Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo Tanzania

0
0
Kutana Na Mnajimu wa Nyota na Mtaalam wa Tiba Asili Africa na Dunia kwa Ujumla Kutoka ANJUAN COMORO AL_WATWAN MAFUSHO sasa yupo East Africa (Atakuwa Nairobi,Mombasa,Uganda,Burundi,Rwanda na Sehemu Yoyote Atakayo hitajika.. Tanzania Atazunguka Mikoa Yote..)

AL_WATWAN MAFUSHO Ni Mtafiti wa Dawa za Mitishamba na ana uzoefu wa zaidi ya Miaka 18 katika kutoa Huduma zake.. Amesha toa Huduma zaidi ya Nchi 23 Duniani..
AL_WATWAN MAFUSHO Bado anaendelea Kupokea Salam na Shukrani nyingi kwa wale wote waliofanikiwa baada ya kupata HUDUMA na wale wanao Endelea Na TIBA MBALIMBALI..
      Anatibu kwa Kutumia Dawa za Asili ya Africa, Dawa za Kiarabu, Majini na QUR-AN Ukiwa Nchi yoyote...

Kwa Matatizo ya Fuatayo..
•Love spell
•Money spell casting
•Traditional Healer
•Protection Rituals
•Marriage Spells(to heal marriage problems and restore Affection
•Traditional bad luck Removal
•To Prevent divorce and bind lovers together

 MAGONJWA kama > Miguu kuwaka Moto na kufa Ganzi,Kuvimba tumbo,Kisukari, Ngiri ya ndani na Ngiri ya Nje(Busha) Chango kwa Kina Mama,Kifungua Kizazi kwa waliofungwa kishirikina)..Ulijari(Nguvu za kiume?
MAPENZI.Kumrudisha Mpenzi ndani ya Saa  12 tu.. Kumtuliza(Limbwata) Akusikilize na Akupatie chochote unacho hitaji kwa Wakati. Hutuliza wana Ndoa na na Kuzuia Talaka.. Kama Mpenzi wako Anaishi na Mtu mwingine Anao Uweza wa Kusambalatisha mahusiano yao ndani ya Nusu saa tuu(Mfarakano)...

MAFANIKIO.. Mali Bila Masharti, Bahati kwa Wachimba madini.. MAGIC WALLET, PETE ya Bahati, KUSHINDA BAHATI NASIBU na Kusafisha NYOTA(Nuksi Mikosi).. Umaarufu, Heshima mahala pa Kazi,Cheo kazini. Mafuta maalum Yenye Nguvu ya Ziada..
(Amesaidia Watu maarufu, Wachungaji na Wafanya Biashara wengi Duniani)
KINGA..Huzuia Kabisa Chuma Ulete na Kukupa Kinga ya Mwili na Biashara na Kujilinda na mali zako.Humaliza kabisa Kesi ndani ya siku 12 tu(Zindiko) nk..
PIA HUMALIZA KAZI ZILIZOACHWA AU KUSHINDIKANA....
Acha Kuhangaika Njoo Umaliziwe Tiba yako

AL_WATWAN MAFUSHO

Piga Simu +255 759 084 996

Ndoa ya Flora Mvungi na H Baba Yapumulia Mashine..Flora Adai Anamajukumu Mengine

0
0
MSANII wa filamu Bongo, Flora Mvungi amefunguka kuwa, madai ya kwamba yeye na mumewe Hamis Baba ‘H- Baba’ hawako pamoja yametokana na kila mmoja kubanwa na majukumu yake.
Akizungumza na Ijumaa, Flora ambaye kwa sasa anasomea mambo ya Uandishi wa Habari katika Chuo cha Royal kilichopo Ubungo jijini Dar alisema muda mwingi anautumia kusaka elimu na mambo yake binafsi hivyo kuwa mbali na H-Baba ambaye naye huwa jijini Mwanza kwa ishu za kisanii.

“Wanasema eti nimeachana na H-Baba, siyo kweli ni majukumu tu, yeye yuko na mambo yake na mimi nina mambo yangu na hatushirikiani katika mambo ya sanaa ndiyo maana yanaibuka hayo. Ndoa yetu iko poa tu na niseme tu kwamba nampenda sana mume wangu,” alisema Flora ambaye ni mama wa watoto wawili.

Tundu Lissu na Chadema Wanafaidika na Nini Kuzuiwa Kwa Bombadia na Makinikia?

0
0
Najiuliza nishindwe kupata majibu au hawa wenzetu wa Chadema wakiongozwa na Lissu sio watanzania?

Kiukweli wanasheherekea sana kusikia kwamba "Bombadia" limekamatwa na litapigwa mnada na wanaotudai, hivi likipigwa mnada upande wa chadema hasa Lissu anapewa faida gani?

Mbali na bombadia, kutwa kucha wanapiga kelele kuhusu makinikia na wazi kabisa chadema hawataki serikali ishinde vita hii ya ufisadi kiuchumi
Hivi wanafaidika na nini?

