.

DIAMOND Ampeleka Zari Dubai...Waomboleza Kwa Staili ya Kipekee...Washabiki Watoa Mapovu

$
0
0

Zarithebosslady na Diamond Platinumz baada ya msiba wa mama yake Zari mama mkwe wa diamond kuisha hivi punde waamua kwenda kujiliwaza pande za dubai na kupost mavideoz online. watu wengi wameonyesha kutopenda kwa kuwa zari hajaomboleza vya kutosha msiba wa mama yake.


Je Mdau ni sawa kufanya mambo hayo hata ikiwa arobaini ya msiba haijafika?

TOA MAONI YAKO

HOJA Mbili zilivyomtoa TUNDU Lissu Mahabusu Dar

$
0
0

Hakimu Wilbard Mashauri jana alitumia hoja mbili kumpa dhamana, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu aliyekuwa mahabusu tangu Julai 19 akituhumiwa kwa uchochezi.

“Upendo wa dhati” ulioonyeshwa na jopo la mawakili 18 waliojitokeza kumwakilisha na rekodi yake nzuri, vilitosha kumshawishi hakimu huyo mkazi mkuu kumuachia Lissu, ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS).

Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki, alikuwa katika hali ya kawaida wakati hakimu Mashauri akisoma uamuzi wake wa pingamizi la dhamana lililowekwa na upande wa mashtaka na baada ya uamuzi huo alitoka nje akitabasamu, akipunga juu mkono wake wa kushoto huku akinyoosha vidole viwili kuashiria nembo ya Chadema.

Katika mkono mwingine alikuwa ameshika chupa ya maji ya kunywa ya lita moja ambayo mwanasheria huyo amewahi kuliambia gazeti hili kuwa huhakikisha anaibeba kila anapokamatwa na polisi kwa ajili ya kuitumia kama mto anapokuwa mahabusu.

Mwanasheria huyo alikuwa amevalia suti ya rangi ya bluu na fulana nyekundu na alisindikizwa na askari wengi kuelekea eneo la kutia saini dhamana kabla ya kumsindikiza hadi kwenye gari lake.

Tofauti na siku nyingine ambazo hupata nafasi ya kuzungumza na waandishi wa habari, baada ya kupata dhamana, Lissu hakufanya hivyo jana kutokana na kutakiwa na askari hao aondoke eneo hilo.

Ulinzi uliimarishwa na ni watu wachache waliomlaki kwenye viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya polisi kuwazuia wengi katika lango la kuingilia.

Lissu alikamatwa siku tisa zilizopita akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) alikoenda kwa ajili ya safari ya Kigali nchini Rwanda kushiriki mkutano wa wanasheria Afrika Mashariki.

Alisomewa mashtaka siku tatu baadaye akituhumiwa kutoa lugha ya uchochezi dhidi ya Rais.

Mara baada ya kukamatwa, mmoja wa mawakili wake, Fatma Karume aliiambia Mwananchi kuwa polisi hawakutaka Lissu adhaminiwe kwa madai kuwa upelelezi ulikuwa haujakamilika.

Kabla ya kupelekwa mahakamani, polisi walimpeleka nyumbani kwake na kupekua na baadaye kutaka kuchukua kipimo cha mkojo, jambo ambalo Lissu alikataa kwa hoja kwamba kipimo hicho hakina uhusiano na makosa wanayomtuhumu.

Julai 24, alipelekwa mahakamani lakini hakupewa dhamana baada ya upande wa mashtaka kudai amekuwa akirudia kufanya kosa hilo, huku mawakili wake wakisema hadi sasa hajapatikana na kosa na kwamba polisi wamekuwa wakimkamata tangu mwaka 2015 na hakuna upelelezi uliokamilika hadi sasa.

Lakini jana, Hakimu Mashauri alimpa Lissu dhamana akieleza kuwa upande wa mashtaka umeshindwa kutaja kesi ambayo mwanasheria huyo mkuu wa Chadema amewahi kuruka dhamana.

