Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Erick Shigongo: Hatimaye Ndoto Yangu ya Kujiunga Chuo Kikuu Imetimia sasa.....

0
0
Mjasiriamali na Mtunzi wa vitabu mashuhuri nchini Tanzania, Erick James Shigongo anatarajia kurudi shule na kusoma elimu ya shahada baada ya kuhangaika muda mrefu kutafuta nafasi hiyo, huku akisukumwa na masimango na matusi ya mitandaoni.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Erick Shigongo ameandika waraka mrefu akielezea safari yake kitaaluma na furaha aliyonayo, ya kuweza kufikia ndoto yake ya kuwa na elimu ya chuo kikuu, licha ya kuwa na mafanikio makubwa kwenye kazi zake za utunzi na maisha kiujumla.



“Ndoto imetimia, hatimaye naingia Chuo Kikuu, nikiwa mtoto nilitamani sana kusoma hadi chuo kikuu lakini sababu ya umasikini na mazingira magumu hasa shule nilizosoma, sikufaulu mtihani wa darasa la saba, nikarudia darasa la saba katika shule nyingine lakini bado sikufaulu, nilijiona mjinga! Nikajaribu kupitia njia ya ‘vikozi’ vidogo ili hatimaye niingie chuo kikuu lakini sikufanikiwa, nikaachana na ndoto hiyo na kuanza ujasiriamali”, ameandika Erick Shigongo.


Erick Shigongo alendelea kuandika akisema kuwa ndoto yake hiyo imefanikiwa baada ya kujiunga na mfumo wa RPL ambao hufanya watu wenye uzoefu fulani katika jamii bila kuwa na elimu, na kuwapa nafasi ya kusoma elimu ya juu, ndipo alifanikiwa kupata nafasi mwaka huu, baada ya kufeli mwaka jana.


“Nikakusanya vitabu vyangu ambavyo nimekwishaandika na kuvipeleke Tume ya Vyuo Vikuu na kuomba niruhusiwe kufanya mtihani huo, nikaruhusiwa, mwaka jana nikafanya na kufeli, sikukata tamaa, mwaka huu nikafanya tena na kufaulu, hivyo mwezi wa tisa ninaanza mwaka wa kwanza “, ameandika Erick Shigongo.

Picha ya Lemutuz Akila Wali Maharage Yazua Maswali, Baada ya Kujifananisha na Billgates

0
0

Huku mitandani watu wanajiuliza kuwa eti kula wali maharage ni kujishusha ? baada ya Lemutuz kupost picha akiwa anakula wali maharage huku akiwa ameuganisha na ile ya Billgates ....

Soma Comment ya Lemutuz hapo juu alafu utuambie kama kula wali maharage ni kujishusha....

Neymar Afunguka Baada ya kucheza Mechi Yake ya Kwanza Paris St-Germain

0
0


 Neymar Afunguka Baada ya kucheza  Mechi Yake ya Kwanza Paris St-Germain
Neymar alifunga bao mechi yake ya kwanza katika klabu yake mpya ya Paris St-Germain baada ya kununuliwa kwa rekodi ya dunia ya £200m kutokaBarcelona.

Raia huyo wa Brazil alichangia katika mabao yote matatu yaliyofungwa na PSG dhidi ya Guingamp ambao wamefanikiwa kudumisha rekodi yao ya kushinda 100% mwanzo wa msimu.
Jordan Ikoko alifungua ukurasa wa mabao kwa kujifunga baada ya pasi ya Neymar kwa Edinson Cavani kuzimwa

Neymar kisha alimsaidia Cavani kufunga kwa pasi safi kabla ya nyota huyo wa uruguay naye kumpa pasi Neymar ambaye alifunga dakika za mwishomwisho akiwa hatua sita hivi kutoka kwenye lango.
PSG wamnunua Neymar kwa rekodi ya dunia ya £200m
Mchezaji huyo wa Brazil mwenye miaka 25 alichezeshwa upande wa kushoto lakini alihusika kati safu ya mashambulizi.

Alitamba sana uwanjani kwa kugeresha na kushambulia, ingawa mengi ya makombora yake yalizimwa kabla yake kufanikiwa kufunga dakika za mwisho.

Neymar aligusa mpira mara 128 - mara pili kwa wingi mechi ya ligi Ulaya
Akilinganishwa na washambuliaji wenzake Edinson Cavani na Angel di Maria
Makombora6, pamoja na yaliyozimwa(sawa na Cavani na Di Maria)

Real Madrid Waionyesha Barcelona Waichapa 3-1 Wakiwa Pungufu uwanjani

0
0



Real Madrid Waionyesha Barcelona Waichapa 3-1 Wakiwa Pungufu uwanjani
Klabu ya Real Madrid imefuta uteja dhidi ya Barcelona kwa kuichabanga goli 3-1 na kutwaa ubingwa wa kombe la Super Cup nchini Hispania.


Ronaldo akipachika mpira wavuni dakika chache kabla ya kupigwa kadi nyekundu.

Licha ya Mshambuliaji wao tegemezi wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo kupata kadi nyekundu kunako dakika ya 82, Madrid walionekana kutokata tamaa na kupambana zaidi.

Goli la kufungua akaunti ya magoli ya Real Madrid lilipatikana kunako dakika ya 60 ya kipindi cha pili baada ya Beki wa Barcelona, Gerard Pique kujifunga kabla ya Ronaldo na Asensio kuonesha viwango vyao na kutupia goli kila mmoja.

