Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Lissu Amekosea Nini Nchi Mpaka Kufanyiwa Hivi- Nyarandu

$
0
0
Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu amesema kitendo cha Tundu Lissu kusalimika kifo kwenye tukio la kupigwa risasi ni Mungu tu ndiye aliandika, lakini kinamuumiza zaidi huku akilaumu ameikosea nini nchi mpaka kufanyiwa hivyo.

Lazaro Nyalandu ameyasema hayo kwenye ukurasa wake wa facebook, akiwa mkoani Mbeya ambapo alishiriki maombezi ya Tundu Lissu ambayo yalifanyika siku ya jana.
"Nimekuja Mbeya kulikumbusha Taifa kuwa kupigwa kwa mmoja wetu ni kupigwa kwetu sote, kuumizwa kwake ni kuumizwa kwetu sote, na kudhulumiwa kwake huyo mmoja ni dhuluma dhidi ya kila Mtanzania. Tundu Lissu amepona kwa kuwa imeandikwa, naamini, ndani ya moyo wake akiwa katika maumivu lukuki aliyonayo, atakuwa anajiuliza nimekukosea nini Tanzania", ameandika Lazaro Nyalandu
Lazaro Nyalandu amekuwa miongoni mwa watu wanaofuatilia kwa karibu matibabu ya Tundu Lissu jijini Nairobi, huku akiimiza watanzania kuendelea kumuombea ili aweze kupona kabisa na kurejea kwenye hali yake ya kawaida.

Waziri Makyembe Afuta Mashindano ya Miss Tanzania

$
0
0
Waziri Makyembe Afuta Mashindano ya Miss Tanzania
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amesema wizara yake imefuta mashindano ya Miss Tanzania kwa sababu yaligubikwa na ubabaishaji mwingi katika uendeshaji wake.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Dkt. Mwakyembe ameeleza hayo baada ya kupita takribani miezi mitatu tokea alipokabidhiwa zawadi yake Miss Tanzania 2016/2017, Diana Edward ambayo ilizua maneno mengi katika mitandao ya kijamii wakidai zawadi hiyo ya gari waliyompatia Miss huyo ilikuwa imechakaa na kupewa nje ya wakati na kushusha hadhi ya mashindano hayo pamoja na kuvunja moyo kwa watu ambao walikuwa na lengo la kushiriki katika mashindano mengine yajayo.
"Mimi na wizara yangu tuna mikakati tofauti kabisa, tungependa vitu vyote tunavyo vianzisha viwe na muendelezo na siyo vianzishwe leo keshokutwa vimekatika. Niwatolee mfano kidogo tulikuwa na Miss Tanzania hapa chini lakini nimepiga marufuku kwa sababu ya uswahili mwingi ambao mimi siwezi kuukubali nikiwa kiongozi wa hii wizara, kwa hiyo nimewakatalia wote hakuna cha miss Tanzania", amesema Dkt. Mwakyembe.
Pamoja na hayo, Dkt. Mwakyembe ameendelea kwa kusema "Endapo watataka kuendesha hayo mashindano nitahitaji zawadi ya mshindi wa kwanza kama ni gari iletwe ofisini kwangu niione na waniachie funguo yake pia zawadi ya mshindi wa pili hivyo hivyo ndipo nikaporuhusu. Maana kila mwaka zawadi ya mshindi wa kwanza imekuwa ikisumbua kutolewa kwa muhusika. Sasa huo mchezo hapana, hatuwezi kuona ukiendelea, ubabaishaji siyo kwa Tanzania ya leo"
Kwa upande mwingine, Dkt. Mwakyembe amesema sasa anachokifanya ni kukaa chini na baadhi ya wadau wa masuala ya 'fashion' ili waweze kuyaboresha mashindano hayo yaweze kuwa bora na kufanyika kila mwaka bila ya kuwa na ubabaishaji.

Serikali Yamjia juu mtumishi Aliyeshinda CCM

$
0
0
Serikali Yamjia juu mtumishi Aliyeshinda CCM
Serikali mkoani Morogoro imemtaka mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya Mvomero, Salvatory Richard aliyeshinda nafasi ya Uenyekiti wa Wazazi wa CCM wilayani humo kuchagua utumishi wa umma ama siasa.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Clifford Tandari amesema haiwezekani kwa mtumishi wa umma kutumikia nafasi ya kisiasa kwani sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma zinakataza.

