Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Yanga Kumkosa Tshishimbi Mechi ya Kesho

$
0
0
Yanga Kumkosa Tshishimbi Mechi ya Kesho
Klabu ya Yanga imeeleza kuwa imejiandaa vyema kuelekea mchezo wa ligi kuu ya soka Tanznaia Bara kesho dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Akiongea na Wanahabari leo kwenye makao makuu ya klabu msemaji wa Yanga, Dismass Ten amesema timu hiyo imejiandaa vya kutosha na inahitaji pointi tatu muhimu kwenye mchezo huo.
“Timu imejiandaa vizuri, sisi ni mabingwa watetezi kwahiyo tunahakikisha tunachukua pointi tatu muhimu na hatutadharau mechi”, amesema Ten.

Aidha kocha msaidizi wa timu hiyo Shadrack Nsajigwa amesema wachezaji wote wapo vizuri isipokuwa Amis Tambwe ambaye alikuwa majeruhi lakini tayari ameshapata kibali cha daktari na anaendelea vizuri na mazoezi.

Yanga ambayo ipo nafasi ya sita ikiwa na alama 8 itamkosa nyota wake wa Kimataifa kiungo Tshishimbi Kabamba ambaye anatumikia adhabu ya kukosa mechi moja baada ya kupata kadi 3 za njano katika mechi 3 zilizopita.

Mwanaume Aliyeshauriwa na Mganga Kufanya Mapenzi na Punda Atupwa Jela

$
0
0
Mwanaume Aliyeshauriwa na Mganga Kufanya Mapenzi na Punda Atupwa Jela
Mwanamme mmoja nchini Afrika Kusini aliyetambulika kwa jina la Ntando Mankungwini ametupwa jela mwaka mmoja baada ya kukutwa akifanya mapenzi na Punda.

Ntando (23) alikutwa usiku wa Jumatano ya septemba 20 mwaka huu kwenye zizi la nyumba jirani na nyumbani kwao mjini Mount Fletcher, Afrika Kusini akiwa nyuma ya punda usiku wa manane, kitendo ambacho wamiliki wa punda huyo walijua kuwa ni mwizi ila walikuja kustuka baada ya kumlika tochi na kumkuta akiwa utupu.

Wamiliki hao wa punda walimkamata na kumpeleka polisi na ndipo mtuhumiwa alikutwa na makosa ya unyanyasaji wa wanyama.

Mtuhumiwa akiwa Mahakamani alikiri kosa hilo la kufanya mapenzi na punda huyo huku akieleza kuwa alitekeleza sharti alilopewa na mganga wa kienyeji.

Ntando amesema alienda kwa Mganga wa Kienyeji kusaka dawa ya kuongeza nguvu za kiume na ukakamavu, ndipo aliposhauriwa kutembea na Punda.

Tayari mahakama ya mwanzo wilayani Mount Fletcher, Cape Town imetoa hukumu jana kwa kumfunga mwaka mmoja jela kwa kosa la unyanyasaji wa wanyama.

Uchaguzi wa Marudio Kenya Pasua Kichwa Matumaini Yafifia

$
0
0
Uchaguzi wa Marudio Kenya Pasua Kichwa Matumaini Yafifia
Matumaini ya kufanyika uchaguzi wa marudio kwa kura ya urais Oktoba 26 yamefifia baada ya jana wawakilishi wa vyama vya Jubilee na muungano wa Nasa kushindwa kukubaliana kuhusu masuala muhimu katika mazungumzo ya maandalizi.

Muungano wa Nasa ulipinga hatua ya Jubilee kushinikiza kupitishwa miswada yenye lengo la kufanyia marekebisho sheria za uchaguzi na ikatangaza mgomo mkubwa kila Jumatatu na Ijumaa kuanzia wiki ijayo katika kile ilichodai ni juhudi za “kuikomboa nchi kutoka Jubilee”.

Wakionekana kutoshangazwa na mgomo wa wapinzani, wabunge wa Jubilee bungeni walifupisha muda wa kuanza kutumika Sheria ya Uchaguzi (Marekabisho) za mwaka 2017 ambazo pamoja na mambo mengine, zinataka kupunguza mamlaka ya mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC), na kuwaadhibu wagombea watakaojitoa kushiriki uchaguzi wa marudio.

Pia mswada unapendekeza kuchukuliwa hatua kali kisheria dhidi ya maofisa watakaokataa kutia sahihi fomu 34A na 34B, ikiwamo kutumikia kifungo cha jela miaka 5. Mahakama imenyimwa mamlaka ya kubatilisha ushindi wa rais ukipendekeza kura zilizoko kwenye masanduku zihesabiwa upya, kando na sheria zingine.

Ilipendekezwa sheria hizo ziwe zimeiva na kuanza kutumika baada ya siku 14 lakini wabunge walibadili muda wa mwisho wa marekebisho hayo kutumika iwe siku moja tu.

IEBC yenyewe ikielezea namna ilivyojiandaa kwa uchaguzi wa marudio kama ulivyopangwa, imesema mapendekezo ya marekebisho hayo siyo ya lazima kwa sababu mambo yote ambayo tume ilikuwa na uhuru kusimamia majukumu yake.

