Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Shuhudia Arusi ya Lulu na Joti...Jua Ukweli wa Mambo Hapa

$
0
0
This is what Lulu captioned the first photo!!! On her INSTAGRAM account “N now u can Kiss the BRIDE����....... Samahani Waheshimiwa Wabunge...hii ni kazi tu...sirudii tena...msituweke kwenye ile List cc @wemasepetu #Ndukiiiiiiiiii Cc @jotimdebwedo @tmt_tz

Then,


Mdee Atoboa Uozo, Ahoji Safari za Rais Kupewa bil. 50/-,Awataka Wakulima, Wafugaji Kuipiga Mawe CCM

$
0
0
MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA), amewataka wakulima, wafugaji kuipiga mawe Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kutenga sh bilioni 50 kwa ajili ya safari za rais huku ikitenga sh bilioni 51 kwa maendeleo ya kilimo.

Akichangia hotuba ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2014/2015, Mdee alisema serikali haina nia ya dhati ya kuutokomeza umasikini, ikiwemo kuwawezesha wakulima, wafugaji na wavuvi.

Alibainisha kuwa katika bajeti ya mwaka jana, serikali iliahidi asilimia 10 ya bajeti itakwenda kwenye kilimo, lakini ikaishia kutenga asilimia nne, na bajeti ya mwaka 2014/2015 imetenga sh bilioni 51 kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya kilimo.

Alisema kiwango hicho kimepishana kidogo na kile kilichotengwa kwa ajili ya safari za Rais Jakaya Kikwete, ambazo zimetengewa sh bilioni 50.

“Wakulima, wafugaji na wavuvi wanapaswa kuipiga mawe Serikali ya CCM, hapa mmetuletea bajeti, lakini ukiangalia kwa kina utaiona haina dhamira ya kuwasaidia wananchi,” alisema.

Mdee, alisema bajeti ya Wizara ya Kilimo kila mara imekuwa ikitengewa fedha, lakini hazifiki kwa walengwa, hivyo mipango mbalimbali imeshindwa kutekelezeka.

Alisema kuwa serikali kupeleka huduma kwa wananchi ni lazima na sio hiyari, hivyo wabunge wa upinzani wanapokosoa utendaji wa serikali hawafanyi jambo baya bali wanatekeleza wajibu wao.

Aliongeza kuwa serikali kila mara imekuwa ikipewa ushauri mbalimbali, lakini inashindwa kutekeleza jambo linalosababisha kukosa mapato yanayotakiwa.

Alisema miaka minne iliyopita upinzani ulipendekeza kodi ya mishahara kwa wafanyakazi ishuke chini ya asilimia 10, lakini serikali ilishindwa kutekeleza jambo hilo hadi hivi sasa ilipoamua kushusha kutoka asilimia 13 hadi 12.

Aliongeza kuwa Kamati ya Bajeti inafanya kazi kwa niaba ya Bunge na imelalamika inatoa mapendekezo serikalini lakini inapuuzwa hali inayoonyesha serikali haina dhamira ya kutafuta vyanzo vipya vya mapato visivyowaumiza wananchi.

Mkosamali amvaa Chenge

Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi), aliituhumu Kamati ya Bajeti kuwa inafanya vikao visivyo na tija ilimradi ihalalishe wajumbe wake kupewa sh 500,000 kwa kila kikao.

Alisema anashangazwa na kamati hiyo kuendelea kulalamikia kupuuzwa kwa ushauri wanaoutoa kwa serikali wakati wana uwezo wa kutoa azimio la kukataa bajeti hadi walichokishauri kifanyiwe kazi.

“Jamani tuwe wakweli hapa, sisi tunalalamika tu wakati uwezo wa kubadilisha mambo tunao, tukubaliane hapa kuikataa bajeti hii mpaka serikali itakapoleta bajeti yenye tija kwa taifa.

“Kamati ya mzee Chenge taarifa yao inalalamika kuanzia mwanzo mpaka mwisho halafu inasema inaunga mkono bajeti, hivi kama si unafiki ni nini? Inakaa hivi sasa na mashirika kujadili kuwapunguzia kodi… hii ni rushwa tupu,” alisema.

Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), alisema serikali imeshindwa kutumia ushauri wa kuanzisha kituo cha uvuvi wa samaki katika bahari kuu, ambako samaki wanavuliwa bila kulipiwa ushuru na kampuni kubwa.

“Nyinyi serikali mna tatizo gani kila mwaka tunawapa ushauri na wataalamu wenu wanaandika ripoti zinazoonyesha umuhimu wa kuanzia kituo cha uvuvi katika bahari kuu, huko tunapoteza mapato mengi lakini hamjali, nyinyi akili zenu zinawaza nini?” alihoji.

Mbunge wa Kisarawe, Suleiman Jaffo (CCM), alisema kiwango cha asilimia kilichopunguzwa kutoka katika kodi inayotozwa kwenye mishahara ni kidogo na hakina msaada kwa wafanyakazi.

Alisema serikali inapaswa kujikita zaidi kwenye kutafuta vyanzo vipya vya mapato badala ya kila kukicha kuwabana wafanyakazi na wananchi.

Baada ya Kudondoka Kutoka Kwenye Gari na Kufariki Maiti yakaa eneo la ajali saa 21

$
0
0
MWILI wa Idd Shamba aliyefariki dunia kwa ajali ya barabarabi katika Kijiji cha Engaruka wilayani hapa, imekaa barabarani kwa zaidi ya saa 21 ikisubiri polisi na daktari kufika eneo la tukio kwa ajli ya kupima ajali hiyo na kuufanyia uchunguzi mwili huo kabla kwenda kuzikwa.

Polisi walifika eneo la tukio majira ya saa saba mchana ikiwa ni saa 18 tangu kutokea kwa ajali hiyo ambapo baada ya kumaliza kazi ya kukagua na kupima eneo la ajali, mwili huo ulihamishiwa chini ya mti kuukinga na jua usiharibike wakati wakisubiri daktari kuja kuufanyia uchunguzi.

Tanzania Daima ilishuhudia wananchi na viongozi wa Kata ya Engaruka wakiulinda mwili huo wakati akisubiriwa daktari kutoka Mto wa Mbu ambaye naye alifika eneo la tukio majira ya saa 10 jioni.

Ajali hiyo ilitokea Juni 12 mwaka huu baada ya Shamba kudondoka kutoka kwenye gari la mizigo aina ya Toyota DCM, lenye namba za usajili T 995 AMB lililokuwa likitokea mnadani Engaruka kwenda Kijiji cha Selela.

