Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Hongera Husna Abdul na Gea Habib Kwa Kumudu Kipindi cha Leo Tana Bila Uwepo wa Dina Marios

0
0
Nawapongeza sana Husna Abdul na Gea Habib kwa kunogesha kipindi cha Leo Tena. Kipindi kimechangamka sana. Husna amefit vizuri sana na hamna mapungufu. 

Kuna baadhi ya watu walidhani kuondoka kwa Dina Marios kipindi kitadorora sana kumbe wala wadada wanakamua vizuri sana. Big up sana Gea unatukosha sana na HEKA HEKA.

Diamond, Wema Sepetu Anaolewa Lini?

0
0
Dear Diamond
Najua uko busy sana ma Chanell za pesa pamoja na Show za Music rejea ujumbe hapo juu huyo ni mtoto wa watu Ana wazazi kama wewee

Sidhani wazazi wanafurahia kukuona nae kila mara embu fanya cha maana umweke mtoto ndani huyo ni Halali yako sitaki kusikia tena mmeachana itaniuma sana, Wema Sepetu ni Nyota Ingaayo kuwa pembeni yako kumechangia mafanikio yako na kuzidi kupendwa kwako na mashabiki....Fanya kweli Vidudu Mtu visije ingilia kati tena.....
Mimi Shabiki wako Mpendwa

Chidi Benzi Achefua Mashabiki kwa Kuvuta Bangi Jukwaani

0
0
Hapo akiwa anavuta Bangi bila ya uwoga... Pembeni ni Baunsa akimwomba akiustaarabu asivute bangi hiyo lakini chid akawa hajili na kuendelea kufanya yake 
Chini benz Jana Jumapili wakati anafanya show New maisha Club Dodoma alifanya kitendo ambacho baadhi ya mashabiki walimwona kweli jamaa sasa ameshaanza kuwa chizi.

wakati akiwa anafanya Show Katikati ya baada ya mzuka kumpanda Chid alichafua hali ya hewa baada ya kuzama mfukoni na kutoka Bonge la kipisi cha Bangi kilichoshiba na kukiwasha pale pale jukwaani bila hata Uwoga... Hapo ndipo Baunsa wa Maisha kabla akambadilikia kama Mbogo na kumpora hiyo bangi ili asiendelee kuivuta. Kitendo hicho cha kuvuta bangi Club kimeshushia heshima Msanii huyo ambaye ni kioo cha Jamii

Mafikilizo Wamkubali Diamond Kwenye Kuimba Ona Picha Mbali Mbali Wakiwa Studio Jana

0
0




Hatimae mpango wa Mafikizolo wa South Africa ambao ni mastaa wa hit single ya ‘khona’ waliochukua tuzo mbili kwenye MTV Africa music awards 2014 kufanya kolabo na Diamond umefanikiwa kwenye usiku wa June 9 2014.
Diamond pamoja na mameneja wake wawili ambao ni Salam na Bab Tale waliongozana mpaka kwenye studio za msanii mkongwe aitwae Oskido ili kurekodi kolabo hiyo ya Mafikizolo, kundi la Afrika kusini lililorudi kwenye chati kupitia mikono ya Oskido.

 Mafikizolo waliomba kurekodi wimbo na Diamond baada ya kushawishika kufanya nae kolabo hivyo wakaahidi kushughulikia gharama zote za kumuongezea Diamond muda wa kuendelea kukaa South Africa pamoja na kubadili ticket ya ndege ili wakamilishe kazi yao.

Imegundulika Wadada Wamjini Hutumia Hizi Tight Kufanya Makalio Yao Kuwa Makubwa

0
0

Angalia Vizuri Picha ya Chini Huyu Mdada anaedaiwa kuwa na makalio makubwa Kenya Amevaa Tight ya Aina Hiyo Nyeusi ..Inasemakana Pia Hata Kina Agness Masogange Huvaa Tight Hizo ili Kubonyeza Makalio na Kuonekana Yametoka na Kuwa makubwa zaidi 

Imebainika kuwa Dar Ndio Mkoa Ghali Kuliko Yote Tanzania

0
0
WAKATI Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart) awamu ya kwanza, unapanga kuongeza nauli za daladala kwa wakazi wa Dar es Salaam ili kukabiliana na tatizo sugu la foleni, taarifa ya matumizi ya kaya binafsi Tanzania Bara, zimeonesha kuwa Mkoa wa Dar es Salaam, ndio mahali ghali zaidi nchini.

Gazeti hili lilichapisha kwa mara ya kwanza habari kuwa Dart awamu ya kwanza ikianza, nauli ya basi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam kwenda na kurudi vituo vikubwa vikiwemo vya Kariakoo, Posta na Kimara, itapanda kutoka nauli ya chini ya Sh 400 ya sasa mpaka Sh 700 na 800 kwa ruti moja.

Taarifa hiyo ya kaya, ambayo Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii, Ephraim Kwesigabo, alisema jana kuwa ni ya awali tu na taarifa yenyewe itatolewa hivi karibuni, imeonesha kuwa mkoa huo ndio wenye gharama kubwa ya maisha.

“Mfano, bei za vyakula ni kubwa jijini Dar es Salaam, ukilinganisha na maeneo ya vijijini, hivyo gharama ya kulipia mlo wa mtu mmoja kwa siku ni ya juu kwa jiji la Dar es Salaam,” imeeleza taarifa hiyo. Hata hivyo, taarifa hiyo inayoangalia viashiria vya umasikini kwa kuchambua mahitaji muhimu ya mwanadamu, iliyo katika tovuti ya Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS), imefafanua pia kuwa mkoa huo ndio wenye idadi ndogo ya masikini nchini.

“Kaya za jijini Dar es Salaam zina kiwango kidogo cha umasikini wa mahitaji ya msingi, ukilinganisha na kaya zinazoishi katika miji mingine na maeneo ya vijijini. “Ukijumuisha watu wote wenye umaskini wa mahitaji ya msingi nchini, inakadiriwa asilimia mbili (1.5) wanaishi jijini Dar es Salaam, asilimia 14.4 wanaishi maeneo mengine ya mijini na asilimia 84.1 wanaishi vijijini,” alisema.

Kuhusu umiliki wa nyumba, taarifa hiyo imeeleza kuwa wakati asilimia 76 ya kaya nchini zinamiliki nyumba wanazoishi, jijini Dar es Salaam ni asilimia 37 tu ya kaya zinazomiliki nyumba wanazoishi na kaya zilizobakia, asilimia 63 ni wapangaji.

“Uwiano huu (wa nyumba za kuishi) ni mkubwa katika maeneo ya vijijini, ambako asilimia 89 ya kaya wanamiliki nyumba wanazoishi, huku umiliki wa nyumba katika maeneo mengine ya mijini ukiwa asilimia 58,” imeeleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ingawa ni ya awali, lakini iliyochambua vema umasikini kwa kuangalia mahitaji ya lazima na mahitaji muhimu ya Watanzania, imebaini hadhi za nyumba wanazoishi Watanzania kwa ujumla imekuwa ikiboreka.

“Asilimia 66 ya kaya mwaka 2011/12 zinaishi katika nyumba zenye paa za kisasa ukilinganisha na asilimia 55 ya kaya mwaka 2007.

“Vivyo hivyo, asilimia 73 ya kaya zinaishi kwenye nyumba zilizojengwa kwa kuta imara mwaka 2011/12 ukilinganisha na asilimia 33 za mwaka 2007,” imeeleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kuta imara zinajumuisha zilizojengwa kwa mawe, matofali ya saruji, au matofali ya kuchoma na paa za kisasa ni zile zilizojengwa kwa mabati. Katika mawasiliano, taarifa hiyo imeeleza kuwa umiliki wa simu za mkononi unatofautiana sana kwa maeneo.

