Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Msigwa Aingilia Kati Suala la Msukuma na Kamanda wa Polisi Geita

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA Peter Msigwa amezidi kushikilia suala la Mbuge wa Geita Mjini na RPC wa Geita na kusema kuna jambo kati yao lakini anashindwa kuelewa inakuaje mbaka sasa TAKUKURU inashindwa kuwahoji wote wawili.

Msigwa amesema hayo kupitia mtandao wake wa Twitter zikiwa zimepita siku kadhaa toka Mbunge na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Joseph Msukuma kudai kuwa ana siri nyingi za Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Mponjoli Mwabulambo na kudai atazitoa siri hizo ikiwa Kamanda wa Polisi huyo hatamuomba msamaha kwa kitendo alichomfanyia ikiwa pamoja na kumkamata na kumlaza rumande.

"Msukuma amesema anajua siri za RPC wa Geita , TAKUKURU kwa nini hamjiongezi kuwahoji wote wawili, kuna kitu hakipo sawa kinaendelea hapa" aliandika Mchungaji Msigwa
Mbunge wa Geita alikamatwa na jeshi la polisi na kulazwa rumande kwa masaa 24 kufuatia vurugu zilizofanywa katika mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) lakini alipotoka Mbunge huyo alianza kumshtumu RPC wa Geita na kusema anafahamu mambo yake mengi, akahitaji kuombwa msamaha ndani ya siku tatu na RPC huyo huku akiahidi kutoa siri zake kama hatafanya hivyo.

Huddah Amchana Diamond, ‘A King Lion Without a Heart for Others is Called a Pus*y’

$
0
0
Diamond Platnumz ni kama centre ya ubuyu Bongo. Mrembo wa Kenya Huddah Monroe ameonekana kuwa upande wa adui yake Zari The Bosslady katika sakata zito la Diamod kuzaa na Hamisa Mobetto.

Baada ya bosi huyo wa WCB kuonekana kuishinda kwa asilimia kubwa vita ya usaliti kwa kuzaa nje, kupitia mtandao wa Snapchat, Huddah ameamua kumshushia maneno mazito msanii huyo. Haya ndio maneno aliyoandika Huddah kwenye mtandao huo.


BAD News: Mwanamke Tajiri zaidi Duniani Afariki Dunia

$
0
0
Mwanamke anayetajwa kuwa tajiri zaidi duniani ambaye na mrithi wa Kampuni ya L’Oreal Ufaransa, Liliane Betterncourt amefariki dunia akiwa na miaka 94.

Liliane ambaye utajiri wake ulitajwa na jarida Forbes na Orodha ya Matajiri Duniani (Bloomberg Billionaire Index) kuwa ni wa Dola za Marekani bilioni 44 sawa na Shilingi trilioni 105.6, amefariki nyumbani kwake lakini kumekua na habari kwamba mwanamama huyu alikua na tatizo la akili.

Akiwa na umri wa miaka 15 Liliane alijiunga na kampuni ya baba yake ya L’Oreal ambayo ilijishughulisha na vipodozi ili kujifunza kuendesha biashara hiyo na mwaka 1957 akiwa na 24 alirithi rasmi kampuni hiyo ya baba yake ambayo aliiendesha mpaka alipoiacha akiwa na miaka 89 mwaka 2012 kutokana na matatizo hayo ya kiafya.

Mkuu wa Wilaya Momba Aamua Kuwaonyesha Chadema Nguvu yake

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Momba mkoani Songwe, Jumaa Irando ameamua kutunishiana misuli na madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma kwa kuwaagiza watendaji wa Serikali wasifanye nao kazi.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni mwendelezo wa kutunushiana misuli baina ya vigogo hao baada ya Agosti madiwani hao kupitia kwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Ally Mwafongo kutamka kuondoa ushirikiano na Irando wakidai anaingilia mipango ya halmashauri.

Mwafongo alitoa tamko hilo kwa nyakati tofauti akiwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani na mikutano ya hadhara iliyokuwa ikiandaliwa na Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka na katika kikao cha kamati ya fedha cha halmashauri hiyo kilichoketi Septemba 14.

Akizungumza jana ofisini kwake, Irando alisema agizo lake limeanza kutekelezwa Septemba 18 na aliwataka watendaji wote wa Serikali kuanzia ngazi ya ofisi kuu, kata na mitaa kuacha kutekeleza maagizo, uamuzi, maelekezo, ushauri au maombi mbalimbali ikiwamo posho inayotolewa na mwenyekiti wa halmashauri hiyo pamoja na madiwani wake.