Tume imesema sheria za sasa zinatosha kuendesha uchaguzi wa marudio wala hawahitaji nyingine. "Tumetambua dosari zetu na maeneo yanayopaswa kushughulikiwa na kuimarishwa. Hatuhitaji sheria nyingine kuendesha uchaguzi wa Oktoba 26, 2017," alisema Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati Alhamisi alipozungumza na waandishi wa habari juzi katika Ukumbi wa Bomas of Kenya baada ya mkutano kati ya tume hiyo, muungano wa Nasa na Jubilee kuvunjika kutokana na kutokuwepo makubaliano.

Chebukati alisema makosa yaliyotajwa na Mahakama ya Juu wakati wa kubatilisha uchaguzi wa urais wa Agosti 8, hayakutokana na upungufu wala ukosefu w sheria. "Hitilafu zilizotajwa hazikutokana kwa sababu ya ukosefu wa sheria. Tumerekebisha 'nyumba yetu' na ninalihakikishia taifa kuwa Oktoba 26 sharti tufanye uchaguzi kama ilivyoagiza mahakama," alisema.

Juhudi za kujadili kuhusu maandalizi ya uchaguzi huo juzi hazikuzaa matunda baada ya ujumbe wa Nasa ukiongozwa na Seneta wa Siaya James Orengo, kuondoka katika ukumbi wa mkutano huo kwa kile walichodai ni kughadhabishwa na mswada wa Jubilee bungeni wa kutaka kubadilisha sheria za uchaguzi.

"Ifahamike wazi sipingi mswada huo, lakini kwa sasa tuna sheria za kutosha," alisisitiza Chebukati.

Kuhusu uwezekano wa baadhi ya wagombea kujiondoa kushiriki uchaguzi huo wa marudio Chebukati alisema hajapokea barua wala taarifa yoyote ya kujitoa kushiriki kutoka kwa mgombea yeyote wa kiti cha urais.

"Tumeshachapisha majina ya wagombea wawili wa kiti hicho katika Gazeti la Serikali, na hakuna aliyeniletea barua akisema hatashiriki uchaguzi," alisema.

Uchaguzi wa marudio utawashirikisha wagombea wawili tu, Rais Uhuru Kenyatta ambaye anapeperusha bendera ya Jubilee, na aliyewa kuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kwa tiketi ya muungano wa Nasa.

Mwenyekiti huyo aliwaambia waandishi wa habari kwamba katika mkutano mwingine ujao hatahitaji wawakilishi bali wagombea urais wenyewe yaani Uhuru na Raila.

"Mkutano wa leo (Alhamisi) hatujaafikiana kwa sababu ya mswada ulioko bungeni. Katika mkutano ujao wa upatanisho, tutahitaji wagombea wa urais wenyewe kuhudhuria," alieleza.

Jubilee

Viongozi wa Jubilee wamesema mswada wa kubadilisha sheria za uchaguzi uliowasilishwa bungeni umewakasirisha Nasa kwa sababu umefunga mianya yote ya kususia kushiriki uchaguzi wa Oktoba 26.

Jubilee inasema Nasa wanataka kuzua mvutano kwa sababu wametambua mswada huo unawashurutisha kushiriki uchaguzi kwa kuwa umeondoa vikwazo vyote vilivyotajwa na Mahakama ya Juu wakati ikitoa maelezo yake kwa kina ya kufutilia mbali ushindi wa Rais Kenyatta.

"Wenzetu wameghadhabika kwa sababu tumeziba mianya yote ya kutoepuka kushiriki uchaguzi wa Oktoba kupitia mswada huo," alisema Seneta wa Elgeiyo Marakwet, Kipchumba Murkomen nje ya Ukumbi wa Bomas of Kenya baada ya mkutano kuvugika.

"Tunachotaka ni uchaguzi wa huru, haki na wazi," akaongeza Seneta huyo.

Nasa inashikilia kuwa haitashiriki uchaguzi huo wa Oktoba 26, hadi pale IEBC itakapofanya mabadiliko ikiwamo kumfurusha Mkurugenzi wake Ezra Chiloba na maafisa wengine. Pia hawataki kuhusishwa kwenye uchaguzi huo kampuni ya mawasiliano ya Safaricom, ya uchapishaji karatasi za kupiga kura Al-Ghurair (Dubai) na Safran Morpho (Ufaransa).

"Sisi tumejiandaa kushiriki uchaguzi huo, tunajua wenzetu hawajajiandaa ndio maana wana sarakasi nyingi," alieleza Murkomen.

Ujumbe wa Ancelotti Baada ya Kufukuzwa

$
0
0
Ujumbe wa Ancelotti Baada ya Kufukuzwa
Baada ya kufutwa kazi aliyekuwa kocha wa Bayern Munich Carlo Ancelotti ameishukuru bodi ya timu hiyo kwa kumwamini pamoja na ushirikiano waliompa katika kipindi chote alichofundisha timu hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ancelotti ameandika “Imekuwa heshima kubwa kuwa sehemu ya historia ya Bayern Munich. Napenda kuishukuru Klabu, Wachezaji na zaidi mashabiki wa kushangaza ambao sijawahi kukutana nao tangu nianze kufundisha soka”.
Mtalaam huyo wa ufundi mwenye miaka 58 alipoteza kibarua chake jana mchana baada ya bodi ya Bayern Munich kuketi na kocha huyo na kuazimia kutoendelea na mkataba wake uliokuwa unamalizika 2019.
Baadhi ya wachezaji wa Bayern Munich Thiago Alcantala, Frank Ribery, Robert Lewandowski na Arturo Vidal wamemshukuru Ancelotti kila mmoja akieleza kwa namna ambavyo amefaidika kuwa chini ya kocha huyo kwa msimu mmoja

Asilimia 60 ya Mashuka ya Mwananyamala Yamedaiwa Kupotelea Muhimbili

$
0
0
Asilimia 60 ya Mashuka ya Mwananyamala Yamedaiwa Kupotelea Muhimbili
Asilimia 60 ya mashuka ya hospitali ya Wilaya ya Kinondoni ya  Mwananyamala yamedaiwa kupotelea Muhimbili.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Dk Festo Duganga alisema hayo leo wakati wa ziara ya mkuu wa wilaya hiyo hospitalini hapo.

