Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

UKATILI...Mwanamke Ashikiliwa na Polisi Kwa Tuhuma za Kumpaka Pilipili Ukeni Binti yake

$
0
0

Mahakama ya Karmo Jijini Abuja nchini Nigeria inamshikilia mwanamama Mercy Segun, 42 kwa tuhuma za kutia pilipili katika uke wa mtoto wake na kumsababishia maumivu makali.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa siku ya Jumatano Agosti 30, 2017 na anashikiliwa kwa makossa matatu ya jinai, shambulio la mwili pamoja na kumsababishia maumivu makali mtoto huyo mwenye umri wa chini ya miaka 18.

Jirani wa mama huyo aitwaye Gift, alitoa taarifa ya tukio hilo katika kituo cha polisi cha Karmo ambapo Polisi walifanya uchunguzi na kumtia mbaroni mama huyo mara moja. Mpelelzi wa Polisi Florence Auhioboh aliieleza mahakama

JE, ni Kweli Diamond Anafanyiwa Figisu Figusu ili Ashuke Kimuziki au Yeye Ndo Tatizo?

$
0
0
JE, ni Kweli Diamond Anafanyiwa Figisu Figusu ili Ashuke Kimuziki au Yeye Ndo Tatizo?
Kumekuwa na malalamiko mengi sana kutoka kwa mashabiki wa WCB wakidai kuwa Diamond pamoja na Team yake anafanyiwa figisu na watanzania ili ashuke na sababu kibao..Je hizi stori zina ukweli au ni ndo mfa maji haishi kutaptapa.

To my side pamoja na kuwa ni shabiki wa WCB damu sioni kama ni kweli Diamond anafanyiwa figisu ila yeye ndo anasababisha haya naweza nikatoa sababu mbili tatu za kuunga hoja:

1.SHOW OFF
Hichi ndo kitu namba kinacho muangusha Diamond pamoja na Team yake. Diamond amekuwa mtu wa show off sana kila kitu anachofanya kiwe cha siri au cha kawaida ambacho hakina umuhimu wowote ataposti kwenye kurasa zake za mitandao, hii inamshushia heshima kwa kasi sana.

2.UROPOKAJI NA KUDHALILISHA WANAWAKE
Hakuna watu wenye uwezo mkubwa wa kumfanya mwanamziki au msanii yeyote mahali popote awe star zaidi ya wanawake, wanawake wana nguvu kubwa sana kwenye sanaa kwa ujumla. Sasa mshikaji wangu baada ya kumpata huyu bibi wa kiganda anawaona wanawake wote wa kibongo kama mashudu tu vile, na kuonyesha dharau za waziwazi kwa mfano kitendo cha kumwita hamissa mobeto "Bitch" kimeudhi watu wengi sana na mimi pia nikiwemo.

3.KUTAKA ASIKIKE YEYE TU NA WASANII WAKE.
Kitendo cha Diamond kutoa wimbo masaa machache baada ya mpinzani wake watu wengi wamektafasli kama ni ushamba na kutokujiamini na kutaka asikike yeye tu kuliko wasanii wengne. Watanzania tunatamani kuwepo na kundi kubwa la wasanii waliotoboa international sasa inapotokea kuzibiana riziki kwa kweli hili halikubaliki...

4.KUMUWAZA SANA MSHINDANI WAKE (KIBA) KULIKO UBORA WA KAZI.
Zamani Diamond alikuwa anatoa nyimbo nzuri tu na alikuwa hatumii nguvu nyiiingi kuzipromote hii ni kwa sababu alikuwa anatumia muda mwingi kuziandaa kwa umakini mkubwa lakini tokea beef lianze naona linamuchanganya sana inaonekana anatumia muda mwingi sana kumuwaza mpinzani wake kuliko ubora wa kazi. Na siku Mondi ukiacha kumuwaza Kiba ndo siku utakayokuwa huru na utaanza kutoa nyimbo nzuri zilizokamilika siyo hizi liipua lipua unazotoa siku izi


Maoni yako yanakaribishwa huo juu ni mtazamo wangu tu

By kifimbocheza_

Kwanini Kupiga Punyeto sio Jambo Baya....Hizi Ndizo Faida zake Muhimu Sana Kiafya

$
0
0
Ukweli ni kwamba, jambo la kujichua/kupiga punyeto limekuwepo kwa miaka mingi sana. Ni sawa kabisa na ni jambo la kawaida kama unaogopa kupiga punyeto, lakini ni vizuri ukajua kwamba watu wamekuwa wakifanya hicho unachokiogopa kwa karne nyingi sana zilizopita.

