Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Yanga Kuvana na Mtibwa Sugari Leo Yaahidi Ubingwa

$
0
0
Yanga Kuvana na Mtibwa Sugari Leo Yaahidi Ubingwa
YANGA leo inacheza na Mtibwa Sugar katika Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, lakini imetamba kushinda.

Wakati Mtibwa ikiwa kileleni, Yanga yenyewe ipo nafasi ya sita ikiwa na pointi nane, lakini kocha msaidizi wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa amesema kuwa wamejiandaa kushinda mchezo huo.
Nsajigwa alisema wanataka kushinda mchezo huo ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kutetea ubingwa wao.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Nsajigwa alisema wanajua Mtibwa ni timu nzuri iliyojiandaa kwa ushindani msimu huu lakini watakabiliana nayo ili kuhakikisha wanapata ushindi.

“Tumejiandaa vizuri kwa ajili ya kuhakikisha tunapata matokeo mazuri katika mechi yetu na Mtibwa japokuwa naamini itakuwa na ushindani mkubwa kwani wapinzani wetu wapo vizuri msimu huu.
“Katika mechi hiyo tutamkosa Tshishimbi (Papy Kabamba ana kadi tatu za njano) lakini nafasi yake kuna mchezaji ambaye tayari tumemwandaa kwa ajili ya kuiziba hivyo ni matumaini yetu kuwa tutafanya vizuri,” alisema Nsajigwa.

Kwa upande wake, Kocha wa Mtibwa, Zuberi Katwila amesema moto walioanza nao msimu huu ndiyo huohuo watakaoendelea nao leo dhidi ya Yanga.
“Tunaiheshimu Yanga lakini kwa sasa sisi ni bora kuliko wao na ndiyo maana tunaongoza ligi kwa hiyo tumejipanga kuhakikisha tunaibuka na ushindi,” alisema Katwila.

Serikali ya Awamu ya Tano Chini ya Rais Magufuli ni Sikivu- Mgandilwa

$
0
0
Serikali ya Awamu ya Tano Chini ya Rais Magufuli ni Sikivu- Mgandilwa
Wananchi wa Kigamboni wakiongozwa na viongozi wa wilaya wamejitokeza na kufyeka pori la NAFCO lililoko kata ya Somangila, eneo ambalo ni hatarishi kwa usalama wa raia. Akiongea mara baada ya usafi huo Mkuu wa Wilaya amesema Rais Magufuli ni msikivu

Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Mhe Hashim Mgandilwa alianza kwa kuwashukuru wananchi kwa kuwa watulivu kwa muda wote ambao walikuwa wakilalamikia pori hilo huku serikali ikiwataka wawe na subira wakati taratibu za ufutaji zinaendelea.

"Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ni sikuvu inayodhamiria kuleta maendeleo kwa wananchi ndiyo maana Rais Magufuli amesikia kilio chenu na kuamua kuifuta hati ya Shamba hili ili liwe mikononi mwa serikali, tuendelee kuiunga mkono serikali na sitaki kuona mtu anafanya siasa katika hili, tufanye kazi" alisisitiza Mgandilwa.

Mbali na hilo Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni amewapa wananchi wiki moja kuanzia leo kuendelea kusafisha eneo hilo kwa kufyeka vichaka na kukata miti kwa matumizi yao ya nyumbani kama kuni au shughuli za ujenzi.

Hata hivyo Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Mhe Dkt. Faustine Ndungulile pia amewataka wananchi kuendelea kushikamana kwa Umoja katika shughuli mbalimbali za maendeleo kwani Kigamboni itajengwa na wote. Pia amewaomba wananchi waendelee kuiunga mkono serikali yao kwani imetatua kero zao kubwa pamoja na Rais Magufuli kuifuta mamlaka ya Uendelezaji wa Mji wa Kigamboni (KDA) ambayo ameipigia kelele kwa muda mrefu bungeni.

Pori hilo ambalo lililosafishwa leo na viongozi mbalimbali wa Kigamboni awali lilikuwa likimilikiwa na mfanyabiashara Yusuph Manji ambaye alishindwa kuliendeleza na serikali kuamua kulichukua.

Mwigulu Agundua Tiba ya Watu Wasiojulikana

$
0
0

Mwigulu Agundua Tiba ya Watu Wasiojulikana
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu  Nchemba amesema kutengeneza mioyo yenye maadili  mema kwa wazazi, watoto na jamii kwa ujumla ni miongoni mwa suluhisho la kudumu la jamii kutokuwa na watu wasiojulikana.