Pia, alisema amemuagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji huo, Kastory Msigala kuwajulisha wananchi namna ambavyo watapata huduma katika kipindi hicho.

Mkurugenzi mtendaji huyo alikiri kupata maelekezo kutoka ofisi ya mkuu wa wilaya na kuwa tayari maelekezo hayo ameyapeleka kwa watendaji walioko chini yake.

Akizungumza kwa simu jana, Mwafongo alisema bado hajapata taarifa za maandishi kuhusu tamko la mkuu wa wilaya lakini amesikia tetesi kuhusu uamuzi huo.

Hata hivyo, alipoulizwa, Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, Elia Ntandu alishauri jambo hilo kumalizwa mezani badala ya kuendekeza malumbano ambayo yanaathiri maendeleo ya wananchi.

Mwananchi:

Mbunge Bashe Afunguka Yanayoendelea 'Tutaacha Tabia ya Kulaumiana'

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Mohamed Bashe amefunguka na kuwataka watanzania kwa ujumla kuacha tabia ya ulalamikaji katika mambo yao wanayoyafanya bali wanapaswa kuweka juhudi ili waweze kufanya vizuri vitu vyao.

Bashe ameeleza hayo kupitia ukurasa wake maalumu wa instagram asubuhi ya leo, huku nchi ikiwa imetanda wingu kubwa la baadhi ya watu kuilalamikia serikali kwa kila jambo wanalofanyiwa bila ya wao wenyewe kutambua kuwa wanatengenezewa misingi mizuri ya taifa lao la Tanzania. Baada ya serikali ya awamu ya tano kuanza kushughulikia vitendo vya rushwa katika sehemu mbalimbali za kutolea huduma pamoja na watu wanaokwepa kodi na kupelekea mzunguko wa pesa kwa baadhi ya watu kuwa mgumu, kwa kuwa walikuwa wanategemea njia za magendo kuendesha maisha yao.

"Sisi kama viongozi, wananchi na kama taifa, tusiwe walalamikaji tufanye juhudi katika kila jambo kulifanya vizuri. Juhudi huendana na jitihada na jitihada huanzia ndani ya nafsi na akili, na ili jitihada ichukue nafasi ni lazima tubadili 'attitude', hulka. Tukibadili tabia tutaacha kuwa watumwa wa 'historian' na tutaacha tabia ya kulaumiana na kuanza kuchukua hatua za kufanya juhudi", ameandika Bashe.

Mwanamke wa Kitanga ndani ya Daladala Balaa Tupu

$
0
0
Hawa wanawake wa kitanga wamezid jamani heeeeee.....

Alikuwa kapanda na bwanake kwenye daladala wamekaa siti moja, mwanamke kamchukua bwanake akamuegesha kwenye kifua chake akawa anamuimbia nyimbo za kimahaba, halafu sio kwa sauti ya chini chini ilikuwa sauti kubwa tu mpaka kila mtu akawa anashangaa na kulalamika kuwa mahaba yao wakafanyie chumbani....

Alipokuwa anashuka akasema "mi ndio mtoto wa kitanga, nimefundwa nikafundika wenye kununa wapasuke twende tukalale laazizi wangu" hahahahahaha

Alinipenda Sana Kabla Hajapata Kazi, Sasa Kapata Kazi Ananiona Bwege

$
0
0

Najuta ni kiherehere cha moyo wangu kukupenda,kukuthamini na jukujali.

Naombeni msaada,ni mpenzi wangu yapata 1&half year katika mahusiano ni binti ambaye tulifahamiana nae siku moja alipokuja na mama yake mdogo ofisini kwangu kupata huduma,

huyu mama yake mdogo ni mtu ninaefahamiana nae hivyo basi akaona haina budi kunitambulisha kwa mwanae nami nikaona ni vizuri kuanzia hapo binti yule alianza kunizoea na kuonesha dalili zote za kunitaka hata baadhi ya siku hufunga safari na kuja kunisalimia.

nami sikua na hiyana huwa sipendi kumkwaza mtu nikawa nampa ushirikiano tu mzur.

kutokana na ubize wa kazi yangu muda wa story huwa sina nikamwambia kama hutojali uwe unakuja saa 12jioni muda ambao nipo off ila sijui kama mama yako mdogo atakubali akasema hilo halina shida nikimwambia nakuja kwako hawezi kunikatalia kiukweli hilo jibu lake lilinipa ulakini!!

