Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Kimenuka.. Almasi Yenye Thamani ya Sh. Bilioni 32 Yanaswa Airport ikisafirishwa Kwenda Ubelgiji

$
0
0
Kimenuka.. Almasi Yenye Thamani ya Sh. Bilioni 32 Yanaswa Airport ikisafirishwa Kwenda Ubelgiji
Yana thamani ya shilingi bilioni 32.8 na yalikuwa yakisafirishwa kwenda nchini Ubeligiji.

Madini hayo yamekamatwa katika uwanja wa ndege ukionekana kutolewa Mwadui kwenda Ubeligij chini ya kampuni moja ya Afrika Kusini ambao Naibu Waziri wa Nishati na madini atazungumza na waandishi wa habari katika uwanja wa ndege wa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Zari Afanya Haya Mara Baada ya Kuolewa na Diamond Platnumz

$
0
0
Juzi kati Celeb wakiganda muke ya diamond platnumz msaniii mkubwa Tanzania baada ya kuelewa aliamua kwenda kwao, huko alifanya mambo mengi na alionekana mwenye furaha muda wote mpaka pale alipofika kwenye kaburi la mama yake na kufanya haya. VIDEO:

Diamond Tena...Aachia Nyimbo Mpya na Patoranking Inayoitwa Love you Die..Itazame Hapa

$
0
0

Diamond hongera sana na bandika bandua zako.... Kijana unajua safi sana. Hii nyimbo inakuwa ya Africa. Itazame Hapa:

Wakati Tunashabikia ya Kenya,Tanzania Haina Jaji Mkuu zaidi ya Miezi 8

$
0
0
Hakika Tanzania ni inatakiwa iingie kwenye vitabu vya kumbukumbu kama nchi ya maajabu duniani

Wakati wanatanzania wanashabikia na kukesha mitandaoni wakijadili demokrasia ya Kenya,wao hata Jaji Mkuu wa kutoa maamuzi mazito kama hayo hawana.

Licha tu ya kutilia mashaka upatikanaji wa Jaji huyo Mkuu lakini hata uwepo wake tu umekuwa kizungumkuti.

Watanzania wengine wanahoji mbona wapinzani hawakwenda mahakamani kupinga uraisi wa JPM?

 Wenzetu Kenya wamepigania katiba yao na kuapa kuisimamia. Mihimili yao nimekuwa huru kufanya maamuzi.

Njoo hapa kwetu ! Uliza Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi anateuliwa na nani, Kamishna anatueliwa na nani, Jaji anateuliwa na nani?

Na hali inavyoendelea hivi hakuna aliyedhubutu kunyanyua mdomo, ukiacha wachache kama kina Tundu Lissu ambao wamejitoa bila kujali chochote

Naona Vingozi wengi wa TZ jana wamefunguka kuzungumzia mambo ya Kenya wakati ya kwenu yamewashinda na hamuwezi hata kuzungumzia tu?

Ulishawahi kuona wapi nchi ya Kidemokrasia,Wananchi wanaiogopa serikali?
Serikali ndio inatakiwa kuwaogopa wananchi.

By OKW BOBAN SUNZU/Jamii Forums

TANZIA: Bi Hindu Afariki Dunia

$
0
0
TANZIA: Bi Hindu Afariki Dunia
Mbunge mteuliwa wa chama cha wananchi (CUF), Bi Hindu Mwenda amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

Taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa CUF, Abdul Kambaya imesema kuwa Bi Hindu amefariki jana jioni baada ya kuugua kwa siku kadhaa japo hajaeleza kiundani chanzo cha kifo chake lakini amesema taratibu nyingine zinazofuata zitaelezwa hapo baadaye.

Marehemu Bi Hindu alikuwa ni miongoni mwa wabunge wapya waliotangazwa na Tume ya Uchaguzi kuchukua nafasi ya wabunge nane ambao walivuliwa uanachama na kupoteza sifa ya kuwa wabunge na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba


Mnaosubiria Ndoa Yangu na Nahreel Mtasubiria Sana- Aika

$
0
0
Mnaosubiria Ndoa Yangu na Nahreel Mtasubiria Sana- Aika
BAADA ya tetesi kuzagaa kuwa mwanadada Aika Mariale na mpenzi wake wa siku nyingi, Nahreel, wanaounda kundi la muziki wa kizazi kipya la Navy Kenzo, wapo kwenye mipango ya ndoa, mwanadada huyo amefunguka kuwa hakuna kitu kama hicho kwa sasa.

