Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104715 articles
Browse latest View live

Muda wa Kukutana na Daktari Vituo vya Afya Waimarika- Twaweza

$
0
0
Muda wa Kukutana na Daktari Vituo vya Afya Waimarika- Twaweza
Kuna dalili za kupungua muda wa wagonjwa kumuona daktari baada ya utafiti kuonyesha wale waliokuwa wakisubiri kwa zaidi ya saa moja, idadi yao imeshuka kwa asilimia tano ndani ya miaka mitatu iliyopita.

Utafiti mpya wa asasi ya kiraia ya Twaweza uliozinduliwa leo Agosti 30 unabainisha idadi ya wananchi wanaosubiri kumuona daktari kwa zaidi ya saa moja imeshuka kutoka asilimia 25 mwaka 2014 hadi asilimia 20 mwaka huu.

Hii ina maana kuwa, kwa sasa ni mtu mmoja kati ya watu watano wanaoenda kituo cha afya ndio husubiri zaidi ya saa moja kupata huduma kulinganisha na mtu mmoja kati ya wanne miaka mitatu iliyopita.

“Upo ushahidi unaoonyesha kuwa, muda wa kusubiri huduma katika vituo vya afya umepungua kidogo kulinganisha na miaka ya nyuma ambayo wananchi saba kati ya 10 (asilimia 70) walisubiri chini ya saa moja mwaka 2014,” inasomeka sehemu ya ripoti ya utafiti huo unaoitwa, “Afya kwanza! Wasemavyo wananchi kuhusu huduma za afya. Muhtasari unatokana na takwimu za Sauti za Wananchi”.

Mbali na mafanikio hayo, utafiti huo wa toleo la 19 la Sauti za Wananchi unabainisha kuwa, wananchi sita kati ya 10 (asilimia 61) wanapata huduma za afya katika vituo vya afya vya Serikali, kiwango ambacho kimesalia kama ilivyokuwa mwaka jana.

Mwaka 2014, idadi ya wananchi waliokuwa wakipata huduma za afya kwenye vituo vya umma ilikuwa ni takriban watano kwa kila 10 sawa na asilimia 45.

Utafiti huo uliohusisha sampuli ya wananchi 1,801 unaeleza kuwa, ni asilimia 16 hadi 20 ya waliohojiwa huenda hupata matibabu kwenye vituo vinavyomilikiwa na watu binafsi, makanisa au mashirika yasiyo ya kiserikali.

“Idadi hii haijabadilika sana kati ya mwaka 2014 na 2017,” inaeleza sehemu ya ripoti hiyo iliyofanywa kwa njia ya simu kati ya Mei 11 hadi 25 mwaka huu.


Bob Junior Azidi Kuchoshwa Atupa Dongo Jingine

$
0
0
Bob Junior Azidi Kuchoshwa  Atupa Dongo Jingine
Bob ambaye pia ni producer wa mziki katika studio za Sharobaro rekodi, amekuwa akifululiza kurusha makombola yake ambayo yanaashiria kumlenga mtu fulani kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo leo hii ameandika;

“HAAAHAHA!!! NGUVU YA MUNGU HAIZUILIKI USHAJIJUA KAMA KADOGO DOGO EEH…. NA BADOO KWA HAYA MAMBO YAKO YAKITOTO KAMA USEMAVYO BUT NAENDELEA KUFANYA AMBAYO NIMEUMBWA KUFANYA KAMA MUNGU ALINITUMA KWA WEMA KWAKO BASI ATANILIPA NINACHO STAHILI MAANA UMEZIDI KEJELI NA DHARAU SASA ANAE KUHUKUMU NDIO UTAKAE PAMBANA NA WEWE MR.KADOGO DOGO 🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂😂 #GIVEME,

Hata hivyo bado haijabaanika kuwa mkali huyo ana mlenga nani ama anatafuta attention kwa watu ili aweze kuachia ngoma yake mpya hivi karibuni.


Uingereza Yaitaka China Kuzungumza na Korea Kaskazini

$
0
0
Uingereza Yaitaka China Kuzungumza na Korea Kaskazini
Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May amesema kuwa Uingereza itaimarisha juhudi zake kukabiliana na ukatili wa Korea Kaskazini wa kufanyia majaribio makombora yake , lakini akaitaka China kuimarisha ushawishi wake dhidi Pyongyang.
Akizungumza wakati alipokuwa akielekea nchini Japan kwa ziara, alilaumu Korea Kaskazini kwa vitendo vya uchokozi.

Ziara hiyo ya waziri mkuu pia inalenga kupigia debe biashara mbali na kuwahakikishia washirika wake kwamba hatua ya Uingereza kujiondoa katika muungano wa Ulaya haitaathiri chochote.Bi May amesisitiza kuwa majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini ni kinyume na sheria.
Alisema:Tutaongeza juhudi zetu na washirika wetu wa kimataifa kuishinikiza Korea Kaskazini kusitisha vitendo hivyo vinavyokiuka sheria.

Amesema kuwa Uingereza imeshirikishwa katika mazungumzo ya kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini mbali na kutafuta mabadiliko ambayo China inaweza kufanya.
Amesema kuwa China ina jukumu kubwa huku akiitaka Beijing kufanya kila iwezalo kuishinikiza Korea Kaskazini.

Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe alitaja jaribio hilo la kombora la Kaskazani kama tishio lisilo la kawaida kwa taifa lake huku baraza la usalama la Umoja wa Mataifa likiishutumu Korea Kaskazini kwa pamoja.

Wakikutana usiku wa Jumanne mjini New York, baraza hilo lilitaja urushaji wa kombora hilo kama wa kikatili huku likitaka Korea Kaskazini kusitisha jaribio lolote la makombora yake.
Lakini Korea Kaskazini imetoa ishara ya kurusha makombora zaidi ,ikisema kuwa hatua yake ya kurusha kombora kupitia anga ya Japan ni mojwapo ya mipango yake ya kijeshi katika eneo la Pacific.

