Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Wambura, Wambura Bado Ngoma Nzito Simba

$
0
0
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

0712461976
KAMATI ya rufani ya shirikisho la kandanda Tanzania, TFF chini ya mwenyekiti wake, mwanasheria Julius Lugaziya leo mchana inaendelea kumalizia kujadili rufani ya mgombea aliyeenguliwa kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi wa Simba unaotarajia kufanyika juni 29 mwaka huu, Michael Richard Wambura.
Kikao cha kamati hiyo kilianza jana majira ya saa 5:00 asubuhi katika hoteli ya Courtyard, Upanga, jijini Dar es salam na kuahirishwa saa 4:30 usiku, lakini ngoma ililala bila kufikia maamuzi na leo hii kamati inatarajia kukutana tena saa 6:00 mchana ili kumalizia na kufikia maamuzi ya mwisho.
Hamu ya wadau wengi wa soka na wanachama wa Simba wanahitaji kufahamu kama Wambura anarudishwa au anaondolewa rasmi katika kinyang`anyiro hicho.
Jana kamati ya Lugaziya alifikia sehemu nzuri kwa kuhoji pande zote mbili kwa maana ya wakata rufaa na wakatiwa rufaa na leo wanaanza kupitia maelezo yao na kuyapima uzito na kufanya maamuzi.
Mtandao huu umekuwa ukipokea simu na jumbe fupi za simu kutoka kwa wadau wake wakiuliza nini maamuzi ya kamati ya rufani ya TFF iliyokutana jana.
Jana timu yetu ilipiga kambi maeneo ya Courtyard kufuatilia `ngado kwa ngado` kinachoendelea kwenye kamati hiyo ili kuja na jibu sahihi, lakini kulikuwa na usiri mkubwa mno, japokuwa kila mtu alikuwa anasema lake.
Hata siku moja, mtandao huu hauandiki taarifa ambayo haijathibitishwa na vyonzo makini.
Ukipita kwenye mitandao ya kijamii, watu wengi wanaandika kuwa Wambura karudishwa wengine wanasema kaondolewa.
Taarifa hizi si rasmi kwasababu maamuzi hayajafikiwa mpaka sasa.
Kuna uwezekano hatima ya Wambura ikajulikana leo jioni, kwahiyo wadau wetu kuweni na subira.
Taarifa za kwenye mitandao si za kiziamini kwa asilimia zote kwasababu kuna uhuru wa kuandika na kuchapisha habari. Wengine wapo kwa ajili ya kuwavutia wasomaji, lakini sisi hatufanyi kazi kwa misingi hiyo.
Hatujapata taarifa rasmi na wahusika walisema wanakaa tena leo, kwa maana hiyo taarifa rasmi itatoka leo.
Asante kwa kuwa nasi na tutazidi kuwafahamisheni kinachoendelea kwa wakati huu.

- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=1833#sthash.cvx32ghD.dpuf

Exclusive Video: Diamond Akiwa Jukwaani na Davido Wakiimba Number 1 Remix

$
0
0
Hukutazama performance ya Diamond Platnumz na Davido Bongo5 ilikuwa ndani ya ukumbi wa ICC jijini Durban, Afrika Kusini kukuletea uhondo huo. Tazama video za performance zao hapa.

Diva 'Stress For Who for What! Nina Uamuzi wa Kumpenda Mwanamuziki Yoyote...Mmetumwa Najua'

$
0
0


Diva 'Stress For Who for What! Nina Uamuzi wa Kumpenda Mwanamuziki Yoyote...Mmetumwa Najua'

Mrembo Aaguka Kutoka Juu ya Spika na Kufariki Dunia Wakati Akicheza Mziki

$
0
0
Nimetumiwa story hii na chanzo ambacho hakikujitambulisha, na ni stori iliyoambatanishwa na picha, ni story ya binti aliyevunjika shingo yake na kufariki katika tamasha la kucheza muziki mitaani (street dance) katika mitaa ya Jamaica weekend weekend iliyopita.
Chanzo cha habari hii kimeeleza kuwa binti huyo alikuwa ni dancer wa muziki katika style ya acrobatic dance na alikuwa akicheza kicha chini miguu juu juu ya speaker ndipo alidondoka na kuvunja shingo kisha kupoteza maisha.
Kila mtu alishtuka alipodondokea kichwa

Ratiba ya Mechi za Kombe la Dunia Kwa Masaa ya East Afrika

$
0
0
Hapa ni kwa masaa ya kawaida nyumbani east Africa....fahamu muda gani timu uipendayo itashuka Dimbani
Click Hapa: RATIBA

Mwenyekiti wa Baraza la Maimamu Nchini Kenya Auawa kwa Risasi

$
0
0
Mwenyekiti wa baraza la maimam na muhubiri maarufu nchini Kenya Sheikh Mohammed Idris, ameuawa kwa kupigwa risasi mjini Mombasa.

Sheikh Mohammed Idris ameuawa karibu na msikiti ulio karibu na nyumbani kwake eneo la Likon baada ya kuvamiwa na kundi la watu waliokuwa na silaha, wakati akitoka nyumbani kuelekea msikitini.