Taarifa Kutoka Chadema Kuhusu NDEGE ya Serikali iliyotakiwa Kuja Mwezi Huu Yakamatwa CANADA

0
0

Ifuatayo ni taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mnadhimu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.








Taarifa hii imekuja baada ya jana Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Zuberi Kabwe kupitia mtandao wa Twitter kumuuliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa kwamba nini kimetokea mpaka ndege nyingine aina ya Bombardier iliyotakiwa kuwasili nchini mwezi Julai kutowasili nchini mpaka sasa.

Profesa Mbarawa alimjibu kwamba kuna taratibu za mwisho zinafanywa kabla ya ndege hiyo kuwasili nchini, lakini itawasili.

Habari Mbaya Kwa Wanaongalia Video za Ngono Kwenye Simu.....

0
0

Hatujaribu kumhukumu mtu yeyote kwa mazoea yake. Kila mmoja ana uhuru wa kutumia simu yake kufanya anachojisikia yeye (hata ikiwa ni kwa kuangalia video za ngono kutoka mtandaoni au zilizohifadhiwa ndani ya kifaa hicho).

Lakini inatakiwa uwe makini kama kuwa unapakua app za bure za ngono kwa kutumia simu yako ya Android, kama ambavyo mtaalamu wa ulinzi mtandaoni wa kampuni ya teknolojia ya Dell, Alex Dubrovsky alipogundua kwamba kuna udukuzi unaofanywa ili kuziathiri app hizo.

Wadukuzi wametengeneza mfumo wa kuiathiri simu unaofichwa ndani ya app hizo ambazo zina uwezo wa kuifunga simu ya mtumiaji na hata kukuzuia usiweze kuifuta app hiyo kutoka kwenye simu yako unapotaka kufanya hivyo.

Dubrovsky na timu yake ya watafiti walmebainisha kuwa wadukuzi wana uhakika kabisa wa kutumia app za ngono kufanya mashambulizi yao: mtumiaji anapakua app na kuwapa wadukuzi njia ya kuingia kwenye simu yako na kuitumia kama ipo kiganjani kwake na kwamba inawapa uwezo wa kufanya chochote. Na kwa wale wanatumia Android toleo la 4.4 KitKat, wadukuzi wanaweza kuifunga kabisa simu yako na kukuzuia usiweze kuifungua tena kama wakitaka.

“Kutokana na teknolojia ya sasa, ushambuliaji wa aina hii bado unafanywa kwa kiwango kidogo lakini inaelekea utaongezeka kwa kasi kadri muda unavyosonga mbele,” ameandika Dubrovsky. “Kinachoshangaza ni kwamba mpaka sasa, waliofanyiwa udukuzi huu hawajawahi kuombwa pesa ili simu zao zifunguliwet, na pia kwakuwa bado waliokumbana na udukuzi huu wameweza kutumia tena simu zao ni ishara kwamba mfumo huu wa udukuzi haujaanza kutumiwa kwa kiwango cha juu.”

Kwahiyo, ingawa aina hii ya udukuzi bado ipo kwenye hatua za awali ambao kwa sasa walengwa ni watumiaji wa mifumo ya zamani ya simu za Android na kwa kutumia app za ngono pekee, inatabiriwa kuwa baada ya muda udukuzi huu utatumiwa kwenye mifumo ya kisasa zaidi na app nyingine nyingi zaidi (kama wadukuzi wakiweza kupita kwenye mfumo wa ulinzi wa  Google).

Sumatra, Tanroads na Polisi Waikana Faini ya Sh 200,000 ya Mwendokasi...Watoa Ufafanuzi Huu

0
0

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinazozua mkanganyiko kwenye mitandao ya kijamii kuhusu faini zinazotoshwa na Wakala wa Usimamizi wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa madereva wanaozidisha mwendo wa magari au kufanya makosa mengine ya barabarani.

Kufuatia mkanganyiko huo, Balozi wa Usalama Barabarani (RSA) ambao hujitolea kutoa elimu ya usalama barabarani kuhakikisha watumiaji wote wa barabara wanakuwa salama.

Katika ufafanuzi huo uliotolewa na RSA, kwanza walianza kujibu swali ambalo liliulizwa na wengi kama TANROADS ina mamlaka ya kupiga faini kwa kosa la mwendokasi.

TANROADS kama mamlaka ya usimamizi wa barabara chini ya Sheria ya Barabara (ROADS ACT 2007) inayo mamlaka ya kuwaadhibu wale wote wanaokiuka mwendo uliooneshwa kwenye alama za barabarani au kadiri ya maelekezo yao.

Mamlaka haya wanayapata kwa mujibu wa kifungu cha 32(2) cha Sheria ya Barabara, Na.13 ya mwaka 2007. Hata hivyo, ili mtu atozwe faini chini ya sheria hiyo ni hadi atiwe hatiani.