Goli la kufuta machozi la Barcelona lilifungwa na Lionel Messi kunako dakika dakika ya 77 kwa njia ya penati baada ya Luis Suarez kuangushwa kwenye eneo la penati, Tazama magoli yote hapa chini




Hivi Ndivyo Dkt. Cheni Alivyonusurika Kifo Baada ya Kupata Ajari Mbaya

0
0

Hivi Ndivyo Dkt. Cheni  Alivyonusurika Kifo Baada ya Kupata Ajari Mbaya
Muigizaji wa kitambo Bongo, Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’ amenusa kifo baada ya kupata ajali mbaya baada ya gari lake kupasuka tairi la mbele na kuparamia nguzo kisha kupata maumivu makali kwenye bega la mkono wa kushoto.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu, Cheni alikumbwa na mkasa huo usiku wa Alhamisi iliyopita maeneo ya Bamaga-Mwenge, Dar, wakati akitokea Tegeta kwenye sherehe ya mmoja wa jamaa zake ambapo alipofika eneo hilo, ghafla tairi la upande wa kulia lilipasuka na kukosa mwelekeo kisha kuivaa nguzo iliyopo pembeni kabla ya kukwama kwenye jiwe kubwa.

 “Dah! Ni kweli nilipofika pale Bamaga, ghafla nilisikia gari limekuwa zito na hapohapo tairi la mbele likapasuka. Gari lilikosa mwelekeo nikalielekeza kwenye nguzo, ninamshukuru Mungu sikupata jeraha kubwa, nimeumia bega la kushoto ila ninaendelea vizuri,” alisema Dk Cheni.

'Qeen Of Maasai' ya Rich Kutoa Fundisho kwa Jamii Namna Mwanamke Anaweza Kubadirisha Jamii

0
0

 .
'Qeen Of Maasai' ya Rich Kutoa Fundisho kwa Jamii Namna Mwanamke Anaweza Kubadirisha Jamii
Msanii mkongwe katika filamu Bongo, Single Mtambalike ‘Rich’ yupo mbioni kuachia kazi yake ya Queen of Maasai mwanzoni mwa Septemba ambayo anaonyesha jinsi gani msichana anaweza kubadili maisha ya jamii yake.

 Rich alisema waigizaji wengi wanakimbilia kutengeneza filamu za kimapenzi, lakini yeye kama mkongwe, ameamua kuonyesha jinsi msichana mdogo anavyoweza kubadili maisha ya jamii yake kama akipata fursa na kujielewa.

“Hii ni filamu iliyochezwa umasaini, inaonyesha jinsi msichana wa kimasai anavyoweza kubadili maisha ya jamii yake. Tumezoea wamasai ni wafu-gaji, wasi-ojali elimu, lakini katika filamu hii inaonyesha mageuzi katika jamii yanaweza kufanywa na msichana, tofauti na fikra za wengi kuwa wanaume ndiyo wa kubadili mambo,” alisema Rich ambaye ni mmoja wa waigizaji mahiri nchini

Hizi Ndizo Picha za Nicki Minaj Zilizompagawisha Mchungaji wa Kanisa Moja Marekani

0
0

Hizi Ndizo Picha za Nicki Minaj Zilizompagawisha Mchungaji wa Kanisa Moja Marekani
Mchungaji mmoja nchini Marekani ameonyesha kukubali picha maarufu ya msanii wa rapa wa Young Money, Nicki Minaj mpaka kutupia comment ya Utamu….

Hizi Ndizo Picha za Nicki Minaj Zilizompagawisha Mchungaji wa Kanisa Moja Marekani
Nicki Minaj alipost picha hii kwa watu wake milioni 82 na mchungaji Dewberry akatupia comment hio,





Kilichonifurahisha Kutoka Kwa Billgates ni Kuwa Hatembei na Mabaunsa au Walinzi Licha ya Utajiri wake

0
0
Kuna jambo la kufurahisha kama sio la kushangaza Tajiri na multi millionaire na mtu mwenye brand kubwa na ushawishi Bill gates anatembea bila ya kuwa na mabaunsa au walinzi.Tajiri huyu ana utajiri wa Dollar Billion 90

 Diamond na Utajiri wake wa Bilioni 1 akiwa na Mlinzi wake

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo Jumatatu

0
0

BREAKING: MCT Yatoa Ripot ya Uchunguzi wa Uvamizi Studio za CloudsTV

0
0



BREAKING: MCT Yatoa Ripot ya Uchunguzi wa Uvamizi  Studio za CloudsTV
Baraza la Habari Tanzania (MCT) limezindua Ripoti ya Hali ya Vyombo vya Habari hapa nchini kwa mwaka 2016 (State of the Media Report) ambapo ripoti hiyo hutolewa kila mwaka ili kuushirikisha umma.

Pia Baraza hilo linatoa ripoti kuhusu kuvamiwa kwa Studio za Clouds Media na kubaini jinsi tukio hilo lilivyoathiri uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa uhariri.

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Baraza hilo amesema ripoti hiyo haina lengo baya, bali ni kuweka bayana hali ya tasnia ya habari na kwamba hambo hilo si mara ya kwanza kwani baraza hilo limekuwa likitoa ripoti kama hizo kila mwaka.

“Hatujafanya uchunguzi huu kwa kuwa tuna mapenzi na Clouds Media wala kwa sababu tuna mahusiano na Mkuu wa Mkoa, badala yake tumetoa ripoti hii kwa mujibu wa katiba ya MCT,” alisema katibu

Uhuru Kenyatta Atampa Wakati Mgumu Lowassa Uchaguzi wa Tanzania 2020

0
0

Ukizichakata vizuri nadharia zilizomfanya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kukatwa mapema kwenye kinyang’anyiro cha urais CCM mwaka 2015 ni tabia ya kudhihirisha nguvu na silaha zake.

Lowassa alijiweka wazi kwa kila kitu kiasi kwamba iliwapa urahisi viongozi wa juu wa CCM waliokuwa na malengo ya kumzuia asipate tiketi, kujua ni wakati gani katika mchakato na hatua ipi ya kumuondoa.