Amesema, ukosefu wa mashine za kufulia mashuka unasababisha kutumia Sh16milioni kwa mwezi kutokana na kutumia mashine za Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

"Mashuka yetu tunapeleka kufua Hospitali ya Muhimbili, lakini asilimia 60 ya mashuka hayarudi kwakuwa si rahisi  kuyatambua," amesema Dk Duganga

Dk Duganga amesema licha ya changamoto nyingi, Hospitali hiyo imefanikiwa kuongeza mapato kutoka Sh25milioni hadi Sh30milioni kwa wiki.

Amesema, kiasi hicho cha fedha kinatokana na malipo ya huduma kupitia michango pamoja na bima ambapo asilimia 70 hutumika kwa ajili ya kununua vifaa tiba pamoja na dawa huku asilimia 30 kwa ajili ya maboresho ya miundombinu.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Daniel Nkungu alisema, Hospitali hiyo ina watumishi 300 huku ikiwa na upungufu wa watumishi 200 hasa manesi na wauguzi ambao wanahitajika kukidhi mahitaji.

"Wakati Hospitali hii inajengwa mwaka 1973 ilikuwa inatoa huduma kwa watu wachache lakini kumekuwa na ongezeko kubwa la watu hasa wajawazito na watoto," amesema

Amesema, idadi hiyo ni ndogo ukilinganisha na wagonjwa 2500 wanaofika kila siku hospitalini hapo kwaajili ya kupatiwa huduma hali inayosababisha watumishi waliopo kufanya kazi zaidi ya muda wao wa kazi.

Mkuu wa Wilaya hiyo Ally Hapi alisema ni kweli  uhakiki wa vyeti umeleta athari kwenye Hospitali nyingi ikiwamo ya Mwananyamala huku akiahidi kufikisha suala hilo kwa Wizara ya Utumishi pamoja na Waziri wa Fedha kwaajili ya kuomba kuongeza watumishi hospitalini hapo.

"Inawezekana Vituo vyote vinakuwa treated bila kuzingatia idadi ya watu na mahitaji, mimi nimeona kuna shida," amesema

"Hospitali ya Mwananyamala inaweza ikawa inahudumia watu wengi kuzidi Hospitali ya Rufaa ya Bugando (Mwanza),lakini tutaendelea kuwashauri viongozi wetu ili kwa sisi ambao tuna idadi kubwa ya watu tuongezewe watumishi," amesema Hapi

Aidha, aliutaka uongozi wa hospitali hiyo kusimamia vizuri matumizi ya dawa zinazotolewa Bohari ya dawa (Msd) huku akiwaonya baadhi ya watumishi wenye tabia ya kuziuza kwa wagonjwa.

Madee Amtolea Povu Dudu Baya Amtaka Wabishane kwa Kazi Sio ManenoManeno '

$
0
0
Madee Amtolea Povu Dudu Baya  Amtaka Wabishane kwa Kazi Sio ManenoManeno '
Msanii wa muziki Bongo, Madee amemjibu msanii Dudu Baya aliyedai kuwa wimbo ‘Sikila’ si mzuri.

Msanii huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Sema’ ameiambia E-Newz ya EATV kuwa anachukulia hayo ni kama maoni yake binafsi kwani hakuna ambaye anafanya kitu bila kupingwa na msanii hawezi kutoa ngoma kila mtu akaikubali.

“Hatusikii kazi tunasikia maneno, kwa hiyo hivyo ni vitu ambayo kwangu mimi huwa navipisha tu, ukitaka kubishana nakuonyesha kazi yangu hii hapa, nadhani huo ndio msingi bora ambao tunatakiwa tuwaelekeze wezentu wanaojaribu kutoka nje ya mistari,” amesema Madee.

“Wengi ambao nilikuwa nao, nilianza nao miaka hiyo 17 ndio ambao sasa hatuwasiki zaidi utawasikia wanaongea hiki na kile lakini still Madee bado anatoa ngoma watu wanapokea na show zinafanyika na maisha yanaendelea vizuri tu,” amesema.

Ngoma Sikila ambayo Madee amemshirikisha Tekno kutoka nchini Nigeria alifanya video katika mtindo wa katuni (animation) kitu ambacho Dudu Baya alieleza kuwa hakiendani na Madee aliyemfahamu hapo awali.

Majambazi Wapora Msikitini, Wamjeruhi Mlinzi kwa Panga

$
0
0
Majambazi Wapora Msikitini, Wamjeruhi Mlinzi kwa Panga
WATU wanaosadikiwa kuwa ni majambazi, wamevamia Msikiti Mkuu wa Ijumaa ulioko Kata ya Igunga Mjini wilayani hapa mkoani Tabora, kisha kumjeruhi mlinzi na kupora baadhi ya vitu ikiwemo vitabu vya dini ya Kiislamu.