Akipiga stori na Mikito Nusunusu, Aika wa nahreel alisema watu  wanapenda kuzusha mambo wasiyoyajua na suala hilo halipo kabisa wala hakuna anayewaza kitu hicho kwa sasa zaidi ya kufikiria jinsi ya kuandaa kazi nzuri za kuwakata kiu mashabiki wao.

“Suala la mimi kuolewa watu watasubiri sana maana hata mipango hiyo haipo kabisa nashindwa hata kulizungumzia, ndoa yetu si leo wala kesho kama ikifika wakati mambo yakiwa tayari tutaweka wazi ila ni huko baadaye sana,” alisema Aika.

Taifa Stars Kuumana na Botswana Leo

$
0
0
Taifa Stars Kuumana na Botswana Leo
Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na Botswana, leo Jumamosi zinapambana kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam katika mchezo wa kirafiki.
Mchezo huo ni wa kufuata Kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa). Timu zote zinautumia mchezo huo kama maandalizi ya mechi zao za kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa Afrika (Afcon).

Katika mchezo huo, mwamuzi wa kati anatarajiwa kuwa Elly Sasii akisaidiwa na Soud Lillah (Line 1) na Frank Komba (Line 2) wakati mwamuzi wa akiba (Forth Official) atakuwa Israel Nkongo.
Kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga, alisema: “Kikosi chetu kipo tayari kwa mchezo huu ambao kwetu

ni muhimu kwa maana mbili, moja ni kujiandaa na michezo ijayo ya kufuzu Afcon, lakini pili ni kutafuta nafasi ya kupanda kwenye viwango vya Fifa.
“Kikubwa Watanzania wajitokeze uwanjani kutusapoti kwani vijana wamenihakikishia kwamba wana uwezo wa kushinda mchezo huu.”

Kwa upande wake Kocha wa Botswana, Major David Bright, alisema: “Tumekuja lakini bado tuna uchovu wa safari, lakini tunatarajia kuwa na mchezo mzuri dhidi ya Tanzania kwani hii si mara ya kwanza kwa timu hizi kukutana.

“Nimepewa kikosi hiki hivi karibuni, lakini nimejaribu kuchukua wachezaji wale wazoefu na naamini tutafanya vizuri. Mechi hii ni kipimo kwetu kwa ajili ya kujiandaa na mechi za kufuzu Afcon.”


Halima Mdee Apigania Haki za Watoto wa Kike

$
0
0
Halima Mdee Apigania Haki
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee amesema jamii ina wajibu wa kupigania haki za watoto wa kike dhidi ya mifumo isiyokubali mabadiliko kwa kuhakikisha wanapata fursa ya kupata elimu na kushika nafasi za uongozi.

Mdee ambaye ni Mbunge wa Kawe, amepinga jitihada za kuwakwamisha wasichana wanaopata mimba wakiwa masomoni kutoendelea na masomo.

Amesema kikwazo hicho ni mojawapo ya vinavyopaswa kupewa jukwaa na wadau kutoa ufumbuzi badala ya kuwahukumu na kuwanyima nafasi ya pili.

Mdee amesema hayo katika kituo cha watoto yatima cha Samaritan Village eneo la Moshono jijini hapa alipokabidhi msaada ikiwa ni hatua ya kuunga mkono taasisi zilizojitolea kulinda haki za watoto waliokosa fursa baada ya wazazi wao kufariki dunia.

Mdee aliye jijini hapa kuongoza maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa Chadema amesema kumekuwa na ukatili ndani ya jamii ambao wakati mwingine umesababisha baadhi ya wa watoto kujikuta kwenye vituo hivyo.

Amesema katika maadhimisho hayo wameamua kujishughulisha na mambo ya kijamii kwa sababu ndipo misingi ya chama chao ilipo na kimeweza kupiga hatua kisiasa kutokana na kutetea masilahi ya wanyonge na haki kwa jumla.

Mdee amesema hatatishwa wala kukata tamaa kuzungumzia mambo anayoona yanapaswa kukemewa kwa sababu ya kuogopa kukamatwa kwa kuwa yeye ni kiongozi na atatimiza wajibu wake wa kuwasemea wasioweza kusimama hadharani.

Mratibu wa kituo cha Samaritan Village, Josephat Mmanyi amesema wanalea watoto  50 wenye umri wa kuanzia mwaka mmoja hadi miaka 21 ambao wapo katika ngazi mbalimbali za masomo.


