Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Shinda Gari la Bure...Shindano hili ni la Bure Usipuuzie tu

$
0
0
Jee!! Katika Maisha yako umewahi kuwa na ndoto ya kumiliki Gari lako?  Kama jibu ni Ndio Basi Kampuni ya Kijapan inakupa Fasi ya kushinda Gari Buree yani Buree bila kulipa chochote..

Chakufanya ni kubofiya neno SHINDA GARI hapo chini na kisha Bonyeza Neno APPLY NOW kwa kujisajili...

Kumbuka huduma hii ni ya Bure kabisaaaaa...


>> SHINDA GARI <<



Jinamizi la Watu Wasiojulikana Lazidi Umiza Watu..Dereva wa Mbunge Ajeruhiwa Kwa Shoka

$
0
0

Tarime. Suezi Dan Maradufu (45), dereva wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche ameshambuliwa na watu wasiofahamika usiku wa kuamkia leo na kumjeruhi usoni.

Akiwa amelazwa katika hospitali ya Mji wa Tarime, Maradufu amesema jana Alhamisi saa mbili usiku akitoka nyumbani kwake kwenda kwa  mbunge alivamiwa na watu wawili waliomjeruhi kwenye paji la uso.

Maradufu amesema alikuwa akienda kwa Heche ili wasafiri kwenda Nairobi nchini Kenya kumwona Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa jijini humo baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma.

Dereva huyo amesema baada ya kuvamiwa  na watu hao, walimpiga kwa shoka kwenye paji la uso na walipora begi lake la nguo.

Mrimi Zabron ambaye ni katibu wa mbunge Heche anayemuuguza dereva huyo amesema alifikishwa hospitali saa nane usiku.

Amesema kwa usaidizi wa ndugu wa Heche alifikishwa hospitali na ameshonwa nyuzi sita kwenye jeraha.

Zabron amesema safari ya Heche iliyokuwa ifanyike jana saa nne usiku, imefanyika leo asubuhi.

Amesema mbunge huyo amesafiri na kaka yake ambaye ni Katibu wa Chadema Mkoa wa Mara, Chacha Heche.

Maskini..Kumbe Manji Amenyang’anywa Udiwani kwa Makosa ya Mwaka 2016

$
0
0

Maskini..Kumbe Manji Amenyang’anywa Udiwani kwa Makosa ya Mwaka 2016
Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Chaurembo amesema aliyekuwa Diwani wa Mbagala Kuu (CCM), Yusuf Manji alivuliwa cheo hicho kwa kosa la kutohudhuria vikao sita vya mwaka 2016 bila kutoa taarifa.

Manji aliyekumbwa na mikosi ya kesi tangu mwaka huu uanze juzi aliachiliwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam akiwa na wenzake watatu waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kukutwa wakiwa na mabunda 35 ya vitambaa vinavyotumika kutengeneza sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) zenye thamani ya Sh 192.5 milioni.

Kesi hiyo imefutwa baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP) kusema hana nia ya kuendelea nayo.

Mbali na kesi hiyo, Manji pia anakabiliwa na kesi ya matumizi ya dawa za kulevya aina ya heroin aliyosomewa Februari 17, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Septemba 6, Meya Chaurembo aliwaambiwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa walimwondoa kwenye nafasi ya udiwani kwa kukosa sifa ikiwa pamoja na kutohudhuria mikutano sita ya Baraza na Kamati za  Madiwani.

Hata hivyo, Manji alishaeleza kuhusiana na kutokubaliana na hatua ya kumvua udiwani na mara baada ya kuachiwa huru, aliulizia kuhusu malalamiko yake aliyowasilisha mahakamani hapo kuhusu udiwani wake yako vipiu lakini Hakimu Shaidi alimueleza kwa kuwa yuko huru ataenda kulishughulikia hilo.

Akizungumza jana kwa njia ya simu na gazeti hili, Chaurembo alisema makosa ya Manji yalitendeka mwaka 2016 kabla hata mikosi ya kukamatwa na kufunguliwa kesi haijaanza.

Mwananchi

Ajirusha Akiwa uchi kwenye Kundi la Simba..Kilichompata Hata Kaa Asahau

$
0
0
Chile. Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni,  kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Franco Luis ameshambuliwa na kundi la simba baada ya kujirusha ndani ya bustani ya wanyama hao akiwa uchi.

Luis  aliwaacha mdomo wazi watu waliofurika kwenye bustani hiyo ya Santiago  mwishoni mwa wiki ambao wengi waliambatana na  familia zao.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la Uingereza, kijana huyo mwenye miaka 20, alikimbizwa hospitali baada ya walinzi wa bustani hiyo kumuokoa kwa  kuwaua simba wawili waliokuwa wanamshambulia.

Uongozi wa bustani hiyo ulithibitisha tukio hilo na kudai kwamba kijana huyo alishambuliwa akiwa uchi wa mnyama baada kuvunja uzio na kuingia kwenye kundi hilo.

Mkurugenzi wa Santiago Alejandra Montalva alisema walijua kijana huyo aliingia  kwenye bustani hiyo kama wateja wa kawaida wanavyolipa tiketi  kwa lengo  la kutembelea hapo.

‘‘Baada ya kufanya malipo kama mteja wa kawaida kijana huyo hakupita kwenye njia inayotumiwa na wateja bali aliezua paa la simba hao na kutumbukia ndani na kuanza kushambuliwa,’’ alisema

Alisema ni kitendo cha kushangaza kwani kila mtu alishikwa na bumbuwazi baada ya kumuona kijana huyo akijirusha kwenye kundi hilo la simba na kuanza kupigana nao.

Alisema askari wa bustani hiyo walitumia nguvu za ziada kuhakikisha wanaokoa maisha ya kijana huyo, ambaye hawajafahamu fika kama alikuwa na akili timamu.

