Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Raia Wawili wa China Wafukuzwa Nchini

$
0
0

Raia Wawili wa China Wafukuzwa Nchini
Uongozi wa mkoa wa Morogoro umewakamata raia wawili kutoka nchini China na kuwaamuru kurejea kwao baada ya kukaidi mara kadha amri zilizokuwa zikiwataka kusimamisha shughuli walizokuwa wakizifanya kinyume cha sheria katika kiwanda wanachokimiliki cha Marumaru cha Zhong Fenq kilichpo katika kijiji cha Maseyu.

Hatua hiyo inakuja baada ya Waziri mkuu kutoa agizo kutokana na malalamiko ya Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Omary Mgumba kuwa wawekezaji hao kutoka China wanaendesha shughuli za uchimbaji bila ya kuwa na kibali.

Ambapo Mgumba alieleza kuwa tangu mwaka 2010 wawekezaji hao wameendesha shughuli zao bila kulipa kodi za Serikali na tozo za halmashauri, hivyo kuikosesha Serikali mapato.

Mbunge huyo ambaye machimbo hayo yako jimboni kwake, alisema licha ya uongozi wa mkoa kwenda eneo hilo na kuizuia kampuni kuendelea na uchimbaji hadi itakapopata vibali ilikaidi na kuendelea na shughuli zake kama kawaida.

Majaliwa alisema iwapo wahusika watabainika kuwa hawajafuata sheria, kanuni na utaratibu hatua zichukuliwe dhidi yao ikiwa ni pamoja na kuwaondoa katika eneo hilo chini ya ulinzi na kuwasiliana na ubalozi wa China nchini.

Hatimae, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt Stephen Kebwe alitoa agizo kwa vyombo vya ulinzi kuwakamata raia hao na kuamuru warudishwe nchini kwao baada ya kugundulika wanafanya kazi bila kufuata utaratibu,sheria, na kanuni za nchi.



Ester Bulaya Atoa Neno kwa Wananchi

$
0
0
Ester Bulaya Atoa Neno  kwa Wananchi
Mbunge wa Bunda Mjini kwa tiketi ya (CHADEMA) Ester Amos Bulaya amefunguka kwa kuwashukuru wananchi wa Bunda, Mara na Watanzania kiujumla kwa kuacha kufanya mambo yao na kumuombe yeye kipindi alipokuwa anaumwa.

Bulaya ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa twitter ikiwa zimepita wiki mbili tokea Mbunge huyo kuzidiwa na kupelekwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi baada ya kupewa rufaa katika hospitali aliyokuwa amelazwa awali ya Mkoa wa Mara.
"Namshukuru Mungu naendelea vyema, asanteni wanabunda, Mara na Watazania wote kwa maombi yenu, afya yangu inazidi kuimarika. 'God is good", aliandika Bulaya.



Hali ya Ukavu Katika Baadhi ya Maeneo Yaja- TMA

$
0
0
Hali ya Ukavu Katika Baadhi ya Maeneo Yaja- TMA
Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imesema mtawanyiko hafifu wa mvua na vipindi virefu vya ukavu vinatarajiwa kujitokeza katika baadhi ya maeneo katika kipindi cha msimu wa mvua wa Oktoba hadi Desemba mwaka huu.

Mkurugenzi mkuu wa TMA, Dk Agness Kijazi amesema hayo leo Jumatatu mikoa itakayoathirika ni Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro na visiwa vya Unguja na Pemba.

Dk Kijazi amezitaka mamlaka husika kama vile wadau wa afya, menejmenti za maafa, mamlaka za miji na wadau wengine kuchukua hatua stahiki katika kupunguza athari mbaya zinazoweza kutokea katika msimu wa mvua za vuli 2017.

"Wafugaji wanashauriwa kuvuna mifugo yao ikiwa katika hali nzuri kiafya na pia kuvuna maji na wahifadhi malisho ili kukidhi mahitaji katika kipindi cha upungufu," amesema Dk Kijazi.

     

Wenye Mamlaka ya Kuniagiza ni Wananchi wa Nzega Pamoja na Rais Ila Siagizwi na Kila Mtu

$
0
0
Wenye Mamlaka ya Kuniagiza ni Wananchi wa Nzega Pamoja na Rais Ila Siagizwi na Kila Mtu
Naibu Waziri wa Afya, Hamisi Kigwangalla amefunguka na kusema haagizwi na kila mtu kwa kuwa ni kiongozi bali wenye mamlaka ya kufanya hivyo ni wananchi wake wa Nzega vijijini pamoja na maagizo anayoyapata kutoka Rais  wa nchi.

Mh. Kigwangalla ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo watu mbalimbali wamekuwa na mawazo tofauti tangu alipohoji suala la ajira nchini na baadhi ya watu kumuagiza kwa Mh. Rais kufikisha ujumbe kuhusu hali ilivyo mitaani haswa kwa vijana.
 Kutokana na ombi hilo Mh Kigwangala alijibu kwa mtindo wa swali na kusema, "Mnanitukana halafu mnanituma? Wenye mamlaka ya kuniagiza ni wananchi wa Nzega Vijijini tu kwa upande mmoja, na Rais kwa upande wa pili! wengine No" Dkt. Kigwangalla.
Pamoja na jibu hilo wapo ambao walihoji uongozi wake wa kuwatumikia viongozi wa Nzega wakati yeye ni Naibu Waziri wa Tanzania
"Yes...natumikia sekta tano za Wizara kwa maelekezo na maagizo ya Rais tu basi! Ambayo yapo kwenye dhamana aliyonipa, siagizwi na kila mtu" Kigwangalla

Kupitia ukurasa wake huo ambao umechangamka tangu wiki iliyopita alipoweka maoni yake juu ya usaili wa awamu ya kwanza kwa wanaotafuta ajira katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) uliyofanyika Agosti 30, 2017 na kuuliza kwamba kama picha hiyo inaashiria ukubwa wa tatizo la ajira nchini au watu wanachagua sana kazi za kwenda jambo ambalo liliibua mijadala mingi ambapo wengine wakihoji kwa nini yeye kakubali kuajiriwa.