Mmiliki wa Facebook Billionea Mark Zurckerberg Apata Mtoto Mwingine

$
0
0
Mmiliki wa Facebook Billionea Mark Zurckerberg Apata Mtoto Mwingine
MKE wa Bilionea mwanzilishi na mmiliki wa mtandao maarufu duniani wa Facebook, Marc Zuckerberg ambaye ni daktari wa watoto nchini Marekani amejifungua mtoto wa kike juzi Jumatatu, Agosti 28, usiku.

Mtoto huyo ambaye ni wa pili kwa bilionea Zuckerberg na mkewe Priscilla Chan, amepewa jina la August.

Baada ya August kuzaliwa, Zuckerberg ameandika barua ya wazi kwa mtoto wao wa kwanza ambauye pia ni wa kike, Max aliyezaliwa mwaka 2015 akimuasa kucheza na mdogo wake.

 “Mimi na Priscilla tuna furaha sana kwa kumpata mtoto wetu August. Tumemuandikia barua  kuhusu ulimwengu tunaamini atakua na tunaamini hatakua haraka haraka” ameandika bilionea huyo katika ukurasa wake wa Facebook.


Huyu Hapa Staa wa Arsenali Aliyehama Timu Hiyo Leo

$
0
0
Huyu Hapa Staa wa Arsenali Aliyehama Timu Hiyo Leo
Wakati mashabiki wa Arsenal wakiendelea kujiuliza kuhusiana na hatma ya staa wao Alex Sanchez kama ataondoka au la, huku Chelsea wakiwa wameafikiana bei na Arsenal kuhusu kumsajili Alex Chamberlain kwa dau linalotajwa kufikia pound milioni 35.

Leo August 30 2017 beki wao Kieran Gibbs aliyecheza kwa mismu kumi ndani ya club ya Arsenal ameuzwa kwa pound milioni 7 kutoka Arsenal na kujiunga na West Bromwich Albion, beki huyo amejiunga na West Bromwich Albion kwa mkataba wa miaka minne.

Kieran Gibbs anaondoka Arsenal baada ya kucheza timu ya wakubwa kwa miaka kumi toka apandishwe mwaka 2007 kutoka timu za Arsenal ya vijana, Gibss hadi anaondoka Arsenal ameshinda mataji matatu ya FA, Community Shield mawili na amefunga jumla ya magoli 6 katika mechi 230 alizoichezea Arsenal.





Amini Afunguka Sababu ya Kutompongeza na Kutompa Zawadi Linah Alipojifungua

$
0
0
Amini Afunguka Sababu ya Kutompongeza na  Kutompa Zawadi Linah Alipojifungua
Msanii wa Bongo Flava, Amini amefunguka mambo kadhaa kuhusu aliyekuwa mpenzi wake Linah tangu alipojifungua.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ‘Yamoyoni’, ameiambia XXL ya Clouds Fm aliposikia Linah amejifungua alimuombea tu ila hakuweza kumpatia zawadi yoyote.

“Sikuwahi kumpongeza wala kumpelekea zawadi kwa sababu sifahamu anapokaa, vile vile sina mawasiliano naye. Niliposikia amejifungua mtoto wa kike nikasema Mwenyenzi Mungu amfanyie wepesi na mtoto wake na waweze kuishi vizuri katika maisha yao,” amesema.

“Yeye hakuwahi kunikosea hata mimi sikuwahi kumkosea kwa hiyo sikuwa na sababu ya kusema kitu gani bwana, ila kimoyomoyo nilimuombea dua kwa sababu alikuwa anahitaji sana mtoto,” ameongeza.

Wawili hao ambao muziki wao ulitambulika kupitia THT walikuwa mapenzini kipindi cha nyuma kabla ya kila mmoja kuanza maisha mapya ya kimahusiano.


Siwezi Jifananisha na Lulu Diva : Malaika

$
0
0
Siwezi Jifananisha na Lulu Diva : Malaika
Msanii wa Bongo Flava, Malaika amesema hawezi kujilinganisha na Lulu Diva kwani kila mmoja anafanya aina yake ya muziki.

Hata hivyo ameeleza kuwa Lulu Diva ni msanii mpya ambaye pia anafanya vizuri, hivyo wale wanaowalinganisha hawafanyi kitu kibaya.

“Sijui, siwezi kujilinganisha, ni watu ambao wanaona ndio wanaweza kutulinganisha lakini naweza kusema Malaika ni Malaika. Ukinisikiliza vizuri katika miziki yangu and the way navyotunga,” ameiambia E-Newz ya EATV na kuongeza.

“Sijafanikiwa sana kusikiliza miziki yake lakini najua ule mmoja ‘Usimuache’, kwa hiyo najua yupo tofauti na mimi, aidha kuna vitu anapenda kutoka kwangu. Unajua kuna mtu anaweza kuwa ni fan mpaka anafanya vitu kama wewe, so inawezekana pia yupo hivyo,” amesisitiza.

Masikini Inasikitisha... Moyo wa Yusuph Manji Wawekewa Vyuma Ili Kumsaidia Kupumua

$
0
0
Maskini Moyo wa Yusuph Mnji Wawekewa Vyuma Ili Kumsaidia Kupumua
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKIC), Prof. Mohammed Janab ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo August 30, 2017 kuwa moyo wa Mfanyiabiashara Yusuf Manji umewekwa vyuma ili kumsaidia kupumua.

Prof. Janab ambaye ni Daktari wa moyo na Shahidi wa kwanza upande wa uetetezi ameyasema hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha wakati akitoa ushahidi katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili Manji ambapo akiongozwa na Wakili wa utetezi, Hajra Mungula, alisema yeye ni Daktari wa moyo wa Taasisi ya JKIC.

Amesema anamfahamu Manji baada ya kufikishwa katika Taasisi hiyo February 2017 akiwa mwenye matatizo ya moyo na kuongeza kuwa alipofikishwa hapo alifanyiwa vipimo na jopo la madaktari lililobaini Moyo wake umewekewa vyuma ambapo akaingizwa mipira maalum na kubaini kwamba upo katika hali nzuri.

