Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Je Dada Unahitaji Kuwa Mrembo na Ule Muonekano Bomba wa Kisuperstaa na Kaka Kuwa Mtanashati? Waone Hawa

$
0
0
Je Dada unahitaji kuwa Mrembo na ule muonekano bomba wa kisupersta, kaka unahitaji kuwa mtanashati na mvuto zaidi wa KIUME?fika black beauty company utatimiza ndoto zako,hawakosei hata siku moja kwa products original na zenye matokeo yaharaka sana,bila madhara, BLACK BEAUTY COMPANY  ni kampuni yenye uzoefu wa hali ya juu sana

1)kuongeza hips,makalio,mapaja@150000
(b)kuongeza hips,makalio,mapaja na miguu@200000/=
2)kuongeza miguu ,kuondoa vigimbi@120000/=
3)kuwa mweupe mwili mzima (Rangi moja)@150000/=
4)Kupungua mwili mzima@150000/=
5)kupunguza tumbo@100000/=
6)kupunguza au kuongeza matiti@100000/=
7)kukuza nywele@100000/=
8)kuondoa michirizi @100000
9)kuondoa madoa,mabaka na chunusi sugu@100000/=
10)kuongeza uume na nguvu za kiume@150000/=
Dawa zetu niuhakika sana100%na utaletewa popote ulipo,mikoani tunatuma,nje ya nchi tunatuma DHL,ofic zetu zipo kariakoo msimbazi police,

Karibuni kwa mawasiliano zaidi WhatsApp +255657778924,au call0743534406 au unaweza kutufollow
👇👇👇👇👇👇
@black_beauty_company

Alikiba Na Diamond Waendelea Kuchuana Vikali Views Youtube.....Kiba Aendelea Kuongoza

$
0
0
Alikiba Na Diamond Waendelea Kuchuana Vikali Views Youtube.....
Wimbo mpya wa Alikiba ‘Seduce Me’ ulioachiwa Ijumaa hii unaendelea kutrend kupitia mtandao wa video wa YouTube huku nafasi ya pili ukifuatiwa na wimbo mpya wa WCB, Zilipendwa.

Video ya muimbaji huyo wa RockStar400 mpaka sasa ina views 1,225,781 ikiwa ni video ya kwanza kuachiwa kabla ya WCB iliyoachiwa jioni yake.

Video ya WCB ‘Zilipendwa’ mpaka sasa ina views 736,323  ikiwa ina saa 12 toka iachiwe kupitia YouTube.

Kitendo cha WCB kuachia video ya wimbo huo muda mchache baada ya Alikiba kuachia Seduce Me, kumewafanya mashabiki wa wasanii hao kushindanisha project hizo mbili ambazo bado zinashindana kupitia mtandao wa YouTube.


Wawili hao kila mmoja anaonyesha bado ana hasira na mwenzake kwani kila mmoja anamtishia mwenzake ataachia ngoma nyingine.

Alikiba anadaiwa kutweet kwamba wimbo ‘Secude Me’ alikuwa anatesh mitando huku akidai ngoma kamili inakuja.

Kwa upande wa Diamond naye kupitia meneja wake Sallam amedai kwamba baada ya ‘Zilipendwa’ wataachia wimbo mpya ambao Diamond ameshirikiana na msanii mkubwa wa kimataifa.

 Itazame  ZILIPENDWA  ya  Diamond

Floyd Mayweather Aweka Rekodi Mpya Ulimwengu wa Ndondi..Tazama Picha 8 Jinsi Alivyomchapa McGregor

$
0
0
Floyd Mayweather Aweka Rekodi Mpya Ulimwengu wa Ndondi..Tazama Picha 8 Jinsi Alivyomchapa McGregor
Bondia Floyd Mayweather ameweka rekodi katika ulimwengu wa ngumi baada ya kushuka ulingoni mara 50 bila kupoteza hata pambano mara moja.

Rekodi hiyo mpya ameiweka leo (Agosti 26 kwa saa za Marekani) baada ya kumdhibiti Conor McGregor ambaye alikuwa ni hasimu wake katika pambano lililokuwa likisubiriwa kwa hamu katika mzunguko wa 10 na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa alama 87 dhidi ya 84 za Conor.