Inayotia mtu hatiani ni mahakama, hivyo ukikamatwa na TANROADS unatakiwa kufikishwa mahakamani na huko ukipatikana na hatia uweze kutozwa kiasi cha shilingi 200,000 au jela mwaka 1, na sio vinginevyo.

Jambo jingine lilitotolewa ufafanuzi baada ya kuzua maswali ni kama kweli faini za barabarani zinazotozwa kwa kosa la mwendokasi sasa ni sh 200,000 na inagawanyika mara tatu yaani kiasi cha shilingi 90,000 kinaenda SUMATRA, Shilingi 30,000 kinaenda Polisi na inayobaki ni ya TANROADS.

RSA wameeleza kwamba, madai hayo ni upotoshaji. Faini ya chini ya sheria ya barabara ni shilingi 200,000 kwa kuzidisha mwendo kinyume na kifungu cha 32(2) na haigawanyiki.

“Haiwezekani kutozwa faini zaidi ya moja kwa kosa hilo hilo. Kwani sheria inasema mtu hataadhibiwa mara mbili kwa kosa hilo hilo alilolitenda mara moja. Iwapo mtu ameadhibiwa mara mbili adhabu hiyo ya pili ni batili. Ndio kusema kwamba, hata mamlaka zote 3 ziwepo pamoja, ukikamatwa umezidisha mwendo utaadhibiwa mara moja tu na mamlaka ile iliyokukamata.”

Mabalozi hao walilazimika kulielezea hilo baada ya kuwepo swali kama inawezekana mtu mmoja akaadhibiwa na mamlaka zote tatu kwa pamoja endapo zitakuwa barabarani kwa wakati mmoja eneo moja zinafanya operesheni.

Kuhusu uwepo wa sheria 3 kwa jambo hilo hilo moja la kuzidisha mwendo, imeelezwa kwamba kila sheria ilitungwa kipindi tofauti na nyingine na kila sheria inasimamiwa na mamlaka yake bila mamlaka moja kuiingilia nyingine.

SUMATRA anasimamia Transport licensing Act Cap 317 na kanuni zake, ambapo faini ni kati ya shilingi 200,000 na 500,000. TANROADS inasimamia Roads Act 2007 pamoja na kanuni zake za mwaka 2009, ambapo faini ni shilingi 200,000 huku Polisi wakisimamia Sheria ya Usalama Barabarani (Road Traffic Act Cap 168) ambapo faini yake ya papo kwa papo ni shilingi 30,000 bila kujali ukubwa au udogo wa kosa.

Kila mamlaka inasimamia sheria yake na kwamba mamlaka moja mfano Polisi hawawezi kukuandika faini kwa kutumia sheria ya TANROADS. Kama watataka kufanya hivyo watalazimika kukukabidhi kwa mamlaka hiyo.

Washirikishe na wenzako waweze kupata elimu ya usalama barabarani.

Aliyekuwa Mwenyekiti Kamati ya Makinika Ateuliwa Kuongoza Kampuni ya Serikali

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Abdulkarim Hamis Mruma kuwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta (TIPER).

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi, Emmanuel Buhohela uteuzi wa kiongozi huyo umeanza tarehe 17 Agosti, 2017.

Wengi watamkumbukwa Profesa Mruma kwa umaarufu wake aliojizolea wakati akiongoza kamati ya wataalamu waliofanya uchunguzi kwa lengo la kubaini kiwango cha madini kilichokuwemo katika makontena yenye mchanga wa madini yanayoshikiliwa maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kamati hiyo iliyoteuliwa Machi 29 mwaka wakati wa kuwasilisha ripoti ya uchunguzi wake ilisema kwamba imebaini mambo mengi ikiwa ni pamoja na uwepo wa dhahabu kiasi kikubwa kwenye makinikia. Katika makontena 277 yaliyozuiliwa kulikuwa na tani saba za dhahabu yenye thamani zaidi ya shilingi Trilioni moja nukta moja nne saba.

Aidha, katika uchunguzi hiyo Kamati ilibaini uwepo wa madini ya shaba, fedha , sulphur pamoja na chuma ambayo yote kwa pamoja hayakuwa yakibainishwa wakati wa usafirishaji mchanga.

Kabla ya uteuzi huo mpya wa Agosti 17, Prof. Abdulkarim Hamis Mruma alikuwa ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Jiolojia Tanzania.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya August 19

0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya August 19

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo....

0
0

Baba Yake Daimond Aibuka na Kumshauri Mwanae Kuoa Wake Wawili

0
0




Baba Yake Daimond Aibuka na Kumshauri Mwanae Kuoa Wake Wawili
Baba Mzazi wa Msanii Diamond Platinum, Abdul Naseeb amefunguka kuhusu tetesi zinazoendelea za mtoto wake kutajwa kuwa ndiye mzazi halali wa mtoto wa mlimbwende Hamisa Mobeto anayetambulika kwa jina la Abdul Naseeb ambalo ndiyo jina la baba yake na Diamond.