Hata kwa mfuatiliaji wa juujuu alijua kabisa kuwa nguvu na jeuri ya Lowassa kuelekea kuipata tiketi ya CCM kuwania urais ilikuwa kwa viongozi wa CCM wa mikoa, wajumbe wa Kamati Kuu (CC), Halmashauri Kuu (Nec), vilevile Mkutano Mkuu.

Lowassa akijionyesha wazi hivyo, alikuwa anafahamu wazi kwamba kikwazo chake kikubwa kuelekea kuwa Rais wa Tanzania kilikuwa tiketi ya kuwa mgombea urais wa CCM, kisha kikwazo cha kuipata tiketi hiyo ni uongozi wa juu wa chama.

Sasa basi, kanuni ni kwamba unapokuwa kwenye mapambano ya aina yoyote yenye alama za vikwazo hupaswi kudhihirisha nguvu zako. Endapo kikwazo kinakuwa ni watu wenye nguvu kuliko wewe, kuonyesha japo chembe ya uimara wako ni hatari sana.

Kuelekea kuitwaa tiketi hiyo, Lowassa alikuwa anakabiliwa na kikwazo cha watu ambao si tu walikuwa na nguvu ya kulazimisha uamuzi kwenye chama, bali pia walikuwa na mamlaka makubwa kwenye nchi.

Kati ya mbinu 36 za kushinda mapambano zilizochorwa karne ya tano na Jenerali wa China ya Kale upande wa Kusini (Southern Qi), Wang Jingze na kuwekwa kwenye kitabu cha Qi , ile ya kwanza ingemsaidia Lowassa.

Baada ya Mfalme Gao kufariki dunia, alifuata mjukuu wake, Mfalme Xiao Zhaoye ambaye alimteua mjomba wake, Xiao Luan kuwa Waziri Mkuu. Xiao Luan alimpindua Mfalme Xiao Zhaoye (mpwa wake) na kumuua kwa hoja kuwa alikuwa hatoshi ufalme.

Xiao Luan ndiye Mfalme Ming ambaye baada ya kujitangaza Mfalme wa Southern Qi, alianza kuua watu ambao walikuwa ni ndugu damu ya moja kwa moja kutoka kwa Mfalme Xiao Zhaoye mpaka Mfalme Gao. Alitaka kukifuta kizazi chote ili abaki salama.

Wang Jingze alipoona mnyororo wa vifo, alijua naye zamu yake ya kuuawa imewadia, ndipo alipozama chini kuandika mkakati wenye mbinu za kumpindua Mfalme Ming.

Mkakati huo ndiyo ambao nautumia hapa kuonyesha jinsi nadharia zake kama zingetumika, Lowassa angeweza kushida tiketi ya kuwa mgombea urais CCM 2015 kisha kuwa Rais.

Somo lililompita Lowassa

Katika mbinu hizo, ya kwanza inasema vuka bahari bila ufahamu wa mfalme. Hapo Wang alimaanisha kuwa kwa sababu alikuwa kwenye mapambano na mfalme, yaani mtawala, ilikuwa lazima apange mipango yake bila kumfanya Mfalme Ming amshutukie. Unaficha lengo kuu, ukitanguliza lengo bandia ili adui asikushtukie unataka nini.

Wang alikuwa Jenerali wa Southern Qi, hivyo vikosi vya jeshi la China Kusini vilikuwa chini yake, kutokana na uwezo huo, ingedhaniwa yeye kumpindua au kumuua Mfalme Ming ni rahisi. Hata hivyo, alitambua nguvu ya mfalme, ndiyo maana alituliza kichwa na kuandika mbinu hizo 36.

Lowassa alifahamu kuwa Rais Jakaya Kikwete hakuwa radhi naye kuelekea kuwa mgombea urais wa CCM na hatimaye kuwa Rais. Kikwete pia ndiye alikuwa mwenyekiti wa CCM.

Kwa kutambua hilo, Lowassa alipaswa kumheshimu na kumhofia zaidi Kikwete maana alikuwa na nguvu nyingi za kuzuia ndoto zake za kuwa Rais. Kwa maana hiyo, Lowassa alipaswa kufanya siasa za kumzunguka Kikwete, bila kumwonyesha mahali nguvu yake ilipo.

Lowassa alipaswa kuvuka bahari bila Kikwete kujua. Ilitakiwa Kikwete kila akisaka alama za uimara wa Lowassa azikose. Hiyo ingempa wakati mgumu wa kujua mahali pa kimdhibiti.

Mathalan, Lowassa alikatwa kabla ya kufika kwenye mkutano wa Kamati Kuu uliotakiwa kupitisha majina matano ya kwenda Nec ambayo ilichagua watatu kuingia Mkutano Mkuu.

Uamuzi wa kukata jina la Lowassa kabla ya kuingia Kamati Kuu, ulisababishwa na ukweli uliokuwa wazi kwamba nguvu yake ilikuwa kubwa kuanzia Kamati Kuu, Halmashauri Kuu mpaka Mkutano Mkuu.

Kwa maana hiyo, Lowassa alivuka bahari kwa kelele, hivyo kumshtua mwenyekiti na vigogo wa chama ambao waliamua kumkabili kwa kumuondoa kwenye kinyang’anyiro kabla ya kuingia kwenye maeneo ambayo Lowassa aliyategemea sana.

Tafsiri kila hatua na ‘chachandu’ za kisiasa ambazo Lowassa alinogesha mwaka 2015, mpaka akaonekana tishio, Kikwete aliona siyo kitu kwa sababu alijua mahali pa kumdhibiti. Usipambane na mwenye mamlaka ukimwonyesha jeuri yako ilipo.

Sura ya tatu ya mbinu za kushambulia, ya pili ‘Borrow a corpse to resurrect a soul’. Tafsiri isiyo rasmi ni kodisha maiti ufufue nafsi. Hata hivyo, kile ambacho Wang alikimaanisha ni kuwa ukishajua mbinu za adui unazikodi kisha unazitumia au timu yake pia unaichukua.