McGregor alianza vizuri pambano hilo kwa kumtwanga Mayweather lakini baadae kibao kilimgeukia huku akitupiwa makonde na kushindwa kujibu.

Baada ya pambano hilo lililofanyika katika uwanja uliopo Las Vegas, Mayweather amesema kuwa Conor ni mpiganaji mzuri kuliko alivyodhania lakini ameweza kuwapa mashabiki wake na wapenzi wa ngumi, kile walichokuwa wakikisubiria kwa hamu.

Mayweather amesema kuwa hilo lilikuwa ni pambano lake la mwisho na ana uhakika kwamba alichagua mshindani mzuri (Conor) ambaye alimpa ushindani mkubwa.

Hapa chini ni baadhi ya picha kutoka kwenye pambano hilo;








Chadema Yapokea Kwa Masikitiko Taarifa ya Kuungua Kwa Ofisi ya Mawakili

$
0
0
Chadema Yapokea Kwa Masikitiko Taarifa ya Kuungua Kwa Ofisi ya Mawakili
Dar es Salaam.Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa masikitiko taarifa za kuvamiwa kwa  ofisi za Kampuni ya Mawakili wa Kujitegemea ya IMMMA ya Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano na Mambo ya Nje John Mrema ilisema kwamba Chadema  inafahamu kuwa kwa mujibu wa Mikataba ya Kimataifa Mawakili wana haki ya kufanya kazi zao kwa uhuru na faragha wakati wa kutoa huduma zao kwa wateja wao na wananchi kwa ujumla. Ikumbukwe pia kuwa kwa  mujibu wa Sheria ya Mawakili (The Advocates Act) Mawakili ni Maaofisa wa Mahakama ambao huisaidia Mahakama katika kutenda haki.

‘’Kwetu Chadema tunaona kuwa hili ni shambulio dhidi ya Mahakama kwani maafisa wake wameshambuliwa’’ imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Kwa hiyo uvamizi wa ofisi za Mawakili unalenga kukiuka misingi ya ya Sheria na Mikataba ya Kimataifa inayolinda haki za Mawakili . Chama kinapenda kutoa rai kwa vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kutoa taarifa kwa umma ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wahusika wanapelekwa kwenye vyombo vya Sheria ili Sheria zichukue mkondo wake.

Aidha kitendo hiki kimefanywa na watu waoga wanaodhani kuwa kwa kufanya hivyo kutawafanya Mawakili wawe na hofu nchini na washindwe kutimiza wajibu wao, hivyo basi CHADEMA kinawatia moyo Mawakili wote nchini wasikubali kuingia hofu wala woga kutokana na tukio hili bali waendelee kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria.

Mwananchi:

Mwimbaji Aslay ni Bandika Bandua...Tazama Hapa Video ya Wimbo wake Mpya Unaitwa Pusha

$
0
0
Wakati Alikiba na WCB wakichuana ku-trending kupitia Youtube, msani wa Bongo Flava Aslay naye ameachia tena video yake mpya ya’ Pusha’, hii imekuwa kawaida kwa msanii huyo kuachia video mfululizo kwa mwaka huu.

VIDEO:

Kitu DC Ally Hapi Amemwandikia Alikiba Baada ya Kutoa ‘Seduce Me’

$
0
0
Baada ya mwimbaji staa wa Bongofleva Alikiba kuachia video ya wimbo wake mpya ‘Seduce Me’ August 25, 2017, wimbo huo umeonekana kupokelewa vizuri hata na viongozi wa kisiasa ambao hawakuficha hisia zao.

Mmoja wa wanasiasa ambao wameonesha kuupokea vizuri wimbo huo ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi ambaye alitumia Instagram yake kuuelezea.

DC Hapi aliandika
”Nimekuelewa sanaa wajina @officialalikiba. Kazi imeenda shule. Nidai zawadi kwa muziki huu wa ukweli. Keep the fire burning!🔥 #seduceme.”

ESMA KAULIZWA: Mama Diamond Alikua na Hali Gani Baada ya ile Picha ya Dimpoz?

$
0
0
ESMA KAULIZWA: Mama Diamond Alikua na Hali Gani Baada ya ile Picha ya Dimpoz?
Instagram ilichafuka juzi kati baada ya Mwimbaji Ommy Dimpoz kupost picha akiwa na Mama mzazi wa Diamond Platnumz ikiwa ni moja ya njia alizotumia kujibu mashambulizi ya diss ya wimbo wa Diamond Platnumz.

