Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

MBOWE "JPM Anakotupeleka Siko".....Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamis ya August31

$
0
0

MBOWE "JPM Anakotupeleka Siko".....Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamis ya August31

Tanzania Yatajwa Kwenye Orodha ya Nchi Zenye Mishahara Mikubwa Afrika

$
0
0
Shirika la Numbeo limetoa orodha ya nchi kumi zenye mishahara mikubwa zaidi barani Afrika. Hili ni shirika kubwa zaidi duniani la ukusanyaji wa taarifa za majiji na nchi. Shirika hili linatoa taarifa za mara kwa mara kuhusu hali za maisha duniani ikiwemo gharama za maisha, upatikanaji wa nyumba za kupanga, huduma za afya, foleni za barabarani, uhalifu na kiwango cha uchafuzi wa mazingira.

Zifuatazo ni nchi kumi za kiafrika zenye viwango vya juu zaidi vya mshahara:

1. Libya

Libya ndiyo nchi inayoongoza barani Afrika kwa kuwa na viwango vikubwa vya mishahara. Nchi hii yenye utajiri wa mafuta imejulikana kwa zaidi ya miongo minne ya utawala wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Hayati Muammar Gaddafi na machafuko yaliyofata baada ya kifo chake. Na pamoja kwa machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini humo mpaka sasa yanayosababisha hali ya usalama kuwa tete, kiwango cha kawaida cha mshahara kwa mwezi baada ya makato ya kodi ni shilingi milioni tatu na laki nane (3,800,000)

Ingawa machafuko nchini Libya yamekuwa ni kikwazo kikubwa barani Afrika, kiwango cha hifadhi ya mafuta kwenye nchi hiyo kinachokadiriwa kuwa mapipa bilioni 48 kunaifanya nchi hiyo sio tu kuwa moja ya nchi kumi zenye utajiri mkubwa zaidi wa mafuta duniani lakini pia Serikali yake inawafurahisha wananchi kwa kuwapa viwango vya juu vya mishahara pamoja na kufanya gharama za maisha kuwa chini.

2. Zambia

Jambo kubwa zaidi litakalokufanya uhamie kwenye nchi hii isiyo na bahari ni idadi kubwa ya wanyamapori. Ina mbuga na hifadhi nyingi sana, jambo linaloweza kuwa la kuvutia sana kama moja ya vitu unavyopendelea ni kufanya safari za mbugani. Kiwango cha kawaida cha mshahara kwa mwezi nchini Zambia ni shilingi milioni tatu na laki tatu (3,300,000), na kwa hakika huu ni mshahara mkubwa kwa yeyote yule. Gharama za kodi za nyumba na maisha kwa ujumla nchini Zambia zipo chini. Pamoja na viwango vikubwa kiasi hiki, Zambia kwa sasa inapitia katika mgogoro wa kisiasa na mifumo yake ya kiuchumi na kisheria bado inafata mfumo wa uendeshaji wa kikoloni.

3. Afrika Kusini

Mwisho wa siku kila mmoja anataka kazi yenye mshahara mzuri. Nchini Afrika Kusini, kazi zinazotokana na taaluma za Sheria, Umeneja wa mifumo ya kompyuta na teknolojia, waongoza ndege, udhibiti wa mafuta ya petroli, uhandisi wa majengo na uhandisi wa programu ni baadhi ya ajira zenye mishahara mizuri zaidi nchini humo. Kiwango cha kawaida cha mshahara nchini humo ni shilingi milioni mbili na laki sita (2,600,000+), ingawa wazungu bado mpaka sasa wanaishi maisha mazuri zaidi.

4. Namibia

Uchumi wa Namibia unaendeshwa na sekta ya madini – kuchimba, kusafisha na kusafirisha kwenda nje ya nchi. Sekta ya madini inachangia asilimia 11.5 ya pato la Taifa lakini inaiingizia nchi hiyo zaidi ya asilimia 50 ya fedha za kigeni.

Pia, Namibia ni moja ya nchi tano zinazozalisha madini ya uranium kwa wingi zaidi na pia wana utajiri mkubwa sana wa madini ya almasi. Ingawa uchumi wa nchi hiyo unaathiriwa sana na kupanda na kushuka kwa soko la dunia pamoja na ukame unaoikumba mara kwa mara, mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi nchini humo ni shilingi milioni moja na laki sita (1,600,000) kwa mwezi.

