Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Steve Nyerere Agoma Kuwataja Mashoga Bongo Movies

$
0
0
MWENYEKITI wa Klabu ya Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amekataa katakata kuwataja wanachama wanaodaiwa ni mashoga ndani ya klabu hiyo ya jijini Dar.

Akizungumza na Amani juzikati jijini Dar baada ya kuombwa kuwataja wadaiwa hao, Steve alisema hashindwi kuyaanika majina yao, bali uongozi wake kwenye chama hicho si kuingilia mambo binafsi bali kuunganisha umoja na mshikamano kwa ajili ya tasnia ya filamu za Bongo.

“Hilo suala kila mtu ananiachia mimi nilizungumzie kwa kukanusha au kuweka majina hadharani ya wanaodaiwa ni mashoga. Hadi namaliza uongozi wangu sitafanya hivyo,” alisema Steve.

Siku za hivi karibuni baadhi ya vyombo vya habari viliwahi kuripoti suala la kuwepo kwa mastaa mashoga kwenye klabu hiyo yenye nguvu ya ushawishi wa fedha mjini.

Polisi nchini Kenya yamnasa mtu anayedaiwa kuendesha Account ya Twitter inayomilikiwa na Al Shabaab

$
0
0
Maafisa wa polisi wa Kenya wamemtia nguvuni mshukiwa anayetuhumiwa kuendesha akaunti ya Twitter ambayo ina uhusiano na kundi la kigaidi la Al shabaab na uliotoa habari kwamba Al shabaab walihusika kutekeleza mauaji eneo la Mpeketoni kaunti ya Lamu.

Kwa mujibu wa Ripota  Julius Kepkoech  toka  Kenya, Katibu wa wizara ya Mambo ya ndani na usalama wa taifa, Mutea Iringo amethibitisha kwamba Ismail Omondi ametiwa nguvuni Tarehe 18 June mwaka huu ambapo hata hivyo Iringo amekanusha kwamba mshukiwa huyo hana uhusiano wowote na Al Shabaab.

Iringo amesema, “Unaweza kuona kwamba yule anayekiri kuhusika na Alshabaab si mmoja wa kiongozi wa kundi hilo,”.

Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo awali alisema kupitia ukurasa wake wa Twitter kwamba:  “Aliye kizuizini kwa sasa ni mshukiwa anayeendesha mtandao wa kijamii unaodhaniwa kutumiwa na Al shabaab kukiri kuhusika na uvamizi”

Hata hivyo Kimaiyo hakutoa taarifa zaidi kuhusiana na washukiwa.

Ismail Omondi ni mshukiwa wa tatu kutiwa nguvuni kuhusiana na mauaji yaliyotokea Mpeketoni siku ya Jumapili na Jumatatu ambapo zaidi ya watu 60 wamepoteza maisha.

Mapema  siku ya Jumatano, mshukiwa mwingine Ahmed Abdallah anayetuhumiwa kumiliki gari lililowabeba wavamizi hao alikamatwa huku Salim Dyana naye akikamatwa na polisi kwa tuhuma za kuliendesha gari lililowabeba wavamizi kuelekea Mpeketoni Lamu.

Dotnata 'Nachukizwa na Watu Wenye Kasumba ya Kumsema Vibaya Mwigizaji Wema Sepetu ‘Beutiful Onyinye’, Waache.'

$
0
0
MJASIRIAMALI na mwigizaji wa sinema za Kibongo, Illuminata Poshi ‘Dotnata’ ameibuka na kusema anachukizwa na watu wenye kasumba ya kumsema vibaya mwigizaji Wema Sepetu ‘Beutiful Onyinye’, waache.

Akipiga stori na paparazi wetu Dotnata alisema anakerwa sana na watu wanaokuwa na chuki na mwigizaji huyo ambaye yeye anamchukulia kama lulu katika tasnia ya uigizaji.

“Siwapendi wanaomchukia Wema ambaye mimi huwa namuona kama nyota katika sanaa, wamuache mtoto wa watu afanye kazi zake, si watafute kazi za kufanya kuliko kumuongelea mabaya,” alisema Dotnata pasipo kuwataja majina watu hao.