Kwenye hii video kuna mahojiano na Dada wa Diamond Platnumz Esma Platnumz na Mume wake Petitman ambapo moja ya maswali aliyoulizwa Esma ni kuhusu hali ya Mama Diamond baada ya Dimpoz kupost ile picha.

Esma alicomment kwenye hiyo picha ya Ommy Dimpoz na kumtaka mwimbaji huyo kutomuhusisha mama yake na ‘maugomvi yao’ ambapo baada ya kuhojiwa leo , Esma amesema Mama yake alikua kimya tu na hakuongea chochote kuhusu ile picha… unaweza kutazama kwenye hii video hapa chini

 VIDEO:

TAZAMA Pambano Zima la Ngumi Kati ya Floyd Mayweather na Conor McGregor Lililoisimamisha Dunia Usiku wa Leo

$
0
0
Kama ukiweza kuangalia live nimekuwekea hapa chini Video Ikionyesha Pambano zima la ngumi kati ya Floyd Mayweather na Conor lilifanyika usiku wa leo...Mayweather akiibuka mshindi

VIDEO:


Kutana na Mtatibu Wanyota za Binadamu Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka Comoro

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU WANYOYA ZA BINADAMU DUNIANI KOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO

KWA SASA YUPO TANZANIA MAALIM FADHILI RASHIDI ANA IWEZO WAKUJUWA JAMBOLAKO NAKULI TATUWA KWAMUDA MFUPI

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE

MAALIM FADHILI RASHIDI NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA MIGUU KUWAKA MOTO

KISUKARI VIDONDA VYATUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI PUMU ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIE POTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM ANATOWA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI YEYOTE

NAKUMILIKI MALIZA MAJINI KWAYULE ANAE HITAJI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZA KIUME ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASA (24)

ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YAMVUTO WABISHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE

KUSAFISHA NYOTA NAKUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHAKUTESEKA NJOO UWONE MIUJIZA YA MAALIM FADHILI RASHIDI CALLING+255719362806/ +255763276239

KWA WHATSAPP IMO +255785786436

Aunty Ezekiel Aongelea Urafiki wake na Wema Kupungua, Diamond na Alikiba

$
0
0
Mwigizaji wa Bongo Aunty Ezekiel amekaa kwenye EXCLUSIVE INTERVIEW na AyoTV kwenye red carpet Mlimani City Dar es salaam kwenye uzinduzi wa movie mpya ya Wema Sepetu na kujibu maswali yasiyopungua matatu.

KUHUSU UHUSIANO WAKE NA WEMA KUPUNGUA:

Mimi nahisi labda mazingira ambayo tunaishi, mimi nimenza kuishi na mtu na yeye amekua mwenyewe… labda mimi huku  nakuwa busy na mtoto kwahiyo tunatofautiana mazingira ambayo tunaishi lakini kusema uhusiano umepungua kutokana na sababu nyingine sio kweli” – AUNTY EZEKIEL

Joyce Kiria Aibuka na Kuwafungukia Wakaa Uchi Mitandaoni na Kutegemea Wanaume

$
0
0
KUTOKANA na matukio ya baadhi ya wanawake kujianika uchi mitandaoni kushika kasi, Mtangazaji wa Kipindi cha Wanawake Live, Joyce Kiria ameibuka na kuwapa somo kwamba, waachane na kujiuza, kisa njaa na kama wanapenda umodo, basi wafuate kanuni na taratibu za kimaadili na si kutumia njia hiyo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Joyce alisema kuwa, anashangazwa na wanawake wanaojianika uchi mitandaoni hivyo kuwataka waache kwani baadaye watajutia baada ya kupata madhara makubwa.

“Mimi mwenyewe maisha ya kutegemea wanaume kwa kutafuta fedha nimeyaishi na yalinitesa sana maana unajikuta unajichosha na kujiingiza kwenye mambo ya hatari,” alisema Joyce. Joyce alimalizia kwa kusema kuwa, mwisho aliamua kutumia akili na hadi sasa ni mjasiriamali na fedha anayoipata anaifurahia kwani anaamini ni jasho lake.

