Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104428 articles
Browse latest View live

Kauli ya Michael Wambura Baada ya Kurudishwa Kwenye Uchaguzi wa Simba

0
0
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

SAA chache baada ya kamati ya Rufani ya shirikisho la kandanda Tanzania, TFF, chini ya mwenyekiti wake, Wakili Julius Mutabazi Lugaziya kumrudisha, Michael Richard Wambura kwenye uchaguzi wa Simba sc, mgombea huyo amesema sasa haki imetendeka na uchaguzi utakuwa wa amani.

Wambura amezungumza na mtandao huu dakika chache zilizopita na kusema kuwa anaufananisha ushindi wake kama mchezo wa mpira wa miguu.

“Mpira wa miguu una mechi ya nyumbani na ugenini, unaweza ukafungwa ugenini, ukashinda nyumbani, bila kujali umeshinda goli ngapi, lakini ninachoweza kusema ni kwamba haki imetendeke, matokeo yametoka, tujipange kwenda kwenye uchaguzi ili wanasimba wapate viongozi wao wanaowataka”. Amesema Wambura.

Mgombea huyo ameongeza kuwa hiki sio kipindi tena cha kutafuta mchawi, bali ni kipindi kinachohitaji wanasimba kuwa makini.

“Ni kipindi cha kuwa makini, kuweka sera zetu hadharani, malengo yetu hadharani, ili wana Simba wapate fursa ya kuchagua kwa sera, nadhani hilo ndio ombi langu”. Ameongeza Wambura.

Hata hivyo, Wambura amesema kesho ataongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Simba mtaa wa Msimbazi, kariakoo jijini Dar es salaam.

- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=1912#sthash.rYmIk93x.dpuf

Breaking News:Soko la Karume Lateketea Kwa Moto Usiku

0
0



Usiku wa kuamkia leo umekuwa mbaya kwa wafanya biashara wa Eneo la karume baada ya mabanda ya wamachanga katika eneo hilo kuteketea kwa moto , Chanzo cha moto huo kinadaiwa kuwa ni  "Mama Ntilie" (ambao inasemekana huchemsha maharage na kuyaacha usiku ili yaive vizuri)

Moto ulikuwa ni mkubwa sana kiasi cha Fire kushindwa kuuzima ikichukulia walichelewa kufika katika eneo la tukio , Soko la karume ni lile lililo pale karibu na kiwanda cha bia cha TBL

Majibu ya Mbunge Salvatory Machemli kuhusu Picha za Utupu Zilizosambazwa Zenye Sura Yake.

0
0
Siku chache zilizopita kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii zilisambazwa picha mbalimbali za Wabunge wa Bunge la Tanzania zikionyesha wakiwa kwenye sehemu za faragha sehemu ambazo hutumiwa zaidi na wapenzi na zaidi ni namna ya picha hizo maana zingine zilikua ni zaidi ya nusu utupu.
Salvatory Naluyaga Machemli mbunge wa Ukerewe kupitia Chadema ni miongoni mwa wabunge waliotajwa kuwepo kwenye orodha hiyo na ni baada ya kusambaa kwa picha zinazomuonyesha akiwa na binti wakiwa zaidi ya nusu utupu,Soudy brown kaongea nae majibu na kila kilichozungumzwa kipo hapa.

Bonyeza play kusikiliza.

Picha za Gari Mpya ya Ney wa Mitego Aliyojinunulia Mwenyewe Kama Zawadi ya Siku yake ya Kuzaliwa

0
0
mastar mbalimbali wa Tanzania wamekua wakionyesha magari yao ambayo mengi yamekua ya kifahari,kwa mwaka 2014 ni mwaka unaonyesha wasanii wengi kumiliki magari ya gharama zaidi,mpaka sasa ni zaidi ya wasanii watano ambao wameonyesha magari yao ya kifahari.
Star wa single mbalimbali ikiwemo Nakula Ujana Ney wa Mitego nae yupo kwenye list ya wasanii wanaomiliki magari haya ya thamani hii ya Ney wa Mitego ni Nissan Morano ya mwaka 2007 na hii inakamilisha gari la pili kwenye kipindi kifupi baada ya ile Toyota Mark X.
Kwa maelezo ya mwenyewe Ney ingawa hakutaka kutaja bei kamili aliyonunulia lakini kasema ni zaidi ya Milioni 35 za Kitanzania,na hii aliinunua kama zawadi kwake siku ya June 09 alipokua
anaadhimisha siku yake ya kuzaliwa.




Waganga wa Kutibu Kwa Kutumia Ngono na Nguo za Ndani Wakamatwa Temeke

0
0
POLISI Mkoa wa Temeke, imewakamata vijana wawili wanaodaiwa kujifanya waganga wanaotoa tiba kwa wanawake, ambayo masharti yake ni kushiriki nao ngono bila kinga na kuacha nguo za ndani, ili zifanyiwe dawa zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Englibert Kiondo, alidai vijana hao Juma Hemedi (32) na Abrahman Mulsin, wote wakazi wa Tandika, baada ya kushiriki ngono na wagonjwa wao huwaambia waache nguo za ndani.