Baadhi ya jumbe ambazo zipo kwenye ukurasa wa Mh. Kigwangala zenye maoni tofauti
Aidha pamoja na majibu ya kiongozi huyo hususani kuwataka vijana wajiajiri  wapo ambao wamemtaka yeye kama angeonyesha mfano kwa kukataa nafasi ambayo amepewa na Rais Magufuli  ili watu waamini kwamba ni muumini wa kujiajiri.

Pamoja na swali hilo kutoka kwa wachangia hoja, Mh. Kigwangalla alijibu "Ulitegemea nikatae kuitumikia nchi yangu. Ulitegemea nitumwe kazi na Rais wa nchi yangu nikatae? Uzalendo wa wapi huo. Nidhamu ya wapi hiyo?



Bomu la Vita Kuu ya Dunia Yatenguliwa na Wataalamu

$
0
0
Bomu la Vita Kuu ya Dunia Yatenguliwa na Wataalamu
Wataalamu wa kutegua mabomu mjini Frankfurt, Ujerumani siku ya Jumapili walifanikiwa kutegua bomu kubwa ambalo halikuwa limelipuka ambalo liliangushwa wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.

Bomu hilo la tani 1.4 kutoka Uingereza liligunduliwa katika eneo la ujenzi Jumatano.

Habari hizo zilipokelewa kwa shangwe na watu zaidi ya 65,000 ambao walikuwa wamehamishwa maeneo yao kwa sababu za kiusalama baada ya bomu hilo kuteguliwa.

Hiyo ilikuwa idadi kubwa zaidi ya watu kuhamishwa tangu kutokea kwa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia nchini Ujerumani, na shughuli hiyo ilihusisha mamia ya maafisa wa serikali.

Maeneo ambayo watu walihamishwa yalikuwa katika mtaa wa Westend, na ni pamoja na hospitali kadha, nyumba za kuwatunza wagonjwa na hata katika Benki Kuu ya Ujerumani.

Inaaminika kwamba kuna mamia ya maelfu ya mabomu ya wakati wa vita ambayo hayakulipuliwa ambayo yametapakaa kote Ujerumani.

Wazee wa Manispaa ya Ubungo Wapata Neema

$
0
0
Wazee wa Manispaa ya Ubungo Wapata Neema
Wazee zaidi ya 7,000 wa Manispaa ya Ubungo, wamekabidhiwa vitambulisho vya msamaha wa wa matibabu bure kwa wazee ili kuwasaidia wasiojiweza kupata huduma hiyo.

Mpango huo umezinduliwa leo Jumatatu na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ambapo alikabidhi kadi hizo kwa wazee zaidi ya 100 kwa niaba ya wenzao katika viwanja vya Tip -Sinza.

Mwalimu ameeleza kufurahishwa na hatua iliyochukuliwa na Manispaa ya Ubungo kwa kutimiza ahadi ya Rais John Magufuli ya  kuweka  utaratibu huo wa matibabu bure.

"Nimefurahishwa na hatua hii. Leo natangaza ramsi mmeingia katika rekodi zangu za kuwa manispaa inayowajali wazee. Mimi mwenyewe niwahi kukaa Ubungo wakati nasoma chuo kikuu mlimani nawashukuru sana kwa jambo hili,"amesema Mwalimu.

Amesema wazee wana changamoto mbalimbali ikiwamo kipato kidogo jambo linalosababisha miongoni kushindwa kupata matibabu kwa ufanisi hivyo hatua hiyo itasaidia kupata huduma hizo.

Aliongeza kuwa ni hatua hiyo ni njia ya kuwaelekea katika bima za afya kwa wazee kama mkakati wa Serikali wa kuwasaidia wazee hao.

Mwalimu alitumia nafasi kuwaihidi viongozi wa manispaa ya hiyo atawajengea wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji katika mojawapo ya vituo vya afya vya Ubungo.

Meya wa Ubungo,  Boniface Jacob amesema  manispaa hiyo imejipanga ipasavyo katika kuhakikisha wazee wanapata huduma hiyo ya bure.

"Wengine walizani ni utani, nawaambia sisi hatuna mzaha ndiyo maana leo tumemwita waziri kuja kuzindua. Kauli mbiu yetu ni 'mzee kufa kwa kukosa matibabu sasa basi',"amesema Jacob.w

Serikali Kuwarudisha Kwao Raia Watatu wa China.....

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt Kebwe Stephen Kebwe, ameagiza kukamatwa mara moja na kurejeshwa nchini mwao raia watatu wa China wanaodaiwa kuwepo nchini bila kibali na kuendesha shughuli za uchimbaji wa madini katika eneo la Maseyu Morogoro.

Dkt Kebwe ametoa maagizo hayo jana Septemba 3 kufuatia maagizo aliyopewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa mkoani humo ambapo alimtaka RC na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kwenda katika Kijiji cha Maseyu kufuatilia utendaji wa kampuni ya Zhong Fenq kama inafuata sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Waziri Mkuu alitoa maagizo hayo wakati akizungumza na viongozi na watumishi wa Kiwanda cha Philp Morris kinachotengeneza sigara aina ya Marlboro akiwa katika ziara yake ya kukagua maendeleo ya viwanda mkoani Morogoro.