“Wakati kiasi cha asilimia 78 ya kaya za maeneo mengine ya mjini na asilimia 88 ya kaya za Dar es Salaam, zinamiliki angalau simu moja ya mkononi, ni asilimia 45 tu ya kaya za maeneo ya vijijini zinazomiliki angalau simu moja ya mkononi,” ilieleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo, imeeleza kuwa mstari wa masikini, unaonesha masikini wa mahitaji ya msingi nchini na ambaye yupo katika mstari wa umasikini wa mahitaji yamsingi ni anayepata Sh 36,482 kwa mwezi, wakati maskini wa chakula ni anayepata Sh 26,085 kwa mwezi.

“Kwa kutumia takwimu hizi, matokeo yanaonesha kuwa zaidi ya robo (asilimia 28.2) ya watu wote waishio Tanzania Bara, wako chini ya mstari wa kiwango cha umaskini wa mahitaji ya msingi na asilimia 9.7 ya watu wote wapo chini ya mstari wa umaskini wa chakula,” imeeleza taarifa hiyo.

Hata hivyo, taarifa hiyo imeonesha kuwa kiwango cha umaskini wa mahitaji ya msingi kwa Tanzania Bara kimekuwa kikipungua kwani mwaka 2007, kilikuwa asilimia 33.6.

“Matokeo ya awali yanaonesha kupungua kwa kiwango cha umaskini kati ya 2007 na 2011/12. Upimaji wa mwenendo wa umaskini utaainishwa kwenye Ripoti Kuu ya Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi, 2011/12,” imeeleza taarifa hiyo.

Hesabu zilizopigwa na wataalamu wa takwimu walioandaa taarifa hiyo, zimebainisha kuwa kunahitajika Sh bilioni 103.3 kwa mwezi (sawa na zaidi ya Sh trilioni 1.2 kwa mwaka), ili kuondoa umaskini wa mahitaji ya msingi kwa watu waishio chini ya mstari wa umaskini Tanzania Bara.

Pia imeelezwa kuwa kama watu wote wangegawanywa katika makundi matano yanayolingana na ukubwa wa matumizi yao kuanzia wa chini hadi wa juu, matumizi ya watu wa kundi la juu (matajiri sana) ni mara nne (4) ya matumizi ya kundi la chini (maskini sana) kwa Tanzania Bara.

Katika elimu, taarifa hizo zimeonesha kuwa asilimia 20 ya Watanzania (Tanzania Bara) wenye umri wa miaka 15 au zaidi hawana elimu ambapo kwa mwaka 2007 ilikuwa ni asilimia 19.

Aidha, uandikishwaji katika shule za msingi kwa watoto wenye umri kati ya miaka 7 hadi 13, umeshuka na kufikia asilimia 78 kwa mwaka 2011/12 ikilinganishwa na asilimia 84 katika mwaka 2007. Hata hivyo kwa upande wa sekondari, uandikishaji umetajwa kuongezeka kutoka asilimia 15, mwaka 2007 mpaka 29, mwaka 2012.

Wabunge wa Tanzania EAC wapinga spika kung’olewa

0
0
WABUNGE wa Tanzania katika Bunge la jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA), wamesisitiza kutounga mkono hoja ya kumng’oa Spika wa bunge hilo, Margaret Zziwa, kwa kuwa haina maslahi na Tanzania na wana Afrika Mashariki kwa ujumla.

Hayo yameelezwa jana na wabunge watatu miongoni mwa wabunge hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa Wabunge wa EALA Tanzania, Adam Kimbisa ambapo alisema baada ya kuchunguza kwa umakini walibaini kuwa katika jaribio hilo la kumng’oa spika kuna ajenda ya siri.

Alisema kuwa hoja hiyo haina maslahi ya Tanzania na iko kinyume na malengo ya ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, pia wamebaini kuwa hoja yenyewe ni sehemu ya mchezo mchafu wa ajenda ya siri ya kujaribu kuweka mbele maslahi ya baadhi ya wanachama wachache ndani ya jumuiya hiyo badala ya kuzingatia maslahi mapana ya jumuiya hiyo.

“Tuhuma zilizotajwa dhidi ya Spika wa EALA kuhusu yeye kuonesha upendeleaji, ujeuri na mapungufu mengine ya uongozi zimegundulika kuwa hazina mashiko wala mantiki,” alisema Kimbisa.

Aidha, alisema kitendo kilichowashtua ni kumekuwa na majaribio ya baadhi ya wabunge wa EALA kutoka nje ya Tanzania na viongozi wa sekretarieti ya jumuiya hiyo kutaka kulazimisha sahihi za baadhi ya wabunge wa Tanzania kutumika kinyume na utaratibu kuunga mkono azimio hilo, jambo linalodhihirisha kuwepo kwa ajenda ya siri katika sakata hilo dhidi ya maslahi ya Tanzania na jumuiya kwa ujumla.

Alisema wabunge watatu wa EALA kutoka Tanzania ambao awali waliunga mkono hoja hiyo kwa sahihi zao, baadae waliamua kuipinga kwa kutoa sahihi zao kwa hiari yao wenyewe baada ya kuchunguza kwa umakini zaidi na kugundua mchezo huo, ambapo walimwandikia barua Katibu wa Bunge wa EALA kumweleza uamuzi wao.

“Hoja yenyewe kisheria ni batili kwa kuwa haikuwasilishwa bungeni ndani ya siku saba tangu ilipopelekwa kwa Katibu wa Bunge na pia imekosa sahihi za kuungwa mkono na wabunge wanne kutoka kila nchi mwanachama wa jumuiya kama kanuni zinavyotamka.

“Tunaomba uongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ngazi zote, ikiwemo sekretarieti ya jumuiya kuheshimu maamuzi ya wabunge wa EALA kutoka Tanzania,” alisema.

Alisema awali wabunge watano wa bunge hilo wa Tanzania kati ya tisa walionesha kuunga mkono hoja hiyo lakini baada ya kubaini kuwepo kwa mchezo mchafui na ajenda ya siri wabunge watatu waliondoa sahihi zao na kufanya idadi ya wabunge kutoka Tanzania kupinga hoja hiyo kufikia saba kati ya tisa.

Alisema wabunge hao wameshapoteza muda mwingi, fedha na rasilimali nyingine katika kujadili hoja hiyo isiyo na tija.

Alisema sasa wanahitaji kuweka jitihada zao katika kazi myuhimu ya kutetea maslahi ya wananchi wa Afrika Mashariki.

Naye Katibu wa Wabunge wa EALA wa Tanzania, Shy-Rose Bhanji alisema, awali alikuwa mstari wa mbele kuunga mkono hoja hiyo lakini alikuja kubaini kuwa kuna vikao vya siri vinaendelea juu ya sakata hilo, jambo lililofanya aamuue kupinga hoja hiyo.

“Ni kweli nilikuwa mstari wa mbele kutaka aondolewe lakini baada ya kutafakari na kuchunguza kwa makini chanzo halisi niligundua kuwa hoja hii haina maslahi kwa Watanzania na sisi ni wazalendo tuko kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania,” alusema.

Alisema kuwa Spika huyo ni binadamu hivyo hawezi akakosa mapungufu hivyo baadhi ya wabunge wanataka kutumia udhaifu huo kumngo’oa katika nafasi hiyo.

Mnigeria mwingine anaswa na ‘unga’ Dar

0
0

Raia wa Nigeria, Anthony Ifeanyichukwa Okafor (52), amekamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akidaiwa kumeza kete 100 za dawa za kulevya aina ya cocaine ambazo thamani yake bado haijafahamika.

Tukio hilo limetokea takribani siku 22 baada ya raia mwingine wa Nigeria, Olabisi Ibidun Cole (65) kuvunja rekodi ya umri wa watu wanaokamatwa wakiwa na dawa za kulevya katika uwanja huo.

Cole alikamatwa Jumatatu ya Mei 19, mwaka huu saa tisa alasiri akijiandaa kwenda Paris, Ufaransa kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia, akiwa amemeza kete 82 aina ya heroini zilizokuwa zimefungwa kwenye karatasi zinazofanana na ganda la sigara, ambazo si rahisi kuonekana katika mitambo.

Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa (pichani) alisema jana kuwa mtuhumiwa huyo alidai kuwa amefika nchini kumfuata rafiki yake wa kike aliyekutana naye Hong Kong, China na baadaye Douala, Cameroon.

