Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Tundu Lissu Noma Sana....Awachana Mwakyembe na Prof Kabuni.....Adai Wanaogopa Kutumbuliwa na Rais

$
0
0
Rais wa (TLS), Tundu Lissu amefunguka na kusema wabobezi wa sheria nchini akiwepo Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo pamoja na Waziri wa Katiba Na Sheria Prof Palamagamba Kabudi wanamsikitisha kwa kuwa wanashindwa kuishauri vizuri serikali

Tundu Lissu alisema hayo jana wakati akiongea na waandishi wa habari na kudai kuwa wataalam na wabobezi wa sheria ndani ya serikali wamekuwa hawatekelezi wajibu wao vizuri kuishauri serikali vizuri kuhusiana na masuala ya sheria jambo ambalo linaleta athari katika nchi, ikiwepo kuzuiwa kwa ndege ya Tanzania aina ya Bombardier Q400-Dash 8

"Bungeni kulijitokeza mjadala na nikazungumza lakini Dr Mwakyembe na Profesa Kabudi walinijibu kuwa sisi kama nchi huru hatuwezi kuogopa kushtakiwa katika mahakama ya Kimataifa kwa kuvunja mikatba na kuvunja wajibu wetu kwa Jumuiya ya Kimataifa kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa tulioisaini na ambayo sisi ni wanachama. Nisema hapa kwa masikitiko makubwa kabisaa wanasheria waliobobea ambao wanatakiwa kumuelekeza Mhe. Rais sawa sawa wamekuwa hawatekelezi wajibu wao kwa sababu pengine ya kuogopa kutumbuliwa au kwa sababu zingine ambazo zipo kinyume na taaluma zao kabisa moja wapo wa ushauri wa namna hii ni hizi kauli kwamba hatutakiwi kuogopa kushtakiwa katika mahakama za kimataifa ni ushauri ambao ukitoka kwa mwanasheria unasikitika kabisaa"alisema Tundu Lissu 

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini TUCTA Yaliamsha Dude, Ataka Waliofukuzwa Kwa Vyeti Feki Walipwe

$
0
0
Shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini TUCTA limeiomba serikali kuwapa mafao ambao walikuwa watumishi wa serikali na baadaye kuondolewa kwa kosa la kugushi vyeti ama kuwa na vyeti feki.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo Rais wa shirikisho hilo, Tumaini Nyamhokya  amesema kuwa mbali na watumishi hao kuwa na makosa ya kutumia vyeti feki lakini ni watumishi ambao waliweza kulitumikia taifa kwa uaminifu.

Katika hatua nyingine Rais wa shirikisho la amesema kuwa endapo kuna watumishi wa umma wanavyeti feki vinavyosomeka kama vya darasa la saba shirikisho litawachukuliwa hatua  kwa kuweka majina yao bayana na kuongeza kuwa waraka uliotolewa na wizara ya utumishi wa umma na utawala bora haujatoa ruhusa kwa wakurugenzi wa halmashauri na mashirika kuwaondoa kazini watumishi wenye vyeti feki vya darasa la saba.

Kwanii Wanaume Waaminifu Kwenye Uhusiano Huachwa.....

$
0
0

Kuachwa na mpenzi kwa sababu umekuwa ni muaminifu sana yaonekane ni jambo lisiloingia akilini lakini linatokea.

Moja ya mambo ya ajabu unayoweza kuwa ushawahi kuyasikia ni kwamba mara nyingine uamuzi wako wa kuwa mwanaume mwema sana na unayejitahidi kufanya uhusiano wako wa kimapenzi uwe mzuri muda wote unaweza kukugharimu na kujikuta unaachwa kabisa.

Haitakiwi kuwa hivyo lakini mara nyingine inatokea, na inatokea kwa sababu wazo la mwenza wako kuhusu uhusiano wa kimapenzi laweza likawa tofauti na ulionao wewe. Wengine wana mawazo hasi kuhusu jinsi uhusiano/ndoa inavyotakiwa kuwa.

Hii ndio sababu hutakiwi kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na mtu asiye na vipaumbele sawa na vya kwako au asiye na mtazamo mmoja wa kimaisha kama ulionao wewe.

Usipozingatia hilo, utajikuta unaingia kwenye uhusiano na mtu ambaye hatakujali vya kutosha kwakuwa labda humfokei au kumpiga anapokukosea – au utajikuta ameshakupanda kichwani na kuanza kukudai mambo ambayo huwezi kuyatimiza lakini ukajikuta unajitutumua kumtimizia kwa sababu unataka kumfurahisha mpenzi wako na analijua jambo hilo.

Kwa sababu baadhi ya wanaume wanapenda kulinda siri na kuwaachia uhuru wapenzi wao, wanajikuta wakiwapa ruhusa wanawake zao kwenda popote wanapojisikia bila kuwafatilia wanachofanya.

Nini kinafata baada ya hapo? Mwanamke anatoka, anatafuta mchepuko na kukusaliti. Mwisho inakufanya wewe mwanaume uonekane mjinga mbele ya wengine.

Tatizo ni kwamba tabia hii inaibuka kutokana na mazoea ya watu kuingia kwenye uhusiano wakiwa wameficha tabia zao halisi na kuja kufungua makucha yao baada ya kuona ameshaishi na wewe kwa muda mrefu kiasi kwamba huwezi tena kumuacha.

Hii inasababisha wanaume walioathirika kutokana na tabia kama hizi kutoka kwa waliokuwa wapenzi wao wasiweze kuwaamini wanawake wengine tena kwa kuona kwamba wote ni sawa na wale waliowaumiza na kusababisha wasiweze kuwaonesha wenza wao wapya mapenzi kwa kiwango cha juu wakihofia kuumizwa tena.

Kuwa mpole, mkarimu na mwenye upendo wa hali ya juu kwa mpenzi wako ndio jambo linalotarajiwa kwenye uhusiano. Mtu hatakiwi kufanywa ajisikie vibaya kwa kumuonesha mapenzi ya kweli mwenza wake.

Kama wewe unakuwa muaminifu na mwema kwa mpenzi wako lakini umekuwa unadharauliwa au ukaachwa kutokana na tabia hiyo, kaa ukiwa na amani kabisa kwamba lawama za kuvunjika kwa uhusiano huo hazikuhusu wewe – lawama ni za mpenzi wako aliyeshindwa kujua wewe umekuwa mwema kiasi gani kwake.

Msemaji wa Serikali Akiri Ndege Mpya ya Bombardier Q 400-Dash 8 Kushikiliwa Nchini Canada. Awatupia Lawama Wanasiasa...

$
0
0

Ununuzi wa ndege ya 3 ya Bombadier umeingiliwa na mgogoro uliotengenezwa na wanasiasa na watu wasioitakia mema Tanzania.

"Wanasiasa waliotengeneza mgogoro huo wanahujumu maendeleo ya nchi na usalama wa raia"-Kaimu Mkurugenzi Mkuu-Idara ya Habari Zamaradi Kawawa

Ndege ya 3 ya Bombadier ipo na inakuja kwahiyo wananchi waiamini Serikali yao. Serikali imesikitishwa na ushiriki wa wanasiasa na baadhi ya watu kuhujumu maendeleo ya nchi.

Watanzania tuwe wazalendo kulinda,kutetea na kukabiliana na hujuma zozote zinazorudisha nyuma maendeleo ya Nchi.