Basi jioni tukawa tunaenda sehemu ya utulivu tunapiga story sana tunapata chakula then tunaondoka tuliendelea hivyo kwa muda mrefu huwa anakuwa kama na kitu cha kutaka kuniambia lakini anashindwa kila usiku lazima anipigie simu na asubuhi lazima aniulize umeamkaje.

kutokana na tabia zake nzuri alizozionesha kwangu nikaona pengine Mungu ndo kanionesha mke mwema nikamtongoza japo sikutumia nguvu hata kidogo alitabasam na kufurahi nakumbuka alinikumbatia na kunipiga busu hadi nilihisi kuwewesuka kwa joto lake.

Nikawa namhudumia kila alichokitaka nilimpatia na alinipenda na kuniheshimu kama mume wake.

Nakumbuka aligombana na mama yake mdogo akawa kahamia kwa dada yake ni mbali kidogo huko nadhani maisha yalikuwa ya shida,alikuwa akinipigia simu "leo baby sijala"nikawa namsaidia akiugua namtumia pesa za matibabu,

SASA basi miezi miwili imepita kapata kazi basi ni dharau mwanzo mwisho simu hapigi,text hanitumii hata nikimtext baada ya masaa mawili ndo anareply tena shortly wiki tatu zimepita kanipigia simu anaumwa bila hiyana nikaenda kumuona na nilimpa kila kitu anachohitaji mgonjwa sikutaka maongezi nikaondoka zangu hadi leo sijawasiliana nae sababu ninahasira nae sana na ninataka nimfanyie kitu ambacho hatakisahau ili iwe fundisho au nyie wanajamvi mnanishauri nini?

Kitu Mzee Abdul Amemshauri Mwanae Diamond Platnumz Baada ya Mtoto na Hamisa

$
0
0
Diamond Platnumz kuzaa na Hamisa imekua gumzo sana Tanzania na sasa ni zamu ya kusikia ushauri wa Baba Mzazi wa Diamond Platnumz Mzee Abdul mwenyewe akimshauri mwanae, tazama kwenye hii video fupi hapa chini

VIDEO:


Maafisa wa Tanzania Wasifiwa Kwa Kubana Matumizi Mkutano wa UN New York; Togo, Mali, Nigeria ni Kufuru

$
0
0
MAREKANI: Kituo kimoja cha habari kimeripoti matumizi makubwa ya wawakilishi wa nchi za Afrika waliopo katika mkutano wa Umoja wa Mataifa jijini New York.


  • Aidha wametoa pongezi kwa Wawakilishi wa Tanzania walioripotiwa kukaa kwenye Hoteli ya bei rahisi kulinganisha na mataifa mengine.
  • Wawakilishi wa Gabon wanaishi Plaza Hotel inayodaiwa kulipiwa Dola 1000 hadi 15,000 huku wawakilishi wa Nigeria wakilipia Dola 800 Pierre Hotel
  • Wawakilishi wa Mali wao hutumia kati ya Dola 800 hadi 9,000 kwa usiku mmoja katika Hoteli ya Waldorf-Astoria.
  • Wawakilishi kutoka Swaziland wameonekana wakiwa na bidhaa za gharama kutoka duka la Bergdorf Goodman.
 


=======
As diplomats congregate for the United Nations General Assembly, delegations from some of the poorest countries in the world are spending extravagantly in New York City while their homelands struggle, NBC 4 New York's I-Team has discovered. 

“The lavish spending is just endemic of autocratic politics as a whole,” said Alastair Smith, a politics professor from New York University and co-author of “The Diplomat’s Handbook.”

He believes the U.N.’s Manhattan address has become a distraction from the intended work of the General Assembly.

“They are here for the shopping, the food the wine, the dining. If it was in a less attractive place, I'm sure fewer people would want to come as hangers-on,” said Smith.

On Monday, I-Team cameras found several visitors with the U.N. delegation from Swaziland walking out of high-end retailer Bergdorf Goodman. The women had Bergdorf Goodman shopping bags, though they said the items inside were just gifts.

According to U.N. data, nearly 70 percent of Swazi people survive on less than $2 a day. The nation has one of the highest AIDS rates: 18 percent of the population is HIV positive.

Despite those struggles back home, numerous members of the Swaziland U.N. entourage are staying at the luxury Mandarin Oriental Hotel, the I-Team has learned.

Also staying at the Mandarin Oriental were members of the delegation from Togo. According to one U.N. report, 2.4 million Togolese citizens live on less than $1.25 a day.

Diplomats from Gabon were staying at the Plaza Hotel, where rooms go for a $1,000 to $15,000 a night.

Nigeria’s delegation is keeping five vehicles parked outside the Pierre Hotel where the cheapest room is about $800 a night – or roughly what most Nigerians earn in two years.

