Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Pesa Kitu Kingine Aisee...Bondia Floyd Mayweather Amethibitisha Kuwa na Wapenzi Saba

$
0
0
Bondia Floyd Mayweather ambaye kwa sasa anafurahia kwa kufanikiwa kulinda rekodi yake ya kutopoteza pambano hata moja katika mapambano yake 50 baada ya kufanikiwa kumpiga Bondia Mc Gregor kwa Technical Knock Out (TKO) round ya 10 katika pambani la round 12.

Mayweather ameripotiwa na mtandao wa dailymail.co.uk kuwa pambano lake na Mc Gregor ndio pambano lake la mwisho na ameamua kustaafu mchezo wa ngumi, japokuwa kuna watu wanaweza kufikiria kuwa atarudi tena ulingoni.

Hata hivyo Mayweather katika interview hiyo amethibitisha kuwa na wasichana saba katika mahusiano ya kimapenzi kwa sababu kuwa na msichana mmoja ni sawa na kuwa hauna kabisa.

Nina wasichana wangapi? kama saba hivi ambao tunatoka out kwenda kula na wengine nasafiri nao kuwa nae mmoja pekee karibu ni sawa na kuwa hauna kabisa" Floyd Mayweather

Mrembo Flaviana Kakasirishwa na Wanaomsema Vibaya Kisa Mwembamba na Amekondeana

$
0
0
Mwanamitindo Mtanzania anayeishi na kufanya kazi Marekani Flaviana jana September 12, 2017 alitoa ya moyoni kwenye akaunti yake ya Instagram kuhusu watu wanaomsumbua kwa kuzungumzia mwili wake ulivyo mwembamba na kumwambia awe anakula ili aongezeke.

SIKILIZA HAPA:

Baba; Mtoto Wako Mtundu, Amekunya Mkononi, Je, Utaukata au Kuusafisha na Kumsafisha?

$
0
0
Huu ni uzi wa swali la hypothetical situation kuhusu wewe kama Baba wa Familia, Mtoto Wako Mtundu, Amekuny.a Mkononi, Jee Utaukata Mkono, au Utausafisha na Kumsafisha?.

Baba ukiachiwa mtoto, halafu akikuny.a mkono, hauukati, wala humchapi mtoto, bali utausafisha mkono, na utamsafisha mtoto na kuendelea kumbeba.

Rais wa nchi ni kama baba, rais wote wa Tanzania ni kama watoto, hata wakikunye.a mkono, haupaswi kuwachapa, kuwasusa, bali kuwakumbatia na kuwa support.

Hata kama taratibu zimekiukwa, lakini huyu ni mtoto wa Tanzania, ni Mtanzania mwenzetu, kwa vile alikuwa very vocal kumhusu baba na serikali yake, baada ya kushambuliwa, mtu yoyote lazima angehofia uangalizi wa baba kwa hisia kuwa ni hasira za baba, hivyo wako very right, kwenda mahali salama.

Lakini despite all, serikali yetu bado has a duty of care, Bunge letu bado has a duty of care kumhudumia na kugharimia matibabu na ikibidi kutoa support ahamishiwe kwenye nchi yenye matibabu bora zaidi.

Kunyoosha huku mikono kutoa support, ni unconditional and despite all the odds kwa sababu kila mzazi has a duty of care kwa watoto wake regardless of anything!.

Ifike mahali, viongozi wetu, waogope kitu kinachoitwa karma, ambapo wewe kama ni kiongozi, ni kama baba, you have a duty of care kwa raia wako wote, if there is anything you can do to help out, please do!, tena do it now before its too late!.

Karma inaelekeza, if there is something bad that has happened to someone, uwe unahusika, a huusiki, but there is something you can do to help out, but you don't do kwa sababu tuu taratibu hazikufuatwa, au kwa sababu unanyooshewa kidole, karma inaelekeza just ignore everything, maneno, vidole na taratibu zilizokiukwa, just do what you can do to help out. Mtume balozi wetu pale aka assess the situation and if there is something you can do, please do!.