Diwani wa kata hiyo, Pashet Sengerwan (CCM), alisema kuwa mwili huo ulifanyiwa uchunguzi kwenye eneo la ajali kisha kuzikwa Juni 13, majira ya saa 11 jioni kwenye makaburi ya kijijini hapo bila kuwasubiri ndugu zake waliokuwa wakitokea Singida.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Liberatus Sabas, alisema tayari wameshamhoji mmiliki wa gari hilo, Sauli Kitomari huku wakiendelea na juhudi za kumtafuta dereva wa gari hilo ambaye alitoroka mara baada ya kutokea ajali hiyo.

Alisema kuchelewa kwa polisi kufika eneo la tukio, kulitokana na kukosekana kwa kituo cha polisi kwenye eneo la Engaruka ambalo pia lina tatizo la mawasiliano ya simu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Moduli, Dowika Kasunga, alisema hali hiyo ilisababishwa na tatizo la mawasiliano na mamlaka husika kwani katika Kata ya Engaruka ili upige simu, lazima uende umbali mrefu kutafuta mawasiliano hayo.

Huyu Ndiye Mpenzi Mpya wa Irene Uwoya! Azungmzia Tofauti ya Umri wao na Mipango Yao.

$
0
0
Mkali wa Sound Track ambaye pia ni mkali wa kuvunja (dancer) amezungumzia uhusiano wake na muigizaji mrembo wa Bongo Movies, Irene Uwoya.

Akiongea na tovuti ya Times Fm, Msami alizunguka sana mbuyu kutaka kutoa maelezo kuhusu ukweli wa mambo kati ya wawili hao lakini kwa mara ya kwanza aliamua kuiambia tovuti ya Times Fm kauli yake kutokana na jinsi alivyoulizwa.

“Kaongea kwa upole huyu jamaa, kaapproach ili apate jibu. Ni kweli (kicheko)…nimekuridhisha lakini, nimeamua kukuridhisha.” Amesema Msami..

Muonekano wa Irene Uwoya na Msami kwa muonekano uliwafanya wengi wazungumze kwenye mitandao ya kijamii kuwa Msami amegeuka Serengeti Boy kwa Uwoya ambaye wanaamini anamzidi sana umri. Lakini ukweli ni kwamba Msami ni mkubwa kwa Uwoya. Chukua hiyo!

“Unajua mimi mwanzo, Serengeti Boy nilikuwa sina tafsiri yake kabisa yaani. Yaani ile deeply nilikuwa sina tafsiri yake kabisa yaani. Kwa hiyo leo ndio nimepata tafsiri yake ‘Serengeti Boy’ kumbe ni mtu ambaye amezidiwa umri. Tofauti na mimi nilivyokuwa nawaza kuhusu Serengeti Boy.

“Lakini mbona nikasema kama ni hivyo, as we are best friends lakini (joke), lakini mbona mimi nimemzidi umri Uwoya. Lakini mimi ni mkubwa kwake sema yeye ananizidi umri. Mimi ni mkubwa kwake nimemzidi miezi mingi…yaani wewe jua nimemzidi miezi mingi. Mimi ni mkubwa kwa Uwoya.” Alisisitiza Msami 

Katika hatua nyingine, Msami ameeleza mpango wake na Uwoya kutoa filamu ya pamoja na jinsi filamu itakavyokuwa.

Amesema katika filamu hiyo yeye ndiye mhusika kuu na kwamba ni filamu ambayo itahusisha dance na muziki. Filamu hiyo itatoka mwaka huu lakini bado haijapata jina rasmi na tarehe ya kutoka.

“Movie inakuja very soon, watu wakae tayari.” Amesisitiza

Watoto wa Will Smith Hulala na Nyoka 10 Chumbani, Wengine Hawajafungwa

$
0
0
Watoto wa Will na Jada Smith, Willow na Jaden wana mengi ya ndani ambayo wengi walikuwa hawayafahamu.

Kwa mujibu wa US Weekly, Willow Smith mwenye umri wa miaka 13 hulala na nyoka kumi chumbani kwake na baadhi yao hawajafungwa kabisa!

Lakini sio pekee ambaye ana mapenzi na nyoka hao, kaka yake Jaden pia huwachukulia nyoka wa dada yake kama wapenzi wake kwa kuwa huwa wanaingia chumbani kwake na kulala nae kitandani huku wakijizungusha mwilini kwake!

Willow ameshawazoea nyoka hao kwa kuwa alianza kuishi na nyoka wa kwanza mwaka 2008 wakati akiwa na umri wa miaka 7 tu.

Jada Pinkett aliwahi kulimbia jarida la Rebok mwaka jana kuwa yeye anawapenda sana nyoka na mwanae Willow pia amekuwa anawapenda daima.

“Anaweza kwenda kwenye store ya nyoka akachukua nyoka mmoja na akajizungushia. Sikuwahi kumgusa nyoka hapo kabla, na nilikuwa siwezi kuwashika…..nimekuwa nampenda Willow daima tangu mwanzo. Nilimwambia Willow, ‘umemfanyia mama msaada mkubwa. Umenisaidia kushinda uoga’.

Picha ya mhalifu yawavutia Wanawake, Wapanga Kuchangisha Pesa Kumtoa Jela

$
0
0
Kitengo cha polisi cha Stockton, California kimezua mjadala mpya baada ya kupost kwenye Facebook picha za mhalifu ili kipate msaada wa taarifa zaidi za raia lakini kilichotokea na kuwa picha hiyo imewavutia zaidi wanawake walibaki kuzungumzia uzuri wa mwanaume huyo.

Picha ya mhalifu huyo aliyetajwa kwa jina la Jeremy Meeks (30) anayekabiliwa na kiesi ya kumiliki bunduki kinyume cha sheria imepata likes zaidi ya 66,000 na comments zaidi ya 20,000 kutokana na uzuri wa mhalifu huyo.

Jeremy anatakiwa kutoa kiasi cha $900,000 ili aachiwe huru. Lakini wanawake wengi waliocomment kwenye picha hiyo wanazungumzia kuhusu kuchangia pesa ili wamtolee dhamana.

Baada ya Mambo Kuwa Mazito GWAJIMA Ajitosa Kumwokoa Mume wa FLORA MBASHA

$
0
0
Wakati  mume wa mwimba Injili Bongo,  Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha akiachiwa huru kwa dhamana kufuatia kesi ya kudaiwa kumbaka shemejiye, Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la jijini Dar es Salaam, Josephat Gwajima ameibuka na kunena mazito kuhusiana na sakata hilo.

Mbasha aliachiwa kwa dhamana juzi akitokea Gereza la Keko, Dar baada ya kupandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Juni 17, mwaka huu na kusomewa mashitaka mawili ya ubakaji ambayo hata hivyo, aliyakana.
ILIVYOKUWA KORTINI

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, mheshimiwa Wilbeforce Luago siku hiyo ya Juni 17, alitoa hoja kwamba upande wa jamhuri hauna pingamizi hivyo dhamana ipo wazi.