Kamanda Kiondo alidai baada ya kupata malalamiko, Jeshi la Polisi lianzisha msako na kuwapekua waganga hao, ambapo walikutwa na nguo za ndani za kike 22, ambazo alisema zitakuwa ushahidi wa kuingiliwa kimwili kwa wanawake hao. Vitu vingine wanavyodaiwa kukutwa navyo ni pembe, tunguli, makopo ya dawa na vibuyu.

“Sheria iko wazi, inasema mganga anapofanya ngono kama uganga anakuwa amebaka, na hii ni kwa mujibu wa Sheria ya Kanuni ya Adhabu 130 sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002,” alisema Kamanda Kiondo.

Kwa mujibu wa madai ya Kamanda Kiondo, vijana hao wamekuwa wakijifanya waganga wa tiba asili, husambaza vipeperushi sehemu mbalimbali za jiji kutafuta wateja.

Mbali na tiba hiyo ya kupata watoto, inayotolewa kwa kushiriki ngono na mganga, Kamanda Kiondo alidai watuhumiwa hao wamekuwa wakidai kutibu magonjwa mengine kama kisukari, vidonda vya tumbo, nguvu za kiume, kukuza maumbile, kupata kazi, kufaulu mtihani, mvuto wa biashara, kumilikishwa jini na kupewa pete ya bahati.

 Katika tukio lingine, Polisi inamshikilia kijana mwingine mkazi wa Tandika Devis Corner, Maalim Kimti Rita au kwa jina lingine, Joseph Rita anayedaiwa kutapeli Sh milioni 11 akijidai kumfanyia dua mfanyabiashara aweze kukuza biashara yake.

Alidai kuna mfanyabiashara mwanamke ambaye alitoa Sh milioni 11 kwa Maalim Rita, akidanganywa kuwa atafanyiwa uganga ili afanikiwe katika biashara yake, lakini alipoona hakuna alichopata, akaamua kutoa taarifa Polisi.

Kamanda Kiondo alisema jamii inapaswa kuelimishwa kuachana na mambo hayo, kwa sababu tiba yake haipo kwa waganga wa jadi na kwamba hakuna uhusiano kati ya kufaulu na kwenda kwa waganga isipokuwa bidii ya kazi.

“Watu wengi wamelalamikia matukio ya namna hiyo, sasa tumeamua kuweka wazi kwa umma kwa kuwa watu wanateketea kwa kukosa elimu… watu wanauza nyumba magari na mali zao, kwa ajili ya kupata fedha za kupeleka kwa waganga wakiamini kuna tiba, huu ni utapeli vijana kama hawa hawawezi kukupa utajiri wala mtoto,” alisema Kamanda Kiondo.

Alisema waganga hao wamepata vyeti vya kufanyia kazi hiyo ya uganga wa jadi, lakini wanachofanya ni kinyume na kazi hiyo ambapo aliahidi vyeti vyao kuchunguzwa, kuona wamevipataje na kuwasiliana na Wizara ya Maliasili na Utalii, ili watambue pembe wanazotumia ni za mnyama gani.

Unakumbuka Mauaji ya Erasto Msuya? Mahakama Yaelezwa A-Z Jinsi Alivyouwawa Kwa Kutumia Bunduki ya SMG

0
0
Moshi. Bunduki ya kivita aina ya Sub Machine Gun (SMG) iliyotumika kumuua mfanyabiashara tajiri wa Mirerani, Erasto Msuya, ilinunuliwa kwa Sh4 milioni nchini Kenya, Mahakama imeelezwa.

Imeelezwa pia kwamba wauaji wanne waliokwenda eneo la tukio kutekeleza mauaji hayo, walilipwa Sh5 milioni kila mmoja na washirika wao wakilipwa Sh3 milioni kila mmoja.

Hayo yamo katika maelezo ya mashahidi 57 kwa washtakiwa yalisomwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa Kilimanjaro, Munga Sabuni juzi na mawakili wa Serikali, Stella Majaliwa na Florentina Sumari waliokuwa wakipokezana kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni.

Msuya aliyekuwa anamiliki vitega uchumi kadhaa, aliuawa kwa kumiminiwa risasi Agosti 7, mwaka jana saa 6:30 mchana Mijohoroni wilayani Hai, Kilimanjaro na katika maelezo yake, mtaalamu aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu, Dk Paulo Christopher alisema ulikuwa na matundu 26 ya risasi yaliyotokana na risasi 13 zilizoingia na kutokea upande wa pili zikichanachana utumbo, mapafu, ubongo na bandama.

Ushahidi huo unadai kuwa katika eneo la tukio, polisi waliokota maganda 22 ya risasi za SMG.

Mtaalamu wa makosa ya kijinai ya kompyuta, Koplo William Obeid alieleza kuwa katika kufanikisha mauaji hayo, laini mpya tano za Airtel zilisajiliwa kienyeji, zote zikiwa na jina la Motiti Ndoole na laini iliyotumika kumvuta marehemu eneo la tukio ilikuwa 0682405323.

Katika ushahidi huo, Inspekta Samwel Maimu alidai kuwa washtakiwa walikiri kosa na kueleza kuwa bunduki aina ya SMG ilinunuliwa Namanga, upande wa Kenya. Inspekta Maimu alidai kuwa mshtakiwa wa kwanza, Shariff Mohamed ndiye aliyetoa Sh4 milioni za kununua silaha hiyo na kutoa fedha za kusajili line mpya tano za simu.