 Atoa sababu

 Kwa upande wake kijana huyo alisema alifanya kitendo hicho cha kustaajabisha kila mtu kutokana na ufunuo alioshushiwa na  Mungu.

Shuhuda

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Cynthia Vasquez alisema  baada ya Luis kujirusha ndani ya bustani hiyo, simba waliokuwa ndani hawakumdhuru kwanza.

“Cha kushangaza simba hao walianza kucheza naye,”alisema Vasquez

 Vasquez ambaye alikuwa miongoni mwa wageni waliotembelea bustani hiyo, alisema baada ya dakika chache   Lius alisikika akipiga kelele. “Walianza kumrarua...alipiga kelele aliita jina la Yesu,”alisema.                      

Alisema kelele hizo ziliwavuta watu wengi ambao walifika kushuhudia tukio hilo.

Vasquez alisema walinzi waliofika kuokoa maisha ya Luis walilazimika kufyatua risasi juu ili kuwatawanya watu. “Waliingia baada ya kuwaua simba hao na kumtoa Luis ambaye alikuwa ameshajeruhiwa vibaya,” alisema.

Baba aongea

Baba mzazi wa Luis alisema  alishaanga kusikia watu wanapiga kelele na alipofika katika eneo la tukio alimkuta kijana wake akiwa amejeruhiwa vibaya na simba.

Wote Tumeongea Kuhusu Tundu Lissu Lakini Kwa Huu Wimbo wa Aslay Aliyomuimbia Lissukatuzidi!

$
0
0

Bonyeza Play Kusikiliza



Lissu Get well soon!
kuna watu bwana eti wasiojulikana,
Wazalendo raha hatuna,
Tanzania amani hakuna,
wasidhani sisi ni wajinga sana,
kwa hili tunaumia roho zetu,
kwani lisu lipi baya alilofanya,
Mbona mwaharibu taifa letu,

Mwambieni ama zake ama zetu,
tutakufa nae

Mwambieni ama zake ama zetu,
tutakufa naye.

Sababu yake amani hakuna,
Ama zake ama zetu,
tutakufa naye.

Yalianzia kibiti Pwani,
na kutekana watu jamani,
siyo kama raia hatuoni,
kwa Lissu mmetugusa moyoni,


Nini chanzo bwana au ni kusema ukweli,
wasidhani sisi ni wajinga sana,
kwa hili tunaumia roho zetu,
kwani Lisu lipi baya alilofanya,
Mbona mwaharibu taifa letu?

Mwambieni ama zake ama zetu,
tutakufa naye,

Mwambieni ama zake ama zetu,
tutakufa naye.

Kwa sababu yake amani hatuna!

Naombeni Ushauri Kila Nikifanya Mapenzi Bila Zana Napata Ujauzito

$
0
0
Mimi ni Msichana wa Miaka 25 , Tatizo langu ni kuwa kila nikifanya mapenzi na mvulana bila kutumia zana lazima nipate mimba, nilianza kuwajua wanaume toka nikiwa na miaka 21 siku niliyotolewa bikira nilipata mimba pia ikanibidi niitoe kwa vile nilikuwa nasoma ..sasa kuanzia kipindi hicho nikifanya tu lazima nipate mimba nimeshatoa mimba kumi na tano mpaka sasa, Nimejaribu kufuata Calender lakini wapi...Je hili ni Tatizo ama nimelogwa ? Nimekuwa mtu wa kufanya abortion kila wakati mpaka naogopa sasa nisije haribu kizazi changu nikashindwa kuzaa muda muafaka wa kuwa na mtoto....................

Help pliz

Mimi Mdau ..Msinitukane jamani

Jeshi la Polisi Limeapiga Marufuku Maombi ya Kumuombea Tundu Lissu Yaliyopangwa Kufanyika Jumapili

$
0
0
Jeshi la Polisi Yapiga Marufuku Maombi ya Kumuombea Tundu Lissu Yaliyopangwa  Kufanyika Jumapili
Kamishna Kanda maalumu ya Dar es salaam, Lazaro Mambo Sasa amepiga marufuku maandamano na maombi yanayotaka kufanywa na CHADEMA siku ya Jumapili kumuombea Tundu Lissu kwenye uwanja wa TP Sinza Dar es Salaam na kusema hiyo siyo sehemu ya maombezi.

Lazaro Mambo Sasa amesema hayo leo wakati akifanya mahojiano na waandishi wa habari na kusema kuwa hawezi kuruhusu mkusanyiko wa watu na kuwataka watu ambao wanataka kumuombea Tundu Lissu kwenda kwenye nyumba za ibada na kumuombea lakini si kufanya mkusanyiko huo ambao wao CHADEMA wanataka kufanya.

"Hatutaruhusu mkusanyiko wowote usio na kibali, yapo maeneo ambayo kimsingi yanaendesha maombi hayo, yapo makanisa ipo misikiti na mahali pengine ambako pengine ni rasmi kwa shughuli hiyo, kupitia kwenu nasema hakutakuwa na kusanyiko hilo, yapo maneno ambayo yanaendelea kutolewa kupitia taarifa zao walizotoa ambayo maneno hayo kimsingi kila anayesikiliza anajua nia yao ni nini. Na sisi tukishaona kuna viashiria vya uvunjifu wa amani hatuwezi kuhurusu mkusanyiko wa watu kwa hiyo mkusanyiko wa maombi hayo ni marufuku, tunaruhusu mwenye uwezo hata wa kukesha kanisani aende kwani ni mahali rasmi kwa maombi" alisisitiza Mambo Sasa