Hakimu Mashauri alisema hakuna uthibitisho kuwa Lissu aliwahi kuruka dhamana na hiyo haitoshelezi kumuweka mahabusu kwa sababu ya usalama wake.

Hoja ya pili iliyomuweka Lissu nje kwa dhamana ni ile ambayo Hakimu Mashauri aliitaja kuwa ni “upendo wa dhati”.

Alisema Lissu anawakilishwa na mawakili 18, kitu kinachoonyesha wana upendo kwake na ndiyo maana walisimama kidete.

Lissu aliachiwa huru baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao kila mmoja alisaini dhamana ya Sh10 milioni.

Pia, ametakiwa asitoke nje ya jiji la Dar es Salaam bila ya kuwa na kibali cha mahakama na wakili wa Serikali, Simon Wankyo alisema upelelezi umekamilika na ameiomba mahakama ipange tarehe kwa ajili ya mshtakiwa huyo kusomewa maelezo ya awali na Hakimu Mashauri amepanga asomewe Agosti 24.

Awali, baada ya mahakama kuweka masharti ya dhamana, kesi iliahirishwa kwa muda kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 3:30 kusubiri wadhamini ambao walikuwa wamezuiwa kuingia eneo la mahakama kutokana na ulinzi mkali uliokuwepo jana.

Baadaye, wadhamini waliingia kuwasilisha nyaraka zao, kabla ya Lissu kuachiwa huru na saa 3:50 asubuhi na kuondoka.

Jopo la mawakili wa Serikali linaundwa na Kishenyi Mutalemwa, Wankyo, Paul Kadushi na Tulumanywa Majigo, wakati Lissu anawakilishwa na mawakili 18 wakiongozwa na Karume na Peter Kibatala.

Katika kesi hiyo, Lissu anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi Julai 17 akiwa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam, aliposema “Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ina ubaguzi wa kifamilia, kikabila, kikanda na kidini”.

Chato nao wadhaminiwa

Wakati hayo yakifanyika Dar, Mahakama ya Wilaya ya Chato nayo imetupilia mbali pingamizi la dhamana dhidi ya washtakiwa 51 ambao ni viongozi na wanachama wa Chadema ambao wameshtakiwa kwa kukusanyika katika Kata ya Muganza bila ya kibali. Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Jovith Kato alitoa uamuzi huo juzi baada ya kupitia hoja za pande zote mbili.

Alisema kwa mujibu wa Ibara ya 13 (6) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni marufuku mshtakiwa wa makosa ya jinai kutendewa kama mtu mwenye kosa hilo mpaka itakapothibitika.

Washtakiwa hao walidhaminiwa na watu wawili kila mmoja ambao walitakiwa kuweka dhamana ya Sh500,000.

Install App Namba Moja Tanzania Kwa Habari za Udaku na Mengine.....Udaku Special App

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza HAPA Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

ONGEZA Hips, Makalio, Kuwa Softi na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Products hizi

$
0
0
PENDEZA SASA:-ONGEZA HIPS, MAKALIO NA MAPAJA, KUWA MWEUPE NA SOFTI, ONGEZA MAUMBILE YA KIUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO N.K @markson_beauty_pr Tunakuletea bidhaa bora zenye matokeo ya uhakika na haraka zisizo na kemikali wala madhara. Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa kiafya. NB. Matokeo ni uhakika na garantii na risiti 🍉🌿🍅🍍🍒🍉🍓🍅🍒 BIDHAA ZETU:- 1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @130,000/=
2.Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200,000/=
(b)Vidonge @180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @150,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @130,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a)SHARK POWER gely ya kupaka (Inaongeza inch 6-7) @150,000/= (b)Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/= (C)HANDSOME UP ORIGINAL- kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo @250,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150,000/=
7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @130,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @130,000/= (b)Mkanda wa kawaida @100,000/= (c)Micro-computer belt wa umeme @200,000/=
9.Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @130,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @130,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @120,000/=
12.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/= Wasiliana nasi :- (+255) 0767447444 au. 0714335378 TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. 👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ............... Follow us on instagram @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

BAADA ya Kiki Kumwishia..Harmorapa Amgeukia Rais Magufuli....