Ivory Coast 1-2 Colombia

$
0
0
Ivory Coast sasa wanahitaji kushinda mechi yao ya mwisho dhidi ya Ugiriki ilikuwa na matumaini ya kumaliza katika nafasi ya pili ya kundi hilo na kusonga mbele katika hatua ya maondoano.
Colombia inaongoza kundi hilo ikiwa na jumla ya alama 6 huku Ivory Coast ikiwa ya pili na alama 3 kufuatia ushindi wao wa kwanza dhidi ya Japan.
Japan inashikilia nafasi ya tatu.
Ugiriki ni ya mwisho katika kundi C.

Ukweli Kuhusu Tetesi za Lady Jay Dee Kuomba Msamaha kwa Ruge wa Clouds FM

$
0
0
Judith Daines Wambura Mbibo, known as Lady Jaydee  a Tanzania  R&B/Zouk/Kwaito singer ,
Denial a rumors that she apology Ruge Mutahaba….. These fiction was written on Gazeti  la Udaku…. Today On her Instagram  account she posted the Gazeti font page pic and she wrote  this…."Katika ulimwengu huu kumbe bado kuna watu wanafikiri wanaweza kutunga uongo na dunia ikawaamini??? Duuuh! mmechelewa sana Ila km hiyo ni ndoto yenu, basi endeleeni kuota na km ni njia tu ya kujiingizia kipato, bs kila kheri. Mi nipo, mtanikuta tu.... "

 
Before this she posted this ……

BBC Waianika Vibaya Tanzania Tena!

$
0
0
Baada ya kufanikiwa kwenye pembe za ndovu, BBC wametukung'uta tena. Safari hii ni kwenye madini ya tanzanite. Wanadai tanzanite inachimbwa na watoto. Wameweka video ya "the gemstone mined by child labour". Huu utakuwa ni mkakati wa makaburu wa tanzaniteone ambao mara zote wameutangazia ulimwengu kuwa tanzanite yao pekee ndiyo halali maana haichimbwi na watoto. Hili ni pigo jingine kwa ndugu zetu wanaotegemea tanzanite kuendesha maisha yao

Mzee wa Upako Anamvua nguo GWAJIMA Hadharani

$
0
0
Kasema Gwajima anafanya hadaa kwa wafuasi wake, kasema kama kweli anafufua misukule, mbona hafufui watu wanaofahamika?
Hafufui baba na mama zetu, hafufui majirani zetu, anafufua tusio wajua?

Gwajima mzee wa HUMMER3 na wafuasi wake mna lolote la kuoangea?

Sikiliza na Download Wimbo Mpya wa Chege na Temba-Wauwe

$
0
0
Baada ya kutoka taarifa kadhaa za video ambayo ndani yake pia yupo Jokate,leo Chege na Temba wameamua kuuachia rasmi wimbo wao walioupa jina la Wauwe.zitumie hizi dakika 3 kusikiliza na kutoa maoni yako hapo chini ili baadae wakipita wasome ulichokisema kuhusu wimbo huu mpya ambao kashirikishwa Malomboso kutoka Yamoto Band.
Bonyeza play kusikiliza.

Wajeruhiwa kwa Risasi za Moto Baada ya Kunaswa Wakicheza Ngoma za Vigodoro Wakiwa Utupu

$
0
0
Watu watatu wakazi wa Mwananyamala Jijini Dar Es Salaam wamejeruhiwa katika tukio lililohusisha risasi za moto linalodaiwa kufanywa na polisi baada ya kukutwa wakikesha kwenye ngoma maarufu za Kigodoro, ambazo tayari zimekwishapigwa marufuku na jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa kumi na nusu jioni katika eneo la shule ya msingi kisiwani ambapo mmoja  wa  majeruhi hao  tayari amekwisahruhusiwa kurudi nyumbani na mwingine akiendelea na matibabu kwenye hospitali ya Mwananyamala.

Wakiwa kwenye ngoma hiyo maarufu Jijini Dar es Salaam ya Kigodoro, eneo la Kisiwani mwananyamala, mara gahfala polisi walivamia eneo hilo, na kusimamisha shughuli nzima kwa madai ya kucheza wakiwa hawana nguo, jambo ambalo ni kinyume na maadili.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa kipolisi Kinondoni Kamishna msaidizi Camillius Wambura anathibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Sakata la Mumewe kusota Rumande Kwa Ubakaji….Flora Mbasha Ajikuta Akiambulia AIBU ya Mwaka.