Hizi Hapa Basabu za Wema Sepetu Kutoshiriki Uzinduzi wa Idriss

$
0
0
Hizi Hapa Basabu za Wema Sepetu Kutoshiriki Uzinduzi wa Idriss
Diva anayebamba kunako tasnia ya filamu Bongo, Wema Sepetu, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kushindwa kuhudhuria uzinduzi wa viatu vya x- wake, Idriss Sultan, kutokana na fundi kumharibia nguo yake.

Wema ameonyesha kusikitishwa kwa kitendo hiko, hasa ukizingatia kwamba Idriss alimsapoti kwa asilimia kubwa katika uzinduzi wa filamu yake ya Heaven Sent. Na kupitia ukurasa wake wa Instagram, amemuomba radhi na kumuelezea kilichotokea.
“Siku zote tunavutia sana kwenye red kapeti, nimejisikia vibaya sana kwa kushindwa kuhudhuria katika uzinduzi wako jana usiku, ndiyo maana nimeshawishika kusema samahani, nimehuzunika sana.

“Ni kweli wewe ulikuja kwenye uzinduzi wa filamu yangu na ukanisapoti sana, hamuwezi amini jana mpaka na saluni nimeenda, nilikuwa tayari kwa kuja, ila kilichotokea, Dah! Elisha kaniharibia nguo yangu, nimelia kama mtoto, sijui imekuwaje, maana Elisha hajawahi kabisa kunizingua kwenye nguo zangu ila ndiyo bahati mbaya sikuwa na nguo nyingine ya kuvaa na muda ulikuwa umeshakwenda, maduka ya nguo yote yalikuwa yamefungwa. Wenyewe mliona Idriss alivyopendeza halafu mimi ndiyo niende nikiwa sijapendeza.

“Labda hili siyo muhimu kwenu, lakini muonekano mzuri kwenye red kapeti ni muhimu jamani, yaani sijui hata niseme nini, kwa jinsi alivyonisapoti , inaumiza sana kwamba nimeshindwa kuwepo jana.
“Naombeni mnisaidie kumuelewesha japo anielewe maana najua kama binadamu, lazima amejisikia vibaya sana,” ameandika Wema.

Kikwete Atoa Neno Uchaguzi wa Kenya

$
0
0
Kikwete Atoa Neno Uchaguzi wa Kenya
Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete amefunguka na kudai atamkumbuka aliyekuwa rais mteule wa nchi ya Kenya, Uhuru Kenyatta kwa kuweza kuwa mtu wa kidemokrasia wa dunia katika zama za sasa.

Ridhiwani Kikwete ameeleza hisia zake hizo kupitia ukurasa wake wa twitter mapema leo baada ya Mahakama ya Juu nchini Kenya kutengua matokeo ya uchaguzi mkuu upande wa rais nchini humo kutokana na Tume ya Uchaguzi IEBC kukiuka Katiba na Sheria ya uchaguzi.
"Utakumbukwa kama mtu wa kidemokrasia wa dunia katika zama zetu, hiyo ni ukweli na ninakuombea", aliandika Ridhiwani Kikwete.

Pamoja na hayo, Ridhiwani Kikwete aliendelea kwa kusema "niliwahi kusema najifunza jambo kutoka Kenya, leo imethibitika wakati Mahakama inafungua kurasa mpya ya kumbukumbu ya maamuzi", alisisitiza Ridhiwani Kikwete.

Huu hapa chini ndiyo ujumbe wa Ridhiwani Kikwete aliouandika kuhusiana na maamuzi ya Kenya yaliyotolewa na Mahakama ya Juu nchini humo.

Maamuzi yaliyotolewa na Mahakama ya Juu nchini Kenya leo Septemba mosi yameweza kusimua hisia za watu wengi duniani kwa kila mmoja kuwa na mawazo tofauti juu ya tukio hilo lililoweza kuwa la kihistoria nchini humo.

Lowasa Ampa Pole Uhuru Kenyatta Baada ya Kufutiwa Matokeo ya Urais na Mahakama

$
0
0
Lowasa Ampa Ampa Pole Uhuru Kenyatta Baada ya Kufutiwa Matokeo ya Urais na Mahakama
Mjumbe wa kamati kuu ya (CHADEMA) na Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa amefunguka na kutoa pole kwa aliyekuwa Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta kufutia mahakama ya juu nchini humo kufuta matokeo ya uchaguzi wa Urais uliofanyika Agosti 8, 2017.