”July 2017 alirudishwa tena katika Taasisi yetu akiwa na tatizo hilo la moyo pamoja na maumivu ya mgongo na kutokuwa na usingizi.”

Prof. Janab amesema alivyorudi hapo walimpokea kama mgonjwa aliyetibiwa nje ya nchi na ripoti ilionyesha ametibiwa Florida, Marekani.

Alipoulizwa na Wakili Mungula kama mgonjwa aliyewekewa vyuma katika moyo anaweza kutumia dawa za kulevya, Prof. Janab alijibu kwamba huwa haruhusiwi kufanya baadhi ya mambo ikiwemo kuvuta sigara, kutumia Heroin.>>>”Hivyo kama akitumia athari zake ni kwamba mirija ya moyo itaziba, kisha atatakiwa afanyiwe upasuaji mkubwa zaidi.”

Prof. Janab ameongeza kuwa katika awamu ya pili ya Manji kurudi hospitalini hapo walimsaidia kumtibia maumivu aliyokuwa nayo kwa kumpa Drip ya Paracetamol’s na Sindano ya Tram a do.

Akijibu hoya ya Wakili wa Serikali, Timony Vitalis kwamba matumizi ya dawa za kulevya yanaweza kusababisha ugonjwa wa moyo, Prof. Janab alijibu ndio.

Kesi imeahirishwa hadi August 31, 2017 kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.



DAYNA NYANGE: Sina Wasiwasi Ninaposikia Roma Anataka Kutoa Nyimbo Kwakuwa Akurupuki

$
0
0
DAYNA NYANGE: Sina Wasiwasi Ninaposikia Roma Anataka Kutoa Nyimbo Kwakuwa Akurupuki
Kutokana na ukaribu wake wa kifamilia na Roma, msanii wa Bongo Flava Dayna Nyange amesema rapper huyo huwa hakurupuki kuachia ngoma kutokana na kile ambacho anaandika.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Chovya’, amesema kutokana na hilo huwa hana wasiwasi anaposikia Roma anataka kutoa wimbo.

“Ukimuangali Roma ni mwanamuziki yupo tofauti na watu wengi, yaani hata huwezi kuanza na kumlinganisha na mtu mwengine kwa sababu ya aina ya muziki ambao ameuchagua, I know him, yupo vizuri kichwani, ana uwezo, anajielewa na yupo makini,” Dayna ameiambia Bongo5.

“Watu wanajua Roma ni mtu ambaye haogopi chochote lakini kwenye kazi zake ni mtu ambaye anakuwa na uogo, hakurupuki kuachia kazi, mpaka aamua asema hii inatoka,” ameongeza.

Roma kwa sasa anatamba na ngoma yake ‘Zimbambwe’, ngoma hii ilitoka August 10 hadi sasa ina views 1,283,106 katika mtandao wa Youtube.


Leseni za Usajiri wa Magazeti na Majarida Waanza Kutolewa

$
0
0
Leseni za Usajiri wa Magazeti na Majarida Waanza Kutolewa
PIX0Serikali kupitia Idara ya Habari (MAELEZO) imeanza rasmi utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari kwa kutoa leseni kwa vyombo vya machapisho yakiwemo Magazeti na Majarida.

Akizungumza katika makabidhiano ya leseni hizo Jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi amesema  utoaji wa leseni ni utekelezaji wa agizo rasmi lililotolewa Agosti 23, 2017 lililowataka wamiliki wote wa machapisho kujisajili upya na kupewa leseni kwa lengo la kuifanya tasnia ya Habari kuwa taaluma rasmi kama zingine.

“Leseni hizo zimeanza kutolewa rasmi Agosti 23 na zoezi hilo litaendelea hadi Oktoba 15, 2017 na baada ya hapo wale amabo watachapisha magazeti  na majarida bila kuzingatia Sheria hiyo watakuwa wametenda kosa la jinai”, alisema Dkt. Abasi.

Katika zoezi hilo Dkt. Abbasi alitoa leseni kwa vyombo vinne ambavyo ni Jarida la Nchi Yetu linalomilikiwa na Idara ya Habari MAELEZO, gazeti la Daily News, Habari Leo pamoja na Spoti Leo ambayo ni magazeti ya Serikali.

Dkt. Abbasi ametoa wito kwa vyombo vingine vya habari ambavyo bado havijaanza taratibu za upataji wa leseni visisubiri hadi dakika za mwisho za mchakato huo ili kuepuka msongamano na usumbufu usio wa lazima.

“Nitumie fursa hii kuwaalika ambao hawajapata leseni wafanye haraka, Tanzania Standard Newspaper (TSN) walitimiza masharti ndani ya siku tatu ndio maana leo wamepata leseni hizo, hakuna urasimu wala nia mbaya ya kufungia baadhi ya machapisho kama wengi wanavyodai bali ni katika kutekeleza matakwa ya Sheria”, alisisitiza Dkt. Abbasi.

Kwa upande wake Mhariri Mtendaji wa TSN Dkt. Jim Yonazi ameviasa Vyombo vingine vya Habari kutekeleza agizo hilo ili kupata uhuru mpana katika uwajibikaji pamoja na kuwa mfano wa kutii Sheria bila shuruti ili taaluma ya habari iendelee kuheshimika kwa jamii.

“Ukifanya kazi kihalali unakuwa na uhuru wa kufanya kazi vizuri, ubunifu unaongezeka na unafanya biashara bila wasiwasi”, alisisitiza Dkt.Yonazi.


TFF Yatangaza Majina 8 ya Wagombea Uongozi TPLB

$
0
0
TFF Yatangaza Majina 8 ya Wagombea Uongozi TPLB
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imetangaza majina nane ya wagombea ambao yamepita katika mchujo wa awali kuwania nafasi mbalimbali katika Kamati ya Uongozi (Management Committee) ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Waliopitishwa ni kuwania uenyekiti wa Management Committee ni Clement Sanga na Ahmed Yahya wakati Shan Crysostoms ameptishwa kuwania nafasi ya makamu mwenyekiti.