$
0
0
Wakati jana mumewe Emmanuel Mbasha (32) akipandishwa kizimbani kwa mara ya pili kwa soo la ubakaji wa shemejiye, mwimba Injili kinara Bongo, Flora Mbasha (31) amepitia katika hatua tatu za aibu.
 
Mbasha ambaye naye ni mwimba Injili na mfanyabiashara alitarajiwa kupandishwa kizimbani jana kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Ilala, Dar akitokea mahabusu Keko akikabiliwa na mashtaka mawili ya ubakaji wa shemejiye mwenye umri wa miaka 17.

Habari kutoka kwa mtu wa karibu wa Flora ambaye alihama nyumbani na kwenda kuishi hotelini maeneo ya Sinza, Dar, kitendo hicho kilimuingiza staa huyo kwenye hatua ya tatu ya aibu na kujikuta akiwa katika masikitiko makubwa.

AIBU YA KWANZA
Kwa mujibu wa mtu huyo wa karibu aliyeomba hifadhi ya jina, aibu ya kwanza inayomuuma Flora ni ile ya ndoa yake kuingia kwenye gogoro kisha kudaiwa kutengana na mumewe kinyume na kile anachokihubiri kupitia nyimbo zake zinazopendwa na wengi ndani na nje ya Bongo.
 
“Unajua lile neno la ‘mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake, bali mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe’ (Mithali 14:1) linamfanya awe na aibu mbele za watu.

“Unaambiwa kanisani (anasali Kanisa la Ufufuo na Uzima la Mchungaji Josephat Gwajima kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, Dar) anaona aibu hasa kwa waumini wenzake.

“Flora amedumu na Ima (Mbasha) kwenye ndoa kwa miaka 12 hivyo kutokea kwa kilichotokea ni aibu kwani tayari walikuwa wamekomaa tofauti na walipoona wakiwa na umri mdogo.

“Hebu fikiria, mtoto amekuwa mkubwa, anaposikia mama ana matatizo na baba si ni aibu jamani? Cha msingi tuwaombee wamalize matatizo yao, inaweza kusaidia kuifuta aibu hiyo kwani imeandikwa ‘Ndoa na iheshimiwe na watu wote…’ ( Waebrania 13 : 4 -),” alisema mnyetishaji wetu akisisitiza kuwa akitajwa  ataonekana mvujishaji wa mambo ya siri ya wanandoa hao.
AIBU YA PILI

Chanzo hicho kiliendelea kutiririka kuwa aibu ya pili inayomkabili Flora ni skendo ya yeye kudaiwa kuhamishia makazi kwa mchungaji wake, Gwajima.
 
Katika aibu hiyo, mumewe alinukuliwa na gazeti la Uwazi akimlalamikia mchungaji huyo amwachie mkewe kwani yeye ndiye alisababisha sakarakasi zote hizo za ndoa yake.

Ilidaiwa kuwa kwa mke wa mtu achilia mbali mhubiri kwa njia ya nyimbo, kitendo cha kukumbwa na skendo nayo ni aibu pia.
 
“Kwa mtumishi kutajwa kwenye jambo kama hilo lisilo na mrengo wa kupendeza masikioni mwa watu, ni aibu kuu,” kilidai chanzo hicho.

AIBU KUU YA TATU

Ilisemekana kuwa achilia mbali ndoa, mambo ya mchepuko lakini aibu kuu ya tatu kwa Flora, ni kashfa ya ubakaji wa shemejiye inayomkabili mumewe Mbasha.

“Unajua usifikirie kwamba mume akipata aibu mke anaweza kuikwepa. Hawezi kwa sababu ‘wanazungumza lugha moja’ (yaani ni mwili mmoja). Ona sasa mume anapandishwa kizimbani kwa ubakaji.
 