Shamsa Ford Adhamiria Kubadilika Mana Anahisi Siku za kufa Zimekaribia

$
0
0
STAA wa sinema za Kibongo, Shamsa Ford amefunguka kuwa, anatamani kumfuata aliyekuwa staa wa Taarab, Mzee Yusuf kwa kuokoka kwani anahisi siku za kufa zimekaribia.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Shamsa alisema kuwa, kila kukicha anajikuta anatamani kuokoka na kuacha kila kitu anachokifanya, abaki kusali tu kwani ana hofu sana ya Mungu, lakini hajui ataanzaje, ingawa anajitahidi. “Nimejaribu kusali sala tano kila siku.

Kuna wakati ninasahau lakini kuna siku ninasali zote, ninaamini taratibu nitakuwa kama Mzee Yusuf, ninamuomba sana Mungu,” alisema Shamsa.

Video ya ‘Seduce Me’ ya Alikiba Yavunja Rekodi ya ‘Salome’ ya Diamond Platnumz

$
0
0
Rekodi ya video ya muziki iliyotazamwa na watu wengi kwa muda mfupi kwenye mtandao wa Youtube nchini Tanzania iliyokuwa inashikiliwa na video ya wimbo wa Salome wa Diamond Platnumz, imevunjwa na video ya wimbo mpya wa Alikiba ‘Seduce Me’.

Video ya wimbo wa Salome ilitazamwa na watu milioni 1 kwa siku mbili huku video mpya ya Seduce Me imetumia masaa 37 yaani siku moja na masaa 13 kufikisha views milioni 1 na kuweka rekodi ya video iliyotazamwa zaidi kwa muda mfupi Tanzania na Afrika Afrika mashariki kwa ujumla.

Kwa sasa video inayoongoza kushikilia rekodi ya kutazamwa zaidi kwa muda mfupi barani Afrika baada ya kutoka ni Video ya Closer ya Wizkid ambayo ilitazamwa na watu milioni 1 kwa masaa 23.

Hata hivyo bado video ya Salome inashikilia rekodi ya video iliyotazamwa zaidi ndani ya wiki moja kwa kufikisha watazamaji milioni 3.

Je, kwa mwendo huo video ya ‘Seduce Me’ yenye siku mbili tangia itoke na tayari imetazamwa mara milioni 1.2 itavunja rekodi ya ‘Salome’ kutazamwa mara milioni 3 kwa siku 7?

Mahujaji 100 Waachwa Solemba Airpot. Sheikh Dar Aiwakia Kampuni iliyowatapeli

$
0
0
Mahujaji 100 Waachwa Solemba Airpot. Sheikh Dar Aiwakia Kampuni iliyowatapeli
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum amesema taasisi iliyokusanya fedha kwa waumini wapatao 100 na kushindwa kuwasafirisha kwenda hija, isakwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Tangu Agosti 23, waumini hao wamekwama Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya taasisi hiyo (jina linahifadhiwa kwa sasa) kuchukua hadi Sh10 milioni kutoka kwa kila hujaji, lakini ikashindwa kufanikisha safari hiyo.

Sheikh Salum alisema jana kuwa kuna haja kwa wahusika wa taasisi hiyo kusakwa, kukamatwa na kushtakiwa mahakamani kwa kuwa licha ya kuwatapeli mahujaji hao, imesababisha washindwe kutimiza azma yao ya kufanya ibada hiyo.

“Zipo taasisi zenye tabia ya kuwatapeli waumini na hii si mara ya kwanza. Niwape faraja mahujaji waliokwama kwamba kama mwaka huu hawajasafiri labda Mwenyezi Mungu alipanga wasafiri mwaka ujao. Cha msingi ni kuwa makini na kampuni za aina hii,” alisema.

“Kuna waumini wengine wamezuiwa kuingia Saudi Arabia kwa sababu taasisi zilizowasafirisha nazo hazina vibali vya kuingia huko. Sasa ni kwa nini wasafirishe watu wakati wanajua wazi kwamba hawajatimiza vigezo?”

Baadhi ya waumini waliokwama kusafiri wameiomba Serikali kuingilia kati ili warejeshewe fedha zao. Walisema mpaka jana jioni hawakuwa na taarifa zozote kuhusu safari yao, wakati fedha zote walishailipa taasisi hiyo yenye ofisi zake Kariakoo jijini hapa.