Pia alidai kuwa mshtakiwa huyo, ndiye aliyetoa Sh3,350,000 zilizotumika kununulia pikipiki mbili moja aina ya Toyo na nyingine King Lion zilizotumiwa na wauaji siku ya tukio.

Katika maelezo hayo yaliyosomwa mahakamani, mshtakiwa wa kwanza (Shariff), anadaiwa kueleza namna alivyotoa maagizo ya kusajiliwa kwa line mpya.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kueleza kuwa mshtakiwa wa saba, Ally Mussa ndiye aliyemshauri atoe jiwe moja la Tanzanite litakalotumika kumshawishi marehemu Msuya. Katika maelezo hayo, ilidaiwa kuwa ndiye aliyelipa Sh4 milioni za kununua bunduki hiyo ya SMG na kwamba siku ya tukio aliibeba kwa gari lake hadi eneo la tukio na kuwakabidhi wauaji.

Katika ushahidi huo, mshtakiwa wa tano, Karim Kihundwa anadaiwa kueleza kuwa yeye ndiye aliyemmiminia risasi marehemu ambazo hajui idadi yake na kwamba bunduki hiyo aina ya SMG waliinunua Namanga na ilihifadhiwa nyumbani kwa Shariff sambamba na pikipiki zilizotumika.

Katika maelezo yake, mshtakiwa wa saba, Ally Mussa au Majeshi anadaiwa kueleza kuwa ndiye aliyepewa kipande cha madini na kwenda kumuuzia marehemu hotelini kwake SG Resort siku moja kabla ya mauaji.
Mshtakiwa huyo anadaiwa kukikiri kuwa siku hiyo alikwenda na vipande vitatu vya madini lakini akakataa kuuza vipande viwili akisema yuko na wenzake na kukubaliana kufanya biashara siku inayofuata na kwamba siku ya mauaji, yeye ndiye aliyemtumia ujumbe wa maandishi ya simu marehemu na kukutana naye na kwenda naye hadi eneo la mauaji.

Katika maelezo yake shahidi huyo anadaiwa kusema: “Tulipofika Mjohoroni, Erasto alishuka ili kukutana na Karimu, mimi nikabaki kwenye gari, ndipo Karim akatoa bunduki na kuanza kummiminia risasi Erasto.”

Alidai kuwa baada ya mauaji hayo, alipakia pikipiki aina ya Toyo iliyokuwa ikiendeshwa na Karimu aliyekuwa na bunduki hiyo ya SMG.

Mshtakiwa wa pili, Shaibu Jumanne maarufu kama Mredii, anadaiwa kueleza kuwa Julai 26 mwaka jana, Shariff alimfuata na kumweleza kuwa kuna kazi ya kumuua Erasto.

“Nilimweleza siwezi kuifanya ila nitamtafutia vijana wa kufanya. Alinipa Sh300,000 na kunijazia mafuta ‘full tank’ niende kuwatafuta Ally Majeshi na Jalila,” ushahidi huo umedai.

Kesi hiyo, imehamishiwa Mahakama Kuu ya Tanzania na inasubiri kupangiwa Jaji.

Wizi NMB Mwanga: Wakenya Wawili Wahukumiwa Kifo

0
0
Raia wawili wa Kenya, Samweli Saitoti (Saimoo) na Michael Kimani (Mike), wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), PC Michael Milanzi mwaka 2007.

Raia hao ambao walipambana na polisi jijini Arusha kwa saa sita wakijihami kwa silaha za kivita yakiwamo mabomu ya kurusha kwa mkono na bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG), walifanya mauaji hayo yaliyoambatana na uporaji wa Sh239 milioni mali ya Benki ya NMB, Julai 11, 2007.

Pia, Jaji Kakusulo Sambo wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, amemhukumu Mtanzania, Calist Kanje kwenda jela miaka mitano kwa kuwasaidia wauaji hao wasikamatwe na polisi baada ya kufanya mauaji.

Akitoa hukumu hiyo jana, Jaji Sambo alisema upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Ladslaus Komanya, Stella Majaliwa na Ignas Mwinuka, umethibitisha mashtaka hayo pasipo shaka.

Jaji Sambo alisema ushahidi wa mashahidi 18, umethibitisha kuwa raia hao wa Kenya ndiyo walioshirikiana kwa pamoja, kumuua polisi huyo ambaye taifa bado lilikuwa likihitaji utumishi wake.

“Kulikuwa na hoja ya utetezi kuwa hawakutambuliwa kikamilifu lakini PC Naftali Ashery aliyekuwa lindo na marehemu aliwatambua vilivyo wauaji hao tena kwa ukaribu,” alisema. Alisema Mahakama imeridhika kuwa maungamo waliyoyatoa mbele ya walinzi wa amani ambao ni mahakimu waliyatoa kwa hiari bila kushurutishwa.

Mahakama imeukataa utetezi wa washtakiwa hao kuwa wakati wa mauaji hawakuwa nchini, akisema ushahidi wa vinasaba (DNA), umethibitisha walikuwapo nyumbani kwa mshtakiwa Kanje.

Jaji alisema kwa kuwa washtakiwa hao walikwenda kwa Kanje na yeye akawasaidia wasikamatwe na kuwatorosha, hilo ni kosa la kusaidia wahalifu baada ya kufanya mauaji.