Mlinzi aliyejeruhiwa ni Juma Mussa (55), mkazi wa Mtaa wa Nkokoto kata ya Igunga ambaye amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Igunga na hali yake bado ni mbaya. Mkuu wa Wilaya ya Igunga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, John Mwaipopo alithibitisha kutokea kwa uhalifu huo na mtuhumiwa mmoja amekamatwa pamoja na vitu vilivyoibwa.

Alimtaja mtuhumia huyo kuwa ni Juma Mponi (45) ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Stendi ya Mabasi mjini Igunga, na kutamba kuwa hakuna jambazi atakayetoka salama Igunga kwa kuwa polisi wamejipanga kikamilifu kukabiliana na matukio kama hayo.

Akizungumza kwa shida akiwa wodini, mlinzi huyo alisema shambulio hilo limetokea Septemba 25, mwaka huu saa 8 usiku, ambako watu hao walifika msikitini hapo kisha kurusha jiwe kwenye eneo alilokuwa amekaa.

Alisema baada ya kuona jiwe hilo, aliamua kusimama na mara jambazi mmoja aliruka uzio wa msikiti kisha akaingia na kuanza kumshambulia kwa mapanga kichwani. Alibainisha kuwa wakati akishambuliwa, aliona majambazi wengine wakifungua milango ya msikiti na mmoja wao akimweleza mwingine “wewe maliza kabisa huyo mlinzi.”

Hata hivyo, mlinzi huyo aliendelea kuuomba msaada kwa kupiga kelele ili asaidiwe, hali iliyowafanya majambazi kukimbia kusikojulikana wakiondoka na baadhi ya mali za msikiti. Mhasibu wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa, Issa Said Feruzi alitaja vitu vilivyoibiwa na majambazi hao kuwa kuwa ni misahafu minne, feni moja, saa kubwa, vitabu vya hitima 30, kitabu cha mapato na matumizi, daftari za Tabligh nne, maikrofoni na stendi yake, miswala miwili; vyote vikiwa na thamani ya Sh 374,000.

Hata hivyo, alisema vitu vyote vimepatikana na viko Kituo cha Polisi Igunga; huku Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Melchades Magongo amekiri kumpokea Juma Mussa, akieleza kuwa alimpokea hospitalini hapo akiwa na majeraha kichwani ambayo yanaonesha alikatwa na kitu chenye ncha kali. Dk Magongo alisema hali ya mlinzi huyo bado si nzuri akiendelea kupatiwa matibabu zaidi katika wodi namba nane hospitalini hapo.

Serikali Yaifungia Gazeti la Raia Mwema kwa Siku 90

$
0
0
Serikali Yaifungia Gazeti la Raia Mwema kwa Siku 90
Serikali imesitisha uchapishaji na usambazaji wa gazeti la kila wiki la Raia Mwema kwa muda wa siku 90 kuanzia leo.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk Hassan Abbasi amesema leo Alhamisi kuwa agizo hilo pia linahusu toleo la mtandaoni.

Dk Abbasi amesema adhabu hiyo inatokana na toleo namba 529 la Septemba 27 hadi  Oktoba 3 lililochapisha habari ya uchambuzi inayosomeka “Urais utamshinda John  Magufuli.”

Mwenyekiti wa Bodi ya Raia Mwema, Jenerali Ulimwengu amesema wameambiwa sababu ya kusitishwa kwa gazeti hilo ni habari hiyo.

Ulimwengu amesema kwa sasa wanashauriana kuona ni nini cha kufanya.



Dk Abbasi amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari kuwa, Serikali inasisitiza uchambuzi huo ni maoni ya Raia Mwema  ya haki (fair comment), hata hivyo, kwa bahati mbaya, na nia ovu, makala hiyo ilisheheni nukuu za kutunga na zisizo za kweli zikimsingizia Rais John Magufuli.

Amesema gazeti hilo pia limewahi kuonywa kwa makosa mbalimbali.



Amesema nukuu za uongo, kutungwa na zenye nia mbaya zikidai Rais alipata kusema ni, “Suruali za zamani msizitupe, mtazihitaji baadae,” na “Watakaobaki  Dar es Salaam baada ya mwezi wa saba watakuwa wanaume kwelikweli.”



Dk Abbasi amesema walipotakiwa kuthibitisha wapi iwe ndani au nje ya nchi Rais alipata kutoa kauli hizo, wahariri wa Raia Mwema waliomba muda ambao walipewa. “Wakarejea na kuthibitisha kuwa hawana ushahidi huo, wakakiri kosa na kuomba radhi.”



Mkurugenzi huyo amesema bado Serikali inaamini Watanzania wakiufanyia mzaha upotoshaji wa taarifa na uchochezi katika zama hizi za Tehama amani na utulivu uliopo kwa miaka mingi utapotea na kukaribisha maafa kama ilivyotokea kwingineko duniani.



“Serikali, katika uamuzi huu, uliochukuliwa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Waziri wa Habari katika kifungu cha 59 cha Sheria ya Huduma za Habari Na. 12, 2016, imetoa adhabu ndogo tofauti na ukubwa wa kosa kwa kuwa wahariri wa gazeti hili hawakufanya tashtiti, wamekiri kosa,” amesema.

Dk Abbasi amesema kupitia hilo, wamejifunza mambo kadhaa kuhusu changamoto za kiwango cha weledi wa uandishi wa habari nchini kiasi cha kuwalazimu kutoa ufafanuzi wa kina kwa faida ya umma na tasnia yenyewe; kwamba uandishi ni taaluma adhimu na yenye haki na wajibu vinavyopaswa kufuatwa na si kufanyiwa dhihaka.

