Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Ndanda Yajipanga Kuzoa Poindi 6 Kwenye Michezo Yake Miwili

$
0
0
Ndanda Yajipanga Kuzoa Poindi 6 Kwenye  Michezo Yake Miwili
Ndanda yapania Ndanda FC imetamba kuondoka na alama 6 kwenye michezo yake miwili ya ligi kuu Tanzania bara mkoani Mbeya ambapo tayari imeshachukua alama 3 dhidi ya wenyeji Mbeya City wiki iliyopita na kesho inakutana na Prisons.

Msemaji wa Ndanda FC, Idris Bandali amesema kuwa timu yao imejiandaa vyema kwa wiki nzima ikiwa Mbeya na wanasubiri kuchukua alama tatu mbele ya wenyeji Prisons kwenye mchezo wa raundi ya tatu ligi kuu Tanzania Bara.
"Timu imejiandaa vyema, wiki yote hii tumekuwa hapa Mbeya wachezaji wamezoea hali ya hewa na tunategemea tutacheza vizuri na kuondoka na alama 3 ili kutimiza sita katika mechi zetu za Mbeya", amesema Bandali.

Bandalli pia ameeleza kuwa ripoti ya mwalimu baada ya mazoezi ya leo asubuhi inaonesha hakuna majeruhi yoyote kwenye timu hivyo wachezaji wote wapo tayarI kwa mchezo wa kesho. Ndanda ina alama 3 ikiwa imeshinda mechi moja na kupoteza moja dhidi ya Azam FC.



Kwa Hali Ilivyo Sasa Tanzania ni Wazi Amani Haipo Kama Zamani- Jay Dee

$
0
0
Kwa Hali Ilivyo Sasa Tanzania ni Wazi Amani Haipo Kama Zamani- Jay Dee
Msanii mkongwe wa muziki wa bongo fleva Lady Jaydee amefunguka na kusema kwa hali ilivyo sasa Tanzania ni wazi kuwa amani haipo kama alivyokuwa kipindi cha nyuma na kudai hali hiyo inaleta hofu miongoni mwa wananchi.

Lady Jaydee alisema hayo kwenye kipindi cha Planet bongo na kusema kitendo cha Mbunge Tundu Lissu pamoja na Meja Jenerali mstaafu wa JWTZ, Vincent Mritaba kupigwa risasi na watu wasiojulikana ni wazi kuwa amani ya nchi haipo.

"Ni kweli Tanzania hakuna amani kwa sababu kitendo cha mtu kupigwa risasi hadharani inatishia amani ukizingatia kuna wasanii wengine walikuwa wanatekwa unaogopa, sehemu yenye amani vitu kama hivyo haviwezi kutokea, na kitendo cha Meja mstaafu wa JWTZ kupigwa naye risasi inaongeza kabisaa Tanzani kuwa amani haipo naweza kuwa sina la kusema ila nikaishia kusikitika tu" alisema Lady Jaydee
Aidha Lady Jaydee anasema matukio haya yanaotoa picha mbaya kuwa kama nchi tunakokwenda si sehemu nzuri
Mbali na hilo Lady Jaydee kwa sasa ameachia video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la 'I miss you' uliotengenezwa na mtayarishaji Man Water kutoka Combination Soound.

Balozi Atamani Kumkutanisha Magufuli na Trump

$
0
0
Balozi  Atamani Kumkutanisha Magufuli na Trump
Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini, Dk Inmi Patterson amesema anatamani kumpeleka Rais John Magufuli katika ziara ya wiki tano nchini mwake.

Kaimu Balozi huyo ameyasema hayo hivi karibuni nyumbani kwake jijini Dar es Salaam katika hafla ya kumkaribisha ofisa mpya wa masuala ya kijamii ubalozini, Brinille Ellis.

“Mwaka 1960 mwalimu Julius Nyerere alifanya ziara ya wiki tano nchini Marekani katika mpango wa kubadilisha uzoefu wa viongozi… wiki tano ni kipindi kirefu, siyo? Kwa hiyo aliweza kutembelea majiji kadhaa,” alisema na kuongeza:

“Natamani ningempeleka Rais (John) Magufuli pia katika ziara ya wiki tano Marekani ili na yeye atembelee maeneo kadhaa,” alisema kaimu balozi huyo na kuibua kicheko kutoka kwa watu waliohudhuria hafla hiyo.

Dk Patterson ameyasema hayo wakati Rais Magufuli akiwa amemaliza zaidi ya miaka miwili madarakani bila ya kufanya ziara nje ya Afrika. Katika hotuba zake kadhaa, Rais Magufuli amesisitiza kuwa hapendi kusafiri nje ya nchi mara kwa mara kwa sababu bado kuna kazi kubwa anayopaswa kuifanya nyumbani.

Tangu achaguliwe Oktoba mwaka 2015, Rais Magufuli ametembelea nchi za Afrika Mashariki na nje ya hapo amewahi kutembnelea Ethiopia tu. Amekuwa akihimiza mabalozi wa Tanzania nje kuzifanya kazi ambazo viongozi wakuu wa nchi wanazifanya wanapofanya ziara katika nchi hizo.

Hata hivyo wakati Rais Magufuli akijizuia kusafiri nje ya nchi, juhudi zake zimewezesha marais takribani 15 kuitembelea Tanzania na kuleta manufaa makubwa kwa nchi.

Wakati huo huo, kaimu Balozi Patterson alisema ili kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Marekani ni vema uhuasiano huo ukaanza katika ngazi ya watu binafsi.

