Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Utata Kuungua kwa Ofisi ya Wakili Fatuma Karume Magai Aeleza Kilichotokea

$
0
0
Utata Kuungua kwa Ofisi ya Wakili Fatuma Karume Magai Aeleza Kilichotokea
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uwakili ya IMMMA, Sadoc Magai ameelezea kilichotokea katika ofisi yao baada ya kudaiwa kulipuliwa akisema alipata taarifa za tukio hilo saa 11 alfajiri na baada ya kufika ofisini hapo alikuta tayari Jeshi la Polisi likiendelea na shughuli zake.

Amesema kuwa chanzo cha tukio hilo hakijajulikana lakini alikuta mapipa ya Petrol, pia vioo vimepasuka na mlango mkubwa wa kuingilia ofisini humo umebolewa kwa kitu kinachoonekana ni mlipuko.

Hata hivyo, eneo hilo lina walinzi wawili ambao wamekutwa maeneo ya Kawe wakiwa hawajitambui mithili ya watu walioleweshwa.

>>>”Hakuna majeruhi na hakuna kilichoibiwa zaidi ya athari za jengo, ambapo jengo hili lina ofisi za mawakili 25.” – Sadoc Magai.


Maskini Mobetto Mambo Yazidi Kumchachia, Wema na Zari Waungana

$
0
0
Maskini Mobetto Mambo Yazidi Kumchachia, Wema na Zari Waungana
MAMBO yanazidi kuwa mambo! Lile saga la mwanamitindo wa kitaifa na kimataifa, Hamisa Hassan Mobeto, kudaiwa kuzaa na msanii wa bongo Fleva linazidi kuchukua sura mpya kila kukicha, nyuma yake kukiwa na sarakasi nyingi ambazo siyo za nchi hii.

Ubuyu mpya mjini unadai kwamba, staa mwenye jina kubwa Bongo, Wema Isaac Sepetu amejitosa kwenye sakata hilo akidaiwa kuungana na mpenzi wa sasa wa Wema, Zari…  msanii huyo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwa ajili ya kumbutua Hamisa kwa kuwa jamaa huyo pia aliwahi kuwa mpenzi wa Wema (x boyfriend wake).

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na Wema, baada ya Hamisa kutikisa kwa ishu hiyo na kuungwa mkono na Wabongo wengi huku Zari akibaki peke yake, Wema na timu yake (Team Wema), wanadaiwa kuungana na Zari kwa ajili ya kumsaidia kujibu mashambulizi mitandaoni.

“Yaani kila kukicha mambo yanazidi kupamba moto kwenye mitandao ya kijamii. Unajua Zari alikuwa anashambuliwa kama mpira wa kona na wengine walikuwa wakimponda Wema kuwa alishindwa kuzaa na jamaa huyo ‘so’ Hamisa amempiga bao. Sasa Wema alichukizwa na watu wanaomsema vibaya wakimhusisha na tukio la Hamisa kuzaa na msanii huyo.

“Unaambiwa ghafla Wema amekuwa akionesha chuki za waziwazi anapoona au kuonesha habari inayomsifia Hamisa kuzaa na jamaa huyo.

“Na kweli upepo umeanza kubadilika maana Zari naye ameanza kupata sapoti ya kumshambulia Hamisa kutoka kwa Team Wema,” kilimwaga ubuyu chanzo hicho. Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, Risasi Jumamosi lilimtafuta Wema na kumuuliza juu ya yeye na timu yake kuungana na Zari katika kumshambulia Hamisa ambapo katika hali ya kushangaza, mwanadada huyo alikiri kumchukia Hamisa bila kutaja sababu.

Wema alisema kuwa, huko nyuma alikuwa na mapenzi makubwa kwa Hamisa, lakini hivi karibuni amejikuta tu hampendi.

“Nimekuwa simpendi tena kabisa na hata sasa hivi ukiniuliza sababu, siwezi kukujibu ni kwa nini simpendi.

“Huko nyuma nilikuwa ninampenda, lakini katika hali ya kawaida, simpendi tena,” alisema Wema. Hamisa anadaiwa kuzaa na msanii huyo ambaye amezaa na Zari watoto wawili kabla ya kusemekana kumtelekeza huku wazazi wa jamaa huyo wakipokea baraka hiyo kwa mikono miwili.

 

Yeriko Nyerere Aguswa na 'Zilipendwa' Ya Diamond Asema Diamondi Anakipaji Halisi

$
0
0
  Yeriko Nyerere Aguswa na 'Zilipendwa' Ya Diamond Asema Diamondi Anakipaji Halisi
Mwanachama wa Chadema Yeriko Nyerere amesema kuwa yeye kuwa amemsikiliza AliKiba na Diamond na kusema kuwa Diamond ni mwanamziki wa kipaji halisi.

Kada huyo wa Chadema ametweet maneno hayo kupitia ukurasa wake wa Tweeter leo kuonyesha hisia juu ya wasanii hao ambao wote wametoa nyimbo kwa kufuatana.