Agizo hilo limefuatia malalamiko ya Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Omary Mgumba kuwa wawekezaji hao kutoka China wanaendesha shughuli za uchimbaji wa mabo katika kijiji cha Maseyu wilayani Morogoro bila ya kuwa na kibali.

Mgumba alisema tangu mwaka 2011 wawekezaji hao wameendesha shughuli zao bila kulipa kodi za Serikali na tozo za Halmashauri, hivyo kuikosesha Serikali mapato.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu katika kijiji cha Maseyu kuna Wachina wa kampini ya Zhong Fenq wanachimba mabo na hawana kibali na hakuna kodi yoyote wanayolipa Serikalini tangu mwaka 2010 walipoanza uzalishaji.”

Mbunge huyo ambaye machimbo hayo yako jimboni kwake aliongeza kwamba licha ya uongozi wa mkoa kwenda katika eneo hilo na kuizuia kampuni kuendelea na uchimbaji hadi itakapopata vibali walikaidi na kuendelea na shughuli.

Waziri Mkuu amesema hakuna muwekezaji anayeruhusiwa kufanya kazi bila ya kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi. Hivyo ameagiza kesho Mkuu wa Mkoa afuatilie Wachina hao na kuona namna gani wamezingatia sheria za nchi.

Alisema iwapo watabaini kwamba wawekezaji hao hawajafuata sheria, kanuni na taratibu hatua zichukuliwe dhidi yao ikiwa ni pamoja na kuwaondoa katika eneo hilo chini ya ulinzi na kuwasiliana na ubalozi wa China Nchini.

Baada ya Mkuu wa Mkoa  wa Morogoro kubaini ukweli katika hilo, ametoa amri raia hao kukamatwa mara moja na kurejeshwa nchini China kutokana na kukiuka za kiukwekezaji ikiwamo kuishi na kufanyakazi nchini bila vibali.

Pia Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa watu wote wenye nia ya kutaka kuwekeza katika miradi mbalimbali nchini Tanzania kuhakikisha wanafuata sheria, kanuni na taratibu za uwekezaji.

Hatimaye Kenya Yatangaza Tarehe ya Uchaguzi wa Marudio Baada ya Mahakama Kufuta Matokeo

$
0
0
Tume ya Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC) imetangaza kuwa uchaguzi wa marudio nchini humo utafanyika Oktoba 17, 2017 baada uchaguzi wa awali ambao ulifanyika Agosti 8 mwaka huu kufutwa.

Uamuzi wa kurudiwa kwa uchaguzi nchini Kenya umefuatia maamuzi ya Mahakama ya Juu  kutangaza kwamba uchaguzi wa urais wa awali ulikuwa ni batili kutokana na kutofuata kanuni, sheria na taratibu za nchi.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na tume hiyo, inaeleza kuwa kufuatia kikao kulichofanyika leo, hiyo ndio itakuwa tarehe ya uchaguzi wa marudio na kwamba wagombea watakaokuwa katika karatasi ya kupigia kura watakuwa ni wawili tu ambao ni Rais Uhuru Kenyatta ambaye mgombea mwenza ni William Ruto na Raila Odinga ambaye mgombea mwenza ni Stephen Musyoka.

Baadhi ya wagombea ambao walikuwa katika uchaguzi wa awali, wamepinga vika kuondolewa katika kinyang’anyiro hicho na kusema kwamba watakwenda mahakamani kwa sababu kitendo hicho ni ubatili mtupu.


Kenya iliweka historia ya kuwa taifa la kwanza barani Afrika kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais baada ya upinzani kwenda mahakamani kulalamikia mapungufu katika zoezi zima la uchaguzi.

Kwa upande wake Kenyatta ambaye alitangazwa mshindi kwa 54% alisema kwamba hakubaliani na maamuzi ya mahakama na kwamba watu sita hawawezi wakakaa na kupinga kilichofanywa na mamilioni ya Wakenya.

Kwake Odinga alisema hiyo ilikuwa ni historia kwa Kenya, Afrika na hata dunia huku akiahidi kuwa katika uchaguzi wa marudio atashinda. Hata hivyo Odinga katika moja ya mazungumzo yake alisema kwamba hatoshiriki uchaguzi huo kama baadhi ya maofisa wa tume ya uchaguzi hawatoondolewa akidai walikuwa sababu ya kuvugika kwa uchaguzi wa awali.

Kimenuka...Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Acacia imetangaza nia ya Kusitisha Uchimbaji wa Dhahabu Chini ya Ardhi

$
0
0
NI kitimtim! Kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia imetangaza nia ya kusitisha uchimbaji wa dhahabu chini ya ardhi kwenye mgodi wa Bulyanhulu mkoani Shinyanga na hivyo kuwapo kwa uwezekano wa kupungua kwa ajira kwenye mgodi huo.

Taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo, ambayo humilikiwa kwa kiasi kikubwa na kampuni ya Barrick Gold yenye kumiliki mgodi wa Bulyanhulu, ilieleza sababu kadhaa za kuwapo kwa kusudio hilo, mojawapo ikiwa ni kuwapo kwa mrundikano wa makinikia yenye thamani ya dola za Marekani milioni 265 (zaidi ya Sh. bilioni 500).

Taarifa hiyo ilieleza kuwa usafirishaji makinikia kwenda nje ya nchi ulizuiwa na serikali tangu Machi 3, mwaka huu na kwamba sasa, licha ya kuchukuliwa kwa hatua kadhaa za kupunguza matumizi ili kuendana na athari za zuiio hilo, Acacia iligusia matumaini iliyo nayo juu ya mazungumzo yanayoendelea baina ya Barrick na Serikali kuhusiana na suala hilo.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Medard Kalemani, hakupatikana jana kuelezea tangazo hilo la Acacia kuhusiana na nia hiyo ya kusitishwa uchimbaji wa chini ya ardhi kwenye Mgodi wa Bulyanhulu. Simu yake iliita bila kupokelewa.