Hii inamaanisha kwamba kupiga punyeto ni jambo la kawaida kabisa ingawa kuna dhana potofu inayohusishwa na kitendo hiki. Jambo la kuvutia zaidi ni kwamba takwimu zinaonesha kwamba asilimia kubwa ya wanawake na wanaume wote wanaamua kufanya jambo hili wanapojisikia. Hatutakiwi kuwa wanafiki kwenye hili, ila tunachotakiwa ni kujua faida na hasara za kujiingiza kwenye kupiga punyeto.

Zifuatazo ni faida za kupiga punyeto kama yawezekana ulikuwa hujui kwamba jambo hilo lina manufaa:

Dawa tosha ya kukulaza

Kujishika sehemu zako za siri au kupiga punyeto inasaidia kupunguza shinikizo la damu na kusababisha kutengenezwa/kuachiwa kwa endorphins, aina ya kemikali inayohusika na kupunguza mfadhaiko (stress) na kuufanya mwili ulegee. Hii ndio sababu kwanini neva za fahamu zinatulia baada ya kumaliza jambo hili, bila kusahau hisia za usingizi zinazofuata baadaye.

Inasaidia kuzuia maumivu wakati wa hedhi

Kwa wanawake, kujiridhisha mwenyewe unapokuwa katika siku zako kunafanya mzunguko wa damu kwenye nyonga kuongezeka, jambo litalofanya maumivu yapungue. Hali unayoipata wakati unafika kileleni pia inaweza kusaidia na bila shaka inazidi starehe unayojipa kwa kutumia maji ya moto, wanawake wanalielewa vizuri hili.

Inakupa fursa nzuri zaidi kujistarehesha kimapenzi

Kama msemo unavyosema, mazoezi hufanya uliweze jambo kwa umaridadi wa hali ya juu. Washauri wa maswala ya ngono wanashauri kwamba, wanawake ambao hawajawahi kufikishwa kileleni kwa tendo la ndoa wanatakiwa kuanza kujipa raha hiyo yeye mwenyewe. Hii itawafanya waweze kuyajua vizuri zaidi maumbile yao na kuweza kujigusa sehemu ambazo zinawapa raha zaidi. Utaweza kujijua mwenyewe vizuri zaidi ikiwa ni pamoja na kiwango gani cha starehe kinaweza kukukidhi.

Inasaidia kuzuia saratani ya tezi dume

Hii yawezekana ikawa ni habari njema sana kwa wanaume wengi. Punyeto inasemwa kuwa inasaidia kupunguza hatari za kupata kansa ya tezi dume. Sumu huwa zinajikusanya kwenye mrija wa mkojo lakini kumwaga manii kunafanya sumu hizo zitolewe nje ya mwili jambo linalompunguzia mwanaume hatari ya kupata saratani hii.

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Ijumaa.....

$
0
0

Mwakyembe: Wapuuzeni Wanaodai Bombardier ni Mbovu.....

$
0
0
WATANZANIA wameaswa kuyapuuza maneno ya watu wachache hususani wanasiasa wanazusha kuwa ndege za serikali aina ya bombardier ni mbovu, kwa kuwa watu hao hawana utaalamu wa kutambua jambo hilo.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (pichani) alitoa rai hiyo katika mahojiano maalumu na waandishi wa habari akiwa katika chumba cha abiria kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe alipokuwa akijiandaa kusafiri kutoka Mbeya kwenda jijini Dar es Salaam kwa kutumia ndege ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) mapema wiki hii.

Dk Mwakyembe alisema wapo watu wamekuwa wakipiga kelele za uzushi kwamba serikali imenunua ndege mbovu, jambo ambalo siyo la kweli kwani mchakato wa upatikanaji wa ndege hizo ulianza muda mrefu ukiwashirikisha wataalamu mbalimbali kwa kuzingatia mazingira ya nchi pamoja na viwanja vilivyopo.

“Kuna watu wanasema ndege hizi ni mbovu sasa watuletee za kwao ambazo siyo mbovu. Kwanza hawana hata utaalamu wa kujua ndege nzima au mbovu pia wanachoangalia ni kutumia pangaboyi tofauti na zingine lakini ubora ni uleule,”.

Breaking News: Mahakama ya Kenya Yafuta Matokeo ya Urais...Uchaguzi Kurudiwa

$
0
0

Supreme Court Of Kenya has Ordered CANCELLATION of Uhuru Kenyatta August Win and orders a repeat of Presidential elections

As was highly expected Njoki Ndungu and Justice JB Ojwang ruled against the decision

Its a 4:2 judgement for Raila Odinga

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

KIMENUKA Bavicha Wahoji, Kwa ni CHADEMA Pekee Ndio Wanaokamatwa?

$
0
0
KIMENUKA Bavicha Wahoji, Kwa ni CHADEMA Pekee Ndio Wanaokamatwa?

