Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Harmonize Amkingia Kifua ZARI HASSAN Swala la Kujirusha Baada ya Msiba wa Mama yake.....

$
0
0
Baada ya watu kuhoji vipi Baby Mama wa Diamond Platnumz, Zari The Boss Lady anajiachia ile mbaya akila bata wakati ni siku kadhaa tu zimepita tangu afiwe na Mama yake mzazi, Harmonize ameamua kumteta Zari.

Harmonize ambaye naye walikuwepo katika bata hilo Mombasa nchini Kenya, amesema mtu akipata matatizo halafu akapelekwa sehemu nzuri kwa ajili ya kufurahi ni kitu cha kumshukuru Mwenyenzi Mungu.

“Kwa sababu haikuwa rahisi, unajua kufiwa na mazazi sio kitu kidogo. Tumefika (Mombasa) tumemkuta yupo fresh, yaani kasharidhika na matokeo kwa sababu anajua hakuna binadamu atakuja kuishi milele,” ameiambia XXL ya Clouds Fm na kuongeza.

“Kwanza ukiona mtu anazungumza hiyo ujue haijui dini, kwa sababu dini imeandika kila mtu atakufa, kifo ni kitu cha lazima, ukiwa unaijua dini huwezi kuhofia suala la kifo. Mtu kafariki ni lazima uumie ila ni lazima maisha mengine yaendelee kwa sababu hata ukae ndani miaka sita hawezi kurudi,” amesema Harmonize.

PENDEZA na Kessy Products, Kutoa Mvi, Kurefusha Nywele, Tengeneza Shepu na Mengine

$
0
0

PENDEZA NA KESSY PTODUCT:-MSIMU MPYA WA 2017_ BIDHA AINA ZOTE KWA UBORA MZURI%
PATA DAWA ZA ASILI ZISIZO NA MAD, HARA NA MATOKEO NI KWAHARAKA BAADA YA WEEK

1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA _80,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO FIGA UMBO (8) NA KUJAZA HIPC NA KALIO @ KUPAK _80,000/
@ KUNYWA AU VIDONGE _130,000/ 4) KUPUNGUZA NYAMA ZA MIKONO TUMBONI ZILIZOTEPWETA _80,000/
5) PUNGUZA KITAMBI KWA HARAKA KWA DAW HIZI ZA KUNYWA
@) KUNYWAA _100,000/
@) VIDONGE _100,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KGM 150 ADI 80 KIASI UNACHOTAK WEWE KWA DAW HIZI
@) DAW YAKUNYWA YA _100,000/
@) VIDONGE VYA HARAKA _100,000/
7) PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KWA MUDA WA WEEK MOJA _70,000/
8) ONGEZA MAZIWA NA SAIZ UNAYOTAKA WEWE _70,000/
9) ONGEZA MWILI MZIMA NA KUKUPA HAMU YAKULA KWA RIKA LOLOYE _80,000/
10) TOA MICHIRIZI SUGU PIA NA ILE YAKUJIFUNGUA MWILI MZIMA _70,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KATIKATI YA MAPAJA _70,000/
13) KUWA MWEUP NA SOFTI MWILI MZIMA NA KUTOA WEUS MACHON NA VIMISHIPA VIDOGO VIDOGO @ MAFUTA YA KUPAKA _80,000/(@) VIDONGE (WHITE SOLUTION) _120,000/
14) ONDOA NDEVU NA VINYWELEO MWILINI _80,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME NA KUIMARISHA MISHIPA ILIYO LEGEA KWA DAW HIZ
@) JEL KUPAKA (MEN GEL) _70,000/
@) VIDONGE (MAXMAN) _80,000/
16) ONGEZA MAUMBIL YA KIUME SAIZI UNAYOITAKA WEWE KWA:
@) (HANDSOME UP) MASHINE _170,000/
@) JELI YAKUPAKA INABORESHA ANZIA NCHI (4 ADI 6 )_100,000/ PIA NA VIDNGE VYAKE VIPO
17) RUDISHA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WALIOPOTEZA KUTOKANA NA NGIRI, KISUKARI NA MAGONJWA MENGINE KWA _80,000/
18) RUDISHA USICHAN(BIKRA)Na KUTO UCHAFU SEHEMU ZA SIRI _80,000/
19) FANYA USO WAKO KUWA MKAVU NAKUTOA VIJIPELE ILIYOSABABISHWA NA MAFUTS MAKALI _80,000/
20) ONDOA MAKUNYANZI USONI _70,000 (21) ENGEZA MGUU WAKO _70,000/ TUNAPATIKAN K/ KOO NA SINZ
MAPAMBAN, KWA MIKOAN DUNIAN KOTE UTAPATA

(+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product
Delivery POPOTE ULIPO,

AGNESS Masogange yamkuta ya Wema

$
0
0
Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia mkuu wa Serikali amesema mkojo wa mrembo Agness Gerald 'Masogange' umekutwa na chembechembe za dawa za kulevya aina ya heroine na oxazepam (Diacety Imophine).

