Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Serikali ya Japani Yatoa Fedha Kujenga Njia Zaidi Nane Barabara Morocco -Mwenge

$
0
0




Serikali ya Japani Yatoa Fedha Kujenga Njia Zaidi Nane Barabara Morocco -Mwenge
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameishukuru Japan kwa kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi Jijini Dar es Salaam ikiwemo upanuzi wa barabara ya Mwenge – Morocco utakaoiwezesha barabara hiyo kuwa na zaidi ya njia nane.



Rais Magufuli alitoa shukrani hizo jana alipokutana na kufanya mazungumzo na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. Ichiro Aisawa ambapo ujenzi wa barabara ya TAZARA, ujenzi wa Daraja la Gerezani njia nne, na barabara ya Bendera tatu hadi Kamata.

Aidha Rais Magufuli alimuomba Mhe. Ichiro ambaye ni mwakilishi wa wabunge wa Japan wanaoshughulikia masuala ya Afrika kuwahamasisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Japan kuja kuwekeza hapa nchini na ameahidi kuwa Serikali itahakikisha uwekezaji wao unalindwa kama itakavyofanya kwa kampuni ya kutengeneza rangi ya Kansai Plascon ambayo awali ilijulikana kama Sadolin, na kampuni inayozalisha Betri za Panasonic hapa nchini, ili uwekezaji huo ulete manufaa hapa nchini.

Hizi Ndizo Taarifa za Awali Kuhusu Moto Ulioteketeza Soko la Sido

$
0
0


Hizi Ndizo Taarifa za Awali Kuhusu Moto Ulioteketeza Soko la Sido
Natoa pole kwa wote walioathirika na janga la moto kwa wafanyabiashara soko la Sido. Soko la Sido lilianza kuungua saa 21.32 Hrs jana usiku na kuteketeza mali za wafanyabiashara wa soko la sido.
Pamoja na kutoa pole niwashukuru wananchi, vyombo vya ulinzi kwa ushirikiano na kazi kubwa ya kudhibiti moto usiendelee kuleta madhara makubwa zaidi.
Serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Mbeya imeunda kamati  ya kufanya tathmini ya kujua hasara na chanzo cha Moto huo .

Tunaomba wananchi waendelee kuwa watulivu na watoe ushirikiano kwa kamati hiyo ili tuweze kujua chanzo cha moto na hasara iliyopatikana
Aidha vyombo vya ulinzi vinaendelea kuchunguza kujua kama moto huo utakuwa umesababishwa na mtu/watu uchunguzi huo bado unaendelea
Nirudie tena kuwapa pole wote walioathirika na janga na Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu

Esther Sumaye Yamkuta Sawa na ya Mumewe, Frederick Sumaye

$
0
0

Serikali imefuta umiliki wa shamba la ekari 473, lililokuwa linamilikiwa na Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, Esther Sumaye na mengine manne ya ekari 2,661 ya Kampuni ya Noble Agriculture Enterprises Limited, inayomilikiwa na mfanyabiashara Jeetu Patel baada ya kushindwa kulipia kodi ya ardhi na kutoyaendeleza.

Huo ulikuwa ni muendelezo wa serikali kuyatwaa mashamba ambayo wamiliki wake kwa muda wameshindwa kuyaendeleza au kulipia kodi.

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ilieleza kuwa Rais Magufuli amefuta mashamba pori 14 yenye ukubwa wa zaidi ya ekari 14,341 katika wilaya za Kilosa, Mvomero na Kilombero mkoani Morogoro. Mashamba ya Esther Sumaye na Patel ni miongoni mwa mashamba hayo yaliyofutwa na Rais.

Baada ya kufuta mashamba hayo, Waziri William Lukuvi alisema kuwa Rais amewaagiza Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya kuhakikisha mashamba hayo yanasimamiwa vizuri na kugawiwa kwa wananchi hasa wenye uhitaji ambao wapo jirani na mashamba hayo.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Lukuvi amewaonya viongozi wenye nia ya kujipenyeza kwa lengo la kuchukua maeneo kwenye mashamba hayo na kwamba wale watakaojipenyeza watajulikana na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Stephen Kebwe alisema kuwa awali serikali ya mkoa ilifanya uchunguzi na kubaini uwepo wa mashamba pori 223 huku Wilaya ya Kilosa ikiongoza kwa kuwa na mashamba 198.

Ndoa Mpya ya Nawal ni Yadaiwa Kuwa ni FAKE? Mwenyewe Kayasema Haya…

$
0
0
U heard ya XXL ya Clouds FM leo August 15, 2017 inamuhusu mke wa zamani mwimbaji wa Bongofleva Nuh Mziwanda, Nawal aliyefunga ndoa na mwanaume mwengine hivi karibuni na kuwa gumzo…sasa new stori ni kwamba ndoa inadaiwa kuzua utata.

Inadaiwa kuwa ndoa mpya ya Nawal sio halisi, ni FAKE na anadaiwa kufanya hivyo ili kumuumiza roho Nuh Mziwanda.