Nzowa alisema mtuhumiwa huyo alisema rafiki yake huyo wa Tanzania ni mpenzi wake na wako pamoja katika kazi hiyo.

Kamanda wa Polisi wa Uwanja wa Ndege, Hamisi Selemani alisema wauzaji wa dawa hizo siku hizi wamegundua mtindo mpya wa kuwatumia watu wazima ili wasigundulike kutokana na mwonekano wao.

“Muda si mrefu ametoa kete mbili na kufikisha 100 na anavyoonekana bado ataendelea kutoa nyingine, tunaye hapa tunaendelea kumhoji,” alisema Selemani na kuongeza kuwa alikamatwa Jumamosi iliyopita saa saba usiku akitokea Douala kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.

Alisema alikamatwa baada ya maofisa wa uwanja huo kufuatilia mwenendo wa taarifa zake za safari na kuangalia nchi alizokuwa akisafiri.

“Tunapomkagua mtu tunaangalia taarifa zake jinsi alivyosafiri, tunaangalia nchi zenye matukio ya kuuza na kuchukua dawa za kulevya,” alisema na kuongeza:

“Watu wanaofanya biashara hii ni wajanja sana na hujiamini kama huyu Mnigeria, alituambia tufanye kazi yetu yeye yupo fresh, hana kitu na tulipomfanyia uchunguzi wa kina tukabaini amemeza dawa za kulevya.

“Huyu alitumia ujanja wa kwenda nchini Cameroon kwa kuwa nchi ile haitengenezi dawa hizo hivyo alipitia huko aweze kuja hapa nchini asigundulike,” alisema.

Mbasha:Gwajima Niachie Mke Wangu Flora

0
0
Na Makongoro Going’
MUME wa mwimba Injili Bongo, Flora Mbasha anayedaiwa kumbaka binti wa miaka 17 (jina lipo), Emmanuel Mbasha ameibuka mzimamzima na kumtaka Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo la jijini Dar, Josephat  Gwajima amuachie mke wake, yaani Flora.

Akizungumza kwa machungu kwa njia ya simu kutokea alikojihifadhi huku akionesha waziwazi hasira juu ya hisia zake, Mbasha alisema:

“Nimesika mke wangu baada ya matatizo yetu amehamia nyumbani kwa Gwajima. Nataka mumwambie Gwajima aniachie mke wangu, mbona ananifanyia hivyo?”

KINACHOMSHANGAZA
Mbasha ambaye mpaka sasa hajulikani alipo, aliendelea kudai kwamba kinachomshangaza zaidi ni kwamba, Flora amekiuka utamaduni wa Kiafrika, kwamba kama mke na mume wamegombana kiasi cha kushindwa kuishi nyumba moja, mke anakwenda kwao lakini hilo la Flora kukimbilia kwa Gwajima ndilo la ajabu zaidi kwake.

“Kama kweli Flora ameshindwa kuishi nyumbani kwetu (Tabata-Kimanga) kwa nini asiende Morogoro kwa mama yake. Au kwa nini asirudi Mwanza kwenye chimbuko la familia ya mzee Moses Kulola?
“Yeye badala yake amechukuliwa na Gwajima na kwenda kuishi naye nyumbani kwake. Mimi sijapenda, sijapenda na sitapenda kamwe,” alisema Mbasha.
ATUHUMU MTOTO KULIPIWA ADA YA SHULE 
Akiendelea kutoa la moyoni, Mbasha alituhumu kuwa mke wake kwa sasa ana pesa nyingi licha ya kwamba wakati matatizo ya yeye kutuhumiwa kubaka yanatokea na kuingia mitini alimwacha hana kitu.
Anasema: “Wakati matatizo yanatokea Flora nilimwacha mweupe. Mtoto wetu (Elizabeth) alitakiwa kupelekwa shule, kwa hiyo ina maana hakwenda.

“Sasa nasikia mtoto amelipiwa ada na anakwenda shule. Nani kamlipia ada mwanangu kama si Gwajima? Mimi naumia sana, kwa nini iwe hivyo? Kama Gwajima ameamua mke wangu kukaa kwake kwa ajili ya kumsaidia kipindi hiki cha matatizio ajue mimi sijapenda.
“Yeye Gwajima ana mke wake, najua hawezi kusema kitu kwa sababu Gwajima ni kila kitu lakini sijapenda.”

GWAJIMA SASA
Jumamosi iliyopita, Uwazi lilimtafuta Mchungaji Gwajima kwa njia ya simu ambapo alisema hataweza kuzungumza kwa sababu yupo Mikumi akielekea Dar.
Uwazi: “Sawa, lakini inadaiwa Flora yupo kwako. Hata jijini Dar habari zimeenea kwamba yupo kwako. Mbasha mwenyewe pia amesema mke wake yupo kwako. Unasemaje kuhusu hili?”
Gwajima: “Flora hakai kwangu na wala sijui alipo. Hao wanaosema anaishi kwangu si wa kweli. Hata mkija kwangu hamtamkuta Flora.”

UWAZI LAMSAKA FLORA
Uwazi lilianza kuingia mitaani kumsaka mwimbaji huyo kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya kiintelejensia.
Ilikuwa kazi kubwa sana iliyoanza saa mbili na nusu asubuhi ya Jumapili na ilipofika saa tano, Flora alipatikana kwenye hoteli moja (jina tunalo) iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.
Alikuwa akijiandaa kwenda kanisani ikabidi hekima zitumike ili aweze kutoa dakika ishirini tu za mahojiano ambapo alikubali.

KUMBE ULIANZA UGOMVI
Akizungumzia kuhusu ugomvi katika ndoa na tuhuma ambazo mumewe anadai kuhusika nazo, Flora alikuwa na haya ya kusema:

“Mimi sina ugomvi na mume wangu Mbasha ninampenda sana ila ninamshangaa kutoa  taarifa yetu ya ndani  katika vyombo vya habari.

“Nimeshtushwa sana na kitendo hicho  kwani kama ingekuwa  ni ugomvi baina yake  na mimi tungekaa chini  na kuyamaliza kama wanandoa. Siamini kama njia hii anayoitumia italeta suluhu, bali itaendeleza matatizo.”

KUHUSU MADAI YA UBAKAJI 
“Nakumbuka ilikuwa asubuhi ya Ijumaa ya wiki mbili zilizopita, Ima (Emmanuel) aliniambia nijiandae kwenda ofisini kwetu kuangalia shughuli, alinipitisha ofisini kisha yeye akarudi nyumbani.
“Baadaye alinipitia ofisini kurudi nyumbani. Nilimkuta  binti mlalamikaji akiwa  hana raha na  hali siyo nzuri, nilimuuliza tatizo ni nini hakuniambia.

“Ilipofika Jumapili nilimwambia mume wangu twende kanisani  lakini alikataa, nilimuomba ufunguo wa gari ili mimi niende  na familia, akagoma. Ndipo ugomvi  ulipoanzia, nilimuuliza umekuwaje? Mbona uko hivi? Au  umechanganyikiwa? Alinijibu anataka aondoke  aniache na familia.
“Baadaye akabadilika, akasema hapana haiwezekani yeye akaondoka, bali mimi ndiyo niondoke.”

ATISHIWA KUCHINJWA
“Nilimuomba tuwaite  watu wazima  ili waje  kutupatanisha, akaniambia nikiondoka kwenda kutafuta watu atanichinja.

“Niliamua kuachana naye, nilimpigia simu rafiki yangu mmoja aje anipitie  na gari  kwenda kanisani, lakini huyo rafiki yangu alipita na kuniambia kuwa  amepata  dharura  hivyo asingenipeleka kanisani.
“Nikamrudia mume wangu na kumwambia mbona kama umerogwa? Akasema ndiyo amerogwa, nikamwambia twende kanisani ukaombewe, akakataa. Matokeo yake akanikaba shingoni mpaka nikashindwa kuongea.