5. Mauritius

Nchi hii ambacho ni kisiwa kilichopo nje kidogo ya pwani ya Kusini-Mashariki mwa Afrika kina historia ndefu ya kuwa na utulivu wa kisiasa, utawala bora pamoja na uwajibikaji wa uwazi wa Serikali yake. Ni moja ya nchi za Afrika zenye uchumi mzuri zaidi ikiwa na idadi ya watu milioni 1.3. Mshahara wa kawaida nchini Mauritius ni shilingi milioni moja na laki tano (1,500,000) kwa mwezi.

6. Tanzania

Hii ni nchi ya sita kwa nchi za bara la Afrika zenye viwango vya juu vya mshahara ambapo mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi unakadiriwa kuwa ni shilingi laki tisa (900,000). Zaidi ya nusu ya wafanyakazi nchini Tanzania wapo kwenye sekta ya kilimo kama njia kuu ya kuwasingizia kipato. Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, Tanzania imeweza kuwa na uchumi imara na unaokua kwa asilimia saba kila mwaka katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Kiwango cha umaskini kimeendelea kupungua na vita dhidi ya Rushwa inayoongozwa na Rais John Magufuli inabaki kuwa msingi imara wa ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

7. Morocco

Tangu mwezi Oktoba mwaka 2016 nchi ya Morocco imekuwa kwenye mgogoro mkubwa sana wa kisiasa. Kwa sasa, nchi hiyo ina muunganiko mkubwa wa vyama vya siasa unaojumuisha vyama sita vya siasa nchini humo. Kilimo bado kinachangia asilimia 15 ya pato la Taifa. Pamoja na nchi hiyo kukumbwa na ukame mkubwa mwaka 2016, bado waliweza kuweka rekodi ya mavuno mengi zaidi ya nafaka. Katika nchi ya Morocco, mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi ni shilingi laki tisa (900,000).

8. Zimbabwe

Mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi nchini Zimbabwe ni shilingi laki nane (800,000). Nchi hii inayoongozwa na Rais Robert Mugabe tangu kupata kwa uhuru wake inatabiriwa kuwa itaweza kuwa na uchumi bora zaidi ya sasa na kupunguza umaskini iwapo itadhibiti hali ya kisiasa na kufikia makubaliano kuhusu kufanyika kwa siasa na sera za ushindani kwenye uwekezaji.

9. Ghana

Nchi hii imepiga hatua kubwa sana kwenye kujenga demokrasia imara. Ni nchi inayosifika kwa kuwa na mfumo huru wa Mahakama pamoja na uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza kwa wananchi na wanaharakati. Mshahara wa kawaida nchini Ghana ni shilingi laki saba (700,000) kwa mwezi. Uchumi wa nchi hii unategemea zaidi sekta ya mafuta, sekta nyingine zisizo za mafuta zina mchango mdogo kwenye uchumi wa nchi hiyo.

10. Algeria

Pamoja na bei ya mafuta kuporomoka kwenye soka la dunia, bado uchumi wa Algeria uliweza kukua kwa asilimia 3.8 mwaka 2016 ingawa pia yategemewa uchumi wake utashuka kati ya mwaka 2017 na 2019. Kiwango cha kawaida cha mshahara nchini Algeria baada ya makato ya kodi ni shilingi laki sita na elfu hamsini (650,000), kiwango ambacho ni kikubwa ukilinganisha na nchi nyingine nyingi za Afrika.

Matiti Yamtesa Mrembo Lulu Michael Uzinduzi wa Filamu ya Wema Sepetu Mlimani City

$
0
0
MUIGIZAJI nyota wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ mwishoni mwa wiki iliyopita aligeuka kuwa gumzo baada ya nguo aliyovaa kuonekana kumtesa kutokana na matiti yake kutaka kuchomoza kila wakati.

Tukio hilo lilitokea katika Ukumbi wa Cinema, Mlimani City Jumamosi iliyopita wakati wa uzinduzi wa Filamu ya Heaven Sent ya muigizaji mwenzake, Wema Sepetu ambayo ilikutanisha mastaa wa fani mbalimbali nchini.

