Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

RAIS Magufuli Awakosoa Wanaodai Akae Madarakani Kwa Miaka 20

$
0
0

Mh Raisi Kasema Hawezi kukaa Madarakani Miaka 20 Kama wananchi wanavyohitaji Kwani ni Kinyume Na Katiba

MANJI Mambo Magumu...Kuendelea Kusota Selo...

$
0
0

MANJI Mambo Magumu...Kuendelea Kusota Selo... Mahakama Kuu Tanzania imekubali pingamizi lililowekwa na serikali na hivyo kutupilia mbali maombi ya dhamana ya mfanyabiashara Yusuf Manji.

Toa maoni yako

Kutana Mtaalam wa Tiba Asili Mwenye Uwezo Mkubwa wa Kutatua Matatizo Kwa Nyota na Dua

$
0
0

KUTANA NA TABIBU MWENYE KUBRI KUTOKA KWA ALAH MAALIM ISSA NAJIMU. NI SHARIFU
MWENYE UWEZO WA KUBAINI TATIZO LAKO PUNDE TU UNAPO MFANYIA MAWASILIANO KUPITIA
WASAA NA SIKU KWA MAWASILIANO:-
MAALIM ISSA NAJIMU KUTOKA MKOA WA TANGA MWAMBONI MAGOFU KATA YA NGUVU MALI
NCHINI TANZANIA, NI TABIBU MWENYE KUBRI TOKA KWA ALAH ANATIBU KWA NJIA YA VITABU VYA
QUR-AN, DAWA ZA ASILI PAMOJA NA DAWA ZA KIARABU.
ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE / MKOA WOWOTE KWA MATATIZO YAFUATAYO:-
 ULIJALI (NGUVU ZA KIUME)
 MIGUU KUWAKA MOTO
 KUTAFSIRI NDOTO
 MFARAKANO WA WANANDOA
 MFARAKANO KAZINI
 KUPANDSHWA CHEO
 KUTOA PETE YA BAHATI
 ANAO UWEZO WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUBASHIRI
 KUFUNGUA UZAZI KWA WALIYO FUNGWA KWA NJIA YA USHIRIKINA
 KUTOA VIFUNGO VYOTE VILIVYO FUNGWA IKIWA NI KWENYE MWILI WA BINADAMU
/MAJUMBANI NA KWENYE BIASHARA.
 ANA UWEZO MKUBWA WA KUPANDIKIZA NYOTA YA KUMPATA YEYOTE UMPENDAYE KWA
KUMUOA AU KUWA NAYE.
 ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIYE MBALI PIA ALIYE CHUKULIWA KWA NJIA YA MSUKULE
 ANAO UWEZO WA KUUAq KESI SUGU NA PYA NDANI SIKU 7 TU.
 MENGINEYO MENGI ZAIDI YALIYO KUWA SUGU PIGA-
 Mobile; 0717 70 32 41.
 WhatsApp 06226 535419.

Video MPYA: Mabibi na Mabwana ni Rayvanny tena.. Katuletea ‘Chuma Ulete’

$
0
0
Mwimbaji kutoka WCB Rayvanny amerudi kwenye TV na hii video mpya inaitwa ‘Chuma Ulete’ enjoy dakika 4 na sekunde 48… ukishaitazama hapa chini usisahau kutoa comment yako umeipokeaje.

Mwanamuziki Q Chief Kabadili Dini? Aelezea Ukaribu Wake na Mchungaji Anthony Lusekelo 'Mzee wa Upako'

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva Q Chief ambaye hivi karibuni ameachia ngoma yake mpya ya 'Naogopa', amezungumzia suala la kubadili dini na kuingia kwenye dini nyingine, baada ya kuwa karibu na mchungaji Anthony Lusekelo.

Akizungumza na mwandishi wa East Africa Television, Q Chief amezungumzia suala hilo na kusema huwa familia yake upande wa mama ni Wakristo na ana amini katika Mungu, lakini sio rahisi kwake kubadilisha imani yake.

"Familia yangu upande wa mama wengi ni wakristo, lakini wamegawanyika kutoka kwenye uislam kwenda ukristo, baba yangu ni muislam, babu yangu ana msikiti kwa hiyo sio jambo jepesi kutoka kwenye dini yangu imani yangu kwenda kwenye imani nyingine, naamini Mungu ndiye jibu sahihi, lakini huwa nachukua ushauri wa viongozi wa dini tofauti tofauti", alisema Q Chief
Q Chief aliendelea kwa kuzungumzia kitendo chake cha kuwa karibu na Mchungaji Anthony Lusekelo 'Mzee wa Upako', na kusema Mchungaji huyo ni sawa na kaka yake na anapenda anavyomshauri.

"Kuna siku moja nilipigiwa simu usiku kama saa saba hivi, kupokea ni Mzee wa Upako nikashtuka, nikasema kuna kitu gani au zali zimenindondokea! lakini nikagundua ni shabiki yangu namba moja, na siku zote amekuwa akitamani kunishauri, kunijenga kiimani lakini pia kuzungumza na mimi kama kijana, kwamba lolote unalopitia usisahau Mungu amekuweka kwa sababu, na Mungu yupo kuwainua wale walioanguka, naheshimu ushauri wake kama kiongozi, kama kaka mshauri kama mchungaji", alisema Q Chief.

January Makamba Abaki njia Panda Baada ya Watu Aliowafukuza Kazi NEMC Kurudishwa Kazini Kinyemela

$
0
0
Maswali mazito yameibuka juu ya uamuzi wa Serikali kuwarudisha kazini kimyakimya wajumbe saba wa bodi na watendaji waandamizi wanne wa Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), siku chache baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba, kuwasimamisha.