Mkemia Elias Mulima (40) ameiambia mahakama mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kwamba sampuli ya mkojo wa Agness zilizowasilishwa kwao zilikua na chembechembe za dawa za kulevya.

Mulima ambaye ni shahidi wa kwanza katika kesi ya Masogange kukutwa na dawa za kulevya Februari 15, 2017 Dar es salaam akiongozwa na Wakili wa Serikali Constantine Kakula, Shahidi huyo amedai kuwa Februari 15 mwaka huu katika ofisi ya Mkemia mkuu Dar es salaam akiwa ofisini alipokea vielelezo kutoka Jeshi la Polisi vilivyowasilishwa na koplo Sospeter na WP Judith kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ili kubaini kuwa ni dawa za kulevya au la.

Pia shahidi huyo ameongeza kwa kudai kuwa iliwasilishwa na fomu maalumu ya dawa za kulevya ambayo ilikua na namba DCEA 008 na alifanya usajili na kuipa namba ya maabara 446/2017 ambapo Mshtakiwa alipewa kontena maalumu kwa ajili ya sampuli ya mkojo.

Pamoja na hayo Wakili wa utetezi Nehemiah Nkoko alipinga kupokelewa kwa kielelezo hicho kwa sababu Polisi walitakiwa kuiomba Mahakama ili wachukue vipimo vya Mshitakiwa lakini hawakufanya hivyo na kudai ni kinyume na sheria 63 CPA.

Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 28/2017  ambapo siku hiyo inatarajiwa kutoa uamuzi wa kupokea ama kutopokea vielelezo vya sampuli ya mkojo wa Agnes Masogange kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

MSAMI Afunguka Jinsi Alivyotongozwa na IRENE Uwoya

$
0
0
Staa wa Bongo Fleva, Msami Baby, anayetamba na kibao chake kipya cha So Fine, alichomshirikisha rapa machachari, Chemical amefungukia taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa, Irene Uwoya, alimtongoza.

Msami ambaye amevunja amri ya 6 na staa huyo wa Bongo Muvi kwa takribani miaka miwili, amefunguka kama ifuatavyo:

“Ni kweli tulikuwa wapenzi kwa muda wa miaka miwili, ila swali la nani alianza kumtongoza mwenzake hilo halina umuhimu hivyo siwezi kuliongelea.
“Kwa mara ya kwanza tulikutana lokesheni kwa ajili ya kushuti muvi yake ambayo ilinihitaji kutokana na uwezo wangu wa kucheza, hapo ndipo mahusiano yetu yalipoanzia, na mpaka sasa hakuna aliyewahi kumtamkia mwenziye kwamba amemuacha, tuliachana hewanihewani tu.”

NA ISRI MOHAMED/GPL

MASKINI...Mwanamke Aolewa Saa 10 Jioni, Afariki Saa 7 Usiku na Kichanga Tumboni.....

$
0
0
DAR ES SALAAM: Hii inauma sana! Wakati wengi wakitamani kuingia kwenye ndoa ili kuyafurahia maisha hayo, kwa binti Zai Mkiwa, mkazi wa Mtoni Kijichi jijini hapa, imekuwa tofauti kwani amejikuta akiyaonja maisha ya ndoa kwa saa chache na kisha kufariki, Amani linakudadavulia habari hii ya kusikitisha.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini kilichohudhuria msiba wa binti huyo, Zai ambaye alidaiwa kuwa na ujauzito mchanga, alionekana ni mwenye siha njema hadi siku ya harusi, Jumapili iliyopita (Julai 30, mwaka huu) kabla ya kukutwa na umauti usiku wa saa 7 siku hiyo.
“Yaani marehemu alikuwa na afya njema kabisa, na siku ya harusi yake hakuonesha hata dalili zozote za kuumwa japo kuna wakati alisema anahisi kama kuishiwa nguvu.

FULL KUTABASAMU
“Muda mwingi alikuwa akitabasamu, alifurahia ndoa yake kwelikweli kama unavyojua watoto wa kike wanavyofurahia siku hiyo muhimu katika maisha yao,” kilisema chanzo hicho.

NDOA ILIFUNGWA SINZA MAPAMBANO
Kikizidi kufunguka chanzo hicho kilieleza kuwa, siku ya tukio, mumewe aliyefahamika kwa jina moja la Yasin, alifika nyumbani kwa babu wa marehemu, Mzee Msafiri anayeishi Sinza Mapambano jijini hapa na kukamilisha taratibu zote za ndoa na baada ya zoezi hilo kukamilika, Zai aliambatana na mumewe kwenda nyumbani kwao, Mtoni Kijichi.


…Hali ilivyokuwa siku ya harusi yake.