Lulu aliyekuwa amependeza kwa mavazi yake, akiwa amevalia gauni jeusi refu lenye mpasuo mkubwa, alijikuta akipata taabu ya kuirudisha nguo yake sehemu ya kifuani, kwani kila wakati matiti yalionekana kutaka kutoka nje, lakini akawa anafanya kazi kubwa ya kuirudishia.


“Jamani muoneni Lulu anavyohangaika na hiyo nguo, sasa tangu nyumbani hakujua kama inamsumbua abadilishe? Au ndiyo mbwembwe za kutaka watu waone nido zake zilivyo nzuri?” alisikika akisema shabiki mmoja aliyeonekana kumfuatilia sana muigizaji huyo.

Licha ya Lulu, mastaa wengine kibao wa filamu walihudhuria uzinduzi huo na mashabiki wa kawaida wa tasnia hiyo, huku Wema Sepetu mwenyewe akiwa amesindikizwa na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, mshindi wa Big Brother Hotshot, Idris Sultan.

STORI: RICHARD BUKOS

Dogo Janja Anyoosha Maneno Kuhusu Irene Uwoya, ‘Nampenda Sana’

$
0
0
Msanii wa Bongo Flava, Dogo Janja amezungumzia taarifa zilizokuwa zikidai kuwa anatoka kimapenzi na Muigizaji wa filamu Irene Uwoya.

Rapper huyo ambaye ameachia ngoma mpya leo ‘Ngarenaro’ amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds Fm kuwa ukaribu wao ulikuwa wa kawaida tu na hakuna kilichokuwa kinaendelea kati yao ingawa watu waliwachukulia vinginevyo.

“Nampenda sana yule dada lakini kuwa na mazoea naye kidogo kumezua maneno mengi,” amesema Dogo Janja.

July mwaka huu zilienea taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa wawili hao wameonakana jijini Mwanza katika matanuzi  ya nguvu kitu kilichozua minong’ono kuwa wapo mapenzini.

NIYONZIMA Kafunguka: Ni Kuhusu Uhusiano Wake na Jini Kabula Uliotaka Kuvunja Ndoa yake

$
0
0
Kabla ya Jini Kabula kuwa katika matatizo aliwahi kunukuliwa akisema aliwahi kuwa mapenzini na staa wa soka wa Simba SC, Haruna Niyonzima na kuzua mzozo kwenye mitandao ya kijamii kwa kuwa Niyonzima kwenye ndoa hivyo kumsababishia matatizo ndani ya familia yake.

Ayo TV na millardayo.com zimempata Haruna Niyonzima kwenye EXCLUSIVE na kufunguka kila kitu akisema hakuwahi kuwa mapenzini na msichana huyo licha ya kwamba kuzungumza kwenye vyombo vya habari.

Aidha, kuhusu mkewe kulisikia hilo alisema haikuwa rahisi kuchukulia kawaida ingawa ni muelewa na alijaribu kuelewa jambo hilo.

Bonyeza Play hapa chini kumsikia Niyonzima

SOMA Nafasi za Ajira Mbali Mbali Zilizotangazwa Siku ya Leo

$
0
0

Mh Rais Chapa Kazi, Ukicheka na Kima Utavuna Mabuwa, Usigeuke Nyuma...Kipindi cha Mpito Maumivu Lazima...Asichomoke Mtu

$
0
0
Kuna watanzania wengine wana akina za ki-zwazwa sana. Kila siku wanalalamika, ooh mara Rais hivi...ooh mara kafanya vile. Mnataka afanyeje? Afanye kama kila mtu anavyotaka amekuwa malaika?Ukiulizwa wewe umefanya nini utajibuje?

Tanzania ilishakuwa ya watu wachache walewale wanaojuana, watu maarufu.