Nchemba ameitoa  kauli hiyo jana  wakati wa maadhimisho ya miaka 57 ya Ushirika wa Wanafunzi wa Kiinjili wa Tanzania (Tafes) yaliyokwenda sambamba na kusherehekea miaka 27 ya uwepo wao hapa nchini.

Tafes ni taasisi isiyo kiserikali inayojishughulisha na kuwajengea uwezo wa kiroho wanafunzi wa vyuo vikuu ili wawe na misingi bora ya uongozi katika ngazi mbalimbali.

Amesema maandalizi ya maadili mema yaanza katika ngazi ya familia na taasisi za kiroho na kwamba, Serikali inawaandaa watu kwa shule, kiafya, lakini afya na uaminifu wa kiroho utatoka kwenye taasisi hizo.

Nchemba ambaye pia Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), amesema uhalifu wa kikatili ni zao la kutokuwapo kwa hofu ya Mungu kwenye mioyo ya watekelezaji wa matukio ya aina hiyo.

"Labda niwaambieni kuna watu wana roho mbaya na wengi wana uwezo kufanya vitu vibaya. Wakati Serikali tunashughulikia jambo hilo, tunazipongeza jitihada kama hizi zinazolenga kubadilisha jamii nzima inayofanywa na Tafes," amesema  Nchemba.

Alisema watu wa vyuo vikuu wana famalia zao na kwamba wakiwa maadili mema itawasaidia kuwaelimisha jamii zinazowazunguka kuhusu misingi bora  ya maadili.

"Tukiwa na watu waliolelewa katika misingi ya imani ya aina hii, hatuwezi tukapata watu wasiojulikana na jambo hili linaniudhi sana. Hatuwezi tukawa na watu wasiojulikana, wanaotenda uhalifu  na kukimbia kusikojulikana na tutashughulika na nguvu ya dola," amesema  Nchemba.

Mbali na hilo, Mwigulu ameongeza kwamba  Tafes kwa kazi wanayoifanya huku akitumia msemo wa nahau ya' Usione vyaelea ujue vimeundwa'.

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Bodi ya Tafes, Profesa Lazaro Busagala amesema  lengo la taasisi hiyo ni kuwatengeneza na kuwajengea uwezo wanafunzi wa vyuo vikuu wa kuwa na maadili mema.

Alisema wametumia nafasi ya maadhimisho hayo kupeana moyo namna ya kuwasaidia  kiroho na kimaadili wanafunzi wa vyuo vikuu ili baadaye wasiwe viongozi wazembe na wala rushwa.

"Hadi sasa Tafes imeweza kuwafikia wanafunzi 5000 wa vyuo vikuu mbalimbali," amesema Profesa Busagala.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya hafla hiyo, Dk Grace Kazoba amesema walitumia maadhimisho hayo kuweka msisitizo wa misingi bora itakayowasaidia wanafunzi hao.

Hiki Hapa Kisa cha Juma Abduli Kuongezewa Mbinu

$
0
0
Hiki Hapa Kisa cha Juma Abduli Kuongezewa Mbinu
KATIKA kuhakikisha timu yake inapata ushindi kwa kutumia mipira ya pembeni, Kocha wa Yanga, George Lwandamina amemuongezea mbinu beki wake wa kulia, Juma Abdul.

Lwandamina amefanya hivyo katika mazoezi ya timu hiyo wiki hii kuelekea mechi ya leo ya Ligi Kuu Bada dhidi ya Mtibwa Sugar itakayochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Abdul ni kati wachezaji wanaotengeneza mabao kutokea pembeni kutokana na kusifika kwa uwezo wake mkubwa wa kupiga krosi, faulo na kona zenye macho kuelekea lango la adui.

Championi Jumamosi, lilikuwepo kwenye mazoezi ya Yanga kwenye Uwanja wa Uhuru karibu wiki hii yote na kuona jinsi Abdul anavyoongezewa mbinu na Lwandamina.

Lwandamina alionekana akimuelekeza Abdul jinsi ya kupiga krosi za katikati ya uwanja na kutosubiria kupiga hadi akifika pembeni kwenye kibendera.

Kocha alionekana kila wakati akimuelekeza beki huyo huku akimsisitiza kabla ya kupiga krosi hizo anatakiwa awaangalie washambuliaji wake walipo ili waweze kufunga kwa faida ya timu.