Kwa mujibu wa kamati hiyo, Ramadhan Mahano na Hamisi Madaki wamepitishwa kuwania nafasi ya Ujumbe wakitokea klabu za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

James Bwire na Almas Kasongo wamepitishwa kuwania Ujumbe wakitokea klabu za Ligi Daraja la Kwanza. Brown Ernest hakupitishwa kwa sababu hakuthibitishwa na klabu yake.

Edga Chubura amepitishwa kuwania ujumbe akitokea klabu za Ligi Daraja la Pili.

Wagombea kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji wa Bodi ya Ligi Kuu ni marais au wenyeviti wa klabu husika. Wagombea wanatakiwa kuwa wenyeviti au Marais wa klabu husika.

Nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania inagombewa na klabu za Ligi Kuu pekee.

Uchaguzi huo wa kamati hiyo utafanyika Jumapili Oktoba 15, 2017 jijini Dar es Salaam na unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za Uchaguzi za TFF toleo la 2013.


Mapya Yaibuka Sakata la Kusajiliwa kwa Buswita

$
0
0
Mapya Yaibuka Sakata la Kusajiliwa kwa Buswita
Sakata la kiungo wa Yanga SC aliyesajiliwa msimu huu kutoka Mbao FC Pius Buswita kufungiwa mwaka mmoja kucheza mpira lapata sura mpya baada ya katibu mkuu wa Yanga ndugu Charles Boniface Mkwasa kulitolea ufafanuzi.

Buswita amekumbana na rungu la TFF la kutojihusisha na soka kwa mwaka mmoja baada ya kile kinachodaiwa kusajili vilabu viwili kwa wakati mmoja yaani Yanga SC na Simba SC . Simba ndio waliomwekea pingamizi TFF ikidaiwa kawatapeli hivyo kufungiwa mwaka mmoja.

Mkwasa asubuhi ya leo akiongea na kituo cha redio ya EFM amekiri kupokea barua ya hukumu hiyo ikiwaeleza hawataweza kumtumia mchezaji huyo kwa mwaka mmoja kama adhabu yake . Mkwasa amesema kama klabu pia wameiandikia TFF barua kupinga uamuzi huo na kulieleza jambo hilo kwa kina sambamba na maelezo ya mchezaji husika .

” Simba SC wanasema Pius wamemsajili tarehe 2 juni 2017 ilihali kipindi hicho alikuwa ndani ya mkataba na Mbao FC kitu ambacho ni makosa kwa sababu hawakuwafuata Mbao . Sisi tumewafuata Mbao na mchezaji husika na tukamsajili , wakatupa stakabadhi zetu pia release letter kama viambatanisho . Sasa hao Simba walimsajili Pius yupi? ilihali mkataba wake na Mbao umekwisha tarehe 7 August?! Hii ina maana kwanza kabisa Simba ndio wana makosa katika hili kumsajili mchezaji wa watu akiwa ndani ya mkataba bila kuonana na waajili wake. Katika hili Mbao ndio wana haki kuwashitaki Simba ” alieleza Mkwasa.

Mkwasa kaenda mbali kwa kusema waliokuwa wakimrubuni kijana huyu kwa milioni 5 kupitia wazazi wake ni wapenzi wa Simba Mwanza ambao dhamira yao ilikuwa ni kuvuruga usajili huu hivyo TFF walitakiwa kusikiliza pande zote kabla ya kutoa hukumu ( natural justice ) kuliko walivyofanya.

” sisi na Azam tuligongana kwa Hozza wa Mbao lakini mwisho wa siku tukaona isiwe tabu kwa sababu mchezaji husika kaonesha mapenzi ya kwenda Azam , tulipewa pesa zetu na kuliacha suala hilo bila ugomvi , kwanini Simba ?! ” aling’aka Mkwasa.

Sakata hili kuna kila dalili ya taratibu za kiusajili kukiukwa pia hukumu kutoka bila kusikiliza kwa kina pande zote . Hali ambayo imewapelekea Yanga na mchezaji husika kukata rufaa TFF kwa hukumu waliyotoa.

Afisa habari wa Simba SC ameeleza suala la mchezaji huyo wanaweza kulipeleka katika mahakama za kiraia kwa kesi ya utapeli.





HESLB Yaongeza Muda wa Uombaji Mkopo Vyuo Vikuu

$
0
0
HESLB Yaongeza Muda wa  Uombaji  Mkopo  Vyuo Vikuu
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeongeza muda wa wanafunzi kuwasilisha maombi ya mikopo.

Hatua hiyo imeelezwa inalenga kutoa nafasi kwa wanafunzi walioshindwa kufuata masharti kuyakamilisha. Mkurugenzi Mkuu wa bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru amesema muda huo umeongezwa hadi Septemba 11 badala ya Septemba 4.

“Tumesogeza mbele kwa siku saba zaidi ili walioshindwa kufuata vigezo wakati wa kujaza fomu wafanye hivyo,” amesema.

Amesema hadi kufikia jana Agosti 29, wanafunzi waliojitokeza walikuwa 49,282 lakini ni 15,473 waliokamilisha maombi kwa njia ya mtandao.


Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Zitto Kabwe Atamani Wapinzani Waungane Kuing’oa CCM Madarakani

$
0
0
Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameeleza umuhimu wa vyama vya upinzani kuungana akisema ndio mkakati pekee utakaoing’oa CCM madarakani.

Zitto alisema hayo wiki iliyopita katika mahojiano maalumu na Mwananchi kuhusu mambo mbalimbali ya kisiasa yanayoendelea nchini na ndani ya ACT -Wazalendo.

ACT-Wazalendo haikuwa ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita, ikiviachia vyama vya Chadema, NCCR-Mageuzi, NLD na CUF kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi za urais, ubunge na udiwani.

