Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Jioni ya Leo

0
0

Zijue Dalili, Athari na Tiba ya Upungufu wa Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo na Kuongeza Uume...

0
0
ZIJUE DALILI, ATHARI NA TIBA YA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO NA KUONGEZA UUME. Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), UNYWAJI WA POMBE, HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k. Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo. Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6.5 hadi 7 @150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari na kuweza kurudia tendo @150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130,000/= BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA. KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE KAMA
>Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
>Kuondoa mvi milele zisiludi @150,000/=
>Kutengeneza shepu (hips, makalio na mapaja) 200,000/=
>Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni @130,000/=

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255) 0767447444 na 0714335378 

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Inasikitisha Sana..Mwenyekiti wa Kijiji Afia Kifuani mwa BINTI Gesti Akiwa Anachepuka

0
0
INASIKITISHA sana! Mwenyekiti wa Kijiji cha Mkamba Kata ya Kimanzichana mkoani Pwani aliyetambuliwa kwa jina moja la shabani anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 50, anadaiwa kufia kifuani mwa binti mwenye umri wa chini ya miaka 30, wakiwa kwenye gesti moja iliyopo Mzinga-Mbagala jijini Dar.

IJUMAA WIKIENDA LATONYWA

Mara tu baada ya kujiri kwa tukio hilo lililoibua simanzi nzito, Ijumaa Wikienda ambalo huwa halilazi damu kufika eneo la tukio na kuanika kila kitu, lilitonywa na chanzo chake, mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo lilifika na kuibuka na mkanda kamili wa sakata hilo. Wawili hao walidaiwa kufika kwenye gesti hiyo na kuomba huduma ya kulala kabla ya kutokea kwa tukio hilo baya.

WALITOKEA KIMANZICHANA

Mwenyekiti huyo alikumbwa na umauti Agosti 11, mwaka huu ambapo kwa mujibu wa meneja wa gesti hiyo, Hamadi Haji, walipofika, wawili hao walichukua chumba tangu Agosti 8, mwaka huu wakitokea huko Kimanzichana. Meneja huyo aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, baada ya kulipia chumba, wawili hao walikuwa wakifika usiku kulala na mchana walikuwa wakitoka kwenda kwenye mihangaiko yao. “Sijui walikokuwa wakienda, lakini walikuwa wakirudi usiku na kujifungia chumbani.

MSHANGAO

“Lakini katika hali ya kushangaza leo (Ijumaa iliyopita) asubuhi, mwanamke aliyekuwa na mwenyekiti alinifuata na kuniambia mwenzake huyo hamwelewi kwa sababu ghafla alianza kumbadilikia na kukoroma kwa mlio ambao haukuwa wa kawaida.

“Yule mwanamke aliniambia kiongozi huyo alikuwa na dozi fulani aliyopewa baada ya kutoka hospitalini kwa sababu hakuwa vizuri kiafya na hilo ndilo lililowaleta Dar. “Alisema alimkatalia sana wasifanye tendo la ndoa, lakini usiku mzima alikuwa akimlazimisha. “Yule mwanamke alitueleza kuwa baada ya jamaa kumbembeleza sana na kumuongezea na vishawishi vingine, mwanamke alisema alijikuta akilegeza msimamo kisha akamkubalia asije akaona labda hampendi. “Baada ya kumkubalia ndipo wakaanza kufanya yao.

 .
MUUNGURUMO WA AJABU

“Aliendelea kutusimulia kuwa wakati wakiendelea kufanya yao ndipo alipoanza kumsikia mwenzake akitoa muungurumo wa ajabu huku akimng’angania kifuani. “Alitusimulia kuwa alipoona hivyo, akaanza kumshangaa, lakini ghafla alimuona akitupatupa miguu na mikono.

“Alisema baada ya kuona hivyo, alijinasua na kumwangalia mwenzake kwa makini ndipo akamshuhudia akitupatupa mikono na miguu peke yake. “Yule binti alisema kila alipojaribu kumsemesha, jamaa alikuwa hawezi kujibu lolote hivyo alikaa muda fulani akijua mwenzake labda amekumbwa na jambo la kawaida na atarejea kwenye hali yake.

UKIMYA WATAWALA

“Alisema tofauti na matarajio yake, jamaa aliendelea kuwa kimya na hapo ndipo alipoingiwa na hofu. “Alipoona hivyo, ndiyo akaja kunigongea kwenye ofisi yangu. Mimi nikaenda naye kwenye chumba chao kiitwacho Mikumi na kumkuta jamaa amelala kwa staili ambayo hata mimi mwenyewe sikuilewa.

“Ilibidi nimpigie simu mwenyekiti wa serikali ya mtaa wetu, aje tushirikiane kumuangalia,” alisimulia meneja wa gesti hiyo na kuongeza: “Muda mfupi baadaye, mwenyekiti aliwasili na viongozi wenzake na kuingia kwenye hicho chumba ambapo walipomuangalia jamaa, waliniambia kuwa huenda amefariki dunia. “Hapo ndipo wakapiga simu polisi ambao walifika na kuuchukua mwili huo baada ya kugundua jamaa alikuwa amekwishafariki dunia.”


Kufuatia sakata hilo, Ijumaa Wikienda lilifika kwenye ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Mzinga A na kumkuta mwenyekiti wa mtaa huo, Chande Mpwati ambaye alithibitisha kutokea kwa tukio hilo mtaani kwake na kueleza jinsi alivyoshiriki katika kwenda kuukagua mwili wa marehemu na kumuhoji binti aliyekuwa naye.

MAPENZI YA SIRI

Mpwati alisema kuwa, alipomuhoji binti huyo alimwambia kwamba jamaa huyo alikuwa ni mpenzi wake wa siri kwa kuwa ana familia yake kijijini kwao, Mkamba maana mwanamke huyo naye ni mkazi wa huko hivyo walikuja Dar kwa ajili ya mwanaume huyo kutibiwa ambapo walinionesha makaratasi ya hospitalini ndipo umauti ukamfika wakiwa wanafanya mapenzi. “Mwili wake ulichukuliwa na polisi kwenda kuhifadhiwa Hospitali ya Temeke na yule binti alichukuliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi,” alisema mwenyekiti huyo.

KAMANDA TEMEKE

Ijumaa Wikienda lilizungumza na Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, ACP Gilles Muroto ambaye alisema kuwa ishu hiyo ilikuwa haijamfikia mezani kwake, lakini aliahidi kufuatilia kwa watu walio chini yake.

Amber Lulu Kanasa Kwa Bwana Mpya....Adai Anampenda Hadi Anatamani Kujiteka........

0
0
Muuza nyago (video queen) ambaye hivi sasa amejitosa kwenye Bongo Fleva, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’ ameamua kuwadorishia wenzake kwa kujishaua laivu na bwana’ke mpya.

Nusanusa ya Ijumaa Wikienda ilibaini kwamba, bwana huyo mpya wa Amber ni msanii wa Bongo Fleva anayekwenda kwa jina la Zulfika Hamisi ‘Jamwehe’ ambaye ilisemekana kwamba, ndiye aliyemshawishi mrembo huyo kufuta tatuu za mpenzi wake wa zamani, David Genz ‘Young D’.


Juu ya bwana’ke huyo mpya, Amber Lulu alilieleza Ijumaa Wikienda kuwa, sasa hivi ameamua kumuweka hadharani mpenzi wake bila kuhofia chochote kwani hata wale ‘nyakunyaku’ wa mabwana wa wenziye watagonga mwamba kwake.


Amber Lulu.
“Nampenda hadi natamani kujiteka, kiukweli hapa nimekufa hadi sijielewi. Ndiyo maana sioni aibu yoyote kujiachia naye na bado nitaonesha watu kuwa hata mimi najua kupenda,” alisema Amber Lulu anayekimbiza na ‘lijisongi’ lake la Watakoma.
Amber Lulu asiyeishiwa vimbwanga kama yule Amber Rose wa Marekani aliongeza kuwa, kwa sasa amejipanga kutulia tuli kwa jamaa huyo kwani ameona ni mwanaume mwenye malengo na mtazamo tofauti.

