Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

CHADEMA Yatangaza Mgomo Kushindikiza Kutolewa kwa Mbunge wa Tunduma

$
0
0
CHADEMA Yatangaza Mgomo Kushindikiza Kutolewa kwa Mbunge wa Tunduma
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mgogoro na mkuu wa wilaya ya Momba, Juma Irando kwa kuagiza jeshi la polisi wilayani humo kumuweka ndani kwa saa 48 mbunge wa Jimbo la Tunduma, Frank Mwakajoka kwa madai ya uchochezi.

Katika kikao alichofanya na wanahabari, Mwenyekiti wa CHADEMA, Halmashauri ya mji wa Tunduma, Ali Mwafongo ameleezea kusikitishwa na amri hiyo ya mkuu wa wilaya na kusema kuwa kamwe hawatarudi nyuma huku akiahidi kutompa ushirikiano mkuu wa wilaya huyo.

"Uchungu tunaopata sasa hivi tunajua ipo siku itakuwa furaha kwetu kwani ushindi unakaribia. Kinachofanywa sasa hivi wakumbuke ipo siku watawala watakuwa wapinzani na haya yanayofanywa hayataweza kuturudisha sisi nyuma. Viongozi wetu wamekuwa wakipelekeshwa sana lakini katu hatutokata tamaa kwa sababu ni kazi yetu kusema ukweli na kuwatumikia wananchi wetu" alisema
Mbali na hayo mkuu huyo wa wilaya pia ametuhumiwa kutoa amri ya kushusha bendera za chama hicho hali ambayo imeonesha kuwakera baadhi ya viongozi wakiwemo madiwani.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo, Juma Irando amekiri kutoa amri ya kukamatwa kwa mbunge huyo kwa madai kuwa ametoa kauli ya kudharau mamlaka ya uteuzi.
Mbunge Mwakajoka amekamatwa jana Jumanne na kuwekwa ndani ikiwa ni siku moja tu baada ya Mbunge mwingine wa Jimbo la Vwawa, Paschal Haonga kukamatwa na jeshi la polisi.




Video: Waziri Mwigulu Afunguka Suala la Wakimbizi wa Burundi Kurudishwa

$
0
0
Video: Waziri Mwigulu Afunguka Suala la Wakimbizi wa Burundi Kurudishwa
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba anazungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Wakimbizi wa Burundi…tazama




Ajira Lukuki Zamwangwa Kibiti na Serikali

$
0
0
Ajira Lukuki Zamwangwa Kibiti na Serikali
HALMASHAURI ya Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani imetangaza nafasi 45 za ajira kwa wanaotaka kuwa watendaji wa vijiji wilayani humo.

Imesema imetangaza ajira hizo, ili kupata watendaji wa vijiji watakaoziba mapengo ya waliofariki na walioachishwa kazi kutokana na kuwa na elimu ya darasa la saba.

Kibiti ni miongoni mwa wilaya za mkoa wa Pwani ambazo kwa miaka miwili iliyopita, zimekumbwa na mauaji ya viongozi wa ngazi mbalimbali, wakiwamo watendaji na wenyeviti wa vijiji.

Mauaji hayo yalikuwa yakitekelezwa na watu wasiofahamika, waliokuwa wakivamia nyumba za watendaji hao na kuwaua kwa kuwapiga risasi.

Wilaya nyingine za mkoa huo zilizokumbwa na mauaji hayo ni Rufiji na Mkuranga.

Aidha, kutokana na kushamiri kwa mauaji hayo na vitisho vilivyokuwa vikitolewa na wauaji, baadhi ya watendaji wa vijiji waliripotiwa kukimbia makazi yao wakihofu kuuawa.

Akizungumza na Nipashe kwa simu jana, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, Alvera Ndabagoye, alisema hali ya wilaya yake kwa sasa ni shwari.

Kutokana na kurejea kwa hali ya utulivu wilayani humo, Ndabagoye alisema wameona sasa kuna haja ya kutangaza nafasi za kazi 45 za watendaji wa vijiji.

Ushwari huo unatokana na juhudi za Jeshi la Polisi, mkuu wake Inspekta Generali (IGP) Simon Sirro, ambaye baada ya kuteuliwa amefanikiwa kukomesha mauaji hayo huku jeshi hilo likitangaza kuwaua watuhumiwa 13 wa mauaji hayo kwa mpigo katika shambulizi moja, na wengine kukimbia.

Akifafanua tangazo lake la ajira, Ndabagoye alisema: "Tumetangaza nafasi hizi, ili kuziba pengo la wale ambao wana elimu ya darasa la saba ambao wanatakiwa kupisha wenye elimu ya juu zaidi."

Alisema, pia nafasi hizo zinatokana na kuhitaji watendaji wa vijiji watakaoziba mapengo ya waliofariki.

Alisema mwombaji anatakiwa kuwa na ufaulu wa elimu ya kidato cha nne au sita, aliyehitimu mafunzo ya astashahada au cheti katika fani za utawala, sheria, elimu ya jamii, usimamizi wa fedha, maendeleo ya jamii au sayansi ya sanaa kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma au chuo chochote kinachotambuliwa na serikali.

Alisema miongoni mwa kazi ambazo watatakiwa kuzifanya ni kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unaimarika.
Alisema mwisho wa kutuma maombi hayo ni Septemba 11, mwaka huu.

Mapema mwaka huu Katibu tawala wa Wilaya hiyo, Milongo Sanga, katika kikao cha robo mwaka cha baraza la madiwani, kilichokuwa kikijadili maendeleo ya wilaya hiyo, alisema watendaji wa vijiji vilivyoko wilayani Kibiti wamezikimbia ofisi zao kwa hofu ya mauaji, hivyo kusababisha shughuli mbalimbali za kijamii kukwama.

Katibu Tawala huyo aliwaondoa hofu watendaji hao, hata hivyo, na kuwataka warejee katika ofisi zao, ili kuendelea kutoa huduma kutokana na kuwapo na hali ya amani.

MATUKIO YA MAUAJI
Tangu mwaka 2015, kumekuwa na matukio ya mauaji ya viongozi na askari polisi mkoani Pwani.

Baadhi ya matukio ya kuuawa kwa viongozi mkoani humo ni la usiku wa kuamkia Juni 28, mwaka huu, ambalo viongozi wawili wilayani Kibiti waliuawa na kundi hilo kwa kupigwa risasi.