“Si shabiki wa miziki ya wabana pua wanaooga mara sita kwa siku, lakini nimesikiliza Kiba na Diamond, Diamond ni mwanamziki wa kipaji halisi.” ameandika Yericko Nyerere.
Hata hivyo baada ya post hiyo mashabiki wa pande zote mbili walishusha comment mbalimbali ambapo Yericko Nyerere amesema katika hizo nyimbo ya Diamond ni nzuri.

Mpaka sasa wimbo mpya wa Alikiba ‘Seduce Me’ ulioachiwa Ijumaa hii unaendelea kutrend kupitia mtandao wa video wa YouTube huku nafasi ya pili ukifuatiwa na wimbo mpya wa WCB, Zilipendwa.

Hii Hapa Ratiba ya Msimu Mpya 2017/18 Ligi Kuu soka Tanzania Bara Kuanza Leo

$
0
0
Hii Hapa Ratiba ya Msimu Mpya 2017/18 Ligi Kuu soka Tanzania Bara Kuanza Leo
Pazia la Ligi Kuu soka Tanzania Bara linatarajiwa kuanza kutimua vumbi rasmi hii leo kwa timu mbali mbali kuingia uwanjani na kuanza kwa michuano hiyo mikubwa kabisa hapa nchini.

Msimu huo mpya wa Vpl wa mwaka 2017/2018 wenye jumla ya timu 16 unaanza kwa michezo saba kuchezwa katika viwanja tofauti.
Mabingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) na Ngao ya Jamii, Simba SC leo itatupa karata yake ya kwanza kwa kuwavaa Ruvu Shooting, wakati michezo mingine itakayo pigwa ni Ndanda FC dhidi Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, huku Mwadui FC ikikipiga na Singida United.

Michezo mingine ni Mtibwa Sugar itakayocheza na Stand United, Kagera Sugar dhidi ya Mbao FC, Njombe Mji FC ikitarajia kutupa karata yake ya kwanza kunako Ligi Kuu dhidi ya Tanzania Prisons wakati mchezo wa mwisho ni vijana wa Manispaa ya Mbeya timu ya Mbeya City ikiingia dimbani kukipiga dhidi ya Majimaji FC ya Songea.

Wakati Mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Dar es salaam Young Africans ikatarajia kuingia uwanjani hapo kesho  Agosti 27 mwaka huu kumenyana na Lipuli FC.




Yingluck Shinawatra Atorokea Dubai

$
0
0
Yingluck Shinawatra Atorokea Dubai
Taarifa kutoka Thailand zinasema aliyekuwa waziri mkuu Yingluck Shinawatra ametorokea Dubai baada ya kukosa kufika mbele ya mahakama kusomewa hukumu mjini Bangkok.

Vyombo vya habari nchini vinasema alitorokea kupitia Cambodia na Singapore, kabla ya kusafiri hadi katika taifa hilo la ghuba ambako kakake Thaksin - waziri mkuu wa zamani pia, anaishi uhamishoni.

Yingluck Shinawatra alikuwa anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 10 gerezani iwapo angepatikana na hatia ya uhalifu kutokana na kuzembea kazini katika kesi kuhusu mpango wa ruzuku kwa wakulima wa mpunga unaosemakana kuchangia ushindi wake katika uchaguzi.

IGP Sirro Atoa Onyo kwa Polisi na Kuwataka Kufanya Kazi kwa Kutenda Haki

$
0
0
IGP Sirro Atoa Onyo kwa Polisina Kuwataka Kufanya Kazi kwa Kutenda Haki
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro, amefanya ziara ya kikazi ya siku mbili Arusha na kuwabadilikia baadhi ya polisi na kuwataka kufanya kazi kwa kutenda haki pasipo kujali rangi ya mtu pia amewaonya polisi waonaokwenda kinyume na utaratibu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.
Sirro amewataka polisi wanaokwenda kinyume na utaratibu wa jeshi hilo kuacha mara moja na kuwakumbusha kutenda kazi pasipokumuonea mtu ili kutenda haki kwa wananchi wote na kuleta usawa na kudai yoyote atakayebainika kwenda kinyume na utaratibu hatua zitachukuliwa ikiwemo kushtakiwa kijeshi.

Mbali na hilo IGP Sirro amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi ili kuweza kupata taarifa zinazohusiana na uhalifu na wahalifu kwa wepesi zaidi.



Agizo la Trump kwa Watu Waliobadili Jinsia Kutoajiriwa Jeshini

$
0
0
Agizo la Trump kwa Watu Waliobadili Jinsia Kutoajiriwa Jeshini
Rais Donald Trump ameagiza idara ya ulinzi Marekani kusitisha uajiri katika jeshi wa watu waliobadilisha jinsia zao.

Trump aliashiria hatua hiyo ghafla katika ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter mwezi jana.
Katika ilani kwa waziri wa ulinzi Jim Mattis, Trump amesema Pentagon ni lazima irudishe marufuku hiyo.