At the Waldorf-Astoria, where rooms are between $800 and $9,000 a night, the I-Team found the delegation from Mali, a country where 4.6 million people are battling starvation. A recent U.N. report found Mali is the third poorest nation in the world with a poverty rate near 87 percent.

To be fair, not every poor nation spent so much for hotel accommodations: Members of the Tanzania delegation were found staying at a DoubleTree hotel in Midtown.

Although it may be unseemly for diplomats from poor countries to live ostentatiously during their stays in Manhattan, advocates for business point out there is an undeniable upside to much of the diplomatic extravagance – the boon for New York City’s local economy.

"I don't think it is really up to us to moderate the type of spending that comes from other countries. That's their business,” said Nancy Ploeger, president of the Manhattan Chamber of Commerce. “What I'm concerned with is the economic impact on this city. I like the money. I want the money!"

None of the permanent missions to the UN from Togo, Swaziland, Gabon, Mali or Nigeria returned calls or emails relating to this story.

Nonprofits that monitor developing nations are also becoming increasingly sensitive to the issue of third world rulers spending lavishly abroad.

The group “100 Reporters” is actually holding a contest asking New Yorkers to snap photos of UN diplomats spending ostentatiously.

By one estimate, the ruling classes of third-world nations divert as much as $1 trillion from their developing economies to spend and invest the funds in the U.S. and other Western nations.

“The real underlying motivation for the movement of so much money out of developing countries is the hidden accumulation of wealth,” said Raymond Baker, executive director of Global Financial Integrity, a nonprofit watchdog that monitors capital flows into and out of impoverished countries.

“This is about getting rich secretly and not having to distribute those funds locally,” Baker 

Source:UN Delegates Live Large in NY While Their People Starve

Breaking: Mbunge Peter Msigwa Anashikiliwa na Polisi

$
0
0
Kupitia ukurasa wa Twitter wa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema, ameandika hivi;-

 "Msigwa amekamatwa na Polisi huko Iringa na kushushwa kwa nguvu jukwani  ktk Mkutano halali. Msiogope baada ya giza nene asubuhi hutokea!"

Taarifa hiyo iemethibitishwa na kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Kamishna wa polisi Julius Mjengi, Ambapo ameuleza mtandao huu kuwa Msigwa alikuwa na mkutano wa hadhara leo Septemba 24, katika eneo la Mlandege mkoani humo ambapo anadaiwa kutumia lugha na matamshi ya uchochezi katika hotuba yake.


Hata hivyo Kamanda Mjengi ameongeza kuwa tayari wameanza kumuhoji

Bunge Limeijibu Hospitali ya Tundu Lissu..Waonyesha Mpaka Risiti Kuondoa Utata

$
0
0
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Septemba 24, 2017 limetoa ufafanuzi na uthibitisho wa risiti ya malipo ya fedha za wabunge milioni 43 kwa ajili ya matibabu ya Tundu Lissu ambazo zilichangwa na wabunge na kulipwa hospitali ya Nairobi.

Bunge limelazimika kutoa taarifa hiyo baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa hospitali ya Nairobi mbaka jana ilisema haijapokea fedha hizo kutoka kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Ofisi ya Bunge inapenda kusisitiza kuwa fedha zilizochangwa na Wabunge kiasi cha Tsh. Milioni 43 kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Mheshimiwa Tundu Lissu tayari zimetumwa katika Akaunti ya Hospitali ya Nairobi anakopatiwa matibabu. Fedha hizo zimetumwa kupitia Benki kuu ya Tanzania (BOT) ambapo kwa mujibu wa viwango vya kubadilishia fedha vya BOT kwa siku hiyo ilikuwa ni sawa na Shilingi ya Kenya 1,977,120.58." ilisema taarifa ya Bunge

Taarifa hiyo ya Bunge iliendelea kusisitiza kuwa walituma fedha hizo Septemba 20, 2017
"Kiasi hicho cha Fedha kilitumwa siku ya tarehe 20 Septemba, 2017 kwenda Benki ya Barclays, Tawi la Hurlringham, Akaunti Namba 0451155318 yenye jina la Kenya Hospital Association"

Septemba 22, 2017 Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe alisema kuwa mbaka siku hiyo anatoa taarifa mbalimbali kuhusu Tundu Lissu fedha ambazo wabunge walikuwa wamechanga kwa ajili ya matibabu ya Tundu Lissu zilikuwa hazijafika Hospitali Nairobi Kenya, lakini siku moja baadaye Bunge lilitoa taarifa na kusema walikuwa wameshatuma fedha hizo toka Septemba 20 mwaka huu, baadaye zikawepo taarifa kutoka hospitali ya Nairobi kuwa bado hawajapata fedha hizo kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Pole Pole Afunguka 'Leo Afrika Nzima Inazizima Kwamba Yupo Mwanaume Ambaye Ameweza Kusema Imetosha'

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amefunguka kwa kumsifia Rais John Magufuli kwamba ni mwanaume pekee aliyeweza kuifanya Afrika nzima ikazizima kwa kuweza kupinga vitendo vya unyonyaji kwa taifa la Tanzania.