Mtu hawezi kuifahamu timu unayoitegemea kama hujajiweka wazi. Ndiyo maana baada ya Lowassa kukatwa CCM, Kikwete aliwachukua watu wake muhimu kama Dk Emmanuel Nchimbi, Sophia Simba na wengine kisha kuwapa majukumu muhimu dhidi yake.

Nchimbi na Sophia wote waliingizwa kwenye timu ya kampeni za ushindi wa Dk John Magufuli aliyepitishwa na Mkutano Mkuu kuwa mgombea urais. Huu ndiyo ufufuaji nafsi wa timu ya Lowassa uliokuwa umekatishwa tamaa na uamuzi wa chama.

Kikwete alifanya makusudi kuhakikisha Lowassa anapoondoka CCM, watu wake wenye nguvu kwenye chama wanabaki na kufanya kazi ya kupigania ushindi wa mgombea wao wa urais dhidi ya mtu ambaye walimtaka.

Ni hapo ikashuhudiwa Nchimbi anasimama jukwaani kumnadi Rais Magufuli dhidi ya aliyekuwa mtu wake. Akina Sophia wakawa mstari wa mbele kuhamasisha wanawake CCM ili kukipa ushindi chama dhidi ya Lowassa, japo kwa shingo upande.

Kwa uamuzi huo, kile kishindo cha Lowassa kuhama CCM akiwa na msululu wa watu wazito kikadhibitiwa. Watu wake muhimu walifahamika na walidhibitiwa, kisha kutumika CCM dhidi yake.

Lowassa na Uhuru Kenyatta

Katika Uchaguzi Mkuu Kenya uliofanyika Agosti 8, mwaka huu, Lowassa alijipambanua wazi kumuunga mkono Rais Uhuru Kenyatta ambaye ametetea kiti chake cha urais dhidi ya mpinzani wake mkuu, Raila Odinga.

Lowassa hakuishia kumuunga mkono Uhuru kwa maneno, alisafiri mpaka Kenya na kuhamasisha jamii ya Wamasai kumchagua Uhuru, akitoa sababu kuwa Raila alimsaidia Rais Magufuli kushinda dhidi yake mwaka 2015.

Laiti Lowassa angejua athari za yeye kupanda jukwaani kumnadi Uhuru katika maisha yake ya kisiasa, asingefanya hayo. Pengine alichokifanya ni kumkomoa Raila au kumwonyesha Rais Magufuli kuwa anao marafiki wakubwa kisiasa. Amekosea.

Msisitizo kwake ni kuvuka bahari bila mfalme kujua. Rais Magufuli kwa sasa ndiye mkuu wa nchi. Ikiwa Lowassa ana nia ya kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu 2020, anaweza kujikuta analipa gharama kubwa kwa kitendo chake cha kupanda jukwaani Kenya kumfanyia kampeni Uhuru.

Bila shaka Lowassa anaweza kuhitaji msaada kutoka kwa Uhuru atakapokuwa anagombea urais. Hapo unapiga hesabu kuwa kutoka Agosti 2017 mpaka Oktoba 2020 ni zaidi ya miaka mitatu. Uhuru na Magufuli ni marais katika nchi jirani, zenye kuunda Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Rais Magufuli anaweza kwa kutumia nafasi yake kuhakikisha urafiki wa Uhuru na Lowassa unafutika. Magufuli anaweza kumuweka Uhuru karibu na kufanya naye mipango mikubwa. Uhuru anaondoka madarakani mwaka 2022, hivyo kwa mipango akawa anatamani zaidi Magufuli arejee madarakani ili waikamilishe pamoja.

Siyo kwa kutumia nguvu, ni ushawishi tu katika mbinu za medani. Lowassa atajikuta anaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu 2020, huku watu ambao aliwategemea hawapo naye.

Katika mbinu za kushambulia, ya sita inasema; ‘defeat the enemy by capturing their chief’. Yaani mshinde adui kwa kumteka chifu wao.

Mbinu hii humaanisha kuwa badala ya kumkabili adui moja kwa moja, unamtazama yule mkuu wake anayempa jeuri ya kifedha au mbinu, kisha unamteka. Magufuli anaweza kumteka Uhuru kwa mipango mikubwa na nafasi anayo. Ni Rais wa nchi.

Kati sura ya nne katika mbinu hizo, ya kwanza inasema; ‘remove the firewood from under the pot’. Yaani ondoa kuni chini ya chungu. Tafsiri; si unataka kutibua kilichomo kwenye chungu? Ondoa kuni chakula kisiive. Rais Magufuli akiona kuni inayompasha moto Lowassa ni Uhuru, ataiondoa tu chini ya chungu.

Chanzo: Mwananchi

Mke wa ROMA Afunguka Sababu za Ndugu wa Rapa Huyo Kutoonekana Wakati Alipotekwa

0
0
Kwenye #FNL, Mke wa Rapa ROMA Mkatoliki aliweka wazi jinsi ilivyo anza hadi kuja kuwa mpenzi wa rapa huyo na kisha ndoa. Aweka wazi sakata zima la kutekwa kwa ROMA lilivyo athiri familia yao na kisa cha ndugu zake ROMA kutokuonekana kwenye harakati za kumtafuta ROMA. 

VIDEO:

Chadema Yajipanga Kurudisha Majimbo Yaliyochukuliwa na CCM

0
0

Chadema Yajipanga Kurudisha Majimbo Yaliyochukuliwa na CCM
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Serengeti kimeanza mikakati ya kurejesha majimbo waliyopoteza katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2015.

Majimbo yaliyochukuliwa na CCM katika kanda hiyo yenye Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ni pamoja na jimbo la Musoma mjini (Mara), Maswa, Meatu Mashariki na Magharibi yote ya Mkoa wa Simiyu.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kanda hiyo, John Heche katika kikao cha viongozi wa chadema kanda hiyo kilichofanyika jijini Mwanza jana.