Alipoulizwa Abdul kuzungumza hilo alisema: “Kila siku najifunza na ninaendelea kujifunza vitu vipya ninavyovipata kutoka kwa makocha wangu.
“Ninafurahi kujifunza kiukweli na kikubwa alikuwa akinipa mbinu mbalimbali za ndani ya uwanja,”alisema Abdul.

Roketi Kuanza Kusafirisha Watu Kati ya Miji kwa Kakika

$
0
0
Roketi Kuanza Kusafirisha Watu Kati ya Miji kwa Kakika
Hivi karibuni watu wataweza kusafiri kutoka mji mmoja hadi mwingine kutumia roketi, safari ambayo itachukua dakika chache tu, kulingana na mjasiriamali Elon Musk.
Musk aliahidi haya katika kongamano moja nchini Australia.
Inasemekana kuwa itachukua dakika 29 tu kutoka London hadi New-York.
Musk amesema pia kuwa mwaka wa 2024, ataanza kuwasafirisha watu hadi Mars. Kampuni yake ya SpaceX itaanza kujenga meli za kipekee zitakazofanikisha haya, mwaka ujao.
Kwa sasa kampuni yake inatengeneza ain amoja tu ya roketi; aina ya BFR ambayo inaweza kufanya kazi tofauti tofauti ikiwemo kupeleka watu kwenye mwezi na Mars.
"Safari ambazo watu wengi wanaona kuwa ndefu zinaweza kukamilika kwa chini ya nusu-saa," aliambia umati wa watu mjini Adelaide.
"Baadhi ya wateja wetu wanataka kuona BFR ikiruka mara kadhaa kabla yaya kuwa na imani nayo," Musk alisema.
"Kwa hivyo tunachotaka kufanya ni kujenga roketi kadhaa aina ya Falcon 9 na Dragon, ili wateja wawe na urahisi, na ikiwa wanataka kutumia roketi za kale, bado tuna kadhaa."
Musk, alianza mipango ya kufanikisha safari za Mars mwaka wa 2016, na amerejea na habari zaidi.
Musk amevutia watu wengi sana ambao wamependezwa na miradi yake. Na ingawa ahadi zake mara nyingi zimechukua muda mrefu kutekeleza, baadhi imetimia.
Hii ni pamoja na kutuma na kurejesha roketi 16 duniani baada ya roketi hizo kumaliza misheni yao. Roketi mbili kati ya hizo 16 zimeweza kusafiri tena mara ya pili.
Anasema cha muhimu sana kwake ni kuunda rtoiketi ambazo zinawza kutumika tena na tena kama ndege, kwani ni inagharimu pesa nyingi sana kutengeneza roketi.

Ahukumiwa Miaka 30 Jera kwa Kosa la Kubaka na Kumpa Mimba Mwanafunzi wa Miaka 13

$
0
0
Ahukumiwa Miaka 30 Jera kwa Kosa la Kubaka na Kumpa Mimba Mwanafunzi wa Miaka 13
MAHAKAMA ya wilaya ya Lindi, imemtia hatiani na kumuadhibu kwenda gerezani na kutumikia adhabu ya kifungo kwa muda wa miaka 30, kijana anaetambulika kwa jina la Mussa Saidi, mkazi wa mtaa wa Mitandi manispaa ya Lindi. Baada ya kuthibitika kuwa alimbaka na kumpa mimba mwanafunzi wa shule ya msingi mwenye umri wa miaka 13.

 Akisoma hukumu ya shauri hilo la jinai namba 110 la mwaka 2017, hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Erasto Philly alisema baada ya kusikiliza ushahidi uliotolewa na pande zote mbili (upande wa utetezi na mashitaka) mahakama hiyo iliridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka. Kwamba Mussa alimbaka na kumpa mimba mtoto huyo ambae kwa mujibu wa maelezo ya mwendesha mashitaka wa serikali, EmmanueJohn, ni mtoto  wa mke wake Mussa(mtoto wake wa kambo).

Hakimu Philly alisema ushahidi uliotolewa dhidi ya Mussa mahakamani hapo haukuwa na chembe hata ya shaka kuwa Mussa alitenda makosa hayo ambayo yapo kinyume na sheria za nchi nayamekatazwa kutendwa na mtu mwenye akili timamu kama Mussa.