Alisema mshitakiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili, mfanyakazi wa serikali na wa kutoka katika taasisi inayotambulika sanjari na shilingi milioni 5 kila mmoja. Mshitakiwa alishindwa kutimiza masharti hayo siku hiyo hadi hadi juzi alipotimiza, akaachiwa.
Mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo ambaye ni wakili wa serikali, Nassoro Katuga bila kuchelewa aliitaja kesi hiyo yenye namba CC/186/2004 ambapo rafiki wa Mbasha aliyejitambulisha kwa jina la George Mushi na baba wa mtuhumiwa aitwaye Mwahimu Juma ndiyo waliofanikisha dhamana hiyo. Kesi yake itatajwa tena Julai 17, 2014.
GWAJIMA SASA

Akizungumza na mwanahabari wetu juzi wakati Mbasha akiwa nje kwa dhamana, Mchungaji Gwajima alieleza namna ambavyo sakata hilo limeitikisa Injili nchini Tanzania kutokana na kuibuka kwa madai mengi likiwemo suala la Flora kusemekana amehamia nyumbani kwake kitu ambacho alikipinga.
Gwajima alisema anasikitika sana kuona ndoa ya Flora na Emmanuel Mbasha inatikisika akizingatia Flora ni muumini wake hivyo moja kwa moja ugomvi wao unaonekana kutia dosari mwenendo mzima wa uinjilishaji katika jamii.

“Naumizwa sana na sakata hili lakini hivi karibuni niliamua kuwaita ndugu wa pande zote mbili (Flora na Mbasha) nikazungumza nao kwa kirefu na tukamaliza tofauti zote lakini tatizo likabaki lile la kisheria zaidi (mashitaka ya ubakaji kwa Emmanuel),” alisema Gwajima ambaye makao makuu ya kanisa lake yapo Kawe jijini Dar.
AANDAA TAMKO ZITO

Mchungaji Gwajima alisema kutokana na sakata hilo kugusa Injili, ameandaa tamko zito ambalo atalitoa rasmi atakaporudi safari yake ambayo hakueleza anakokwenda.

“Hatuwezi kukaa kimya juu ya hili, nasafiri lakini nikirudi tu nitatoa tamko rasmi kwa kuwaalika waandishi wa habari,” alisema.

IBADANI JUMAPILI

Katika hatua nyingine, ndani ya ibada ya kanisa hilo iliyofanyika Jumapili iliyopita, Mchungaji Gwajima alitumia dakika kama 15 katika mahubiri yake kutupa kile kilichodaiwa kuwa ni jiwe gizani ambapo wengi waliamini ni kuhusiana na sakata hilo.

“Mimi siyo kama wale, sijibu hoja kama zile, mfano ukiwa unaoga halafu chizi akachukua nguo zako na ukamkimbiza nani ataonekana chizi? Tatizo la Watanzania ni kuwa wakisikia kitu kipya kinaanza kwao badala ya kukithamini wanakididimiza ili kisiendelee, lakini mimi siyo kama wao,” alisema.

Aliongeza: “Mimi kila mwaka naenda Japan na ninawa-lecture Wajapani ambao pia huja hapa kanisani zaidi ya 40 kila mwaka na mwaka huu watakuja Septemba, lakini Watanzania hawashtuki na kuja kujifunza juu ya ufufuo wa wafu wengi wao wanakalia kuandika stori kwenye magazeti lakini mimi siyo kama wale.”
AMEFUNGUKIA SAKATA LA MBASHA?

Ingawa Mchungaji Gwajima hakueleza moja kwa moja kuhusu tukio la Mbasha lakini maneno hayo yalitafsiriwa kwamba ni ya kujibu hoja zinazomhusisha yeye na tukio hilo.

Anaendelea:”Mimi nimehubiri nchi zaidi ya 53 duniani na nyingi za Ulaya na Marekani halafu mtu amekaa Magomeni miaka yote anatengeneza stori ya gazeti, unatarajia niijibu, mimi siyo kama wale nimetumwa na nina kazi natakiwa kuifanya duniani na siwezi kufa mpaka niimalize.”

“Inawezekana mlishawaangamiza wengi kabla ya mimi, kwa kuwatungia stori hizo za uongo lakini mimi siyo kama wale na mwezi huu wa nane ninaendelea na mkutano Iringa, waache waandike lakini mimi ni chombo kingine na siyo kama wale.”
DONGO GIZANI?

Baadhi ya waumini waliokuwa katika ibada hiyo, walibaki njia panda na katika giza nene ingawa wengi waliamini alitupa vijembe katika sakata la Mbasha haswa alipokuwa akisema, ‘mimi siyo kama wale’.


Hiki Ndicho Alikiandika Flora Mbasha Jana

$
0
0
Kama unaweza kushiriki maombi haya pamoja nami, Mungu akukumbuke, na kama upo kwa ajili ya kuhukumu, pia Mungu akukumbuke. Math7:1 Msihukumu msije mkahukumiwa ninyi, kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayo hukumuwa; na kipimo kile mpimiacho ndicho mtakacho pimiwa.
Math5:44 Lakini mimi nawaambia, wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi.
‘ Mungu wewe ni Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu. wewe ni Mkuu sana, wewe ni mwanzo tena mwisho zaidi yako hakuna na hatakuwepo. umesema ktk 1wathesalonike5:18 shukuruni kwa kila jambo maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu ktk kristo Yesu. ahsante Mungu maana wewe uliijua jana yangu, leo na kesho itakuwaje.Mungu wa amani unitakase kabisa nafsi yangu, mwili wangu na roho yangu unihifadhi, wewe BWANA ni mwaminifu.
Ktk Isaya43;19 umesema,Tazama nitatenda neno jipya: sasa litachipuka je hamtalijua sasa? nitafanya njia hata jangwani na miito ya maji nyikani. BWANA mapenzi yako yatimizwe, tenda lililo kusudi lako juu yangu. ktk Math14:14 umesema, mkiniomba neno lolote kwa jina langu nitalifanya. ukasema ktk Marko10:27 Yesu akawakazia macho akasema, kwa wanadamu haiwezekani, bali kwa Mungu sivyo: maana yote yanawezekana kwa Mungu.
Maombolezo3:31-32 Kwa kuwa BWANA hatamtupa mtu hata milele, maana ajapo mhuzunisha atamrehemu kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.
Mungu inua moyo wangu sasa, wewe ndiyo msaada pekee wa kweli. Ninaamini utatenda makuu kama ilivyoandikwa ktk Zaburi 108;13 Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, maana yeye atawakanyaga watesi wetu. Bwana wewe ni mtu wa vita, Bwana ndilo jina lako,pigana sasa ninakuachia wewe.
ninashuka mbele zako ninaungana na wenye uhai wanne ktk Ufunuo4;6-11 kukuabudu wewe nikisema, 11 Umestahili wewe BWANA wetu na MUNGU wetu,kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa.
Zab23;4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami.
AMEN