Mhe. Edward Lowassa anasema yeye bado ataendelea kumuunga mkono Uhuru Kenyatta kwani ni kiongozi mwenye kusimamia Demokrasia na mwenye maono ambaye anaweza kuisadia Kenya hivyo ataendelea kumuunga mkono tena katika uchaguzi utaofanyika upya nchini humo.

"Nitumie nafasi hii kumpa pole Uhuru Kenyatta kwa jambo lililotokea lakini nimpongeze kwa kufanya kampeni ya kiume kafanya kazi nzuri sana, ukitazama maoni ya waangalizi mbalimbali walisema uchaguzi ulikuwa wa huru na haki, lakini pia ukitazama orodha ya washindi wa wabunge Jubilee ndiye inaongoza, kwa maseneta na magavana Jubilee ndiyo inaongoza picha hizi mbili zinatoa picha, lakini ikishasema mahakama maamuzi yake ni lazima yaheshimike" alisema Lowassa
Aidha Lowassa amesema kuwa anamuheshimu sana Uhuru Kenyatta kutokana na jinsi ambavyo anaheshimu Demokrasia na kudai katika kipindi cha uongozi chake siku zote amekuwa akilinda Demokrasia ya nchi hiyo kwani wabunge wamekuwa na haki na vyama vimekuwa na haki na kila mtu ana haki.

"Niliwahi kumsikia mama mmoja akimtukana Uhuru Kenyatta matusi ya nguoni kabisaa kiasi kwamba yule mama angekuwa hapa Tanzania siku nyingi angekuwa jela lakini Uhuru Kenyatta alimsamehe na maisha yakaendelea lakini uongozi wake ni uongozi wenye malengo amerithi nchi iliyotoka kwenye ugomvi wa kivita lakini ameweza kuingoza kwa miaka mitano kimya wakifanya maendeleo, na kwa maendeleo nadhani wametupita kwa sababu Uhuru Kenyatta kwa hiyo ni mtu mwenye upeo, makini na mahiri ambaye anaitakia mema Afrika na Afrika Mashariki" alisisitiza Lowassa

SOMA Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo Jumamosi

Kutana na Mtatibu Wanyota za Binadamu Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka Comoro

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU WANYOYA ZA BINADAMU DUNIANI KOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO

KWA SASA YUPO TANZANIA MAALIM FADHILI RASHIDI ANA IWEZO WAKUJUWA JAMBOLAKO NAKULI TATUWA KWAMUDA MFUPI

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE

MAALIM FADHILI RASHIDI NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA MIGUU KUWAKA MOTO

KISUKARI VIDONDA VYATUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI PUMU ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIE POTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM ANATOWA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI YEYOTE

NAKUMILIKI MALIZA MAJINI KWAYULE ANAE HITAJI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZA KIUME ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASA (24)

ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YAMVUTO WABISHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE

KUSAFISHA NYOTA NAKUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHAKUTESEKA NJOO UWONE MIUJIZA YA MAALIM FADHILI RASHIDI

CALLING+255719362806/ +255763276239

KWA WHATSAPP IMO +255785786436

Chirwa Atoa ya Moyoni kwa Timu inzani Wake

$
0
0
Chirwa Atoa ya Moyoni kwa Timu inzani Wake
MUDA mfupi baada ya Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kusema straika wa Yanga, Obrey Chirwa, hana hatia na yupo huru kuitumikia timu yake, mchezaji huyo amezipiga mkwara timu pinzani.

Juzi Alhamisi, kamati hiyo ilisema Chirwa na Deus Kaseke ambaye alikuwa Yanga kabla ya kwenda Singida United, hawana hatia baada ya hapo awali kutuhumiwa kumwangusha mwamuzi, Charles Ludovic.

Wawili hao walituhumiwa kutenda kosa hilo katika mechi yao ya mwisho ya Ligi Kuu Bara msimu uliopita dhidi ya Mbao FC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza ambapo Yanga ilifungwa bao 1-0.

Msuva pekee ndiye aliyekutwa na hatia na amepewa onyo kali. Hata hivyo, kwa sasa Msuva anaichezea Difaa Al Jadida ya Morocco.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Chirwa alisema: “Hata kama ningefungiwa kucheza mechi kadhaa za ligi kuu, naamini wachezaji waliopo wangepambana na kuipa matokeo mazuri timu yangu.