Aidha Kamanda Mambo Sasa ametolea ufafanuzi juu ya wanachama wa CUF ambao waliomba kufanya maandamano siku ya Jumapili Septemba 17, 2017 kwa ajili ya kuwapokea baadhi ya wabunge saba wa chama hicho ambao wameapishwa siku ya karibuni bungeni na kusema jambo hilo haliwezekani na yoyote ambaye atakiuka maagizo hayo basi ataishia mikononi mwa polisi.
"Sambamba na hilo naomba niseme kwa wale wanachama wa CUF ambao wameomba tarehe 17 kuwapokea wabunge wa CUF wanaotoka kuapishwa Dodoma walikuwa wameomba kufanya maandamano waanzie Kimara kuelekea Buguruni tumeshatoa maelekezo kuhusu hilo kuwa maandamano hayaruhusiwi na yoyote atakaye jaribu kufanya maandamano ataishia mikononi mwa polisi" alisema Kamanda Mambo Sasa

Baraza la Vijana CHADEMA (BAVICHA) leo asubuhi lilitoa taarifa kwa umma kuwa siku ya Jumapili litafanya maombezi ya kitaifa kwenye uwanja wa TP uliopo Sinza Darajani kumuombea Mbuge Tundu Lissu ambaye alishambuliwa na risasi na watu wasiojulikana ili aweze kupona kwa haraka na kurudi kuendelea na shughuli zake, jambo ambalo limepigwa na jeshi la polisi.

Naungana na Mh.Rais, Viongozi Wengine na Wananchi Katika Kumuombe Tundu Lissu- Waziri Mjaliwa

$
0
0
Naungana na Mh.Rais, Viongozi Wengine na Wananchi Katika Kumuombe Tundu Lissu- Waziri Mjaliwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, amesema anaungana na Rais Magufuli, viongozi wengine na wananchi, katika kumuombea Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu aliyepigwa risasi.

Akisoma hotuba ya kughailisha bunge mapema leo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amesema anamuombea Tundu Lissu ili aweze kupona na kurejea katika hali yake ya kawaida na kwenye shughuli zake kwa jamii.
“Naungana na Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Mheshimiwa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Spika wa Bunge Job Ndugai, wabunge na wananchi mbali mbali, kumpa pole kwa majeraha na maumivu makubwa anayoyapata, na tunamuombea apone haraka na kurejea kwa familia yake, lakini pia na sisi hapa bungeni kwa shughuli za bunge”, amesema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Leo waziri mkuu ameghailisha shuguli za bunge kwa mujibu wa sheria, mpaka hapo Novemba 7 mwaka 2017 litakapoanza vikao vyake tena

Omog Mguu ndani Mguu Simba Siku zake Zahesabika

$
0
0
Omog Mguu ndani Mguu Simba Siku zake Zahesabika
Mabingwa wa Kombe la Azam Sport Federation Cup ‘ASFC’, Simba SC inatarajia kucheza mchezo wake wa duru la tatu wa Ligi Kuu Tanzania Bara namba 24 dhidi ya klabu ya Mwadui FC utakao pigwa katika dimba la Uhuru Jijini Dar es salaam.

Simba itaingia uwanjani huku ikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare tasa ya bila kufungana katika mchezo uliyopita dhidi ya matajiri wa Dar es salaam klabu ya Azam FC mchezo namba 10 wa duru la pili uliyopigwa Azam Complex Chamazi Agosti 9 mwaka huu.

Kufuatia matokeo ya kutoridhisha ya Simba tangu ilipoanza kuwatambulisha wachezaji wake katika mchezo wao wa Simba Day, mashabiki wa klabu hiyo wamekuwa wakilalamika katika mitandao ya kijamii kwa Kocha Mkuu, Joseph Omog kushindwa kupanga kikosi chake kilicho jaa wachezaji wenye majina makubwa hii inatokana na usajili bora uliyofanywa na timu hiyo msimu huu uliyogharimu zaidi ya Bilioni moja.

Katika mchezo wake wa Simba Day kikosi hicho kilichosheheni wachezaji wenye uzoefu mkubwa kilishindwa kufanya vizuri na kulazimika kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya timu ya Rayon Sports ya Rwanda bao lililofungwa na Mohamed Ibrahim dakika ya 16 kipindi cha kwanza.

Baada ya utambulisho wa wachezaji wake 10 wapya wakiwemo, Haruna Niyonzima na Emmanuel Okwi ikaingia uwanjani Agosti 23 katika mchezo wa Ngao ya Jamii ambao hutumika kufungua pazia la Ligi Kuu walipo cheza dhidi ya mahasimu wao Young Africans, klabu hiyo yenye maskani yake mtaa wa msimbazi ilishindwa kuonyesha makucha yake ya usajili mbele ya mashabiki lukuki waliyojaa uwanja wa Taifa walioamini kuchomoza na ushindi mnono hatimaye kumalizika kwa hatua ya matuta ya mabao 5-4 na kutwaa Ngao hiyo.

Mchezo uliyofuata Simba ikicheza na Mtibwa Sugar ikachomoza na ushindi wa bao 1-0 matokeo ambayo hayakutarajiwa na mashabiki wengi ukilinganisha hasa na uwekezaji uliyofanywa na timu hiyo msimu huu wa 2017/18.

Mara baada ya kuanza kwa msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara Simba ikacheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Ruvu Shooting na kufanikiwa kuchomoza na ushindi mnono wa mabao 7-0 na kuwafurahisha mashabiki wake ambao waliyoonekana kukerwa na matokeo yaliyopita.