Soudy Brown amezungumza na Nawal
”Haina haja ya kuapia mimi najua mwenyewe kwamba nameolewa. Mume wangu nilikuwa naye sasa hivi kaenda kazini mimi nikarudi nyumbani siwezi kupika mwanangu anaumwa, pia tulijisikia kwenda kula sehemu nyingine.” – Nawal

RC Makonda Atangaza Kihama kwa Watumishi wa Serikali Jumaosi

$
0
0
RC Makonda Atangaza Kihama kwa Watumishi wa Serikali Jumaosi
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda Jumamosi hii ataendesha kongamano katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC) Posta kujadili hali za barabara za jiji la Dar es salaam ambapo wananchi watapewa fursa za kueleza hali za barabara kutoka mitaani kwao.

RC Makonda akisalimiana mmoja kati ya wawakilishi wa JICA, Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan, lililojenga barabara ya Samora Avenue pamoja na Bustani ya Kaburi Moja.

Makonda amesema hayo wakati akikabidhiwa barabara ya Samora Avenue pamoja na bustani ya ‘Kaburi Moja’ iliyopo katikati ya Posta Dar es salaam iliyokarabatiwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan, JICA.

Alisema Kongomano hilo litawakutanisha wadau mbalimbali wa barabara wakiwemo Tanroad, wakandarasi pamoja na wananchi kutoka katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.

“Jumamosi hii tutakutana na wadau mbalimbali wa barabara pale JNICC kujadili miundombinu yetu ya jiji la Dar es salaam. Pia tumeandaa utaratibu ambao utawapatia fursa wananchi kutuma taarifa zao juu ya barabara zao kule wanakoishi na kama barabara ni mbaya mkandarasi wa eneo husika ataeleza sababu na akishindwa kueleza tutamtumbua. Barabara zetu zote za Dar es salaam zinatakiwa kuwa safi na zakuvutia,” alisema RC Makonda.

Mapema wiki hii RC Makonda akiwa katika kikao na Bodi ya Barabara, alisema kuwa hataki kuona kwenye mkoa wake barabara zinatengenezwa kwa gharama kubwa halafu zinaharibika kwa muda mfupi na kusababisha Kero kubwa kwa watumiaji wa Barabara.


RC aliwataka wajumbe wa bodi hiyo kuhakikisha wanazuia uharibifu wa barabara unaofanywa magari yanayobeba mizigo mikubwa kupita uwezo wa barabara.

Alisema katika bajeti ya serikali ya mwaka 2017 -2018 imetengwa zaidi ya shilingi Billion 184 kwaajili ya ujenzi wa barabara za mkoa wa Dar es salaam ikiwa ni ongezeko la zaidi ya 5%.

Aidha Makonda aliziagiza makampuni zote zitakazofanya kazi ya ukamataji wa vyombo vya moto na kufanya kazi hiyo kinyume na mkataba hali inayoleta kero kwa wananchi kuvunja mikataba yao.

Hata hivyo Makonda amewataka watendaji hao kuhakikisha miradi yote iliyokusudiwa kutekelezwa na serikali inamalizika kwa wakati.

Katika kikao hicho kimejumuisha Wabunge, mameya, wakuu wa wilaya, wakurugenzi na wataalamu wa sekta ya barabara.

Aliyejifanya Mkurugenzi wa Habari wa Ikulu Kafikishwa Mahakamani leo

$
0
0
Mfanyabiasha Ramadhani Juma amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la kujitambulisha kuwa ni Mkurugenzi wa Habari wa Ikulu, Gerson Msigwa.

Mshtakiwa huyo amesomewa mashtaka na Wakili wa Serikali, Jaqline Nyantori ambapo amedai kuwa kati ya June 28 na July 4, 2017 Dar es Salaam kwa nia ya kudanganya, mtuhumiwa huyo alijitambulisha kuwa ni Gerson Msigwa ambaye ni Mkurugenzi wa Habari wa Ikulu kwa mtu anayeitwa Ladslaus Matindi.

Inadaiwa kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo katika kipindi hicho kwa lengo la kujaribu kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu lakini hata hivyo, mshtakiwa alikana kosa lake na upande mashtaka ulidai upelelezi bado haujakamilika.

Mshtakiwa huyo alipewa masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao watasaini bondi ya Tsh. Milioni Moja na kesi imeahirishwa hadi August 23, 2017.

Uamuzi wa Wabunge Waliofukuzwa CUF Agost 25

$
0
0


Uamuzi wa Wabunge Waliofukuzwa  CUF Agost 25
Mahakama Kuu imeahirisha kutoa hukumu juu ya pingamizi lililowasilishwa na wabunge wanane  wa Viti Maalum wa CUF kupinga Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwaapisha wabunge wapya walioteuliwa na Mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na Msajili wa Vyama,  Prof. Ibrahim Lipumba.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano  anayeunga mkono upande wa Maalim Seif, Mbarala Maharagande, kesi hiyo imeahirishwa hadi  Agosti 25 mwaka huu itakapotoa uamuzi kuhusu suala hilo.

Maharagande aliyasema hayo alipoongea na waandishi wa habari baada ya kutoka  nje ya mahakama hiyo.

Madee Amkana Jack Wolper..Adai Katuni iliyotumika Kwenye Wimbo wake sio Wolper

$
0
0
Msanii Madee Ali ‘Madee’ kutoka kundi la Tip Top Connection amefunguka kuwa anashangazwa na uvumi wa msanii mwenzake, Jackline Wolper kwa kudai kuwa ametumika katika video mpya ya msanii huyo ya ‘Sikila’ bila ruhusa yake.

