Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Mwigizaji Dokii Anaeigiza Kama Mkenya Aamua Kuokoka...Atoa Onyo Hili Kali....

$
0
0
Msanii Dokii amewataka Watanzania waache kumfuatilia maisha yake, kwani maisha yake hayawahusu hata kidogo, hususani kwa kipindi hiki ambacho ameamua kuokoka

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Dokii amesema yeye hajali watu wanachokisema juu yake, kwani anachoangalia yeye ni yale anayoyafanya kwa Mungu wake, hivyo watu wasipoteze muda kabisa kumuongelea.

“Wasiwe busy na mimi na wokovu wangu, acha waongee upuuzi mimi sijali, niko busy na Mungu wangu haijalishi ni msafi au la, sijamwambia mtu nenda club, fanya hivi au ukifanya vile ni dhambi”, alisema Dokii.

Dokii aliendelea kusema kuwa pamoja na yote wanayomuongelea vibaya lakini yeye hayuko hivyo, hata hizo sehemu za starehe anaenda iwapo kuna kazi maalum.

“Sijawahi kwenda club na ndiyo maana watu wanasema hawajawahi kuonana na mimi sehemu za starehe, muda mwengie kama nikienda sehemu ya starehe huenda kuna movie ambayo tunafanya”, alisikika Dokii kwenye Planet Bongo.

Dokii aliendelea kwa kuongelea kitendo cha kuimba wimbo maalum kwa ajili ya ushindi wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyata, na kusema hicho ni kitu cha kawaida kwake kwani hata viongozi wengine alishawahi kuwaimbia.

“Kumuimbia Uhuru Munghai Kenyata si dhambi, siyo yeye tu nimemuimbia Rais Jakaya Kikwete, nimemuimbia Magufuli, nimemuimbia hata Obama alipokuja hapa na watu wakafurahia”, alisema Dokii.

Mwanasheria Tundu Lissu Apinga Ushahidi Uliotelewa Dhidi ya Wema Sepetu

$
0
0
Wakili Tundu Lissu ameukataa ushahidi unaoendelea kutolewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam dhidi ya msanii  Wema Sepetu kwa madai wakili wa serikali aliiambia mahakama kuwa ushahidi huo ulikuwepo lakini  haukuwa ndani ya bahasha.

Ushahidi huo uliowasilishwa kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa serikali ulipingwa na mawakili wanaomtetea Wema Sepetu akiwemo Tundu Lissu pamoja na Peter Kibatala
Ofisa kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali alipeleka vithibitisho anavyotuhumiwa kukutwa navyo Wema Sepetu na watuhumiwa wengine wawili ambavyo ni misokoto miwili ya bangi ambayo ilikuwa imefungwa katika bahasha.

Katika hoja ya wakili wa serikali kwamba bahasha ndiyo ushahidi aliiondoa baada ya kutakiwa kueleza kilichokuwemo ndani ya bahasha ili kitambulike kama ushahidi.

Baada ya kuondoa hoja hiyo, Hakimu wa Mahakama hiyo Thomas Simba alimwamuru mtoa ushahidi kuifungua bahasha, japo upande wa utetezi uliukataa ushahidi huo kwa madai kuwa ndani ya bahasha hiyo kulikuwa na vielelezo vingine ambavyo mtoa ushahidi hakuvieleza awali, kikiwemo kitu kilichodhaniwa kuwa ni karatasi nyekundu.

Baada ya kusikiliza hoja hizo hakimu aliiahirisha kesi hiyo hadi Agosti 18 ili aweze kutoa ufafanuzi juu ya ushahidi huo.

Mkuu wa Mkoa Paul Makonda Atoa Agizo Hili.....

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo amewataka Wajumbe Bodi ya Barabara kuhakikisha fedha zilizotengwa kwaajili ya Ujenzi na Uboreshaji wa Barabara kwa Mwaka 2017- 2018 zinatumika kutengeneza Barabara zenye Ubora.

Makonda amesema hayo wakati wa Kikao cha Bodi ya Barabara ambapo amesema kuwa hataki kuona kwenye Mkoa wake Barabara zinatengenezwa kwa gharama kubwa alafu zinaharibika kwa muda mfupi na kusababisha Kero kubwa kwa Watumiaji wa Barabara.

