Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Nyambizi ya Ujerumani Iliyozama Wakati wa Vita vya Kwanza Vya Dunia Yapatikana

$
0
0
Nyambizi ya Ujerumani Iliyozama Wakati wa Vita vya Kwanza Vya Dunia Yapatikana
Mabaki ya nyambizi ya Ujerumani ambayo ilizama wakati wa vita vya kwanza vya dunia imepatikana huko North Sea na maafisa wanasema kuwa huenda bado miili 23 iko ndani ya manowari hiyo.

Nyambizi hiyo ya UB-II ambayo inatajwa kuwa katika hali nzuri iko mita 30 chini ya bahari nje wa pwani ya ubelgiji.
Video ya kwanza ya wanawake watumwa wa ngono yatolewa
"Nyambizi hiyo iko hali nzuri na tunaamini kuwa huenda miili yote bado imo," alise gavana wa West

Bw. Decaluwé aliwaambia waandishi wa hababri siku ya Jumanne kuwa eneo iliko nyambizi hiyo limewekwa siri kuzuia watu kulikaribia
Nyambizi 11 za Ujerumani kutoka kwa vita vya kwanza vya dunia zimepatikana katika maji ya Ubelgiji lakini chombo hiki kinatajwa kuwa kilicho katika hali nzuri zaidi.
Bomu kubwa la vita vya pili vya dunia kuharibiwa Ujerumani
Nyambizi za UB-II zilijengwa kati ya mwaka 1915 na 1916 na zilikuwa na uwezo wa kuzama hadi umbali wa mita 50.


Rais Magufuli Ameagiza Madini ya Tanzanite Kuwekewa Ulinzi na Jeshi

$
0
0
Rais Magufuli Ameagiza  Madini ya Tanzanite Kuwekewa Ulinzi NA Jeshi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza Jeshi la Wananchi kushirikiana na Suma JKT kujenga ukuta mkubwa kuzunguka eneo lenye madini ya Tanzanite na kuweka mitambo maalum, ili kulinda madini hayo yasiendelee kuibiwa.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo wilayani Simanjiro Mkoani Manyara ambako ameende kuzindua barabara ya lami iliyojengwa kwa bilioni 32.5 ya KIA- Manyara, na kusema kwamba ni lazima ulinzi huo uwekwe ili kuokoa rasilimali za Tanzania zisiendelee kuibiwa na nchi kubaki masikini.

"Eneo la Simanjiro kuanzia Block A mpaka Bolock D ambalo lina madini mengi, ninaagiza Jeshi la wananchi likishirikiana na Suma JKT, waanze kulijengea ukuta eneo lote, wataweka fensi juu na wataweka camera, patawekwa mlango mmoja na itawekwa mitambo maalum, hata kama utameza Tanzanite itaonekana, hata ukificha kwenye kiatu itaonekana", amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli atakuwepo mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku 3, ambapo pia atatoa kamisheni kwa maafisa waliohitimu mafunzo ya jeshi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Septemba 23, 2017.

Kosa Kubwa Alilofanya Diamond Platnumz Jana

$
0
0
Pole sana mdogo wangu Diamond Platinum. Binafsi ni mfuatiliaji wa muziki wako na hua nadiriki hata kununua nyimbo zako katika web yako.Mimi ni shabiki pia wa Swahiba wako Ally Kiba lakini lazima nikiri kwamba umemzidi mbali sana sio meendeleo tu hata plans zako hawezi kufika hata asimame juu ya kiti itachujua miaka kukufikia ulipo.

Tuachane na hayo ndugu twende kwenye point.Kati ya siku ambazo umeonyesha udhaifu mkubwa ni jana...Hukutakiwa kabisa kwenda kwenye media kukiri kwamba umezaa na yule binti(mubeto-sijui kma nimepatia spelling)

Ulitakiwa kukomaa mpaka dakika ya mwisho kwamba hujazaa nae, hii ingekusaidia kutunza heshima yako pamoja na kuimarisha ndoa yako.Wanawake wanaamini sana maneno kutoka kwa mwanaume.Zarinah asingeweza kukwambia kapime DNA hata kama mtoto angetoka copy right na wewe.Mwanamke ni mwepesi sana kusamehe kuliko mwanaume.