Waliouawa siku hiyo ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mangwi, Maiko Nicholaus na Mtendaji wa Kijiji cha Mangwi kilichopo Kata ya Mchukwi wilayani humo. Katika tukio hilo, wauaji pia walichoma moto nyumba za viongozi hao na kutokomea kusikojulikana.

Mauaji hayo yalitokea ikiwa ni wiki tangu kuuawa kwa kupigwa risasi kwa askari wawili wa Kikosi cha Usalama Barabarani wakiwa kazini katika kijiji cha Msafiri, Kata ya Bungu wilayani humo.

Mbali ya kuwaua askari hao, wauaji walichoma moto gari moja na pikipiki moja ya askari hao kisha kutokomea kusikojulikana.

Mei mwaka jana, matukio matatu yalitokea ambayo ni pamoja na kuuawa kwa kupigwa risasi kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyambunga, Saidi Mbwana.

Oktoba aliuawa Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Nyambuga, Ally Milandu baada ya kuvamiwa na watu wanne waliomshambulia kwa kumpiga risasi.

Novemba wenyeviti wawili wa vitongoji vya Kijiji cha Nyambunda waliuawa kwa kupigwa risasi kabla ya kuuawa kwa mfanyabiashara Oswald Mrope ambaye alipigwa risasi mbele ya familia yake katika kitongoji cha Mkwandara, kilichopo Kijiji cha Nyambunga Januari mwaka huu.

Februari yalitokea matukio mawil; la kwanza likihusisha majambazi waliovamia nyumba ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Jaribu, Bakari Msanga ambaye alifanikiwa kutoroka, lakini wahalifu hao walirejea na kuimwagia mafuta nyumba yake na kuichoma moto.

Tukio la pili katika mwezi huo ni la mauaji ya Ofisa Upelelezi wa Wilaya ya Kibiti (OC-CID), Peter Kubezya na Ofisa wa Misitu ambaye alikuwa Mkaguzi wa Kituo cha Ukusanyaji Mapato ya Ushuru katika Kijiji cha Jaribu, Peter Kitundu na mlinzi Rashid Mgamba ambao waliuawa kwa kupigwa risasi.

Machi Jeshi la Polisi liliripotiwa kuwaua watu watatu katika Daraja la Mkapa walipojaribu kukwepa vizuizi vitatu va barabara wakiwa na pikipiki likiwatuhumu kuwa sehemu ya kikundi kinachoendesha mauaji hayo.

Aprili askari nane waliokuwa kwenye gari la polisi wakitoka kubadilishana lindo na wenzao, walipofika eneo la Mkengeni, Kata ya Mjawa wilayani Kibiti, walishambuliwa na majambazi na saba kati yao, waliuawa kwa risasi huku mmoja akijeruhiwa.

Mei viongozi wawili; kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani, Amir Chanjale na aliyekuwa katibu wa chama hicho, Kata ya Bungu wilayani Kibiti, Arife Mtulia waliuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.


Dkt. Makongoro Mahanga Akamatwa na Kufikishwa Mahakamani

$
0
0
Dkt. Makongoro Mahanga Akamatwa na Kufikishwa Mahakamani
Mbunge wa zamani wa Ukonga na Segerea, Dk Makongoro Mahanga amekamatwa na Polisi Mkoa wa Ilala kwa amri ya Mahakama Kuu na amefikishwa mahakamani.

Mahakama iliamuru Dk Mahanga akamatwe na kufikishwa mahakamani kwa kushindwa kutekeleza uamuzi unaomtaka amlipe mdai Kainerugaba Msemakweli Sh14 milioni.

Fedha hizo ni gharama za kesi alizozitumia Msemakweli baada ya kushinda kesi ya madai ya kashfa ambayo Dk Mahanga alimfungulia kwa kumtaja kwenye kitabu chake kinachoitwa: “Mafisadi wa Elimu”.

Katika kitabu hicho anamtaja kuwa ni mmoja wa viongozi wenye shahada za udaktari wa kughushi.

Kati ya kiwango hicho cha fedha, Dk Mahanga ameshalipa Sh6 milioni hivyo anadaiwa Sh8 milioni.

Wanafunzi Ichini India Wafunzwa Kuhusu Njia za Kutoa Talaka

$
0
0
Wanafunzi Ichini India Wafunzwa Kuhusu Njia za Kutoa Talaka
Shule moja nchini India itaanza kuwafunza wavulana wa Kiislamu njia za kutoa talaka kulingana na sheriza za Kiislamu.

Shule ya Dargh-E-Ala Hazrat inayodhibiti madrassa 15,000 za Kiislamu ilitangaza hilo kufuatia agizo la mahakama lililopiga marufuku talaka za moja kwa moja.
Wasomi wa Kiislamu wamedai kwamba talaka za moja kwa moja haziambatani na sheria ya kiislamu.

Kiongozi mmoja wa dini kutoka shule hiyo amesema kuwa wataanzisha kifungu kitakachoangazia maswala ya talaka.

Mtaala wa shule hiyo ambao unaangazia Koran na sheria za kiislamu unazungumzia kuhusu talaka lakini sio kwa maelezo ya kina.

''Tulifanya mkutano wa viongozi wa dini pamoja na wale wa Madrassa baada ya agaizo la mahakama kuu na tumewaelezea jamii kupitia wanafunzi na katika ibada za siku ya Ijumaa kuhusu njia bora za kutoa talaka'', Maulana Shanbudin Racvi kiongozi mkuu wa dini aliambia BBC Hindi.
Aliongezea kuwa hatua hiyo itaelezea vyema kwamba talaka ya moja kwa moja zinazoetekelezwa nchini India haziambatani na sheria za Kiislamu.

Haijulikani ni umri upi wanafunzi hao wote wakiwa wavulana wenye kati ya miaka mitano hadi 16 watafunza kuhusu talaka.

Upande wa Utetezi Umeeleza Sethi Amewekwa Puto Tumboni Kutokana na Matatizo ya Kiafya

$
0
0
Upande wa Utetezi Umeeleza Sethi Amewekwa Puto Tumboni Kutokana na Matatizo ya Kiafya
Upande wa utetezi umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Singh Sethi amewekewa ‘Puto’ tumboni kutokana na ugonjwa unaomkabili hivyo asipohudumiwa inavyotakiwa anaweza kupoteza maisha.

Mbali ya Seth, mwingine ni Mfanyabiashara James Rugemarila ambapo kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12, yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya TSh 309,461,300,158.