“Pia usifikiri watu watasema kashfa ni ya Ima peke yake. Kwanza hata kutamka watu wanasema mume wa Flora. Ikumbukwe aibu ya mume ni ya mke pia. Ni vigumu mno kwa Flora kusema aibu ni ya mumewe pekee,” alitiririka mto habari huyo.
FAMILIA ZATOFAUTIANA

Wakati hayo yakiendelea, habari zinadai kuwa familia za pande zote zinatofautiana huku kila moja ikilaumu nyingine.
Ilidaiwa kuwa upande wa Mbasha unamlalamikia mama wa Flora kuwa anamuunga mkono mwanaye badala ya kusaidia kutuliza hali ya hewa.
Ilielezwa kuwa upande wa Flora wao wanamlaumu Mbasha kwa madai kuwa chanzo cha yote ni mgawanyo wa mali hasa baada ya kuona kuwa hakuna tena ndoa.

FLORA ANASEMAJE?

Akizungumza na Ijumaa juzi kwa njia ya simu, Flora alitoa la moyoni: “Kweli naumia sana tena sana. Kwa sasa kesi ipo mahakamani, siwezi kuizungumzia lakini ndiyo hivyo. Siyo siri nateseka sana.”

Mbasha anadaiwa kumbaka ndugu wa Flora ambaye ni yatima kati ya  Mei 23 na 25, mwaka huu ambapo kesi yake inaendelea kuunguruma baada ya kukaa mahabusu ya Keko kwa siku kadhaa ambapo sheria ndiyo itakayoanika siri zote juu ya sakata hilo.

Crediti: GPL

Vitambulisho vya Kura Vya Sasa Vyafutwa, Kutolewa Upya

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza matumizi ya teknolojia mpya ya Biometric Voter Registration (BVR), katika maboresho ya Daftari la Kudumu la Wapigakura ambayo yatafuta matumizi ya vitambulisho vya kupigia kura vya sasa.

Kwa hatua hiyo, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva ametangaza kuwa: “Katika kura ya maoni ya Katiba Mpya na Uchaguzi Mkuu wa 2015, mpigakura atatumia kitambulisho kipya atakachopatiwa na Tume baada ya kuandikishwa upya katika mfumo huu na si vinginevyo.

Vitambulisho vilivyotolewa katika uandikishaji na uboreshaji uliopita havitatumika tena.”

Akitangaza mpango huo mpya Dar es Salaam jana, Jaji Lubuva alisema Tume hiyo itaanza maboresho ya daftari hilo kwa watu wote wenye sifa za kupiga kura Septemba mwaka huu na kukamilisha kabla ya kura ya maoni ya Katiba na Uchaguzi Mkuu 2015.

BVR ni mfumo wa kuchukua taarifa za mtu za kibaiolojia hasa alama za vidole.

Mwaka 2004, NEC ilianzisha Daftari la Kudumu la Wapigakura ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa taarifa za wapigakura na uhifadhi wa taarifa za kielektroniki.

Sanjari na hilo, tume hiyo ilitoa vitambulisho vya wapigakura ambavyo pia vimekuwa vikitumika kwa shughuli mbalimbali za utambulisho katika maeneo kama benki, polisi, mahakamani, uhamiaji, ukataji leseni, usajili wa simu na mengineyo.

Jaji Lubuva alisema katika kazi hiyo ya uandikishaji, NEC imekusudia kutumia Sh293 bilioni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa, mafunzo ya watendaji na uandikishaji.

Maofisa watakaotumika katika uandikishaji ni pamoja na waratibu wa uandikishaji wa mkoa, maofisa waandikishaji ambao watakuwa ni wakurugenzi wa halmashauri, maofisa wasaidizi watakaokuwa watatu kwa kila jimbo, watendaji kata na waratibu wa elimu.

Mafunzo kwa watendaji hao yanatarajiwa kuanza Julai, 2014 na uandikishaji utaanza Septemba na katika vituo 40,015 kote nchini.

Vituo vya uandikishaji

Jaji Lubuva alisema kwa utaratibu wa sasa, vituo vya kujiandikishia vimeongezeka kutoka 24,919 hadi 40,015 ambavyo vimewekwa katika ngazi za vitongoji, vijiji na mitaa ili kuwezesha kuwa karibu zaidi na wananchi.

Tundu Lissu Ailipua Tena Serikali Kwa Kutoa Taarifa za Ungo

$
0
0
Serikali imeumbuliwa bungeni ikidaiwa kuwasilisha taarifa za uongo kupitia Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu ugawaji wa madawati yaliyonunuliwa kwa ‘chenji ya rada’.

