Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104781 articles
Browse latest View live

Uwoya Apewa Mwaliko na Jaguar Kushuhudia Kuapishwa kwa Kenyatta

$
0
0


Uwoya Apewa Mwaliko na Jaguar Kushuhudia Kuapishwa kwa Kenyatta
Msanii wa filamu za kibongo Irene Uwoya ambaye hivi karibuni amekuwa gumzo baada ya sakata la ndoa yake kuwekwa wazi na mumewe Hamad Ndikumana huku akimtuhumu kuwahi kuwa na mahusiano na msanii kutoka Kenya Jaguar.


Hivi karibuni msanii Jaguar ameshinda ubunge wa jimbo la Starehe kwenye uchaguzi mkuu nchini Kenya, na kukawa na tetesi kwamba Irene Uwoya amealikwa kushuhudia kuapishwa kwa Rais Uhuru Kenyata huku mualiko huo ukitolewa na Jaguar.

Akizungumza na mwandishi wetu Irene Uwoya amekiri kupewa mualiko huo na kusema kama atapata nafasi atahudhuria sherehe hizo, lakini aligoma kufunguka kama kweli ana mahusiano na msanii Jaguar.

"Kwanza huwa sipendi masuala ya mahusiano yangu kuweka wazi kwenye vyombo vya habari, na kuhusu kwenda Kenya nikapata nafasi nitahudhuria nimepewa mualiko, lakini kwa sasa nashoot hivyo nikipata nafasi nitahudhuria", alisema Irene Uwoya.
Sherehe za kuapishwa kwa Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyata zinatarajiwa kufanyika tarehe 29 mwezi huu nchini Kenya, zitakazohudhuriwa na mamia ya wananchi wa Kenya.


Aden Rage: Yanga Jiandaeni kwa Kichapo Kitakatifu Mechi ya Ngao ya Jamii....Tupeni Tuu Hiyo Ngao Bila Mechi...

$
0
0
Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage ameitaka timu ya Mabingwa wa ligi kuu Tanzania Bara Yanga, wajiandae kupokea kichapo kitakatifu katika mechi ya Ngao ya Jamii itakayochezwa mnamo Agosti 23 mwaka huu katika uwanja wa Taifa.

Aden Rage amefunguka hayo ikiwa zimebaki siku chache kuanza kwa mtifuano huo huku akiwashangaa wanayanga kwa uwamuzi waliyoufanya kuenda kujificha mjini Pemba.

"Kama mimi ningekuwa kiongozi wa Yanga tarehe 23, ningesema hiyo Ngao ya Jamii wazee chukueni maana kila nikiangalia pale wa kumzuia Emmanuel Okwi, John Boko sioni, sasa Haruna Niyonzima naye zile majaro anazozitupa zinaleta raha, kwa hiyo nina uhakika tarehe Agosti  23, al manusura kama wamepata bahati watakula 7, sasa wanakuja kukutana na Simba. Sisi huko nyuma hatujapata ubingwa muda mrefu ni sawa sawa na Simba aliyejeruhiwa ukikukuta naye njiani hana msalie Mtume lazima akumalize tu. Na sijui wameenda Pemba kufanya nini, labda wanaenda tu kuchuma karafuu,” alisema Ismail Rage

Pamoja na hayo, timu ya Simba na Yanga zote kwa pamoja zimekimbilia mjini Zanzibar kwa lengo la kujiweka sawa kuelekea mtanange huo wa kukata na shoka ambao mpaka sasa kila mmoja anamtambia mwenzake kumfunga kutokana na ubora wa usajili waliyofanya katika msimu mpya wa

Jackline Wolper Amshushia Povu Madee na Techo Kwa Kutengeneza Katuni Inayofanana na yeye Kwenye Wimbo wao Mpya

$
0
0
Muigizaji wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper  hajapenda kitendo cha msanii mwenzake kumtengezea katuni aliyoitumia katika video yake bila makubaliano  na hivyo kamvaa na kumpa ONYO Kali.

Kupitia amtandao wa Instagram Wolper ameandika maneno yanayoashiria kukerwa na kitendo hicho cha msanii wa muziki, Madee a.k.a Rais wa Manzese na kumtaka msanii huyo awasiliana naye endapo atahitaji kufanya biashara hiyo.

"Embu ona jamani macho natia huruma kama na upwiro kilo 200 …hii mikaka yetu yakibongo kuna mida inaboa kuna mida inakuwa powa ..sasa Madee Rais wamnzese nikuulize swali…ulishindwa nini kunyanyua ka cm kako nakunipgia ata kinafk nakunambia unanivdio queen katuni sjui sanam unajua wewe…." Ameandika Wolper na kuongeza;

"Acha dharau wewe pumbavu piga cm omba kwanza….ata kma umlipi m2 sisi tunasaidiana wote wasanii leo kwangu kesho kwako,🙄👉. nakunishika kimahaba umenishika una dhambi wewe kaka na suit umenivalia kma unaenda kutoa posa kwa masawe🙄..sasa onyooo siku nyingne ombaga utapewa acha kuparamia kama vile unaomba round kwa kimada wako kwanza unitafute utoe ata faini ya kuniweka macho kama nimevuta ugoro…ila nyimbo kali nisiwe mchoyo nanimependa idea ila mwambie alinichonga nakunipa hyo shepu nitampasua 🙄"

Madee alitumia sura ya Wolper katika video yake mpya ‘Sikila’ ambayo amemshirikisha Tekno kutoka nchini Nigeria.