Heche ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Tarime vijijini amesema katika kikao hicho wamewaagiza viongozi waende kwenye majimbo kukaa vikao vya ndani kuanzia ngazi ya msingi hadi kanda kuweka misingi itakayokiwezesha kushinda kwa kishindo uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2019 na Uchaguzi mkuu 2020.

“Tumetoka na maazimio kadhaa, kwanza viongozi wanapotoka hapa kuanzia ngazi za mashina wakafanye vikao vya ndani lengo ni kukomboa majimbo tuliyopokonywa, hiyo ni kwa ajili ya maendeleo kwa mfano ukiangalia halmashauri zinazoongozwa na Chadema zinaongoza kwa miradi ya maendeleo,” amesema Heche

Pia, amewataka wanachama kutokata tamaa kuhusiana na matukio ya kidhalimu yanayondelea ya kuwakamata na kuwaweka ndani viongozi wa chama hicho na kuzuia mikutano ya hadhara ambayo imeruhusiwa kikatiba, badala yake waendelee kupambana mpaka ushindi utapatikana.

Amesema kuna vitisho vingi vinavyotolewa dhidi ya viongozi vikilenga kufifisha demokrasia na nafasi ya watu kushindana kisiasa ili watu waamini CCM kwa nguvu, lakini watapambana navyo bila kuchoka hadi hatua ya mwisho.

“Kuanzia wenyeviti, madiwani na wabunge, wanaokamatwa na kutishwa, tutawalinda na kuendelea kuwapa ushirikiano msaada wowote kisheria hata wanachama wanaotishiwa na kushindwa kufanya kazi zao,” amesema Heche

Mbunge Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga, Salome Makamba amesema kadri serikali inavyozidi kutumia nguvu kubwa kudhibiti kuiminya demokrasia, ndivyo inavyozidi kuwapa nafasi ya kufanya maamuzi magumu na picha mbaya “sio tu kwamba chadema huwa hatushindi, tunashinda ila hatutangazwi.”

Mbunge viti Maalumu Mkoa wa Mara, Catherine Ruge amesema rasilimali kubwa waliyonayo ni nguvu ya umma hivyo watwalinda viongozi wote wanaofanyiwa vitendo vya uzalilishaji kwa kutumia pia msaada wa sheria.




Mabango Ruksa..Waziri Mkuu Atoa Agizo Wananchi Wasizuiwe Kuonyesha Wanapotembelewa na Viongozi wa Nchi.

0
0
Mabango Ruksa..Waziri Mkuu Atoa Agizo Wananchi Wasizuiwe Kuonyesha Wanapotembelewa na Viongozi wa Nchi.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametaka mabango yanayoonyeshwa na wananchi kwa viongozi wa kitaifa wanapowatembelea yasiwe yanazuiwa kwa vile yanakuwa yanaelezea changamoto wanazokabiliana nazo.

Majaliwa alisema hayo baada ya kuona mabango yaliyoinuliwa na wananchi kwenye mkutano wake na wananchi mwishoni mwa juma lililopita mjini Sikonge mkoani Tabora huku wananchi hao wakitakiwa kuyashusha.

“Siku nyingine msirudie na kuanzia sasa waacheni wananchi waonyeshe mabango yao kwani ndiyo njia wanayotumia kuonyesha hisia zao kwa yale wanayokumbana nayo na kuwasababishia kero,” alisema Majaliwa.

Kutokana na hali hiyo, Waziri Mkuu aliwaagiza wasaidizi wake wayakusanye mabango yote wayaandike kisha wampelekee yaliyomo akiahidi kwamba atayafanyia kazi.

Alieleza kuwa malalamiko mengi kwenye mabango hayo yanahusu kero za vyama vya msingi vya ushirika na migogoro ya ardhi na kumtaka Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri kutenga siku kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi huku akiwa na wakuu wa idara mbalimbali.

Hiyo siyo mara ya kwanza kwa wananchi kuinua mabango kwa viongozi wa kitaifa. Julai 22 huko Kigoma wakati wa ziara ya Rais John Magufuli, wananchi waliinua mabango yao ili ayasome huku wakizuiwa na walinzi.

“Waacheni, waacheni tu jamani…jamani mtulie nitayasoma yote. Nimeyaona yote ndiyo maana nayapitia na wasaidizi wangu wanayapiga picha nyinyi msiwe na wasiwasi,” alisema Rais Magufuli wakati akihutubia katika Uwanja wa Lake Tanganyika huku wananchi wakikazana kumwonyesha mabango yao.

Hali kama hiyo ilijitokeza tena huko Tabora Julai 23, wakati Rais Magufuli akiwahutubia wananchi na kuwataka washushe mabango yao kwa sababu wananchi walikuwa wakipiga kelele, jambo lililokatisha hotuba yake.

“Naomba myashushe mabango yenu ili niendelee na hotuba yangu,” alisema Rais Magufuli lakini wananchi waliendelea kuyainua juu, jambo lililoonyesha kumkera, “Nimesema shusheni hayo mabango, la sivyo siyashughulikii. Ukitaka hata ukayatandike kwenye kitanda cha mke wako, siyasomi.”

Akitoa maoni yake kuhusu vitendo vya wananchi kuinua mabango yao kwa viongozi wa kitaifa, Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Benson Bana alisema hiyo inaonyesha kukua kwa demokrasia nchini.

Alisema wananchi wanatafuta namna ya kufikisha ujumbe kwa viongozi wa kitaifa juu ya mambo ambayo Serikali za mitaa au mkoa zimeshindwa kukabilaiana nazo au wameshindwa namna ya kuwafikia.

“Huko ndiko kupevuka kwenyewe na kukua kwa demokrasia. Viongozi kwenye maeneo hayo wameshindwa kutatua kero za wananchi ndiyo maana wananchi wanaona bora watumie fursa ya kueleza kero zao kupitia mabango,” alisema.