TAZAMA VIDEO:


Askofu Gwajima Aongea Kwa Mara ya Kwanza Kuhusu Kuileta ‘Private Jet’ yake Tanzania

$
0
0
Askofu wa kanisa la ufufuo na uzima Josephat Gwajima ameongea kwa mara ya kwanza kuhusu kuileta PRIVATE JET yake Tanzania ambayo ameinunua Marekani. Kwenye hii video fupi hapa chini Gwajima amesema “Mimi nasema kwenye maisha yangu sishindwi hata sasa hivi nimekuja hapa Marekani narudi na Private Jet, nanunua…. why not? wale mlio Tanzania mnisikie anaeleta ngebe namkata ngebe kwa jina la Yesu“

 TAZAMA HII VIDEO HAPA CHINI KUMTAZAMA….

Maskini...Yusuph Manji Yupo hoi, Ashindwa Kufika Kortini

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeshindwa kusikiliza utetezi katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili mfanyabishara Yusuf Manji baada ya kuelezwa kuwa anaumwa.

Wakili wa mshitakiwa, Hajra Mungula alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa kesi imekuja kwa ajili ya utetezi lakini wamepata taarifa kuwa mshitakiwa hajafika. Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 8 mwaka huu kwa ajili ya utetezi. Mahakama hiyo ilitakiwa kuendelea kusikiliza kesi hiyo jana kwa upande wa utetezi ambapo tayari shahidi mmoja ameshatoa ushahidi wake.

Wakati huo huo, katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Manji na wenzake watatu, imeahirishwa hadi Septemba 8, mwaka huu kwa sababu hiyo hiyo. Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Meneja Rasilimali watu wa Kampuni ya Quality Group Ltd, Deogratius Kisinda (28), Mtunza stoo, Abdallah Sangey (46) na Thobias Fwere (43), mkazi wa Chanika wanakabiliwa na mashitaka ya uhujumu uchumi.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa mshitakiwa Manji anaumwa na kwamba upelelezi haujakamilika lakini wanaendelea kusisitiza upelelezi ukamilishwe.

Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 8 mwaka huu. Inadaiwa Juni 30, mwaka huuu maeneo ya Chang’ombe A wilayani Temeke Dar es Salaam, washitakiwa wote kwa pamoja, walikutwa na askari polisi wakiwa na mabalo 35 ya vitambaa vinavyotumika kutengenezea sare za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) vyenye thamani ya Sh milioni 192.5.

Pia inadaiwa Julai mosi mwaka huu, maeneo ya Chang’ombe A, wilayani Temeke, Dar es Salaam, washitakiwa wote walikutwa na askari polisi wakiwa na mabalo nane ya vitambaa vinavyotumika kutengenezea sare za JWTZ vyenye thamani ya Sh milioni 44. Katika mashitaka ya tatu, inadaiwa Juni 30, mwaka huu maeneo ya Chang’ombe A, washitakiwa walikutwa wakiwa na mhuri wa JWTZ ambao uliandikwa ‘’Mkuu wa Kikosi 121 Kikosi cha JWTZ’’ bila kuwa na uhalali kitendo kinachohatarisha usalama wan chi.

Pigo Jingine Kwa Chadema..Mahakama Yaamua Uchaguzi wa Ubunge Kurudiwa Longido

$
0
0
Mahakama ya Rufani Tanzania imebariki Uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Longido mkoani Arusha kurudiwa baada ya kutupilia mbali rufaa iliyokatwa na aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Onesmo Ole Nangole kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Ole Nangole alikata rufaa hiyo dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk Stephen Kiruswa ya kupinga hukumu iliyotolewa Juni 29, mwaka jana katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha na Jaji Sivangilwa Mwangesi aliyeamuru uchaguzi urudiwe kutokana na upungufu uliyojitokeza.

Naibu Msajili wa mahakama hiyo, Ester Mkwizu alisema mahakama hiyo imetupa rufaa hiyo kwa kuwa ina upungufu wa kisheria baada ya kukosekana kwa kielelezo namba nne na namba nane kwenye kumbukumbu ya rufaa.

Kwa mujibu wa Wakili wa Dk Kiruswa, Edmund Ngemela alidai mahakama imekubaliana na hoja za wajibu rufani kuwa ili mahakama ipitie ushahidi upya uliotolewa mbele ya Jaji Mwangesi, kwamba vielelezo vikikosekana ni lazima itupiliwe mbali.

Dk Kisurwa ambaye aliwakilishwa na mawakili Ngemela, Dk Masumbuko Lamwai na Daudi Haraka, alipinga matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi Nangole katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, kwa hoja za kuwepo kwa wapiga kura kutoka nchi jirani ya Kenya walioletwa na Ole Nangole.