“Hapa mapepe yangu kwishnei kabisa na huwezi kuamini nipo tayari hata kwa ndoa,” alisema Amber Lulu. Kwa upande wake, jamaa huyo alifunguka kuwa, ana nia ya kweli na Amber Lulu na yupo tayari kwa lolote. “Ninampenda sana Amber (Lulu), ni mwanamke wa tofauti na wanavyomchukulia,” alisema Jamwehe.
Stori: Imelda Mtema, Dar

Wasanii wa Bongo Nani Kawaroga? Kila Msanii Anataka Kwenda Kimataifa Kumbe ndo Mnajiaribia...

0
0
Wote wamekalilishwa neno "kimataifa" utacheka sana namna wanavyokazania huu ujinga... Madee katoa nyimbo mpya kamshirikisha Tekno wa Nigeria alooo nyimbo ni mbaya dunia nzima, shishi kamshirikisha mdada wa Nigeria asee nyimbo ukiidownload unaifuta saa hio hio baada ya kumaliza kuiskiliza, yote tisa joh makini ndio kachekesha sanaa, katoa nyimbo na davido ni mbaya ukiiskiliza mpaka unaweza kuumwa kichwa, nyimbo nzima unaskia tu kataa kataa leetaa hawa nani kawaroga?

Mbaya zaidi wanatumia mamilioni kuwalipa wasanii hao wanaowaita wa kimataifa na utengenezaji wa videos ambazo hakuna anaejisumbua ata kuziomba kwenye TV stations.

Tulitegemea labda wasanii wetu hawa watakua wajanja na wabunifu kidogo labda, ila wao wameimba kama wanaija tu hali inayopelekea kupoteza muda na fedha.

Kujua ni kujua tu, hakuna aja ya kupoteza muda kwa watu ambao ata nao hawajatoboa kimataifa kama uyo sijui IYO nk., sasa hawa wanao jiupgrade na kujiita wa kimataifa ila wanategemea show moja ya fiesta maishani wanajiskiaje wakiona mtoto mdogo kama Aslay tu ambae video Zake uenda ni za elf 50 tu ila uswahilin kote nchini zinapigwa kama nyimbo za taifa na youtube ngoma zake zinatoboa views million Mpaka 2+, lazima watajidharau tu ila na kwa vile wasanii hawa ni mbumbumbu Hawawezi kureason hapo.

Sasa unakuta msanii chege alishafanya nyimbo mpaka na run town ila sasa nna uhakika hata malawi hawajui kama kuna mbumbumbu anaitwa chege, huyu simlaumu kwakua amekua akilazimisha fani, ila sana wale wenzake daaah hasa joh maskini huyu yeye tulijua anatoboa maana davido huyu huyu kabisa? Davido kaishika africa kwa sasa unapata bahati adhimu alaf unaimbaa kataa kataa leta wewe umerogwa au? Hio hela ya mavideo ya gharama ya nyimbo mbaya kama hio si bora uyo msanii angeenda kununulia ng'ombe tu zikaja kumsaidia maishani.

Anyway, wasanii wetu bado hawajajua kua wanapoteza muda na fedha kutafuta vitu wasivyovijua, big up diamond wasaidie ndugu zako.

Mjumbe wa kihenga hauwawi.

Mambo 8 Muhimu ya Kuzingatia kutoka Kuajiriwa Hadi Kujiajiri

0
0
Kuna sababu mbalimbali kwanini mtu atake kuajiri, badala ya kuajiriwa, mfano kipato kidogo anachopata katika kazi husika, hitaji la kutaka uhuru zaidi binafsi wa kufanya kazi, hitaji la kuweza kutoa ajira kwa wengine na zaidi sana kuweza kutumia vema kipaji na uwezo wa kuzalisha ambao katika kazi ya sasa mtu hapati nafasi ya kufanya hivyo.

Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu, haiwezekani tuu , ukaacha kazi na kusema ok, acha nijiajiri.

Makala hii inachambua mambo ya msingi ya kujiandaa na kuyafahamu kabla mtu hajaamua kuacha kuajiriwa.

Mkakati ni muhimu
Wazo au ndoto isiyo na mkakati wa kuitimiza ni upuuzi yaani ndoto hiyo au wazo hilo halina maana, hivyo basi ndoto yako ya kujiajiri siku moja, ni lazima iwekewe mkakati wa kuifanikisha ikiwa ni pamoja na muda hasa wa lini utaitimiza hiyo ndoto.

Katika kuweka mkakati huu wa kutimiza ndoto yako, fanya utafiti wa kina kuhusu mipango yako binafsi ya maisha, mtazamo wako kuhusu maisha, mpenzi/mke wako, familia yako, na hali ya jamii kwa ujumla inavyoenda kama vile mabadiliko ya hali ya kisiasa, teknolojia, na uchumi.

Tengeneza malengo ya aina ya shughuli unayotaka kuifanya ukiacha kuajiriwa, na pima uwezekano wa shughuli hiyo kufanyika kweli na kama itakulipa. Utambue pia aina ya watu na rasilimali nyingine utakazozihitaji, na jinsi utakavyozipata.

Unahitaji fedha
Ndio, unahitaji kiasi cha fedha za kutosha kununua vifaa na malighafi za kutengenezea bidhaa yako. Pia unahitaji fedha za kuwalipa wafanyakazi wako, na zaidi sana , unahitaji fedha za kuendesha maisha yako na familia yako , kwa kipindi fulani kabla ya biashara kuanza kukulipa mshahara. Hivyo kabla haujaacha kibarua chako, hakikisha umetengeneza bajeti ya kutosha na una akiba ya kutimiza mahitaji ya bajeti yako. Usingependa uache kazi halafu uanze kuwa omba omba kwa rafiki na jamaa, au uanze kujuta.

Network ni muhimu
Kumbuka katika kujiajiri kwako, utahitaji wateja, washirika, wafanyakazi na hata washauri mbalimbali ili mambo yako yaende vizuri. Hivyo, wakati ukiwa umeajiriwa ndio wakati wako muafaka wa kutengeneza na kupanua wigo wako wa watu unaowafahamu na waliokaribu nawe.

Kumbuka kuendeleza mawasiliano kwani watu hawapendi kuona wewe unataka kuwatumia tuu kisha unawatupa. Endeleza mawasiliano walau hata kwa salamu tuu. Zaidi sana, heshimu watu wote, hata usiowafahamu au wale unaodhani 'sio watu muhimu'.

Jenga taswira nzuri kwa jamii kwa lugha fasaha, picha na matukio mengine, usifanye watu wakufikirie vibaya.

Usipitwe na wakati: Hakikisha kuwa unafuatilia taarifa za matukio, dili na watu wanaohusiana na aina ya shughuli unayopanga kuifanya wakati utakapojiajiri. Hii itakusaidia kupata uzoefu na kusoma alama za nyakati, na pengine kutambua fursa nyingine zaidi.

Endelea kujifunza zaidi kuhusu kazi yako, watu na jamii kwa ujumla kwani kujiajiri kunahitaji uzoefu zaidi, na zaidi sana uwezo wa kupambana na changamoto nyingi ambazo nyingine haujawahi kukutana nazo kabisa, ila taarifa za awali na kujua jinsi mambo yanavyoenda kwa ujumla katika jamii vitakufanya ushinde changamoto.

Maana halisi ya biashara
Baada ya kuacha kuajiriwa, hautarajii kuwa mtu wa ‘kuganga njaa’ yaani kufanya biashara ili mradi tuu hela iingie, lakini haujui mwelekeo wa biashara yako upoje, na wala hakuna mkakati wa kuikuza na kuimarisha biashara husika.

Biashara inahusu kutimiza mahitaji ya watu, kwahiyo ili mradi utakuwa na uwezo mkubwa wa kutimiza mahitaji ya watu, na kuendelea kuhamasisha watu zaidi kuja kwako uweze kutimiza mahitaji yao , basi biashara itakua, na itaendelea kuwa endelevu.