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva ambaye haishiwi vituko, Harmorapa amekunwa na utendaji kazi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt John Pombe Magufuli wa kubana fedha kitu ambacho kimewafanya watanzania kutumia pesa kwa nidhamu.


Harmorapa amesema kipindi hiki cha awamu ya Rais Magufuli kimewafanya watanzania kuithamini pesa ikiwa ni pamoja na kupunguza matumizi yasiyo na ulazima kitu ambacho ni tofauti kabisa na kipindi cha nyuma.

“Kwanza mimi nimpe tu pongezi kwa sababu amefanya watu wengi sana wajue kuhangaika na wajue kufanya kazi tofauti na kipindi cha nyuma watu walikuwa wazembe”,amesema Harmorapa baada ya kuulizwa swali la kuhoji utendaji kazi wa Rais Magufuli kwenye kipindi cha Twenzetu cha Times FM.

Hata hivyo, Harmorapa amesema awamu hii ya tano Serikali imekuwa ikihimiza sana vijana kufanya kazi kuliko kuendekeza starehe kitu ambacho kimewafanya vijana wengi kujituma na kupata molali ya kufanya kazi.

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Chasikitishwa na Bunge Kutengeua Uteuzi wa Wabunge 8 CUF

$
0
0
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimelitaka Bunge la Tanzania kusitisha maamuzi yake dhidi ya Wabunge wa CUF.



Soma taarifa kamili:

DAVID Kafulila Apewa Tuzo....Sakata la Escrow Lamweka Kwenye Ramani Upya....

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusi David Kafuli amepewa Tuzo ya Heshima  Mpiga Filimbi katika vita vya Ufisadi.

Tuzo hiyo amepewa baada ya kuibua hoja zilifichua Ufisadi na Mafisadi waliokula pesa na kubadhilisha Maslahi ya Umma.

Ujasiri wa Kafulila kuibua masuala hayo ndio ulimuibua kwenye Tuzo hiyo aliyopewa na Watetezi wa Haki za Binaadamu VIDEO:

EXCLUSIVE: Ester Bulaya Afunguka Gharama Aliyoitumia Kwenye Kesi yake na Wasira

$
0
0
July 28 201 7 Mahakama ya Rufaa ilitupilia  rufani iliyofunguliwa na wapiga kura wa jimbo la Bunda mjini katika kesi ya uchaguzi wa kupinga matokeo yaliyompa ushindi mbunge wa jimbo hilo, Ester Bulaya.

Wapiga kura hao ambao wanampigania aliyekuwa Waziri wa Chakula, Kilimo na Ushirika na mgombea ubunge wa CCM Jimbo la Bunda Mjini, Stephen Wasira, wapo wanne ambao ni; Magambo Masato, Matwiga Matwiga, Janes Ezekiel na Ascetic Malagila.

Uamuzi huo umetolewa na  Naibu Msajili wa mahakama hiyo, Elizabeth Mkwizu ambapo amesema, upande wa walalamikaji uliwasilisha hoja 10 za kupinga ushindi wa Bulaya, lakini hoja hizo hazikuwa na mashiko, hivyo zinatupiliwa mbali.

Miongoni mwa hoja zao ni “Stephen Wassira, hakualikwa katika mchakato wa kujumlisha kura suala hili linaweza kuathiri matokeo ya uchaguzi kwa kushindwa kumtambua mgombea wala chama chake,” Sasa baada ya ushindi huo AyoTV na millardayo.com imempata Ester Bulaya anazungumzia ishu ya gharama alizotumia kipindi cha kesi yake na kingine ni mambo mawili ambayo hatayasahau kwenye kesi hiyo……..