Polepole ameeleza hayo kupitia ukurasa wake maalumu wa facebook mchana wa leo huku akinukuu baadhi maneno aliyowahi kuyatoa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambayo yalikuwa wazi kabisa yakiongelea namna ya kujikomboa ili bara la Afrika kiujumla liweze kufikia uhuru wake wa kiuchumi.

"Leo Afrika nzima inazizima kwamba yuko mwanaume ambaye ameweza kusema imetosha 'enough is enough' siyo haki na ni unyonyaji kuchukua madini yetu katika namna ambayo haki yetu inapokwa. Ndugu Magufuli ana amini sana katika sekta binafsi na hasa katika ujenzi wa uchumi wa viwanda sambamba na sekta ya umma. Lakini ana amini zaidi katika sekta binafsi inayojiendesha kwa kanuni za maadili ikiwemo kulipa kodi. Anaamini katika uwekezaji kutoka nje, lakini unaotambua kwamba sisi ni taifa huru na tunayo haki ya kunufaika kutokana na utajiri wa rasilimali zetu", ameandika Polepole.

Aidha, Polepole amesema CCM imemleta Rais Magufuli katika wakati muafaka ambapo nchi ilikuwa inaelekea pabaya.

"Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemleta ndugu Magufuli wakati muafaka wakati tunamuhitaji zaidi mtu kama yeye. Ukisoma maelezo na nukuu za Mwalimu Nyerere katika maelezo yangu ya awali juu ya maono ya Mwalimu Nyerere utaungana nami kusema ile aina ya uongozi mpya katika bara la Afrika, Tanzania tumekuwa kinara wa kwanza na wengine watafuata ili bara la Afrika lirejeshe heshima yake ya uhalisia na asili", amesisitiza Polepole.

Kwa upande mwingine, Polepole amesema ipo siku ataeleza ni kwanini Rais Magufuli amekuwa zawadi katika taifa la Tanzania kwenye kipindi hiki.

Tundu Lissu Amtumia Salamu Waziri Ummy Mwalimu...Adai Atamjibu Mwenyewe

$
0
0
RAIS wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu,  ameibuka na kusema, “vijembe vinavyorushwa na Ummy Mwalimu,” Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, “vitajibiwa na mimi mwenyewe,”

Akihutubia mkutano wa nusu mwaka wa mawakili nchini (AGM), kaka mkubwa wa Lissu, Alute Mughwai Lissu, ameeleza kuwa ameelekezwa na mdogo wake huyo, kutomjibu Ummy Mwalimu, badala yake kazi hiyo itafanywa na yeye mwenyewe.

Alute ambaye ni wakili wa kujitegemea anayefanya shughuli zake mkoani Arusha ameuambia mkutano huo, “nimeongea na Lissu leo saa nne asubuhi. Amenielekeza kuwa familia isijibu hoja za waziri Ummy Mwalimu.”

Amesema, “kazi hiyo itafanywa na yeye mwenyewe mara akataporejea nchini kutoka kwenye matibabu yake nje ya nchi. Ameahidi kuendeleza mapambano ya kudai haki bila kuchoka.”

Wakili Alute amesema, Lissu amemueleza kuwa “hatarudi nyuma katika harakati zake za kutetea haki na demokrasia nchini. Ameapa kupambana hadi tone lake la mwisho.”

Kwa mujibu wa Alute, afya ya Lissu inaendelea vizuri na anawashukuru madaktari wanaomtibu kwenye hospitali ya Nairobi alikolazwa. Amewataka wajumbe wa mkutano huo kuendelea kumuombea.

Alute alikuwa akitoa salamu kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa TLS uliofanyika jana mjini Arusha.

Hii ni mara ya kwanza kwa Lissu kuzungumza kwa simu tokea aliposhambuliwa kwa risasi na wanaoitwa na serikali, “watu wasiofahamika,” ambako alimiminiwa rundo la risasi zilizolenga kuondoa maisha yake.

Wakati huohuo, akiongea na Azam TV, Alute Lissu amesema kwamba familia yake imemwandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakiomba uchunguzi wa tukio la kushambuliwa mdogo wake ufanywa na vyombo kutoka nje ya nchi, kwani katika mazingira ya sasa jeshi la polisi haliko tayari na haliko huru kufanya uchunguzi huo kwani hadi sasa hakuna mtu yeyote aliyekamatwa.