“Ile video haijamuonyesha mtu sura zaidi ya kuwa na katuni hivyo nashangaa kusikia hivyo, kikubwa ni kuwa hajatumika yeye bali ametumika mwanamke mwingine kutoka Nigeria na anabidi aelewe ile sio picha bali ni mfano wa taswira tu,”alisema.

Akizungumzia mapokeo ya wimbo huo alisema kuwa mashabiki walishtuka kwasababu hawajawahi kuona kitu kama hicho kwa hapa nyumbani, lakini anashukuru Mungu mapokeo yamekuwa mazuri kwasababu wapo wanaosifia ubunifu na wapo wanaopinga ubunifu huo.

Ally Kiba Awachanganya Mashabiki Wake

$
0
0


Ally Kiba Awachanganya Mashabiki Wake
Mkali wa sauti na mwenye 'hit song' ya 'Aje', Alikiba amewaacha njia panda watu wake wa karibu pamoja na mashabiki wa kazi zake baada ya yeye kuweka picha katika mtandao wake wa Instagram ukiwa na neno 'wananiita Kipusa'

Muda mchache kupita mashabiki hao walimiminika katika picha hiyo kwa kutoa maoni yao binafsi, huku wengine wakijaribu kubashiri kuwa  huenda ni ujio wake mpya wa nyimbo anayotarajiwa kuiachia katika siku za hivi karibuni.

Miongoni mwa ujumbe zilizokuwa zikitawala chini ya tangazo hilo ni pamoja na;
Rajo Jr: Alikiba bana, katisha na atapita hivi hivi na kutuacha na mihamu yetu hahaha. King ni 'undefined musician' unaweza kuta kipusa siyo nyimbo ila kauliza tu kuwa wanamuita kipusa?, kwa sababu tuna hamu ya kumsikia tumewaza ngoma mpya.

Careen Candy: Nafuu leo imekua siku nzuri maana ulishaanza kuniboa hata wanangu wakikuona kwenye runinga walikuwa wakiniita lakini sikuweza kutoka ndani.

Official george :siye tunataka ngoma, hatutaki maneno maana tumechoka kunyanyasika huku mtaani.

Costz himself: Tunavyoijua 'Team' Fulani muda huu watakuwa wanapanga kuishambulia kipusa, na wahakikishieni Kipusa ikitoka basi na wao wote wataachia ngonjela zao zinazopigwaga shuleni akija mgeni.

Inno_Kalinga: Waachie washindane na jina la nyimbo kwa wiki mbili kwanza.

Karim Issa: Mungu akusimamie unstoppable utuletee ngoma Kali, maana tumechoshwa na mavuvuzela.

Babesh Sultan: sawa si kwa kutususa hivi king, wengine washapata matatizo ya moyo kusubili ngoma. Iachie mzee baba kitaani hatuna raha kabisa.


Kwa upande mwingine, hayo yote yametokana na ukimya wa kipindi kirefu cha Alikiba jambo ambalo limepelekea mashabiki zake kuanza kufurahia jambo ambalo hata hawalifahamu kiundani kwamba Kipusa ni ujio wa nyimbo yake mpya au pengine msanii huyo ameamua kubadilisha jina na kujiita hivyo au pengine ameamua kuja na 'product' zake ambazo zitakuwa zikiitwa kwa jina hilo.

Alikiba siku ya Jumamosi anatarajia kufanya show katika mji wa New York, Marekani ambapo atakuwa na wasanii wengine kama P Square, 2 Face Idibia, Tiwa Savage  pamoja na Cassper Nyovest.














Mugabe: Waliowaua Wazungu Hawatashtakiwa

$
0
0

Mugabe: Waliowaua Wazungu Hawatashtakiwa
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameambia umati wakati wa sherehe za siku ya mashujaa kwenye mji mkuu wa Harare, kuwa watu ambao waliwaua wakulima wazungu wakati wa mabadiliko ya mifumo ya ardhi nchini humo hawatashtakiwa.

"Ndio tuna wale waliouwawa wakati walipinga. Hatuwezi kuwashtaki wale waliowaua. Ninauliza mbona tunawashtaki?" alisema Mugabe.
Wakati wa ukoloni, ardhi nzuri ilitengewa wazungu na mwaka 2000, bwana Mugabe aliongoza kutwaliwa kwa ardhi hiyo kutoka kwa wakulima 4000.

Rais Mugabe awali alikiri kuwa mifumo ya ardhi ya nchi hiyo ilifeli na mwaka 2015 alisema:
"Nafikiri mashamba tuliyowapa watu ni makubwa, hawawezi kuyasimami.
Kutaliwa ghafla mashamba kutoka kwa wakulima wazungu, inaonekana kuwa sababu kuu ya kuporomoka kwa uchumi wa Zimbabwe tangu mwaka 2000.

Roma Aibukia Clouds FM Akiwa na Stamina...Washangaza Watu Kwa Kutumia Majina ya Zari na Wema

$
0
0
Roma na Stamina wametinga studio za clouds fm wamevaa jezi.

Jezi ya RomaMkatoliki Imeandikwa WEMA ya Stamina Imeandikwa ZARI.
.
Unadhani wana maana gani?

Mawazo Yangu Juu ya Rich Mavoko....Lolote Atakalofanya au Kwenda Tunaliona Jina la Diamond...

