Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Baraza la Mawaziri Nchini Kenya Lapitisha Bajeti ya Uchaguzi wa Marudio

$
0
0
Baraza la Mawaziri Nchini Kenya Lapitisha Bajeti ya Uchaguzi wa Marudio
 Baraza la Mawaziri, katika kikao chake kilichofanyika Alhamisi ikulu chini ya mwenyekiti wake Rais Uhuru Kenyatta lilipitisha bajeti ya Sh10 bilioni kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi wa marudio wa rais uliopangwa Oktoba 26.

Kiasi hicho cha fedha ni pungufu kwa Sh2 bilioni hasa ikizingatiwa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ilikuwa imeomba Sh12.2 bilioni kwa ajili ya shughuli za uchaguzi wa marudio baada ya ule wa kwanza uliompa ushindi Rais Uhuru Kenyatta kufutwa na Mahakama ya Juu mapema mwezi huu.

"Baraza la Mawaziri leo (juzi) limeidhinisha kutolewa Sh10 bilioni ili kugharimia uchaguzi wa marudio kwa kura ya urais. Kiasi hicho kimetolewa kwa kuzingatia mapendekezo ya bajeti iliyowasilishwa na IEBC," imesema taarifa ya msemaji wa ikulu Manoah Esipisu.

Awali Katibu wa Baraza la Mawaziri Henry Rotich alikadiria kwamba uchaguzi wa marudio unaweza kugharimu zaidi ya Sh15 bilioni ikiwa 'shughuli zinazohusu kwa upana usalama zitaingizwa'.

Rais wa Korea Kaskazini Amesema Trump ''Atalipia'' Kauli Zake

$
0
0
Rais wa Korea Kaskazini Amesema Trump ''Atalipia'' Kauli Zake
Kim Jong-un amesema kauli za "wazimu'' rais wa Marekani Donald Trump zimemshawishi kuwa alikuwa sahihi kutengeneza silaha kwa ajili ya Korea kaskazini.
Katika kauli yake binafsi ambayo haikutarajiwa, kupitia vyombo vya habari vya taifa, Bwana Kim alisema kuwa Bwana Trump ''atalipia" hotuba yake ya hivi karibuni katika Umoja wa Mataifa.
Jumanne wiki hii rais wa Marekani alisema kwamba kama Marekani ikilazimishwa kujilinda ''itaiangamiza kabisa'' Korea Kaskazini.
Bwana Trump pia alimkejeli Bwana Kim akimuita "rocket man" anae andaa mpango wa ''kujiangamiza ".
Korea Kaskazini imekuwa ikifanya majaribio ya makombora, na ilifanya jaribio la sita la nuklia licha ya majaribio hayo kulaaniwa kimataifa.

Waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini Ri Yong-ho, ambaye awali alilinganisha hotuba ya Bwana na "sauti ya mbwa anayebweka ", ameonya kuwa utawala wa Pyongyang unaweza kufanya jaribio la bomu la sumu ya nuklia aina ya katika bahari ya Pacific kujibu tisho la rais wa Marekani.
"Bomu hilo linaweza kuwa bomu zito zaidi la majini aina hiyo kuwahi kufyatuliwa katika bahari ya Pacific," Bwana Ri alinukuliwa na shirika la habari la Korea Kusini -Yonhap.
Hata hivyo aliongeza kusema kuwa:" Hatufahamu juu ya hatua gani zinaweza kuchukuliwa kama itakavyoagizwa na kiongozi Kim Jong-un."
Marekani na Korea Kaskazini zimekuwa katika malumbano makali katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni.

TCRA Yatangaza Lengo la Kuboresha Usalama wa Mitandao ya Kijamii

$
0
0
TCRA Yatangaza Lengo la Kuboresha Usalama wa Mitandao ya Kijamii
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jones Kilimbe amesema lengo la serikali kuboresha sera na kanuni za mitandao ya kijamii ni kutaka kuweka usalama katika nchi pamoja na kutumiwa vyema ili iweze kuleta maendeleo.

Dkt. Kilimbe amebainisha hayo wakati alipofungua warsha na vyombo vya habari vya mtandaoni 'online media' na kusisitizia kuwa kutokana na ukuaji wa mitandao ya kijamii ni vyema ikatumika vizuri na kuzingatia utu pamoja na staha.

