Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Diamondi Ajivunia Kuwa Baba wa Watoto Watatu Atupa Dongo kwa Waliomwita Mgumba

$
0
0
Diamondi Ajivunia Kuwa Baba wa Watoto Watatu Atupa Dongo kwa Waliomwita Mgumba
Ni kweli ukitaka kumuuwa paka lazima ufanye kazi kwa kuwa ana ‘roho saba’? Basi inawezekana kumteketeza Diamond lazima ufanye kazi pia.
Msanii huyo amewajibu wabaya wake kupitia mtandao wa Instagram, baada ya kuonekana kuibuka mshindi katika vita ya mtoto aliyezaa na mrembo Hamisa Mobetto.

Daimondi ameandika hivi kupitia instagramu yake “Chawa KATU hauliwi kwa DOLE GUMBA…… Leo kawa Baba WATATU yule walomuitaga MGUMBA….”🔥🔥


Korea Kaskazini Yaifananisha Hotuba ya Trump na Mbwa Anayebweka

$
0
0
Korea Kaskazini  Yaifananisha Hotuba ya Trump na Mbwa Anayebweka
Mwanadiplomasia wa cheo cha juu wa Korea Kaskazini ameifananisha hotuba ya Trump kwa Umoja wa Mataia na kibweko cha mbwa.
Akihutubia baraza kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatano, Bw Trumo alisema kuwa ataiharibu Korea Kaskazini ikiwa itakuwa tisho kwa Marekani na washirika wake.

Matamshi ya waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Ri Yong-ho, ndiyo ya kwanza rasmi ya Korea Kaskazini tangu hotuba ya Trump

Korea Kaskazini imendelea na mpango wake wa nyuklia na kukiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa.
"Ikiwa Bw Trump anafikiri kuwa atatuletea hofu kwa sauti ya mbwa anayebweka basi hiyo kwake ni ndoto."

Akizungumza kuhusu kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jon-un, Bw Trump aliuambia Umoja wa mataifa kuwa Bwana Kim ako katika mikakati ya kujitia kitanzi.

Bwana Ri anatarajiwa kutoa hotuba yake kwa Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa.
Wataalamu wanasema kuwa Korea Kaskazni imaharakisha mipango yake ya kuunda makombora ya masafa marefu na mipango yote ya nyuklia.

Tarehe tatu Septemba Korea Kaskazini ilitangaza kuwa imefanya jaribio lake la sita la nyuklia.

Mbao FC Imeahidi Kuichakaza Simba na Kubeba Pointi 3 Leo

$
0
0
Mbao FC Imeahidi Kuichakaza Simba na Kubeba Pointi 3 Leo
Klabu ya Mbao FC kutoka jijini Mwanza imeahidi leo kuchukua ushindi dhidi ya Simba na kubeba pointi tatu katika mchezo wa Ligi Kuu Bara unaochezwa leo katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mbao FC ambao wao ni wenyeji wa mchezo wamejigamba kushinda mchezo huo kwa kutumia nafasi ya wenyeji wao kuigalagaza klabu ya Simba ambayo nayo imetinga jijini Mwanza toka mwanzoni mwa wiki kujiandaa dhidi ya Mbao FC.

"Siku ndio leo vijana wenu tunajitupa Uwanjani kuumana na Simba kwenye Ligi Kuu ya Vodacom. Jitokezeni kwa wingi CCM Kirumba kutupa hamasa vijana wenu ili kuhakikisha mnyama anakaa mapema. Mechi itakuwa ngumu lakini sisi ndio wenyeji kwa hiyo tuna kila sababu ya kushinda maana mcheza kwao hutunzwa" Imesema taarifa ya Mbao FC

Klabu ya Mbao FC ni kati ya klabu ambayo iliipa shida Simba msimu uliopita katika mechi walizokutana ambapo Simba alishinda mechi hizo lakini ni kwa shida sana.