Aidha, Msemaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Benny Mwaipaja, alipoulizwa juu ya athari zinazoweza kutokea kiuchumi kutokana na uamuzi huo wa Acacia, alisema hawezi kuzungumzia chochote kwakuwa hajaisoma taarifa hiyo.

Katika taarifa iliyowekwa kwenye tovuti rasmi ya Acacia na kuthibitishwa na kampuni hiyo nchini jana, ilieleza kusudio lake la kupunguza shughuli za uzalishaji kwenye mgodi huo kwa maelezo kuwa zuio usafirishaji makinikia limeathiri takribani asilimia 35 ya uzalishaji wa kampuni hiyo kwa mwaka huu.

Ilieleza zaidi kuwa Acacia imekuwa na ongezeko la hifadhi ya makinikia yenye thamani ya takribani dola za Marekani milioni 265 nchini, kulinga na thamani ya sasa katika soko la dunia.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa ili kuzuia hasara ya mapato, Acacia imechukua hatua kadhaa ili kupunguza gharama za uendeshaji na gharama za kimtaji kwa lengo la kulinda ajira na mtaji.

"Licha ya hatua hizo, kupotea kwa mapato, pamoja na gharama za takribani dola za Marekani milioni 65 katika kodi isiyo ya moja kwa moja na gharama kutokana na mabadiliko mengine katika mazingira ya uendesheaji biashara, imechangia gharama kuu ya takribani dola za Marekani milioni 210 mwaka huu," taarifa hiyo ilieleza.

Kadhalika, katika taaria hiyo ilielezwa kuwa kama sehemu ya matokeo ya awali ya taarifa za fedha kwa mwaka huu, walitangaza kuwa wanafikiria kupunguza zaidi gharama za uendeshaji katika mgodi wa Bulyanhulu ikiwa zuio la makinikia halitaondolewa hadi kufikia mwisho wa robo ya tatu ya mwaka wa fedha.

Ilielezwa katika taarifa hiyo kuwa athari za zuio, pamoja na kudorora kwa mazingira ya uendeshaji biashara, zimeleta hasara ya takribani dola za Marekani milioni 15 kwa mwezi katika mtiririko wa fedha kwenye mgodi na hivyo kumefanya operesheni za mgodi wa Bulyanhulu zisiwe stahimilivu.

"Hivyo basi, Acacia imeamua kuanza mpango wa kupunguza operesheni na matumizi pale Bulyanhulu ili kuboresha ustahimilivu wa biashara yetu kwenda mbele. Mpango huu utahusisha utunzaji wa mali zote zisizohamishika na mitambo, ili kuwezesha mgodi kurejea katika utendaji wa kawaida, pale zuio litakapoondolewa na mazingira ya uendeshaji biashara kutulia," Acacia walieleza katika taarifa yao.

"Kwa sasa, majadiliano kati ya Barrick na Serikali ya Tanzania yanaendelea. Acacia inaendelea kuunga mkono majadiliano hayo na bado inaamini kwamba suluhu itakayotokana na majadiliano ndiyo njia bora zaidi kwa wadau wote."

Taarifa hiyo ilieleza zaidi kuwa baada ya kutolewa kwa tangazo hilo, Bulyanhulu itaanza majadiliano na wadau wake kama sehemu ya mpango wa kupunguza shughuli za operesheni.

"Kama sehemu ya utekelezaji wa mpango huu, shughuli za chini ya ardhi zitasitishwa na uchenjuaji wa miamba unapangiwa kusitishwa ndani ya wiki nne," taarifa hiyo inaeleza.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa utekelezwaji wa mpango huo unatarajiwa kusababisha kupunguzwa kwa wafanyakazi kutoka idadi ya sasa ya wafanyakazi 1,200 na wakandarasi 800.

KUUNGA MKONO SERIKALI
Aidha, Acacia imesisitiza kuwa inaunga mkono serikali katika harakati zake za kuboresha maendeleo ya kijamii na kukuza uchumi.
"Acacia inasisitiza kwamba inaunga mkono malengo ya Serikali ya Tanzania ya kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.”

Ilieleza kuwa katika miezi sita ya kwanza ya 2017 pekee, Acacia imelipa dola za Marekani milioni 53 (Sh. bilioni 117) katika kodi na mrahaba kwa Tanzania na kuwezesha miradi inayohudumia zaidi ya watu 40,000 katika jamii zinazozunguka migodi yake.

"Zaidi ya wafanyakazi na wakandarasi 5,000 hufanya kazi katika migodi ya Acacia, huku zaidi ya asilimia 95 ya wafanyakazi wetu wakiwa wazawa,” ilisema sehemu ya taarifa.

Mei, Rais John Magufuli aliunda kamati teule mbili kuchunguza makontena 277 ya makinikia yaliyozuiwa bandarini na zote mbili kutoa ripoti iliyoonyesha kuwapo kwa upotevu mkubwa wa mapato.

Siku chache baada ya kutolewa kwa ripoti za kamati hizo, Mamlaka ya Mapato (TRA) iliipelekea Barrick madai ya kodi iliyolimbikizwa pamoja na adhabu jumla dola za Marekabni bilioni 190 (takribani Sh. trilioni 420).

Rwanda: Polisi Wamkamata Mwanamke Aliyetaka Kuwania Urais na Kumpinga Rais Kagame....

$
0
0
Polisi nchini Rwanda wamesema wanamzuilia mwanasiasa wa upinzani Diane Rwigara, mamake na dadake.

