Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live

Ndugai: Lissu Awezi Kutibiwa Kwa Kuchangishana Michango

$
0
0
Ndugai: Lissu Awezi Kutibiwa Kwa Kuchangishana
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amefunguka na kudai matibabu ya Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu hayawezi kufanyika kwa kuchangishana michango kwa kuwa ana bima yake na haki zake ndani ya Bunge.

Spika Ndugai ameeleza hayo leo asubuhi wakati akizungumza kwenye kipindi cha EA BreakFast kutoka East Afrika baada ya kuulizwa swali kwamba kuna utaratibu gani endapo mbunge akiumia ama akiumwa akiwa kazini.

"Utaratibu ni kwamba wabunge wote wana bima pamoja na mimi mwenyewe, Mawaziri wote wana bima ndani ya bunge kwa sababu ni wabunge kwanza kabla ya kuwa Mawaziri. Kwa hiyo bima zao ndiyo zinazo wahudumia na tuna hudumiwa kupitia hospitali serikali, tunalazwa kama watanzania wengine wowote wale. Ikitokea yanahitajika matibabu ya nje, yatatoka mapendekezo kule Muhimbili kwamba matibabu yake yanapaswa yakitibiwe nje kwa sababu ya upungufu wa jambo fulani hapa nchini", amesema Spika Ndugai.

Pamoja na hayo, Spika Ndugai aliendelea kwa kusema "Tukirudi kwa Mhe. Lissu ni kwamba tulikuwa wote hapa Dodoma, baada ya kuombwa na familia pamoja na Mhe. Mbowe kwamba ni vyema apelekwe kutibiwa hospitali ya Nairobi nchini Kenya tulikubaliana basi ni vizuri aende huko. Lakini alienda huko kama vile ni hospitali binafsi, nje kidogo ya mkondo ule wa kawaida. Kwa hiyo bado bima yake ipo hapa bungeni na utaratibu wa kumtibu upo".

Aidha, Spika Ndugai amesema bunge kwa ujumla haliwezi kumtupa Mhe. Lissu hata kidogo kuhusiana na masuala ya matibabu yake.

"Sisi kama bunge hatujamtupa mwenzetu na bahati nzuri serikali imetoa tamko halijamtupa ni suala la kuwekana sawa, badala ya matamko kwenye vyombo vya habari, magazeti ambayo yamekuwa yakipotosha tu na kuleta malumbano ambayo hayana sababu. Kwa hiyo wito wangu kwa nafasi zote zinazohusika ikiwa ni pamoja na familia ya Lissu, CHADEMA, uongozi wa bunge na serikali endapo tukikaa pamoja hakuna ambacho kitashindwa kuzungumzika, hatuwezi kumtibu mwenzetu kwa michango ya kuchangishana wakati ana bima yake na haki zake", amesisitiza Spika Ndugai.
Bonyeza hapa chini umsikilize mengine mengi zaidi aliyozungumza Mhe. Spika wa bunge, Job Ndugai hii leo.


Korea Kaskazini Yaongezwa Kwenye Zuio la Kuingia Marekani

$
0
0
Korea Kaskazini Yaongezwa Kwenye Zuio la Kuingia Marekani
Marekani imepitisha vikwazo vipya vya zuio la kuingia nchini humo,ikiiongeza nchi ya Korea kaskazini raia wake kutoingia katika taifa hilo ambapo mengine yaliyoingizwa katika vikwazo hivyo ni Venezuela na Chad .
Sababu zilizopelekea Marekani kuweka vikwazo kwa raia wa nchi hizo kuingia nchini humo ni pamoja na usalama wa nchi zao kuwa duni na ukosefu wa ushirikiano.
Hatua hiyo ya Marekani imetoa masharti tofauti kati ya nchi na nchi ambapo Venezuela,wale waliozuiwa ni wafanyakazi wa serikali na familia zao.
Raia wa Nigeria wazuiwa kuingia Marekani
Urusi yashutumu vikwazo vya Marekani kuhusu viza
Jaji adhoofisha marufuku ya Trump dhidi ya mataifa 6 ya Kiislamu
Sudan nayo imeondolewa katika nchi sita za kiisamu ambazo Rais Trump alikuwa ameziwekea vikwazo.
Nchi ambazo bado ziko kwenye marufuku ya Rais Trump ni pamoja na Iran,Libya,Somalia na Yemen.