"Mawasialiano ya mtandao (online) yameendelea kukua mpaka sasa kuna 'online TV' zaidi ya 50 na 'blogs' zaidi ya 150 huku TV zikiwa 32 tu hivyo ni vyema zikatumika vyema bila kufanya uchochezi wa aina yeyote", amesema Dkt. Kilimbe.

Aidha, Dkt. Kilimbe amesema kutokana na ukuaji wa mitandao ya kijamii umeweza kuonesha jinsi teknolojia ilivyopokelewa vizuri kwani taarifa zimeweza kupatikana kwa haraka endapo ukiwa na simu ya mkononi.

"Kutokana na mapokeo mazuri inabidi mitandao hii itumiwe vizuri kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa. Pia nashauri iwepo sera na kanuni za kufanikisha mitandao hii itumike vyema kimaendeleo na ndiyo maana serikali imeamua kuja na maboresho ambayo yatakuwa bora na salama, pia TCRA itakuwa bega kwa bega" amesema Dkt. Kilimbe.

Kwa upande mwingine, Dkt. Kilimbe ametoa wito kwa wale ambao hawajajiunga na chama cha Tanzania Bloggers Network (TBN) kufanya hima kujisajili kwani ni vyema kuwa na chombo kinachosimamia masuala yanayowahusu na kuwakutanisha pamoja.


Mama Daimond Aamua Kumfuta Machozi Zari Amwagia Sifa Hizi

$
0
0
Mama Daimond Aamua Kumfuta Machozi Zari Amwagia Sifa
Baada ya Zari kuonekana kutokuwa na furaha baada ya kusalitiwa na baba watoto wake Diamond Platnumz kwa kuzaa na mrembo Hamisa Mobetto, Mama mkwe wake Sandrah Michael ameamua kumpooza machungu japo kidogo.

Sandrah ambaye ni mama mzazi wa Diamond, amemtumia ujumbe Zari kupitia mtandao wa Instagram.

Pendeza na Kessy Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa Bila Madhara yoyote

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA


1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/
(21) ENGEZA  MGUU_80,000/

 TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM

(+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO

Makonda Ahamishia Maduka ya Magari (Show rooms) Kigamboni

$
0
0
Makonda Ahamishia Maduka ya Magari (Show rooms) Kigamboni
Kuanzia Januari mwakani, maduka yote ya magari (show rooms ) jijini hapa yatakuwa eneo moja wilayani Kigamboni.

Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam imesema imetenga eneo la Kibada wilayani Kigamboni kwa ajili ya maduka hayo kwa magari mapya na yaliyotumika.

Eneo hilo kwa ajili ya mauzo ya magari makubwa na madogo litaanza kutumika Januari ili kurahisisha upatikanaji wa huduma.

Akizungumza na wadau na wafanyabiashara wa magari ofisini kwake leo Ijumaa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema wameamua kutenga eneo moja la kuuzia magari kwa kuwa kufanya hivyo kuna faida kuu tatu.

Amesema faida ya kwanza ni mwananchi kuwa na uwezo wa kununua gari sehemu moja na akapata nafasi ya kuchagua analolipenda kwa kadri awezavyo katika eneo moja.

“Ukiwa sehemu moja ni rahisi kufanya uamuzi baada ya kuona ubora wa gari au magari unayotaka,” amesema.

Mkuu huyo wa mkoa amesema faida ya pili ni kwa wafanyabiashara wa magari kuonyesha bidhaa zao kwa wateja wanaowafikia katika eneo la soko na hakutakuwa na kificho kama ilivyo sasa.

Amesema faida ya tatu  ni kuiwezesha Serikali kukusanya kodi kwa ufanisi kwa kuwa kutakuwa sehemu moja na huduma zote zikiwemo za bima na namba za magari zitakuwa zikipatikana katika eneo hilo ambalo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) watakuwepo.