1. Watu walikuwa wamehodhi maeneo makubwa nchi nzima, wakati hawayafanyii kazi

2. Wafanyabiashara wengi walikuwa hawalipi kodi


3. Wafanyakazi hewa, dawa hewa, mishahara hewa, pembejeo hewa,vyeo hewa

4. Wakubwa walikuwaga wanajitanua sana, walikuwa wanatunyanyasa sana. Utafikiri sisi ni wakimbizi

5. Mamikutano ya hadhara yalikuwaga kila siku makelele, wanakusanya watu ambao wanatakiwa wafanye kazi

6. Viongozi wa Serikali walikuwaga wanajilipa double payments, wanasafiri nje ya nchi kutanua tu makundi kwa makundi


7. Vimemo tu ndo vilikuwa mpango mzima. Undugu tu kila kona

8. Mafuta hewa, posho hewa, safari hewa, maiti hewa, kodi hewa


Ingekuwa ni wewe,

1. Vijana wote walioko mtaani wangekuwa wameajiliwa?

2. Watumishi wangekuwa wamepandishwa madaraja, mishahara na kupata uhamisho?

3. Ungekuwa umeondoa foleni jijini Dsm?

4. Ungeruhusu kila mtu aishi anavyotaka?

5. Ungekubali mtu akukashifu mtaani bila sababu yoyote?

Tusipotoshe umma.Tulishafikia mahala ambapo ili kuleta maisha bora, ni lazima baadhi ya watu waumie. Ilikuwa ni lazima jasho litoke.

Mtu ameingia madarakani mnataka shida zote ziondoke, ngumu ndugu zangu.
Yaani ilikuwaga taabu tupu.

Maisha mazuri yanakuja na ndo maana tunaona Mh Rais kama anatukomesha, hatupendi. Siyo hivyo.Mh Rais yupo pamoja nasi. Hiki ni kipindi cha transition tu, mambo mazuri yanakuja na kuja kwake ndo hizi harakati zinazoendelea.

Baba mwenye nyumba lazima uwe "fit" kuijenga nyumba yako. Maandalizi ni lazima yafanyike, watu wakaze mikanda. Maisha ya asali na maziwa yanakuja ,very soon tutasahau yote haya.

Tuchape kazi, Mh Rais ni mtanzania mwenzetu. Mambo mazuri yanakuja.Ana nia nzuri na sisi na ndo maana mnamuona hana mbwembwe ,yupo tu hapa nchini .Hatoki mtu hapa.

By Hivi Punde/JF

Watoto Wanne Waliodaiwa Kutekwa Wawili Wapatikana

$
0
0
Watoto Wanne Waliodaiwa Kutekwa Wawili Wapatikana
IKIWA ni siku chache baada ya vyombo vya habari kuripoti kuhusu kupotea kwa watoto wanne waliodaiwa kutekwa, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha kupatikana kwa watoto wawili na kumshikilia mtu mmoja aliyekutwa na watoto hao katika Kata ya Olasiti .

Kamanda Mkumbo amesema jeshi lake linaendelea na upelelezi kuhakikisha watekaji wote wanapatikana kwani tukio hilo sio la kufumbia macho na pia lina hatarisha amani kwa wakazi waJjiji la Arusha.

Wazazi watoto waliopatikana wameeleza kuwa watoto wao waliletwa na dereva wa boda boda mara baada ya watekaji kupatiwa namba ya balozi na kuwaagiza kuwarudisha nyumbani watoto Ayub Fred na Bakari Suleman.

Mama mzazi wa Bakari amesema ni faraja kuona mwanae amerudi salama nyumbani mara baada ya kumpoteza kwa siku nne mara baada ya kutekwa na watu wasio fahamika.
Amesema wazazi wengine wasikate tama kwani jeshi la polisi bado linaendelea na msako wa kuwapata watoto wengine wawili Maurin David pamoja na Ikram Salim ambapo mpaka sasa hawajulikani walipo.

Awali watekaji hao waliripotiwa kuwapigia simu wazazi wa watoto hao ili wawapatie pesa ndipo wawarudishe watoto hao majumbani mwao.


Jux Alizwa na Penzi la Vanesa Mdee Atamani Kurudiana Nae Tena

$
0
0
Jux Alizwa na Penzi la Vanesa Mdee Atamani Kurudiana Nae Tena
Msanii wa muziki bongo fleva Juma Jux aonyesha bado anahitaji uwepo wa aliyekuwa mpenzi wake msanii Vanessa Mdee, kwa kushindwa kuvumilia maumivu ya kuachana na kuweka bayana kwamba atafarijika sana endapo atamuona tena kwa mara nyingine.

Jux amebainisha hayo kupitia ukurasa wake Instagram ambapo  ameandika ujumbe unaohusu kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, na kusema miaka ya nyuma alikuwa hafanyi sherehe kutokana alikuwa na mpenzi wake Vanessa kwenye siku hiyo nakujiona kama amesherehekea  lakini kwa sasa hayuko naye tena anatamani hata aende kuhudhuria tu kama rafiki na itakuwa faraja kubwa kwake.