Shilole Amwaga Chozi Kisa Barua Hii Aloandikiwa na Mtoto Wake

$
0
0


Shilole Amwaga Chozi Kisa Barua Hii Aloandikiwa na Mtoto Wake
Mwimbaji wa Bongofleva Shilole kupitia Instagram yake ameelezea hisia zake juu ya kilichomtoa machoni baada ya kuisoma barua aliyoandikiwa na binti yake wa pili Rahma aliyoiandika kwa lugha ya Kiingereza.

Shilole baada ya kusoma barua hiyo aliamua kuandikia ujumbe ulioashiria hisia za furaha hadi kumtoa machozi akiamini kuwa amemkuza binti huyo kwa sababu ya umri aliokuwa nao hakudhani kama angeweza kuandika maneno yenye ujumbe mzito wa aina hiyo.

Shilole ameandika>>>>”Rahma binti yangu umeniliza na hii barua yako. Siamim km Mungu amenikuzia kiasi hiki mpk leo katoto kangu ka pili kananiandikia maneno mazito hivi. Nakupenda sn mwanangu wewe na dada yako ndio urithi wangu na furahayangu….Nikivurugwa hukoo na ya ulimwengu nikitud nyumban nyio ndio faraja yangu.

“Simkufuru Mungu kwa kuishi maisha ya shida niliyopitia, sisikitiki kwa kukosa elimu bora na kutimiza ndoto zangu nyingi nilizokuwa nazo nachojua MIPANGO YA MUNGU SIO KAMA YA MWANADAMU….Namshukuru kwa kila alichonipa, jina, umaarufu, rizki, marafiki na ndugu wa kweli lkn zaidi WATOTO wangu ambao kila iitwapo leo ndio mnanipa nguvu ya kuamka kupambana kuvumilia matusi vikwazo na kila vipingamizi. Nataka msome mtimize mdoto zenu nizeeke nikiona mnakuwa mabinti wa kuigwa na mumpendeze Mungu na wanadamu.

“KAMA KUNA JAMBO NINAJIVUNIA KULIFANYA SAHIHI DUNIANI NA SIJAWAHI LIJUTIA NI MIMI KUKUBALI KUWA MAMA. By the way ndugu zangu sijui kidhungu nimekielewa vizur.” – Shilole.



Mke wa Mugabe Kufikishwa Mahakamani Afrika Kusini

$
0
0

Mke wa Mugabe Kufikishwa Mahakamani Afrika Kusini

Mama Mugabe alikamatwa jana na alikuwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo kwa kosa la kumshambulia mrembo huyo anayedaiwa kuwa ni mpenzi wa mtoto wake.
Johannesburg, Afrika Kusini. Grace Mugabe, ambaye ni mke wa Rais Robert Mugabe aweza awe amewafanyia ubabe watu kadhaa nchini kwake lakini kitendo cha kumshambulia, kwa waya wa umeme, mrembo mwenye umri wa miaka 20 kimemweka matatani.

Mama Mugabe alikamatwa jana na alikuwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo kwa kosa la kumshambulia mrembo huyo anayedaiwa kuwa ni mpenzi wa mtoto wake.

“Imeandikwa katika mitandao mingi ya kijamii kwamba mrembo wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 20 inadaiwa alishambuliwa na mwanamke mmoja maarufu katika Hoteli ya Sandton mjini Johannesburg,” msemaji wa polisi Vish Naidoo alijibu vyombo vya habari kwa baruapepe. Mrembo huyo jana Jumatatu, “alileta malalamiko ya kushambuliwa kwa lengo baya la kudhuriwa mwili.”

Naidoo alikataa kutaja jina la mtuhumiwa kwa sababu alikuwa hajafikishwa mahakamani

Lakini Waziri wa Mambo ya Ndani, Fikile Mbalula amemtaja mwanamke huyo kuwa ni Grace Mugabe na kwamba alijisalimisha polisi.

"Anashikiliwa na polisi kwa sababu alitoa ushirikiano, na akajisalimisha yeye mwenyewe,” Waziri wa Mambo ya Ndani, Fikile Mbalula aliliambia jana shirika la habari la eNCA.  Fikile alisema Grace anatarajiwa kufikishwa kortini Jumanne

Waziri huyo alisema Grace lazima ajibu mashtaka dhidi yake maana yeye waziri hawezi kwenda Zimbabwe, akampiga mtu na akatarajia suala hilo litafunikwa chini ya zulia.

Chama tawala cha Zimbabwe, Zanu-PF kilisema kwa ujumbe wa Twitter kwamba Grace “alishambuliwa” lakini wanashukuru kwamba “ni mzima na yuko salama”. Hakukuwa na maelezo ya kina.

Zanu PF walituma ujumbe mwingine tena wakisema Mama Mugabe anaendelea vizuri baada ya kwenda Afrika Kusini kutibiwa kifundo cha mguu




Shamsa Aford Ampongeza Rais Magufuri kwa Kubana Matumizi

$
0
0




Shamsa Aford Ampongeza Rais  Magufuri kwa Kubana Matumizi
Muigizaji wa Filamu Bongo, Shamsa Ford ameonekana kuvutiwa zaidi na sera ya Rais Dkt. John Magufuli ya kubana matumizi.



Kupitia mtandao wa instagram Shamsa ameeleza kuwa kutokana na utaratibu huo wa Rais Dkt. Magufuli kila kijana kwa sasa anafanya kazi kwani hapo awali wengi wao walipenda vya kupewa.