Pamoja na madai hayo ilidaiwa pia Chadema ilitumia magari kusindikiza na kubeba masanduku ya kupigia kura, Mkurugenzi wa Uchaguzi kutangaza matokeo baada ya mgombea wa CCM kutolewa nje na kutokea kwa vurugu ndani ya chumba cha kuhesabu matokeo.

Aidha kutokana na madai hayo, Jaji Mwangesi aliamuru kwamba kwa kuzingatia kanuni, sheria na ushahidi uliotolewa mahakama imetengua shauri hilo na kwa kujiridhisha kwamba mchakato mzima haukuwa wa haki na huru hivyo mahakama inaamuru uchaguzi urudiwe upya.

Tayari Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshatangaza kujiweka sawa kwa uchaguzi huo mdogo utakaofanyika baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutangaza tarehe.
Facebook Twitter

Madhara Ya Kuchaguliwa Mwenzi Wa Kuishi Naye Katika Mahusiano Ndoa

$
0
0
Mtanzania? Ni imani yangu kuwa uko salama rafiki na unaendelea vizuri katika harakati zako za kila siku kuhakikisha unapata kile unachokitaka kwenye maisha yako. Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya siku hii ya leo ameweza kutustahilisha tena kuiona siku hii ya leo. Kwa hiyo rafiki, tutumie muda huu wa leo vizuri kwani leo ni siku bora ambayo haitokuja tena kutokea katika maisha yetu hapa duniani.

Mpendwa rafiki, napenda kukualika tena katika makala yetu ya leo tuweze kujifunza kwa pamoja yale ambayo nimeweza kukuandalia siku hii ya leo. Hivyo basi, nakusihi ungana nami mwanzo hadi mwisho wa makala hii ili tuweze kusafiri wote kwa pamoja. Leo tutakwenda kujifunza juu ya madhara ya kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye kwenye maisha ya mahusiano. Je ni madhara gani rafiki? Karibu rafiki tuweze kujifunza wote kwa pamoja.

Katika moja ya matatizo yanayowasumbua watu duniani basi moja wapo ni mambo ya mahusiano. Mahusiano haya yanaweza kuwa mahusiano ya uchumba, mahusiano ya ndoa na nk. Sasa katika mahusiano ya ndoa wapo watu wengi sana wanaruka hatua muhimu sana ambazo baadaye zinakuja kuwaumiza vibaya. Hatua hizo muhimu ni urafiki na uchumba kwa hiyo, ikitokea watu wamekutana ndani ya miezi miwili, mmoja na kukimbilia kufunga ndoa ndio hawa wale wanaokuja kujuta kwa nini walifanya maamuzi hayo.

Mpendwa msomaji, malengo mahususi ya somo letu la leo ni madhara ya kuchaguliwa mwenza katika maisha ya mahusiano. Ziko jamii tofauti duniani zenye utaratibu au utamaduni wa kuwachanguliwa watoto wao wenza pale wanapokua wamekaribia ule umri wa kuishi ya maisha ya ndoa kama mke au mume. Wazazi wa jamii za kuwatafutia watoto wao wenza bado wapo mpaka leo katika zama hizi za taarifa na pengine unafahamu watu ambao wanafanya jambo hili kwenye jamii iliyokuzunguka.

Kwa mfano, mtoto tokea akiwa mdogo anawekewa ‘’ oda’’ mapema kuwa wewe utaolewa na mtu fulani au utamuoa mtu bila kujali unataka au la. Kwa hiyo, tabia hii inawanyima watoto wengi kuwa na mtu Yule anayempenda badala yake wanakuwa na watu ambao siyo chaguo lao la kutoka moyoni. Utamaduni huu unakuwa ni kama kumnyima mtu kuishi maisha anayotaka hapa duniani.
Unaporuhusu wazazi wakuchagulie mwenza wa kuishi naye katika maisha ya ndoa kwanza inakuwa ni utumwa wa hali ya juu. Kwanini?

Kwa sababu kuchaguliwa kufanya kitu ambacho hukipendi katika maisha yako ni utumwa. Vivyo hivyo, kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye ni utumwa pia. Unapokuwa unachaguliwa mwenza wa kuishi naye unakuwa unavunja hatua muhimu sana katika kuelekea maisha ya ndoa ambayo ni urafiki na uchumba. Kupitia hatua hizi unaweza kumchunguza mwenzako ni mtu wa namna gani, falsafa yake ya maisha ikoje, ni mtu chanya au hasi, ni mtu wa kuigiza maisha au ni mtu halisi anayeishi bila kuigiza maisha na mambo mengine mengi unayotaka kuyajua kutoka kwa mwenzako.