Jaji Sambo alisema Kanje ndiye aliyeficha gari aina ya Toyota Land Cruiser mali ya Mahakama ya Kimataifa ya Rwanda (ICTR), lililotumika katika ujambazi huo na kwamba ushahidi wa wafanyakazi wawili wa mshtakiwa huyo, unathibitisha kuwa ndiye aliyetoa maelekezo kwa dereva wake ili akalitelekeze gari hilo eneo la Uwanja wa Ndege wa KIA.

Mahakama hiyo imeamuru kiasi cha fedha, Dola 8,145 za Marekani na Sh1,769,000 walizokutwa nazo raia hao wa Kenya, zikabidhiwe Benki ya NMB, Mwanga zilikoibwa.

Mazito Yaibuka Siku 14 George Tyson Bado Hajazikwa

0
0
KAMA huna taarifa, habarika sasa kwamba, mwili wa aliyekuwa mwongoza filamu za Kibongo, marehemu George Otieno Okumu ‘Tyson’ (41) aliyefariki dunia Mei 30, mwaka huu kwa ajali mbaya ya gari nchini Tanzania na kusafirishwa kwao,Kenya bado haujazikwa huku mazito yakiibuka kuhusiana na msiba huo!

Chanzo cha ndani kimeliambia Amani kwamba, mwili huo utazikwa keshokutwa Jumamosi kijijini kwao huko Kisumu baada ya kukaa mochwari kwa siku kumi na nne tangu kifo.

WAOMBOLEZAJI WAENDELEA NA SHUGHULI ZAO 
Katika hali ya kushangaza, utamaduni wa Kenya si kama wa Bongo, misiba hupewa kipaumbele siku za mwishoni mwa wiki, hasa Jumamosi.

“Kwa sasa mwili upo mochwari, unasubiri kuzikwa Juni 14 (mwaka huu). Kwa hiyo ukifika kwenye nyumba yenye msiba ambayo ipo Donholm, Phase 5 jijini Nairobi, unaweza kusema hakuna msiba.

Watu wanaendelea na shughuli zao za kila siku, kama kwenda sokoni na sehemu nyinginezo.
“Kifupi huwezi kujua kama kuna msiba. Huu ndiyo utaratibu wetu hapa Kenya, si kama huko Tanzania,” kilisema chanzo hicho.

Kikaendelea: “Ila Ijumaa ijayo, ndiyo kidogo kutaonesha kama kuna msiba kwani mwili utachukuliwa kwa ajili ya taratibu za kuaga kisha Jumamosi utapelekwa Kisumu, kwenye Kijiji cha Siaya ambako marehemu atazikwa.”

MONALISA, SONIA WALALA HOTELINI
Habari zaidi zinadai kuwa, baada ya kufika jijini Nairobi na mwili wa marehemu, mtalaka wa marehemu, Yvonne-Cheryl Ngatikwa ‘Monalisa’, mtoto wake, Sonia George Otieno na mama wa Monalisa, Suzan Lewis ‘Natasha’ walikuwa wakilala hotelini badala ya msibani.

WAREJEA BONGO KIMYAKIMYA BILA KUMZIKA TYSON
Ikazidi kuelezwa kwamba, licha ya kulala hotelini, wiki iliyopita, Mona, mama yake na Sonia walirejea Bongo kimyakimya ili kuendelea na shughuli nyingine za kila siku.

MKE MWINGINE AZUA BALAA
Wakati ya Monalisa yakiwa hivyo, aliyewahi kuwa mke wa marehemu, Beatrice naye amedaiwa kuzua balaa.

Habari zinadai kwamba, balaa la Beatrice lilianzia jijini Dar ambapo inasemekana baada tu ya kifo cha Tyson, yeye alikwenda nyumbani kwa marehemu na kuzuia kadi ya benki.
“Beatrice alikamata kadi ya benki  (ATM) na kusema ana 

haki nayo licha ya kwamba hadi anaaga dunia marehemu alikuwa akiishi na mwanamke mwingine aliyejulikana kwa jina moja la Lucy.

“Ikatokea kutoelewana kati ya Beatrice na Lucy, Beatrice akawa na kadi lakini hajui password, Lucy anajua. Mwishowe, Beatrice aliamua kumpa kadi ndugu wa Tyson aitwaye Felix Owino,” kilisema chanzo hicho.

NAYE ALALA KWA NDUGU NAIROBI
Habari kuhusu Beatrice zikaendelea kudai kwamba, naye kama Monalisa, alipofika jijini Nairobi na mwili wa marehemu alikuwa akilala kwa ndugu zake badala ya msibani.

“Sijajua nini kilitokea msibani kwani baada ya kufika Nairobi na mwili wa marehemu, Beatrice naye akawa analala kwa ndugu zake na si kwenye nyumba iliyofikia msiba,” kilisema chanzo.

MONALISA AZUNGUMZA NA AMANI
Baada ya kuzinyaka taarifa hizo, juzi Amani lilimsaka Mona kwa njia ya simu ili kujua anasema nini kuhusu mambo yaliyoelekezwa kwake.

KUHUSU KURUDI BONGO
“Ni kweli nimerudi na Sonia na mama. Ilibidi turudi kwa vile Sonia ana mitihani ya darasa la saba wiki ijayo,” alisema Monalisa.