Kuhusiana na serikali kuitaka familia iandike barua ya kuomba matibabu kwa ajili ya Tundu Lissu, kaka yake huyo alisema mdogo wake huyo ambaye anatibiwa Nairobi amemwambia suala hilo atakuja kulizungumzia yeye akiwa ni mbunge mwenye haki zote za kupewa matibabu kama wabunge wengine.

Vyanzo: Mwanahalisi na Azam TV.

Waziri Mwijage aAkiri Kukwamishwa na Baadhi ya Taasisi Serikalini

$
0
0

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage amelalamikia baadhi ya taasisi za serikali kumkwamisha kwenye utekelezaji wake kwa kuchelewesha kutoa vibali kwa wawekezaji.

Mwijage amesema hayo kwenye uzinduzi wa Bodi mpya ya TIC jana jijini Dar es salaam huku akiitaka bodi hiyo kuchukua jukumu hilo la kuwaambia ukweli taasisi za serikali zinazokwamisha uwekezaji nchini kwa kuchelewa kutoa kibali na kusema kuwa watambue mchezo wao huo ni mauti kwa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

“TIC nategemea mtakuwa na jukumu la kuziambia taasisi za zingine za serikali kwamba hamfanyi vizuri na kwamba mchezo wenu ni mauti kwetu, kama mimi natafuta wawekezaji nasafiri, nabembeleza, nasalimia watu ambao wasingepata nafasi ya kusalimiana na mimi, nakosa kukaa na familia yangu, nakosa kukaa kwenye jimbo langu, nasafiri nazunguka naleta wawekezaji halafu yupo mtu anatumia mwezi mzima au miaka miwili kutoa kibali, TIC mnapaswa mniambie” amesema Waziri Mwijage kwenye uzinduzi wa bodi mpya ya TIC.

Kwa upande mwingine, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF),  Bwana Godfrey Simbeye ametahadharisha wanasiasa kuhusu kauli zao zinazowakatisha tamaa wawekezaji kuacha mara moja.

Mbunge Peter Msigwa:Polisi Hawawezi Kunipangia Nini cha Kusema na Wala sio Majukumu

$
0
0

Anaandika Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Peter Msigwa.

"Polisi hawawezi kunipangia nini cha kusema na wala sio majukumu Yao. Wamenikamata nikitimiza majukumu yangu ya kibunge! SITANYAMAZA!"

Madhara ya Unywaji Pombe kwa Mama Mjamzito

$
0
0
Mtoto awapo tumboni hupata chakula (maji na virutubisho lishe) vyote kupitia kwa mama yake. Mama akila mlo ulio kamili awapo mja mzito mtoto pia hupata mlo kamili na iwapo mama hapati mlo kamili huwa hivyo kwa mtoto pia. Je mtoto anakulaje awapo tumboni? Chakula huingia mwilini kwa mtoto anayekuwa tumboni mwa mama yake kupitia kondo la nyuma au ‘placenta’ kwa Kiingereza. Hivyo mama anywapo pombe vilevile nayo huingia kwa mtoto kupitia kondo la nyuma.

Pombe hujipenyeza kwa kasi katika kondo la nyuma la mama na kiwango cha kilevi katika mwili wa mtoto (blood alcohol level) huwa sawa na kiwango cha pombe kilichomo katika mwili wa mama. Kwamba humuoni mtoto awapo tumboni si hoja sana kwani ushahidi unaonyesha kwamba athari za unywaji pombe wa mama una matokeo hasi katika ukuaji wa mtoto. Yaani baadhi ya athari huwa na matokeo ya kudumu ikiwa ni pamoja na kudumaa kwa akili za mtoto pindi anapozaliwa, madhara ya jumla katika ukuaji wa mwili hasaa ubongo wa mtoto.

Iwapo ulikunywa pombe ukiwa mjamzito, je ni zipi dalili za athari za pombe kwa mtoto? Ingawa dalili ni nyingi, makala haya yatajikita katika dalili za kudumaa kwa akili ya mtoto baada ya kuzaliwa. Mtoto mwenye tatizo hili hupata taabu kuwakumbuka ndugu na jamaa wa karibu hata wale anaoshinda nao nyumbani.

Ingawa watoto wa umri huu hupendelea kucheza na vitu vinavyowazunguka, mtoto huyu hapendi ‘kujishughulisha’ na vitu vinavyomzunguka. Unashauriwa kumpeleka mtoto kwa wataalamu wa afya kupata msaada zaidi pindi unapohisi mtoto ana tatizo.

