Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Hii Hapa Siri ya Bill Nass Kutoa Nyimbo Kali

$
0
0
Hii Hapa Siri ya Bill Nass Kutoa Nyimbo Kali
Msanii wa Bongo Flava, Bill Nass amesema kuendelea kujifunza vitu vipya katika muziki ndio sababu ya kuendelea hit song.

“Kikubwa ni kuendelea kukomaa, kuendelea na kasi kwa sababu muziki kila siku unakua, kwa hiyo kama mimi sikuwi nipo pale pale ina maana muziki utamuacha,” ameiambia Bongo5.

“Kwa hiyo ni kuendana na kasi ya muziki namna unavyokua , pia kuna vitu vipya nimevipanga na tumeanza na Sina Jambo, tumewekeza humo tunataka tuone ni namna gani tunaweza tukapata faida  tukawekeza katika project nyingine all in all ni kuendelea kusapoti muziki mzuri na vitu vingine vikubwa vinakuja,” amesisitiza.

Ngoma mpya ya Bill Nass ‘Sina Jambo’ ni ya tano kutoa tangu alipotoka na ngoma yake ya Raha na kufuatiwa na Ligi Ndogo, Chafu Pozi na Mazoea.


Hawa Hapa Viongozi Wa Serikalini Walioguswa na Nyimbo ya Seduce Me ya Ali Kiba

$
0
0

Hawa Hapa Viongozi Wa Serikalini Walioguswa na Nyimbo ya Seduce Me ya Ali Kiba
Kiongozi Mwingine ambaye aliwahi kuwa waziri wa Nishati na Madini Willium Ngereja naye ameonekana kuguswa na wimbo huo na kuamua kumpongeza Kiba n kuandika Hivi kweenye Ukueasa wake wa Instagram

"King @OfficialAlikiba : Nyimbo ya Seduce me umeitendea haki tasnia ya muziki nchini pia utaitambulisha nchi yetu kimataifa. Hongera"

Mwingine ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Ally Hapi ameweka hisia zake hadharani kwa kumsifia Alikiba kwa uzuri wa wimbo wake  mpya wa ,Seduce me’ huku  akiahidi kumpatia zawadi yoyote aipendayo

Mhe. Hapi ameshindwa kuzuia hisia zake juu ya wimbo huo mpya wa Alikiba ikiwa ni siku chache zimepita tangu msanii huyo aachie ngoma hiyo  baada ya kukaa mwaka 1 na miezi kadhaa tangu alipotoa wimbo wake wa Aje .

“Nimekuelewa sanaa wajina @officialalikiba. Kazi imeenda shule.Nidai zawadi kwa muziki huu wa ukweli.Keep the fire burning!”,ameandika Mhe Ally Hapi.

Wimbo huo ambao tayari umeshavunja rekodi ya kutazamwa zaidi kwenye mtandao wa Youtube nchini Tanzania unaonekana kuwazutia mastaa kibao hapa nchini akiwemo Wema Sepetu.


JE Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kufika Kileleni Haraka na Kushindwa Kurudia Tendo?

$
0
0
JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUFIKA KILELENI HARAKA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k. Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250000@250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7 @150000@150,000/=
3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130000@130,000/= BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA. KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255) 0767447444 na 0714335378

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. < WELCOME ALL>

Lulu Michael Ampiga Dongo Babu Kubwa Diamond Baada ya Kutoa Wimbo ili Auzime wa Ali Kiba

$
0
0
Lulu Michael Ampiga Dongo Babu Kubwa Diamond Baada ya Kutoa Wimbo ili Auzime wa Ali Kiba

Mrembo kutoka kiwanda cha filamu Bongo, Elizabeth Micheal maarufu Lulu ameamua kutupa jiwe gizani katika mtandao wa kijamii wa Twitter ambapo ameandika umeshagundua kitu kizuri ukikifanya kwa nia mbaya hakifanikiwi kwa uzuri wote.

Kupitia mtandao huo Lulu ameandika “Hivi Umeshagundua Kitu Kizuri Ukikifanya kwa Nia Mbaya Hakifanikiwi Na Uzuri wake woooooote…!😒.”


Kauli ya mrembo huyo imetafisiriwa kuwa ni ndogo kwa WCB, baada ya kuachia ngoma siku sawa na Alikiba, kitendo ambacho ngoma ya Alikiba imeonyesha ikiwa na kasi ya kupata views wengi na kutreanding kwa muda mrefu.

Na Laila Sued

Rais Magufuli Atoa MAAGIZO Mazito TAKUKURU

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kutokuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua pale wanapokuwa na ushahidi dhidi ya watu wanaojihusisha na vitendo vya rushwa.

Mhe. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo  tarehe 28 Agosti, 2017 alipotembelea na kuzungumza na wafanyakazi wa TAKUKURU katika ofisi za makao makuu ya taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam.

“Kuna mambo mengi ya hovyo yanafanyika, tumehakiki pembejeo za ruzuku na kubaini madai ya Shilingi Bilioni 48 ni hewa, tumebaini wafanyakazi hewa zaidi ya 19,500, tumebaini kaya masikini hewa 56,000 zilizopaswa kupata fedha TASAF, tumebaini wanafunzi hewa 5,850 waliotakiwa kupata mkopo, kuna vichwa vya treni 11 vimeletwa bila kuwepo mkataba na mengine mengi, haya yote yanafanyika kwa rushwa, nataka kuwaona mnachukua hatua stahiki” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amesema ana imani na TAKUKURU na amewataka wafanyakazi wa taasisi hiyo kufanya kazi kwa kuzingatia weledi, uzalendo na uadilifu mkubwa na kwamba Serikali itafanyia kazi changamoto zinazowakabili.

Katika mkutano huo Mhe. Rais Magufuli amepokea masuala mbalimbali kutoka kwa wafanyakazi wa TAKUKURU na amewaahidi kuwa Serikali itayafanyia kazi ili kuboresha maslahi yao na mazingira ya kazi.