Idara hiyo ya ulinzi itaamua hatma ya watu ambao wamebadiisha jinsia na ambao tayari wanalitumikia jeshi .
Agizo hilo pia linasitisha nafasi ya wanajeshi wa kiume na wa kike kufanyiwa upasuaji wa kubadili jinsia zao

Baa Zilizobomolewa Zaendelea Kufanya Biashara Kwenye Magofu Yao

$
0
0
Baa Zilizobomolewa Zaendelea Kufanya Biashara Kwenye Magofu Yao
Wamiliki wa baa zilizobomolewa kupisha upanuzi wa Barabara ya Morogoro eneo la Kimara Stop Over wameendelea kufanya biashara kwenye masalia ya majengo yao, wakitundika miamvuli kwa ajili ya kuwakinga wanywaji.

Baa zaidi ya saba zimebomolewa na kati ya hizo tano pia imo Hoteli ya 5N iliyopo eneo la Suka kutokana na majengo hayo kuwa ndani ya mita 121.5 za hifadhi, kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Kuu.

Waandishi wa Mwananchi walishuhudia baadhi ya wafanyakazi wa baa na vibanda vya biashara wakiwa wametundika miamvuli kwa ajili ya kivuli kwa wateja wao.

Msimamizi wa Tulivu Bar aliyekataa kutaja jina lake, alimwambia mwandishi kuwa wataendelea na biashara eneo hilo.

“Hata hatujui. Sisi tunaendelea tu kufanyabiashara hapa mpaka (Rais John) Magufuli aje mwenyewe,” alisema mfanyakazi huyo.

Alisema hawawezi kuacha kufanya biashara kwa kuwa inawasaidia kuendesha maisha na hawana pa kwenda, hivyo wanawasubiri Tanroads waende kutoa vifusi na mabati ili wajenge vibanda kwenye magofu ya baa zao.

Pia, wamiliki wa baa hizo huendelea na biashara hata nyakati za usiku wakitumia taa ndogo za betri na wengine kandili, baada ya huduma ya umeme kukatwa kutokana na bomoabomoa.

“Biashara inaendelea japo tunawahi kufunga, lakini tunafanya biashara chini ya miamvuli kama unavyoona,” alisema mmoja wa wafanyakazi wa baa ya Tulivu.

Baa nyingine ambayo inaendelea na biashara ni Bliz Pub ambayo mbali na jengo kubomolewa, wateja wao hujisitiri kwenye magofu yaliyosalia nyakati zote za mchana na usiku.

Mbali na baa, wamiliki wa maduka ya huduma mbalimbali kama za fedha, vinywaji, mama lishe na wauza chipsi waliobomolewa, nao wameendeleza biashara kwenye majengo yaliyobolewa, wakidai wanafanya hivyo kwa kuwa hawana sehemu ya kwenda.

“Tunafanyia nje biashara maana vibanda vimebomolewa na hatuna pa kwenda,” alisema Hamisi Juma ambaye alikuwa na kibanda cha kukaanga chipsi eneo la Stop Over.

Mfanyabiashara mwingine ambaye alikutwa akifanya biashara nje eneo la Kimara Suka, Juma Seleman, alisema amesikitishwa na kitendo cha kubomolewa kibanda chake.

“Kwa sasa sina sehemu maalumu ya kwenda hivyo nimeamua kuendelea na biashara hapa nje,” alisema.

“Kwa kweli mpaka sasa sijui nitaenda wapi maana sina eneo jingine. Hapa ndipo nilipopategemea.”

Alisema mbali na kufanyia nje hali ya biashara kwa sasa si nzuri kwa sababu walikuwa wanategemea wafanyabiashara wengine waliokuwapo maeneo hayo kama wateja wao.

Lilian Michael anayefanya biashara ya chakula Kimara Stop Over alisema kwa sasa anafanya biashara yake katika mazingira magumu baada ya kibanda chake kubomolewa.

Alisema ataendelea na biashara yake kwenye mabaki hayo ya kibanda chake.

“Nimelipa kodi hapa hata miezi mitatu haijaisha, nitaendelea na biashara yangu hapa katika mazingira haya hadi hapo nitakapopata pesa ya kulipia sehemu nyingine,” alisema.

Alisema juzi Tanroads walivyokwenda kubomoa na baadhi ya vitu vyake viliharibika, hasa vyakula.

“Walikuja tukiwa tayari tumeshaanza kupika, vyakula vyetu vikamwagika. Kwa kweli kwangu jana (juzi) ilikuwa hasara, lakini sina jinsi. Ndio nchi yetu hii,” alisema.

Wakati Lilian akilalamikia biashara yake ya chakula kuwa ngumu, hali hiyo pia ipo kwa muuza duka la vinywaji baridi aliyejitambulisha kwa jina la Richard Nkwasi aliyesema hajui aende wapi kuendelea na biashara yake.