Taarifa kutoka katika eneo hilo zinasema kuwa Sheikh Mohammed Idris alikuwa akipata vitisho vya mara kwa mara kutoka kwa kundi la vijana wa kiisilamu wanaodai mabadiliko, na amewahi kutoa taarifa za vitisho hivyo na kusema kuwa anahofia maisha yake.

Decemba mwaka jana Sheikh Idris na mpinzani wake Mohamed Khalifa walinusurika kifo baada ya msikiti wao kuvamiwa na vijana zaidi ya 100, ambao walitawanywa na polisi.

Mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya kumbukumbu ya Pandya, mjini Mombasa

Pamekuwa na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya viongozi maarufu wa dini katika mazingira ya kutatanisha.

R.I.P Sheikh Idris

Je Urembo wa Kujichubua ni Urembo? Soma Kisa cha Mwanamitindo Maarufu Nchini Kenya Vera Sidika

$
0
0
Swala la kubadili rangi ya ngozi limekuwa kama msumari moto, kunao wanaoliunga mkono na wale wanaolipinga swala hilo katu hawawezi kulifanya.
Baadhi wanasema kuwa ni wanawake wasiojithamini na kujiamini pekee ndio wenye kujichubua ngozi.

Mjadala huo ukiendelea, wasichana wengi wanajitafutia umaarufu sio Marekani na Uingereza tu bali hata katika kanda ya Afrika ya Mashariki. Wasichana hao wamekuwa wakifanya kila wawezalo ili kupata huo umaarufu.
Mmoja wa wasichana hao ni Vera Sidika anayejulikana sana nchini Kenya na Afrika mashariki kwa kuwa na makalio makubwa ambayo ndiyo yaliyompa umaarufu wake baada ya kuonekana katika wimbo mmoja wa video uitwao 'You Guy' ambao baadaye ulipigwa marufuku nchini Kenya.

Vera amejizidishia umaarufu kwa kubadili rangi yake ya ngozi, zamani kidogo akiwa mweusi na sasa amejichubua na kuwa mweupe na pia kuwaambia watu kuwa kubadili rangi ya ngozi yake ni yeye mwenyewe kujitakia. Hiyo isiwashughulishe watu.
Vera anajulikana kwa kuwa na mazoea ya kujipiga picha hasa za makalio yake na kuziweka kwenye mitandao ya kijamii. Vara analinganishwa sana na Kim Kardhashian hasa kwa sababu ya umbo lake.
Kazi ya Vera hasa ni ya uwanamitido lakini mbali na hilo Vera hulipwa ili kufika kwenye karamu mbali mbali , kwenye disco na katika hafla mbali mbali za watu mashuhuri. Yeye pia hulipwa kuwa katika kanda za video za wanamuziki maarufu Afrika Mashariki.
Alifichua kupitia televisheni Ijumaa kuwa alitumia maelfu ya dola kubadili rangi ya ngozi yake na kujifanya mweupe.
Shughuli hiyo aliifanyia nchini Uingereza na ilimgharimu karibu milioni 15 pesa za Kenya, hizo ni dola 170,000 na kwamba tayari kuna watu wengi wanaotaka sana kujichubua ngozi na kufanana na Vera, kwa mujibu wa mwanadada huyo.

Vera anasema kuwa watu wamemsema sana kwenye mitandao ya kijamii vibaya kwa sababu ya anavyoendesha maisha yake. Amewataja kama wanafiki kwa sababu anasema huku wakiendelea kumsema na kumkosoa kwa kujichubua, wamekuwa wakimuuliza alichofanya ili na wao watafute pesa wakafanye hivyo kwa wanataka sana kufanan naye.
Mtindo wa wanawake kujichubua ni swala tata nchini Kenya. Sio kama India ambako vipodozi vya kujichubua huuzwa wazi wazi. Nchini Kenya bidhaa hizo, huuzwa kimagendo.
Wataalamu wanasema, wanawake wengi wanaendelea kujichubua licha ya hatari za bidhaa zinazouzwa kimagendo.
Swala la wanawake kijichubua barani Afrika lilianza kujadiliwa waziwazi pale ambapo msanii raia wa Cameroon Dencia kuzindua rasmi bidhaa zake za kuchubua ngozi ziitwazo, Whitenicious.

"Nikifa Sitaki Kusifiwa" - Riyama Ali, Akerwa na Tabia ya Wasanii Kuleta Maigizo Kwenye Misiba

$
0
0
RIYAMA Ali mwigizaji wa kike asiye na kashifa katika tasnia ya filamu Bongo, amefunguka kwa kusema kuwa kama kuna msanii mwenzake au mtu mwenye mapenzi naye angependa kama ana sifa kuhusu yeye katika umahiri wa kuigiza na mengineyo basi atumie nafasi hiyo akiwa hai, haitaji kusifiwa akifariki kwani anaamini kuwa sifa hizo hatasikia.



 “Nasema mapema kabisa sitaki kusifiwa nikifa, sifa mtu uipate ukiwa hai kama ni faida au kufurahia mwenyewe ujionee lakini nimeshafumba macho kuna faida gani, sisikii sioni haya ya nini kwangu miye?,”anasema Riyama.