Wanasheria wa Uingereza Watuma Waraka Mzito kwa Rais Magufuli Baada ya Tukio la Kushambuliwa kwa Risasa Tundu Lissu

$
0
0
Wanasheria wa Uingereza Watuma Waraka Mzito kwa Rais Magufuli Baada ya Tukio la Kushambuliwa Risasa Tundu Lissu
KUFUATIA matukio ya kukamatwa mara kadhaa na baadaye kupigwa risasi na watu wasiojulikana kwa Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), Chama cha Wanasheria cha Bar Human Rights Comitee cha nchini Uingereza, kimetuma waraka mzito kwa Rais wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Magufuli.
Sehemu ya waraka huo imelaani vikali matukio hayo na kutaka chombo huru kipewe nafasi ya kufanya uchunguzi. Nakala ya waraka huo imetumwa pia kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, IGP, Spika, na Jaji Mkuu wa Tanzania.


Bondia Jake LaMotta Afariki Akiwa na Miaka 95

$
0
0
Bondia Jake LaMotta Afariki Akiwa na Miaka 95
Bondia wa zamani wa uzito wa kati na mchekeshaji Jake LaMotta,amefariki dunia akiwa na miaka 95.
Mke wake amesema LaMotta amefariki nyumbani kwake kwa ugonjwa wa homa ya mapafu.
Alikuwa mpiganaji maarufu zaidi miaka ya 40 na 50.
Atakumbukwa kwa uvaaji wa kaptula yenye mistari ya chuichui na wakati fulani alikua akiingiza uchekeshaji wakati akipigana jambo lililomfanya mpinzani wake kuishia kucheka na yeye kushinda.

Rooney Kukatwa Mshahara wa Wiki Mbili na Klabu ya Everton

$
0
0
Rooney Kukatwa  Mshahara wa Wiki Mbili na Klabu ya Everton
Klabu ya Everton ya nchini Uingereza imemlima adhabu ya kukatwa mishahara ya wiki mbili mshambuliaji wake Wayne Rooney kufuatia kukutwa na kosa la kuendesha gari akiwa amelewa.
Fedha hizo zitapelekwa kwenye kituo cha watu wenye uhitaji maalum.
Everton ina mradi wa kusaidia watu wasiojiweza na imesema fedha hizo zitasaidia sana.
Rooney mwenye miaka 31 aliomba kusahemewa ili aepuke adhabu hiyo.
Siku ya Jumatatu alikuhumiwa kutoendesha gari kwa miaka miwili baada ya kukamatwa Septemba 1 akiwa anaendesha gari huku amelewa.
Atafanya pia kazi za jamii kwa siku mia moja.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Kampuni ya Ukamataji wa Magari Dar Yafutiwa Mkataba

$
0
0
Kampuni ya Ukamataji wa  Magari Dar Yafutiwa Mkataba
Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita amefuta mkataba wa kampuni ya ukamataji wa magari Mwamkinga Auction Mart kwa kile kilichodaiwa amekuwa ikifanya kazi kwa kutozingatia matakwa ya mkataba ikiwemo kuwatoza watu faini  kuanzia Sh 200,000 hadi Sh 300,000.

Mwita amesema halmashauri ya jiji iliingia mkataba na kampuni hiyo Aprili 1 mwaka huu ili kudhibiti uegeshaji wa magari katika maeneo yasiyo rasmi yaliyopo katika Manispaa ya Temeke na Kigamboni.

Amesema halmashauri hiyo ilifuatilia kwa karibu utendaji wa kazi wa kampuni hiyo baada ya kupata malalamiko ya wananchi na kujidhihirisha kwa ushahidi uliojitosheleza kuwa ilikuwa ikifanya kazi kwa kutozingatia mkataba waliokubaliana nao.

"Mkataba wake tumesitisha kuanzia Septemba 19 mwaka huu na nimesikia bado wapo barabarani wanakusanya hizo faini hivyo hawatakiwi kuonekana na wakiendelea watachukuliwa hatua za kisheria,” amesema Mwita.

Mwita amesema kampuni hiyo inatakiwa kuondoka kwenye maeneo waliyopangiwa kufanya kazi hiyo na kuhakikisha inakabidhi mashine zote za kukusanyia mapato ya halmashauri hiyo zikiwa katika hali nzuri.