Kwa sababu, if something will happen, kwa sababu you didn't do anything to help out, na ulikuwa na uwezo wa kusaidia na kuzuia hiyo something is happen, then, the karma of what happens will also be upon you kwa kushindwa kutimiza wajibu wako kumhusu raia wako!.

Hii karma jamani haijui nani ni nani, wala haijalishi mamlaka ya kidunia hii, karma is real, tutimize wajibu wetu ipasavyo kuepuka a bad karma, kwa kutenda mema, hata kwa wabaya wetu, ili kujenga karma njema.

Namalizia kwa swali hili, Jee Wewe Kama Baba, Mtoto Wako Mtundu Sana, Akikuny.a Kwenye Mkono, Jee Utaukata?, Utamchapa?, au Utamsusa?, au Utausafisha na Kumhudumia kwa Kumsafisha?.

Get Well Soon, TL.

By Pascal Mayalla

SOMA Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo ikiwemo Ajira 90 Serikalini

$
0
0

Kutana na Mtatibu Wanyota za Binadamu Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka Comoro

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU WANYOYA ZA BINADAMU DUNIANI KOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO

KWA SASA YUPO TANZANIA MAALIM FADHILI RASHIDI ANA IWEZO WAKUJUWA JAMBOLAKO NAKULI TATUWA KWAMUDA MFUPI

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE

MAALIM FADHILI RASHIDI NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA MIGUU KUWAKA MOTO

KISUKARI VIDONDA VYATUMBO PUMU TEZI NA UVIMBE TUMBONI PUMU ANA UWEZO WAKURUDISHA MTU ALIE POTEA KIMAZINGIRA

(MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA

KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABU MAALUM ANATOWA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI YEYOTE

NAKUMILIKI MALIZA MAJINI KWAYULE ANAE HITAJI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZA KIUME ANAYO

DAWA YA KUONGEZA HIPSI SHEPU KUWA NA UMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHURUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASA (24)

ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YAMVUTO WABISHARA KUUZA MALIYAKO KWA HARAKA KUZUIYA CHUMA ULETE

KUSAFISHA NYOTA NAKUONDOA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI ACHAKUTESEKA NJOO UWONE MIUJIZA YA MAALIM FADHILI RASHIDI

CALLING+255719362806/ +255763276239

KWA WHATSAPP IMO +255785786436

Spika Amjibu Lema Asema Bunge Haliwezi Kusimama kwa Shambulio la Lissu

$
0
0
Spika Amjibu Lema Asema Bunge Haliwezi Kusimama kwa Shambulio la Lissu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, amejibu tuhuma za mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, na kumtaka asipotoshe wananchi, bali apeleke malalamiko yake kwenye kamati.

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akiendesha bunge, na kusema kwamba bunge lina utaratibu wake kwenye kila jambo linalohusika bungeni hapo.

"Lema asipotoshe wananchi aende hadharani kwenye kamati kuzungumzia hayo, bunge haliwezi kusimama kwa shambulio la Lissu bali kanuni zinasema mbunge akifariki bunge linasimama kwa siku moja. Na iwapo Spika akiletewa jambo la maadili linapelekwa kamati ya maadili, suala la jinai linapelekwa polisi", amesema Spika Ndugai

Pia Spika Ndugai amesema suala la Tundu Lissu kuchangiwa fedha za matibabu na wabunge wakati yeye alitibiwa nje ya nchi ni kwamba matibabu ya Tundu Lissu yameenda kinyume na utaratibu wa bunge.

"Wabunge wanaopelekwa nje (India) wanapewa rufaa kutoka hospital ya Muhimbili lakini si kama alivyopelekwa Lissu", amesema Spika Ndugai.
Pamoja na hayo Spika Ndugai amesema anamsamehe Godbless Lema na kuwataka watu kumsamehe kwani hajui alitendalo.

Hapo jana mbunge wa Arusha Godbless Lema alimlaumu Spika Ndugai kuwa anashindwa kutetea kiti chake, kwa kuzidi kuwakandamiza wabunge wa upinzani hususan suala la kupigwa risasi kwa Tundu Lissu.