Kama ni kweli ulishamwambia Zari kuhusu mtoto wa nje basi hukua na haja ya kwenda kuatangaza aisee.Ona sasa kila mtu hata watoto wadogo wamejua kwamba ulimsaliti mkeo(japo not official) lakini navojua huu mwaka wa nne kama sio wa tatu uko na huyo mama(zarinah).Wanawake wanataka heshima, wanataka kuthaminiwa.Ikiwa umeweza kwenda na yule mdada chumbani unapolala na yule mama hataweza tena kukuamini.Umemvua nguo kabisa aisee.Hana hamu tena ya kuja Tz, yale mapicha picha airport sidhani kama atapiga tena.

Zile show off zenu nadhani hazitakuwepo tena.Naanza kuona mwisho wa uchumba wenu.

Sasa yule mama atakugeuza anavotaka.Tegemea kulia sana katika swala la mapenzi.

Mdogo wangu bado kidogo ufikishe miaka 30.Karibu sana katika umri huu kijana.Sisi wengine tuna uzoefu sana katika haya mambo.Hata tukutwe live tunakana kwamba sio kweli na tunasamehewa.

Sina hakika kama ushauri wa wewe kwenda kwemye media uliutoa kwa Babu tale ama fella.

Maana naamini wao ni wajuzi zaidi wa haya mambo na hivo wasingekushauri kwenda kutangaza kama vile unaomba msamaha watanzania.

Sisi tunaweza kukusamehe lakini yule mama hawezi kabisa.Atakutesa sana mi nakushuri bora uachane nae kabisa aise.Tegemea kuona mapicha ya uchi na clips za mitombo akiwa na majamaa halafu uchune tu maana tayar ushamchafua kwa hiyo atalipiza.

Kumbuka hana cha kupoteza hata akiachana na wewe.Yeye sio hao wanaotaka elfu 70 kwa siku yeye anapesa yake.

Ulitakiwa kuomba ushauri kwa wakubwa na wazoefu wa mambo kabla hujaenda kukiri mbele ya watanzania mil 24 wapiga kura wenye akili timamu na above 18 waliokua leo hii wanakuangalia unapuyanga.
Tegemea heshima yako kushuka sana mwaka huu.

Mubeto hana tofauti na akina Giggy na amber lulu sijui, ambao ni kama day-waka.Kwamba apate deal ndio aingize mkwanja au afanya vibiashara vidogo vya mission town apate mshiko.

Sasa hivi atakufanya wewe kitega uchumi.Nimesikia umesema anataka mil 5 kila mwezi(What)?.kwa maana nyingine ni kwamba kale ka faidi kote kwenye biashara zako za nguo atakua anachukua mubeto.

Hili ni kosa kubwa sana na pengine siku hii hutaisahu.Hakukua na haja yoyote ya wewe kutangaza ingebaki kama tetesi tu.

Hata kama alivujisha picha, you could tell zarinah kwamba , she was ma chick by then kwisha!.Kwani wanagapi wana zalishwa na kuachwa wanakua ma single mother?.

Kama mtoto si unao wawili?.Ulishindwa nn kumhudumia kimya kimya.Alichotaka yule mubeto ni kujulikana kwamba kazaa na wewe lakini pia alipata sapoti kubwa kutoka kwa ma x wako, huu mchezo uliujua lakini umeingia king.Wao daima hawafurahi kabisa wewe kua na yule mama maana ni kama vile umewadharau baada ya kuwamega na kuwaacha.So lengonlao uharibikiwe na ndo wanafanikiwa hivo.

Kulikua na maandalizi ya kufungua kesi kwamba umemkana mtoto lakini pia ungeweza kumhudumia mtoto but sio kwa mil 5 kwa mwezi!

Unaenda kufilisika bro niamini.Najua utasema kwamba oohh unapiga hela ndefu lakini siongelei hela naongelea saikolojia yako kwa sasa itakunyima raha miaka na miaka na hii itakutafuna niamini.

Na kama ikitokea yule bibi akaghairi ushirikiano na wewe please usije kufanya kosa kumrudia yeyote kati ya wale ulioisha wapitia.Hawatakua na jipya zaidi ya kukufilisi, ni bora umfuate yule wa big brother kama ni kweli ulimpiga pia. Aisee ila na wewe hatari.


Museveni Ataka Upelelezi Ufanyike Kubaini Sababu ya Ajari wa Watu 13 wa Familia Moja

$
0
0
Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema upelelezi kubaini sababu za ajali iliyosababisha vifo vya Watanzania 13 waliokuwa wakitoka harusini nchini humo unaendelea.