Akimnukuu Efward Murrow, mwandishi mkogwe wa radio nchini Marekani, Dk Patterdson amesisitiza kuwa mahusiano ya watu binafsi ndio msingi wa kujenga na kuimarisha uhusiano baina ya taasisi au nchi.



   

Msekwa Atoa Neno Utendaji wa Ndugai Namna ya Uendeshwaji wa Bunge

$
0
0
Msekwa Atoa Neno Utendaji wa Ndugai Namna ya Uendeshwaji wa Bunge
Spika mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa ametia neno akigusia utendaji wa Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyeingia katika msuguano na baadhi ya wabunge wa upinzani.

Ndugai ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kongwa mkoani Dodoma hakuwa na wakati mzuri katika Bunge lililomalizika jana kutokana na kupishana kauli na wabunge, Zitto Kabwe, Said Kubenea, Godbless Lema na Peter Msigwa.

Alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu Spika Ndugai alivyojikuta akitumbukia katika mvutano huo, Msekwa alisema: “tulifundishwa na Mzee Mwinyi(Ali Hassan) kila kitabu na zama zake.”

Amesema ingawa wakati wa uongozi wake hakukuwa na malumbano ya namna hiyo lakini hilo halimanishi kuwa Spika wa sasa anaendesha mambo kinyume na Kanuni za Bunge.

Amesema anachokifanya Spika Ndugai kinatafsiri aina ya uongozi alionao ambao siyo jambo la kushangaza kuona ukitofautiana na mfumo aliokuwa akitumia wakati akiwa katika kiti hicho.

“Hii ni staili yake ya uongozi na ndiyo mabadiliko ya uongozi wenyewe,” amesema Msekwa wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu na kurudia tena maneno hayo akisema “ ni staili yake na kila kiongozi anakuwa na mfumo wake wa kuongoza mambo.”

Lakini amesema kwa kufanya hivyo hajakosea lolote kwa vile yale aliyokuwa akiyazungumza na kuyatolea maamuzi yako ndani ya Kanuni za Bunge.

“Spika ametumia mamlaka yake sioni kama kuna ubaya wowote,” amesema Msekwa ambaye amewahi pia kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM.

Amesema hata yeye alipochukua nafasi hiyo kulikuwa na maspika wengine waliomtangulia waliokuwa na mfumo wao wa kuendesha Bunge na kisha naye akawa na wake pia.

“Baada ya mimi walikuja wengine ambao nao pia walikuwa na staili yao ya uongozi,” amesema.

Hatua ya Ndugai kudai kuwa anaweza kumzuia Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe asizungumze bungeni kwa muda wote uliobaki na hana cha kumfanya imezusha mjadala mkubwa nchini huku baadhi ya wasomi wameikosoa kauli hiyo wakisema hana mamlaka hayo kisheria.

Spika Ndugai alitoa kauli hiyo hivi karibuni baada ya Zitto kunukuliwa katika akaunti yake ya Twitter akimkosoa kiutendaji.

Mzozo kati ya Spika Ndugai na Zitto ulianza baada ya kiongozi huyo wa ACT – Wazalendo kusema kwamba Bunge limewekwa mfukoni na mhimili fulani wakati alipotoa maoni kuhusu ripoti mbili za kamati ya Bunge za almasi na Tanzanite.

Kutokana na kauli hizo, Spika Ndugai aliagiza mbunge huyo ahojiwe na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge huku akimshtaki kwa wapigakura wake akisema licha ya kwamba mbunge wao yupo nchini hajafika bungeni kuwawakilisha na yeye (Spika), hana taarifa.

 Wakizungumzia matamshi hayo baadhi ya wasomi walisema kauli kama hiyo haikupaswa kutolewa na Spika.

Baadhi ya wanasheria walisema kauli ya Spika Ndugai imelenga kuwanyamazisha wabunge wasiwe huru kutoa maoni yao kwa mujibu wa Katiba.



Korea Kaskazini Imetangaza Lengo la Kuwa na Jeshi Lake Kuwa Sawa na la Marekani

$
0
0
Korea Kaskazini  Imetangaza Lengo la Kuwa na Jeshi Lake Kuwa Sawa na la Marekani
Korea Kaskazini imetangaza kuwa lengo lake kuu kijeshi kwa sasa ni kuhakikisha inakuwa na uwezo sawa na Marekani.

Shirika la habari la Korea Kaskazini lilitoa taarifa hiyo baada ya kombora la majaribio la mwisho kufanywa, ikisema kuwa kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong-Un, amesema kuwa hataki kusikia Marekani ikisema itakabiliana na Korea Kaskazini kijeshi.

KIongozi wa taifa hilo Kim Jong un ameapa kuhakikisha kuwa taifa hilo linaafikia mpango wake wa kinyuklia kulingana na vyombo vya habari vya taifa hilo.

Lengo lake ni kuhakikisha jeshi la tifa hilo lina uwezo sawa na lile la Marekani kulingana na chom,bo cha habari cha KCNA kilichomnukuu kiongozi huyo.


Matamshi ya bwana Kim yanajiri baada ya taifa hilo kufanyia majaribio kombora lake kupitia anga ya Japan, likitajwa kuwa kombora lililosafiri kwa umabli mkubwa zaidi

.Hatua hiyo imesbabishwa mgawanyiko miongoni mwa mataifa ambayo yaliunga nyuma ya uMoja wa Matifa dhidi ya Korea kaskazini siku chache zilizopita.