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alitoa tuhuma hizo jana, wakati akichangia mjadala wa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2013/2014, akisema Serikali imewadanganya wabunge kwa kuwa hakuna kitu kilichofanyika.

Alisema katika majibu ya Serikali kumekuwa na mkanganyiko mkubwa kwa kuwa imetangaza kununua madawati 93,740 na kuyagawa katika halmashauri mbalimbali nchini wakati siyo kweli.

Alisema kwa mtindo huo, Serikali imelidanganya Bunge pamoja na Watanzania kwa kuwa imetangaza madawati hewa ambayo hayapo.

“Wabunge kama kweli mnatimiza majukumu yenu na hampo hapa kwa masilahi yenu tu, hebu hojini halmashauri zetu zimepelekewa haya madawati 93,000 yanayozungumzwa humu au mnapiga makofi tu? Serikali inadanganya tunatakiwa tuihoji tuiwajibishe,” alisema.

Lissu ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alitoa mfano wa mgawo huo kwenye Halmashauri ya Ikungi, Singida kwamba ilitangazwa kupelekewa madawati 508 lakini amekwenda jimboni na hakukuta dawati hata moja.

Alisema uchunguzi wake umebaini kuwa hata katika wilaya mbalimbali ikiwamo ya Iringa, hakuna kitu kama hicho.

“Jana sikuwa hapa bungeni nilikwenda kwenye halmashauri yangu, hakuna dawati hata moja. Hata Halmashauri ya Iringa kwa Mchungaji Msigwa (Peter) hapa ananiambia hakuna dawati hata moja, mnatudanganya ili iweje?” Aliwashauri wabunge wengine kufanya utafiti katika maeneo yao iwapo kuna madawati ambayo yamepelekwa kutokana na fedha zilizorejeshwa na Serikali kama chenji ya rada.

Lissu alisema ni maneno matupu ambayo yamekuwa yakiwahadaa wabunge na kuwafanya wasahau wajibu wao wa kuisimamia Serikali na kujikuta ni washangiliaji wakati wote. Lissu alisema kinyume na taarifa hizo za Waziri Mkuu, Bunge jana lilikuwa limeelezwa na Naibu Waziri (hakumtaja) kuwa madawati hayo hayajagawanywa.

Katika kipindi cha maswali na majibu, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Kassim Majaliwa akijibu swali la nyongeza la Ibrahim Sanya (Mji Mkongwe - CUF), kuhusu madawati hayo, alisema kwa kuwa madawati hayo bado yanagawanywa, watakaa na kuangalia utaratibu mzuri wa kuyafikisha Zanzibar.

Lissu pia alisema fedha ambazo zilitajwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospter Muhongo kuwa ni pato la Watanzania ni uongo kwa kuwa ni mali ya wamiliki wa migodi.

Alisema takwimu za waziri zimesababisha Watanzania kuamini kuwa wameingiza fedha nyingi ilihali kiasi kilichoingia hakifikii hata asilimia 10 ya pato la wawekezaji.

Mitandao ya Kijamii Sasa Kudhibitiwa na TCRA...Onyo kwa Wanao Penda Kutukana Wenzao Kwenye Comments

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), inajipanga kuja na mfumo wa kompyuta utakaoratibu taarifa zote zinazopakiwa mtandaoni ili kukabiliana na vitendo vya udhalilishaji vinavyofanywa na watu wasio na maadili ya uandishi wa habari.

Hayo yalisemwa na mkurugenzi wa teknolojia ya habari na mawasiliano wa mamlaka hiyo, Dk Joseph Kilongola katika kongamano la kimataifa la habari lililo andaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na kufanyika jijini hapa kwa mara ya kwanza, mwaka huu.

“Licha ya kuwaelimisha wadau wa habari hasa wamiliki wa ‘blog’ juu ya kuzingatia maadili ya uandishi kwa kila wapakiacho mtandaoni, sasa tunakuja na cyber security itakayosimamia upashanaji habari,” alisema Dk Kilongola.

Alisema mfumo huo utafanya pia kazi ya kuchuja habari zote kabla hazijawekwa mtandaoni na utatoa ulinzi kwa jambo lolote linalotishia usalama katika sekta yoyote ya uchumi na kabla madhara hayajatokea, wahusika watakuwa wameshajulikana.