Msanii huyo amesema kuwa imekuwa tabia kwa baadhi ya wasanii kuleta maigizo katika misiba ya wasanii inapotokea mara nyingi waonapo televisheni ujipanga kwa ajili ya kuhojiwa na waandishi basi hata kama marehemu alikuwa na ugomvi naye basi atajifanya jana kabla ya umauti walikuwa wote na kumwachia usia kama rafiki.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Semeni Sana ila Nimeamua Nitakwenda na Tattoo ya Shilole Kaburini-Nuhu Mziwanda

$
0
0
Jana Tuliweka Habari na Picha Kuhusu Mchumba wa Shilole Anajulikana kama Nuhu Kujichora Tattoo Mkononi ya Jina la Shilole "Shishibaby" Leo Amesema Hajali na yuko IN LOVE he can do anything for Love ..Yupo Radhi Kuzikwa na Tattoo ya Shilole ...
Mnasema Semeni Sana Mtu Yupo In LOVE ......

Mrembo Aliye Piga Picha na Komba Chumbani Aibuka na Kusema Haya

$
0
0


SIKU chache zimekatika baada ya tukio la kusambaa mitandaoni kwa picha tata zenye pozi kati ya mheshimiwa Komba na mrembo aliyejulikana kwa jina moja la Angel.

Hatimaye mrembo huyo ameibuka na kuanika mambo mazito kama si makubwa, Risasi Mchanganyiko linakudadavulia.

Awali katika gazeti hili toleo la Jumamosi iliyopita ukurasa wa mbele kulikuwa na habari hiyo ikiwa na kichwa; KHAA! KOMBA! Katika habari hiyo picha zilizomuonesha mheshimiwa Komba akiwa na mrembo huyo zilipamba ukurasa huku mwenyewe (Komba) akidai ni picha za kutengeneza).

OFM YAINGIA MITAANI
Kwa vile Komba alikataa picha si zake huku baadhi ya vyombo vya dola kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) vikitangaza kuingia kazini kumtafuta sosi wa picha hizo, ilibidi timu makini ya Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ kutoka Global Publishers iingie kazini kumsaka mrembo huyo kwa udi na uvumba.

YATUMIA NUSU SIKU
OFM ambayo huwa haishindwi kitu, ilitumia nusu siku ya Ijumaa iliyopita na kufanikiwa kuinasa namba ya simu ya mkononi ya Angel pamoja na picha nyingine ikiwepo iliyotumika ukurasa wa mbele wa gazeti hili.

Aidha, ilibainika kwamba, mrembo huyo anaitwa Angel Kissanga, mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, bila ajizi Paparazi wetu alimwendea hewani Angel na kumuuliza kama ana habari zozote kumhusu yeye.
Angel: “Habari kama zipi? Mimi sina habari zozote.”

Paparazi: “Hujaona kwenye mitandao ya kijamaii wameweka picha zako ukiwa katika mapozi tata na mheshimiwa Komba?”
Angel: “Ngoja kwanza, nitakupigia.”

MUDA UNAKWENDA, ANGEL ARUDIWA
Baada ya kuona muda unakatika bila mrembo huyo kupiga simu kama alivyokuwa ameahidi, paparazi wetu alimrudia hewani ambapo safari hii simu yake ilipokelewa na mwanamke aliyejitambulisha kuwa ni dada wa Angel.

“Mimi si Angel, ni dada yake. Angel amepandwa na presha baada ya wewe kumwambia kuna picha zake na mheshimiwa Komba kwenye mitandao.
“Unajua ngoja nikuambie ukweli. Mdogo wangu ameshtuka sana, hivi hapa tupo Hospitali ya Micco Sinza, amelazwa.”

PAPARAZI ATIA TIMU HOSPITALINI
Kusikia hivyo, paparazi wetu alifunga safari hadi kwenye hospitali hiyo ambapo kweli mrembo huyo alikuwa amelazwa kwa matatizo ya presha ya kupanda.

Mwanamke aliyejitambulisha kuwa ni mama mdogo wa Angel alimjia juu paparazi wetu akidai yeye ndiyo chanzo cha mwanaye huyo kupandwa na presha ghafla, akamtimua asimuone mgonjwa.

MAZUNGUMZO YA BAADAYE
Siku iliyofuata, paparazi alibahatika kuzungumza na Angel ambaye aliweka wazi mambo yake kuhusu picha hizo kama ifuatavyo:

“Mimi nataka kusema kwamba picha nimeziona, nazifahamu kweli ni mimi.”
Paparazi: “Ni kweli ulipigwa ukiwa na mheshimiwa Komba?”
Angel: “We jua tu kwamba picha nazijua. Zilipigwa na simu ya LG.”
Paparazi: “Alipiga nani?”

Angel: “Nimesema nazifahamu.”
Paparazi: “Hiyo simu ni ya nani?”
Angel: “We wa nini?”
Paparazi: “Okey, mheshimiwa Komba unamfahamu?”
Angel: “Namfahamu ndiyo.”
Paparazi: “Ni nani wako?”

Angel: “Nimekwambia namfahamu.”
Paparazi: “Sasa mbona mheshimiwa Komba anasema picha zimetengenezwa?”
Angel: “Mimi sijui sasa.”