Mwongozo wa kitaalamu wa makuzi ya mtoto unaonesha kwamba mtoto wa umri wa miezi sita anapaswa kuwa na uwezo wa kufanya mengi ya mambo yafuatayo; toka anazaliwa anapaswa kuweza kugeuza shingo lake kufuata mwelekeo sauti inakotokea, aweze kushika miguu yake akiwa amelala kifudifudi, aweze kukuangalia anapokuwa ananyonya / kula, aweze kutabasamu aonapo nyuso na kusikia sauti za watu anaowafahamu, aweze kulia anapoudhiwa / ama akiwa hajisikii vizuri (mgonjwa, njaa, nk.), apate kutoa sauti mbalimbali ikiwapo kwikwi ndogondogo na hata kupiga kelele na mwisho awe na tabia ya kutaka kutia kila akishikacho mdomoni mwake.

Moja ya njia kuu za kumlinda mtoto na madhara yatokanayo na unywaji pombe ni kwako mama mjamzito kuacha kunywa pombe mara tu unapogundua una ujauzito. Iwapo huwezi kabisa kuacha kunywa pombe basi unashauriwa kwenda kwa daktari na kupata ushauri zaidi. Kumbuka kuacha kunywa pombe katika hatua yoyote ya ujauzito kutakuongezea nafasi ya kujifungua mtoto mwenye afya na siha njema.

Chanzo: Mwananchi

Joshua Nassari: 'Nipo Tayari Kujiuzulu Ubunge..Nina Ushahidi Madiwani Kupewa Rushwa Kujiuzulu'

$
0
0
Mbunge wa Chadema wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari ameweka rehani ubunge wake  baada ya Rais John Magufuli kumpokea aliyekuwa diwani wa chama hicho aliyejiuzulu akisema ni kwa sababu ya kuunga mkono juhudi za Rais.

Nassari amedai ana ushahidi wa kielektroniki unaoonyesha madiwani hao walivyopewa rushwa ili wajiuzulu nafasi zao.

Hata hivyo, diwani wa Kata ya Kimandolu, Mchungaji Rayson Ngowi ambaye amepokewa na Rais Magufuli juzi  baada ya kujiuzulu Chadema akizungumzia tuhuma hizo alisema madai hayo hayana ukweli wowote na kama Nassari ana ushahidi ni vyema angeutoa hadharani.

Ngowi aliwashauri Chadema mkoani Arusha watatue matatizo yaliyopo ndani ya chama hicho na wasitafute visingizio kwa kuwa yeye ameamua kujiuzulu kwa kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli na hajapewa rushwa yoyote.

Diwani mwingine aliyejiengua katika chama hicho wa Kata ya Muriet, Credo Kifukwe alisema hakuna chochote alichopewa kama rushwa kwa lengo la kujiuzulu, akimshauri Nassari autoe hadharani ushahidi anaousema na si kushusha tuhuma zisizo na mashiko.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Nassari alisema ushahidi huo ameuhifadhi ndani ya ‘flash disc’ na yuko tayari kumkabidhi Rais Magufuli na vyombo vya uchunguzi.

Mbunge huyo alisema endapo ikithibitika kuwa ushahidi wake ni wa uongo yuko tayari kujiuzulu nafasi yake ya ubunge.

“Ninao ushahidi na kama Mheshimiwa Rais yuko tayari niko tayari kumpatia ninayo flash, ushahidi ninao kwa muda mrefu na tulijua watapokelewa juzi madiwani wawili lakini mmoja amekataa akaenda mmoja,” alisema Nassari.

Alidai kwamba  kwa kipindi kirefu alipokuwa masomoni nchini Uingereza alikuwa akijiuliza ni kwa nini madiwani katika Mkoa wa Arusha wamekuwa wakijiuzulu na ndipo alipoamua kufanya uchunguzi wa kina.

Nassari akiwa ameambatana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema katika mkutano huo, alisema alianza kufanya uchunguzi Mei kwa kutumia vifaa vya kielektroniki alivyovinunua nchini Uingereza na kubaini kwamba baadhi ya madiwani wanaojiuzulu walipewa rushwa ya fedha, ahadi ya vyeo na ya makazi.

Alisema uchunguzi juu ya tuhuma za madiwani hao kujiuzulu aliufanyia ndani ya ofisi ya umma akisisitiza hakuna diwani wa Chadema mkoani Arusha ambaye amejiuzulu kwa kumuunga mkono Rais Magufuli bali wamepewa rushwa.