"Tulikuwa na kikao asubuhi na tumeiagiza Halmashauri ya Mvomero kumchukulia hatua stahiki mtumishi huyo kwani kanuni na taratibu za Serikali haziruhusu mtumishi kutumikia nafasi hizo mbili," amesema.

Tandari amesema mtumishi huyo ataeleweshwa taratibu za utumishi wa umma zilivyo ili aamue kama atabaki serikalini ama ataenda kutumikia siasa.





Katibu tawala huyo amewaonya watumishi wa Serikali mkoani humo kuhakikisha wanapitia na kuelewa kanuni za utumishi wa umma vizuri ili kuondoa migongano isiyo ya lazima.

"Tumekuwa tukitoa elimu mara kwa mara kwa watumishi wetu kuhusu sheria na kanuni za utumishi wa umma lakini sijui kwa nini hawazingatii," amesema Tandari.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mvomero, Florent Kyombo amesema tayari wameshaanza kuchukua hatua katika kushughulikia swala hilo.

"Leo tumewaandikia CCM barua ili kwanza tupate uthibitisho wa maandishi kwamba ni kweli mtumishi wetu amechaguliwa katika nafasi husika,” amesema.

Amesema CCM wakishathibitisha kuhusu mtumishi huyo ndipo halmashauri itakapoanza utaratibu wa kumtaka aamue kuacha kazi au aombe likizo bila malipo ili aweze kutumikia kwanza nafasi aliyoipata.

Kyombo amesema halmashauri itafuata sheria, kanuni na taratibu za kuongoza Serikali katika kushughulikia suala la Richard.

Katibu wa Wazazi wa CCM wilayani Mvomero, Ally Castro amesema kwa upande wa chama Richard alikuwa na haki ya kuchaguliwa na wanachama wametimiza wajibu wao.



"Katika chama tunahimizwa kuchagua kiongozi mwenye kipato halali na huyu ana kipato halali lakini pia CCM ni ya wakulima na wafanyakazi, sasa shida iko wapi," alihoji Castro.

Ambe Lulu Awapa Mkavu Wasanii Wanaowasema Video Vixen Kuingia Kwenye Muziki

$
0
0
Ambe Lulu Awapa Mkavu Wasanii Wanaowasema  Video Vixen Kuingia Kwenye Muziki
Wimbi la video vixen kuhamia katika kuimba limeonekana kukuwa kila kukicha. Amber Lulu amewachana wasanii ambao wamekuwa wakiwachukia warembo hao wa video wanapoamua kuingia katika tasnia ya kuimba.

Kazi ya video vixen Bongo imekuwa ikichukuliwa isiyofaa na haieleweki huku warembo wake wakionekana wenye tabia mbaya kupita kiasi. Akiongea na Bongo5, Lulu amesema, “Kitu kibaya walikiona kwao, kwa sababu kila siku wapo na unavyozidi kuwepo kila siku kila msanii unatakiwa kuwa na kitu kipya.

“Wao waavyoona watu wapya wanavyozidi kutokeza katika kitu wanachokifanya wao hizo ni jelous tu. Nadhani kitu kizuri wao wanatakiwa kufanya ni kutupa support sisi halafu kuona mwisho wa siku utakuwaje,” ameongeza.

“Wao wanang’ang’ania hili game hawataki watu wapya halafu hawataki watu wapya wakati wao hawana vitu vipya vya kufanya watu kuwavutia. Sisi ndio watu tunavitu vipya watu wanataka kuangalia mambo mengine kabisa sio kila siku unamuona nani kasimama kwenye steji na MIC yake anaimba tu.”


Msajili wa Mahakama ya Juu Achunguzwa

$
0
0
Msajili wa Mahakama ya Juu Achunguzwa
Wale waliodhani uchunguzi ulioagizwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ungeishia kwa maofisa wa juu wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuangalia ushiriki wao katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Agosti 8 watakuwa wamekosea.

Leo timu ya wachunguzi iliyoundwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) na kikosi cha kupambana na rushwa ilifanya kikao cha kuanza uchunguzi mpana pamoja na mwenendo wa Msajili wa Mahakama ya Juu, Esther Nyaiyaki.