Profesa Florens Luoga kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) alitahadharisha dhidi uhuru na haki ya matumizi ya majukwaa mbalimbali ya mawasiliano kuwa yanapaswa kuzingatia maadili ili kuepusha athari zinazoweza kujitokea katika jamii.

“Kila teknolojia mpya huja na athari zake. Maendeleo ya teknolojia ya habari nayo yamekumbwa na hilo. Athari zake zimeanza kujitokeza.

“Maadili ya kitaaluma ni vyema yakazingatiwa na wote wanaojihusisha na upashanaji habari ili kuchangia maendeleo yaliyokusudiwa,” alisema Profesa Luoga.

Alihimiza wataalamu wa habari kuhudhuria makongamano ya kitaaluma yanayoandaliwa.

Sitakaa Nimwamini Mwanamke Maisha Mwangu

$
0
0
Nimeamini ule msemo wa mwanamke sio ndugu yako na sitakaa katika maisha yangu nimwamini mwanamke, sijaamini kama Frorah angemwacha Mbasha aingie jela ama kweli hujafa hujaumbika hivi kweli mwanaume hata kama mmekosana unaweza kukubali apelekwe jela, wanawake sio hawana ubinadamu...Naamini kabisa Flora alikuwa na uwezo mkubwa wa kuingilia hilo na kuyamaliza kinyumbani...Nahakika asilimia 100 Mbasha akifungwa Jela baada ya miaka kadhaa atajutia alichofanya cha kukaa na kuangalia mume wake akienda Jela Bila Msaada wowote....Flora angeibuka Shujaa Kama Angeibuka na Kufuta kesi na kuyamaliza kifamilia 
Je wewe Kwa hilo Unasemaje?

Kinachoendelea Simba Kinakatisha Tamaa

$
0
0
KAMA zilivyo klabu nyingine, klabu ya Simba nayo ina nafasi yake ya kipekee katika suala zima la maendeleo ya soka la Tanzania.
Simba kama zilivyo klabu nyingine nayo inatakiwa kuwa imara ili kutoa ushindani ambao utakuwa na maana kubwa katika kuifanya Ligi Kuu Bara iwe na msisimko na hivyo kuwa na mchango wake katika kuiinua soka la Tanzania.
Hata hivyo kwa mambo yanayoendelea Simba kwa sasa tuna hofu kama Simba itakuwa moja ya timu tishio kwenye Ligi Kuu Bara msimu wa 2014-15.
Kinachoendelea Simba kwa sasa hakitoi dalili zozote za Simba  itakayokuwa tayari kutoa ushindani kwenye Ligi Kuu na hata kujiwekea mazingira ya kucheza michuano ya kimataifa kwa kushika nafasi ya kwanza au ya pili katika ligi hiyo.
Wakati tunaandika makala haya bado hakuna uhakika wa wachezaji gani watakaoichezea Simba msimu ujao, kocha atakuwa nani na benchi la ufundi kwa ujumla litakuwaje.
Unaweza kuona hali ya aina hiyo katika klabu nyingine lakini ukweli ni kwamba kuna tofauti kubwa kwa kuwa klabu hizo kwani tayari zimeanza usajili, zimekamilisha au zinafanya mazungumzo na wachezaji, makocha na benchi la ufundi kwa ujumla.
Kwa Simba ni tofauti na yote hayo hayafanyiki kwa sababu moja tu. Uchaguzi! Inashangaza kuona kwamba uchaguzi ambalo ni tukio la siku moja linakuwa sababu ya kukwamisha mambo mengi ya Simba.
Hali hii hasa ndiyo inayotusikitisha na kutushangaza kibaya zaidi kama ambavyo tulisema katika maoni yetu toleo lililopita kwamba huu uchaguzi unaosubiriwa, kwa hali ilivyo sasa ni kama haujulikani lini utafanyika.
Wakati uchaguzi haujulikani, ligi inajulikana itaanza Agosti 24 mwaka huu, wakati uchaguzi haujulikani ukomo wa kusajili wachezaji wa Ligi Kuu Bara unajulikana.
Sambamba na yote hayo muda wa kocha kuandaa timu nalo ni jambo muhimu ambalo haliwezi kusubiri muda.
Hata hivyo wakati tukishangazwa na kusikitishwa na kinachoendelea Simba bado tuna wajibu wa kujiuliza anayeitwa Mkurugenzi wa Ufundi Simba, Moses Basena kwa sasa anafanya kazi gani?