$
0
0
Ana nyimbo nzuri sana, ni mtunzi mahiri sana wa mashairi na pia dogo ana muonekano, but siku zote kitu kitakachokufanya aendelee kuonekana wa kawaida na hakui kimuziki ni theory flan inaitwa "playing as a son of". theory hii kiukweli ndio ilimkimbiza neymar pale barcelona, japo ni waandishi wachache sana walioandika hili na hata inaelezwa ndio kitu halisi alichomuambia rafiki yake Gabriel Jesus.

Asingeweza kuwa mkubwa namba moja dunian kama angeendelea kucheza as a son of lionel messi pale Catalunya, alihitaj kuwa nje ya messi kuimarisha empire yake na ukubwa wake.

Theory hii pia ilitaka kumkimbiza kyrie irving wa Cleveland Cavaliers, anahtaj kuwa mkubwa zaid bt haitawezekana kama ataendelea kucheza as a son of lebron james. Theory hii ndio wachambuzi wa kikapu pale NBA walimueleza Paul George aliyetoka Pacers kwenda Oklahoma kuwa hautakuwa mkubwa tena kama unaenda kucheza as a son of Russell Westbrook, vivyo hvyo kwa zitto kabwe aliona hataweza kuwa the great kama ataendelea kuwa chin ya mbowe na akaamua kutaka kugombea uenyekit na alipogonga mwamba akaamua kujitoa. rich mavoko hautakuwa mkubwa zaid ya hapo ulipo kama utaendelea kuwa a son of diamond platnumz, utaendelea tu kuprevail na hautapotea but hutakuwa zaid tena.

Wanamuziki wote wanaoshine under the umbrella of somebody huwa hawakui. Rejea Mayokhoun wa Davido, still hajulikan, rejea Bred wa Davido pia hayuko on air kivile. Yuko wapi Correde Bello a son of Don Jazz? Hata Tekno kama sio kustukia kujitoa kwa Davido asingekuwa star mkubwa Afrika.

Fally na wengineo walijitoa chini ya kaka zao ndio wakajulikana zaid Afrika. Miaka 7 au 8 iliyopita ulikuwa ukichukuliwa kama mtu pekee tanzania uliyekuwa ukishindanishwa na diamond. But now unasimamishwa level za baraka, rayvan na neddy. Walichofanya diamond na joh makin ni akili kubwa mno. walihofia majina kudondoka baadae, na wakaamua kujenga empire ili kila memba wa empire lolote atakakofanya au popote atakapokwenda atakuwa anamuwakilisha yeye, ndio maana rich mavoko lolote afanyalo na popote aendapo tunaliona jina la diamond platnumz likipepea na si jina la rich mavoko.

NI MAWAZO NA MATAZAMO WANGU..
NINI MAWAZO NA MTAZAMO WAKO? (Free Discussion)

By Alvinroley

JE Kwanini Watumishi wa Mungu Hawamuelewi Goodluck Gozbert Katika Uimbaji wake?

$
0
0
Praise the lord..
Hivi kwanini watu wamejaribu kumuandama Goodluck Gozbert mara nyingi watumishi wa Mungu wamekuwa wakimuona wa dunia na sababu zao kubwa ni uvaaji wake.

Uimbaji wake hapa wanapenda kuzungumzia suala la kutungia baadhi ya wasanii wakidunia nyimbo kama baraka prince na wengine...

Suala lingine ya kuwa uimbaji wake hajawahi taja jina la Yesu kwenye nyimbo zake

Nyie mnamuelewaje kwani??? Anaimba nyimbo za Dini au za kidunia?

By Herufi Kubwa/JF

Hiki ndio Kilichomtia Uchizi Jini Kabula.....Mpaka Kudai yeye ni Ndugu na Rihanna

$
0
0
Msanii wa muziki Issabela Mpanda ambaye ni rafiki wa Karibu wa Mariam Jorwa au jini Kabula ambaye hivi karibuni amepata matatizo ya kurukwa na akili, ameweka wazi kilichomsababishia shoga yake huyo kuchanganyikiwa.

Akizungumza na mwandishi wetu, Issabela amesema daktari ambaye anamtibia Kabula amesema kuwa rafiki yao alikuwa na msongo wa mawazo, lakini kwa sasa yuko sawa.

Pia Issabela ameweka wazi kile ambacho Watanzania wengi walikuwa hawakifahamu kuhusu ugonjwa na matibabu ya Kabula, na kuhusu mtu ambaye amekamatwa kwa kufanya tukio la uhalifu au uvunjaji wa sheria juu ya Kabula.

Mbinu Tata Za Kumfanya Mwanamke Ajigonge Kwako Kirahisi

$
0
0
#1 Mfanye mwanamke ajieleze kwako
Unaweza kumuuliza swali kama “Ni kitu gani ambacho kinakufanya unique/tofauti na wengine?”
Ama kumwambia, “Wewe unakaa mdogo sana kiumri kwangu. Ni kitu gani ambacho uko nacho ambacho kitaziba pengo hilo?”

Ataanza kukupatia sababu ambazo anajiona kuwa yeye ni unique – kiufupi atakuwa akijaribu kujieleza zaidi ili ajipendekeze kwako/ umpende zaidi. Yaani atakuwa anajaribu kuhakikisha kuwa unaridhika na kila kitu ambacho atakwambia.