Watanzania, Tuunge mkono jitihada za Rais Magufuli katika kuleta maendeleo bila kujali itikadi ya chama, kabila au dini. Kuhusiana na mgogoro wa ununuzi wa ndege hatua za Kidiplomasia na sheria zimeanza kuchukuliwa ili kumaliza jambo hili.

Nionyeshe marafiki wa Mh Tundu Lissu Nami Nitakuonyesha Oligaki, Aristrokasi na Timokrasi

$
0
0
Nimepata nafasi ya kumsikiliza Mh Tundu Lissu alipozungumzia suala la la ndege ya bombardia ambayo serikali ya Tanzania inailipia ili iinunue kule nchini Kanada. Lakini kwanza ninaona ni vyema nieleze matabaka ambayo yanaweza kujengeka kwenye jamii kabla ya kutoa maoni yangu kuhusu suala hili.

Wataalam wa sayansi ya jamii wanasema, kutokana na unyonyaji au uporaji wa uchumi ambao unaweza kufanywa kwa njia mbalimbali za kifisadi na kikundi cha watu husababisha kujengeka kwa matabaka katika jamii. Tabaka la kwanza ni la matajiri ambalo humilki sehemu kubwa ya uchumi wa nchi kwa njia ya ufisadi au unyonyaji. Kwa lugha ya kigiriki, tabaka hili linaitwa origarchy (oligaki).

Oligaki huweka rais wao madarakani ili waweze waweze kuendelea kupora utajiri kwa kumtumia rais waliyemweka madarakani. Oligaki wataweka majaji wao kwenye mhimili wa mahakama ili wakiwa na kesi waweze kushinda. Oligaki wataweka watu wao kwenye vyombo vya usalama, wataweka wabunge na madiwani wao ili maamuzi yatakayopitishwa yaweze kuwanufaisha wao.

Kuwepo kwa tabaka hili husababisha kuwepo na matumizi makubwa ya fedha kwenye chaguzi. Oligaki hutumia fedha nyingi kuwanunua watu ili wawapitishe wagombea wao kwenye chaguzi hizo. Wagombea wanaofadhiliwa na oligaki hupita makanisani, misikitini na kwenye jamii wakitoa misaada mbali mbali ili wapate kukubalika hatimae wachaguliwe. Lakini baada ya kuchaguliwa hutetea maslahi ya oligaki badala ya maslahi ya wananchi.

Tabaka la pili ni lile la marafiki au ndugu wa oligaki. Tabaka hili huitwa aristrocracy (asistrokasi). Aristrokasi ni watu waliowekwa na origaki ambao wapo kwenye taasisi za fedha, ubalozi, serikalini, na vyama vya siasa. Tabaka hili kazi yake ni kutetea na kulinda maslahi ya mafisadi ambao hutafuta kushika au wameshika njia kuu za uchumi za nchi na hivyo tabaka hili huwa na upinzani mkubwa na serikali na kwenye bunge kwa lengo lakutetea maslahi ya matajiri. Aidha, tabaka hili hujivika ngozi ya kondoo, kwa kujiita watetezi wa watu wanyonge.

Tabaka la tatu ni la watu wenye tamaa ya madaraka, tabaka hili huitwa timocracy (timokrasi). Watu walioko kwenye tabaka hili huunga mkono hoja za oligaki na aristrokasi na hutamani siku moja waingie kwenye matabaka hayo. Timokrasi ni watu wasio na msimamo wowote, kwani wametawaliwa na tamaa na makuu na kiburi na ubinafsi. Timokrasi ni wepesi kuwasaliti wananchi. Hawana chembe ya uzalendo kwa nchi yao. Timokrasi ni wanafiki. Na mnafiki humtukuza yeyote, kwa lolote, kwa matumaini ya chochote; ndivyo walivyo.

Tabaka la nne ni la wanachi maskini wanaotegemea maisha bora kutoka kwenye serikali walioichagua.

Matabaka haya yamejengeka kwa kasi sana hapa nchini kuanzia mwishoni mwa utawala wa rais Mkapa. Kutokana na kuwepo kwa matabaka haya watanzania masikini waliendelea kushuhudia utajiri wan chi hii ukiwanufaisha watu wachache walioko kwenye matabaka ya oligaki,aristrokasi na timokrasi. Serikali ya awamu ya tano imeonyesha dhamira ya kweli ya kuhakikisha rasilimali za nchi hii zinawanufaisha watu watanzania wote. Lakini ni dhahiri pia kwamba tabaka la oligaki, aristrokasi na timokrasi hawafurahishwi na jitihada za serikali hivyo wanapambanma kuhakikisha juhudi za serikali hazifanikiwi. Ni dhahiri nchi yetu iko kwenye vita ya uchumi. Vita hii ni ngumu sana kupita vita ya kupigania uhuru. Katika vita hii ya uchumi, wapo watanzania watakaogeuka mawe na kuwa wasaliti wakiungana na oligaki lakini wakijificha kwa kuvaa ngozi ya kondoo, wakijifanya ni watetezi wa watanzania maskini wakati ni watetezi wa mafisadi(oligaki).

Hivi Karibuni nilipata nafasi ya kumsikiliza Mheshimiwa Tundu Antipas Lissu mbunge wa jimbo la Singida Mashariki alipokuwa akichangia kuhusu suala la hatua ambazo zimechukuliwa na seriklai kuhusu makinikia au mabaki ya mchanga kutoka kwenye migodi ya dhahabu. Kwa upande wangu nilimuona alitumia lugha kali sana na alikuwa na ghadhabu. Nilijiuliza sana kuhusu mchango alioutoa na ghadhabu alizoonyesha. Imebidi nijaribu kufuatilia misismamo yake, huu ni mtazamo wangu tu.

Mwaka 2015 wakati Lowassa anahamia Chadema kutoka CCM nilipata taabu kubwa nilipomwona Tundu Lissu akiwa ndiye alikuwa akimtetea Lowassa kuhamia Chadema na akimlaumu Dk Slaa.
Wakati wa kampeni 2015 UKAWA ilikuwa na kazi ngumu kuwashawishi watanzania kuhusu suala la ufisadi. Ajenda ya ufisadi ikafa. Uchaguzi ukafanyika, watanzania wakaamua waendelee kuongozwa na CCM. CCM ikaunda serikali.

Serikali ya CCM chini ya uongozi wa John Pombe Magufuli (JPM) ikaanza kushughulikia suala la ubadhirifu, uzembe, na maadili kwa watumishi wa umma. Watumishi wengi walichukuliwa hatua kali na serikali ya CCM chini ya uongozi wa JPM. Mtakumbuka, kuna kiongozi a;liyekuwa analipwa mishahara 17. Mtakumbuka uozo kwenye bandari ya Dar es salaam. Na mtakumbuka kwamba walipatikana wafanya kazi hewa zaidi ya elfu 10, wanafunzi hewa na suala la madawa ya kulevya.
Tundu Lissu na Chadema walilalamika juu ya hatua zilizochukuliwa na serikali, wakisema watu hao waliochukuliwa hatua wanaonewa au utaratibu uliotumika ni mbovu. Mashaka yangu juu ya Mheshimiwa Tundu Lissu yakazidi kuwa makubwa.

Lakini pia mtakumbuka kuhusu suala la UKUTA. Wabunge wa UKAWA walikuwa wakifunga midomo wakiwa bungeni wakidai demokrasia pana. Lakini kwa sasa ni dhahiri kwa watu wengi kuwa ndani ya CCM kuna demokrasia pana kuliko ndani ya Chadema. Hili limedhibitishwa na uchaguzi wa wabunge wa bunge la Afrika Mashariki. CCM ilifanya mchakato wa kidemokrasia kuwapata wabunge wa Afrika Mashariki kuliko ilivyokuwa ndani ya Chadema. Haya yote yaliyofanyika ndani ya Chadema Lissu akiwemo na ni mwanasheria Mkuu wa Chadema. Ninaanza kujiridhisha kwamba Mheshimiwa Tundu Lissu siye niliyemfahamu.