" Sikuwahi kufanya 'party' yoyote tena sababu nilikuwa na rafiki, mpenzi na mtu wa karibu kuliko mtu yoyote kwenye maisha yangu. Sasa hatuko tena karibu kama mwanzo, tumebaki kuwa marafiki wa kawaida tu. Uwepo wake tu ulikuwa ni zaidi ya chochote kwenye siku yangu ya kuzaliwa, kuongea na yeye au ujumbe wake tu ilitosha kukamilisha siku yangu. Ila sasa sidhani kama itakuwa kama mwanzo, nitafarijika sana kama nitamuona hiyo siku", aliandika Jux.

Jux hivi karibuni akiwa kwenye mahojiano na kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, amekiri kuwa bado ana hisia juu ya Vanessa Mdee, ambaye pia alishawahi kusikika akikiri bado anampenda Jux na ataendelea kumpenda.


TANZIA: Baba Mzazi wa Lwandamina Afariki Dunia

$
0
0
TANZIA: Baba Mzazi wa Lwandamina Afariki Dunia
Klabu ya Yanga yapatwa na msiba wa kuondokewa na baba yake mzazi kocha mkuu mwenye uraia wa Zambia, George Lwandamina.

Hayo yamethibitishwa na Afisa habari wa klabu hiyo Dismas Ten na kusema ni kweli kocha wao amepatwa na msiba wa mzazi wake huko kwao Zambia na tayari wameshafanya mpango wa kumsafirisha Lwandamina kwenda kuhudhuria msiba huo.
"Lwandamina ameondoka leo nchini Tanzania kuelekea nyumbani kwao Zambia kwa ajili ya mazishi ya baba yake, ila akifika huko ndiyo tutaweza kujua tarataibu za mazishi kwa kuwa shuguli zote zinafanyikia huko kwao", alisema Ten.

kocha mkuu wa Yanga George Lwandamina
Lwandamina ambaye amejiunga na Yanga Novemba, mwaka jana (2016) inadaiwa baba yake mzazi alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kupooza na kufariki usiku wa Jumanne Agosti 29 mwaka huu.

Urusi Yasema Vikwazo Dhidi ya Korea Kaskazini Havitafua Dafu

$
0
0
Urus Yasema Vikwazo Dhidi ya Korea Kaskazini Havitafua Dafu
Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu.

Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang .

Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana.

Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini.

Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Nandy Afunguka Vitu Ambavyo Anavutiwa Navyo kwa Dogo Janja na Bill Nass

$
0
0
Nandy Afunguka Vitu Ambavyo Anavutiwa Navyo kwa Dogo Janja na Bill Nass
HIT maker wa ngoma ya Wasikudanganye, Faustina Charles ‘Nandy’ amesema kuwa anavutiwa na kila kitu ambacho wasanii wenzake wawili; Dogo Janja na Billnas hivyo kwake yeye, hao ndiyo chaguo lake.

Akizungumza na Showbiz Extra, Nandy alisema, mbali na kwamba wasanii hao kuwa washkaji zake wa karibu na kuhusishwa nao na skendo za mapenzi lakini uwezo wao katika kazi unamfanya kuwa shabiki namba moja wa waimbaji hao.

“Kwa Billnas na Dogo Janja huniambii chochote, kwa hapa Bongo hao ndiyo wasanii wangu bora, napenda kile wanachofanya cheki wanavyovaa, cheki muziki wao, cheki wanavyojua kwenda na wakati, kwa kweli sina sababu ya kutowashabikia ingawa nimekuwa nikihusishwa kutoka nao kimapenzi lakini hakuna ukweli wowote,” alisema Nandy.

Ridhiwani Kikwete Amvaa Waziri Khamis Kigwangala Adai Anaweza Kuwa ni Mchochezi

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amemvaa Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.Khamis Kigwangala na kumwambia anaweza kuwa sehemu ya wachochezi kwa anachokifanya.

Ridhiwani Kikwete amebainisha hayo kupitia ukurasa wake wa twitter baada ya  Mhe. Kigwangalla kuonyesha kusikitishwa na kitendo kilichofanywa na Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma katika kuwafanyia usaili baadhi ya wataalamu waliojitokeza kwenye usaili  wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambao umefanyika mapema leo Agosti 30, 2017.