Wimbo Mpya wa Diamond Platnumz Alioutoa Leo Wavunja Rekodi ya Ali Kiba ndani ya Masaa

$
0
0

Video ya wimbo mpya wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Hallelujah umefikisha watembeleaji milioni moja ndani ya saa 16 tangu ulipowekwa katika chaneli ya Youtube na kuwa wimbo uliowahi kutazamwa na watu wengi ndani ya muda mfupi nchini.

Wimbo Hallelujah uliowekwa saa sita usiku, unaivunja rekodi iliyowekwa mwezi ulipita na Seduce Me wa Alikiba ambao ulifikisha watembeleaji milioni moja ndani ya saa 37 uliowekwa katika mtandao wa Vevo. Diamond katika wimbo huo amewashirikisha wasanii wa Jamaica, Morgan Heritage.

Hallelujah ulifikisha watembeleaji milioni moja ilipofika saa kumi jioni.

Muda mchache kabla ya kufikisha watazamaji milioni moja Diamond aliwashukuru mashabiki wake kwa kuupokea vizuri wimbo huo.

“Nawashukuru kwa kuniunga mkono, tuzidi kusonga mbele ili dunia ione uwezo wa mtoto wa Kitanzania, “ aliandika katika mtandao wa Instagram.

 0      

Wanaume Washindwa Kuzalisha kwa Sababu ya Kubwia Mirungi Same

$
0
0
Imeelezwa kwamba idadi kubwa ya wanaume hawana uwezo wa kuzaa kutokana na utumiaji wa dawa za kulevya kwa muda mrefu ikiwemo mirungi na bangi.

Kutokana na hali hiyo  Mbunge wa Same Mashariki Naghenjwa  Kaboyoka, amemwomba Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kuingilia kati ili kuokoa vijana.

Kaboyoka amesema  wananchi wengi wanajishughulisha na ulimaji wa zao hilo bila kuogopa sheria hususan  za mamba vunta na Gonja.

Amesema sababu ya ulimaji na utumiaji wa bangi na mirungi ni  kutokuwepo kwa kituo cha polisi katika maeneo hayo.

Amesema ameshaongea na Waziri Nchemba ambaye na  amemuahidi kujenga  kituo cha polisi katika maeneo hayo

ili kupunguza ulimaji wa mirungi na bangi lakini ni mwaka sasa umeshapita.

“Nikiwa  katika bunge la mwisho niliongea na Katibu Mkuu wa Mambo ya Ndani kwamba ulimaji wa mirungi, bangi pamoja na uhalifu ni mkubwa na unazidi kushika kasi katika tarafa hizo."amesema Kaboyoka

Kaboyoka  amesema  usafiri wa kwenda kuripoti matukio ya kihalifu ni changamoto ya usafiri ambapo basi linatoka saa nane usiku hadi kurudi kesho yake.

 “Sasa fikiria wahalifu watapelekwaje ,na nani atenda kuripoti na basi linaloondoka sa nane, hivyo uhalifu unazidi kuongezeka kutoka na kwamba hakuna wakuwakamata”amesema Kaboyoka.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya hiyo,Sospeter Magonera  amesema wanapinga vikali kilimo hicho cha mirungi kutokana na kwamba kipo kinyume na sheria za nchi.

“Kilimo hicho kinachangia kwa asilimia kubwa kuharibu nguvu kazi ya jamii pamoja na nguvu kazi ya Taifa hali ambayo inarudisha maendeleo ya taifa nyuma”amesema Sospeter

Hata hivyo,diwani wa kata ya mamba miamba, Michael Mauya amesema uvutaji wa bangi na utumiaji wa mirungi umechangia kwa asilimia kubwa vijana kuishiwa nguvu za kiume hali ambayo imechangia kupungua kwa idadi ya watoto katika tarafa hizo.

 0    

Hamisa Mobeto Ashauriwa Kupigania Ndoa Kuwa Mke wa Pili Kwa Diamond Platnumz

$
0
0

MSANII wa filamu Bongo, Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ amemtaka mwanamitindo Bongo, Hamisa Mobetto kupigania ndoa kwa Mbongo Fleva aliyezaa naye, sababu dini yake inamruhusu kuwa mke wa pili.


Akipiga stori na Star Mix, Sabby alisema kuwa, pamoja na yote yaliyotokea ni vyema mwanadada huyo asivunjike moyo kama bado anamuhitaji mzazi mwenziye huyo, licha ya kuonekana ameelemea kumuhitaji Zarinah Hassan `Zari Boss Lady’ anapaswa kukomaa hadi ndoa ifungwe.

“Namshauri Hamisa asikubali kirahisi kumkosa baba wa mtoto wake, kama vipi huyo jamaa awaoe wote wawili Zari mke mkubwa na Hamisa mke mdogo maana dini imeridhia wake hadi wanne,”alisema Sabby.

Shilole Adaiwa Kumtesa Mpenzi Wake Mpya Uchebe Kama Alivyokuwa Anamburuza Mziwanda

$
0
0
MKALI wa miondoko ya Mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ anadaiwa kumtesa mpenzi wake, Ashiraf Uchebe na kwamba imefikia kipindi anamgombeza mbele za watu kama mtoto mdogo. Kwa mujibu wa chanzo, kiliitonya Star Mix kuwa, juzikati katika Ukumbi wa Maisha Basement, Kijitonyama jijini Dar, Shilole alionekana akimkoromea Uchebe.