Rafiki, watu wanaoishi na wenza wao kwenye maisha ya ndoa kwa kuchanguliwa na kwenda kuanza kuishi maisha ya urafiki, uchumba na ndoa kwa wakati mmoja huwa wanashinda sana. unakuta mwenzako anaishi falsafa tofauti kabisa na wewe ulivyotarajia. kwa mfano, wewe falsafa yako ni kuishi chini ya kipato chako na unakuta mwenzako anataka kuishi juu ya kipato kwa kufanya mambo ambayo hayana ulazima kwenye maisha. Lakini kama ulikuwa umemgundua mwenzako na kumsoma vizuri katika hatua za uchumba ungeweza kufanya maamuzi mapema kwa kumpima kama mtu huyo anakufaa au la kulingana na vigezo vyako.

Kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye katika zama hizi ni aibu kwa kweli kwani ni kuchaguliwa kufanya chochote ambacho hukipendi ni utumwa katika maisha yako. Kumbuka rafiki, hata mzazi akikuchagulia mpenzi ambaye wewe humpendi na ukakubali utakua umejichagulia wewe mwenyewe kuingia shimoni. Kwa hiyo, hata wazazi wakikuchagulia kuishi na mwenza ambaye wanampenda wao ni kama kuchaguliwa maisha ya kuishi hapa duniani. Licha ya kuchaguliwa maisha wewe ndiye utakayeenda kuishi hayo maisha na wala siyo wazazi watakaopata raha au shida, ukiingia shimoni wao hawatakuwepo bali wewe ndio utawajibika.

Hatua ya kuchukua leo; usikubali kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye katika maisha yako. Ishi na mtu unayempenda kutoka moyoni, ishi na mtu ambaye mliweza kupitia hatua za urafiki, uchumba ukamjua vizuri tabia zake ni mtu wa namna gani. Fanya kitu ambacho unakipenda ndio furaha ya kweli katika maisha ambapo utapata mafanikio makubwa yenye furaha na ubora wa hali ya juu.

Kwa kuhitimisha, tunaishi karni ya ishirini na moja na hatuko tena katika zama za mawe bali tupo katika zama za taarifa. Kuwa chachu ya mabadiliko kwa kuvunja utumwa huo katika jamii uliyopo siyo unasoma na kupata elimu ya juu bado ukirudi nyumbani wazazi wanakushurutisha kuoa au kuolewa na mtu Fulani bila ya ridhaa yako mwenyewe. Wewe ndio mwenye maamuzi ya maisha yako kwa sababu hakuna mtu mwingine atakaye ishi maisha yako zaidi ya wewe mwenyewe.

Mbunge Ridhiwani Kikwete Baada ya Matokeo ya Uchaguzi Kenya Kubatilishwa

$
0
0
Moja kati ya stori ambazo zimewashitua wengi Ijumaa ya leo September 1 2017 ni kuhusiana na maamuzi ya Mahakama Kuu nchini Kenya kubatilisha matokeo ya uchaguzi Mkuu uliyofanyika August 8 2017 na Uhuru Kenyata kuibuka mshindi wa Urais dhidi ya Raila Odinga.

Jaji Mkuu David Maraga ameagiza uchaguzi Mkuu mpya utafanyika ndani ya siku 60 kwa mujibu wa sheria na katiba na umebatilishwa kwa sababu IEBC hawakuwa wameandaa uchaguzi huru na haki.

Kila mmoja amepokea uamuzi huo kitofauti, mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete ameandika mtazamo wake kupitia ukurasa wake wa instagram “Niliwahi Sema najifunza jambo toka Kenya, Leo inathibitika wakati Mahakama inafungua kurasa Mpya ya Kumbukumbu ya Maamuzi.#KenyaDecides“

Rais Uhuru Kenyatta Atoa ya Moyoni Baada ya Matokeo ya Urais Kenya Kutenguliwa na Mahakama...Adai Akubali ila.....

$
0
0
Aliyekuwa Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta ,ametoa msimamo wake juu ya uamuzi wa mahakama uliotolewa leo wa kurudiwa kwa uchaguzi a urais, na kusema kuwa hakubaliani nao ingawa anaheshimu uamuzi huo.

Akizungumza katika Ikulu ya Kenya muda mfupi baada ya uamuzi wa mahakama kutolewa, Uhuru Kenyatta amesema anaheshimu uamuzi uliotolewa na mahakama wa kufuta matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi, lakini hakubaliani na uamuzi huo.

“Hii ni muhimu kwetu kama Wakenya kuheshimu uamuzi wa sheria, binafsi sikubaliani na uamuzi uliofanywa leo, lakini naheshimu”, alisema Uhuru Kenyatta.