“Nilipanga hapa tangu Januari Mosi na nililipa mwaka mzima. Sasa leo naenda kupanga wapi? Na kwa pesa ipi?” alihoji.

“Jana(juzi) walikuja tu hapa ghafla wakaanza na zoezi lao kama unavyoona chupa zimevunjika na baadhi ya mayai hapa yamevunjika. Lakini sina jinsi, siwezi kupingana nao ila mimi hapa siondoki,” alisema.

Majengo hayo, yanayohusisha nyumba za makazi na biashara, yanabomolewa kupisha upanuzi wa barabara ya Ubungo Kiluvya ambayo inatumiwa na magari mengi yanayoingia jijini Dar es Salaam.


Kimenuka Bob Junior Aliamsha Dude Atoa Ujumbe Mzito Kwa Diamond Platnum

$
0
0
Kimenuka Bob Junior Aliamsha Dude Atoa Ujumbe Mzito Kwa Diamond Platnum
Producer aliyeshiriki kutambulisha kipaji cha Diamond Platnumz ‘Bob Junior’ amemwaga malalamiko yake kumlenga Diamond Platnumz Aka SIMBA akidai Simba kamla mpeka yeye…

“SIMBA NILIE MZOEA SIKU ZOTE NI SIMBA RAFIKI NI SIMBA NDUGU NI SIMBA KIPENZI LEO KAONA HAKUNA NYAMA MBUGANI KAAMUA KUNILA HADI MIE KWELI SIMBA HANA URAFIKI NA WAANADAMU MYAMA ATABAKI KUWA MYAMA NA BINAADAMU MYONGE ATABAKI KUWA MYONGE ACHA NIWE MYONGE ILA MUNGU NDIO MFALME NA YEYE NDIO ANAE TETEA WALE WANYONGE KAMA MIMI BABA MUNGU ULIE JUU HUKUMU UTAITOA WEWE….“

Ujumbe huu umetajwa kumuhusi Diamond ambaye Aka yake ni SIMBA na kwamba inasemekana Bob Junior alimuomba Diamond msaada na staa huyu akashindwa kumsaidia.


Haya Hapa Maswali Matano Kutoka kwa CUF ya Maalim Seif kwa Ndugai

$
0
0
Haya Hapa Maswali Matano Kutoka kwa CUF ya Maalim Seif kwa Ndugai
SIKU moja baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kusema hafanyi kazi na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, upande wa chama hicho unaomuunga mkono katibu mkuu huyo, umeibuka na kumhoji Spika maswali matano huku wakimkumbusha kauli yake aliyowahi kuitoa ya kumtambua Seif.

Maelezo hayo yalitolewa na  Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa CUF, Salim Bimani,

“Wakati wa kugombea ubunge wa Afrika Mashariki alitamka bungeni kuwa CUF ina matatizo.

“Akasema kuna CUF ‘A’ na CUF ‘B’ na akampokea Twaha Taslima ambaye alikuwa mgombea halali aliyepitishwa na kikao halali cha Baraza Kuu chini ya Katibu Mkuu, Maalim Seif.

“Pia akapokea wagombea hao haramu waliopelekwa na huyo Msajili ambao walipitishwa kutokana na Barua ya Profesa Lipumba (Mwenyekiti wa CUF, anayetambuliwa na msajili Profesa Ibrahim Lipumba). Hawa wote akawaruhusu waingie katika uchaguzi,” alisema.

Alisema kama Spika wa Bunge hawezi kufanya kazi na Katibu Mkuu wa CUF, ndani ya Bunge wapo wabunge wanaomuunga mkono Maalim Seif, hivyo awatoe wote.

“Ndugai alifanya maamuzi bila kufanya tafiti, chama kina kesi mahakamani dhidi ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Huwezi kufanya maamuzi mengine yoyote bila kwanza kutumia hekima tu na busara kusubiri kuuliza angalau huku ni kwema?

“Hili suala liko kwenye mahakama na Katibu Mkuu amechaguliwa na  Mkutano Mkuu mwaka 2014. Hivyo chombo kinachoweza kumwondosha ni Mkutano Mkuu wa Taifa.



“Makao Makuu ya Chama yako Zanzibar, Dar es Salaam ni Ofisi Kuu. Katibu Mkuu ni Taasisi, huwezi kusema Katibu Mkuu hajaenda Buguruni alafu ukapanga nafasi yake  akaimishwe mtu… Huo ni uvurugaji na uuaji wa demokrasia katika vyama vya siasa,” alisema Bimani.

Bimani pia alihoji ikiwa Bunge linatunga sheria ikiwamo ya  Vyama vya Siasa, je, Spika alijiridhisha kwenye Katiba ya CUF kama kuna Kaimu Katibu Mkuu?

Bimani aliendelea kuhoji kwamba hata kama Spika amejitetea kuwa anapewa taarifa na Msajili wa Vyama vya Siasa, lakini hakuona kama msajili ameshtakiwa mahakamani?