Mmoja wa watu waliokuwa wasafiri, Ummy Sekibo alisema licha ya jitihada za kutoa taarifa kwenye taasisi za kidini, vyombo vya habari na Jeshi la Polisi bado wameshindwa kuondoka.

“Hakuna matumaini tena kama taasisi hii inaweza kutusafirisha, maana tangu Agosti 23 tumeganda hapa na hatujui tufanye nini,” alisema Sekibo.
Ummy alisema kwa sababu lengo lake lilikuwa ni ibada, ameanza mchakato wa kutafuta fedha nyingine haraka ili aweze kusafiri huku akiendelea kushughulikia fedha zake ‘alizotapeliwa.

Mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Rajab Tendwa, alisema kila muumini amelipa fedha kulingana na makubaliano na taasisi hiyo. Walilipa kati ya Sh8.5 milioni hadi Sh10 milioni.

Paul Makonda Aamua Kufunguka Kuhusu Diamond na Alikiba, Adai Anapenda Ugomvi wao..Lakini....

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar ss Salaam Paul Makonda ameamua kuandika maoni yake kutokana na kile anachokiona kuhusu wasanii wa Bongofleva wanaoshindanishwa kimuziki ambao ni Alikiba na Diamond.

RC Makonda ameaandika maneno 17 kwenye Instagram ambayo yanawahusu mastaa hao wanaotajwa kuwa wana ushindindani kimuziki akionesha kufuraishwa na kazi za mastaa hao lakini akiwaonya tofauti zao kutovuka mipaka na kuvunja sheria au tamaduni za kitanzania.

“Tofauti zenu mimi nazipenda, kwani zinaleta ushindani mzuri kwenye mziki. Ila naomba mzingatie sheria na Utamaduni wetu..” – RC Makonda

Sheikh wa Mkoa: Waliokwamisha Mahujaji Kwenda Hija Wasakwe

$
0
0
Sheikh wa Mkoa: Waliokwamisha Mahujaji Kwenda hija Wasakwe
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum amesema taasisi iliyokusanya fedha kwa waumini wapatao 100 na kushindwa kuwasafirisha kwenda hija, isakwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Tangu Agosti 23, waumini hao wamekwama Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya taasisi hiyo (jina linahifadhiwa kwa sasa) kuchukua hadi Sh10 milioni kutoka kwa kila hujaji, lakini ikashindwa kufanikisha safari hiyo.

Sheikh Salum alisema jana kuwa kuna haja kwa wahusika wa taasisi hiyo kusakwa, kukamatwa na kushtakiwa mahakamani kwa kuwa licha ya kuwatapeli mahujaji hao, imesababisha washindwe kutimiza azma yao ya kufanya ibada hiyo.

“Zipo taasisi zenye tabia ya kuwatapeli waumini na hii si mara ya kwanza. Niwape faraja mahujaji waliokwama kwamba kama mwaka huu hawajasafiri labda Mwenyezi Mungu alipanga wasafiri mwaka ujao. Cha msingi ni kuwa makini na kampuni za aina hii,” alisema.

“Kuna waumini wengine wamezuiwa kuingia Saudi Arabia kwa sababu taasisi zilizowasafirisha nazo hazina vibali vya kuingia huko. Sasa ni kwa nini wasafirishe watu wakati wanajua wazi kwamba hawajatimiza vigezo?”

Baadhi ya waumini waliokwama kusafiri wameiomba Serikali kuingilia kati ili warejeshewe fedha zao.

Walisema mpaka jana jioni hawakuwa na taarifa zozote kuhusu safari yao, wakati fedha zote walishailipa taasisi hiyo yenye ofisi zake Kariakoo jijini hapa.

Mmoja wa watu waliokuwa wasafiri, Ummy Sekibo alisema licha ya jitihada za kutoa taarifa kwenye taasisi za kidini, vyombo vya habari na Jeshi la Polisi bado wameshindwa kuondoka.

“Hakuna matumaini tena kama taasisi hii inaweza kutusafirisha, maana tangu Agosti 23 tumeganda hapa na hatujui tufanye nini,” alisema Sekibo.

Ummy alisema kwa sababu lengo lake lilikuwa ni ibada, ameanza mchakato wa kutafuta fedha nyingine haraka ili aweze kusafiri huku akiendelea kushughulikia fedha zake ‘alizotapeliwa.

Mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Rajab Tendwa, alisema kila muumini amelipa fedha kulingana na makubaliano na taasisi hiyo. Walilipa kati ya Sh8.5 milioni hadi Sh10 milioni.

Mwananchi:

Ongeza Hips, Makalio na Mapaja, Kuwa Mweupe na Softi, Ongeza Maumbile ya Kiume na Hamu ya Tendo

$
0
0
MAMBO HAYOOOO!! ONGEZA HIPS, MAKALIO NA MAPAJA, KUWA MWEUPE NA SOFTI, ONGEZA MAUMBILE YA KIUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO N.K @markson_beauty_pr Tunakuletea bidhaa bora zenye matokeo ya uhakika na haraka zisizo na kemikali wala madhara. Zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa kiafya. NB. Matokeo ni uhakika na garantii na risiti


BIDHAA ZETU:- 1.Kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @130000@130,000/=
2.Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa:-
(a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @200000@200,000/=
(b)Vidonge @180000@180,000/=
(c)BOTCHO 10× ya kupaka @170000@170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @130000@130,000/=
(11)Vidonge @150000@150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150000@150,000/=
5.Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a)SHARK POWER gely ya kupaka (Inaongeza inch 6-7) @150000@150,000/= (b)Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/= (C)HANDSOME UP ORIGINAL- kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo @250000@250,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150000@150,000/=
7.Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @130000@130,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @130000@130,000/= (b)Mkanda wa kawaida @120000@120,000/= (c)Micro-computer belt wa umeme @200000@200,000/=
9.Kupunguza maziwa na kuyasimamisha hata kwa walionyonyesha @130000@130,000/=
10.Kushepu miguu (CHUPA YA BIA) na kuondoa vigimbi @130000@130,000/=
11.Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @120000@120,000/=
12.Kurudisha usichana (bikra) @120000@120,000/=

Wasiliana nasi :- (+255) 0767447444 au. 0714335378

TAHADHARI: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. 👉🏻Ili kuona bidhaa zaidi na shuhuda za waliotumia bidhaa zetu. ............... Follow us on instagram @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Kimenuka...Rais wa TLS Tundu Lissu Atangaza Mgomo

$
0
0
Mwanasheria mkuu wa CHADEMA na Rais wa chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Mhe Tundu Lissu, amewataka mawakili wote nchini kugoma kwenda mahakamani siku ya jumanne na jumatano, kuonesha kupinga vitendo walivyofanyiwa mawakili wenzao wa IMMMA, ambao ofisi yao imechomwa moto.


Tundu Lissu amesema kitendo hicho kinaingilia uhuru wa wanasheria na taaluma ya sheria pia kinahatarisha uhuru wa mahakama na utawala wa sheria kwa ujumla huku akiwataka mawakili wote nchini walio chini ya Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS),  kutokwenda  mahakamani kufanya kazi zao.

“Baraza la uongozi linawataka wanachama wa TLS nchi nzima kususia kuhudhuria katika mahakama pamoja na mabaraza ya aina zote kati ya siku za jumanne na jumatano ya tar 29 na 30 Agosti 2017, kwa lengo la kuwaunga mkono mawakili wa IMMMA, na kuonyesha kutokukubaliana kwetu na vitendo vya kihalifu vya kuwashambulia mawakili hao kwa mabomu”, amesema Mhe Tundu Lissu leo kwenye mkutano wake na Waandishi wa Habari.

SOMA ZAIDI- Nimeshtushwa na tukio la bomu kwenye Ofisi ya Mawakili – Zitto

Hata hivyo Tundu Lissu amesema Ofisi za IMMMA Advocates zimelipuliwa kwa mabomu na kusababisha baadhi ya nyaraka kupotea kitu ambacho kitawafanya Mawakili hao kushindwa kufanya kazi kiufasihi.

“Mawakili wa IMMMA wameshambuliwa ofisi zao zimepigwa mabomu, nyaraka zimepotea zingine zimeungua moto, hawataweza kwenda mahakamani kwa sababu vitendea kazi vyao vimeharibiwa, sisi mawakili wengine wote nchi nzima, tuna wajibu wa kuwaunga mkono mawakili wa IMMMA kwa kutoenda mahakamani vile vile, akiumizwa mmoja tumeumizwa wote, kwa hiyo tunawataka wanachama wetu popote walipo kesho kutwa wasiende mahakamni, wasiende kwenye mabaraza yoyote ili kuwaunga mkono wenzetu ambao wameshambuliwa”,amesema Lissu.