Mkutano huo umehudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Anjellah Kairuki, Katibu Mkuu Dkt. Laurian Ndumbaro na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Valentino Mlowola.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi na wataalamu wanaosimamia utekelezaji wa miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa mradi wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stieglers’ Gorge Hydropower Project), ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) na ujenzi wa barabara mbalimbali nchini, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Katika Mkutano huo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Matogolo Kalemani ametoa taarifa ya maandalizi ya awali ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa umeme wa Stiegler’ Gorge na kwamba zabuni ya kuanza kwa ujenzi huo itatangazwa tarehe 30 Agosti, 2017.

Mhe. Rais Magufuli amesema fedha za kuanza kwa ujenzi wa mradi huo mkubwa utakaozalisha Megawatts 2,100 zitakazoingizwa katika gridi ya Taifa zipo.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

28 Agosti, 2017

Kiba Aonyesha Jeuri Mbele ya Diamond Seduce Me Yagonga Views Milioni 2 Ndani ya Siku 3

$
0
0
Msanii wa Bongo Flava, Alikiba amezidi kuweka rekodi kupitia wimbo wake mpya ‘Seduce Me’ ambapo kwa sasa umefikisha views Milioni 2 ndani siku tatu.

Hapo awali wimbo huo uliweka redodi ya kufikisha views milioni 1 ndani ya saa 37 sawa na siku moja na masaa 13 na kuweka rekodi ya video iliyotazamwa zaidi kwa muda mfupi Tanzania na Afrika Afrika mashariki kwa ujumla, hivyo kuipuku video ya wimbo wa Salome ya Diamond iliyotazamwa na watu milioni 1 kwa siku mbili.

Kwa sasa video inayoongoza kushikilia rekodi ya kutazamwa zaidi kwa muda mfupi barani Afrika baada ya kutoka ni Video ya Closer ya Wizkid ambayo ilitazamwa na watu milioni 1 kwa masaa 23.

By Peter Akaro

Polisi Watoa Majibu ya Uchunguzi Ofisi za Mawakili wa IMMMA Kulipuliwa Bomu

$
0
0
Polisi Watoa Majibu ya Uchunguzi Ofisi za Mawakili wa IMMMA Kulipuliwa Bomu
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, leo limesema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa watu wasiojulikana utambulisho wao na idadi yao walifika katika ofisi za Mawakili wa IMMMA Advocates wakiwa katika magari mawili na kujifanya ni maaskari na kuwarubuni walinzi na kuondoka nao katika gari mojawapo kabla ya kulipua jengo hilo.

Walinzi hao wanadaiwa kukutwa baadaye maeneo ya Kawe wakiwa hawajitambui.

Imedaiwa kuwa kundi lililobaki liliingia katika ofisi hizo hilo na kuweka vilipuzi vilivyotengenezwa kienyeji, ambavyo vililipuka muda mfupi baada ya watu hao kuondoka eneo hilo na kusababisha uharibifu wa wa mali na jengo la ofisi hiyo pamoja na majengo ya jirani.

Jeshi hilo limesema kuwa linaendelea kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini watu waliofanya tukio hilo na kujua dhamira yao ili wafikishwe katika vyombo vya sheria kwani wajibu wa jeshi la polisi ni kulinda raia na mali zao na kamwe haliwezi kuhujumu maisha ya watu na mali za wananchi

Aidha, jeshi hilo limewaomba waathirika wa tukio hilo na wananchi kwa ujumla kuwa watulivu wakati vyombo vya dola vikiendelea na upelelezi wa tukio hilo

Ali Kiba Ataja Sababu ya Wimbo Wake Mpya Kupokelewa Vizuri

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva Nchini Ali Kiba amefunguka juu ya siri inayomfanya awe anapata mapokezi makubwa kwa mashabiki wake  kila anapotoa kazi mpya kuwa ni kazi nzuri ambazo amekuwa akizifanya.

Akizungumza Juma tatu hii ndani ya ‘Planet Bongo’ya East Africa Radio,Ali Kiba  alifunguka kuwa kazi nzuri ndio zinazomfanya awe anapata mapokeo makubwa sana kutoka kwa mashabiki wa muziki wake na wala si kitu kingine kama ambavyo imezoeleka kwa baadhi ya wasanii walio wengi kutumia ‘kiki’ kwa ajili ya kupata mapokeo makubwa ya kazi zao.

‘’Mi nafanya kazi nzuri ndio mana mapokeo ya kazi zangu kwa mashabiki yanakuwa makubwa na sio kitu kingine ninacho kifanya katika kazi yangu zaidi ya kufanya kazi nzuri’’alisema Ali kiba.

Ali Kiba ameanza rasmi kufanya ziara katika vyombo mbali mbali vya habari kwa ajiri ya kuutambulisha wimbo wake mpya ‘Seduce Me’ ambao unatamba sana kwa sasa huku akiongozana na mtayarishaji wa kazi hiyo ‘Man Walter’ kutoka katika studio za Combination Sound

Wanawake Wote Mkiwa Kama Huyu Wote Mtaolewa: Yeye Kwake Mwanaume ni Malighafi

$
0
0
Wanawake Wote Mkiwa Kama Huyu Wote Mtaolewa: Yeye Kwake Mwanaume ni Malighafi
Jamani....

Nikiwa safari kuelekea Nairobi nilifanikiwa kuonana na mama mmoja Mchaga aliyefanikiwa sana. Ana hoteli Arusha, Moshi na pia ana export kahawa.

Nilijiuliza sana huyu mama amewezaje?
Ikabidi nianze kumchimba.

Aliponiambia wanaume ni Malighafi, nilishtuka sana. Nikaomba anidadavulie ....

G: Unasemaje ? Wanaume ni malighafi? Sikuelewi? Una maana gani?

M: Usinielewe vibaya, kwanza inabidi ujue maana ya malighafi. Nadhani unajua malighafi ni nini. Malighafi ni bidhaa inayohitaji kuongezewa thamani ili upate faida zaidi. Au unahitaji kuisindika kabisa ili iwe na thamani kwa faida yako.
Mimi kama mwanamke kwangu mwanaume ni malighafi inayotakiwa kuongezewa thamani kwa faida yangu.

