Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

"Baby Kama Huwezi Kuja Kunichukua Nakuja na Tax, Utalipa, Kama Huwezi Basi Mie Siwezi Panda Dala Dala'"

$
0
0


Mdada wa mjini Akichat na Boyfriend wake:

'Baby,kama huwezi kuja kunichukua nakuja na taxi utalipa,kama hutaki basi,mi siwezi kupanda Daladala Iam a DIVA''
''Okay Baby,gari haina mafuta na sina hela ya taxi,kama huwezi kupanda daladala basi,I am a DIVA''
Hivi kuwa Diva ndo hupandi Daladala??

Babako mwenyewe anafanya Shirika la Reli anagombania gari za Tandika deile,  Eti we mwanawe Diva, Diva my beuatiful legs!

Wanaume Tuache Ubahili Tuwatunze Wapenzi Wetu

$
0
0
Kwanza nianze kwa kukili kua maisha ni magumu sana nadhani kila mtu anajua.

Na katika mahusiano ya mapenzi kati ya me na ke lazima kunakua na tofauti ya kipato, yaani Mara nyingi wanaume wanakua na hali mzur kimapato kuliko mwanamke.

Nieleweke vizur kua si maanishi kua wanawake wote wanakipato duni LA hasha.

Ningependa kuwashauri wale wenye wapenzi WA kike mambo haya yafuatayo:-

1. Ujue tofauti ya kuchunwa na kuhudumia unapokua na mpenzi ujue ni jukumu lako kumpendezesha anapopendeza watu watajua we ndio kidume uliemwezesha.

2 .Sio mpaka akuombe ndio umpe. jaribu kumfaam hali ya maisha na kipato chake ujue kukisia cha kumpa kwa matumizi yake.

3.Usiulize ya nini,ikitokea mpz amekuomba HELA usiulize ya nn ye ni MTU mzima awezi kukuomba HELA akaenda kuchambia.

4. Kutumia pesa nyingi sehemu ya starehe.
Kuna watu wanaenda mpaka hotel ya nyota 5 kustarehe akitumia zaidi ya laki tano.cha ajabu baada ya kutoka hotel anamwacha mpz wake 10000 ya nauli.
Huu ni ujinga bora ungeenda ata lodge ya nafuu ye ukamwacha na HELA ya kutosha.

5.Tenga ata 10% ya mshahara MPE yeye aangalie kama kuna kitu cha kurekebisha arekebishe.

NB.
APA ni kwa wale Wanaume wanaowazidi kipato wanawake wao sio wanawake wenye vipato vizur.

Tusiwe wataalamu wakutafuta Gspot wakati ukiombwa ata 1000 unanuna mapenzi ni pamoja na kupunguzia makali ya maisha.

Yeyote mwenye chochote anaweza kuongezea apo.

Amuua Ndugu yake wa Damu Kisa Makalio Makubwa ya Mwanamke

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaizidizi Jonathan Shanna Warioba, ametoa onyo kali kwa wananchi wenye tabia za udhalilishaji kwa wanawake kuacha tabia hiyo mara moja huku akisema kwamba udhalilishaji umesababisha kifo.

Kamanda Shanna amelazimika kusema hayo  hayo wakati akizungumza na kituo hiki akitolea ufafanuzi juu ya tukio la mauaji ya mkazi wa Kijiji  cha Vilabwa Wilaya ya Kisarawe Imma Habibu ( 26).

Kwa mujibu wa Shanna Marehemu aliuwawa juzi majira ya saa mbili asubuhi wakati walipokuwa kijiweni na wenzake baada ya kutokea ugomvi kati yake na Ramadhani Habibu (23) ambaye ni ndugu yake, baada ya mwanamke mmoja ambaye anadaiwa kuwa maumbile makubwa (makalio) kupita, mbele yao.

Alisema baada ya mwanamke huyo kupita mbele yao walianza mabishano ambapo marehemu alisema mwanamke huyo ana makalio makubwa na Ramadhani alisema ni makalio ya kawaida na makubwa.

Kamanda Shanna alieleza kuwa baada ya mabishano hayo ndipo ulipozuka ugomvi hadi kufikia hatua ya Ramadhani kumuua kaka yake kwa kumchoma kisu kifuani upande wa kuliana na alifariki dunia akiwa njiani anapelekwa hosptali ya kisarawe.

Alisema jeshi la polisi linamshikilia mtuhumiwa kwa kufanya mauaji hayo na kuwa atafikishwa mahakamani mara moja  na kuwa amekubali kuwa amefanya mauaji hayo.

Kufuatia,tukio hilo kamanda Shanna aliendelea kutoa onyo kwa wananchi na  vijana wanaoshinda vijiweni kuacha tabia ya udhalilishaji hasa kwa wanawake na kuwa ni kufanya hivyo ni kosa kisheria na kuwa kama kuna mtu aliyefanyiwa vitendo vya namna hiyo atoe taarifa polisi na atafikishwa mahakamani.