Hapo ndipo unapobaini kwamba Simba imejiwekea mfumo mzuri lakini haitaki kuusimamia mfumo huo kwani tulidhani huu ungekuwa wakati wa Basena kufanya kazi ya benchi la ufundi hadi kocha mpya atakapopatikana.
Tulidhani huu ungekuwa wakati wa sekretarieti ya Simba kukaa na Basena na kuangalia mambo yajayo ikiwamo usajili, maandalizi ya ligi na kocha ajaye ambaye atakabidhiwa jukumu la kuinoa Simba.
Pia tulidhani huu ungekuwa wakati wa Simba kuandaa programu ya muda mfupi ili ianze kufanyiwa kazi na hatimaye iwe na matunda hata uongozi mpya utakapoingia madarakani.
Lakini yote hayo hayaangaliwi na kibaya zaidi ni kwamba hata viongozi waliopo madarakani hawataki kufanya lolote kwa ajili ya Simba ya baadaye kwa sababu ya uchaguzi.
Ukweli ni kwamba pamoja na umuhimu wa uchaguzi bado jambo hilo halitoshi kuwa sababu ya kusimamisha kila kitu ndani ya Simba.
Na kama kweli uchaguzi ni tatizo basi ni kwa nini kusiwe na programu ya muda mfupi ambayo itatumika kukamilisha baadhi ya mambo likiwamo hili la usajili ambalo katika Simba ni kama lipo njia panda.

KOLETA: Bado Nakula Ujana, Sina Mpango wa Kuolewa

$
0
0
Mwanadada kutoka tasnia ya filamu Bongo, Coletha Raymond ‘Koleta’ amesema kwamba suala la yeye kuolewa siyo la leo wala kesho na kwamba anakula ujana kwanza.

Akipiga stori na paparazi wetu juzikati, Koleta alisema kwa sasa hafikirii kabisa suala la kuingia kwenye maisha ya ndoa kwa kuwa, kila jambo na muda wake na bado Mungu hajamuonesha mwanawume wa kweli, ni bora akaendelea kuwa ‘singo’.

Kuolewa! Mmmh! Hapana kwanza, bado niponipo mpaka pale Mungu atakaponipa mwanaume sahihi wa kuwa naye. Ndoa kujipanga bwana, si kukurupuka tu, acha nile ujana kwanza,” alisema Koleta.

Arnold Kayanda 'Siku Hizi Vipindi vya Jioni Redioni Vimepungua Utamu, Huwezi Linganisha Tulivyokuwa Mimi na G-Habash

$
0
0
"Huyu ni ndugu yangu Captain Gardner G Habash. Juzi kati tulikutana kwenye radio mpya mjini , walituomba maoni mawili matatu kuboresha. Nimemkumbuka! Gardner nilipojiunga Clouds FM yeye alishakuwa maarufu sana. Tofauti na watu maarufu wa wakati huo, alinipa nafasi sana na hata akafikia kuwa ananifanya Co-captain mara moja moja. Siku moja aliniambia, "nataka kuondoka nitakuachia 'Kipindi'". Alipoondoka hawakunipa 'kipindi'. Baada ya miezi kadhaa waliniita 'niokoe Jahazi'. Watu wanasema nilivaa vizuri viatu vya G. Habash (Sidhani kama nilimfikia hata nusu). Ingawa kila mtu ana mtazamo wake lakini pengine utaniunga mkono kuwa siku hizi vipindi vingi vya jioni vimepungua utamu. Hakuna tena uchambuzi wa kina wa masuala nyeti unaofanyika kiburudani, hakuna tena Maelezo juu ya muziki yaliyokuwa matamu kuliko muziki wenyewe unaozungumziwa. I publicly #ThankYou Captain Gardner G Habash" 
Anold Kayanda

Diva 'Chege Alinilazimisha Kushiriki Katika Video yake Sikumuomba'

$
0
0
Diva 'Chege Alinilazimisha Kushiriki Katika Video yake Sikumuomba'