Rais John Pombe Magufuli amedhubutu kuchukua hatua juu ya upotevu wa mapato yaliyotokana na kupelekwa makinikia nje ya nchi na kuagiza uchunguzi ufanyike. Ripoti ya uchunguzi imefichua ufisadi wa kutisha kwenye usafirishaji wa makinikia nje ya nchi. Watanzania wengi wazalendo waliosikiliza ripoti hiyo wameumia sana kwa taarifa zilizomo kwenye ripoti hiyo. Watanzania tumenyonywa kiasi cha kutosha.

Mliopata nafasi ya kumsikiliza Mheshimiwa Tundu Antipas Lissu, amesema Rais amefanya jambo la hovyo sana. Na alionekana kukasirika sana. Hiki kimenishitua sana na ninashawishika kuamini kwamba Lissu hayuko sawa, ana ulemavu usioonekana kwa macho. Tundu Lissu ni mwanasheria mzuri sana lakini amekosa roho ya kuipenda nchi yake, amekosa chembe ya roho ya uzalendo.
Nina amini vyama vya siasa vinatakiwa kuungana katika masuala ambayo yana maslahi mapana kitaifa kama hili suala la makinikia kupelekwa nje ya nchi. Aidha, wataalamu wanatakiwa kujitokeza kutoa ushauri namna ya kuboresha ripoti iliyotolewa na kuisaidia serikali ili iweze kuisaidia serikali kuchukua hatua sitahiki. Lakini Tundu Lissu alikebehi au kudhihaki hatua ikliyochukuliwa na serikali.

Wapo watanzania wengi waliomwamini sana Tundu Lissu na wanataabika na misimamo yake ya hivi karibuni kama ninavyotaabika mimi.

Serikali ya awamu ya tano imefanya utaratibu wa kununua ndege kutoka Canada kwa lengo la kuboresha usafiri wa anga na kuinua utalii nchini. Bila shaka watanzania wengi wanaunga mkono jitihada hizi za serikali kwani ilikuwa ni aibu kwa nchi yetu ilipokuwa haina ndege hata moja.
Siku chache zilizopita, Mh Tundu Lissu ameeleza kuwa ndege aina ya bombardier mali ya serikali ya Tanzania imeshikiliwa huko Kanada na kampuni moja ya ujenzi kutokana na kuidai serikali ya Tanzania. Iwe ni kweli au siyo kweli hoja yangu siyo hiyo. Kinachoendelea kunitaabisha ni kwa nini Mh Tundu Lissu anaonekana kufurahia nchi kupata tatizo hili na matatizo mengine yaliyopita. Haonyeshi kusononeshwa nchi yake inapopata matatizo au misukosuko. Nchi inapopata matatizo au misukosuko Mh Lissu huchekelea. Mtakumbuka serikali ilipochukua hatua dhidi ya ubadhirifu kwenye halmashauri Mh Lissu alisema wafanyakazi waliotumbuliwa walionewa na alisema atawatetea mahakamani, kwenye suala la makinikia Mh Lissu alisema Rais amefanya maamuzi ya hovyo sana na serikali itashitakiwa. Juzi Mh Tundu Lissu alionekana kufurahia ndege ya bombardier kushikiliwa na Kanada. Mh Lissu ni mbunge angeweza kuishauri serikali akiwa bungeni lakini ameona ni vizuri kwake kuidhalilisha serikali kwenye vyombo vya habari.

Mh Lissu haoni kabisa nia njema ya serikali ya kununua ndege ili kuboresha usafiri wa anga nchini. Mh Lissu haoni kabisa nia njema ya serikali kuhakikisha madini yetu yanawanufaisha watanzania, mh Lissu haoni kabisa jitihada za serikali kupiga vita ubadhirifu kwa watumishi wa serikali na halmashauri zetu, Mh Tundu Lissu haoni kabisa jitihada za serikali kuboresha elimu na huduma za afya ? Ghadhabu za Mh Lissu zinatokana na nini hasa ? Au Mh Lissu ana mtetea nani katika hoja zake kama haoni jitihada za serikali zinazowalenga wanachi maskini ?

Je katika misimamo ambayo Mh Lissu ameionyesha kwenye suala la makinikia, suala la ununuzi wa ndege, anampigania au ana mtetea nani ? Nionyeshe marafiki wa Mh Tundu Lissu nami Nitakuonyesha Oligaki, Aristrokasi, na Timokrasi.

By Fred Mpendazoe

Taarifa Nyingine ya Mwanamke MTANZANIA Kukamatwa na Dawa za Kulevya India....

$
0
0
Mamlaka katika Mji wa New Delhi, India zimearifu kuwa zimewakamata Wanawake wawili wa Kiafrika baada ya kuwakuta na Dawa za Kulevya aina ya cocaine yenye thamani ya Dollar Milioni 6 za Marekani.

Katika taarifa zilizochapishwa na DNA INDIA zimesema Narcotics Control Bureau (NCB) imemkamata mwanamke Mtanzania sanjari na Mnigeria wakati wanabadilishana dawa hizo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Indira Gandhi, Delhi Jumatano August 16, 2017.

Kwa mujibu wa Maafisa wa NCB, kufuatia upelelezi uliofanywa, walifanikiwa kumkamata Mtanzania huyo aliyetambulika kwa jina la Beatrice Kemmy Ndyetabula ambaye ana umri wa miaka 40, mara tu alipowasili kwa Ndege ya Go Air flight akitokea Mumbai.

Afisa Mkuu wa NCB alisema:
”Alikuwa amebeba mabegi mawili. Ilikuwa wakati wa kukaguliwa ndipo zilibainika 4 kg za cocaine zikifungwa kwenye vifungashio 27. Alisema kwamba aliwasili Mumbai akitokea Kenya kisha akasafiri hadi Delhi kuukabidhi mzigo huo kwa muhusika.”

Maafisa hao walisema baada ya kumhoji, mwanaume ambaye alikuwa amkabidhi mzigo huo ambaye anafahamika kwa jina la Augustin, naye alikamatwa.

Wema Sepetu na Idriss Wamerudiana? Hichi Hapa Kaandika Wema Kuhusu Idriss Sultan, na Idriss Akaandikiwa Pia..

$
0
0
Moja ya stori inayoenea kwa sasa kwenye mitandao mbalimbali ni kuhusu hii ya Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu ambaye hakuficha hisia zake na kuziweka wazi kwa kuandika ujumbe kwenye Instagram yake kuhusu Idriss Sultan.

Kama utakumbuka Wema na Idriss waliwahi kuwa mapenzini ambapo tangu kuachana kwao hapakuwa na stori zozote zilizowahusu wawili hao lakini leo kupitia Instagram yake Wema ameandika:
”Nikisema sitojivunia ntakuwa ni muongo na mnafki…Proud of you sana…Cant wait for these babies to launch…Im sure zitakuwa Killer…Cause one thing I know is that “Classy” defines you alot better than anything…😊 #SultanXForemen… Goodmorning World.” – Wema Sepetu



Baada ya ujumbe huo wa Wema Sepetu, naye Idriss Sultan aliandika kwenye Instagram yake:
“MOOD: Unakuta kakuposti tu wakati mmekulana block hadi kwenye email 😂… Dahhh 🙈 we mwanamke utakuja uniue 😅.. Thank you mke 😉 … Msishtuke, kwanzia lini mke anaachwa hata aolewe😂. Mungu Ibariki hii launch jamani #sultanXforemen” – Idriss.