Nikamwambia unaniua ndipo akaniachia.
“Nilichukua gari la watu na familia yangu tukaenda kanisani. Kufika kanisani nilimweleza Mchungaji Gwajima tatizo lililonipata, akaniambia nirudi tu nyumbani kama hali itakuwa mbaya ataangalia cha kufanya.

“Baada ya ibada nilimwambia mdogo wangu arudi nyumbani na watoto, mimi nikaenda kukaa mahali nikiwaza cha kufanya.”

BINTI AMPIGIA SIMU
“Ilipofika kesho yake (Jumatatu) nikapigiwa simu na yule binti akidai anaondoka nyumbani kwa sababu shemeji yake amemdhalilisha sana. Nilimwambia asiondoke kuna mtu atakwenda kumchukua mchana kumleta nilipokuwa.

“Alipoletwa nilishangaa kumkuta katika hali ambayo hawezi kutembea sawasawa. Nikamuuliza vipi? Ndipo akanielezea jinsi mume wangu alivyomfanyia.”

BINTI AENDA HOSPITALI
Flora aliendelea kusema kuwa, binti mwenyewe aliamua kwamba anakwenda hospitali kucheki afya. Akasindikizwa na mdogo wake Flora. Kule vipimo vilionesha kweli aliingiliwa kimwili. Madaktari walimshauri aende polisi.

“Ndipo akaenda polisi na kutoa maelezo na kuandikiwa faili ambapo mume wangu akawa anatafutwa.
“Mume wangu amekuwa akisambaza habari kwamba nina mwanaume sijui nani! Hicho kitu hakipo. Hata mwaka jana nilikwenda Uingereza lakini tulikuwa wote.”

KUHUSU KUWA NA PESA, MTOTO KULIPIWA ADA
Kuhusu madai kwamba mtoto amelipiwa ada, yeye hana pesa, Flora alisema:
“Pale kanisani waumini walipojua nina matatizo na mume wangu na sipo nyumbani, walipitisha harambee ambapo niliweza kupata shilingi milioni tisa ndiyo maana  mtoto akaenda shule na mimi nikabaki na za matumizi maana kila kitu kuhusu akaunti ya benki anakijua mume wangu.”

MBASHA AOMBA KESI IFUTWE
“Mume wangu aliniomba msamaha baada ya haya mambo kutokea, nimemsamehe. Aliniomba nifute kesi polisi, nikamwambia si mimi niliyepeleka kesi polisi. Mimi siwezi kumsaliti yeye, kwanza nampenda sana Mungu kisha yeye.”

AKUTWA AMEVUA PETE YA NDOA
Uwazi lilimkuta Flora akiwa hana ile pete ya ndoa iliyozoeleka kuwepo kwenye kidole chake. Alipoulizwa alisema hakuna uhusiano wa pete kutokuwepo kidoleni na ugomvi.

FAMILIA YACHAFUKA
Mwimbaji huyo alikwenda mbele zaidi kwa kusema kwamba ugomvi kati yake na mume wake umesababisha familia kuchafuka maana umekuwa gumzo katika kila kona ya mtaa.
GPL


House Girl Aliyeng'atwa Mwili Mzima na Bosi Wake Atoa Siri Nzito

0
0
Stori: Haruni Sanchawa
NYUMAya pazia! Yule msichana Yusta Lucas (20) mwenyeji wa Mkoa wa Tabora ambaye alifika jijini Dar kufanya kazi ya u-hausigeli na kufanyiwa ukatili wa kutisha na bosi wake kisha habari zake kuandikwa, ametoa siri nzito, Uwazi limemegewa.

Akizungumza kwa uchungu na gazeti hili akiwa wodini kwenye Hospitali ya Mkoa wa Kitabibu Kinondoni, Mwananyamala jijini Dar, Yusta ambaye amefanya kazi kwa tajiri yake huyo kwa miaka mitatu alisema:
“Kwanza nataka watu wajue kuwa mwajiri wangu ni binamu yangu, alinileta hapa Dar kwa ajili  ya kumsaidia kazi za ndani pamoja na kumlelea mwanaye.

“Kipigo hasa kilianza mwanzoni mwa mwaka huu ikiwa ni pamoja na kuning’ata kwa meno mwili mzima, ndiyo maana mwili wangu wote unaonekana una mabakamabaka.
“Mateso yangu majirani walikuwa wakiyajua kutokana na kilio changu lakini walikuwa wanashindwa kunisaidia kwa sababu ya ushirikiano mdogo.

“Kwanza nashangaa sana kwa adhabu yake ya kuning’ata meno mpaka damu zinabaki kwake. Je, kama nina virusi vya Ukimwi si na yeye anavipata?
“Sijajua alikuwa anapata wapi ujasiri wa kuning’ata meno. Kwa kweli nimeteseka kwa muda mrefu sana. Mungu ndiye anajua, lakini nawashukuru sana majirani walioliona hilo na kuamua kuchukua hatua.”

KUHUSU MAISHA YA TAJIRI WAKE
Aidha, Yusta alianika mienendo mitano ya bosi wake huyo na kusema imekuwa ikimshangaza sana.

MWENENDO WA KWANZA
“Mimi katika kuishi kwangu pale sijawahi kumwona jirani yeyote amekuja ndani kusalimia wala yeye kwenda kwa jirani kufanya hivyo jambo ambalo si la kawaida.”

MWENENDO WA PILI
“Yeye (bosi wake) hana mume. Lakini tangu nimeishi pale kwa miaka mitatu sijawahi kumwona mwanaume ameingia ndani ya nyumba achilia mbali wanawake wenzake, hata mgeni. Kifupi yeye ni yeye kwa pale nyumbani kama ana marafiki labda wanakutana mbali.”

MWENENDO WA TATU
“Muda wake wa kurudi nyumbani siku zote ni usiku mnene, amewahi sana ni saa mbili usiku. Kwa hiyo, muda mwingi mimi ndiyo huwa nyumbani.”

MWENENDO WA NNE
“Anajiweza, sijui kwa nini aliamua kunifanyia hivi. Maana mtu ana gari, anaendesha mwenyewe na anasema ana hela, ndiyo maana namshangaa kuniadhibu kwa kuning’ata kwa meno.”

MWENENDO WA TANO
“Sikumbuki lini nimewahi kumwona akicheka. Muda mwingi anaonekana amekasirika tu kiasi kwamba nimekuwa nikimwogopa siku zote.”

OMBI KWA SERIKALI
Yusta alisema kufuatia matatizo makubwa yaliyompata ameiomba  serikali imsaidie  aweze  kurudi nyumbani kwao Tabora.

SHUKURANI KWA MAJIRANI
Yusta alitoa shukurani kwa majirani  waliojitokeza kuokoa maisha yake ambapo alisema kama wasingekuwa wao hajui ingekuwaje.

MANENO YA MUUGUZI
Kwa upande wa hospitali hiyo, muuguzi  kiongozi  wa zamu siku hiyo, Mahija Swalehe alikemea tabia za waajiri wa wafanyakazi wa ndani kuwatesa na kuiomba serikali kuliangalia suala hilo kwa jicho la tatu ili kukomesha vitendo hivyo.

TUJIKUMBUSHE
Yusta alikumbwa na masaibu hayo kwa muda mrefu hadi hivi karibuni majirani wakiwa na polisi walipovamia nyumba hiyo na kumkamata bosi wake kisha kumpeleka Kituo cha Polisi cha Oysteraby, Dar ambako anashikiliwa na yeye kupelekwa Hospitali ya Mwananyamala kwa matibu baada ya kukutwa na majeraha.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Camillius Wambura amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa ametiwa mbaroni.
GPL

Boko Haram Wateka Wanawake 20 Kuongezea Idadi

0
0
Wakati bado kuna vilio na mipango ya kuwaokoa wasichana 200 wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haram la Nigeria, watu wanaosadikika kuwa ni wanajeshi wa kundi hilo wamevamia na kuteka wanawake wengine 20 kutoka kwenye eneo lile lile walilowateka wasichana awali.