Kwakuzingatia ukweli huo, hakimu Philly alisema mahakama hiyo ilimudhibu adhabu ya miaka 30 kwa kosa la kubaka. Ambalo ni kinyume cha sheria namba 130 vifungu vya 1 na 2 (1) cha sheria ya adhabu sehemu ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Vilevile kwakosa la kumjaza mimba mwanafunzi, mahakama hiyo ilimuadhibu miaka 30,ikiwa  utekelezaji wa sheria ya elimu ,kifungu namba 60A(3) cha sheria hiyo fungu la 553 kama lilivyorekebishwa mwaka 2002 na marekebisho mengine ya pili yaliyofanyika mwaka 2016.

Huku akiweka wazi kwamba utekelezaji wa adhabu hiyo utafanyika kwa pamoja.Hivyo Mussa atatumikia adhabu hiyo kwa muda wa miaka 30 pekee. Lakini  pia hakimu huyo alisema mahakama kwakuzingatia ukweli kwamba mtoto amekatizwa masomo. Mussa ametakitakiwa kumlipa  shilingi 1,000,000/= kama fidia.

Awali mwendesha mashitaka wa serikali,Emmanuel John aliileza mahakama hiyo kwamba mwezi Agosti mwaka huu akiwa nyumbani kwake mtaa wa Mitandi alimbaka na kumsababishia kupata mimba mtoto huyo mdogo wa kike ambae ndoto zake za kufika mbali kielimu zimekatizwa bila kutarajia. Hivyo aliiomba mahakama hiyo imuadhibu adhabu kali ili iwefundisho kwa wengine wanaotamani kutenda makosa ya aina hiyo.

Mussa licha ya kuiomba mahakama imuhurumie kwa kumpa adhabu ndogo kwakuwa hanarekodi mbaya ya kutenda makosa,ana wazazi,make na watoto ambao wote wanamtegemea. Hata hivyo kiwango,muda wa kutumikia na aina ya adhabu vilibaki kuwa hizo na kusababisha kuwa gumzo kutoka kwa watu wanaofahamu na wasiomfamu kijana huyo hapa Lindi.

Diamond Afunguka Sababu ya Kujitoa Kwenye Vevo

$
0
0
Diamond Afunguka Sababu ya Kujitoa Kwenye Vevo
Mwanamuziki Diamond Platnumz amelitolea ufafanuzi suala la mtandao wa YouTube na Vevo baada ya kuzuka sintofahamu kuhusiana na chaneli hizo mbili za kurushia nyimbo za wasanii.

Katika maelezo yake pia ametoa sababu za kuuita wimbo Hallelujah alioutoa juzi usiku. Wimbo huo uliowekwa saa 38 zilizopita umetazamwa na watu milioni1.6 katika mtandao wa YouTube.

Diamond amesema licha ya kujiunga na mtandao wa Vevo, aliamua kuachana nao kutokana na masuala ya maslahi kutomridhisha.

Amesema kulinganisha YouTube na Vevo kwa mtu anayejua masuala ya mitandao ni sawa na kulinganisha baba na mtoto.

“Vevo wanauza Youtube hivyo moja kwa moja mtandao ninaoutumia kuweka kazi zangu ndiyo ambao unanilipa zaidi na ndiyo mtandao mama, ni kweli niliingia Vevo hapo awali lakini kutokana na kushidwana kwenye maslahi niliamua kuachana nao,” amesema mwanamuziki huyo.

Kwanini alitumia neno Hallelujah?

 Meneja wa mwanamuziki huyo, Salaam Sharaf amesema jina la wimbo huo limetumika kama kionjo cha kusifu uumbaji wa Mungu na si kama wengi wanavyotafsiri.

Salaam hakuishia hapo alitolea mifano ya baadhi ya wasanii hapa nchini ambao wamewahi kuweka neno Mashaalah katika nyimbo zao, huku wengine wakitumia neno Halelluya maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi akiwemo mwanamuziki Nameless katika wimbo wake “Nasinzia”.

“Wakati anatunga mashairi yake lengo lilikuwa kusifia uumbaji, mbona wapo wasanii wengi hapa nchini wametumia neno Mashaallah, Hallelujah maana yake ni kumtukuza na kumsifu Mungu lina tofauti gani na Mashaalah?” amehoji Salaam.

Hata hivyo amesema watu wanaozungumzia suala hilo wanatafuta namna ya kuonekana wanaongea na iwapo wanaona kuna mahali mambo hayajakaa sawa ni vema wakaenda kwenye vyombo vya sheria, “Nafikiri hawana jipya wameshindwa watasema nini kuhusu wimbo huu, hawana sababu ya msingi.”