Akizungumza katika kipindi cha SHILAWADU cha Clouds TV Ijumaa hii, Baba Diamond ameeleza kuwa kama Diamond ameamua kumpa mtoto huyo jina lake ni upendo na inaonesha thamani kwake.


Baba Diamond amesema hawezi kumlaumu mwanaye Diamond kwa kilichotokea kwani yeye ni msanii mkubwa anakumbana na vishawishi mbalimbali, hivyo cha kufanya asiendekeze zinaa awaoe wanawake aliozaa nao (Hamisa Mobeto na Zarina Hassan) na awatendee haki kwa kutoa huduma sawa.

Kuhusu wajuukuu zake, Mzee Abdul ameeleza kuwa yeye anawapenda wote ingawa hajawahi kumuona hata mmoja.

Alhamisi hii Diamond aliandika maneno makali mtandaoni yaliyohusishwa kwenda Mobetto ambaye siku chache zilizopita alitangaza jina mwanaye kuwa Abdul Naseeb. Hatua hiyo iliwafanya mashabiki wengi ambao walitaka kumjua baba wa mtoto huyo wa Mobetto kuwa ni Diamond.

Hata hivyo mpaka sasa mkali huyo wa wimbo Eneka hajawahi kutoa neno lolote juu ya mtoto huyo licha ya mama yake pamoja na dada yake Esma kuonekana mara kadhaa wakimtembelea mrembo huyo wakati alipojifungua katika hospitali moja jijiji Dar es salaam.

Nuh Mziwanda Akata Tamaa Ya Kuoa Tena na Kumuachia Mungu

0
0


Nuh Mziwanda Akata Tamaa Ya Kuoa Tena na Kumuachia Mungu
MWANAMUZIKI Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ ambaye hivi karibuni mkewe, Nawal alifunga ndoa na mwanaume mwingine amefunguka kuwa, kwake kuoa tena anamuachia Mungu.
Akibonga na Mikito Nusunusu, Nuh alisema baada ya mkewe kuondoka na kuamua kuolewa bila kumpa talaka suala la kuoa au kutokuoa anamuachia Mungu na kwamba hajaathirika chochote kuhusiana na mkewe kumuacha ila anachofanya kwa sasa ni kuongeza bidii katika kazi.
“Namwachia Mungu ndiye anayejua kama nitaoa au sitaoa tena, ikitokea sawa na isipotokea inakuwa sawa tu kwa sasa moyo wangu una amani tele na nimerudi kwenye dini yangu ya Kikristo, kuhusu mwanangu ataendelea kuwa wangu na mahitaji yote muhimu natoa kama baba,” alisema Nuh.


NIKKI WA PILI : R.O.M.A Ajawahi Kuniangusha Kwenye Uandishi wa Zake za Kiharakati

0
0



NIKKI WA PILI : R.O.M.A Ajawahi Kuniangusha Kwenye Uandishi wa Zake za Kiharakati
STAA wa muziki wa Hip Hop Bongo, Nickson Simon ‘Nikki wa Pili’ amempigia saluti msanii mwenzake, Ibrahimu Musa ‘R.O.M.A Mkatoliki’ kwa kusema anamkubali kwa kuwa hajawahi kumuangusha kwenye uandishi wa ngoma zake kali za kiharakati.

Akichonga na Mikito Nusunusu Nikki alisema, amekuwa shabiki wa nyimbo za R.O.M.A ambazo ni za kiharakati kwa muda mrefu na hajawahi kumuangusha hata mara moja kwenye utunzi na maudhui ya ngoma zake ikiwemo hii mpya ya Zimbabwe.

.
“Licha ya kuwa nami ni mwanamuziki wa Hip Hop lakini namkubali sana R.O.M.A maana kila ngoma anayotoa ni kali, hata huu wimbo wake wa Zimbabwe umenisababisha niendelee kumwona katika jicho pana zaidi, naziona tuzo kadhaa kwa rapa huyo, ukweli ni kwamba anajua kutunga, anajua kuyachezea maneno vile anavyotaka, kweli jamaa anatisha sana,” alisema Nikki.

Keisha Atilia Shaka Uwezo wa Gigy Money na Amber Lulu Kwenye Muziki

0
0

Keisha  Atilia Shaka Uwezo wa Gigy Money na Amber Lulu  Kwenye Muziki
Msanii wa Bongo Flava, Keisha ametilia shaka uwezo wa Amber Lulu na Gigy Money katika muziki huo.



Muimbaji huyo ambaye alitamba na ngoma kama Nalia, Uvumilivu, Nimechoka n.k, ameiambia Planet Bongo ya EA Radio kuwa haoni kama wasanii wapo serious.

“Gigy nadhani kama anatania hayuko serious, yeye na Amber Lulu wanajaribu bado sijaona ni serious musician,” amesema Keisha.

Hata hivyo Keisha hakusita kummwagia sifa Lulu Diva kwa uwezo anaoonyesha katika muziki wake, “anajitahidi, sijui nani anamtungia ana melody nzuri na akiongeza jitihada atafika mbali zaidi,” amesema.