Wiki iliyopita polisi walikuwa wametangaza kuwa mwanasiasa huyo anatuhumiwa kughushi nyaraka wakati alipotaka kuwania urais mapema mwezi wa 8 huku familia yake ikituhumiwa kukwepa kulipa kodi.

Kwa mujibu wa walioshuhudia, polisi wapatao 10 wameingia kwenye makazi anamoishi mwanasiasa huyo na familia yake mtaa wa Kiyovu mjini Kigali na kuruka juu ya lango baada ya kukataliwa kufunguliwa na kumkamata mwanasiasa huyo pamoja na Mamake na dadake.

Duru za polisi zimesema kwamba polisi wameamua kwenda kuwakamata baada yao kukosa kuripoti katika idara ya upelelezi ya polisi CID kwa mara kadhaa.

Juhudi za BBC kumtafuta msemaji wa polisi ili kupata maelezo zaidi hazikufanikiwa.

Wiki iliyopita, polisi wa Rwanda walitangaza kufanya upekuzi katika makazi ya mwanasiasa huyo na kutangaza kwamba ni sehemu ya upelelezi wa mwanzo kuhusu ambayo ni pamoja na kosa la kughushi nyaraka na kukwepa kulipa kodi.

Diane Rwigara alikataliwa kugombea kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika mwezi wa 8 uliopita na baadae akaanzisha vuguguvu la kukosoa utawala wa nchi hiyo.

Shilole Afungukia Kichapo Alichopewa na Mchumba ake

$
0
0
MKALI wa Bongo Fleva na Bongo Movies, Zuwena Mohamed ‘Shilole au Shishi Baby’ anadaiwa kubondwa na mpenzi wake wa sasa anayejulikana kwa jina moja la Uchebe, kisa kikisemekana ni wivu wa kimapenzi.

Chanzo makini kililiambia Ijumaa Wikienda kuwa, hivi karibuni Shishi alikwenda kwenye shoo mkoani Morogoro akiwa na Uchebe, akiwa jukwaani shabiki alipanda na kumshika kimahaba, alipomaliza shoo ndipo mchumba’ke huyo akamshushia kipigo.

Baada ya kuunyaka ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilimsaka Shishi ambaye alifunguka:
“Ni kweli kulitokea mgogoro wa kawaida, ilikuwa Zanzibar na siyo Morogoro. Unajua jamaa hatumii kilevi, sasa mimi nilimkwaza kwa sababu nilitaka kuendelea kunywa ndiyo tukapishana kauli.

Kuhusu wivu ni kweli anao na huyu ni mwanaume nampenda sana siyo kama wengine waliopita,” alisema Shishi anayekimbiza na ngoma yake mpya ya Kigori.

Abiria Aliyetamka ‘Allah Akbar’ Asababisha ndege Kuchelewa Kuondoka Airport

$
0
0
Abiria tisa wamezua taharuki kwenye kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Zaventem, nchini Ubelgiji baada ya mmoja wao kutamka matamshi yaliyosikika ‘Allah Akbar’ kwa sauti kubwa mara kadhaa.

Watu hao tisa walitolewa na maaskari kwenye ndege ya shirika la Ryanair, na kuamriwa mizigo yao kutolewa kwenye ndege ili kukaguliwa zikiwa zimebakia dakika 10 kabla ya ndegehiyo  kuondoka.

Ndege hiyo ililazimika kuchelewa kwa masaa manne ikipisha ukaguzi wa mizigo ya watu hao, ambao walitambuliwa kuwa ni raia wa Ubelgiji.

Polisi mjini Brussels wamethibitisha taarifa hizo kupitia kituo cha Runinga cha VTM Nieuws kwa kusema kuwa ni kweli tukio hilo limetokea siku ya Jumamosi Tarehe 2 Septemba ambapo wavulana hao tisa walikuwa wanasafiri kutoka Mjini Brussels kwenda Madrid, Hispania.

“Tumepokea taarifa hizo za wanaume tisa waliokuwa wakisafiri kutoka Ubelgiji kwenda Madrid, Hispania lakini walipoingia kwenye ndege mmoja wao akaanza kutamka kwa sauti ‘Allah Akbar’ akimaanisha ‘Mungu mkubwa’ kama mara sita hivi ndipo askari wa usalama wakamtoa kwenye ndege pamoja na wenzake wote kwa ukaguzi”,amesema Peter De Waele msemaji wa jeshi la Polisi mjini Brussels .

Kwa mujibu wa taarifa kutoka gazeti la Top 24   abiria walioshuhudia tukio hilo wamesema lilitokea baada ya ndege hiyo kuchelewa masaa matatu kuruka na ndipo mtu huyo akaanza utani akitamka ‘Allah Akbar’ huku akicheka.

Hata hivyo abiria hao nane walirudishwa kwenye ndege baada ya ukaguzi kufanyika na ndege kuendelea na safari yake, ingawaje mpaka sasa bado haijawekwa wazi sababu za kupekuliwa kwa watu hao kwa mara ya mbili huku mitandao mingi duniani ikiandika kuwa ni hofu ya ugaidi iliyotanda nchini Ubelgiji.

Nipo Namibia Kila Mtu Anamuulizia Rais Magufuli....Ukweli Amerudisha Heshima ya Taifa Letu – Humphrey Polepole

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole ameshangazwa na raia wa Namibia kwa kumtaja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John P Magufuli  kila sehemu nchini humo huku akisema kuwa ni sifa kwa taifa letu.

  Polepole ambaye yupo nchini Namibia kikazi kwa mujibu wa maelezo yake amesema kila mtu anayekutana nae nchini humo anamuulizia Rais Magufuli.

