Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Makamu wa Rais Akiri Kuchepuka nje ya Ndoa.....

0
0
Makamu wa Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, amekiri wazi kuwa na mchepuko nje ya ndoa miaka 8 iliyopita lakini amekana taarifa zinazosambaa nchini humo kuwa anawapenzi wengi huku akidai taarifa hizo zina lengo la kumchafulia jina.

Bwana Ramaphosa amesema anaamini kuwa taarifa zinakuzwa ili kumuharibia mipango yake ya kugombea urais kupitia Chama The African National Congress (ANC), wakati Rais Jacob Zuma atakapong’atuka madarakani.

Taarifa kutoka Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) zinasema kuwa wadukuzi walidukua mawasiliano yake kwa njia ya barua pepe ili kuthibitisha uhusiano wake wa siri nje ya ndoa na daktari mmoja nchini humo.

Kwenye mahojiano yake na gazeti la Sunday Independent la nchini Afrika Kusini, Bwana Ramaphosa amekiri kuwa na mwananmke nje ya ndoa miaka nane iliyopita ila taarifa za sasa zina lengo la kumchafulia jina huku gazeti hilo likieleza kuwa lilikatazwa na Ramaphosa kuchapisha e-mail zilizodukuliwa.

Cyril Ramaphosa ana mke na watoto wanne na ni mfanyabiashara mkubwa na ni moja ya viongozi wenye ushawishi ndani ya Chama tawala nchini Afrika Kusini ANC, na ana nafasi kubwa ya kumrithi Rais Jacob Zuma, kwenye uchaguzi ujao.

Jaji David Maraga wa Kenya Ametuonyesha Tofauti Kubwa Kati ya Msomi na Aliye Elimika

0
0

Zifuatazo ni sifa za Mtu aliye Elimika
Haogopi
Anajiamini
Hayumbishwi
Kuuwawa Kwake ni sehemu ya Uzalendo wake kwa nchi aliyopo
Ana maamuzi ya mwisho na ya Kishujaa
Msikivu na makini mbele ya Hoja husika
Humtumainia sana Mwenyezi Mungu

Zifuatazo ni sifa za Mtu Msomi
Usomi wake ni wa GPA tu na siyo wa Kiutendaji
Mwepesi Kushawishika
Mnafiki
Muoga sana wa Kufa / Kuuwawa
Huwa si mtulivu na asiyejielewa muda mwingi kuwa anataka nini
Anapenda sana Kujipendekeza na Mfitini
Humkumbuka Mwenyezi Mungu pale tu akiwa na shida au vyuma Kwake vimemkazia


Je na Wewe mwana JF baada ya Jaji David Maraga kutuonyesha kweli maana halisi ya Mtu aliye Elimika unadhani na Wewe hapo ulipo kutokana na hali yako ya Maisha na Utendaji wako hadi kwa Wanasiasa na Viongozi wetu nao wameelimika kama ' Jaji ' au wengi wetu / wengi wao ni Wasomi tu?

Karibuni.

Chid Benz Amvuta Jay Z, Asema ile ya 2PAC Alikua Anatania, Ukweli ni huu

0
0
Baada ya sakata la kusema amefanya collabo na Tupac na kuleta mtafaruku mkubwa kwa mashabiki huku wakimtolea maneno makali wakisema amesha athirika kiakili kwa madawa ya kulevya kwa kuwa Tupac ni marehemu, sasa Chid Benz kuja na collabo na Jay Z.

Akifanya mahojiano kwenye kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na East Africa Television and Radio, Chid Benz amesema Collabo hiyo ameifanya na Jay Z huku 'chorus' yake ikifanywa na mke wa msanii hyo Beyonce, lakini anataka atoe 'chorus' hiyo na amuweke msanii wa Bongo Linah Sanga.

Chid Benz aliendelea kusema kuwa kauli hiyo anaitoa akiwa yuko sawa na sio mtu aliyelewa na madawa ya kulevya, na kwamba collabo hiyo imeshafanyika na cd yake ipo nyumbani kwa mama yake 'Mama Chid'.