G: Sijakuelewa kabisa mama.

M: Sisi wanawake tuna nguvu isiyo kawaida. Mungu akikupa mwanaume, ni kama malighafi ...unatakiwa kuongeza thamani, kumtengeneza unavyotaka kisha unamtumia kuwa unavyotaka. Mwanamke anaweza kumwamsha mwanaume aliyelala na kumfanya kuwa Rais, au mwanamuziki mkubwa halafu anaweza kumtumia kuwa anavyotaka. Wanawake wa siku hizi, wakipewa mwanaume wanataka awe amekamilika yaani finished product ili wamtumie. Huo ni ujinga. Wanawake tumeumbwa kuhamasisha. Tumeumbwa kumpandisha mwanaume. Mwanaume ni kichwa lakini kwenye familia mwanamke ni moyo.

G: Bado sijakupata kabisa.

M: Ngoja nikupe mfano. Mume wangu mimi alikuwa mwanafunzi wa chuo nilipokutana naye, mlevi na asiyejielewa kabisa. Lakini kuna kitu cha tofauti nilichogundua...alikuwa na akili. Kwangu ilikuwa ni malighafi yenye utajiri. Nikapiga mahesabu yangu, nikaingia kwenye mahusiano. Nikampa anachokitaka akapagawa. Kisha nikashika usukani. Nikatafuta njia akaacha pombe, akawa msomaji sana mpaka akafaulu chuo kikuu. Amemaliza uinjinia, nikampelekesha akanioa. Ninamjua wapi pa kumgusa. Alipomaliza chuo, nikamwambia sitaki awe mwajiriwa akagoma. Uoga. Nikamwacha, mshahara ulipoanza kuingia nilishika mimi .... Nikimpa anatumia pombe. Nikaanza kuchukua akiba yeye bila kujua, nikanunua mashamba, viwanja, nikaanzisha mgahawa. Nikamwita kama mgeni rasmi kuja kuzindua. Nikampeleka kwenye mashamba niliyonunua. Akapagawa. Nikahamisha akili yake yote, kwangu.
Tukaanza kushirikiana pamoja mpaka tukasimamisha hoteli. Mume wangu alikuwa hapendi biashara lakini baada ya kumbadili akapenda biashara kunizidi. Unajua nini kilitokea. Aliacha kazi na kuweka nguvu kwenye hoteli ndogo, tukafanikiwa mpaka hoteli kubwa ikajengwa.

Mashamba zaidi yakanunuliwa. Watoto wetu wanasimamia biashara zetu. Mume wangu ni mpambanaji hatari kwasasa. Unajua kwanini? Kwangu alikuwa ni malighafi, nikaamua kuongeza thamani.

G: Aisee!! Eeh?

M:Wanawake wa siku hizi wanatafuta wanaume walioongezewa thamani, ili wawatumie. Ukiona mwanaume yupo juu fahamu kuna starring nyuma ya pazia aliyesababisha. Mwishoni wanatumika wao kama vyombo vya kujistarehesha na kutupwa. Mwanamke unatakiwa kuwa na akili mara nne ya mwanaume, na usijivune kama una akili. Ukikuta mwanaume ana akili na unajua unaweza kumtengeneza chukua na ongeza thamani.

Ukichukua kilichoongezwa utapigwa tu. Utaachwa. Wewe unayesubiri mwanaume wako atengenezwe na wengine ili ule vya dezo. Ukitendwa, ukitupwa na kuchakazwa, usilie. Ongeza thamani ya malighafi yako.

Mfano kama mimi mchaga nikiolewa na mwanaume ndani ya miaka mitano hamjajenga, asihukumiwe mwanaume. Mwanamke ndiyo kimeo. Kama ukishindwa kumbadili mwanaume awe unavyotaka either hujapendwa, au wewe ni mvivu mpenda dezo, au hujui nguvu ya mwanamke kwa mwanaume au mwizi au mbinafsi au umejisahau kuwa ndoa ni ujasiriamali kama ujasiriamali mwingine.

Mwanamke ni msababishaji, uliza matajiri wakubwa duniani. Uliza watu wakubwa maarufu, uliza akina Napoleon, uliza akina Obama, uliza akina Albert, uliza utajua....nyuma yao kuna nguvu inayosababisha mambo makubwa.

COPIED FROM SOMEWHERE..!

Street teache

Nini Tena Kimemsibu Mwanamuziki Hamorapa?....Nimezimiss Kiki zake

$
0
0
Nini Tena Kimemsibu Mwanamuziki Hamorapa?....Nimezimiss Kiki zake
Wakuu kwema?
Hivi huyu mmakonde aliyepata kiki kwa ishu za ajabu ajabu kama vile kukimbia bastola iliyonyoshwa kwa mh Nape na mengine mengi mbona kimya.
Amepotelea wap wakuu.
Anayejua ukimya wake atupe ubuyu kiaina basi.

Mbunge Msukuma Amjibu Tena Tundu Lisu Kuhusu Kauli yake ya Kuwataka Wanasheria Wagome

$
0
0
Siku moja baada ya Rais wa TLS na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kutoa wito kwa Mawakili wote ambao ni Wanachama wa chama hicho kususia shughuli za Mahakama, Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Msukuma amejitokeza na kumpinga.

Licha ya kusikitishwa na kitendo cha kuvamiwa na kulipuliwa kwa Ofisi za IMMMA Advocates, Msukuma amesema kitendo cha Chama cha Mawakili kutangaza mgomo ni kutowatendea haki wateja wao kwa siku zote watakazoamua kususia shughuli za Mahakama.

”Watanzania kwa pamoja tunalaani kitendo kilichofanywa kwenye Ofisi za IMMMA Advocates kwa sababu ni kitendo cha kinyama na kihalifu. Tunamuomba IGP Sirro afanye juu chini kuhakikisha watu hawa wanakamatwa.