Mwananchi limedokezwa kuwa hivi sasa watumishi hao, akiwamo Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Vedasto Makota wanaendelea na kazi zao kama kawaida kwa maelekezo ya mamlaka za juu.

Wiki mbili zilizopita, Makamba alitangaza kutengua uteuzi wa wajumbe saba wa Bodi ya NEMC na kuwasimamisha wakurugenzi wake wanne ---Manchare Heche, Deus Katwale, Andrew Kalua na Benjamin Dotto--- kwa tuhuma kadhaa ikiwamo ya ucheleweshaji wa vibali vya ukaguzi wa mazingira na tuhuma za rushwa.

Alisema NEMC ina upungufu mkubwa kiutendaji huku akiwatuhumu baadhi ya watendaji kwa kuwasaidia watu wenye masilahi nao na kushindwa kutoa maelezo ya kuridhisha pale walipotakiwa kufanya hivyo.

“Kulingana na mamlaka niliyonayo chini ya Sheria ya Mazingira Kifungu cha 19 (2), nimeamua leo kutengua uteuzi wa wajumbe wote saba wa Bodi ya NEMC ili baadaye niteue wajumbe wapya ambao wataenda na kasi na ari tunayoihitaji sasa katika kuelekea uchumi wa viwanda. Mwenyekiti wa Bodi, ambaye mamlaka yake ya uteuzi ni Mheshimiwa Rais, ataendelea kuwepo hadi Mheshimiwa Rais atakapoteua mwingine.”

Pia alisema, “Tumewasimamisha kazi baadhi ya watendaji wa NEMC kuruhusu uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili kabla ya kuchukua hatua zaidi.”

Makamba alimteua Dk Elikana Kalumanga kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NEMC.

Hata hivyo, baada ya hatua hiyo, imeelezwa kwamba wote walioondolewa wamerejeshwa kimyakimya. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Vedasto Makota hakupatikana kuzungumzia suala hili na mmoja wa waliosimamishwa kazi, Heche hakukataa wala kukubali kwamba amerudishwa kazini, akisema hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa liko chini ya mamlaka ya waziri.

Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa tangazo hilo la Makamba halikudumu kwa zaidi ya wiki moja baada ya mamlaka za juu kuagiza hali irudi kama ilivyokuwa awali.

Baadhi ya watu walio ndani ya NEMC wamedai kuwa uamuzi huo wa Serikali utaathiri kwa kiasi kikubwa utendaji wa Baraza hilo la Mazingira linalokabiliwa na changamoto nyingi kiasi cha mchango wake katika masuala ya uhifadhi wa mazingira kuhojiwa mara kwa mara.

“Hapa palishageuka kama himaya ya watu fulani tu. Hakuna kinachoenda. Malalamiko ni mengi kutoka jumuiya ya wafanyabiashara na wenye viwanda. Sio siri tena kwamba rushwa imetawala hasa katika eneo la utoaji vibali vya mazingira,” alisema ofisa mmoja wa daraja kati wa NEMC kwa sharti la kutotajwa jina.

“Kuna ukiritimba mkubwa kutoa cheti cha mazingira na mtu kama akiwa tayari kutoa pesa anapata hata ndani ya siku mbili tu. Kama huna utasumbuka sana,” alisema ofisa huyo.

Wizara ya Viwanda na Biashara imewahi kusikika mara kadhaa ikilalamikia ucheleweshaji wa utoaji wa vibali vya mazingira kama moja ya mambo yaliyozorotesha jitihada za Serikali za ujenzi wa viwanda nchini.

Akiwa katika ziara ya kikazi Mkoa wa Pwani mwezi uliopita, Rais John Magufuli alionyesha waziwazi kukerwa na ucheleweshaji wa vibali vya mazingira unaofanywa na NEMC na alizungumzia suala hilo mara mbili katika mikutano yake ya hadhara.

Mbali na ucheleweshaji wa vibali vya mazingira, rushwa inatajwa kukithiri ndani ya wakala huyo wa mazingira huku watendaji wakidaiwa kuwatoza faini wenye viwanda kinyume cha sheria na wakati mwingine kuwatisha ili watoe rushwa kwa ahadi ya kuwapunguzia faini.

Akitoa mfano, ofisa mwingine wa NEMC aliyeomba kutotajwa jina amesema baadhi ya maofisa waliwahi kukitoza kiwanda cha kuchinja nyama ya punda mjini Dodoma kinachomilikiwa na raia wa China faini ya Sh240 milioni kinyume na Sheria za Mazingira.

Suala hilo linadaiwa kufika mezani kwa waziri Makamba ambaye baada ya uchunguzi na kuweka vielelezo mezani zikiwamo risiti za tozo, ikagundulika wawekezaji hao walilipa Sh20 milioni tu huku watu wa NEMC wakiondoka na Sh100 milioni baada ya kukubali kuwapunguzia Wachina hao kiasi cha faini.

Ofisa huyo alidai kuwa watendaji hao waliamua kughushi mukhtasari kuonyesha kwamba mwekezaji huyo aliomba kupunguziwa faini.

Taarifa zinasema kuwa watendaji wote wa NEMC waliotajwa kwenye mukhtasari huo baada ya kubanwa walikikiri kuwa hawakuhudhuria mkutano uliozaa mukhtasari huo na kwamba hawana mamlaka ya kumpunguzia mtu faini isipokuwa waziri peke yake.