Amani: “Lakini yule si baba yake? Kwa nini asimzike?”
Monalisa: “Nimeshakwambia labda kama una lingine.”

MADAI YA KULALA HOTELINI
Amani: “Kuna madai kwamba ulipokuwa msibani Kenya, wewe, mtoto na mama yako mlikuwa mkilala hotelini badala ya msibani, ni kweli?”
Monalisa: “Ni kweli.”

Amani: “Kwa nini sasa?”
Monalisa: “Nafasi ilikuwa ndogo, kwa hiyo tulikuwa tunakwenda kulala hotelini, asubuhi tunaenda msibani.”

Amani: “Mona turudi kwenye kitendo cha kurudi Bongo. Kama Sonia ana mitihani, kwa nini asirudi na mama yake wewe ukabaki kusubiri mazishi?”

Monalisa: “Misiba ya kule si kama huku Tanzania, kule siku za misiba ni Jumamosi tu, siku nyingine watu wanaendelea na mambo yao. Sasa na walivyochelewa kuzika sisi wengine huku (Tanzania) tuna kazi za watu (nadhani tenda za filamu) inabidi kurudi ili kuzifanya.”

BEATRICE, LUCY HAWAKO HEWANI
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, juhudi za kuwatafuta Beatrice na Lucy ziligonga mwamba baada ya simu zao kutokuwa hewani. Wote wapo jijini Nairobi, Kenya wakisubiri kuzika keshokutwa.

KUHUSU MAREHEMU TYSON
George Tyson alifariki dunia kufuatia ajali mbaya ya gari aina ya Toyota Noah, iliyotokea eneo la Gairo Morogoro. Marehemu na wenzake ambao walijeruhiwa na wanatibiwa mpaka sasa, walikuwa wakitokea Dodoma kwenda Dar.

Mungu ailaze mahali pema peponi. Amina.
GPL

Wenje: Uchumi wa Tanzania Unakua Kwenye Makaratasi na Mifuko ya Watawala

0
0
"Amesema ni muhimu mjadala huo wa kitaifa kwakua hali mbaya sana kiuchumi,misamaha ya kodi imekua mikubwa,wakubwahawalipi kodi wakati wauza vitumbua wanalipa kodi,uchumi unakua kwenye mifuko ya watawala.Hivyo tuwe na mjadala wa kitaifa wa uchumi tujadiliane na tupate muafaka wa uchumi wetu kwa pamoja"

Hivi huwa wabunge wanakatwa kodi kwenye mishahara yao? Wenje, tuanzie hapo kwanza.

Penny 'Mungu ni Mkubwa Ki Ukweli Nilikuwa na Hali Mbaya Kiafya'

0
0
MTANGAZAJI wa maarufu wa runinga Bongo, Peniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa ugonjwa uliompiga juzikati ulikuwa ‘serious’ kiasi cha kuona ni Mungu tu amemwokoa.

Akichezesha taya na paparazi wetu, Penny alisema anamshukuru Mungu anaendelea vizuri kwani alikuwa na hali mbaya baada ya kubanwa na ugonjwa wa Athma kwa siku tatu nzima akiwa anasaidiwa kupumua na mashine ya oxygen.

“Ukweli nilikuwa na hali mbaya huwa nasumbuliwa na Athma mara kwa mara lakini naweza kubanwa kwa siku moja ila ya safari hii imekuja kwa nguvu sana kwa sababu ilikuja na mafua makali jambo lililosababisha nilazwe kwa siku tatu katika Hospitali ya  AAR huku nikipumua kwa kutumia mashine, kweli Mungu ni mkubwa, ninaendelea vizuri,”

Shilole'Nuhu Mziwanda Ana Love ya Ukweli Kwangu Mpaka Najiuliza Alikuwa Wapi Siku Zote"

0
0
Siwezi kusema na mimi nitajichora tattoo ya jina lake ila na mimi siku nikiamua nitajichora tu kwa mapenzi, Kiukweli ana love ya kweli kabisa tofauti na wanaume ambao nilikuwa nao, watu walikuwa wanapenda tu wasikie wanatoka na Shishi kwa kutafuta Kick na nini Lakini Nuhu kama Nuhi ana Upendo wa Pekee Kabisa Yaani hadi inafika hatua nasema alikuwa wapi siku zote ..Wanasema Mungu Akitaka kukupa Kitu Hakuandikiii Barua

Video:Bonyeza Hapa Ujionee Jinsi Soko la Karume Lilivyoteketea Kwa Moto Usiku wa Kuamkia Leo

0
0
Bonyeza Hapo chini Kuona Video Jinsi Soko la Karume lilivyoungua kwa Moto Usiku ni Huzuni na Majonzi Tele kwa wafanya Biashara

Wema Sepetu Na Diamond Waanza Kushika Headlines NchinIi Nigeria, Tazama Hapa

0
0

Katika hali isiyo ya kawaida, sababu tulishazoea kuona Diamond na Wema Sepetu wakiwa wana-make headlines kwenye mitandao ya huku Tzee, hii ya sasa hivi mpya, sahz ni hadi huko nchini Nigeria wakizidi kuzungumzia muonekano wa couple hao, hasa walivyotokea ndani ya tuzo za Mtv zilizofanyika siku chache tu zilizopita.