Mabomu ya Machozi Yarindima Geita Kuwatawanya Madiwani

$
0
0
Mabomu ya Machozi Yarindima Geita Kuwatawanya Madiwani
 Polisi wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi na madiwani waliofunga  barabara ya kuingia kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM).

Katika tukio hilo leo Alhamisi asubuhi, madiwani wawili na baadhi ya wananchi wamekamatwa na polisi.

Kabla ya kutumia mabomu, polisi walitoa onyo wakiwataka wananchi na madiwani hao kutawanyika kwa amani lakini waligoma.

Madiwani wa  halmashauri mbili za Wilaya ya Geita jana Jumatano walitanga mgogoro na GGM wakishinikiza kulipwa Dola 12 milioni za Marekani zinazotokana na ushuru wa huduma kuanzia mwaka 2004 hadi 2013.

Walitangaza kuzuia magari ya mgodi kwa    kufunga barabara  na pia kufunga maji yanayoingia mgodini kutoka Ziwa Victoria.

GGM iliwatangazia wafanyakazi wake jana kutofika kazini leo kutokana na mgogoro huo.

Polisi hivi sasa wameimarisha ulinzi kwenye maeneo ya Nungwe uliko mradi wa kusambaza maji mgodini, eneo la uwanja wa ndege na geti la kuingia mgodini.

Mkuu wa Wilaya ya Geita, Herman Kapufi na mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma wameingia mgodini baada ya madiwani na wananchi kutawanywa.

Sina Ugomvi na Gabo Wala Simuonei Wivu Ila Namtaka Abadilike- Duma

$
0
0
Sina Ugomvi na Gabo Ila Namtaka Abadirike- Duma
Msanii wa filamu bongo, Daudi Michael maarufu kama 'Duma' amefunguka na kudai hana ugomvi wa aina yeyote na muigizaji mwenzake, Gabo Zigamba ila alichokifanya ni kumtaka abadilike ili aweze kutoa kazi zake wananchi wapate kukiona anachokifanya.

Duma amebainisha hayo baada ya kutoa kauli yake siku za hivi karibuni ya kudai Gabo ndiye chanzo cha tasnia ya filamu kulega lega kwani ameaminiwa na watanzania wengi lakini ameshindwa kuwatendea haki kwa kutoa kazi tangu alipopata tuzo ya muigizaji bora wa kiume pamoja na filamu bora ya mwaka zilizoandaliwa na kutolewa na uongozi wa EATV LTD mnamo mwezi wa 12 mwaka 2016.

"Sina cha kumuonea wivu Gabo, ila mimi siwezi kumuongelea Ray Kigosi, Jacob Stephen (JB) au Rado kwa sababu hao ni watu wa kubwa kwangu lakini 'career' yangu inapokuwa inakosea ni lazima niseme ili mradi mambo yawe sawa tusiweze kukwama huko tunapoenda, mimi nina uchungu sana na hii 'industrial' nafanya kwa sababu ya watanzania wote hata niliyoyaongea sina ugomvi na Gabo na wala siyo mbaya wake", amesema Duma.

Pamoja na hayo, Duma ameendelea kwa kusema "Gabo anatakiwa ajiongeze ili aweze kutanua wigo mkubwa hata nje ya Tanzania aweze kufahamika juu ya anachokifanya. Tunahitaji watu wa kuitoa 'industrial' hapa ilipo na kuipeleka nje ya nchi kama yeye anaona hawezi atatuachie kazi yetu arudi nyumbani", amesisitiza Duma.

Kwa upande mwingine, Gabo amesema imetosha kwa yeye kumzungumzia Gabo kwa sasa kwa madai hana jambo jipya la ku-postiwa katika mitandao ya kijamii lakini kupitia yeye anaweza akapata bahati hiyo kwa sababu hana kazi yeyote aliyoifanya katika tasnia ya filamu.