Mtoa taarifa wetu anadokeza kuwa hata bodi ilipofikishiwa suala hili ikasema watu hao wapewe onyo wakati kosa ni la wazi kabisa.

“Huku ni kulindana tu na NEMC isipokuwa overhauled (fumuliwa) tusitegemee chochote. Hizi ni zama za accountability (uwajibikaji) na kwa kweli kuna mambo hayaendi sawa humu mwetu. Sisi tukiboronga madhara kwa nchi ni makubwa kuliko watu wanavyoona,” alisema ofisa huyo wa NEMC.

Alipotafutwa kwa simu, waziri Makamba alikataa katakata kuzungumzia suala hilo. “Sisi tuko vizuri tu na tunatekeleza mipango ya Serikali kama kawaida. Sina zaidi ya hilo,” alisema.

Habari kutoka ndani ya wizara zinasema kukithiri kwa matatizo ndani ya NEMC kuliwahi kumsukuma Waziri Makamba kuwaita watendaji wake na kuandaa mkakati wa kuyashughulikia, wakilenga zaidi suala la utoaji vibali vya mazingira kwa kuangilia muda unaotumika kwa kazi hiyo, gharama na kuziba mianya yote ya rushwa.

Vyanzo vyetu vinasema kuna wakurugenzi ambao wanakabiliwa na tuhuma za wazi za kukiuka sheria za utumishi wa umma ikiwamo rushwa na ndizo zilizomsukuma Waziri Makamba kuwasimamisha kazi akijipanga kufanya mabadiliko makubwa ndani ya NEMC.

Watu wanaofuatilia kwa karibu sakata hili wanasema makundi yenye masilahi ya kiuchumi na NEMC hawakupendezwa na mwelekeo wa Makamba katika kuifumua NEMC ndipo wakaanza mkakati wa chini kwa chini kukabiliana naye.

Makundi hayo ndiyo yanayodaiwa kuiteka NEMC na yanalaumiwa kwa kukwamisha juhudi mbalimbali za wizara na Serikali kwa miaka mingi sasa kama vile kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki na kudhibiti viwanda dhidi ya uchafuzi wa mazingira na kujenga jumba za kifahari ndani ya hifadhi za fukwe mbalimbali.

Haijulikani ni nani, katika mazingira gani na kwa sababu ipi aliamuriwa ‘kumzima’ Waziri Makamba lakini vyanzo vyetu ndani ya NEMC vinaonya kuwa uamuzi huo utaadhiri utendaji kazi wa baraza na kumpunguzia waziri mamlaka ya kiutawala dhidi ya Baraza hilo.

Habari zinasema tayari Wangwe, alikwishapewa barua ya kuondolewa NEMC na kurudishwa Hazina.

Wafuatiliaji wanahoji pia ni jinsi gani Makamba atapeleka uso wake na kuanza kufanya kazi na kundi la watu ambao hana imani nao tena na alikwishaamua kuwaondoa kazini.

“Huu uamuzi sijui umechukuliwa na nani lakini jambo lililo wazi ni kwamba utamuondolea kabisa waziri moral authority (mamlaka ya kimaadili) kutimiza mipango yake na watu hawa waliorudishwa. Hali hii nina hakika imemshushia hadhi hapo wizarani na itakuwa imemvunja sana moyo,” alisema mtoa taarifa huyo.

Wadadisi pia wanahoji endapo mikakati iliyopo ya kuifumua NEMC na kuifanya ifanye kazi kwa ufanisi na uadilifu zaidi itatekelezwa katika mazingira ya sasa.

Kwa upande mwingine, suala hili kwa namna moja au nyingine limeiweka majaribuni vita ya Rais Magufuli dhidi ya rushwa na utendaji usioendana na kasi yake hasa ikizingatiwa hata aliwahi kuonyesha kutoridhishwa na ufanisi wa NEMC.

“Tatizo ni wazi kabisa hawa watu walishafeli kabisa katika majukumu na Makamba aliona ili mambo yaende lazima awaondoe. Sasa changamoto kwa huyu bwana (Makamba) ni kuhakikisha kazi na mipango yake vinaendelea katika hali ya vikwazo vilivyo mbele yake,” anasema.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema inawezekana waziri huyo kijana hakufanya mawasiliano ya kutosha kabla ya kuchukua uamuzi wake.

“Hili haina tafsiri nzuri. Nchi nyingine waziri huwa anajiuzulu kwa sababu mamlaka yake yamevizwa. Inawezekana alichukua hatua hiyo bila mawasiliano ya kutosha. Sidhani kama walimpa go ahead (ruhusa) halafu wa-reverse (wageuke),” anasema Profesa wa Chuo Kikuu Katoliki cha Ruaha (RUCU), Gaudence Mpangala.

“Unajua mfumo wa utawala wetu wa sasa walio chini ya Rais mara nyingi wanachukua hatua kwa kudhani wanampendeza Rais au waonekane wanafanya kazi lakini si mara zote hiyo inafanya kazi.”

Profesa wa Sayansi ya Siasa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Benson Bana alisema hatua ya Serikali kubadili uamuzi ya Makamba inaashiria kuwa hakufanya mawasiliano ya kutosha kabla ya kuchukua uamuzi wake.

“Nafikiri inawezekana ni tatizo la mawasiliano na mamlaka. Unajua kimsingi Makamu wa Rais ndiye mwenye dhamana. Waziri hana instruments. (mamlaka). Sasa kuvunja bodi ni dhamana ya Makamu wa Rais. Swali kubwa la kujiuliza hapa ni je, Makamu wa Rais alijulishwa na kuridhia mpango wa Makamba? Kama hakuridhia inawezekana ndiyo sababu mambo yamekuwa hivyo,” alisema Bana.