"Wito kwa wale wanaokiuka haki za binadamu kwa kumdhalilisha mtu waache mara moja, mfano kisheria hata kumkonyeza mtu ni kosa la jinai hivyo unapaswa kufika polisi, na tutamfuatilia kisha kumpeleka mahakamani" Kamanda Shana amefafanua

Pia kamanda Shanna ametoa rai kwa wanawake kuvaa nguo zinazositiri maungo yao ili kuepusha vishawishi na matamanio kwa wanaume

Rose Ree Kajibu Kuhusu Wanao Sema Muonekano Wake

$
0
0
Rapa wa kike kutokea The Industry, Rosa Ree ni miongoni mwa mastaa waliotoa burudani ya nguvu kwenye jukwaa la FIESTA 2017 Mwanza ambapo baada ya show, Ayo TV ilimnasa kupiga naye story na kufunguka alipoulizwa kuhusu wanaouzungumzia muonekano wake.

VIDEO:

Hii Hapa Video ya Kijana Aliyejirusha Ghorofani Kama Mchezo Lakini Akaumia Vibaya na Kufariki Dunia

$
0
0
Ruzo Boniface Amlima amefariki dunia baada ya kujirusha toka ghorofa ya 13 wakati akizindua mchezo wa kujirusha toka ghorofani.

Huu ni mchezo mpya hapa Tanzania na aliyefariki ndiye kiongozi muasisi wa mchezo huo.

Na kwa waliobahatika kuona kwenye tv hakukuwa na maandalizi yoyote Yale, yaani ni kama jamaa aliamua kujiua mwenyewe, nimeshangaa Sana.

Angalia VIDEO:

Kutana na Mtabibu wa Asili Allan Shariffu Musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH shariffu musa Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na shariffu musa Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Maalim Hussein Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 629793352 au watsap
+255 679119679

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Ile Gari Aina ya RAV 4 Aliyopewa Hamisa Mobeto na Diamond Platnumz Yaibua Zengwe

$
0
0
BADO mrembo aliyezaa na Mbongo Fleva, Hamisa Mobeto ameendelea kutengeneza vichwa vya habari, safari hii, gari lake aina ya Toyota Rav 4 alilopewa na msanii huyo, linadaiwa kuibua zengwe kwa kile kinachoelezwa kuwa ilikuwa msanii huyo ampe mama’ke, akabadilisha maamuzi ghafla na kumpa Mobeto.

TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo cha kuaminika kilicho karibu na familia ya Mobeto kimenyetisha kuwa, msanii huyo aliagiza gari hilo lenye thamani ya shilingi milioni ishirini na tano kabla ya Mobeto kujifungua na ilikuwa amzawadie mama yake mzazi. “Yule msanii alikuwa anataka kumpa ile Rav 4 mama yake sasa ilipotua nchini ndiyo wakati ambao Mobeto alikuwa amejifungua kwa hiyo akaona bora ampe mzazi mwenziye huyo mpya kwanza halafu mama yake akaahidi kumuagizia gari lingine. “Sasa nasikia mama wa msanii hakufurahishwa na kitendo hicho.
Kidogo alimaindi kwani tayari yeye alishajiandaa ku-drive mkoko mpya. Akabaki anaumia na moyo wake,” kilisema chanzo hicho na kuongeza: “Hata pale mama wa msanii huyo alipoenda hospitali kumuona mjukuu wake kwa mara ya kwanza, alikuwa hana furaha sana lakini ndiyo hivyo, atafanyaje sasa wakati aliambiwa amuwakilishe mwanaye ambaye alikuwa nje kikazi.”

MAMA MOBETO AFUNGUKA
Mama’ke Mobeto, Shufaa Lutigunga alipotakiwa kuzungumzia zengwe hilo, aliomba aachwe kwani kwa sasa mambo mengi sana yamezungumzwa kuhusu yeye na mwanaye ambayo yamesababisha usumbufu mkubwa. “Jamani wenzenu sasa hivi mambo yamekuwa mengi sana kuhusu mimi na mwanangu. Ngoja tupumzike kidogo jamani,” aliomba aachwe mama Mobeto. Alipotafutwa Mobeto na mama wa msanii, simu zao ziliita bila kupokelewa hadi tunakwenda mitamboni. Hivi karibuni, msanii aliyezaa na Mobeto, alifunguka mambo mengi redioni kuhusiana na uhusiano wake na mrembo huyo likiwemo suala la kumnunulia gari hiyo ya Rav 4.
Kama hiyo haitoshi, alisema aliteketeza fedha nyingi kulea tumbo kwa kumpa shilingi elfu 70 kila siku, baadaye akampa hela ya kujifungua shilingi milioni saba kisha alipojifungua, akampa shilingi laki tano. Hata hivyo, baada ya kujifungua, msanii huyo alisema Mobeto alikuwa na tamaa ya kuomba apewe shilingi milioni laki tano kila wiki hali iliyomfanya msanii huyo azungumze na mwanasheria wake ambapo mwisho wa siku walikubaliana ampe shilingi laki mbili kila wiki.