Na uzuri wa kutumia mbinu hii ni kuwa kadri mwanamke anavyokuwa mrembo ndivyo zaidi utakavyohitajika kumfanya ajihitimishe kwako, usiogope kumuuliza maswali ambayo yatamlazimu ajihitimize kwako. Muulize maswali mazito. Muulize maswali ambayo itakuwa ngumu kwake kujihitimu kwako.

Na kitu cha kufurahisha kuhusu wanawake warembo, ni kuwa wamezoea kufukuziwa na wanaume kiasi cha kuwa ukianza kuuliza maswali na kujihitimu kwako, atafall na wewe zaidi. Hii ni kwa sababu hawajazoea kuulizwa maswali kama hayo. Hawajazoea kuambiwa, “Wewe si mwanamke type yangu.” ama, “Ningekutongoza lakini unanikumbusha ndugu yangu wa kike mdogo.”

Pia unapaswa kuhitimisha wanawake kulingana na ladha yako. Labda kwa mfano hupendi wanawake wanaovuta sigara, kunywa pombe nk, basi mhitimishe kwa kutumia mambo haya. Usimfiche. Mwambie ukweli. Kumwambia mambo kama haya kutamfanya ajue vigezo vyako. Unampa challenge na yeye kutaka kutimiza vigezo vyako. Mbinu hii ni rahisi ya kumuwin kirahisi na kumfanya akufukuzie.

#2 Tumia Mwili wako
Mara ya kwanza unapoongea na mwanamke huwa anaangalia kando. Wewe ndie uko wazi, unaongea na yeye, unamwangalia, lakini yeye ameangalia kando kabisa.

Hapo kuna ile hisia ambayo inakuja ndani yako kuwa huyu mwanamke hamakiniki na wewe kabisa.

Well, hapa ndipo unatumia mbinu funge ya kuiga vile ambavyo anafanya yeye. Wakati umemuapproach, si lazima umuangalie mzima mzima kwanza, unaweza kuangalia kiupande. Na akiongea kitu ambacho umependezwa nacho, unaweza kutumia mwondoko wazi kwa kuangalia upande wake. Na akisema kitu ambacho hujapenda basi tumia mwondoko funge kwa kuangalia kando.

Mbinu hii hufanya kazi kwa kuchukua atenshen na umakinifu wa mwanamke. Atamakinika kwa kila neno ambalo atakwambia. Mwishowe itajeuka kuwa ni yeye ndiye anayekufukuzia na wala si wewe. Mbinu hii pia inampa confidence ya kutamka mambo ambayo si rahisi kutamkwa na mwanamke hivihivi.

#3 Ongea Kwa Kujiamini na Amri Ndani yake
Katu mwanamke hawezi kukufukuzia kama utatumia toni saidizi kama, “Mambo waendeleaje?” ambapo sentensi kama hii toni ya sauti inapanda mwishoni. Kama vile unauliza swali. Matumizi ya sentensi hizi zitakufanya uonekane mtu mdhaifu, mhitaji, na utafanya wanawake wakukimbie.

Lakini ukitumia toni saidizi zilizovunjwa kwa mwanamke kama, “Hey! Njoo hapa! Waendeleaje!”  unatoa sauti ya kuamrisha na ya kutoa maelekezo.

Na kwa kuwa uasili wa mwanamke ni kufuata amri, atakujibu kwa kutafuta toni saidizi ili aweze kujihitimisha kwako.

Atakwambia, “Mmh, jina langu ni Mamito?” huku akitaka umthibitishe.

So, ukimwambia, “Sasa, mpangilio wako ni upi!? kwa toni saidizi iliyovunjwa, atakujibu...

“Mmh, mimi mwanafunzi nasomea...huu ni mwaka wangu wa...”

Kiufupi hapa anajaribu kujieleza zaidi kwako kulingana na vile sauti yako ilivyotoka. [Soma: Jinsi ya kuwa mwanaume bora ya wote]

#4 Weka nafasi na Pozi Katika Maongezi yako
Unapoongea na mwanamke, hutaki kuona umepalilia maongezi bila mpangilio, badala yake huwa unataka nafasi angalau kurudi nyuma kiasi kuyapa maongezi yenu nafasi ya kupumua. Unaruhusu kuwe na angalau kimya ndani yake. Kimya ambacho kinaenda polepole. Na nafasi ambayo utampa mwanamke nafasi ya kujileta kwako ili kuteka atenshen yako.

So mpe mwanamke nafasi ya kujiekeza kwako, na utagundua kuwa mwanamke huyu anakusaidia pakubwa kuyafanya maongezi yenu yanawiri.

Atafurahi kukupa namba yake ya simu kwa kuwa anakufukuzia.

Atafurahi kukutana na wewe katika deti ya pili.

Na hatakutatiza zile nyakati za mwisho mwisho za kumuomba penzi.

Sababu 20 Kubwa Ambazo Zinakufanya wewe Mwanaume Usipate Mpenzi

$
0
0
Tangu ujielewe umekuwa single. Huna girl friend ama mpenzi yeyote yule. Kuna yule mwanamke jirani yako kila siku unamwona. Unamtamani lakini hutaki kumuapproach. Kiufupi unaishi kiupweke ilhali marafiki zako kila wakati wanaonekana na wanawake tofauti tofauti.