Source: Mwananchi

Ebitoke Baada ya Kukutana na Ben Pol

$
0
0
Mwimbaji wa RnB Ben Pol katika kuthibitisha kuguswa na ombi la mchekeshaji Ebitoke aliyetaka wafunge naye ndoa alipost picha kwenye Instagram yake na kuandika ujumbe wa shukrani kwa kuzipokea hisia zake.

Sasa new story baada ya tukio hilo ni kwamba Ayo TV na millardayo.com zimempata Mchekeshaji Ebitoke kwenye EXCLUSIVE Interview ambapo kaelezea hisia zake baada ya kukutana na Ben Pol.

“Kwanza napenda kumshukuru sana Meneja wangu kwa sababu yeye ndiye alifanya mpaka mimi nikakutana na Ben Pol na pia nimefurahi sana nimekutana na Ben Pol kwa sababu ni ndoto ambayo nilikuwa naisubiria kwa muda mrefu sana. Nimetimiza ndoto yangu na ombi langu.

“Ben Pol ni mtu mzuri kwa ukweli, nilivyokutana naye mwenyewe alifurahi sana. Kuniona mimi ali-appreciate mwenyewe nilifurahi. Alikuwa kwenye furaha ya ajabu ambayo sikutegemea.

“Nilitegemea kwamba nikikutana na Ben Pol atanichukulia sijui mtu gani lakini to be honest Ben Pol kanipokea vizuri sana na pia tumeongea mengi. Nimemuelezea hisia zangu ambazo nilikuwa nazielezea hadharani, ye mwenyewe nimemuelezea. Tumeongea vingi but sitaweza kuvisema vyote.” – Ebitoke.

VIDEO:

Nafuu Njaa ikuue sio Nikuletee Chakula – Rais Magufuli

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaonya watanzania wenye tabia ya uvivu kuwa katika utawala wake hata toa vitu vya bure kwa watu ambao hawataki kujituma kwenye kazi wakisubiri msaada.


Akihutubia wananchi wa wilaya ya Korogwe mkoani Tanga waliohudhuria uzinduzi wa kituo cha mabasi (Stand) wilayani humo, Rais Magufulina amesema kuwa watu wanaopenda kukaa vijiweni bila kujishugulisha huku wakilalamika njaa na hakuna pesa, ni bora wafe na njaa.

“Wakati wa kukaa kwenye magenge na kupiga maneno umepitwa na wakati, mnakaa kwenye pool unasubiri vitakuja hakuna, vya namna hiyo nataka kuwaeleza havitakuja kwenye utawala wangu, mnakaa mnasubiri tuna njaa tunataka mtuletee, mimi njaa nafuu ikuue kuliko nikuletee chakula, kwa sababu kama mwenzako ana chakula wewe una njaa, hatuwezi tukavumilia vitu vya namna hiyo”, amesema Rais Magufuli.

Hata hivyo Rais Magufuli amesisitiza kuwa dhamira yake ni kuifanya Tanzania iendelee kwa kusonga mbele kwahiyo hataogopa chochote ataendelea kuongea ukweli hata kama wavivu watamchukia.

Video: Roma Afichua Siri ya Mrembo Aliyemkatikia Jukwaani

$
0
0
Rapper Roma amefichua siri ya mrembo aliyemkatikia jukwaani katika show yake ya Dar Live kitendo ambacho kililalamikiwa na mke wake katika mitandao ya kijamii.

Roma amesema mrembo huyo alipandishwa jukwaani na mke wake baada ya kuona mrembo wa awali hafanyi vizuri katika uchezaji.

“One of interested story, huwezi amini yule baby aliyepanda kukatika wife ndiye aliyemleta jukwaani, mwanzo nilipanda na binti mmoja ambaye alisema anajua kucheza na anaweza akaperform vizuri ule wimbo, nilivyopanda naye hakuonyesha ushirikiano mzuri, namlazimisha akatike akawa anaona aibu,” Roma ameiambia Bongo5 na kuongeza.

“Sasa wife alikuwa kwenye ile show akamuona demu anakatika vizuri  akamwambia ebu nenda kacheze na shemeji yako, na yule akaja kaweuka kweli, kafanya shughuli mpaka wife akajutia uamuzi wake kwa nini alimtuma aje jukwaani, sema was nice show,” amesema Roma.

July 5 Mwaka huu mke wa Roma kwenye ukurasa wake wa Instagram alieleza kukerwa na kitendo cha mrembo huyo, “Kuwa Na Mume Msanii Wakati Mwingine Ni #Stress Nyie Acheni Tu Jamani!!!  Aaaf kuna vibinti ndiyo kama vinafanya makusudi Kama Huyu!!! Nilitamani Nipande Jukwaani Nikamshushe,” aliandika. VIDEO:

Tundu Lissu Amchana Waziri Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Charles Mwijage

$
0
0
Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) na Mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu amefunguka na kumchana Waziri Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw. Charles Mwijage kuwa anahamasisha vijana kujiajiri wakati yeye analialia.

Mh Tundu Lissu amesema hayo baada ya kuona video ya Waziri Mwijage akisema kuwa yeye anaipenda sana kazi yake ya Uwaziri na kusema watu ambao wamepewa viwanda wasitake kumponza akapoteza nafasi hiyo.

"Niwaambie watu wote mniepushe na kikombe hiki wote mliopewa viwanda kwa bei ya kutupwa nimepewa amri hivyo viwanda vifanye kazi, naomba msiniponze nina watoto na hii kazi ninaipenda" alisikika Waziri Mwijage.