Lazima tuyaonyeshe mataifa yaneye uwezo mkubwa vile taifa letu litakavyokamilisha mpango wake wa kinyuklia licha ya vikwazo visivyoisha, bwana Kim alinukuliwa na chamobo cha habari cha KCNA

Alisema kuwa lengo la Korea Kaskazini ni kuwa na jeshi lenye uwezo sawa na lile la Marekani ili kuwazuia watawala wa marekani kutotaja swala la kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Korea Kaskzini

Katika mkutano wa dharura, baraza la Usalama la umoja wa Mataifa, lilishutumu Korea Kaskazini kwa kufyatua Kombora juu ya Japan, lakini likasisitiza kuwa hakutakuwepo na vikwazo zaidi dhidi ya taifa hilo.

Awali Marekani ilionya kuwa Korea Kaskazini itashambuliwa kijeshi iwapo vikwazo ilivyowekewa havitatekeleza chochote.
Lakini Uchina kwa upande wake ilihimiza Marekani ikome kutoa vitisho na badala yake ianze kufanya mashauriano.

Mimi ni Binadamu Mtu Anaponinyanyasa na Kunidhalilisha Natumia Mmlaka Niliyonayo- Ndugai

$
0
0
Mimi ni Binadamu Mtu Anaponinyanyasa na Kunidhalilisha Natumia Mmlaka Niliyonayo- Ndugai
Spika wa Bunge, Job Ndugai amefunguka na kusema kuwa yeye hana tatizo lolote na Mbunge Zitto Kabwe, Saed Kubenea na Godless Lema ila amedai yeye ni binadamu hivyo mtu anapomnyanyasa na kumdhalilisha hutumia mamlaka aliyonayo kufanya maamuzi.

Ndugai amesema kuwa yeye kama kiongozi wa Bunge anamamlaka na madaraka makubwa kuliko hata yaliyoandikwa na kusisitiza kuwa anao uwezo wa kumsimamisha Mbunge asiongee chochote bungeni mbaka muda wa mbunge huyo utakapokwisha.

"Siyo kila kitu huandikwa katika mahusiano ya kikazi lakini kiongozi wako wa kazi ana mamlaka na madaraka makubwa kuliko hata yaliyoandikwa si kila jambo lazima liwe ni kanuni, narudi tena nimesikia watu wakibisha bisha ninao uwezo kama spika, zipo kanuni zinamruhusu Spika wa Bunge kwa kadri anavyoona inafaa kwa busara yake namna gani aongoze bunge, huwezi kuwa unatukana bunge unamtukana huyo spika halafu huyo huyo Spika anakupa nafasi uzungumze kwa sababu yeye ni malaika? Mimi ni binadamu mwenye damu na nyama kama wengine" alisema Ndugai

Spika wa Bunge aliendelea kutoa ufafanuzi juu ya baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kupotosha umma au kumzungumza mambo ya bunge kwa njia isiyo na staa kupitia mitandao hiyo ya kijamii na kumdhalilisha yeye na kusema yeye pia atatumia mamlaka yake kuona anafanya nini juu ya wabunge hao.

"Kwa jinsi unavyoninyanyasa na kunidhalilisha mbele ya watu na mimi nitatumia madaraka yangu na mamlaka niliyonayo niliyopewa na nchi na Mungu kuona nini nifanye katika mamlaka niliyonayo" alisisitiza Ndugai

Spika wa Bunge Job Ndugai alisema kuwa ana uwezo wa kumzuia mbunge Zitto Kabwe asizungumze chochote ndani ya bunge kwa kipindi chote cha ubunge

Mwanamke Mkongwe Zaidi Duniani Afariki Dunia

$
0
0
Mwanamke Mkongwe Zaidi Duniani Afariki Dunia
Mwanamke mmoja wa Jamaica anayedhaniwa kuwa mtu mkongwe zaidi duniani Violet Mos Brown amefariki akiwa na umri wa miaka 117.

Waziri Mkuu wa Jamaica alitangaza kufariki kwa mwanamke huyo kupitia mtandao wa Twitter.
Vyombo vya habari vya nchini vilisema alifariki kwa utulivu katika hospitali moja katika mji wa Montego Bay.

Violet Moss Brown, aliyekuwa mtu mkongwe zaidi mapema mwaka huu, alizaliwa mwaka 1900.
Alisema kuwa aliweza kuishi muda mrefu na kwamba aliweza kula karibu kila kitu isipokuwa ngurue na kuku.
Alisema pia hakunywa pombe kali.

Kamusoko Aondolewa Kwenye Kikosi cha Yanga Kitakachooneshana Ubabe na Majimaji Leo

$
0
0
Kamusoko Aondolewa Kwenye Kikosi cha Yanga Kitakachooneshana Ubabe na Majimaji Leo
Nahodha wa Yanga, Thaban Kamusoko ameondolewa kwenye kikosi cha Yanga kitakachocheza na Majimaji leo huku Mzambia, Obrey Chirwa akianza mechi yake ya kwanza msimu huu.

Kamusoko aliumia kwenye mchezo dhidi ya Njombe Mji lakini alifanya mazoezi hadi Jana Ijumaa lakini Daktari wa Yanga, Edward Bavu ameona ni vyema akapumzishwa.

Kwa upande wa Chirwa, ameingia kwenye kikosi cha kwanza leo baada ya kupata dakika chache kwenye mchezo uliopita.