“Kwanini alifuata matakwa ya Msajili?  Yani Msajili anamwingiza kwenye shimo na yeye anaingia?” alihoji.

Alichosema Ndugai juzi

Akizungumza na waandishi juzi katika ofisi ndogo za Bunge zilizopo Dar es Salaam, Ndugai alisema hawezi kufanya kazi na Maalim Seif kwa sababu hayupo ofisini hivyo nafasi yake inakaimiwa na mwingine.

Alisema msimamo huo ni suala la utaratibu kwa sababu mwenye kumbukumbu za vyama vya siasa na viongozi wake halali ni Msajili wa Vyama vya Siasa, hivyo kama msajili akisema hamfahamu mtu na yeye lazima asimfahamu.

“Kwa hiyo linapotokea jambo kwenye chama ambacho kina mvutano, kazi yangu ni kumuuliza huyo mweka hazina wa vyama vya siasa kwa maana hiyo niliyoieleza kwamba ‘kuna huyu’, ‘aah huyu simfahamu’  basi na mimi nakuwa simfahamu. Akisema namfahamu basi na mimi nakuwa namfahamu.

“Lazima twende kwa utaratibu, ni sawa na taasisi fulani ambayo inatakiwa iandikishwe Brela (Wakala wa Usajili wa Leseni na Biashara) mnanielewa?  Ikatuandikia Bunge jambo fulani, lazima tuiulize Brela ‘bwana unamjua huyu’? Akisema hatumjui maana yake na mimi simjui.

“Sasa siwezi kuzuka nikawa nawatambua watu ambao hawatambuliwi na Brela, kwa maana hiyo ya makampuni na kadhalika, siwezi kuwatambua watu ambao hawatambuliwi na msajili kwa sababu huko ndiko vyama vinakopeleke Katiba zao, huko ndiko vyama vinakopeleka mabadiliko ya kumbukumbu zao za  mikutano ya mabadiliko yoyote yale,” alisema Ndugai.

Alisema Machi mwaka huu alipata barua kutoka kwa Msajili iliyomweleza kwamba amepata taarifa rasmi kuwa Maalim Seif Hamadi hayupo ofisini, hivyo majukumu ya chama hicho yatatekelezwa na Naibu Katibu Mkuu wake hadi hapo itakapoelezwa vinginevyo.

“Huo ndio msimamo wa tangu Machi kwa mujibu wa barua niliyokuwa nimeandikiwa kama rekodi ya kufanyiwa kazi, sasa ninapoletewa barua na mtu huyo baadaye ungekuwa wewe ungefanyaje?

“Wakati umekwishaharifiwa kwamba huyo mtu hayupo ofisini, sasa swali la kwanza ni kumuuliza huyo mtu amesharudi ofisini? Akikwambia hapana sasa barua naandikia wapi, Kongwa? (Kwenye Jimbo la Ndugai).

“Kwa hiyo inakuwa ngumu kidogo. Ni tatizo la kwao hamuwezi kumlaumu Spika au mtu mwingine. Ni usafi wa kufanya ndani kwao wenyewe, wakifanya usafi wao sisi wala hatuna tatizo.

“CUF ikisema inakutambua wewe sisi tutapinga?  Hili ni la kwao na wanajua zaidi wao kuliko sisi, tuwaachie wao wenyewe jukumu la kusafisha nyumba yao,” alisema Ndugai

Timu ya Simba Yachapa Mtu 7 Bila...Okwi Akifunga Magoli Manne......

$
0
0
Mchezo wa #VPL kati ya Simba na Ruvu Shooting umemalizika: Simba 7 vs 0 Ruvu Shooting
Magoli ya Simba Yamefungwa na:
Okwi (4)
Kichuya (1)
Erasto Nyoni (1)
Juma Liuzio (1)

Mume Wangu Amempa Mimba Mdogo Wangu....Naombeni Ushauri

$
0
0
Habari

Nimekuwa kwenye wakati mgumu kwa muda sasa.

Nimeolewa na Nina miaka miwili kwenye ndoa lakn sikuwa tayari kuzaa kwakuwa tulikubaliana mpaka nimalizie masomo yangu ya masters ambayo natarajia kumaliza mwaka huu.

Tumekuwa tunaishi vizuri tu na mume wangu nikimtii na kuwajibika kwa majukumu yangu yote kama mke kwa mumewe pamoja kuwa Ninafanya kazi na kusoma pia.

Mimi ni muajiriwa lkn mume wangu wangu ni mfanyabiashara kariakoo.

Nina mdogo wangu ambaye aligraduate mwaka jana akaomba akae kwangu wakati anatafuta kazi, sikuona shida nikamkubalia.

Tangu aje tumekuwa tukiishi vizuri tena kwa amani.

Kama Dada nilijitahidi kumtengea mdogo wangu bajeti yake toka kwenye mshahara wangu kwa kila mwenzi iliaweze kumudu kufuatilia mambo yake kirahisi.