Hii ni hali ambayo inatokea kwa wanaume wengi duniani. Usijione kama ni wewe pekeako. So shida huwa inatokea wapi? Nesi Mapenzi tumekuja na sababu ambazo zinakufanya wewe ubaki single milele.

#1 Hautaki kujaribu. Kuna wanaume wengi ambao wanalalamika kuwa hawana wachumba lakini hapo hapo hawatii bidii kuhakikisha kuwa wanatafuta mmoja. Usipojaribu kutongoza mwanamke basi utabaki hivyo hivyo single milele.

#2 Unatafuta mwanamke aliyekamilika. Wanaume wengine hufanya kosa la kutafuta wanawake warembo zaidi katika hii dunia. Hili ni jambo ambalo hutalipata. Kama utasema hutafuti mwanamke mpaka awe anafanana na Masogange ama Huddah Monroe basi utangojea sana.

#3 Hauko huru. Si jambo baya kuishi na wazazi wako. Wanaume wengi bado huishi na wazazi wao. Lakini kuna time ikifika, haswa miaka ya mwisho mwisho ya ishirini, unahitajika angalau ujitenge kiasi. Kwa nini? Hii ni ishara ya kuonyesha wanawake kuwa umekuwa mkubwa...unless uwe mswahili itakubalika.

#4 Kama umekataliwa, unakata tamaa. Kukataliwa ni hali ya maisha. Itakuwa labda hata umekataliwa kazi ama kujiunga na shule flani. Hio pia ni kukataliwa. Haina utofauti na kukataliwa na mwanamke. Lakini sasa shida yako ni kuichukulia binafsi. Yaani ukikataliwa na mwanamke mmoja basi wewe unaamua kujitenga kabisa na wanawake. Haifai.

#5 Bwana Mzuri. Kuwa mtu mzuri na karimu ni jambo zuri. Lakini pia ujue kuwa wanawake hawapendi mwanaume ambaye ni mzuri kupindukia. Kama hauko ngangari ama mkakamavu basi hufai. Wanawake wote utawaita mashemeji.

#6 Kila kitu ni wewe. Kuna wanaume ambao katika kila mazungumzo lazima waingilie kati. Wao ndio wanaanza mazungumzo na kumalizia.Wanapenda sana atenshen. Hii ni tabia ambayo wanawake wanaichukia na hawapendi aina hii ya wanaume. Kama unajijua uko na hii tabia basi ni vigumu kwako kuwa na girlfriend.

#7 Unahitaji kuoga. Tuseme kweli. Kuna wanaume wengine ni vigumu kwao kuoga. Kila wakipita sehemu yeyote unaskia harufu mbaya. Wanawake hawapendi aina hii ya wanaume. Kinachohitajika kufanya ni kuoga na sabuni. Nenda kinyozi unyoe nywele. Labda ilikuwa ni ishu ndogo ya usafi wa mwili ndio ilikuzuia usimpate mwanamke unayemtamani.

#8 Hujiamini. Wanaume wengi huwa hawajiamini ikija katika swala la kutongoza. Wasiwasi, kujishuku, woga kunafanya wengi wabaki single. Jeuka sasa ama itakuwa ngumu kwako.

#9 Unangojea akuaproach wa kwanza. Kama wanawake wangekuwa na uwezo wa kuapproach wanaume dunia ingekuwa sehemu nzuri yakuishi. Lakini sivyo. Ni wanawake kidogo sana ndio wanamoyo huo. So usingojee mwanamke akuapproach. Anza wewe ama utabaki hivyo hivyo.

#10 Unaona aibu katika kundi lako. Wanawake hawapendi wanaume wanaoona haya. Si vibaya kuwa na hulka ya kuona aibu, lakini usizidishe. Wanawake watakuona uko na tatizo. Itakuwa vigumu kwako kumuaproach na itakuwa vigumu kwake kukukubali.

#11 Hujui kusawazisha kati ya kazi na kujiburudisha. Mwanaume lazima ajipe time ya kujiburudisha. Kama utasema siku nzima wiki mfululizo utakuwa ukifanya kazi time ya kutangamana na wanawake itakuwa lini?

#12 Unakaa nyumbani na kuangalia movie wikendi nzima. Kuangalia movie ni jambo zuri. Lakini jua kwamba ukiwa unaangalia movie wikendi nzima basi nawe hutapata kumwona mwanamke unayempenda. Unapaswa kwenda kula bata ukajifurahishe na marafiki zako wakutambulishe kiumeni.

#13 Huonyeshi kuwa unampenda. Labda ni kweli unampenda lakini hujawahi kumuonyesha kuwa kweli unampenda. So nyinyi wawili ni marafiki wa dhati. Usipomuonyesha kuwa unampenda basi atakuingiza katika himaya ya urafiki akufungie huko milele.

#14 Umejenga ukuta wa hisia. Labda mbeleni kuna mwanamke alikutenda. Ama umeshuhudia rafiki yako akitendwa. So na wewe umeamua kuweka hisia zako mbele. Lakini kama unataka mwanamke basi lazima uubomoe ukuta huo na uanze kutangamana na wanawake hata kama unaogopa.

#15 Unataka maisha yaliyokamilika kabla hujatongoza mwanamke. Unataka nyumba, gari, kazi nzuri...naelewa. Lakini kama unangojea upate vitu hivi vyote kabla upate mwanamke, jua haitafanya kazi. Huwezi kupanga maisha kama yanaendelea.