 VIDEO:

Pendeza na Kessy Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa Bila Madhara yoyote

0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA


1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/
(21) ENGEZA  MGUU_80,000/    

 TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM                      (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO,

Mtoto wa Mobetto Azidi Kumpasua Kichwa Zari Aamua Kumfungia Safari Hadi Bongo Kupata Ukweli

0
0
Mtoto wa Mobetto Azidi Kumpasua Kichwa Zari Aamua Kumfungia Safari  Hadi Bongo Kupata Ukweli
BAADA ya maneno mengi kusemwa Bongo kufuatia madai ya bwana’ke kuzaa na mwanamitindo mwenye jina kubwa, Hamisa Hassan Mobetto, mwanamama mjasiriamali mwenye jina kubwa Afrika Mashariki, Zarina Hassan Tiale ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuendelea kuliamsha dude baada ya kutinga Bongo na kuanza kudodosa ili kupata ukweli wa ishu hiyo.

Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho ni makini, awali Zari alitinga Bongo mapema wiki iliyopita na kupigwa chabo na ‘wadakuz’ akiwa nyumbani kwa jamaa huyo ambaye ni msanii wa Bongo Fleva huko Madale jijini Dar.

Ilidaiwa kwamba, hata hivyo, hakukaa sana kwani aliondoka kwenda kwenye kumbukumbu ya siku 40 za kifo cha mama yake, Halima Hassan nchini Uganda kabla ya kurejea Bongo wikiendi iliyopita.
“Kwa taarifa yenu Zari amejaa tele Bongo na lengo lake ni kuchimba na kupata ukweli juu ya madai ya Hamisa kuzaa na bwana’ke.

“Unajua akiwa Sauz hapati mtiririko mzuri wa kinachoendelea Bongo ndiyo maana ameona aje kuchimba mwenyewe ili ajue mbivu na mbichi na ajue nini cha kufanya,” kilidai chanzo hicho.
Kilizidi kutiririsha madai kwamba, endapo Zari atabaini ukweli kuhusu mzazi mwenzie huyo kuzaa na Hamisa, basi kuna uamuzi mzito atachukua.

Hata hivyo, gazeti hili lilizungumza na mmoja wa memba wa familia ya msanii huyo ambaye amezaa na Zari watoto wawili ambaye alithibitisha uwepo wa mwanamama huyo, lakini akaomba hifadhi ya jina.

“Wewe jua tu kwamba, yupo, amejaa tele. Kuhusu hayo mambo yake na Hamisa mimi sijui maana sijamsikia akilizungumzia. So labda anafanya kimyakimya,” alisema memba huyo wa familia.

Kwa upande wake Hamisa, habari zilizolifikia Ijumaa Wikienda katika dakika za lala salama kuelekea kiwandani zilidokeza kuwa, mrembo huyo kwa sasa ameamua kumuhudumia mwanaye mwenyewe na kwamba, maandalizi ya shughuli ya 40 ya kumtoa mtoto wake huyo yamepamba moto.

Shughuli za Bunge la 11 Kuanza Kesho Mjini Dodoma

0
0
Shughuli za Bunge la 11 Kuanza Kesho Mjini Dodoma
Mkutano wa nane wa Bunge la 11 unatarajiwa kuanza kesho mjini Dodoma.

Kwa mujibu wa ofisi ya Bunge ratiba ya bunge itatolewa leo baada ya kamati ya uongozi kukutana na kuamua uwasilishwaji wa mswada iliyopo

Katika mkutano huo wabunge wa chama cha Cuf wanatarajiwa kuapishwa kutokana na baadhi ya wabunge kufukuzwa baada ya kukikuka utaratibu na miongozo ya chama hicho ikiwa ni pamoja na kutohudhuria vikao.

Juzi mbunge mmoja ambaye alitarajiwa kuapishwa na wenzake kesho Mbunge mteule wa Viti Maalum Hindu Mwenda alifariki dunia na kuzikwa jana makaburi ya Kisutu.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF, upande wa Profesa Ibrahim Lipumba, Magdalena Sakaya amesema chama hicho kimepokea kwa masikitiko kifo cha

Hindu alifariki dunia ghafla nyumbani kwake Kibada Kigamboni.

Sakaya amesema  Hindu alikuwa ni mpambanaji  na mtu mwenye kukijenga chama hicho  kuanzia miaka ya 90  hivyo ni pigo kubwa kuondoka kwake.

‘’Hata ukifika  Tabora leo hii hakuna mwanachama wa CUF asiyemjua Hindu’ ’amesema Sakaya.