Lakini katika mahojiano na Mwananchi, Zitto alionekana kutambua umuhimu wa umoja katika kupambana na chama hicho kikongwe nchini ambacho kimeongoza nchi kwa zaidi ya miaka 50, kikianzia na jina la Tanu kwa Bara na ASP kwa visiwani.

“Kwa mazingira ya siasa yaliyopo nchini, ushirikiano miongoni mwa vyama vya upinzani kukabiliana na CCM ni jambo lisilokwepeka,” alisema Zitto, mwanasiasa wa kizazi kipya ambaye hajawahi kuwa CCM kama ilivyo kwa wanasiasa wengi wa upinzani.

“ACT Wazalendo tunalitambua hilo ndio maana tunafanya juhudi kubwa kujenga chama chenye nguvu kitakacholeta chachu ya ushindi kwa kushirikiana na vyama vingine.

“Hakuna chama cha siasa chenye nguvu kinachokubali kuungana na kingine kilicho dhaifu. Ndio maana tunajenga chama kuongeza nguvu na ushawishi kisiasa ili tukiungana kusiwepo chama kinachonyonya nguvu ya kingine.”

Kauli ya Zitto ni tofauti na msimamo ambao amekuwa akiuonyesha tangu aondolewe Chadema mapema mwaka 2015 na alitumia kampeni za chama hicho kuponda Ukawa. “Kama unataka siasa za mbwembwe nenda CCM, kama unataka siasa za ulaghai nenda Ukawa, na kama unataka siasa za msingi siasa za issues ni ACT Wazalendo,” alisema Zitto Agosti 28, 2015 wakati harakati za uchaguzi zikiwa zimepamba moto.

hivyo, katika matukio ya hivi karibuni, Zitto amekuwa akishirikiana na viongozi wa vyama vingine, hasa Chadema ambayo ilikuwa na mgogoro naye kwa muda mrefu.

Zitto na Chadema walionyesha dalili za kuanza kuondoa tofauti zao wakati wakipinga uamuzi wa Serikali kufuta matangazo ya moja kwa moja ya shughuli za Bunge.

Oktoba mwaka huo, Zitto aliisifu Ukawa kwa jinsi ilivyopambana na CCM katika Uchaguzi Mkuu uliopita, lakini akasema ACT-Wazalendo haitajiunga na umoja huo kutokana na miiko iliyojiwekea katika Azimio la Tabora.

Katika uchaguzi huo, Ukawa ilimsimamisha waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ambaye aliweka rekodi ya upinzani kwa kupata kura milioni 6.07 ambazo ni takriban mara mbili ya kura zote ambazo wapinzani wamekuwa wakipata tangu kurejeshwa kwa siasa za ushindani mwaka 1992.

Akijibu swali la kituo kimoja cha televisheni kama atagombea urais mwaka 2020, Zitto pia alidokeza umuhimu wa ushirikiano.

“Kwa mazingira yaliyopo sasa, suala la kugombea au kutogombea urais lisiwe maamuzi ya mtu mmoja. Kwa sasa tunahitaji kwenda kwenye uchaguzi wa 2020 vyama vya upinzani tukiwa united front.Tukiwa tunashirikiana, si kuungana kwa sababu vyama vina itikadi tofauti,” alisema Zitto akijibu swali hilo mapema mwaka huu.

Katika kipindi hicho cha kuanzia mwaka 2015, viongozi wa vyama vingine, hasa Chadema walikuwa wakimrushia maneno Zitto na chama chake, wakisema hawatakubali ajiunge Ukawa.

Kuhusu mpango huo wa kuifanya ACT Wazalendo kuwa kubwa, alisema wameandaa mikakati kadhaa ya kukabiliana na changamoto, hasa za kifedha.

“Tumejiwekea mkakati wa kuhimiza kila mwanachama kuchangia Sh1,000 kila wiki, au Sh4, 000 kwa mwezi kugharamia uenezi na ujenzi wa chama; tumegawa kadi zaidi ya 400,000 na iwapo wanachama 100,000 pekee watachanga, tunatarajia kukusanya Sh400 milioni kwa mwezi,” alisema Zitto.

Alisema fedha hizo zitasaidia mikakati ya kujenga chama kuwa cha kimkakati.

Kuhusu kukamatwa mara kwa mara kwa wanasiasa wa upinzani, Zitto alisema:“Naumizwa sana kuona viongozi, hasa wa upinzani wakikamatwa kwa kutekeleza wajibu na majukumu yao ya kikatiba ya kuisimamia, kuikosoa na kuishauri Serikali; kibaya zaidi amri za kukamata viongozi wakiwemo wabunge zinatolewa hadi na wakuu wa wilaya.”

Zitto aifikiria ‘Ukawa’ kuing’oa CCM madarakani

VIDEO: PAUL Makonda Asitisha Bomoa Bomoa Dar es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda WAMESITISHA zoezi la BOMOA BOMOA kwa Nyumba zaidi ya elfu kumi na saba (17, 000) zilizotangazwa KUBOMOLEWA na Baraza la Hifadhi ya Mazingira NEMC.

Hatua ya kusitisha zoezi hilo, Imekuja kufuatia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda KUZUNGUMZA na Mhe Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kuhusiana na Sintofahamu ya bomoa bomoa hiyo ambayo AMEMUELEZA Mhe Rais Magufuli kuwa Taarifa za BOMOA BOMOA ya Nyumba elfu kumi na saba iliyotolewa HAIKUFIKA ofisini Kwake Jambo ambalo ni tofauti na Taratibu za Utendaji kazi wa Serikali.