Kinyume cha hapo, ushindani utakutoa katika biashara kwani wateja watakambilia kwa wengine. Biashara sio tuu kupata wateja, ni vile kuweza kuendelea kupata wateja na kuendelea kupanua biashara.

Inabidi uipende shughuli husika unayoifanya, na uweze kutimiza mahitaji ya wateja kupitia biashara husika.

Muda wako mwingi utautumia katika shughuli yako mpya utakayojiajiri hivyo, kama ambavyo kazi uliyonayo pengine ‘inakuboa’, hakikisha ajira yako binafsi ‘haikuboi’.

Umuhimu wa wafanyakazi
Watendaji wa shughuli husika za biashara yako utakayoianzisha ni muhimu wawe wenye ujuzi na uzoefu wa kutosha wa kufanya shughuli husika, na uweke mikakati ya kuwapatia nyenzo zote muhimu za kufanyia kazi ikiwemo teknolojia na mazingira mazuri ya kazi. Hivyo basi wakati unajiandaa kujiajiri tilia maanani hili katika bajeti yako ya kuajiri. Usingependa wafanyakazi wao wajisikie vibaya kama vile wewe ulivyojisikia vibaya katika ajira yako fulani (pengine ajira yako ya sasa). Muda huu ambao umeajiriwa, ndio muda pia muafaka wa kusaka 'vipaji'- yaani watu ambao utafanya nao kazi utakapojiajiri.

Inakuhusu wewe 
Mafanikio yako katika kujiajiri yanategemea mambo mengi ila zaidi sana yanakutegemea wewe. Je, nini hasa sababu yako ya kutaka kujiajiri?

Ni kweli una bidhaa au huduma haswa ya kupeleka sokoni itakayokufanya iendeshe maisha yako na kuiendeleza biashara husika au ni hasira tuu za jinsi bosi wako anavyokuchulia hapo ofisini kwako, au kwakuwa mshahara uliopo sasa haukutoshi. Je, mipango yako mingine ya maisha ipoje?

Ndoto zako za kusoma, au kuishi sehemu tofauti tofauti, pengine mkoa mwingine tofauti na uliopo sasa, au pengine hata nchi husika. Je, yote hayo yanaathiri vipi mipango na mikakati yako ya kujiajiri, bila kusahau msukumo toka kwa familia yako.

Ndoto sahihi
Ni kweli kuwa upo sahihi kufikiria au kuota kufanya biashara kubwa na yenye mafanikio sana, lakini kumbuka mafanikio hayaji kwa usiku mmoja, na hata kama yatakuja kwa usiku mmoja, inahitajika kazi ya muda mrefu kuyafanya yawe endelevu.

Hivyo basi, usingoje wakati ‘muafaka’ wa wewe kuwa na kiasi kikubwa cha fedha au kwamba ‘umeyaset’ vema mambo yote.

Anza kidogo kidogo, kubali kufanya makosa, na tambua kuwa hata kama utafanya uchambuzi na uchunguzi wa kutosha kuhusu soko, jamii na teknolojia, hali halisi unayoenda kukumbana nayo inaweza kuwa tofauti na ile uliyojifunza wakati wa uchambuzi au uchunguzi wako kwakuwa hicho unachoenda kufanya ni kipya hakikufanyiwa uchambuzi, bali unakifanya kutokana na uchambuzi uliofanya hapo awali.

Kuna mtu mwingine atakuja kutumia makosa au mafanikio yako kupanga mambo yake.

Uhuru Kenyatta Pao Sana..Asema Ruksa Kuandamana wa Wasioridhishwa na Matokeo..Aamuru Polisi Wasizuie

0
0
HABARI: Rais Mteule wa Kenya, Uhuru Kenyata asema wananchi wanaruhusiwa kuandamana kwani ni haki yao kikatiba...amewaamuru Jeshi la Polisi kuacha kutumia nguvu kupita kiasa...ila Serikali haitavumilia watakaoharibu mali za umma.

Kijana Epuka Ndoa na Wanawake Wenye Kazi Hizi........

0
0
Mwalimu :
Wengi wenu mna dhana potofu kwamba ukioa mwalimu mpo in safe side. Hawa watu akili zao zimelala fofofo. Mtu anayeridhirika na ujira wa laki 3 kwa mwezi kwa kutoa sadaka siku zake 30 kwa mwezi ni wa kumuepuka. Hana changamoto mpya katika maisha. Akirudi kazini yuko exhausted kabisa, atapata wapi muda wa kuwaza vitu vipya huku bado hajasahihisha?? Unless atakua ni mtu unayemtumia kwa sex tu, ana madhara hata kwa akili ya watoto atakaowazaa yawezekana wakawa na akili mgando pia.

Askari :
Hawa watu siitaji kuwaelezea sana. Acha wachukuane wao kwa wao. Kama wewe ni raia wa kawaida ukitaka kuumia moyo kwa kupigiwa oa hawa watu. Mafunzo ya kijeshi kawaida yanaharibu saikolojia yao. Kauli mbiu ya huko mafunzoni kwao ni kwamba wanawake wapo jeshini kwa ajili ya kuburudisha mjeshi wa kiume na kumpa morali. Ko kiungo chake si mali yake. Achilia mbali kukuendesha.

Nurse / Wauguzi :
Kama una mpango wa familia yako kustawi kiuchumi, epuka hawa watu. Kazi zao zinawa train kutoa msaada ( kazi za kujitolea ). Mioyo na akili zao hubadilika kabisa na kuwa kimsaada na kuhurumia zaidi. Hii ni mbaya sana kwa maisha ya kibiashara/kiuchumi. Ingawa the first law of being rich is giving out but kwa hawa huwa ni too much. Wema usizidi uwezo.

Madactari :
Kutokana na nature ya kazi zao ni vigumu mno kwa ustawi wa familia. Kama una ndoto ya kuipeleka mbali kiuchumi familia yako waepuke. Muda wao mwingi hutumika kuwaza kazi zao na kutoa huduma. Ni rare sana kumkuta dactari yuko shap nje box. Unless umuweke kwa kukuzalia na huduma za kimwili, hata hivyo unahitaji uwe mvumilivu kwelikweli muda wowote anakurupushwa kazini.

Waajiriwa wa mabenki. ( Tellers & Accountants).
Kuishi mtoni haimaanishi wewe ni msafi. Kuna watoto mnajidanganya hawa watu wana pesa kutokana na kazi zao. Hawa hawana tofauti na kundi la kwanza hapo juu. Moja ya wanyonywaji wanaoongoza nchini ni hawa. Mikopo ya nyumba na vigari huwasahaulisha kabisa kama wananyonywa. Ma teller wanalipwa hadi laki 4, accountants wanapewa >1m for 12 hrs a day for 30 days. Ukiamua kuoa hawa hakikisha ana kubali kuacha kibarua chake, wanakuwaga wachakarikaji at least but wakiacha.

Wasaidizi maalumu wa watu binafsi :
Wasemaji wa mabosi fulani, makarani wa mabosi, na wengineo. Mara nyingi huwa ni nyama za hao mabosi, Lkn unaweza kuoa kama huna wivu wa mapenzi. Mara mia ukaoa muhudumu wa hoteli.

Msomi asiye na kazi :
Mara mia tatu kuoa mjinga asiye na kazi kuliko hawa nyumbu wamekula pesa ya serikali alafu wanapanga foleni kusubiri kuwa watumwa wa watu. Akili yao 80% wanawaza ngono vichwani. Mjinga asiye kazi unaweza bahatika kupata mwenye mwamko akawa wa faida kwako ila kwa sababu tu hakupata mwanga akaishia kubaki iddle.


USHAURI WA BURE ( option kuchukua):
Kuna kazi watu wake mnawadharau mno lakini kwa kutokana na uzoefu wangu maishani it's 100 better kuwachangamkia.

Wafanya biashara wadogo( haijalishi udogo wa level gani).
Akili za hawa wanawake zimechamka mno. Akili iliyochamka ina faida lukuki kwa mtumiaji. Ashajua ujanja wa kuingiza mkwanja, kuoa hawa ni kuwa na advantage ya goli la ugenini.