“Yaani hadi aibu, Shilole sijui kwa nini aliamua kufanya vile, kuna wakati alikuwa akimnyooshea vidole na kumsuka,” kilisema chanzo kilichohudhuria ukumbini hapo.

Star Mix baada ya kuunyaka ubuyu huo, ilimvutia waya Shilole ambapo alisema; “Jamani watu wanajua kukuza mambo na kuniona kama mimi ni mkorofi kila wakati kwenye mapenzi, lakini siamini kabisa kwenye mapenzi hakuna ugomvi wala purukushani kwani vyote nisehemu ya mapenzi.”

Global

Baadhi ya Wachungaji Wachukizwa na Wimbo Mpya wa Diamond Kutumia Jina la "Hallelujah" Waomba Ufungiwe

$
0
0

Kutoka facebook ameandika Mchungaji Zakayo Nzogere:

"Tafadhali tusaidiane kufikisha ujumbe huu...
TUNATAKA JUKWAA LA WAKRISTO TANZANIA LINALOJUMUISHA BARAZA LA TEC, CCT NA CPCT LITOE TAMKO DHIDI YA WIMBO WA "DIAMOND" AMBAO AMETUMIA NENO "HALLELUJAH" WAKATI MAUDHUI YA WIMBO WAKE HAYAENDANI NA MAADILI YA KIKRISTO.
MATUMIZI YA NENO HILO KATIKA WIMBO HUU YANAUDHI.
PIA NAOMBA WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO AFIKISHIWE UJUMBE HUU.
PIA TUNAITAKA BASATA IZUIE WIMBO HUU HADI MANENO HAYO YAONDOLEWE.
CC. Bishop David Batenzi, Bishop Tarcisius Ngalekumtwa, Bishop Alex Malasusa"

JE una Tatizo la Nguvu za Kiume, Kukosa Hamu ya Tendo, Kushindwa Kurudia Tendo au Maumbile Madogo ?

$
0
0
JE, UNA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, KUKOSA HAMU YA TENDO, KUSHINDWA KURUDIA TENDO AU MAUMBILE MADOGO YA UUME? SOMA HAPA 👇👇👇👇 Tatizo la kukosa au upungufu wa nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, sio Tanzania tu bali duniani kote. Kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile madogo sio ugonjwa ila ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili.

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME HUSABABISHA MAMBO KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa ☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni ☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. @natural beauty pro. Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye kisukari kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL ni kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250000@250,000/=
2.VIG RX CREAM-Ni dawa mpya ya kuongeza maumbile inayoongeza hadi nchi 7.5 inapatikana kwa @200000@200,000/= 3.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150000@150,000/=
4.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kurudia tendo hata mara 3 bila kuchoka @150000@150,000/= KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- @natural2162 @natural2162 @natural2162

Wasiliana nasi Popote ulipo duniani kwa no
(+255)0759029968 na 0659618585 

NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na hazina kemikali wala madhara kwa mtumiaji. Zimethibitishwa kiafya.

Zari, Wema Sepetu, Jokate, Dj Fetty, Irene, Shilole Walivyoshikwa na Wimbo Mpya wa Diamond 'Hallelujah'

$
0
0
Si Zari The Bosslady Lady pekee aliyeukubali wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliowashirikisha Morgan Heritage, hata maex wa muimbaji huyo wameuzimia. Wema Sepetu, Jokate Mwegelo waliowahi kuwa na uhusiano na Diamond nao wanauimba. Irene mrembo wa video ya Kwetu aliyewahi kudaiwa kuwa side chick wa Mondi naye ameunga mstari. Mastaa wengini ni pamoja na Shilole na Dj Fetty.. VIDEO:

VIDEO:Baada ya Hallelujah kuvunja Record ya Seduce Me! Quick Rocker Ameongea haya!

$
0
0
Baada ya Hallelujah kuvunja Record ya Seduce Me! Quick Rocker Ameongea haya!
VIDEO"

Nay wa Mitego Atoa Neno Kwa Wasanii Wanaotumia Uchawi

$
0
0

Msanii wa muziki Bongo, Nay wa Mitego amefunguka juu ya wasanii wanaotumia uchawi katika muziki wao.

Rapper huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Makuzi’ ameiambia XXL ya Clouds Fm kuwa msanii akiamini katika ushirikina kuna kipindi kile anachokiamini kinaishiwa nguvu.

“Umefika muda karibia Tanzania nzima inaamini kwenye kile ambacho nakifanya, hii ni ndele tosha, ni zaidi ya ndele, sijua mtu ambaye anaamini hivyo” amesema Nay.

“Halafu ndele huwa zina mwisho ukifika muda maana wewe ndio umemaliza hata uimbe vipi, hata umshirikishe yesu bado watu hawaelewi” ameongeza.

Katika hatua nyingine Nay amezungumzia uwezo wake katika performance jukwaani kwa kudai kuwa yeye Juma Nature wa pili kwani msanii huyo amekaa muda mrefu bila kutoa nyimbo ila bado anakubalika.