“Huwezi amini kumbe ni kama alikuwa anatuaga vile, maana tumesherehekea pale kwa nderemo na vifijo, wakaondoka zao na mumewe lakini ilipofika saa 7 usiku, tunaambiwa amefariki dunia,” kilisema chanzo hicho.
ALIANZA KUTAPIKA
Chanzo hicho kilieleza kuwa, ndugu wa karibu na marehemu walipopewa taarifa za msiba huo, walielezwa kuwa Zai alipofika nyumbani kwa mumewe, saa chache kabla ya kukata roho, alianza kutapika na mumewe akamkimbiza Hospitali ya Mbagala Zakhem lakini bahati mbaya, alifariki.
“Walifika salama salmini, wakahifadhi zawadi mbalimbali walizokuwa wamepewa na kisha kulala. Ilipofika saa saba usiku nasikia ndiyo akaanza kutapika na mumewe alipoona hali inazidi kuwa mbaya akalazimika kumkimbiza hospitalini, lakini alipofikishwa tu akafariki akiwa mikononi mwa madaktari,” kilisema chanzo hicho.

MSIBA WAWEKWA ALIPOOLEWA
Chanzo hicho kiliendelea kuweka bayana kuwa, asubuhi ya Jumatatu, Julai 31, mwaka huu, ndugu walikusanyika nyumbani kwa babu wa marehemu, Sinza-Mapambano ambapo taratibu zote za msiba ikiwemo mazishi zilifanyika pale.
“Palepale tuliposherekea harusi ndipo tulipokusanyika tena kwa ajili ya msiba. Yaani lile turubai lililotumika katika sherehe ya harusi yake ndilo hilohilo lililotumika wakati wa msiba wake, inauma sana! Tukaomboleza pale na baadaye mida kama ya saa 10 jioni, mwili wa Zai ulienda kuzikwa katika Makaburi ya Sinza,” chanzo kilizidi kueleza.



NI NDANI YA MASAA 24 TU!
Ukweli ni kwamba, mambo yote hayo yametokea harakaharaka mno, ni ndani ya saa 24 tu! Kila kitu kwenye maisha ya binti huyo kikabaki kuwa historia ya majonzi na masikitiko kwa ndugu na jamaa waliobaki duniani.

MUMEWE ABAKI NA MACHUNGU
Kwa mujibu wa chanzo hicho kilisema kikiwa makaburini hapo, mume wa marehemu alionekana kama mtu aliyepigwa na bumbuwazi, haamini kwa kilichotokea, hajielewielewi kwani hata kuzungumzia undani wa mazingira ya kifo cha mkewe hakuweza.

KABLA YA NDOA ALIUMWA
Inasemekana, siku chache kabla Zai hajaolewa, aliishiwa nguvu na kukimbizwa hospitali lakini alitibiwa na kurejea nyumbani na hata ilipofika siku ya harusi, alikuwa mzima wa afya.

BABA AZUNGUMZA
Gazeti la Amani lilifanikiwa kuzungumza na baba wa marehemu, Ketel Madua ambaye alisema amepokea kwa masikitiko makubwa kwa kuondokewa na binti yake huyo, saa chache baada ya kumuoezesha. Gazeti hili linatoa pole kwa ndugu na jamaa kwa msiba wa Zai.
STORI: ALLY KATALAMBULA NA BONIFACE NGUMIJE, AMANI

PAMBANA na Hali yako...."Not a Big Deal Kuwa na Kiserengeti"- Shilole

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya asiyeisha vituko Shilole amemtetea mwanaume wake mpya baada ya tuhuma za kutoka na serengeti boys.

Msanii Shilole.
Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Shilole amesema kwa sasa yeye hana mahusiano na wanaume ambao amewazidi umri, kwani mpenzi wake wa sasa ni mwanaume halisi (gentle man) na amemfanya awe na mawazo ya kuwa mke.

"Mwanaume wangu wa sasa sio serengeti boys, ni gentle man, anajielewa na pia ni mtu mzima, ananifanya mpaka nifikirie kuolewa niwe mke, yaani sio serengeti boy kabisa, na pia hataki kabisa mambo ya mitandao na ndio maana simuweki wazi", alisema Shilole.

Hata hivyo Shilole ambaye leo ameachia wimbo wake mpya unaoitwa 'Kigori', amewatetea watu ambao wana mahusiano na wanaume wanaowazidi umri (serengeti boys) na kusema siyo kitu cha ajabu kwani umri ni namba tu, kinachomata ni mapenzi.

"Kwani kitu gani...!! age is just a number, watu wanaangalia mapenzi bwana so its not a big deal kuwa na kiserengeti", alisema Shilole.

Hapo nyuma Shilole alishawahi kukumbwa na sakata la kuwa na mahusiano na wanaume wenye umri mdogo (serengeti boys) akiwemo aliyekuwa mpenzi wake Nuhu Mziwanda.