Waajiriwa wa secta binafsi department za accounts, Sells & Marketing & Project planning & Development.
Akili za hawa watu huwa ziko active muda wote kutokana na nature za kazi zao. Ni faida kwako uliye na ndoto za kufika mbali kiuchumi. Ukikosa wa secta binafsi oa hata wa serikalini. Mkishawaoa baada ya muda ni vizuri watoeni huko, wafanye mambo yanayohusu familia( kiuchumi).

Mnaweza kuongeza na wengineo...............................................!!

Samahanini sana kwa niliowagusa.....


Hii Ndiyo Misemo Inayotufanya Tusitimize Ndoto Zetu

0
0
Baada ya kufanya uchunguzi wangu wa kina nikaja kugundua ya kwamba kuna baadhi ya misemo ambayo imekuwa ukiturudisha nyuma sana kwenye safari yetu ya kuyasaka mafanikio, hii ni kutokana na mara kadhaa ukijaribu kufanya baadhi ya vitu vya msingi yanakujia maneno au misemo hiyo eidha uliwahi kuambiwa na jamii ya watu wanaokuzunguka au wewe mwenyewe.

Maneno hayo ndiyo yamenifanya nikumbuke mpaka hadithi ya sungura baada ya kukosa ndizi kwa muda mrefu akajipa maneno ya kwamba "sizitaki mbichi hizi" nafikiri nitakuwa nimekukumbusha mbali kidogo juu ya hadithi hii.

Ndivyo hata sisi tumekuwa tukitumia maneno hayo, ndiyo ambayo yamekuwa yakijirudia kila siku katika maisha yetu, najua utakuwa unashangaa ila huo sio muda wa kushangaa bali ni muda wa kibatilisha maneno hayo, inawezekana nimekuacha kidogo ngoja nikukumbushe misemo hiyo au maneno hayo ambayo kimsingi yamekuwa yakikukwamisha kupata Mafanikio.

Ifuatayo ndiyo misemo ambayo inakukwamisha kupata Mafanikio.

1. Haraka haraka haina baraka.
Mara kadhaa umekuwa ukijaribu kufanya vitu vya msingi vyenye kukuletea manufaa ila kwa kuwa kuna baadhi ya watu wanao kuzunguka wamekuwa wakiona kile ambacho unachokifanya mwisho wa siku kwa kuwa kina changamoto nyingi watakuambia maneno hayo kwamba haraka haraka haina baraka kwa kuwa wewe ndiyo mfanyaji wa jambo hilo unaamua kupunguza juhudi za kiutendaji wa jambo hilo.

Na ukichunguza kwa umakini wanaokwambia maneno hayo wao tayari wapo mahali fulani kimafanikio. Kumbuka kuwa kauli hiyo inazungumzia muda na muda haumsubiri mtu hata siku moja na moja ya uchunguzi ambao umewahi kufanywa juu ya muda waligundua ya kwamba kila mtu anayo saa lakini hana muda. Huo ndio ukweli watu kwenye simu zao wana saa lakini hawana muda wa kuleta mabadiliko binafsi na jamii kwa ujumla.

2. Pole pole ndio mwendo.
Hayo ni maneno ambayo umekuwa ukiishi nayo na kuamini kuwa kila kitu kitafanikiwa kwa hatua uliyo nayo. Ukweli ni kwamba kwa kila jambo ambalo unalifanya hakikisha unafanya kwa uhakika na ufanisi wa kutosha ili kupata matokea.

Mara nyingi tumekuwa na maisha yaleyale kila siku kwa sababu unamini ya kwamba polepole ndio mwendo, huenda ikawa ni kweli. Ila tatizo linakuja kufanya vitu pole pole ambavyo havileti matokea chanya ya kimaisha, unajua kwa nini? kwa sababu unafanya mambo yako kwa staili ya aina moja.
Kwa mfano kama ni biashara umekuwa ukisubiria wateja tu na huna muda wa kuwafuata wateja harafu unasubiri hiyo pole pole iwe mwendo utasubiri sana.

Hata watu ambao wamefanikiwa na wao walikuwa wanaamini sana Kuwa pole pole ndio mwendo huku wakiongeza juhudi za kutaka kufanikiwa kwa kasi zaidi, na moja ya njia ambayo walizitumia ni kufanya kazi  kama watumwa na leo hii wanaishi kama wafalme.

Hivyo ni muda wako muafaka na wewe kubadili njia za kutafuta mafanikio hayo tofauti na njia ulizozizoea.

Pia ni lazima ujue ya kwamba maneno yamekuwa yana nguvu sana. Kwa mfano kuna baadhi ya watu wamekuwa na tabia ya kusema nipo nahangaika, ni kweli kama ni miongoni mwa watu ambao utahangaika sana. Badili tabia kauli zako kuanzia leo, utafanikiwa.

Nukuu ya Leo; chochote bila chochote huwezi kupata chochote.

Je, Uke Wako Unatoa Harufu Mbaya? Hii Ndio Jinsi ya Kumaliza Tatizo Lako

0
0
Wanaume wengi kila kukicha huwa wanalalamika kuwa inaboa na inakera kupeana Raha na Utamu na Mwanamke ambae sehemu zake za siri zinanuka. Inawatoa out of the mood, mwisho wake wanaconcetrate kudo fasta, wamalize hamu zao kila mtu aondoke.

Wapo baadhi ya wanawake wanajijua wanasumbuliwa na hili tatizo lakini cha kushangaza hawana muda wa kutafuta solutions za kumaliza tatizo lao (wanaishia kuchekwa kuwa vituko vya mtaa bila kujijua bcoz hawajui kuwa matatizo yao ya uke kutoa harufu mbaya,yanasimuliwa na wale wanaume ambao washawahi kulala nao wakiwa wanapiga story na marafiki zao maskani mtaani).

lakini wapo wanawake wachache wenye busara,ambao wanajijua wanasumbuliwa na hili tatizo na wangependa kujua sababu na jinsi ya kulimaliza,na hao ndio wamenifanya mie niandike hii post
Nitaanza kuelezea sababu kisha nitaelezea ni jinsi gani unaweza kumaliza tatizo lako.

Sababu zinazosababisha uke kutoa harufu mbaya ni kama zifuatazo,

1.BACTERIAL VAGINOSIS
Kwa mujibu wa madaktari bingwa,inasemekana kuwa hili ndio tatizo namba moja linalosababisha uke kutoa harufu mbaya.Inawezekana ukawa msafi mpaka mwisho lakini ukisumbuliwa na hili tatizo basi lazima uke wako utatoa harufu mbaya.

Kila uke una bacteria ambao wapo naturally kwa ajili ya afya njema ya uke wako,Lakini kama ikitokea hawa Bacteria wakazidi na kuwa wengi kupita kiasi ambacho uke wako unaweza kuhimili ndio hapo hiki kitendo kinaitwa Bacterial Vaginosis.

Sababu zinazosababisha Bacterial Vaginosis hazijulikani kwa usahihi lakini madaktari wanasema inaweza ikasababishwa na kitendo cha kupeana Raha na Utamu bila condom especially kama vitu vilivyoingia kwenye uke wako wakati wa kupeana Raha na Utamu vilikuwa vichafu(vitu kama vidole au mashine ya mwanaume,or may b dildo etc) au mara nyingine inatokea naturally bila sababu.

Ukitaka Kujua kuwa unasumbuliwa na Bacterial Vaginosis,utajikuta unapata Dalili zifuatazo;

Uke kutoa maji maji mazito au mepesi yenye rangi ya njano(yellow) au Brown yenye harufu mbaya
Maumivu kwenye maeneo ya kiuno au nyonga
Unaweza usipate au ukapata maumivu ya kichwa.
Uke wako unaweza ukawa unawashwa au usiwashwe (ur vagina might itch or not)


2. YEAST INFECTION
Hili Pia ni Tatizo,lipo kama la Bacterial Vaginosis.tofauti yake ni kuwa kwenye Bacterial Vaginosis waliokuwa wamezidi ni bacteria lakini huku wanaozidi ni fungus candida albicans. Ni wanawake wachache huwa wanapata Bacterial Vaginosis lakini wanawake wengi lazima wapate Yeast Infection japo mara moja katika maisha yao.