Hatua hiyo imekuja baada ya mpiga kura Rashid Mohammed kuwasilisha malalamiko Ijumaa iliyopita kupitia kwa mwanasheria wake Kioko Kilukum akidai ripoti ya uchunguzi wa matokeo ya uchaguzi au fomu zake ilighushiwa.

Mohammed alidai kwamba ripoti ya uchunguzi iliyotumiwa na majaji wengi katika hukumu yao dhidi ya matokeo ya urais yanayobishaniwa ilikuwa na ugunduzi tofauti na nyaraka zilizotumiwa na Jaji Njoki Ndung'u.

Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa (EACC) ilisema timu hiyo iliundwa mara baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Mohammed.

Mwishoni mwa wiki DPP, Keriako Tobiko aliviagiza vyombo vya dola kuanzisha uchunguzi dhidi ya maofisa wa juu wa IEBC kuangalia ushiriki wao katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Agosti 8 ambao matokeo yake yalifutwa na Mahakama ya Juu Septemba Mosi.

Tobiko amewapa siku 21 DCI Ndegwa Muhoro na yule wa EACC, Halakhe Waqo kumkabidhi matokeo ya uchunguzi wao.

“Kwa hiyo ninakuandikia kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 157 (4) ya Katiba na Sheria ya Makosa ya Uchaguzi 2017 ili kukutaka ufanye uchunguzi wa pamoja, wa kina na wa haraka katika makosa na uhalali ulioonekana na Mahakama Kuu kufanywa na IEBC katika uchaguzi wa rais kwa lengo la kuamua ikiwa uchaguzi ulikuwa na makosa mengine ya jinai yanayoweza kuwa yalisababishwa na maofisa wa IEBC,” alisema Tobito.

Agizo hilo la DPP limekuja wakati IEBC ilitarajiwa leo kutoa jibu kuhusiana na masharti yaliyotolewa na muungano wa Nasa unaotaka uwapo mkutano baina ya pande zinazoshiriki kabla ya uchaguzi wa marudio uliopangwa kurudiwa Oktoba 26.

Uamuzi huo kwa namna yoyote usipotekelezwa unaweza kuathiri mwenendo wa mchakato wa uchaguzi huo katika mazingira yanayoonyesha kwamba ndani ya Tume ya Uchaguzi na Mipaka ‘kunawaka moto’, kutokana na maofisa wake wa ngazi za juu kutakiwa na Nasa wajiuzulu kwa kuboronga uchaguzi huo.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa EACC Halakhe Waqo alisema timu yao na ile kutoka DCI itafanya kazi pamoja kwa vile suala linalochunguzwa linafahamika.

Mwanamke Aliyetajwa Kuwa Mwenye Uzani Mkubwa Zaidi Duniani Amefariki

$
0
0
Mwanamke Aliyetajwa Kuwa Mwenye Uzani Mkubwa Zaidi Duniani Amefariki
Mwanamke raia wa Misri ambaye aliaminiwa kuwa mtu mwenye uzani mkubwa zaidi duniani amefariki kwenye hospitali moja katika umoja wa falme za kiarabu
Eman Ahmed Abd El Aty alikuwa amepelekwa nchini India kufanyiwa upasuaji wa kupunguza uzito wa mwili.
Vyombo vya habari viliripoti kuwa alikuwa amepunguza uzito kwa kilo 300 kutoka kwa uzito wa kilo 500 lakini akafariki kutokana matatizo mengine ya kiafya.
Taarifa za hospitali zinasema kwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 37 alikuwa na ugopnjwa wa moyo na matatizo ya figo.
"Tunatuma rambi rambi na maombi yetu kwa familia," taarifa ya hosptali ilisema.
Mwanamke apunguza uzani wa kilo 500 hadi kilo 250
Bi Abd El Aty amekuwa kwenye hospitali huko Abu Dhabi tangu mwezi Mei baada ya kuhamishiwa huko kufuatia upasuaji aliofanyiwa nchini India.
Kabla ya hajafanyiwa upasuaji familia yake ilisema kuwa hakuwa ameondoka nyumbani kwake kwa miaka 25.
Kutokana na hali kwamba hakuwa ametoka kitandani kwa miaka 25, kulikuwa na hatari kwake kuugua maradhi ya kupumua na ili kusafirishwa madaktari walichukua tahadhari kubwa na kumpa dawa za kuyeyusha damu mwilini.
Kitanda alichosafirishwa nacho ni kitanda maalum kilichoundwa na mafundi wa Misri kwa kufuata matakwa ya shirika la ndege la EgyptAir.
Kilikuwa na mitambo na vifaa vya huduma ya dharura.
Familia ya Eman Ahmed inasema kuwa alikuwa na uzani wa kilo 5 alipozaliwa kabla ya kupatikana na ugonjwa wa matende, ugonjwa ambao unasababisha kufura kwa mwili kutokana na maambukizi ya vimelea.
Wakati alipofikisha umri wa miaka 11, uzani wake uliongezeka maradufu na akaugua kiharusi ugonjwa uliomuacha kitandani kwa kipindi kirefu cha maisha yake.
Aliyekuwa na uzani wa kilo 500 apungua hadi kilo 174
Baada ya kampeni kupitia mitandao iliyofanywa na dada yake, aliweza kusafiri hadi mjini Mumbai kupata msaada wa madakatari wa India.
Hata hivyo alihamishwa tena kutoka India baada ya familia yake kutofautiana hadharani na madaktari wa India.

