Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Watoto Watatu Majeruhi wa Lucky Vincent Arusha Waungana na Wenzao na Kuanza Masomo

$
0
0
Watoto Watatu Majeruhi wa  Lucky Vincent Arusha Waungana na Wenzao na Kuanza Masomo
Wanafunzi watatu; Doreen Mshana, Wilson Tarimo na Sadia Awadh walionusurika katika ajali iliyoua wenzao 32, walimu wawili na dereva mmoja wamerejea darasani jana.

Mkuu wa Shule ya Lucky Vincent Efraim Jackson alisema jana kuwa wanafunzi hao waliokuwa wakitibiwa nchini Marekani, wameonyesha ari ya masomo na wamewaandalia programu maalumu itakayowawezesha kusoma kwa haraka na kuelewa sehemu kubwa ya mtalaa ambao hawakuusoma wakati wakiwa kwenye matibabu.

“Hivi ninavyoongea na wewe wapo kwenye jaribio la kuwapima. Wapo darasani na wenzao lakini tutakuwa tunawatenga na kuwafundisha kwa saa nne hivi kwa siku ili waweze kufidia sehemu waliyoikosa awali,” alisema.

Lazaro, Lema wampinga RC

Wakati watoto hao wakirejea shule kuendelea na masomo, viongozi wa kisiasa wameendelea kuzozana kuhusu rambirambi za ajali hiyo.

Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo kuzikabidhi familia tatu za watoto hao Sh23.2 milioni ambazo awali zilikuwa za rambirambi, Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wamepinga hatua hiyo.

Juzi, Gambo alikabidhi fedha hizo na kusema Serikali na wadau walichangia kwa ajili ya shughuli nzima za mazishi ya marehemu 35 waliofariki kwenye ajali hiyo na hivyo kukabidhi kiasi kilichobaki kwa familia hizo ili ziwasaidie.

Katika mapokezi ya watoto hao kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Agosti 18, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghirwa kwa niaba ya Makamu wa Rais, Samia Suluhu aliagiza Serikali mkoani Arusha kutoa Sh20 milioni ambazo ni sehemu ya michango hiyo kwa ajili ya mfuko wa elimu wa Stemm kusomesha watoto hao.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika juzi katika eneo la Sanawari, Meya Lazaro alisema badala ya Gambo kutekeleza maagizo ya Makamu wa Rais, amekabidhi fedha zilizobaki kwa familia jambo ambalo ni kinyume.

Alisema yeye (Lazaro) alikamatwa na kuwekwa mahabusu baada ya kumtaka Gambo arejeshe rambirambi na kusisitiza kwamba kinyume chake kiongozi huyo amerejesha fedha hizo sehemu ambayo si sahihi.

“Niliwekwa ndani wakati wa rambirambi, Makamu wa Rais ameagiza Gambo arejeshe fedha za rambirambi alizokusanya badala ya alivyoelekezwa yeye amewaita watoto ofisini kwake,” alisema Lazaro.

Wakati Lazaro akisema hayo, Lema alisema alichofanya Gambo ni funzo kwa viongozi wengine kuacha kupokea maagizo ya mdomo kutoka kwa viongozi wa Serikali.

“Viongozi wamekuwa wakitoa maagizo, kamateni wapinzani na kuwapiga, sasa kumbe kama hamjapewa maandishi ipo siku yatawarudia,” alisema.

Alisema kilichofanywa na Gambo ni kupingana na maagizo ya Makamu wa Rais aliyesema fedha ziwekwe mfuko wa elimu, yeye Gambo amezigawa.

Hata hivyo, Lema alisema hayo yanatokea kutokana na msiba huo tangu ulipotokea ulitawaliwa na mgawanyiko na hila za kisiasa na sasa Mungu anafanya miujiza viongozi kugongana.  


Mkemia Mkuu Abanwa Utoaji Holela wa Vibali vya Kuingiza Kemikali Bashirifu

$
0
0
Mkemia Mkuu Abanwa Utoaji Holela wa Vibali vya Kuingiza Kemikali Bashirifu
Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samuel Manyele amehojiwa na Mamlaka ya Kuthibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa siku mbili mfululizo kuanzia juzi kuhusu utoaji kiholela wa vibali vya kuingizia nchini kemikali bashirifu.

Uingizaji na usambazaji wa kemikali bashirifu hufanyika chini ya udhibiti wa hali ya juu wa mamlaka za kitaifa na kimataifa kuzuia uwezekano wa kuchepushiwa katika utengenezaji wa dawa za kulevya aina ya heroin na cocaine.

Taarifa zinasema Profesa Manyele, ambaye juzi alihojiwa kwa siku nzima, alichukuliwa tena jana mchana kwa mahojiano zaidi yaliyofanyika makao makuu ya DCEA, Upanga jijini Dar es Salaam.

Hadi tunakwenda mitamboni Profesa Manyele alikuwa bado mikononi mwa DCEA, kwa mujibu wa taarifa ambazo Mwananchi ilizipata, na kuna taarifa zaidi kuwa huenda akaendelea kushikiliwa hadi leo.

Kuhojiwa kwake kwa siku mbili kumetokea sambamba na uamuzi wa Rais Magufuli kumuondoa Mihayo Msikhela kutoka katika nafasi yake ya kamishna wa oparesheni wa DCEA, na kumteua Luteni Kanali Frederick Milanzi kushika wadhifa huo.

Juzi, Rais John Magufuli alifanya mazungumzo Ikulu jijini Dar es Salaam na Kamishna Mkuu wa DCEA, Rodgers Siyanga aliyemhakikishia kuwa mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini yanapata mafanikio makubwa.