Shuhuda wa tukio hilo ameiambia BBC kuwa watu hao waliokuwa na bunduki waliwalazimisha wanawake hao kupanda gari walilokuja nalo huku wakiwatishia kwa kuwanyooshea midomo ya bunduki.

Jeshi la Nigeria bado hatoa tamko lolote kuhusu tukio hilo lililotokea katika maeneo ya wafugaji wa kabila la Fulani.

Jeshi hilo la Nigeria limekuwa likikosolewa kwa kushindwa kuchukua hatua na kudhibiti maeneo ya kaskazini Mashariki.

AIBU:Jay Z Aonekana Mtaani Akiwa Amevaa Nguo ya Kike

0
0
Uchaguzi wa mavazi unahitaji umakini wa hali ya juu la sivyo wanaojua mavazi wanaweza kukuumbua wakati unadunda kama tenesi mtaani.

Mr Hov, Jay Z ameripotiwa kuwa alikutwa mitaa ya jiji la New York akiwa amevaa jezi (Jersey) ya mpira wa miguu ya Rodarte ambayo ilitengenezwa maalu kwa wanawake yenye namba 5 kubwa kwa mbele.

Kutokana na hatua hiyo, watu wameendelea kujiuliza kama Jay Z alikuwa amevaa jezi ya Beyonce mke wake kuonesha upendo, au alinunua nguo hiyo makusudi.

Jay Z na mke wake Beyonce huvaa mavazi ya Rodarte, na Jumapili iliyopita wawili hao waliwasili New York na Beyonce alikuwa amevaa sweta la Rodarte likiwa limeandiwa Radarte.

Inaelezwa kuwa hata miaka ya nyuma kwenye video za nyimbo za Jay Z alikuwa akitupia jezi za kike ila watu walikuwa hawafuatilii kwa umakini!

Kabla hujabisha au kulibali, pitiapitia video za nyimbo za Jay Z za miaka ya 1990 na mwanzoni mwa miaka ya 2000.

Serengeti Boy wa Shilole Nuhu Mziwanda Amechukua Uamuzi Mgumu Juu ya Penzi Lake Kwa Shilole

0
0

"Kwasababu Nampenda Mpenzi Wangu Shilole Nimeamua Kujichora Tattoo ya Jina Lake 'Shishibaby' Kwenye Mkono wangu, wakati nachorwa iliuma sana kuliko tattoo yangu ya Kwanza na hii Tatoo Haita Futika Milele na Milele" Nuhu Mziwanda aliandika maneno hayo 

Naye Shilole Alipost Picha hiyo ya Tatto na Kusema "Thanks My Love for This Umeonyesha Love ya Ukweli"

Je wewe Unaona ni Sahihi Kujichora Tattoo ya Jina la Mpenzi wako ambae hata bado hamjui kama mtaoana ? Na je Mkiachana itakuwaje?

How Mining Firms are Milking Tanzania Dry

0
0
As Tanzanians wait for the 2014/15 national budget with bated breath, a new report shows that the government loses about $248 million (Sh415 billion) annually in tax revenue through misinvoicing by mining companies alone.

Falling revenue in the current financial year has led to speculation that the government will raise taxes and impose new ones on consumers in its budget proposals to be tabled in Parliament on Thursday.

Although wide ranging in scope, the Global Financial Integrity (GFI) report fingers Tanzania’s mining sector as a major culprit in over-invoicing, which accounts for a big chunk of the estimated $1.87 billion the country loses each year through the malpractice.

Experts argue that if the government clamps down on tax fraud, the money saved could be enough to finance a significant portion of the Sh18 trillion-plus budget plan.

MPs have been debating ministerial budgets in Dodoma in the past fortnight during which they put the government to task over budget plans that are not implemented.

A number of lawmakers have warned that they will not approve the budget proposals to be tabled by Finance minister Saada Mkuya without assurances on how the government plans to raise the money.

Details of the GFI report focusing on the mining sector have been released by the US-based International Centre for Investigative Journalism (ICIJ).

Reports on how mining companies have been ripping the country off over the years are not new, but the fresh details should add credence to claims that not enough is being done to deal with tax cheats.

This is happening despite Tanzania being a signatory to the Extractive Industries Transparency Initiative (Teiti), which aims to increase transparency in the mining tax regime. Teiti is set to release its fourth report later this month. Teiti coordinator Athuman Kwariko was last week quoted as saying the initiative had played a pivotal role in the doubling of revenue from the extractive industry to Sh800 billion.

But since the GFI report was released, neither the Tanzania Chamber of Minerals nor individual mining companies have commented on the findings.

Illicit flows and secretive tax practices are robbing many nations, particularly in Africa, of riches that could go towards development and stability, according to the report.

GFI says developing countries lose about $424 billion each year when importers and exporters mislead governments about the value of goods and services.

This dishonesty – known as trade misinvoicing – accounts for nearly 80 per cent of all the money that developing countries lose each year through illegal means. Trade misinvoicing occurs when companies charge too much (over-invoicing) or too little (under-invoicing) for imports or exports. Depending on the laws in place, this allows companies to pay less in taxes or receive more generous government assistance.

“Mining companies could be over-inflating their import costs to shift capital out of Tanzania illicitly with the added kick-back of lower taxable income due to artificially inflated inputs,” the GFI report says.

The Citizen could not independently verify the authenticity of the data, but judging from the figure mentioned, the amount lost during the past 11 years amounts to over $2.48 billion.

The report estimates that the government misses out on about $248 million per year in tax revenue from mining companies as a result – a substantial amount for a country in need of funds for development.

Weak governance and companies seeking to reduce their taxes are not the only players in this game. GFI found that most of Tanzania’s misinvoiced trade is with Switzerland and Singapore – two reputed tax havens.

Only six per cent of Tanzania’s imports come from Switzerland and Singapore, yet the countries accounted for 67 per cent of Tanzania’s total import misinvoicing over ten years.

Ney wa Mitego Ajinunulia Gari Mwenyewe Kama Zawadi ya Siku ya Kuzaliwa Kwake

0
0
Jana ilikuwa ni Siku ya Kuzaliwa kwa Mwanamuziki Ney wa Mitego na aliamua kufanya sherehe kwa mara ya kwanza kusherehekea siku hiyo kwa vile huu ndio mwaka wake wa kwanza kuwa na mafanikio katika muziki , Ney aliandika haya katika profile yake

"Nimejinunulia Gari Aina ya Murano Kama zaiwadi ya Birthday yangu , Limenigharimu Shilingi Mil 36 za Kitanzania , ni la Mwaka 2007 so bado ni Jipya Kabisa, One Love kwa mashabiki wangu

Makosa Makubwa Wanayoyafanya Wanawake linapokuja Swala la Kupenda..!

0
0
Je wewe ni mtu wa kupenda ghafla, yaani mwanaume anapokutamkia kwamba anakupenda huwa unamuamini kwa kiasi gani, unakuwa ni mwepesi wa kumuamini na kujitoa kwa ajili yake au unakuwa na kujivuta vuta ili kujiridhisha kabla ya kuingia katika uhusiano? Hebu fikiri kabla ya kuamua, jipe muda kwani hakuna jambo lililo jema kama subira linapokuja swala la kupenda. Subira itakuepusha kupoteza muda wako katika mahusiano ambayo hayana mashiko wakati dhamira yako ilikuwa ni kumpata mwenzi mwenye sifa muafaka, pale utakapoingia mahali ambapo sipo. Kwa kawaida kutoka katika uhusiano huo kuna gharama kubwa na kunaweza kukusababishia matatizo mengi yakiwemo ya kiafya.