Mwanazuoni huyo alisisitiza kwamba kuna haja ya kuimarisha mifumo ya mawasiliano kati ya wananchi na viongozi wao wa Serikali za mitaa mpaka mkoa ili kumaliza changamoto zao bila kuzifikisha kwa viongozi wa kitaifa.

“Viongozi wa mikoa wawe na mawasiliano ya karibu na wananchi, wawe wanajibu meseji zao na kuwafikia katika maeneo yao. Hiyo itasaidia kupunguza mabango kwa viongozi, japo siyo jambo baya pia kuinua mabango,” alisema.

Katibu Mkuu wa Chama cha Kijamii (CCK), Renatus Muabhi alisema kitendo cha wananchi kuonyesha mabango kwa viongozi kinaonyesha udhaifu wa Serikali katika kukabiliana na changamoto za jamii husika.

Alisema mara nyingi askari wamekuwa wakiwazuia wananchi kupaza sauti zao ndiyo maana nao wameamua kuja na mtindo wa kutumia mabango kufikisha ujumbe kwa viongozi wao wa kitaifa. “Katiba yetu inaruhusu uhuru wa kutoa maoni bila kujali kwamba yatawafurahisha au kuwakera viongozi. Askari wasitumie nguvu kuwanyamazisha wananchi kwa sababu ni haki yao ya msingi,” alisema Muabhi.

Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha Ruaha (Rucu) alimpongeza Waziri Mkuu kwa kutambua umuhimu wa sauti ya umma na kusisitiza kwamba hiyo ni njia moja wapo ya kufikisha ujumbe kwa wananchi.

Alisema siyo jambo baya kwa wananchi kuinua mabango yao kwa viongozi kwa sababu wakati mwingine wanawakumbusha juu ya mambo ambayo wanatakiwa kuyafanyia kazi.


Jeshi la Uganda Lasema Halipo Tayari Kuingia Kenya Kudhibiti Usalama

0
0

Jeshi la Uganda Lasema Halipo Tayari Kuingia Kenya Kudhibiti Usalama
Jeshi la Uganda Jeshi la Uganda la UPDF limekanusha taarifa kuwa liko tayari kuingia nchini Kenya kusaidia kudhibiti hali ya usalama nchini humo baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa wiki iliyopita.

Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi, huku mpinzani wake mkuu Raila Odinga akiyapinga matokeo hayo.

Waziri wa mawasiliano nchini humo Frank Tumwebaze amesema jeshi la Uganda haliwezi kutumwa nje kushiriki operesheni ya kijeshi kisiri.

Msemaji wa jeshi la Uganda Richard Karemire, kupitia taarifa, amesema Kenya ni nchi huru na usalama wake umo chini ya serikali ya nchi hiyo.
Aidha, amesema Uganda haijapokea ombi kutoka kwa Kenya kutuma majeshi yake nchini humo au kuomba usaidizi.

Bodi ya MBOMIPA Yatumbuliwa ...Waziri Maghembe Ameitaka TAKUKURU Kuchunguza na Kuwachukulia Hatua

0
0




Bodi ya MBOMIPA Yatumbuliwa ...Waziri Maghembe Ameitaka TAKUKURU Kuchunguza na Kuwachukulia Hatua
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amevunja bodi ya udhamini ya jumuiya matumizi bora ya Maliasili kwa tarafa za Idodi na Pawaga (MBOMIPA) mkoani Iringa kwa kutosaidia wananchi na kufanya kazi kifisadi zaidi pamoja na kuvunja mikataba yote .

Prof Maghembe alifikia uamuzi huo wakati wa ziara yake katika jumuiya hiyo ya MBOMIPA na kufanya mkutano na wajumbe wa Bodi hiyo kabla ya kuvunjwa.

Prof. Maghembe alisema anashangazwa kuona MBOMIPA inajiendesha kwa hasara na kuomba omba kwa wahisani fedha za kujiendesha wakati kimsingi asasi hiyo ilipaswa kuwa msaada mkubwa kwa wanachama wao ambao ni vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo.

“Hii ni aibu kubwa kwa chombo hiki ambacho kinapaswa kuwa msaada kwa jamii chenyewe kimegeuka kuwa ombaomba, hivi inawezekana vipi MBOMIPA kuomba hadi msaada wa sare na mataili mawili kwa wahisani. Hili ni jambo la aibu kifupi halikubaliki hakuna cha mwekezaji hapa wala cha bodi tunaanza upya vitu vyote tunaanza sifuri,” alisema Prof. Maghembe.

“Tutajidanganya kabisa kusema kwamba tuendelee na bodi ya Mbomipa kama ilivyo tutajidanganya kabisa, kwahiyo kuanzia leo nimeivunja bodi ya MBONIPA rasmi leo hapa.”

Aidha Waziri Maghembe ameagiza taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kuanza uchunguzi wake na kuwachukulia hatua wote waliohusika na ufisadi katika bodi hiyo ya MBOMIPA.

Hiki Ndicho Chanzo Cha Waumini Kulikimbia Kanisa

0
0

Hiki Ndicho Chanzo Cha Waumini Kulikimbia  Kanisa
Waumini wa Kanisa la Freedom Pentecostal Bible Tanzania lililopo Kibamba kwa Mangi wamelikimbia kanisa lao baada ya kukumbwa na bomoabomoa na jana, ibada ya Jumapili ilihudhuriwa na waumini 10 tu.

Kanisa hilo ni miongoni mwa nyumba 30 za ibada zilizokumbwa na bomoabomoa hiyo ili kupisha upanuzi wa Barabara ya Morogoro kuanzia Kimara hadi Kiluvya ikiwa ni agizo la Serikali linalotekelezwa na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads).

Akizungumza jana kanisani kwake, mchungaji wa kanisa hilo, Braun Sikapizye alisema kabla ya kubomolewa lilikuwa na waumini 150 ambao alisema aliwatafuta kwa shida kwa miaka 16.