“Sijui niseme nini maana zilikuwa zimebaki siku chache tu aende Dodoma kuapishwa baada ya kuteuliwa na Tume ya Taifa ya

Uchaguzi (NEC) mwezi uliopita,” amesema Sakaya ambaye pia ni Mbunge wa Kaliua Tabora.



Fid Q: Nawaonea Huruma Sana Watoto wa Kizazi Hiki ni Ali Kiba na Fresh Remix

0
0
Fid Q: Nawaonea Huruma Sana Watoto wa Kizazi Hiki ni Ali Kiba na Fresh Remix
Msanii mkongwe wa muziki wa hip hop kutoka Mwanza, Fareed Kubanda maarufu kama Fid Q, amesema anasikitishwa na hatama ya maisha ya kizazi cha sasa, kwani kimeharibiwa kwa kiasi kikubwa na mitandao.


Rapa huyo amesema kizazi cha sasa hakina muda kabisa wa kujisomea vitabu ili waweze kujiongezea ujuzi, kwani mabadiliko ya teknolojia yamechukua sehemu kubwa ya maisha yao.

“Nawaonea huruma sana watoto wa kizazi hichi, mtu anatoka mapumziko anakutana na stori ya Alikiba katoa fresh remix, itamvuruga kabisa kwenda kuzingatia somo la hesabu ambalo linafuatia, sijui tunafanyaje lakini nawaonea huruma sana, sababu mi ni zao la analojia”, Fid Q alikiambia kipindi cha Bongo Fleva Top 20 cha EA Radio weekend hii.

Fid Q ambaye kwa sasa yupo na kazi mbili sokoni ambazo ni ‘Ulimi Mbili’ na ‘Fresh’, amesema kwa kipindi hiki cha digitali anapata changamoto kubwa anaposoma vitabu mitandaoni, kwani muda mwengine hukutana na matukio mengine yanayomfanya asitishe zoezi hilo, tofauti na kama angekuwa anasoma kitabu cha kawaida.



Dayna Apata Funzo Asimulia Alivyotelekeza Akiwa na Mimba

0
0
Dayna Apata Funzo Asimulia  Alivyotelekeza Akiwa na Mimba
Msanii Dayna amesema kwamba kitendo cha kupata mtoto kabla hajatimiza umri wa miaka 18 ni tukio ambalo limempa somo kubwa maishani mwake, kwani mpaka sasa anaogopa kuruka ruka.

 Dayna amesema kwamba pamoja na baba wa mtoto wake kumtelekeza, anapambana kuhakikisha mtoto wake anapata mahitaji yake huku akidai hatorudia kutokuwa makini anapoingia kwenye mahusiano.

"Mimi nilikuwa mdogo sana, unajua sisi wanawake tunafundishwa kupenda, nimejifunza sana, huoni mpaka sasa Rahma ana miaka sijui 10 na kitu lakini hana ndugu yake?, kwa sababu napambana kuhakikisha mtoto wangu anapata mahitaji yote.  Mimi nilijifungua nikiwa mdogo sana hata miaka 18 sikufikisha, nilikuwa na chuki na baba wa mtoto wangu sana lakini nilimuomba Mungu aniondolee roho ya chuki kwa sababu hata nikivimba naye yeye ndiyo baba yake", alisema Dayna.
Dayna ambaye kwa sasa ana kazi mpya ya 'Chovya', amesema iwapo baba mtoto wake atakuja kudai mtoto wake atampa bila kinyongo, kwa kuwa yeye ndiye baba halali wa huyo mtoto na wala hakuna mwingine.

Hakimu Atoa Siku 14 kwa Pande Mbili Kuwasilisha Hoja Katika Kesi ya Lissu ya 'Dikteta Uchwara

0
0
Hakimu Atoa Siku 14 kwa Pande Mbili Kuwasilisha Hoja Katika Kesi ya Lissu ya 'Dikteta Uchwara
Upande wa mashtaka umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa imefunga ushahidi katika kesi ya ‘Dikteta Uchwara’ inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Wakili wa Serikali, Mutalemwa Kishenyi amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa kuwa kesi hiyo imeitishwa kwa ajili ya ushahidi, lakini wamemaliza ushahidi.