Hapa chini nitajaribu kueleza makosa kadhaa ambayo wanayafanya wanawake linapokuja swal la kupenda:

1.Kumbadili mtu awe vile utakavyo:
Usije ukajidanganya kwamba unaweza kumbadilisha mtu mzima na akili zake. Kama umepata mwanaume ambaye kwa mtazamo wako unamuona ana sifa muafaka lakini anatabia ambazo huzipendi kwa mfano ulevi au kuvuta sigara vitu ambavyo vinakukera sana, usije ukajidanganya kwamba unaweza kumbadilisha na akaacha tabia hizo, anaweza kuacha kwa muda tu ili kukuvuta ukiingia kingi imekula kwako, tabia hiyo inaweza kujirudia. Ni vyema kama kuna tabia ambazo umezipenda lakini zipo ambazo huzipendi kutoka kwa mwenzi wako, basi weka uzingativu kwenye zile tabia unazozipendfa na zile usizozipenda achana nazo, kama ataamua mwenyewe kuziacha sawa lakini kama akiamua kuendelea nazo, basi zisikuumize kwani unaweza kujikuta ndoa yako inakuwa na migogoro isiyokwisha kwa sababu ya kuonekana una ghubu kwa kujaribu kumbadilisha mwenzi wako na mwisho wake upendo unakuwa haupo na kisirani katika ndoa kinaongezeka. Kitendo cha kuonekana kuwa na ghubu kinaweza kumuingiza mwanaume katika tabia nyingine mbaya ya kutotumia muda mwingi kukaa nyumbani kwake na kutafuta kampani nyingine, kama akipata kampani ambayo siyo nzuri anaweza kuangikia katika nyumba ndogo ambayo itamkubali bila masharti.


2.Njoo tuishi:
Unaweza kukutana na mwanaume ambaye ana nyumba nzuri au amepanga nyumba nzuri na ana kila kitu ndani pamoja na usafiri, anakuwa mwepesi kukupa funguo za nyumba yake ili uhamie muishi pamoja, lakini haweki msimamo wake wazi kwamba ana matarajio gani na wewe. Kabla ya kukubali kupokea funguo na kuhamia kwake jiulize kama unampenda kwa dhati au umekubali kwa sababu ya nyumba yake nzuri. Kumbuka nyumba na vitu vingine vinavyotizamika kwa macho (material things) havina mashiko linapokuja swala la kupenda. Kupenda kunahusisha vitu vya ndani kama vile kupenda kwa dhati bila masharti wala kuangalia sifa za nje, kuwa na amani moyoni kila umwonapo mpenzi wako, kuwa na furaha wakati wote mnapokuwa pamoja, kupatwa na msisimko wa mapenzi kila umwonapo au usikiapo sauti yake nk. Lakini kama utamkubali mwanaume kirahisi kwa sababu tu kakukabidhi funguo za nyumba yake wakati huna mapenzi ya dhati ni janga kubwa kwa sababu hivi vitu vya nje vinaweza kutoweka kirahisi, sasa je ikitokea si mapenzi nayo yatakuwa yamekwisha? Kumbuka kwamba kile kilichokupeleka kwake hakipo.

3.Amekuwa ni liwazo kwako
Liwazo linaweza kuwa sehemu ya mapenzi lakini hivi vitu haviendi pamoja. Unaweza kuwa na mwanaume ambaye mnapendana na mnakamilishana hii ni tofauti na mwanaume unayempenda na ukamgeuza kuwa liwazo pale unapohisi upweke. Jiulize, je ni kwamba mnapendana na mnafurahi kuwa pamoja au unampenda kiasi kwamba huwezi kuishi bila uwepo wake. Hapa nazungumzia utegemezi wa kihisia, yaani unakuwa king’ang’anizi mpaka mwanaume anakuona kero, badala ya kufurahia mahusiano yenu mwanaume anakuona kuwa ni kero kutokana na kuwa tegemezi wa kihisia. Hakuna mwanaume anayependa mahusiano ya aina hii anachoka haraka kihisia na atajitahidi kwa kila namna kukukwepa na ikiwezekana kukutosa na kutafuta ustaarabu mwingine jambo ambalo litakuumiza sana.

4.Mwanaume king’ang’anizi:
Mwanaume kutongoza na kukataliwa siyo jambo linalowashughulisha sana kwao kujaribu na kukosa ni sehemu ya maisha, lakini lipo suala la kung’ang’ania, yaani mwanaume kumfuatilia mwanamke kwa hali na mali na kujitoa ili kuhakikisha anampata mwanamke anayemtaka. Huu ni mtego wa mapenzi, kwani kwa mwanaume kung’ang’ania na kufuatilia mwanamke kwa muda mrefu bila kuchoka hata asumbuliwe kiasi gani haimaanishi kwamba mwanaume huyo amempenda mwanamke huyo. Wakati mwingine ni matamanio tu ndiyo yamemsukuma kutokana na sifa za nje alizo nazo mwanamke huyo. Kupenda kwa mwanaume kunahusisha zaidi sifa za nje kuliko za ndani na ndiyo maana mapenzi ya aina hiyo hayadumu yanaanza kama kichaa na kuyeyuka ghafla kama kipande cha barafu juani. Pale mwanamke anapokutana na mwanaume king’ang’anizi na asiyekubali jibu la hapana, kabla ya kukubali ajiulize kama anakubali kuwa na mahusiano na mwanaume huyo kwa sababu amempenda kwa dhati au kwa sababu ya uking’anga’nizi wake? Kumbuka kwamba wapo baadhi ya wanawake wanaweza kumkubali mwanaume tu kwa sababu amemfuatilia sana, anajiwa na huruma anakubali kuwa na mausiano naye siyo kwa sababu amempenda bali kwa sababu ya huruma. Ni vyema ukajiuliza kama na yeye atathamini huruma yako au akishapata alichokitaka atakugeuka na kuwa mwiba mchungu kwako? Tafakari na chukua hatua.

5.Baada ya kupanda mbegu mmea ukachipua
Umekuwa na uhusiano na mwanaume huyu kwa muda mrefu, lakini hakuwahi kukutamkia kwamba ana matarajio gani na wewe kuhusiana na swala la ndao, ghafla unakoma kuziona siku zako… Mimba hiyo! Je unafanyaje?
Kwanza naomba ufahamu kwamba, kupata mimba haimaanishi ndiyo kuolewa. Hili ni kosa ambalo wanalifanya wanawake wengi tena wa kiwango cha kutosha, wanaamini kwamba kubeba mimba kutawahakikishia kuolewa na mwanaume aliyempa ujauzito. Kwa huku kwetu sheria haziwabani sana wanaume linapokuja swal la kulea mimba na matunzo ya mtoto kwa hiyo mwanaume kumtosa mwanamke aliyebeba ujauzito siyo jambo la kushangaza. Wanawake ambao ni single mother wanajua kuhusu jambo hilo. Kwa hiyo kama unabeba mimba fanya hivyo ukiwa umejiandaa kujitwika changamoto zitakazojitokeza na usije ukajifariji ukidhani kutakuwa na masaada kutoka kwa mwenzi wako, utakuwa unajidanganya. Kama akikubali mfunge ndoa sawa, kama akikubali kulea mimba na mtoto atakeyezaliwa pia ni sawa, akikataa wala usivunjike moyo, simama imara na songa mbele na maisha kwani kuzaa kabla ya ndao siyo mwisho wa maisha, yapo maisha tena mazuri sana ukiwa na mwanao. Kwanza unaye mtu wa kukuliwaza, na pili utakuwa umajihakikishia kwamba wewe si mgumba, na tatu leo na kesho umekuwa mtu mzima unaye wa kukushika bega kuliko kutegemea ndugu zako.