Baada ya Kupigwa Marufuku Uwanja wa Taifa Sasa Simba, Yanga Kukutana CCM Kirumba

$
0
0
Baada ya Kupigwa Marufuku Uwanja wa Taifa Sasa Simba, Yanga Kukutana CCM Kirumba
SIKU moja baada ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupiga marufuku kutumika kwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam uliopo katika matengenezo, mechi ya Simba na Yanga sasa itachezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Mechi hiyo itachezwa Oktoba 28, mwaka huu na awali ilielezwa ingechezwa kwenye Uwanja wa Taifa ambao ulielezwa ukarabati wake ungekamilika Oktoba 25, mwaka huu.

Hivi karibuni serikali kupitia kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe ilisema Simba na Yanga hazitaweza kuutumia Uwanja wa Taifa kwa mechi ya Oktoba 28 kwani ukarabati wake utakuwa bado haujakamilika.

Kikosi cha timu ya Simba.
Badala yake serikali ikasisitiza kwamba, uwanja huo utakuwa tayari kuanza kutumika ifikapo Januari mwakani.
Kwa jinsi hali ilivyo, Tanzania hakuna uwanja mwingine wa kuruhusu mechi hiyo kuchezwa zaidi ya Kirumba ndiyo maana Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) litalazimika kuipeleka huko.

Mechi hiyo ya watani itachezwa kwenye uwanja huo kama ilivyopangwa Oktoba 28, mwaka huu.
“Unadhani hii mechi itapelekwa wapi? Hapa Tanzania hakuna uwanja mwingine utakaoweza kuchukua watazamaji wengi kama Kirumba hivyo kwa vyovyote vile mechi itachezwa hapo,” kilisema chanzo chetu.

Hizi Hapa Sababu ya Ongezeko la Wanawake Kujifungua kwa Upasuaji Duniani

$
0
0
Hizi Hapa Sababu ya Ongezeko la Wanawake Kujifungua kwa Upasuaji Duniani
Wataalamu wameeleza kuwa unene wakupita kiasi kwa wanawake husababisha wanawake hao kuwa kwenye hatari ya kujifungua kwa njia ya upasuaji pindi wanapopata ujauzito.

Imeelezwa pia kuwa kesi za watu wanawake kujifungua kwa upasuaji zinaongezeka duniani kote na kutokana na masuala hayo ya uzito mkubwa lakini pia ni hatari wanayokuwa nayo wanawake wanaopata ujauzito kwenye umri mkubwa.

Upasuaji wakati wa kujifungua uko wa aina mbili ikiwa ni pamoja na ule ambao hupangwa mapema hasa kutokana na sababu za kiafya kama mtoto kuwa amelala upande usiotakiwa au mtoto ni mkubwa zaidi wakati upasuaji wa pili ni ule wa dharura ambao hufanyika endapo kuna tatizo wakati wa kujifungua.

Maafisa Ardhi Waliogawa na Kuuza Viwanja vya Polisi Kukamatwa

$
0
0
Maafisa Ardhi Waliogawa na Kuuza  Viwanja vya Polisi Kukamatwa
Mkuu wa wilaya ya Kahama Bw. Fadhili Nkurlu amemuagiza Mkuu wa Upelelezi wilayani Kahama, George Bagyemu kuwakamata na kuwafikisha mahakamani maofisa ardhi waliogawa na kuuza viwanja vilivyopimwa na kutengwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha polisi.

Mkuu wa Wilaya huyo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Kahama amesema hayo leo baada ya kutembelea na kuona jinsi ambavyo maafisa hao wa ardhi walivyoweza kuuza robo tatu ya eneo la chuo cha maendeleo jamii Kahama likiwa limeuzwa kwa watu binafsi na kujengwa nyumba.

Katika hatua nyingine fadhili Nkurlu amemuagiza mfanyabiashara maarufu wilayani Kahama aliyeuziwa eneo la polisi Bw.Jeremiah Ndasa pamoja na wengine kuvunja ukuta na misingi ya nyumba wayojenga katika eneo hilo na kuliacha wazi kwa matumizi ya serikali.
Aidha Mkuu wa Upelelezi wilayani Kahama, George Bagyemu amesema maeneo yote ya polisi yaliovamiwa na kujengwa yako katika ramani huku Afisa Ardhi mteule Kahama Bw.Yusuph Shabani akijitetea mbele ya mkuu wa wilaya.