MAALIM Seif Jiondoe CUF Ukajiandae Kugombea Rrais na Chama Kipya

$
0
0
Nidhahili sasa kuwa Seif huwezi kutoboa huu mwamba wa Cuf ninacho mushauri yeye na wabunge wote wanao muunga mkono wajiondoe Cuf wajiunge na chama chochote cha siasa ili wajiandae na uchaguzi wa 2020

Kuna hatari ya maalim Seif kujiunga na chama kipya wakati uchaguzi umekaribia hiyo itamunyima nafasi ya kupata ushindi.Nina uhakika wakijiondoa wote wakajiunga na chama chenye nguvu viti vyote vya ubunge watashinda.

Ruzuku Cuf inategemea wabunge wakuchaguliwa.kama Cuf itapoteza wabunge wakuchaguliwa wote bila shaka itakosa luzuku ya serikali na kiburi cha prf lipumba kitaishia hapo

By Stujadiliane

UKWELI Mchungu: Shujaa Wa Tanzania Hachaguliwi Kwenye Makongamano Yanayofanyika Nje Ya Nchi

$
0
0


By Fred Mpendazoe

Shujaa wa Tanzania Hachaguliwi kwenye Makongamano yanayofanyika nje ya nchi yetu. Hao ni Mashujaa Wao.

Katika mitandao ya kijamii na baadhi ya magazeti yameandika kuhusu baadhi ya wanachama wa chama kimoja cha siasa hapa nchini kukamatwa na polisi na kuwekwa mahabusi na baadae kuhojiwa na kupelekwa mahakamani. Wanachama hawa wamekamatwa kwa tuhuma mbalimbal zikiwemo kufanya uchochezi au kukaidi maelekezo waliyopewa na vyombo vya usalama. Wengine wamekamatwa kwa kutumia lugha chafu kwa viongozi hasa wa chama kinachotawala ambao wamepata ridhaa ya watanzania wengi kuongoza nchi. Kama makongamano yanayofanyika nje ya Nchi yetu wanawaona watu hawa ni mashujaa, ni mashujaa wao siyo mashujaa wa Nchi yetu.

Serikali ya JPM ndiyo iliyochaguliwa na watanzania wengi na iko kikatiba, hivyo ni halali. Hivyo serikali ya JPM siyo ya dikteta.Kumekuwepo madai kwamba JPM anawanyanyasa watanzania na hashauriki. Siyo kweli, JPM analo baraza la mawaziri linalomshauri na anacho chama chake kinachomshauri. Pia anao watalaam wanaomshauri katika masuala mbalimabali.Hivyo hola hizi hazina mashiko.
Kwa muda mfupi, serikaliya JPM imeonyesha mwelekeo wenye kuleta matumaini kwa mwatanzania.


  • JPM ameonyesha dhamira ya kweli ya kupiga vita ufisadi ukilinganisha na baadhi ya vyama vinavyompigia kelele kwamba ni dikteta.
  • JPM anapiga vita rushwa, uzembe kwenye serikali, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.
  • JPM anachukua hatua kuhakikisha rasilimali za nchi zinawanufaisha watanzania wengi
  • JPM anasimamia kwa karibu watendaji na kufuatilia kwa karibu kero za wanachi, hakuna ombwe la uongozi.
  • JPM ameweza kuchukua maamuzi magumu, mfano elimu bure; mchanga wa madini usipelekwe nje ya nchi.
  • Hatua alizochukua JPM dhidi ya wizi bandarini na sehemu nyingine zinaonyesha uzalendo wake.
  • JPM anatekeleza vizuri ilani ya uchaguzi ya chama chake kilichopewa ridhaa kuongonza na watanzania.


Kwa hatua hizo alizochukua JPM ni mtanzania yupi mzalendo ambaye amenyanyaswa au kuonewa kwa hatua hizo ? Au kwa hatua hizi mtanzania yupi anagandamizwa ?

Kwa ujumla, JPM ameleta heshima kwa nchi yetu hadi nchi za nje zinaanza kuchukua hatua ambazo JPM amezichukua hapa Tanzania.

Mtanzania yoyote anayenung’unika kwa hatua hizi zilizochukuliwa na serikali ya JPM ni dhahiri uzalendo wake una walakini na nidhahiri pia anapigania maslahi yake binafsi au ya kukudi cha watu fulani wachache wala si maslahi mapana ya nchi yetu.

Lakini pamoja na hayo yote baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani tena wenye elimu nzuri wana mkejeli na kumwita JPM eti dikteta uchwara, KWELI INASIKITISHA.

Lakini, ni kwa lipi hasa wamwite dikteta uchwara?
Wapo wanachama wa chama kimoja wanawasifu hawa viongozi waliokamatwa na kuachiwa kwa dhamana eti ni mashujaa.

Je ni kipi cha maana na heshima kwa nchi yetu wanachokipigania hadi waitwe mashujaa?

Ushujaa wao ukowapi? Je kukamatwa na kuwe kwa rumande kwa kuitukana serikali ni ushujaa ?