Tunalalamika maisha ni magumu sana labda kwakuwa hatujazoea hii hali..Ila mm nakupongeza sana raisi wangu kwa kazi unayoifanya. kwanza umetusaidia vijana kuwa wabunifu kila siku.Tulikuwa tumezoea kupewa tu na kazi hatufanyi ila kwa sasa naona kila kijana anafanya kazi kwa bidii na kuheshimu pesa vizuri.Hii itasaidia hata kwa uchumi wa nchi kukua kutokana na kwamba kila kijana anafanya kazi kwa bidii..Mungu akubariki sana Raisi wangu na azidi kukulinda kwa kila mwenye nia mbaya na wewe #UZALENDOKWANZA#

Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambao ulimuweka madarakani Rais Dkt. Magufuli, Shamsa alikuwa akimpigia debe Edward Lowassa ambaye alikuwa akiungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa.

Watuhumiwa 13 CUF Watoka Nduki Mahakamani Wakihofiwa Kukamatwa Tena

$
0
0

Watuhumiwa 13 CUF Watoka Nduki Mahakamani Wakihofiwa Kukamatwa Tena
Wanachama 13 wa Chama Cha Wananchi (CUF) kinachoongozwa na Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na msajili wa Vyama Vya Siasa Profesa Lipumba wametoka nduki mahakamani baada ya kesi yao kufutwa.

Watuhumiwa hao 13 wamekimbia ndani ya Mahakama wakihofia kukamatwa tena baada ya hakimu kuondoa kesi yao mahakamani hapo leo, Wakili wa watuhumiwa hao Bw. Hashimu Bakari amesema kuwa kesi inapofutwa ina maana kuwa mtuhumiwa hana hatia yoyote na anatakiwa kuondoka na kurudi zake nyumbani.

"Ndani ya miezi sita iliyopita kila tukija mahakamani kwa kila mwezi upande wa Jamhuri na upande wa DPP wanasema upelelezi umekamilika wanakuja na hoja za awali lakini hoja hazisomwi kwa hiyo mahakama tukufu 225 kifungu kidogo cha kwanza na vifungu vinavyofuata kuifuta kesi kwa sababu kesi inatakiwa kuanza kusikilizwa baada ya siku sitini tangu upelelezi kukamilika lakini hii kesi ilianza toka mwezi wa 11, mwaka 2016 mpaka leo haijaendelea sasa kesi imefutwa" alisema Wakili Hashimu

Aidha Wakili huyo anasema kesi kufutwa tafsiri yake ni kwamba watu wako huru na wanaweza kwenda nyumbani
"Kwa nchi za kidemokrasia tafsiri ya kesi kufutwa maana yake ni kwamba mshtakiwa hana kosa yupo huru anatakiwa kurudi nyumbani kuendelea na mambo mengine ya ujenzi wa taifa, kama kuna utaratibu mwingine wa Jamhuri kumkamata mtuhimiwa unafuata kama ilivyokuwa katika kesi ya awali " alisema Wakili Hashimu

Wafuasi hao wa CUF wameachiwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa chini ya kifungu cha 225 cha Sheria ya Makosa ya Jinai lakini kifungu hicho kinaruhusu upande wa mashtaka kuwakamata tena washtakiwa pale wanapoona inafaa, watuhumiwa hao waliona wakimbie kuepuka kukamatwa tena jambo ambalo baadhi ya polisi na magereza walionekana kuwadhibiti watuhumiwa hao ili waweze kuwakamata tena.

Rais wa Misri Ampongeza Rais Magufuli kwa Kupambana na Rushwa na Ufisadi

$
0
0



Rais wa Misri Ampongeza Rais Magufuli kwa Kupambana na Rushwa na Ufisadi
Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri amesifu ushirikiano kati ya taasisi za Tanzania na Misri zinazoshughulikia mapambano dhidi ya rushwa na kumpongeza Rais John Pombe Magufuli kwa kuonesha mfano wa uongozi bora unaopambana na maovu katika nchi yake.

“Nampongeza Rais Magufuli kwa jitihada zake za kupambana na rushwa na ufisadi na huo ni mfano wa sifa za uongozi bora” alieleza Rais Al Sisi wakati akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam.

Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Tanzania (TAKUKURU) na Taasisi ya Udhibiti wa Utawala ya Misri (Administration Control Authority of Egypt) zimekuwa na ushirikiano wa karibu kwa kubalidilishana utaalamu, uzoefu na mbinu katika kutekeleza majukumu yao.

Katika mkutano, huo ambao uliofanyika mara baada ya kumalizika mazungumzo rasmi kati ya nchi hizo, Rais Al Sisi alieleza dhamira ya nchi yake ni kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuunga mkono jitihada za kuleta amani barani Afrika na kuendelea kuwa na msimamo mmoja katika masuala ya kimataifa.

“Tunampongeza Rais Magufuli na Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika kutafuta amani barani Afrika hasa katika eneo la Maziwa Makuu” Rais Al Sisi alisema na kumpongeza Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kwa jitihada zake za usuluhishi katika mgogoro wa Burundi.

Rais huyo ambaye alikuwa nchini kwa ziara rasmi ya siku mbili, ameeleza kutambua mzigo mkubwa inaoubeba Tanzania katika kushughulikia migogoro ikiwa ni pamoja na kuhudumia maelfu ya wakimbizi kutoka katika nchi mbalimbali.

Katika mkutano ambao ulihutubiwa pia na mwenyeji wake Rais Magufuli, Rais huyo wa Misri alieleza utayari wa nchi yake kuendeleza na kuimarisha uhusiano wake na Tanzania kwa kuhimiza kubuni na kutekeleza miradi ya pamoja, kuongeza biashara na uwekezaji pamoja na kubadilishana wataalamu.