Taarifa iliyotolewa juzi na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa, inasema Siyanga alimueleza Rais mikakati inayotumika kupambana na tatizo la dawa za kulevya. Haikueleza kwa kina masuala mengine ambayo Rais Magufuli alizungumza na Siyanga.

Ingawa mamlaka haziko tayari kuthibitisha, kuhojiwa kwa Profesa Manyele kunahusishwa kwa kiasi kikubwa na wimbi la kukamtwa kwa kemikali bashirifu ambazo uagizaji, uhifadhi na usambazaji wake husimamiwa na ofisi yake.

Katika miezi ya karibuni, DCEA ilikamata mamia ya tani za kemikali bashirifu katika Bandari ya Dar es Salaam, bandari kavu na kwenye maghala ya watu binafsi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka DCEA, waagizaji wengi walikiuka utaratibu na kushindwa kueleza wanakosambaza kemikali hizobaada ya kuingizwa nchini.

Tukio la kwanza la kukamatwa kwa kemikali hizo lilitokea Mei baada ya maofisa wa DCEA kukamata lita zaidi ya 5,000 za aina mbalimbali za kemikali bashirifu, mali ya mfanyabiashara wa jijini Dar es Salaam, Benedict Assey.

Baada ya kukamatwa kwa shehena hiyo iliyokuwa katika maghala yaliyopo Mwenge (Dar es Salaam), Bagamoyo (Pwani) na Kilimanjaro (Moshi), iligundulika kuwa kibali cha kughushi kilitumika kuagiza mzigo huo, huku kibali cha usajili cha kampuni iliyoagiza mzigo huo ya Techno Net Solution kikionekana kimekwisha muda wake.

Maghala hayo yalionekana kutokidhi viwango vilivyowekwa kisheria, kama umbali kutoka makazi ya watu.

Mathalani, licha ya ghala la Mwenge kuwa katikati ya makazi ya watu, ofisi ya Mkemia Mkuu haikuchukua hatua pamoja na ukweli kuwa ilikuwa ikifanya ukaguzi mara kwa mara.

Mwezi uliofuata mamlaka hiyo ilikamata tena makontena mawili yaliyokuwa na lita zaidi ya 6,000 za kemikali hizo hatari ndani ya bandari kavu iliyopo Tabata Relini, Dar es Salaam. Shehena hiyo iliyoagizwa kutoka Ufaransa na India, ni mali ya Assey.

DCEA inadai kuwa ilimtaka mmiliki huyo atoe nyaraka na orodha ya watu au taasisi zilizouziwa kemikali hizo, lakini alishindwa kufanya hivyo.

Na mwezi uliopita tu, DCEA ilikamata makontena mengine 10 yenye zaidi ya lita 200, 000 za aina tofauti za kemikali bashirifu katika Bandari ya Dar es Salaam zilizoagizwa kinyume cha sheria kutoka Swaziland.

DCEA ilisema imebaini kampuni inayotuhumiwa kwa uingizwaji huo, ilianza kazi hiyo tangu mwaka 2016 na tayari ilishaingiza lita milioni 1.5 za kemikali hizo na kupelekwa kwa kampuni moja iliyoko Mbezi Luis.

Mamlaka ilisema pia kuwa baada ya uchunguzi zaidi, iligundua kuwa kampuni hiyo inajihusisha na kuuza magari na si kutunza wala kuchakata kemikali, jambo lililowastua na kufanya uchunguzi wa kina.

Kamishna wa ukaguzi na sayansi jinai wa DCEA, Bertha Mamuya aliwahi kuiambia Mwananchi kuwa kwa kawaida kemikali hizo hutumika kutengenezea dawa za binadamu, za wadudu na mbolea lakini magenge ya wahalifu huzitumia kutengeneza heroin na cocaine katika maabara za ufichoni.

Kwa mujibu wa Sheria ya Kemikali za Viwanda na Walaji (Usimamizi na Udhibiti) ya mwaka 2003, Ofisi ya Mkemia Mkuu ndiyo yenye mamlaka ya kutoa vibali vyote vya uingizaji wa kemikali bashirifu, kufanya ukaguzi katika maghala kuona kama yanakidhi viwango na kufuatilia matumizi yake.

Kuna tuhuma kuwa ukwasi wa baadhi ya watumishi wa ofisi hiyo unatokana na kutoa vibali vya uingizaji wa kemikali kinyume cha sheria.

“Imefika wakati watu wanaagiza kiasi kikubwa cha kemikali bashirifu na shehena inapowasili bandarini ndipo wanaanza ku-process (kutafuta) vibali kwa Mkemia Mkuu,” alisema mtaalamu mmoja wa kemikali DCEA aliyeomba kutotajwa jina.

Mapema mwaka jana, Ofisi ya Mkemia Mkuu iliingia katika kashfa kubwa baada ya kontena za kemikali bashirifu aina ya aceti anhydride zenye thamani ya Sh28 bilioni kukamatwa nchini Pakistani likitokea Tanzania.

Inadaiwa kuwa kontena hilo lilitokea China huku wamiliki wake wakipewa vibali vya kuingiza kemikali hizo baada ya kuzieleza mamlaka kuwa zingezitumika katika kiwanda cha korosho. Hata hivyo, habari zinadai kuwa kontena hilo lilihifadhiwa Kurasini jijini Dar es Salaam kabla ya kupata vibali kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu na kupelekwa Pakistan ambako lilikamatwa.

Maofisa wawili wa ofisi ya mkemia mkuu waliwahi kukamatwa na kuhojiwa kuhusiana na utoaji vibali kwa shehena hiyo, lakini kesi dhidi yao ilishindwa kuendelea katika mazingira yasiyoeleweka.

Machi mwaka huu, maofisa wengine wawili wa ofisi hiyo hiyo walikamatwa na DCEA na kuhojiwa kwa saa kadhaa kwa madai ya kusaidia usafirishwaji wa kontena hilo kwenda Pakistan.