Katika mzunguko wa pili wa Ligi kuelekea mchezo wao na Azam FC, klabu ya Simba ilipata fursa ya kucheza michezo kadhaa ya kirafiki ambapo ikicheza na baadhi ya timu kutoka Zanzibar, ikicheza na Gulioni FC na Mlandege zote za Visiwani. Kisha kucheza na Azam na kupata matokeo ya sare matokeo ambayo yameonekana kuzua maswali mengi ya wapenzi wa timu hiyo na kuamini kuwa Kocho Mkuu, Joseph Omog ameshindwa kupanga kikosi hasa msimu huu ukilinganisha na uwezo mkubwa wa wachezaji waliyopo.



Simba SC inaelekea katika mchezo wake na Mwadui siku ya Jumapili huku kuna umuhimu mkubwa kwa timu hiyo kuondoka na pointi tatu ili kutuliza presha ya mashabiki wanao amini ubora wa kikosi chao licha ya kwamba watawakosa wachezaji  wao wanne walio majeruhi, Haruna Niyonzima, Juma Liuzio, Erasto Nyoni na Shomari Kapombe.



Wakati mashabiki wakiendelea na wimbo wa kusisitiza kwa benchi la ufundi kumchezesha kiungo, Jonas Mkude nafasi ya kucheza mara kwa mara  msimu huu.



Kenyatta Ametaka Kufutwa kwa Kampeni ya Kumuondoa Jaji Mkuu Maraga

$
0
0
Kenyatta Ametaka Kufutwa kwa Kampeni ya Kumuondoa Jaji Mkuu Maraga
Mgombea urais wa Kenya kupitia chama tawala cha Jubilee Uhuru Kenyatta, ametaka kufutwa kwa kampeni ya kuondoa Jaji Mkuu wa nchi hiyo David Maraga, iliyoanzishwa na mbunge wa chama hicho.

Uhuru Kenyatta amesema ni vyema kuacha Mahakama ifanye kazi zake na wao kuangalia zaidi kwenye uchaguzi wa urais unaofuatia ili kutetea nafasi ya chama hicho kubaki madarakani.

"Tumekubaliana kurudi kwa wapiga kura na masanduku ya kupigia kura, naelewa maumivu yenu na matendo yenu, lakini tuna uchaguzi wa kushinda Oktoba 17, hilo ndio linatakiwa liwe kipaumbele chetu, iacheni mahakama", amesema Uhuru Kenyatta.

Hapo jana mbunge wa chama cha Jubilee Ngunjiri Wambugu alianzisha kampeni ya kumuondoa madarakani Jaji Mkuu wa nchi hiyo David Maraga, kutokana na kile alichokiita utendaji mbaya baada ya kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais nchini humo Septemba 1 mwaka huu, na kutaka urudiwe.

Huu Hapa Utabiri wa Canavaro kwa Yanga Kuelekea Mechi ya Kesho Dhidi ya Majimaji

$
0
0
Huu Hapa Utabiri wa Canavaro kwa Yanga Kuelekea Mechi ya Kesho Dhidi ya Majimaji
Nahodha wa timu ya Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amefunguka na kudai mechi yao ya kesho dhidi ya Majimaji FC itakuwa ngumu kutokana na hali ya kiwanja kutokuwa vizuri huku akiahidi watafanya kila wawezalo ili kutoka na pointi tatu.

Canavaro ameeleza hayo kupitia ukurasa wao maalum wa timu ikiwa imebaki siku ya leo tu, kushuka katika dimba la Majimaji lililopo mkoani Ruvuma katika mchezo wa ligi kuu mzunguko wa tatu.
"Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kufika salama Songea, lakini kuelekea mchezo wetu wa kesho dhidi ya Majimaji naamini utakuwa mgumu sana kutokana na wapinzani wetu wamejiandaa vizuri ila kwa upande wetu tumejiandaa vizuri zaidi yao kwa sababu tunajua kila mechi ni fainali kwetu", amesema Canavaro.
Pamoja na hayo, Canavaro ameendelea kwa kusema "Japokuwa tunafahamu tutakutana katika mazingira magumu ikiwemo kiwanja siyo kizuri lakini kwetu sisi ushindi ni muhimu ili tuweze kupata pointi 3 na tuweze kurejea nyumbani tukiwa na jumla ya alama sita", amesisitiza Canavaro.

Nahodha wa timu ya Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro'
Kwa upande mwingine, Canavaro amekiri kwamba ligi kuu ya safari hii imekuwa ngumu kwa kuwa kila timu imejipanga vizuri katika kusaka pointi tatu kila iingiapo uwanjani lakini kwa niaba ya timu yake ameahidi watatetea ubingwa wao ili kikombe kizidi kubaki Jangwani

Magari Mabovu 26 ya Polisi yazidi Kumpa Kiki PAUL Makonda.....Picha

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda leo September 15, 2017 amefanya ziara Kilimanjaro kukagua ukrabati wa magari mabovu 26 ya Jeshi la Polisi DSM ambayo awali yalikaa kwa muda usiopungua miaka mitano bila kufanya kazi.

Magari hayo sasa yamekamilika na yanatembea na katika wiki mbili zijazo yatakabidhiwa rasmi kwa ajili ya kuongeza na kuboresha ulinzi katika Mkoa wa Dar es Salaam kutokana na kukarabatiwa kwa mfumo kisasa tofauti na awali.

RC Makonda ameridhika na muonekano wa sasa wa magari hayo ambayo yatarejea barabarani huku akifanikiwa kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambacho kingetumika kununua magari mengine.

Wako baadhi ya wananchi walibeza hili wazo langu la kuyakarabati magari haya kwa kiwango cha Kimataifa, lakini sasa nafurahi kuona ndoto yangu imekuwa kweli. Ni jambo jema kwa Mkoa wetu.” – RC Makonda.