“BONUS!Best Dressed Pair: Diamond Platnumz & Wema Sepetu
Wema looks glamorous in that black dress and Diamond looks fab in his beige suite.They look fab in each other’s arm”-By Jaguda.com
Kupitia mtandao wa habari huko nchini Nigeria wa Jaguda(www.jaguda.com),, Diamond Platnumz na mpenzi wake Wema Sepetu, wametokea kupamba kwenye headlines ya mtandao huo kwenye sehemu ya fashio, ikizungumzia jinsi wawili hao walivyopendeza, siku hiyo ya tuzo za Mtv, haikuwa wao tu, habari hii ilikuwa inazungumzia zaidi utafiti liofanya na wadao huko nchini Nigeria kutaka kujua nani alitokelezea zaidi na nani aliboronga kwenye upande wa fashion siku hiyo, huku matokeo yakielezea jinsi wawili hao wakiwa wanakimbiza kwa jinsi walivyokuwa wamependeza zaidi katika event hiyo, na kuandikwa kuwa ndio Best Dressed Pair.”

Huyu Ndiye KASA Aliyetabiri BRAZIL Kuifunga CROATIA kwenye mechi ya Ufunguzi Leo

0
0
BAADA ya pweza Paul aliyekuwa akiishi Ujerumani kujizolea umaarufu wakati wa Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini, fainali za mwaka huu nchini Brazil ameibuka mtabiri mwingine aitwaye Cabeção au Big Head.

Big Head ambaye ni kasa mwenye umri wa miaka 25, anayeishi katika kijiji cha Praia Do Forte nchini Brazil ameitabiria nchi yake ya Brazil kuibuka na ushindi katika mechi ya ufunguzi kwenye Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Croatia kesho.

Big Head ameanza kazi yake hiyo jana, Jumanne kwa kutabiri mechi ya ufunguzi kati ya Brazil na Croatia. Kasa huyo anafanya utabiri kwa kuchagua vyakula. Alichagua mmoja wa samaki waliokuwa wananing’inia katika bendera za Brazil, Croatia na kwenye mpira.

Mwanzo alikwenda kama anakula samaki aliyekuwa kwenye mpira ambapo angemaanisha sare, ila baadaye alielekea katika bendera ya nchi yake Brazil na kula samaki akimaanisha ushindi kwa wenyeji kwenye mechi ya kesho itakayochezwa saa 5 usiku.

Utabiri wa Big Head umeonekana kuwa wa kawaida na baadhi ya wapenzi wa soka maana kikosi cha Brazil kinaonekana kuwa kizuri zaidi kuliko Croatia, japo bado hakuna mwenye uhakika wa nani ataibuka kidedea kwenye mechi hiyo!

World Cup: Neymar na Oscar Wafanya Kweli, Crotia Huo Kwa Brazil

0
0
WACHEZAJI Neymar na Oscar wamepeleka vilio Croatia baada ya kuipa ushindi wa mabao matatu timu yao ya Brazil kwenye mechi ya ufunguzi wa Fainali za Kombe la Dunia 2014 zinazofanyika nchini Brazil.

Croatia walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 11 ambalo ni la kujifunga likiwekwa kimiani na beki Marcelo wa Brazil.

Baadaye wenyeji Brazil walikuja juu na kusawazisha bao hilo kupitia kwa mchezaji wao mahiri anayefananishwa na Pele, Neymar kwa shuti la mbali lililomuacha mlinda mlango wa Croatia, Stipe Pletikosa katika dakika ya 29 ya kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili Neymar aliipatia Brazil bao la pili kwa mkwaju wa penalti ambao kipa Pletikosa alijaribu kuupangua lakini ukajaa wavuni na kuwapa wenyeji ushindi wa 2-1 dakika ya 71. 

Mchezaji wa Chelsea, Oscar alihitimisha furaha ya waandaaji fainali hizo kwa bao lake la tatu dakika ya 90 ya mchezo.

Mpaka mwisho, Brazil 3, Croatia 1.

Leo michuano hiyo itaendelea ambapo Cameroon watavaana na Mexico, Uholanzi wakikwaana na Hispania huku Chile wakipepetana na Australi

Ukatili Mwingine Tena..Mfanyakazi wa Ndani Mwingine Ajeruhiwa Vibaya na Bosi Wake

0
0
HAUSIGELI aitwaye Melina Mathayo mwenye umri kati ya miaka 15, ameumizwa vibaya sehemu za kichwani na kulazwa katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam baada ya kupigwa na bosi wake aitwaye Yasintha Rwechungura mkazi wa Boko.

Akiongea na mwanahabari wetu akiwa katika hospitali hiyo, Melina amesema amekuwa akipigwa na bosi wake huyo mara kwa mara kwa kutumia waya, brenda na vifaa vingine japo alikuwa akiogopa kusema.

Vitendo hivi vya ukatili vinaonekana kushamiri kwa sasa ikiwa ni siku chache baada ya hausigeli aitwaye Yusta kuripotiwa kung'atwa na bosi wake aitwaye Amina Maige aliyepandishwa kizimbani leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni.

Binti huyo aliyeletwa Mwananyamala leo alfajiri akiwa na hali mbaya amefanya kazi kwa miaka miwili nyumbani kwa mama huyo mwenyeji wa mkoani Kagera.