6.Pesa inapokuwa sehemu katika kupenda.
Wapo baadhi ya wanawake kabla ya kumkubalia mwanaume wanaangalia anamiliki kitu gani, amesoma kwa kiwango gani, ana kazi ya aina gani, anafanya shughuli gani, anazo fedha za kutosha au yuko katika mazingira ya utafutaji yanayoashiria neema huko mbeleni. Sikatai kwamba wanawake kabla ya kumkubali mwanaume wanataka kujihakikishia usalama, na kama nilivyowahi kusema hapa mara nyingi kwamba usalama kwa mwanamke maana yake ni mtu kuwa na fedha, tofauti na zama za kale za mawe ambapo uwindaji na kilimo kilimuweka mwanaume shupavu katika nyanja hizo kukimbiliwa na wanawake. Siku hizi hayo hayapo, fedha imekuwa ni njia ya mkato katika kupata kila kitu. Kwa mwanamke fedha ni mtego umnasao kama panya na kipande cha nguru mtegoni. Siku hizi ukiwa na fedha una uwezo wa kumpata mwanamke umtakaye, fedha imekuwa kama tufani, inabeba waliomo na wasiokuwemo, hata wale watakaotokwa na povu kupinga hoja hii, nadhani hawajapata bahati ya kukutana na wanaume wenye fedha, laiti wangepata wasingeweza kusimama hapa na kupinga hoja hii. Kwa ushauri tu, si vibaya kuangalia mwanaume mwenye muelekeo wa kutafuta lakini hicho kisiwe ni kigezo namba moja, kwani kama akikuonyesha sifa hizo kabla ya kuingia kwenye uhusiano kisha ukaingia na baadaye ukagundua mwanaume huyo si mali kitu wenyewe mnaita mwanaume suruale, utaumia sana. 

7. Uzuri wa kitandani
Ninaposema uzuri wa kitandani namaanisha kuridhishana katika tendo la kujamiiana, kwa kawaida wanawake ndiyo wahanga wakubwa linapokuja swala la njaa chumbani, wao ndiyo kwa asilimia kubwa hawaridhishwi na wenzi wao katika tendo. Siyo kwamba waume zao wana udhaifu, la hasha, inawezekana wanazo nguvu kama za simba, lakini kwa kawaida tendo la kujamiiana haliwi zuri eti kwa sababu tu mwanaume anazo nguvu kama za simba, bali inahitaji usanii na utundu ukiwemo werevu wa kihisia kuweza kumfikisha mwanamke kileleni. Wanaume wengi kwa sababu ya mazoea wanadhani swala la kumfikisha mwanamke kileleni ni kutwanga kwa kutumia msuli. Si kweli hata kidogo, ni kumuandaa mwanamke kwa maneno matamu kabla hata ya kuelekea kitandani. Kwa hiyo wapo wanaume wenye ufundi huo linapokuja swala la kujamiiana, nia mafundi hodari wenye uwezo wa kuwafikisha wenzi wao peponi, lakini inawezekana katika maeneo mengine ya kimaisha wakawa watupu kabisa. Siyo wawajibikaji, wanyanyasaji wakubwa, hawana staha, hawawaheshimu wenzi wao na ni wenye vurugu kichwani. Wakati mwingine mwanamke anaweza kunasa kwa sababu hiyo tu, ya ufundi wa kitandani, lakini akajikuta anaishi katika machungu kutokana na kutothaminiwa na kunyanyaswa kupita kiasi. Kinachomuweka si kingine ni ile starehe ya muda mfupi wawapo kitandani tu basi. Kuna haja ya kujiuliza, Je ni kitu gani hasa kinachokufanya umpende mwenzi wako? Kama utamkubali na udhaifu wake na una uwezo wa kuhimili hizo tabia zisizofaa kwa maana kwamba hazikuumizi kihisia (kitu ambacho si rahisi sana kwa wanawake) ni sawa, lakini kama huwezi, sikushauri kuingia katika uhusiano wa aina hiyo, kwani ni kujitafutia kaburi la mapema.

Mwigulu Nchemba Afutilia Mbali Vikao vya Chai Serikalini "Maendelo Kwanza"

0
0
Vikao vya chai marufuku
Katika kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima, Mwigulu alisema fedha zitapelekwa kwenye mambo muhimu.
ìKama hali ngumu na wananchi wanalazimika kula mlo mmoja kwa siku, walioko ofisini pia wanaweza kukosa chai ili kuwezesha mambo mengine muhimu yafanyike kwa wakati.
Tunachotaka wizara zibane matumizi tubaki na yale yenye umuhimu. Tunaomba wenzetu kwenye wizara watuunge mkono ili kuhakikisha bajeti hii inakwenda na wakati kwa maana ya mgawo wa fedha badala ya kuchelewa kama ilivyo sasa,î alisema.
Mwigulu alisema jambo lingine la nne litakalozingatiwa ni usimamizi wa fedha zinazopatikana kwani pamoja na makusanyo kidogo, lakini pia kuna uvujaji.
ìTunataka fedha inayopatikana na kupangiwa kazi fulani itumike kwa shughuli iliypokusudiwa kama. Tutahakikisha tunasimamia na kudhibiti matumizi yake,î alisema.
Alisema lengo ni kuhakikisha matumizi yaendane na thamani kwa uhalisia wa jambo
Naibu Waziri huyo wa fedha alisema eneo la tano ambalo litaangaliwa ni eneo la fedha ambazo hazitokani na kodi bali zinachangwa na wananchi na wadau wengine katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Alisema eneo hilo ni muhimu mbalo serikali inaona kuna haja ya kulisimamia vizuri ili kuhakikisha fedha za wa wananchi zinatumika vizuri.
ìKuna wakati wananchi wanachanga fedha kwa ajili ya ujenzi wa zanahanati au jengo la ofisi. Wakati mwingine fedha zao zinakuwa nyingi kuliko zinazotolewa na serikali.
ìUnakuta wananchi wamejenga jengo baadae anakuja mhandisi anasema ujenzi wake haukufutwa vigezo hivyo livunjwe. Hili litaangalia haiwezekani fedha za wananchi zikapotea bure ndio maana tumeweka kipaumbele katika eneo hili,î alisema.
Alisema upotevu wa fedha ni upotevu, hivyo serikali itakuwa makini katika fedha za umma zinachangwa na wananchi katika miradi ya maendeleo.

Nape Avuna Aibu SAUT Mwanza (Picha)

0
0
Atumia asilimia 90 ya hotuba yake kuwashambulia dr Slaa,Lissu ,CDM na UKAWA,
mkutano wake wasogezwa mbele ili kuwasubiria watu wafike uwanjani
Magari yasomba watu kutoka nje ya SAUT baada ya wanafunzi wa SAUT kutojitokeza uwanjani hapo
Awafanisha upinzani na vichaa,asema yeye alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi bora 3 waliofaulu kati ya 100 Bukumbi primary

Katibu wa itikadi na uenezi taifa wa CCM jana alijikuta anavuna aibu ya mwaka pale alipojikuta anahutubia watu waachache tofauti na gharama zilizotumika na malengo ya mkutano huo,kwani kwa mujibu wa taarifa za awali zilizotolewa na uongozi wa CCM tawi la SAUT Mwanza,walisema wamemwandalia mkutano huo kwa ajili ya kuja kuongea na wasomi wa chuo kikuu cha mtakatifu Agustino (SAUT) tawi la Mwanza pamoja na kuwa mgeni rasmi katika mahafali ya kuwaaga wanafunzi wa CCM chuoni hapo,awali mkutano huo ulikuwa uanze saa 8 kamili za mchana lakini ulilazimika kuchelewa kuanza na kusogezwa mbele mpaka saa kumi na dakika 27 jioni kutokana na kukosa watu,kwani mpaka kufikia saa 9 za mchana watu walikuwa wachache sana hali iliyowalazimu CCM SAUT kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa kuanza kuratibu zoezi la kuhamasisha watu wasombwe na magari kutoka kwenye matawi mengine yaliyoko mjini Mwanza.