Maalim Seif Amjia Juu Msajili Sakata la Kufukuzwa Uanachama Wanachama Saba wa CUF

0
0

Maalim Seif Amjia Juu Msajili Sakata la Kufukuzwa Uanachama Wanachama Saba wa CUF
Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amemjibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Mhe. Jaji Francis S.K.Mutungi kuhusu sakata la kufukuzwa uanachama wanachama saba wa CUF na kuhusu kutomtambua yeye kama Katibu wa CUF.

Maalim Seif amedai kuwa wao kama CUF hawakubaliani na maamuzi ya Jaji Mutungi kumtambua Profesa Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF kwa kuwa wao tayari walishamfukuza uanachama hivyo si mwanachama wa CUF na wala hana sifa ya kuwa kiongozi katika chama hicho.
"Mheshimiwa Msajili unafahamu fika kuwa Profesa Ibrahim H. Lipumba mwenyewe aliamua kujiuzuilu uenyekiti wa taifa wa Chama cha CUF. Pamoja na kuniandikia mimi nikiwa Katibu Mkuu na pia Katibu wa Mamlaka iliyomchagua (Mkutano Mkuu wa Taifa) kunijulisha kuwa amejiuzulu, pia alikwenda kwenye mkutano na waandishi wa habari akatangaza hadharani kuwa amejiuzulu"
Maalim Seif alizidi kufafanua

"Hatimaye Mkutano Mkuu wa Taifa wa CUF ukaitishwa na Katibu Mkuu akatoa taarifa ya kupokea barua ya kujiuzulu kwa Profesa Ibrahim Lipumba nafasi yake ya Uenyekiti wa Taifa wa Chama. Nikaisoma barua yake mbele ya Mkutano Mkuu wa Taifa, na baada ya mjadala wa kina maamuzi yakachukuliwa kwa mujibu wa matakwa ya Katiba ya CUF ya 1992 (Toleo la 2014) kwa kupiga kura. Wajumbe 437 wakakubali kujizulu kwa Profesa Lipumba dhidi ya Wajumbe 14 waliokataa. Hivyo Profesa Ibrahim H. Lipumba kuanzia siku aliyojiuzulu si Mwenyekiti wa Taifa wa CUF. Profesa Lipumba hana mamlaka ya kukiongoza Chama chetu" alisisitiza
Aidha Maalim Seif anasema kutokana na maamuzi hayo ya CUF baadaye Profesa Lipumba alikuwa akilalamika kwa Msajili wa Vyama Vya Siasa kufuatia maamuzi hayo na baadaye Msajili alitoa msimamo wake kuwa anamtambua Lipumba kama Mwenyekiti wa Taifa wa CUF ingawa Katibu Mkuu wa CUF anasema msajili hana uwezo huo wa kumrudisha Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF

"Najua kuwa alikulalamikia, ukaniletea barua zake za malalamiko na ukataka maoni ya Chama. Nikakujibu kwa maandishi. Kwenda na kurudi ukatoa kile ulichokiita Msimamo wa Msajili juu ya kadhia iliyokikumba Chama! Huo ni Msimamo sio hukumu. Maana kama ni hukumu ningetarajia katika huo ulioita msimamo ungeeleza kuwa kwa uwezo uliopewa na kifungu Na. kadhaa cha Sheria ya Vyama vya Siasa Na.5 ya 1992, au kwa mujibu wa uwezo uliopewa na Katiba ya CUF ya 1992 (Toleo la 2014) katika kifungu Na. kadhaa umeamua kumrudisha Profesa Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CUF. Lakini hukuweza kuonyesha uwezo wako wa kisheria au kikatiba kumrudisha Profesa Lipumba kuwa Mwenyekiti wa Taifa CUF kwa sababu huna uwezo huo kwa mujibu wa sheria za nchi wala kwa mujibu wa Katiba ya CUF" alisema Maalim Seif
Katibu Mkuu wa CUF amesema wao wanazidi kumshangaa msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Mutungi kuendelea kushirikiana na Profesa Lipumba hata katika mambo ambayo yanatia aibu kama kutaka kutoa ruzuku za chama na kumpa Lipumba na genge lake.

"Tunaloshuhudia ni kila kukicha unaendelea kumuunga mkono Profesa Lipumba hata katika mambo ya aibu ya kula njama na Profesa Lipumba kumuwezesha atoe ruzuku ya CUF kinyume na matakwa na taratibu zilizowekwa katika Katiba ya CUF ya 1992 (Toleo la 2014). Narudia kusema kuwa Prof. Lipumba si Mwenyekiti wa Taifa wa CUF. Lakini kutokana na vitendo vyake vya kukosa nidhamu katika kusababisha vurugu katika kikao cha dharura cha Mkutano Mkuu wa Taifa wa chama chetu, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, kwa uwezo lillonao kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya CUF, lilimfukuza Profesa Ibrahim Lipumba uanachama wa CUF. Taarifa hiyo pia nilikuletea, lakini umeamua kuitia kapuni ili kutimiza matakwa yako binafsi.