#16 Unaenda katika sehemu zisizofaa. Kama unaenda gym ya wanaume, ama kwenda kilimanjaro kukwea milima huku ukitarajia ukutane na wanawake basi unaota. Wanawake hawapatikani sehemu hizo. Jaribu kwenda baharini, supermarket, klabu huko hukosi wanawake.

#17 Unafikiria sana bila matendo. Wewe ni yule ambaye tayari ushapanga jinsi utakavyomfanyia mwanamke ambaye bado hata huna namba yake. Changamka ujeuza fikra zako kuwa matendo.

#18 Unafanya mambo haraka haraka. Unampenda huyu mwanamke sana. Leo umetoka naye deti. Kesho na kesho kutwa unataka mtoke deti. Kila siku unataka utoke naye. Kufanya hivi kutamtishia na utamfanya akimbie.


#19 Unajiona spesho. Mbele ya mwanamke usijifanye spesho. Usianze kujigamba kuwa wewe ni hivi na hivi ama uko na hili na lile. Kama wewe ni spesho pia wanawake hujiona spesho zaidi yako.

#20 Hujui kutangamana. Kando na kujiona spesho unapenda kumdharau. Unamwonyesha kuwa yeye si lolole.  Hapa wanawake watakutenga na utajikuta pekeako.

Ok. Haya ni baadhi ya mambo ambayo yanakufanya uwe mpweke usiwe na mwanamke yeyote. Kama una moja wapo ya tabia hizi basi badilika sasa.

Raila Odinga Bado Kichwa Ngumu...Hajakubali Kushindwa Uhuru Kenyatta...Sasa Kuchukua Maamuzi Haya

$
0
0
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga ametangaza kwamba muungano wake wa National Super Alliance utawasilisha kesi mahakamani kupinga ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliofanyika Jumanne wiki iliyopita.

Bw Odinga alikuwa amesema ingawa muungano huo ulikuwa umeapa kutowasilisha kesi kortini wakati huu, wameona ni heri kufanya hivyo "kufichua uovu uliotokea wakati wa uchaguzi mkuu."

"Tumeamua kwenda kortini kufichua jinsi uongozi wa kompyuta ulivyofanikishwa," amesema Bw Odinga akiwahutubia wanahabari mtaa wa Lavington, Nairobi.

"Hawa ni viongozi wa kompyuta. Kompyuta ndiyo iliwataga, kompyuta iliangulia, kompyuta iliwatoa. Vifaranga vya kompyuta."

Kiongozi huyo amesisitiza msimamo wa NASA kwamba uchaguzi haukuwa huru na wa haki.

Amesema mitambo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi IEBC ilidukuliwa na matokeo kuvurugwa kumfaa Bw Kenyatta ambapo kulikuwa na pengo kiasi fulani kati yake na Bw Odinga muda wote wa kutangazwa kwa matokeo.

"Mtindo huu ulitokea pia katika maeneo mengi uchaguzi wa ugavana. Jambo kama hili halijawahi kutokea katika uchaguzi wa kidemokrasia pahala pengine popote duniani. Lakini ilitokea hapa," alisema.

Bw Odinga amesema udukuzi huo una uhusiano na kuuawa kwa meneja wa teknolojia katika tume hiyo Chris Msando ambaye aliuawa wiki moja kabla ya uchaguzi.
Samahani, kisakuzi chako hakiwezi kuonesha ramani hii

Aidha, kiongozi huyo ameishutumu tume ya uchaguzi akisema imekuwa ikitangaza matokeo ya uchaguzi bila kutoa Fomu 34A za kuonyesha matokeo yalivyokuwa katika vituo vya kupigia kura.
Bw Odinga mesema uchunguzi wa muungano huo umebaini udanganyifu mwingi ulitokea, na akawashutumu waangalizi wa uchaguzi ambao walisema uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.

Waziri mkuu huyo wa zamani amesema upinzani uliwasilisha kesi mahakamani kupinga matokeo mwaka 2013 lakini hawakutendewa haki, na kusema "Uhuru (Kenyatta) alishinda 100%, nasi tukashindwa 100%."

"Mahakama inaweza kutumia hii kama nafasi ya pili ya kujitakasa, au inaweza kuamua kuharibu mambo kabisa," amesema.

Jamii ya kimataifa ilikuwa imehimiza upinzani, pamoja na wagombea wengine ambao hawakuwa wameridhishwa na uchaguzi, kutumia mifumo iliyowekwa kikatiba kutafuta haki.

Kwa mujibu wa matokeo ya IEBC, Rais Kenyatta alipata kura 8,203,290 huku naye Raila Odinga akipata kura 6,762,224.

Wivu wa Mapenzi Wasababisha Wapenzi Kujiua Mwananyamala....Mwanaume Aua na Yeye Kujiua

$
0
0
Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Maria Pius amezikwa leo makaburi ya Mwananyamala kwa Kopa baada ya mpenzi wake kumuua kwa kumpiga na kitu chenye nchi kali kisha mwili wake kuutupa kwenye shamba huko Chanika jijini Dar es Salaam.