Undani Sakata la Mnenguaji wa Kundi la Kanga Moko Aliyepigwa Risasi na Askari Polisi

$
0
0
Mnenguaji  wa Kundi la Kanga Moko, Zawia Hamis  ambaye usiku wa Jumatano iliyopita alipigwa risasi mbili mwilini  na mtu aliyedaiwa ni askari polisi, ameweka undani wa sakata hilo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi  juzi nyumbani kwake Mwananyamala jijini Dar, majeruhi huyo alisema tukio hilo lilijiri maeneo ya Mwananyamala- Kisiwani karibu na Ofisi za Chama cha Wananchi (Cuf) na kuongeza kuwa, kisa ni kubishana na askari huyo aliyetaka kuzimwa kwa matarumbeta kutoka kwenye kikundi chao kilichokuwa kikipita eneo hilo.

Sisi tulikuwa tukipita na matarumbeta, askari wakatusimamisha na kutuamuru tuyazime kisha kutaka kutukamata watupeleke kituoni eti serikali imekataza.


“Tuliwaambia mbona ni mapema sana kwani ilikuwa saa kumi alasiri na Kova alisema ngoma za Kanga Moko, Kigodoro na nyingine zisipigwe usiku. Pia tuliwaambia tulichokuwa tukikifanya si ngoma hasa, ni matarumbeta tunapita kuwaalika watu kuwa leo kuna shughuli sehemu.

“Baada ya majibu hayo ndipo askari mmoja hakutaka hata kuendelea na mazungumzo, alitoa bastola kiunoni na kunipiga risasi mbili, moja kiunoni, nyingine kwenye mbavu halafu akapiga tena hovyo hewani risasi zilizobaki. Kwa kweli nimeumia sana,” alisema Zawia.
  
Mnenguaji huyo alisema kutokana na hali yake kuwa mbaya alipelekwa Kituo cha Polisi cha Mwinjuma na kupewa Polisi Fomu No. 3 (PF3) kisha kukimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni, Mwananyamala kwa ajili ya matibabu ambapo  kwa mujibu wake alitolewa risasi mbili.  

Baada ya kuzungumza na majeruhi huyo, waandishi wetu walikwenda kwenye Kituo cha Polisi Mwinjuma ambako ndiko alikoripoti PF3.

Askari mmoja wa kituo hicho (jina lipo) alisema hawezi kusema lolote kuhusu tukio huku akiweka wazi kwamba, afande aliyempiga risasi mnenguaji huyo anajulikana hivyo mlalamikaji anaweza kwenda mbele ya sheria.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Dar, Camillius Wambura hakupatikana kwa simu juzi kuzungumzia tukio hilo.



Njemba anaswa akiwalawiti watoto kwa kuwahonga ubuyu

$
0
0
MKAZI wa mmoja wa Kijiji cha Igurubi Tarafa ya Igurubi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuwaingilia kimwili watoto wenye umri wa chini ya miaka kumi, baada ya kuwarubuni kwa kuwapa ubuyu na Sh 500 taslimu.

Hayo yamethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Suzana Kaganda aliyesema tukio hilo ni la juzi katika Mtaa wa Muhaya Kijiji cha Igurubi. Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Sudi Seif (47).

Alisema mtuhumiwa huyo anadaiwa kuwatendea unyama watoto hao, kwa kuwalaghai kuwapa ubuyu na pesa, endapo wangemkubalia kufanya tendo la mapenzi.

Alisema kwa kuwa watoto hao walikuwa wadogo, alifanikiwa kuwashawishi, na alianza kwa kumchukua mtoto wa kwanza mwenye umri wa miaka 5 na miezi 4, anayesoma chekechea Shule ya Msingi Igurubi.

Kamanda huyo aliongeza kuwa, akiwa chumbani na mtoto huyo alimwingilia kimwili katika sehemu zote za siri na kumsababishia maumivu makali hadi wazazi wake walipomgundua wakati aliporudi nyumbani muda wa jioni.
Alidai kuwa baada ya tukio hilo kwa mtoto wa kwanza, alimchukua mtoto mwingine mwenye umri wa miaka 9 anayesoma darasa la pili Shule ya Msingi Ikonda Kata ya Igurubi, aliyemfanyia kama mtoto wa kwanza.

Kaganda alisema baada ya matukio hayo, mtuhumiwa aliendelea kujipumzisha nyumbani kwake, lakini ghafla alivamiwa na kundi la wanakijiji waliopanga kumdhuru.

Hata hivyo, mtu huyo aliokolewa na askari wa Kituo kidogo cha Polisi Igurubi, waliomchukua na kumpeleka Kituo kikuu cha Polisi mjini Igunga.

Kaimu Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Mashaka Hilaly alithibitisha kuingiliwa kimwili kwa watoto hao na kusema wameharibiwa vibaya katika sehemu zote za siri, hali iliyolazimu kuwalaza hospitalini

Breaking News:Ajali Mbaya yatokea Maeneo ya Makongo na Kuuwa Watu 18..Photos

$
0
0



Gari aina ya Toyota Coaster inayofanya safari zake kati ya Ubungo na Tegeta jijini Dar es Salaam imepata ajali mbaya leo mchana baada ya kugongana na gari lingine na kusababisha vifo vya watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 18 katika eneo la Makongo Sekondari jijini Dar.
Inasikitisha Jamani ...RIP
By Pendo Lyimo

Napenda Kudate na Wanaume Maarufu Tu, Wasio na Jina hapa Mjini kwangu Takataka

$
0
0
Hii kitu imenitokea sana mara nyingi 
Napenda kudate na wanaume maarufu tu na pindi nikiwa ktk mahusiano na mwanaume maarufu najickia nipo salama sana hata kama hanisaidii chchte nainjoy mbaya kuliko nikiwa na mtu aso na jina hapa town 
Tatz nikiwa na mtu hata kama ananijali na anasifa zote lkn hana jina nakuwa mnyonge simfurahii
Nawezaje kuondokana na hili tatizo

Papii Kocha na Baba yake Nguza Viking Wawatoa Watu Machozi Baada ya Kutumbuiza Maadhimisho ya Magereza Day

$
0
0
Msanii Nguza Viking (kulia) na Mwanae Jonson Nguza Maarufu kwa jina la Papii Kocha ambao wanatumikia Kifungo chao kwenye Gereza la Ukonga jijini Dar,wakiwa na Bendi ya Wafungwa wakiimba Wimbo Maalum kuhusu Urekebishaji wa Wafungwa unavyofanyika Magerezani,Wanamuziki hao walitumbuiza katika Maadhimisho ya Magereza Day yaliyofanyika Juni 20, 2014 katika Viwanja vya Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga. Tukio hilo lilifanya watu kuwalilia kwa uchungu

Kauli ya Wema Sepetu Baada ya Picha ya Mama Yake Mzazi Kueditiwa na Kuwa Chafu Kama zile za Kina Komba

$
0
0
Jana Kimetokea kitu cha Kusikitisha sana Instagram, Account Moja inayojiita Home_ya_jiji_team_dengue walichukua Picha ya Mama yake Wema na Kuiedit na kumzalilisha mama wa watu Bila Kosa lolote kisa ni Huyu Dengue ni Team tofauti na ile ya Wema , Ki ukweli Imesikitisha Wengi sana ....Baada ya Watu wengi kulaani hicho kitendo Mwenye Account hiyo ali delete picha lakini akawa imeshasambaa sana kwa watu ...