Mara nyingi Yeast Infection hutokea Naturally au inaweza kusababishwa na aina ya vyakula au vinywaji unavyokula au kunywa especially kama vimejaa yeast(vyakula vyote vinavyotengenezwa na hamira,pombe etc) Ukitaka kujua kama unasumbuliwa na Yeast Infection,utajikuta unapata Dalili zifuatazo;

Uke wako ukawa unawashwa au usiwashwe (ur vagina might itch or not) Maumivu kama uke unaungua pale unapokuwa unajisaidia haja ndogo (when u pee) Uke kutoa maji maji mazito yenye rangi nyeupe kama jibini(cottage cheese)


3. SEXUALLY TRANSMITTED DISEASES (STDs)
Kuna baadhi ya magonjwa yanayosababishwa na kupeana Raha na Utamu bila Condom,kama vile Chlamydia na Gonorrhea(kaswende na kisonono),kama ukiyapata huwa yanasababisha Uke kutoa Harufu mbaya kwa sababu dalili zake zinahusiana na kutokwa na maji maji yenye harufu mbaya.

4. VAGINAL OR CERVICAL CANCER
Unapokuwa una kansa ya uke au kansa ya mlango wa kizazi(cervical cancer),kutokwa na maji maji yenye harufu mbaya ni sehemu ya dalili zake.Unapojiona kuwa una tatizo la uke kutoa harufu mbaya,ni heri na itakuwa busara ukienda hospitali,kama ni kansa ya mlango wa kizazi itakuwa sio ngumu kuitibu kama ukiwahi mapema.

5. POOR HYGIENE
Inawezekana pia tatizo la uke wako kunuka linasababishwa na uchafu. May b unaoga mara moja tu kwa siku au siku nyingine hata hauogi. Hauna mazoea ya kufua nguo zako za ndani(underpants),na ikitokea siku umezifua basi hata hauzisugui zikawa safi.n.k

MAMBO UNAYOTAKIWA KUFANYA UKITAKA UKE WAKO USITOE HARUFU MBAYA

1. OSHA UKE WAKO KWA MAJI SAFI KILA UNAPOMALIZA KUJISAIDIA HAJA NDOGO(PEE)
Asilimia kubwa ya wanawake hawana mazoea na utaratibu huu.Ni utaratibu muhimu katika maisha ya kila siku ya mwanamke. Unapokuwa unajisaidia haja ndogo,most of the tym lazima utakuwa umechuchumaa/umechutama(umesquat),haja ndogo yako inapokuwa inatoka,lazima kutakuwa na mabaki kidogo kidogo yatakurukia na kubakia kwenye lips za nje au za ndani za uke wako(labia majora or minora).

Hayo mabaki baada ya muda yatachanganyika na jasho(sweat) na kutengeneza harufu mbaya,kwa hiyo ili kujiepusha na yote haya,ni heri ukaosha uke wako kwa maji safi kila ukimaliza kujisaidia haja ndogo.

2. UKIWA UNAOSHA SEHEMU ZAKO ZA SIRI,TUMIA MTINDO(STYLE) WA KUPELEKA MKONO KUTOKA MBELE KURUDI NYUMA
Kuna baadhi ya wanawake teyari wameshazoea kusafisha sehemu zao za siri kwa kupeleka mkono kutoka nyuma kuja mbele.Huu mtindo sio mzuri kiafya kwa kuwa huko nyuma kuna Tigo (anus), na kwenye Tigo kumejaa uchafu na bacteria wengi tu.Sasa wakati unajisafisha,unapopeleka mkono nyuma unakuwa kama unazoa bacteria na uchafu kutoka kwenye Tigo,halafu ukauleta mkono mbele unakuwa unawaacha hao bacteria na uchafu kwenye uke wako. Na huo ndio mwanzo wa uke wako kutoa harufu mbaya na kupata infections za ajabu ajabu.

Ukitaka kuwa salama,haijalishi kuwa umemaliza kujisaidia haja kubwa au ndogo,au wakati unaoga,ukitaka kusafisha sehemu zako za siri,tumia mtindo wa kupeleka mkono mbele kurudi nyuma ili usije kuwaleta bacteria na uchafu wa Tigo mbele.

3. VAA NGUO ZA NDANI ZENYE ASILI YA PAMBA(COTTON)
Pamba(cotton) ina uwezo wa kupitisha hewa hata kama ni kidogo sana. Na sehemu za siri za Mwanamke zinahitaji flow ya hewa inayopita,nyingine iwe inaingia na nyingine iwe inatoka.Hii flow ya hewa hata kama ni ndogo itasaidia kufanya sehemu zako za siri kuwa fresh muda wote na utapunguza uwezekano wa uke wako kutoa harufu mbaya.

Na pia punguza kuvaa nguo za kubana sana muda wote,nguo za kubana zinasababisha majasho sehemu za siri na ukizingatia hamna flow ya hewa kwenye sehemu zako za siri basi lazima hayo majasho yataanza kutoa harufu mbaya.

4. USIVAE NGUO YA NDANI MOJA SIKU NZIMA
Kwa jinsi maumbile ya Mwanamke yalivyo,unatakiwa kubadili nguo ya ndani mara mbili au tatu kwa siku.

May b ulivaa nguo ya ndani asubuhi,ikifika mchana,ingia ladies room(bafuni/chooni),Vua Nguo yako ya Ndani,kisha unaweza ukaoga mwili mzima(which is better) au ukasafisha sehemu zako za siri.Nguo ya ndani uliyovua unaweza ukaifua(which is better) au ukaikunjakunja na kuiweka ndani ya kipande cha khanga au kitenge ndio uweke kwenye handbag yako ili kama ikitokea ukaopen handbag yako in public,watu wataona khanga au kitenge,hawatojua ndani umeweka nini.

5. PUNGUZA KULA VYAKULA VYENYE SUKARI AU YEAST KWA WINGI
Unaweza ukapunguza uwezekano wa kupata Yeast Infection au Bacteral Vaginosis kwa kuacha au kupunguza kula vyakula vyote vyenye sukari au yeast kwa wingi.

Vyakula hivyo ni kama vile vyakula vyote vinavyotengenezwa na hamira,pombe/bia n.k
Ukizidisha Vyakula au vinywaji hivi,ina maana utakuwa unazidisha yeast mwilini,na wakizidi kwenye uke utapata yeast Infection,mwisho wake uke wako utaanza kutoa harufu mbaya.

6. BADILI PADS ZAKO MARA KWA MARA UNAPOKUWA KWENYE SIKU ZAKO
Ili kuzuia uke wako usitoe harufu mbaya kipindi ambacho upo kwenye siku zako,inashauriwa kubadili ur pad mara kwa mara(may b after each 4 or 6 or 8 hours,it will depend how many pads can u afford per day) Kubadili pads mara kwa mara kunasaidia ujisikie upo comfortable,inazuia bacteria kujikusanya,inasaidia kupunguza uwezekano wa kupata infection na mwisho inaondoa uwezekano wa uke wako kutoa harufu mbaya.

7. NYOA (SHAVE) NYWELE ZAKO ZA SEHEMU ZA SIRI MARA KWA MARA
Nywele zako za sehemu za siri zinapokuwa ndefu,unakuwa umetengeneza maficho(hiding place) ya kila aina ya uchafu kuanzia jasho,majimaji yatakayokuwa yanakutoka ukeni ukiget aroused,mabaki ya haja ndogo n.k Ili kuepusha yote haya ni heri ukawa unazikata nywele zako za sehemu za siri mara kwa mara.