Cannavaro : Okwi Ana Kinarua Kigumu Kutoka kwa Washambuliaji wa Yanga

$
0
0
Cannavaro : Okwi  Ana Kinarua Kigumu Kutoka kwa Washambuliaji wa Yanga
BEKI kisiki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amesema kuwa licha ya mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi kufunga mabao sita hadi sasa, lakini ana kibarua kigumu mbele yake kutokana na upinzani atakaokutana nao kutoka kwa washambuliaji wa Yanga, akiwemo Amissi Tambwe.
Okwi ndiye mchezaji anayeongoza kwa kufumania nyavu kwa kuwa na mabao sita hadi sasa.
Lakini Tambwe ambaye anaanza mazoezi leo Jumatatu, akiwa uwanjani kufunga huwa ni jadi yake, hatua ambayo inampa matumaini Cannavaro kuwa mshambuliaji huyo ataweza kumfikia Okwi na kuleta ushindani.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Cannavaro amesema kuwa, mabao sita ya Okwi kwa sasa siyo kigezo cha mshambuliaji huyo kuweza kutwaa ufungaji bora msimu huu na kudai kuwa atakutana na upinzani mkali kutoka kwa washambuliaji wa Yanga akiwemo Tambwe mara baada ya kurejea.
“Ni vigumu kumhakikishia kuwa Okwi anaweza kuwa mfungaji bora katika kipindi hiki kwani tunaamini muda upo na kwa upande wetu kuna Tambwe ambaye bado hajarejea, tunaamini atafanya vizuri na kuleta ushindani kwenye mbio za ufungaji bora.
“Pia kuna wachezaji kama Chirwa (Obrey), Ngoma (Donald) na Ajibu (Ibrahimu), wanao uwezo wa kufunga vizuri na hata kuwania ufungaji bora, hivyo ligi bado na tunaamini watafanya vyema,” alisema Cannavaro.
 Khadija Mngwai, Dar es Salaam.

Maalim Seif Azidi Kuichanganya CCM

$
0
0
Maalim Seif Azidi Kuichanganya CCM
CCM imewataka wananchi kuendelea na shughuli zao za kujiletea maendeleo kama kawaida na kuachana na ilichoita upotoshaji unaofanywa na Katibu Mkuu wa Cuf, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa ataapishwa kuwa Rais wa Zanzibar karibuni.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk Abdallah Juma maarufu Mabodi alitoa kauli hiyo baada ya Maalim Seif kuendelea kutoa kauli hiyo kwa wananchi.

Mabodi alisema hakuna kiongozi wa CCM hata mmoja aliyewahi kufanya mazungumzo na Maalim Seif, kuhusu suala la kukabidhiwa madaraka.

Alisema kilichopo ni kiongozi huyo wa upinzani kutoa taarifa zisizo rasmi kwa jamii, huku baadhi ya wananchi wakipata taharuki.

“Amini kuwa hatujawahi kukaa na mahasimu wetu hao hata siku moja kujadili suala la hali ya siasa Zanzibar, hasa kuhusu hili la mabadiliko ya kiongozi, wao wana kazi zao za kisiasa na sisi tuna kazi zetu ambazo tunaendelea kuzifanya ili kujiweka tayari kwa ushindi uchaguzi wa mwaka 2020,” alisema Mabodi.

Kauli ya Mabodi imekuja kufuatia Maalim Seif kuendelea kutoa kauli za kuwaweka njia panda juu ya uwapo wa mabadiliko ya uongozi Zanzibar.

juzi, Maalim Seif akiwa katika kongamano maalumu lililoandaliwa na Jumuiya ya Vijana wa chama chake (Juvcuf) kupitia wanafunzi wa vyuo vikuu, alisema huu ni wakati wa wananchi kukaa tayari kupokea mabadiliko ya uongozi.

Maalim Seif alisema atakakabidhiwa madaraka ya urais hivi karibuni.

“Nataka mfahamu hakuna hata mtu mmoja mwenye nguvu ya kunizuia kuapishwa kuwa Rais wa Zanzibar, kinachofanyika sasa ni CCM kuhangaika tu ila mambo mazuri yaja,” alisema.

Alisema akiwaambia vijana hao kuwa haki ya Wazanzibari haitapotea. (Imeandikwa na Haji Mtumwa na Muhammed Khamis)

Msaga Sumu Afunguka Sababu ya Wasanii wa Singeli Kupotea Katika Game

$
0
0
Mfalme wa singeli nchini Tanzania, Msaga Sumu amefunguka na kudai wasanii wengi wa singeli wanatapotea katika muziki kwa sababu ya kutokuwa na heshima kwa watu wanaowazunguka kwenye kazi zao.