Uhuru Kenyatta aliendelea kwa kusema kwamba “mamilioni ya Wakenya walisimama kwenye mstari wakafanya uamuzi wao, lakini watu 6 wamekwenda kinyume, nyinyi kama wakenya mliamua na kuwachagua kwa wingi viongozi wa Jubilee, mahakama wamefikia uamuzi tunauheshimu na hatukubaliani nao”, alielezea.

Pamoja na hayo Uhuru Kenyatta amesema kwa kuwa wanaheshimu uamuzi wa mahakama, wako tayari kurudi kwenye kampeni na kupiga kura tena kama ambavyo mahakama imetaka.

“Hatupo vitani na kaka zetu, nyinyi mjipange na sisi tunajipanga, tuko tayari kurudi kuongea na wakenya kuwaambia yale tunataka kufanya, tafadhali acheni ukabila, acheni utengano uzeni sera mshindane na zetu, acha Wakenya waamue, watu 6 hawawezi badilisha nia ya wananchi milioni 40, Wakenya ndio wataamua “, alisema Uhuru Kenyatta.

Uhuru Kenyatta hakuishia hapo aliendelea kwa kuwasihi wakenya kudumisha amani, bila kujali itikadi za vyama na ukabila, ili kuendelea kuijenga Kenya iliyo bora.

“Na tena Wakenya wenzangu nasema amani, jirani yako atabaki kuwa jirani yako, tupo tayari kurudi kwa wananchi na ajenda hiyo hiyo tuliyo wapelekea watu wetu ya kujenga umoja wa nchi yetu, sisi ni kitu kimoja, sisi ni jamii ambayo inaitwa Wakenya na hivyo ndivyo itakuwa”, alisema Uhuru Kenyatta.

Leo asubuhi Makama ya juu zaidi ilitoa uamuzi wa kesi ya uchaguzi iliyofunguliwa na muunganiko wa vyama vya upinzani nchini Kenya (NASA) dhidi ya Tume ya Uchaguzi iliyosimamia uchaguzi huo ambao Uhuru Kenyatta aliibuka mshindi, na kuamua kufuta matokeo hayo huku ikitaka urudiwe baada ya siku 60.

Wema Sepetu Aikacha Shughuli ya Idriss Sutan.....Afunguka na Kumuomba Msamaha Idriss

$
0
0
Mwigizaji staa na Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu usiku wa August 31, 2017 alishindwa kutokea kwenye uzinduzi wa bidhaa mpya ya Idriss Sultan licha ya Idriss kuwepo kwenye uzinduzi wa movie mpya ya mrembo huo siku kadhaa nyuma.

Ayo TV na millardayo.com zilimpata Idriss ambaye alisema alitarajia Wema kuibuka kwenye tukio hilo ingawa alirikiri kuwepo changamoto ambayo huenda ilimzuia kutohudhuria.

Sasa leo September 1, 2017 kupitia kwenye Instagram yake Wema Sepetu ameweka wazi kilichomkwamisha asifike kwenye tukio hilo.

”We Compliment one another on the Red Carpet… Dats wat we do… We make each other look better than wat we already are… I feel sooo bad not showing up at your launch last night & this is me right here saying Im sorry… Its haunting me, The fact that wewe ulikuja kwenye premiere yangu na ukani support.

“Hamuwezi amini jana mpaka na salon nimeenda, I was getting ready kwa ajili ya launch ya Dris, Ila wat happened… Dah… Elisha kaniharibia nguo yangu, I cried like a baby maana it was late, na sijui wat went wrong maana Elisha hajawahi kabisa kunizingua kwenye nguo zangu ila ndo bahati mbaya… Sikuwa na nguo nyingine ya kuvaa and it was already late.

“Maduka ya nguo yote were closed and I had no second option… Wenyewe mliona Dris alivyopendeza alafu mimi ndo niende looking awful… Sikuweza fanya chochote… Maybe this wont make sense kwenu but it makes alot of sense kwangu mimi… Red Carpet appearances are Major jamani… Yaani sijui hata niseme nini… Dris Im Sorry… I had to do this here…

“Since y’all have seen how Dris has been there for me… It hurts soo much that nimeshindwa kuwepo jana… If only I had another option wallahy… Ila nilishapanga kuvaa that particular nguo na ndo ikaharibiwa… Nihisi kufa… Once again Im sorry Dris… I’ll make it upto u… Naombeni mnisaidie kumwelewesha japo anielewe… Maana najua as a human being lazima amejiskia vbaya sana… 😔😔😔


Bob Junior Azidi Kumvua Nguo Diamond Platnumz...Adai ana Dharau na Kebehi

$
0
0
Msanii  na mtayarishaji wa muziki kutoka studio za Sharobaro rekodi, Bob Junior ameamua kutaja jina la msanii Diamond Platnumz kuwa ndiye anaye lengwa na madongo anayoyatoa kupitia mtandao wa Instagram kwa sasa.
Akiongea na Bongo5, Bob amesemakuwa yeye harushi madongo kama wanavyotafsiri watu bali yeye anachokiongea ni ukweli mtupu kwa msanii huyo.