ANGEL ATAKIWA KUTIA TIMU GLOBAL
Baada ya mazungumzo hayo, paparazi alimtaka msichana huyo kufika kwenye ofisi za magazeti ya Global ambapo alikubali.

Hata hivyo, baadaye alisema amebatilisha baada ya baba yake kuingilia kati sakata la picha hizo akidai yeye ndiye atakuwa msemaji mkuu.
Habari za chini kwa chini zilidai kwamba, kusita kuweka miguu kwa Angel kwenye ofisi za Global kulitokana na zuio la mheshimiwa mmoja ambaye alimchimba mkwara kwamba asitoe ushirikiano wowote na vyombo vya habari.

MASWALI MUHIMU
Maneno ya Angel na mheshimiwa Komba yanapingana. Mmoja anasema picha zilitengenezwa, mwingine anazitambua na zilipigwa kwa simu ya LG, nani mkweli? (endelea kufuatilia Magazeti Pendwa ya Global Publishers).

ANATAJWA PAULINA
Mbali na kupishana kwa maneno ya wawili hao, mwanamke mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Paulina anatajwa kuwa nyuma ya sakata hilo.

Mwanamke huyo anadaiwa wakati fulani kuingia kwenye mzozo na Angel na akaja kudai ameipata simu yenye picha za mrembo huyo na mheshimiwa bila kujulikana alikoipata. Je, aliipata kwa Angel au mheshimiwa Komba? 
(endelea kusoma magazeti ya Global).

Taifa Stars Mzigoni Leo Kuwawinda Msumbiji (Black Mambaz)

$
0
0
IKIWA ni harakati ya kuikabili Msumbiji `Black Mambas` katika mchezo wa mwisho kuwania kupangwa hatua ya makundi kusaka tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika, AFCON mwakani nchini Morocco, Taifa stars inatarajia kuingia tena kambini leo (Juni 11) mwaka huu.

Julai 20 mwaka huu, Taifa Stars itaanza nyumbani uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam na wiki mbili baadaye itasafiri kwenda mjini Maputo kucheza mechi ya marudiano. Mshindi wa jumla ataingia hatua ya mwisho ya makundi.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa na kambi ya siku tatu jijini Dar es Salaam ikijumuisha wachezaji 28. Kwa mujibu wa programu ya Kocha Mart Nooij, Stars itaingia tena kambini Juni 24 mwaka huu.

Wachezaji wanaotakiwa kuripoti kambini ni Deogratias Munishi, Aishi Manula, Benedictor Tinoko, Kelvin Yondani, Said Moradi, Nadir Haroub, Joram Nason, Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Edward Charles, Aggrey Morris na Pato Ngonyani.

Wengine ni Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Amri Kiemba, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Said Juma, Haruna Chanongo, Himid Mao, Said Ndemla, John Bocco, Simon Msuva, Kelvin Friday, Ramadhan Singano, Khamis Mcha, Mrisho Ngasa na Mwegane Yeya

shaffihdauda

Hatimae Michael Wambura Apigana Mpaka Kimeeleweka Simba

$
0
0
KAMATI ya Rufani ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemrejesha kuwania Urais wa Klabu ya Simba, Michael Wambura ambaye alikuwa ameenguliwa.

Habari zilizopatikana jana usiku wakati tukienda mitamboni, zilieleza kuwa Wambura amerejeshwa na Kamati hiyo inayoongozwa na Mwanasheria Julius Lugaziya, baada ya kikao cha vuta nikuvute.

Kikao cha Kamati hiyo chini ya uenyekiti wa Lugaziya, kilimalizika Dar es Salaam jana usiku, ambapo baadhi ya waandishi wa habari walitaka kufahamu hukumu ya rufani hiyo ya Wambura, na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Boniface Wambura alisema majibu yatatoka leo.

“Taarifa mtapewa kesho (leo), leo siwezi kuongea lolote,” alisema Wambura mara baada ya kurejea kwenye ofisi za TFF, katikati ya Jiji akitokea kwenye kikao hicho cha rufani.

Alirejea ofisini kabla ya kumalizika kwa kikao hicho. Juzi, Kamati hiyo ilikutana hadi saa tano usiku kwenye Hoteli ya Protea Oysterbay, na jana waliendelea na kikao hicho kwenye ofisi za TFF kuanzia asubuhi hadi saa sita mchana na baadaye kuhamia Hoteli ya Southern Sun ambako walikamilisha kazi yao iliyokuwa inasubiriwa na mashabiki wa soka nchini.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, inadaiwa kuwa kikao hicho kilikuwa na mvutano miongoni mwa wajumbe hasa katika kufikia maamuzi yao.

Hadi jioni, tayari wajumbe walikuwa wamekamilisha kazi yao, lakini maamuzi ‘yakawa magumu’ kufikiwa.

Kamati ya Uchaguzi ya Simba chini ya Mwenyekiti Damas Ndumbaro ilimuengua Wambura kuwania nafasi hiyo kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Juni 29, kwa madai si mwanachama halali wa klabu hiyo, kitendo ambacho mhusika hakukubaliana nacho na ndipo kukata rufaa ili kupata haki yake.

TFDA Yatoa Ushahidi wa ARVs ‘Feki’ Mahakamani

$
0
0
MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA) imedai ilikagua na kugundua dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARVs) zilizotengenezwa na Kiwanda cha Tanzania Pharmacentical Ltd (TPL) kinachomilikiwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida ni bandia.