Ikiwa Profesa Ibrahim H. Lipumba sio mwanachama wa CUF, hawezi kabisa kuwa kiongozi wa Chama, hasa nafasi ya juu kabisa katika Chama. Kinachotokea kikiongozwa nawe na Ofisi yako ni ubabe, kutojali sheria za nchi wala Katiba ya Chama chetu ilimradi mufikie lengo lenu" alisema Maalim
Mbali na hilo Maalim Seif aliweka msimamo wake kuwa Chama Cha Wananchi CUF hakiendeshwi na hisia za mtu wala hakiwezi kupangiwa kiongozi na kudai ni CUF ni taasisi inayoongozwa na sheria za nchi na Katiba na si vinginevyo.

"Mheshimiwa Msajili napenda utambue kuwa CUF ni taasisi, tena Taasisi makini. Kinaendeshwa na kuongozwa kwa mujibu wa sheria za nchi na Katiba ya Chama hicho pamoja na Kanuni ambazo hutungwa na mamlaka husika kila inapohitajika. Sisi viongozi wa CUF tunajitahidi kuongozwa na sheria za nchi, Katiba ya Chama na Kanuni zake katika kukiendesha chama. Hatuongozwi na matakwa ya mtu yeyote, hata kama mtu huyo ni Msajili wa Vyama vya Siasa. Ninavyofahamu Msajili hana mamlaka ya kupandikiza watu anaowataka kuwa viongozi wa chama chetu. Msajili hana uwezo wa kuingilia maamuzi halali ya vikao halali vya Chama chetu. Viongozi huchaguliwa /kuteuliwa na wanachama wenyewe/viongozi halali wa chama" alisisitiza Maalim Seif

Shilole; Nimepata Haja ya Moyo Wangu Tayari Nipo Kwenye Maandalizi Mazuri ya Ndoa Yangu

0
0

Shilole; Nimepata Haja ya Moyo Wangu Tayari Nipo Kwenye Maandalizi Mazuri ya Ndoa Yangu
Msanii Shilole 'Shishi Trump' amefunguka kwa kudai yupo katika maandalizi yake ya mwisho ya kuolewa huku akiwasisitizia mashabiki zake kuwa safari hii hakuna maneno mengi kama zamani kwa kuwa amepata haja ya moyo wake.


Shilole amebainisha hayo baada ya baadhi ya mashabiki zake kutomuamini kwa kauli zake kwa kuwa mara nyingi ameonekana kuwa mwenye 'drama' nyingi katika mambo ya msingi anayowataarifu watu.
"Nipo kwenye maandalizi mazuri ya ndoa yangu lakini safari hii hakuna tena longo longo kama ambavyo 'sometimes' watu walivyozoea blah blah maneno mengi lakini mwanzo nilikuwa sijapata mahali pakufia lakini sasa hivi nimepata inabidi tu nikubali kufa", alisema Shilole.
Pamoja na hayo, Shilole ameendelea kwa kusema "Mungu  akiamua kukuletea vitu vyake, anakuletea tu pale ambapo wewe hukutegemea wala kuwaza kama utapata. Unabaki kusema 'realy' hivyo haya yote ni mipango ya Mungu".
Kwa upande mwingine, Shilole amebainisha kuwa chanzo cha kukutana na mume wake mtarajiwa ni katika sherehe ya msanii Linah Sanga ya 'birthday' iliyofanyikia mjini Zanzibar na ndiyo hapo mapenzi mubashara yakaanza mpaka leo.


Kagame Awaponda Wazungu Katika Sherehe za Kuapishwa

0
0



Kagame Awaponda Wazungu Katika Sherehe za Kuapishwa
Rais Paul Kagame wa Rwanda jana amliapishwa kuongoza taifa hilo kwa miaka mingine saba baada ya kushinda kiti hicho kwa asilimia 98 katika uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni.
Akihutubia baada ya kuapishwa, Kagame alikemea Mataifa ya Magharibi yanayokosoa Afrika na kuilazimisha kufuata mitindo na mifumo ya utawala wa Kimagharibi huku akiwaasa viongozi wa Afrika kupigania kujiwezesha kwa mataifa yao kama linavyofanya taifa lake.

 Marais kutoka nchi 19 za Afrika walishiriki akiwemo, Rais Mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ambaye alichaguliwa tena Agosti 8 kuendelea kuiongoza nchi hiyo baada ya kumshinda Raila Odinga.
Wengine ni marais na Wakuu wa Serikali za Mataifa ya Afrika waliohudhuria sherehe hiyo, alikuwepo Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.

Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo ilimtuma Spika wa Bunge Obe Minaku nayo Tanzania ikawakilishwa na rais mstaafu Benjamin Mkapa. Burundi haikuwakilishwa lakini alikuwepo Rais wa zamani Pierre Buyoya aliyealikwa miongoni mwa marais wastaafu.
Rais Kagame alieleza kuwa miaka 23 baada ya Rwanda kukumbwa na mauaji ya kimbari wananchi wake sasa waliamua kujenga taifa linalojiwezesha.