Rais wa Ufilipino Aruhusu Mwanaye Auwaweutwa Atakapokutwa na Mihadarati

$
0
0
Rais wa Ufilipino Aruhusu Mwanaye Auwaweutwa Atakapokutwa na Mihadarati
Rais Rodrigo Duterte amesema ikiwa ushahidi usiotiliwa shaka utatolewa kuthibitisha tuhuma za usafirishaji dawa za kulevya ambazo zinamkabili mtoto wake wa kiume na mwanasiasa kijana ataacha auawe na kwamba polisi watakaomuua watalindwa wasishtakiwe.

Mwezi huu, mtoto wa Rais Duterte, Paolo Duterte (42) alifikishwa mbele ya Kamati ya Seneti kwenda kukanusha madai yaliyowasilishwa na mbunge wa upinzani kwamba ni mfuasi wa genge la China linalofanya uhalifu wa kimataifa ambaye alisaidia kuingiza shehena ya dawa aina ya crystal methamphetamine kutoka China.

Rais Duterte hakuzungumzia tuhuma hizo moja kwa moja bali alirejea kauli aliyoitoa mwaka jana wakati wa kampeni kwamba hakuna mtoto wake hata mmoja anayejihusisha na mihadarati, lakini ikiwa watajihusisha watakabiliwa na adhabu kali kuliko zote.

"Nilisema hapo awali: 'Ikiwa watato wangu watajihusisha na dawa za kulevya, wauawe ili watu wasiwe na cha kusema’,” alisema Duterte Jumatano katika mkutano na wafanyakazi wa serikali ikula.

"Kwa hiyo nilimwambia Pulong (jina la utani la Paolo): 'Amri yangu ni kwamba uuawe ikiwa utakamatwa. Na nitawalinda polisi watakaokuua, endapo ni kweli,” alisema.

Duterte, 72, alishinda uchaguzi mkuu kutokana na ahadi aliyoitoa ya kuendesha kampeni isiyo ya kawaida ya kutokomeza genge la wahalifu katika jamii kwa kuua hadi wasafirishaji na watumiaji 100,000.

Tangu alipoapishwa katikati ya mwaka 2016 na kuingia ikulu, imeripotiwa polisi wameua zaidi ya watu 3,800 katika opereshani ya kupambana na wanaojihusisha na mihadarati huku maelfu wengine wakiuawa katika mazingira ya kutatanisha.

Rais Kenyatta na Raila Odinga Wakutana Katika Mazishi

$
0
0
Rais Kenyatta na Raila Odinga Wakutana Katika Mazishi
Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa Upinzani Raila Odinga wamekutana kwa mara ya kwanza tangu kufutiliwa mbali kwa matokeo ya uchaguzi wa urais wa Agosti 8 na mahakama ya juu.
Wawili hao pamoja na viongozi wengine ,wengi kutoka chama tawala cha Jubilee wamehudhuria mazishi ya aliyekuwa Meya wa Nairobi Samuel Mbugua , babake aliyekuwa mwakilishi wa wanawake katika kaunti ya Nairobi Rachel Shebesh katika shamba lake huko Kiambu.
Rais Kenyatta na Raila Odinga wamekuwa na misimamo mikali kuhusu marudio ya uchaguzi mkuu huku kiongozi wa Nasa akisisitiza kwamba mahitaji yake ni lazima yaafikiwe kabla ya uchaguzi mwengine kufanyika.
Miongoni mwa viongozi waliokuwepo ni gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu na Seneta wa Nairobi Johnson Sakaja .
Hatua ya Odinga kuhudhuria mazishi hayo inaonyesha urafiki mkubwa ambao amekuwa nao na familia ya Mbugua.
Bwana Mbugua aliwahi kufanya kazi naye katika chama cha ODM.
Wakati huohuo ODM ilimteuwa bi Rachel Shebesh kuwa mbunge wake mwaka 2007 na 2012 kabla ya kujiunga na chama cha rais Kenyatta cha TNA 2012.


Staili 3 za Kujamiiana Ambazo ni Hatari Kwa Wanaume

$
0
0

Staili 3 za Kujamiiana Ambazo ni Hatari Kwa Wanaume
Tafiti zimebaini kuwa hizi ndizo aina kuu tatu za ufanyaji wa mapenzi zinazoweza kupelekea mwanaume kupata madhara ya kuvunjika kwa uume.

Kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika ‘dog style’, ‘missionary’ na ‘cowgirl’ zimeelezwa kuwa ndizo zinazoongoza zaidi kusababisha kuvunjika kwa uume.

Ripoti iliyochapishwa katika jarida la “international journal of Impotence” ilichunguza wanaume 90 wenye umri wa kati ya miaka 18-66 walikumbwa na tatizo la kuvunjika kwa uume.

Utafiti huu uliwagawanya waathirika hao katika makundi sita kulingana na ukubwa wa tatizo ambayo yalihusisha: Punyeto, aina ya ufanyaji wa mapenzi ambao mwanaume huwa juu ‘missionary’, ‘dog style’, ufanyaji wa mapenzi ambao mwanamke hukaa juu ‘Cowgirl’ na nyinginezo.

Utafiti ulibaini kuwa wanaume 69 kati ya wenye madhara ya kuvunjika kwa uume wamesababishwa na ufanyaji wa mapenzi.
Matokeo ya utafiti huu yalibaini kuwa wanaume 37 walipata madhara ya kuvunjika kwa uume kutokana na kufanya mapenzi kwa aina ya ‘dogstyle’

Wanaume 23 walipata madhara ya kuvunjika kwa uume kutokana na ufanyaji wa mapenzi wa aina ambayo mwanaume hukaa juu wengi huiita ‘kifo cha mende’ au ‘missionary style’.

Aina ya ‘dogstyle’ iliripotiwa kusababisha madhara kwa wanaume wengi kuliko aina nyingine japo madhara yake hayakutofautiana sana.

Unashauriwa kutambua ni aina ipi ya ufanyaji wa mapenzi ambayo inaweza kukusababishia madhara ya kuvunjika kwa uume na kama unaipendelea basi ni vyema ukaifanya kwa uangalifu mkubwa, japokuwa wakati mwingine inakuwa ni vigumu kukumbuka.

Hamisa Mobetto Amtunishia Zari ‘Waambie Waliopanga Mwenye Nyumba kaja’

$
0
0
Acha movie iendelee. Hamisa Mobetto jamani ni shida – azidi kumtia presha Zari The Bosslady.

Wiki hii Hamisa, Zari na Diamond wameteka vichwa vya habari mpaka nje ya nchi, hasa baada ya baba wa mtoto kufahamika. Vita iliyopo sasa hivi ni kuhusu malkia halali ambaye ataimiliki ikulu ya Madale.

Hamisa ameonyesha kutupa mawe gizani kupitia mtandao wa Snapchat na yameonekana kumfika mlengwa wake ambaye ni Zarina Hasssan (mama Tiffah). Kubwa zaidi ambalo limewashangaza wengi ni ujumbe alioandika wa kutamani kuzaa watoto mapacha na kujinadi kuwa yeye ndio mama mwenye nyumba.

Haya ndio aliyoyaandika Mobetto kwenye mtandao huo.




VIDEO: Mbowe Afunguka Mazito Kuhusu Tundu Lissu....

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe leo Septemba 22, 2017 amezungumza na vyombo vya Habari Jijini Dar es salaam kuhusu hali ya Tundu Lissu na mengine yanayoendelea nchini kwasasa. ambapo ameeleza kuwa yeye kama kiongozi wa Chama anadiriki kusema kwamba mshukiwa namba moja wa shambulio la Tundu Lissu ni vyombo vya ulinzi na usalama wa nchi hii.

VIDEO:

Tunda Afunguka Kuhusu Nyumba Inayodaiwa Kaipata Kwa Kuuza Madawa ya Kulevya.........

$
0
0
Mrembo Tunda ambaye ni 'video vixen', amefunguka kuhusu tetesi zilizopo kwamba nyumba anayomiliki imetokana na kufanya biashara ya dawa ya kulevya, na kusema hizo taarifa hazina ukweli wowote juu ya madai hayo.

Akipiga stori na Big Chawa kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio, Tunda  amekiri kumiliki mjengo huo na kusema siyo kweli kwamba nyumba hiyo imetokana na kuuza dawa za kulevya.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Polisi Wanamsaka Mwanamke Anayejisaidia Hadharini....