Rais MUGABE Kweli Dikteta...Aamuru Siku ya Kuzaliwa Kwake Iwe ni Sherehe ya Kitaifa Nchi Nzima

$
0
0
Serikali ya Zimbabwe imetangaza kuwa siku ya kuzaliwa Rais Robert Mugabe ambayo ni 21 February itaadhimishwa kama sikukuu ya kitaifa.

Tangazo hilo limetolewa August 18, 2017 na Waziri wa Mambo ya Ndani Dr. Ignatius Chombo akisema hilo ni kwa ajili ya heshima ya Rais Mugabe ambaye ameiongoza Zimbabwe tangu ilipopata Uhuru.

Siku hiyo itaitwa ‘Robert Gabriel Mugabe National Youth Day’.

Mbali na heshima hiyo, Miji na Majiji mengi ya Zimbabwe ina barabara zilizopewa jina lake.

Kanuni Kumi '10' Muhimu za Kuwa Mke Mwema Katika Ndoa....Ikizishindwa Imekula Kwako

$
0
0

UHALISI WA MAISHA:
Maisha halisi ya mwanamke anayetarajia kuwa mke/ mke tayari hii ni kumaanisha kuwa wanawake mashujaa tunapaswa kuishi maisha ambayo yanatutambulisha kama mfano wa kuigwa ili tunapozungumza na kufundisha mabadiliko tuwe tunazungumza uhalisia wa maisha yetu ambao unajengwa na haya yafuatayo;

UVUMILIVU:
Kuwa mvumilivu katika maisha yake ya kila siku hasa ukizingatia kuwa tunakutana na mambo mbali mbali yasiyotuvutia katika mahusiano yetu, mengine ni magumu na yanayokwenda kinyume kabisa na matakwa yetu au mazoea yetu ya binafsi. Ifahamike kwamba wewe kama mwanamke shujaa inapotokea umekutana na mambo kama haya hupaswi kuonyesha hasira zako wazi wazi kama vile; chuki, kulaumu, ugomvi, vurugu, malalamiko, manung’uniko, machafuko, kulipa kisasi au aina yoyote ya uharibifu kutokea kwako au ndani mwako. Hivyo mwanamke shujaa huwa ni heri kila anapokuwa kwani hutunza amani ya eneo alipo.

UPENDO WA DHATI:
Maisha ya upendo wa halisi na sio wa kinafki kwa jamii inayomzunguka. Tabia ya upendo wa halisi ina thamani kubwa sana kuliko mali nyingi, pesa, elimu ya juu n.k. wewe unaweza kabisa kuwa na elimu ya juu sana na pesa nyingi sana lakini pasipo upendo wa halisi ni sawa na kusema kopo zuri kwa nje na ndani hamna kitu. Nguzo kuu ya maisha ya mwanamke shujaa ni Upendo wa dhati na uhalisia.

UTII KWA KWA JAMII:
Maisha halisi ya utii katika jamii inayokuzunguka  ili kuweza kuyafanyia kazi yale yote uliyojifunza na pia kuyatenda kwa ufasaha pasipo kupita kona yoyote. Utii  kwa jamii ni ufunguo mmoja wapo utakaokusaidia kufanikisha mambo yako na malengo yako kama mwanamke shujaa.

UAMINIFU KATIKA JAMII:
Kuishi maisha ya uaminifu wa kweli na uhalisia katika jamii inayomzunguka. Uaminifu wa kweli huonekana nyakati zote na siyo tu wakati mtu anapokuwa mbele za watu wanaomjua bali hata wale wasiomjua na hata anapokuwa mahali peke yake aweze kutunza uaminifu wake kwa faida ya jamii nzima. Mwanamke shujaa hujitahidi sana kutunza uaminifu wake katika sekta zote.

UNYENYEKEVU WA KWELI:
Kuishi maisha halisi kabisa ya unyenyekevu kwa jamii inayomzunguka, unyenyekevu ni kinyume kabisa na kiburi, majivuno, kujigamba, kujikweza, kujiinua, kujiona,na hata kjitanguliza mbele kwa kila jambo. Mwanamke shujaa huwa ni mnyenyekevu wakati wote na hana makuu daima.

UWAJIBIKAJI WA DHATI:
Maisha halisi ya uwajibikaji akiangalia majukumu yake yote yanayomkabili na kuhakikisha anafanya kwa moyo bila kuwa na tabia ya kusaidiwa majukumu yake. Mwanamke shujaa ni mfano wa kuigwa kutokana na uwajibikaji wake.

USHIRIKIANO WA DHATI:
Ushirikiano katika jamii inayomzunguka. Sisi wanawake mashujaa yatupasa kujua dhahiri kuwa kazi ya kubadili tabia na kufanya wengine wabadilike kwa lengo la kupata familia bora ni lazima kuwa na ushirikiano wa kweli ambao utajenga tabia ya kuaminiana na kunai mamoja katika harakati hizi za kuandaa/ kujenga familia bora.

UTARATIBU WA KAZI/MPANGILIO:
Katika utaratibu wa maisha yake, pamoja na mpangilio mzuri wa mambo yanayomzunguka hii itakusaidia kuwa na muda mzuri wa kufanya shughuli zako na pia kutekeleza majukumu yako ya kila siku kama mwanamke shujaa. Hakuna njia yoyote ya kukuwezesha kukua na kuendelea katika maisha yako bila kuwa na utaratibu na mpangilio wa mambo yako.

KUFANYA TATHIMINI:
Kuweza kufanya tathimini ya yale yote anayoyafanya katika maisha yake ya kila siku, pengine ni mfanyabiashara, mfanyakazi, mkulima n.k kama mwanamke shujaa yakupasa kutathimini shughuli zako kama zina leta faida/hasara kwa familia na jamii yako inayokuzunguka. Ukiona faida ni kubwa unaendelea na hiyo shughuli lakini kama hasara ni kubwa unajiweka katika nafasi ya kubadilisha aina ya shughuli mara moja bila kupoteza wakati.

Maamuzi ya Hussein BASHE kwa Watoto Wanne Waliomtabiria Ubunge Mwaka 2015

$
0
0
‘MANENO YANAUMBA’ ni msemo ambao wengi huutumia na mmoja wa wanaouamini ni pamoja na Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe ambaye aliwahi kutabiriwa na wanafunzi wa kike wa Shule ya Msingi kuwa atakuwa Mbunge.