Msaga Sumu amebainisha hayo kupitia kipindi cha FRIDAY NIGHT LIVE (FNL) kutoka EATV baada ya kupondwa kwa maneno makali kwa kipindi kirefu na wasanii wenzake huku wengine wakimwambia hajui lolote katika muziki huo anaouimba.
"Wasanii wa singeli mimi naamini wananiponda sana, tena nikikaa kimya hivi ndiyo wanasema nimefulia kabisa, kumbe mwenzao huwa najitungia sheria zangu huku nikiwaangalia wao. Lakini huwa nawaambia ukweli kwamba siku zote kwenye muziki ukiwa na heshima unaweza kufika mbali, kwa kuwa heshima ndiyo kila kitu. Lakini hawa wasanii wa singeli wengi watafeli kwa sababu heshima hawana, wanajifanya wanavimba kutokana na nyimbo zao moja moja walizokuwa nazo", amesema Msaga Sumu.
Mtazame hapa chini Msaga Sumu akifunguka kuhusu wasanii wanaomponda pamoja na mambo mengine.

Spika Job Ndugai 'Mbowe Acha Kupotosha Matibabu ya Tundu Lissu'

$
0
0
Spika Job Ndugai 'Mbowe Acha Kupotosha Matibabu ya Tundu Lissu'
Freeman Mbowe
SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amemtaka Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe kuacha kupotosha taarifa za ushiriki wa Bunge katika tiba ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu anayeendelea na matibabu nchini Kenya.

Akihojiwa na gazeti hili jana kuhusu kauli za juzi za Mbowe, Ndugai alifafanua kuwa anashangazwa na kitendo cha Mbowe kulichukua suala la ugonjwa wa Lissu kisiasa. Alisema kuwa ni utaratibu wa kawaida kwa Bunge, au ofisi yoyote ile inayotumia Bima iwapo inataka mgonjwa wake kuhamishiwa hospitali nyingine, lazima itoe taarifa ya daktari inayoelezea kuhamishwa kwa mgonjwa huyo (rufaa).

Spika alisema huo, siyo tu utaratibu wa bunge, bali pia wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya (NHIF) inayotumiwa na wabunge wote nchini, unaotaka kupewa taarifa za kitabibu kutoka hospitali anayotibiwa mgonjwa, kama anataka kuhamishiwa kwingine. Kuhusu suala la Mbowe kuandika barua ya maombi ya kuomba Lissu akatibiwe nje ya nchi, Ndugai alisema kwa kuwa Lissu hawezi kuandika barua hiyo, ni wazi kuwa Mbowe ndiye ambaye angetakiwa kumwandikia.

Alisema ilikuwa ni mistari miwili tu ambayo ingesaidia kufanikisha tiba za Lissu nje ya nchi na alimtaka Mbowe kukubali ofa ya serikali ya kutaka kugharamia tiba za Lissu. “Mimi kama mbunge na Mtanzania, napenda kuona Lissu anapona na anarejea nchini,” alisema Spika na kusema anashangazwa na kauli ya Mbowe, eti kwamba yeye (Ndugai) amekwamisha fedha za matibabu wakati zile zilikuwa ni taratibu tu za kikazi.

Ndugai aliongeza kuwa “Nilishangaa pia kusikia kwa eti zile shilingi milioni 43 zilizochangwa na wabunge hawajepewa, ilihali zilishalipwa kwenye akaunti namba 0451155318 ya benki ya Barclays tawi la Hurlringham yenye jina la Kenya Hospital Association kwa tiba.

Sasa sijui ni nini tena ndugu yangu Mbowe anachotaka?” Juzi katika mkutano wake na waandishii, Mbowe alisema kuwa Bunge likiongozwa na Spika Ndugai lilikuwa kikwazo cha kumsaidia Tundu Lissu kutibiwa, huku akisema kuwa alitoa mashati ambayo yalikuwa ni usumbufu, mfano ya kumwambia aandike barua ya kuliomba bunge limpeleke nje ya nchi Lissu kwa matibabu. Kwa mujibu wa Mbowe, Spika alitaka Lissu akatibiwe Hospitali ya Taifa ya Muhimbili au kwenda India, ili hali wao walikuwa wakitaka aende Nairobi nchini Kenya.

Maneno ya Godblee Lema Baada ya Kukamatwa Msigwa 'Msiogope Baada ya Giza Nene Asubuhi Utokea'

$
0
0
Maneno ya Godblee Lema Baada ya Kukamatwa Msigwa 'Msiogope Baada ya Giza Nene Asubuhi Utokea'

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema ameeleza baada ya Mbunge wa Iringa Mjini kukamatwa jana wakati akiwa katika mkutano wake katika kata ya Mlandege Manispaa ya Iringa.

Lema kupitia ukurasa wake wa Twitter baada ya mbunge huyo kukamatwa amesema kuwa wasiogpe baada ya giza nene asubuhi hutokea.

Msigwa amekamatwa na Polisi huko Iringa na kushushwa kwa nguvu jukwani ktk Mkutano halali. Msiogope baada ya giza nene asubuhi hutokea!