Wakili Mwandamizi wa Serikali, Osward Tibabyekoma alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati wa usikilizwaji wa awali wa kesi inayomkabili Madabida na wenzake ya usambazaji wa dawa hizo bandia na kusababisha hasara ya Sh milioni 148.

Licha ya Madabida ambaye ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda hicho, washitakiwa wengine ni Mkurugenzi Uendeshaji, Seif Shamte, Meneja Masoko, Simon Msoffe na Mhasibu Msaidizi, Fatma Shango.

Wengine ni wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) ambao ni Meneja Udhibiti Ubora, Sadick Materu na Ofisa Udhibiti Ubora, Evans Mwemezi.

Mbele ya Hakimu Mkazi Nyigulila Mwaseba, Tibabyekoma alidai , kiwanda cha TPL kiliingia mkataba na MSD kutengeneza dawa hizo na mwaka 2011 waliagizwa watengeneze dawa hizo.

Alidai kati ya Aprili 5 na Aprili 11 walipeleka makopo 12,252 ya dawa bandia na kulipwa Sh milioni 148.3 kupitia hundi mbili. Alidai Aprili na Mei mwaka 2012, MSD ilisambaza dawa hizo katika vituo vyake vya kanda.

Inadaiwa Agosti mwaka huo, TFDA ilipata taarifa kuwa kuna dawa hizo ambazo ni bandia, wakaagiza kila kanda ifanye ukaguzi.

Aliendelea kudai kuwa baada ya ukaguzi waligundua dawa zilizotengenezwa na kiwanda hicho ni bandia, zina mwonekano tofauti na dawa zilizotakiwa kutengenezwa hivyo waliamuru dawa hizo zirudishwe na zote zilibainika kuwa bandia.

Baada ya kusomewa maelezo ya awali, pamoja na wafanyakazi wa TPL kukiri kiwanda hicho kutengeneza dawa za ARV na kukubali kwamba waliingia mkataba na MSD, lakini walikataa kuwa dawa hizo zilikuwa bandia.

Hakimu Mwaseba aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 30 mwaka huu itakapotajwa tena na Julai 28 mwaka huu watakapoanza kusikiliza mashahidi kwa upande wa Jamhuri.

Inadaiwa Aprili 5 mwaka 2011, Madabida, Shamte, Msoffe na Fatma waliisambazia MSD makopo 12,252 ya dawa bandia, ikionesha zimetengenezwa Machi 2011 na mwisho wa matumizi Februari mwaka jana.

Wanadaiwa pia walijipatia Sh milioni 148.35 kwa madai kuwa ni malipo halali ya dawa hizo.

Materu na Mwemezi wanadaiwa, kati ya Aprili 5 na 13, 2011, Dar es Salaam, wakiwa waajiriwa wa MSD, walishindwa kutumia uwezo wao wote kuzuia kutendeka kwa kosa hilo. Pia washitakiwa wote walisababisha hasara ya Sh milioni 148.3 kwa kusambaza dawa bandia.

Malawi Wameanza Chokochoko Ndege yao Yaonekana Ikifanya Doria Ileje, Wananchi Wataaruki

$
0
0
MBUNGE wa Ileje, Aliko Kibona (CCM) ameomba Serikali ieleze juu ya ndege kutoka Malawi, ambayo imekuwa ikitia hofu wananchi wa Ileje, kwa kuzunguka angani kila mara.

Mbunge huyo alisimama kutoa hoja hiyo baada ya kipindi cha maswali na majibu na kuomba mwongozo wa Spika, Anne Makinda kuhusu suala hilo. Kibona alisema:

“Nazungumzia jambo mahsusi linalotokea katika mpaka wa Tanzania na Malawi katika Jimbo la Ileje. Kwa sasa kuna ndege kutoka nchi ya Malawi inazunguka katika vijiji jirani na tayari imeleta hofu kwa wananchi; na watoto hawawezi kusoma. Ninaomba mwongozo wako kama nipo sahihi. Naitaka Serikali kwanza ieleze ile ndege inatoka wapi na inafanya nini; na Pili naitaka Serikali imfahamishe Mkuu wa Wilaya ya Ileje kuhusu ndege hiyo ili naye awafahamishe wananchi ili wasiwe na hofu”.

Mbunge huyo alisema aliamua kuleta hoja hiyo bungeni, kwa kuzingatia uhusiano uliopo hivi sasa baina ya Tanzania na Malawi. Baada ya maelezo hayo ya Kibona, Spika alisema:

“Suala la Mheshimiwa Kibona linahitaji kufanyiwa kazi sana”. Serikali inaendelea na vikao vyake na itampatia majibu Kibona baada ya kutafakari na kujadili suala hilo.

Alinipenda Sana Kabla Hajapata Kazi, Sasa Kapata Kazi Ananiona Bwege

$
0
0
Najuta ni kiherehere cha moyo wangu kukupenda,kukuthamini na jukujali.