Lema' Nassari ni Wabunge Halali Tushikamane Kuleta Maendeleo- JPM

$
0
0
Lema' Nassari ni Wabunge Halali Tushikamane Kuleta Maendeleo- JPM
Rais Magufuli amewazungumzia wabunge wawili wa (CHADEMA) Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema pamoja na Mbunge  wa jimbo la Arumeru Mashariki Mhe. Joshua Nassari kuwa ni wabunge halali wa majimbo hayo kwa kuwa wananchi ndiyo waliwachagua.

Rais Magufuli amesema hayo leo aliposimamishwa na wananchi wa Sangisi katika kata ya Akeri nje kidogo ya Mji wa Arusha akiwa njiani kurejea jijini Dar es Salaam leo Asubuhi na kusema yeye atabaki kuwa Rais wala hawezi kubadilika na kuendelea kuwatumikia Watanzania wote.
"Uchaguzi umeshakwisha sasa ni maendeleo mliamua mkamchagua Magufuli na ndiyo Rais na mimi nitakuwa Rais wala sibadiliki na nitawatumikia Watanzania wote, mliamua mkamchagua Mhe. Lema wa CHADEMA kuwa Mbunge wenu yule ni Mbunge halali, mkaamua kumchagua Nassari kuwa Mbunge wenu ni Mbunge halali kwa hiyo tushikamane sisi kama Watanzania kuleta maendeleo yetu uchaguzi ulikwisha tusubiri mwaka 2020" alisema Rais Magufuli
Mbali na hilo Magufuli amewataka Watanzania kuleta maendeleo ya kweli bila kubagua vyama na kubagua dini zetu na bila kubagua makabila na kusema yeye kama kiongozi wa nchi hajaweza kuwabagua na ndiyo maana anafanya mambo ya maendeleo katika majimbo hayo ikiwa ni pamoja na kupeleka barabara

Odinga na Wafuasi Wake Kuandamana Kesho

$
0
0
 Odinga na Wafuasi Wake Kuandamana Kesho
Muungano wa upinzani nchini Kenya NASA, umesema siku ya Jumanne utaongoza maandamano ya wafuasi wake nje ya Ofisi ya Tume ya Uchaguzi jijini Nairobi, kushinikiza mabadiliko ndani ya Tume hiyo kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi mpya wa urais tarehe 26 mwezi Oktoba.

Kiongozi wa muungano huo Raila Odinga ametangaza kuwa, hawatakubali kufanyika kwa Uchaguzi huo iwapo Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Ezra Chiloba na maafisa wengine wataendelea kuandaa uchaguzi mpya.

Naibu rais William Ruto ambaye pia ni naibu kiongozi wa chama cha Jubilee ameshutumu kauli ya Odinga na kueleza ni mbinu ya kiongozi huyo wa upinzani kutotaka Uchaguzi.

Mvutano wa kisiasa unaendelea nchini Kenya, huku ikiripotiwa kuwa Tume ya Uchaguzi inapanga kukutanana wawakilishi wa pande zote mbili za kisiasa, kukubaliana kuhusu maandalizi ya Uchaguzi mpya.