Aliyesambaza Taarifa za KuonekanaKachero Katika Hospitali ya Lissu Afikishwa Mahakamani

$
0
0
Aliyesambaza Taarifa za KuonekanaKachero Katika Hospitali ya Lissu Afikishwa Mahakamani
MKAZI mmoja wa Kigamboni, Mbutusyo Mwakihaba (40), amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kusambaza ujumbe katika mtandao kwamba kachero wa Usalama wa Taifa ameonekana jijini Nairobi karibu na hospitali aliyolazwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mbutusyo amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  na kusomewa shtaka linalomkabili mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Wakili wa Serikali Janeth Magoho alidai mshtakiwa anakabiliwa na kosa la kusambaza taarifa za uongo chini ya kifungu namba 16 cha Sheria ya mtandao namba 4 ya mwaka 2015.

Janeth amedai Septemba 11, mwaka huu kupitia mtandao wa ‘WhatsApp’ mshtakiwa aliandika “Huyu ni Kachero wa Usalama wa Taifa anatambulika kwa jina la Jose anaonekana Nairobi karibu na hospitali alikolazwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu…Mwaxcheni mwenzenu”.

Mshtakiwa alikana kutenda makosa hayo, upelelezi wa kesi haujakamilika ambapo Hakimu Nongwa alikubali kumpa dhamana kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika watakaosaini dhamana ya Sh milioni tano kila mmoja ambapo mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti hayo na kurudishwa mahabusu hadi Oktoba 12, mwaka huu.

Serikali Yakiri Kuongezeka Kwa Vifo Vinavyotokana na Uzazi

$
0
0
Serikali Yakiri Kuongezeka Kwa Vifo Vinavyotokana na Uzazi
Vifo vinavyotokana na uzazi vimeongezeka kutoka 432 kwa vizazi hadi laki moja katika kipindi cha mwaka 2012-2013 hadi kufikia 556 mwaka 2016-2017 sawa na kina mama 900 wanapoteza maisha kila mwezi na thelathini kila siku nchini wakati wa kujifungua.

Takwimu hizo zimetolewa jijini Dar es Salaam na waziri wa afya, Mhe. Ummy Mwalimu alipokuwa anapokea mashine ya kisasa ya kutoa dawa ya usingizi wakati wa upasuaji iliyotolewa na taasisi ya utepe mweupe ambapo amesema katika kukabiliana na tatizo hilo ifikapo mwezi juni 2018 serikali itaongeza vyumba vya upasuaji kutoka 109 hadi 279.

Akizungumza baada ya kukabidhi mashine hiyo mratibu wa kitaifa wa taasisi ya utepe mweupe Bi. Rose Mlay amesema ongezeko hilo la vifo linasikitisha na kumuomba waziri kuhakikisha anaendelea kuweka mkazo katika suala la upatikanaji wa huduma za dharura na kwa haraka kwa mama mjamzito hasa maeneo ya vijijini.

Kwa upande wake katibu mkuu wa wizara hiyo Dkt. Mpoki Ulisubisya ambaye pia ni mtaalamu wa usingizi ameelezea namna mashine hiyo inavyofanyakazi,uwezo wake na faida zake kwani haihitaji mitungi ya gesi wala umeme na ina uwezo wa kuonyesha viashiria vya hatar

Mwigulu Aliibua Upya Sakata la Nape Kutolewa Siraha Adharani

$
0
0
Mwigulu Aliibua Upya Sakata la Nape Kutolewa Siraha Adharani
Kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba kwamba mtu aliyemtolea bastola hadharani Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye si askari wa Jeshi la Polisi imeibua upya mjadala kuhusu suala hilo.

Waziri Mwigulu alitoa kauli hiyo juzi wakati akizungumza katika kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Clouds baada ya mmoja wa wasikilizaji kutaka kujua kama mtu huyo aliyemtolea bastola Nape alikamatwa au hajakamatwa.

Baada ya kauli hiyo, wadadisi wa masuala ya kisiasa wametaka waziri Mwigulu ambaye Jeshi la Polisi liko chini yake kuueleza umma mtu huyo kama si askari ni nani au awachukulie hatua askari walioshindwa kumchukulia hatua mtu huyo.

Nape alikumbana na kadhia hiyo Machi 23 ikiwa ni saa chache kupita tangu Rais John Magufuli alipotangaza kumwondoa kwenye Baraza la Mawaziri akihudumu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Baada ya kuondolewa asubuhi, siku hiyohiyo mchana Nape alipanga kufanya mkutano na waandishi wa habari katika Hoteli ya Protea jijini Dar es Salaam ambako alikuta zuio la vyombo vya dola na alipolazimisha alijikuta akitolewa bastola mbele ya waandishi wa ndani na nje akitakiwa kurudi ndani ya gari lake na asifanye mkutano huo.

Tangu kutokea kwa tukio hilo, kumekuwapo mijadala hasa ikilenga kujua kwa nini hatua hazichukuliwi kwa mtu huyo licha ya video na picha mbalimbali zinazomwonyesha akitoa bastola na kumnyooshea Nape zipo na zinasambaa mitandaoni.

Mjadala huo ulitua katika Bunge la Bajeti lililokutana Aprili na hata katika mkutano wa Bunge uliomalizika wiki tatu zilizopita mjini Dodoma, baadhi ya wabunge wakitaka suala hilo na matukio mengine yajadiliwe ndani ya Bunge jambo ambalo halikufanyika.

Spika wa Bunge, Job Ndugai alichukua uamuzi wa kuitaka Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama chini ya Mwenyekiti wake, Balozi Adadi Rajabu kulishughulikia suala hilo na taarifa yake ilikuwa isomwe katika mkutano huo wa Bunge lakini ilishindikana na inatarajiwa kusomwa Novemba.