Melina alikuwa akiongea na mwanahanbari wetu akiwa na mpira wa kuongezewa damu mwilini na amehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala amethibitisha kutokea tukio hilo.

Sikiliza wimbo mpya wa Diamond Platnumz – Mdogo Mdogo.

0
0
Miezi kadhaa iliripotiwa kuvuja kwa wimbo huu ambao uko kitofauti kidogo na aina ya muziki anaoufanya Diamond Platnumz,huu ni umeshakamilika na ameutoa kwa ajili yako unaitwa Mdogo Mdogo.
Bonyeza play kusikiliza.

Habari Njema Kwa Walio Ajiriwa, Kodi ya Mishahara Kupungua

0
0
SERIKALI imepunguza kiwango cha chini cha Kodi ya Mapato ya Mishahara (PAYE) hadi asilimia 12 kutoka asilimia 13.

Serikali pia imeahidi kuongeza kima cha chini cha mishahara, ambacho hata hivyo hakikutajwa.

Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum amelieleza Bunge mjini Dodoma kuwa, katika Bajeti ya Serikali ya Sh trilioni 19.8, Serikali inalenga kukusanya mapato ya kodi na yasiyo ya kodi ya Sh trilioni 12,18, kati ya hizo, mapato ya kodi ni Sh bilioni 11.31 na mapato yasiyo ya kodi, ni Sh bilioni 859.8.

Aidha, mapato yanayotokana na vyanzo vya halmashauri ni Sh bilioni 458.5.

Waziri Mkuya alisema Serikali inaendelea na jitihada za kupata misaada na mikopo ya masharti nafuu, ambapo inatarajia kupokea Sh trilioni 2.94. Kati ya fedha hizo misaada na mikopo ya kibajeti ni Sh bilioni 922.1, Mifuko ya Kisekta Sh bilioni 274.1 na miradi ya maendeleo Sh trilioni 1.75.

Waziri Mkuya alisema kwa nia ya kuendeleza miradi ya miundombinu nchini, Serikali itakopa katika soko la ndani Sh trilioni 3. Kati ya hizo, Sh bilioni 689.56 ni za kugharimia miradi ya maendeleo na Sh trilioni 2.3 ni kwa ajili ya kulipia hatifungani na dhamana za Serikali zinazoiva.

Pia itakopa Sh trilioni 1.3 kutoka masoko ya fedha ya nje kwa masharti ya kibiashara kwa ajili ya kugharimia miradi ya maendeleo.

Akizungumzia mgawanyo wa fedha, Mkuya alitaja Sekta ya Elimu kuwa ndiyo iliyotengewa fedha nyingi kuliko sekta yoyote katika sekta za kipaumbele zilizoteuliwa katika Mpango wa Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).

Sekta hiyo kwa mujibu wa Mkuya, imetengewa Sh trilioni 3.466, ambapo kati ya hizo Sh bilioni 307.3 zimetengwa kugharimia mikopo ya elimu ya juu.

Fedha zilizobakia zimepangwa kutumika kuimarisha ubora wa elimu ikijumuisha miundombinu ya elimu, ambapo Waziri Mkuya alisema lengo ni kusaidia upatikanaji wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia, kuimarisha na kujenga madarasa na maabara.

Pia Serikali katika sekta hiyo, imekusudia kuhakikisha vijana wanapata fursa za ajira, hivyo juhudi zimewekwa kuimarisha vyuo vya ufundi stadi vilivyo chini ya Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Stadi (VETA).

Sekta ya pili kwa kupewa mgawo mkubwa ni Miundombinu ya usafirishaji, ambapo Sh trilioni 2.1 zimetengwa na kati ya hizo, Sh bilioni 179.0 ni kwa ajili ya ununuzi wa mabehewa na ukarabati wa Reli ya Kati. Aidha Waziri Mkuya alisema Sh trilioni 1.4 ni kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa barabara na madaraja.

“Azma hii inalenga kupunguza msongamano wa magari mijini, gharama za usafiri na usafirishaji wa bidhaa na huduma, na hivyo kupunguza mfumuko wa bei.”

Sekta inayofuata kwa kutengewa kitita kikubwa cha fedha ni Afya, ambayo Waziri Mkuya alisema Sh trilioni 1.59, zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa dawa, kuzuia magonjwa ya mlipuko, chanjo za watoto, ujenzi wa zahanati na kudhibiti maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi na malaria.

Sekta ya Kilimo, imetengewa Sh trilioni 1,08, kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya Ukanda Maalumu wa Kilimo wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT).

Pia fedha hizo zimelenga kutumika kwa ajili ya ujenzi wa maghala na masoko; na upatikanaji wa mikopo kwa ajili ya kukuza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Waziri alisema Serikali itaendelea kuwekeza kwenye ugani kwa kuimarisha vyuo vya utafiti katika kilimo na kuhakikisha kunakuwa na maofisa ugani wa kutosha na mbegu bora.

“Hatua hii itaimarisha uzalishaji wa mazao, usalama wa chakula na kuhakikisha upatikanaji wa masoko ya uhakika,” alisema.

Kwa upande wa Nishati na Madini, Serikali imetenga Sh trilioni 1,09, kati ya hizo Sh bilioni 290.2 zimetengwa kwa ajili ya Wakala wa Umeme Vijijini (REA), ili kusambaza umeme vijijini.