Baada yakuwa nae kwa miaezi mitano nikaanza kuona mabadiriko kadhaa.
Akawa karibu na mume wangu sana, sikujali nikajua ni ushemeji tu.

Siku moja nilirudi nyumbani mapema sikukuta mtu.

Nikaendelea na maandalizi ya chakula cha jioni, nikiwa jikoni nikasikia sauti ya mume wangu na mdogo wangu wanabishana.

Niliposogea dirishani nisikilize vizuri huku nikichungulia nje nikaona dogo analia na mume wangu anambembeleza huku akimfuta machozi.

Nikatulia nione nini kinaendelea, nikasikia mume wangu anamwambia itabidi tuitoe maana Dada yako akijua wote tutakuwa nawakati mgumu..

Nikachukua simu yangu nikawa nawarekodi, baada ya muda wakaingia ndani nami nikajifanya sijui chchte.

Sikuwauliza chchte nikijipa muda wa kufanya utafiti zaidi.

Baada ya wiki, mdogo wangu akaniambia kuwa ana shida na Mimi.

Nikamsikiliza akaniambia kuwa ana mimba..

Sikuhamaki wala kuonyesha kama najua chchte, nilimuulize nani muhusika akajibu hajui.

Nikamwambia kama hujui sina namna ya kukusaidia siku ukijua utaniambia nijue jinsi ya kukusaidia.

Akaanza kulia na kunipigia magoti huku akisema nisamehe Dada, nikamwambia wala hujanikosea.

Nikamwambia wewe ni mtu mzima umeamua kuzaa kunashida gani?

Baba wa mtoto naamini yupo kwahiyo sikuhukumu.

Akasema, kuna jambo nataka nikwambie..
Niikamwambie aniambie..
Akasema lakini naomba unisamehe, shemeji ndo amenipa mimba.

Kwakweli niliumia sana, nikamuuliza wana muda gani tangu waanze mahusiano akajibu ni miezi minne sikujibu neno, nikaendelea na shughuli zangu.

Mume wangu alikuwa matembezi, aliporudi nikawaita wote wawili, nikamwambie Dogo aseme alichoniambia mbele ya shemeji yake.

Akasema tena ana mimba ya shemeji yake..mume wangu kusikia vile akataka kuwa mkali..

Nikamwambia hana haja ya kufoka, nikanyamaza sikusema wala kulaumu chchte.

Nikaamua kuwaita wazazi wangu na wake pia bila wao kujua,

Walipo kuja nikawambie Mimi ndiye niliyewaita lkn mume wangu na mdogo wangu ndiyo wanachakuwaambia.

Walipoulizwa wanasemaje dogo akaeleza kuwa anamimba ya shemeji yake..

Mume wangu alipoulizwa kwa unyonge sana alikubali. Wazazi wakaniuliza Nina maamuzi gani?
Nikawajibu nimeamua kumuachia mume mdogo wangu.

Wazazi wakanisihi nimsamehe na tuendelea na maisha ya ndoa..na dogo arudi kwa wazazi.

Niliwakatalia nakuwambia kuwa nisingeweza kuvumilia ndoa ya aina Ile..nikamwambia wasijipotezee muda wao kuniambia cha kufanya niliwaita waje wasikie uchafu niliofanyiwa then baada ya hapo mimi ndo nitoe maamuzi
Nilisisitiza maamuzi yangu nikutoendelea na ndoa tena.

Waliniambia nisichukue uamuzi bila kutafakari wakanipa wiki tatu za kufikiria Leo hii ni siku ya nane tangu nipewe muda wa kutafakari..

Niliwaomba niwe mbali na watuhumiwa wangu kipindi cha kutafakari.

Nikawasihisi watuhumiwa wao ndo wanipishe nyumbani kwangu, maana tunapoishi ni kwangu.

Wameondoka na sijui walipo kwenda.

Binafsi sijisikii kuendelea kuishi na huyu mwanaume ingawa kweli tumeshafunga ndoa lkn siwezi kuwa na raha ya ndoa ktk mazingira kama haya.

Najiuliza heshima yangu iko wapi?

Jamii inanionaje?

Na mtoto atayezaliwa ntamuonaje?

Naona dhambi hii ni kubwa sana siwezi kuibeba.

Wadau naomba msaada maamuzi niliyochukua naweza kuwa sahihi? Nisaidie plz.

Naomba Please sihitaji matusi wala mizaha nahitaji ushauri na faraja.

Naamini katika wingi wamashauri hapakosi hekima.

Ukimuita Msichana Mwende Out Akaja na Marafiki zake Kadhaa Kukukomoa, Basi we Fanya Hili Kumfunza Adabu

$
0
0
Ukimuita Msichana Mwende Out Akaja na Marafiki zake Kadhaa Kukukomoa, Basi we Fanya Hili Kumfunza Adabu
Mwanaume mwenzangu, ukimwita msichana kwa ajili ya mtoko akaja na rafiki zake ili akukomeshe. Wewe wajali sana wale rafiki zake piga nao story, waonyeshe picha zako kadha wa kadha.