Naombeni msaada,ni mpenzi wangu yapata 1&half year katika mahusiano ni binti ambaye tulifahamiana nae siku moja alipokuja na mama yake mdogo ofisini kwangu kupata huduma,

huyu mama yake mdogo ni mtu ninaefahamiana nae hivyo basi akaona haina budi kunitambulisha kwa mwanae nami nikaona ni vizuri kuanzia hapo binti yule alianza kunizoea na kuonesha dalili zote za kunitaka hata baadhi ya siku hufunga safari na kuja kunisalimia.

nami sikua na hiyana huwa sipendi kumkwaza mtu nikawa nampa ushirikiano tu mzur.

kutokana na ubize wa kazi yangu muda wa story huwa sina nikamwambia kama hutojali uwe unakuja saa 12jioni muda ambao nipo off ila sijui kama mama yako mdogo atakubali akasema hilo halina shida nikimwambia nakuja kwako hawezi kunikatalia kiukweli hilo jibu lake lilinipa ulakini!! 

Basi jioni tukawa tunaenda sehemu ya utulivu tunapiga story sana tunapata chakula then tunaondoka tuliendelea hivyo kwa muda mrefu huwa anakuwa kama na kitu cha kutaka kuniambia lakini anashindwa kila usiku lazima anipigie simu na asubuhi lazima aniulize umeamkaje.

kutokana na tabia zake nzuri alizozionesha kwangu nikaona pengine Mungu ndo kanionesha mke mwema nikamtongoza japo sikutumia nguvu hata kidogo alitabasam na kufurahi nakumbuka alinikumbatia na kunipiga busu hadi nilihisi kuwewesuka kwa joto lake.

Nikawa namhudumia kila alichokitaka nilimpatia na alinipenda na kuniheshimu kama mume wake.

Nakumbuka aligombana na mama yake mdogo akawa kahamia kwa dada yake ni mbali kidogo huko nadhani maisha yalikuwa ya shida,alikuwa akinipigia simu "leo baby sijala"nikawa namsaidia akiugua namtumia pesa za matibabu,

SASA basi miezi miwili imepita kapata kazi basi ni dharau mwanzo mwisho simu hapigi,text hanitumii hata nikimtext baada ya masaa mawili ndo anareply tena shortly wiki tatu zimepita kanipigia simu anaumwa bila hiyana nikaenda kumuona na nilimpa kila kitu anachohitaji mgonjwa sikutaka maongezi nikaondoka zangu hadi leo sijawasiliana nae sababu ninahasira nae sana na ninataka nimfanyie kitu ambacho hatakisahau ili iwe fundisho au nyie wanajamvi mnanishauri nini?

Kama Sio kwa Vitisho Alivyovitoa Zitto kwa CHADEMA Nahisi yangemkuta kama ya Chacha Wangwe

$
0
0
Ladies and Gentlemen.

Friends and Enemies.

Nadhani mnayakumbuka maneno haya...

''MIMI NIMEAGA KWETU NA YEYOTE ANAEFIKIRIA KUNIGUSA KWA NAMNA YOYOTE SIDHANI HATA PANYA HUKO KWAO KAMA ATASALIMIKA''...

Hayo yalikuwa ni maneno ya zitto kabwe kuwaambia wanachadema wenye hila za kila aina na husda kwake za kisiasa na kimaisha kwa ujumla.

Hivi majuzi chuki hizo na uzandiki za chadema zimejidhihirisha zaid baada ya viongozi wa juu wa chama hiko kukacha kuhudhuria mazish ya mama mzaz wa zitto kabwe na kukimbilia kwenye harusi ya mbunge wao huko Arusha.

Hicho ni kipimo kidogo sana cha utu na uwajibikaji hata kama kifo hutokea bila taarifa lakini kwa ulimwengu wa sasa na ufanis wa usafiri wangeweza kuchukua hata chopa kwenda kuonesha ubinadamu wao.

Kwani ukiachilia mbali kuwa mama yule kuwa mzazi wa hasimu wao zitto kabwe pia alikuwa ni mjumbe wa kamati yao kuu ya chama.

Thats why nawaambia kuwa chuki ambayo wahafidhina wa chadema especially top level of management wanayo dhidi ya zitto kabwe siyo ya kifani.

Nashawishika kuamin kama zitto kabwe asingetoa vitisho vike dhidi yao leo hii yangeshamkuta yaliyokamkuta marehemu chacha wangwe.

Hawa jamaa sio watu.

Hakuna asiejua kwamba CCM HAS FAILED US AS A NATION.!!

We cant denie that...CCM HAS FAILED US POLITICALLY EVEN ECONOMICALLY.

UCHUMI WETU UNAPUMILIA MASHINE.

HALI YA UMASKINI HUKU VIJIJIN INATISHA.

THE GAPE BETWEEN THE HAVES AND HAVES NOT LINAZID KUONGEZEKA KILA SIKU.

Tuna kila sababu ya kubadilisha uongozi huu wa CCM.

Especially kama sisi wanakusini ndio kabisa.

In 50 years of indepedence barabara toka Mtwara to dsm haijaisha up to this very moment lakin gesi with less than a year wanauwezo wa kuifikisha bagamoyo kwa bomba.

Its very fascinating.

Sasa basi nani wa kumpa trust ya kuwapa taifa hili??chadema or cuf?

Hell no.