Kutokana na wimbi la ukamataji wa kemikali hizo hatari, Profesa Manyele alijitokeza kwenye vyombo vya habari hivi karibuni akionya kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wafanyabiashara wanaokiuka utaratibu wa uingizaji, usafirishaji na uhifadhi wa kemikali bashirifu.

Alikuwa akifafanua kukamatwa kwa tani zaidi ya 6,000 za kampuni ya Tecno Net Scientific.

Profesa Manyele alifanya tena mkutano na waandishi wa habari hivi karibuni na kukiri kwamba ofisi yake imelemewa na kiwango kikubwa cha kemikali za matumizi ya nyumbani na viwandani zinazoingizwa nchini kila siku.

Alisema ongezeko hilo linatokana na watu wengi kuagiza mzigo wa kemikali bila kufuata sheria.

Alisema kabla ya kutoa onyo hilo, waingizaji walikuwa wakifanya hivyo kinyume cha sheria na walikuwa wakiagiza kwanza mizigo na inapowasili au kukaribia kuwasili, ndipo wanaanza kuomba kibali au usajili kwa mara ya kwanza.    


Moni Amtolea Makavu R.O.M.A Kutokana na Wimbo wa Zimbabwe

$
0
0
Moni Amtolea Makavu R.O.M.A Kutokana na Wimbo wa Zimbabwe
Baada ya Rapa Roma Mkatoliki kuachia ngoma ya Zimbawe inayozungumzia matukio ya kutekwa, msanii Moni Centrozone amefunguka na kumlalamikia Roma kuzunguzia tukio hilo pasipo kumuhusiasha mtu yoyote kwenye wimbo na kudai amejichukulia kama kinara mkuu.

Akizungumza na eNewz ya EATV Moni amedai kuwa anamshangaa msanii huyo kujizungumzia yeye binafsi kwenye ngoma ya Zimbabwe wakati tukio hilo liliwakuta wote na pia walikubaliana kutozungumza jambo lolote lile kuhusiana na yale yaliyowatokea lakini Roma yeye akaamua kufanya ndivyo sivyo.

"Kajiongelea yeye mwenyewe katika wimbo, kazungumzia nafsi ya kwanza umoja. Alisema atakaa kimya hataki kuzungumzia tukio la utekwaji lakini kaja katoa 'ngoma' ambayo inazungumzia mambo kibao kuhusu kilichotutokea. Itakuwa haina maana yeye kuni-mind mimi nikitaka kuzungumzia yaliyotukuta kipindi kile", alisema Moni.

Pamoja na hayo, Moni aliendelea kwa kusema "Nikipata 'vibe' naweza kuamua na mimi nikatoa dude lolote ambalo litanizungumzia mimi peke yangu na maisha yangu jinsi nilivyotekwa, kwa sababu kuna matukio ambayo na mimi nayakumbuka kipindi napatiwa mateso kwa sababu ngoma iliyotoka haikuniwakilisha mimi. Roma kajizungumzia mwenyewe kama ndiyo muhusika mkuu, huwezi kujua na mimi naweza kuwa nimeshaandaa mipango yangu ya kuzungumza kwani njia zipo nyingi".

Hata hivyo Moni amesema haijalishi ni muda gani atachukua na yeye kusema chochote kuhusiana na kilichowahi kumtokea wakati akiwa ametekwa baada ya Roma kuachia ngoma ya Zimbabwe.
"Haijalishi kama nitaandaa 'press' kuelezea umma kilichotukuta au nitaanda wimbo wangu kuzungumzia na mimi kilichonikuta, kwa sababu haya ni maisha yangu na mimi sijazaliwa na mtu nimezaliwa peke yangu", alisisitiza Moni.

Fid Q Azikana Team Kiba na Diamondi Achukizwa na Ommy Dimpozi

$
0
0
Fid Q Azikana Team Kiba na Diamondi Achukizwa na Ommy Dimpozi
Baada ya maneno kuwa mengi kuhusu ngoma yake ya Fresh Remix, Fid Q amefunguka na kusema hakujua kama mistari ya Diamond ilikuwa na lengo la kumdiss Alikiba kwa sababu yeye ni mtu wa hip hop na hajui chochote kuhusu Bongo Flava.

Rapper huyo ameeleza kuwa alikuja kujua hilo wakati wimbo umeshatoka hata hivyo hakuona kama kuna kibaya kilichofanyika kama inavyodai ila hajapendezwa na kitendo cha Ommy Dimpoz kuchukulia suala hilo binafsi zaidi na kuondoa maana ya burudani.

“Ok nyimbo imeshatoka na ndio imekuwaa hivyo nikaangali kama upande ule mwingine watasikia hii kitu na you know it entertainment industry, wataipokea kama biashara yenyewe ilivyo, huenda nao wakasema Fid na sisi tunataka hii beat because am cool both of side, mimi siyo tema Diamond, siyo team kiba nawapenda wote ningewagea beat,” amesema.

“Lakini niwe muwazi hiyo hope ilifutwa nilipokutana na post ya Ommy Dimpoz, kwamba ameweza kubadilisha ile burudani yote na kuipeleka katika kitu binafsi kabisa, imeniondolea lile vibe,” Fid Q ameiambia Clouds Tv.

Hata hivyo Fid Q ameongeza kuwa alichofanya Diamond siyo disrespect kwa Alikiba bali ni battle skills na siyo taarabu kwa watu wengi walivyokuwa wakidai katika mitandao.