Amesema haiwezekani mtu amesimama kwa dakika moja unafunga gari lake kwa mnyororo na kumwandikia faini ya Sh 200,000 hadi Sh 300,000 ambayo haipelekwi kwenye halmashauri hiyo.

“Hiyo kampuni ilikuwa inafanya kazi hadi saa tatu usiku tofauti na makubaliano ya mkataba unavyosema mwisho saa 12 jioni.”

Amesema anaendelea kufuatilia kwa Wilaya ya Kinondoni na Ilala  ambapo kama wataenda tofauti na mikataba inavyosema watasitishwa mikataba yao.

Mwita amesema lengo la halmashauri hiyo siyo kumkandamiza mwananchi bali kusimamia sheria ili watu wazifuate lakini imeonekana tofauti.

 "Na nimesikia wanakusanya hadi shilingi milioni nne kwa mwezi ambazo haziwasilishwi hapa halmashauri ya jiji,” amesema.

Breaking News:Serikali ipo Tayari Kugharamia Matibabu ya Mbunge Lissu Mahali Popote Duniani

$
0
0
SERIKALI imesema kuwa ipo tayari kuingia kugharama zozote ili kumpeleka kwenye matibabu mahali popote duniani Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Tundu Lissu iwapo watapokea maombi kutoka kwa ndugu na familia yatakaothibitishwa na daktari kuwa anahitaji huduma ya madaktari wa bingwa zaidi.

Akitaka apelekwe Marekani,Ujerumani na mahali mengine ikiwemo India tunaweza kumpelekea iwapo watapeleka maombi serikali kutaka ifanyie hivyo ili kuweza kuhakikisha anapata matibabu.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Tanga ambapo alisema wakipita maombi watatekeleza suala hilo haraka iwezekanavyo.

"Serikali haitakataa wala kushindwa kumuhudumia Tindu Lissu yeye ni Mtanzania kama wanavyohudumiwa wengine hivyo wao wapo tayari kuhakikisha anapata matibabu bora nje ya nchi "Alisema

Serikali Yatoa Tamko Zito Mali za Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC)

$
0
0
Serikali Yatoa Tamko Zito Mali za Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC)
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba ameagiza kupitiwa upya mali zote zilizokuwa zikimilikiwa na Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC). 

Ametoa agizo hilo akizindua bodi mpya ya wakurugenzi ya nafaka na mazao mchanganyiko mjini hapa.

Dk Tizeba amesema mali zote za NMC ambazo hazikuuzwa zitamilikiwa na bodi hiyo.

Amewataka kuingia upya mikataba  na kuisimamia ili kuondoa ubabaishaji uliokuwa ukifanya na baadhi ya watu waliojimilikisha mali za Serikali kama vile  maghala na mashine.

Waziri amesema lengo la Serikali kuanzisha bodi hiyo ni kuhakikisha inasimamia pamoja na mambo mengine mali ambazo hazikubinafsishwa zilizoko Mwanza, Iringa, Arusha na Dodoma. 

“Changamoto zilizojitokeza wakati wa NMC na Gapex lazima bodi ikabiliane nazo kwa umakini na kuzifanyia kazi ili zisijitokeze tena,” amesema.

Dk Tizeba ameagiza bodi hiyo kujihusisha na usambazaji wa pembejeo za kilimo na usindikaji ili kuondoa matatizo ya upatikanaji wake na kuongeza thamani za mazao ya wakulima. 

Kaimu mkurugenzi wa bodi hiyo, John Maige amesema watashirikiana na wakulima na wadau wengine na kwamba, watafanya kazi kwa ushindani kama taasisi huru ya kiuchumi.

Amesema bodi itahakikisha inatumia mali ilizopewa na Serikali kujenga uwezo wa kimtaji.

Bodi ina uwezo wa kununua mazao mchanganyiko kutoka kwenye vikundi vya wakulima katika mikoa ya  Iringa, Ruvuma, Songwe, Mbeya na Njombe.