”Misri na Tanzania hatma yao ni moja,  tutaendelea kushirikiana kwa hali na mali na kwa kuwa tuna dhamira, matumaini yetu makubwa ni kufanikiwa” Rais Sisi alisisitiza.

Kabla ya mkutano huo na wanahabari, Rais wa Misri alikuwa na mazungumzo ya faragha na mwenyeji wake Rais Magufuli na baadae kuhudhuria mazungumzo rasmi ya mashauriano kati ya Tanzania na Misri.

Odinga Ashindwa Kuanika Namna Alivyoibiwa Kura

$
0
0
Odinga Ashindwa Kuanika Namna Alivyoibiwa  Kura
Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) umeahirisha kikao cha kutoa tangazo kuhusu mweleko wa chama hicho kufuatia uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Kiongozi wa muungano huo Raila Odinga alikuwa ameahidi kwamba angetangaza ni hatua gani atachukua leo baada ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa Ijumaa, ambapo mpinzani wake Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi.

Ajenti mkuu wa Nasa Musali Mudavadi amesema sasa muungano huo unapanga kutoa tangazo keshi Jumatano.
"Tunasikitika kwamba mashauriano yanachukua muda mwingi kuliko ilivyotarajiwa na Nasa kwa hivyo hawataweza kuwahutubia Wakenya kama walivyotarajia leo."

Bw Mudavadi hata hivyo amesema mashauriano "yanaendelea na yanaendelea vyema".
Hapo jana, Bw Odinga alikuwa ametoa wito kwa wafuasi wake kususia kazi kabla ya kutoa tangazo kubwa leo.

Watu wengi hata hivyo walionekana kupuuza wito wa kususia kazi.
Baada ya kutokea kwa maandamano katika baadhi ya maeneo ambayo ni ngome ya upinzani mitaa ya Mathare na Kibera jijini Nairobi na mji wa Kisumu, hali ya utulivu ilianza kurejea Jumatatu.

Mawakili Kesi ya Wema Wapinga Ushaidi wa Bangi

$
0
0
 





Mawakili Kesi ya Wema Wapinga Ushaidi wa Bangi
Wakili wa mrembo Wema Sepetu, Tundu Lissu  amepinga kupokelewa kwa kielelezo cha ushahidi wa msokoto mmoja na vipisi 2 vya bangi Mahakamani, vinavyodaiwa kukutwa nyumbani kwa Wema Sepetu.

Lissu amepinga kielelezo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya Wakili wa Serikali, Costantine Kakula kumuongoza shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka, Mkemia kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Elias Mulima.

Aidha, Lissu amedai kuwa kielelezo cha ushahidi kisipokelewe kwa sababu ndani ya bahasha yenye ushahidi kuna vitu zaidi ya msokoto mmoja na vipisi viwili vinavyodaiwa kuwa ni bangi akisema vipisi 2 vyen

Amba Lulu Akili Kujichubua na Awatolea Povu Wanaomsema

$
0
0


Amba Lulu Akili Kujichubua na Awatolea Povu Wanaomsema
Video queen aliyeikacha fani yake na kuzamia kwenye muziki wa Bongo Fleva, Amber Lulu amekiri kuwa anajichubua rangi ya ngozi yake na kuwatolea mapovu wanaomsemasema kuhusu ishu hiyo.
Staa huyo anayetamba na ngoma yake ya Watakoma, aliyomshirikisha mkali wa Hip Hop Bongo, Country Boy, amewatolea mapovu watu wenye tabia ya kuchukua picha zake za miaka ya nyuma na kuzifananisha na za sasa, kisha kumsema kuwa anajichubua.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, amejibu mapigo kama ifuatavyo:
“Pale unapoona watu mapovu kibao ooh mweusi sasa na wewe si ujichubue. Au huna hela za kiduka cha usiku? Maisha ni mafupi sana.
“Mimi na feki, sasa mbona mnani-follow mna-like tena kuiga ndo msiseme, muulize tu Amber unatumia mkorogo gani, maana sio kwa mabadiliko hayo.
amber lulu

“Mimi napambana na tube zangu, pambana tu na wewe na hali yako. Kujichubua nijichubue mimi hasira upate wewe duh! Unazionea huruma pesa zangu wakati natafuta kwa jasho langu, kivipi.

“Na mwisho wake haimhusu mtu ngozi yangu pesa yangu mikono yangu naupaka vizuri maisha yangu.
Na hizo TBT ni za kitoto hapo nimekuwa mtu kabisa ngoja niwape kiboko kabisa sasa.

“Siogopi kwa sababu ndiyo mimi ndipo nilipotokea na ndivyo nilivyo kuwa wewe.
Tena sasa hivi nataka wa Kiarabu niwe Mhindi kabisa Waarabu nicheki Dm nizidi mie,” ameandika Amber Lulu.

Fid Q Asema 'Zimbabwe' ya R.O.M.A Utakuwa Wimbo Mkubwa kwa Mwaka Huu

$
0
0


Fid Q  Asema 'Zimbabwe' ya R.O.M.A Utakuwa Wimbo Mkubwa kwa Mwaka Huu
Rapa Fareed Kubanda 'Fid Q' amefunguka kuhusiana na wimbo mpya wa Roma Mkatoliki 'Zimbabwe' na kudai kuwa msanii huyo amejua kukamata hisia za mashabiki kwa kuimba ukweli uliyomtokea miezi michache iliyopita huku akimsifu ndivyo hip hop unavyotaka.