Wakati uo huo, kiongozi wa mashtaka nchini Kenya Keriako Tobiko, ameagiza kuchunguzwa kwa Tume ya Uchaguzi nchini Kenya baada ya kufutwa kwa matokeo ya Uchaguzi wa urais mwezi uliopita.

Tobiko ameagiza Polisi na maafisa wa tume ya kupambana na ufisadi kuchunguza iwapo wafanyikazi wa Tume hiyo waliohusika na udanganyifu uliosababisha matokeo hayo kufutwa.

Bola Kufananishwa na Young Killer Ila Kufananishwa na Mla Unga Young Dee Sitaki- Dogo Janja

$
0
0
Bola Kufananishwa na Young Killer  Ila Kufananishwa na Mla Unga Young Dee Sitaki- Dogo Janja
MSANII wa Hip Hop nchini Dogo Janja aliyekaa kimya juu ya kauli za Young Killer na Young Dee, sasa kafunguka na kusema Young Killer alimwambia  hamuwezi ni kwa sababu alishakuwa  role model wake, lakini alisema  hakupenda  Young Dee kumuita yeye ni kifaranga.
Alipoulizwa juu ya kauli ya Young Dee kumuita kifaranga, alifunguka: “Mimi pia sipendi kufananishwa na kifaranga japo sijakataa kufananishwa na Young Killer kwa sababu alishawahi kuwa role model wangu, kwa hiyo kufananishwa naye si  kitu kibaya, lakini kufananishwa na mla unga  Young Dee ndiyo sipendi tena mnakosea kabisa.
“Young Dee akiacha kula unga tutakaa mezani tuzungumze lakini kufananishwa naye sasa hivi sitaki kwani ni mtu ambaye ukimuacha nyumbani kwako unawaza vitu vyako kama TV, radio na vingine.  Je,  utavikuta salama,  maana asije kuiba kwenda kuuza,” alisema Dogo Janja
Hawa ni vijana wanaofanya vizuri kwenye muziki wa Hip Hop  nchini, ambako pia watu wanawafananisha kutokana na wote wanavyoimba kwa aina ya kurap ila kwa kila mmoja hapendi kufananishwa  na mwenziye

Benki Inayodaiwa Kuchangia Mauaji wa Kimbari Rwanda Yafanyiwa Uchunguzi

$
0
0
Benki Inayodaiwa Kuchangia Mauaji wa Kimbari Rwanda Yafanyiwa Uchunguzi
Ufaransa imeanzisha uchunguzi dhidi ya benki ya BNP Paribas, kufuatia madai kuwa ilihusika na mauaji kimbari nchi Rwanda mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu 800,000 waliuawa.
Mashirika matatu ya umma yamepeleka kesi mahakamani dhdi ya benki hiyo, wakiilaumu kwa kupitisha dola milioni 1.3 kwa muuza silaha.
Pesa hizo zilitumiwa kununua silaha na kukiuka azimio la marufuku ya silaha la Umoja wa Mataifa.
Papa Francis aomba msamaha kwa mauaji Rwanda
UN: Huenda Sudan Kusini ikakumbwa na mauaji ya kimbari
UN: Kuna hofu ya kutokea mauaji ya kimbari Sudan Kusini
Kanali wa kabila la Hutu ambaye alipokea silaha hizo, Theoneste Bagosora, anatumikia kifungo cha miaka 35 jela kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Mauaji ya kimbari nchini Rwanda yalizuka baada ya ndege iliyokuwa imembeba Rais Juvenal Habyarimana kutoka kabila la Hutu ilidunguliwa Aprili tarehe 6 mwaka 1994.
Wanamgambo wa Hutu kisha wakawaua watu wa Tutsi walio wachache katika kipindi cha siku 100.

Ajari Yaua na Kujeruhi Zaidi ya60 Barabara ya Shinyanga Kwenda Mkoani Mwanza

$
0
0
Ajari Yaua na Kujeruhi 60 Barabara ya Shinyanga Kwenda Mkoani Mwanza
Mtu mmoja amefariki na wengine zaidi ya 60 kunusurika kifo katika ajali ya basi la kampuni ya Allys Sports kupinduka katika barabara kuu ya Shinyanga kwenda Mkoani Mwanza.