“Mheshimiwa Rais anapambana na rushwa lakini kuondoka kwa madiwani ni mfumo wa rushwa anaopambana nao niko tayari kujiuzulu nafasi yangu ya ubunge endapo ikithibitika ushahidi wangu ni wa uongo,” alisema Nassari.

Madiwani wapatao 10 wa Chadema wamejiuzulu kwa nyakati tofauti. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole ameshawahi kunukuliwa akikanusha tuhuma za kupewa rushwa madiwani wanaojiengua kutoka Chadema na kujiunga na CCM.

Polepole Julai alikaririwa akisema iwapo Chadema ina viongozi wanaoweza kuhongwa na wakahongeka basi ni chama cha  ovyo kwa kuwa chama kilicho imara na watu wake wapo safi hawawezi kuhongeka.

Alitoa kauli hiyo mjini Bagamoyo alipohudhuria mahafali ya Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu (Tahliso) Mkoa wa Pwani.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatatu

Mbunge wa Iringa Peter Msigwa Aachiwa kwa Dhamana

$
0
0
Mbunge wa Iringa Peter Msigwa Aachiwa kwa Dhamana
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema) Peter Msigwa ameachiwa huru jana usiku  kwa dhamana baada ya kukamatwa akiwa kwenye mkutano wa hadhara.

Msigwa ameachiwabaada ya kudhaminiwa na wadhamini wawili Alex Kimbe pamoja na Mwenyekiti wa Bavicha Iringa  Leonce Marto , saa nne usiku .

Msigwa alishushwa  jukwaani kwa nguvu  akiwa anahutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Mlandege Manispaa ya Iringa na anatuhumiwa kwa kosa la uchochezi dhidi ya vyombo vya usalama .

Marto  amesema  mikutano yake imefungiwa na hapaswi kuendelea na ziara yake katika kata nyingine  mpaka hapo OCD atakapo amua vinginevyo.

Leo  Mbunge anatakiwa kuripoti kwa RCO na huenda kesi ya uchochezi ambayo tayari imeshafunguliwa jalada lake ikapelekwa mahakamani .

Amesema  Mbunge huyo  atazungumza na vyombo vya habari leo mchana  kuweka wazi madhila yaliyompata wakati akitekeleza wajibu wake kwa wananchi.

Msimamo wa Askofu Munga Kuhusu Hali ya Usalama Wapongezwa na Wananchi

$
0
0
Msimamo wa Askofu Munga Kuhusu Hali ya Usalama Wapongezwa na Wananchi
Kitendo cha Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dk Stephen Munga kuzungumzia hali ya usalama nchini na kuweka bayana msimamo wake, kimepongezwa na wananchi na kutaka viongozi wa madhehebu mengine kuiga mfano huo.

Katika ibada maalumu ya kuliombea amani Taifa iliyofanyika katika Kanisa la KKKT jijini Tanga juzi jioni, askofu huyo aliweka bayana kwamba Serikali haiwezi kukwepa lawama kutokana na matukio yanayotokea nchini kwa kuwa inao wajibu wa kulinda raia.

Alisema matukio ya kuchomwa mabweni ya wanafunzi, kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Meja Jenerali mstaafu wa JWTZ, Vincent Mritaba na kutekwa kwa watoto mkoani Arusha, yamewatia hofu wananchi.

Alisema Serikali inao wajibu wa kudhibiti matukio kama hayo yasitokee na kuonya kwamba yakiachwa, yanaweza kuifanya Tanzania kuwa kama nyumba iliyoingiwa na joka linalowagonga na kuwaua watoto, huku likiwa halionekani na kuzua hofu kubwa.

Alisisitiza kuwa amani iliyopo ni lulu isiyotakiwa kuachwa ipotee.

Katika maombi hayo ambayo waumini walifurika kanisani hapo na kulazimika wengine kusimama nje, waliwaombea wanaoendesha unyama dhidi ya wasiokuwa na hatia waangamizwe.

Wakizungumza kuhusiana na mahubiri hayo, baadhi ya wakazi wa Tanga walisema Askofu Munga ameonyesha njia kwa viongozi wengine, “Ninachojua hata kwa masheikh kuna hadithi zinazowatahadharisha kuwa kila mchunga, siku ya kiyama ataulizwa aliwachungaje aliokuwa akiwaongoza ili wasipotee, kama hakutekeleza hilo atambue kuwa hakuna atakayemtetea,” alisema muumini wa kanisa hilo, Julius Mjata.

Mkazi mwingine, Ramadhani Manyeko alisema sheikh au askofu asiyepaza sauti kutokana na hali ilivyo hivi sasa, ajitathmini upya kama anatosha.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images