Mbunge Lijualikali Ashikiliwa Polisi

$
0
0
Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali na viongozi watatu wa Chadema wilayani Malinyi wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kufanya kusanyiko lisilo halali.

Mbunge huyo amekamatwa leo Alhamisi saa 12:40 jioni akitoka kwenye kikao cha ndani cha chama hicho kilichofanyika katika Kijiji cha Makerere wilayani Malinyi.

Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati, Alfonce Mbassa amesema baada ya kumaliza kikao, mbunge huyo na viongozi wengine walipanda kwenye magari ili  kuondoka lakini ghafla lilitokea gari la polisi na askari walimuamuru Lijualikali ashuke.

"Tulishuka wote kujua tatizo ni nini lakini askari walimhoji Lijualikali kwa nini amekwenda kufanya siasa Malinyi wakati yeye ni mbunge wa Kilombero," amesema Mbassa.

Amesema walijaribu kuwaelewesha polisi kwamba kilikuwa ni kikao cha ndani lakini askari walisisitiza kuwa lilikuwa kusanyiko lisilo halali.

Amewataja waliokamatwa pamoja na mbunge huyo kuwa ni Mwenyekiti wa Chadema Malinyi, Emmanuel Lukindo; Katibu wake, Sadi Lyampawe na Katibu wa Uenezi wa wilaya, Lucas Lyambalimu.

"Lakini tulivyowabana polisi wametuambia wameelekezwa na Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Majura Kasika kuwakamata," amesema Mbassa.

Alipotakiwa kuzungumzia tuhuma hizo, mkuu wa wilaya Kasika amesema ni kweli ameagiza polisi kumkamata mbunge huyo kwa kuwa anafanya siasa nje ya jimbo lake.

"Ndiyo, nimetoa maelekezo akamatwe maana hakuna mbunge anayeruhusiwa kufanya siasa nje ya jimbo lake na tunaendelea kumshikilia kwa mahojiano," amesema Kasika.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leons Rwegasira amesema hajapata taarifa za kukamatwa kwa mbunge huyo.

"Nipe muda nifuatilie nitakujulisha maana bado sijapata taarifa za kukamatwa kwa mbunge huyo," amesema Rwegasira.

 

Meya Ubungo Akomaa na Makonda

$
0
0
Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob ameapa kuendelea kupambana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ili kuhakikisha mashtaka aliyoyafikisha Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma dhidi ya kiongozi huyo wa mkoa yanafanyiwa kazi na kusisitiza kuwa hayuko tayari kuyafuta.

Jana, Meya Jacob alifika kwenye ofisi hiyo ya Sekretarieti katika kile alichosema kuwa ni kuitika wito kuhusiana na suala lake alilofikisha hapo.

“Nitaeleza kwa kifupi tu kile tulichojadiliana huko juu na Sekretarieti,” alisema Meya Jacob baada ya kushuka kutoka ghorofa ya nne ya Jengo la Sukari zilipo ofisi hizi na kukutana na waandishi wa habari waliokuwa wakimsubiri.

Meya huyo ambaye mahojiano yake na Sekretarieti yalidumu kwa takriban saa nne, alidai kwamba amekuwa akiombwa kufuta shauri hilo na mara kadhaa.

Alidai kwamba watendaji wa Sekretarieti walimwarifu kuhusu ombi la mkuu wa mkoa kukutana naye kwa ajili ya kushauriana jinsi ya kulimaliza shauri lake.

Hata hivyo, hakuna ofisa wa Sekretarieti aliyekuwa tayari kuzungumzia mahojiano na meya huyo wakisema msemaji ni Kamishna Honoratus Seleke ambaye ilielezwa kuwa yuko Dodoma.

Meya huyo amemshtaki Makonda kwenye tume hiyo akidai kwamba ameghushi vyeti jambo ambalo ni kinyume cha maadili ya utumishi wa umma.

“Mkuu wa mkoa ametumia jina lisilo lake na amekula kiapo kwa kutumia jina ambalo pia siyo lake mambo ambayo kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 398 ni kosa na ndiyo maana nimeiomba Sekretarieti isimamie sheria wala isiangalie jambo lingine,” alisema : “Lakini sasa nasikia serikali ya mkoa wanataka tumalizane… mimi nasema hili haliwezekani lazima lifikishwe mwisho wake.

“Najua baraza hili halina mamlaka ya kumwajibisha mkuu wa mkoa litakachofanya ni kutoa ushauri tu, mtu mwenye mamlaka ya kufanya hivyo ni Rais lakini itakuwa jambo la heri iwapo tukajulishwa ukweli kwamba tunafanya kazi na Daudi Albert Bashite au la… sisi tukijua hilo hatutakuwa na kinyongo tutaendelea kumpa ushirikiano” alisema.