Wakili wa utetezi, Joseph Mwakandege amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa mteja wake Seth anatakiwa apelekwe Hospital ya Taifa Muhimbili lakini hadi sasa hajapelekwa na ni dhahiri upande wa mashtaka umedharau amri mbili za Mahakama.

”Ugonjwa uliosababisha Seth atakiwe kwenda Muhimbili ni baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa ambapo tumboni kwake kumewekwa Balloon ‘Puto’ hivyo asipohudumiwa ipasavyo inaweza kusababisha kifo, naomba mshtakiwa apelekwe Muhimbili kwa sababu ni Hospitali ya juu na yenye vifaa na watalaamu wa kutosha“


Akijibu hoja hizo, Wakili wa Serikali Vitalis Peter amedai kuwa Magereza hawapangiwi wampeleke wapi mshtakiwa ambaye ni mgonjwa bali wana utaratibu, Hospitali na watalaam wao.

”Mshtakiwa alianza kupelekwa Hospital ya Magereza, kisha Hospital ya Amana ambapo alikutana na daktari mtalaam kutoka Muhimbili na aliweza kumuangalia afya yake, hivyo hoja ya kwamba hatujatekeleza amri ya Mahakama sio kweli.”

Baada ya kusema hayo, Hakimu Shahidi amesema alishatoa amri mara mbili kwamba Seth akatibiwe Muhimbili na kusisitiza akatibiwe >>>”Nasisitiza tena, mshtakiwa akatibiwe Muhimbili, sioni kama kuna sababu ya kulumbana, kesi imeahirishwa hadi September 14, 2017.”


Mkuu Wa Mkoa Mjini Magharibi Atoa Taarifa Kuhusu Sikukuu Ya Eid El Hajj Kesho

$
0
0
Mkuu Wa Mkoa Mjini Magharibi Atoa Taarifa Kuhusu Sikukuu Ya Eid El Hajj Kesho
Ndugu wananchi wakaazi wa Mkoa wa Mjini Magharibi wasikilizaji na watazamaji.
ASSALAMU ALAYKUM,

Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyenzi Mungu kwa kutujaalia neema ya uhai, uzima, amani na utulivu katika Mkoa wetu wa mjini Magharibi.

Ndugu wananchi kama mjuavyo kuwa siku ya Ijumaa ya tarehe 1/9/2017 tutasherehekea sikukuu ya Eid El Hajj ambapo waislamu wote duniani wataungana na mahujaji waliopo Makka Saudi Arabia baada ya kukamilisha nguzo ya tano ya kiislam kwa kutekeleza ibada ya Hijja ambayo ni lazima kwa mwenye uwezo.

Ndugu wananchi pamoja na wakaazi wote wa Mkoa wa Mjini Magharibi  napenda nichukuwe fursa hii  kutoa taarifa inayolenga kuwanasihi na kukumbushana mambo muhimu ya kuzingatiwa  katika kipindi chote cha skukuu na  baada ya skukuu ndani ya Mkoa wa Mjini Magharibi ili kuendeleza na kudumisha amani iliyopo.

Kwa mwaka huu wa 2017 swala ya eid itafanyika Wilaya ya Magharibi B katika kiwanja cha Dimani na Baraza la Eid litafanyika Bweleo katika eneo la mapumziko la wananchi karibu na nyumba mpya za Fumba.

Jambo la msingi nawaomba wananchi wote tusherehekee sikukuu hii katika hali ya Amani na utulivu kama ilivyo desturi yetu.

Napenda kuwahakikishia wananchi kuwa Serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama itaendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ndani ya Mkoa katika kipindi chote cha sikukuu.

Vilevile, vitendo vya ukiukwaji wa sheria za usalama wa barabarani vinavyofanywa na baadhi ya madereva wazembe  vitadhibitiwa na kutakuwa na operesheni maalum ya ukaguzi wa vyombo vyote vya moto yakiwemo magari na vyombo vya magurudumu mawili.

Tahadhari ya kudhibiti mwendo itachukuliwa kwa kuwekwa vizuizi katika maeneo mbali mbali ya barabara ili kuepusha ajali zinazoweza kugharimu uhai wa wananchi wetu.

Hivyo, napenda nitoe wito kwa madereva wa vyombo vya moto hasa madereva wa daladala na wamiliki wa vyombo binafsi vya usafiri kuchukua tahadhari ya hali ya juu hususan wakati wa jioni    wanapowapeleka watoto  katika viwanja vya skukuu. Aidha, tunawaomba watumiaji wa vyombo hivyo kuhakikisha kuwa vyombo vyao vimekaguliwa na mamlaka husika za ukaguzi na kupatiwa ruhusa ya kukubalika kwa vyombo hivyo kutumika barabarani kisheria ikiwa ni pamoja na kuwa na leseni ya njia(road licence) pamoja na bima (insurance). Hivyo, kwa taarifa hii, Mkoa unaagiza kuwa wale wote ambao vyombo vyao havijapasishwa na mamlaka husika, wasiviingize vyombo hivyo barabarani kwani kufanya hivyo ni kuvunja sheria za nchi na kusababisha ajali zinazoweza kuepukika.

Pia, naomba nitumie fursa hii kuwakumbusha madereva na utingo wa daladala kutopandisha  viwango vya nauli nyakati za usiku kwa njia zote za  Mkoa wa Mjini Magharibi.
Kuhusu Viwanja vya sikukuu, vitakavyotumika ni  (29) na vitaanza shughuli zake wakati wa alasiri na muda wa kufunga utatofautiana kutokana na mazingira ya viwanja hivyo kama ifuatavyo.

Wilaya ya Mjini
Viwanja vya skukuu  ambavyo vitatumika ni Mnazimmoja, Viwanja vya Demokrasia (Kibandamaiti), Kariakoo, Mnara wa kumbukumbu (mapinduzi square), Jamhuri Garden, Mnazi mmoja na Forodhani park mbapo viwanja hivi vyote vitaanza shughuli zake kuanzia saa 10:00 jioni na kufungwa saa 4:00 usiku.

Wilaya ya Magharibi “A”:
Viwanja vitakavyotumika ni kiwanja cha Dole, Kihinani Melinane, skuli ya Mbuzini, Jazira Kigorofani, Jazira, Skuli ya maandalizi ya Mfenesini na Zanzibar Park (Viwanja hivi vitaanza saa 10:00 na kumaliza saa 4:00 usiku.