Baada ya kuona video hiyo Mh Tundu Lissu anasema kuwa mawaziri mbalimbali wamekuwa vinara kuhubiri majukwani na kuwahamasisha vijana waliomaliza vyuo mbalimbali kwamba wanatakiwa kujiajiri wakati wao wenyewe wameshindwa kufanya hivyo.

"Waziri analia kuwa ni yatima, ana watoto, anaipenda kazi, Majukwanii wanahamasisha vijana waliokopeshwa fedha za kugharamia masomo wajiajiri" alisema Tundu Lissu.


Jana Rais Magufuli amemsifu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa kuanzisha viwanda mbalimbali lakini amesema kuwa anachukizwa na Waziri huyo anapokuwa mzito kufanya maamuzi ya kupokonya viwanda mbalimbali ambavyo havifanyi kazi na kusema sasa anataka kusikia watu wakinyang'anywa viwanda hivyo.

Duniani Kwa Sasa ina Marais Watano tu...Magufuli Akiwa Mmoja Wapo....

$
0
0
Kwa maoni yangu na kwa kuangalia kwa makini kulingana na mahitaji ya kidunia kwa sasa kuna wanaume watano tu ndio wanaweza kusimama wakaongea na mimi nikaelewa kuwa hawa in maraisi ingawa wote wana mapungufu yanayofanana juu ya Democracy.....

Magufuli :

Rais anayepigania masilahi ya watanzania kwanza na wazungu baadae..

Kafanikiwa kuwabana wazungu walipe Kodi kama alivyofanya kwa acacia.

Kama alivyofanya kwa wafanyabisha wengine kukimbia bandari ya Dar kisa tu sheria ya kodi iliyokuwepo toka enzi za kikwete ilianza kusimamiwa kwa umakini...

Kilichonivutia zaidi ni idadi ya miradi aliyoizindua ndani ya miaka miwili kama fly over DSM, Ujenzi wa Reli ya dar morogoro,miladi ya kiisitoria ya maji tabora, Sengerema ambako watu wako karibu na ziwa kilometer 3 walikuwa hawana maji miaka 55 ya Uhuru?...,na mwisho mradi wa bomba la mafuta kwenda Uganda hili ndio historia bora kabisa likikamilika...

Jambo lililonifuraisha zaidi mwaka huu wa fedha tupo na Ajira 52000 kiukweli kama tutashindwa kumsapoti Rais kwenye mambo muhimu ya kitaifa kama haya basi inabidi tupimwe mkojo.

Rais anayepambana na wahujumu uchumi bila kumungunya maneno,nimependa falsafa yake kiufupi ni Rais ambaye Huwezi kumlingania na Rais yeyote Africa kwa sasa nisijue kama atachoka lakini kazi anayofanya zile muhimu'

Kwana nikiri kuwa mimi ni msomaji mzuri wa magazeti ya ulaya kama Daily mail,The guardian, na the Sun....

BBC, CNN na Majarida pia ya marekani hayawezi kupitisha week bila kumuongelea Rais Magufuli kwenye habari zao..

Magazeti pia ya Kenya ,Nigeria,and south Africa hawa jamaa kila week lazima waandike tukio la rais Magufuli'..

Level za Magufuli kwa sasa ni watu kama

Vladimir Putin



Rais wa urusi ambaye aliikua urusi ikiwa na hali mbaya kiuchumi na kuipaisha na kuwa super power in the world..

Naweza pia kumlinganisha Magufuli na Rais wa Marekani.

Donald Trump

Ambabaye hana mzaha na masilahi ya wananchi marekani ...

Ambaye mwezi July pekee katengeneza ajira 270,000 wakati mwaka wake wa fedha unaanza.

Mwingine ambaye naweza kumlinganisha na Rais magufuli ni Rais wa North Korea bwana

Kim-Jong-Un


Ambaye pia hataki mzaha na masilahi ya watu was north Korea....

Rais wa mwisho duniani ambaye naweza kumkinganisha na Rais magufuli ni Rais Wa Philippines

Rodrigo Duterte 


Ambaye naye hataki kabisa wauza madawa ya kulevya kama alivyo rais wetu.

Marais waliobaki wengi ni very weak na hawaendani na wakati wa dunia inataka nini kwa sasa....

Kuna muda uwa namkosoa rais wetu lakini kwenye swala la kusimamia masilahi ya taifa nipo naye bega kwa bega Rais wetu ni Rais bora kabisa duniani kwa sasa narudia tena hakuna Rais wa africa anayeogopwa na kufatiliwa na watu wengi duniani kama alivyo Rais Magufuli'

Tumuunge mkomo Rais tujenge Tanzania vyama vipo vitaendelea kuwepo sioni ubaya wa sisi kuweka itikadi pembeni na kumsaport kwenye mambo muhimu ya kitaifa kama haya anayoyafanya Rais wetu Ccm, Chadema,Cuf vitapita lakini Tanzania itabaki.


Jamii Forums/technically

Uchaguzi Kenya: Uhusiano wa KENYA na Tanzania Kuwa Shakani iwapo.......!!!

$
0
0
Kesho ni siku ya Uchaguzi Mkuu nchini Kenya na viashiria vinaonesha kama ilivyokawaida kwa Tawala za Kiafriak,Rais aliyeko Madarakani kwa sasa Uhuru Jomo Kenyata huenda akashinda kwa kishindo dhidi ya mpinzani wake Raila Omolo Odinga.