$
0
0
Polisi nchini Marekani wanamsaka mwanamke mkimbiaji ambaye amepewa jina la ‘mchafuzi kichaa’ kwa kuwa anatabia ya kijisaidia haja kubwa nje ya nyumba za watu.

Mwanamke huyo amekuwa akiacha kinyesi chake nje ya nyumba za watu kwa zaidi ya mara saba kwa wiki za hivi karibuni ,licha ya kwamba kuna vyoo vya umma karibu.

Inawlezwa kuwa watoto wa jirani walimuona mwanamke huyo wakati alipokuwa akijisaidia,akiwa amechuchumaa karibu na nyumba Colorado.

Idara ya polisi mjini humo imesema kuwa tabia ya aina hiyo ni ya “ajabu”.

Alikiba Anena Seduce Me Kushindanishwa na Zilipendwa, ‘Sijafuatilia Wala Siwezi’

$
0
0
Wakati ngoma ya Alikiba Seduce Me imetoka ilikuwa ikipanishwa na ile ya Diamond/WCB ‘Zilipendwa’ hasa katika mtandao ya Youtube, lakini Alikiba amefunguka na kusema hakuwahi kufuatilia hilo kabisa.

“Sijafuatilia hiyo, na wala siwezi kufuatilia, mimi nilikuwa naangalia Saduce Me watu wanatuma screen shoot katika instagram, muda mwingine naangalia viewers wamefika wangapi, that’s it, sikuweza kuangalia wimbo mwingine wowote,” Alikiba ameiambia Bongo5.

Hadi sasa ngoma hizo katika mtandao wa YouTube zina views zaidi ya milioni 5, Seduce Me ikiwa na views milioni 5.8 na Zilipendwa views milioni 5.9.

Ofisi ya Bunge yamjibu Mh. Mbowe kuhusu milioni 43 zilizochangwa na wabunge

$
0
0
Ofisi ya Bunge inapenda kuutarifu umma kuwa tayari kiasi cha fedha cha Milioni 43 zimeshatumwa katika hospitali ya Nairobi kiasi kwaajili ya matibabu ya Mhe. Tundu Lissu.

Soma taarifu kamili:



Kutamani Kungonoka Kila Dakika....Je Huu ni Ugonjwa ?

$
0
0

Habarini zenu
Mimi ni msichana na ninaomba mnisaidie kwani ninasumbuliwa sana na Ashki za kujaamiana kila muda.
Tatizo hili lilinianza takribani miaka kama 3 iliyopita baada ya kutumia vidonge vya kupunguza unene.

Dawa hizo nilizinunua toka kwa rafiki yangu mmoja ambae aliniambia alitumiwa na kaka yake aliyekuwa Thailand.

Vina rangi ya kijani kibichi na muundo wake ni kama kidonge cha Ampicilin. Ni kwamba vilinisaidia kwani nilipungua ila sasa ukaibuka ugonjwa huu.

Naomba mwenye kufahamu tiba anisaidie kwa maana naadhirika mjini hapa....Yaani kila saa mimi huku chini nanyevuka hata nisiposhikwa...

Please nipe ushauri ...
Joan Sekioni

Jinsi Wanawake Wanavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume Kwa Wanaume zao

$
0
0

Jinsi Wanawake Wanavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume Kwa Wanaume zao
1: KAULI
Miongoni mwa mambo ambayo mwanaume hataki kuyasikia yakitoka kwenye kinywa cha mwanamke ni kuambiwa HAWEZI TENDO LA NDOA. Mwanamke akimwambia mwanaume wakati au baada ya tendo kuwa hawezi, atakuwa amemsababishia tatizo kubwa la kisaikolojia ambalo litampelekea kupotea nguvu za kiume taratibu.

Msaada unaohitajika kwa mwanamke anayekutana na mwanaume dhaifu kwenye tendo si kumwambia hawezi, bali ni kumtia moyo na kumsaidia kuweza. Wanawake wamewasababishia waume zao upungufu wa nguvu za kiume kwa kuwaambia maneno kama haya: “Yaani siku hizi sijui umekuwaje, yaani huwezi kazi kabisa!”