“Nilishtushwa sana na matamko yaliyotolewa na Rais wa TLS, Tundu Lissu jana kwamba anatangaza mgomo wa Wanasheria kuanzia kesho na keshokutwa. Najiuliza kama Tundu Lissu anatangaza mgomo wa Wanasheria, hiyo ndiyo hukumu ya kumpata mvamizi?

“Nadhani Wanasheria waisaidie Polisi kumgundua ni nani. Kama kuna taarifa Tundu Lissu mpaka anafikia kusema tukigoma atapatikana aliyefanya haya matendo, aisaidie Polisi waweze kumkamata haraka.” – Joseph Msukuma.

Watuhumiwa wa Kula Nyama za watu Waendelea Kushikiliwa

$
0
0
Wanaume wanne ambao wanatuhumiwa kuwala watu nchini Afrika Kusini wametupilia mbali ombi lao la kutaka kuachiliwa kwa dhamana.

Wanne hao walikuwa wamefika kortini kwa kikao cha kuomba dhamana lakini hata kabla ya ombi lao kusikilizwa katika mahakama ya Estcourt.

Kesi yao itatajwa tena mwishoni mwa mwezi ujao.

Mwandishi wa BBC Nomsa Maseko aliyekuwepo mahakamani anasema mmoja wao alikuwa anatokwa na machozi.

Nje ya ukumbi wa mahakama, makundi ya watu waliandamana kupinga kuachiliwa huru kwa washukiwa hao kwa dhamana.

Miongoni mwa walioshtakiwa ni mganga wa kitamaduni ambaye anatuhumiwa kuwafanya wateja wake wale nyama ya binadamu kwa ahadi kwamba ingewasaidia kutajirika na kufanikiwa maishani.

Walikamatwa baada ya mmoja wao kudaiwa kufika katika kituo cha polisi na kuambia maafisa wa polisi kwamba alikuwa "amechoka" kula nyama ya binadamu.

Alipohojiwa zaidi, mwanamume huyo alichomoa mguu na mkono wa binadamu.

Polisi kisha waliandamana na mwanamume huyo hadi kwenye nyumba moja

KwaZulu-Natal ambako viungo zaidi vya binadamu vilipatikana.

Baadhi ya walioandamana nje ya mahakama leo walikuwa na mabango na walikuwa wakiimba kwa Kizulu: "Tunataka kuwaona wauaji."

Wengine walikuwa wakiimba: "Sisi sio Hungry Lion, na wala sio Nando's. Sisi ni binadamu na hatufai kuliwa."

Hungry Lion na Nando's ni maduka mawili maarufu kwa uuzaji wa chakula nchini humo.

Kutana na Mtatibu Wanyota za Binadamu Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka Comoro

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU WANYOYA ZA BINADAMU DUNIANI KOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO

KWA SASA YUPO TANZANIA MAALIM FADHILI RASHIDI ANA IWEZO WAKUJUWA JAMBOLAKO NAKULI TATUWA KWAMUDA MFUPI

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE

MAALIM FADHILI RASHIDI NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA MIGUU KUWAKA MOTO

KISUKARI VIDONDA VYATUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI PUMU ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIE POTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM ANATOWA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI YEYOTE

NAKUMILIKI MALIZA MAJINI KWAYULE ANAE HITAJI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZA KIUME ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASA (24)

ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YAMVUTO WABISHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE

KUSAFISHA NYOTA NAKUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHAKUTESEKA NJOO UWONE MIUJIZA YA MAALIM FADHILI RASHIDI CALLING+255719362806/ +255763276239

KWA WHATSAPP IMO +255785786436

MANGE "Mwisho wa Ubaya Aibu...Diamond Alitaka Kumwaribia Ali Kiba Lakini........"

$
0
0

Mrembo Mange Kimambi Amefunguka Makubwa Baada ya Kumaliza Zoezi alilolianzisha Instagram la kupokea Video za watu mbali mbali na kuzipost huku wakicheza wimbo mpya wa Ali Kiba.....Amefunguka Haya Hapa Chini:

Mangekimambi_ - Hey guys, tumefikia mwisho wa #SeduceMeChallenge
.Hongera kwetu sisi wooooote. Credit should go to you Ali Kiba's fans kwa kukinukisha. Bila nyinyi kunitumia videos nisingekuwa na material za kuposti...... Kazi yangu ilikuwa ndogo, kazi kubwa ilikuwa kujirekodi those amazing creative videos....

I'm bummed kuwa nimebaki na maelfu ya video ambazo sikuweza kuposti! Haki siku nyingine itabidi nininue iphone 7 plus kabla ya issue Kama hiii, maana nimepata shida ya storage Jamani. Mpaka nilikiwa nadata .... .

Nawaomba msahama wooote ambao sikuposti video zenu na sikujibu malalamiko yenu whatsapp, sikuweza kuwajibu woote mmoja mmoja . Naomba mjue kuwa wooote mlituma video nzuri Ila sikuweza kuposti zoooote!!!

Lastly niseme kuwa kilichotokea the last few days kiwe Funzo kwa wanamuziki wetu, mashabiki wanataka mziki tu sio maskendo na makiki yasio na mpango. Kiba kawaonyesha kuwa kufanikiwa sio lazma uwe na wanawake 20 au uwe una tukana wanawake zako mitandaoni, au uwe unatukana mashabiki wasiokukubali au uwe Namameneja wapenda drama. Hatujawahi kumsikia @sevenmosha anachamba watu. .

Pia tumejifunza kuwa roho Mbaya hailipiiiiiii, mwisho wa ubaya huwa ni aibu.... Haikuwa na haja ya wao kutaka kumwaribia mwenzao. That's was so unfair Jamani! Mimi sikuwa na mpango wa kufanya promo kwa Kiba ila roho iliniuma sana 😭Haki nilipata shock, sikuamini vijana wadogo vile wanaweza kuwa wanyama kiasi kile, sikujua wanamchukia Kiba kiasi kile. Nilikuwaga nachukulia beef lao kama utani flani hivi, I never took their beef seriously ila juzi ndo nikajua those boys are cruel.Nilipoona Kiba anachezewa rafu bila sababu nikasema I have to do something,?fortunately na nyinyi pia mlikuwa tayari kuchukua hatua. Kwa kweli tumewanyoooooosha yani naamini kabisa wamejifunza na hawatorudia tena..... Tuwasamehe bure hawajui walitendalo!! .