“Tulilazimika kupambana ili kulinda haki zetu na kufanya kile ambacho ni kizuri kwetu na tutaendelea kufanya hivyo. Lakini Rwanda haiwezi kuwa mfano pekee lazima kila mwananchi wa Afrika, kila taifa lipiganie kuishi bila kuetegemea wengine au bila kujali wengine wanavyotaka. Wanataka mifumo inayofanya kazi vizuri kwetu tuibadilishe na mifumo yao ambayo wananchi wao wameanza kupoteza imani nayo,” alisema Kasgame.

Mara tu baada ya uchaguzi kufanyika Marekani ambaye ni mshirika wa karibu wa Rwanda licha ya kupongeza wananchi wa Rwanda kwa uchaguzi nchi hiyo ilisema kulikuwa na dosari zilizojitokeza kabla na wakati wa uchaguzi.
Isitoshe nchi hiyo ilipokea shingo upande mabadiliko ya katiba yaliyompa fursa rais Kagame kugombea muhula wa tatu madarakani.
Rais Kagame hakutaja ajenda yake ya miaka 7 ijayo, lakini baadhi ya wananchi wameeleza kufurahishwa na mafanikio ya utawala wake.

Goodluck Gozbert Akwapua Tuzo Marekani

0
0



Goodluck Gozbert Akwapua Tuzo Marekani
Msanii wa nyimbo za injili nchini Goodluck Gozbert amepata tuzo ya msanii bora wa kiume kutoka Afrika Mashariki mwaka 2017 katika tuzo za Sauti Awards zinazotolewa kila mwaka kwa wasanii wa nyimbo za injili.

Goodluck ameshukuru kwa kuweza kupata tuzo hiyo na kusema kuwa alimuomba Mungu aweze kumpa heshima na Mungu amejibu maombi yake ya siku zote
"Kwangu mimi hii tuzo ni kitu kikubwa sana hivyo namshukuru Mungu kwa hiyo heshima kwa sababu moja ya kitu ambacho Mungu aliniahidi ni kuniheshimisha, na hii tuzo kwangu ni tuzo ya heshima na kwangu kimekuwa kitu kikubwa kwani Mungu ameniheshimisha na ni moja kati ya ahadi zake, kwangu ni kitu kikubwa sana namshukuru Mungu" alisema Goodluck

Aidha Goodluck amedai kuwa kile alichoimba kwenye wimbo wake 'Ipo siku' ni mapito ambayo yeye mwenyewe amepitia katika maisha ya kila siku na kudai wimbo huo uliweza kuwa mkubwa sana na kufungua shuhuda nyingine nyingi za watu ambao nao walikuwa na magumu kuliko yeye lakini waliweza kufanikiwa kupita na kusimama sehemu nyingine katika maisha yao.

JB:Naachana na filamu na kuwaachia vijana ili nitunze heshima yangu

0
0


JB:Naachana na filamu na kuwaachia vijana ili nitunze heshima yangu
MSANII mkongwe wa filamu nchini, Jacob Steven ‘JB’ ametangaza kujiengua katika uigizaji na sasa ameanzisha Taasisi ya Barazani Entertainment ili kulinda heshima yake.
Katika mahojiano maalum katikati ya wiki hii, JB ambaye anachukuliwa kama mmoja wa waigizaji mahiri kuwahi kutokea, hajaondoka moja kwa moja katika filamu bali amebadili nafasi na sasa atakuwa msambazaji.

“Nimeshakuwa muigizaji na mtengenezaji na nimekuwa nikipeleka filamu zangu na wenzangu mahali palepale siku zote, halafu tunapanga foleni kusubiri kulipwa. Sasa unapofikia hatua kama hii, lazima utazame nje ya boksi.

“Naachana na filamu na kuwaachia vijana ili nitunze heshima yangu, maana nikiendelea, iko siku watanivunjia heshima ambayo nimeijenga kwa miaka mingi,” anasema JB.
“Wasanii tumejichangisha na kuunda taasisi iitwayo Barazani Entertainment, hii itahusika na usambazaji filamu kwa njia za kisasa zaidi. Ni mtandao unaohitaji muda, lakini nikuhakikishie kwamba haya ni mapinduzi makubwa katika filamu.
“Barazani Entertainments itaajiri kijana mmoja, ambaye sisi tutamuita venda, kwa kila nyumba 500 nchi nzima. Katika eneo hili, tunategemea kuwa ajili zaidi ya vijana 9000. Kazi yao itakuwa ni kusambaza filamu kwa haraka popote itakapohitajika.