Mfanyakazi wa Benk Adakwa Sakata la Shambulio la Meja Jenerali Mstaafu

$
0
0
Mfanyakazi wa Benk Adakwa Sakata la Shambulio la Meja Jenerali Mstaafu
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limewakamata watu wawili akiwamo mlinzi wa Suma JKT na mfanyakazi wa NBC, Tawi la Tangibovu wanaotuhumiwa kuhusika na tukio la kujeruhiwa kwa risasi, meja jenerali mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Vincent Mritaba.

Kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa alisema jana kuwa Septemba 11, saa 11 jioni maeneo ya Tegeta Masaiti, jeshi hilo lilipata taarifa ya Mritaba kuvamiwa na watu wawili wasiojulikana ambao walimjeruhi kwa risasi begani, tumboni na mkononi na kumpora Sh5 milioni.

Alisema tukio hilo lilitokea baada ya mstaafu huyo kutoka kuchukua fedha hizo katika benki hiyo tawi la Tangibovu akiwa kwenye gari lake.

Mambosasa alisema alipofika nyumbani kwake alipiga honi na alifunguliwa geti na mlinzi wake, Godfrey Gasper.

Alisema geti lilipofunguliwa ghafla pikipiki iliyokuwa na watu wawili ilisimama na kulifuata gari huku wakiwa na silaha aina ya bastola. Watu hao walishambulia upande wa kulia wa dereva na kioo cha mbele.

Mambosasa alisema cha kushangaza wakati mlinzi huyo anaenda kufungua geti silaha yake aina ya shotgun yenye namba TZCAR9644, aliiacha chini ya kitanda ndani ya kibanda chake cha ulinzi.

Alisema wakati wa tukio watuhumiwa walimwambia akimbie katika eneo hilo na yeye alitii amri hiyo, jambo ambalo linatia shaka.

“Ninavyojua askari wa Suma JKT anapewa mafunzo ya ukakamavu haiwezekani uache silaha chini ya kitanda unakwenda kufungua geti kitu ambacho sikubaliani nacho,”alisema.

Alisema walipofuatilia mawasiliano ya mmoja wa wahudumu wa benki hiyo walibaini alikuwa anapanga mipango na watu mbalimbali wanaokwenda katika benki hiyo. Alisema msako mkali unaendelea ili kuwabaini watuhumiwa waliohusika katika tukio hilo.

Pia, alisema wanaendelea kuwasaka watu waliohusika na uhalifu kwenye ofisi ya mawakili ya Prime Attorneys na watakapokamatwa watachukuliwa hatua za kisheria.

Wakati huohuo, Kamanda Mambosasa alisema wamemuua mtu anayetuhumiwa kwa ujambazi, Anaf Kapela ambaye alishiriki katika matukio mbalimbali likiwamo la mauaji ya askari nane na kupora silaha saba katika tukio la Mkengeni Kibiti mwaka huu.

Mambosasa alisema matukio aliyoshiriki mtuhumiwa huyo ni mauaji ya mkuu wa upelelezi Wilaya ya Newala 2013, uvamizi wa Kituo cha Polisi cha Stakishari jijini Dar es Salaam 2015, kuua askari watatu na kupora silaha mbili aina ya SMG katika Benki ya CRDB eneo la Mbande, Benki ya Access iliyopo Mbagala, Benki ya NMB iliyopo Mkuranga na uhalifu mwingine uliotokea 2016.

Dkt Cloud: Hali ya MC Pilipili Inazidi Kuimarika Yupo Chini ya Uangalizi

$
0
0
Dkt Cloud: Hali ya MC Pilipili Inazidi Kuimarika Yupo Chini ya Uangalizi
Hali ya mchekeshaji Emmanuel Mathias maarufu kama MC Pilipili inazidi kutengemaa baada ya kupata ajali siku ya Jumanne akiwa Mkoani Shinyanga.

Kauli hiyo imetolewa na Daktari wa Hospitali ya Bugando, Dk. Cloud asema Emmanuel Mathias (MC Pilipili) yupo chini ya uangalizi na anaendelea vizuri na matibabu.