Msigwa alishushwa jukwaani kwa nguvu akiwa anahutubia mkutano katika kata ya Mlandege huku akituhumiwa na kosa la uchochezi dhidi ya vyombo vya usalama.


Manji Aonyesha Mahakama Uhibitisho wa Dawa Alizokuwa anatumia

$
0
0
Manji Aonyesha Mahakama Uhibitisho wa Dawa Alizokuwa anatumia
Mfanyabiashara Yusuph Manji, leo Jumatatu amepanda kizimbani kujitetea katika shtaka linalomkabili la matumizi ya dawa za kulevya ambapo akiongozwa na Wakili wake Hajra Mungula.

Manji ameionyesha Mahakama udhibitisho uliotumwa na daktari wake kutoka Marekani kwa njia ya baruapepe wa aina ya dawa alizokuwa akitumia

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Rais Magufuli Atoa Agizo Uhamisho wa Wafanyakazi

$
0
0
Rais Magufuli Atoa Agizo Uhamisho wa Wafanyakazi
Rais John Magufuli amerejea agizo lake la kupiga marufuku mfanyakazi yeyote kuhamishwa kituo cha kazi pasipo kulipwa stahiki zake.

Ametoa agizo hilo leo Jumatatu, baada ya kusikiliza kero za wananchi wakiwemo wafanyakazi waliolalamika kuhamishwa vituo vya kazi bila kulipwa stahiki zao.

Rais Magufuli amezungumza na wananchi wa Sangsi nje kidogo ya Jiji la Arusha na wa Pacha ya Kia akiwa njiani kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) kurejea Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara ya siku sita mkoani Arusha.

Akizungumzia kero za wananchi wa Pacha ya Kia waliolalamikia tatizo la uhaba wa maji, kunyang’anywa maeneo ya biashara na waliokuwa walinzi wa uwanja wa ndege kudai haki zao, Rais Magufuli ameziagiza mamlaka husika kushughulikia matatizo hayo.

Rais Magufuli amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kutatua kero za wananchi na kuwahudumia bila kuwabagua kwa misingi ya itikadi za kisiasa, dini na ukabila.

Amesema katika kutimiza azma hiyo, Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara ya Usa River - Arusha inayojengwa kwa gharama ya Sh139 bilioni; mradi wa maji wa Arusha utakaogharimu Sh42 bilioni; mradi wa kusambaza umeme katika vijiji zaidi ya 200 na mingine inayotekelezwa katika maeneo hayo.

“Nina uhakika ninyi wakazi wa Arusha mnaona inavyobadilika, kabla ya kujengwa barabara hii kulikuwa kunatokea ajali nyingi na kuna watu walikufa pale kwenye daraja, inawezekana wengine wameanza kusahau, wanaozaliwa sasa hivi wanaweza kuona haya si chochote lakini hii ni ishara ya kupanda kwa uchumi wetu, uchumi unapopanda na miundombinu inakuwa mizuri,” amesema.

Waziri wa Afya Ametoa Agizo kwa Hospitali ya Muhimbili Juu ya Rufaa ya Matibabu ya Nje

$
0
0
Waziri wa Afya Ametoa Agizo kwa Hospitali ya Muhimbili Juu ya Rufaa ya Matibabu ya Nje
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ametoa agizo kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuhakikisha haitoi rufaa ya matibabu nje ya nchi ikiwa wana uwezo wa kutibu maradhi husika hapa nchini.

Ummy amesisitiza wataalamu kutowaogopa wanasiasa ikiwa wana uwezo wa kumtibu mgonjwa hapa nchini haina ulazima wa kumwandikia rufaa nje ya nchi hata akiwa ni Rais John Magufuli.

Ametoa agizo hilo leo Jumatatu wakati akipokea msaada wa vifaa vipya kwa ajili ya vyumba viwili vya upasuaji vya watoto wadogo na wodi ya watoto ya upasuaji vyenye thamani ya Dola za Marekani 675,000 sawa na Sh1.5 bilioni,  kutoka kwa wataalamu na wahisani kutoka nchini Uingereza kupitia taasisi ya Archie Wood Foundation.

"Rais aliponiteua aliniagiza kwamba lazima niachane na rufaa za nje, hatuwezi kuachana nazo ikiwa magonjwa yanayoweza kutibiwa ndani yatatibiwa nje," amesema Ummy.

Amesema Watanzania wana imani na  Muhimbili  na hivi sasa wengi wanatoka hospitali za kulipia na kufuata matibabu ila changamoto iliyopo ni majengo lakini wapo mbioni kujenga jengo la ghorofa kwa ajili ya wagonjwa wa kulipia.