“Niko Namibia kwa kazi ya CCM na kila mtu anamuulizia Magufuli, Magufuli, Magufuli. Huyu Magufuli amerudisha maradufu heshima ya Taifa letu”,ameandika Polepole kwenye ukurasa wake wa Twitter.

 Humphrey Polepole ni moja ya viongozi wa CCM ambao wanasiasa wengi wanadai kuwa nafasi aliyopewa kwenye chama hicho ni kubwa kulinganisha na uwezo wake akiwemo  Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

BREAKING NEWS: Wabunge wa Upinzani Wagoma Kuingia Bungeni

$
0
0
BREAKING NEWS: Wabunge wa Upinzani Wagoma Kuingia Bungeni
Taarifa kutokea Bungeni Dodoma ni kuhusu Wabunge wa Upinzani wamegoma kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge wakati Mkutano wa Nane wa Bunge la 11 ukiendelea kwa madai kuwa hawakufurahishwa na maamuzi ya kufukuzwa Wabunge 8 wa Viti Maalumu wa Chama cha Wananchi CUF.

Mkutano wa Nane wa Bunge la Jamhuri umeanza leo Mjini Dodoma na moja ya mambo yaliyopo kwente ratiba ya mkutano huo ni kuapishwa kwa Wabunge wapya 8 wa Viti Maalumu ambao wameteuliwa kuziba nafasi za Wabunge 8 wa Viti Maalumu waliofutwa CUF.

Kutana na Mtabibu wa Nyota Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH...AL_WATWAN MAFUSHO

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH...
 AL_WATWAN MAFUSHO

ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote

..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na AL_WATWAN MAFUSHO Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA).
Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?
Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
AL_WATWAN MAFUSHO Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa  PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.
Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA.
 Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.
Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,
HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Whatsapp +255 759 084 996 

Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote..

Odinga Ampa Shavu Ali Kiba Amtumia Ndege Binafsi Kwenda Kenya

$
0
0

Odinga Ampa Shavu Ali Kiba Amtumia Ndege Binafsi Kwenda Kenya
Upepo mwanana bado unaendelea kumpuliza, staa namba moja wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ baada ya mgombea anayewakilisha Muungano wa Vyama vya Upinzani nchini Kenya (NASA), Raila Omolo Odinga, kudaiwa kumuita nchini humo. Kwa mujibu wa chanzo kisicho na chembe ya shaka, Kiba anayesumbua kwa sasa na wimbo wake wa Seduce Me, alipata mwaliko huo mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwa ni saa chache mara baada ya Odinga kushinda kesi ya uchaguzi Katika Mahakama ya Juu aliyokuwa amemfungulia Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ambaye mambo yalimuwia mazito.

Kenyatta alitangazwa mshindi wa nafasi ya urais na Tume ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IBEC) katika uchaguzi uliofanyika nchini humo Agosti 8, mwaka huu ambapo Odinga alifungua kesi hiyo mahakamani. Baada ya mahakama kupitia hoja za pande zote, iliufuta uchaguzi huo kwa kueleza kuwa tume ya uchaguzi haikuzingatia uadilifu.

ODINGA KICHEKO

Mara baada ya hukumu hiyo kutolewa mahakamani, Odinga alizungumza na wanahabari na kueleza hisia zake akisema alifurahishwa kwa kitendo cha mahakama hiyo kutenda haki hivyo kuwataka wapiga kura wake kujiandaa kwa uchaguzi wa marudio unaotarajiwa kufanyika baada ya siku 60 tangu hukumu hiyo itoke.

TUJIUNGE NA CHANZO

Kwa mujibu wa chanzo hicho makini kilicho karibu na Kiba, uongozi wa NASA ambao ulimtumia Kiba katika kampeni za uchaguzi wa awali, haraka ulimtumia mwaliko kwa ajili ya pati maalum ya kusherehekea hatua ya ushindi huo nchini Kenya.

“Yaani Kiba nyota inazidi kumuwakia. Baada tu ya Odinga ‘kumgaragaza’ Kenyatta kortini, wamemuita Kiba haraka sana ili aende kusherehekea nao ushindi huo. Si unajua tena alikuwa sehemu ya watu waliompigia kampeni Odinga katika uchaguzi uliopita?” Kilinyetisha chanzo hicho. Katika mazungumzo yake na Ijumaa Wikienda, chanzo hicho kilizidi kushusha ubuyu kuwa kutokana na umuhimu wa Kiba na kazi kubwa aliyoifanya wakati wa kampeni, NASA waliamua kumtumia Kiba ndege binafsi (private jet) ili awahi sherehe hiyo ya kukata na shoka na ikiwezekana wafanye mazungumzo ya ‘kuliamsha dude’ la shoo kampeni.

“Wamemtumia ndege fasta na hivi ninavyoongea na wewe, Kiba amesharuka na ndege, amesepa zake Kenya kwa ajili ya kuwahi ishu hiyo maalum. Wanaheshimu sana mchango wa Kiba hivyo hawakuwa tayari kumkosa,” kilisema chanzo hicho.

KENYATTA MAMBO MAZITO

Chanzo hicho kilizidi ‘kunyunyiza’ kwa kueleza kuwa, kutokana na jinsi Kiba anavyokubalika nchini Kenya na ukizingatia sasa hivi anakimbiza na Seduce Me, mambo yatakuwa mazito kwa mgombea wa Chama Tawala cha Jubilee, Kenyatta. “Wewe sasa hivi kila kona ni Wimbo wa Seduce Me. Umeshafikisha watazamaji zaidi ya milioni tatu tangu utoke na haujafikisha hata wiki mbili, atawashawishi sana Wakenya, sasa unategemea Kenyatta atakuwa na hali gani?” kilihoji chanzo hicho.