Aliitaka sekretarieti hiyo kutembea katika kweli ili uamuzi wake uendelee kuweka kumbukumbu itakayoheshimika daima.

“Sekretarieti iamue moja, ifanye maamuzi yatayoifanya iheshimike milele au itoe uamuzi utakaofanya idharaulike milele,” alisema.

Mwananchi

Mama Mwenye Nyumba Anataka Kuniozesha Mwanae Kinguvu Nguvu

$
0
0
Husika na kichwa cha habari hapo juu,

Mimi ni mpangaji nimepanga nyumba moja hapa mjini na nina kama miezi sita kwenye hii nyumba niliyopanga ambayo mpangaji ni mimi mwenyewe mama mwenye nyumba ni mjane yaani single mother na ana watoto watatu wote wa kike.

Kinachonisukuma kuomba ushauri hapa ni nyenendo za huyu mama na binti yake mmoja yule wa pili, yaani huyu mama anaforce mwanae nimuoe yaani niishi nae gheto kwangu niwe nalala naye na kuamka naye.

Kila chakula kikiiva naletewa nguo nafuliwa na hadi maji bafuni napelekewa na wanafanya yote haya si kwamba mimi nataka hapana ni kwa lazima, yaani chakula unaletewa ki nguvu nguvu kama ni wali unakuwa hadi ushamwagiliziwa maharage na mchuzi sasa kwa mazingira haya ni vigumu sana kukataa.

Jana binti kaja usiku kuniletea msosi na hakurudi tena ndani kwao akabaki hadi asubuhi, mimi leo nimeondoka kwenda kazini nimemuacha gheto nimerudi nimekuta kapika chakula chetu wawili tofauti na chao kile cha kwa mama yake.

Sasa kwa staili hii ya kuja gheto Jana usiku na leo nimemkuta kapika si tiari nishakabiziwa mzigo hivi.

Ushauri wenu nifanyaje? Nihame hii nyumba au nifanye nin?


LONDON BABY

Mrembo wa Picha za Utupu Agness Amtolea nje Duma..Adai zile Voice Note ni Utani

$
0
0
Mrembo Agness amemkana muigizaji wa ‘Siri ya Mtungi’ Duma kwa kudai hawana mahusiano ya kimapenzi na bali  ni marafiki.

Akiongea na Bongo5, mrembo huyo amedai kuwa wao ni marafiki  wakaribu na ila ni mwanaume mwenye vigezo vya kuwa naye.

“Am not sio wapenzi ni marafiki tu wakawaida na zile voice notes ni mimi kweli ila ilikuwa utani,” amesema mrembo huyo amabye amekuwa akiweka picha zake za utupu katika mtandao wa Instagram.

Pia akaongeza kuwa Duma ni mwanaume hivyo anaweza akawa  naye katika mahusiano ya kimapenzi.

Mke wa Jose Chameleone Ashuhudia Mmewe Akitandikwa Mabanzi na P-Funk Majani Kampala

$
0
0
Kwa wale wanaofuatilia mziki wa bongo fleva, na wa afrika mashariki kwa ujumla matumaini yangu ni kwamba mnamjua mtayarishaji wa beats maarufu kwa jina p-majani kinywele kimoja,

Mwaka 2005 na 2006 alitayarisha mlio wa mziki ambao ulitumika kwa wimbo wa mwanamziki nguli Joseph Haule maarufu kwa jina Professor J, wimbo kwa jina unaitwa nikusaidieje,

Jose chameleone kwa ujanja ujanja akasema akaiba beat ile na kutumia kwenye mziki wake wa bombo crat, ambayo ilifanya vyema nchini uganda,

Baada ya mwenye mali kugundua kuwa kaibiwa, akawasiliana na chameleone. na majibu ya chameleone ikawa kama anaomba msamaha fulani hivi na akaahidi kulipa dola za kimarekani 2400, miaka ikakatika miwili bila kulipa , majani akakaa kimya kwa kujua kwamba basi ngoja asamehe,

Mwaka 2008 nchini kenya kulikuwapo na programu ya kutumia miito ya simu ya ala zinazoendana na beats au milio ya mziki iliyotengenezwa na wasanii mbali mbali au watayarishaji , MTN ilishirikiana na kampuni ya nje ya uganda waka lounge hiyo program kenya, ule mwito wa beat ya nikusaidieje ukatumika kwenye ring tone , na wakalipa dollar 12,000 Jose akaenda akiwahi akachukua hiyo hela, jambo ambalo limemkwaza sana bwana p-funk akamtext chameleone akakaa kimya

Hatua alizochukua majani ni kwenda KOSOTA, wakamzungusha akaenda uganda kudai kwenye chama cha wanamziki na utayarishaji wa filamu, wakamzungusha saana, akaamua kuachana nayo,