Viwanja vyengine ni Skuli ya Maandalizi Mfenesini, Garagara, Kijichi kwagube, Stella Darajabovu, Kihinani Zantel, Skuli ya Regezamwendo na Mwakaje (Viwanja hivi vitaanza saa 10:00 na kumaliza saa 1:00 usiku)

Wilaya ya Magharibi “B”
Viwanja vitakavyotumika ni : Skuli ya Sekondari Biashara, Viwanja vya Magereza, Maungani, Kwa bamgeni Pangawe, Kiembesamaki kwa Abdalla Rashid, Kinuni, na Fumba (Viwanja hivi vitaanza saa 10:00 jioni na kumaliza saa 4:00 usiku)

Viwanja vyengine ni : Nyarugusu, Magirisi na Skuli ya Private Kwarara Progressive ambavyo vitaanza saa 10:00 jioni na kumaliza saa 1:00 usiku)

Viwanja ambavyo havikutajwa havitaruhusiwa kufanyika skukuu.
Aidha, Kwa upande wa Wilaya ya Magharibi “B” kutakuwa na kiwanja kipya cha skukuu katika eneo la kupumzikia la fukwe ya bahari ya fumba eneo linalojengwa nyumba za  kisasa za makaazi fumba.
Serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na Idara ya Usafiri na leseni imeandaa usafiri maalum wa daladala ya rout ya Fumba kwa lengo la kuwarahisishia wananchi kufika na kurudi katika kiwanja kipya cha skuu kiliopo fumba kwa urahisi.

Ndugu wananchi, nachukua nafasi hii kuendelea kukumbusha kuwa suala la upigwaji muziki ni marufuku katika viwanja vyote vya  sikukuu, wakati ambapo katika vilabu na kumbi za starehe  wataendelea kufuata utaratibu wa muda uliowekwa  na Serikali ambapo watatakiwa kupiga muziki kuanzia saa 2:30 usiku na kumaliza sa 6:00 usiku. isipokuwa holi la bwawani na ukumbi w ngalawa ambayo mwisho ni saa 8 usiku.

Serikali ya Mkoa itaendelea kufuatilia utekelezwaji wa maagizo haya na kuwachukulia hatua za kinidhamu kwa mujibu wa sheria wale wote watakaokiuka taratibu hizi.

Ndugu wananchi kuhusu uuzwaji wa vyakula katika viwanja vya skukuu nawaomba sana wafanya biashara wote kufuata taratibu na miongozo iliyowekwa na serikali kupitia  Mabaraza ya manispaa kwa kushirikiana na Wizara ya afya kwa kupata vibali vya kufanya biashara pamoja na kuimarisha usafi wakati wote ili kuepusha athari zinazoweza kutokea ikiwemo mripuko wa maradhi ya kipindupindu.

Ndugu wananchi Napenda nitoe nasaha zangu kwenu wazazi na walezi kutowaacha watoto wadogo kutembea peke yao katika barabara na viwanja vya sikukuu ili kupunguza tatizo la kupotea kwa watoto katika kipindi hicho.

Kabla ya kumalizia taarifa yangu hii, ninawakumbusha wananchi wote kufuata maagizo ya Serikali kwa kutii sharia bila ya shuruti.

Ndugu wananchi kwa kuwa hivi sasa nakaimu nafasi ya Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja naomba nitumie fursa hii kuwanasihi wananchi wezangu wa Mkoa huo kuendelea kudumisha amani na utulivu katika kipindi hiki cha sikuu na siku zijazo.

Namuomba Mwenyezi Mungu atujaalie kuendelea kuwa na Amani na utulivu katika Mkoa wetu wa Mjini Magharibi na Mkoa wa Kaskazini unguja na Zanzibar kwa ujumla

Tunamuomba Mwenyezi Mungu awajaalie ndugu zetu waliokwenda kutekeleza ibada ya hijja awakubalie hijja zao na warejee nyumbani wakiwa salama.

Na kwale ambao  bado hawaja jaaliwa kwenda kutekeleza ibada hiyo tumuombe Mwenyezi Mungu kwa Baraka zake atushushie neema hiyo ili nasi tuweze kutekeleza nguzo hiyo ya kiislam.
Eid Mubarak.


‘Seduce Me ya ALI KIBA’ Yaipiga Tena Kikumbo ‘Zilipendwa’, Yarudi Kileleni kwa Kishindo

$
0
0
Mafahari wawili wakishindana zinazoumia ni nyasi. ‘Sedece Me’ na ‘Ziipendwa’ zazidi kupigana vikumbo katika Mtandao wa YouTube.

Ngoma ya ‘Sedece Me’ yarudi kwenye kiti chake cha namba moja trending kwenye mtandao huo baada ya kupokonywa nafasi hiyo kwa masaa kadhaa na wasanii wa WCB kupitia wimbo wao mpya, Zilipendwa.

Alikiba kupitia wimbo wake huo alikaa katika nafasi hiyo ya uongozi kwa siku tano huku wimbo huo ukiwa umetazamwa zaidi ya mara 2.5 milioni huko YouTube kabla ya kushushwa Jumatano hii na wimbo wa ‘Zilipendwa’ wa WCB ambao nao walionja kukalia kiti hicho kwa masaa machache na kurudisha kijiti kwa aliyekuwa nacho.

Mpaka sasa ‘Seduce Me’ tayari umejitengenezea rekodi kadhaa kwenye mtandao huo ikiwemo kufikisha views milioni moja ndani ya masaa 38.

Pamoja na Umaarufu Alio nao ALIKIBA Kwa Nini Bado Maskini na Diamond Platnumz ni Mwanamuziki Tajiri?

$
0
0
Naombeni uzii huu usichukuliwe kiushabiki bali uchukuliwe kama haki ya kila mtu kutoa ya moyoni pasipo kuvunja sheria

Kwa mda mrefu msanii Alikiba amekuwa yupo kwenye game la mziki na amejizolea umaarufu mkubwa kwa kazi zake nzuri na kujipatia mashabiki wengi huku wengine wakimuita "KING" wa bongofleva.