MENEJA WA KIBA AFUNGUKA

Ijumaa Wikienda lilimvutia waya mmoja wa mameneja wa Kiba, Aidan Seif ambaye alithibitisha mualiko huo wa Kiba, lakini hakutaka kuuzungumzia kiundani, zaidi ya kusema anawashukuru Watanzania kwa kuendelea kusapoti muziki mzuri.
“Ni kweli ameitwa Kenya lakini nisingependa kulizungumzia sana hilo kwa undani. Kikubwa niwashukuru Watanzania na niwaombe tuendelee kusapoti muziki mzuri kutoka kwa Kiba na wanamuziki wote wa RockStar4000,” alisema Aidan.
KIBA AENDELEA KUWEKA REKODI

Wakati hayo yakiendelea, Seduce Me ya Kiba imeendelea kuweka rekodi ya kutazamwa zaidi kwenye Mitandao ya YouTube, Vevo na itunes hivyo kushika namba moja kwa Afrika Mashariki.


BEEF LINGINE? Miss Kiki Adai Mwanamuziki Rosa Ree Anaiga, Hana Heshima

$
0
0
BEEF LINGINE? Miss Kiki Adai Mwanamuziki Rosa Ree Anaiga, Hana Heshima
Moja ya rapa staa wa kike anayefanya vizuri kwa sasa Bongoflevani Miss Kiki amefunguka na kudai kuwa hakuna rapa wa kike Bongo ambaye anaweza kumpa shida na kusema rapa mwingine wa kike Rosa Ree ambaye ana hits kadhaa hampi challenge na kwenda mbali zaidi akisema style anayotumia ana-copy.

Miss Kiki amedai Rosa Ree anamuiga Stella Mwangi akisema pia hana heshima kwa kuwa walishwahi kuitwa kwenye interview moja lakini hakutokea kwa sababu ya utovu wa nidhamu.

Bonyeza Play hapa chini kusikiliza Full story

Mapya Yaibuka Sakata La Utekaji watoto Askari FFU Adakwa Katika Sakata Hilo

$
0
0
Mapya Yaibuka Sakata La Utekaji watoto Askari FFU Adakwa Katika Sakata Hilo
Wakati Mtuhumiwa wa matukio ya utekaji watoto, Samsom Petro (18), ambaye jana alifikishwa Arusha kwa ajili ya kuonyesha sehemu alipowaficha watoto, amebainika kuwa anaishi na kaka yake ambaye ni askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) cha mjini hapa.

Inadaiwa kuwa askari huyo pia anashikiliwa na polisi kwa mahojiano tangu Agosti 27 wakati kikosi maalum cha polisi kilipozingira nyumba aliyopanga.

Petro, ambaye alikamatwa juzi akiwa Katoro mkoani Geita, anatuhumiwa kuwateka watoto wawili, Moureen David(6) na Ikram Salim(3) na hadi jana jioni alikuwa ameandamana na polisi katika eneo la Njiro ambako alidai aliwatelekeza watoto hao.

Akizungumza na Mwananchi, Lina Kajuna ambaye ni mmiliki wa nyumba ya aliyekuwa amepanga askari huyo wa FFU, alisema ana miaka miwili tangu ampangishe.

Kajuna alisema mtuhumiwa wa utekaji, Samson Petro alifika Arusha mwezi Juni na amekuwa akiishi na kaka huyo na tangu amefika amekuwa akimuona kuwa na tabia ambazo sio nzuri, kama wizi wa kuku.

“Alipofika muda mfupi tulianza kuona matukio ya wizi nikaibiwa kuku na pesa mimi nikamlalamikia kaka yake lakini akasema tuendelee kumchunga,”alisema

Alisema baada ya hali ya wizi kuendelea, alikwenda kulalamika kwa balozi wa eneo wanaloishi ambalo ni Mtaa wa Olkeria, Daniel Kichau kutaka wamchunguze.

Hata hivyo, alisema wakati akichunguza, ndio matukio ya utekaji yakaanza na tangu Agosti 25 alitoweka nyumbani hadi jana walipopata taarifa kuwa amekamatwa.

Akizungumzia tukio hilo, mwenyekiti wa Mtaa wa Olkerian, Daudi Safari alisema jana kuwa kikosi chao cha wananchi walifika kwenye nyumba hiyo na kubaini alikuwa anaishi na askari huyo wa FFU .

“Tumemuhoji mama mwenye nyumba ametupa ushirikiano mkubwa na ni kweli Samson alikuwa anaishi kwenye nyumba yake na kaka yake ambaye alikamatwa tangu Agosti 27,” alisema.

Katika msako wa jana, polisi walikwenda peke yao na mtuhumiwa na kuwaacha wazazi wa watoto hao wakiwasubiri kituo kikuu cha polisi. Baadhi ya askari walisema wanaendelea na msako wa watoto hao.


Marekani Yailaumu Korea Kaskazini kwa Kuomba Vita

$
0
0
Marekani Yailaumu Korea Kaskazini kwa Kuomba Vita
Balozi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa ameilaumu Korea ya Kaskazini kwa kulazimisha vita kutokana na majaribio yake ya makombora ya mara kwa mara.
Nikki Haley ametaka kuwepo kwa muda wa dharura wa Baraza la Umoja wa Mataifa utakao jibu majaribio hayo kwa hatua kali.
"Vita sio kitu ambacho Marekani ingetaka," alisema. "Hatutaki vita kwa sasa lakini uvumilivu wa nchi yetu hautuzuii."

Baadae, kupitia mazungumzo ya simu na Rais Trump, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema atahimiza kuwepo kwa vikwazo vikali kutoka umoja wa nchi za ulaya dhidi ya Pyongyang.
Hata hivyo, China imesisitiza wito wake wa kutaka pande zote zirudi katika meza ya mazungumzo.