Kweli sasa yametimia ambapo kwa kukumbuka tukio hilo, Bashe leo August 19, 2017 kupitia ukurasa wake wa Instagram aliandika ujumbe maalum kwa watoto hao akisema…

”Mwaka 2015 wakati namaliza mkutano ktk kiwanja cha Ushirika watoto hawa wakike Wakiwa wamevaa Uniform zao za shule ya Msingi Ushirika walinisimamisha wakasema maneno yafuatayo”

“Kaka Bashe sisi tunasali kanisani Kila Jpili sisi watatu kukuombea Ushinde na huyu Mwenzetu yeye huwa anakuombea kwenye madrasa Yao uwe Mbunge , nikawauliza kwanini mnaniombea Walijibu tu KITOTO tunakupenda”
“Mimi kwangu sikusahau hili jambo sikulichukulia kwa wepesi niliwatafuta Jana nimewapata Wako Form one na huyo Mdogo yupo darasa la Sita nimeenda kuwatembelea mtaani kwao na kuwaambia Maombi yenu Mungu aliyapokea nimeamua kuanzia sasa nitawasomesha na kuwagharamia Elimu yenu kadri Allah atakavonijaalia”

“Watoto hawa kwangu ilikua deni Hawakua wapiga kura bali walikua na Upendo na mimi na kitu peke ambacho waliweza kuona ni muhimu kunisaidia ni Maombi kwa Mungu ili niwatumikie that’s why my five yrs Agenda namba 1,2,3 ni Elimu AGenda namba 2 ni Afya .Upendo huo walonionyesha kwangu ni deni na mm Upendo nitakaowapa ni ELIMU Naomba Allah a nisaidie”

Jinamizi la TALAKA Linavyotafuna Ndoa za Watanzania////

$
0
0

Ndoto za wanandoa wengi wanapooana huwa ni kuishi pamoja hadi kifo kinapowatenganisha. Vivyo hivyo, wazazi wao, ndugu na jamaa hupenda kushuhudia wanandoa hao wakifanikiwa katika safari ya maisha yao ikiwamo kuwa na familia imara yenye watoto wenye afya bora.

Hata hivyo, siyo wanandoa wote hutimiza ndoto hizo. Kasi ya wanandoa nchini kupeana talaka imeongezeka mara mbili ndani ya miaka sita ya hivi karibuni, jambo linalotishia mustakabali wa ‘taasisi’ hiyo muhimu kwa maisha ya binadamu.

Utafiti wa kufuatilia kaya Tanzania (National Panel Survey) wa mwaka 2014/15 uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) unaonyesha kuwa kiwango cha talaka kimeongezeka kutoka asilimia 1.1 mwaka 2008/09 hadi asilimia 2.1 mwaka 2014/15.

Hii ina maana kuwa kwa sasa kila watu 100 wenye umri wa kuoa au kuolewa waliopo nchini, wawili wametalakiwa kutoka mmoja mwaka 2008/09. Ikumbukwe kuwa utafiti huo unabainisha kuwa watu takriban 40 kwa kila 100 wanaopaswa kuoa au kuolewa bado hawajaingia kwenye ndoa.

Mbali na talaka, kuna wanandoa takriban wanne kwa kila 100 ambao wametengana, jambo linaloashiria huenda nao wakatalikiana siku zijazo iwapo hawatapata suluhu ya kudumu ya tofauti zao.

Kuvunjika kwa ndoa hizo kunawaweka watoto katika maisha magumu ya kukosa mapenzi ya wazazi wote wawili na hata baadhi yao kujikuta wakiingia mitaani kuwa ombaomba kutokana na kukosa huduma stahiki za malezi.

Wataalamu wa masuala ya saikolojia, takwimu na walimu wa dini wanaonya kuwa mwenendo huu ni hatari kwa mustakabali wa Taifa ikizingatia kuwa ndoa ni moja ya taasisi muhimu za kujenga upendo, amani na mshikamano.

Takwimu zinavyoeleza

Matokeo ya utafiti huo uliochapishwa mwaka huu yanakwenda sanjari na yale ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 yaliyobainisha kuwa watu 715,447 walikuwa wametalikiwa (sawa na watu watatu kwa kila 100) wenye umri wa kuoa au kuolewa.

Mikoa ya Kusini Unguja, Mtwara, Mjini Magharibi, Lindi na Kaskazini Unguja inaongoza kwa kiwango cha talaka huku kiwango kikiwa zaidi ya asilimia nne ambacho ni juu ya wastani wa kitaifa wa asilimia tatu kwa takwimu za Sensa mwaka 2012.

Siyo wote wanaotalakiana mahakamani hupeleka matamko ya talaka kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) baada ya takwimu za wakala huo kuonyesha idadi ndogo ya talaka, lakini mwenendo wake unapaa kwa kasi.

Pamoja na kuwa talaka zilizosajiliwa ni chache, Rita inabainisha kuwa zinaongezeka mwaka hadi mwaka kwa kuwa Dar es Salaam pekee zimeongezeka kutoka 106 mwaka 2014 hadi 149 mwaka jana jambo linalosadifu hali halisi iliyotolewa na NBS.

Rita, WLAC zinasemaje?

“Inawezekana kabisa talaka ni nyingi kuliko takwimu zetu kwa kuwa wengi hawaji kusajili matamko ya talaka kutoka mahakamani ili tuwapatie vyeti,” anasema Meneja wa Masoko, Habari na Elimu kwa Umma wa Rita, Josephat Kimaro.

“Tumeanza mchakato wa kuwasiliana na mahakama ili baada ya kutoa tu matamko ya talaka watuletee takwimu zote ili tupate picha kamili.”

Taarifa za Rita zinaonyesha kuwa baadhi ya ndoa zimedumu muda mfupi chini ya mwaka mmoja ikiwamo iliyochukua miezi minane iliyojumuisha kipindi cha mashauriano, kuendesha kesi mahakamani hadi kusajili tamko la talaka Rita. Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inaeleza kuwa tamko la kutengana au talaka hutakiwa kutolewa na mahakama pekee baada ya kujiridhisha na sababu za wanandoa kufanya hivyo.

Kifungu cha 100 cha sheria hiyo kinaeleza kuwa mahakama haiwezi kusikiliza shauri la talaka kwa ndoa zenye umri chini ya miaka miwili na ili isikilize ni lazima ijiridhishe kuwa kuna mmoja wa wanandoa anateseka kupindukia.

Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) kinaeleza katika kijitabu cha ufafanuzi kuhusu sheria ya ndoa kuwa, “mazoea ya wanandoa kupeana talaka mitaani aidha kwa maandishi au kwa mdomo, hizo si talaka kwa mujibu wa sheria ya ndoa.”

“Ni lazima talaka itolewe na mahakama ili kila haki ya mwanandoa itamkwe bayana,” inaeleza sehemu ya kitabu hicho ya WLAC kilichotolewa mwaka 2013.

Kauli za mwathirika

Mwananchi limebaini kuwa ukosefu wa uaminifu na kubadilika tabia baina ya wanandoa ni miongoni mwa sababu kuu zinazofanya wanandoa kutalikiana.

Esther (siyo jina lake halisi) alitalikiana na mumewe mwaka jana baada ya kubaini kuwa alikuwa amebadilika tabia ikilinganishwa na wakati wa uchumba.

“Zamani alikuwa ananishirikisha kwa kila jambo, msikivu, mpole na mfanyakazi aliyeonekana kuwa baba bora wa familia. Lakini baada ya kuoana alianza kuwa mkali hata kwa vitu vidogo licha ya kumwambia kwa upole,” anasema Esther.

Esther (37) anaeleza kuwa kabla ya kuachana na mumewe waliyeoana baada ya kufahamiana kwa miezi tisa, aliwashirikisha wazee wa karibu, familia zao hadi viongozi wa dini lakini bado mwanaume huyo ‘hakuambilika’ jambo lililosababisha waachane.

“Sikupenda tutalikiane kwa kuwa tuna mtoto mmoja, lakini vitimbi vyake vilifanya maisha yawe ya mateso wakati wote. Angalau kwa sasa napumua na nasikia ameshaoa mke mwingine huenda huyo ndiye aliyekuwa akimsumbua,” anasema.