Awali hapo zilitoka habari kuwa mchekeshaji huyo yupo katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu akisubiria kufanyiwa vipimo.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule alithibitisha kutokea ajali hiyo ambapo alieleza kuwa Mc Pilipili alikuwa akimkwepa mwendesha baiskeli katika Kijiji cha Bubiki, Kata ya hmkoani humo.

Vanessa Anathamani Kubwa Kwangu- Jux

$
0
0
Vanessa Anathamani Kubwa Kwangu- Jux
MSANII wa muziki wa RNB nchini, Juma Jux, anayetamba na wimbo wake mpya wa ‘Utaniua’ amefunguka juu ya uhusiano wake na mwanamuziki wa Tanzania, Vanessa Mdee, kuwa kwake kwanza ni familia yake halafu anafuata Vanessa Mdee.

Alipoulizwa na mtandao huu kuhusu uhusiano wake na Vanessa, alisema: ”Nampenda Vanessa kuliko msichana yeyote yule na sitegemei kumuacha, hata familia yangu inajua kuwa nina upendo Mkubwa kwa Vanessa.

“Nikiwaga mbali na Vanessa huwaga asubuhi nikiamka cha kwanza naingiaga Instagram kumuangalia baada ya hapo ndo nampigia simu siwezi, kumpigia simu bila kuangalia picha zake. Kiufupi nampenda sana Vanessa,“ alisema Jux.Kuhusu kupata mtoto, Jux alifunguka kwamba:

“Sa’hivi natamani kupata mtoto na nina mpango huo kwa sasa wa kujipanga kupata mtoto na mpenzi wangu pia mtoto wangu wa kwanza nataka nimuite jina la Karim na si jina jingine zaidi ya hilo.”

Matibabu ya Tundu Lissu Milioni 10 Kwa SIku Chadema Yaomba Msaada Jumuiya ya Kimataifa

$
0
0
Matibabu ya Tundu Lissu Milioni 10 Kwa SIku Chadema Yaomba Msaada
Chadema imetangaza kuanzisha kampeni maalumu kuchangisha fedha kwa ajili ya kumgharimia mbunge wake, Tundu Lissu anayeendelea kupata matibabu mjini Nairobi huku matibabu yake yakigharimu Sh 10 milioni kwa siku.

Kutokana na ukubwa wa gharama hizo chama hicho tayari kimeziomba jumuiya za kimataifa ikiwamo Ujerumani na Jumuiya ya Umoja wa Ulaya(EU) kuangalia kama inaweza kusaidia matibabu ya mwanasiasa huyo.

Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdalah Safari amesema leo Ijumaa kuwa pamoja na gharama za kumtibu Lissu kuwa kubwa lakini chama kitaendelea kumpigania ili kuokoa maisha yake.

“Unajua chama tumepoteza watu wengi sana, kama vile Ben Saanani, Dk Slaa ( Willbroad) lakini tuna mahaba makubwa na ndugu yetu Lissu hivyo tunaendelea kupigania maisha yake. Gharama  anazotumiwa kutibiwa ni kubwa mno maana kwa siku inagharimu kiasi cha Sh10 milioni sasa sisi peke yetu hatuwezi ndiyo maana tumeamua kuomba msaada toka kwa rafiki zetu,” amesema.

Amesema chama kimeunda kamati maalumu ambayo inaratibu michango ya Lissu na moja ya eneo ambalo wamewasilisha maombi yao ni kwa Serikali ya Ujerumani na Umoja wa Ulaya.

“Siwezi kusema hadi sasa nini tumejibiwa ila ninachojua kamati inaendelea kufuatilia... unajua wale Wajerumani ni ndugu zetu maana chama cha CDU ni marafiki zetu na tumewaandikia,” amakati wa kubeba uchumi wa taifa

Watu Wawili ‘Wasiojulikana’ Wauawa na Polisi..Walikuwa na Silaha Yenye Risasi 41

$
0
0
Songea. Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limewaua watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakati wakirushiana risasi na polisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Gemini Mushy amesema tukio hilo limetokea jana Jumatano saa 2:45 usiku katika Kijiji cha Nangungulu Wilaya ya Tunduru.