2 : UJUZI

Wanawake wengi hasa waliopo kwenye ndoa, wanapuuza ujuzi kwenye tendo la ndoa. Hawajishughulishi kumsaidia mwanaume ‘kuwika’, si wabunifu na watundu, jambo hili humfanya mwanaume kushiriki tendo kwa kutegemea kupanda kwa hisia zake mwenyewe, hivyo anapokuwa amechoka au ana mawazo, hawezi kusisimka kwa vile hapati ushirikiano toka kwa mwenzake.

Pamoja na wengi kutokuwa wajuzi, lakini wapo wengine ambao ni watundu mno kwenye sita kwa sita kiasi cha kumfanya mwanaume ajione kama mgeni wa mchezo huo.

Kimtazamo, wanaume hupenda sana ushindi wakati wa ‘kazi’, lakini pale wanapogeuzwa ‘chekechea’ hupunguza uwezo wa kujiamini na kuruhusu hofu kuongezeka mawazoni mwao, hivyo kuwasababishia tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Inashauriwa kwamba, mwanamke anapokuwa na uelewa mkubwa wa masuala ya mapenzi hasa wakati wa tendo, asioneshe kiwango kikubwa kwa haraka bali amchukulie mwenzake kama mwanafunzi, asiwe na maneno kama: “Leo nakuja kukupa vitu adimu kuliko vya juzi, hakuna kulala kasi mtindo mmoja.” Kauli hizi huwaogopesha wanaume na kuwafanya wapungukiwe na nguvu.

3:USAFI
Mwanamke anapokuwa si msafi, huweza kumsababishia mwanaume matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume. Sote tunafahamu umuhimu wa usafi wa mwili na kero za uchafu wakati wa tendo, hivyo ni wazi kuwa mwanamke akiwa mchafu atamfanya mwanaume apoteze msisimko na uwezo wa tendo la ndoa. Unadhifu wa mavazi na mwili ni muhimu sana katika mapenzi.

4:GUBU
Jambo lingine linaloweza kumsababishia mwanaume upungufu wa nguvu za kiume ni gubu au karaha za maneno ya uchokozi yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Uchokonozi wa mambo, ugomvi, usaliti na hali ya kutokuwa na staha ni mambo yanayosababisha tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Mwanamke anapokuwa mwingi wa maneno ya kashfa, dharau na matusi huweza kumfanya mume amchukie na kutopenda kushiriki naye tendo. Uchunguzi unaonesha kwamba wanawake walioolewa wenye tabia hii, huwafanya waume zao wawe na msisimko wa kimapenzi kwa wanawake wa nje kuliko wake zao hao.

5:USALITI
Tabia ya usaliti kwa mwanamke ni chanzo kingine cha mwanaume kupata tatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Mwanaume anapoona, kuhisi au kubaini kuwa anasalitiwa, huumia sana moyoni, maumivu ambayo hatimaye humfanya muhusika kuwa na mawazo mengi ambayo humuondolea hamu ya tendo.

Dokta Bianca P. Acevedo kutoka Chuo Kikuu cha California

Mbowe Amshukuru Mange Kimambi na Wema Sepetu Kwa Kuhamasisha Michango ya Tundu Lissu

$
0
0
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amewashukuru Watanzania wanaoendelea kumchangia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwataja wanaoongoza katika kuhamasisha uchangiaji mitandaoni akiwamo Mange Kimambi na Wema Sepetu.

Mbowe amesema mpaka leo Ijumaa jumla ya Sh204 milioni zimepatikana katika michango hiyo pamoja na msaada wa hali ambao wamekuwa wakipewa na Watanzania.

“Tunawashukuru wanaoendelea kuchangisha, tunamshukuru Mange Kimambi kwa kuwahamasisha diaspora kuchangia na katika mitandao akishirikiana na Wema Sepetu na wengine,” alisema Mbowe.

Mange alianzisha kampeni ya kumchangia Lissu katika mtandao wa Gofundme akilenga kupata dola za Marekani  50,000 na mpaka kufikia leo saa 10.41 katika mtandao huo kiasi cha dola za Marekani 23,380 ilikuwa imepatikana ambayo ni wastani wa Sh51.3 milioni.

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images