Congrats Kiba, Sasa watanzania tunasubiria kuvote kwenye Awards... Yaaaaaas!

Jerry Muro Ageukia Siasa...Amchana Chana Vibaya Rais wa TLS Tundu Lissu

$
0
0
Tundu Lissu, TUNDUNI
Na Jerry C. Muro

Nianze kwa Kutoa pole kwa jumuiya nzima ya wanasheria nchini, pole yangu sio ya tukio la IMMA advocates, Bali pole yangu ni ya kuchagua Rais wa TLS Chama Chenu 'MAHIRI' cha wanasheria Tanganyika - TLS Ndugu Tundu Lissu ambae AMEDHIHIRISHA kuwa ameanza Rasmi Safari ya Kuizika TLS, kupitia taarifa yake kwa vyombo vya Habari kuhusiana na Tukio la IMMA advocates.
Nianze kwa kuweka msingi wa HOJA yangu kuwa sifurahishwi na kilichotokea kwenye IMMA advocates, ila pia SIFURAHISHWI zaidi na "AKILI NDOGO" za Rais wenu katika hatua za AWALI za kushughulikia suala hili.

Mimi ni Profesional communicator kama mwandishi wa Habari, na Nyinyi wanasheria ni Profesional kwenye Sheria, ukisoma na Kusikiliza kwa umakini TAARIFA ya Mhe Rais wa TLS utagundua makosa makubwa sana ya KIUFUNDI ambayo yanaifanya taarifa nzima kuwa kama taarifa ya Mfalme "****" na kwa sisi MAFUNDI wa taarifa tunasema taarifa ikikosewa katika UANDAAJI na UWASILISHWAJI inakuwa imekosa MASHIKO, na hivyo taarifa nzima kuwa BATILI.

KWANINI BATILI
1. Taarifa iliyowasilishwa na Rais wa TLS tayari kwa kiasi kikubwaa ilishatolewa na Chama cha wananchi CUF #teammaalim, ukisoma taarifa ya cuf ambayo ilitoka siku moja kabla ya hii ya Rais utaona nachosema, ila hii ya Rais imewaka mbwembwe ya Vifungu Vifungu vingi vya SHERIA tu, ila taarifa zote zimeonyesha kuwa IMMA advocate ni WABIA katika kazi mana cuf inatetewa na IMMA advocate na Rais Lissu anatetewa na IMMA advocate hivyo wote WANAOMBELEZA DHORUBA YA MMBIA WAO., japo TLS ni Chama na Lissu ni Rais, na ni mteja wa IMMA katika hoja hii ya kwanza nimalizie kwa kusema tu Hoi taarifa ni BATILI kwa kuwa Imekuwa taarifa ya KISIASA na Imetolewa na wanasiasa wa vyama viwili tofauti, japo Mmoja ni Rais wa TLS, hapa utaona sasa Hatari ya kuwa na Rais wa TLS ambae ni mwanasiasa.

2. Taarifa ni BATILI kwa kuwa imeanza kwanza kwa KUHUKUMU kuwa Ofisi za IMMA advocate zimepigwa BOMU na POLISI, japo hizi ni taarifa za AWALI lakini kwa maoni yangu TAARIFA haikupaswa kujielekeza kwenye kazi za mamlaka nyingine, mana kama mmeshajua waliolipua ni POLISI basi hamkuitaji kutoa taarifa Bali kufuata SHERIA kuwashtaki POLISI.
Katika hoja hii MWENDELEZO wake inasema wanavitaka vyombo husika wakiwemo "WATUHUMIWA" Polisi kufanya uchunguzi, mbele zaidi tena wanataka kukutana na "MTUHUMIWA" boss wao IGP, hivi hii ni SAWA WANASHERIA, mnataka kukutana kufanya nini tena na IGP au mkurugenzi wa usalama wa taifa ambae majuzi juzi hapa wakati wa Sakata la Bombadier Rais "WENU "alishema kuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa" ANAMFUATILIA FUATILIA "sasa iweje Leo aombe mwenyewe kukutana na" MTESI " wake, NDIO MANA NASEMA HAPA KUNA TATIZO YA HIKI CHAMA KUONGOZWA NA MWANASIASA, labda niwakumbushe tu hawa wanasiasa enzi ya Lowassa Walisema" mwizi" alipokwenda kwao wakamuita mfalme wa AMANI hawa ndio wana SIASA.

3. Taarifa ni BATILI, kwa sababu taarifa inataka WANASHERIA kugoma jumanne na jumatano, huu ni MGOMO ambao katika taarifa yao wanaomba ufanywe UCHUNGUZI, lakini pia kwenye taarifa yao wanaomba kuonana na kaimu Jaji Mkuu ambae mmekuja kusema tena hapo Chini ASUSIWE hamtaki kwenda kwenye mahakama anazoziongoza, JAMANI mnajua mnachofanya? Hii ni sawa na KUJITEKENYA MWENYEWE KISHA UKACHEKA MWENYEWE. nadhani Wasomi wana Sheria tukubaliane katika jambo moja MGOMO au KUONANA na "WATESI "wenu huwezi kushika mambo mawili kwa wakati Mmoja lazima MOJA litaponyoka.

4. Hii taarifa ni BATILI, kwa sababu imemtangaza MGOMO pasipo kusema ADUI ni Nani, hivi Hebu tuambieni mnagoma mkilenga KUMUUMIZA Nani? Kuwaumiza wateja wenu walioko MAGEREZANI au? Hivi nyinyi hii kazi ya UANASHERIA ni ya kujitolea katika kazi zenu zote? Hivi hakuna pesa mmechukua za wateja wenu ambazo mnapaswa kuzifanyia kazi, au TUSEME na nyinyi "WEZI" mnachukua hela za wateja wenu kisha mnagoma?
Hebu mtuambie Nani ADUI YENU basi.