Alisema askari polisi wakiwa doria waliwaua wanaume wawili ambao wanakadiriwa kuwa na umri wa miaka 20-30 baada ya majibizano ya risasi.

Kamanda Gemini alifafanua zaidi kuwa watu hao walikuwa na silaha aina ya SAR na risasi zake 41 pamoja na pikipiki ambayo namba zake za usajili zimehifadhiwa.

Alisema polisi wakiwa doria waliona pikipiki ikiwa imesimama hivyo walisimama ili kuikagua ndipo abiria akitoa bunduki na kuanza kuwashambulia askari ambao nao walijibu mashambulizi na kufanikiwa kuwazidi maarifa na kupoteza maisha palepale.

Alisema katika tukio hilo hakuna askari aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha.

Kamanda amewaomba wananchi kutoa taarifa za wahalifu  wanaojihusisha na matukio ya utumiaji silaha kama wanawafahamu au pindi wanapowatilia shaka.

Amewataka wananchi kujitokeza kutambua miili ya watu hao ili waweze kuchukuliwa na ndugu zao.

Spika Job Ndugai Ampa za uso Lema, Adai Lema Anapotosha Umma Bunge Haliwezi Simama

$
0
0
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, amejibu tuhuma za mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, na kumtaka asipotoshe wananchi, bali apeleke malalamiko yake kwenye kamati.

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akiendesha bunge, na kusema kwamba bunge lina utaratibu wake kwenye kila jambo linalohusika bungeni hapo.

"Lema asipotoshe wananchi aende hadharani kwenye kamati kuzungumzia hayo, bunge haliwezi kusimama kwa shambulio la Lissu bali kanuni zinasema mbunge akifariki bunge linasimama kwa siku moja. Na iwapo Spika akiletewa jambo la maadili linapelekwa kamati ya maadili, suala la jinai linapelekwa polisi", amesema Spika Ndugai

Pia Spika Ndugai amesema suala la Tundu Lissu kuchangiwa fedha za matibabu na wabunge wakati yeye alitibiwa nje ya nchi ni kwamba matibabu ya Tundu Lissu yameenda kinyume na utaratibu wa bunge.

"Wabunge wanaopelekwa nje (India) wanapewa rufaa kutoka hospital ya Muhimbili lakini si kama alivyopelekwa Lissu", amesema Spika Ndugai.

Pamoja na hayo Spika Ndugai amesema anamsamehe Godbless Lema na kuwataka watu kumsamehe kwani hajui alitendalo
Hapo jana mbunge wa Arusha Godbless Lema alimlaumu Spika Ndugai kuwa anashindwa kutetea kiti chake, kwa kuzidi kuwakandamiza wabunge wa upinzani hususan suala la kupigwa risasi kwa Tundu Lissu.

BREAKING NEWS: Mahakama Yamuachia Huru Manji

$
0
0
BREAKING NEWS: Mahakama Yamuachia Huru Manji
Mahakama imemuachia huru mfanyabiashara Yusuf Manji katika kesi ya uhujumu uchumi baada ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) kuwasilisha hati mahakamani hapo ikionyesha kuwa hana nia ya kuendelea na kesi dhidi yake.

Manji na watuhumiwa wenzake watatu walikuwa wakikabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na plate number mbili za magari ya serikali.

Watuhumiwa wengine walioachiwa huru kwenye kesi hiyo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja.


JE Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kufika Kileleni Haraka na Kushindwa Kurudia Tendo?

$
0
0
JE, UNA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUFIKA KILELENI HARAKA NA KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume husababishwa na mambo mengi kama KISUKARI, UNENE ULIOPITILIZA, KUJICHUA (MASTER BLASHION), HOMONI kushindwa kufanya kazi ipasavyo n.k. Upungufu wa nguvu husababisha tendo la ndoa kutokufanyika kwa kujiamini na kwa usahihi na hivyo kusababisha ndoa na mahusiano kuvunjika.

BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Uume kusinyaa katikati ya tendo ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. Kwa kutumia mimea na matunda @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250000@250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 6 hadi 7 @150000@150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200000@200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni @130000@130,000/= BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA NA ZIMETHIBITISHWA KIAFYA. KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr @markson_beauty_pr

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa (+255) 0767447444 na 0714335378

  NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Kikosi Maalum cha Kupambana na Matukio ya Mashambulio ya Risasi Kuanzishwa na Serikali

$
0
0
Kikosi Maalum cha Kupambana na Matukio ya Mashambulio ya Risasi Kuanzishwa na Serikali
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa imesema imepanga kuunda kikosi maalum kitakachohusisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama ili kupambana na matukio ya kihalifu ikiwemo mashambulio yanayohusisha silaha za moto

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi leo bungeni wakati alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Mkoani (CUF) Twahir Mohamed alipouliza ni kwa nini Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) lisihusishwe katika kukomesha matumizi ya silaha na mauji ya raia wasiokuwa na hatia yeyote nchini huku akitolea mfano kwa tukio la shambulio la Meja Jenerali Mstaafu Vicent Mirataba pamoja na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ambao wote walishambuliwa na risasi katika siku tofauti ndani ya mwezi huu.

Waziri Mwinyi amesema hapana shaka kuwa kazi ya Jeshi la ulinzi ni kulinda mipaka ya nchi, lakini pale linapohitajika kutoa msaada katika maeneo mengine, chombo hicho kipo tayari kufanya hivyo.
"Ni dhahiri kwamba kazi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania( JWTZ) ni kulinda mipaka, lakini pale ambapo linahitajika au linaombwa kusaidia mamlaka nyingine, iwe za kiraia au iwe vyombo vingine vya ulinzi na usalama, basi wanakuwa tayari kufanya hivyo", amesema Dkt. Mwinyi.

Pamoja na hayo, Waziri Mwinyi ameendelea kwa kusema "Kwa hali ilivyo sasa itaundwa 'task force' (kikosi maalumu) itakayojumuisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama, ili kuweza kulifanyia kazi tatizo hili la uvunjifu wa amani ndani ya nchi na sina shaka juu ya kazi hiyo kwa kuwa naamini imeshaanza", amesisitiza Waziri Mwinyi.
Kwa upande mwingine, Dkt. Mwinyi amewahakikishia Watanzania na kusema jukumu hilo litatekelezwa mapema ili hali ya usalama ipatikane ndani ya nchi.




Hakimu Hawa Mbogo Achukizwa na Upande wa Jamhuri Kushindwa Kumpeleka Sethi Hospitali kwa Matibabu

$
0
0
Hakimu Hawa Mbogo Achukizwa na Upande wa Jamhuri Kushindwa Kumpeleka Sethi Hospitali kwa Matibabu
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imechukizwa na upande wa mashtaka kwa kushindwa kutekeleza amri ya kumpeleka mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme IPTL, Harbinder Sigh Sethi akatibiwe Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Hatua hiyo inatokana na Wakili wa Sethi, Melchisedeck Lutema kumueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa Sethi hajapelekwa Hospital ya Muhimbili kama Mahakama ilivyoagiza.

Lutema alidai kuwa katika mashauri yaliyopita Mahakama ilitoa amri mara kadhaa ikielekeza mshitakiwa huyo apelekwe Hospitali ya Muhimbili lakini haijatekelezwa.

”Naiomba Mahakama itumie busara ili kuhakikisha mshtakiwa anapelekwa Hospital na kwamba wa kuthibitisha kama ametibiwa au la ni mshtakiwa mwenyewe.”

Hakimu Shaidi alipomuuliza Sethi kama ameshatibiwa, alijibu hajatibiwa na kutokana na hatua hiyo, Hakimu Shaidi alisisitiza mshitakiwa huyo apelekwe katika Hospitali ya Muhimbili kama ilivyotoa maagizo awali.

”Ni wazi oda ya Mahakama lazima ifuatwe, haiwezekani kila siku tukija hapa tunaongea kitu kimoja tu hii haipendezi.”

Alisema mshtakiwa anatakiwa kupelekwa Muhimbili kwa sababu maalumu walizoeleza hapo awali kuwa ana puto tumboni.