Hamna madongo mimi nimeongea fact, nimeongea ukweli na ukweli ubaki kuwa ukweli. Mimi naishi katika ukweli maisha yangu yote nikiamua kumsaidia mtu namsaidia hadi nguvu yangu ya mwisho anasimama, chochote ulichokiona Instagram yangu vingi ni vya ukweli.” amesema msanii huyo.

Pia akaongeza kuwa ” Kuna mtu naye anajiita simba na yeye ndiyo muhusika inamuhusu hiyo. Nimekuwa ni kifanya naye kazi sana lakini dharau na kebehi imetawala sana kwake kuja kwangu, nimefanya naye kazi kwa mapenzi ya mwenyezi mungu kwa sababu wakati anakuja alikuwa akirap nikamshauri aachane na kurap tuimbe.Nikaja nikamfanyia albamu ambayo ilifanya vizuri kutoka kwangu, ‘kamwambie’ bwana Nassibu Diamond Platnumz ni nyimbo ya kwanza kufanya naye na ikampa tuzo tatu, ni nyimbo ambayo mpaka leo hii sikuchukua hata shilingi moja.” TAZAMA VIDEO:

Mrembo Huddah Monroe Afunguka Makubwa 'Mimi sio Msagaji Napenda Sana DI..CK'

$
0
0
Kila mtu ana maisha yake na maamuzi yake katika kila jambo analofanya. Mastaa wengi wamekuwa wakitoa kauli tata mara kwa mara kupitia mitandao ya kijamii.

Mwanamtandao Huddah Monroe kutoka Kenya, anazidi kuibua utata wa kauli zake kutokana na alivyoama kueleza ni kitu gani anapenda zaidi kukifanya. Kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram mrembo huyo ameweka maneno yanayoashiria akipenda sana kufanya tendo la ngono kuliko kitu kingine.

I miss my KING! And for those who keep asking on my DM! I am not BIS.EXUAL! I DON’T do WOMEN! I love DI..CK too much!😍😁 Most of my friends are G.AY 💯and I love them to death but I don’t swing that way with women! Sawa? Thanks . Love you! ❤️ #STARGAL, ” ameandika mrembo huyo.

Kumvumilia Mwanaume Asiyekupa Nipa Hela Nacho Kipaji....Mimi Nimeshindwa Walahi!

$
0
0
Naitwa Fatuma Kutola Mwananyamala, kwa hili mimi sijui ila nikipata Mwanaume asiyenihonga sioni raha ya mapenzi hata kidogo, Yaani Mwanaume akinitongoza alafu akionekana hana mwelekeo wa kunipa hela simpi papucha, nasikia wadada wengine wanavumilia na wanaume wasiowapa hela eti sababu wazuri kisura sijui wanawaita Ben ten sikuhizi...yaani kwangu hata uwe mzuri kivipi bila hela ni Big Nooooooooooooo.......Yahitaji moyo aiseeee au nina kasoro?

Chadema Msijifiche Nyuma ya Kivuli cha Supreme Court ya Kenya......

$
0
0
Leo majira ya mchana dunia ilishuhudia tukio kubwa zaidi la mahakama ya juu zaidi ya Kenya kuubatilisha uchaguzi uliofanyika mwezi wa 8 nchini humo.

Kwanini naliita tukio la kihistoria duniani? Ni kwasababu malalamiko ya kasoro za uchaguzi juu ya mfumo wa kidigitali yalishatolewa hata nchini marekani lakini walioshindwa nchini humo(chama cha Democrat) walishindwa kuchukua hatua ya kwenda kuhoji kwenye mahakama zao, kitu ambacho NASA ya Kenya ilithubutu.

Katika kuthubutu huko, watu mbalimbali hapa nchini kwetu walimbeza sana Raila Odinga, na wengine kumuita sore looser ambaye hajawahi kukubali kushindwa.

Lakini baada ya uthubutu huo, leo hii mahakama imetangaza kurudiwa kwa uchaguzi huo ndani ya siku 60.

KWANINI UAMUZI WA MAHAKAMA YA JUU YA KENYA UMEWAUMBUA CHADEMA? 