Kama ndivo itakavokuwa basi huenda matokeo hayo ya kaanzisha mnyukano mwingine mpya kabisa ndani ya Afrika Masharaiki. Nitaeleza. Kampeni za uchaguzi zimehitimishwa juzi Ijumaa kule jijini Nairobi huku Edward Ngoyayi Lowassa akimpigia kampeni za nguvu Uhuru Jomo Kenyata mgombea wa tiketi ya JUBILEE. Edward Ngoyayi Lowassa ni PM mstaafu wa Tanzania na ndiye aliyekuwa mgombea wa Urais Tanzania mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA under UKAWA na kuwa mshindi wa 2 kwa JPM akizoa takribani kura miilioni 6 na ushei.

Raila Omolo Odinga mgombea Urais kwa tiketi ya NASA ni rafiki kipenzi wa Rais wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli. Hapa ndipo kwenye kiini cha sintofahamu baada ya matokeo ya Uchaguzi nchini Kenya hapo 8/8/2017. Ikumbukwe kwamba Raila Omolo Odinga anachuana vikali na Uhuru Kenyata wa JUBILEE. Raila ni PM mstaafu nchini Kenya wakti wa awamu ya Mwai Kibaki. Je, nini kitatokea katika uhusuano wa Kenya na Tanzania kama Uhuru Kenyata atashinda ambaye anasaidiwa wenya kampeni na Edward Lowassa mpinzani wa Magufuli? Yamkini mambo yatakuwa supa iwapo Raila Jaramogi Oginga Odinga atashinda ambaye ni rafiki kipenzi wa John Pombe Magufuli. Tusubiri hatima ya mchuano huu kwani bado masaa machache tu kuingia siku ya 8/8 ifikapo usiku wa manane. Mungu ibariki Kenya, Mungu ibariki Tanzania na Mungu ibariki Afrika na watu wake.Amina.

Jokete Mwegelo Ajibebisha Kwa Thierry Henry wa Arsenal

$
0
0
MWANAMITINDO ‘the big name’ Bongo, Jokate Urban Mwegelo ‘Kidoti’, wikiendi iliyopita alinaswa na mapaparazi akiwa amejibebisha (jokate ajibebisha kwa henry)  kwa staa wa soka wa mamtoni, Thierry Henry  ambae ni mchezaji wa zamani wa Timu ya Arsenal ya England.

Kwa mujibu wa picha hizo zilizosambaa mitandaoni jana, wawili hao walikutana Johannesburg nchini Afrika Kusini katika Ligi ya Mpira wa Kikapu (NBA) ya Afrika kwa mwaka 2017.

Jokate ambaye ni Balozi wa NBA kwa upande wa Afrika alihuduria mashindano hayo yaliyokutanisha timu za NBA kwa wachezaji wenye asili ya Afrika na wale wa mataifa mengine. Katika hali iliyoibua sintofahamu na maswali kibao, katika picha moja alionekana na mavazi tofauti na yale aliyoonekana nayo awali, lakini picha zote akiwa na Henry katika sehemu iliyosadikiwa kuwa ni hotelini huku wakionekana ni wenye furaha.

Picha hizo zilivuja ikiwa ni miezi kadhaa tangu Jokate alipoonekana na mastaa wengine wakubwa wa muziki nchini Marekani, Jay-Z na Beyonce.

Kupitia ukurasa wake jana, Jokate alitundika picha hizo na kuandika: “Nahamia Arsenal rasmi, naomba ushauri, lakini naambiwa Arsenal ni stress tupu.”

VIPI KUHUSU UHUSIANO WAKE NA ALIKIBA?

Kwenye suala la uhusiano wa kimapenzi, bado penzi la Jokate na mwanamuziki Ali Kiba ni kizungumkuti ambapo wamekuwa wakiachana na kurudiana.

Rais Magufuli Afunguka Kuhusu Kutawala Kwa Miaka 20

$
0
0
Watu mbalimbali wamekua na maoni juu ya utendaji kazi wa Rais wa awamu ya tano Dr. John Pombe Magufuli akiwemo Mstaafu Mwinyi, Wananchi na hata baadhi ya Wabunge bungeni walisikika wakisema wanatamani Rais huyu atawale kwa muda mrefu.

Leo wakati Rais Magufuli akiwa kwenye ziara yake Tanga amenukuliwa akijibu hicho kinachosemwa kuhusu yeye kuendelea kukaa madarakani hata baada ya muda wake kumalizika.

JPM amesema hawezi kukaa madarakani kwenye Urais kwa miaka 20 kama alivyoombwa pia na Mbunge Steven Ngonyani kwasababu ni kinyume na katiba.

Job Opportunities at TIGO Tanzania


Mwanumuziki Harmonize Apata Kigugumizi Gharama za Mjengo wake

$
0
0
Msanii wa Muziki Bongo, Harmonize ameshindwa kuweka wazi gharama alizotumia hadi sasa katika nyumba yake anayojenga.

Muimbaji huyo kutoka label ya WCB, amesema ndio kwanza anaanza na Mungu akijalia mwakani mwishoni inaweza ikawa imeisha na nyumba hiyo ni ghorofa.

“Kwa hiyo flow ya kwanza tayari bado ya pili, kidogo kidogo tunajikongoja tukipata 200 tunaweka. Sio kitu kizuri kusema (gharama) nadhani lakini imetumia hela nyingi,” ameimbia XXL ya Clouds Fm na kuongeza.

“Siwezi nikakadiria lakini imekula hela nyingi, show zenyewe hizi kwa mwaka sita/saba na usawa wenyewe ulivyo mgumu lakini nashukuru sio show pekee zinazonipatia hela kuna mishe nyingine, kwa hiyo siwezi kujua ni kiasi gani imekula lakini imekula hela nyingi,” amesema Harmonize.