Waziri wa Ofisi ya Rais anayeshughulikia Jiji la Kampala, Bety Kamya akisoma salamu za rambirambi kutoka kwa Rais Museveni amesema licha ya kutoa pole kwa familia, kiongozi huyo ameagiza uchunguzi wa sababu za ajali ufanyike.

Amesema pia amewapongeza maharusi, Dk Aneth na Dk Trease Ibingira na amewatakiwa maisha mema ya ndoa.

Mbali ya hilo, amesema anawaombea ili kukabiliana na kipindi kigumu walichonacho.

Amesema Rais anawashukuru Watanzania kwa kuwa wavumilivu katika kipindi kigumu cha kupoteza wapendwa wao.

"Nakabidhi vyeti hivi vya vifo vya ndugu zetu 13 nawapa pole sana," amesema Waziri Kamya akimkabidhi vyeti hivyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angellah Kairuki.

Waziri Kairuki amesema Rais John Magufuli amepokea taarifa ya vifo hivyo kwa mshtuko na alitoa maelekezo ya kupokewa miili hiyo, kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Jeshi Lugalo, kuagiwa hapo na kusafirishwa kwa maziko.

Amesema maagizo hayo wanaendelea kuyatekeleza ikiwa ni pamoja na kutoa magari kwa ajili ya kusafirisha miili hiyo.

Waziri Kairuki amesema kwa namna isiyo katika wakati wa kawaida, anawapongeza maharusi na kuwatakia maisha mema.

"Haya ni mapenzi ya Mungu, hili lisiwanyong'onyeshe maharusi," amesema Kairuki.

Ameishukuru Serikali ya Uganda kwa kukodi ndege kuirudisha nyumbani miili hiyo.

Heche Awatupia Lawama Polisi Kumchukua Kubenea Hospitali Kwaajiri ya Kuhojiwa

$
0
0
Heche Awatupia Lawama Polisi Kumchukua Kubenea Hospitali Kwaajiri ya Kuhojiwa
Mbunge wa jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA, Saed Kubenea ameshindwa kuhojiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge kufuatia hali yake kuwa mbaya na kulazwa katika Dispensary ya bunge mjini Dodoma.

Kubenea alikamatwa na polisi jijini Dar es Salaam jana na kupelekwa Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama  ya Bunge lakini ameshindwa kuhojiwa kufuatia hali yake kiafya kutokuwa nzuri jambo lililopelekea kulazwa.

Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche amethibitisha hilo na kulilaumu jeshi la polisi kumkamata Saed Kubenea akiwa hospitali ili tu aende kuhojiwa Dodoma.

"Baada ya Mhe. Kubenea kufikishwa Dodoma ameshindwa kuhojiwa kwasababu imethibitika anaumwa sana na sasa yuko Dispensary ya bunge amelazwa. Ni aibu kwasababu inatumika nguvu kubwa na gharama bila sababu ili tu kuwaumiza wabunge wa upinzani. Polisi wanamchukua mbunge kutoka hospital kisa wito wa kamati ambayo maamuzi yake ni mwezi wa kumi na moja, vitendo hivi vya kinyama tunavyofanyiwa hata serikali za wakoloni hawakuwafanyia watu weusi" alisema John Heche

Kubenea Ashindwa Kuhojiwa na Kamati ya Bunge Alazwa Katika Zahanati ya Bunge

$
0
0
Kubenea Ashindwa Kuhojiwa na Kamati ya Bunge Alazwa Katika Zahanati ya Bunge
Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea amepelekwa katika zahanati ya Bunge baada ya kujihisi vibaya.

Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde amesema leo Jumatano kuwa, Kubenea amefika mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na amewaeleza kwamba hali yake si nzuri.

Kutokana na hilo, amesema amepelekwa kwenye zahanati hiyo na hali yake itakapoimarika atahojiwa na kamati.

Mbunge huyo ambaye alipelekwa Dodoma kwa ndege leo asubuhi, jana Jumanne alisema alikuwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay  wilayani Kinondoni akisubiri utaratibu wa safari hiyo ya kwenda kuhojiwa kama Spika wa Bunge Job Ndugai alivyoagiza.