Wema Kwa uchungu aliandikia Message hii hapa chini kwa uchungu:

Lowassa Atangaza ‘Uamuzi Mgumu’

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa ametangaza kuanza kwa hatua za kuyarejesha kwenye Mamlaka za Serikali za Vijiji mashamba 21 ya wawekezaji  yenye ukubwa wa zaidi ya ekari 10,000,  ambayo hayajaendelezwa.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lomooti, Kata ya Lolkisale wilayani humo alipokwenda kutembelea boma la kisasa la mfugaji Isaya Lembekure, Lowassa alisema  haiwezekani wananchi wa Monduli kukosa ardhi wakati, kuna ardhi yao iliyohodhiwa na wachache bila kuendelezwa.

 “Monduli tumechoka na uuzwaji wa ardhi. Kila mahali ni matatizo ya uuzwaji wa ardhi. Sasa tunatangaza kuanza mchakato wa kuyarejesha mashamba yote ya wawekezaji ambayo hayajaendelezwa. Tayari hatua mbalimbali zimeanza kuchukuliwa ili kuyarejesha,” alisema Lowassa.

Tamko hilo la Lowassa, lilipokewa kwa shangwe na wananchi wa Wilaya ya Monduli na limekuja wakati migogoro ya ardhi baina ya wawekezaji na wananchi na  wakulima na wafugaji imeshamiri nchini.

Licha ya kutoa agizo hilo, Lowassa ameendelea kukemea uuzajiwa wa ardhi wilayani humo, unaofanywa kinyume cha taratibu na Serikali.

“Kuanzia sasa kiongozi wa kijiji atakayebainika kuhusika kuuza ardhi kinyemela, ang’olewe kupitia mikutano ya vijiji,” alisema Lowassa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya  Monduli,  Twalib Mbasha alisema tayari halmashauri hiyo imeanza maandalizi ya kuyarejesha mashamba hayo kwa kuwataka  wahusika wa mashamba hayo kujieleza kwa nini hawajayaendeleza hadi leo.

“Halmashauri inakusudia kuyafuta mashamba yote yasiyoendelezwa na yaliyotelekezwa, hii ni kutokana na kushindwa kufuata masharti ya ardhi kama ilivyoanishwa na sheria ya Ardhi namba 4,999 fungu la 44 na fungu la 48. Nimetoa siku 90 watu hawa wajieleze,” alisema Mbasha.

Aliyataja mashamba yanayotarajiwa kurejeshwa kwenye mamlaka za Serikali za Vijiji kuwa ni Meru Enterprises namba 10, ACU LTD namba 2390, TANFORM LTD  47, TANFORM 44  na Melembuki Kitesho Mollel namba 974 katika Kijiji cha Lolkisale.

Mashamba mengine ni The Monduli Parents Sec School, Musa Mamuya namba 2278 lipo Makuyuni, David Pello 2275, Hillary Gadi namba 2474, Khalifan Said Masoud 2276, Masoud Said Masoud 2277 yapo Kijiji cha Mswakini Juu.

Alitaja pia yaliyopo katika kijiji hicho ni ya Lucas Petro Kambei namba 2597 na Rungwa game Safari Ltd namba 2765.

Alisema mashamba mengine  ni Omary Daudi Mshana 1571, Saidi Rashid Lena  namba 2549 yaliyopo Kijiji cha Naitolia, wakati mashamba mengine ni ya T.R Msuya namba 3, Esimingori Estate Ranch namba 7/2, Saburi Estate Ltd namba  7, Musa Y. Mamuya yaliyopo Makuyuni

Skendo Chafu Zamkimbiza Masogange Bongo, Aamua Kwenda Kuishi South Afrika Kuepuka Vidole vya Watu

$
0
0
Imebainika kuwa Mwanadada Agness Masogange ameihama nchi na kwenda kuishi South Africa Kutokana na Skendo zinazomkabili kubwa ikiwemo ile ya Madawa ya Kulevya Ambayo alikamatwa South Africa lakini alishinda kesi na kuachiwa..Rafiki yake wa karibu aitwaje Jeniffer alihabarisha mtandao huu na kusema Agness Ameenda huko ili kutulia kwasababu hapa Bongo kila mahali alikuwa ananyooshewa Vidole kitu ambacho alikuwa akipendi kabisa...Si kweli amepata Maisha mazuri kama alivyosema.

Alikiba: Sina bifu na Diamond lakini alinikosea na nikaumizwa na nilisha samehe

$
0
0
Msanii Alikiba ameamua kufungaka na kuweka waZi kili kinacho hitwa tofauti au bifu kati yake na Msanii Diamond!Kwanza lazima tukubaliane kuwa ALikiba ni mmoja wa Wasanii wasio penda maneno na malumbano na wasanii wenzie ndio maana hukaa kimya. Kwanza Alikiba alisema hana bifu na diamond na hana sababu ya kuwa na bifu nae japo yanayo ongelewa yana muumiza sana na aliamua kuondokana na hayo yote busara ya haraka ilikuwa kukaa kimya.

Aliendelea kusema aliumizwa sana aliposikia kuwa amefuta mistari ya diamond kwenye wimbo wa Single boy ambao aliimba na lady jaydee na hakuimba kabisa na diamond na hata producer aliye record wimbo huo alithibitisha. Aliendelea kusema kuwa aliumizwa sana na uongo huo kuhusu yeye na hakupenda kuuongelea sana kwa sababu ange onekana anatafuta kick wakati hakuKuwa na kitu kama hicho.

Pia Alikiba aliamua kusema kuwa aliumizwa sana na kitendo cha Diamond kufuta mistari yake kwenye wimbo wa Lala salama maana Diamond hakumwambia kwanini kafanya hivyo na hadi leo hakuwai kumwambia. Alisema hilo swala amechukulia kama na Kitendo cha mtu kuomba mtihani wako aangalizie alaf baadae ana kurudishia mtihani wako na kusema sitaki majibu yako au ana yafuta yote alaf unategemea atajisikiaje? na alisema yeye alisha samehe lakini Diamond alimkosea na hadi leo hawakuwai kukutana.