Aidha, Sh bilioni 151 zimetengwa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam na Sh bilioni 90 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa mtambo wa kufua umeme kwa kutumia gesi wa Kinyerezi I.

“Hatua hii inalenga kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika na kupunguza gharama zake na hivyo kuvutia uwekezaji na kuongeza ajira,” alisema.



Sekta ya Maji imetengewa Sh bilioni 665.1 kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya maji mijini na vijijini ikiwa ni pamoja na kuendelea na ujenzi wa visima katika vijiji 10 kwa kila halmashauri na kukamilisha ujenzi wa bomba la maji kutoka Ruvu Chini hadi Dar es Salaam.

Katika Utawala Bora, Serikali imetenga Sh bilioni 579.4 kwa ajili ya kuimarisha utawala bora, ikiwa ni pamoja na kugharimia Bunge Maalumu la Katiba; vitambulisho vya Taifa; Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2014; kuhuisha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura; maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015; mapambano dhidi ya rushwa na utoaji wa haki kwa wakati.

Katika jitihada za kuongeza mapato zaidi, Waziri wa Fedha ameondolewa mamlaka ya kusamehe kodi katika maeneo muhimu, ambapo Waziri Mkuya aliwaomba wabunge waiunge mkono Serikali, katika hilo ili kurahisisha usimamizi wa kodi nchini na hivyo kutoa unafuu kwa walipa kodi, na kuongeza mapato ya Serikali.

“Serikali itachukua hatua kuu mbili muhimu. Kwanza, kutoa taarifa ya misamaha ya kodi kila robo mwaka kwa kuwatangaza walionufaika na misamaha kwenye Tovuti ya Wizara ya Fedha.

“Hatua hii itasaidia kuleta uwazi na uwajibikaji katika suala la misamaha ya kodi na kuwafanya wananchi wajue ni nani anayenufaika na misamaha hiyo,” alisema.

Pili, alisema Serikali itatoa taarifa ya kina ya misamaha yote ya kodi iliyotolewa na kuiwasilisha bungeni kila mwaka, ili wabunge mpate nafasi ya kujadili na kutoa maoni yenu.

Huyu Ndio Amina Maige Aliye Mng'ata ng'ata Mfanyakazi wake wa Ndani Hapa Akipandishwa Mahakani, Wananchi Wamzomea

0
0
Pichani ndio Mwanamke anayejulikana kwa jina la Amina Maige Aliyeingia Katika Headlines week iliyopita baada ya kukutwa na Tuhuma za Kumjeruhi mfanyakazi wake wa Ndani kwa Kumg'ata ng'ata na Meno mwili mzima , Hali ilikuwa Tete wakati akiwa anapandishwa mahakamani wananchi na wanaharakati mbali mbali walikuwa mahakamani hapo wakitaka aonyeshwe sura yake baada ya kushushwa kwenye gari huku amejifunika Kichwa...

Angalia Video hapa Chini Ujionee:

Unyama Mkubwa: Mtoto Afungwa Minyororo Miezi Minne Kwa Mganga wa Kienyeji Kisa Deni la Matibabu

0
0
MATUKIO ya ukatili dhidi ya watoto, bado yameendelea kushika kasi kwenye maeneo mbalimbali nchini ambapo katika Mkoa wa Simiyu, mtoto mwenye umri wa miaka 17 (jina tunalihifadhi), mkazi wa Bariadi Mjini na mwanafunzi wa Shule ya Msingi Bariadi, amejikuta akifungwa minyororo mikononi na miguuni kwa miezi minne nyumbani kwa mganga wa kienyeji.

Mganga huyo amefahamika kwa jina la Mdeli Msanja ambaye aliamua kufanya ukatili huo baada ya wazazi wa mtoto huyo ambaye anamatatizo ya akili, kushindwa kumlipa pesa za matibabu.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Charles Mkumbo, alisema wazazi wa mtoto huyo walikubaliana na mganga huyo kumlipa sh. 260,000 kama mtoto wao atapatiwa matibabu na kupona.
“Pamoja na wazazi kukubaliana na mganga husika, hali ya mtoto haikuweza kubadilika wala kupata unafuu hivyo waliomba kumchukua mtoto wao kitendo ambacho kilipingwa na mganga kwa madai ya kutolipwa pesa zake ambazo walikubaliana,” alisema.

Alisema mganga huyo aliamua kumchukua mtoto huyo na kumfungia chumbani kwake kwa minyororo miguuni na mikononi kwa kipindi cha miezi minne akidai pesa zake na kuwapa wakati mgumu wazazi wake.

Kutokana na msimamo wa mganga huyo, mama mzazi wa mtoto huyo Malita James (46), alilazimika kwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi Bariadi kuhusu mateso anayoyapata mwanaye kwa mganga.

“Polisi walishirikiana na Dawati la Jinsia kufanya uchunguzi wa tukio hili na walipofika kwa mganga, walimkuta akiwa amemfunga minyororo miguuni na mikononi,” alisema Kamanda Mkumbo.

Aliongeza kuwa, polisi walimkamata mganga huyo ambaye hakuwa na kibali cha kutoa tiba za asili, pia alikamatwa na nyara za Serikali ambazo ni pembe moja ya swala na mikia miwili ya nyumbu ambapo uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.

Viewing all 104428 articles
Browse latest View live




Latest Images