Katika hatua nyingine, Geofrey Mwashiuya na Raphael Daudi wameingia kwenye kikosi cha kwanza kwa mara ya kwanza msimu huu.

Daudi aliingia akitokea benchi katika mechi mbili za mwanzo lakini leo ameanza badala ya Kamusoko.

Yanga itavaana na Majimaji leo saa 10 jioni na tayari mashabiki wameanza kuingia uwanjani.


Jukata Yataka Mabadiriko ya Katiba Mpya Yafanyike Kabla ya Kuingia Kwenye Uchaguzi Mkuu Ujao

$
0
0
Jukata Yataka Mabadiriko ya Katiba Mpya Yafanyike Kabla ya Kuingia Kwenye Uchaguzi Mkuu Ujao
Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) limeitaka Serikali ifanye mabadiliko ya msingi katika Katiba kabla ya kuingia kwenye maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao.

Jukata imesema mabadiliko hayo ya msingi  yafanyike iwapo  hakuna uwezekano wa kukamilisha mchakato wa Katiba Mpya kabla ya uchaguzi wa mwaka 2020, kama ambavyo dalili zinazidi kuonyesha.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Jukata, Hebron Mwakagenda amesema kwa hali ilivyo dalili ya kupatikana Katiba Mpya hakuna, kutokana na kutotengwa bajeti kwa ajili ya mchakato huo.

Amesema ipo haja ya kurekebisha angalau mambo ya msingi ambayo yamelalamikiwa na wananchi kwa kipindi kirefu.

Amesema kutokana na hilo yafanyike mabadiliko muhimu katika Katiba iliyopo ikiwamo kuwapo na uhuru kamili ya tume ya uchaguzi Zanzibar.

Aliyataja mabadiliko hayo ni kuwa na uhuru kamili wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Amesema mabadiliko hayo pia yaangalie kuwapo kwa fursa ya mgombea huru katika uchaguzi, ikiendana na kutokuwa na masharti makali yanayokatisha tamaa.

Amesema pia Katiba ibadilishwe na iwe na nafasi ya kuhoji matokeo ya uchaguzi wa Rais mahakamani na pia kuwezesha vyama vya siasa kuungana kikatiba na kisheria kwa lengo la kusimamisha mgombea mmoja.

“Hili siyo la vyama vya upinzani pekee, hata chama tawala CCM itafikia mahali kitahitaji kuungana na vyama vingine kusimamisha mgombea mmoja."

“Siasa zinabadilika sana na chenyewe ni kama kipo ukingoni, hivyo hili liangaliwe na lipewe nafasi kwenye Katiba,” amesema Mwakagenda.

Aliyataja mabadiliko mengine ni kurejesha mfumo wa ushindi katika uchaguzi wa Rais kwa kigezo cha kupatikana kwa kura zisizopungua 50 jumlisha moja

Watu 20 Wanashikiliwa na Polisi kwa Kukutwa Wakifundishana Kufanya Mapenzi ya Jinsia Moja

$
0
0
Watu 20 Wanashikiliwa na Polisi kwa Kukutwa Wakifundishana Kufanya Mapenzi ya Jinsia Moja
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi-Unguja linawashikilia watu 20 kwa tuhuma za kukutwa wakifundishana kufanya mapenzi ya jinsia moja.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi Mkoa wa Mjini Magharib Hassan Nassir amesema watu hao wamekamatwa wakati wakipatiwa mafunzo ya namna ya kuzitambua haki zao yaliyokuwa yakitolewa na taasisi iliyotambulika kwa jina la Bridge Initiative.

Hata hivyo hatua hiyo imekuja mwezi mmoja baada ya kauli ya mkuu wa mkoa huo ambaye pia ndio mwenyekiti wa ulinzi na usalama RC Ayoub Mahamoud kutamka kukomesha vitendo hivyo mara moja ambavyo vinaiharibu sifa ya Mkoa huo.

Mabli na hilo mkuu huyo wa Mkoa akiliongoza Jeshi la Polisi tayari yuko katika operesheni ya kuzidhibiti biashara ya Dawa za kulevya, ambapo zaidi ya Vijana 50 mkoani humo walikubali kuachana na matumizi ya dawa hizo.

LWANDAMINA:Mashabiki wa Yanga Jitokezeni kwa Wingi Uwanjani Kuupokea Ushindi Dhidi ya Majimaji

$
0
0
LWANDAMINA:Mashabiki wa Yanga Jitokezeni kwa Wingi Uwanjani Kuupokea Ushindi Dhidi ya Majimaji
Kocha wa Yanga, George Lwandamina amewaambia mashabiki wa Yanga wajitokeze kwa wingi uwanjani kwani nafasi ya kikosi chake kushinda dhidi ya Majimaji ni kubwa.

Lwandamina amesema kikosi chake kiko imara kuwakabili Majimaji licha ya kwamba uwanja siyo mzuri sana.

"Ni mechi ngumu lakini tuna uwezo wa kushinda. Tutacheza soka la kupambana na kujituma zaidi," alisema Lwandamina.

"Hatufahamu sana wao wamejipanga vipi lakini muhimu kwetu ni kuwa na timu nzuri ya ushindani," alisema kocha huyo.