Harmonize kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Sina’ ambayo katika video yake amemshirikisha msanii mwenye heshima yake katika Bongo Flava, Mr Nice.

Mambo 7 Ambayo Mwanamme Hapaswi Kumfanyia Mke wake

$
0
0

Mambo 7 ambayo mwanaume apaswi kumfanyia mke wake..

1. Usimpige.
2. Usimtukane na kumshushia heshima.
3. Usimfanye ajihisi hapendwi na anamkosi.
4. Usimbake.
5. Usimsaliti na kujionyesha kabisa kwamba una saliti.
6. Msikilize pale anapokua na stress, mpe muda wako, mkumbatie na mpe maneno ya faraja.
7. Mpe zawadi, hata kama ni ndogo kiasi gani kwake ni alama tosha.

Waethiopia 72 Wanaswa Chalinze Wakiingia nchini

$
0
0
HUKU serikali ikiwa inaweka mikakati ya kukabiliana na wimbi la wahamiaji haramu nchini, Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limewakamata wahamiaji haramu 72 kutoka Ethiopia kwa tuhuma za kuingia nchini bila ya kibali.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Kituo cha Wilaya ya Kipolisi Chalinze, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Jonathan Shana alisema wahamiaji hao walikuwa safarini kwenda Afrika ya Kusini.

Kamanda Shana alisema wahamiaji hao walikamatwa Jumamosi saa 3:30 asubuhi kwenye Pori la Ranchi ya Taifa (NARCO) Kata ya Vigwaza, Chalinze wilayani Bagamoyo. “Mbali ya wahamiaji hao haramu, pia tunamshikilia Rajabu Hitaji (30) mkazi na mfanyabiashara wa Vigwaza baada ya msako mkali uliofanywa na makachero wa Jeshi la Polisi baada ya kupata taarifa kuwa kuna wahamiaji haramu wameingia bila ya kibali,” alisema Kamanda Shana.

Alisema wahamiaji hao haramu baada ya kugundua kuwa kuna gari la polisi linawafuatilia, waliingia kwenye hifadhi hiyo kwa lengo la kujificha, lakini msako mkali uliofanywa uliwabaini na kukamata kundi la kwanza la watu 63 ambao walikaa sehemu ambayo gari haliwezi kufika.

“Baada ya kuwakamata wahamiaji hao haramu kundi la kwanza askari waliendelea na msako ambapo waliwakamata wahamiaji wengine tisa waliokuwa wakijaribu kutaka kutoka kwenye pori hilo,” aliongeza Kamanda Shana. Alisema wahamiaji hao haramu wanatarajiwa kukabidhiwa Idara ya Uhamiaji kwa ajili ya hatua za kisheria pamoja na mfanyabiashara aliyekamatwa anayetuhumiwa kuwasafirisha.

Mwanamke Ukiwa na Tabia Hizi 7, Lazima Mwanaume Akukimbie

$
0
0
1. CHOKOCHOKO
Wanaume wengi huwa hawapendi chokochoko. Hawapendi mwanamke ambaye yeye kila wakati ni kuanzisha chokochoko ambazo zinazalisha ugomvi. Wanaume wengi hawapendi mabishano. Hawapendi ugomvi hivyo mwanamke anapokuwa hodari wa kuleta chokochoko, huepukwa.

Ni vyema basi mwanamke akachunga kauli. Akawa si mtu wa kuchimbachimba vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Asiwe na kisirani. Kinywa chake kitawaliwe na maneno matamu, yatakayomtia moyo mpenzi wake, yatakayomfariji na yatakayomfanya apende kuzungumza naye.

Mara nyingi mwanaume akiona mke au mpenziwe ni mtu wa kupenda chokochoko, mara nyingi humuepuka. Anajitahidi kadiri ya uwezo wake kukaa naye mbali. Ataona ni bora achelewe kurudi nyumbani akakutane na marafiki baa, wapige stori ili muda uende na akirudi nyumbani asiwe na muda wa kuzungumza na mwenzi wake, yeye ni kula na kulala.

2. KUTORIDHIKA
Wanaume wengi wanachukia kuwa na wanawake wasioridhika. Baadhi ya wanawake hata uwape nini huwa hawaridhiki. Wanawasumbua wapenzi wao kwamba hawawatimizii mahitaji. Mwanaume anajitoa kumpa zawadi mpenzi wake, haridhiki tu.

Anaanza kuikosoa. Anasema haifanani na yeye, eti si ya hadhi yake. Akipewa fedha anasema hazitoshi. Kila siku ni malalamiko. Hampi nafasi mpenzi wake ya kufurahia uhusiano wao.  Anamfanya kila anapokutana naye awaze atapigwa mzinga.

Bahati mbaya sasa kila atakachopewa haridhiki. Anatamani kikubwa zaidi. Wanaume wengi siku hizi wanaichukia tabia hiyo. Hawapendi kuwa na mwanamke ambaye haridhiki na kile kidogo walichojaliwa. Wanaume wengi wakiona hivyo huwa wanaanza kumuepuka mwanamke wa ‘sampuli’ hiyo.

Kwake kunakuwa hakuna jema. Badala ya kumshauri mpenzi wake mbinu za kujikwamua kiuchumi yeye ni lawama tu. Kila siku analalamika kwamba wanaume wengine wanawapa wapenzi wao mahitaji muhimu lakini wa kwake hamtimizii.