"Unaweza dhani unauliza swali kumbe nawe unakuwa sehemu ya wachochezi! Mhe. Waziri unaweza kuwa hujui kusoma lakini picha inatoa jibu sahihi", aliandika Ridhiwani.

Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma leo Agosti 30, 2017 ilifanya usaili kwa ajili ya nafasi za kazi katika Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) ambapo takribani watu 30,000 walijitokeza huku ikiwa watu 400 pekee ndiyo wanaotakiwa.

Dereva Aliyesababisha Ajari ya Treni Morogoro Akutwa na Mashtaka 30

$
0
0
Dereva Aliyesababisha Ajari ya Treni Morogoro Akutwa na Mashtaka 30
Dereva wa daladala aliyesababisha ajali iliyoua wanafunzi watatu na abiria wengine 27 kujeruhiwa mkoani Morogoro amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka 30, likiwemo la kuendesha gari kwa uzembe na kugonga treni ya abiria ya Shirika la Reli Tanzania (TRL).

Katika Mahakama ya Wilaya ya Morogoro, Charles Petro ambaye alipata majeraha kwenye ajali hiyo amesomewa mashtaka mbele ya Hakimu Joyce Mkoi.

Wakili wa Serikali, Caristus Kapinga amedai Agosti 24 asubuhi, kwenye makutano ya reli na barabara eneo la Tanesco, Manispaa ya Morogoro mshtakiwa alitenda makosa hayo.

Kapinga amedai kwa makusudi, huku akijua kufanya hivyo ni kosa mshtakiwa aliendesha gari aina ya Nissan kwa uzembe na kugonga treni ya abiria iliyokuwa ikitokea Dodoma kwenda Dar es Salaam.

Kutokana na ajali hiyo, wanafunzi watatu walifariki dunia na abiria 30 walijeruhiwa wakiwemo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari zilizoko Kihonda na Msamvu katika Manispaa ya Morogoro.

 Mshtakiwa amekana mashtaka yote na  hakimu ameahirisha kesi Hadi Septemba 13 itakapotajwa.

Upande wa mashtaka umedai upelelezi haujakamilika. Mshtakiwa amepelekwa  rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya  Sh10 milioni na mwingine kuwasilisha hati ya mali isiyohamishika.


Odama Afunguka Sababu ya Kutofanya Sherehe Kubwa Siku Yake ya Kuzaliwa

$
0
0
Odama Afunguka Sababu ya Kutofanya Sherehe Kubwa Siku Yake ya Kuzaliwa
STAA wa filamu Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amefunguka kuwa hakuweza kufanya sherehe kubwa kwenye siku yake ya kuzaliwa kwa sababu anaona kufanya hivyo ni kama utoto.

Akizungumza na Amani, Odama alisema ameamua kutofanya kitu kubwa mpaka atakapokuwa mzee, itakuwa na maana kubwa kuliko kufanya kila mwaka.

“Huwezi amini yaani hata kama zamani nilikuwa nafanya hivyo basi nilikuwa bado akili yangu haijachangamaa kabisa lakini mambo ya sherehe kubwa nitafanya nikiwa mzee kwa sasa tena hapana,” alisema Odama ambaye bethidei yake ni Agosti 26.
Stori zinazo husiana na ulizosoma



“Hakuna Mtu Anayeninunulia Nguo Wala Kunipa Pesa” Agnes Masogange Ataja Sababu Asizoogopa Kuuza Mwili wake

$
0
0
“Hakuna Mtu Anayeninunulia Nguo Wala Kunipa Pesa” Agnes Masogange Ataja Sababu Asizoogopa Kuuza Mwili wake
Aliyekuwa video vixen mkali kutoka Bongo Agnes Masogange amefunguka kuhusu maisha yake huku akigusia kuwa watanzania wengi wanapenda kumponda bure.

Katika mahojiano yake na Gazeti la Mwanaspoti mrembo huyu alisema Kuwa hana dhiki ikiwa atafikia kiwango cha kuuza mwili wake ili ajitafutie. Masogange alisema,

“Watu bana!, mimi sina dhiki ya kufikia kuuza mwili wangu eti nipate pesa na kuhusu zile picha kipindi kile nilizopiga hazikuwa za utupu sema basi tu watanzania tunapenda kuzusha sana. Na mtu kuenda Sauzi ndio ameenda kujiuza?,” Masogange aliliambia Gazeti la Mwanaspoti.
Aliongeza kuwa hakuna mtu anayemnunulia mavazi anayovaa wala kumpa pesa ya matumizi yake kwa hivyo hakuna anayeweza kumwambia chochote.