Lakini pamoja na umaarufu wake alionao na mashabiki wengi aliojizolea lakini bado Alikiba ni mtu mwenye maisha ya ya chini tu ambayo hayafanani kabisa na umaarufu wake

Tukija upande wa pili wa mwanamuziki Naseeb Abdul ~Diamond Platnumz yeye si wazamani sana kwenye game kama alikiba lakini nayeye ametokea kufanya kazi nzuri na kujizolea mashabiki wengi na umaarufu lakini hajaweza kufikia record ya The king himself Alikiba

Lakini ukija kwenye maswala ya maendeleo ambayo ndio kipimo cha kazi anayofanya msanii utagundua kuwa Diamond platnumz amejizolea utajiri wa kutisha zaidi ya King himself Alikiba.

Kutokana na kazi ya mziki Diamond platnumz ameweza kujipatia utajiri mkubwa ikiwemo kuachia mijengo mingi ya maana hapa town na mengine South Africa. Diamond amefunguka zaidi kwa kuanzisha biashara zake za Chibu perfume na Diamond karanga ambazo zinafanya vizuri nzuri sokoni bila kusahau mikataba yake ya matangazo na makampuni makubwa wakati king Kiba hana biashara ya maana wala maendeleo yoyote kumzidi Naseeb


Diamond platnumz amejenga ofisi yake ya kisasa na kufungua studio yake ya wasafi records ambayo inahusika kutengeneza ngoma zote za wasafi na wasanii wengine kutoka nnje kitu ambacho Alikiba hadi leo hana ofisi wala studio yake binafsi


Diamond ameanzisha Label yake mwenyewe ya Wasafi records ambayo inawasimamia wasanii wakali kama
~Rich Mavoko
~Harmonize
~Rayvanny
~lavalava
Na mtandao wa wasafi.com ambao anauza nyimbo zake na za wasanii wengine online. Label ya wasafi imekuwa ni chanzo kikubwa cha kupiga mkwanja mrefu kwa Diamond platnumz hadi ilifika kipindi TRA wakamkadiria kodi hadi swala hilo likatinga bungeni

Huku Diamond platnumz ni msanii pekee anaeilipa kodi kubwa serikali kuliko msanii yeyote hapa tz, Akiwapiku wasanii wengi wakongwe na wapya ambao wamekuwa wakimchukia lakini wengi wao hata mlango wa TRA hawaujui nikimaanisha wanaendesha kazi zao kiujanja ujanja lakini Diamond platnumz ameonyesha mfano kwa kuilipa kodi serikali kwa kazi zake zote


Wakati upande wa pili wa Alikiba yeye bado amesainiwa na Sony music na hana label yake mwenyewe wala wasanii anaowasimamia,Na wala sina uhakika kama anailipa kodi serikali kama anavyofanya Platnumz

Ukiingia katika account zao za youtube alikiba ana followers 60,000 na Platnumz anao followers 650,000 na kupitia account zao za youtube Diamond anavuta pesa ndefu kutoka youtube kutokana na video zake nyingi anazoweka kwenye account yake na followers wengi alionao

Diamond platnumz ameweza kutoa ajira kwa
~Mameneja 2
~Madancer 5
~producer 1
~Bodyguard 1
~Photographer 1
~Mtu wa IT 1
~Mbunifu 1
~Muhasibu 1
~wasanii chini ya label yake 5
Jumla 19


Ukipiga hesabu hapo Diamond platnumz anaspend zaidi ya 100 millions kwa ajili ya kulipa mishahara tu kwa crew yake au wafanyakazi wa label yake ya wasafi kwa kila mwezi huku mshahara mkubwa ukienda kwa wasanii walio chini ya lebel yake kulingana na mikataba yao

Ukija upande wa pili wa alikiba yeye ni mwajiriwa tu wa sonny music hamlipi mtu mshahara lakini maisha yake hayafanani kabisa na misifa anayopewa na mashabiki wake Mwisho wa siku utagundua kuwa alikiba anaambulia sifa tu kutoka kwa mashabiki zake mitandaoni kakini Diamond ni real money maker nikimaanisha mashabiki wanaompaka sifa Alikiba mchana ndio hao hao Wanaomtajirisha Diamond platnumz wenyewe

Na wapo watakaokuja kusema hapa kuwa alikiba sio mtu wa show off lakini msema ukweli ni mpenzi wa mungu pesa na maisha aliyokuwa nayo Alikiba hata aizidishe mara 10 hamfikii Diamond platnumz japo watu hao hao wanampaka mafuta mwa mgongo wa chupa alikiba kwa sifa ndio hao hao wanaomtajirisha Platnumz

mziki duniani kote sasa hivi ni pesa ndio mpango mzima lakini najiuliza mziki wa alikiba ni wa kuingiza pesa kutokana na kazi nzuri au ni mziki wa sifa mbona hana maendeleo yoyote?

---------------------------------------------------------------------------------------

USHAURI WANGU KWA PLATNUMZ D

Nakuomba uachane na hili bifu ulilojiwekea na alikiba kwani sio saizi yako kabisa umemzidi kimaendeleo kwa asilimia kubwa na unafanya kazi ya kumpromote tu na sikingine

Diamond platnumz level zako ni za akina Davido yaani ilibidi uweke bifu na mtu ambaye ni saizi yako Nakusihi achana nae na wala usishindane nae kwani yeye ndio anafaidika zaidi na hili bifu na anapenda liendelee. Alikiba saizi yake ni akina Dully sykes,TID,Q CHIEF,Bobjunior ndio wa kuekeana bifu lakini sio wewe

Wewe ni boss wa label kubwa ya WCB na umetoa ajira kwa vijana wengi hivyo huwezi kulingana wala kushindana na msanii Local anayefanya kazi chini ya label asiye na brand yake anayetegemea media kumpromote, hana studio wala ofisi yani yupo yupo tu,huko ni kujiaibisha tu

By mtotomtamuu

Kutana na Mtatibu Wanyota za Binadamu Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka Comoro

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU WANYOYA ZA BINADAMU DUNIANI KOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO

KWA SASA YUPO TANZANIA MAALIM FADHILI RASHIDI ANA IWEZO WAKUJUWA JAMBOLAKO NAKULI TATUWA KWAMUDA MFUPI

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE

MAALIM FADHILI RASHIDI NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA MIGUU KUWAKA MOTO

KISUKARI VIDONDA VYATUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI PUMU ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIE POTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM ANATOWA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI YEYOTE

NAKUMILIKI MALIZA MAJINI KWAYULE ANAE HITAJI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZA KIUME ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASA (24)

ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YAMVUTO WABISHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE

KUSAFISHA NYOTA NAKUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHAKUTESEKA NJOO UWONE MIUJIZA YA MAALIM FADHILI RASHIDI

CALLING+255719362806/ +255763276239

KWA WHATSAPP IMO +255785786436

BREAKING NEWS: Kamati ya Nidhamu TFF Yawatolea Tamko Msuva, Chirwa NA Kaseke

$
0
0
BREAKING NEWS: Kamati ya Nidhamu TFF Yawatolea Tamko Msuva, Chirwa NA Kaseke
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imemkuta na makosa ya utovu wa nidhamu aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga anayekipiga nchini Morocco, Simon Msuva ambaye imempa onyo kali la barua.