Fid Q amesema kuwa Zimbabwe ni wimbo uliyokuja kufanya mapinduzi makubwa kwenye 'industry' ya hip hop kwa mwaka 2017 pia kuutaja kuwa huwenda ukawa ndiyo wimbo mkubwa kwa mwaka huu.

"Roma kajua kuteka hisia za mashabiki zake, Zimbabwe ni wimbo mkubwa sana kuwahi kutokea mwaka huu ukizingatia. Umevunja rekodi ndani ya siku moja kwenye Youtube. Alichokifanya Roma ndicho hip hop inachotaka, hakuna mtu ambaye alikuwa hajui kama Roma katekwa na watu walikuwa wakimsubiri kuona anarudi vipi kwa hiyo nampongeza kwa kuwa amezingatia kiu ya mashabiki zake", alisema Fid Q.

Kwa upande mwingine, Fid Q amewataka wasanii kufanya kazi zilizokuwa na ubora na zitazoishi muda mrefu na siyo kukimbilia kolabo za kimataifa ambazo hazitawasaidia kufika mbali kama jinsi wanavyotaka.
Kwa sasa Fid Q anatamba na ngoma mbili alizoziacha ambazo ni 'Ulimi mbili pamoja Fresh'

Mrema Afichua Siri..Kumbe Alikuwa Akiugua Kansa na Magufuli Ndio Amemsaidia Mpaka Akapona....

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Msamaha kwa Wafungwa (Parole), Augustine Mrema ametoa shukrani zake kwa Rais John Magufuli kwa kumsaidia kupata matibabu nchini India na kufanikiwa kupona ugonjwa wa kansa.

Mrema alisema kwa sasa utendaji wake wa kazi utaimarika kwa kuwa ameshapona ugonjwa uliokuwa ukimsumbua na kushindwa kutumikia wananchi na Taifa.

Akizungumza mbele ya waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Mama Mwokozi jijini Dar es Salaam, alisema kuanzia sasa atamsaidia vizuri Rais katika nafasi yake ya kuwatetea wafungwa kupitia msamaha wa Bodi ya Parole.

Alisema amefikia hatua ya kutoa shukrani kwa sababu ya muujiza aliopata kutoka kwa viongozi wa Serikali na dini waliomuombea.

Paroko Kiongozi wa kanisa hilo, Cathbert Magaga aliwataka waumini wengine kuiga mfano wa Mrema wa kutoa shukrani na siyo kunyamaza kwa kuwa Mungu atawasaidia.

Video Jinsi Wanachama wa CUF Walivyoachiwa Mahakani Kisutu na Kutimua Mbio Kuhofia Kumatwa Tena....

$
0
0
Jeshi la Polisi na Maofisa Magereza leo August 15, 2017 lililazimika kutumia nguvu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili kuwadhibiti wafuasi na wanachama 13 wa Chama cha Wananchi CUF walioachiwa huru.

Wafuasi na wanachama hao wameachiwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa chini ya kifungu cha 225 cha Sheria ya Makosa ya Jinai.

Hatua ya Polisi na Magereza kuwadhibiti wafuasi hao inatokana na kifungu hicho cha sheria kuruhu upande wa mashtaka kuwakamata tena washtakiwa pale wanapoona inafaa ambapo haikujulikana ni washtakiwa wangapi waliokamatwa kwa sababu wengi wamekimbia.

VIDEO:

Madaktari wa Serikali Wanaojiongezea Kipato Kwenye Hospitali Binafsi Kukiona...

$
0
0
Serikali inatarajia kutoa mikataba ya uwajibikaji kwa waganga wakuu wa mikoa, wilaya na waganga wafawidhi wa hospitali zote nchini ifikapo mwezi ujao na ambayo itadhibiti wale wanaojikita zaidi katika hospitali binafsi kwa ajili ya kutafuta kipato cha ziada.

Kwa mujibu wa mikataba hiyo, daktari atakayeshindwa kufikia malengo atakuwa amejiachisha kazi mwenyewe.

Akizungumza na Nipashe juzi, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Dk. Zainabu Chaula, alisema lengo la mikataba hiyo kwa waganga wakuu wa mikoa, wilaya na waganga wafawidhi wa hospitali ni kuboresha huduma za afya kwa kuwa haziridhishi.

“Huu mkataba utakuwa ni kwa kila mwaka, lakini sio wa kutishana na wala sio jambo jipya ni la kawaida… tunachotaka ni uwajibishaji,” alisema Dk. Chaula.

“Tunatamani uanze kutolewa Septemba mwaka huu (mwezi ujao), hivyo tutawaita, ili kuwajulisha kuhusiana na hili kwa kuwa kutakuwa na kikao mwezi huu.”

Dk. Chaula alisema kwa madaktari wanaofanya kazi katika vituo vingine vya afya huku majukumu yao waliyopangiwa na serikali wakiyaacha watadhibitiwa na mkataba huo.

“Hapo ndipo tutaondoana,” alisema Naibu Katibu Mkuu (Tamisemi) huyo. “Mtu anaacha kuona wagonjwa, anaenda kwenye kliniki yake (binafsi) anapata pesa na huku nako anadai fedha.”

“Mimi nimesomea udaktari (na) ninafanya kazi zangu kwa uadilifu, nilitamani wote wawe kama mimi.

“Sasa mtu akienda kinyume siwezi kumuacha.

“Tunachokitaka ni huduma za afya ziwe bora.”

Dk. Chaula alisema mkataba huo umeshaandaliwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, isipokuwa kuna baadhi ya vipengele vya kufanyia maboresho.