Mara baada ya magari kadhaa kusomba watu,iliwalazimu pia kukodisha vikundi vya maigizo na mziki wa asili kuja kutoa burudani ili kuwavuta wananchi wafike uwanjani hapo,zoezi ambalo kimsingi nalo lilikwama kwa kushindwa kuzaa matunda hali iliyopelekea katibu huyo mwenezi wa CCM kuanza kuhutubia hivohivyo kwa watu wachache,ikumbukwe kuwa awali zilivuja taarifa ya Nape kupitia serikali ya wanafunzi chuoni hapo kuchinja ng'ombe 3 na mbuzi 10 usiku wa kuamkia siku ya mkutano huo,

Bwana Nnauye alijikuta akitumia zaidi ya asilimia 90 kuwashambulia na kuwaongelea wapinzani hasa Dr Slaa,Lissu ,CHADEMA na UKAWA,hali iliyowakera wasomi wachache waliofika mkutanoni hapo na baadhi ya raia wakazi wa maeneo jirani na chuo,wakiongea kwa masharti ya kutotajwa majina wasomi na raia hao walihoji faida ya mkutano ule kwa wanafunzi na raia wanaoishi maeneo jirani na chuo hicho kwamba hawakuona tija ya mkutano ule kwani walitegemea kma kiongozi wa chama tawala angeongelea masuala mbalimbali ya kitaluma yanayowakabili wanafunzi na mfumo wa elimu kwa ujumla,huku kukiwa na taarifa kwamba kuna baadhi ya maeneo ya chuo hicho hayana huduma ya maji takribani mwezi 1 sasa,walisema hawakwenda pale kuambiwa habari za dr Slaa wala UKAWA,bali walikwenda pale kusikiliza sera na majibu ya kero zao zinazowakabili,nao raia waliokuwa wakitoa maoni baada ya mkutano walisema walishangazwa na namna Nape alivyotumia mda mrefu kuwaongelea wapinzani huku akiacha kuzungumzia kero yao ya mda mrefu ya migogoro ya ardhi eneo la Luchelele ambapo vigogo kadhaa wa CCM na serikali wamejimilikisha mapande makubwa ya ardhi huku wakiwafukuza wakazi wazawa wa eneo hilo.

AWAFANANISHA WAPINZANI NA VICHAA

Wakati akiendelea kuhutubia,mara mara alisikika akiwaita wapinzani ni vichaa huku akiunga mkono wapinzani kunyimwa uwanja huo kufanyia mkutano wa siasa kwa madai kwamba hawana sera zaidi ya kutaka kuwaambukiza wasomia pia aliendelea kusema CCM ni chama dora wanauwezo wa kufanya lolote kwa wakati wowote huku akisema serikali yote kwa mfano ipo pale,miongoni mwa viongozi wa serikali waliokuwepo pale huku wamevaa mavazi rasmi ya chama cha Mapinduzi ,bwana Nape aliendelea kuwapolomoshea wapinzani matusi na kashfa kwa kusema "kale kababu kameshajichokea,kameshakuwa kalemavu wa mkono kapumzike ili sisi vidume tupige kazi"

VURUGU ZA ZUKA /MWANAFUNZI WA SAUT AKAMATWA

Mwanafunzi wa mwaka wa 3 anaesomea masomo ya mawasiliano ya umma chuoni hapo Nicholaus Kilunga,alijikuta akipigwa na walinzi wa CCM na wanaCCM na baadae kukamatwa na polisi kwa kosa la kumtaka Nape azungumzie ufisadi wa bilioni 200 za IPTL kupitia kwenye account ya Escro,mwanafunzi huyo alishikiliwa kwa zaidi ya saa moja hatua iliyopelekea wanachama wa CDM SAUT kuanza kukusanyika kwa wingi kushinikiza mwenzao huyo aachiwe huru kwani hakuwa na kosa lolote,dalili za kutokea vurugu mkutanoni hapo zilianza kuonekana mapema hasa pale Nape alipokuwa akimponda dr Slaa kwamba anakuja kuwadanganya watu kwa maneno ya "people's "huku wanafunzi waliokuwa mkutanoni hapo kuitikia "powerr"hali iliyowakera CCM.

KAULI YA RAIS WA SAUT YAZUA UTATA NA KUWAGAWA WANAFUNZI
Katika hatua nyingine leo chuoni hapa kumezuka sintofahamu na kuongeza hali ya uhasama na sintofahamu kufuatia kauli aliyoitoa rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo hicho mkutanoni jana ndugu Philibert Saimo,pale alipokaribishwa awasalimie wageni na watu waliofika kwenye mkutano huo,huku akiambatana na makamu wake wa rais,waziri mkuu,spika wa bunge la wanafunzi chuoni hapo na waziri wa michezo alitamka maneno haya"Nimeamua kujiunga na CCM,kwa wale wote ambao hawataki kuongozwa na rais ambaye ni mwanachama wa CCM,wale wasio wa CCM na wale wanaoipinga CCM chuoni mjiandae kuhama chuo"kauli ambayo imezusha sintofahamu chuoni hapa hasa ikizingatiwa kwamba kiongozi wa serikali ya wanafunzi hapaswi kujihusisha na vikundi vyenye mlengo wa kidini,kikabila na kisiasa huku ibara ya 53 ya sheria zinazoongoza vyuo vikuu ikikataza siasa kufanyika vyuoni,wanafunzi wengi wameutaka uongozi wa chuo hicho umchukulie hatua kwani hakuchaguliwa na wanaCCM pekee wala kuchaguliwa awahudumie CCM pekee,wakiendelea kusema kwa wale wasiokuwa na vyama vya siasa ama wale wanafunzi wafuasi wa vyama vya upinzani hawatakuwa huru kwenda kupata huduma kwenye serikali hiyo,
Na alipotafutwa na kuhojiwa juu ya kauli yake hiyo,rais wa chuo hicho bwana Saimon alisema yeye anahaki ya kujiunga na chama chochote cha kisiasa,na kwamba pamoja yeye kuwamwanaCCM atahudumia watu wote bila kujari vyama vyao,katika mkutano huo jumla ya wanachama 2 walijiunga na CCM wakitokea CDM nao ni rais wa mwaka jana chuoni hapo bwana Dovakamwene Mcheshi na huyu rais wa sasa Philibert 
By kilunganicholaus@yahoo.com

Sijamaliza Ashasinzia au Ndo Nina Kibamia

0
0
Wakuu swali, 

Nina msichana wangu nimekaa naye miaka miwili sasa, mwanzoni ilikuwa ngumu sana kufika kule kunako wakati wa ku do, nikajitahidi sana kuongeza maufundi sasa hali imebadilika sijamaliza ashamaliza na kusinzia kabisa usingizi wakati bado niko juu yake nashughulika.

yaani huwa inakuwa like nina do mtu ambaye hayuko duniani hadi baadaye kabisa baada ya nusu saa hivi ndo anashtuka, swali langu ni hiyo ni kawaida au ana shida manake ni mda hajaniona nikimaliza kwani alikwisha sinzia au ndo nina kibamia akimgusi kunako?

Man United yaingia Mkenge kwa Moyes

0
0
KWELI Manchester United iliingia mkenge kwa David Moyes baada ya kila kitu alichokifanya klabu hapo kugeuka kuwa majanga.

Baada ya kocha huyo kuisababisha hasara kubwa ya kupoteza mamilioni ya pesa kutokana na kushindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya miamba hiyo ya Old Trafford itapata hasara kubwa kwa kiungo wao Marouane Fellaini, ambaye alisajiliwa na kocha huyo.

Kocha Mkuu mpya wa kikosi hicho, Louis van Gaal amesema haoni kama kiungo huyo anaweza kupata nafasi kwenye timu hiyo msimu ujao na kwamba yupo sokoni kwa pauni 15 milioni kitu ambacho kitaifanya Man United kuingia hasara ya pauni 12.5 milioni.

Fellaini alinunuliwa na Moyes mwaka jana kwa ada ya pauni 27.5 milioni, lakini kwa msimu mzima aliocheza kwenye kikosi hicho cha Man United hakufunga bao hata moja kitendo kinachomfanya kocha mpya, Van Gaal afichue bayana kwamba atakapoingia Old Trafford basi hamtaki mchezaji huyo.

Kiungo huyo Mbelgiji kwa sasa yupo kwenye fainali za Kombe la Dunia na kikosi cha Ubelgiji nchini Brazil na kitu kipekee kitakachomfanya aendelee kubaki Old Trafford msimu ujao kama atafanya kweli kwenye fainali hizo.

Hata hivyo, licha ya Man United kukubali kumuuza kwa hasara, hakuna klabu yoyote iliyojitokeza kutaka kumsajili kiungo huyo kitendo kijachothibitisha kwamba mzigo huo bado unaikabili timu hiyo.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images