 

LINAH: Sikua Nimejipanga Kupata Mtoto Kama Kipindi Nilichokua Ninauhitaji Nikawa Najaribu Haiingii

$
0
0
LINAH: Sikua Nimejipanga Kupata Mtoto Kama Kipindi Nilichokua Ninauhitaji Nikawa Najaribu Haiingii
Msanii wa bongo fleva, Linah Sanga amefunguka na kudai hakuwa amejipanga kwa kipindi hiki kuwa na mtoto ila anamuomba Mungu isiwe kigezo cha yeye kupotea katika muziki ili aje kuwa mfano kwa wasanii wenzake wa kike wanaogopa kubebea ujauzito.

Linah amebainisha hayo kupitia kipindi cha FRIDAY NIGHT LIVE 'FNL' kutoka EATV baada ya kuwepo imani kwa baadhi ya watu wakidai msanii akioa, akiolewa hata akijifungua na mtoto mara nyingi hawezi kuendelea kufanya vizuri katika kazi zake kwa kuwa majukumu ya ulezi yanaongezeka na kupelekea kupotea katika 'industrial' ya muziki.
"Nina muomba Mungu usiku na mchana nisije kupotea katika 'game' kwa sababu ya uzazi, ili iwe mfano hata kwa wengine ambao watakuja nyuma yangu, labda wanaogopa kuzaa kwa kufikiri watapotea. Ila mimi nafikiri ni jinsi mtu mwenyewe anavyoishi na mashabiki zake", amesema Linah.
Pamoja na hayo, Linah ameendelea kwa kusema "Sikuwa nimejipanga kupata mtoto katika kipindi hiki ila nilikuwa na-wish nipate ujauzito nizae lakini sikufahamu ni lini itanitokea hivyo. 'So' kipindi kile nilichokuwa na-wish nikawa kila nikijaribu haingii, nikajisahau na kujikuta imekuja hata sikutarajia, lakini kwa kuwa nilikuwa nina uhitaji nikasema hakuna neno. Japo nilishauriwa vitu vingi sana mwanzoni lakini nikasema hapana kwa kuwa nimetaka kuzaa acha nifanye hivyo", amesisitiza Linah.
Kwa upande mwingine, Linah amesema kwa anajipa mapumziko katika kufanya kazi zake na kuwataka mashabiki zake wamvumilie mpaka mwakani (2018) katika miezi ya mwanzoni ndipo atakapoachia kazi yake mpya.

Wananchi Wa Kilimanjaro Wahaha na Bomoabomoa Wamtaka Waziri Lukuvi Kuingilia Kati

$
0
0
Wananchi Wa Kilimanjaro Wahaha na Bomoabomoa Wamtaka Waziri  Lukuvi Kuingilia Kati
 Wananchi wa mtaa wa Fonga kata ya Pasua, mkoani Kilimanjaro wamemwomba Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendelo ya Makazi, William Lukuvi kuingilia kati bomoabomoa inayoendelea mkoani humo.

Wananchi hao walisema kuwa maeneo yaliyowekwa alama ya X yana hati miliki ambayo walipewa na Wizara ya Ardhi.

Hata hivyo mmoja wa waathirika hao, Charles Msuya amesema wao sio wavamizi na wamepewa kihalali maeneo hayo na Manispaa ya Moshi

Amesema wamekua wakilipia majengo hayo kila mwaka tangia

wamilikishwe maeneo hayo rasmi na Manispaa.

“Nikirejea nyuma, Oktoba, 2007 kipindi cha Waziri wa Ardhi wakati huo Rais John Magufuli alikuja katika maeneo yetu na kuhutubia wananchi na moja wapo ya vitu alivyoagiza ni mkurugenzi chini ya mkuu wa mkoa aliyekuepo kipindi hicho kuhakikisha  wananchi wa eneo hilo wanapewa hati miliki na ndiyo watu walianza kujenga na hadi sasa wanaendelea kujenga.

Antony Kisinga ambaye ni mmiliki wa majengo mbalimbali ya biashara eneo hilo amesema kitendo  kinachofanywa na Kampuni ya Reli ni uonevu kutokana na kwamba miaka 10 iliyopota hajawahi kufuatwa na mtu yeyote kuhusiana na eneo hilo.

“Sasa napewa notisi ya kuvunja nyumba kwa siku 30 kwa mtu ambaye hajawahi kuninyooshea kidole wala hajawahi kuongea na mimi nilishtuka sana, hiki ni kitendo cha kibabe,”amesema Kisinga.

Hata hivyo alisema kuwa kutokana na kwamba ana nyaraka zote za umiliki wa eneo hilo na yeye sio mvamizi.

Kwa upande wake diwani wa kata hiyo, Charles Mkalakala amesema bomoabomoa hiyo imewaathiri watu wengi kutokana na eneo hilo kubadilishwa matumizi na Manispaa ya Moshi.

“Ni vizuri Serikali ikaangalia kuhusiana na zoezi hili kutokana na

kwamba kila mu ana hati miliki na kwamba hati ni mali ya Serikali, cha msingi Serikali iangalie kama walikubali kubadilisha matumizi basi wawaachie wananchi maeneo haya,”amesema Mkalakala.

Zoezi la bomoabomoa lilianza kutikisa Moshi baada ya Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli(Rahco), kutia timu mkoani hapa na kuvunja zaidi ya nyumba 500 .