Viongozi wa dini

Viongozi wa dini ambao hufungisha ndoa na kutatua matatizo yanayowakuta wanandoa wanasema haishangazi kuona talaka zikiongezeka kutokana na kushuka kwa maadili miongoni mwa wanandoa ikiwamo uwapo wa muda mfupi wa wachumba kufahamiana vyema. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Baraza Kuu la Kiislamu Tanzania (Bakwata), Sheikh Khamis Mataka anasema kuongezeka kwa talaka ni matokeo ya udhaifu katika taasisi ya ndoa ambayo wahusika wake wanatakiwa wadumu kwa upendo na umoja hadi kifo kinapowatenganisha.

“Kabla ya ndoa unatakiwa uone uliyempata kuwa ana vigezo vinavyotakiwa ikiwamo kujiridhisha tabia na familia yake, uwezo wa kijamii na kama anaweza kuwa mwanajamii,” anasema.

“Bahati mbaya ndoa nyingi kwa sasa ni matokeo ya kukurupuka. Unakuta mwanandoa hajui hata historia ya mwenzie kitu wanachoangalia ni ana mali kiasi gani au anafanya kazi shirika gani.”

Kuingia kwenye ndoa wakati wanandoa wakiwa ‘vipofu’ wa historia ya kila mmoja, kwa mujibu wa Sheikh Mataka kunafanya ndoa ianze kuyumba mara tabia halisi zitakapoanza kujitokeza na kusababisha watalikiane.

Mbali na kutojua historia, Padri wa Kanisa Katoliki, Festo Liheta wa Parokia ya Mtakatifu Kamili ya Kiwalani jijini Dar es Salaam anaongeza kuwa kuongezeka kwa uelewa wa haki za wanawake, kukua kwa kipato miongoni mwa wanandoa na matatizo ya unyumba yanachangia ongezeko la talaka.

Padri Liheta anasema kiutamaduni wanaume wanapenda kutawala, lakini kwa sasa wanawake wengi wanazijua haki zao na hawataki zivunjwe kinyume na wenza wao ambao hawajafikia katika uelewa huo. “Mambo ya kiuchumi yanachangia sana ndoa kuvunjika. Mtu anavyokuwa na uwezo wa kifedha hawezi kukubali kunyanyasika kwa kuwa anaweza kujitegemea tofauti na zamani ambapo akina mama walivumilia kutokana na kipato duni,” anasema Padre Liheta ambaye alifanya utafiti kuhusu kuvunjika kwa ndoa wakati akihitimu Shahada ya Uzamili.

Mbali na masuala ya kipato, padri huyo anasema matatizo ya tendo la ndoa nayo yanachochea ukosefu wa uaminifu hasa pale mmoja anaposhindwa kumridhisha mwenzake.

“Zamani tendo la ndoa lilikuwa kwa ajili ya kuzaa tu, lakini kwa sasa ni pleasure (starehe) hivyo mtu asiporidhika anaenda kutafuta nje. Hapa wanaume wanabidi wajitahidi kuwaridhisha wake zao ili kumaliza mifarakano inayotokana na unyumba,” anasema.

Akifafanua jambo hilo, Sheikh Mataka ambaye ni mwalimu wa dini ya Kiislamu anaeleza kisa cha hivi karibuni alichosuluhisha kilichomhusisha kijana mmoja aliyemkuta mkewe akifanya mawasiliano ya mara kwa mara na mwanaume aliyekuwa na uhusiano naye miaka ya nyuma.

“Pamoja na kumuonya hakusikia. Yule mwanaume anayewasiliana naye alimwambia kuwa ni mwanamke aliyekuwa anamfuata na siyo yeye,” anasimulia Sheikh Mataka akitafsiri kesi hiyo kama mfano wa wanandoa kukosa uaminifu.

NBS yatia neno

Talaka zinazoongezeka kwa kasi haziathiri tu wanandoa husika, bali familia nzima ikiwamo zile zilizozalisha wanandoa.

“Kuongezeka kwa talaka kunahatarisha kuongezeka kwa familia za mzazi mmoja,” anasema Mtakwimu Mwandamizi wa NBS, Abbasy Mlemba . “Watoto wanakosa haki ya kuishi na wazazi wote wawili na hili litaongeza umaskini kwa watoto na kuwafanya wawe ombaomba mitaani, watumikishwe kazi na kuongeza uhalifu na mimba za utotoni.”

Mwarobaini wa talaka

Ili kupunguza tatizo la mifarakano ya awali, Padri Liheta anawasihi wachumba kupeana muda wa kufahamiana vyema kabla ya ndoa ikiwamo kujua asili ya wenza hao, eneo anapotoka kila mmoja, ukoo na wazazi kufahamiana.

Sheikh Mataka anasema uchumi hauwezi kuwa sababu ya wanandoa kutalikiana hivyo watu wanaotaka kuoa au kuolewa wanatakiwa kujitathmini vyema na kuwa na upendo na dhamira ya kweli ya kuingia kwenye ndoa ikiwamo kuwa tayari kuhimili changamoto.

Serikali inasema kuwa inafahamu suala hilo na imeshaanza kutekeleza mikakati ya kulipunguza ili kutengeneza ustawi bora wa familia na Taifa.

Msemaji wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto upande wa maendeleo ya jamii, Erasto Ching’oro anasema wamebaini kuwa mbali na madhara kwa familia, pia ukosefu wa utulivu baina ya wanandoa unapunguza uzalishaji na kurudisha nyuma jitihada za kuelekea nchi ya uchumi wa kati.

“Serikali inataka watoto walelewe na wazazi wote wawili ili kuongeza usalama wao katika kila nyanja ya maisha yao. Hivyo kwenye mpango kazi miaka mitano tumepanga kupunguza kiwango cha talaka kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2021,” anasema Ching’oro.

Katika mpango huo ulioanza kutekelezwa Julai mwaka huu hadi mwaka 2021, Ching’oro anasema wanawashirikisha viongozi wa dini na kimila, asasi za kiraia na maofisa ustawi na maendeleo ya jamii katika utoaji elimu ya uhusiano na ndoa ili kupunguza talaka na ukatili wa wanawake na watoto.

Mwananchi

SOMA Nafasi za Ajira zilizotangazwa Leo Jumapili

$
0
0

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kufika Kileleni Haraka na Kushindwa Kurudia Tendo?

$
0
0
JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUFIKA KILELENI HARAKA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k. Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-

1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250000@250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7 @150000@150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130000@130,000/= BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA. KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255) 0767447444 na 0714335378

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako

MAALIM Seif Aendelea Kula Sahani Moja na Msajili wa Vyama Vingi, Amlima Barua Kali

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ameendelea kulia na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kutokana na kile alichodai ni hujuma anazozifanya dhidi ya chama hicho akishirikiana na Profesa Ibrahim Lipumba.

Maalim Seif alieleza hayo juzi katika barua yake ya kumjibu Jaji Mutungi kuhusu hatua yake ya kuwatambua Profesa Lipumba kama mwenyekiti halali wa CUF na Magdalena Sakaya kama kaimu katibu mkuu wakati viongozi hao walisimamishwa uanachama kwa tuhuma mbalimbali.

Katibu mkuu huyo alifikia uamuzi wa kumjibu Jaji Mutungi baada ya ombi lake la kuwafukuza uanachama wabunge wawili; Sakaya (Kaliua) na Maftaha Nachuma (Mtwara Mjini) kugonga mwamba kutokana na msajili kumtambua Sakaya kama kaimu katibu mkuu kufutia maelezo aliyopewa na Profesa Lipumba.