”Nia ya kufanya hivyo ni afya ya mshtakiwa ili awe na afya njema. Hakuna sababu za kuja Mahakamani kama amri za Mahakama zinakuwa hazifuatwi. Naendelea kusisitiza na haifurahishi naomba apelekwe Hospitali.”

Awali katika kesi hiyo Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leonard Swai alidai  shauri limekuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kudai kuwa mshtakiwa alipelekwa Hospitali ya Magereza na kwamba alitibiwa na mtaalamu Dotto Pakacha ambaye anampatia matibabu kila anapolalamika huwa wanamuona.

”Kwa utaratibu wa Hospitali, Magereza hawajawahi kuwasilishiwa vyeti vya matibabu ili Daktari ajue anaanzia wapi kwenye kutoa matibabu.”

Aidha, alidai mshtakiwa alishapelekwa Hospitali ya Amana na kutibiwa na jopo la madaktari ambao walichukua vipimo ili wakamfanyie MRI Muhimbili.

”Tunaendelea na upelelezi kwa sababu kuna mashtaka ya kughushi yanahusisha Taasisi zaidi ya moja. Tunaomba Mahakama itupe muda ili tukamilishe upelelezi.”

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi September 29, 2017.


Wabunge wa Jubilee Kenya Waliamsha Dude Wamtaka Jaji Mkuu Ang'oke Kwenye Nafasi Yake

$
0
0
Wabunge wa Jubilee Kenya Waliamsha Dude Wamtaka Jaji Mkuu Ang'oke Kwenye Nafasi Yake
Jaji Mkuu wa Kenya, David Maraga ameingia matatani baada ya wabunge wa Jubilee kutaka ang’oke kwenye nafasi hiyo ikiwa siku chache baada ya jaji huyo kutengua matokeo ya urais yaliyompa ushindi mgombea Uhuru Kenyatta.

Mbunge wa Nyeri Mjini kwa tiketi ya Jubilee, Ngunjiri Wambugu amefungua mashtaka katika Tume ya Majaji akitaka Jaji Maraga ang’olewe kwa kile alichokieleza kuwa ‘utendaji wake mbaya’.

Mbunge huyo aliyewasilisha mashtaka yenye kurasa 14 ameomba Tume ya Majaji kwa kushirikiana majaji na mahakimu kuanzisha uchunguzi dhidi ya  Jaji Maraga ili kubaini mwenendo wake tangu alipoteuliwa kwenye wadhifa huo.

Wambugu anadai kuwa Jaji Maraga ametekwa na kundi la mashirika ya kiraia ambayo yamekuwa yakiendesha kampeni dhidi ya urais wa Kenyatta tangu mwaka 2013.

Pia, anadai jaji huyo alimzuia Jaji Mohamed Ibrahim kushiriki katika kesi iliyofunguliwa na mgombea wa Nasa, Raila Odinga aliyekuwa akipinga matokeo ya urais. Jaji Ibrahim alikatiza siku ya pili kusikiliza kesi hiyo kutokana na kuugua.





Wajitosa Kusoma Albadiri Kuwatambua Wasiojulikana Waliomshambulia Lissu

$
0
0
Wajitosa Kusoma Albadiri Kuwatambua Wasiojulikana Waliomshambulia Lissu
Baraza la vijana wa CHADEMA wilayani Muheza Mkoani Tanga, wamethibitisha kutaka kusoma albadili ili kumjua mtu aliyempiga risasi mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Akizungumza na mwandishi wa habari wa East Africa Television mwenyekiti wa BAVICHA wilaya ya Muheza Mkoani Tanga bwana Joseph Saja amesema wameona ni vema kufanya hivyo ili kuisaidia serikali kuweza kuwatambua watu wasiofahamika, ambao wameweka rehani maisha ya Mwanasheria mkuu wa CHADEMA Tundu Lissu.

Bwana Saja amesema albadili hiyo haina lengo la kumdhuru mtu, isipokuwa wawatambue watu hao na kuwashikisha adabu, ili iwe somo kwa wengine na vitendo hivyo visiendelee kufanyika.

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images