Niyonzima Yupo Fiti Katika Mpambano wa Kesho Dhidi ya Majimaji

$
0
0
Niyonzima Yupo Fiti Katika Mpambano wa Kesho Dhidi ya Majimaji
Mshambuliaji wa Simba Haruna Niyonzima amefanya mazoezi na kikosi cha Simba kwenye Uwanja wa Kirumba leo Jumatano kujiandaa na mchezo wa kesho dhidi ya Mbao FC.

Niyonzima hakuweza kucheza mechi iliyopita dhidi ya Mwadui iliyofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kutokana na kuwa majeruhi.

Wachezaji wengine wawili watakaokosa mchezo wa kesho ni Shomari Kapombe na Said Mohammed Nduda pamoja na Bukabu Bundara ambaye ana matatizo yake binafsi.

Askari wa JWTZ Auwawa kwa Kupigwa Risasi

$
0
0
Askari wa JWTZ  Auwawa kwa Kupigwa Risasi
Askari wa jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) aliyefahamika kwa jina la Praivate Mussa Jumanne Muryery ameuawa kwa kupigwa risasi na kundi la waasi akiwa kwenye ulinzi wa Amani nchini DRC Congo.

Kwa mujibu wa taarifa ya (JWTZ) inasema kuwa askari wake huyo alifariki Septemba 17, 2017 na kufuatia shambulio hilo Umoja wa Mataifa umeunda bodi ya uchunguzi kuchunguza tukio hilo.


Mahakama Imewaachia Huru Vigogo wa Mabasi Yaendaayo Kasi

$
0
0
Mahakama Imewaachia Huru Vigogo wa Mradi wa Mabasi Yaendaayo Kasi
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru vigogo watatu wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka(DART), akiwemo mtendaji mkuu wa mradi huo, Asteria Mlambo na mwenzao.

Akitoa hukumu hiyo leo Jumatano ni Hakimu Mkazi Mkuu, Respicious Mwijage amesema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi 10 wa upande wa mashtaka, vielelezo na ushahidi wa upande wa utetezi ameona upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka yote yaliyokuwa yakiwakabili vigogo hao pasipo kuacha shaka.

Mbali na Mlambo wengine walioachiwa huru ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Evodius Katale, Mwanasheria Mkuu wa DART, Francis Kugesha na mkurugenzi wa kampuni ya Yukan, Yuda Mwakatobe.

Washtakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kusababisha hasara ya Sh 83.5 milioni.

Katika kesi hiyo ilidaiwa kuwa Septemba Mosi na Oktoba Mosi, mwaka 2013 maeneo ya  Kinondoni Dar es Salaam, Mlambo, Katale na Kugesha wakiwa wafanyakazi wa mradi huo, walishindwa kutekeleza majukumu yao vizuri na kuisababishia Serikali hasara ya Sh 83.5 milioni.


Mahakama ya Juu Nchini Kenya Imetoa Sababu za Kufutwa Matokeo ya Urais

$
0
0
Nibu jaji mkuu nchi Kenya Philomena Mwilu, amesema kuwa kushindwa kwa IEBC kufuata agizo la mahakama kuhusu madai yaliyoibuliwa na upinzani, inaonyesha kuwa madai ya udukuzi yalikuwa ni ya ukweli.

Jaji Mwilu amesema mahakama ilikubaliana madai ya upinzani kuwa matokeo yalitangazwa kabla ya matokeo yote kutoka kwa vituo 40,000 kupokelewa.
"Uchaguzi haukuwa na uwazi na hatukuwa na lingine ila kuufuta," jaji alisema.
Jaji Mwilu amesema tume ya IEBC ilitegemea ripoti za waangalizi wa uchaguzi kuamua kuwa uchaguzi ulikuwa wa haki.

Waangalizi walikosolewa vikali wakati uchaguzi ulifutwa kwa kuharakisha kusema kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wenye uwazi.
Kwa upande wake jaji mkuu nchini Kenya David Maraga, amesema kuwa upinzani hakubaini madai yao kuwa kampeni za rais zilitumia fedha za umma kugharamia kampeni zao.
Jaji Maraga amesema kuwa sampuli kadha za fomu zilionyesha kuwa hazikuwa na mihuri rasmi, zingine hazikwa na sahihi na namba za usajili wala alama rasmi.
Amesema kuwa uchaguzi haukufutwa tu kwa sababu ulikuwa na hitilafu, lakini kile amekuwa akikichunguza ni ikiwa hitalafu hizo zilishawishi matokeo.