Wakimbizi 18 wa Burundi Wauawa DR Congo

$
0
0
Wakimbizi 18 wa Burundi Wauawa DR Congo
Maafisa wanasema kuwa takriban wakimbizi 18 wa Burundi wameuawa na vikosi vya usalama mashariki mwa taifa la Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo .
Wengi wengine wamejeruhiwa.
Maafisa wa DR Congo pamoja na wanajeshi wanadaiwa kuwafyatulia risasi wakimbizi hao walipokuwa wakifanya maandamano ya kupinga mpango wa kuwarudisha nyumbani.
Makumi la maelfu ya raia wa Burundi walitoroka taifa hilo wakati za wa ghasia za 2015 kufuatia hatua ya rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula mwengine wa tatu.
Utawala wa Burundi unasema kuwa ni salama kwa raia kurudi nyumbani .

Lazaro Nyalandu Atinga Nairobi Kumjulia HaliTundu Lissu Nairobi

$
0
0

Lazaro Nyalandu Atinga Nairobi Kumjulia HaliTundu Lissu Nairobi i
Mbunge wa Singida Kaskazini Mhe. Lazaro Samuel Nyalandu amemtembelea Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu jijini Nairobi nchini Kenya kumjulia hali kufuatia mbunge huyo kupigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma.

Lazaro Nyalandu amesema kuwa kwa niaba ya watu wa Singida na Watanzania wote ametoa salamu za pole kwa mke wa Tundu Lissu kwa kuwa bado hajapata nafasi ya kumuona kiongozi huyo na kusema anasubiri kama ataweza kupata nafasi ya kumuona usiku wa leo kama madaktari wataruhusu.

"Nimefika hospitali ya Nairobi mapema leo kumjulia hali Mh. Tundu Lissu madaktari wanaendelea kumfanyia matibabu, na bado hatujaruhusiwa kumuona. Kwa niaba ya wana Singida na Watanzania wote, nimetoa salaam za pole kwa mke wake, na bado nasubiri uwezekano wa kuweza kuonana naye usiku wa leo endapo madaktari wataruhusu" alisema Nyalandu

Aidha Mbunge huyo amewataka Watanzania kijumla kuendelea kumuombe Mbunge Tundu Lissu ili aweze kupona na kurejea nchini akiwa mzima wa afya njema
"Cha muhimu zaidi, sote tuendelee kumuombea Mungu amtendee wema, na kumponya katika majira haya ya kujaribiwa kwake. Katika yote ndani ya yote, ikawe heri kwake" alisema Nyalandu
Mbunge Tundu Lissu alishambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa Makao Makuu ya nchi jijini Dodoma na baadaye kusafirishwa kupelekwa jijini Nairobi Kenye kwa matibabu ambapo mpaka sasa yupo huko akiendelea kupata matibabu.


Spika Mstaafu Msekwa Afunguka Haya Kuhusu Utendaji Kazi Wa Spika Ndugai Bungeni Unaolalamikiwa

$
0
0
Spika mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa ametia neno akigusia utendaji wa Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyeingia katika msuguano na baadhi ya wabunge wa upinzani.

Ndugai ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kongwa mkoani Dodoma hakuwa na wakati mzuri katika Bunge lililomalizika jana kutokana na kupishana kauli na wabunge, Zitto Kabwe, Said Kubenea, Godbless Lema na Peter Msigwa.

Alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu Spika Ndugai alivyojikuta akitumbukia katika mvutano huo, Msekwa alisema: “tulifundishwa na Mzee Mwinyi(Ali Hassan) kila kitabu na zama zake.”

Amesema ingawa wakati wa uongozi wake hakukuwa na malumbano ya namna hiyo lakini hilo halimanishi kuwa Spika wa sasa anaendesha mambo kinyume na Kanuni za Bunge.

Amesema anachokifanya Spika Ndugai kinatafsiri aina ya uongozi alionao ambao siyo jambo la kushangaza kuona ukitofautiana na mfumo aliokuwa akitumia wakati akiwa katika kiti hicho.

“Hii ni staili yake ya uongozi na ndiyo mabadiliko ya uongozi wenyewe,” amesema Msekwa wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu na kurudia tena maneno hayo akisema “ ni staili yake na kila kiongozi anakuwa na mfumo wake wa kuongoza mambo.”

Lakini amesema kwa kufanya hivyo hajakosea lolote kwa vile yale aliyokuwa akiyazungumza na kuyatolea maamuzi yako ndani ya Kanuni za Bunge.
“Spika ametumia mamlaka yake sioni kama kuna ubaya wowote,” amesema Msekwa ambaye amewahi pia kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM.

Amesema hata yeye alipochukua nafasi hiyo kulikuwa na maspika wengine waliomtangulia waliokuwa na mfumo wao wa kuendesha Bunge na kisha naye akawa na wake pia.
“Baada ya mimi walikuja wengine ambao nao pia walikuwa na staili yao ya uongozi,” amesema.

Hatua ya Ndugai kudai kuwa anaweza kumzuia Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe asizungumze bungeni kwa muda wote uliobaki na hana cha kumfanya imezusha mjadala mkubwa nchini huku baadhi ya wasomi wameikosoa kauli hiyo wakisema hana mamlaka hayo kisheria.

Spika Ndugai alitoa kauli hiyo hivi karibuni baada ya Zitto kunukuliwa katika akaunti yake ya Twitter akimkosoa kiutendaji.

Mzozo kati ya Spika Ndugai na Zitto ulianza baada ya kiongozi huyo wa ACT – Wazalendo kusema kwamba Bunge limewekwa mfukoni na mhimili fulani wakati alipotoa maoni kuhusu ripoti mbili za kamati ya Bunge za almasi na Tanzanite.