Je kuwekwa rumande na baadae kupata dhamana kwa kuandamana bila kibali cha polisi ni ushujaa ?

Je kukamatwa na vyombo vya dola kwa kukaidi maelekezo ya vyombo hivyo ni ushujaa?Hapana. Kama kwenye mikutano au makongamano yanayofanyika nje ya Nchi wanawaita mashujaa ni mashujaa wao siyo mashujaa wetu.

Wanachokifanya wanachama hawa ni upotoshaji wenye lengo la kuvuruga amani ya Nchi yetu. Watanzania tukatae upotoshaji huu na tuwapuuze. Nawasihi watanzania tuiunge mkono serikaliya JPM.

Juzi kwenye mkutano mkuu wa Chama cha Demokrati huko Marekani Mama Obama amewatahadharisha na kuwataka wamarekani kuwapuuza viongozi wanaotukana ovyo hadharani kwani wanajenga fikra mbaya kwa vijana wa Marekani. Mama Obama alikuwa anamzungumzia mgombea wa chama cha republican ambaye nimsema ovyo, ambaye ana lugha ya matusi kwa viongozi na amekuwa akimtukana rais Obama kwenye mikutano.

Mama Obama ameuliza, Je vijana wa Marekani wanajifunza nini kwa viongozi hawa wanaotumia lugha chafu hadharani? Ni dhahiri maadili ya vijana wa Marekani yatakuwa hatarini. Kwa mtazamo huo wa Mama Obama, vijana wetu hapa Tanzania wanajifunza nini wanaposikia lugha za matusi kutoka kwa viongozi wa vyama vya siasa ?.

Vita ni siasa inayomwaga damu kwani haina majadiliano wala ushawishi. Ni ugomvi.Vyama vya siasa viepukane na ugomvi. Vijenge hoja na viwashiwishi watanzania kuhusu sera zake.

Je ikitokea kijana akamwambia baba yake kwamba ni baba uchwara atajisikiaje?Au akakuambia wewe mama ni mama uchwara. Je utafurahi jirani yako akimpongeza huyo kijana na kumwita shujaa ?

Je haiwezekani kudai haki na demokrasia na kutoa maoni na kuikosoa serkali bila kutumia matusi na kejeli kwa serikali iliyoko madarakani?.Upinzani ujifunze kwamba, siasa za kiuanaharakati kwa Tanzania hazikubaliki. Tanzania iliisha pata Uhuru wake.

Tukumbuke Nyerere alidai uhuru kwa kutumia hoja za msingi hadi wakoloni wakatoa uhuru. Siasa ni vita isiyo mwaga damu. Ni majadiliano na ushawishi. Hata sasa inawezekana kudai haki, kutoa maoni na kuikosoa serikali bila kutumia lugha ya matusi.

Mtu yeyote asiyetaka kuongozwa hawezi kupata fursa ya kuogoza.

By Fred Mpendazoe

Toa Maoni Yako

RAIS Magufuli Sio wa Mchezo..Aamuru Mgambo Kurudisha Eneo la EKARI 50

$
0
0
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli ameamuru eneo la ekari 50 lililopo Mkata mkoani Tanga ambalo walipewa Mgambo JKT miaka saba iliyopita kwa ajili ya kujenga kiwanda na wakashindwa kuliendeleza, walirudishe haraka kwa serikali ya kijiji ili lipangiwe matumizi mengine.

Hayo ameyasema leo wakati akiwa njiani kuelekea Tanga kwa ajili ya kumpokea mgeni wake, Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda ambapo kesho wataweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Kaskazini mwa Tanga.

Rais Magufuli amekuwa akisisitiza kuwa wawekezaji au taasisi itakayopewa eneo kwa ajili ya kujenga kiwanda lazima ifanye hivyo, kushikilia eneo bila kuliendeleza kutasababisha mhusika anyang’anywe eneo hilo na apewe mwingine mwenye uwezo wa kuliendeleza.

Aidha rais ametoa onyo kwa viongozi waliohusika kuhujumu kwa kujinufaisha na fedha kiasi cha Tsh milioni 500 za ujenzi wa Hospitali ya Mkata kuwa wajiandae kuzirudisha ama kwenda gerezani.

KUFURU..Mmiliki wa Ngurdoto Kuzikwa nje ya Hoteli yake

$
0
0
Mfanyabiashara maarufu ambaye pia ni mmiliki wa hoteli za kitalii nchini,Maleu Mrema anatarajiwa kuzikwa katika eneo la hoteli Yake ya kitalii ya Ngurdoto iliyoko nje kidogo ya jiji la Arusha Agosti 9 .

Mrema amefariki hivi karibuni akiwa kwenye matibabu nchini Afrika Kusini katika hospitali ya City garden iliyoko katika mji wa Johannesburg .