Mpaka sasa ni siku moja tangu ofisi ya za mawakili wa IMMMA zilizopo Upanga jijini Dar es Salaam kuungua moto  na waliohusika na uhalifu huo bado hawajajulikana.

Faida za Kulala Bila Nguo Nyakati za Usiku

$
0
0
Mara nyingi tumezoea kula na nguo nyepesi ifikapo usiku, pia kuna watu wengine hujifunika mashuka au blenketi. Kwa mujiu wa makala mbalimbali za afya zinaeleza kuwa si vizuri kiafya kulala na nguo.



Hizi ni faida chache za kuto lala na nguo nyakati za usiku.

1. Hutengeneza uhusiano mzuri ukisaidiwa na kichocheo cha Oxytocin.

Natasha Turner, daktari wa tiba asilia aliyeandika kwenye blogu ya Huff Post Canada, alifichua kwamba kulala karibu au mkiwa mmekumbatiana na mwenzi wako mkiwa bila nguo hufanya mwili kutoa kichocheo kiitwacho Oxytocin kinachofanya ujisikie vizuri. Hii inatokea pale kunapokuwa na mgusano wa ngozi kwa ngozi, hii inaweza kusaidia kuondoa msongo (Stress) na kushuka moyo (Depression). Oxytocin pia inaweza kupunguza shinikizo la damu, kuimarisha tumbo na kupunguza uvimbe kwenye utumbo. Pia, utendaji wako wa tendo la ndoa pengine unaweza kuboreka.

2. Hukufanya ubaki kijana.

Inashauri kuweka mwili katika jotoridi chini ya 21°C ukiwa kitandani na njia nzuri kufanta hivyo ni kulala uchi/mtupu. Hii huruhusu vichocheo vinavyozuia uzee na Melatonin ambayo hudhibiti mzunguko wa kusinzia na kuamka kutenda kazi vizuri. Utajihisi huru, Kulala kitandani kwako, bila kuvaa chochote inakufanya kujisikia huru.

3. Huhamasisha vichocheo vya furaha.

Unapolala na nguo au kulala chini ya blanketi zito unazuia utokaji wa kichocheo cha ukuaji (Growth Hormone/HGH). Hii ina maana hutoweza kupunguza mafuta ukiwa katika usingizi au hautofaidika na ukarabati wa usiku wa mifupa, ngozi na nyama za mwili wako.
Kulala uchi/mtupu pia huthibiti kiwango cha Cortisol, zinazo dhoofisha kinga ya mwili, kupandisha shinikizo la damu na lehemu (Cholestrol), kuvuruga mpangilio wa usingizi, kupunguza hamu ya tendo la ndoa na kuongeza hamu ya sukari.

4. Inatunza afya viungo vya uzazi.

Kina dada, mnafahamu mnaweza kupunguza matatizo ya mabukizi ya fangasi kwa kulala uchi/watupu? Unaweza kupunguza kuzaliana kwa fangasi na uke wako utakushukuru kwa hilo. Vilevile wanaume wanaweza kufaidika kulala uchi/watupu kwa kuwa korodani zinakuwa katika jotoridi la kutosha na uzazi unaongezeka.

5. Mzunguko wa damu unakuwa bora

Hakuna kitu kibaya kama lastiki inayozuia mzunguko wa damu. Ondoa nguo zenye lastiki na utajipata uko na furaha kwa mtiririko wa damu mzuri ndani mwili wako, vile vile inaelezwa kuwa ukiwa hauna nguo inasiaia kutunza ngozi yako kwani inaweza kupumua vizuri.

6. Kutokuwa mvivu

Faida nyingine ni kwamba mara baada ya kuamka unakuwa na ulazima wa kuvaa nguo kwa ajili ya siku hiyo mpya na sio kuamka na nguo zako za kulalia na kutoka nazo nje.

Chanzo Mtandao

Ukweli Mchungu...Kisheria Matonya Hana Haki yoyote ya Kusema Ameibiwa Nyimbo ya Zilipendwa na Diamond....