"Msitoe rufaa ya mgonjwa kama hamjajiridhisha kwamba mnaweza kumtibu hapa hata kama awe Rais, waziri au nani msitoe rufaa kwani maana yake mtakuwa mmeshindwa ni lazima ninyi mseme kwamba hamuwezi na sisi tutashughulikia," amesema.

Amewatahadharisha wataalamu hao na wanasiasa kwamba lazima wahakikishe kweli hawawezi kutibu na kwamba wizara ipo tayari na itawaunga mkono.

Ishu ya Ebitoke Zinanikata Stimu Kabisa- Ben Pol

$
0
0
Ishu ya Ebitoke Zinanikata Stimu Kabisa- Ben Pol
Msanii Ben Pol ambaye inasemekana alikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na mchekeshaji Ebitoke, sasa hivi anaonekana kumuepuka msanii huyo kwa sababu ambazo hazijajulikana kwa haraka, kitendo kinachoonesha kumuumiza kihisia Ebitoke.

Ben Pol ambaye alitafutwa kwa kipindi kirefu na mwandishi wetu na kufanikiwa kumpata kwa shida kutokana na ubize aliosema  anao kwa kipindi hiki, alipomueleza kwamba anataka kuzungumzia kuhusu Ebitoke na kwa nini hapokei simu za mchekechaji huyo, Ben Pol alijibu kwa mkato huku akisema kwamba 'issue' za Ebitoke zinamkata 'stimu'.
"Sasa hivi nipo 'busy' sana kwa sababu nafanya mazoezi ya 'show', lakini kiukweli habari za Ebitoke zinanikata 'stimu' kabisa, 'so' nikitulia naweza nikakucheki", alisikika Ben Pol akimjibu mwandishi wetu.
Wiki iliyopita Ebitoke alikuwa kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, na kulalamika kuwa msanii huyo ambaye alikiri kuwa na hisia naye za kimapenzi sasa hivi hapokei simu zake, na wala hajibu ujumbe mfupi anaomtumia katika simu yake, hivyo akaomba watu wamsaidie kumuuliza Ben Pol, kwa nini amefikia uamuzi huo.

Fisi Azua Taharuki Hospitali, Anaswa Akirandaranda

$
0
0
Fisi Azua Taharuki Hospitali, Anaswa Akirandaranda
Wagonjwa na watumishi wa afya katika Hospitali ya Mji wa Kahama, juzi waliingiwa na taharuki na kutimua mbio ovyo baada ya fisi kuonekana asubuhi akirandaranda katika baadhi ya majengo ndani ya uzio wa hospitali hiyo.

Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk Lucas David alisema fisi huyo alionekana saa kumi na mbili asubuhi bila kufahamu sehemu aliyopitia kuingia ndani na pia hakuna aliyejua alikotokea.

Alisema eneo la hospitali hiyo lina uzio mkubwa, lakini inawezekana fisi huyo alipitia eneo la chuo cha uuguzi ambako kuna matundu yaliyotobolewa na wanafunzi sehemu inayopakana na chumba cha maiti ambacho huenda lango la huko lilikuwa wazi.

Dk David alisema baada ya hali hiyo ya mtafaruku walitoa taarifa ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kahama na watendaji wa Idara ya Wanyamapori walifika hospitalini hapo na kumuua kwa risasi tatu hali ambayo ilituliza taharuki na kazi ndani ya hospitali hiyo ziliendelea kama kawaida.

Wilaya ya Kahama imekuwa na tatizo la kuzagaa kwa fisi ambao wanatishia maisha ya wananchi hasa wafugaji wanaolalamika mifugo yao kuliwa mara kwa mara na wanyama hao, huku jamii nyingine ikihusisha matukio ya kuzagaa kwa fisi hao na imani za kishirikina.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Juma Bakari alisema huenda mnyama huyo alisikia harufu inayotoka katika chumba cha kuhifadhia maiti.

“Huenda fisi huyo aliingilia huko kwa kufuata harufu kwa lengo la kula miili ya watu waliokufa na kuhifadhiwa huko, ndio maana alipitia maeneo hayo hayo,” alisema Bakari. Tukio la fisi huyo kuingia ndani ya hospitali limekuja baada ya Serikali mkoani Shinyanga kuanzisha msako wa kuwaua fisi katika halmashauri zote tatu za Wilaya ya Kahama kutokana na madhara yaliyosababishwa na wanyama hao kwa wananchi.

       

Jaji Mkuu Aliyefuta Matokeo ya Uchaguzi Mkuu Kenya Atua nchini,

$
0
0
Jaji Mkuu wa Kenya, David Maraga ametua nchini katika mkutano wa majaji na mahakimu akionekana kivutio kwa wengine.