JE Umeshawahi Tumia poda ya JOHNSON’S? Ina Skendo ya Kusababisha Kansa ya Kizazi

$
0
0
Mwanamke mmoja nchini Marekani Eva Echeverria, mwenye miaka 63 ameshinda kesi ya madai dhidi ya kampuni ya Johnson & Johnson baada ya kusema kwamba amepata saratani/kansa ya kizazi baada ya kutumia poda ya Johnson’s Baby.

Hukumu hiyo inayomzawadia  dola za Kimarekani  milioni 417 (dola 1 ni zaidi ya Tsh 2,200) mwanamke huyo ambaye amekuwa akipaka poda hiyo kwa miongo kadhaa imewashtua wengi ambao bado wamekuwa wakiitumia bidhaa hii.

Mwanamke huyo anadai kwamba amepata saratani/kansa ya Ovari baada ya kutumia poda hiyo katika sehemu zake za siri kwa miaka mingi, ingawa hukumu hii haina maana ya moja kwa moja kwamba poda hizi ndiyo chanzo kikuu cha kansa hiyo lakini ushindi katika shauri hili unaamsha hali ya tahadhari kwa watumiaji wa bidhaa hiyo.


Sehemu mbaya kwa kampuni hiyo ni kwamba moja ya ushahidi uliotumiwa na wanasheria wa bibi Eva ni memo ya ndani ya kampuni hiyo ambapo wanasayansi wake walidai ya kwamba kukataa ya kwamba marighafu inaweza kuleta kansa ya kizazi kwa wanawake ni sawa na mtu anayekataa ya kwamba uvutaji sigara unaweza sababisha kansa ya koo/mapafu.


Kwa wanawake inabidi kuwa makini katika utumiaji wa poda hii sehemu za siri. Madai makubwa ni kwamba kuna marighafi muhimu ya poda inayotumika, kama ikifanikiwa kuingia ukeni kwa wingi na kwa muda mrefu inaweza kuleta saratani ya kizazi (Ovari)
Mtandao wa TFDA mamlaka ambayo inahusika na madawa na vyakula kwa Tanzania bado haujatoa taarifa yeyote juu ya hili na pengine baada ya muda watautaarifu umma kama wataona kuna haja hiyo, kikuu ni kwamba bado ata Marekani kwenyewe hili jambo halijapata msimamo rasmi wa kisayansi. Wengi wanaamini utafiti zaidi unatakiwa kuendelea.

Unaambiwa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta Aanza Kuiga Sera za Rais Magufuli...

$
0
0
Ikulu ya Jamhuri ya Kenya imepiga marufuku kwa wafanyakazi/watumishi wote wa serikali kusafiri nje ya nchi bila ya kuwa na kibali maalumu kutoka kwa Rais.

Katika barua iliyotolewa Septemba 13 mwaka huu na Ikulu ya Kenya, ilieleza kuwa kuanzia sasa hadi itakapoamuliwa vinginevyo, hakuna mtumishi wa serikali atakayeruhusiwa kutoka nje ya nchi pasi na idhini ya Rais,

Kuondoa utata, barua hiyo iliwataka wahusika waliozuiwa kuwa ni, Makatibu Wakuu wa Baraza, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Makatibu Wakuu, Maafisa katika wizara, Wakurugenzi wa Mashirika na maafisa wengine, Bodi za Wakurugenzi wa Mashirika.

Katika barua hiyo, haikuelezwa sababu za serikali ya Kenya kuweka marufuku hiyo kwa viongozi wake.

Zuio kama hilo la Kenya, limewahi kuwekwa nchini Tanzania ambapo Rais Dkt Magufuli mara tu baada ya kuingia madarakani Novemba 5, 2015 alipiga marufuku safari zote za nje, na kwamba anayetaka kusafiri alihitajika kibali cha rais.

Rais Magufuli aliyeingia madarakani na mpango wa kupunguza matumizi ya serikali alisema baadhi ya viongozi wamekuwa hawafanyi kazi badala yake wanasafiri kila mara, jambo ambalo hawezi kulivumilia chini ya utawala wake.

Shekhe Aliesemekana Atasoma Albadiri Ahojiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Muheza

$
0
0
Shekhe Hilaly ahojiwa na kamati ya ulinzi na usalama baada ya kusemekana atasoma Alhul badr kwa wale wote walioshirikia kumshambulia Mh Tundu Lissu.
Akihojiwa na Clouds Fm, Shekhe Hilaly amekana kuhusika na jambo hilo na kuthibitisha kuwa asubui ya leo aliitwa kwenye kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Muheza.

Jahazi Clouds Fm.

Jinsi ya Kutibu Ukosekanaji wa Nguvu za Kiume Kwa Vyakula Asili

$
0
0

Katika kujitibu tatizo hili jambo la kwanza ni kuelewa ni nini kimesababisha tatizo hilo kwa upande wako.

Njia 13 za kujitibu tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume:

1. Acha mawazo

Mawazo na mfadhaiko huondoa mtiririko mzuri wa damu kwenda kwenye uume na kusababisha nguvu kupungua nguvu za kiume na hata uume wenyewe.

Ikiwa unasumbuliwa na mfadhaiko au stress uangalifu mkubwa unahitajika kabla ya kuamua kutumia dawa yoyote. Katika hali ya mfadhaiko wa akili utokanao na hali ya kushuka kwa uchumi kwa mfano, wanandoa wanapaswa kuwa ni wenye umoja na kujaliana zaidi, shida ni pale kama mke akili yake ni ndogo kwani badala ya kufunga na kuomba kwa Mungu huenda akaenda kukutangaza kwa majirani!.



2. Jitibu magonjwa yafuatayo

Kama tatizo limesababishwa na magonjwa kama kisukari, vidonda vya tumbo, shinikizo la juu la damu au uzito kupita kiasi ni vema ukajitibu kwanza maradhi haya. Tatizo ni kuwa watu wameaminishwa kwamba maradhi haya hayana dawa jambo ambalo si kweli.