Iren Uwoya Avutiwa na Mwanaume Mwenye Ngeu Afunguka Bwana Wake Kuwa na Ngeu za Visu

$
0
0
Iren Uwoya Avutiwa na Mwanaume Mwenye Ngeu Afunguka Bwana Wake Kuwa na Ngeu za Visu
Msanii wa kike wa filamu za bongo ambaye pia aliwahi kuolewa na mcheza mpira kutoka Rwanda, mlimbwende Irene uwoya, amesema mpenzi wake wa sasa ana ngeu nyingi mwilini za kuchanwa visu.

 Irene amesema watu kama hao ndio anaowataka yeye kwani inaonyesha uanaume halisi, na sio mwanaume anakuwa laini kama mtoto wa kike.
"Sijasema napenda wanaume wenye sura mbaya nimesema napenda mwanaume mwenye sura ya kiume, mwanaume uwe na ngeu, mimi bwana wangu ana ngeu, kachanwa visu yani", alisikika Irene Uwoya akimfungukia Big Chawa.
Irene uwoya kwa sasa hajaweka wazi mahusiano yake tangu kuwe na tetesi za kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Msami na amesema hataweka tena mahusiano yake wazi kwa watu.

Mabomu ya Machozi Yarindima Kuwasambaza Wakazi wa Bonde la Msimbazi

$
0
0
Mabomu ya Machozi Yarindima Kuwasambaza Wakazi wa Bonde la Msimbazi
Jeshi la Polisi limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wakazi wa bonde la mto Msimbazi waliokuwa wakipinga kubomolewa makazi yao, na kuwakamata watu takriban 20 wakihusika kufanya vurugu hizo.

Tukio hilo limetokea Septemba 20, 2017  kwenye bomoabomoa ambayo inatekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, yenye lengo la kuandaa eneo ili kupisha mradi mkubwa wa majitaka katika manispaa hiyo.
Wakazi wa eneo hilo wamelalamikia zoezi hilo na kuiomba serikali kuwaonea huruma kwani hawana mahali pengine kwa kwenda kujisitiri.                      
Pamoja na hayo pia eneo hilo la Jangwani lilishapigwa marufuku kwa wananchi kujengwa makazi, kwani ni eneo hatarishi kutokana na kuwa kwenye mkondo wa mto Msimbazi ambao nyakati za masika hufurika.

Yanga Wamaliza Mgomo Waanza Kujinoa kwa Mashambulizi

$
0
0
Yanga Wamaliza Mgomo Waanza Kujinoa kwa Mashambulizi
KIKOSI cha Yanga kimemaliza mgomo wa siku moja waliouweka jana Jumanne kwa kugomea mazoezi kutokana na kuwa na malimbikizo ya mishahara na posha za baadhi ya mechi ingawa wenyewe hawakutaka kuweka wazi.

Ofisa Habari wa Yanga, Dismas Ten alisema wamemaliza mgomo waliouweka wachezaji hao na leo Jumatano walifanya mazoezi kama kawaida katika Uwanja wa Uhuru.

“Tulikuwa kwenye kikao jana cha muda mrefu na tumeingia makubaliano na wachezaji na tumekubaliana kila kitu na ndio maana leo wamefanya mazoezi kama kawaida,” alilisema Ten.

Kikosi hicho kamili leo Jumatano asubuhi walifanya mazoezi kwenye uwanja wa Uhuru kujinoa na mchezo wao na Ndanda wikiend hii.

BAVICHA Yatangaza Kufanya Maandamano

$
0
0
BAVICHA Yatangaza Kufanya Maandamano
BARAZA la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha) Mkoa wa Kagera limetangaza kuandaa maandamano ya amani kulaani tukio la kushambuliwa kwa risasi Mwanasheria Mkuu wa chama chao, Tundu  Lissu  Septemba 7, mwaka huu.

Mwenyekiti wa Bavicha Manispaa ya Bukoba,  Ishengoma Audax alisema licha ya kuandamana watakwenda katika Hospitali ya Rufaa Bukoba kuchangia damu.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Kagera, Francis Rutta alisema wameamua kuandamana kulaani kushambuliwa kwa Lissu na kuvitaka vyombo vya dola kuhakikisha vinawakamata na kuwatia mbaroni wahusika.

“Tunafanya maandamano ya amani hivyo hatutegemei polisi kuzuia maandamano yetu kwa kuwa ni ya amani.