Akizungumza na waandishi wa habari  msemaji wa familia Vincent Laswai amesema kwamba baada ya vikao mfululizo vya familia wameafikiana marehemu azikwe katika eneo la hoteli yake ya Ngurdoto

Awali taarifa zilienea kwamba mwili wa marehemu utasafirishwa kwenda wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro ambako alikozaliwa lakini taarifa hizo zimekanushwa na msemaji hiyo wa familia.

Laswai amesema kwamba mwili wa marehemu unatarajia kuwasili Agosti 7 mwaka huu kutoka nchini Afrika Kusini ambapo utapokelewa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Amesema kwamba baadhi ya wanafamilia,ndugu ,Jamaa Na marafiki watakwenda kuupokea mwili huo katika uwanja wa ndege ambapo familia imetoa usafiri maalum kwa wale watakaoshiriki.

Naibu Waziri wa mawasiliano nchini na Mbunge mstaafu wa jimbo la Arumeru Mashariki,Goodluck Ole Medeye alifika nyumbani kwa marehemu kutoa salamu za pole.

 Medeye amesema  marehemu  alikuwa ni mbunifu ambaye alitumia uwezo wake kusaidia ajira za vijana mbalimbali nchini.


JE Wajua Kinachosababisha Watoto Kuzaliwa Wameungana Hiki Hapa

$
0
0

Kutotibu ugonjwa wa malaria wakati wa ujauzito, matumizi ya vyakula na vinywaji visivyo salama hasa vyenye gesi na tindikali, ni chanzo cha kuzaa watoto wenye maumbile tofauti ikiwamo pacha walioungana.

Vitu hivyo vimetajwa kuwa sababu ambazo huvuruga mfumo wa utengenezwaji wa viungo kipindi ambacho mtoto huanza kukua tumboni.

Hayo yalielezwa jana na daktari bingwa wa upasuaji wa watoto kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Zaituni Bokhari alipokuwa akitoa majibu ya vipimo vya pacha wa kike waliozaliwa hivi karibuni mkoani Morogoro wakiwa wameungana.

Watoto hao walizaliwa katika Hospitali ya Misheni ya Berega, Julai 21.

Dk Bokhari alisema hakuna sababu maalumu mpaka sasa, lakini kuna vitu ambavyo husababisha kujifungua mtoto ambaye si wa kawaida.

“Mama akiwa mjamzito anatakiwa kuhudhuria kliniki mapema kwani kuna maelekezo kuhusu anapaswa ale nini ambacho kitamjenga mtoto, kama vyakula vyenye calcium, protini, atapewa dawa ambazo zitakaza misuli ya mtoto, folic acid zinasaidia kumjenga mtoto akiwa bado tumboni,” alisema na kuongeza kuwa kuna dawa ambazo huzuia maambukizi ya watoto wakiwa tumboni kwani wapo wanaozaliwa wakiwa na malaria.

“Pia, kujifungua katika umri mkubwa, kula vyakula visivyo salama, vinywaji visivyo salama vyenye gesi na tindikali, vyote vinaweza kusababisha kupata shida, lakini wakati mwingine ni matatizo ya kurithi,” alisema Dk Bokhari.

Namna pacha walivyoungana

Akitoa majibu ya vipimo kuhusu pacha hao, Dk Bokhari alisema watoto hao wameungana sehemu ya kifua na tumbo na vipimo vya CT Scan vinaonyesha kuwa kuna baadhi ya viungo vimeshikana.

“Tulipenda pia kujua je, mishipa ya damu wanashirikiana? Imetusaidia kujua kwamba kila mmoja ana mfumo wake, mbali na vipimo vya X Ray, tukaangalia full blood picture bahati nzuri ikaonyesha upande wa damu hakuna shida, wingi wa damu ni mzuri wana damu zaidi ya 12 kwa wao siyo mbaya,” alisema Dk Bokhari.

Hata hivyo, alisema majibu ya CT Scan ya tumbo na kifua yalionyesha kuna baadhi ya viungo wanashirikiana ikiwamo ini na katika moyo kuna chemba nyingi za milango wanazoshirikiana, pia majibu yaliyotokana na kipimo cha ECO yameonyesha kuna muungano katika moyo.

ECO ni kipimo ambacho kinaangalia hali ya moyo kama uko sawa au una tatizo lolote.

“Kutokana na jinsi walivyokaa kuona moyo ilikuwa ngumu kwenye kipimo cha ECO. Wakashauri tufanye kipimo cha ST Scan ya moyo pekee na hivyo kipimo kwa sasa bado hakijafanywa,” alisema.

Kuhusu afya za watoto hao alisema wanaendelea kuangaliwa kwa ukaribu wodini walipo na wanapewa maziwa ya mama kupitia mpira.

Kutenganishwa miezi sita ijayo

Kuhusu kutenganishwa, Dk Bokhari alisema kutokana na majibu hayo kazi hiyo inaweza kufanywa baada ya miezi sita ijayo.