“Hip hop majibizano yapo unakuwa unamgusia vitu vyako kwa kupitia muziki na msanii unashauriwa unapokuwa na ishu na mtu njia sahihi ya kuwasilisha ni kupitia muziki huo huo. Sitaki kusema Kiba alikosea kwa kujibu kwa tweet labda hakujisikia kuingia studio kufanya, yale ni maamuzi yake na menejiment yake hatuna budi kuyaheshimu,” amesema Fid.

Alipoulizwa mtazamo wake ni upi kuhusu beef ya Diamond na Alikiba, Fid alisema  kila mmoja ana team yake ya mtandaoni ambayo ipo imara ila kilichomkuta ni kuoga matusi kutoka kwa team Kiba.

“Kuna mtu aliniambia Fid umefanya ngoma na Diamond tengemea matusi kutoka kwa team Kiba ya online, nimeoga matusi sana ambayo sijawahi kuyaoga. Watu wamenidhalilisha sana, nasikitika kwamba nimevisoma lakini kujibu mtu siwezi kwa sababu wengi wamenihukumu katika vitu ambavyo si vyangu mwenyewe kwa hiyo nimeamua kuwaacha muda utazidi kuwaponya zaidi ,” amesisitiza.

Fresh Remix ni ngoma ya Fid Q ambayo amemshirikisha Diamond na Rayvanny, kutokana mistari ya Diamond kuonekana inamlenga Alikiba, naye alijibu kupitia mtandao wa twitter. Siku iliyofuata Diamond aliachia audio clip katika mtandao wa Instagram ambayo inaaminika ilimlenga Ommy Dimpoz na Alikiba, ndipo Dimpoz alipochua uamuzi wa kuandika maneno makali kwa Diamond na familia yake katika mtandao wa Instagram.

Masogange: Siwezi Kuuza Mwili Wangu Nipate Pesa Sina Dhiki Hizo

$
0
0
Masogange: Siwezi Kuuza Mwili Wangu Nipate Pesa Sina Dhiki Hizo
Video Qeen mkongwe, Agnes Masogange ametamka kwamba sasa ameamua kuachana rasmi na kuuza sura kwenye video kwa vile baby wake hapendi huku pia akitaka watu kuacha kufikiria kwamba anafanya biashara kujiuza.

“Watu bana!, mimi sina dhiki ya kufikia kuuza mwili wangu eti nipate pesa na kuhusu zile picha kipindi kile nilizopiga hazikuwa za utupu sema basi tu watanzania tunapenda kuzusha sana. Na mtu kuenda Sauzi ndio ameenda kujiuza?,” Masogange aliliambia Gazeti la Mwanaspoti.

Aliongeza, “Mimi nilikuwa na biashara zangu nafanya na wanaosema hivyo hawanisaidii chochote,hakuna mtanzania anayeninunulia nguo,hayupo anayenipa pesa waongee tu. Unajua sisi wadada tuna tabia ya kuoneana wivu akiona unafanya vizuri anaanza kukusemea vitu vya ajabu pembeni,”anasema msanii huyo na kuongeza kwamba amepima ukimwi yuko safi,”

Katika hatua nyingine mrembo huyo alikana kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya kama baadhi ya watu wanavyodhani.

Wema Sepetu Kuzindua Filamu Yake Leo Iliyogharimu Milioni 40

$
0
0
Wema Sepetu Kuzindua Filamu Yake Leo Iliyogharimu Milioni 40
STAA ‘grade one’ kunako filamu Bongo, Wema Sepetu amewajibu watu wanaoendelea kumsema kuwa hajui kuigiza kwamba, wajaribu kutupia jicho la tatu kwenye filamu yake mpya ya Heaven Sent ambayo inatoka leo (Ijumaa) ikiwa imetengenezwa kwa gharama ya shilingi milioni 40.

 Wema alisema kuwa ameamua kutumia kiasi kikubwa cha pesa ili filamu ionekane nzuri na yenye hadhi kwa sababu filamu nyingi Bongo zinakuwa mbaya kutokana na bajeti kuwa finyu.

“Naamini kila mmoja anaweza kujua uwezo wangu mkubwa niliopewa na Mungu kwa kuiangalia filamu yangu ya Heaven Sent, ndani ya filamu hiyo utanijua vizuri ni msanii au naleta longolongo na humo nimejitupa utafikiri sio Wema mimi,” alisema

Harmorapa: Kwa Sasa Sina Mawasiliano Mazuri na P Funk,

$
0
0
Harmorapa: Kwa Sasa Sina Mawasiliano Mazuri na P Funk,
Msanii wa hip hop bongo Harmorapa, amefunguka juu ya kitendo cha kumchana mtayarishaji wa muziki ambaye iliaminika anamkubali zaidi, na kukiri kuwa kwa sasa hayuko vizuri na P Funk.

Akizingumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Harmorapa amesema kwa sasa hawana mawasiliano mazuri na P Funk, kwani kuna mambo ambayo yalitokea, yaliyosababisha kutoelewana kwao,

"Nikimzungumzia Majani, kwenye maisha mtu unapitia sehemu nyingi, mfano mimi nafanya kazi kwa mtu halafu maslahi siyaoni, nafanya kazi kwa jasho najituma halafu yeye ndiyo ananufaika, halafu anakuona wewe humfai, na mwisho wa siku ndiyo inakuwa hivyo”, alisema Harmorapa.
Harmorapa kwa sasa ameachia wimbo wake ambao umeonekana kumchana P Funk Majani  ambaye alimsimamia kwenye kazi yake ya Nundu, na kumuunganisha na baadhi ya watu ili aweze kufanikisha kazi zake za muziki.