Wema Amchana Aliyemzushia Kuwa na Ujauzito wa Diamond

$
0
0
Miss Tanzania 2006 pia Actress mwanadada mwenye   nyota ya ajabu ambaye anakimbiza  hapa Tzee Wema Sepetu a.k.a Mrs .Nasibu Abdul alias Daimond Platinum  amemtaja mtu ambaye alimzushia kwamba anaujauzito kwenye mtandao mmoja wa kijamii uiitwao Instagram kuwa ni shabani amri ambaye anapatikana kwa jina ili(@shabani amri5)

Halafu usione nakaa kimya mkaona labda siumii kizazi ulinipa wewe?….. mpaka uniamrishe nizae…Sina kizazi sasa …kama unaweza nipe  nizae..Dah! nawavumilia tu …mi pia binadamu nina moyo…unahisi kwa akili yako sitaki mtoto  ama nini? …Zaa zaa zaa …kama wewe umebarikiwa  kuzaa hongera..Im tired of this kuzaa bullshit….!!!Leave me  and my Life alone “ aliandika wema kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Aibu! Mtaa Wafungwa Baada ya Jamaa Kunaswa Akila URODA na Mke wa Rafiki Yake Huko Mabibo

$
0
0
Mume aliyejulikana kwa jina moja la Ngosha, mkazi wa Mabibo jijini Dar, amemfumania rafiki yake aitwaye Jazira akiwa chumbani na mkewe Jack wakiivunja amri ya sita ya Mwenyezi Mungu.Tukio hilo lilitokea Jumanne iliyopita saa 12 alfajiri ambapo ilidaiwa kuwa Jack alikuwa chumbani na mwanaume huyo ambaye ni mpangaji, wenzake wakipeana maraha.

Imedaiwa kuwa, wawili hao walikuwa wakimtegea Ngosha akitoka kwenda katika shughuli zake, Jazira alikuwa akizama katika chumba cha rafiki yake na kufanya mchezo wa kikubwa.

Wapangaji wenziye na Jack wamedai kuwa, mke huyo wa mtu ambaye ana miezi miwili tangu aolewe kutoka mkoani Tabora, amekuwa kero katika nyumba hiyo kwani amekuwa akipiga kelele za kimahaba nyakati za asubuhi ambapo watu wengi wanakuwa wakielekea kazini.
“Hata sisi wanawake tunaoishi nyumba hiyo tuna waume zetu tunawalilia lakini kinachotusikitisha mwenzetu anamlilia Jazira badala ya mumewe ambaye anakuwa amekwenda kazini,” alisema mmoja wa wapangaji wa nyumba hiyo.

Imeelezwa kuwa, siku hiyo mlinzi wa msikiti alikwenda kumwamsha Ngosha kwenda kusogeza gari lake ili watu wapite na alipofika katika chumba chake, alikuta mlango wa sebuleni ukiwa wazi lakini hakukuwa na mtu, ila chumbani kwake kulisikika redio ikizungumza kwa sauti kubwa.

Jirani mmoja aliyedai kuchoshwa na tabia hiyo, alimshauri mlinzi huyo kwenda kusikiliza kwenye dirisha la chumba hicho na waliposikia sauti za kimahaba wakakubaliana wamtonye mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Kanuni, Mabibo aliyetajwa kwa jina la Asha ambaye alifika na kusikia ‘mchezo’ ukiendelea chumbani

Wakati huohuo, Ngosha akapigiwa simu kuja kushuhudia mchezo huo mchafu wa mkewe alioufanyia ndani ya chumba chake.
Mashuhuda wa tukio hilo walisema, alipofika Ngosha nyumbani na kutonywa kilichotokea  alipandwa na hasira na kuangusha varangati kwa rafiki yake lakini baadaye akatulizwa, akamtaka Jazira amlipe shilingi milioni 1.2 ili amuachie mke moja kwa moja.

JAZIRA ANA LAKI 2

Jazira alisema hakuwa na kiasi hicho isipokuwa anaweza kulipa shilingi laki mbili tu, jambo lililomfanya Ngosha kuomba msaada wa askari mgambo na kumpeleka mgoni wake Kituo cha Polisi cha Urafiki kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images