Kutokana na Sababu hizo, Mhe Makonda amesema Mhe Rais amesikitishwa na TAMKO hilo la kutaka KUBOMOLEWA kwa Nyumba zaidi ya elfu kumi na saba na ametoa pole kwa Wananchi waliokumbwa na TAHARUKI ya TAMKO hilo la Ubomoaji, na kusisitiza kuwa Mhe Rais, Dkt. John Pombe Magufuli HAKUCHAGULIWA kwa ajili ya KUBOMOA Nyumba za watu na kusisitiza kuwa anataka wananchi WANAOISHI katika maeneo HALALI kuachwa mana AMEPATA taarifa kuwa huenda ZOEZI hilo lingekwenda mbali zaidi mpaka kwa Wananchi WASIOHUSIKA. VIDEO:

Muuguzi Awaua Wagonjwa 90 Ili Awafufue Tena

$
0
0
Muuguzi nchini Ujerumani anayetumikia kifungo cha maisha kwa kuwaua wagonjwa sita, imebainika aliwaua wengine 84.

Idadi ya watu aliowaua imemwingiza katika rekodi ya mwanamke aliyefanya mauaji mengi kuliko wote nchini humo.

Mwanamke huyo, Niels Hoegel (40), alifungwa mwaka 2015 baada ya kupatikana na hatia ya kuwaua wagonjwa sita kwa kuwachoma sindano inayosababisha moyo kusimama ghafla.

Mamlaka za nchi hiyo zimekuwa zikifanya uchunguzi wa maelfu ya vifo, ikiwamo kufukua maiti za wagonjwa waliokufa chini ya uangalizi wake katika hospitali binafsi za Delmenhorst na Oldenburg ambazo amewahi kufanya kazi.

Polisi nchini humo wameliambia Shirika la CNN kuwa, wanaamini Hoegel aliua wagonjwa 36 katika Hospitali ya Oldenburg kati ya mwaka 1999 na 2001, na wengine 48 katika Hospitali ya  Delmenhorst.

Pia, wanasema idadi ya watu aliowaua inaweza kuwa kubwa zaidi lakini ushahidi hautapatikana kwa kuwa miili mingi ilichomwa moto, hivyo si rahisi kugundua sababu ya kifo kwa kupima majivu.

Katika mwendelezo wa kesi zake, Hoegel amekiri kuwachoma sindano wagonjwa ili moyo ushindwe kufanya kazi naye ajaribu kuwafufua kwa kuuamsha.

Amesema alitamani kuona anamfufua mtu baada ya kumchoma sindano hiyo na kwamba, alifadhaika aliposhindwa kuwarudishia uhai.

Johann Kuehme, ofisa wa polisi katika Mji wa Oldenburg aliwaambia wanahabari jana Agosti 29 kuwa idadi hiyo ya vifo imewaduwaza.

"Mauaji huenda yasingekuwa makubwa kiasi hiki kama hospitali hizi zingechukua hatua kuchunguza vifo au kutoa taarifa kwa mamlaka kuhusu vifo hivyo ili vichunguzwe,” amesema

Chid Benz: Tupac Yupo Cuba na Tunawasiliana na Nimefanya Wimbo Naye Soon Atakuja Tanzania

$
0
0
Chidi Benz azua jipya mjini, adai 2Pac yuko hai na anaishi nchini Cuba, na wanaongea kila siku na tayari ameshafanya naye ngoma itakayotoka hivi karibuni.

Chidi Benz ambaye kwa sasa anazungumzwa sana kwa skendo za utumiaji wa madawa ya kulevya, akiongea na  eNewz alisema kuwa  "Maneno yanayoongelewa kwamba 2Pac amefariki siyo kweli, Kila siku ninaongea na 2pac na hata sasa hivi nimetoka kuongea naye"

Mimi na 2Pac tumekutana Cuba, na tumefanya nyimbo ya pamoja na Mungu akisaidia hivi karibuni tataachia nyimbo hiyo".

"2Pac ana mpango wa kurudi kwenye muziki, na wimbo wetu tuliorekodi ndiyo utamrudisha. Na hivi karibuni 2Pac atakuja bongo, ila atakuja kimya kimya kama alivyokuja Beckam" Aliongeza Chidi Benz.

Pia Chid aliendelea kwa kusema "Baada ya kukutana na 2Pac tuliamua kurekodi baadhi ya vipande vya video ambavyo tutaanza kuvisambaza kwanza ili kuweza kuwajulisha watu kuwa 2Pac bado yupo hai na kuwaondoa watu fikra za kuwa 2Pac ni marehemu".

Hata hivyo kitu cha kushangaza zaidi ni baada ya Chid kuendelea kusema kwamba anamdai 2Pac kipini chake cha puuani ambacho alimuazima walipokuwa wote nchini Cuba.
Kama ilivyokuwa kwa Young Dee, Chid Benz naye ameonekana kuwa na hali ya kujichanganya sana katika maelezo yake kila aanapoongea.

Hivi karibuni Ali Kiba akiongea na eNewz alishauri serikali iingilie kati suala la Chid Benz na kumpatia matibabu. Na hata kama akibainika anajihusisha na madawa Alikiba alishauri "Chid asifungwe bali apelekwe 'rehab' akatibiwe kwani kumfunga mtu anayetumia madawa ni kumtesa tu".

Barua ya Wazi Kwa Diamond Platnumz Kwa Yanayoendelea Wakati Huu Baina ya Ali Kiba....

$
0
0
Maisha ni zaidi ya kuishi,maisha ni mahusiano na katika hili basi maisha yana maana zaidi ya kuishi.Mfano pale unapo amka asubuhi na kugundua kuwa kuna binadamu kama wewe wanaishi katika dunia hiyo hiyo ambayo na wewe unaishi,inakupa mawazo ya kufanya mipango ya maisha,kama vile kufanya biashara,kutoa huduma au kupokea huduma,moja kwa moja kutoka kwa binadamu wenzako.

Hii ina maana kwamba hata uwe mbinafsi vipi,huta tamani kuishi peke yako duniani,hii inatupa picha kwamba binadamu wenzetu ni wa muhimu zaidi katika kutimiza maisha yetu ya kila siku,hivyo ningeanza kwa kusema maisha ni mahusiano kati ya binadamu na binadamu.


 DIAMOND PLATNUMZ

Umekuwa ukipigania maisha yako ya kila iitwayo leo,naamini unatamani kesho iwe tofauti na leo,uzidi kuimalika katika mapambano yako ya kupata riziki.