Mkuu wa Samsung Afungwa Jela Miaka Mitano

$
0
0
Mkuu wa Samsung Afungwa Jela Miaka Mitano
Mahakama nchini Korea Kusini imemhukumu bilionea anayetarajiwa kurithi kampuni Samsung Lee Jae-yong kifungo cha miaka mitano jela kwa makosa ya utoaji rushwa.
Bw Lee alikuwa ameshtakiwa kuhusika katika rushwa katika kashfa ambayo pia ilichangia kuondolewa madarakani kwa rais wa zamani wa Korea Kusini.

Kesi hiyo ilikuwa imevutia sana umma huku hasira zikiendelea kupanda dhidi ya kampuni kubwa za kibiashara za Korea Kaskazini, maarufu kama chaebols.
Bw Lee, ambaye amekanusha mashtaka yote, alikuwa amekabiliwa na uwezekano wa kufungwa jela hadi miaka 12.

Bw Lee, ambaye pia hufahamika kama Jay Y Lee na amekuwa ndiye kiongozi wa kampuni hiyo kubwa zaidi ya kuunda simu duniani, amekuwa kizuizini tangu Februari akikabiliwa na tuhuma kadha za rushwa.
Miongoni mwa makosa aliyokabiliwa nayo ni utoaji rushwa, wizi wa mali ya umma na kuficha mali nje ya nchi.

Lee, 49, pia alituhumiwa kutoa mchango wa hisani wa won 41bn ($36m; £29m) kwa nyakfu za hisani zilizosimamiwa na rafiki wa karibu wa rais aliyeondolewa madarakani Park Geun-hye, ndipo apendelewe kisiasa.

Waendesha mashtaka wanasema mchango huo ulitolewa kwa mwandani mkuu wa Bi Park ili serikali iunge mkono mageuzi katika mfumo wa usimamizi wa kampuni ya Samsung ambao ungempatia Lee nguvu zaidi katika udhibiti wa kampuni ya Samsung Electronics.

Wakili wa Lee amesema tayari kwamba watakata rufaa uamuzi huo.
"Tuna imani kwamba hukumu hii itabatilishwa," wakili Song Wu-cheol ameambia wanahabari baada ya kusomwa kwa hukumu, kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters.
Hata hivyo, uamuzi huo wa mahakama ni pigo kubwa kwa kampuni hiyo kubwa zaidi na inayofahamika zaidi ya Korea Kusini.

Hukumu hiyo imetilia shaka sasa uongozi wa Lee katika kampuni hiyo.
Amekuwa kaimu mwenyekiti tangu babake Lee Kun-hee alipopatwa na mshtuko wa moyo mwaka 2014.

Kashfa hiyo ya Samsung ilichangia kuondolewa madarakani kwa Bi Park.
Mwandani wake Choi Soon-sil tayari amefungwa jela miaka mitatu kwa makosa ya rushwa.

Masikini Hamisa Mobeto na Mwanae watishiwa Kuuwawa Soma Hapa Alivyofunguka

$
0
0
Masikini Hamisa Mobeto na Mwanae watishiwa Kuuwawa Soma Hapa Alivyofunguka
Sakata la modo ‘grade one’ Bongo, Hamisa Hassan ‘Mobeto’ kudaiwa kuzaa kwa siri na msanii wa Bongo Fleva, limechukua sura mpya baada ya mrembo huyo kufichua kuwa anatishiwa kuuawa wakati wowote yeye na mwanaye wa kiume aliyemzaa Agosti 8, mwaka huu na kumpa jina la Abdul Naseeb a.k.a Prince Dully D’.

TUJIUNGE MBEZI-BEACH
Kwa mujibu wa chanzo makini ndani ya familia ya Hamisa yenye maskani yake Mbezi- Beach jijini Dar anakoishi mrembo huyo, baada ya kujifungua, kumekuwa na sarakasi nyingi zinazoendelea juu ya mwanaye huyo.

TIRIRIKA NA CHANZO
“Unajua baada tu ya kujifungua kulienea habari nyingi kuwa mtoto huyo ni wa msanii huyo hasa baada ya Hamisa kumpa mwanaye jina hilo.

“Kilichofuata, kwanza msanii huyo alikimbilia kwenye media (vyombo cha habari) kukanusha habari hizo ambazo zimekuwa zikizagaa kwa kasi ya moto wa kifuu.
“Unajua jamaa (msanii huyo) alidhani kuna siri chini ya jua kuwa anaweza kuficha jambo hilo maana watu walikuwa wakimchomea kwa mpenzi wake ambaye amezaa naye.

HAMISA SIYO WA MCHEZOMCHEZO
“Ili kumziba mdomo Hamisa, msanii huyo aliona ni bora amkane mapema lakini Hamisa siyo wa mchezomchezo maana aligoma kuficha ishu hiyo.
“Baada ya kuona anaweza akabumburua ishu, msanii huyo alimpiga biti asizungumze na vyombo vya habari kabla ya kumwekea ulinzi wa chinichini kuhakikisha waandishi hawamfikii Hamisa.
“Sehemu pekee ambayo Hamisa aliona jamaa huyo hawezi kumzuia ni kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii hasa Instagram na Snapchat ‘so’ akawa anaposti vipande vya baadhi ya viungo vya mtoto huyo.
“Sasa baada ya kuona hivyo, msanii huyo ambaye alikwenda mara moja tu kumuona mtoto huyo alianza kumpigia simu na kumtumia meseji za vitisho.