Amewataka wajumbe wa Bodi hiyo kuhakikisha wanazuia Uharibifu wa Barabara unaofanywa na Magari yanayobeba mizigo mikubwa kupita uwezo wa barabara.

Katika bajeti ya serikali ya mwaka 2017 -2018 imetengwa zaidi ya shilingi Billion 184 kwaajili ya ujenzi wa barabara za mkoa wa Dar es salaam ikiwa ni ongezeko la zaidi ya 5%.

Aidha Makonda ameagiza makampuni yote yanayofanya kazi ya ukamataji wa vyombo vya moto na kufanya kazi hiyo kinyume na mkataba hali inayoleta kero kwa wananchi kuvunja mikataba yao.

Hata hivyo Makonda amewataka watendaji hao kuhakikisha miradi yote iliyokusudiwa kutekelezwa na serikali inamalizika kwa wakati.

Katika kikao hicho kimejumuisha Wabunge, mameya, wakuu wa wilaya, wakurugenzi na wataalamu wa sekta ya barabara.

Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo Tanzania

$
0
0
Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo East Africa (Atakuwa Nairobi,Mombasa,Uganda,Burundi,Rwanda na Sehemu Yoyote Atakayo hitajika.. Tanzania Atazunguka Mikoa Yote..)

AL_WATWAN MAFUSHO Ni Mtafiti wa Dawa za Mitishamba na ana uzoefu wa zaidi ya Miaka 18 katika kutoa Huduma zake.. Amesha toa Huduma zaidi ya Nchi 23 Duniani..
AL_WATWAN MAFUSHO Bado anaendelea Kupokea Salam na Shukrani nyingi kwa wale wote waliofanikiwa baada ya kupata HUDUMA na wale wanao Endelea Na TIBA MBALIMBALI..
      Anatibu kwa Kutumia Dawa za Asili ya Africa, Dawa za Kiarabu, Majini na QUR-AN Ukiwa Nchi yoyote...

Kwa Matatizo ya Fuatayo..
•Love spell
•Money spell casting
•Traditional Healer
•Protection Rituals
•Marriage Spells(to heal marriage problems and restore Affection
•Traditional bad luck Removal
•To Prevent divorce and bind lovers together

 MAGONJWA kama > Miguu kuwaka Moto na kufa Ganzi,Kuvimba tumbo,Kisukari, Ngiri ya ndani na Ngiri ya Nje(Busha) Chango kwa Kina Mama,Kifungua Kizazi kwa waliofungwa kishirikina)..Ulijari(Nguvu za kiume?
MAPENZI.Kumrudisha Mpenzi ndani ya Saa  12 tu.. Kumtuliza(Limbwata) Akusikilize na Akupatie chochote unacho hitaji kwa Wakati. Hutuliza wana Ndoa na na Kuzuia Talaka.. Kama Mpenzi wako Anaishi na Mtu mwingine Anao Uweza wa Kusambalatisha mahusiano yao ndani ya Nusu saa tuu(Mfarakano)...

MAFANIKIO.. Mali Bila Masharti, Bahati kwa Wachimba madini.. MAGIC WALLET, PETE ya Bahati, KUSHINDA BAHATI NASIBU na Kusafisha NYOTA(Nuksi Mikosi).. Umaarufu, Heshima mahala pa Kazi,Cheo kazini. Mafuta maalum Yenye Nguvu ya Ziada..
(Amesaidia Watu maarufu, Wachungaji na Wafanya Biashara wengi Duniani)
KINGA..Huzuia Kabisa Chuma Ulete na Kukupa Kinga ya Mwili na Biashara na Kujilinda na mali zako.Humaliza kabisa Kesi ndani ya siku 12 tu(Zindiko) nk..
PIA HUMALIZA KAZI ZILIZOACHWA AU KUSHINDIKANA....
Acha Kuhangaika Njoo Umaliziwe Tiba yako

AL_WATWAN MAFUSHO

Piga Simu +255 759 084 996

Kimenuka...Rais Aamuru Watu Nchi Nzima Kupimwa Ukimwi kwa Lazima....