MASWALI MAGUMU ZAIDI TLS.

1. Hivi Mbona walipouwawa *WANASHERIA* na *MAWAKILI* nguli nchini, tena waliowasomesha na kuwafundisha *HAMKUGOMA KUSHINIKIZA HAKI ITENDEKE KAMA HIVI LEO,* au mmesahau Vifo vya *"UTATA"* vya Mawakili Marehemu Kapinga, Marehemu Mvungi, Marehemu Mwaikusa? Kwa kuwa mnasahau ngoja tuwakumbushe tu *HAKUNA NAMNA*, Leo hao wazee wamekuwa *"LIABILITY"* kwenu halafu cuf, Lissu, acaccia zimekuwa *"ASSET"*kwenu?

2. Hivi tangu lini mmeanza kushirikiana press releases na vyama vya siasa mfano cuf?

3. Hivi TLS kimekuwa Chama cha Siasa, au kwakuwa Rais wenu ni mwanasiasa?

4. Mnawezaje kuitenganisha TLS na siasa?

5. Katika Sheria kuna neno linaitwa *"INNUENDO"*hivi mnajua maana ya hilo neno katika Sakata hili la IMMA advocate?

6. Hivi mnajua IMMA advocate ni kampuni "inayotajwa" KUCHOTA mabilioni ya fedha za EPA kupitia kampuni ya DEEP GREEN kiasi cha *BIlioni 8* zilichotwa, mnajua hilo? kama hamjui nendeni Brella kisha mkasome anuani za Kampuni ya *DEEP GREEN,* kisha mtangaze *MGOMO.*

7. Hivi mnajua huyu Rais wenu Lissu akiwa Bungeni mwaka 2012 Aliitaja kampuni ya IMMA advocate kuwa ilizitetea kampuni za TanGold na Deep green microfinances *KUCHOTA* pesa za EPA, halafu Leo HAWAHAWA imma advocate ndio wanaomtetea Lissu katika kesi zake?

Hivi mnajua maana ya vita ya *KIUCHUMI,* adui yako anaweza kutumia *MKEO, WATOTO* na hata Ndugu zako ili mradi *APATE USHINDI.*

Mwisho, Nawapenda sana *WANASHERIA,* mana najua mchango wao katika taifa la Tanzania, nawathamini sana Wanasheria wamaotanguliza *UZALENDO* kwa taifa Lao pamoja na changamoto tunazopitia kama taifa Changa, Nawapenda Wanasheria wanaosem *KWELI* kwa maslahi ya taifa Lao na Sio *MATUMBO* yao.

Sasa Sikilizeni, *AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO.LEO TUNDU, TUNDUNI.*

Wasalamu
*Jerry C. Muro*
*28/08 /2017*

Zitto Kabwe: Nikiteuliwa na Rais Magufuli Kushika Nafasi yoyote Serikalini, Nitakataa

$
0
0
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema hatakubali kuteuliwa na Rais John Magufuli kushika nafasi yoyote, kwa sababu kukubali kitamnyima fursa ya kujenga Chama chake ili kiwe tayari kushinda uchaguzi na kushika dola.

Mbunge huyo wa Kigoma Mjini, ambaye chama chake kimeshatoa viongozi wawili walioteuliwa kushika nafasi za juu Serikalini, amesema ikitokea Rais Magufuli akamteua, atamshukuru na kukataa uteuzi huo.

Zitto alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi jijini Mwanza mwishoni mwa wiki, alipokuwa akijibu swali kuhusu uteuzi baada ya Rais Magufuli kumteua mwenyekiti wa ACT-Wazalendo "Anna Mghwira kuwa mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, na mshauri wa chama hicho, Profesa Kitila Mkumbo kuwa katibu mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Mghwira alivuliwa wadhifa wake, wakati Profesa Kitila alijivua nafasi zote katika chama.

Lakini Zitto hafikirii kufuata mkondo huo.

"Sitakubali uteuzi kwa sababu jukumu langu na viongozi wengine wa ACT Wazalendo ni kukijenga chama ili kipate ushawishi na kuungwa mkono na umma na hatimaye kushika dola", alisema Zitto. 

"Kukubali uteuzi utakaoniondoa na kuniweka kando kwenye jukumu na malengo hayo ni kufifisha matumaini ya maelfu ya wana-ACT Wazalendo".

Kauli hiyo inakuja katikati ya maneno na ubashiri kuwa Zitto, ambaye ana shahada ya uzamili katika masuala ya sheria na biashara, anaweza kuteuliwa kujaza nafasi iliyo wazi kwa muda mrefu baada ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wa Profesa Sospeter Muhongo ya Waziri wa Nishati na Madini.

Akijibu swali kwanini chama chake kiliridhia uteuzi wa Profesa Mkumbo na Mghwira, Zitto alikuwa na sababu tofauti.

"Kwanza, kabla ya uteuzi na hata baada ya uteuzi Profesa Mkumbo ni mtumishi wa umma ndiyo maana uteuzi wake haukushtua", alisema Zitto. 

"Mama Mghwira alikuwa ni mwanasiasa kwa nafasi yake ya uenyekiti wa Taifa, ndiyo maana tulimwondoa ili kumpa fursa ya kumtumikia Serikali. 

Chanzo: Mwananchi

Tshirt na Jinsi ya Manji Yaibua Mengine

$
0
0
Tshirt na Jinsi ya Manji Yaibua Mengine
Huku akitia huruma, baadhi ya wananchi jijini hapa wameibua gumzo kuhusiana na nguo anazovaa mfanyabiashara maarufu, Yusufu Manji ambaye ana kesi mbili zinazomkabili.

Manji ambaye alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Februari 17, mwaka huu amekuwa akikabiliwa na kesi mbili, moja ikihusu uhujumu uchumi na ya pili ni madai ya matumizi ya dawa za kulevya.