Ripoti zinasema kuwa Korea Kaskazini inajiandaa kwa majiribio mengie ya makombora.
Siku ya Jumapili ilifanya jaribio la bomu la chini ya ardhi lililoaminika kuwa na nguvu ya kati ya kilotani 20 na 120.
Kifaa hicho hicho kinaweza kuwa na nguvu mara tatu zaidi ya bomu lililotumiwa kuharibu mji wa Hiroshima mwaka 1945.

China haitaki kuwepo nchi yenye silaha za nyuklia ya Korea Kaskazini na mara kwa mara imeeleza msimamo wake kwa nchi hiyo.
Lakini pia haitaki kuona utawala wa Korea Kaskazini ukiondolewa madarakani. Hii itasababisha mamilioni ya wakimbizi kukimbia kwenda China na kuchangia kuungana kwa Korea ambayo itakuwa chini ya ushawishi wa Marekani.

Waziri Mkuu Kupokea Taarifa ya Ripoti ya Makinikia ya Almasi na Tanzanite Bungeni Kesho

$
0
0
Waziri Mkuu Kupokea Taarifa ya Ripoti ya Makinikia ya Almasi na Tanzanite Bungeni Kesho
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, kesho anatarajiwa kukabidhiwa taarifa za kamati mbili zilizoundwa na Bunge katika Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 kuhusu na makinikia ya almasi na biashara ya madini ya tanzanite.

Kwa mujibu wa taarifa za bunge hafla fupi ya makabidhiano hayo itafanyika katika viwanja vya bunge na viongozi wa kitaifa watakuwepo. Kabla ya Waziri Mkuu kukabidhiwa taarifa hizo, kamati hizo mbili zitakabidhi taarifa zake kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai ambaye naye atakabidhi kwa Waziri Mkuu.

Taarifa hizo mbili zinazosubiriwa kwa makini hasa baada ya taarifa za kamati zilizoundwa na Rais John Magufuli kuibua makubwa katika makinikia kwenye makontena bandarini. Kamati hizo maalumu zote zilikuwa na idadi sawa ya wabunge ambao ni tisa na zililenga kushauri juu ya mfumo bora wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa biashara ya madini ya almasi na Tanzanite hapa nchini.

Kamati iliyohusu almasi ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu ilitajwa kabla ya kuhitimisha shughuli za Bunge la Bajeti. Spika Ndugai aliunda kamati hiyo kupitia Waraka wa Spika namba 3 wa mwaka huu, na kusema: “Kamati hii itatathmini mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya almasi nchini kisha kuandaa mapendekezo mahsusi kwa ajili ya kuishauri Serikali kuhusiana na uendeshaji bora wa biashara ya madini hayo nchini,” alisema.

Uundaji wa kamati hizo umefanyika kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kukabiliana na ‘wizi’ wa mali asili za taifa. Wakati akiunda Kamati hizo alisema pia kwamba ilitokana na pendekezo la Rais Magufuli la kuunda Tume ya kuchunguza na kufuatilia madini ya almasi alilolitoa Juni 12 mwaka huu alipohudhuria mkutano wa kupokea Taarifa ya Kamati yake ya Pili ya Kuchunguza Masuala ya Kiuchumi na Kisheria kuhusu usafirishaji wa makinikia, Kamati ya Profesa Nehemia Osoro na pia kutokana na hoja aliyoitoa wakati akikabidhiwa ripoti ya makinikia.

Wajumbe wa Kamati hiyo ni Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Dk Immaculate Sware Semesi, Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Shally Raymond, Mbunge wa Tumbe (CUF), Rashid Ali Abdallah, Mbunge wa Iramba Mashariki (CCM), Allan Kiula, Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Restituta Mbogo na Mbunge wa Wawi, Ahmed Juma Ngwali (CUF).

Wengine ni Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa (CCM), Mbunge wa Tabora Mjini, Emmanuel Mwakasaka (CCM) na Mbunge wa Ilala (CCM), Mussa Zungu ambaye ni Mwenyekiti. Kamati zote mbili ya almasi na Tanzanite zilitakiwa kuanza kazi Julai 10, na Kituo Kikuu cha kazi kilikuwa katika Ofisi ya Bunge hapa Dodoma.

Aidha, alisema hadidu za rejea za kamati ya almasi ilikuwa ni kuchambua taarifa za Tume na Kamati mbalimbali zilizowahi kuundwa na Serikali kwa ajili ya kushughulikia mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya almasi nchini na kuona Mapendekezo yake na namna yalivyotekelezwa na Serikali.

Nyingine ni Kutathmini mfumo uliopo wa uchimbaji, usimamizi na udhibiti wa biashara ya madini ya almasi nchini na kubainisha manufaa ambayo Serikali inapata kutokana na uwekezaji uliopo katika madini hayo na kubainisha na kushauri kuhusu utaratibu bora unaoweza kutumika katika kusimamia uwekezaji, uchimbaji na biashara ya madini ya almasi nchini.

“Hadidu nyingine ni kushughulikia jambo jingine lolote linalohusiana na mfumo wa uchimbaji, usimamizi na udhibiti wa madini ya almasi nchini,” alisema Kamati ya ufuatiliaji wa uchimbaji wa madini ya Tanzanite yenyewe ilipewa kazi ya kuchakmbua mkataba kati ya shirika la taifa la uchimbaji wa madini Stamico na Tanzania One (TML) na kubainisha faida na hasara kutokana na ubia uliopo. Aidha kamati hiyo pia iliangalia mfumo wa uchimbaji na udhibiti.




Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images