Ulipo anzia sipo ulipo sasa,ulisha wahi kujiuliza ulifikaje hapo?Je ni juhudi zako binafsi (wewe kama wewe).Au ni juhudi za maisha yako (wewe na binadamu wenzako),mi naamini ni vigumu kufanikisha lolote katika hii dunia pasipo na maisha ya binadamu wengine.

Hivyo tukubaliane kwanza kwamba umefika hapo sababu ya binadamu wenzako ambao ulishirikiana nao ndiyo maana ukafika hapo.Pasinge kuwa na binadamu usinge kuwa hapo ulipo,maana ungemwimbia nani,ungeshauriwa na nani,ungeonyesha uwezo wako kwa nani,nani angekutengenezea nyimbo,nani angetizama video zako,hivyo ujue umefika hapo sababu ya watu wote unao wachukia au kuwapenda,kila binadamu huwa na mchango kwa binadamu mwingine moja kwa moja au kinyume chake.

Utajiri,Fadhira na chuki dhidi yako

Kwa bahati mbaya hakuna maskini anayetajirika akakosa timu ya wadai fadhira,sababu utajiri wa maskini hua na mnyororo wa wafanikishaji hadi kufikia utajiri huo,fahamu kuwa utajiri wa maskini una madeni ya fadhira kuliko utajiri wa tajiri,kama nilivyo sema binadamu ndiyo kakufikisha hapo.

Ushauri wa namna ya kurejesha fadhira

Watambue wadeni wa mafanikio yako,na hakikisha huwapotezi katika orodha na kumbukumbu zako,fahamu namna ya kuwalipa wadeni wako wa fadhira na uwalipe haraka.

Ukweli ni kwamba huwezi kuwalipa wadeni wako wa fadhira kwa pesa,au thamani sababu ukifanya hivyo ni sawa na kulipa fadhira,fadhira hailipwi fadhira inarejeshwa,naamini si kwamba waliokusababisha wewe kufika hapo walikuwa wanatoa pesa zao mifukoni na kukupa la hasha inawezekana walitumia muda wa maisha yao hata kama dakika moja kwa ajili yako kutoa hatua ya ngazi hata kama moja ila moja kwenda juu.Watu hawa naamini wanacho hitaji kikubwa kutoka kwako ni HESHIMA na KUTAMBULIKA.

Naamini hata wewe hapo ulipo umelifanyia taifa letu la Tanzania vitu vikubwa kwa kulitambulisha mahali pengi duniani kupitia sanaa ya muziki,naamini kitu kikubwa ambacho unatarajia kutoka katika taifa lako kutokana na kazi hiyo ni HESHIMA na KUKUTAMBUA.Lakini je? Wewe,umeyafanya hayo kwa wale walio kutambulisha Tanzania?

Haijalishi amekuchangia nini,iwe muda wa maisha yake,ushauri wake au vitendo vyake,ambavyo kwa namna moja au nyingine vilisababisha wewe kupiga hatua ya mbele zaidi,yakupasa KUMTAMBUA na KUMHESHIMU,awe mdogo au mkubwa.

Swala la mali na pesa hiyo ni zawadi yako na si lazima kumpa mtu,kama ikitokea mdai fadhira anadai pesa au mali,huyo hakuwa anakusaidia au kukupa fadhira huyo alikuwa anakukopesha fadhira au kukuajiri achana nae.

Chuki dhidi yako

1.Sababu za chuki

*Hujajua namna ya kufurahia mafanikio yako kulingana na jamii unayo ishi nayo.

Nasibu unayakumbuka maisha yako ya Tandale?Maisha ambayo mama yako alikuwa anapigania mpate mlo wa siku?Maisha hayo bado yapo kwa watanzania wengi hadi sasa.

Hivi unajua uliwezaje kupata ridhiki kubwa ambayo inakuhakikishia kupata chakula bila tabu leo hii?Je,uliipata kwa maonyesho ya majivuno ya starehe,na maonyesho ya thamani za mali na vidani vya gharama?

Au uliipata hiyo ridhiki kwa kuheshimu kila uliyemuona atakupa njia,ya kufika hapo ulipo?Kwa hiyo njia uliyo itumia zamani unadhani imepitwa na wakati,ukadhani njia ya majivuno ya mali,starehe na vidani kwa walio kupa mtaji itakusaidia kukubeba zaidi ya pale walipo kufikisha?HAPANA!

Fahamu kwamba wewe ni kioo cha jamii,kioo cha watu ambao wengi ni maskini na wachache matajiri,hivyo watu watapenda kukutazama kama mtu unaye wajali na kuwathamini kwa kile ulicha jaaliwa kukipata,mimi naamini unaweza ukaonekana kwa jamii katika mtizamo tofauti zaidi ya kwamba Diamond Platnumz ni mtu mwenye majivunoya mali na mbwembwe za starehe sababu njia hiyo itakujengea watu wenye chuki hata bila sababu.

*Sababu nyingine ya chuki ni kwamba Diamond Platnumz hutambui thamani yako,kwa hatua uliyo fikia,ulipaswa kujiamini na kuwa na busara ya hali ya juu kabisa.

Hatua uliyofikia kimziki,ni ya kuheshimiwa,Hukupaswa kabisa kwa level zako kuonyesha chuki dhidi ya wasanii wengine, kwa nini usiache chuki hizo zibebwe na kushugulikiwa na mashabiki,na siyo kujiingiza wewe na brand yako.

2.Ushauri

*Jaribu kutumia muda mwingi katika kuonyesha matukio ya kijamii zaidi,kupiga picha na mashabiki zako,kuonyesha picha za matukio ya “charity” mbalimbali unazo zifanya,picha ambazo zitaonyesha uko jirani zaidi na jamii,pia picha za familia yako,zitakufanya uonekane hushangai mafanikio na utaonekana huna ushindani na waliokupa riziki,bali utakuwa ni mtu wa jamii tena mtu wa watu,naamini haita kupunguzia kitu ila itakujenga na kukupa thamani zaidi.