Baada ya kueleza hayo, Lissu amesema Wakili wake Peter Kibatala hayupo, isipokuwa anawasilisha hoja kwamba hana kesi ya kujibu ambapo hata hivyo, Wakili Kishenyi amedai kuwa hakuna kipengele kinachoruhusu mshtakiwa kusema hana kesi ya kujibu ama la.

Kutokana na hatua hiyo, Lissu amedai kuwa hoja za upande wa mashtaka sio sahihi, kwa sababu kifungu cha 230 cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinatoa nafasi kueleza kama kuna kesi ya kujibu ama la akisema

”Hivyo, tunaomba tupate fursa kwamba kwa ushahidi uliopo katika record hakuna kesi ya kujibu.”

Hata hivyo, Wakili Kishenyi alidai kuwa anasisitiza kwamba hakuna kifungu cha namna hiyo, hivyo Mahakama itoe uamuzi kama ana kesi ya kujibu ama la.

Kutokana na mvutano huo, Hakimu Mwambapa amesema anakubaliana na hoja za upande wa mashtaka kwamba hakuna kifungu kinachomruhusu mshtakiwa kueleza kama ana kesi ya kujibu ama la, isipokuwa ana haki ya kuieleza Mahakama.

Hakimu Mwambapa amesema anatoa siku 14 kwa pande zote mbili kuwasilisha hoja zao September 18, 2017 na October 4, 2017 atatoa uamuzi kama mshtakiwa ana kesi ya kujibu ama la.



Korea Kaskazini Inajiandaa Kufanya Majaribio Zaidi ya Makombora

0
0
Korea Kaskazini inajiandaa kufanya majaribio zaidi ya makombora
Korea Kusini inasema kuwa kuna dalili kuwa Korea Kaskazini inapanga majaribio zaidi ya makombora hususan makombora ya masafa marefu.

Maafisa wa ulinzi wamekuwa wakilishauri bunge mjini Seoul baada ya Korea kulifanyia jaribio bomu la nyuklia mwioshoni mwa wiki.
Korea Kusini imejibu kwa kufanya majaribio kwa kurusha makombora kwa kutumia ndege na kutoka ardhini.

Marekani imeonya kuwa tisho lolote kwake na kwa washirika wake litajipigwa vikali kijeshi.
Korea Kusini inasema kuwa ililifanyia majaribio bomu la haidrojeni ambalo linaweza kuwekwa kwa kombora la masafa marefu.

Baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kufanya kikao cha dharura baadaye leo kujadili hatua za kuchukua.
Chang Kyung-soo, ambaye ni afisi kutoka wizara ya ulinzia aliliambia bunge, "tunaendelea kuona dalili za uwezekano wa makombora zaidi ya masafa marefu. Pia tunaweza kutabiri kuwa Korea Kaskazini huenda ikarusha kombora la masafa marefu.

Wizara hiyo pia ililiambia bunge kuwa huenda Marekani ikapeleka manowari wa nyuklia ya kubeba ndege katika rasi ya Korea.

Acacia Kupunguza Shughuli za Uendeshaji na Uzalishaji Mgodi wa Bulyanhulu

0
0
Acacia Kupunguza Shughuli za Uendeshaji na Uzalishaji Mgodi wa Bulyanhulu
KAMPUNI ya Acacia imetangaza lengo lake la kupunguza shughuli za uendeshaji na uzalishaji katika Mgodi wa Bulyanhulu. Uamuzi huu umepelekewa na upungufu wa mzunguko wa pesa uliosababishwa na zuio la usafirishaji wa makinikia kwenda nje ya nchi na mazingira ya uendeshaji kuwa magumu.

Tangu zuio la mchanga wa dhahabu na shaba liwekwe na Serikali mnamo Machi 3, 2017 na kuathiri takribani 35% ya uzalishaji wa mwaka, Acacia imekuwa na takribani mchanga wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 265 ndani ya nchi kulingana na bei za sasa

Katika kusaidia kukabili hasara hizi, Acacia imeamua kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kupunguza uzalishaji katika mgodi wa Bulyanhulu ili kulinda ajira za wafanyakazi na watoa huduma mgodini ambao ni Watanzania.