“Lakini tunaunga mkono uamuzi wa Brlaza Kuu la Taifa Bavicha linaloongozwa na Mwenyekiti Patrobas Katambi,” alisema.

Alisema wamekuwa wakishangazwa na hatua ya polisi kuwazuia wananchi kumuombea Tundu Lissu ikiwa ni pamoja na kukamatwa kwa makada wa chama chao waliovaa fulana zenye ujumbe wa kumuombea.

Alisema  huo ni ukiukaji mkubwa wa demokrasia

Mllinzi wa Makaburi, ‘bebi’ Anaswa kwa Mauaji

$
0
0
Mllinzi wa Makaburi, ‘bebi’ Anaswa kwa Mauaji
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia watu wawili akiwemo mlinzi wa makaburi ya Wangazija yaliyopo Upanga, Mohamed Maganga (61) wakiwa na bunduki mbili aina ya Uzigun na Riffle, bomu la kurusha kwa mkono na risasi 167.

Mbali na Maganga ambaye ni mkazi wa Pugu, mtuhumiwa mwingine aliyekamatwa ni Rahma Almas maarufu Baby (37) ambaye alikiri kuhifadhi silaha hizo zilizotumika katika matukio mbalimbali ya uhalifu, ikiwemo mauaji ya Mkurugenzi na Mwanzilishi-Mwenza wa Shirika lisilo la kiserikali la PALMS Foundation, Wayne Lotter (52).

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa alisema watuhumiwa hao walikamatwa Septemba 16, mwaka huu saa 11:50 jioni, maeneo ya makaburi ya Wangazija yaliyopo Upanga.

“Mtuhumiwa huyo (Baby) aliwaelekeza askari kuwa silaha hizo amezificha katika makaburi hayo, ndipo askari walifika eneo la tukio na mtuhumiwa ambapo walizikuta silaha hizo mbili moja ikiwa ni aina ya Uzigun na Riffle ambayo imekatwa mtutu na kitako chake na namba zikiwa zimefutwa zote huku zikiwa zimefukiwa kwenye shimo,” alifafanua Kamanda Mambosasa.

Alisema Maganga alisaidia kuchimba shimo na kuzilinda silaha hizo na katika mahojiano, alikiri silaha hizo zililetwa na Rahma, lakini hakutoa taarifa hadi alipokamatwa. Alisisitiza kuwa watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Katika hatua nyingine, jeshi hilo linawashikilia watu watano wanaotuhumiwa kuvunja ofisi za Kampuni ya Mawakili ya Prime Attorneys inayomilikiwa na mmoja wa mawakili wa mfanyabiashara maarufu Yusuf Manji, Hudson Ndusyepo.

Kamishna Mambosasa alisema Septemba 12, mwaka huu walipokea taarifa za kuvunjwa kwa ofisi za mawakili hao na kuibwa kasiki iliyokuwa na fedha taslimu Sh milioni 3.7, kompyuta mpakato na nyaraka mbalimbali za wateja wao.

Aliwataja watuhumiwa waliokamatwa ni Said Salehe (47) mkazi wa Mbezi Louis, Mustapha Said (35) mkazi wa Magomeni Mwembechai, Somfi Somfi (52) mkazi Magomeni Mapipa, Iman Mhina (36) mkazi wa Kimara Mwisho na Hussein Suleiman (45) mkazi wa Kigogo Mbuyuni.

“Katika mwendelezo wa tukio hilo watuhumiwa watano wamekamatwa baada ya operesheni kali ya kuwatafuta waliovunja ofisi hiyo ya Prime Attorneys ambao wamekamatwa maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam,” alieleza.

Alifafanua kuwa baada ya mahojiano watuhumiwa hao walikiri kushiriki tukio hilo na kuonesha kasiki la fedha pamoja na mitungi mitatu ya gesi iliyotumika kukatia kasiki hilo. Kwa mujibu wa kamanda huyo, watuhumiwa hao walienda Magomeni Mapipa, Mtaa wa Dosi kwa mtuhumiwa aitwaye Somfi na baada ya kulifungua na kukuta hakuna fedha, walilichukua na kulitelekeza eneo la Kigogo daraja la Madaba.