Kisukari, shinikizo la juu la damu, vidonda vya tumbo na hata uzito kupita kiasi ni magonjwa yanayotibika kabisa hasa kwa kutumia dawa mbadala na kufuata muongozo sahihi katika kula na kunywa kwa kipindi cha majuma kadhaa.

3. Acha vilevi

Kama tatizo linatokana na matumizi ya vilevi, hatua ya kwanza ni kuviacha kwanza hivyo vilevi. Ndiyo kuviacha kwanza, unatakiwa ujiulize mwenyewe kipi ni mhimu kwako ndoa yako au hivyo vilevi? Mtu anayejali vilevi kuliko hata afya yake hafai.

Kuna watu wanajidanganya kwamba ukitumia sijuwi kilevi fulani nguvu zinaongezeka, ni kweli zitaongezeka hapo mwanzoni mwa matumizi ya hicho kilevi lakini kadri siku zinavyoenda ndivyo utakavyoendelea kuwa mtegemezi wa hicho kilevi na itafika siku hata hicho kilevi hakitasaidia kitu na hapo ndipo hatari zaidi ya kutotibika tatizo lako itakapojitokeza.

4. Fanya mazoezi ya viungo

Zingatia sana umhimu wa mazoezi ya viungo. Bila kujishughulisha na mazoezi ya viungo kila siku itakuwa ni vigumu sana kwako kupona tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Kutengeneza mishipa na kupunguza uzito isiwe ndiyo sababu pekee ya kwenda gym. Kama unahitaji nguvu za kiume na uume wenye afya, unahitaji kujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara ili kusafisha mishipa ya damu na hivyo kuongeza kiasi cha utiririkaji wa damu kwenda kwenye uume.

Kama uzito wako upo juu sana na ni mnene fanya mazoezi ya kukimbia (jogging) kila siku kwa mwezi mmoja mpaka miwili. Kama uzito wako upo sahihi tu kwa mjibu wa urefu wako fanya sana mazoezi ya kuchuchumaa na kusimama. Una chuchumaa na kusimama mara 25 mpaka 30, unaweza kupumzika dakika mbili unaendelea tena kuchuchumaa na kusimama hivyo hivyo unapumzika dakika 2 mpaka mizunguko (rounds) mitano kila siku.

5. Tumia kitunguu swaumu

Chukuwa punje 6  za kitunguu swaumu, menya na uzikate vipande vidogo vidogo kisha meza na maji vikombe 2 kutwa mara 1 kwa mwezi mmoja.

Sifa kuu zinazokifanya kitunguu swaumu kuwa na uwezo na faida nyingi mwilini ni kule kuwa kwake na viasili kadhaa (ingredients) ambavyo vinafanya kazi tofauti tofauti. Uwezo wake wa kiutendaji unatokana na sifa zifuatazo:

Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu (vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu.
Husaidia uthibiti wa kiwango cha sukari mwilini kwa kushusha kiwango cha kemikali ya homocystine na hivyo kupunguza madhara ya kisukari.
Ukivikata vipande vidogo vidogo hivi (chop), vitunguu swaumu hutoa kemikali iitwayo kwa kitaalamu kama ‘Allicin’ ambayo ni dawa dhidi ya bakteria, na ‘Phytoncide’ ambayo huua fangasi mbalimbali mwilini.
Unafahamu kuwa kitunguu swaumu ni dawa ya zaidi ya magonjwa 30 mwilini? Soma magonjwa hayo yanayotibika kwa kutumia kitunguu swaumu kwa kubonyeza hapa => Kitunguu Swaumu Hutibu Magonjwa 30.

6. Kula tikiti maji


Tunda hili lina faida nyingi pamoja na kuwa ni chanzo kikuu cha Protini, Mafuta, Nyuzinyuzi, Wanga,Calcium, Phosphorus, Chuma,Vitamin A,B6,C. Potasium, Magnesium, Carotene, anthocyanins na Virutubisho vingine vingi.

Tunda linasaidia kuwa na uwezo mkubwa wa kuimalika kwa misuli na mfumo wa fahamu kufanya kazi zake vizuri na kuondoa katika hatari ya kupata shinikizo la juu la damu.

Faida nyingine 12 za tikiti maji kiafya ukiacha hii ya nguvu za kiume

• Asilimia 92 yake ni maji
• Vitamini A ndani yake huboresha afya ya macho
• Vitamini C ndani yake huimarisha kinga ya mwili,
• Huponya majeraha,
• Hukinga uharibifu wa seli
• Huboresha afya ya meno na fizi
• Vitamini B6 husaidia ubongo kufanya kazi vema
• Hubadilisha protin kuwa nishati
• Chanzo cha madini ya potasiamu
• Husaidia kushusha na kuponya shinikizo la damu
• Hurahisisha mtiririko wa damu mwilini
• Huondoa sumu mwilini

Kula tikiti maji kila siku huku ukitafuna na zile mbegu zake, fanya mara hivi mara kwa mara.

7. Kula ugali wa dona

Kula ugali wa dona kila siku. Ni mhimu kuachana na mazoea ya kula ugali wa sembe. Ugali wa dona una virutubisho vingi na mhimu kwa ajili ya afya ya mwanaume. Kama ugali wa dona unakukera jaribu kufanya hivi, chukuwa mahindi kilo 10 ongeza ngano kilo 3 na usage kwa pamoja, ugali wake huwa ni mlaini, mzuri na mtamu na unaweza kula na mboga yoyote tofauti na lile dona la mahindi peke yake. Fanya hivi katika familia yako kwa maisha yako yote.