Jaji huyo ni mmoja wa majaji wakuu 13 kutoka nchi mbalimbali duniani wanaohudhuria mkutano majaji na mahakimu wa nchi za Jumuiya ya Madola unaofanyika jijini Dar es Salaam kwa siku tatu..

Maraga amegeuka kivutio baada ya kushangiliwa na majaji waliohudhuria mkutano huo wakati alipotambulishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma.

Profesa Juma amempongeza Maraga kwa kuwakilisha mfano bora wa kulinda uhuru wa Mahakama kwa nchi nyingine duniani.

Kiongozi huyo ameonekana akiwa ameambatana na walinzi wanne ambao wanamfuata popote anapotembea nje ya mkutano huo.

Hata hivyo, Maraga amekataa kuzungumza na vyombo vya habari kwa madai amekuja kuhudhuria mkutano huo na siyo kwa jambo jingine lolote.

Mkutano huo umefunguliwa leo Jumatatu na Makamu wa Rais, Samia Suluhu ukiwa na kauli mbiu "Kujenga Mahakama Shirikishi, Thabiti na Inayowajibika."

Jaji Mkuu Aliyefuta Matokeo ya  Uchaguzi Mkuu Kenya Atua nchini,
Jaji Maraga kwa siku za hivi karibuni amekuwa maarufu baada ya kutoa uamuzi wa kufuta Uchaguzi Mkuu wa Kenya uliokuwa umempa ushindi Rais Uhuru Kenyatta.

Katika mkutano huo Samia amesema rushwa ni kitu ambacho kinaondoa uhuru wa Mahakama na utawala wa sheria katika nchi mbalimbali duniani.

Samia amesema Tanzania inachukua hatua dhidi ya rushwa ili kuhakikisha kwamba Mahakama inatenda haki.

Amesema majaji na mahakimu wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha Mahakama inakuwa uhuru kwa kuzingatia maadili ya kazi yao.

"Mahakama ya Tanzania itahakikisha kwamba rushwa haitakuwa sehemu ya utendaji wake. Tumetangaza vita dhidi ya rushwa katika ngazi zote za Serikali," amesema Samia.

Kiongozi huyo wa Serikali amebainisha changamoto kubwa inayozikabili nchi mbalimbali duniani kuwa ni uhaba wa fedha za uendeshaji wa Mahakama, jambo ambalo linaathiri mifumo ya utoaji haki.

Kwa kutambua hilo, amesema Serikali inajitahidi kuongeza bajeti ya Mahakama kila mwaka wa fedha ili kesi ziamuliwe kwa haraka na kwa haki.

Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma amesema bajeti ya Mahakama imeongezeka kwa asilimia 100 na wameanza kutekeleza mipango mbalimbali ya kuboresha utendaji.

Profesa Juma amefafanua kwamba katika mpango wa Taifa wa miaka mitano, Mahakama utakaokamilika 2020, zitajengwa mahakama 48 za wilaya, mahakama 100 za mwanzo na mahakama kuu 13 katika sehemu mbalimbali nchini.



"Bajeti inayokidhi mahitaji ni muhimu sana kwa uhuru wa mahakama. Tumekuwa na changamoto ya uhaba wa majengo ya mahakama lakini tunaendea kukabiliana nalo," amesema.

Panga Wagombea CCM Lawadia...Walioanza Kampeni Kabla ya Muda Kikiona cha Moto

$
0
0
KAMATI Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) za Chama Cha Mapinduzi (CCM), zinakutana wiki hii katika vikao vya kuchuja majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi ngazi za Wilaya.

Taarifa iliyotolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole, ilieleza kuwa Kamati Kuu itakutana keshokutwa na Alhamisi, na Halmashauri Kuu ya Taifa itakaa Jumamosi na Jumapili.

‘Panga’ hilo litawagusa zaidi wagombea ambao wameanza kampeni mapema kabla ya muda uliopangwa, wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaona, na wagombea wanaodaiwa kutoa rushwa, ili kupigiwa kura.

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM, alieleza kukerwa na baadhi ya mambo yanayofanywa na baadhi ya viongozi ndani ya chama hicho na kuapa kukisafisha wakati akikabidhiwa nafasi hiyo na mwenyekiti mstaafu, Jakaya Kikwete Julai 23, mwaka jana.

Aidha, aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Abdallah Bulembo alisema Jumanne iliyopita kuwa kanuni za chama hicho zinawataka wagombea kuchukua fomu kimya kimya, ili wananchi wachague wagombea wanaoona wanafaa kuwaongoza badala ya kuwahadaa kwa mbwembwe na rushwa.