8. NENDA HOSPITALI MAPEMA NA HARAKA TENA SANA
Yaani hata usichelewe,kwani haya matatizo especially Bacteral Vaginosis na Yeast Infection ni matatizo ambayo yanaweza kutibika kwa dawa.Ni heri uwahi mapema ili uongeze uwezekano wa kupona haraka bila matatizo.

Samson Mwamanda Aliye Angua Kilio Baada ya Ally Mayay Kukosa Urais wa TFF Afunguka Makubwa

0
0
Beki wa zamani wa Yanga, Samson Mwamanda ametoa kali baada ya kuonekana akiangua kilio kisa Ally Mayay amekosa urasi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Tukio hilo lilitokea juzi jioni muda mfupi kabla ya matokeo ya uchaguzi wa TFF kutangazwa ambapo alionekana akilia nje ya ukumbi kutokana na kupata tetesi mapema za Mayay kushindwa katika kinyang’anyiro hicho mkoani Dodoma.

Mwamanda ambaye aliitumikia Yanga miaka ya nyuma akitokea Prisons ya Mbeya alipoulizwa sababu ya kutokea hicho alichokifanya alisema kuwa matokeo ya uchaguzi aliyapata mapema hivyo yalimuumiza roho hasa alipobaini kuwa Mayay ameshindwa.

Mwamanda amesema kuwa matokeo ya uchaguzi huo yalivuja na kumfikia kabla hata hatua ya kutangaza haijafika na kumfanya aumie baada ya kuonekana mgombea wake Ally Mayay ameshindwa.

"Nimeumia sana kusikia Mayay amepoteza uchaguzi huku watu wote wa mpira nao wakikosa nafasi zote hata zile za ujumbe hususani Julio (Jamhuri Kihwelo) aliyekuwa na sifa za wazi kupata nafasi hiyo.

"Mimi nilikuwa na nia ya kugombea ila kuna watu walinishauri na kuniambia niache kwani tayari walijua haya yatakuja kutokea, kwa kifupi mimi niwaambie tu mpira kama utaongozwa na watu wa kupangwa hatutapiga hatua yoyote hata siku moja," alisema.

Q Chief Amtusi TID...Adai Ana Matatizo ya Akili

0
0
Msanii Q Chief amemchana swahiba wake wa kipindi kirefu Khaleed Mohamed 'TID' kuwa ana matatizo ya akili na ndiyo maana anazungumza vitu ambavyo visivyomuhusu kwa jamii.

Q Chillah amebainisha hayo baada ya kuwepo na ugomvi miongoni mwao hivi karibuni ambapo TID alihojiwa na EATV kuhusu suala hilo akadai yeye hamfahamu msanii anayeitwa Q chief na wala hana urafiki naye.

“Mimi naona kama watu wazima kila mtu angeangalia na kupambana  na hali yake na kuangalia jinsi gani anaweza kurudi kwenye nafasi yake ya muziki, Kwa nini kila siku anizungumzie mimi nahisi kuna kitu special amekiona kwangu na hataki kuniambia hivyo atakuwa ana matatizo. TID ana matatizo ya kisaikolojia hivyo anatakiwa ajitathmini kiundani, kama mpaka waheshimiwa wameamua kumsaidia lazima aonyeshe muelekeo ili waendelee kuwa na imani na yeye", alisema Q Chillah.

Kwa upande mwingine, Q Chillah amesema hatopenda mambo ambayo ameimba kwenye tungo zake mbalimbali yaje kuwakuta watoto wake

Kwa sasa Q Chief anafanya vyema na wimbo wake mpya 'Naogopa' ambao ameuachia siku za karibuni.

Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo Tanzania

0
0
Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo East Africa (Atakuwa Nairobi,Mombasa,Uganda,Burundi,Rwanda na Sehemu Yoyote Atakayo hitajika.. Tanzania Atazunguka Mikoa Yote..)

AL_WATWAN MAFUSHO Ni Mtafiti wa Dawa za Mitishamba na ana uzoefu wa zaidi ya Miaka 18 katika kutoa Huduma zake.. Amesha toa Huduma zaidi ya Nchi 23 Duniani..
AL_WATWAN MAFUSHO Bado anaendelea Kupokea Salam na Shukrani nyingi kwa wale wote waliofanikiwa baada ya kupata HUDUMA na wale wanao Endelea Na TIBA MBALIMBALI..
      Anatibu kwa Kutumia Dawa za Asili ya Africa, Dawa za Kiarabu, Majini na QUR-AN Ukiwa Nchi yoyote...

Kwa Matatizo ya Fuatayo..
•Love spell
•Money spell casting
•Traditional Healer
•Protection Rituals
•Marriage Spells(to heal marriage problems and restore Affection
•Traditional bad luck Removal
•To Prevent divorce and bind lovers together

 MAGONJWA kama > Miguu kuwaka Moto na kufa Ganzi,Kuvimba tumbo,Kisukari, Ngiri ya ndani na Ngiri ya Nje(Busha) Chango kwa Kina Mama,Kifungua Kizazi kwa waliofungwa kishirikina)..Ulijari(Nguvu za kiume?
MAPENZI.Kumrudisha Mpenzi ndani ya Saa  12 tu.. Kumtuliza(Limbwata) Akusikilize na Akupatie chochote unacho hitaji kwa Wakati. Hutuliza wana Ndoa na na Kuzuia Talaka.. Kama Mpenzi wako Anaishi na Mtu mwingine Anao Uweza wa Kusambalatisha mahusiano yao ndani ya Nusu saa tuu(Mfarakano)...

MAFANIKIO.. Mali Bila Masharti, Bahati kwa Wachimba madini.. MAGIC WALLET, PETE ya Bahati, KUSHINDA BAHATI NASIBU na Kusafisha NYOTA(Nuksi Mikosi).. Umaarufu, Heshima mahala pa Kazi,Cheo kazini. Mafuta maalum Yenye Nguvu ya Ziada..
(Amesaidia Watu maarufu, Wachungaji na Wafanya Biashara wengi Duniani)
KINGA..Huzuia Kabisa Chuma Ulete na Kukupa Kinga ya Mwili na Biashara na Kujilinda na mali zako.Humaliza kabisa Kesi ndani ya siku 12 tu(Zindiko) nk..
PIA HUMALIZA KAZI ZILIZOACHWA AU KUSHINDIKANA....
Acha Kuhangaika Njoo Umaliziwe Tiba yako

AL_WATWAN MAFUSHO

Piga Simu +255 759 084 996

Moto wa Ajabu Wazua Taharuki Kwa Wakazi wa Kitunda.....

0
0
Moto wa ajabu unadaiwa kutokea katika nyumba moja iliyopo maeneo ya Kitunda jijini Dar es salaam na kusababisha taharuki kwa wakazi wa eneo hilo.

Kupitia kipindi cha Leo Tena ya Clouds Fm inadaiwa kuwa moto huo umekuwa ukiwaka kimaajabu katika maeneo tofauti katika nyumba hiyo ikiwemo chumbani na kupelekea kuharibu baadhi ya vitu uikiwemo nguo, na kusababisha wakazi wa nyumba hiyo kushindwa kulala.

Mwanamke wa nyumba hiyo aliyefahamika kwa jina la Mama Vicent ameeleza kuwa moto huo umekuwa ukiwaka kimazingira tofauti na kupelekea kuunguza sehemu hizo ikiwemo dirishani hadi kumaliza madirisha hayo licha ya kufanikiwa kuuzima.

Hata hivyo ameongeza kuwa aliporudi mumewe alimwambia lakini kesho yake ikatokea tena ambapo moto uliwaka katika moja ya kochi lao na kisha kuhamia katika makochi mengine na baadae moto huo ukahamia katika chumbani.

“Moto umekuwa unawaka mara kwa mara ikapelekea majirani kuhamia hapa nyumbani, mimi nikawa nalia nasema jamani ni fulani huyo kwa nini anaiambie hivyo, mkewe akawa anatoka anaenda kumwambia  mumewe kuwa nimemtaja mara moto huo unawaka,”amesema mwanamke huyo.