Washirikishe masuala yako ya kiofisi wape namba zako zote za simu hadi ile ya mezani. Muda wa kuondoka wapatie nauli ya kutosha kisha waelekeze unapoishi wewe na ikibidi hata wanapoishi wazazi wako.

#Myfriend! Next time ukimuita ataogopa hata kuja na mkoba atahisi utaujali mkoba zaidi yake yaani atakuja kama alivyo.

How to Keep your Husband Interested in You!

$
0
0
In a couple, it is natural for the intensity of the passion to go down after several decades of marriage, but when that happens just after a few years of marriage, it maybe problematic. Here are tips for the wife to follow:

Radha is a mother of two kids aged 4 and 2. She is a teacher in a primary school and is also pursuing an MBA. She is very loving and giving and so being rejected doesn’t sit too well with her. And that is exactly what her hubby does all the time. He works in a call centre and has crazy shifts. When he returns, he’s grumpy and complains about how she has kept the house; that it smells. He doesn’t talk to her for weeks and their sex life is also dismal. They have sex like once a week and have been married for only 5 years.

There are many women like Radha who do their best for their families, but due to some reason or the other they are never appreciated for their efforts. She is young, loves her husband and is desperate to do something that would please him as she has no idea why he gets upset with her ever so often. So much so that she would even doubt herself that perhaps she is not wearing the right thing, or not smelling nice.

Radha is in a tough situation. Such behavior is unacceptable for a couple that has been together for just 4 years. At this point, most men run around the house looking to get their wife into the bedroom any chance that they can get.

There is little you can change about his personality with regards to his compulsive behaviour related to cleanliness, but you sure can work on other things. Here are some thoughts: 

Problem: Presence of financial issues which may be worrying him no end.
Solution: Sit down with him and review your finances together to see how he can work less so that he will have quality family and couple time. There is nothing worse for sex than being tired. He can use some anger management classes. A man not talking to his wife because the house doesn't smell right has issues.

Problem: You look messy and unattractive and a far cry from the ‘rose garden’.
Solution: To whatever extent possible, take care of yourself. It hard with two little kids, but even if it is fixing your hair or applying lipstick, it can make a difference in how you feel and how you look. It is sad that so many women do not realize this and that is why man are always looking at all those naughty pictures on the Internet because their wives walk around the house looking so dull and boring.

Problem: You are not exciting enough.
Solution: Buy thongs and G-strings for yourself to sex up your lingerie collection. Just wearing something sexy underneath your clothes will make you feel sexy and it will show. When you are in shorts at home and your pink panty straps shows as you bend in front of him, he will notice. The effect is the same when the top of the bra cup peeks through the camisole. Couples tell me that just switching from shorts to panties while sleeping does the trick too. You get the idea. Learn new ways of pleasing him. Show him such a wild time that he can never ever say no to you.

Note: Men are very visual and more than touching or kissing they get turned on first by what they see (or what they don't see right away).

Fahamu Umuhimu wa Vazi la Kanga Katika Tendo la Ndoa - Lazima Anase

$
0
0
Fahamu Umuhimu wa Vazi la Kanga Katika Tendo la Ndoa - Lazima Anase
Wapo wanawake ambao wameolewa lakini hawaoni hatari kuvaa kimitego bila kujali kuwa, kufanya hivyo ni kuiweka rehani ndoa......Kuna hili vazi la kanga moja ambalo baadhi ya wanawake wamekuwa wakipenda kulivaa hasa maeneo ya mjini, bila kujali ni mchana au usiku, kwenye nyumba ya kupanga au binafsi.

Hapo ndipo penye shida na leo nimeona nilizungumzie ili wale wenye tabia hiyo waache mara moja kama wanazitaka ndoa zao.....Niseme tu kwamba, ukiwa na mumeo chumbani wala sioni tatizo kumvalia kanga moja, wakubwa wanajua faida ya vazi hili katika kuidumisha ndoa.

Pia ikiwa mnaishi peke yenu, siyo hatari hata kidogo kuvaa kanga moja, akazurura nayo sebuleni, jikoni na sehemu nyingine za nyumba yenu. Nasema hivyo kwa sababu, kuvaa minguo kibao mbele ya mumeo naweza kusema ni ushamba, labda kama kuna baridi sana, unaumwa au hauko vizuri na mwenza wako. Kinyume chake unaweza kuvaa vazi hilo na ikawa ni chachu ya mambo yetu yalee.

Shida inakuja pale utakapovaa vazi hilo kisha kutoka na kwenda bafuni kuoga, mbaya zaidi uwe umejaaliwa umbile tata kama langu kisha kwenye nyumba unayoishi kuna wanaume kibao. Unadhani katika mazingira hayo ndoa yako itakuwa salama kweli?