“Kwa sasa mimi bado ni majeruhi, lakini siku si nyingi nitarudi uwanjani kuendeleza mapambano waliyoyaanzisha wenzangu katika kutetea ubingwa wetu wa msimu uliopita.

“Nikirudi uwanjani mashabiki wategemee kuuona moto wangu ule wa siku zote na sasa nitapambana sana kuhakikisha timu yangu inatetea ubingwa kwa mara nyingine kwani tuna kikosi kizuri na cha ushindani,” alisema Chirwa.

Chirwa ambaye anasumbuliwa na goti, msimu uliopita alifunga mabao 12 katika Ligi Kuu Bara huku akiibuka Mfungaji Bora wa Kombe la FA akiwa amefunga mabao sita.

Bweni la Wasichana Lachomwa Moto Kenya Saba Wafariki

$
0
0
Bweni la Wasichana  Lachomwa  Moto Kenya Saba Wafariki
Bweni la Shule ya Wasichana ya Moi iliyopo Kibera jijini Nairobi, limeteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo na kusababisha vifo vya wanafunzi saba huku wengine 10 wakijeruhiwa.

Wazazi wakiwachukua watoto wao.
Waziri wa Elimu nchini humo, Fred Matiang’i amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la kuhudhunisha huku akieleza kuwa vifo na majeraha mengi yametokana na kukanyagana baada ya taharuki na wengine kuruka kupitia madirishani ambapo majeruhi wa ajali hiyo wamekimbizwa Hospitali ya Wanawake ya Nairobi kutibiwa.

Waziri wa Elimu nchini humo, Fred Matiang’iakiwatuliza wanafunzi na walimu wa shule hiyo.
Matiang’i ameifunga shule hiyo kwa wiki mbili kutokana na ajali hiyo na kuwataka wazazi wawachukue watoto wao wakati uchunguzi wa moto huo ukiendelea. Ameeleza kuwa wanafunzi wa kidato cha nne watarudi shuleni hapo Ijumaa ijayo kwa ajiri ya maandalizi ya mtihani wa kuhitimu elimu ya sekondari.

Kauli ya Rich Mavoko Baada ya Diamond Kufanya Remix Wimbo wa Fid Q

$
0
0
Kauli ya Rich Mavoko Baada ya Diamond Kufanya Remix Wimbo wa Fid Q
Msanii wa Bongo Flava kutoka label ya WCB, Rich Mavoko ametoa mtazamo wake baada ya watu wengi kumtupia maneno Fid Q kwa kile walichodai amemruhusu Diamond kutupa vijembe kwa Alikiba kupitia ngoma yake ‘Fresh Remix’

August 21, 2017 Fid Q alitoa remix ya ngoma yake Fresh ambayo aliwashirikisha Diamond na Rayvanny ambapo siku kadhaa mbele Fid Q alikiri kusakamwa vilivyo katika mitandao ya kijamii. Kupitia Nipe Tano ya TBC Fm Rich Mavoko amesema;

“Kwangu mimi its easy kwa sababu hakuna muziki unaokwenda bila majibishano, hata mpira wenyewe kuna mabishano ndio maana kuna mtu kama Haji Manara. Kuna watu wanaongea sana, hivi vitu ndio vinaleta chachu ya muziki, kwa sababu hiyo mitandao yao ndio inafanya watu wanakua , kwa hiyo mimi naona kawaida tu,” amesema.

Rich Mavoko ameshatoa ngoma na Fid Q inayokwenda kwa jina la Sheri.

Naachia Wimbo Wangu Nawakalisha Diamond na Ali Kiba- Z Anto

$
0
0
Naachia Wimbo Wangu Nawakalisha Diamond na Ali Kiba- Z Anto
Msanii wa muziki aliyewahi kufanya vizuri na wimbo Malavidavi, Mpenzi Jini na nyingine nyingi, Z Anto, amefunguka kwa kusema kuwa wiki hii ataachia kazi yake mpya huku akidai haamini kama kazi yake hiyo itashindwa kufanya vizuri kwa kuwa Diamond na Alikiba wameachia kazi zao mpya ambazo zinashindanishwa mitandaoni.


 Z Anto amedai yeye atapita katikati ya Diamond na Alikiba kwa kuwa muziki wake unapendwa na watu wa rika zote na pia hauna makundi kama ulivyo wa wawili wao.