Kampuni ya Acacia bado ina matumaini katika majadiliano yanayoendelea kati ya Barrick na serikali ikiamini yatapelekea muafaka juu ya zuio la makinikia na mazingira ya uendeshaji yatakayowezesha tathmini mpya ya hali ya uendeshaji kwa siku zijazo.







Wanaume Lindi Walia na Vipigo Kutoka kwa Wake Zao

0
0
Wanaume Lindi Walia na Vipigo Kutoka kwa Wake Zao
BAADHI ya wanaume wa Kata  ya  Kilolambwani wilayani  Lindi wamelalamika kuteswa na wake zao kwa kuwashurutisha kufanya kazi kinyume na imani za dini.

Wakizungumza kwa niaba  ya wenzao kwenye utambulisho wa mradi wa usawa na jinsia jana, walisema tangu mashirika na asasi za raia zianze kutoa elimu kuhusu haki za wanawake na watoto tabia za wake zao zimebadilika.

Mmoja wa wanaume hao, Farijala Mchopa, alisema elimu inayotolewa na mashirika hayo inakwenda kinyume na imani ya dini zao na hivi sasa wanawake hao hawatawaliki kinyume na matakwa ya dini yao.

Mchopa  alishauri asasi inayoratibu mafunzo hayo, Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto cha Lindi (LIWOPAC) na shirika la kimataifa la misaada la OXFA, kuhamasisha zaidi    watu wafunge ndoa za serikali  usawa unaohubiriwa uweze kukamilika na  kukubalika  kwa pande  zote.

“Usawa huu ili ukubalike, mashirika haya yahamasishe kuanza mchakato wa kuanzisha vyama na mashirika ya kutetea haki za wanaume   na kuchangishana mahali,”alisema Mchopa.

Msimamizi wa mradi huo, Romana Colman, licha ya kueleza lengo la mradi huo, alisema asasi za  iraia ikiwamo LIWOPAC hazina nia ya kufarakanisha jamii bali haki na usawa ndiyo msingi wa amani na

Mahakama Imeruhusu Polisi Kumuhoji Manji na Wenzake Ili Kukamilisha Upelelezi

0
0
Mahakama Imeruhusu Polisi Kumuhoji Manji na Wenzake Ili Kukamilisha Upelelezi
 Mahakàma ya Hakimu Mkazi Kisutu imeruhusu Mfanyabiashara Yusuf Manji na wenzake wahojiwe na Polisi ili kukamilisha upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo amesema ameruhusu washtakiwa wahojiwe baada ya kuandikiwa barua na Mkuu wa Upelelezi (ZCO).

”Hivyo nikisema Mahakama izuie wasihojiwe itakuwa tunapingana nao, wakati kila siku tunapigiana kelele kuhusu upelelezi kukamilika. Hivyo, sifikirii kesi hii kila siku iwe inatajwa tu.”

Hakimu Shahidi alimkabidhi Manji na washtakiwa wenzake kwa Koplo Dotto ambapo amemtaka hadi kesho kwenye muda wa kazi wawe wamerudishwa Mahakamani.

Mbali ya Manji washtakiwa wengine ni Deogratius Kisinda, Abdallah Sangey na Thobias Fwere.





Z Anto: Kutoka Kimapenzi na Mtu Aliyekuzidi Umri Ili Kutafuta Kiki ni Ushamba

0
0
Z Anto: Kutoka Kimapenzi na Mtu Aliyekuzidi Umri Ili Kutafuta Kiki ni Ushamba
Msanii Z Anto ambaye amewahi kutamba na ngoma kibao kali kama Binti kiziwi, Mpenzi jini amefunguka na kuwachana baadhi ya wasanii wa bongo ambao wanatumia mahusiano ya kimapenzi kama njia ya kutafuta kuzungumziwa katika jamii na kusema huo ni ushamba
 
Z Anto amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Instgram na kuwaambia wasanii kuwa kutoka kimapenzi na mtu ambaye amekuzidi umri kwa lengo la kutaka kuzungumziwa kwenye jamii au kutafuta kiki si jambo jema na halistahili. 