“Hofu kubwa niliyonayo ni kukimbiwa na washirika wakihofia umbali, maana baada ya kuvunja kanisa letu la awali na kuwekewa alama ya X na Tanroads, tumehama eneo tulipokuwa tukiabudia. Sasa huku tulikohamia waumini hawaji,” alisema.

Alisema awali kanisa lao lilikuwa karibu na barabara, lakini sasa wamehamia ndani zaidi, ambako waumini wanalazimika kutembea umbali wa kilomita tatu kulifikia kanisa jambo alilodai kuwa ni kikwazo kwa waumini wake kufika kanisani.

“Najiona kama napoteza waumini maana huku kuna makanisa mengi, najua wengi watakwenda kusali katika makanisa yaliyojirani, hii ni hasara kwangu na sijui nifanyeje ili kuwarejesha natamani nitafute gari niwapakize wote niwalete kanisani,” alisema.

Mzee wa kanisa hilo, Anthony Simundi alisema umepita mwezi tangu wabomoe kanisa lao na wamekuwa wakisalia nje kabla msamaria mwema kujitolea na kuwapa robo ya kiwanja chake ili wajenge kanisa.

“Hii ni Jumapili ya pili tangu tuanze kuabudia hapa, lakini waumini wamekuwa ni wachahe sana kiasi ambacho kinatishia amani ya kanisa kupoteza waumini,” alisema.

Mmoja wa waumini wa kanisa hilo, Neema Marko alisema idadi ya waumini imepungua, “Wiki iliyopita tumesali waumini 10 wakati kwa kawaida huwa tunasali waumini zaidi ya 50,” alisema.

Hali ya Kanisa

Mwanadishi wetu jana alifika katika kanisa hilo na kukuta limejengwa kwa miti na turubai na kufunikwa vitambaa, ukilitazama kwa mbali hutaamini kama ni kanisa unaweza ukafikiri ni kibanda cha wakimbizi.

Aliwakuta waumini saba yaani mchungaji, mzee wa kanisa, watoto wanne na muumini mmoja mtu mzima. Kanisa hilo halina sakafu na limejengwa katikati ya kiwanja ambacho kimezungukwa na vichaka vingi, kwa hali ya kawaida kunaonekana kama shambani.

Upepo ulivuma kwa kasi kiasi ambacho kilisababisha turubai kupiga kelele na kuyumba huku na kule na hata vitambaa na miti iliyojengewa, vilionekana kutaka kung’oka na kupeperushwa na upepo.

Mchungaji wa kanisa hilo alisema alianzisha kanisa lake mwaka 2002 akiwa na waumini watatu. Lilijengwa kwa matope na bati baada ya kupewa eneo na mzee wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika (KKKT) wa Kibamba aliyemtaja kwa jina moja la Kessy.

Mchungaji Sikapizye alisema mwaka 2007 walianza ujenzi wa kanisa la kudumu na kulikamilisha mwaka 2012 kwa kuchangisha waumini wake na wadau mbalimbali akiwamo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki ambaye alichangia Sh1 milioni.

Alidai kuwa hata katibu mkuu mstaafu wa CCM, Yusuph Makamba pia alichangia Sh4 milioni katika ujenzi wa kanisa hilo.

Mwaka 2007 wakati wakianzisha ujenzi wa kudumu, alisema wafanyakazi wa Tanroads walifika na kuweka jiwe la mpaka wa barabara ambalo lilionyesha kwamba kanisa hilo lipo ndani ya hifadhi ya barabara jambo ambalo liliwastua waumini na mchungaji huyo.

“Walikuja vijana wakaweka jiwe nilipowauliza wakasema, ‘Mzee sisi tumetumwa na Serikali bwana.’ Sikutaka kuwafuatilia zaidi kwani niliamini mita za barabara ambazo nilizitambua kwa wakati huo zilikuwa 60.”

“Tuliendelea na ujenzi hadi tulipokamilisha, ndipo wakaja kutuwekea alama ya X wakitaka tubomoe, hatukutaka kubishana nao, tulibomoa wenyewe tukawa tunasalia nje lakini baadaye akajitokeza msamaria mwema akatupatia hili eneo unaloliona hapa leo,” alisema.

“Tunaomba Rais wetu atusaidie mchango walau tuweze kujenga tena kanisa, najua kazi ni ngumu sana kuanza tena kuwachangisha waumini ukiangalia, wenyewe hawaonekani,” alisema.


Usain Bolt Astaafu Rasmi Asema Hatorudi Tena Kama Wengine Wanaostaafu

0
0



Usain Bolt Astaafu Rasmi Asema Hatorudi Tena Kama Wengine Wanaostaafu
Usain Bolt amesema alikuwa "anasema kwaheri kwa kila kitu" na alikuwa "karibu kulia" alipokuwa anafikisha kikomo maisha yake kama mwanariadha katika mashindano ya ubingwa wa dunia jijini London.

Bolt, 30, mshindi wa dhahabu mara nane katika Olimpiki, amestaafu kutoka kwenye riadha baada ya kung'aa sana na kujizolea umaarufu si haba.

"Inasikitisha kwamba inanilazimu kuondoka sasa," alisema raia huyo wa Jamaica, ambaye alikimbia kuzunguka uwanja kuwaaga wachezaji uwanja wa michezo wa London Jumapili usiku wa kufungwa kwa mashindano hayo.

"Nilikuwa nasema kwaheri kwa mashabiki na kwaheri kwa mashindano niliyokuwa nashiriki pia."
Alipoulizwa iwapo atarejea kushindana tena, alijibu: "Nimewaona watu wengi sana wakistaafu na kurudi tena halafu hali yao inakuwa mbaya zaidi au wanajiaibisha.
"Sitakuwa mmoja wa watu hao."