$
0
0
Rais wa Zambia Edga Lungu amesema kuwa kwa sasa ni lazima kila mtu apimwe hali yake ya ugonjwa wa ukimwi nchini humo.

Zambia ni kati ya nchi zenye viwango vya juu zaidi vya ukimwi kusini mwa bara la Afrika kwa asilimia 11.6, huku watu walio na umri wa kati ya miaka 15 na 49, wakiwa na wanaishi na virusi vya ukimwi.

Bwana Lungu alisema kuwa kupimwa na kupewa ushauri na matibabu sio kitu cha kujitolea, katika jitihada za kukabiliana na ugonjwa wa ukimwi nchimi humo.

Alitoa tangazo hilo wakati wa uzinduzi na baraza la ukimwi kwenye mji mkuu Lusaka.
Bwana Lungu alisema kuwa suala hilo limezungumziwa na baraza la mawaziri.

LuLu Diva Akana Uzuri Wake na Mapenzi Aliyotoa Kumpa Dili Kenya....

$
0
0
Msanii wa Bongo Flava, Lulu Diva amesema si kweli kwamba uzuri wake ndio ulipelekea kupata nafasi ya kazi zake kusimamiwa na Main Switch ya Kenya

Muimbaji ameimbia Planet Bongo ya EA Radio kuwa hakumshawishi mtu yeyote kumpatia hiyo nafasi na kwake ilikuja kama surprise hata menejimenti yale ilikuwa haijui.

“Kile kitu kilikuja kwetu lakini ilikuja kwa sababu waliona kuna kitu cha ziada kwa Lulu Diva na kuna nguvu ambayo yeye anaifanya, when come to work mimi nafanya kazi katika hali ya serious, kwa hiyo kile kitu wamekiona kwangu,” amesema.

Kuhusu show aliyoifanya nchini humo na kuleta maneno mengi kuhusu kivazi chake alisema, “sema kama wamemaindi vitu vidogo sana, hapana kutoka walivyona yale mapaja malaini, hayana madoa na nini”.

Hivi Ndivyo Makande yalivyompa Mafanikio na Umaarufu Mkubwa Mpiga Kura Kenya

$
0
0
Mwanaume mmoja nchini Kenya, Martin Kamotho baada ya picha yake kusambaa katika mitandao ya kijamii akiwa kwenye foleni ya kuelekea kumchagua Rais wa Kenya, huku akiwa na mfuko wa makande mkononi ameibuka shujaa kupitia kitendo hicho.

Picha ya Martin maarufu kama Githeriman, ilisambaa na kupelekea apate mafanikio kwa kuzawadia vitu mbalimbali kama vile-: Sehemu ya bure ya kuishi katika maeneo ya Karen, Smart phones ya bure aina ya Samsung S8 iliyotolewa na kampuni ya Safaricom huku watoto wake wakipewa simu aina ya Tecno Canon.


Pia amepatiwa nafasi ya kwenda mapumziko na familia yake katika maeneo ya kivutio yaliopo Kenya, Maasai Mara na Kampuni moja ya kitalii ndiyo imehusika kusimamia mchongo mzima. Vile vile amepatia nguo za bure na duka moja la suti lilopo nchini humo.



Githeriman ameonekana kufanya kitendo cha kishujaa kwa kushiriki uchaguzi huo amabo ni muhimu huku akiwa ana kula jambo ambalo mtu mwingine asinge weza kula hadharani kwa kuhofia kupata aibu ama kuonekana.

JE Bangi Ina Madhara? Zijue Athari za Bangi Kwenye Ubongo na Mwili Wako....

$
0
0
Kama zilivyo dawa nyingine zote, bangi inaathari kwa mwili wa binadamu — baadhi zenye manufaa lakini nyingine zenye madhara. Ingawa wengi wanaifahamu kwa athari zake zinazojulikana kama macho mekundu, kuongeza hamu ya kula, bangi inahusishwa pia na kuweza kupunguza maumivu ya mwili. Baadhi ya watafiti waliwahi kusema kuwa inasaidia hata kwenye kudhibiti kuanguka kutokana na ugonjwa wa kifafa.