“Kwa mfano, kama mtu anataka kununua filamu na yupo Chato, ndani ya saa moja filamu hiyo itakuwa barazani kwake, kwa sababu nyumba ya mteja huyo itakuwa miongoni mwa nyumba 500 za venda wetu. Ndiyo maana tunaitwa Barazani kwa sababu itakufikia hapo hapo ulipo.
“Kwa wasanii, kwanza hata kama wana wazo tu la filamu na hawana fedha, wakija kwetu na tukakubaliana na wazo lake, atatengenezewa filamu na kuiingiza sokoni halafu tutakatana zile gharama baada ya mauzo,” anasema JB.

Kuhusu kudorora kwa soko la filamu nchini, JB anasema: “Tatizo tasnia iliingiliwa, kila mtu anadhani anaweza kuwa msanii, mwongozaji au mtengeneza skripti, tulichodhamiria kukifanya ni kwamba tutasambaza filamu zenye ubora tu na hii tutausimamia wenyewe, tunataka tasnia irudi katika mstari ulionyooka.”


Mkuu wa mikakati wa Rais Donald Trump katika Ikulu ya White House Afutwa Kazi

0
0

Mkuu wa mikakati wa Rais Donald Trump katika Ikulu ya White House Afutwa Kazi
Mkuu wa mikakati wa Rais Donald Trump katika Ikulu ya White House Steve Bannon amefutwa kazi na kuwa msaidizi wa karibuni zaidi wa Trump kuondoka katika wadhifa wake.


Katibu wa mawasiliano na wanahabari katika ikulu hiyo Sarah Huckabee Sanders amethibitisha kwamba Ijumaa ilikuwa siku ya mwisho kwa Bannon kazini.
Kuondoka kwake kumejiri baada ya kutathminiwa kwa wadhifa wake na Mkuu wa Watumishi wa Rais John Kelly.

Bw Bannon ni mtetezi wa taifa mwenye kufuata siasa za mrengo wa kulia.

Alikuwa mkuu wa tovuti ya Breitbart.com na alisaidia pakubwa kueneza ujumbe wa “America First” (Marekani Kwanza) wa Trump wakati wa kampeni za urais mwaka jana.

Lakini wakosoaji wamemtuhumu Bannon, 63, kwa kuwa na chuki dhidi ya wayahudi na kuwa mtu anayeamini katika ubabe wa wazungu.

Bw Bannon anadaiwa kushindania udhibiti wa ikulu dhidi ya mirengo ya watumishi wenye misimamo ya wastani ikulu, wakiwemo baadhi ya jamaa wa Trump.

Bw Trump alianzisha uvumi kumhusu Bannon alipoulizwa kuhusu mustakabali wake wiki iliyopita lakini akajibu: “Tutasubiri tuone.”

Mahojiano ya Bannon na jarida la msimamo huru la American Prospect wiki hii yanadaiwa kumkera Trump.

Bannon alinukuliwa akipuuzilia mbali wazo la kutumia jeshi kutatua mzozo kuhusu Korea Kaskazini, jambo lililotazamwa kama kwenda kinyume na msimamo wa Trump.

Aliambia jarida hilo kwamba Marekani ilikuwa katika “vita vya kiuchumi na China” na kwamba analenga kuwaondoa watu wenye msimamo wa wastani serikali ya Trump ambao anaamini wana msimamo usio mkali sana dhidi ya China.

Bannon baadaye aliambia washirika wake kwamba alidhani alikuwa anaongea akipiga gumzo tu na kwamba hakutarajia angenukuliwa.

Sababu Zilizosababisha Beki Mnigeria wa Yanga Kupigwa Chini Hizi Hapa

0
0




Sababu Zilizosababisha Beki  Mnigeria wa Yanga Kupigwa Chini Hizi Hapa
YANGA imeachana na beki raia wa Nigeria, Yisa Anifowoshe ambaye alikuwa akifanya majaribio kikosini hapo akitokea Al Ittihad ya Oman.
Beki huyo alikuwa akipewa nafasi ya kuziba pengo la Mtogo, Vincent Bossou, lakini akashindwa kulishawishi benchi la ufundi hivyo akakosa ulaji.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Dismas Ten, alisema benchi la ufundi la timu hiyo chini ya kocha mkuu, George Lwandamina raia wa Zambia, liliamua kuachana na beki huyo baada ya kubaini ana uwezo mdogo.

“Yule Mnigeria hakusajiliwa kwa sababu hakuwaridhisha watu wa benchi la ufundi, aliachwa Dar es Salaam wakati wenzake wanakwenda Pemba kuweka kambi.

“Mpaka usajili wa wachezaji wa kimataifa unafungwa Agosti 15, sisi tulikuwa na wachezaji sita tu wa kimataifa ambao ndiyo tutawatumia mpaka kipindi kijacho cha usajili kama kutakuwa na uwezekano wa kuongeza mtu mwingine,” alisema Ten.

Hadi sasa wachezaji wa kigeni Yanga ni Youthe Rostand wa Cameroon, Donald Ngoma na Thabani Kamusoko wote kutoka Zimbabwe, Obrey Chirwa (Zambia), Amissi Tambwe (Burundi) na Papy Tshishimbi kutoka DR Congo.

Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images