Dkt.Rose Migiro Apata Shavu Umoja wa Mataifa

$
0
0
Dkt.Rose Migiro Apata Shavu Umoja wa Mataifa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres ameteua jopo la wataalamu 18 watakaokuwa na kazi ya kuhakikisha wanatumia uzoefu wao kukabiliana na migogoro duniani kwa njia ya kidiplomasia, huku mwanadiplomasia wa Tanzania, Dk Asha- Rose Migiro akiwa miongoni mwa wateule hao.

Hatua ya kuteuliwa Dk Migiro aliyewahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa UN kwenye jopo hilo imeelezwa na wataalamu wa masuala ya diplomasia kuwa ni uthibitisho mwingine wa namna Tanzania ilivyo mshiriki muhimu katika kusaka amani ya dunia.

Jopo hilo ambalo linafahamika kama ‘Bodi ya Ngazi ya Juu ya Ushauri kuhusu Usuluhishi’ limeundwa kwa kuzingatia usawa wa kijinsia na uwakilishi wa kikanda, pia likizingatia historia ya wahusika katika masuala ya diplomasia na utatuaji wa migogoro.

Pamoja na Dk Migiro ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, wengine walioteuliwa ni aliyekuwa mke wa rais wa Msumbiji na baadaye akaolewa na Rais Nelson Mandela wa Afrika Kusini, Graca Machel, Rais mstaafu wa Nigeria, Olesegun Obasanjo, Rais wa zamani wa Chile, Michelle Bachallete na Rais mstaafu wa Finland, Tarja Halonen.

Pia, wamo wanadiplomasia, mawaziri wa zamani, watu waliowahi kuongoza taasisi za kimataifa na watu wengine mashuhuri. Jopo hilo pamoja na kazi nyingine litakuwa na jukumu la kumshauri Katibu Mkuu wa UN kuhusu njia zinazopaswa kuzuia migogoro na kushiriki kutatua mizozo katika maeneo yanayokumbwa na hali hiyo.

Baadhi ya wataalamu wa masuala ya diplomasia wamesema kuteuliwa kwa watu kama Dk Migiro na Graca Machel kwenye jopo hilo kunaonyesha jinsi walivyoiva kidiplomasia na watatoa mchango mkubwa katika kuhakikisha amani inapatikana duniani.

“Mtu kama Dk Migiro ana uzoefu mkubwa wa mambo haya na kuteuliwa kwake kunadhihirisha namna Tanzania ilivyo mstari wa mbele katika kusaidia kupatikana kwa amani duniani,” amesema Innocent Shoo, Mhadhiri wa Chuo cha Uhusiano wa Kimataifa na Diplomasia (CFR).

Amesema Tanzania imekuwa ikishiriki katika utatuzi wa migogoro katika maeneo mbalimbali duniani, hivyo kuteuliwa kwake hakushangazi kwa vile kunaendelea kudhihirisha diplomasia ya Tanzania kwenye eneo hilo.

“Hivi sasa tunaweza kuona jinsi Rais wetu mstaafu Benjamin Mkapa anavyoendelea na upatanishi katika mzozo wa Burundi, wakati Rais Jakaya Kikwete akipatanisha nchini Libya na hata Dk Migiro amewahi kushiriki kikamilifu katika kusaka amani katika eneo la Nchi za Maziwa Makuu wakati alipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania na hata alipokua UN kama Naibu Katibu Mkuu,” amesema.

Kuhusu Graca Machel amesema amekuwa mstari wa mbele katika kupigania usawa ambao mara nyingi unapokosekana huwa chanzo cha kuzuka kwa migogoro mingi duniani.

 “Lakini pia alishiriki katika kusaka amani nchini Kenya wakati wa machafuko baada ya uchaguzi wa mwaka 2007,” amesema.