Mwanaume akiona kila analofanya kwa mpenzi au mkewe haridhiki, hatoi shukurani ni rahisi kupunguza mapenzi kwa mtu wake. Taratibu anaanza kujitoa na hata kuhamishia mapenzi kwa mtu mwingine ambaye atakuwa anaridhika kwa kidogo anachopewa. Ni muhimu kuridhika.

3. KULINGANISHA
Hii nayo ni tabia isiyopendwa na wanaume wengi. Wanaume wanapenda kuishi maisha yao. Wanapenda kuheshimiwa na wapenzi wao. Wanapenda kumsikia mwanamke akisema; ‘hakuna mwanaume mwingine wa kufanana na wewe.’

Mwanaume anapenda kuhakikishiwa kwamba hakuna mwanaume mwingine kama yeye. Yeye ndiye mzuri au bora kuliko wanaume wengine hivyo mwanamke anapoanza kuonesha tabia za kumlimnganisha na mwanaume mwingine linakuwa tatizo kubwa.

Mwanaume anakasirika. Anaona ni rahisi mwanamke wake kumtamani mtu mwingine baki kuliko yeye. Sifa anazozitoa kwa mwanaume mwingine ni nzuri hivyo zinamvutia. Kama zinamvutia siku yoyote anaweza kushawishika kumfuata yule anayemvutia.

Wanawake wanapaswa kuwa makini katika eneo hilo. Hata kama umeona kuna kitu kizuri kimekuvutia kutoka kwa mwanaume mwingine, kamwe usije kumwambia mwenzi wako. Baki nalo moyoni. Jipe moyo kwamba mwanaume uliyenaye ndiye bora kuliko wanaume wote duniani.

4. KUWA TEGEMEZI
Wakati mwingine hata kama huna kitu lakini mwanamke unashauriwa kutojionesha huna kitu. Jioneshe kwamba una kitu hata kama huna. Wanaume wa sasa hawapendi kuwa na mwanamke ambaye kila kitu anategemea kutoka kwa mwanaume.

Hata kama huna kazi lakini ni vyema basi mwanamke akajaribu kufanya biashara ndogondogo ambazo zitampunguzia mwanaume wake makali ya kuombwa fedha kila wakati. Wanaume wanapenda kuwapa wapenzi wao fedha lakini inapozidi kipimo inageuka kuwa kero.

Yani kuanzia mahitaji ya kila siku, saluni, mavazi, ada ya watoto na mengine mengi mwanamke anamtegemea mwanaume. Yeye hataki kujishughulisha hata kidogo. Anataka aletewe, kazi yake kubwa ni kulea familia nyumbani.

Mwanaume akigundua mwanamke ni tegemezi mkiwa katika hatua za mwanzoni, ni rahisi kumkimbia mwanamke na kwenda kwa mwanamke ambaye angalau atakuwa hamtegemei kwa kila kitu. Mwanamke anayejiongeza hata kwa kutoa wazo la kuanzishiwa biashara ambayo itamfanya asiwe tegemezi.

5. KUTOKUA MUELEWA
Mwanaume anapenda mwanamke muelewa. Hapendi mwanamke mbishi. Anatamani kuwa na mwanamke ambaye akimueleza kitu, anajiongeza na kufanya zaidi ya pale mwanaume alipofikiria. Mwanaume anapenda mwanamke atakayeanzisha wazo la kimaendeleo na kumshirikisha mpenzi wake ili walifanye.

Wanaume wanapenda wanawake wanaowaelewa. Kama mwanamke anakuwa si wa kumuelewa mpenzi wake, kumsaidia basi mara nyingi mwanaume humkimbia.

6. KUJITAPA KWA KUWA NACHO
Hakuna mwanaume anayependa kutawaliwa. Wanawake wenye fedha mara nyingi wanakuwa na tabia ya kutaka kuwatawala wanaume. Anataka mwanaume afanye kile ambacho yeye anataka. Fedha zinamvimbisha kichwa na kuona kwamba anaweza kuwa na mamlaka ya kumuamrisha mumewe.

Anatumia fedha zake kama fimbo ya kumchapia mpenzi wake. Ni vigumu sana wanaume kumvumilia mwanamke wa aina hiyo, mara nyingi wanajiepusha naye. Kwa kutumia fedha zake anaweza kupata mwanaume mwingine lakini pia watashindwana katika suala la kumtawala.

7. KUWA BIZE SANA
Wanaume wengi hawapendi mwanamke tegemezi lakini pia wanaume haohao wanachukia mwanamke akiwa bize sana na kazi zake. Mwanaume hapendi kuona mwenzi wake anakuwa bize na kazi au biashara zake kiasi ambacho kitamfanya hata akose muda na mwenzi wake.

Unachotakiwa kufanya hapo mwanamke ni kujigawa. Hakikisha unakuwa bize na kazi lakini si ya kupitiliza maana itamfanya mwanaume akose muda wa kuwa na wewe pale anapokuhitaji, badala yake anaweza kwenda kwa mwanamke mwingine ambaye hayupo bize.

Kama Upo Kwenye Mahusiano Miaka 2 na Msichana na Hujaona Chozi lake, Huyo Hana Mapenzi ya Kweli

$
0
0
Leo nimeona nilete hili jambo, katika ujana wangu nimebahatika na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na zaidi ya msichana mmoja ila kitu nilicho gundua hata wewe jalibu kufanya utafiti

kama upo kwenye mapenzi na mwanamke zaidi ya miaka miwili na hujabahatika walau siku moja
kuona machozi yake basi tambua huyo mwanamke hana mapenzi ya dhati kwako chamsingi
nikuchukua tahadhari mapema OVA.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images