Mfumo wa maonyesho ya vidani na thamani pamoja na maisha ya starehe,hayavutii kwa jamii yetu hii ambayo wewe umetoka nayo,huo ni utaratibu wa Kimagharibi,na siyo kwetu huku.

Jifunze kwa matajiri wakubwa hata hapa Tanzania wanapesa lakini mitandao yao ya kijamii wameitumia katika sura ya kuwa wao ni sehemu ya jamii na wako nayo pamoja katika shida na raha.

* Fahamu kwamba brand yako ni pesa nyingi sana,unachokifanya chochote ni pesa kwa wengine kama isipo kuwa kwako.

Acha kurudia vidato na hilihali ulifaulu vizuri tena sikunyingi,unacho tafuta ni nini?Kwani huko kwenye level zako hakuna mitihani ya juu hadi uanze kurudia vidato,hivi unadhani ikitokea umeenda kufanya mtihani wa kidato cha chini na wewe kidato cha juu,harafu ikatokea ukapitwa na mwanzafunzi wa chini unadhani kitakacho fata ni nini kama siyo aibu na kuzomewa?

Ushindani na mtu uliyemzidi huleta dharau na kuvunja heshima,

Mara nyingine ufahamu kazi yenu hii ni sawa na mchezo wa mpira,kama wewe beki mshambuliaji anaweza akakuchokoza makusudi ili ufanye faulo watu wapige penati,na ubaya kombe hua halibagui mshindi,yoyote aliyeshinda anaondoka nalo.

MAMBO 10 YA KUZINGATIA WEWE DIAMOND PLATNUMZ

1- Epuka kuongele maisha yako kwa watu,ambao huwafahamu vizuri hasa marafiki wapya wa muda mfupi,huwezi jua nani kaja kukupeleleza.

2- Epuka kujenga urafiki wa dhati na uaminifu kwa wanasiasa (urafiki wako uwe wa malengo kama wa kwao ulivyo wa malengo,wakati wote kuwa makini).

3- Kuwa makini unapotaka kurejesha urafiki na mtu uliyegombana nae,inawezekana hakumaliza hasira anaweza akawa anakuja kuleta jipya.

4-Kuwa makini na watu wako wa jirani,marafiki,ndugu,wafanyakazi wenzako inawezekana mnacheka pamoja na kuonyeshana uaminifu,ila msaliti yu kati yenu,usipende kufahamika sana hata kwa wanao kuhusu sana.

5-Usipende kutoa matamko au kujibu hoja kama hakuna ulazima.

6-Siku zote fahamu wewe ni kioo cha jamii,na jamii lazima ijione ikikutizama isije ikawa inaona mtu wa bandia.

7-Fahamu kwamba chuki unazo pata ni mtaji wa mafanikio yako,zinakuja ili kukuboresha kukupa hasira ili ufanye kazi na kukua zaidi,walio fanikiwa duniani ndiyo wenye bahati ya kuchukiwa na ndiyo maana huzidi kufanikiwa sababu,chuki ni mbolea tosha ya mafanikio,ukiona huchukiwi ujue umesha fikia hatua ya Mr. Nice kwani wakikumaliza hawatahangaika na wewe tena watahamia kwa mwingine,kadri unavyo fanikiwa ndivyo kasi ya chuki huongezeka.

8-Fahamu kuwa una marafiki wengi sababu una pesa na una maadui wengi sababu unapesa,ukikosa pesa marafiki na maadui watakukimbia,hivyo kama unapenda pesa basi kuwa tayari kwa hayo.

9-Toa misaada kwa wahitaji,hasa watoto,kinamama na waremavu.

10-Usimwamini mtu hata kama ni dugu yako.

KIKUBWA NACHO KUTABILIA KWA MUJIBU WA SAIKOLOJIA NI KWAMBA UGOMVI USIYO NA SABABU HUISHA BIRA SABABU,NA HUYO UNAYEGOMBANA NAYE LEO BILA SABABU NI RAFIKI YAKO KESHO TENA BILA SABABU.

ILA KWA BAHATI MBAYA KUPITIA UGOMVI HUU USIO NA SABABU UMEZAA MAADUI WENYE SABABU NA HUENDA HAMTA KUJA KUWA MARAFIKI MILELE NA HAWA WAGOMVI WENYE SABABU.

By Jmaiko

Picha: Amber Lulu akipelekwa kituo cha Polisi cha Urafiki kisa picha chafu

$
0
0
Msanii wa muziki na video vixen, Amber Lulu Jumanne hii alipelekwa kituo cha polisi cha Urafiki Ubungo jijini Dar es salaam kueleza kama anahusika katika kusambaza picha chafu mtandaoni ambazo zinamuonyesha akiwa nusu uchi na rapa Young Dee.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo tumezipata, zinadai kwa sasa muimbaji huyo yupo nje baada ya kuhojiwa kwa masaa machache kuhusiana na tukio hilo.

Akiongea na Bongo5 Jumaatano hii shuhuda wa tukio hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe, amesema mrembo huyo alishikiliwa na kituo hicho kwa masaa matatu na baada ya hapo aliachiwa.

“Ni kweli Amber Lulu alikuja na tulimuona hapa kituoni jana kama jioni jioni hivi,” alisema shuhuda huyo ambaye hakutaka atajwe jina lake.

Shuhuda huyo alidai mrembo huyo alifika kituoni hapo akiwa na team yake ya uongozi kutoka Afrika Kusini pamoja na uongozi wa Young Dee.

Bongo5 ilimtafuta meneja wa Young Dee ili kuzungumzia sakata hilo lakini meneja huyo hakuwa anapokea simu hata hivyo alivyotumiwa meseji alisema bado wanalishughulikia tatizo hilo na pale watakapokuwa na taarifa rasmi wataitoa kwa jamii.

Viewing all 104715 articles
Browse latest View live




Latest Images