“Ukishamuona wakili mwenyewe ni Tundu Lissu, wewe ukishamuona wakili mwenyewe ni ghali lakini gharama sio tu kwa wakili, kuna gharama ya kusafiri pia kuna watu wananizunguka na wanakuwa wananiunga mkono kwa wakati wote nakuwa nao kwa hiyo ni mkwanja mrefu nimetumia, ni zaidi ya milioni 100 kwa kipindi chote cha kesi”-Ester Bulaya 
VIDEO:

SIASA Zampoteza Mbowe Bila Kujua

$
0
0
Siasa, uroho na kutojua kumempoteza Mbowe bila kujitambua. Mashabiki wake wengi wanashindwa kulitambua hili.

Mambo yanayompoteza Mbowe ni haya:-

i) Kuzidiwa kisiasa na watu walioko ndani ya chama;
ii) Kashfa nyingi za kibiashara, ngono na ukanda wa chama chake;
iii) Kuuza chama kwa Mh. Lowassa;
iv) Kupungua kwa ushawishi kwa chama chake hasa baada ya kupingana na dhamira yake ya
kutetea taifa na kuanza kutetea wezi;
v) Kushindwa kusimamia matamko na mikakati ya chama chake;
vi) Kupingwa waziwazi na wanachama wake;
vii) Kupungua kwa mikutano ya kujinadi kwa chama chake.

Kutokana na mambo haya, Lissu na Lowassa wamebaki kuwa wakuu wa chama bila kujijua. Kunapotokea kila kitu, yeye amebaki mnyonge na ameshindwa kutetea falsafa ya chama ambayo ilisaidia kukua kwa chama mpaka 2015.
Ni wazi kuwa, kwa sasa tunatarajia kuona mtanange kati ya Lissu na Lowassa siku za hivi karibuni.

Tukae tukisubiri.

By Ufipa-Kinondoni/JF

MADAI ya Petit Man Kumfumania Mkewe Esma na Kidume Kingine Undani Huu Hapa.....

$
0
0
NDOA ya mastaa wawili, Esma Abdulkadiri na Hamad Manungwa ‘Petit Man’ inadaiwa kuwa kwenye machafuko baada ya juzikati kuvuja madai kuwa, Petit alimfumania mkewe na jamaa mwingine, Risasi lina undani na ukweli wa habari hiyo.

Chanzo ambacho kiliomba hifadhi ya jina lake awali kilidai kuwa, wawili hao waliibua varangati la aina yake na kusababisha kufunga mtaa maeneo ya Tandale jijini Dar wanakoishi kutokana na kile kilichodaiwa ni Petit kumfuma Esma na mwanaume mwingine.

“Yaani ilikuwa ni patashika nguo kuchanika kwani ilikuwa ni timbwili la aina yake baada ya Petit kudai amemfumania mkewe na mwanaume mwingine, hali iliyosababisha watu kibao kufurika pale wanapoishi Tandale,” kilidai chanzo hicho.

Baada ya kuinyaka ishu hiyo, Risasi Jumamosi lilianza kwa kumtafuta Esma ambaye kwanza aliangua kicheko kasha akasema kuwa anawashangaa watu wanaoeneza uvumi huo kwani kwenye maisha yake hajawahi kufumaniwa na haitatokea, isipokuwa ilitokea hali ya kutoelewana na watu kudhani alifumaniwa.

“Kugombana ni kawaida kwenye uhusiano lakini watu wanatakiwa kuuliza nini kimetokea siyo kuanza kuzusha maneno, ilikuwa ni kwenye bethidei ya B-12, sasa wakati tunakaribia kuondoka Petit Man alikuwa amelewa sana akawa anafanya fujo, sikupenda nikaamua kuondoka.

“Alipofi ka nyumbani ikatokea ugomvi mkubwa akinilaumu kwa nini niliondoka nikamuacha kule, sasa yale makelele kwa jinsi tulivyokuwa tunazozana nahisi majirani walisikia wakaelewa tofauti na kueneza uvumi huo kwamba nilifumaniwa, ila tumeshayamaliza tupo sawa,” alisema Esma.