8. Tumia chumvi ya mawe


Chumvi ya mawe ya baharini ile ambayo haijasafishwa au haijapita kiwandani ina mchango mkubwa sana katika kutibu tatizo hili. Tumia chumvi hii kwenye vyakula vyako kila siku.

Kama unataka kujifunza mambo mengi zaidi kuhusu umhimu wa chumvi mwilini, bonyeza hapa => Ukweli kuhusu Chumvi na Maajabu yake.

9. Kunywa maji mengi kila siku


Maji ni Uhai
Kunywa maji ya kutosha kila siku bila kusubiri kiu. Kila mtu anahitaji glasi 8 mpaka 10 za maji kila siku. Maji ni mhimu katika kuongeza damu, kusafisha mwili na kuondoa sumu mwilini.

Soma maajabu mengine ya maji kiafya kwa kubonyeza hapa => Jitibu kwa kutumia maji mp3.

10. Tafuna mbegu za maboga



Maajabu mengine ya mbegu za maboga ambayo ulikuwa huyajuwi bado. Utaniuliza kivipi zinaondoa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume? Kwanza kabisa zinaondoa msongo wa mawazo/stress kitu ambacho ni namba 1 katika kusababisha upungufu wa nguvu za kiume, lakini pia zinashusha lehemu (cholesterol), zinatibu kisukari, zinatibu tezi dume (matatizo kama ya ngiri nk), zina protini nyingi ya kutosha na yenye ubora na mbaya kuliko zote ni kuwa zina madini ya ZINKI madini mhimu kuliko kitu kingine chochote kwenye upande wa nguvu za kiume na kinga ya mwili. Bado huelewi? Zina madini ya chuma pia

Uzuri ni kuwa mbegu hizi hazina uchungu wowote, ni tamu kuzitafuna wakati wowote na mahali popote hata ofisini unaweza kuwa nazo pembeni unatafuna huku unaendelea na kazi zako. Sambamba na hilo kama tulivyoona pale juu kwamba zinaongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha kwa upande wa wanaume zinaongeza pia uwingi wa mbegu za kiume (sperm count) ukitafuna mbegu za maboga siku mbili tu utaona ukipiga bao linatoka la kutosha na zito kweli kweli basi ujuwe ni mbegu za maboga.

NAMNA NZURI YA KUTUMIA MBEGU ZA MABOGA KAMA DAWA:

Unaweza kula zikiwa kavu na ndiyo utapata faida nyingi zaidi ingawa mimi napenda kuzikaanga kidogo kama dakika 5 hivi na huwa nazichanganya na maji ya chumvi ya mawe ya baharini kidogo kwa mbali ili kupata radha.

Unahitaji ujazo wa kiganja kimoja cha mkono wako cha mbegu za maboga, ujazo wa kama nusu kikombe cha chai hivi kila siku. Unatafuna na ganda lake hasa kama zimekaangwa tayari

Kwa muda gani? Kwa wiki 3 mpaka 4 kwa ugonjwa wowote kati ya haya niliyoeleza. Kumbuka pia unaweza kutumia mbegu hizi hata kama huumwi chochote!

11. Tumia asali yenye mdalasini


Chukuwa lita moja ya asali safi ya asili ambayo haijachakachuliwa, ongeza vijiko vikubwa 8 vya mdalasini ya unga changanya vizuri pamoja. Acha ndani ya bakuli kubwa ili iwe rahisi kuikoroga vizuri kila unapoitumia. Lamba vijiko vikubwa vitatu kila unapoenda kulala. Fanya hivi kwa mwezi mmoja.

Hata baada ya mwezi mmoja kuisha bado nakushauri uendelee kuitumia asali hivi maisha yako yote au hakikisha haipiti siku bila kunywa au kula chakula chenye asali yenye mdalasini ndani yake. Unaweza kuitumia kila siku kwenye mkate kama mdabala wa siagi au blueband au ukaitumia kwenye juisi na kwenye chai kama mbadala wa sukari. Au unaweza kuweka vijiko vikubwa vitatu ndani ya glasi moja ya maji na unywe yote kutwa mara 2 amabapo husaidia pia kutibu uchovu mwilini.

Soma kazi nyingine 27 za kushangaza za asali yenye mdalasini mwilini kwa kubonyeza hapa => Asali na Mdalasini.

12. Kunywa chai ya tangawizi


Tangawizi ni chakula ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini, na tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume. Inaweza kuliwa mbichi, au kupikwa au kuanikwa na kuwa kama unga.

Ulaji wa tangawizi mbichi nusu saa kabla ya tendo la ndoa husaidia katika kuongeza hamu na nguvu ya tendo la ndoa. Unaweza ukanywa chai ya tangawizi tu nusu saa kabla ya kuanza tendo au unaweza ukatafuna kipande cha tangawizi mbichi kwa ukubwa wa dole gumba la mtu mzima nusu saa kabla ya tendo.

Kunywa chai ya tangawizi mbichi kila siku, katika chai hiyo unayopika ndani yake weka tu maji na Tangawizi mbichi uliyosagia ndani yake (usiongeze majani ya chai humo), kumbuka tangawizi inaoshwa tu na maji na uisagie ndani ya sufuria pamoja na ganda lake la nje. Sasa badala ya kutumia sukari wewe tumia asali kwenye hii chai yako ya tangawizi na ukiitumia hivi kila siku hutachelewa kuona faida zake. Tangawizi peke yake ni dawa ya zaidi ya magonjwa 72 mwilini!

13. Tumia unga au juisi ya msamitu


Unga wa msamitu
Unga au juisi ya msamitu (mtishamba wa porini) ni mzuri sana katika kutibu tatizo la nguvu za kiume na pia unasaidia sana kwa wanaume wenye tatizo la nguvu za kiume hasa lililosababishwa na kujichua au kupiga punyeto kwa muda mrefu kwani unaimarisha sana mishipa ya uume. Pia unaweza kuutumia hata kama unasumbuliwa na tatizo la kisukari. Msamitu unao uwezo mkubwa katika kuongeza hamu ya tendo la ndoa hata kwa kina mama pia.