Zifuatazo ni athari za uvutaji wa bangi kwenye ubongo na mwili wa binadamu:



Watu 600 watoweka kufuatia maporomoko Sierra Leone

$
0
0
Watu 600 watoweka kufuatia maporomoko Sierra Leone
Takriban watu 600 wametoweka kufuatia maporomoko ya matope na mafuriko yaliofanya uharibifu mkubwa katika maeneo kadhaa ya mji mkuu wa Freetown nchini Sierra Leone kulingana na msemamji wa rais.
Rais Ernest Bai Koroma awali aliomba usaidizi wa dharura akisema jamii nzima ilikuwa imeangamia.

Takriban watu 400 wamethibitishwa kufariki baada ya maporomoko ya matope katika eneo la Regent na mafuriko katika maeneo mengine mjini Freertown siku ya Jumatatu.
Shjrika la msalaba mwekundu limeonya kuwa hakuna muda wa kutosha kuweza kuwaokoa manusura.Mazishi ya pamoja ya waathiriwa yanatarajiwa kufanyika siku ya Jumatano ili kupunguza idadu ya wafu katika chumba cha kuhifadhia maiti.

Msemaji wa rais Abdulai Baraytay aliambia BBC kwamba miili ilikuwa ikitolewa katika matope hayoi na vifusi.
Jamii nzima inaomboleza.

''Wapendwa wengine wametoweka , takriban zaidi ya watu 600'' , alisema.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa kwamba wafanyikazi wake nchini Sierra Leone wamekuwa wakisaidia katika juhudi za kuwaokoa manusura.

''Mikakati inawekwa kuzuia mlipuko wowote wa magonjwa yanayosababishwa na maji kama vile kipindupindu , homa ya manjano na kuharisha'', alisema msemaji wa UN Stephane Dujarric.

Masikini Chidi Benz.. Akamatwa Tena Na Madawa ya Kulevya na Polisi

$
0
0

Masikini Chidi Benz.. Akamatwa Tena Na Madawa ya Kulevya na Polisi
Jeshi la polisi  Mkoa wa Ilala, limewakamata watu saba akiwemo msanii wa muziki wa kizazi kipya, Rashid Makwiro maarufu kama ‘Chid Benz’ kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroine.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amesema watuhumiwa hao walikamatwa Agosti 12 mwaka huu  saa 11.50 jioni wakijihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya.

Amesema jeshi la polisi limefanya msako wake na kuwakamata    watuhumiwa hao wakiwa katika eneo ambalo linajihusisha na uuzaji wa dawa hizo.

“Chid Benz na wenzake  wapo kituo cha Polisi cha msimbazi ambapo tunaendelea na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani na kiasi cha dawa zilizokamatwa zimepelekwa kwa mkemia mkuu na itajulikana ni kiasi gani za dawa za kulevya zilizokamatwa,”amesema  Hamduni.

Hamduni amesema jeshi hilo linafanya msako liweze kubaini mtandao mzima unaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na watumiaji ili kuhakikisha wote wanachukuliwa hatua na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Itakumbukwa kuwa , Oktoba 24,2014, Chid alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jiji la Dar es Salaam akiwa na dawa za kulevya, akijaribu kuvuka nazo kwenda mkoani Mbeya kushiriki onyesho la Instagramu Party wakati akijua kuwa ni kinyume cha sheria .

Msanii huyo wa kizazi kipya alikiri shtaka hilo na ndipo , Februari 26 mwaka 2015,  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilipomhukumu kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh900,000 baada ya kupatikana na hatia ya katika makosa matatu likiwemo la  kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi na Heroine yenye thamani ya Sh 40,358.

Hata hivyo msanii huyo alifanikiwa kulipa faini na kukwepa kifungo hicho.


Mfanyabiashara Kizimbani kwa Kukutwa na Sare za JWTZ

$
0
0





Mfanyabiashara Kizimbani kwa Kukutwa na Sare za JWTZ
Casto Onyomolile Ngogo (35) mfanyabiashara wa Kariakoo jijini Dar es salaam, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu shtaka la kukutwa na suruali 5,000 za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).



Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali, Wankyo Simon kwa Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba alidai kuwa Ngogo ambaye ni mkazi wa Tabata Segerea,  alikutwa na vifaa hivyo katika maeneo ya bandari kavu ya Galco Inland Container (ICD) iliyopo Sokota Chang’ombe Juni 15 mwaka huu .