Alisema kwa sasa wanachokifanya ni kuhakikisha wanakuwa na afya njema kwa kumpa mama Rebecca Mwendi lishe zote zinazotakiwa ili aweze kutoa maziwa bora kwa watoto wake.

“Kwa sasa mama yupo na watoto anakaa katika chumba cha ndani kilichopo ICU, amepumzishwa huko karibu na watoto wake anakula vizuri na maziwa yanatoka vizuri na watoto wanakula vizuri, japokuwa aliathirika kisaikolojia lakini kwa sasa yupo vizuri baada ya tiba aliyopewa na wataalamu wa saikolojia,” alisema.

Alisema awali, watoto hao waliozaliwa na uzito wa kilo 4.270 walikutwa na maambukizi kwenye kitovu na mmoja alikuwa hapumui vizuri na kwamba walipofika walianzishiwa dawa ya antibiotic ya mishipa kwa ajili ya kusafisha kitovu chao kila siku. Alisema mwingine alikuwa ameumia paja wakati wa kuzaliwa na baada ya kipimo cha X Ray wataalamu wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) walimtibu.

Upasuaji utakuwaje?

Kuhusu mipango ya upasuaji hapo baadaye, Dk Bokhari alisema kutakuwa na wataalamu wa upasuaji wa watoto kutoka vitengo mbalimbali kutokana na namna walivyoungana na kwamba kazi hiyo itachukua saa nyingi hivyo lazima kila kitu kiwekwe sawa hasa itakapofika kutenganisha ini na moyo, wataalamu zaidi wataongezeka.

“Ni upasuaji ambao tutashirikiana na wataalamu wengi wa aina mbalimbali, madaktari bingwa wa upasuaji wa watoto katika kifua na moyo lakini pia wakati wa kuwatenganisha kuna ngozi inayofunika viungo vya ndani iko ndogo lazima itafutwe, hivyo madaktari bingwa wa upasuaji wa kurekebisha maumbile lazima wawepo,” alisema.

By Herieth Makwetta, Mwananchi

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

HALIMA Mdee Kweli Kichwa Ngumu Ashukia Tena Serikali....Tazama Video Hapa Alichoongea

$
0
0
Siku chache baada ya Serikali kupitia msemaji wake mkuu (Idara ya habari Maelezo) kujibu hoja zilizotolewa na CHADEMA kuhusu hali ya kiuchumi kwasasa kwa kile walichodai ni mbaya, Basi leo August 04, 2017 Waziri kivuli wa fedha na uchumi wa kambi rasmi ya Upinzani bungeni Halima Mdee ameijibu Serikali kwa kusma maibu waliyotoa kuhusu hali ya uchumi kwasasa hayana ukweli. VIDEO:

HAKIKA Rais Magufuli si wa Kuchezea...Adai Mwizi ni Mwizi tu Hata Kama ni Mzungu......

$
0
0
RAIS John Magufuli amesema ifike wakati wizi uliokuwa ukifanywa na baadhi ya viongozi wa serikali wakishirikiana na wawekezaji kutoka nje ukomeshwe ili kuleta maendeleo ya Tanzania kwa ajili ya wananchi wote na si watu wachache kujinufaisha.

Hayo ameyasema leo wakati akiwahutubia wanachi wa Hale wilayani Korogwe wakati akianza ziara yake ya siku tano mkoani Tanga ambapo atashirikiana na Rais Museveni wa Uganda kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani kwenye mwambao wa bahari ya Tanga, Agosti 5 mwaka huu.

“Mlinipa kura nyingi sana na ninawashukuru na ahadi yangu iko palepale kwamba sitawaangusha, unapokuwa na kiongozi anayewatumikia wananchi ni jambo nzuri.

“Hatukuumbwa kwa ajili ya kuwa wasindikizaji wa watu bali tumeumbwa ili kuwa Tanzania yenye neema ndiyo maana hata kwenye kutumbua majipu huwa sijali hata kama ni Mzungu. Wapo Wazungu waliokuwa wamezoea kutumbua dhahabu yetu, nimeamua kuwatumbua bila aibu ili kutengeneza rasilimali za Watanzania kwani mwizi ni mwizi tu, awe Mzungu, awe wa CCM, awe wa Chadema, awe wa CUF au hata kama hana chama.

“Nitasimama kwa ajili ya Watanzania wanyonge bila kujali itikadi zenu kwa sababu lengo langu mimi ni kuleta maendeleo,” alisema Rais Magufuli.

Aidha rais ameeleza kuwa kwa Afrika mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga ni mradi mkubwa ambapo amewataka Watanzania kutumia fursa hiyo kupata maendeleo kwani watu zaidi ya 18,000 watapata ajira.

HATIMAYE Aliyekuwa MKE wa Mbunge Sugu Faiza Ally Apata Mtoto Mwingine

$
0
0
Leo ipo good news inayomuhusu Faiza Ally baada ya kujifungua salama mtoto.