$
0
0
Na Zawadi B Lupelo

Tulipokuwa tukisoma kiswahili mwalimu wetu wa fasihi (kiswahili 2) alipenda sana kutoa tafsiri ya neno mojamoja. Alituambia SANAA ni UFUNDI wa kueleza mawazo yaliyo katika fikra za mwanadamu. Ni kweli mwanadamu ana mawazo mengi sana lakini kuna namna ya kueleza hayo mawazo hivyo basi wanachokifanya wasanii ni ule ufundi wao wa kueleza yale yaliyomo akilini mwao. Kilichomo kwenye akili ya Diamond (mawazo yake) yanaweza yakawemo pia kwenye akili ya mtu mwingine yeyote lakini mtu huyo asiwe na ufundi wa kueleza mawazo hayo kama anavyofanya Diamond Platnumz. Anaweza asiwe na sauti kama yake, anaweza asiwe na uwezo wa kuandika mashairi kama yake, uwezo wa kunata na beat kucheza nk.
Maneno ya mwalimu wetu wa kiswahili 2 hayakuwa mbali na sheria zetu hasa inapokuja kwenye sanaa. Sheria za hati miliki zinatambua uwepo wa ufundi binafsi kwa msanii wa kuwasilisha mawazo aliyonayo ndiyo maana sheria inalinda ule ufundi wa msanii na si vinginevyo.
Ili nieleweke vyema tambueni kwamba katika sheria za hati miliki za wasanii (copyrights laws) kuna kitu kinaitwa ideas na kitu kinachoitwa expression of an idea, sheria haiprotect idea inaprotect expression ya ideas. Kiufupi naweza kusema expression of ideas ndiyo huo ufundi uliotumika lakini ideas ni mawazo. Kama nilivyoeleza hapo juu sometimes ideas (mawazo) yanaweza kufanana lakini hatutegemei ufundi wa kuyaeleza hayo mawazo kufanana.

Katika wimbo wa WCB "Zilipendwa" na ule wa Matonya "Zilipendwa" ukisikiliza kwa makini utagundua kilichomfanya Matonya alalamike ni baada ya kuona ideas za nyimbo hizo mbili zinafanana yaani ideas zao wote wawili ilikuwa ni kuelezea vitu na watu mbalimbali waliokuwa hot au wanafanya vizuri enzi hizo lakini sasa wamepitwa na wakati. Hiyo ndiyo idea ya hizo nyimbo mbili.

Kama nilivyosema awali kufanana ideas si kosa kwa sababu kuna wakati watu huwa na mawazo yanayofanana kuhusu jambo fulani na huenda siyo wao tu wenye ideas hizo wapo watu wengine wengi wenye ideas za namna hiyo lakini ukiwaambia express wataexpress kwa namna tofauti hapo ndipo linapokuja neno sanaa (ufundi wa kuwasilisha mawazo uliyonayo)

Kitu kingine ambacho kimemshtua Matonya ni neno "Zilipendwa", It is obvious kwamba sheria yetu ya hati miliki na siyo sisi tu bali dunia nzima haiprotect maneno, maneno yanakuwa protected kwenye trade marks na service marks mara nyingi majina ya kampuni na bidhaa lakini siyo katika muziki. Katika copyright laws huwezi ukawa na hati miliki ya neno na tukifanya hivyo maana yake maneno mengi sana itabidi yasitumike tena maana maneno zaidi ya asilimia 90 yameshaimbwa.

Sheria yetu ya Tanzania ya hati miliki inaitwa Copyright and Neighbouring rights Act ya mwaka 1999 kifungu cha 5(2)(d) inaeleza kwamba kitu kinachokuwa protected kwenye mziki ni Instrumental na Vocals tu na si neno au vinginevyo hii ni kwa sababu hapo ndipo penye ufundi. Ufundi wa mwanamuziki upo hapo kwenye Vocals na instrumentals na si kwenye maneno kama Matonya anavyotaka kutuaminisha. Msanii hagundui maneno la sivyo Matonya anataka kusema yeye ni muhenga aliyegundua neno " Zilipendwa "

Ni jukumu la Matonya kuthibitisha kama ameibiwa vocal au instrumental na WCB la sivyo hana haki yoyote ambayo imevunjwa.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images