“Mimi nilikuwa na biashara zangu nafanya na wanaosema hivyo hawanisaidii chochote,hakuna mtanzania anayeninunulia nguo,hayupo anayenipa pesa waongee tu. Unajua sisi wadada tuna tabia ya kuoneana wivu akiona unafanya vizuri anaanza kukusemea vitu vya ajabu pembeni,”

Kweli Pesa Inatakatisha, Huu Ndio Muonekano wa Sasa wa STEVE YANGA (Shabiki wa Yanga wa Kulia lia)

$
0
0
Kweli Pesa Inatakatisha, Huu Ndio Muonekano wa Sasa wa STEVE YANGA (Shabiki wa Yanga wa Kulia lia)
Huyu kijana alijizolea umaarufu miaka ya nyuma kutokana na tabia yake ya kulia lia sana pale timu yake ya Yanga ilipokuwa ikipokea kichapo alikuwa anashindwa kabisa kujizuia vile vile alihangaika kushiriki kwenye mashindano ya bongo star search lakini hakupata nafasi.



Hii picha kipindi analia baada ya yanga kupokea kichapo
hapa kipindi anatafuta nafasi Bongo  Star Search
 Hapa kipindi anatafuta nafasi Bongo  Star Search


Huu sasa ndio muonekano wa sasa baada ya kula kitengo pale AZAM na yanga kawahama kabisa

NB:jamaa mwanzoni alionekana kama kituko sasa hivi kala kitengo hata harmorapa akiendeleza janja janja za kiki atatusua tu siku moja.

Manji Ashindwa Kufika Mahakamani Kujitetea Kutokana na Tatizo la Kiafya

$
0
0
Manji Ashindwa Kufika Mahakamani Kujitetea Kutikana na Tatizo la Kiafya
Mfanyabiashara Yusuf Manji ameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo August 31, 2017 kujitetea katika kesi inayomkabili ya dawa za kulevya kutokana na sababu za afya.

Hayo yamesemwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Timony Vitalis kwamba kesi hiyo inaendelea na ushahidi.

Hata hivyo, kesi hiyo haikuweza kuendelea baada ya kutolewa taarifa ya Magereza kwamba Yusuf Manji anaumwa na amepewa mapumziko ya kitanda.

Baada ya kuelezwa hayo, kesi imeahirishwa hadi September 18, 2017.


Hizi Hapa Sababu za Zari Kupungua Mwili Mobetto Atajwa

$
0
0

Hizi Hapa Sababu za Zari Kupungua Mwili Mobetto Atajwa
Mwanamitindo Hamisa Mobeto amedaiwa kuwa sehemu ya kupungua mwili kwa mwanadada mjasiriamali maarufu, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’.

Kwa mujibu wa chanzo makini, tangu Mobeto aanze kuibua mjadala mtandaoni kuhusiana na mtoto wake kudaiwa kuwa ni wa bwana wa Zari, mjasiriamali huyo amejikuta akipungua mwili kutokana na mawazo aliyonayo.

“Zari kapungua mwili kweli jamani. Mobeto amemponza. Amemsababishia watu wamtukane sana Zari kiasi ambacho amekosa amani kabisa. Masikini mtoto wa watu kakonda kweli sasa hivi.

“Ukitazama picha za Zari sasa hivi si Zari yule aliyetoka kujifungua. Tena kwa kawaida tunajua mtu ukitoka kujifungua unanenepa lakini kwa Zari mambo yamekuwa tofauti. Ngoja niwatumie picha yake ya sasa muone,” kilisema chanzo.

Hata hivyo mwanahabari wetu aliingia kwenye ukurasa wa Instagram wa Zari na kujionea jinsi alivyopungua baada ya kuona picha zake mpya na kulinganisha na picha zake za zamani.
Licha ya yeye mwenyewe kutozungumzia suala hilo lakini mashabiki wake walisema amefanya vizuri kujipunguza unene kwani sasa ametokelezea tofauti na zamani.

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images