Bolt alishinda shaba mbio zake za mwisho za mita 100 kisha akaumia na kushindwa kumaliza mbio za kupokezana vijiti za 4x100m Jumamosi usiku.

Hii ina maana kwamba bingwa huyo wa dunia mara 19, ambaye Lord Coe alimfananisha na Muhammad Ali, aliondoka kwa njia isiyo ya kawaida - akisaidiwa kuondoka uwanjani na wenzake, akiwa hawezi kusimama vyema wima baada ya kuumia.

"Kwangu, sidhani mashindano haya yatabadilisha yote niliyoyafanya,2 aliongeza.
"Nakumbuka baada ya kushindwa mbio za 100m, kuna mtu alinijia na kuniambia, 'Usain, usiwe na wasiwasi, Muhammad Ali alishindwa pigano lake la mwisho, hivyo usisikitike sana kuhusu hilo'.

"Nimedhihirisha ustadi wangu, mwaka baada ya mwaka, katika kipindi changu chote nilichoshiriki mbio hizi. Nilikuwa nasema kwaheri kwa kila kitu. Nilikuwa karibu kulia. Nilikaribia sana, lakini machozi hayakutoka."

Mwenyekiti Maalum wa TEF, Atoa Onyo kwa Viongozi Wake

0
0


 Mwenyekiti Maalum wa TEF Atoa Onyo kwa Viongozi Wake
Kufuatia maoni ya baadhii ya watu mbalimbali na waandishi wa habari kutoridhika na maamuzi ya Jukwaa la Wahariri (TEF), viongozi wamepewa onyo la kutorudia makosa baada ya kukiri.

Katika mkutano mkuu uliofanyika Agosti 13, viongozi hao walikiri kuitisha mkutano na waandishi wa habari Agosti 9 bila ya kupata idhini.

Hatua hiyo ilisababisha kujengeka kwa taswira mbaya kiuwajibikaji, kanuni na utaratibu.

Katika taarifa ya Mwenyekiti Maalum wa TEF, Walace Mauggo imeeleza kuwa jukwaa kwa kauli moja limetoa onyo kwa viongozi wake kutorudia yale ambayo yamejitokeza.

“Baada ya kutafakari na kutathmini mwenendo wa mkutano huo, jukwaa lilobaini kuwepo kwa kasoro kubwa wakati wa kurejesha mahusiano wa kikazi na kiongozi ambaye habari zake zilizuiwa kuripotiwa kwa takribani miezi mitano,” imeeleza taarifa hiyo.

Pia wametakiwa kuhakikisha kunapotokea masuala makubwa kama hayo ambayo yashafanyiwa maamuzi na mkutano mkuu na taasisi nyingine za habari yanarudiswa maamuzi kwa wanachama kabla ya hatua za  mwisho.

Mauggo ameeleza kuwa TEF haitasita kuchukua hatua kwa kiongozi au mtu yoyote atakayeonekana kutishia usalama wa wanahabari, uhuru wa uhariri na vyombo vya habari.

Pemba Yaongoza Utafiti wa Wasichana Wanaobaki na BIKIRA Kwenye Umri wa Miaka 25, Dar Yashika Mkia

0
0
Utafiti wa Mabikira kati wa Vigor wa Umri Chini ya Miaka 25 Wasioolewa Bado ........

Utafiti kila mkoa juu ya watoto wa kike wanaojitunza. Utafiti huu umehusu wasichana wanaofika umri wa miaka 25 wakiwa bikira(Virginity percentage at 25 years old).

Kati ya watu mia moja wafuatao wametimiza umri wa 25 wengine hadi kuolewa, wakiwa bikira,

Njia ya utafiti
Kila mkoa wamekuwepo sample spaces 500, yaan wanawake 250, na wanaume 250(lengo la wanaume ni kuwauliza walipooa waliwakutaje, ilikuwa siri). Pia na kuwauliza wanawake, kwa njia ya kiungwana.

Takwimu ni kama hivyo, Pemba ndio yenye wasichana wengi wanaofika umri wa 25 wakiwa Na bikira Na Dar es Salaam ndio yenye wasichana wachache wanaofika umri wa miaka 25 wakiwa Na bikira.

1. Pemba 45%
2. Unguja 43%
3. Manyara 27%
4. Mara 26%
5. Tabora 22%
6. Dodoma 20%
7. Geita 19%
8. Shinyanga 16%
9. Kigoma 15.7%
10. Simiyu 15.5%
11. Morogoro 15
12. Kilimanjaro 14%
13. Rukwa 14%
14. Ruvuma 13.7%
15. Mbeya 13.5%
16. Iringa 13.2%
17. Kagera 13%
18. Katavi 12%
19. Mtwara. 11.6%
20. Pwani 11%
21. Njombe 9%
22. Tanga 8.5%
23. Arusha 8.3%
24.Lindi 8%
25. Singida 7%
26. Mwanza 5%
27. Dar es salaam 3%

Ijulikane kwamba huu utafiti utasaidia wazazi kuwaaasa watoto wao kutojihusisha Na mapenzi wakiwa wadogo, pili kuwaepusha na mazingira yanayoweza kuhatarisha usichana wao.

Pia watoto wa kike wajue kuwa si vyema kupenda chips mayai, lift na kupenda alama za juu darasani wakati hawasomi, hayo yanapelekea kuwaondolea usichana wao na kuolewa wakiwa thamani yao imeshuka.

Pili watoto wa kike wanapoteza sana usichana wao wakiwa mashuleni, vyuoni wengine mpaka makanisani.

Pengine watoto wanaruhusiwa kupanga nyumba wakiwa wadogo sana.

Kauli mbiu:
Tokomeza ukatili dhidi ya mtoto wa kike, linda Usichana wake, Mtunze Na mlinde mdogo wako wa kike Na jirani yako wa kike dhidi ya wahuni.

Mungu Ni Mwema
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images