Juzi, waziri Mwigulu ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi akijibu swali la msikilizaji kuhusu mtu huyo kukamatwa au la akisema: “Ninachofahamu aliyemtishia bastola Nape hakuwa polisi kama ambavyo ilidhaniwa.”

Alisema katika tukio kama hilo, wahalifu wanaweza kutumia nafasi hiyo kufanya watakavyo, lakini uchunguzi wa suala hilo unaendelea.

Jana, gazeti hili lilimtafuta Nape kutaka kujua maoni yake kuhusu kauli ya waziri Mwigulu ambaye alisema kwa kifupi: “Siwezi kuzungumzia hilo kwani sijaona… nikiona nitaweza kuzungumza.”

Itakumbukwa, Aprili 8 mwaka huu, Nape akizungumza jimboni kwake kwa mara ya kwanza tangu alipoondolewa katika nafasi ya uwaziri alisema hakuchaguliwa kwenda kuwa waziri bali kuwatumikia wananchi huku akitoa ushauri kwa Rais Magufuli.

“Namwomba Rais wangu, na huu ni ushauri tu, simlazimishi, ninampa ushauri na kumwomba… kwa sababu matendo haya yanamjengea chuki yeye na wananchi kwa sababu wanadhani yeye ndiye anaowatuma,” alisema.

Nape alisema, “Sasa ili Rais wangu asijengewe chuki lazima ajiondoe kwenye jambo hili na namna ya kujiondoa ni kuunda tume iende kuchunguza imletee ripoti nani yupo nyuma ya haya matendo ya kihuni.” Alisema, “Ili atenganishe CCM na matendo ya wahuni wachache wanaotumia dhamana waliyopewa kuumiza watu na kupoteza watu lazima tume iundwe iende ikatuletee ukweli, ngoja niseme hapa kwani si nipo nyumbani tu… kama nilitolewa bastola si ni sawa na kufa tu, basi nipo tayari.”

Atueleze ni nani

Rais mstaafu wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), John Seka akizungumza na gazeti hili kuhusu kauli ya waziri Mwigulu alisema inaashiria kwamba uchunguzi wa suala hilo la Nape umekamilika hivyo taarifa yake inapaswa kutolewa kwa wananchi.

“Kama waziri amesema si askari, anawajibu wa kusema ni nani, kwani ushahidi wa mazingira upo. Lakini kama hakuwa askari alikuwa ni nani, je, anaruhusiwa kumiliki silaha na je, alitumwa na nani kwa lengo gani,” alihoji Seka.

Alisema, “Na kauli hiyo ya waziri inaashiria uchunguzi umekamilika na kubaini kwamba si askari… nilitarajia jana (juzi) wangemuuliza pale kama si askari wa Jeshi la Polisi ni nani kwani kwa kauli hiyo uchunguzi unaonesha umekamilika.”

Alipoulizwa na gazeti hili kuhusu hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Rajabu alisema: “Siwezi kuyazungumzia masuala hayo katika simu, ‘next week’ nitakuwa bungeni Dodoma utanitafuta.”

Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) mstaafu, Ernest Mangu alisema, “Sina hiyo fursa, waulize walio kwenye nafasi hiyo.”

Alipoulizwa kwamba anaweza kutoa maoni yake na yakafanyiwa kazi ili huyo asiyejulikana akajulikana, Mangu alisema, “Kama watahitaji wataniuliza, wewe unaniuliza kama nani, hayo ni masuala ya kiutendaji.”

Polisi wawajibishwe

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRD), Onesmo ole Ngurumwa alisema kauli ya waziri Mwigulu inazua utata hasa ikizingatiwa Nape alizuiwa kufanya mkutano na aliyetoa bastola aliitoa mbele ya askari wakishuhudia.

“Kitendo cha yule kutoa silaha mbele ya askari tena na RPC Kaganda (aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda) alikuwepo na akaachwa inaonyesha wanamjua ni mwenzao, kama si mwenzao au hawamjui, ilikuwaje atoe silaha hadharani na wamwache bila kumchukulia hatua,” alihoji.

Ole Ngurumwa alisema, “Kama ndivyo, basi Mwigulu awachukulie hatua askari wake waliokuwepo wakati huyo asiyejulikana anatoa bastola kwani ni kosa kutoa silaha hadharani tena mbele ya askari.”

Kauli ya kwanza ya Mwigulu

Itakumbukwa Machi 24 ikiwa ni siku moja tangu Nape kunyooshewa bastola, waziri Mwigulu alitumia akaunti yake ya mtandao wa kijamii kuzungumzia sakata hilo akisema, “Mh. Nape Moses Nnauye sio jambazi, ni Mtanzania, ni mbunge, mjumbe wa NEC wa CCM, hana record ya uhalifu.”

“Kitendo cha mtu kumtolea bastola, sio cha kiaskari, sio cha Kitanzania na sio cha ki Mungu, kama mtu ameweza kutoa bastola mbele ya kamera nawaza mbali ingekuwa kwenye uchochoro angefanya nini,” alisema.

Alisema, “Nahusika na usalama wa raia wote wa Tanzania, nimemwelekeza IGP (Inspekta Jenerali wa Polisi) atumie picha kumsaka mtu yule aliyeinua kufanya kitu cha kihalifu kwa kofia ya uaskari, na kama ni askari basi sheria zinazoongoza taasisi husika zichukue mkondo wake,” alisema


Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images