"Mapenz ni uhuru haitajalisha ulimpenda yupo vipi mrefu mfupi, mnene au mwembamba, mkubwa ama mdogo ila kutoka kimapenzi na mtu aliyekuzidi umri kwa lengo la kutaka watu wakuzungumzie kwenye jamii inayokuzunguka kwa wasanii wenzangu wanasema kutafutia kiki ni ushamba" alisema Z Anto 

Mbali na hilo Z Anto pia amesema anatarajia kurudi rasmi kwenye muziki wa bongo fleva kwa kuachia ngoma yake mpya na kichupa kipya Septemba 8, 2017 siku ya Ijumaa na kusema anaamini ngoma yake hiyo itamrudisha kwenye nafasi yake, kwa kuwa yeye siku zote hufanya muziki mzuri akiamini mashabiki ndicho kitu wanataka. 


Video: Wimbo Mpya wa Saida Karoli Belle 9 na G Nako Ndani ya Kichaka

0
0
Video: Wimbo Mpya wa Saida Karoli Belle 9 na G Nako Ndani ya Kichaka
MSANII mkongwe wa muziki wa asili, Saida Karoli ambaye hivi karibuni amekuwa akitamba na wimbo wake wa Orugambo baada ya kurudi kwenye game ya muziki, mkali huyo leo September 4, 2017 ameliamsha dude kwa kuachia video mpya ya wimbo wake ‘Kichaka’.

Katika wimbo huyo, Saida mwenye sauti ya kipekee, amewashirikisha G Nako wa Weusi na Belle 9 ambao kwa pamoja wameutendea haki wimbo huo.
Ngoma hiyo ambayo imeshutiwa hapa hapa Bongo, imeaandaliwa na Director Hanscana.


Neno la Ali Kiba kwa Mashabiki Wake Baada ya Kumfikisha Watazamaji Zaidi ya Milioni 4 Ndani ya Siku Kumi

0
0
Neno la Ali Kiba kwa Mashabiki Wake Baada ya Kumfikisha Watazamaji Zaidi ya Milioni 4 Ndani ya Siku Kumi
Msanii Alikiba ambaye sasa anatamba na ngoma yake mpya 'Seduce me' amefunguka na kuwapa neno la pongezi mashabiki zake baada ya kuiwezesha ngoma yake hiyo mpya kufikisha watazamaji zaidi ya milioni nne ndani ya siku 10.

Alikiba ametumia ukurasa wake wa Instagram kuwashakuru mashabiki zake na kuendelea kuifanya ngoma hiyo kushika nafasi ya kwanza katika video ambazo zinafanya vizuri Tanzania toka ilipotoka Agosti 25, 2017 na kushuka kwa nafasi moja kwa masaa kadha na baadaye kurejea katika nafasi ya kwanza mpaka sasa.

"Seduce Me imefikisha watazamaji milioni 4 ndani ya siku 10 na bado inaendelea kushika nafasi ya kwanza kwa video zinazo 'trend' Tanzania, nawakubali wote na kuwathamini lakini pia nawapenda sana Tanzania" aliandika Alikiba

Unaweza kuendelea kuburudika na wimbo huu mpya wa Alikiba 'Seduce Me'


Wazili wa Elimu Nchini Kenya Amesema Moto Uliowaua wanafunzi 9 wa Shule Ulianzishwa Makusudi

0
0
Wazili wa Elimu Nchini Kenya Amesema Moto Uliowaua wanafunzi 9 wa Shule Ulianzishwa  Makusudi
Waziri wa elimu nchini Kenya Fred Matiang'i amewaambia waandishi wa habari kuwa moto amboa ulitokea katika shule moja ya bweni kwenye mji mkuu Nairobi mwishoni mwa wiki, ambapo wanafunzi 9 walifariki ulianzishwa makusudi.

"Moto huo haukuwa ajali bali ulianzishwa makusudi", alisema Matiang'i.
Ripoti za vyombo vya habari zilisema kuwa takriban wasichana 10 wa shule ya wasichana ya Moi bado wamelazwa hospitalini.
Awali Matiang'i alisema kuwa shule hiyo itafungwa kwa wiki mbili huku uchunguzi ukianzishwa kuhusiana na sababu ya moto huo.
Hata hivyo alisema kuwa wanafunzi wa kidato cha nne wataendelea na masomo yao ifikiapo siku ya Ijumaa na watasaidiwa kuendelea na masomo yao wakati ambapo wanajianda kufanya mtihani wa kidato cha nne wa KCSE.