“System (mfumo) ya (wa) mkataba huo ni hivi… mimi nafanya kazi na Katibu Mkuu ndiye anayeniangalia utendaji wangu, Katibu Mkuu anakuwa na Waziri,” alisema Dk. Chaula.

“Mkurugenzi wa Tamisemi atakuwa karibu na waganga wakuu wa mikoa 26. Sasa mganga mkuu wa mikoa anaingia mkataba na waganga wakuu wa wilaya; hivyo kila mtu anamshika mwenzake.

“Hivyo mganga mkuu wa mkoa hawezi kukubali kuangushwa na mganga mkuu wa wilaya.

“Mfano waziri ameibua jambo kwenye halmashauri hapo anayewajibika ni mganga mkuu wa mkoa (kwamba) kwa nini hajawajibika?”

Alisema lengo la mkataba huo ni kila mmoja kutimiza wajibu wake bila kutumwa na kutakiwa kujitathmini mwenyewe.

“Mimi nimeteuliwa kwenye eneo la afya hivyo siridhiki na huduma, natamani ziwe nzuri (na), ili ziweze kuwa nzuri tukaona tupeane mikataba, ili kila mtu atimize majukumu yake,” alisema zaidi Dk. Chaula.

“Ndiyo maana tunataka kuwekeana malengo mahususi nikikuambia uniletee taarifa tarehe tano, ni lazima niipate tarehe tano. Usipoileta ina maana utakuwa una shida.
“Yaani nikitaka kitu fulani kikamilike kwa wakati na wewe hujafanya hivyo ina maana hujawajibika.

“Ifike wakati ukiona hujafanya vizuri katika nafasi yako uone hiyo nafasi hustahili, utajiengua mwenyewe… huko ndipo tunakoelekea.”

Dk. Chaula alisema kuwekwa kwa mkataba huo kutasaidia kupatikana kwa mabadiliko katika huduma za afya, ambayo kwa sasa hayawezi kuonekana kwa kuwa hali ilikuwa tete.

“Huu mkataba ni kila mwaka.

“Yaani kwenye mwaka wa fedha tunasimama na kuangalia je, umetimiza majukumu yako? Kama hujakamilisha majukumu yako utashuka, mwingine atapanda.”

MKATABA MWINGINE
Mganga Mkuu wa Mkoa mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alieleza Nipashe kuwa suala hilo la mkataba lilijadiliwa katika mkutano mkuu wa mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya uliofanyika mkoani Dodoma mwezi uliopita.

Alisema wametakiwa kufanya kazi kwa malengo na kuonyesha mikakati ambayo wataitekeleza katika kipindi hicho, hivyo kama daktari hatofanya vizuri, uwezekano wa kupatiwa mkataba mwingine ni vigumu.

“Sisi kila siku tunatakiwa kufanya kazi kwa malengo,” alisema.

“Kwa mfano unasema mimi kwa safari hii nitahakikisha vituo kadhaa vinakamilika, nitahakikisha kutakuwa na upatikanaji wa dawa kwa asilimia 100, ndio malengo yenyewe ambayo tunajiwekea.”

Alisema mfumo huo umepitishwa katika mkutano huo kwa ajili ya watendaji wote – waganga wafawidhi wa hospitali, waganga wakuu wa wilaya pamoja na wa mikoa.
Alisema kwa sasa wanasubiri maelekezo ya serikali namna ambavyo watasaini mkataba huo.

“Tunangoja maelekezo namna ambavyo tutasaini (maana) kwa mfano mimi kama mganga mkuu wa mkoa, naingia mkataba na mganga mkuu wa wilaya,” alisema.

“Lengo la serikali ni kuona huduma za afya zinakuwa bora; yule atakayeshindwa kutekeleza mikakati yake hatapatiwa mkataba (mpya).”

Alisema jambo hilo ni nzuri, tatizo lipo kwa watendaji wavivu wanaoweza kuuchukia mfumo huo.

“Serikali ya sasa inataka tufanye kazi kwa kujituma na kuweka uzalendo mbele kwa wale wanaofanya kazi kwa kusuasua ama wale wenye mikataba na hospitali nyingine wanaweza kuuchukia huo mfumo ila kwa mimi sioni kama kuna tatizo,” alisema.

Chanzo: Nipashe

Mytake:
Ukiona mwenzio ananyolewa wewe tia maji , udaktari usio na mipaka kwaheri !

Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia...

$
0
0
Jeshi la polisi Mkoa wa Ilala, limewakamata watu saba akiwemo msanii wa muziki wa kizazi kipya, Rashid Makwiro maarufu kama ‘Chid Benz’ kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroine.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amesema watuhumiwa hao walikamatwa Agosti 12 mwaka huu saa 11.50 jioni wakijihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya.

Amesema jeshi la polisi limefanya msako wake na kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa katika eneo ambalo linajihusisha na uuzaji wa dawa hizo.

“Chid Benz na wenzake wapo kituo cha Polisi cha msimbazi ambapo tunaendelea na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani na kiasi cha dawa zilizokamatwa zimepelekwa kwa mkemia mkuu na itajulikana ni kiasi gani za dawa za kulevya zilizokamatwa,”amesema Hamduni.

Hamduni amesema jeshi hilo linafanya msako liweze kubaini mtandao mzima unaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na watumiaji ili kuhakikisha wote wanachukuliwa hatua na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Itakumbukwa kuwa , Oktoba 24,2014, Chid alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jiji la Dar es Salaam akiwa na dawa za kulevya, akijaribu kuvuka nazo kwenda mkoani Mbeya kushiriki onyesho la Instagramu Party wakati akijua kuwa ni kinyume cha sheria .