Msamitu pia unatibu magonjwa yafuatayo bila shida yoyote; Pumu, Chango la uzazi, Kupooza mwili, Unaondoa kabisa gesi tumboni na Kuongeza nuru ya macho kuona.

Msamitu unao uwezo pia wa kuongeza ukubwa wa uume wako. Labda utauliza kwa namna gani?, kwa sababu moja ya kazi zake mwilini ni kuponya mwili uliokuwa umepooza, mwili unapokuwa umepooza ina maana hata damu yako pia inakuwa haitiririki vizuri kama inavyotakiwa na tuliona hapo juu kwenye somo hili umhimu wa mzunguko wa damu ulio bora katika nguzu za kiume.

Kwa kuwa mwili ulikuwa umepooza, Msamitu unapokuja kukutibu unakufanya kuwa mtu uliyechangamka na damu yako itaanza kuwa inatiririka kwa mtiririko mzuri zaidi na kama matokeo yake utaanza kuona hata ukubwa wa mheshimiwa unaanza kuongezeka kidogo kidogo. Na hii ni hasa kwa wale ambao walizaliwa na uume wa kawaida lakini sababu ya punyeto, lishe duni au stress walijikuta maumbile yao yanaanza kusinyaa au kupungua badala ya kuongezeka.

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai Amewatadharisha Wabunge Kuwa Makini na Usalama wao

$
0
0
SPIKA wa Bunge, Job Ndugai amewatadharisha wabunge kuwa makini na usalama wao mahali popote wanapokwenda kufuatia matukio mengi ya uhalifu nchini. Akizungumza muda mfupi leo Ijumaa, Septemba 15, kabla ya kuahirishwa kwa Bunge, Ndugai aliwataka wabunge kutokaa sana katika mabaa.

Yaani tuchukue hatua tu katika maisha yetu, kama mnavyosikia matukio ni mengi katika nchi yetu. Ni vizuri usalama unaanza na wewe mwenyewe kwanza,” amesema.

Amesema vyombo vya usalama vinavyowalinda vinakuwa vinaongezea kidogo na kuwataka kutazama nyendo zao za namna ambavyo wanaishi.
Spika Ndugai: Wabunge Tuchukue Hatua za Usalama Wetu

Kwa wale tuliozoea tunarudi nyumbani saa saba usiku, basi tuanze kurudi mapema kidogo. Lakini pia tuangalie usalama wa familia zetu na tuwaambie wapigakura, naona siku hizi watoto wanapotea, watoto wanauawa,” amesema.

Amewataka wabunge kuwapelekea ujumbe huo wananchi kuwa wawe makini na watoto wao wakati wa kwenda shule na maeneo mengine kwa kuhakikisha wanajua mtu anayewapeleka shule na kuwachukua.

Aliwataka wabunge kuendelea kumuombea Tundu Lissu na wale watakaopata nafasi ya kwenda kumuona jijini Nairobi wampelekee ujumbe.
Amesema pia wabunge wawaombee wenzao ambao wamekwenda kumuuguza mbunge huyo. Ushauri huo umekuja siku chache baada ya Lissu kujeruhiwa kwa kupigwa risasi nyumbani kwake Area D mjini Dodoma.

Kamati ya Bunge Yashindwa Kutoa Ripoti ya Tundu Lissu

$
0
0
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge imeshindwa kuwasilisha ripoti juu ya shambulio la risasi la Mbunge wa Sindida Mashariki Tundu Lissu, ambayo ilitakiwa kuwasilishwa leo kabla ya Bunge halijaghailishwa.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Adadi Mohamed Rajabu ambaye ni Mbunge wa Muheza kwa kudai muda waliopewa kukamilisha ripoti hiyo ni mdogo hivyo hawakuwahi kukamilisha.

Kamati hiyo ya Ulinzi na Usalama ya Bunge inatarajiwa kukutana kuanzia kesho ili kujadili na kuiwasilisha ripoti hiyo katika bunge  lijalo litakaloanza mwezi Novemba 2017.

Ikumbukwe kwamba baada ya kutokea tukio la kushambuliwa kwa risasi Tundu Lissu, Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe aliwasilisha hoja ya kulitaka bunge liunde kamati maalum ya kuchunguza tukio hilo ili iweze kubainika aliyefanya tukio hilo, na Spika Mhe. Job Ndugai alikubali na kupitisha hoja hiyo.

Albadiri iliyosomwa Imeanza Kufanya Kazi Yake

$
0
0
 Watu Bwana , Huku Mitandaoni pamechafuka zikuonyesha Baadhi ya Picha Baadhi nimekuwekea hapa zikionyesha eti ndo baada ya Albadiri kusomwa

Zari Naye Ajibu Mapigo..Aposti Picha Akiwa Kwenye Kidate (Outing) na Mwanaume Mwingine

$
0
0
 Zari Ameamua Kufanya ile inayoitwa Mwaga ugali na mie nimwage Mboga, Baada ya tetesi kuwa Diamond alikuwa Zanzibar na Mrembo Dillish.....Leo amekuwa bize kwenye mtandao wake wa Instagram akionyesha kuwa nae ana mtu wake mwingine zaidi ya Diamond ambae wameenda nae Kidate, Mchana alipost picha hiyo hapo chini yenye Caption "Lunch Date" na jioni hii ndio akamalizea kabisa na Picha inayoonyesha Class mbili na kinywaji ikiwa na maana kuwa yupo somewhere na someone special
Toa Maoni yako
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images