Mwaka huu 2017 march marekani kuna watayarishaji wa filamu , katikla filamu moja wakaomba kutumia beat ya P-funk majani ya nikusaidieje lakin wakataka kwanza wawasiliane na muhusika wa mziki, confusion ikaja pale nani wamuone either Chameleon wa bombocrat, au Profesa J wa nikusaidieje,

Baada ya chameleone kujua kuna dili ilo akapanda ndege akaenda USA, akakutana nao wakasaini mkataba wa maisha atalipwa milele kutokana na mauzo ya filamu ile na wakampa advance 50,000 USD, kama advance payment, Yaan milion 120 za Tanzania

Mbabe Majani baada ya kujua hayo akaenda direct kampala kupata go ahead , akapata vibali vyote akaenda USA kushitaki ,taratibu ziko za kisheria ambazo kafuata, kaambiwa kuwa concert mawakili mpaka kwanza awe na USD 20,000 ili kesi yake kusimamiwa,

Chameleone alivyosikia hayo akampigia majani akasema nataka nikuwekee ile dolla 2000 tuliyokubaliana mwanzo ili tusifike mbali, majani akasema nitakutafta,

Wiki hii wamekutana kampala , akamkabidhi kwanza vibao vya kutosha mke akataka kuingilia kati majani akamshika nywele naye mke akaponyoka akakimbia,
si mara ya kwanza kwa chameleone kuwatapeli watu ni tabia yake na ana conflict na ndugu zake na wasanii wa uganda


Kesi ya madai majani kafanikiwa kuifungua marekani na wanaendelea na utaratibu

Uzuri wamekubali kumlipa hao wa hollywood watayarishaji wa movie, na wamesema kumwendea jose chameleone kurefund hela yao na kuchange mkataba

malalamiko ya majani p funk NA VIDEO ILIYOTUMIA MZIKI HUO CHINI IPO NI 1.52 MINUTES WHATCH IT VIDEO:

Hiki Hapa Kisa cha Mbowe Kunyang'anywa Gari Bunge Lafafanua

$
0
0
Hiki Hapa Kisa cha Mbowe Kunyang'anywa Gari Bunge Lafafanua
OFISI ya Bunge imesema Kiongozi wa Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe hajanyang’anywa gari.

Taarifa iliyotolewa na Bunge leo Alhamisi imesema kilichotokea ni kwamba, gari hilo limerudishwa nchini ili dereva afuate utaratibu wa kupata kibali cha kusafiri nje ya nchi.
Mbowe yuko Nairobi nchini Kenya ambako Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu anaendelea na matibabu baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 akiwa nyumbani kwake Area D mjini Dodoma.

Bunge limesema ni kweli gari lenye namba ya usajili STL 4587 aina ya Toyota Prado limetengwa maalumu kwa ajili ya kumuhudumia Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika kutekeleza majukumu yake ya kikazi na binafsi nchini.

“Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni aliomba gari ikamhudumie mjini Nairobi nchini Kenya na Ofisi ya Bunge iliridhia ombi hilo na kuomba taratibu zizingatiwe. Hata hivyo, ofisi iligundua kwamba gari ilikwenda Nairobi na dereva hakupata kibali cha kusafiri nje ya nchi ambacho kila mtumishi wa umma anayesafiri nje ya nchi lazima apate kibali hicho kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi,” imesema taarifa ya Bunge.

Bunge katika taarifa hiyo limesema kwa kuwa utaratibu haukukamilika, dereva aliambiwa alirejeshe gari hilo nchini na kuliegesha katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha hadi utaratibu mwingine utakapokamilika.

“Dereva yupo Dodoma anakamilisha taratibu ili ofisi iweze kumuombea kibali Ikulu ndipo anaweza kurejea nchini Kenya kwa ajili ya kuendelea kumhudumia Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,” imesema taarifa.

Ofisi ya Bunge imesema inasikitishwa kutokana na utaratibu unaotumiwa na Ofisi ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni wa kuzungumzia masuala yanayohusu ofisi hiyo kupitia kwa msemaji wa chama kama inavyoonekana kwenye mitandao ya kijamii akitoa malalamiko kwa niaba ya ofisi hiyo.

“Ni vyema ikaeleweka kwamba Ofisi ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ni kama ofisi nyingine zinazohudumiwa na Sekretarieti ya Bunge ambayo inapaswa kufuata kanuni na taratibu za uendeshaji wa Ofisi na ni kosa kwa mtumishi kwenda kinyume na masharti ya Utumishi wa Umma,” taarifa hiyo imesema.

Imeelezwa katika taarifa kuwa ni dhamira ya Ofisi ya Bunge kuendelea kumhudumia Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa kufuata misingi na kanuni za utumishi wa umma na zile za Bunge bila kuchanganya na siasa.