Msichana Aliyebakwa na Waalimu India Mahututi Baada ya Kuavia Mimba

$
0
0
Msichana Aliyebakwa na Waalimu India Mahututi Baada ya Kuavia Mimba
Msichana wa India ambaye alidaiwa kubakwa na waalimu wawili wa shule katika kipindi cha wiki tatu yuko katika hali mahututi baada ya kulazimishwa kuavia mimba.
Madaktari wameiambia BBC idhaa ya Hindi kuwa ubongo wake umeharibika.
Polisi imemtioa nguvuni Mkuu wa shule yake na mwalimu wake katika jimbo la kaskazini mwa India la Rajasthan.
Polisi wanasema kuwa alipoteza fahamu baada ya washukiwa skumlazimisha kutoa mimba katika hospitali ya kibinafsi.

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 18 alilazwa hospitalini baada ya kuhisi maumivu makali ya tumbo na wahudumu katika shule yake wakabaini kwamba alikuwa mjamzito.
Mwathiriwa wa ubakaji wa miaka 13 India aiomba mahakama kutoa mimba

Hali yake ya afya ilianza kuwa mbaya kwa haraka baada ya kuavia mimba, lakini haijafahamika wazi ni nini hasa kilichoifanya hali yake kuwa mbaya,alisema polisi katika wilaya ya Sikar said.
Shule hiyo iliyopo wilaya ya Sikar, imefungwa kwa sasa na mamlaka katika eneo hilo.
Polisi wanaamini kuwa masomo ya ziada yanayotolewa katika saa ambazo si za kawaida yalitumiwa kuwaita wanafunzi ili kuwezesha vitendo kama hivyo vya unyanyasaji kufanyika.
Bado polisi hawajaweza kurekodi taarifa kutoka kwa muathirika.
"Hili ni tatizo baya na hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wahusika ,"alisema afisa wa polisi Kushal Singh.

Madaktari Nchini Kenya Washangaa Tundu Lissu Kuwa Hai

$
0
0
 Madaktari Nchini Kenya Washangaa Lissu Kuwa Hai
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema madakatari nchini Kenya wameshangazwa kumwona Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa hai kutokana na shambulio la risasi lililotokea Septemba 2017 mjini Dodoma.

Msigwa aliyekuwa miongoni mwa viongozi wa Chadema waliomsafirisha Lissu kutoka Dodoma siku hiyo kwenda jijini Nairobi, aliliambia gazeti hili jana kwamba Lissu alivuja damu nyingi na kama asingepata huduma ya haraka angefariki.

“Tulipofika Nairobi, madaktari walishangaa kuona Lissu akiwa hai, kwa sababu alipoteza damu nyingi sana. Lakini niwashukuru sana madaktari wa hospitali ya Dodoma General kwa huduma waliyotoa kufanya Lissu tufike Nairobi,” amesema Mchungaji Msigwa na kuongeza:

“Nataka tu niwaambie Watanzania kwamba Tundu Lissu wetu aliumizwa sana katika jaribio la kuchukua uhai wake. Watu wasichukulie kama ni jambo dogo, ni jambo kubwa lililoharibu hata akili za watu tuliokuwa karibu naye.”

Mahakama Imemfutia Kesi ya Ugaidi Mbunge wa CHADEMA na Kumuachia Huru

$
0
0
Mahakama Imemfutia Kesi ya Ugaidi Mbunge wa CHADEMA na Kumuachia Huru
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru Mbunge wa Bukoba Mjini (Chadema), Mh.Wilfred Lwakatare  na mwenzake, Ludovick Rwezaura waliokuwa wakistakiwa kwa kosa la kula njama za kutoa sumu kwa nia ya kumdhuru aliyekuwa Mhariri wa Gazeti.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba amewaachia huru washtakiwa hao leo Alhamisi mara baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa kuomba kesi hiyo ifutwe chini ya kifungu cha 91(1) cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai kisha Mahakama kuridhia.
Kishenyi ameomba kesi hiyo ifutwe chini ya kifungu hicho kwa sababu Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hana nia ya kuendelea kuwashtaki washtakiwa hao na  baada ya kutolewa kwa maelezo hayo hakimu aliwaachia huru washtakiwa hao leo.
Pamoja na hayo Mh. Lwakatare amemshukuru Mungu kwa kuwa na siku njema na yenye furaha.