I think punishment ya kuwapa CCM ni kama vile walivyofanya kenya.

Kuwanyima ubunge kwa kura nyingi sana na kuwapa urais tu ili kuondoa kabisa mfumo wa kijinga kule bungeni wa 'Ndioo' na wengi wameshinda.

Sisemi kwamba chadema au cuf wasipewe kura la hasha.wapewe kura nyingi za ubunge ikibid lakini sio kuwakabidhi funguo za taifa hili.

Watatupoteza moja kwa moja wanasiasa sio watu wa kuwaamini.

Binafsi naona chadema wana kazi nzito sana kuwaaminisha watanzania walio wengi kwamba kwenye mobb yao hakuna kasumba za ukanda udini na ukabila.

Mwenye macho haambiwi tazama.na mwenye maskio haambiwi sikia.

Taifa letu tutalijenga au kulibomoa wenyewe.

Wasiaminiwe kiivyo hawa wanasiasa.

Lao wote hawa ni moja tu.

Sema kuna wenye nafuu kias flan lakin kwa chadema mimi nimenawa mikono.

Kukacha msiba kisha kukimbilia harusini!!!?

Daaaah...
Written By THE BIG SHOW Via JF
Toa Maoni Yako

Picha Chafu Za Wema Sepetu Na Diamond Platnumz Zatinga Bungeni..!!

$
0
0
Hilo liliibuka juzi mjengoni katika kipindi cha maswali na majibu ambapo Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Saidi Mtanda alitaka kujua hatua zilizochukuliwa na serikali katika kukabiliana na tabia za watu maarufu kupiga picha zisizo na maadili kisha kuziweka mtandaoni.
Katika kujibu swali hilo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia alisema: “Tunajitahidi kuhakikisha wanaofanya hivyo wanachukuliwa hatua stahili ili kukabiliana na matendo hayo ambayo ni kinyume na maadili.”

Katika kuonesha kutoridhika na majibu ya waziri, Mheshimiwa Mtanda alipopewa nafasi aulize swali la nyongeza alisema: “Mheshimwa spika nahisi swali langu halijajibiwa ipasavyo. Nilichotaka kujua ni hatua ambazo zimechukuliwa kwa baadhi ya watu mastaa kama vile Wema na Diamond ambao hupiga picha zao zisizofaa kisha kuziweka mtandaoni.”
Kufuatia swali hilo, Nkamia alisimama na kujibu kwamba, serikali imeweka mikakati na njia sahihi za kukabiliana na tabia hiyo na kwamba wale ambao watabainika watachukuliwa hatua zinazostahili.

Licha ya majibu hayo, bado wabunge walionesha kutoridhika, hali ambayo Spika Anne Makinda aliiona na yeye akaongezea “Waheshimiwa wanataka kujua na za hivi karibuni zilizovuja mtandaoni” ambapo jibu la Nkamia lilikuwa:
“Mheshimiwa kuhusu hizi picha za juzi zilizosambaa mtandaoni, tunazifuatilia kujua zimeanzia wapi na taarifa zake zikoje kwani hata mimi bado sijaziona ila tutachukua hatua tutakapobaini zilikotokea.

Video: Flora Mbasha Aelezea Kisa cha Mume wake Mbasha Kumtishia Kumuua, na Tuhuma za Kumbaka Shemeji Yake

$
0
0
Muimbaji wa Injili Flora Mbasha amefunguka kuhusu kisa cha mume wake, Emmanuel Mbasha kumtishia kumuua, pamoja na tuhuma za kumbaka shemeji yake mwenye miaka 17, katika Exclusive Interview aliyofanyiwa na Global Publishers.

“Yani alikuwa mpaka ananitukana matusi ya nguoni kama mtu ambaye hajaokoka”, amesema Flora. “Nikahisi labda kuna kitu amabcho kimemuingia, nikamwambia Mbasha au umerogwa ndugu yangu we unaongea vitu gani hivyo, akawa analalamika tu basi we ndio umerogwa sio mimi.”

Flora ameendelea kusema,
“Na kabla sijatoka ndani alisema we lazima leo nikufundishe adabu alinishika tu akaniniga yani mpaka akaniachia maalama kwenye shingo yani hivi ninavyozungumza mpaka saizi bado shingo yangu inauma yale maumivu niliyoyapata hiyo siku. Nikamwambia Mbasha Mbasha Mbasha unaniuwa hata kuongea siwezi”.

“Huo usiku sikurudi nyumbani na asubuhi Jumatatu yule binti akapiga simu hakunipigia mimi alimpigia mdogo wangu mwingine akamwambia tu mimi naondoka ilikuwa mida kama saa 12 kasoro akasema mi naondoka mi shemeji ameninyanyasa amenidhalilisha kanifanyia kitendo kibaya sana, sasa akamuuliza amekufanyia nini akawa hawezi kuongea kwenye simu akamshauri tu kwamba usiondoke subiri dada yako atakapokuja kwanza anarudi muda si mrefu…kwasababu Yule binti tulikuwa tunakaa nae nyumbani sasa ni miaka kama mitatu au mine naishi nae pale nyumbani namtunza mimi ni mdogo wangu kwahiyo nilikuwa naishi nae hapo ndani kwahiyo alikuwa kama ni mtoto wa kwangu mimi tulikuwa tunamlea pamoja na mme wangu.” Amesema Florah Mbasha.