“Ofisi ya Bunge inauhakikishia umma kuwa taratibu zikishakamilika Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ataendelea kuhudumiwa popote atakapokuwa,” imesema taarifa hiyo.

Ommy Dimpozi Apigwa Stop Kuzungumzia Post Ile ya Mama Diamond

$
0
0
Ommy Dimpozi Apigwa Stop Kuzungumzia Post Ile ya Mama Diamond
Msanii wa muziki Bongo, Ommy Dimpoz amesema hawezi  kuzungumzia ishu ya post ya mama mzazi wa Diamond katika ukurasa wake wa Instagram.

Muimbaji huyo amesema kufanya hivyo ni kuamsha hisia upya kwa mambo ambayo yalishapita na hata menejimenti yake imemkataza kuzungumzia suala hilo.

Katika exclusive interview na Bongo5 Ommy Dimpoz amesema asingependa kuzungumzia hayo lakini kikubwa anachoweza kusema ni kwamba mavuguvugu lazima yawepo kwani ndio kuchangamka kwa muziki na ukizingatia Bongo Flava siyo kama kwaya.

“Hayo mengine yanayotokea is just a game lakini siyo vitu vya kushikana mashati au kumwagiana tindikali, hatujafikia huko ila ukiangalia industry zote duniani hayo mambo yapo na vinachagia wanamuziki kuumiza vichwa zaidi,” amesema Dimpoz.

“Tukiongea tunakuwa tunarudisha hayo mambo tena nyuma, mimi mwenyewe sasa hivi hata menejimenti imesema bwana hayo mambo husizungumzie tena.  Hayo mambo tukizungumza tutaamsha hisia, inakuwa haijakaa sawa, nafikiri yaliyopita yamepita,” ameongeza.

Ommy Dimpoz ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Cheche’ aliingia katika vita kali ya maneno mtandaoni mara baada ya kuposti picha akiwa na mama mazazi wa Diamond na kuweka maelezo ambayo yalileta utata mkubwa na kukosolewa vikali, hata hivyo posti hiyo ilikuja kufutwa baada ya muda.

Wadau wa Habari Watoa ya Moyoni Waitupia Lawama Serikali

$
0
0
Wadau wa Habari Watoa ya Moyoni Waitupia Lawama Serikali
Wadau wa habari wamesema taasisi za kiraia, asasi na vyombo vya habari vinaogopa kutoa taarifa zinazoikosoa Serikali kwa kuhofia usalama na vitisho wanavyotoka kwenye mamlaka.

Mtafiti Mwandamizi wa Shirika la Twaweza, Annastazia Rugaba alizitaka taasisi na wadau wote wa utoaji taarifa kutoogopa vitisho, akitolea mfano wa vitisho walivyowahi kukutana navyo katika utoaji wa takwimu.

Kauli hiyo iliibuliwa jana kupitia maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Upatikanaji Taarifa, yaliyokuwa yameandaliwa na Wadau wa Haki ya Kupata Taarifa (CoRI) jijini Dar es Salaam. Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni uamuzi wa Serikali kujiondoa katika Mpango wa Utendaji Kazi wa Serikali kwa Uwazi (OGP), kufungiwa kwa magazeti likiwamo la Mwanahalisi huku wakihoji maslahi ya viongozi katika utekelezaji wa taarifa na ucheleweshwaji kanuni za Sheria ya Kupata Taarifa.

Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Amiri Manento ambaye alikuwa mgeni rasmi, alisema haki ya kupata taarifa inatakiwa kulindwa kwa nguvu zote na kwamba, kuminywa kwake kuna athari katika kuimarisha uwazi, uwajibikaji na utawala bora.

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo, Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda alisema mazingira ya Serikali kunyima uhuru wa mtoa taarifa ni matokeo ya kuendelea kuongozwa na chama na viongozi waliopo katika mfumo unaohitaji kuzuia maovu yanayofanyika. Kibanda alisema Taifa lilitoka gizani, lakini sasa linapitia kipindi kingine kigumu.

Mwandishi nguli wa habari, Jenerali Ulimwengu alisema wanahabari wanaogopa kuuliza maswali wakiogopa kukamatwa na kupewa vitisho huku wanasiasa wa upinzani wakizuiwa kufanya mikutano ya hadhara kuwapatia taarifa wananchi kwa maagizo ya ‘amri kutoka juu’.

“Tumeingia kipindi cha ‘kujingishwa’, yaani tumeendelea kufanywa wajinga, suala la makinikia, Escrow vimeishia wapi, lakini kwa nini kuzuia mikutano ya kisiasa, hakuna sheria inayozuia wanasiasa wasifanye siasa ni kazi yao kutoa taarifa kwa njia hiyo, viongozi wanaogopa kuulizwa maswali na waandishi,” alisema Ulimwengu.