Hata hivyo wakati kesi hiyo inaondolewa mahakamani hapo alikuwapo Mbunge Lwakatare pekee huku mshtakiwaRwezauraakiwa hajafika kwa kile kinachodaiwa kuwa na matatizo ya kifamilia.

Awali Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, ilimfutia kesi ya makosa ya ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare na Ludovick Joseph, baaadaye Jamhuri ilikata rufaa kupinga maamuzi ya Mahakama Kuu. 

Mdee Ampa Pole Kikiwete Asema Waliomzushia Walifikiria Alichotamani Kukisema ila Tatizo Mazingira Sio Wezeshi

$
0
0
 Mdee Ampa Pole Kikiwete Asema Waliomzushia Walifikiria Alichotamani Kukisema ila Tatizo Mazingira Sio Wezeshi
Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee amempa pole Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa maneno ya uzushi wanayozusha juu yake ambayo amekuwa akikanusha mara kwa mara.
Mdee ameeleza kuwa kweli amezushiwa huku akisema waliokuwa wakimzushia walifikilia alichotamani kusema ila mazingira sio wezeshi.

Pole sana Mkuu..na kama kweli umezushiwa waliokuzushia walifikiria ulichotamani kukisema, lakini mazingira sio wezeshi…


Tukio Alilofanyiwa Lissu ni Uhalifu Mkubwa Ushahidi Utakusanywa Hapa Tanzania- Jaji Mkuu

$
0
0
Tukio la Lissu ni Uhalifu Mkubwa Ushahidi Utakusanywa Hapa Tanzania- Jaji Mkuu
Jaji Mkuu wa Tanzania, Ibrahim Juma amesema kuwa tukio la Mhe. Lissu la kupigwa risasi na watu wasio julikana ni uhalifu sio mdogo huku akisema kuwa ushahidi wa tukio hilo utakusanya hapa hapa Tanzania.

Jaji Mkuu, ameyazungumza hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuwa asikudanganye mtu kuwa mtu atatoka nje kuja kukusanya ushahidi huo.

“Tukio la Lissu ni la kihalifu nadhani tumekubaliana uhalifu mkubwa, sio mdogo ni jaribio la kuua lakini kitu cha kwanza ni kukusanya ushahidi na huo ushahidi utakusanywa hapa hapa Tanzania, asikudanganye mtu kwamba mtu atatoka nje atakusanya ndio atakuwa na uwezo wa kukusanya ushahidi , ushahidi tunakusanya hapahapa,” amesema Jaji Mkuu Juma.

Hata hivyo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wiki kadha waliomba uchunguzi wa jambo hilo ukusanywe na watu kutoka nje ya nchi na si hapa Tanzania.

Jezi ya Okwi Yakimbiza kwa Kuuzika Mwanza

$
0
0
Jezi ya Okwi Yakimbiza kwa Kuuzika Mwanza
Jezi ya mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi inauzika zaidi kuliko za wachezaji wengine hapa jijini Mwanza ikiwa ni kuelekea mechi ya Simba na Mbao FC.

Mfanyabiashara Said Hassan anayejishughulisha na uuzaji wa jezi jijini Mwanza, alisema kuwa jezi ya Okwi imekuwa na wateja wengi kuliko nyingine ikifuatiwa ya Haruna Niyonzima.

"Kwa sasa jezi ya Okwi inauzika sana kuliko nyingine na mashabiki wengi wanasema kuwa huyo ndiye mchezaji anayeibeba timu, nyingine kidogo ni ya Niyonzima," amesema Hassan.

Taasisi ya Jakaya Kikweye Yaingia Kwenye Historia

$
0
0
Taasisi ya Jakaya Kikweye Yaingia Kwenye Historia
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa mara ya kwanza imefanya upasuaji kwa mtoto mdogo na kumwekea valvu mbili za moyo za bandia.

Teknolojia hiyo ambayo ni nadra kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, imefanyika chini ya jopo la madaktari kutoka Taasisi ya Moyo BLK ya India na JKCI, ikiwa ni sehemu ya mafunzo kwa vitendo.