Msanii huyo wa kizazi kipya alikiri shtaka hilo na ndipo , Februari 26 mwaka 2015, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilipomhukumu kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh900,000 baada ya kupatikana na hatia ya katika makosa matatu likiwemo la kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi na Heroine yenye thamani ya Sh 40,358.

Hata hivyo msanii huyo alifanikiwa kulipa faini na kukwepa kifungo hicho.

Nimelala na Mwanamke Mke wa Mtu Kitanda Kimoja Usiku Kucha ..........Tukajikuta Tume....

$
0
0
Ni mfanyakazi mwenzangu tumeenda nchi jirani kwa semina ya siku 5.Tulivyofika tu wakati tunacheki hotel ambayo ni nzuri bei kidogo ipo juu ila kampuni wametupa pesa za kutosha sana,Sasa wakati tunajadiliana jinsi ya kufanya yule sister akasema, Kwa nini tusichukue chumba kimoja tukashare ili tusave hizi pesa? Nilijua ananitania lakini akasisitisha kwamba yupo serious.

Tukachukua chumba kimoja chenye kitanda kimoja tukazama ndani.Ile kuingia tu ndani yule sister akasema anataka kuoga sababu ya uchovu wa safari akjifunga taulo kavua nguo kazama bafuni.Picha nyingi sana zikanijia ifikapo usiku itakuwaje? Sababu yeye ni mke wa mtu na mimi nina mke home.

Nikajiapisha sintofanya chochote na huyu sister kwanza tunaeshimiana sana. Nmimi nikaenda kuoga baada ya yeye kutoka nilivyorudi nikakuta ashavaa nguo. Story story kidogo tukashuka chini tukaenda pata dinner mpaka kwenye saa 5 usiku tukarudi room.
Kufika tu yule sister kavua nguo zake hii sasa alivua mbele yangu akapiga night dressing kajitupa bed.

Na mimi nikajipa moyo nikavua nikapiga bukta nikazama bed.Tukapiga story mbili tatu huku tukiwa tumejifunikia shuka moja.
Mara usingizi ukanipitia kushtuka nimemkumbatia ile mbaya nikijua ni wife home kuchek na yeye kanikumbatia na kaweka mguu juu yangu.Ki ukweli hali ilikuwa ngumu sana mpaka mapigo ya moyo yalibadilika.

Ki ukweli usingizi ulikata nikawa nimemkumabatia mpaka asubuh. Palipokucha yaani yule sister hana time akazama zake bafuni katoka kapiga suti yake na mimi nikazama bafuni kutoka tukaelekea kwenye hotel inapofanylika semina.

Jamani hii ndio siku ya kwanza kweli niatweza maliza siku tano bila kuingiza ndoa yangu matatani kwa style hii kweli.
Ila nimeapa kutofanya chochote na huyu sister.
Ee mungu nipe ujasiri.

By Manuu/JF

Naombeni Ushauri Nawezaje Kuachana na Tabia ya Kufanya Mapenzi Kinyume na Maumbile

$
0
0
Hello guys
Nimekuwa na tabia ambayo kwa kweli its not normal, coz tangu nimeanza kubalehe binti wa kwanza kufanya nae ngono alikuwa bikra (sealed kwa mbele), so nikaamua kutumia mlango wa uani kufanya nae mapenzi.

Sasa tangia hapo yani kila mwanamke ninaelala nae lazima nimuombe tigo indirectly, kwenye foreplay nashika makalio na kumtia binti vidole vya nyuma, wengine wanakataa wengine wanakubali.

Nikiona mwanamke mwenye makalio makubwa na malaini ndo nadata kabisa. Note (Im 100% straight guy, nawala wanawake tu) sasa hii tabia cjui itaisha lini?

Kama jamani kuna waliokwisha kumbana na hii hali humu, halafu wakaiacha naombeni tips, sababu hii tabia haitanipeleka mahali pema. Though its hard to get rid of this addiction but naombeni mbinu za kuiacha.

By okoyoko/JF

Mke wa Msanii Mr. Blue Atoa Sababu za Kupigana Mugumi na Mumewe Mara Kwa Mara

$
0
0
Mke wa msanii wa Hip hop bongo Mr. Blue Bi. Wahida maarufu kwa jina la Wahida wa Mr. Blue, ametoa sababu ambayo iliwafanya yeye na mumewe kupigana mara kwa mara.

Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio, Wahda amesema wakati wanamlea mtoto wao wa kwanza wa kiume Heri Samir, walikuwa na changamoto kubwa kwani alikuwa halali usiku kwa kulia, ndipo walipokuwa wanagombana mpaka kupigana na Mr. Blue ili kupokezana kumbembeleza mtoto.

“Kila mtoto anakuja kivyake, kama Heri alikuwa anapenda sana kukesha usiku, Heri tumekesha nae miezi 9 ndiyo kaja kuanza kulala usiku yani ikifika saa 12 ndiyo analala, ikifika usiku kuanzia saa 6 yuko macho mpaka asubuhi, tulikuwa tunapigana sana na baba yake, baba yake anataka kulala huku mtoto analia, tunapokezana tumemlea mpaka miezi 9 ndiyo akaanza kulala vizuri”, alisema Wahida.

Wahida aliendelea kwa kusema kuwa hali hiyo haikujitokeza kwa mtoto wao wa pili wa kike, hivyo walikuwa na wakati mzuri kumlea.