Kutokana na kauli hizo, Spika Ndugai aliagiza mbunge huyo ahojiwe na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge huku akimshtaki kwa wapigakura wake akisema licha ya kwamba mbunge wao yupo nchini hajafika bungeni kuwawakilisha na yeye (Spika), hana taarifa.

Wakizungumzia matamshi hayo baadhi ya wasomi walisema kauli kama hiyo haikupaswa kutolewa na Spika.
Baadhi ya wanasheria walisema kauli ya Spika Ndugai imelenga kuwanyamazisha wabunge wasiwe huru kutoa maoni yao kwa mujibu wa Katiba.

Breaking News: Nyumba ya Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma, yaungua moto

$
0
0

Nyumba ya Mbunge Kigoma Mjini Zitto Kabwe aliyoijenga  wakati akigombea ubunge kwa mara ya kwanza  iliyopo Kibingo, Kata ya Mwandiga mjini Kigoma imeungua moto jioni hii.

Nyumba hiyo iko kiwanja kimoja na nyumba yake ya sasa imeteketea yote na chanzo chake hakijafahamika hadi sasa.

Msaidizi wa mbunge huyo, Nyembo Mustafa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba hata hivyo Zitto hakuwa anaishi kwenye nyumba hiyo.

Amesema Zitto alihama kwenye nyumba hiyo baada ya kujenga nyumba nyingine kubwa kwenye kiwanja hicho hicho na iliyoungua ilikuwa ikitumika kwa dharura.

Tundu Lissu Ametangazwa Shujaa Huko Lagos Nchini Nigeria Magharibi mwa Bara la Afrika

$
0
0

Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tundu Lissu, ametangazwa katika kongamano la kimataifa lililofanyika jijini Lagos, nchini Nigeria, kuwa ndiye mwanasiasa kiongozi katika kutetea matumizi mazuri ya raslimali za taifa lake,anaandika Jabir Idrissa.

Wanakongamano waliokusanyika kujadili amani duniani, wamesema: “Lissu ni kielelezo kizuri cha kiongozi mwenye maadili na shujaa wa haki za binadaamu… mpenda haki na mwanasiasa mkweli anayestahiki kuombewa na wapenda amani hata kufikia kuwa rais katika nchi yake.”

Kwa ujasiri wake katika kukataa dhulma na kuitumia vema fani ya sheria katika kusimamia raslimali za taifa lake, wanakongamano wamesema, “mamilioni ya vijana duniani kote wameanza kuomba kusoma fani ya sheria vyuoni baada ya mitandao ya kijamii zaidi ya 11,000 kuripoti habari zake kwa muda wa siku 11 mfululizo kuliko habari za rais yoyote duniani.”

Taarifa zilizofikia MwanahalisiOnline kutoka Nigeria, zimesema hatua hiyo imefikiwa kwenye kongamano lililomalizika jana likishirikisha vijana wasomi wa Kikristo kutoka vyuo vikuu 283 vya Afrika, Marekani, Asia na Ulaya waliokubaliana kuwa Lissu ni kielelezo kizuri cha kiongozi mwenye maadili na shujaa wa haki za binaadamu.

Profesa Bigs Ezziel kutoka Marekani ambaye katika kongamano hilo la siku tano alifundisha mada ya HAKI, ameonya kuwa nchi nyingi za Afrika bado hazijui thamani ya haki ambayo ndiyo tunu nguzo kuu ya amani na demokrasia.

Akimzungumzia Lissu, Prof. Ezziel alisema wamefuatilia kwa karibu habari za mwanasiasa huyo na kuridhika kuwa ni mtu wa pekee kwa kusema ukweli. “Kwenye Balozi zetu wamekuwa wakituletea mambo yote pale Tanzania bila ya shaka anatakiwa apewe tuzo maalum ili kuwachochea vijana wa kizazi hiki kukataa dhulma.”

Prof. Ezziel ameshauri wasomi wa sheria katika nchi za Afrika kumualika Lissu kwenye vyuo vyao ili atoe elimu itakayowezesha wasomi kuielewa fani ya sheria kwa mapana yake kuliko ilivyo sasa kukikosekana tija hasa ya wanasheria katika nchi zao.

“Ni muhimu tutambue kuwa HAKI ni nguzo muhimu kwa amani, upendo na maendeleo. Mwenyezi Mungu anajitambulisha waziwazi kuwa yu Mungu wa haki… inasikitisha wanasiasa wengi barani Afrika wapo kama mafisi kwa kutamani madaraka badala ya kutamani kumtambua Mungu kwa kufanya yale yanayojenga jamii zao.

“Badala yake wanatumia siasa za kugawa wananchi huku wakitumia nguvu za dola kuharibu amani na utulivu katika nchi zao. Tanzania inakwenda vibaya kutokana na wanasiasa kutoenenda katika kuonesha ni kielelezo cha maadili kama alivyokuwa Mwalimu Nyerere ambaye hakutaka kujilimbikizia mali wala kupenda kutumia nguvu za dola kuonea wananchi,” alisema.

Amehimiza viongozi wa kiroho barani Afrika kumuomba Mwenyezi Mungu kulisaidia taifa la Tanzania ili kulinusuru na balaa linaloweza kutokea kutokana na maongozi yanayokiuka haki za binaadamu huku wakimuombea Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baraka ili kutimiza ndoto yake ya kuona maliasili na raslimali za Tanzania zinanufaisha Watanzania.