Akizungumza baada ya upasuaji huo,  daktari bingwa wa magonjwa ya moyo, Peter Kisenge amesema kwa msaada wa wataalamu kutoka BLK wamefanikiwa kukamilisha upasuaji huo.

Amesema JKCI imekuwa ikifanya upasuaji wa kuweka valvu moja pekee, upasuaji ambao kwa mara ya kwanza ulifanyika mwaka jana.

"Upasuaji huu umewezekana kwa mara ya kwanza Afrika Mashariki na Kati kwa msaada wa BLK. Mgonjwa huyu angepelekwa nje ingegharimu zaidi ya Sh35 milioni," amesema Dk Kisenge.

Amesema upasuaji huo umegharimu Sh14 milioni.

Mwenyekiti wa BLK ambaye ni daktari bingwa wa mishipa mikubwa ya damu, Dk Ajay Kaul amesema wapo tayari kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuhakikisha inafanikiwa katika matibabu.


Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136

$
0
0
 Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136
Makali ya Uchumi , yanazidi kukaza, leo shirika la ndege la Precision Air, limepunguza wafanyakazi 136 wakiwemo cibin crew 10...

Najua wengi humu mtasema hali hii imechangiwa na kufuka kwa ATCL na ushindani toka Fast Jet, lakini this is not the case, nimepanda zote, ATCL, Fast Jet, na ATCL, zote zina suffer, Purchasing power ya Watanzania kusafiri kwa ndege, imepungua, soon mtashuhudia mashirika mengine yakipunguza frequency na mtashuhudia mabenki yakifungasha na kuondoka.

This is not good at all.

Paskali

Msukuma Amshushia Lawama RPC wa Geita na Kusema Ana Roho Mbaya

$
0
0
Msukuma Amtupia Lawama RPC wa Geita na Kusema Ana Roho Mbaya
Mbunge na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma amefunguka na kumtuhumu RPC mkoa wa Geita na kusema ana roho mbaya kwani hajamtendea haki katika kumkamata licha ya kuwa kweli kulikuwa na makosa.

Msukuma amesema kuwa siku ambayo alikamatwa na kuwekwa ndani RPC huyo aliagiza chakula chake alicholetewa kimwage na kutaka Mbunge huyo ale chakula ambacho kinapatikana kituoni hapo jambo ambalo anasema alikataa na kulala na nja kwa sababu ya RPC huyo wa Geita.

"Mimi nilipomaliza kutoa maelezo saa tatu usiku nilikuwa nasikia njaa nikaagiza chakula lakini baadaye nilisikia anaagiza chakula changu kimwagwe halafu saa nane usiku anamtuma askari wake kuniletea chakula kwenye 'hot pot' nikamwambia siwezi kula chakula chenu hicho nikakirudisha nililala njaa na kesho yake si kula mpaka saa tisa alasiri wakaniamisha na kunileta Geita ndiyo nikala chakula cha madiwani" alisema Msukuma

Aidha Msukuma aliendelea kumtuhumu RPC huyo wa Geita kwa kusema kuwa wazungu wamemuwekea mafuta kwenye magari kuwatafuta madiwani wa CCM hivyo anahangaika na kutafuta madiwani badala ya kutafuta majambazi na watu wanaofanya uhalifu.

"Wazungu wamemuwekea RPC mafuta kwenye magari kusaka madiwani badala ya kumuwekea mafuta kusaka majambazi, kule nimekutana na askari wengine wana roho nzuri wanakuhudumia vizuri yaani unaona kabisaa upo sehemu ya usalama, lakini sijawahi kuona mtu ana roho mbaya kama huyu RPC wa mkoa wa Geita" alisema Msukuma

Mbali na hilo Msukuma amempa siku tatu RPC wa Mkoa wa Geita awe amemuomba radhi kupitia kwa wazee wa mkoa huo kwa mambo ambayo ametendea na kusema kama hatafanya hivyo basi yeye ataanika mambo ya RPC huyo hadharani ili wananchi na Watanzania wote wajue.

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images