Hayo amethibitisha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Kamishna Msaidizi wa Polisi, Simon Haule na kusema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi ambao ulipelekea basi hilo kupoteza mwelekeo na kusababisha ajali ya hiyo.
"Majeruhi wengi wa ajali hiyo wamepelekwa katika hospitali ya Kola ndoto iliyopo Mwadui na wengine wamepelekwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa shinyanga kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Dereva wa gari hilo amekimbia mara ilipotokea ajali", amesema Kamanda Haule.
 Kwa upande mwingine, Jeshi la Polisi la mkoa wa Shinyanga limesema linaendelea kumsaka dereva aliyesababisha ajali hiyo na kutoroka ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Pendeza na Kessy Products: Badili Muonekano Wako na Kuweka Mwili Wako Sawa Bila Madhara yoyote

$
0
0
PENDEZA NA KESSY PRODUCT: BADILI MUONEKANO WAKO NA KUWEKA MWILI WAKO SAW KWA PRODUCT ZA ASILI ZISIZO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI, MATOKEO NI KWAARAKA


1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _80,000/
2) KUREFUSH NYWELE  KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 90,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK (B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
  4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _90,000/
5)TOA  KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _80,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_80,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_90,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_90,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MILINI _90,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI_80,000/(B)VIDONGE MAX MAN_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_120,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_90,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_70,000/
(21) ENGEZA  MGUU_80,000/

 TUNAPATIKAN DAR W SALAAM: NAKWA MIKOAN KOTE UTAPATA PIGA CM

(+255) 0719955528
0756259180
0785371237

@dr_kessy_product
Delivery  POPOTE ULIPO

Bilioni 8.2 Zasakwa Kuwarudisha Wakimbizi Makwao

$
0
0
Bilioni 8.2 Zasakwa Kuwarudisha Wakimbizi Makwao
Wito uliotolewa Julai 20 na Rais John Magufuli na Pierre Nkurunziza wa Burundi wakiwa mkoani Kagera kuwataka wakimbizi kwenda kuijenga nchi yao kutokana na usalama kuimarika, umeanza kutafutiwa fedha kutoka jumuiya ya kimataifa.

Katika kutekeleza mpango huo, Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limesema linahitaji Dola 3.7 milioni za Marekani (zaidi ya Sh8.2 bilioni) kuwarudisha nyumbani Warundi walioonyesha nia ya kufanya hivyo.

IOM imesema itashirikiana na Shirika la Wakimbizi Duniani (UNHCR) kufanikisha suala hilo baada ya wakimbizi 12,000 kuridhia kurudi nyumbani ambako taarifa zinasema usalama umeimarika.

Mkakati wa kuwarudisha wakimbizi hao waliowasili nchini tangu Aprili 2015 unatekelezwa baada ya mkutano uliofanyika Agosti 31 na kuwakutanisha maofisa wa Serikali za Tanzania, Burundi na UNHCR kupitisha mpango huo.

Kwa mujibu IOM, mambo kadhaa yaliridhiwa kwenye mkutano huo ikiwamo kufanikisha kuwarudisha kwa awamu wakimbizi 12,000 walio tayari kuanzia Septemba 7 mpaka Desemba 31. “IOM inao utaalamu wa kutosha kuwasafirisha wakimbizi kwa kuwapa mahitaji yote muhimu vikiwamo vipimo vya afya kabla ya kuanza safari,” inasema taarifa IOM.

Katika ushirikiano huo, IOM imedai UNHCR inatakiwa kufanikisha usafiri wao kutoka kambi za Nyarugusu na Mtendeli mpaka ile ya Nduta ambayo ni kituo cha kuondokea nchini. Mikoa 10 imeandaliwa nchini humo kuwapokea wakimbizi wanaorudi, mikoa hiyo ni Ruyigi, Muyinga, Makamba, Kirundo, Rutana, Cankuzo, Karuzi, Bujumbura, Rumonge na Ngozi.

Kibadeni Awapa Neno Wachezaji Asema Wakiliheshimu Soka Litawaheshimu Uzeeni

$
0
0
Kibadeni Awapa Neno Wachezaji Asema Wakiliheshimu Soka Litawaheshimu Uzeeni
Kocha wa zamani wa Simba, Abdallah Kibadeni amewashauri wachezaji wanaocheza Ligi Kuu Bara kuuheshimu kazi yao itawaheshimu watakapokuwa wazee kama yeye.