Pia ameongeza kuwa baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya ikabidi kuita wachungaji wa kanisani nyumbani kwake na kuombea nyumba hiyo ambayo imeteketea kwa moto pamoja na vitu ikaacha kuwaka moto.

Baraza la habari Tanzania (MCT) Walifufua Upya Sakata la Clouds TV na RC Paul Makonda

0
0
Baraza la habari Tanzania (MCT) Jumatatu hii limezindua ripoti mbili juu ya hali ya uhuru wa habari pamoja na tukio la uvamizi wa Kituo cha Clouds Media.


Ripoti hiyo iliyosomwa na mwanasheria mwandamizi Juma Thomas ambaye ni Mwenyekiti wa kamati iliyokuwa na watu wanne, amesema Kitendo cha Makonda kwenda kwenye kituo cha Clouds Media ni kukiuka na kinyume cha Huduma za vyombo vya habari ambapo ripoti hiyo imeweka wazi kuwa Makonda aliingilia uhuru wa Vyombo vya habari na Uhariri wa Habari.

Naye Katibu Mkuu wa MCT, Kajubi Mukajanga amesema tafiti hizo zinafanywa kama inavyoelekezwa na katiba ya baraza hilo.

“Ripoti hizi mbili zinalenga kuangalia hali ya vyombo vya habari kwa mwaka uliopita kwa maana ya hali ya kiuchumi, sheria, usimamizi,mafanikio pamoja na changamoto,”amesema.

Kuhusu sakata la Clouds amesema lengo la utafiti wa tukio hilo ni kutaka kujua kama lilisababisha athari juu ya uhuru wa habari pamoja na uhuru wa uhariri na si vinginevyo.

“Tafiti zimekuwa zikifanyika tangu mwaka 2001. Wakati alipouawa David Mwangosi tulituma timu ya watafiti, vilevile Serikali ilipozuia matangazo ya Bunge tulifanya tafiti. Kwa hiyo huu ni mwendelezo wa kazi za baraza hili,” amesema.

Amesema tafiti hizo zimehusisha timu ya wataalamu wa sheria, vyombo vya usalama pamoja na wanahabari.

Mke wa Roma Adai Hawezi Kurudia Tena Kujihusisha Kwenye Sanaa

0
0
Baada ya kufanya kazi kubwa ya kumuwakilisha mume wake katika kutambulisha wimbo wake mpya 'Zimbabwe' Mke wa Roma Mkatoliki , Nancy amefunguka na kuweka wazi kwamba hii ndiyo itakuwa kazi yake wa kwanza na mwisho kwani hana kipaji cha kazi ya sanaa.

Nancy amefunguka hayo wakati akifanya mahojiano na mwandishi wetu na kusema hana kipaji na uelewa mkubwa wa kazi za muziki lakini pia asingeweza kuacha kumsaidia mume wake katika kumuwakilisha kwenye vyombo vya habari ingawa ni kazi ambayo hadhani kama ataweza kuendelea nayo wakati mwingine.

"Siwezi kuendelea na hii kazi kwani mimi sina kipaji cha kazi hii kama usambazaji wa kazi hizi na idea ya muziki lakini kazi hii imekuja bahati mbaya na nimesimama kama muwakilishi na nimesimama kwenye hiyo nafasi" alisema Nancy

Aidha baada ya kuibuka maswali mengi kuhusu aina ya utambulishaji wa ngoma mpya ya msanii Roma Mkatoliki, Nancy amefunguka kwamba mumewe alishindwa kuacha kuachia wimbo huo kutokana na ukweli kwamba mume wake alishaweka maombi ya Interview kwenye vingi vya habari hivyo isingekuwa busara kutotokea.

"Alishaomba interview kwenye vyombo vya habari kwamba hii wiki atakuwa na kazi mpya lakini akapata safari ya ghafla kwenda huko Zimbabwe na kwa sababu kuanza ku - cancell hizi interview ni kazi kubwa sana hivyo imenibidi mimi nibebe jukumu hili na kulisimamia ili yeye atakaporudi aendelee mimi nitakapoishia".

Aidha Mke wa Roma ameongeza kuwa "Mapokezi niliyoyapata ni tofauti na matarajio yangu kwani mimi sipo sana katika mambo ya muziki kwa sana lakini mapokezi ni makubwa sana na wimbo umeshaanza kufanya vizuri.


EATV

Rais Wetu Aige Mfano wa Mwenzake Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya

0
0
Tumemsikia Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alipolihutubia Taifa lake baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa Kenya, kuwa anawaruhusu wafuasi wa mshindani wake mkuu kisiasa Raila Odinga kuwa wanaruhusiwa kuandamana na kuelezea hisia zao kwa kuwa hiyo ni haki yao ya kikatiba na akaliagiza Jeshi la Polisi la nchi hiyo liyalinde maandamano hayo na wala wasiwazuie wananchi hao kuandamana.

Nimejaribu kulinganisha kauli ya Rais wa Kenya na kauli ya Rais wetu nimeona zinatofautiana sana kama umbali wa kutoka duniani hadi mbinguni!

Tumeshuhudia hapa nchini kwetu Rais wetu akipiga marufuku mikutano yote ya kisiasa ya vyama vya upinzani hadi mwaka 2020 wakati akijiruhusu yeye mwenyewe na chama chake kuendelea na shughuli za kisiasa nchi nzima bila kubughuziwa na Jeshi la Polisi.

Tumewahi kumsikia Rais wetu wakati ule ambapo vyama vya upinzani waliopokuwa wakipanga maandamano waliyoyapa jina la UKUTA, Rais wetu alipiga mkwara mzito kuwa yeye hajaribiwi!

Tumeshuhudia nchini kwetu viongozi kadhaa wa vyama vya upinzani wakikamatwa na Jeshi la Polisi hata pale wanapofanya vikao vya ndani kwa kile ambacho kimekuwa kikiitwa tuhuma za uchochezi kwa kile ambacho Jeshi hilo limekuwa likidai ni maelekezo toka juu.........

Kama nchi yetu inaongozwa kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ambayo inaelezea kuwa nchi yetu ni ya mfumo wa vyama vingi na vyama hivyo vina Uhuru wa kufanya shughuli zao za kisiasa, sasa ni kwa nini Rais wetu anaamua kuivunja Katiba ya nchi yetu na kuamua kuendesha nchi yetu iwe kama ipo kwenye mfumo wa chama kimoja?

Dalili Sita Kwamba Unahitajika Kusitisha Uhusiano Hata Kama Bado Unampenda Kabla Mambo Hayajaaribika...

0
0
Dalili Sita Kwamba Unahitajika Kusitisha Uhusiano Hata Kama Bado Unampenda....
Maisha hayana kanuni maalum, waweza kujikuta unaingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na mtu wa ajabu kabisa na pia yawezekana mtu uliyotamani kuwa naye akakubali kuwa nawe lakini mambo yakaenda tofauti na yalivyokuwa matarajio yako. Yawezekana ikaonekana jambo la ajabu kutafuta ishara za kuachana na mpenzi wako japo kuwa bado unampenda, lakini uhusiano wa kimapenzi unaweza kukatishwa kutokana na sababu nyingi zaidi ya mwenza wako kuwa na mchepuko, na hizi ni ishara sita za kuanza kufikiria kukatisha uhusiano huo kama utaona zinajitokeza mara kwa mara.

1. Unapokuwa huna furaha

Moyo unataka unachokitaka na unataka upewe unachokitaka. Mara nyingine yawezekana moyo wako hauna haja na mpenzi wako wa sasa ambaye ni mzuri, mkarimu na mcheshi. Mara nyingine unachohitaji moyo wako ni kuachana na mpenzi wako ambaye ni mvivu, mbinafsi na katili. Haijalishi sababu ni nini, lakini jambo moja ni la kuzingatia sana: huna haja ya kuendeleza uhusiano wa kimapenzi na mtu kwa sababu tu hutaki kumuumiza.