Wakili wa Serikali, Simon alidai kuwa siku hiyo, mshtakiwa huyo alikutwa na suruali 5,000 za JWTZ zenye thamani ya Shilingi 50 milioni ambazo zimepatikana kwa njia isiyo halali.

Juni 15 mwaka huu, Ngogo anadaiwa kuwa katika eneo hilo alikutwa na maofisa wa Jeshi la Polisi akiwa na tisheti 50 za JWTZ zenye thamani ya Shilingi 500, 000.

Hata hivyo mshtakiwa  hakuruhusiwa kusema chochote kwa sababu shtaka lake Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu.

Barnaba, Gigy Money Wakana si Wapenzi...Picha Waliyopakatana Yawa Gumzo Mitandaoni

$
0
0



Barnaba, Gigy Money Wakana si Wapenzi...Picha Waliyopakatana Yawa Gumzo Mitandaoni
Baada ya Gigy Money na Barnaba  kupiga picha wakiwa wamepakatana na kuzua gumzo kwenye mitandao ya kijamii wakidaiwa kwamba ni wapenzi, Elias Barnaba ‘Barnaba’ na muuza sura Gift Stanford ‘Gigy Money’ wameibuka na kudai kuwa wao si wapenzi.

Awali kulikuwa na nyepesinyepesi zikidai kuwa hiyo haikuwa mara ya kwanza kwa wawili hao kuonekana wakiwa wamepakatana katika maeneo mbalimbali, wakisema baada ya Barnaba kuachana na mkewe, aliamua kujiweka kwa mwanadada huyo asiyeishiwa matukio mjini.

kwa upande wake Barnaba, alisema Gigy Money ni dada yake kama walivyo madada wengine na katika maisha yake haishi kwa skendo hivyo wanaosema hivyo siyo kweli.
Kwa upande wake Gigy, alisema Barnaba ni kaka yake na pia shemeji yake, kwani ni rafiki wa aliyekuwa mpenzi wake, Mo J na hiyo picha walipigwa wakiwa kwenye shoo hivyo hakuna suala la mapenzi kati yao.

Waziri wa Japan Achomwa na Foleni za Dar

$
0
0

Waziri wa Japan Achomwa na Foleni za Dar
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Ichiro Aisawa, amesema nchi yake inahitajika kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha miundombinu ya Dar es Salaam baada ya kushuhudia changamoto ya foleni wanayokutana nayo wakazi wa jiji hilo.


Aisawa ambaye kwa sasa ni Mbunge huko Japan huyo amesema hayo  alipokutana na Rais John Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo ambapo ameahidi kuyafikisha yale aliyoshuhudia nchini Tanzania na kuyapeleka kwa Waziri Mkuu wa Japani, Shinzo Abe.
Mbali na ahadi hiyo aliyoitoa kuhusu changamoto ya foleni, Mbunge huyo pia amempongeza rais Magufuli kwa jitihada mbalimbali anazochukua katika kukabiliana na rushwa na msukumo mkubwa anaoutoa katika suala zima la maendeleo.

Kwa upande wake Rais Magufuli, amemshukuru Waziri huyo wa zamani kwa kuja Tanzania na kusema kuwa serikali yake inatambua mchango mkubwa ambao Japan imekuwa ikiutoa katika suala zima la maendeleo na itaendelea kukuza uhusiano wake na nchi hiyo.
Pamoja na hayo mgeni huyo wa Rais Magufuli, alitembelea baadhi ya miradi inayoendelea kujengwa hapa nchini na kampuni za Japani, ukiwemo mradi wa ujenzi wa barabara za juu (flyover) wa TAZARA na mradi wa umeme wa Kinyerezi.

Kichanga Kilichojeruhiwa na Polisi Nchini Kenya Chafariki

$
0
0


Kichanga Kilichojeruhiwa na Polisi Nchini Kenya Chafariki
Mtoto Samantha Pendo mwenye umri wa miezi sita ambaye alijeruhiwa na maafisa wa polisi nchini Kenya walipovamia nyumba yao, amefariki dunia akiwa hospitali.