Amesema Afrika inahitaji mabadiliko makubwa kisiasa, tofauti na siasa zinazoshuhudiwa zama hizi kwa marais kunogewa na madaraka hata kujifanya Miungu watu. Waruhusu mawazo ya wengi kutawala badala ya kauli ya mtu mmoja kuongoza taifa la mamilioni ya watu. Huko ni kumkataa Mwenyezi Mungu ambaye humsikiliza na kumlisha kila mtu na kila ndege wa angani.

Prof. Ezziel, mwanasheria na mshauri wa sheria kwenye vyuo vikuu 17 vya Palestina, Djibouti, Ghana, Marekani na Jerusalem, amepongeza wanasheria wa Tanzania kwa kumchagua Lissu kuwa rais wa jumuiya ya wanasheria ya Tanganyika. Uamuzi wao wakati wa mkutano mkuu wa Tanganyika Law Society (TLS), amesema umewapata kuheshimika duniani.

Kadhalika, Lissu ametajwa na Dk. Marucus Bahod na Dk. Chris Zulu kuwa “mwanasiasa wa mfano katika karne hii” ambaye ameifundisha dunia umuhimu wa kusimamia haki na sheria na kuifanya taaluma ya sheria kung’aa kwa muda mfupi kiasi cha kusababisha macho yote ya wanazuoni duniani kuiangalia Tanzania kwa kumfuatilia Lissu.

“Ni mwanasheria anayejiamini kutetea matumizi mazuri ya raslimali na maliasili za taifa lake bila ya kujali nguvu kubwa inayotumika na serikali kumkatisha tamaa… mwanasiasa anayeweza kuiongoza Tanzania kwa uwezo wake wa kimaadili na kuitafsiri sheria kwa faida ya Watanzania wote.

“Ni mfano mzuri kwa wanasheria wengine Afrika ambao wanakuwa wazito kusimamia matumizi ya manufaa ya maliasili katika nchi zao na hivyo kuzinyima fursa za maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kutokuwa mbele katika kutetea maliasili za mataifa ya Afrika kunachangia kuua demokrasia, utawala wa haki na sheria,” alisema.

Madaktari hao walisema ni vema wanaotafuta uongozi wa kisiasa barani Afrika wawe watu wema na kamwe wasiruhusu watu wenye visasi kupewa dhamana ya uongozi kwani wakishapata madaraka, huzalisha chuki na fitna katika jamii badala ya maendeleo.

Askofu William Muller kutoka Ujerumani, aliongoza dua ya kuiombea Kenya kuendelea na amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi huu. Nazo nchi za DR Congo, Tanzania, Afrika Kusini, Msumbiji, Ghana, Nigeria, Uganda, Burundi na Gabon zimeombewa ili zirudi kwenye maendeleo makubwa ya kiuchumi.

Emma The Boy Aibuka na Kufunguka Kilichomsibu Kwa Siku Tano Bila Kuonekana

$
0
0
Emma The Boy Aibuka na Kufunguka Kilichomsibu Kwa Siku Tano Bila Kuonekana
Baada ya taarifa kuzagaa kwenye mitandao ya kijamii kutoka kwa ndugu kwamba mtayarishaji wa muziki kutoka THT, Ema The Boy amepotea na ana siku ya tano hajaonekana, Producer huyo ameibuka kupitia mtandao wa Instagram na kueleza kilichomsibu.

Kupitia taarifa hiyo aliyoitoa kupitia mitandao ya kijamii, Ema alisema alikuwa Bagamoyo kikazi na ameomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa ndugu jamaa na marafiki.

Napenda kuchukua nafasi hii kuwajulisha ndugu jamaa na marafiki wote waliokuwa na wasiwasi juu yangu, ukweli ni kwamba nilikuwa Bagamoyo kikazi zangu binafsi, naomba radhi kwa familia, ofisini, na wadau wote kwa usumbufu uliojitokeza
Niko salama na mzima wa Afya .
Ahsanteni.



Katibu Mkuu wa Chama cha Sauti ya Umma Amuangukia Rais Magufuli Amuomba Milioni 32

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Sauti ya Umma Amuangukia Rais Magufuli Amuomba Milioni 32
Katibu Mkuu wa Chama cha Sauti ya Umma(SAU), Jonson Mwangosi na familia ya Dk Paul Kyara inaamuomba Rais John Magufuli kuwaidia kiasi cha Sh32 milioni kwa ajili ya kwenda kutibiwa figo zake mbili  katika hospitali ya Shijiazhuang iliyopo nchini China.

Mwangosi amesema mwenyekiti wa chama hicho Dk Kyara anaumwa figo zote mbili tangu mwaka 2012 ambapo alienda nchini India mara mbili hivyo kwa sasa anafanyiwa matibabu ya kusafisha figo mara tatu katika hospitali ya Regency lakini bado ufumbuzi haujapatikana.

Amesema wakati anaendelea na matibabu hayo walimpata daktari mwenye mawasiliano na daktari wa hospitali ya  Shijiazhuang, Dk Bryat ambaye alimtumia dawa ambazo zimeonyesha mafanikio ikiwemo kupata haja ndogo tofauti na awali alivyokuwa.

Mwangosi amesema kutokana na mafanikio hayo kuonekana hivyo amepewa rufaa ya kwenda kutibiwa katika hospitali hiyo ambapo atatibiwa bila ya kuongezewa figo nyingine.

"Hadi sasa afya ya Kyara sio mbaya kama ilivyokuwa awali kwa sababu sasa anaendelea kutumia dawa za hospitali hiyo hivyo anahitajika akafanyiwe matibabu zaidi nchini China,"amesema.

Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images