“Taarifa zote tunazo, kama kuna mgombea anadhani anaweza kuanza kampeni mapema na asijulikane tumpe pole maana yanayofanyika huko kote mikoani tunayapata na nawahakikishia watakatwa,” alisema Bulembo kuashiria baadhi ya wanaCCM 'watalia' wiki hii.

Dalili kuwa uchujaji wa wagombea katika chaguzi za CCM mwaka huu utakuwa si wa kiwango cha kilichozoeleka ziliongezwa pia na salamu za Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana wakati wa maandhisho ya miaka 40 ya chama hicho mjini Dodoma.

Kinana alisema wakati wa uchaguzi viongozi wamegeuza kuwa mradi wa kujipatia fedha hivyo kuongeza rushwa kuwa kigezo kingine kitakachoondoa wanachama kwenye orodha ya wagombea.

Taarifa iliyotolewa jana na Polepole ilieleza kuwa vikao hivyo vitakaa kwa mujibu wa ratiba yake ya kawaida, pamoja na mambo mengine vitakuwa na kazi ya kujadili, kupitisha na kufanya uteuzi wa mwisho kwa wagombea wa CCM walioomba dhamana ya uongozi katika ngazi ya Wilaya.

"Chama Cha Mapinduzi kinapenda kuujulisha umma wa wanachama wa CCM na Watanzania kwa ujumla kwamba vikao vya uongozi vya taifa, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa, na Halmashauri Kuu ya Taifa vitakaa hivi karibuni," ilisema taarifa ya Polepole.

Aidha taarifa hiyo ilieleza kuwa vikao hivyo vitafanyika katika Jiji la Dar es Salaam.

CCM ndiyo chama tawala ambapo katika Uchaguzi Mkuu uliopita, mbali na kushinda nafasi ya urais, katika majimbo 264 yaliyopo nchi nzima kilipata majimbo 195 sawa na asilimia 73.86 na kati ya kata 3,946 CCM ilishinda kata 2,875 sawa na asilimia 72.68.

CRDB Yampa PAUL Makonda Milioni 100 Kusaidia Ujenzi wa ofisi za Walimu kwa Shule za Msingi na Sekondari

$
0
0
CRDB Yampa PAUL Makonda Milioni 100 Kusaidia Ujenzi wa ofisi za Walimu kwa Shule za Msingi na Sekondari
Paul Makonda
Benki ya CRDB leo Jumatatu imekabidhi msaada wa Sh100 milioni kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa ofisi za walimu kwa shule za msingi na sekondari mkoani hapa.

Mbali na kukabidhi fedha hizo, mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo, DK Charles Kimei ameahidi kuongeza Sh100 milioni katika bajeti ijayo.

"Mwalimu ndio chanzo cha maarifa ya kila mtu, tukitengeneza mazingira mazuri ya ufanyaji kazi kwake hata elimu inayotolewa itakua na kiwango," amesema Dk Kimei.

Amesema ili Taifa liweze kusonga mbele kimaendeleo ni lazima kuwekeza katika kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu na kuweka mazingira bora ya ufundishaji.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi ya Mkoa wa Dar es Salaam, Kanali Charles Mbuge alimhakikishia Dk Kimei kuwa pesa zilizotolewa zitafanya kazi iliyokusudiwa.

"Thamani ya pesa iliyotolewa italingana na kile kitakachofanyika na hii iwe chachu kwa benki nyingine kuweza kuchangia ujenzi huu," amesema Kanali Mbuge.

Mkoa wa Dar es Salaam una jumla ya shule 638 zikiwa na upungufu wa ofisi 402 za walimu.

Chanzo: Mwananchi

Akothee wa Kenya Atoa Kitchen Party Kali Kwa Wanawake wa Kitanzania Hasa Hamisa Mobeto

$
0
0
Akothee wa Kenya Atoa Kitchen Party Kali Kwa Wanawake wa Kitanzania Hasa Hamisa Mobeto
Akothee
Ishu ya Diamond, Hamissa na Zari yazidi kuvuka Border... Na sasa Billionaire wakike kutoka Kenya ambaye pia amewahi fanya kazi na Diamond Yamemfika hapa... Aandikia ujumbe huu wa mafumbo



By @akotheekenya -
But why would I take photos of someone I have just stolen for a sex moment if am not a maliciuos person , I think I can forgive my baby if he is caught in this scenario, why are girls not intelligent , if you succeded & convinced him to bed , then trust me, you can still manipulate his finances without interfearing with his family if you have some brains , so you be his panadol when his main chick is on fire , mbona hamjui kula na vipofu nyie , mbona mashot cut za kijinga ? mmm game yenu iko chini kama kiatu , a man wont be horny forever, and sex wont keep a man, its beyond bed haloooo. goodnight (sijasema mkatafute mabwana za watu , japo munawasaka , na sijataja mtu , leta matusi nikupe raha ) #brains Work , why take evidence of sex , who does'nt know what happens when opposite sex are in bed ? what are you keeping evidence for ? how is hurting his family satisfying your malicious behaviour , it shows clearly you dont even love or want this man , you want this family broken and thats your mission