Profesa Lipumba alimweleza Msajili kuwa Maalim Seif ameshindwa kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kutofika ofisi ya chama hicho zilizopo Buguruni, hivyo akamteua Sakaya ambaye ni Naibu Katibu Mkuu Bara kukaimu ukatibu mkuu.

“Kwa mujibu wa katiba ya CUF mimi, Maalim Seif bado ni katibu mkuu wa chama hiki na nipo hapa nchini, ni mzima na nina akili timamu. Na nafasi yangu haiwezi kukaimiwa na Sakaya ambaye tulishamsimamisha uanachama,” inaeleza barua hiyo.

“Mheshimiwa msajili, nashangaa kwa maelezo yako. Mimi ninavyojua ni kuwa kiongozi anakaimiwa ikiwa hayupo nchini au hawezi kutekeleza majukumu yake. Hivyo ndivyo katiba ya CUF ya 1992 (toleo la 2014) kifungu cha 105 (1) kinavyoeleza.”

Aliongeza kuwa Jaji Mutungi alipokea barua ya Profesa Lipumba Machi 16, 2017 huku yeye akiwa hapa nchini akiendelea na shughuli za chama hasa katika ofisi ya makao makuu ya chama hicho iliyopo Zanzibar kwa mujibu wa katiba ya CUF.

Maalim Seif alisema cha kushangaza Msajili wa Vyama vya Siasa alitoa uamuzi kutokana na maelezo ya mwenyekiti anayetambuliwa na ofisi yake. Kutokana na hilo, mwanasiasa huyo alimtaka Jaji Mutungi kuangalia katiba ya CUF ya mwaka 1992 (toleo la 2014) kifungu Na. 1 (2) vinavyoeleza kwamba makao makuu ya chama hicho yatakuwa katika Mji Mkuu wa Zanzibar na anuani yake itakuwa kama itakavyoamuliwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.

Alisema kifungu cha 1 (3) kinaeleza kwamba kutakuwa na Ofisi Kuu ya Makao Makuu ya Chama Dar es Salaam na anuani yake itakuwa kama itakavyoamuliwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.

“Kwa mantiki hii, Mheshimiwa Jaji Mutungi wewe mwenyewe umeshawahi kuyatembelea makao makuu hayo au bado ofisi iliyopo Buguruni, Dar es Salaam ndiyo Ofisi Kuu ya Makao Makuu?” inahoji barua ya hiyo. Maalim Seif ambaye pia aliwahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, alisema kesi mbalimbali zinazohusu mgogoro wa CUF zimefunguliwa Mahakama Kuu na kwamba, ni vyema Jaji Mutungi angetumia busara kumweleza Profesa Lipumba asubiri hukumu ya mahakama na endapo angekataa msajili na ofisi yake ingejitenga naye.

Mbali na hilo, Maalim Seif alidai kwamba msajili katika barua yake alieleza kwamba amejiridhisha na maelezo ya Profesa Lipumba kuwa yeye hafiki Buguruni na ameshindwa kufanya kazi, lakini hakumtafuta au kumuita ama kumuuliza ili kupata maelezo yake kujua ukweli wa kilichoandikwa na mwenyekiti anayemtambua.  

Mwananchi:

ZITTO Kabwe Aichana Serikali....."Watu Lazima Wahoji Swala la Ndege Mtake Msitake, Msilete Viroja Vyenu"

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Kigoma Ujiji Mh. Zitto Kabwe amekingia kifua kauli inayotolewa na serikali ikiwashutumu vyama vya upinzani kushiriki na kutoa taarifa za ndege kuzuiliwa nchini Uingereza, na kusema kuwa kama wananchi wana kila haki ya kuhoji.

Akijibizana na baadhi ya wananchi kwenye ukurasa wake wa twitter, Zitto Kabwe ameandika akisema suala kama hilo ni lazima watu wahoji, na sio kama hawapendi maendeleo yanayofanywa na uongozi wa Rais Magufuli, isipokuwa wanataka serikali ifanye vitu kwa uhakika zaidi, ili kuepusha kujiingiza kwenye hasara na migogoro kama hiyo.

“Watu ni lazima wahoji mtake mistake, hakuna anayetaka msubiri, tunataka mfanye Kwa  uhakika, tutaendelea kuhoji na lazima  serikali ijibu”, aliandika Zitto Kabwe.

Mh. Zitto Kabwe aliendelea kuandika “hatukutaka mnunue ndege hovyo hovyo, lakini ndege tunataka na tunapanda, mkihojiwa mnaleta viroja, jibuni hoja tu viroja vya nini ?”, aliandika Zitto Kabwe.

Siku ya tar 18 Agosti Mbunge wa Singida Mashariki na mwanasheria mkuu wa CHADEMA Mh. Tundu Anthipas Lissu, alitoa taarifa kuwa kuna mali za Tanzania zimezuiliwa nchini Canada kutokana na deni ambalo serikali inadaiwa na kampuni ya ukandarasi.

 Baada ya taarifa hizo kutolewa na mbunge huyo, serikali ikathibitisha uwepo wa suala hilo na kuongeza kuwa kuna ya watu  wa vyama vya upinzani wameshirikiana na makampuni ya nje kufungua kesi kama hizo, ili kuweka vikwazo kwa serikali kuweza kufanikisha mipango ya maendeleo inayofanywa na serikali ya awamu ya tano.

KUMEKUCHA...Kiongozi wa Kenya Mike Sonko Aamua Kumuiga Rais Magufuli..

$
0
0
Gavana mteule wa jimbo la Nairobi nchini Kenya Mike Sonko, ameingia kitendo cha Rais Magufuli alichofanya baada ya kuingia madarakani cha kuingia mtaani na kufanya usafi, huku akiweka kampeni maalum ya usafi.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Mike Sonko ameweka picha na kuandika kuwa serikali yake itasimima suala hilo ili kuweka mji safi, ili kutunza mazingira na kujiepusha na magonjwa ya kumbukiza.

“Ni muhimu kwetu kujua na kuweka mazingira safi  kwani muhimu kwa maisha yetu, na serikali yangu itawezesha kila kinachohitajika ili kufanya usafi, ili kuonyesha dhamira yetu tumetoa  mapipa ya kutunzia takataka 20, mikokoteni 10, koleo 10, reki 10, viatu, mipira ya mikono  na vitu vingine kwa kila kata hapa Nairobi,  kwa kazi za kawaida:”, aliandika Sonko.

Sonko aliendelea kuandika “Tukitaka kuondokana na kipindu pindu a magonjwa mengine mabaya, tunahitaji kuweka mazingira yetu safi, nahimiza kuacha kutupa taka hovyo, tutumie hivi vifaa ipasavyo na kuhakikisha tunasafisha makazi yetu”, aliandika Sonko.

Mike Sonko aliendelea kusema kuwa wakifanikisha hilo wataweza kuepukana pia na mafuriko, na kuwataka watu wa Nairobi kuwa mawakala wa usafi.


ANAOMBA Ushauri..'Kila Akifika Kileleni Ananing'ata Shingoni'

$
0
0
Nautandika uzi wangu huu hapa kuomba ushauri nifanyaje au dawa yake ni nini katika tatizo hili linalonisibu!