Unadhani wapangaji wenzako watakuheshimu? Sidhani kama itakuwa hivyo. Kwa kuvaa kanga moja ni wazi utapata usumbufu mkubwa kutoka kwa wanaume wakware na wengi watakuona unatangaza biashara. Mumeo naye hawezi kufurahia hilo, labda awe ni miongoni mwa wale malimbukeni.

Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba, unapoingia kwenye ndoa unatakiwa kujitofautisha kabisa na wale ambao wako ‘singo’. Kanga moja ni vazi la kumvalia mumeo tena hasa chumbani.
Usijidhalilishe kuvaa nguo ambayo itakufanya utafsirike tofauti, udharaulike na kuonekana unatangaza biashara wakati una mume.

KIBAHA: Wachina Wadaiwa Kupiga 'Dili zito' Ujenzi wa Stendi Mpya ya Mabasi

$
0
0
Wananchi wa Mji wa Kibaha Mkoani pwani wameilalamikia kampuni ya M/S Group Six LTD inayojenga Stendi mpya ya mabasi kuwauzia kifusi cha mchanga ambacho halmashauri ya mji huo ilitoa bure kwa wananchi ili kupisha ujenzi wa kituo hicho.

Kwamujibu wa mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Kajumbo kutoka kampuni mzawa wa MEG Business Solution ameeleza kuwa Wachina hao wamekuwa wakiwatoza kiasi cha shilingi Elfu 5,000 hadi elfu 20,000 ili kupata kifusi hicho jambo ambalo ni kinyume cha Agizo la mkurugenzi wa  Halmashauri ya Mji wa Kibaha

Hata hivyo Rashid ambaye tayari alikuwa na kibali cha mkurugenzi mkononi cha kupewa kifusi hicho bure amesema magari yake manne yaliyo katika eneo la mradi wa Stendi hiyo inayojengwa karibu na Karakana ya Serikali hato yaondoa mpaka Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa atakapofika katika eneo hilo na kuelezwa jambo hilo.

Baada ya madai hayo Mtandao huu umemtafuta Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Bi.Jenifa Omolo kwa njia ya simu ambaye amesisitiza hafahamu chochote kuhusu hilo ingawa anatambua kifusi hicho kinatakiwa kutolewa bure na hivyo amefahamisha kuwa anafuatilia kama Kampuni hiyo inawauzia wananchi kifusi hicho.

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Idris Sultan Atua ‘Heaven Sent Premiere’ na Wema akiwa na ‘Love Bites’ (Video)

$
0
0
Msanii wa filamu na mchekeshaji, Idris Sultan ametua katika uzinduzi wa filamu ‘Heaven Sent’ ya aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Wema Sepetu akiwa na love bites shingoni. Idris amefunguka vitu mbalimbali kuhusu filamu hiyo pamoja na ‘love bites’ ambazo zinaonekana shingoni kwake.

TAZAMA VIDEO:

Mayweather Sio Mtu Mzuri Amchakaza Chakaza McGregor Kwa Knock Out.....

$
0
0
Bondia Mmarekani Mweusi Mwenye Asili ya Africa Floyd Mayweather Kwa Mara nyingine tena Amedhihirisha kwamba yeye ndio bondia bora Duniani baada ya kumtwanga McGregor Katika pambano lililopigwa round kumi tu ambapo Refa ilibidi akatishe pambano baada ya kipigo kikali alichokuwa anapata McGregor na hivyo Mayweather kushinda kwa Knock Out.....


Korea Kaskazini Yarusha Makombora 3 Baharini

$
0
0
Korea Kaskazini imerusha makombora matatu ya masafa mafupi , jeshi la Marekani limesema.
Makombora hayo yalirushwa kutoka eneo moja katika mkoa wa kaskazini wa Gangwon na kuruka kwa umbali wa kilomita 250 kulingana na maafisa wa Korea Kusini.

Tangu ifanyie majaribio kombora lake la masafa marefu mwezi uliopita, Pyongyang imetishia kurusha makombora yake katika kisiwa cha Marekani cha Guam.

Lakini jaribio hili la hivi karibuni linajiri kufuatia zoezi la kijeshi la pamoja kati ya Marekani na Korea Kusini.

Maelfu ya wanajeshi wa Marekani na Korea Kusini wanaendelea kufanya zoezi la pamoja ambalo hufanywa kwa kutumia Komyupta.

Marekani awali ilikuwa imeripoti kwamba makombora mawili yalikuwa yamefeli , lakini kulingana na tathmini yake mojawapo ya makombora hayo lililipuka wakati huohuo liliporushwa huku mengine mawili yakiruka kwa umbali wa kilomita 250 yakielekea maeneo ya kaskazini mashariki.

Makombora hayo yalirushwa kwa tofauti ya dakika 30 , kulingana na afisa mmoja, Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini ilisema: Jeshi linaangalia kwa umakini hatua ya Korea Kaskazini ya uchokozi.
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images