 Inasemekana siku ya Jumatatu mwanaume huyo ambaye jina lake halijafahamika alimpiga binti huyo na vitu vyenye ncha kali kwa kinachoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi mpaka alipopoteza maisha kisha muaji huyo aliandika ujumbe unaosema wasimatafute muuaji kwani amemuua yeye, kisha ujumbe huo aliuweka kwenye kifua cha binti huyo pamoja na simu mbili, simu ya mtuhumiwa pamoja na simu ya binti huyo.

Baada ya watu kugundua kuwa binti huyo ameuawa na kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola inadaiwa siku ya kesho yake ambayo ni jana mwanaume huyo aliyedaiwa kufanya mauaji hayo naye aliamua kujitoa uhai kwa kujitumbukiza kwenye kisima cha maji na kupoteza maisha.

Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo Tanzania

$
0
0
Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo East Africa (Atakuwa Nairobi,Mombasa,Uganda,Burundi,Rwanda na Sehemu Yoyote Atakayo hitajika.. Tanzania Atazunguka Mikoa Yote..)

AL_WATWAN MAFUSHO Ni Mtafiti wa Dawa za Mitishamba na ana uzoefu wa zaidi ya Miaka 18 katika kutoa Huduma zake.. Amesha toa Huduma zaidi ya Nchi 23 Duniani..
AL_WATWAN MAFUSHO Bado anaendelea Kupokea Salam na Shukrani nyingi kwa wale wote waliofanikiwa baada ya kupata HUDUMA na wale wanao Endelea Na TIBA MBALIMBALI..
      Anatibu kwa Kutumia Dawa za Asili ya Africa, Dawa za Kiarabu, Majini na QUR-AN Ukiwa Nchi yoyote...

Kwa Matatizo ya Fuatayo..
•Love spell
•Money spell casting
•Traditional Healer
•Protection Rituals
•Marriage Spells(to heal marriage problems and restore Affection
•Traditional bad luck Removal
•To Prevent divorce and bind lovers together

 MAGONJWA kama > Miguu kuwaka Moto na kufa Ganzi,Kuvimba tumbo,Kisukari, Ngiri ya ndani na Ngiri ya Nje(Busha) Chango kwa Kina Mama,Kifungua Kizazi kwa waliofungwa kishirikina)..Ulijari(Nguvu za kiume?
MAPENZI.Kumrudisha Mpenzi ndani ya Saa  12 tu.. Kumtuliza(Limbwata) Akusikilize na Akupatie chochote unacho hitaji kwa Wakati. Hutuliza wana Ndoa na na Kuzuia Talaka.. Kama Mpenzi wako Anaishi na Mtu mwingine Anao Uweza wa Kusambalatisha mahusiano yao ndani ya Nusu saa tuu(Mfarakano)...

MAFANIKIO.. Mali Bila Masharti, Bahati kwa Wachimba madini.. MAGIC WALLET, PETE ya Bahati, KUSHINDA BAHATI NASIBU na Kusafisha NYOTA(Nuksi Mikosi).. Umaarufu, Heshima mahala pa Kazi,Cheo kazini. Mafuta maalum Yenye Nguvu ya Ziada..
(Amesaidia Watu maarufu, Wachungaji na Wafanya Biashara wengi Duniani)
KINGA..Huzuia Kabisa Chuma Ulete na Kukupa Kinga ya Mwili na Biashara na Kujilinda na mali zako.Humaliza kabisa Kesi ndani ya siku 12 tu(Zindiko) nk..
PIA HUMALIZA KAZI ZILIZOACHWA AU KUSHINDIKANA....
Acha Kuhangaika Njoo Umaliziwe Tiba yako

AL_WATWAN MAFUSHO

Piga Simu +255 759 084 996

Rapa Roma Mkatoliki Aanza Kuunyemelea Ulaji wa Ubunge 2020

$
0
0
Rapa Roma Mkatoliki amefunguka juu ya harakati ya kuingia Bungeni mwaka 2020 na kusema hiyo ni sehemu nzuri kwake kufunguka mambo mengi ambayo kwenye nyimbo zake huenda anashindwa kuyazungumza kutokana na kutokuwa na kinga.

Rapa Roma Mkatoliki akiwa na Mtangazaji wa kipindi cha NIRVANA, Deogratius Kithama.
Roma Mkatoliki amesema hayo kupitia kipindi cha NIRVANA kinachoruka kila Jumanne kuanzia saa tatu usiku kupitia ting'a namba moja kwa vijana EATV, alipokuwa akiongea na mtangazaji wa kipindi hicho Deogratius Kithama, Roma anakiri kwamba amekuwa akishauriwa sana kugombea Ubunge mwaka 2020 hivyo anadai ataangalia ingawa kwa mazingira anayoyaona yeye Bungeni ndiyo sehemu sahihi yeye kuongelea kero za wananchi.

Kwa Tanzania baadhi ya wasanii ambao walikuwa wakiimba ngoma zinazogusa maisha ya watu kila siku na kuwapigania watu kupitia tungo zao kama Joseph Mbilinyi na Profesa Jay waliweza kuaminiwa na wananchi na kupigiwa kura na sasa ni wabunge wanawakilisha wananchi kupitia chama cha upinzani bungeni, hivyo inawezekana Roma Mkatoliki anataka kufuata nyanyo zao kwani naye amekuwa akifanya harakati na kutetea wananchi kupitia tungo zake kama ambavyo wao walikuwa wakifanya.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live


Latest Images