Nina mpenzi wangu niko kwenye mahusiano mwezi wa tisa sasa hivi,tatizo ni pale tunapokuwa ndani ya sita kwa sita huwa ananing'ata .Hii hali humtokea mara nyingi sana hasa hasa kipindi kile ambacho anakuwa anafika orgasm(female),hapa nilipo ukinikagua vizuri kifuani nina makovu kadhaa hadi kuwa chest game inakuwa aibu

Yani inakuwa shida kiasi natakiwa kujihami mara nikiwa namshughulikia hasa pale anapokuwa anakaribia orgasm kwa kutafuta stail ya kujiweka mbali na mdomo wake-lakini kama unavojua kipindi hiki mtu anaongezeka nguvu mara 100 so mara nyingi mimi naishia maumivu,na nimekuwa type ya wanaume ambao na last long in bed (enough stamina) hivo basi katika one shot naweza hata ng'atwa mara 3

Nikimuuliza mwenzangu anasema yeye hua hajitambui anapofanya kitendo hiko(biting) na kuishia kuni promise atajitahidi kujizuia next time lakini wapi -game inaishiaga vilevile.Kwa hali hii mimi naona kero hadi nafikiria kumuacha hali nampenda tena sana,sasa kabla sijafanya hivyo naombeni ushauri nifanyaje au hii hali inatibika na dawa yake nini?

Abadala

KAULI ya Serikali Kuhusu Wanafunzi Kwenda Vyuo Vikuu Bila Kuhitimu Kidato cha Sita....

$
0
0

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inapenda kuutarifu umma kuwa taarifa zinazosambaa kwa kasi  kwenye mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari

“Serikali yapiga Marufuku Kusoma Shahada bila kupita Kidato cha Sita,” tarifa hiyo siyo ya kweli na haijatolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mh. Joyce Ndalichako.Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako hajatangaza popote na kuwa taarifa hiyo haina ukweli wowote.
Profesa Ndalichako yuko Mkoani Kigoma kwenye ziara ya ufuatiliaji wa Miradi ya Elimu, inayotekelezwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara yake.

Vile vile Wizara inapenda kutoa wito kwa watanzania kuacha kutumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuupotosha umma kwa taarifa ambazo siyo sahihi na  hazina ukweli wowote.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ina utaratibu wake wa kutoa taarifa hivyo inawaomba radhi wale wote waliopata usumbufu kutokana na kusambaa kwa taarifa hiyo.

Imetolewa na:

Mwasu Sware

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini,

WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA

19 Agosti, 2017

KIMENUKA...Zitto Kabwe Adaiwa Kuihujumu NDEGE Mpya Serikali Nchini Canada....

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amekanusha vikali taarifa zinazosambazwa kwamba ameshiriki katika kuhakikisha ndege mpya ya serikali iliyonunuliwa nchini Canada inashikiliwa kufuatia deni ambalo serikali inadaiwa.

Katika taarifa aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Facebook, Zitto amesema kwamba madai hayo nitakata zinazotengenezwa na wapika propganda.

“Mimi binafsi filosofia yangu ni rahisi Sana ‘My Country, Right or Wrong’. Maneno yanayosambazwa kuwa nimeshiriki kuwezesha ndege ya Bombardier iliyonunuliwa na Serikali kwa niaba ya ATCL kukamatwa huko Canada ni takataka tu zinazosambazwa na wapika propaganda.“

Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo alisema kwamba, suala la ndege ya serikali kuzuiwa Canada lisifanywe ni la ushabiki kama ushabiki wa mpira. Ni suala la Nchi hili na mjadala wake uwe na hadhi hiyo. Kitendo cha Msemaji wa Serikali kulaumu wanasiasa kwa jambo la kisheria kama hili ni utoto. Hakuna mwanasiasa anayeweza kushirikiana na kampuni za kigeni kuhujumu nchi.

Alisema wao kaka vyama vya upinzani ambavyo vipo nje ya serikali wajibu wao ni kuhoji jambo lolo na pia ni haki yao kupata taarifa zozote kutoka mahala popote zitakazosaidia kuisimamia Serikali.

“Wajibu wa Serikali ni kujibu hoja zinazoibuliwa. Majibu ya Msemaji wa Serikali yanataka kuligeuza suala hili kuwa la kisiasa na watu wameangukia kwenye ushabiki huo. Hili ni suala la kisheria na suala la nchi ambayo sisi wote tuna maslahi ya kuona inakwenda mbele,” alisema Zitto.

Kuhusu ndege ya serikali kuzuiliwa kutokana na deni inalodaiwa, Zitto alisema, nchi kudaiwa sio dhambi. Hata mataifa makubwa duniani yanadaiwa. Watu binafsi tunadaiwa sembuse Serikali? Mimi ninadaiwa madeni ya uchaguzi mpaka sasa na wengine wamenipeleka mahakamani. Sio dhambi kudaiwa. Muhimu ni 1) Deni limetokana na nini? Ni maamuzi mabovu ya kisiasa? 2) unalipa deni hilo au kuweka mikakati ya kulipa?

Serikali yetu inafahamu kuwa nchi yetu ina madeni mengi na miongoni mwa madeni hayo yameshaamuliwa na mahakama. Kinachopaswa ni kuwa na maarifa ya kupita ili kuzuia mali zetu nje kuzuiwa kama ilivyo kwa ndege hii. Serikali iwe wazi kuhusu suala hili la ndege. Je! Ile ya Boeing (Terrible Teen) ipo salama? Madeni mengine yenye amri ya mahakama ni yepi? Kwanini Serikali inasubiri kuhojiwa ndio itoe taarifa? aliandika Zitto Kabwe.

Zitto ameitaka serikali kuelezea nini kimetokea na iachane na tabia ya kutafuta mchawi kwamba wanasiasa ndio waliosababisha ndege hiyo kuzuiwa.

Kwa mujibu wa Tundu Lissu, ndege hiyo imezuiliwa nchini Canada na Kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd inayoidai serikali USD 38.7 milioni (Tsh 87 bilioni). Ndege hiyo mpya ya serikali ina thamani ya Tsh 70.4 bilioni.

TANZANIA Yashinda na Kuwa Nchi Bora Zaidi Kuwa Utalii Afrika 2017

$
0
0
Mtandao wa safaribookings.com wa nchini Uholanzi imefanya uchunguzi na upembuzi wa kina katika nchi mbalimbali za Afrika ili kuweza kujua nchi ambayo ndiyo kituo bora cha utalii kwa mwaka 2017.

Katika uchunguzi huo, Tanzania imeibuka kuwa kituo bora cha utalii Afrika kwa mwaka 2017 huku ikifuatiwa na Zambia na Botswana.

Machapisho zaidi ya 2,500 yalitumika katika uchunguzi huo. Ushirikiano mwingine ulipatikana kutoka watalii kutoka maeneo mbalimbali dunia.



Nyaraka nyingine zilipatikana kutoka kwa waandishi maarufu wa vitabu vya kuongozea watalii kama Lonely Planet, Rough Guides, Frommer’s, Bradt and Footprint ambao pia ni watalaamu kutoka SafariBookings.

Mtandao huu ulifanya uchunguzi kama huu mwaka 2013 ambapo Tanzania iliibuka mshindi. Kwa kipindi cha muda mrefu hawakufanya tena utafiti sababu ya mambo kubadilika, lakini jambo ambalo halijabadilika ni ubora wa Tanzania.

Baadhi ya waliohojiwa walisema kuwa, Tanzania ni bora kutokana na uwepo wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Bonde la Ngorongoro (Ngorongoro Creater). Wengine walisema Tanzania kuna wanyama wa aina mbalimbali, lakini pia huduma zinazotolewa kwa watalii ni bora zaidi Afrika.
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images