2. Kama unataka kitu kingine tofauti

Kuwa na watoto. Kubadili kazi. Kuhama mji. Kununua nyumba. Maamuzi kama haya ni makubwa ambayo inabidi mkubaliane kuyafanya. Wapenzi walio tayari kuacha au kufanya jambo kwa ajili ya mwenzie huwa ni uhusiano wenye furaha. Hata kama unampenda mtu kiasi gani, mara nyingine maisha yanawaelekeza kwenye njia tofauti. Kama kweli unaitaka kazi uliyopata mji au nchi nyingine na mpenzi wako hataki kabisa uondoke, si lazima ukubali kwa ajili yake. Baadhi wanafikia muafaka lakini wengine hawawezi. Ikiwa hivi, hii ni ishara kwamba uendelee na mipango yako.

3. Kama kila muda unawaza kuachana naye

Huna haja ya kuwa na sababu. Kama kila mara unapata mawazo na fikra za kusitisha uhusiano wako, hata kama huna hakika sababu hiyo ni ipi, muda wa kuendelea na maisha yako umefika. Yawezekana ukaumia kwa kumuacha lakini pia yawezekana ukahisi umetua mzigo mkubwa uliokuwa unakuelemea. Hisia zote hizo ni za kawaida. Usijione kuwa ni mkosaji sana.

4. Hamfikii suluhisho la migogoro yenu

Mara nyingine unafanya kila jitihada kuwa katika uhusiano mzuri lakini mnajikuta mnagombana kwa mambo yaleyale. Au mna mgogoro mkubwa na kwamba kila mnavyojaribu hamfikii muafaka wa kuitatua na kusababisha kila zuri kwenye uhusiano wenu lisahaulike. Huwezi kumlazimisha mpenzi wako abadilike. Kama hamuwezi kupata muafaka wa tatizo lenu, au kama ni jambo linalohitaji mabadiliko makubwa ambayo hutaki kuyafanya basi yawezekana ni wakati muafaka wa kuanchana kabla mambo hayajaharibika zaidi.

5. Hupati unachohitaji

Watu wengine hawawezi mapenzi ya mbali. Wanahitaji kuwa karibu na wapenzi wao. Baadhi wanapenda kuwa na mpenzi mkimya, mwenye kujali na baadaye wanagundua kuwa hawawezi kuendelea na uhusiano na mtu wa aina hiyo. Wengine wanajikuta kwenye uhusiano na mtu ambaye anahitaji mambo tofauti kabisa na anayohitaji yeye.

Yawezekana mtu wa aina hii ndiye uliyekuwa unamhitaji lakini mwisho wa siku, kama mahitaji yako hayatimii yawezekana ufikiria kukatisha uhusiano huo. Ni sawa kujiweka mbele kwenye vipaumbele vya maisha yako.

6. Kama anakutesa

Hili ni jambo ambalo watu wengi walio kwenye uhusiano hawapendi kulizungumzia, lakini ni kawaida kabisa kujisikia vibaya baada ya kuachana na mtu ambaye alikuwa anakunyanyasa kiakili, kimwili au kimapenzi. Hilo halimaanishi kuwa unatakiwa kumng’ang’ania, inamaanisha unatakiwa kufikiria mambo mengine na kuendelea na masiha yako.

Kuachana na mpenzi ni jambo gumu, lakini ni gumu zaidi iwapo mtu unayeachana naye bado unampenda na kumjali. Kama umeshafikia uamuzi wa kuachana na mpenzi wako, jiamini mwenyewe na maamuzi yako, mara zote.

Dulla Makabila Adata na Penzi la Bongo Movie

0
0

Dulla Makabila Adata na Penzi la Bongo Movie
Msanii wa Singeli nchini Tanzania, Dullah Makabila anatarajia kufunga pingu za maisha na Husna Sajent ambaye ni muigizaji wa bongo movie hivi karibuni huku baadhi ya watu wakimshangaa Makabila kuamua uamuzi wa kutakumuoa mwanamke aliyemzidi umri.


Mipango hiyo ya Harusi ya Dullah imewekwa wazi na meneja wa Snura HK wakati akizungumza katika kipindi  cha eNewz kutoka EATV na kusema yeye kama mshenga anatamani kuona ndoa anayounganisha iweze kuleta matunda mazuri ya ndoa kwa kuzaa angalau watoto wawili na kuendelea.

"Kwa sasa nategemea kusimamia ndoa ya Bi. Husna na Dulla Makabila ambao wamekuwa katika mapenzi kwa muda mrefu sasa, natumaini ndoa yao itadumu kwa muda marefu tofauti na ilivyokuwa ndoa ya Nuh Mziwanda kwa kuwa ni watu wazima na wanapendana kweli", alisema HK.

Pamoja na hayo, HK amesema ameshangazwa sana kitendo cha kuvunjika ndoa ya Nuh Mziwanda ambayo yeye ndiyo alikuwa mshenga wake japo hakutaka kuweka wazi sababu ya kuvunjika kwa ndoa hiyo.

Kwa upande mwingine, HK amesema kilichotokea kwa Nuh Mziwanda hapendi kukiona tena kikiwatokea Dullah Makabila na mke wake mtarajiwa.

Kim Jong-un Akabidhiwa Mpango wa Kushambulia Guam

0
0




 Kim Jong-un Akabidhiwa Mpango wa Kushambulia Guam
Kiongozi wa Korea Kaskazini amepokezwa habari kuhusu mpango wa taifa hilo wa kutaka kurusha kombora hadi katika kisiwa cha eneo la pacific cha Guam kinachomilikiwa na Marekani kulingana na ripoti za vyombo vya habari.

Lakini ripoti hiyo imesema kuwa itachunguza vitendo vya Marekani kabla ya kuchukua hatua ya kurusha kombora hilo katika kisiwa cha Guam.

Wiki iliopita, Korea Kaskazini ilionya kwamba mikakati inawekwa kushambulia eneo ambalo ndege za kijeshi za Marekani zimekita kambi.
Kumekuwa na cheche za maneno kati ya Marekani na Korea kaskazini.

Ripoti hiyo ya kitengo cha habari cha KCNA ilisema kuwa Kim Jong un aliutazama mpango huo kwa muda mrefu na kuujadili na maafisa wakuu wa jeshi.
Kamanda wa jeshi la kimkakati la Korea Kaskazini sasa anasubiri agizo baada ya kuandaa shambulio hilo la Guam.

Lakini ripoti hiyo pia imeongezea kwamba kiongozi wa Korea Kaskazini atachunguza mienendo ya Marekani kabla ya kutoa uamuzi wowote, hatua inayoonekana kupunguza kasi ya cheche za maeneo kati ya mataifa hayo mawili.

Mwandishi wa BBC Yogita Limaye mjini Seoul anasema kuwa hatua hiyo itapunguza wasiwasi na kuzuia mgogoro wa kijeshi katika eneo la Korea.
Wanahewa wa Marekani wamepiga kambi katika kiswa cha GuamHaki miliki ya pichaREUTERS

Mwandishi mwengine ameongeza kuwa baada ya siku kadhaa za vitisho kutoka Pyongyang ,inaonekana kwamba rais Kim Jong Un sasa anataka kunyamaza na kutazama hali ,lakini katika taifa lenye siri kubwa kama Korea Kaskazini huwezi kuwa na hakika.

Wachanganuzi wanasema inamaanisha kwamba Pyongyang haiko tayari kutekeleza shambulio katika kisiwa cha Guam, kwa hivyo huenda inachukua muda.

Hatua hiyo inajiri baada ya waziri wa ulinzi nchini Marekani James Mattis kuonya kwamba shambulio lolote linaweza kusababisha vita vikali, na iwapo Pyongyang itarusha kombora kuelekea Guam basi ''itakuwa vita''.

Ameambia maripota kwamba Jeshi la Marekani litatetea taifa hilo kutoka kwa shambulio lolote wakati wowote na kutoka kwa taifa lolote.

Pia aliwahakikisha raia wa Guam ,ambapo kuna kambi za kijeshi za Marekani kwamba takriban watu 160,000 wanalindwa na akasema iwapo kombora litarushwa ''tutalitibua''.

Viewing all 104417 articles
Browse latest View live


Latest Images