Ameweka wazi kuwa aliamua kuwa kimya ili watu waongee lakini hana tatizo na Diamond. Katika hili sikuona sababu ya Diamond kutomwambia Alikiba kuwa wimbo naufanya upya na nimetoa mistari yako maana sikuipenda na nimeamua kuimba mwenyewe.

Wafahamu Mastaa wa Bongo Waliotoka Familia Bora Zenye Uwezo

$
0
0
Hakuna mtu asiyejua maana ya watoto wa kishua
basi kama yupo basi maana halisi ya neno hili ni
wale watoto waliozaliwa kwenye familia
zinazojiweza au unaweza kuita familia Bora. Mara
nyingi wasanii wengi huwa wanatokea maisha
duni na kupigana na maisha hadi kufikia walipo
sasa. Kipindi Diamond akiacha shule kwa kukosa
pesa ya kumsomesha nana elimu yake kuishia
A’level , Hawa wengine walikua wapo shule
wakisoma na kuishi vizuri.
Hawa ndo baadhi ya watoto wakishua
ambao kwasasa ni celebrities…

Vanessa Mdee

Vanessa Hau Mdee au unaweza kumuita Vee au
Vee Money alizaliwa mjini Arusha mwaka 1988.
Vanessa mdee alikuzwa na baba yake Sammy
Mdee (kwasasa ni marehemu )ambaye alikua ni
mtu mzito kwenye nchi hii na mama yake sophia.
Akiwa na umri mdogo Vanessa aliweza kusafiri
nchi mbalimbali duniani. Vanessa Mdee alikulia
miji ya New York , Paris , Nairobi na Arusha.

Nisher

Nisher ni mtoto wa Mtumishi wa Mungu Mh Nabii
GeorDavie anayeongoza huduma ya Ngurumo ya
Upako yenye makao yake jijini Arusha. Nisher
amekulia katika maisha mazuri na hadi ni
wakishua bado. Baba yake aliweza kumsaidia
Nisher kufungua studio yenye thamani kama ya
milioni 15 ili mtoto wake aendeleze kipaji
alichonacho.

Jokate Mwengelo

Huyu unaweza kumuita mtoto wa Oysterbay
kwani ndio alipokulia huku baba yake akifanya
kazi serikalini. Kumbuka Jokate alizaliwa
washington DC nchini Marekani ambapo wazazi
wake walikua wakifanya kazi huko. Alipomaliza
high school katika shule ya Loyola ndipo
alipogombania Miss Tanzania mwaka 2006 na
kushika nafasi ya 2.

Lucci

Jina lake halisi anaitwa Luciano Tsere au
unaweza kumuita Lucci ambaye ni producer
maarufu nchini. lucci amezaliwa tarehe 30
September mwaka 1985 Lusaka Zambia, akiwa ni
mzaliwa wa nne, wa mwisho kuzaliwa na akiwa
mtoto wa kiume pekee kwenye familia yao. Lucci
naye kama jokate amekulia Obey kwenye familia
bora ambapo kwasasa mzee wake ni balozi wa
Tanzania.

Wema Sepetu

Wema Sepetu ni msichana anayetoka kwenye
Familia ya kibalozi akiwa ni mtoto wa mwisho
katika familia ya wasichana wanne wa Balozi
Isaack Sepetu Ibrahimu (marehemu).Wema
sepetu alizaliwa mnamo mwaka 1988 katika
hospitali ya ST. Andrew’s jijini Dar es Salaam na
ni mtoto wa mwisho kuzaliwa huku
akisoma elimu yake ya primary na sekondari
katika shule ya ACADEMIC INTERNATIONAL
iliyopo jijini Dar es Salaam kabla ya kwenda
Nchini Malaysia kusomea mambo ya biashara za
kimataifa katka chuo cha Limkokwing University.

Barabara Mradi Mabasi Mwendo Kasi ni Janga, Usalama Wake ni wa Hatari kubwa Mabilioni Yameliwa na Wajanja?

$
0
0
Wakati wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwa na matumaini makubwa ya kuondokana na msongamano wa magari kutokana na ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo haraka (BRT), uchunguzi wa NIPASHE umebaini kwamba mradi huo utaleta maafa makubwa.

NIPASHE imethibitisha kwamba barabara mpya inayojengwa sambamba na ya mabasi yaendayo haraka, imepunguzwa upana wake kutoka mita sita hadi tano, hivyo kufanya madereva kuwa na wakati mgumu wakati wa kupitana (overtake).

Upana wa mita tano kila upande ni kuanzia kwenye ukingo wa barabara ambako umejengwa ukuta (capstone).

Kuna kila dalili kuwa mradi huu ambao umekuwa gumzo kwa kila kiongozi anayetoa majibu ya kuondoa msongamano jijini Dar es Salaam, umegubikwa na ufisadi.

Ufisadi huu unatokana na ukweli kwamba wakati Mtaalamu Mwandamizi wa masuala ya usafirishaji wa Benki ya Dunia (WB), Mhandisi Yonas Mchomvu, anasema kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa katika BRT, barabara hiyo ingehamishiwa pembeni mwa ile ya mradi, ikiwa na upana sawa na ule wa awali, hali ni kinyume chake.

“Labda kama ni kwa mtazamo wa macho na baada ya kuweka zile kingo, upana wa barabara ile ukaonekana ni mdogo, lakini ilipaswa ‘kusogezwa’ kwa vipimo vya awali,” anasema alipozungumzia mradi huo hivi karibuni.

Hata hivyo, NIPASHE ilipima barabara hiyo eneo la Kimara-Korogwe na kubaini kwamba upana wake ni mita tano upande mmoja na mita upande wa pili.

Upande huo ni tofauti kabisa na ule ulikuwako awali wa mita sita kila upande, huku kukiwa na upana wa mita 1.5 kila upande kwa ajili ya waendesha baiskeli na watumiaji wengine.

Upanda huu mdogo wa sasa mbali ya kuwa kikwazo cha kutatua foleni na msongamano, pia unaibua suala muhumu wa thamani ya fedha katika mradi huo unaotokana na mkopo kutoka Benki ya Dunia ulitazamiwa kutumia dola za Marekani milioni 290 (Sh. bilioni 493 (kwa viwango vya Dola moja kwa Sh. 1,700).

NIPASHE imethibisha kwamba katika barabara kuu nne za Dar es Salaam, Mandela, Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi zote zina upana wa mita sita na kuendelea, huku ya Morogoro inayojengwa upya ikiwa na upana wa mita tano.

Mandela ina upana wa mita sita kila upande, Sam Nujoma mita 6.5 kila upande na Ali Hassan Mwinyi mita sita kila upande.