HAMISA AISHI KWA HOFU
“Wewe fikiria Hamisa na kichanga chake sasa anaishi kwa hofu maana jamaa amemuambia kama atafunguka kuwa amezaa naye atamuondoa uhai yeye na mtoto wake.
“ Hali hiyo imeifanya family ya Mobeto iwe na hofu kubwa na ili kujiweka salama, aliona ni bora aende polisi kuripoti ili kama kutakuwa na jambo lolote baya litakalomkuta yeye na mwanaye, basi mhusika atakuwa ni msanii huyo.
“Mwanzoni tulidhani ni ishu ndogo lakini kwa vitisho anavyopokea Hamisa, vinamnyima raha na kumfanya alie tu.
HAMISA ATIA HURUMA

“Kiukweli Hamisa anatia huruma sana na anahitaji msaada kwa sababu mbali na msanii huyo pia anapata vitisho kutoka kwa mpenzi wa jamaa huyo.
“Sasa watu wanajiuliza, wakati anatembea naye hakujua kuwa kinaweza kupatikana kiumbe? Na kwa ustaa wake anashindwa nini kulihendo suala hilo kwa busara ili lisimchafulie kuliko kutoa vitisho hivyo?” kilifunguka chanzo chetu hicho na kuongeza:
“Hata kwenye ukurasa wake wa Snapchat, Hamisa ameshatahadharisha juu ya kutishiwa kuuawa yeye na mwanaye.”
Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, Ijumaa liliperuzi kwenye ukurasa wake huo na kukutana na ujumbe wa Hamisa uliosomeka:
“Mlidhani atafia tumboni enh…au mlijua nitafia leba…. nyie siyo Mungu na hamtakaa kuwa kamwe…& if anything bad and I mean anything bad happens to me or my son hatutawaacha salama!!!”

HUYU HAPA HAMISA
Kufuatia hali kuwa tete huku Hamisa akidaiwa kuwa kwenye msongo, Ijumaa lilimtafuta staa huyo ambapo kwa mara ya kwanza katika mahojiano maalum alikiri kupokea vitisho kutoka kwa msanii huyo na kwamba ameamua kutokaa kimya na badala yake kwenda kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama ikiwemo kwa Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Makosa ya Jinai (DCI).
‘MIMI NA MWANANGU TUNAUAWA WAKATI WOWOTE’
“Ni kweli mimi na mwanangu tunauawa muda wowote. Nina ushahidi wa kutosha wa vitisho so nimeona ni vyema nitoe taarifa kwenye vyombo vya usalama,” alisema Hamisa kwa kifupi na kuahidi kulifungukia suala hilo kwa kirefu zaidi muda si mrefu.
TUMEFIKAJI HAPA?

Tetesi za Hamisa ambaye ni mwanamitindo wa kitaifa na kimataifa na video queen matata kutoka na msanii huyo zilianza baada ya kufanya naye kazi katika ‘project’ ya wimbo.
Mara baada ya kujifungua, mama na dada wa msanii huyo walikwenda hospitalini kumjulia hali Hamisa, jambo ambalo lilisherehesha sakata hilo kuwa mtoto huyo ni damu yao.
Awali mrembo huyo ambaye kabla ya sakata hilo alizaa mtoto wa kike na bosi wa redio, alimfungulia mwanaye huyo akaunti ya Instagram kwa jina ‘Tanzania Baby’, lakini baadaye aliibadilisha na kuiita Abdul Naseeb_tz ambayo kwa sasa ina wafuasi zaidi ya laki moja.

Alichokipost Diamond Baada ya Ali Kiba Kuachia Wimbo Wake

$
0
0
Alichokipost Diamond Baada ya Ali Kiba Kuachia Wimbo Wake wa
Muda mfupi baada ya mwimbaji staa Alikiba kuachia video ya wimbo wake mpya ‘Seduce Me’ leo August 25, 2017, staa mwingine wa Bongofleva kutokea WCB, Diamond Platnumz amepost picha kwenye Instagram.

Diamond amepost picha ya mtu akicheka kitu kilichowafanya mashabiki kuunganisha matukio wakidai huwenda picha hiyo ni ujumbe baada ya kuusikia wimbo wa Alikiba.



Kutana na Mtatibu Wanyota za Binadamu Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka Comoro

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU WANYOYA ZA BINADAMU DUNIANI KOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO

KWA SASA YUPO TANZANIA MAALIM FADHILI RASHIDI ANA IWEZO WAKUJUWA JAMBOLAKO NAKULI TATUWA KWAMUDA MFUPI

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE

MAALIM FADHILI RASHIDI NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA MIGUU KUWAKA MOTO

KISUKARI VIDONDA VYATUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI PUMU ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIE POTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM ANATOWA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI YEYOTE

NAKUMILIKI MALIZA MAJINI KWAYULE ANAE HITAJI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZA KIUME ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASA (24)

ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YAMVUTO WABISHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE

KUSAFISHA NYOTA NAKUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHAKUTESEKA NJOO UWONE MIUJIZA YA MAALIM FADHILI RASHIDI CALLING+255719362806/ +255763276239/

KWA WHATSAPP IMO +255785786436/

Hili la Jackline Wolper Liwe Fundisho Kwetu Wanawake Wote Wanaopenda Serengeti Boys

$
0
0
Habarini za Weekend wanajamvi. Naomba niende moja kwa moja kwa Wanawake wenzangu wale Walioingia kwenye mtindo wa kuwataka au kuwakubalia Mahusiano ya Kimapenzi Wavulana wadogo alimaarufu Mario au Serengeti boys au Mwendo kasi kwa hapa kwetu Tz.

Jamani hawa vijana watawapeleka pabaya wanawake wengi mitaani nyumba zinaparaganika maelewano hakuna, mapenzi ya kawaida tu na Wanaume Watu Wazima nayo yanavunjika kitu mwendo kasi.

Naomba tuelewe ya kwamba hawa Wadogo zetu au Watoto wetu wavulana hivi Viserengeti viko kimasilahi zaidi wanataka kujikwamua kimaisha kutokana na hali ngumu mtaani wanatafuta kitonga eee upo hapo shoga. Wakisha timiza lengo lao au wakipata kitonga zaidi watakuacha kwenye mataa tena kwa aibu ujione kama Dunia nzima inakubana, atakutia stress na kukuhujumu kama siyo kukufilisi. Kikubwa hata shukrani hawana. Tofauti na mwanaume mtu mzima Mara mia atakuonea huruma kwanza yeye mwenyewe anajiona fahari kuwa nawe.