Daktari Sam Oula wa Hospitali ya Agakhan ambapo mtoto huyo alilazwa alikiri kumpokea mtoto huyo siku ya Jumamosi, na kusema alikuwa katika hali mbaya wakati wakimpokea hospitali hapo.

Baba mzazi wa mtoto huyo Bw. Joseph Abanja alitoa taarifa za kifo hicho, na kusema kuwa wakati tukio linatokea mtoto wake alikuwa amebebwa na mama yake na walikuwa ndani ya nyumba, na ndipo polisi walitokea na kurushia bomu la machozi, kasha kuwavamia wakiwa ndani na kumpiga mke wake na kuanguka chini, alipoangua ndipo alipomuumiza mtoto kwa kuwa aliangukia kichwa.
Taarifa zinasema polisi hao walikuwa wakiwatawanya watu ambao walikuwa wanaandamana wakipinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 8 mwaka huu.

Rais wa Algeria Amtimua Waziri mkuu

$
0
0


Rais wa Algeria Amtimua Waziri mkuu
Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria amemfukuza kazi waziri wake mkuu Abdelmadjid Tebboune, ambaye aliteuliwa katika nafasi hiyo miezi isiyozidi mitatu.
Hakuna sababu zilizotajwa za kuondolewa kwake kazini.
Lakini hatua hiyo imekuja siku kadhaa baada ya Rais kumtumia barua kali bwana Tebboune kutaka mabadiliko ya sera.
Tayari waziri mkuu mpya ametajwa kuwa ni Ahmed Ouyahia ambaye alikuwa mnadhimu mkuu wa Rais.


Soko la Sido Lateketea kwa Moto Usiku wa Kuamkia leo

$
0
0

Soko la Sido Lateketea kwa Moto Usiku wa Kuamkia leo
Soko la Sido Mkoani Mbeya limetetekea kwa moto usiku wa kuamkia leo na kutekteza mali mbalimbali ambazo thamani yake wala chanzo cha moto huo mpaka sasa hazijafahamika.

Akithibitisha kutokea kwa moto huo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya William Ntinika amesema kuwa moto huo ambao uliwaka mpaka saa saba za usiku ulikuwa mkubwa na kuteketeza mali zote katika eneo la kuuzia vyakula.

Ntinika amesema kuwa jitihada mbalimbali zilifanyikaka katika kudhibiti moto huo bila kuzaa matunda ikiwani ni pamoja na kikokisi cha zima moto, Jkt, pamoja na magari ya zima moto ya kiwanda cha Songwe lakini moto ulikua mkubwa zaidi wakati ukiendelea kuwaka.


Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuwa anataraji kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na pamoja na wilaya kukutana hii leo kwa ajili ya kufanya tathmini na kuunda tume itakaoyochunguza chanzo cha ajali hiyo.

Hizi Hapa Nafasi za Ajira Mbali Mbali Zilizotangazwa leo

$
0
0

Faiza Ally Atoa Povu..'Mniache na Maisha yangu Nimechagua Kuwa Hivyo'

$
0
0
MUIGIZAJI anayejipatia umaarufu kutokana na vituko, Faiza Ally amewataka watu wanaomkosoa kuachana naye kwa vile hayo ndiyo aina ya maisha aliyoamua kuishi (life style).

Alitoa kauli hiyo kufuatia watu mbalimbali kumkosoa kwa kitendo chake cha kuonekana akiwa mitaani na mtoto wake aliyezaliwa hivi karibuni, huku wakosoaji wakisema ilikuwa ni mapema mno kumtembeza mitaani hasa kwa kuwa hata siku 40 hajafikisha tangu azaliwe.

“Unajua kila mtu ana life style yake, haya ni maisha yangu niliyochagua na mambo yanabadilika, naishi kuendana na wakati, kwa hiyo nawashauri watu waache kukariri, siyo lazima watu wote tufanane,” alisema.

Mapya yaibuka Uchaguzi TFF, Baadhi Hawaamini Kama Kweli Haki ilitendeka....

$
0
0
IKIWA ni siku nne tu zimepita tangu Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kufanya uchaguzi na kuwapata viongozi wake, baadhi ya waliokuwa wagombea katika uchaguzi huo wameibuka na kutoa yaliyo moyoni mwao.

Katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa St Gasper uliopo mkoani Dodoma, Wallace Karia alichaguliwa kuwa Rais mpya wa TFF huku Michael Wambura akichaguliwa kuwa Makamu wa Rais.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, aliyekuwa mgombea wa urais, Shija Richard, pamoja na kuwapongeza washindi katika uchaguzi huo, alisema mchakato mzima uligubikwa na ‘usiri’ na kuwafanya baadhi ya wagombea kutokuwa na imani na kile kilichokuwa kikiendelea katika mchakato mzima wa upigaji na kuhesabu kura.

“Niombe uongozi mpya ulioingia madarakani kubadilisha kasoro za kikatiba zinazoweza kutia mashaka mchakato mzima wa uchaguzi, kwa mfano Kamati ya Uchaguzi kuteuliwa na wajumbe wa Kamati ya Utendaji ambao ni wagombea hii ni kasoro kubwa inayoweza kutia mashaka uhuru wa Kamati hiyo,” alisema Shija..

Alisema kuna haja ya kubadilisha katiba ili inapotokea mchakato wa uchaguzi umeshaanza na kunahitajika mabadiliko ya Kamati ya Uchaguzi, taasisi nyingine huru ipewe jukumu la kubadilisha Kamati ya Uchaguzi.

“Rais na Kamati yake ya Utendaji wawe na uwezo wa kuteua Kamati ya Uchaguzi pale tu mchakato wa uchaguzi unapokuwa haujaanza, lakini ukianza alafu rais ambaye pia ni mgombea anapoteua kamati ya uchaguzi inatia wasiwasi,” alisema Shija.

Malalamiko kama hayo pia yalitolewa na Fredrick Mwakalebela aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Urais katika uchaguzi huo.

Mwakalebela ambaye ni Katibu Mkuu wa zamani wa TFF, alisema kuwa kitendo cha mgombea mmoja ambaye alikuwa ndani ya uongozi uliomaliza muda wake kutoulizwa swali wakati wa kujinadi kwa wajumbe kunatia shaka.

“Ni kitu ambacho akiingii akilini, mgombea mmoja kutoulizwa swali wakati alikuwepo kwenye uongozi ambao unatuhumiwa kwa ubadhilifu, na hata kitendo cha kutoruhusiwa kulinda kura zetu na kuwaondoa wajumbe nje mara baada ya kupiga kura kinatia shaka, tutaamini vipi kama haki ilitendeka,” alisema Mwakalebela.

Hata hivyo wagombea hao waliwatakia heri viongozi wote walichaguliwa katika kutimiza majukumu yao wakiwa viongozi wapya wa TFF.

Kesi ya Kugushi Nyaraka ya Aveva na Kaburu Yazidi Kuwaweka Lumande

$
0
0


Kesi ya Kugushi Nyaraka ya  Aveva na Kaburu Yazidi Kuwaweka Lumande
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Agosti 16, 2017 imeahirisha kwa mara nyingine kesi ya kutakatisha fedha na kughushi nyaraka inayowakabili Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange maarufu Kaburu hadi Agosti 30 mwaka huu kutokana na upelelezi kutokamilika.

Kesi hiyo imeahirishwa mbele ya Hakimu Victoria Nongwa baada ya Wakili wa upande wa mashitaka kueleza kuwa kwa vile nyaraka za kughushi maandiko zinahitaji utaalam kuzibaini, hivyo kitengo maalum cha kubaini maandishi kinaendelea kufanya uchunguzi ili kukamilisha upelezi huo ambapo aliomba kesi hiyo isogezwe mbele kwa siku 14 ili kukamilisha uchunguzi.

Hakimu Victoria Nongwa aliutaka upande wa mashtaka kukamilisha haraka upelezi wao ili kesi hiyo ianze kusikilizwa ambapo aliisogeza hadi Agosti 30 ili kuwapa nafasi kukamilisha upelelezi wao huku watuhumiwa wakirudishwa gerezani.

Aveva na Kaburu wanashtakiwa na TAKUKURU wakikabiliwa na tuhuma za kughushi nyaraka za Klabu ya Simba na kutakatisha dola za Marekani 300,000 (zaidi ya Sh milioni 650) na wamekuwa rumande tangu Juni 29, mwaka huu.
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images