Hofu ya udanganyifu katika barabara ya Morogoro inazidi kuwa na nguvu kwani vipimo vilivyochukuliwa na NIPASHE eneo la Kimara –Gereji ambako haijajengwa upya umeonyesha kuwa ina upana wa mita sita na pembeni mita 1.5 kila upande, hivyo kuonyesha dhahiri kuwa eneo la kuanzia mradi BRT Kimara –Mwisho hadi makutano na Bibi Titi Mohammed, barabara hiyo imeminywa sana.

Kulingana na upana huo mpya ambao ni dhahiri unaibua suala la usalama kwenye barabara hii, kiasi cha mita mbili zilizopunguzwa, kinaibua suala jingine ya kiasi kikubwa cha fedha ambacho hakijulikani kimekwenda wapi.

Kipande cha barabara ya Morogoro kutoka Kimara- Mwisho hadi makutano na Bibi Titi Mohamed, kinakadiriwa kuwa na urefu kilomita 15. Upana wa mita mbili unaopungua katika barabara hiyo ni sawa na urefu wa barabara yenye kilomita tano ikiwa na upana wa mita sita.

Kwa mujibu wa takwimu kutoka Wizara ya Ujenzi gharama za ujenzi wa kilomita moja ya barabara kuu ya lami inakadiriwa kufikia Sh. bilioni 1. Kwa maana hiyo, ni dhahiri kwamba kiasi ‘kilichookolewa’ kwa eneo lililopunguzwa kinafikia Sh. bilioni 5.

Hakuna taarifa zinazoeleza bayana sababu za kupunguzwa kwa upana huo wala mahali fedha ‘zilizookolewa’ zilipopelekwa.

Mbali na suala la uwezekano wa ufisadi katika mradi huu, mfumo wa ujenzi wake ambao umeongeza kona nyingi, nao umezidisha mazingira hatarishi yanayoweza kusababisha ajali za mara kwa mara kama ilivyowahi kutokea kwa nyakati tofauti hivi karibuni.

Siyo Wizara ya Ujenzi wala Wakala wa Usimamizi wa Barabara Dar es Salaam (Tanroad), walitoa maelezo juu ya sababu za kuminywa kwa barabara hiyo kwa kiwango hicho.

Barabara ya Morogo ni mfano mmoja tu juu ya mambo yanavyokwenda ovyo katika sekta nzima ya ujenzi wa barabara nchini.

NIPASHE imefanya uchunguzi na kubaini kuwa, ujenzi wa barabara ni miongoni mwa miradi ya maendeleo ambayo ufujaji wa fedha za umma unafanyika kwa namna tofauti, sehemu kubwa ikielekezwa katika huduma za kitaalamu.

Hujuma zinazofanywa katika miradi ya barabara, zimekuwa chanzo kikuu cha ujenzi duni unaochangia kuharibika kwa miundombinu hiyo muda mfupi baada ya kukamilika kwake.

Kwa kawaida, barabara zinazojengwa kwa viwango tofauti vya lami, zinatarajiwa kutumika kwa kati ya miaka 10 hadi 16 kabla ya kufanyiwa matengenzo makubwa.

Lakini barabara hizo zimebainika kuharibika chini ya muda huo baada ya kukamilika kwake.

UPUNGUZAJI WA VIPIMO VYA BARABARA
Moja ya mbinu zinazotumiwa na wadau wanaoshiriki ujenzi na kuikagua miradi ya barabara, ni kupunguza vipimo vya upana kwa kiasi kidogo kisichoweza kugundulika kwa urahisi hususani na wananchi wa kawaida.

Vyanzo tofauti vilivyofanikisha kufichuka kwa siri hiyo vinaeleza kuwa, mbinu hiyo inatekelezwa ili kuokoa kiwango cha fedha kwa mkandarasi, ambazo hata hivyo hazirejeshwi hazina, bali kuwafikia watu binafsi.

Hata hivyo, taarifa zinazohusu ufisadi huo zinapatikana huku vyanzo vyake, vikisisitiza usiri wa kutojulikana, kwa sababu za usalama binafsi na ulinzi wa ajira zao.

HALI ILIVYO SINGIDA
Mmoja wa wahandisi katika Manispaa ya Singida, ambaye hataki jina lake litajwe gazetini, anasema kwa miaka mingi, miradi ya ujenzi wa barabara imekuwa ikihujumiwa kwa namna tofauti.

Mhandisi huyo, anatoa mfano wa ufisadi unaofanywa kupitia upunguzwaji wa vipimo vya barabara, umekithiri kwenye miradi nyingi na kwamba inasababisha upotevu wa fedha na kudidimiza ubora wa miundombinu hiyo.

Chanzo hicho kinaeleza kuwa, kwa kawaida barabara nyingi kama zinazounganisha mikoa, zimekuwa zikijengwa kwa upana unaofikia mita nane.

Lakini, barabara hizo zimekuwa zikipunguzwa kwa kipimo (mathalani) cha kuanzia mita 0.5 hadi moja na ambazo si rahisi kubainika pale ujenzi wa mradi unapokamilika.

“Unapojenga barabara na kupunguza mita 0.5 kutoka upana wa mita nane, si rahisi ikagundulika kwa watumiaji wa barabara isipokuwa mpaka kwa wanaohusika na upimaji,” kinaeleza chanzo hicho.

Chanzo hicho kinaeleza kuwa, kiasi kama hicho kinapopunguzwa, kinaokoa fedha kwa kadri ya urefu wa barabara, ingawa kwa ujumla wake, fedha zinazopotea ni nyingi.

“Hapa unaweza kuziona mita 0.5 ni ndogo, lakini kwa hakika zinapojumuishwa kwa urefu wa barabara yote, unakuta ukubwa wake unahusisha kiasi kikubwa cha fedha kinachoishia mifuko mwa wajanja wachache,” kinaeleza.

MIRADI YA WAFADHILI
Ingawa ni hivyo, imebainika kuwa miradi mingi ya barabara inayojengwa kwa kutumia fedha za ndani, ama mikopo pasipo kuwapo usimamizi madhubuti, imetekelezwa kwa kiwango cha chini ikilinganishwa na thamani ya fedha.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano wa Zanzibar, Juma Malik Akil, anasema ushahidi wa kimazingira unaonyesha kutokuwapo usimamizi mzuri wa miradi hiyo, hivyo kusababisha kiwango duni cha barabara zinazojengwa.

“Hizi barabara zinazojengwa na kufuatiliwa kwa karibu na wafadhili, kwa kiasi fulani zinakuwa na ubora unaotakiwa, lakini zinazosimamiwa na mamlaka za ndani ya nchi, hapo kuna matatizo sana,” anasema alipokutana na ujumbe wa WM mjini Unguja hivi karibuni.