Baadhi ya wananchi wamekuwa wakidai kwamba wamekuwa wakimshuhudia Manji akija mahakamani akiwa amevaa tisheti ya rangi nyeusi kwa zaidi ya mara kumi, jambo ambalo limeleta gumzo kwa kuwa wanaamini ana nguo nyingi.

“Hatujui sababu, huyu bwana ni tajiri sana lakini kila akifika mahakamani anavaa tisheti nyeusi ileile, kwa nini?” alihoji mwananchi mmoja. Wapo waliomuonea huruma na kudai kwamba inawezekana anafanyiwa figisufigisu kwa kutoruhusiwa kupelekewa nguo na wengine wanadai kwamba inawezekana ameamua mwenyewe awe hivyo kama alivyoamua kutonyoa ndevu.

UWAZI liliamua kumtafuta mtaalamu wa utabiri (Astrologer), Maalim Hassan Yahya Hussein na kumuuliza kuhusu gumzo hilo na amesema nguo hiyo nyeusi anayovaa mfanyabishara huyo ina maana kubwa.

Akizungumza na gazeti hili, Maalim Hussein alisema nguo nyeusi kinyota ina maana nyingi kama vile kuonesha huzuni, msiba, au kupatwa na mkosi. Maalim Hassan aliongeza kuwa inaweza kuwa ni kwa sababu hizo alizozitaja kwamba mshitakiwa anajua kwamba huu ni wakati wake wa huzuni.

“Ni kwamba Manji anajua kuwa yupo shimoni, hivyo anatakiwa afanye kila linalowezekana ili kujinasua, na ndiyo maana ameweka mawakili ili wamnasue kule shimoni,” alisema Maalim Hassan.
Akifafanua zaidi mtabiri huyo alisema nguo nyeusi huonesha pia kwamba ni siku ya mikosi ambayo kinyota ni Jumamosi.

Hivyo mtu kuvaa nguo nyeusi iwe ni shati, suruali, jinzi au soksi, inamaanisha ana huzuni na ndiyo maana watu wengine wakifiwa huvaa nguo za rangi hiyo na kwa wale wenye imani nyingine huona kuwa nguo za rangi hiyo huashiria mkosi, hivyo huwa hawazivai hata kama ni siku ya msiba,” alisema.

 “Kwa hiyo Manji kuvaa tisheti nyeusi au viatu vyeusi na soksi nyeusi au jinzi nyeusi siyo kwamba hana nguo au viatu vya kubadilisha lakini haina maana kwake kuvaa makoti makubwa ya rangi nyingine kwa sababu ana matatizo, ana huzuni na ni kama yupo shimoni kinyota,” alifafanua mnajimu huyo. Akaongeza:

“Amini kwamba Manji ataendelea kuvaa hivyo mpaka kesi zake zitakapokwisha na licha ya nguo nyeusi hata ndevu zake nyeusi kaziachia, hazinyoi, sababu ni hiyohiyo siyo kwamba hana fedha za kununua wembe wa kunyolea.” Manji hivi sasa ana kesi mbili mahakamani, moja ni tuhuma ya kuhujumu uchumi na ya pili inahusu madai ya kutumia madawa ya kulevya aina ya heroine.

Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha ambaye anasikiliza kesi ya madawa, wiki iliyopita alisema baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi watatu wa upande wa mashtaka
ameridhika kuwa mshtakiwa huyo ana kesi ya kujibu hivyo ana haki ya kujitetea na kuita mashahidi. Wakili wa Manji, Hudson Ndusyepo alidai kuwa mteja wake atajitetea kwa njia ya kiapo na wana mashahidi 15.

Pia aliomba hati ya wito (samansi) kwa ajili ya kuwaita mashahidi hao. Kesi imeahirishwa hadi kesho Agosti, 30 na 31,2017 ambapo Manji ametakiwa aanze kujitetea. Awali upande wa mashtaka ulisema ungeita mashahidi wasiozidi 10 kutoa ushahidi lakini watatu ndiyo waliotoa ushahidi kwenye kesi hiyo.

Manji alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Februari 16, 2017 akidaiwa kuwa kati ya Februari 6 na 9, 2017 katika eneo la Upanga Sea View Ilala alitumia dawa za kulevya aina ya heroine.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, Manji alikana kuwa siyo kweli na kwenye kesi hiyo anawakilishwa na Mawakili Alex Mgongolwa, Hudson Ndusyepo na Mosses Kimaro ambapo alipata dhamana baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa ambaye alisaini bondi ya Sh. milioni 10.

Hata hivyo, mfanyabiashara huyo, licha ya kupata dhamana katika kesi ya kwanza, yupo rumande kutokana na kesi ya uhujumu uchumi ambapo anadaiwa alikutwa na vitambaa vya jeshi la wananchi na mihuri ya makamanda wa jeshi hilo la lile la kujenga taifa.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilipoketi Agosti 25, mwaka huu iliutaka upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo ili matokeo ya kesi hiyo yajulikane mapema. Rai hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya Wakili wa Serikali, Wankyo Simon kueleza upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na wataeleza hatua ulipofikia katika tarehe itakayopangwa tena.
Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba aliutaka upande wa mashtaka kuhakikisha wanajitahidi kukamilisha upelelezi ili matokeo yake yajulikane mapema ambapo aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 31, 2017.

Mbali ya Manji, washtakiwa wengine ni Deogratius Kisinda, Abdallah Sangey na Thobias Fwere ambao wanakabiliwa na mashtaka saba chini ya sheria ya Uhujumu Uchumi na Usalama wa Taifa kwa kukutwa na vitambaa vinavyotengeneza sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania vyenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 200 na mihuri.



Ali Kiba: Simba Simuogopi Hata Kidogo

$
0
0
Ali Kiba: Simba Simuogopi Hata Kidogo
Msanii Alikiba ambaye ni shabiki  wa klabu ya Yanga, amesema haiogopi wala kuihofia timu ya Simba hata kama wameanza vizuri kwa kugawa kichapo katika mechi za awali Ligi Kuu huku akidai mpira unadunda na muda wowote Simba itapotea.