Mwanamke unaweza kosana na Wazazi, ndugu, jamaa na marafiki kwa ajili ya havi vitoto jamani. Tafadhali tujitathimini kwa kina kabla ya kujitumbukiza kwenye Mahusiano na Wavulana Wadogo WA Shule, Bodaboda, Madereva Bajaji, Wasafisha kucha, Wauza urembo n.k tutakuja kujutia maishani na kuona kama tumedhalilika.

Nimpe pole tu mdogo wangu kiumri Jackline Wolper  Yaliyopita si ndwele agange ya jayo kwa kuwa ameamua kuongea basi ameshapona maana katua zigo kifuani na moyoni, ni wakati wake sasa kuwa na mtu WA heshima kama yeye atulie nae ana kila kitu cha kuitwa "Wife Material" hana haja ya kuhangaika na hivyo vitoto vya Jana havijui hata maana ya namna ya kutumia K na Wapenda miserereko. Maisha bado yanaendelea na Watu wengi bado tunampenda kwa jinsi anavyojituma kutafuta maisha atumie njia halali inayompendeza Mungu atapata faraja ya milele , Amina.

Basi ni hayo tu nimeona ni-share nanyie wapendwa. Samahani kama kuna mtu itakuwa nimemkwaza kwa namna yoyote ile siyo kwa makusudi Bali ni kuelimishana tu " Wanawake majanga yetu yanakaribiana, Kitabu chetu ni Kimoja na Mungu wetu ni mmoja yule wa Huruma na Upendo".
Karibuni.

TAZAMA YALIYOMPATA JACK WOLPER HAPA CHINI:

Maromboso wa Yamoto Band Rasmi Ndani ya Wasafi WCB?

$
0
0
Nimepokea baadhi ya video mpya kutoka kwa wakali mbali mbai wa Bongofleva, na mojawapo ni ‘‘Zilipendwa’ ya kundi zima la WCB ambapo ndani yake tumeona uwepo wa Maromboso ambaye alikuwa kweye kundi la Yamoto Band.

Je ndo amesainiwa na label ya WCB? maana hakuna ilipoonyeshwa kuwa ni wimbo wa WCB kumshirikisha Maromboso japo tumemuona Maromboso ndani.

EXCLUSIVE: Ushauri wa Huddah kwa Alikiba na Diamond ‘ni umama’

$
0
0
Huddah ambae ni Mrembo kutoka Kenya aliepata umaarufu wake kupitia shindano la Big Brother Africa, ni shabiki mkubwa wa Bongofleva na amekua akifatilia vitu vingi vinavyoendelea kwenye muziki huu ambao ni mkubwa pia nchini Kenya.

Baada ya kusikia kuhusu beef inayoendelea, Huddah kama shabiki mwingine yeyote ametoa ushauri wake na alianza kwa kusema “napenda muziki wa Bongofleva, Wakenya wanapenda sana Alikiba… mimi napenda muziki wa Alikiba lakini hata Diamond sidhani kama ni mbaya, mziki wake ni mzuri na ni Mfanyabiashara”

UNATAKA KUJUA NINI ZAIDI HUDDAH AMEONGEA? BONYEZA PLAY HAPA CHINI

Polisi Yachunguza Mlipuko Kwenye Ofisi za Wanasheria

$
0
0
Polisi Yachunguza Mlipuko Uliotokea Kwenye Ofisi za Wanasheria
 Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya amethibitisha kushambuliwa ofisi za wanasheria za IMMMA saa 8 usiku wa kuamkia leo Jumamosi, Agosti 26.

Mkondya amesema polisi wanafanya uchunguzi kujua ni nini kilihusika katika tukio hilo la mlipuko.

“Tupo hapa eneo la tukio, uchunguzi unaendelea na ukikamilika tutawapa taarifa zaidi, ila hatujajua kama bomu limehusika,” amesema Mkondya.

Ameeleza hadi sasa hakuna watu wanaoshikiliwa kuhusika na tukio hilo.

Mmoja wa viongozi wa Kampuni ya IMMMA, Sadock Magai amesema hakuna wizi ambao umefanyika katika mali zilizokuwa ndani.

“Tuwaachie Jeshi la Polisi wafanye kazi yao,” amesema Magai.

Ofisi za wanasheria wa kampuni hiyo zipo Barabara ya Umoja wa Mataifa eneo la Upanga jijini hapa.

Miongoni mwa wamiliki wa kampuni hiyo ni Fatma Karume, ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.


Ali Kiba Avunja Rekodi Kwenye Accont Yake ya 'Vevo'

$
0
0
Ali Kiba Avunja Rekodi  Kwenye Accont Yake ya 'Vevo'
Msanii Alikiba ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Seduce me' ambao ameuachia jana amevunja rekodi na kuwapagawisha mashabiki katika mtandao wake wa YouTube katika account yake ya 'Vevo' kutokana na wimbo huo kuwa na kasi kubwa ya watazamaji.

Katika mtandao huo ambao Alikiba ameweza kuweka jumla ya video mbili 'Aje Remix' ambayo kwa zaidi ya miezi sita imeweza kutazamwa na watu zaidi ya milioni moja na kuchangiwa kwa jumla ya 'comment' 1000 huku video yake mpya 'Seducce me' ndani ya masaa 24 imeweza kufikisha watazamaji zaidi ya laki sita na kuchangiwa na watu zaidi ya elfu 6000 ndani ya muda mfupi.