Inafahamika kwamba Ndugu Edward Lowasaa alifanya official endorsement kwa upande Raisi Uhuru Kenyatta, akishawishi kabila la wamasai nchini humo kumchagua Uhuru ili awe tena raisi wa kenya kwa mara nyingine.

Mara baada ya matokeo ya uchaguzi huo, bwana Lowassa alimpongeza ndugu Kenyatta kwa ushindi, tena akisisitiza kia uchaguzi ulikua wa Huru na wa Haki!!!

Mbaya zaidi wafuasi wengi wa Chadema, walilipuka mtandaoni na kushangilia ushindi huo wa kenyatta kwa kusisitiza kua uchaguzi huo ulikua wa "huru na haki".

Katika hali ambayo ni ya kushangaza, hata wasimamizi wa uchaguzi waliotokea nchi za ulaya nao walisema uchaguzi wa kenya ulikua huru na wa haki. Wasimamizi hawa baada ya tukio la leo tumeibua mambo mawili, kwanza, inawezekana walifahamu kua maslahi yao chini ya Kenyata yangelindwa vizuri au pili, hiyo dhana ya demokrasia na uhuru wa uchaguzi wanayoisema kua nchi za Afrika zinashindwa kusimamia haina uthamani wowote kwao hata itakapovunjwa, kwasababu sio rahisi kusema kua hawakufahamu kasoro hizo.

MAANA HALISI YA UCHAGUZI WA HURU NA HAKI ALIYOKUA ANAIMAANISHA NDUGU LOWASSA NA WAFUASI WA CHADEMA.

kwa miaka mingi, kama sio yote, ndugu lowassa alikua ni mwanachama wa CCM, Chama ambacho kimelalamikiwa kwa manuva mengi waliyowahi kuyafanya kwenye chaguzi mbalimbali zilizopita.

Na ifahamike kwa ngazi aliyofikia ndugu lowassa alikua ni master mind wa magumashi mengi sana ambayo pengine hata wanachadema wengi wakigundua watabaki midomo wazi, au wanayajua ila hawana locus standi ya kuhoji kwasababu tayari yupo ndani ya chama chao.

Kwa maana hiyo kwa uzoefu wa umafia wa chaguzi alizowahi kushiriki akiwa kama sehemu ya chama tawala, uchaguzi wa uhuru na haki alioumaanisha ni uchaguzi wa magumashi na figisu ambao mahakama ya juu ya kenya imeufuta leo.

Kwa lugha rahisi tunaweza tukasema lowassa alirudia kwenye zama zake za umafia kama alivyokua enzi zake, au lowassa alikua kwenye sura yake halisi.

Na kwabahati mbaya sana wanachama wa chadema wakaingia kwenye mkenge huo wa kusapoti umafia.

Umafia ambao ulionekana dhahiri ni pamoja kuuwawa kwa mkuu wa tume ya uchaguzi kwenye maswala ya kimtandao huku akikatwa vidole na kuonekana ameingia kwenye akaunti yake ya kazini siku kadhaa baada ya kufa, nafkiri ni kwa kutumia vidole hivyo vilivyopotea.

Kwahiyo wanachama wa chadema wakajikuta wanashangilia umafia, ikiwemo damu ya marehemu msando chini ya kivuli cha uchaguzi huru na haki.

KINACHOENDELEA KWA SASA MITANDAONI. 

katika hali ambayo ni kushangaza, tena bila aibu, wafuasi wa chadema wanaipongeza mahakama ambayo imesema uchaguzi huo wa kenya ambao wao walisisitiza kua ulikua wa "huru na haki".

Kwa maana hiyo wanashangilia mahakama ambayo inabatilisha misimamo yao.

Mkenge ambao waliingizwa na mafia wa uchaguzi ndugu lowassa ni dhahiri umewaaibisha, umedhihirisha unafki wao.

Naomba kuwasilisha.

By Muwindaji/JF

Bikra Zinapotea Siku za Sikukuu, Wazazi Mnachangia Kuharibu Hiki Kizazi

$
0
0
Habari za mida wakuu mbalimbali
Leo siku ya Sikukuu ya IDDI Mchana nimejionea jinsi vitoto vya kike vinavyo randa randa mtaani kwetu vimejiachia balaa, Yaani watoto chuchu SAA alafu wanaita hatari ila nimegundua wasichana wengi huanza mahusiano kama siyo kubikiriwa siku kama za Leo za sikukuu kwani wengi wanapewa nafasi au kuruhusiwa kutoka bila kuchungwa basi unakuta msela wa jirani hapo kashapewa ahadi anakwenda kubatua kitu bila hiyana
Ewe mzazi unamwachiaje binti mdogo azurure na ilhal una jua kashavunja ungo ?

Tuweni makini na mabinti zetu jamani
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images