Alikiba ameeleza hayo muda mchache alipomaliza mahojiano kwenye kipindi cha Planet Bongo kutoka East Africa Radio akiwa ameongozana na mtayarishaji wake wa wimbo mpya wa 'seduce me', Man Water ambao kwa sasa unazidi kuwa gumzo katika mtandao wa 'Youtube' kwa kufika watazamaji Milioni mbili.

"Simba hainitishi, Simba anafungiwa bandani ndiyo nimuogope mimi ?, kama kawapiga 7-0 Ruvu Shooting ni vijana wengine sisi hatuna shida japo ametufunga katika mechi ya watani wa jadi lakini hiyo ni kawaida na ndiyo maana ukisikia mpira unadunda maana yake ni kwamba mchezo unabadilika", alisema Alikiba.
Pamoja na hayo Alikiba aliweza pia kuzungumzia sakata la kuondoka kwa mchezaji ambaye alikuwa anampenda kwa umahiri wa kulisakata kabumbu  ambaye ni Haruna Niyonzima katika timu yao na kwenda Simba.

"Sidhani kwa kuondoka kwa mchezaji Haruna Ninyozima katika klabu yetu kama itaweza kutuletea madhara yoyote yale japo alikuwa ana kiwango kikubwa sana na ninamkubali, lakini ninaimani tumepata vyuma vingine vyenye nguvu kama vilivyoondoka ndiyo uzuri wa Yanga wana 'replace', ukibandua tu tunabandika japokuwa klabu imeingiza mpunga hatuna shida", alisema Alikiba.
"Ninachowaombea Yanga wakaze kwa kuwa naamini wana uwezo mkubwa sana na wachezaji wazuri sidhani kama kuna mapungufu yoyote yakawadhohofisha wachezaji au wana Yanga wakarudi nyuma. Sisi 'always' daima mbele hicho ndicho najua mimi", alisisitiza Alikiba.

Kwa upande mwingine, Alikiba amesema haoni hatari yoyote kwa klabu yake kutoa sare ya bao 1-1 na timu ya Lipuli FC mchezo uliyopigwa Agosti 26 mwaka huu katika mechi za ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuwa bado Ligi haijanza kushika kasi huku akijipa matumaini kuwa timu yake itakuja kufanya maajabu katika mechi zijazo

Korea Kaskazini Yaijaribu Japan

$
0
0
Korea Kaskazini Yaijaribu Japan
Korea kaskazini imerusha makombora yake ambayo yalipita Japan kabla ya kudondokea baharini.
Makombora hayo yalisafiri kuelekea mashariki karibu kilomita elfu moja juu ya kisiwa cha Japan cha Hokkaido.

Tukio hilo limechochea tahadhari ya hatari ambayo watu walielekezwa kujificha katika maeneo yaliyo chini ya ardhi ama kwenye majengo yaliyo imara.
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amesema urushwaji huo wa makombora ambao haujawahi kutokea , umeleta kitisho kikubwa kwa taifa lake.Hakuna juhudi zilizofanywa na Japan kulitengua kombora hilo lakini ilitoa onyo la kiusalama ikiwaambia raia wake katika eneo la Hokkaido kujificha chini ya majumba yaliojengwa ardhini.

Wanajeshi wa Marekani na Japan wanafanya zoezi la pamoja katika eneo hilo la Hokkado, rais wa Korea Kusini Moon Jae-in aliagiza uwezo wa utumiaji wa nguvu ili kujibu shambulio hilo.
Ndege nne za Korea Kusini zilifanya zoezi la kurusha makombora siku ya Tuesday.
Bwana Abe alisema kuwa amezungumza na rais wa Marekani Donald Trump na kwamba wote wamekubaliana kuiongezea shinikizo Korea Kaskazini.

Katika mfululizo wa majaribio yake ya makombora ya hivi karibuni Korea kaskazini haijawahi kurusha makombora yaliyopita juu ya ardhi ya nchi hiyo, hivyo tukio hili la sasa limeleta wasiwasi mkubwa.

Katika siku za hivi karibuni Pyongyang ilijaribu kombora lake lililopata mafanikio kutokana na uwezo wake wa kuweza kuifikia Marekani na kuonyoa kuwa inasimamia mipango yake ya kushambulia kwa makombora eneo la Marekani la Guam, kilomita elfu mbiili kusini mashariki mwa Japan.

Jeshi la Polisi Lawashikiria Walimu wa Wawili kwa Kufanya Mapenzi na Wanafunzi

$
0
0
Jeshi la Polisi Lawashikiria Walimu wa Wawili kwa Kufanya Mapenzi na Wanafunzi
Walimu wawili waliokuwa wakifanya mazoezi kwa vitendo katika shule ya sekondari ya Kikala wilayani Lushoto mkoani Tanga wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kufanya mapenzi na wanafunzi wawili wa kidato cha tatu shuleni hapo.

Akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Lushoto ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, January Lugangika amesema waalimu wa wanafunzi hao wamekikuka maadili ya ualimu na kwamba watachukuliwa hatua zaidi huku akiongeza kuwa tabia hizo zinaleta kichefu chefu kwa jamii.

Aidha mwenyekiti huyo amedai kuwa ushahidi wa tukio hilo umethibitishwa na Daktari ambaye aliwafanyia vipimo na kuthibitisha ni kweli kitendo hicho kilifanyika
Kwa upande wa Afisa elimu wa sekondari Wilaya ya Lushoto Kassim Singato amesema endapo kutakuwa na masomo ya ziada ni lazima yafahamike muda yanapoisha ili wazazi waweze kufuatilia mwenendo wa watoto wao.

"Inabidi wazazi muwafatilie watoto wenu kwa kila hatua, mjue wanafanya nini shuleni na kama mzazi humfatilii anaweza kufanya mambo usiyoyajua na badala yake ukashtukia ana mimba ya miezi hata sita," alisema Singato.
Watuhumiwa wa tukio hilo ni mwalimu Fredriki Shebila na Saddat Mohamed
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images