Tazama Video
Bongo5/GPL

Majambazi Yavamia Kituo cha Polisi Kimanzichana na Kuua Askari Mmoja na Kujeruhi!

$
0
0
Tukio hilo limetokea usiku wa saa nane katika Kituo cha Polisi Kimanzichana ambapo askari walikuwa lindo. Wakaja watu kama wanne hivi kwanza wakiwa na mwenzao ana bandeji akijifanya majeruhi wamekuja kuchukua PF3 wakamtibie. Kumbe ni majambazi wana mapanga wameyaficha kwenye makoti. 

Ghafla wakaanza kuyatoa na kuwashambulia askari na mgambo waliokuwa kituoni. Askari Ngonyani ambae sasa ni marehemu alijitahidi kupambana nao lakini alizidiwa nguvu na kumkata kata kwa mapanga pamoja na mgambo wawili waliokuwa kituoni hapo. 
Baada ya tukio hilo, majambazii hayo yalipora bunduki mbili za poliso aina ya SMG na Magobore mawili yaliyokuwa yakihifadhiwa kituoni hapo. 

Nje kulikuwa na sakari mmoja wakike alikuwa nje kwenye gari alijificha kwa kuwa hakuwa na silaha muda huo, na ndiye aliyetoa taarifa kituo kikuu cha Mkuranga mjini kwa OCD.

Bw. Ngonyani alifia hospitali ya wilaya akipatiwa matibabu, na mgambo wawili wanaendelea na matibabu, ila mmoja hali yake imekuwa mbaya na amehamishiwa Muhimbili.

Mnawachukuliaje watu wa GNLD na Forever Living Products?

$
0
0
Jumatano ya wiki iliyo pita , nikiwa maeneo ya Mlimani City, nilikutana na mdada mmoja niliyekuwa nimepotezana naye for like 2 years..Aliomba namba zangu za simu kisha akaniuliza kama nitakuwa na nafasi jumapili ya wiki hiyo around saa saba mchana. I told her what is the problem? akaniambia kuna meeting muhimu sana ambayo angependa kuona na mimi nikishiriki. Nikamwambia hakuna shida. Siku hiyo akaniomba tukutane maeneo ya mwenge, nikamdrive hadi pale ITV kwenye ukumbi wa mikutano wa GNLD. She told me it was a GNLD meeting. She is a member, she has invited me to listen to what they are doing and may be if interested nijiunge nao pia. Nilitaka kurudi hapo hapo but nikasema ngoja niende kuwasikia wana kitu gani kipya ambacho sijawahi kukisikia mahali., ( I knew about this cra.p ) since 2001 and i know what they are actually doing ). 

WAKATI WA KUTOA USHUHUDA

Baada ya introduction na kabobo kutoka kwa aliyekuwa msemaji mkuu wa hiyo meeting, ikafikia zamu ya watu mbalimbali ambao ni memba wa GNLD kutoa shuhuda zao. Huyo msichana alikuwa miongoni mwa walio toa ushuhuda. 

I WAS SO SO DISAPOINTED WITH THEM.

She said, nimejiunga GNLD tangu mwaka 2009 and blah blah, Now ninaingiza PESA NYINGI SANA KWA MWEZI!
Ninaingiza shilingi LAKI SITA KWA MWEZI! ( Hivi kweli Graduate wa Chuo Kikuu anaweza kuwa na mawazo mgando kiasi hiki! Shilingi laki sita kwa mwezi ni pesa ambayo mtu anaweza kuongea na kujisifu mbele ya watu? Hii ni hela unayo takiwa kuingiza kwa siku moja bana acheni ujinga nyie.

Others were talking like, NIMEFIKA HADI NAIROBI MIMI! HUWEZI KUAMINI! UKINIONA UNANICHUKULIA POA, ILA NIMEFIKA HADI NAIROBI KWA KAZI HII HII?

( Seriously kweli! kufika Nairobi nalo ni jambo la kujisifu mbele ya kadamnasi ! )

Wengi wao wanaongea kuhusu laki nne kwa mwezi na utoto utoto kama huo..

BRAINWASHERS : Wakati wa shuhuda kuna jamaa huwa wanasimama na kuongea utoto mwingi like u know nilikuwa meneja wa T.R.A mkoa but nimeacha baada ya kuona GNLD inanilipa.. Mwingine akasema " Nilikuwa muhasibu BARICK, nalipwa MILIONI NNE kwa mwezi, ila nimeacha kazi baada ya kuona GNLD ndio mpango. Plus utoto utoto mwingine kama huo..

Mwisho wa siku i told her, please be serious even for a second, how dare you bring me to a place like this. What do u take me for? or what kind of a fool do u think i am? do u confuse me with a looser or something ? Do i look like someone who is joking about his life? U shall not tell me about this cra.p again... 

Kiukweli niliona amenidhalilisha sana, i say..

These people, are realy dont know what is going on in their lives na wanahitaji kukombolewa. Kuwa describe hawa watu wa GNLD na FOREVER LIVING PRODUCTS in a single word, they are " LOOSERS".
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images