Mbali na Msuva, wengine waliokuwa wakijadiliwa na kamati hiyo kwa utovu wa nidha kwenye michezo ya mwisho ya Ligi Kuu Tanzania Bara ni Obrey Chirwa (Yanga) na Deus Kaseke (Yanga) ambao wamesamehewa.

 

Serikali Yataifisha Magari Yaliyoingizwa Nchini Kinyume cha Sheria

$
0
0
Serikali Yataifisha Magari Yaliyoingizwa Nchini Kinyume cha Sheria
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetaifisha jumla ya magari sita yakiwepo magari matatu aina ya Ranger Rover Sports yaliyoingizwa nchini kinyume na sheria baada ya watuhumiwa hao kukiri kuwa wamefanya kosa hilo.

Rais Magufuli mwezi Machi mwaka huu alipokwenda bandarini alikuta kuna makontena yenye magari ndani yake huku wamiliki wa makontena hayo wakidai  makontena hayo yalikuwa na nguo na mabegi  lakini baada ya kufunguliwa zilionekana gari za kifahari zikiwa kwenye makontena hayo, jambo ambalo lilionekana wamiliki wa mahari hayo walikuwa wakiingiza magari hayo kinyume na utaratibu na sheria za nchi.

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, DPP Biswalo Mganga amesema kuwa baada ya mahakama kuwakuta na hatia raia hao wakigeni ambao walidai kuwa kontena hizo zilikuwa na nguo na mabegi wakati ni magari hivyo serikali imetaifisha magari yao na sasa kuwa magari ya serikali.

"Rais hao wamekiri makosa yao yote mawili na kutokana na kukiri kwao mahakama imewatia hatiani na ikaamuru yale magari yote matatu kuyataifisha kuwa mali ya serikali na kila mmoja anatakiwa kulipa faini ya milioni 133 kufidia hasara ambayo serikali imepoteza na kila mmoja anatakiwa kulipa tena milioni tano kama faini ambayo mahakama imewalipisha , wakishindwa kulipa faini hiyo watakwenda jela miaka mitatu" alisema Biswalo

Aidha Biswalo amesema kuwa magari yote sita ambayo Rais Magufuli aliyakuta bandarini yametaifishwa na kuwa mali ya serikali

Mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu Rais Magufuli alifanya ziara ya kushtukiza bandarini na kukuta kuna makontena ambayo wamiliki wake walidai ni makontena ya nguo na mabegi na nyaraka zilionyesha hivyo lakini yalipofunguliwa zilikuwa ni gari za kifahari, hivyo watu hao walikuwa wakikwepa kulipa kodi na kuitia hasara serikali.

Agnesi Masogange Akutwa na Kesi ya Kujibu Atakiwa Kujitetea

$
0
0

Agnesi Masogange Akutwa na Kesi ya Kujibu Atakiwa Kujitetea
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imesema video Queen, Agnes Gerald ‘Masogange’ ana kesi ya kujibu katika kesi ya kutumia dawa za kulevya, hivyo anapaswa kujitetea.

Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri amesema kuwa amekubaliana na hoja za ushahidi wa upande wa mashtaka, ambapo mshtakiwa amekutwa na kesi ya kujibu na ana haki ya kujitetea.

Baada ya kuelezwa hayo, Masogange amesema atajitetea kwa njia ya kiapo na atakuwa na mashahidi 3.

Kesi imeahirishwa hadi October 12, 2017 ambapo Agnes Masogange ataanza kujitetea.




Waliopanga Ratiba ya Ligi Kuu Kuwajibishwa na TFF

$
0
0
Waliopanga Ratiba ya Ligi Kuu Kuwajibishwa na TFF
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Alfred Kidao amesema kuwa ameagizwa na rais wa Shrikisho hilo, Wallace Karia kumwandikia barua Mtendaji mkuu wa Bodi ya Ligi ili kuwaadhibu viongozi wa Bodi ya Ligi waliohusika na kupanga ratiba.

Kumekuwa na malalamiko kutokana na Bodi hiyo kupanga ratiba ya ligi ambapo walishindwa kuzingatia kuwa kuna michezo ya kimataifa ambayo itahusisha timu za taifa jambo ambalo limesababisha baada tu ya mchezo mmoja tu, ligi hiyo ikapanguliwa tena.

“Nimeagizwa na rais nimwandikie barua mtendaji mkuu wa bodi ya ligi ili aweze kuwachukulia hatua viongozi wa bodi hiyo waliohusika na kupanga ratiba hii pamoja na kwamba walikuwa na kalenda lakini bado wamekosea,” alisema Kidao.

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi ni Boniface Wambura ambaye sasa atakuwa na jukumu la kuchukua hatua kwa wasaidizi wake.

Mahakama Imekataa Kupokea Vielelezo vya Msokoto wa Bangi Kwenye Kesi Inayomkabili Wema Sepetu

$
0
0
Mahakama Imekataa Kupokea Vielelezo vya Msokoto wa Bangi Kwenye Kesi Inayomkabili Wema Sepetu
Bado kesi ya Mwigizaji Wema Sepetu kuhusu bangi inaendelea kwenye Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Dar es salaam ambapo leo ilikua ni siku nyingine tena kesi hiyo imeendelea.

Mpya ya leo ni kwamba Mahakama hiyo imekataa kupokea vielelezo vya ushahidi wa msokoto na vipisi viwili vya bangi vilivyotolewa na upande wa mashtaka katika kesi inayomkabili Wema na wenzake.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo amesema Mahakama haiwezi kupokea vielelezo hivyo kwa sababu vina kasoro >>> “Nakubaliana na hoja kwamba msokoto wa bangi na vipisi vina kasoro kwa kuwa shahidi hakuvifafanua Mahakamani“

Kesi hiyo imeahirishwa hadi September 12/2017.