Alisema upelelezi unaendelea ili kuwabaini watumiwa wengine walioshiriki katika tukio hilo. Wakati huo huo, watuhumiwa watatu wa ujambazi akiwamo anayejulikana kwa jina la Shafi aliyetoka gerezani hivi karibuni kwa rufaa akitumikia kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha, wamefariki dunia kutokana na majibizano ya risasi walipokwenda kufanya uhalifu kwenye ghala lililopo maeneo ya Tazara.

Mtuhumiwa mwingine anayejulikana kwa jina la Babu Jaffari ambaye ana matukio mbalimbali ya unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo, ambaye kwa mara ya mwisho alikuwa akiripoti Kituo cha Polisi Chang’ombe na mtuhumiwa Mbegu maarufu kama Malon ambaye anatafuta kazi za kupora.

“Majambazi hao walifariki wakati wanapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu baada ya kuvuja damu nyingi na msako mkali unaendelea kumsaka jambazi aliyetoroka na gari waliotumia majambazi hao,” alieleza.

Akielezea tukio hilo, alisema Septemba 15, mwaka huu, saa 11:20 jioni maeneo ya Vingunguti- BECCO Mkoa wa Kipolisi Ilala, askari wa kikosi cha kupambana na ujambazi walipata taarifa kuwa kuna majambazi wanakwenda kufanya tukio la kiuhalifu kwenye moja ya maghala yaliyopo maeneo la Tazara.

Aidha, alisema askari waliweka mtego na kulisimamisha gari aina ya Toyota Mark II rangi ya blue, ambalo namba zake za usajili hazikufahamika na baada ya kugundua kuwa askari wanawafuatilia majambazi hao, walianza kuwashambulia askari kwa risasi ndipo askari wakajibu mashambulizi na kuwajeruhi.

Alisema eneo la tukio palikutwa bastola moja aina ya Browning yenye risasi tatu moja, ikiwa chemba tayari kwa kutoka maganda matatu ya risasi zilizofyatuliwa kutoka katika bastola ya majambazi.

Zari Azidi Kutoa Povu Ajiliwaza na Mkwanja Wake Uliojaa Banki

$
0
0
Zari Azidi Kutoa na Povu Ajiliwaza na Mkwanja Wake Uliojaa Banki
KUFUATIA sakata la mzazi mwenziye kuchepuka na kuzaa na mwanamitindo maarufu Bongo, mwanamke shupavu na mjasiriamali, Zarinah Hassan ‘The Boss Lady’, amesema hakuna cha kumliza juu ya sakata hilo kwani akaunti yake benki imejaa mkwanja wa kutosha.

Zari alitoa povu kwenye komenti aliyomjibu shabiki wake ambaye alikuwa akimuonea huruma na kusema kwamba anajua kuwa ameumizwa sana na kitendo hicho cha ‘Baby’ wake kuzaa na Hamisa Mobetto, sema tu analilia kwa ndani.

Mpaka saa Zari bado hajaweka wazi kuwa ataendelea na mzazi mwenziye huyo ambaye ni mwanamuziki wa Bongo Fleva, au atachukua hatua gani, ikiwa ni siku moja tu imepita tangu mzazi mwenziye huyo akiri hadharani kuwa mtoto wa Mobetto ni wake.

Maskini Mbowe...Anyoosha Mikono na Kudai Kazi ya Upinzani Awamu ya Tano ni Ngumu

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe ameleeza kuwa kazi ya upinzani ni ngumu sana.

Mbowe amesema kuwa licha ya vitisho na kila aina ya hujuma wanazofanyiwa kamwe hawawezi kurejea nyuma.

Kazi ya Upinzani ni ngumu, hasa katika zama za utawala wa awamu ya tano, ambae inaonekana hatambui na kuthamini mchango wa Wapinzani kama walivyokuwa watangulizi wake.
Licha ya vitisho na kila aina ya hujuma tunazofanyiwa kamwe hatuwezi kurejea nyuma, bali tutafanya kazi zetu kwa tahadhari kubwa kuliko ilivyokuwa miaka ya nyuma ambapo tulikuwa na Uhuru mkubwa wa kujieleza na Serikali kufanyia kazi mambo tunayosema.
Huwezi kuendesha nchi bila kuruhusu ukosoaji, iwe kutoka upinzani au kwenye chama unachokiongoza, unapowazuia watu wasipumue na kutoa madukuduku yao, unatenegeneza hasira kubwa ndani ya jamii.

Mbunge Tundu Lissu yupo mjini Nairobi Kenya kwenye matibabu kufuatia kupigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma.