Kwa upande wake Petit Man alipotafutwa na kuulizwa kuhusu madai hayo ya kumfumania mkewe na mwanaume mwingine alisema: “Ni kweli ulitokea mtafaruku baina yetu lakini tumeshayamaliza haya mambo kifamilia.”

 RISASI JUMAMOSI

OMMY Dimpoz Akana Kufundishwa Kuendesha Gari na DEMU

$
0
0
Msanii Ommy Dimpoz ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Cheche' amefunguka na kusema aligoma kabisa kujifunza au kufundishwa gari na demu wake mpaka siku alipokuja kununua gari yake ya kwanza ndipo alijifunza kupitia gari yake.

Ommy Dimpoz amesema hayo kupitia kipindi cha 'Bongo Flava Top 20' kinachorushwa na East Africa Radio na kudai kuwa demu wake alikuwa akimcheka sana kuona hajui gari na alikuwa akimpa sana gari yake ili ajifunze lakini yeye aligoma mpaka siku ambayo alinunua gari yake na kujifunza kupitia gari yake.

Mbali na hilo Ommy Dimpoz amefunguka kuwa mtu pekee aliyemsukuma kununua gari kwa mara ya kwanza alikuwa ni dereva bajaji ambaye alikuwa akimtumia sana kwenye safari za hapa na pale.

"Huwezi kuamini mimi nilikuwa sipendi sana kununua gari sababu nilikuwa naona maisha yangu yanakwenda maana zangu zilikuwa bajaji, sasa siku moja yule dereva bajaji aliniambia unajua wewe umekuja msanii mkubwa sana mambo ya kutumia bajaji uache sasa. Nikaona huyu mtu ambaye nampa ridhiki ananiambia maneno haya tena nikaona isiwe kesi kesho yake nikaingia mtaani na kutafuta gari, nakumbuka nilipata Rav 4 baada ya hapo ndiyo nikajifunza gari kupitia gari yangu mwenyewe" alisema Ommy Dimpoz

Aidha Ommy Dimpoz amewatoa wasiwasi mashabiki wake na kusema 'video' ya wimbo wake mpya 'Cheche' ipo tayari muda mrefu na kama mambo yatakwenda sawa basi ataachia wimbo huo wiki ijayo.

"Unajua video nilifanya kitambo toka mwezi wa Ramadhan lakini nilitaka kupima uzito wa 'Audio' nione je kweli watu wanapenda 'Video' kuliko 'Audio' so nilichigundua sasa ukiweka nguvu kubwa katika kufanya 'Audio' nzuri basi kazi itafanya vizuri tu kama ambavyo kazi yangu inafanya vyema saizi kwa sababu niliwekeza nguvu kwenye 'Audio' na ikitoka Video ndiyo kwanza itakuwa ngoma kama ni mpya" alisisitiza Ommy Dimpoz

RAIS Donald Trump Afuata Nyayo za JPM Tumbua Tumbua Viongozi Wazembe....!!

$
0
0
Rais Donald Trump wa Marekani amemteua Waziri wa Mambo ya Ndani, John Kelly kuwa mkuu wa utumishi wa Serikali baada ya kumwachisha kazi Reince Priebus.

Priebus amefanya kazi kwenye Serikali hiyo kwa muda wa miezi sita tu.

Baada ya miezi kadhaa ya uvumi kuhusu hatima ya Priebus, Trump ametangaza uamuzi wake kwenye mtandao wa Twitter akiwasili mjini Washington.

Awali, Trump alitoa hotuba jijini New York ambayo aliitumia kummwagia sifa Kelly kwa kazi anayofanya katika wizara hiyo.

Amesema ,"Nina furaha kuwafahamisha nimemteua waziri John Kelly kuwa mkuu wa utumishi wa Serikali katika Ikulu."

Hivi ndivyo DIAMOND alivyozima Povu la Wanaomsema Vibaya yeye na Mpenzi wake Zari

$
0
0
Diamond Platnumz ameamua kuwaumbua waliokuwa wakisema kwamba penzi lake za Zari limekufa.