Kamanda Mkondya Aanza na Kibarua Kigumu Atakiwa Kuwakamata Vigogo Bodi ya Korosho

$
0
0
Kamanda Mkondya Aanza na Kibarua Kigumu Atakiwa Kuwakamata Vigogo Bodi ya Korosho
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Naibu Kamishna Lucas Mkondya, ameanza kazi katika kituo chake hicho kipya kwa kibarua kizito cha kutakiwa kuwakamata vigogo wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) wanaotuhumiwa kusambaza pembejeo zilizopita muda wa matumizi.

DCP Mkondya ambaye kabla ya kwenda Mtwara alikuwa Kaimu kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, ameagizwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego, kuwakamata vigogo hao, akiwamo Mkurugenzi Mkuu wa CBT, Hassan Jarufu.

Dengego aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa, amepokea taarifa kutoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara kuhusu kuwapo kwa dawa za kuua wadudu kwenye mikorosho ambazo zimekwisha muda wa matumizi kwa ajili ya kupelekwa kwa wakulima wa zao hilo katika msimu wa mwaka 2017/18.

Baada ya kupata habari hizo, alifanya ziara fupi kwenye ghala la viuatilifu la Mtwara na kugundua kuna dawa za maji zaidi ya lita 400 zilizokwisha muda wake na zikiwa na vifungashio vyenye majina tofauti na dawa zilizomo ndani.

Vifungashio hivyo vimeonyesha kuwa dawa hizo zilitengenezwa mwaka 2017 huku dawa zilizomo ndani ambazo pia muda wake wa matumizi umeisha zikionyesha kutengenezwa mwaka 2012.

Vigogo wengine wanaotakiwa kukamatwa kwa amri ya Dengego ni Meneja Rasilimali Watu wa Bodi hiyo, Shauri Mokiwa, Mkurugenzi wa Kilimo na Ubanguaji, Luseshelo Silomba na mkurugenzi wa kampuni inayohusika na ulinzi wa ghala hilo.

"Serikali ya mkoa imesikitishwa sana na jambo hili ambalo limeendelea kufanywa na watendaji wa Bodi ya Korosho. Ofisi yangu haitafumbia macho jambo lolote litakaloonekana kutia doa azma ya serikali kuwainua wakulima," alisema Dendego.

Wakati Dendego akitoa amri hiyo, Kamanda Mkondya alisema hadi jana mchana jeshi lake lilikuwa linawashikilia watu watatu kwa tuhuma hizo.

Aliwataja watu haio kuwa ni Felista Onestina ambaye ni mtunza ghala na katibu mahususi wa Mkurugenzi Mkuu wa CBT, Emiliana Salia na Husna Rajabu wote wakiwa watunza ghala.

"Bado tunaendelea na ufuatiliaji wa tukio hili hadi ngazi za juu ili kuhakikisha watuhumiwa hawa tunawakamata kwa ajili ya mahojiano na hatua zaidi," alisema Mkondya.

Wamachinga wa Ubungo Wapewa Siku 3 Kuondoka

$
0
0
Wamachinga wa Ubungo Wapewa Siku 3 Kuondoka
WAFANYABISHARA wadogo wadogo, maarufu kama wamachinga, zaidi ya 2,000 walio katika makutano ya barabara za Morogoro, Sam Nujoma na Mandela katika eneo la Ubungo Mataa, Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam-

Wamepewa siku tatu kuondoka katika maeneo hayo kwa hiari, ili kupisha ujenzi wa mradi wa barabara za juu (fly over).

Baada ya amri hiyo, wamachinga hao waliridhia kuhamia katika soko la Mawasiliano, ambalo limetengwa na Manispaa ya Ubungo kwa ajili yao, baada ya kufanya mazungumzo na Meya wa Manispaa hiyo, Boniface Jacob.

"Tunawapa siku tatu, leo (jana) endeleeni na shughuli zenu hadi Jumamosi mchana muanze kuondoka," alisema Meya Jacob. "Atakayekutwa hapa Jumapili, mimi simo."

Alisema aliamua kufanya mazungumzo na wamachinga hao, ili kuwapatia suluhisho la wapi pa kwenda kufanya biashara zao badala ya kuwaacha na maswali.

Aidha, Meya Jacob alisema wametenga eneo lenye ukubwa wa hekari 12 katika kituo cha Mawasiliano, ambacho ni moja ya vituo vikubwa vya daladala, ambalo litatosha wafanyabiashara 5,000.

"Wamachinga mlioko kando ya barabara eneo hili la Ubungo ni 2,000," aliwaambia meya huyo. "Mawasiliano kuna eneo la kutosha la wafanyabiashara 5,000."

"Hivyo nawasihi kuhamia kule na kama atakuwapo atakayelazimisha kubaki hapa ahakikishe anakaa nje ya mipaka iliyoweka kwa ajili ya kazi hii au kwenda eneo lolote ndani ya jiji la Dar es Salaam."

Jiwe la msingi la mradi huo liliwekwa na Rais John Magufuli mahala hapo Machi 20, mwaka huu.

Rais Magufuli, katika hotuba yake ya uzinduzi, alitaka ujenzi ukamilike kabla ya miaka miwili na nusu ya ratiba ya ujenzi.

BILIONI 186.8/-
Jacob pia alisema vijana wenye ujuzi mbalimbali watapata ajira katika mradi wa flyover na kwamba mama lishe ameshawapatia fursa ya kuwauzia chakula wafanyakazi na vibarua zaidi ya 5,000 watakaohusika na mradi huo.

Mradi wa flyover Ubungo utajengwa na mkandarasi kampuni ya China ya CCECC kwa Sh. bilioni 188.7, ambapo kati ya hizo, Benki ya Dunia (WB) imetoa Sh. bilioni 186.8 na serikali Sh. bilioni 1.9 za usanifu mradi.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Kayombo, alisema mradi huo unatarajiwa kuanza muda wowote. Alionyesha mipaka, kuzungumza na wafanyabiashara hao pamoja na kuwapa muda wa kuondoka eneo hilo.

Mfanyabiashara katika eneo hilo la Ubungo Mataa, Jumanne Nasoro, alisema hawana budi kupisha eneo hilo kwa sababu wasipopisha wanaweza kuharibiwa mali zao.

Pia aliiomba serikali kukarabati na kuweka miundombinu imara katika masoko wanayopangiwa kuhamia, ili kuondokana na changamoto ya wateja kutokuingia humo kwa sababu mbalimbali.