Awali, Mwenyekiti wa CoRI, Kajubi Mukajanga alisema kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifai haijawahi kutokea uongozi uliowahi kukandamiza uhuru wa kupata habari kwa Watanzania.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) ambaye pia ni Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbasi hakuwa tayari kuzungumzia tuhuma hizo.


Upinzani Kenya Waitisha Maandamano Makubwa Wiki Ijayo

$
0
0
Upinzani Kenya Waitisha Maandamano Makubwa Wiki Ijayo
Muungano wa upinzani nchini Kenya umeitisha maandamano ya umma kupinga mapendekezo ya kuifanyia mabadiliko sheria ya uchaguzi.

Wabunge wanaoegemea upande wa serikali wanafanya hima kupitisha mswada ambao utamwezesha Uhuru Kenyatta kutangazwa rais bila ya kufanyika uchaguzi ikiwa upinzani utasusia marudio ya uchaguzi tarehe 26 mwezi Oktoba.

Wanachama wa upinzani walitoka nje wakati upande wa serikali ukitumia wingi wake bungeni kuharakisha mabadiko ambayo yatasababisha mswada huo kuwa sheria kabla ya marudio ya uchaguzi.

Kati ya yale yaliyo kwenye mswada huo ni kuruhusu mgombea kutangazwa rais bila ya kufanyika uchaguzi ikiwa mgombea mwingine atasusia uchaguzi.

Viongozi wa upinzani Kenya wazuiwa kwenye uwanja wa ndege Nairobi
Upinzani kuandamana Kenya
''Zaidi ya 100 walifariki'' katika maandamano Ethiopia
Marudio hayo ya uchaguzi yana wagombea wawili, Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga.
Mswada huo pia unasema kuwa mahakama ya juu haiwezi kufuta matokeo ikiwa mfumo wa eletroniki utafeli
Kufeli kwa mfumo wa kupiga kura kwa njia ya eletroniki ndio ilikuwa sababu kuu ya kufutwa kwa matokeo ya urais.

Mgombea wa Upinzani Raia Odinga amekashifu hatua hizo kama jaribio la kuiba kura na kumpendela rais Uhuru Kenyatta.
Ametisha maandamano ya kote nchini kila Jumatatu na Ijumaa kuanzia wiki ijayo.

Suti ya Maalim Seif Iliyozidi Kipimo Yaleta Gumzo Mitandaoni

$
0
0
Suti ya Maalim Seif Iliyozidi Kipimo Yaleta Gumzo Mitandaoni
SUTI ya Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, inayoonekana kuzidi kipimo cha kawaida, imezua mjadala katika mitandao ya kijamii.

Maalim Seif alivaa suti hiyo mwanzoni mwa wiki alipokwenda kumjulia hali Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, aliyelazwa hospitalini jijini Nairobi, Kenya.

Lissu amelazwa katika Hospitali ya Nairobi baada ya kupigwa risasi tano na watu wasiojulikana wakati akiwasili nyumbani kwake, Area D, mjini Dodoma Septemba 7, akitokea bungeni.

Katika picha aliyopiga kiongozi huyo akiwa pamoja na watu wengine, mke wa Lissu na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Maalim Seif alionekana amevaa suti yenye vipimo vikubwa tofauti na ilivyozoeleka, hali iliyozua gumzo katika mitandao ya kijamii.

Katika picha hiyo pia anaonekana aliyekuwa mgombea mwenza wa Urais wa Ukawa katika Uchaguzi Mkuu uliopita, Juma Duni Haji.

Katika picha hiyo, Maalim Seif alionekana pia ameshika fimbo, huku suti aliyovaa yenye rangi ya kijivu ikiwa imemzidi kwa ukubwa.

Picha hiyo ya Maalim Seif imekuwa kwenye mjadala katika makundi mbalimbali ya kijamii hasa ya mtandao wa WhatApp huku wengi wakijiuliza ni kitu gani kimemkumba kiongozi huyo mkubwa ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar.

Nipashe, lilifanya jitihada za kumtafuta Maalim Seif, ili aelezee undani wa suti aliyovaa, lakini simu yake haikupatikana.

Wananchi mbalimbali walitoa maoni yao kwenye mitandao pamoja na WhatsApp, Facebook na Instagram wakihoji ni fundi gani aliyemshonea suti hiyo Maalim Seif.

Moja ya mtu aliyechangia mjadala huo aliandika "Aliyemshonea hiyo suti Mungu anamuona!"

Wengine waliandika "uwiii hiyo ni suti ya karne", "hii suti haijapata kutokea jamani" na "mbona kubwa au fundi hakutaka kitambaa kibaki?"

"Fundi aliyeshona hii suti mwambieni anywe soda kwa hela yake," aliandika mchangiaji mwingine na wengine wakaandika "duuu huyu fundi Mungu anamwona kwa alichokifanya" na "hiyo fashion ya suti haijapata kutokea".