Kasi hii si ya kawaida ukilinganisha na video ambayo ipo toka miezi sita iliyopita lakini ni wazi kuwa huenda kasi hii kubwa ya utazamwaji wa video hii unachangiwa na mapokeo mazuri ya washabiki wa muziki wa Alikiba ambao wanajikuta kila wakati wakitaka kuitazama video hiyo.
Haya ni baadhi ya maoni ya watu ambao wameweza kuitazama video hiyo na kufunguka ya moyoni mwao

Zito Kabwe Ashtushwa na Tukio La Bomu Ofisi ya Mawakili

$
0
0
Zito Kabwe Ashtushwa na Tukio La Bomu Ofisi ya Mawakili
Nimeshtushwa na tukio la bomu kwenye ofisi ya Mawakili wa IMMMA Advocates. Wakati tunaendelea kupata Taarifa zaidi nawasihi wanasheria wa kampuni hiyo kuwa na moyo wa subra na ninawapa pole Sana.

Kuna haja ya uchunguzi Huru kuhusu matukio ya aina Hii kwani yanamwelekeo fulani. Tukio kama hili lilitokea Kwa Wakili Omar Said Shaaban ambaye alikuwa anamtetea Ndugu Mansour Yusuf Himid. Sasa aina hiyo hiyo ya uhalifu imefanywa dhidi ya ofisi anayofanya kazi Wakili Fatma Karume ambaye ni mpwa wa Mansour. Tusiache mambo haya kuzoeleka hata kidogo.

OKWI: Nitapambana na Kuipa Ushindi Timu Yangu

$
0
0
OKWI: Nitapambana na Kuipa Ushindi Timu Yangu
STRAIKA wa Simba, Emmanuel Okwi raia wa Uganda, amesema kuwa kuanzia leo katika mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani atapambana kuhakikisha anafunga na kuipa ushindi timu yake.

Okwi aliyesajiliwa na Simba kwa mara nyingine akitokea SC Villa ya Uganda, licha ya kucheza michezo sita hadi sasa ukiwemo wa Yanga, amefunga mabao mawili pekee.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Okwi amesema kutokana na kutofunga mabao mengi, atajitahidi kuanzia leo kwenye mchezo dhidi ya Ruvu afunge ili kuipa ushindi Simba.

“Sipo tayari kuiona timu yangu inakosa matokeo, hivyo nitapambana leo nifunge ili tupate ushindi ambao mashabiki wetu wanahitaji.

“Lakini ili niendelee kulilinda jina langu lisishuke basi nitahakikisha nafunga kila mchezo ulio mbele yangu kwa maana kikosi chetu ni kizuri na kuna watu wazuri na wenye uwezo mkubwa, hivyo ushindi kwetu ni lazima kwa kila mchezo,” alisema Okwi.

Lwandamina Aula Yanga Aongezewa Mkataba

$
0
0
Lwandamina Aula Yanga Aongezewa Mkataba
Kocha wa Yanga, George Lwandamina hana mpango wa kuondoka, maana tayari ameongezewa muda wa kuendelea kufanya kazi Jangwani.

Uongozi wa Yanga umeamua kumuongezea mkataba wa mwaka mmoja kocha wake George Lwandamina raia wa Zambia baada ya ule wa awali kumalizika Julai 16, mwaka huu.

Katika mkataba wake uliopita, Lwandamina aliiwezesha Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita na kuifikisha katika nusu fainali ya Kombe la FA kabla ya kutolewa na Mbao FC ya Mwanza.

Katibu Mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa amesema  mchana kuwa, wameamua kumuongezea mkataba Lwandamina baada ya kuridhishwa na kazi yake.
“Tunaingia mkataba mwingine wa mwaka mmoja na Lwandamina kwani ule wa mwanzo umeisha na sasa kila kitu kipo tayari hivyo muda wowote tena kwa uwazi kabisa atasaini mkataba mpya.

“Tumejitahidi kwa uwezo wetu kuboresha mkataba wake mpya kwa kumuongezea maslahi kidogo ili apate motisha ya kufanya kazi yake ipasavyo,” alisema Mkwasa.
Lwandamina alitarajiwa kusaini mkataba huo muda wowote kuanzia jana mchana ili awe na uhakika wa kuendelea kufanya kazi yake kwa uhuru na kujiamini

Korea Kaskazini Yarusha Makombora Baharini

$
0
0
Korea Kaskazini Yarusha Makombora Baharini
Korea Kaskazini imerusha makombora matatu ya masafa mafupi , jeshi la Marekani limesema.
Makombora hayo yalirushwa kutoka eneo moja katika mkoa wa kaskazini wa Gangwon na kuruka kwa umbali wa kilomita 250 kulingana na maafisa wa Korea Kusini.

Tangu ifanyie majaribio kombora lake la masafa marefu mwezi uliopita, Pyongyang imetishia kurusha makombora yake katika kisiwa cha Marekani cha Guam.
Lakini jaribio hili la hivi karibuni linajiri kufuatia zoezi la kijeshi la pamoja kati ya Marekani na Korea Kusini.

Maelfu ya wanajeshi wa Marekani na Korea Kusini wanaendelea kufanya zoezi la pamoja ambalo hufanywa kwa kutumia Komyupta.

Marekani awali ilikuwa imeripoti kwamba makombora mawili yalikuwa yamefeli , lakini kulingana na tathmini yake mojawapo ya makombora hayo lililipuka wakati huohuo liliporushwa huku mengine mawili yakiruka kwa umbali wa kilomita 250 yakielekea maeneo ya kaskazini mashariki.
Makombora hayo yalirushwa kwa tofauti ya dakika 30 , kulingana na afisa mmoja.
Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini ilisema: Jeshi linaangalia kwa umakini hatua ya Korea Kaskazini ya uchokozi.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images