Wakati huo huo, Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob amesema wameanza ukarabati wa soko na eneo la Mawasiliano kwa ajili ya kurahisisha kuingia na kutoka ndani ya soko hilo.

"Kuna mpango pia wa kupitisha barabara ya mwendo kasi kwa ajili ya kushusha abiria katika kituo cha Mawasiliano hali ambayo itasaidia kuboresha biashara katika soko letu katika siku za usoni," alisema Jacob.
 

Wolper Alizwa na Umati wa Vijana Uliojitokeza Jana Kufanya Usail TRA

$
0
0
Wolper Alizwa na Umati wa Vijana Uliojitokeza Jana Kufanya Usail TRA
Msanii wa filamu bongo, Jacqueline Wolper aumizwa baada ya kuona idadi kubwa ya watu waliojitokeza kufanya usaili wa TRA jana na kusema anawaonea huruma yatima ambao hawana mtu wa kuwapigania ili kuweze kupata kazi hizo.

Wolper amebainisha hayo baada ya picha iliyokuwa ikionyesha umati wa vijana waliojitokeza kwa wingi kufanya usaili  wa TRA kwa awamu ya kwanza ambao umefanyika jana na kuendelea leo ambao umeandaliwa na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

"Nikiangalia picha kama hizi naumiaga sana na nilivyo na machozi ya karibu basi nalia kabisa. Yaani naona hata wadogo zangu ni miongoni mwa hawa wanaopigania nafasi ya kupewa kazi na ukizingatia nimesomesha kwa tabu sana tena nilikuwa sina hata biashara huku nikisaidiana na wazazi wangu. Roho inauma pale ambapo mdogo wako anakwambia Dada nimepata kazi ya kujishikiza kwa wiki tatu nitalipwa laki na nusu kule Mkoani Mbeya kijijini tena hapo ni uliyemfikiria akipata 'degree' yake atakuja japo kuinua familia ama ajitegemee mwenyewe lakini siyo hivyo", aliandika Wolper.

Pamoja na hayo, Wolper aliendelea kwa kusema "mimi najiuliza unaposema ipo siku sijui hiyo siku ni ipi. Haya wote hao waliojitokeza huku wanaohitajika ni wachache yaani kwa uwiano ni kama mtu mmoja achaguliwe kati ya watu 140 kwa sababu ni watu 56,000 kwa nafasi 400 kama 'data' ziko sahihi, Mungu wangu bora hata mdogo wangu ataomba hela ya vocha na kula na kulala atapata. Lakini vipi waliyosomeshwa na wazazi wa kambo au kwa msaada", alihoji Wolper.
Huu ndiyo ujumbe aliyoandika Wolper katika instagram yake.

Jacqueline Wolper siyo mtu wa kwanza kuonyesha hisia zake juu ya tukio lililotokea siku ya jana katika usaili huo kwa maana kila aliyeweza kuona picha hiyo hakuweza kujizuia kutoa dukuduku lake la moyoni.

Jeshi la Polisi Lawaonya Wakina Amber Lulu na Wengine Wanaopiga Picha za Utupu na Kuzirusha Mitandaoni

$
0
0
Jeshi la Polisi Lawaonya Wakina Amber Lulu na Wengine Wanaopiga Picha za Utupu na Kuzirusha Mitandaoni

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam limetoa onyo kwa watu wanaopiga picha za utupu na kuzirusha mitandaoni, huku likisema kuwa litawachukulia hatua watu hao kwani wanavunja sheria.

Akizungumza na mwandishi wa East Africa Television, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP), Lazaro Mambosasa, amesema vitendo hivyo ni uvunjaji wa sheria za makosa ya kimtandao na haviwezi kuvumilika.

“Hilo ni kosa kama kosa lingine, ni uvunjaji wa sheria za makosa ya kimtandao, mtu yeyeote akija kulalamika Jeshi Polisi halitalifumbia macho, kwa sababu vitendo hivyo ni udhalilishaji wa utu wa mtu wa hali ya juu na haviwezi kuvumilika, ukithibitika unafanya kitendo hicho Jeshi la Polisi halitakuacha salama, litakuchukulia hatua kwa mujibu wa sheria”, alisema Kamanda Mambosasa.

Vitendo vya upigwaji wa picha za utupu na kuwekwa kwenye mitandao ya kijamii vimekuwa vikishamiri nchini Tanzania, ambapo hivi karibuni msanii Amber Lulu alifikishwa katika kituo cha polisi cha Ubungo kwa kosa hilo

MADEE: Sikuwahi Kuwa na Ugomvi na Afande Sele Ila Tulikua Tunagongana Kimashairi

$
0
0
MADEE: Sikuwahi Kuwa na Ugomvi na Afande Sele Ila Tulikua Tunagongana Kimashairi
Msanii wa Bongo Flava kutoka Tip Top Connection, Madee amedai hakuwahi kuwa na tatizo na Afande Sele kama ilivyokuwa ikisemekana.

Madee ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Sikila’ ambayo amemshirikisha Tekno kutoka Nigeria amesema kilichokuwa kinatokea kati yao ni kugongana kwa mashairi.

“Hamna tatizo, kwani kulikuwa na tatizo, matatizo yalikuwa kwenye mashairi ndio yalikuwa yanasuguana. Hatujawahi kuwa na mataizo mashairi ndio yana mataizo yanapokutana huko redioni lakini tukikutana bro vipi na ni mtu muhimu sana kwangu,” amesema Madee.

“Nimemuangalia kuna vitu vingi sana nimejifunza kupitia yeye. Hivi vitu vilikuwa vinazungumzwa na watu tu, watu ndio huwa wanatengeneza haya mambo,” ameiambia Bongo5.

Kwenye wimbo wa Madee, ‘Nisikilize’ Madee aliwahikusema ‘yule mkulima alidai eti namgeza, alitamba zamani miaka hii hajaweza, anaumia kwanini mwanzo alicheza, hawezi kuosha nywele ana uhaba wa fedha’.

Pia katika wimbo wa Afande Sele ‘Kingdom’ kuna mstari unasema ‘hip hop itakulipa vipi wakati unaimba matusi, unatukana ma-ras, unadiss waasisi halafu bado unadiriki kujiita rais wakati huna hata ofisi labda ni rais wa huko kwenu uwanja wa fisi’

Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images