Magufuli 'Mungu Ametupa Madini Lakini Hayatusaidii Tunapata Shida tu'

$
0
0

Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee iliyobarikiwa na mwenyezi Mungu kuwa na madini ya Tanzanite duniani, lakini madini hayo bado hayatusaidii kwa chochote kwani matatizo bado yapo pale pale.

“Kuna changamoto nyingi zinazolikabili taifa letu, Changamoto zipo zingine ambazo tumezidekeza sisi wenyewe, ni kwa sababu tumeshindwa kusimamia rasilimali zetu, nchi hii ni tajiri, na nyinyi ndugu zangu wa Simanjiro ni mashahidi, kwamba nchi hii ni tajiri, historia ya dunia hii inazungumza wazi kwamba wananchi wa Simbanjiro na Tanzania tulipendelewa na mwenyezi Mungu tukapewa madini ambayo hayapo mahali kokote kwenye dunia hii. Nenda Marekani, nenda Uingereza, nenda Urusi, nenda China, hakuna madini yanayoitwa Tanzanite yanachimbwa, yanachimbwa hapa Mererani, lakini tujiulize sisi wote Watanzania na Wanamererani haya madini yanatusaidia sisi? Mungu ametupa madini lakini sisi tunapata shida.“amesema Rais Magufuli leo asubuhi wakati akihutubia wakazi wa Simanjiro.

Rais Magufuli leo jumatano ameanza ziara yake mkoani Arusha ambapo amefungua barabara ya Lami kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) hadi Mererani wilayani Simanjiro

Mtatiro: Amri ya kumkamata Zitto yatolewa..Lakini Mbona Hatuoni Bunge Likiwahoji Wakuu wa Taasisi Mbali Mbali Kwa Utendaji Mbovu?

$
0
0
Katibu wa Bunge, mhe. Kashililah ameviagiza vyombo vya dola vimsake kumkamata na kumfikisha mhe. Zitto Kabwe mbele ya kamati ya maadili Dodoma. Mimi najiuliza bado, hivi hii ndiyo kazi kubwa ya bunge kikatiba?

Mbona hatuoni Bunge likimuita na kumuhoji Waziri wa Fedha na Gavana wa Benki Kuu kwa kuchukua Mkopo wa Trilioni 1.2 bila kulihusisha bunge na tena mkopo wenyewe ukiwa ghali na malipo yake ni "damu na jasho" za wanachi?

Mbona hatuoni Bunge likiwahoji wakuu wa taasisi mbalimbali za serikali kwa uzembe na utendaji mbovu?

Mbona hatuoni Bunge likimhoji RPC wa Dodoma kwa hadi leo kushindwa kuwakamata watu waliompiga risasi Tundulisu mchana kweupe tena kwenye eneo lililokuwa linapaswa kulindwa kwa uhakika?

Yani tunashuhudia bunge ambalo kazi yake kuu ni kupambana na wabunge wake, kuwadhalilisha, kuwaogofya, kuwashughulikia na kuwaumiza. Hili ni Bunge la Tanzania kwa mujibu wa katiba?

By Julius S. Mtatiro

Bunge Lafunguka, Ndugai Haendeshwi na Serikali Kama Wasiasa Wanavyodai

$
0
0
Bunge la Tanzania limetoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali na kusema Spika wa Bunge, Ndugai haendeshwi na serikali kama ambavyo wanasiasa wamekuwa wakisema na kudai watu hao wanalenga kumchafua, kumshambulia Spika wa Bunge na kumkosanisha na wananchi.

Katika taarifa iliyotolewa Septemba 20, 2017 na Bunge imesema kuwa kitendo cha viongozi hao kusema bunge la kumi na moja halina meno, halitekelezi wajibu wake na kudai kuwa bunge hilo na Spika wa Bunge wanaendesha na serikali si kweli kwani ni uongo na uzushi wenye lengo la kulichafua bunge pamoja na Spika wa Bunge Job Ndugai.

Mbali na hilo taarifa ya bunge imeweza kutolea ufafanuzi wa mambo mbalimbali ikiwepo kauli ya kusema bunge la sasa linaendeshwa kibabe, limetolewa ufafanuzi kuhusu sakata la matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu pamoja na baadhi ya viongozi kufikishwa kwenye Kamati mbalimbali za Bunge kwa ajili ya mahojiano.

Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images