Amejitolea mfano yeye mwenyewe kuwa alitenga muda wa kuutumikia mchezo huo ndiyo maana unampa heshima mpaka leo kuendelea kula matunda ya kazi hiyo licha ya kwamba hachezi.

"Kila mchezaji akijiuliza kwa nini baadhi ya majina ya wakongwe ndiyo yangang'ara mpaka sasa, watataka kufahamu kwamba walifanya nini, hilo litawasaidia kujituma kwa bidii ili na wao waje kupata heshima hiyo," alisema.

Amewageukia wale ambao wanacheza Simba na Yanga kwamba kuvaa jezi tu inawapa hatua ya jamii kuwajua wapo wapi, huku akiwasisitiza jambo la pili kuwa wazitendee haki ya kuonyesha uwezo uwanjani.

"Klabu hizo zinahitaji watu wenye uwezo wa juu na siyo mladi unavaa jezi zao bila uwezo, wajitume itasaidia hata timu ya Taifa Stars, kuwa kwenye kiwango cha juu," alisema Kibadeni.

Niki wa Pili Afunguka Juu ya Maisha Aliyopitia

$
0
0
Niki wa Pili Afunguka Juu ya Maisha Aliyopitia
Msanii Nikki wa Pili amesema maisha ambayo ameyapitia akiwa bado mdogo, ndio sababu inayomfanya azidi kufanya makubwa kwenye maisha yake.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Nikki wa Pili amesema alipitia changamoto nyingi ikiwemo kuuza sambusa kwenye vilabu vya pombe akiwa na baba yake, akiwa na umri mdogo kabisa.
“Nilikuwa nauza sambusa kwenye vilabu vya gongo na baba, kila siku nilikuwa nazunguka na sambusa zangu, nimefanya hivyo tangu nipo darasa la 3 mpaka namaliza la 7, lakini ndio hustle zilizotufanya tufanye makubwa zaidi”, amesema Niki wa Pili.
Niki wa pili ambaye hivi karibuni ameachia wimbo wake mpya wa Kihasara, ni miongoni mwa wasanii wachache sana hapa bongo ambao wana elimu na upeo mkubwa wa kufikiri mambo, licha ya maisha duni aliyopitia.

Makamo wa Rais Afungua Mkutano wa Majaji Dar

$
0
0
Makamo wa Rais Afungua Mkutano wa Majaji Dar
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu leo amefungua mkutano Mkuu wa Mwaka wa chama cha majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola katika ukumbi wa mikutano wa Benki Kuu (BoT) jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo umezinduliwa leo Septemba 25, 2017 ambapo utafanyika kwa siku tatu ukiwa na kauli mbiu isemayo “Mahakama Madhubuti inayowajibika na Jumuishi”, pia kutakuwa na mada mbalimbali kutoka kwa viongozi ambao ni Majaji na mahakimu.
Makamu wa Rais amewakaribisha wageni wote na kuwasihi wawe huru kuendelea na serikali iko pamoja nao katika muda wote wa mkutano huo.
Akizungumza mara baada ya kufunguliwa kwa mkutano, Mwenyekiti wa Chama cha Mawakili Tanzania, Ignas Hatusi amesema kuwa Mkutano huo una lengo la kujenga Mahakama shirikishi, Mahakama inayowajibika na Mahakama Dhabiti kiutendaji kwa kuimarisha utendaji wa taasisi za kimahakama.
Mkutano huo umehudhuriwa na washiriki wapatao 354 wakiwemo 13 ambao ni Marais na Majaji kutoka Austaria, Zambia, Afrika Mashariki na Pakistani

Mad Ice Ashangazwa na Uwepo wa Harmorapa Katika Muziki

$
0
0
Mad Ice Ashangazwa na Uwepo wa Harmorapa Katika Muziki
Msanii wa muziki Bongo, Mad Ice ameelezwa kushangazwa na uwepo wa Harmorapa katika muziki na kujulikana kama msanii wakati hana uwezo huo.

Mad Ice Ashanzwa na Uwepo wa Harmorapa Katika MuzikiMuimbaji huyo ambaye anaishi nchini Finland ameiambia Planet Bongo ya EA Radio kuwa Harmorapa anafaa katika uchekeshaji na siyo muziki na kitendo cha vyombo vya habari kuendelea kumsapoti ni kuua sanaa.