Wahida na Mr. Blue wana watoto wawili mmoja wa kiume mwenye miaka mitano, na wakike anatarajiwa kutimiza miaka miwili mwezi wa 10 mwaka huu.

Kufanya Mapenzi Kwa Wiki Mara 3 Kunapunguza Kupata Shambulio La Moyo (Heart Attack) Kwa Asilimia 50%

$
0
0
Utafiti umebainisha kwamba kufanya mapenzi angalau mara tatu kwa wiki kunapunguza uwezekano wa kupatwa Heart Attack (Shambulio la Moyo) kwa 50% ukilinganishwa na yule ambaye anapitisha wiki nzima bila kupiga mambo yetu. Pia utafiti huo unasisitiza ya kwamba mwenye Kufanya Mapenzi killa siku anaondoa uwezekano wa kupata Heart Attack kwa Asilimia 100%

ZIJUE FAIDA ZA KUFANYA MAPENZI

Kiafya
Tendo la ndoa ni moja kati ya mazoezi ya mwili. Wataalamu wanasema kwamba, unapofanya tendo hilo mara tatu kwa wiki husaidia kupunguza kiasi cha mafuta mwilini na pia endapo mtu
atafanya tendo mara tatu kwa wiki kwa kipindi cha mwaka mzima ni sawa na kukimbia maili 75.

Tendo la ndoa huongeza takriban vizalisha nguvu 150 kwa nusu saa ambayo ni sawa na kukimbia dakika 15 kiwanjani.

Kuongeza mwendo wa damu
Tendo la ndoa husaidia kuongeza kasi ya mtiririko wa damu kwenye ubongo na sehemu nyingine ya viungo vya mwili, hii huchangia kuongeza kasi ya mapigo ya moyo na kuboresha mfumo wa upumuaji. Msukumo thabiti wa damu mpya yenye oxygen na homoni zenye chembe chembe hai zinapopenya kwenye mishipa ya damu husaidia katika uunguzaji wa chakula, pia huondoa kiasi cha uchafu ambao ungesababisha mishipa na kushindwa kufanya kazi na kumfanya mwanadamu apate maumivu ya mwili.

Hupunguza mafuta yenye kileo (Cholesterol)
Tendo la ndoa huweka sawa uwiano wa mafuta yenye kileo (Cholesterol) nzuri na cholesterol mbaya na wakati huo hupunguza kwa ujumla kiasi cha mafuta yenye kileo mwilini.

Kupunguza maumivu
Wakati wa kufanya mapenzi, homoni iitwayo oxytosin huzalishwa mwilini ambayo husababisha kuzalishwa kwa homoni iitwayo endorphin ambazo hupunguza maumivu kama vile kuvimba sehemu za viungo (arthritis) maumivu ya shingo (Whiplash) na maumivu ya kichwa.

Ulinzi wa tezi ya kibofu (mwanaume)Majimaji yanayozalishwa katika tezi ya kibofu (prostate) yakizidi husababisha kuleta matatizo mwilini. Tendo la ndoa la mpangilio huondoa uzalishaji wa majimaji hayo yenye madhara.

Mabadiliko ya ghafla ya tendo la ndoa huelekea kuleta matatizo yahusianayo na tezi ya prostate.

Kupunguza mfadhaiko wa moyo
Kujitosheleza na kupumzisha mwili baada ya tendo la ndoa ni muhimu kwa kutuliza akili na kurekebisha mzunguko wa damu mwilini. Watu wenye kushiriki tendo la ndoa wanatajwa kushinda mfadhaiko na kupata usingizi mnono hasa mara baada ya kumaliza kufanya mapenzi.

Huongeza uzalishaji wa homoni za kiume(testosterone) na za kike (Oestogen)
Faida nyingine inayopatika ni kuongeza uzalishaji wa homoni za kiume na za kike likiwemo suala zima la msukumo wa kufanya tendo hilo ambapo mhusika hutosheka zaidi ya yule ambaye hana mazoea ya kufanya mapenzi. Hata hivyo, baadhi ya madaktari wamegundua kwamba ongezeko la homoni za kiume/ kike huweza kuwakinga wanadamu na magonjwa ya moyo.

Kuishi muda mrefu huku ukionekana kijana
Wakati wa tendo la ndoa homoni iitwayo DHEA huzalishwa mwili mzima. Hii husaidia msisimko wa mapenzi kuongezeka.

Kutokana na elimu hiyo DHEA ni kemikali yenye nguvu duniani ambayo husaidia kuweka sawa kinga ya mwili, huongeza ufahamu, kuimarisha mifupa, kutengeneza na kuimarisha afya na kuimarisha mishipa ya moyo (Cardiovascular).

Hupunguza baridi na mafua
Elimu inaonesha kuwa wanaofanya tendo la ndoa mara moja au mbili kwa wiki huongeza 30% ya uzalishaji wa chembe chembe hai za mwili ziitwazo Immunogloulin A ambazo huwa na kazi ya kuulinda mwili dhidi ya magonjwa.

Hizo ni faida chache tu za kufanya tendo la ndoa.
NB: Jambo kubwa la kuzingatia ni kuwa faida hizi hupatikana kwa ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na hofu ya kufumaniwa au kuumbuliwa

HAYA KWA WANA NDOA FANYENI MAPENZI JAPO KWA WIK MARA 3 MUPATE FAIDA ZA TENDO LA MAPENZI NDANI YA NDOA. KWA WALE WASIOWA HAWAPATI HIZI FAIDA SHAURI YENU MSIE OWA OWENI MUPATE FAIDA ZA TENDO LA NDOA
Viewing all 104781 articles
Browse latest View live




Latest Images