Kupitia Instagram yake leo August 3, 2017 Faiza Ally amethibitisha kuwa amebahatika kujifungua mtoto, akiweka picha ya mtoto huyo na kuweka maneno ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuandika>>>”ALHAMDULILLAH 🙏🏽 @lijunior_well come to the world baby 👶”

MSEMAJI wa Simba Haji Manara Azidi Kutoa Tambo Dhidi ya Yanga..Adai Mwaka Huu ni wa SIMBA

$
0
0
Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Timu ya Simba, Haji Manara amefunguka na kusema kuwa mwaka huu lazima Simba itachukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara na kuvunja utamaduni wa Yanga kuchukua kombe hilo mfululizo.

Haji Manara amesema hayo leo wakati wa hafla ya kukabidhi jezi na vifaa vya michezo kwa timu zitakazoshiriki Ligi Kuu Bara 2017/2018 iliyoandaliwa na mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu Bara
Mbali na hilo Manara aliomba fedha ziwe zinawaishwa kidogo ili kuweza kusaidia vilabu vingine vidogo ambavyo vinachangamoto kubwa ya mapato ili kusaidia vilabu hivyo kufanya maandalizi kwa wakati.

"Tuangalie hizi timu za mikoani zinapata changamoto nyingi sana tuombe pesa zitoke kwa wakati ili timu ziweza kupanga bajeti zao za usafiri na mambo mengine lakini niseme tu mwaka huu Simba lazima ishinde ubingwa wa Ligi Kuu Bara 2017/2018" alisema Haji Manara

Klabu ya Simba imeshindwa kuchukua Ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa misimu minne sasa huku watani wao wa jadi Yanga wakichukua ubingwa huo mara tatu mfululizo, hivyo kama Simba mwaka huu itashinda inaweza kuvunja mwiko wa Yanga kuchukua ubingwa mfululizo.

App ya Ajira Yako ni Mkombozi Kwa Wanaotafuta Kazi Tanzania...Install Kwenye Simu yako sasa

$
0
0
JE una Tafuta Ajira au Unataka Badilisha Ajira uliyonayo?

Fanya Kuinstall App ya Ajira Yako Kwenye Simu ili kusoma na Kuapply Nafasi za kazi zinazotangazwa kila siku katika magazeti....


Bonyeza HAPA Kuinstall Bure

KIMENUKA...Kufuatia Kumruhusu Mtoto Kurusha Ndege, Kibarua Cha Marubani Chaota Mbawa

$
0
0
Serikali nchini Algeria, imewafukuzwa kazi marubani wawili wanaofanya kazi katika shirika la ndege la serikali baada ya kumruhusu mtoto wa miaka 10 kuendesha ndege.

Mtoto huyo anayedaiwa kuwa ni yatima alikuwa akiendesha ndege aina ya Air Algerie, iliokuwa na abiria ndani na ilifanya safari zake katika mji wa Algiers hadi Setif.

Zoezi la mtoto huyo kuendesha ndege lilifadhiliwa na kurekodiwa kituo cha El Bilad TV, ambapo walionyesha tukio zima huku kijana huyo akiwa amevalia sare za rubani.

Baada ya video na picha kusambaa za kijana huyo akiongoza ndege, ndipo serikali ilichukua hatua ya kuwafukuzwa kazi Marubani hao mnamo Julai 29 mwaka huu.

Also Read: Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo Bonyeza

UHAMISHO Neymar Utata Mtupu....La Liga Yagoma Kumuachia Wanasheria Wavamia

$
0
0

Shirikisho la soka nchini Hispania limeingilia kati usajili wa mchezaji wa kimataifa wa Brazili, Neymar Dos Santos kujiunga na Paris Saint-Germain kwa ada ya uhamisho wa pauni milioni 198 kiasi ambocho kinamfanya kuweka rekodi ya dunia akitokea Barcelona.

Zikiwa zimesalia saa chache kuhitimisha kwa usajili huo wa Neymar kumeibuka wingu zito katika usajili huo unaotarajiwa kuvunja rekodi ya dunia, chama cha soka cha nchi hiyo kimesema PSG walishajaribu kutuma dau hilo kwa Barcelona ili kujaribu kuvunja mkataba wa mshambuliaji huyo lakini La Liga walikikataa kiasi hicho cha pesa.

Uhamisho wa mshambuliaji wa Barcelona, Neymar umepingwa vikali na La Liga huku ikigomea sheria inayotumika kumsajili mchezaji huyo

Wanasheria wa PSG wamewasili katika shirikisho hilo (La Liga) mjini Madrid  leo  Alhamisi katika kuhakikisha wanazima jaribio la La Liga kumzuia mbrazili huyo mwenye umri wa miaka 25.

Una Tatizo la Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo?

$
0
0
JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUFIKA KILELENI HARAKA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?

Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k. Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250000@250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 @150000@150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130000@130,000/= BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA. KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255) 0767447444 na 0714335378 

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images