“Nimemsikia huyu Harmorapa, hapo ndipo nimekuja nimesikitika kabisa, unajua tunaharibu sanaa yetu sisi wenyewe kuna wasanii ambao wanahitaji kupewa fursa, wasanii tunajituma lakini sometime media zinatuangusha,” amesema Mad Ice.

“Nimemuana ila naona ni mtu kama ni mchekeshaji lakini ninapoona unamlinganisha na msanii kama Grace au Vanessa nitaona kuna kitu kinakusumbua kichwani,” ameongeza.

Katika hatua nyingine Mad Ice amewataja Vanessa Mdee, Grace Matata na Lameck Ditto kuwa ni wasanii ambao wanatakiwa kutazamwa kama mfano kwani wanafanya muziki mzuri.


Watumishi Mkoani Geita Wakamatwa kwa Kuiba Dawa za Serikali

$
0
0
Watumishi Mkoani Geita Wakamatwa kwa Kuiba Dawa za Serikali
WATUMISHI wawili wa zahanati ya Kata ya Kakubilo wilaya na mkoa wa Geita wamekamatwa na wananchi wakidaiwa kuiba dawa  za  serikali na vifaa tiba na kuficha kwenye makazi yao kwa lengo la kupelewka kwenye maduka binafsi ya dawa.

Mkuu wa Wilaya ya Geita,  Herman  Kapufi, akithibitisha kukamatwa  kwa  watumishi wa sekta ya afya wa zahanati hiyo, aliwataja kwa majina kuwa ni Peter Matono, mtunza  stoo ya dawa na mhudumu Enock Ngidangida na kusema walikamatwa na wananchi wakiwa wameficha dawa na vifaa tiba zenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni saba kwenye makazi yao.

Kapufi alisema kuwa serikali haitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria madaktari na wahudumu wa afya watakaobainika kujihusisha na tabia hiyo.

Alisema watuhumiwa hao kwa sasa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani hapa.

Rais Magufuli Amariza Ziara Yake Mkoani Arusha Arejea Dar

$
0
0
Rais Magufuli Amariza Ziara Yake Mkoani Arusha Arejea Dar
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewasili jijini Dar es salaam mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku sita mkoani Arusha.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda pamoja na viongozi wengine wa Mkoa wa Dar es Salaam mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam wakati akitokea Mkoani Arusha.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam wakati akitokea Mkoani Arusha.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda pamoja na viongozi wengine mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam wakati akitokea Mkoani Arusha.

Mwanamume Aliyekuwa Ameficha Kilo Moja ya Dhahabu Kwenye Utumbo Wake Akamatwa Sri Lanka

$
0
0
Mwanamume Aliyekuwa Ameficha Kilo Moja ya Dhahabu Kwenye Utumbo Wake Akamatwa Sri Lanka
Mamlaka nchini Sri Lanka zimemkamata mwanamume ambaye alijaribu kusafirisha dhahabu na vito vya karibu kilo moja, alivyokwa ameficha kwenye utumbo.
Maafisa wa forodha walipata gramu 904 za dhahabu yenye thamani ya dola 29,370 ndani ya utumbo wake.
Choo kilichotengezwa kwa dhahabu kutumika na umma
Mwanamume huyo raia wa Sri Lanka mwenye umri wa miaka 45, alikuwa safarini kwenda nchini India, lakini akasimamishwa kwenye uwanja wa kimataifa wa Colombo.
Kumekuwa na visa kama hivyo miaka ya hivi karibuni.
Watu hununua dhahabu maeneo kama Dubai na Singapore ambapo bei ni ya chini na kisha kuisafirisha hadi India ambapo bei yake ni ya juu.
Majambazi waiba dhahabu ya kilo 70
Maafisa wa forodha waliiambia BBC kuwa walimshuku mwanamume huyo kwa sababu alikuwa akiotembea kwa njia isiyo ya kawaida.
Vifaa vya kutambua chuma kisha vinatambua mkoba uliokuwa umefungwa mfuko wa plastiki na kufichwa ndani ya utumbo.
Aliyefunga kilo 25 za dhahabu kwenye mapaja akamatwa uwanja wa ndege
Wiki iliyopita mwanamke mmoja raia wa Sri Lanka alipatwa na maafisa wa forodha akiwa ameficha gramu 314.5 za dhahabu kwenye utumbo wake.
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images