Tukio kama hilo la Maalim Seif, liliwahi kumtokea kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Steven Wasira baada ya koti alilovaa kufungwa vishikizo vilivyopishana mwaka 2015.

Wasira alifikwa na mkasa huo akiwa katika Sherehe za Utume zilizoandaliwa na Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA).
Wakati wa upigaji picha, alionekana vishikizo vya koti lake vikiwa vimepishana.

TID Atangaza Nia ya Kugombea Ubunge wa Kinondoni 2020 Je Atamng'oa Mtuli?

$
0
0
TID Atangaza Nia ya Kugombea Ubunge wa Kinondoni 2020 Je Atamng'oa Mtuli?
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Khalid Mohamed maarufu kama T.I.D, ametangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Kinondoni, kwenye uchaguzi ujao unaotarajiwa kufanyika mwaka 2020, na kumng'oa mbunge wa sasa wa jimbo hilo Maulid Mtulia.

Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, TID amesema sababu inayomsukuma kugombea nafasi hiyo ni kutokana na mbunge wa sasa kushindwa kulitimizia mahitaji yake jimbo hilo, hivyo atatumia nafasi hiyo kuhakikisha anamng'oa ifikapo 2020, kwa kuwa yeye anafahamu vizuri matatizo ya Kinondoni kutokana na kuwa mzawa wa mahali hapo.

Akiendelea kuzungumzia suala hilo, TID amesema iwapo atapewa dhamana ya kuliongoza jimbo hilo, atahakikisha anatatua matatizo yote yanayowakabili watu wa Kinondoni, likiwemo janga la madawa ya kulevya.

Muna Love Ndio Chanzo cha Bifu Kubwa la Young Dee , Janjaro- Sholo Mwamba

$
0
0
Muna Love Ndio Chanzo cha Bifu Kubwa la Young Dee , Janjaro- Sholo Mwamba
Msanii wa Singeli bongo Sholo Mwamba ametoa siri ambayo wengi walikuwa hawafahamu juu ya ugomvi wa Young Dee na Dogo Janja na kusema Muna love ndio chanzo cha bifu hilo kubwa kwa sasa.

Akizungumza kwenye eNewz ya East Africa Television, Sholo Mwamba amesema alishawahi kuwakuta wasanii hao na bosi wake 'Muna Love' wakijiachia na kueleza kwamba 'Madogo' hao wanagombania penzi la Muna love.
"Wahuni hawa nimeyasikia mazingira yao sema wanayumba kimazingira fulani, habari zao miyayusho, tena ving'asti tu wanajisahau, si wenyewe tunawakuta kwa bi mkubwa wamekaa miguu juu, mambo yao yametokea wanagombania mademu, baada wafanye muziki wao wanafelisha michongo, sababu zao wanagombania bi mkubwa wanafugwa fugwa tu na bi mkubwa", amesema Sholo Mwamba.
Sholo Mwamba ameendelea wa kusema kwamba pamoja na kwamba ameshagombana na bosi wake huyo lakini hakuweza kumuita Young Dee au Dogo Janja baba, kwani ni jambo ambalo halimuingii akilini.
"Mimi siwezi kumuita Dogo Janja baba, siwezi kumuita Young Dee baba, hata ukiangalia ugomvi wao sababu ni demu na demu mwenyewe ni bosi wangu", amesema Sholo Mwamba.
Young Dee na Dogo Janja sasa hivi wamekuwa paka na panya, huku wakitishiana usalama kila mmoja kwa kutaka kumpiga mwenzake akimuona.

Dimond, Hamisa Mobetto Wampost Wema Sepetu na Kumtakia Siku Yake ya Kuzaliwa

$
0
0
Dimond, Hamisa Mobetto Wampost Wema Sepetu na Kumtakia Siku Yake ya Kuzaliwa
Diamond Platnumz na Wema Sepetu bado ni maBest Friend na kila wakati hupeana ushirikiano kwenye mambo tofauti wanayofanya.

Jana ikiwa ni Birthday ta Wema Sepetu, Diamond Platnumz amempost akiwa na Idris Sultan na Kuandika “Happy birthday Madam….🎂”


Naye Mobetto akamua kufuata nyayo za mzazi mwenzake Diamondi na kumposti wema huku akisindikiza kwa ujumbe mzuri.

Mashabiki wa Hamisa Mobetto wamemsifia Model huyu baada ya Kumpost Wema Sepetu kwenye Birthday Yake jana.

Hamisa amepata Sifa hizi kutokana na Imani iliyojengeka hivi karibuni baada ya kupata mtoto wa Diamond Platnumz kuwa Urafiki wake na Ex wa Staa huyu ‘Wema Sepetu’ Umekufa.

Fahamu kuwa mahusiano ya Diamond na Wema Sepetu yalikuwa miongoni mwa mahusiano maarufu zaidi Afrika ya mastaa wawili.

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images