Miongoni mwa barabara zilizojengwa kwa ufadhili wa WB visiwani Zanzibar na zinazotajwa kuwa miongoni mwa zenye ubora ni zile za Paje-Pingwe, Matembwe-Pongwe na Mkwajuni-Nungwi.

SHINIKIZO LA MADIWANI/WABUNGE
Uchunguzi huo unabaini kuwa shinikizo za kisiasa zimekuwa miongoni mwa vyanzo vinavyochochea ujenzi duni wa barabara hususani zinazounganisha maeneo ya ndani ya mikoa.

Shinikizo za kisiasa, zinatajwa kupitia vikao vya mabaraza ya madiwani, ambapo wawakilishi wa wananchi wakiwamo wabunge ni wajumbe wake.

Mhandisi wa jiji la Arusha, Afwilile Lamsy, anasema katika utumishi wake kwenye fani hiyo kwa zaidi ya miaka 10, ameshuhudia kuwapo madiwani na wabunge wanaoshinikiza ujenzi wa barabara kuyafikia maeneo wanayoamini kuwapo wapiga kura wengi.

Mhandisi Lamsy, anasema shinikizo hizo zinafanywa wakati ambapo bajeti za halmashauri husika zinaposomwa na fedha kutengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hasa kwa kiwango cha lami.

Inapotokea hali hiyo, baadhi wa wabunge na wenye nguvu ya kufanya maamuzi, wamekuwa wakihitaji mgawanyo wa fedha kidogo zinazotengwa, kuelekezwa kwenye ujenzi ama ukarabati wa barabara nyingi na zenye urefu mkubwa, pasipo kuwianisha na fedha zilizopo.

“Wapo wataalamu waadilifu wanaobuni mikakati mizuri ya ujenzi wa barabara, lakini inapowasilishwa na kujadiliwa kwenye baraza la madiwani, wawakilishi hao wa wananchi wanaipinga,” anasema.

Kwa mujibu wa Mhandisi Lamsy, hali hiyo ipo katika maeneo mengi ya halshauri za wilaya, manispaa na majini nchini.

Anatoa mfano kuwa, inaweza kutokea wahandisi wakapendekeza kujengwa barabara tatu kati ya 10 zilizopo kwenye halmashauri husika, kila moja kwa kilomita moja ya kiwango cha lami.

“Lakini ikifikishwa baraza la madiwani, wanapinga na kutaka fedha zilizotengwa zitumike kujenga barabara nyingi ikibidi zote kwa kupitisha greda na kumwaga vifusi,” anasema.

Barabara ni miongoni mwa miundombinu inayoligharimu taifa fedha nyingi na ambayo kama usimamizi wake ungefanikisha kuwapo kwa ubora, ni dhahiri kwamba zingechochea kasi ya maendeleo na kurahisisha mawasiliano.
CHANZO: NIPASHE

My Take:

Kifungu 27 (1) za Sheria ya barabara namba 13 ya 2007, Tangazo la Serikali No 21 ya tar 23 Januari 2009 kinataja upana wa chini kabisa kwa njia za barabara za lami (Roadway Lane) kwa Barabara Kuu zote hapa nchini (Trunk roads) kuwa usipungue mita 3.25.

Hivyo kama njia 2 (mbili) za Barabara ya Morogoro zimejengwa kwa Mita 5 tu badala ya mita 6.5 (yaani Mita 2.50 kwa kila njia badala ya Mita 3.25) Sheria ya barabara Na 13 ya 2007 na Kanuni zake za 2009 vitakuwa vimevunjwa hivyo Serikali isikubali kupokea barabara hiyo kabisa kwani hata kabla haijaisha tayari watanzania wameshaanza kupoteza maisha.

Na tunamtaka Mhe John Magufuli ahakikishe mkandarasi anaifanyaia barabara hiyo marekebisho mara moja.

Wabunge acheni siasa na Misamaha ya Kodi, Haikwepeki ni lazima iwepo!

$
0
0
 Ninashangazwa sana na Baadhi ya Wabunge wanapochangia hoja zao toka majuzi kuhusu Bajeti ya Wizara ya Fedha, wakilalamika sana kuhusu Misamaha ya Kodi kwa wawekezaji bila ya kutoa Alternative, I mean wawekezaji wanasamehewa kodi Dunia nzima sio Tanzania tu. Kama Serikali haiwezi kuweka mikakati ya kodi ambayo ni rafiki kwa wawekezaji wala sio siri kwamba wawekezaji watakwenda nchi nyingine ambayo ina mazingira rafiki na biashara zao. Ningetegemea Mbunge mmoja asimame na kutoa solutions za namna ya kusamehe kodi na kuhakikisha Taifa linanufaika kwa sababu ndivyo inavyofanyika Dunia nzima na ndipo tatizo letu lilipo aidha hatujui nini cha kufanya ili misamaha ya kodi kwa wawekezaji itusaidie kama nchi zingine, au tunajua ila tunafanya makusudi kwa masilahi ya binafsi.

- Muwekezaji anatakiwa kubanwa mbavu kwamba kweli atasamehewa kodi, lakini analazimishwa kujenga Shule katika eneo lake la biashara au kuajiri vijana wengi kwenye biashara yake ndivyo Dunia nzima wanavyofanya. Na kwenye hili ni muhimu sana Manispaa kupewa madaraka zaidi ya waliyonayo sasa kwa sababu ndivyo inavyofanyika kwenye Mataifa yaliyoendelea, Manispaa wanakuwa na mamlaka ya Kodi ndani ya Manispaa, matokeo ni kwamba kama mazingira ya kodi Ilala hayapo sawa Muwekezaji anahamia Temeke maana kule anakuta mazingira rafiki ya kodi, na infact Manispaa zinakuwa kwenye competition ya wawezekaji.

- Ukienda Swaziland ni kwamba Muwekezaji anapewa msamaha wa kodi kwenye madini, lakini analazimishwa kutoa mchango katika kuendeleza mifugo yao, Marekani Muwekezaji anasamehewa kodi lakini analazimishwa kutoaa ajira kubwa kwa vijana. Tatizo tulilonalo sio misamaha ya kodi, isipokuwa ni mikataba ya misamaha ya kodi Bunge likae chini na kutengeneza Sheria itakayotoa madaraka zaidi kwa Manispaa ili ziweze kuwa na uamuzi wa mwisho kuhusu misamaha ya kodi kwa wawekezaji ndani ya Manispaa zao.

- WABUNGE WETU WAACHE KULALALAMIKA KUHUSU MISAMAHA YA KODI, HAIKWEPEKI WATOE MUONGOZO NAMNA YA KUISIMAMIA MISAMAHA YA KODI!!

LE MUTUZ SYSTEM
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images