“Wote nawaweza sana, muziki wangu ni mtamu na hauna makundi kwahiyo kila mtu anaweza kuusikiliza hata hao bila shaka ni mashabiki wa muziki wangu ndio maana nikasema kuogopa kuachia ngoma sasa hivi kwaajili ya Diamond na Alikiba utakuwa ni ujinga,” alisema Z Anto.

Aliongeza “Binafsi najiamini sana kwa sababu muziki wangu ni mzuri na tayari kuna platfom ambayo niliiweka toka kipindi cha nyumba sema tu ukimya wangu ndio umewapa nafasi hawa ndugu zangu lakini sioni kama nitatizo kwasababu bado nafasi yangu naiona,”

Muimbaji huyo amesema anajua muziki umebadilika sana ndio maana na yeye amejipanga kuvingine ili kukabiliana na watu ambao wanashindana kwa sasa kwenye muziki.

“Kila mtu anatakua kuwa juu zaidi ya mwenzake na ukimya wangu umewapa nafasi wasanii wengi sana na lengo langu ni kufanya vizuri zaidi ndio maana nikasema sishindani na Diamond wala Alikiba mimi nitapita katikati yao na mashabiki ndio wenye maamuzi ya mwisho katika hili kwahiyo mimi ningesema tusubiri kazi mpya waisapport halafu ndio tuanze kupima,” alisema Z Anto.

“Mimi naamini msanii yoyete anaweza kufanya vizuri zaidi ya hata wakongwe kama akijipanga vizuri muziki una sifa hiyo, kwahiyo mimi naweza kusema lolote linaweza kutokea kwenye muziki lisiwe leo au kesho muda ukifika hauwezi kushindana nao, wakati ni ukuta,” alifafanua zaidi.

Katika ujio wake muimbaji huyo amesema tayari ameandaa audio na video ambayo itaanza kutoka na kuleta picha mpya katika muziki wake.

“Kazi zipo tayari kwa sababu ni nyingi naanza na moja moja, siku yoyote kuanzia leo nitaachia kazi moja na baada ya upepo wa hapo nitaendelea kasi hiyo hiyo kadri mambo yanavyokwenda,” alisema Z.


Katika Maisha Hakuna Anayejua Kitatokea Nini Siwezi Kumsema Vibaya Vanessa- Jux

$
0
0
Katika Maisha Hakuna Anayejua Kitatokea Nini Siwezi Kumsema Vibaya Vanessa- Jux
Mkali wa muziki wa RnB Bongo, Jux amesema ingawa wameachana na Vanessa Mdee siyo sababu ya kumsema vibaya.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Utaniua’ ameiambia E-Newz ya EATV kuwa analazimika kuwa na nidhamu hiyo kwa sababu kwenye maisha kuna leo na kesho.

“Unajua katika maisha hakuna anayejua kesho kutatokea nini, mimi siwezi kutoa kauli yoyote kwa sababu Vanessa bado nampenda. Tumefanya vitu vingi sana, nampenda na nitaendelea kumpenda kwa kushirikiana kwenye mambo mengi,” amesema Jux.

Katika hatua nyingine alipoulizwa iwapo Vanessa atamfuata na kumtaka warudiane kama atakuwa tayari, Jux alijibu;

“Siwezi nikaliongelea hilo, sijajua kwa hiyo moment itakuwaje, mimi naishi pia siwezi jua kesho nitakutana na nani kitatokea nini, huwezi jua yeye atakutana na nani kitatokea nini, so siwezi nikatoa hilo jibu sasa hivi lakini tuone itakavyokuwa, tunaendelea kuishi you never know,” amesema.

Kipindi cha mapenzi yao waliweza kutoa wimbo wa pamoja uitwao Juu, pia walishirikishwa katika wimbo wa Nikki wa Pili ‘Safari’.



Ben Aibukia Kwenye Muziki wa Singeli

$
0
0
Ben Aibukia Kwenye Muziki wa Singeli
Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho nchini, Ben Branco Selengo amefunguka na kusema sasa ameamua kuimba muziki wa singeli huku akiwataka wakali wa singeli kujipanga kwani amekuja kuchukua pesa zilizopo kwenye muziki wa singeli.

Ben anasema kwenye filamu hakuna msanii ambaye anaweza kuchukua nafasi yake hivyo ameamua kwenda kwenye muziki kutafuta mkwanja huku akidai kuwa ataendelea kufanya filamu kama kawaida yake.

Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images