Kulingana na gazeti la Daily Nation nchini humo, mwanafunzi mmoja wa kidato cha kwanza ambaye alikuwa miongoni mwa wale waliotibiwa baada ya kisa hicho alisema kuwa moto huo ulianza mwendo wa saa saba usiku.
Watoto 20 wafariki katika ajali Afrika Kusini
Alisema kuwa bweni lililochomeka lilikuwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza na kwamba kulikuwa na makelele ya wanafunzi waliojaribu kujinusuru.

Mabadiriko ya Ratiba ya Ligi Kuu Yamtibua Kocha wa Yanga

0
0
Mabadiriko ya Ratiba ya Ligi Kuu Yamtibua Kocha wa Yanga
Kocha Mkuu wa Yanga, George Lwandamina amechoshwa na kitendo Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania TFF kubadili mara kwa mara ratiba ya Ligi Kuu Tanzania bara na kusema kitendo hicho kinaathiri utaratibu wa klabu hiyo.

Lwandamina amesema hayo kupitia katika ukurasa wa facebook wa Yanga na kusema kuwa timu yake leo ilipaswa kusafiri na kuelekea mjini Njombe ambapo ilitakiwa icheze na klabu ya Njombe Mji Septemba 6 baada ya ratiba ya awali kubadilishwa ambapo walitakiwa kukutana Septemba 3, 2017.

"Inasikitisha kuona ratiba ya ligi ikibadilika mara kwa mara, jambo hili lina athari kubwa, tulipanga kusafiri leo kwa ajili ya mchezo wa tarehe 6,lakini sasa tunalazimika kuongeza siku zaidi, hii ina maana kuwa 'program' zote zilizowekwa awali zinavurugika" alisema George Lwandamina.

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF) imefanya mabadiliko ya ratiba ya Ligi Kuu Tanzania bara 2017/2018 kwa mara ya tatu ambapo sasa michezo yote ambayo ilipaswa kucheza Jumatano ya wiki hii itachezwa siku ya Jumamosi Septemba 9, 2017 na baada ya hapo ndipo itatoa ratiba nyingine ya Ligi Kuu Tanzania Bara 2017/2018.



Jaji Mstaafu Thomas Mihayo Kuongoza Kamati ya Kutafuta Zabuni Timu ya Simba

0
0
Jaji Mstaafu Thomas Mihayo Kuongoza Kamati ya Kutafuta Zabuni Timu ya Simba
Klabu ya Simba imemtangaza Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu, Thomas Mihayo kuwa  mwenyekiti wa kamati maalum ya  kumtafuta mzabuni ambaye atanunua hisa  asilimia 50  za timu hiyo  kwa mujibu wa mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Afisa Habari wa klabu hiyo, Hajji Manara imesema kuwa mbali ya Jaji Mstaafu huyo, wajumbe wengine wa kamati hiyo ni  Wakili Damas Ndumbaro, Mbunge wa Ilala, Azzan Zungu, mtaalam wa masuala ya manunuzi,  Yussuf  Majjid Nassor na Abdulrazak Badru ambaye ni Mkurugenzi wa Bodi ua Mikopo ya Elimu ya Juu Tanzania.

Manara alisema kuwa kamat hiyo itakutana  Septemba 7 (Alhamis) kuanza kazi ya kuwajadili wanachama ambao watataka kuzinunua hisa hizo ambapo watafuata sheria za manunuzi ya umma.

Sheria hiyo inawapa wanachama hao kukaa siku 45 kabla ya kumtangaza mzabuni wa timu hiyo kwa mujibu wa sheria. Klabu ya Simba imepyisha muunda mpya wa uendeshaji ambapo kwa sasa itakuwa chini ya utaratibu wa hisa.

Klabu hiyo itamiliki hisa 50 ambazo ni sawa na Sh bilioni 20  na asilimia zilizobaki zitakuwa kwa ajili ya wanachama au wabia ambao watagawana asilimia 50  (Sh bilioni 20).

“Nawaomba wanachama kuwa na utulivu mkubwa kwa kipindi hiki ambacho ni muhimu kuifanya klabu kuwa bora ndani na nje ya uwanja. Lengo ni kuwa katika mfumo wa kisasa ambao utaifanya klabu yetu kuwa bora Tanzania na nje ya mipaka yake,” alisema Manara.

Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images