Pia amewajibu wanaotaka mpenzi wake abaki akiwa mnyonge baada ya kupata matatizo ya kufiwa na mama yake mzazi wiki chache zilizopita.

“Kuna vichupi kunuka wanajifanya wanajua sana uchungu wa Misiba ya watu…. Mtoto wa watu katoka katika matatizo mfululizo, anatakiwa apelekwe sehem tulivu apetiwepetiwe adekezwe apate faraja!…sasa kama nyie hamna mabwana wa kuwafanyia hayo, Msijifanye ni Tamaduni na kulazimisha kila mtu awe kama nyie, eti kutwa nzima ajifungie chumbani kulia… Pambaneni na Mahusiano yenu…! Nina siku 5 za kumpetipeti… leo ndio kwanza Ya kwanza 😛.” ameandika Diamond Instagram.

Diamond amefikia hatua hiyo baada ya watu kumponda mpenzi wake Zari The Boss Lady, ambaye siku ya jana alikuwa Instalive na mkali huyo wa Eneka wakijiachi kimahaba, hali iliyofanya mitandao ya kijamii kumponda kuwa anaonyesha hana uchungu wa kufiwa na mzazi wake, kazi yake ni kujiendekeza na mapenzi

ZITTO Kabwe Awapa Somo Wanaopinga MITAA Kupewa Majina ya Wachezaji

$
0
0
ZITTO Kabwe Awapa Somo Wanaopinga MITAA Kupewa Majina ya Wachezaji
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amewataka wanao lalamika juu ya baadhi ya mitaa ya Kigoma kupewa majina ya wachezaji wa kikosi cha Taifa Stars kilicho shiriki AFCON mwaka 1980  waache ubinafsi.


Wachezaji wa Stars  mwaka 1980 wapatiwa majina ya Mitaa

Zitto ameyasema hayo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Facebook

Nimesikia malalamiko ya baadhi ya watu kuhusu kuipa baadhi ya Mitaa yetu majina ya wachezaji wa Taifa Stars ya mwaka 1980 iliyoshiriki AFCON Lagos.

Lalamiko kubwa ni kwamba kwanini tutoe majina ya watu ambao sio wa Kigoma kwenye Mitaa ya Kigoma Ujiji. Nataka kuwaambia watu hao kuwa kuna watu wa Kigoma wana majina kwenye miji mingine.

Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha ni heshima ya Sheikh Amri Abeid Karuta wa Ujiji. Unapokataa Peter Tino asipewe jina Kigoma unasema na Arusha nao wafute jina la Uwanja. Hoja Hii ni nyepesi na iliyojaa ubinafsi na upofu wa kuona mambo.

Taifa Stars ya Mwaka 1980 itakuwa na mitaa 25 tu. Pia haina maana kuwa watu wengine waliocheza mpira hawatapewa majina. Huwezi kuwa na mitaa Kigoma bila Edibily Jonas Lunyamila ama Nteze John Lungu.

Unawezaje kumwacha Juma Kaseja ambaye amekuwa Nahodha wa Taifa Stars miaka 10? Unamwacha vipi Mavumbi Omar, Kitwana na Kasim Manara? NK. Ieleweke tu kwamba hawa wa Taifa Stars ya mwaka 1980 watakuwa eneo Moja wakati wengine watakuwa sehemu tofauti.

Mfano Kata ya Bangwe wamependekeza jina la Shem Karenga kwenye moja ya mitaa ya Kata hiyo. Watu wengi watapewa mitaa. Viongozi wetu wa Dini waliopita kama Almarhum Sheikh Tofiki Ibrahim Malilo, Sheikh Khalfan Kiumbe, Sheikh Idi Kiburwa, Askofu Kahurananga, Askofu Gerald Mpango nk. Wabunge wote wa zamani wa Wilaya ya Kigoma na Kigoma Mjini.