Msigwa Kwenda Mahakamani Kulishtaki Jeshi la Polisi

$
0
0
Msigwa Kwenda Mahakamani  Kulishtaki Jeshi la Polisi
Mbunge wa Iringa Mjini(Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amesema atalishitaki Jeshi la Polisi, kwa tuhuma za kuingilia majukumu yake ya kikazi pale anapokuwa akitimiza wajibu wake wa kibunge ikiwemo kuongea na wananchi.

Mchungaji Msigwa amesema atakata rufaa kwa sababu polisi wamezuia mikutano yake ya leo na kesho ambayo alitarajia kufanya katika kata za Kihesa na Kitwiru kwa madai ya kukiuka masharti alipohutubia katika Kata ya Mlandege.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu, Mchungaji Msigwa amesema chombo pekee kinachoweza kumtia hatiani kwa kufanya uchochezi ni Mahakama na sio polisi.

“Jana walinikamata tangu saa 11:30 na kuanza kunihoji mpaka  saa 3:15 usiku kwa tuhuma za kufanya uchochezi lakini mimi nakataa sijafanya uchochezi kwa sababau hakuna mtu anaweza kunizuia kuongea na wananchi wangu, wanadai nimeleta hofu na kuvichonganisha vyombo vya dola na wananchi,” amesema Mchungaji Msigwa .

Amesema mpaka muda huu yupo nje kwa dhamana na tayari ameripoti polisi asubuhi leo Jumatatu amehojiwa lakini ameambiwa ataitwa tena kwa mahojiano zaidi.

“Mimi niko tayari hata kama wangeniweka ndani wiki mbili siogopi kwa sababu sitanyamaza nitaendelea kuongea na sitaacha kusema kilichomtokea Tundu Lissu na ili kuninyamazisha ni lazima waniue kwa sababu nishajiandaa kisaikolojia,” amesema Mchungaji Msingwa.

Akizungumzia hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Julius Mjengi amesema walimkamata Msigwa kwa kuwa alikuwa anatoa maneno ya uchochezi kwa wananchi aliokuwa anawahutubia mkutano wa hadhara Kata ya Mlandege.

Mgengi amesema bado jeshi hilo linaendela na upelelezi juu ya tuhuma hizo na mara utakapokamilika watamfikisha mahakamani mbunge Msigwa.

Mwili wa Watekaji Watoto Kuzikwa na Jiji

$
0
0
Mwili wa Watekaji Watoto Kuzikwa na Jiji
Mwili wa mtuhumiwa aliyedaiwa kuhusika na matukio ya utekaji watoto katika jiji la Arusha, Samson Petro (28) ambaye alifariki baada ya  kupigwa risasi na polisi Septemba 7 mwaka huu unatarajiwa kuzikwa na jiji baada ya kutelekezwa na ndugu zake.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu mhudumu wa chumba cha kuhifadhi miili katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Fransis Costa  amesema tangu mwili huo ukabidhiwe na polisi hakuna ndugu aliyejitokeza.

Costa amesema baada ya mwili huo kuhifadhiwa tangu Septemba 7 sasa wanatarajia kuwapa jiji la Arusha ili wauzike.

"Kwa utaratibu wetu mwili unapokosa watu wa kuzika tunatoa taarifa jiji ili uzikwe," amesema.

Petro ilidaiwa kuwateka na kuwaua watoto wawili, Ikram Salim(3) na Moureen David(6) wakazi wa Arusha

Neema Yashuka TFF Yaingia Mkataba Mnono

$
0
0
Neema Yashuka TFF Yaingia Mkataba Mnono
Shirikisho la soka nchini TFF, leo Septemba 25 limesaini mkataba na benki ya KCB wenye thamani ya shilingi 325,000,000.

Akiongea wakati wa kusaini mkataba huo Rais wa TFF Wallace Karia amesema huo ni ushahidi kuwa shirikisho lina ushirikiano na wadau mbalimbali wa mpira nchini.

Aidha Karia amesema fedha hizo zitaelekezwa kwenye kukuza vipaji vya soka pamoja na maendeleo ya soka nchini kwa ujumla.
Huu ni mkataba mkubwa wa kwanza kusainiwa na shirikisho hilo tangu uongozi mpya chini ya Rais Wallace Karia uingie madarakani August 12 mwaka huu.

Viewing all 104766 articles
Browse latest View live




Latest Images