Wakuu wa Mikoa wa Zamani waliohudumu Kigoma na Mameya wa zamani. Wazee wetu Viongozi wa Kisiasa Kama Mzee Lukandamila, Mzee Nayingo, Mzee Kasisiko, Mzee Menge. Pia Viongozi wa Kitaifa na Kimataifa Kama vile Prof. A M Babu, Che, Josina Machel, Titi Mohammed, Mwami Ntare, Kassim Majaliwa nk. Wafanyabiashara maarufu wa Kigoma na watu wengine waliochangia Kwa njia mbalimbali maendeleo ya Kigoma.

Kuna watu wana mchango maalumu Kwa kigoma na sio watu wa Kigoma lazima kuwaenzi, mtu Kama Sam Ruhuza unawezaje kuacha kumuenzi japo Kwa Mtaa? Mzee Bella Karumba? Shein ? Jaffer?

Hili ni zoezi kubwa na sio la Taifa Stars tu.

Ni zoezi la kutambua mitaa Kwa majina na vibao vya mitaa. Tunaishukuru kampuni ya MihanGas Kwa kukubali ombi letu la kudhamini vibao vya Mitaa Manispaa nzima. Majina ya Mitaa yanaendana na usafishaji wa mitaa pia ili kuwa na mji msafi na endelevu. Kidogo tutafika, hata Mbuyu ulianza Kama Mchicha, alimalizia Zitto Kabwe.

By Hamza Fumo

RC Makonda Akabidhiwa Ripoti ya Wezi na Magari na Vifaa Dar, 73 mbaroni

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amekabidhiwa ripoti ya wezi wa magari pamoja na vifaa vya magari na Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam Lucas Mondya ikiwa ni miezi kadhaa toka mkuu huyo aliagize jeshi hilo baada ya matukio ya namna hiyo kushamiri ndani ya mkoa huo.

Akiongea na waandishi wa habari Jumamosi hii wakiwa ndani ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es salaam Lucas Mondya alisema katika opesheni hiyo kali jumla ya wahumiwa 73 wamekamatwa na kupekuliwa na kukutwa na vifaa mbalimbali vya magari ikiwemo side mirrors, taa za magari, power windows, radio, injector pump, starter na seat cover.

“Tarehe 19 mwezi wa saba mweshimiwa RC Makonda ulitoa maagizo kwa jeshi la polisi kwamba unatupatia siku saba kuhakikisha tunasambaratisha mtandao wa wezi wa vifaa vya magari pamoja na magari baada na sisi tumelitekeleza hilo tayari kuna watu 73 tunawashikilia, Kinondani wamekamatwa watuhumiwa 29, Ilala wamekamatwa wahutumiwa 33 na mkoa wa kipolisi Temeke wamekamatwa wahumiwa 11,”

Alisema jumla ya power windows zilizokamatwa ni 40, Raidio 12, Taa za magari aina mbalimbali 105, side mirrors 92, vitasa vya magari 109, wiper switch 7, Tampa 4, left pump3, Air cleaner 1, Booster 3, show grill 6, machine za kupandisha vino 1 na tyre used 2.

Pia alisema katika mahojiano na wahutumiwa wote waliokamatwa wapo walioshindwa kuvitolea maelezo vifaa hivyo ni namna gani na wapi wamevipata.

Wahutumiwa wote bado wanaendelea na mahojiano na uchunguzi bado unaendelea ili kubaini mtandao wote unaojihusisha na wizi huo wa vifaa vya magari ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahamani kwa hatua zaidi.

Kwa upande wa RC Makonda alisema yeye anataka kuhakikisha jiji la Dar es salaam linakuwa salama ili kutimiza gamma ya Rais John Magufuli katika kutatua changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili wananchi wake.

KOREA Kaskazini NOMA Waunda Kombora la Kutungua Marakeni Moja Kwa Moja

$
0
0
Korea Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kufanya jaribio la kombora lake la  pili la masafa marefu ICBM, huku ikitoa onyo kali kwa Marekani kuwa inauwezo wa kushambulia eneo lolote lililopo nchini humo.

Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un amesema kuwa jaribio hilo limebaini kuwa Marekani yote ipo katika rada ya Korea Kakazini na sasa inaweza kushambuliwa wakati wowote kwa makombora hayo.

Aidha, Rais wa Marekani, Donald Trump amesema kuwa jaribio hilo ni la kijinga na ni kitendo cha kichokozi na cha hatari kilichotekelezwa na utawala wa Korea Kaskazini, ambapo ameongeza kuwa hali kama hiyo isipodhibitiwa inaweza kusababisha athari kubwa kwa jamii.

Kombora hilo lilionekana kuwa na nguvu zaidi kuliko lile la kwanza.

Kombora hilo lililoanguka karibu na ufuo wa Japan limeshutumiwa kimataifa huku Rais Donat Trump akisema jaribio hilo lilifanywa kiholela na ni hatari.

Kombora hilo lilionekana kuwa na nguvu zaidi kuliko lile lililojaribiwa mapema mwezi huu kwa kuwa lilikuwa angani kwa zaidi ya dakika 47, kulingana na taarifa zilizotolewa na Pyongyang na ambapo lilienda kwa mwendo wa kilomita 1,000. Lilidondoka karibu na Ufuo wa Japan.

Vikosi vya kijeshi vya Marekani na Korea Kusini vilivanya zoezi la kijeshi kwa pamoja ambapo makombora kadhaa yalilipuliwa na wizara ya ulinzi kutangaza kuwa silaha maalumu zitawekwa nchini humo.

Muda mfupi baada ya jaribio hilo, Korea Kusini, Japan na Maafisa wa Marekani waliripoti data kuhusu eneo na umbali, pamoja na muda uliochukuliwa na kombora hilo.

==>Ijapokuwa tathmini kamili haijakamilishwa, vitu kadhaa vilibainika.
Kwanza, data iliyopo inaonyesha kuwa kombora hilo lina uwezo wa kuruka umbali wa kilomita 10,400.

Kombora hilo linaweza kurushwa na kufika mji wa New York.

Pili Marekani iliripoti kwamba Korea Kaskazini ilirusha kombora hilo kutoka Mupyong -ni Korea Kaskazini.

Eneo hilo lilikuwa tofauti ikilinganishwa na taarifa za awali ambazo zilifanikisha jaribio yaliotabiri kurushwa kwa kombora la Kusong.

Hata hivyo, China imeshutumu jaribio hilo huku ikitaka pande zote zinazoshutumiana kuvumiliana na kutoendelea na majaribio hayo kwani yanaweza kusababisha madhara makubwa na kuhatarisha usalama wa eneo husika.

SALAMU za Rais wa TFF, Jamal Malinzi Kutoka Gerezani Hizi Hapa

$
0
0
Rais wa TFF anayemaliza muda wake Jamal Malinzi amewatumia salamu viongozi wa TFF na kuwatakia uchaguzi mwema unaotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu.

Aidha, Malinzi katika salamu hizo, ameishukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli, wadhamini mbalimbali, washirika na wadau wa soka kwa ushirikiano walioutoa katika kipindi chote cha uongozi wake.

Salamu hizo ambazo zimetolewa kupitiwa kwa mawakili wake zilieleza kuwa anaamini kwamba TFF watafanya uchaguzi vizuri na viongozi watakaopatikana wataweza kuendeleza programu muhimu.
Malinzi alilazimika kujiondoa kwenye uongozi wa TFF na kushindwa kutetea nafasi yake baada ya kuwekwa rumande tangu Juni 29 kwa tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.

Malinzi, Katibu wake, Selestine Mwesigwa pamoja na Mhasibu wa TFF, Nsiande Isawafo Mwanga walipelekwa rumande Juni 29 baada ya kusomewa mashitaka 28 ya kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF iliyopo katika banki ya Stanbic, Dar es Salaam.
Viewing all 104702 articles
Browse latest View live




Latest Images