Tamasha la Fiesta Lmchanganya Dudu Baya Atamani Kufanya Shoo Nyingine

$
0
0
MSANII wa kitambo kwenye Bongo Fleva, Dudubaya amefunguka kuwa anatamani kuendelea kuonyesha makeke yake kwenye Tamasha la Fiesta linaloendelea kwenye mikoa tofauti baada ya hivi karibuni kupanda jukwaani wakati tamasha hilo likiwa mkoani Mwanza.

Dudubaya alipata nafasi ya kupanda jukwaa la Fiesta Mwan­za baada ya kuitwa jukwaani na msanii Bernard Paul ‘Ben Pol’.

Akizungumza na Cham­pioni Jumamosi, Dudubaya aliyetamba na ngoma kibao kama Mpenzi, Nakupenda Tu na nyinginezo kibao amesema anatamani kuen­delea kuonyesha makeke yake baada ya kupata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wakati akikamua kwenye tamasha hilo.


“Kiukweli natam­ani nipate tena nafa­si ya kupanda jukwaani kwenye Fiesta kwa sababu ya mapokeo ya aina yake niliyoyapata waka­ti nikiimba ngoma zangu am­bazo ziliwakosha watu wengi akiwemo mkuu wa mkoa wa hapa,” alisema Dudu Baya.

Ali Kiba Kufunguka Kuusu Kuachia Wimbo Wake Mpya

$
0
0
Ali Kiba Kufunguka Kuusu Kuachia Wimbo Wake Mpya
Msanii Alikiba ameweka wazi mipango ya mkongwe wa muziki Abby Skillz, kuwa muda si mrefu atakuja na ngoma yake mpya baada ya ngoma yake ya 'Averina' ambayo alikuwa ameshirikishwa yeye pamoja na Mr Blue ambayo ilitoka mwaka jana.

Alikiba
Alikiba amesema hayo wakati akimpa pongezi mkongwe huyo baada ya kufanikiwa kufunga ndoa jana na mchumba wake Andoya khalifa Mrimi.
"Hongera mkongwe nakutakia kheri na mafanikio katika ndoa yako na ngoma mpya inafuata" aliandikwa Alikiba kupitia katika mtandao wake wa Instagram

Abby Skillz ni kati ya wasanii ambao walidaiwa kuwa chini ya usimamizi wa Alikiba kupitia 'Label' yake ya King's Music ambapo Alikiba aliwahi kusema kuwa baada ya kuachia wimbo wake mpya ambao ni 'Seduce Me' alisema baada ya hapo utakuwa ni wakati wa wasanii waliopo kwenye Label yake hiyo kutoka na ngoma zao pia.

Ally Hapi Aagiza Kupitiwa Upya Mkataba wa Mwekezaji wa Kituo cha Mabasi cha Makumbusho

$
0
0
Ally Hapi Aagiza Kupitiwa Upya Mkataba wa Mwekezaji wa Kituo cha Mabasi cha Makumbusho
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi ameagiza kupitiwa upya kwa mkataba wa mwekezaji katika Kituo cha mabasi cha makumbusho baada ya kubaini kuwapo kwa ubadhirifu.

Mkataba huo ni kati ya Manispaa ya Kinondoni na Kampuni ya Eastern Capital Limited kwa ajili ya kuendesha kituo hicho.

Akiwa ziarani hapo  leo, Hapi ameelezwa na wafanyabiashara wakiwamo bodaboda,  bajaji na machinga kuwa mwekezaji huyo amekuwa akiwalipisha kodi kubwa na michango bila kuwapa risiti wala kutoelezwa matumizi ya tozo hizo.

Hapi alitaka kupata ufafanuzi wa kina kwamba  fedha hizo zinapelekwa Manispaa na kama wanatoa risiti za EFD lakini haikuwa hivyo.

"Ni marufuku kukusanya fedha nje ya mkataba, kinachokuongoza ni mkataba sasa nataka kujua hicho unachotoza kama hakipo kwenye mkataba nani aliyekutuma?,"

"Namuagiza Mkurugenzi wa Manispaa, apitie upya mkataba  huu na kama hauna tija uvunjwe," amesema

Ametoa siku tatu kwa Kampuni hiyo kutoa taarifa za makusanyo ya fedha pamoja na kueleza kiasi cha kodi walicholipa tangu kuanza kwa mkataba.

Meneja miradi wa Kampuni hiyo, Haidary Salum amesema makusanyo na tozo zikiwamo usafi, umeme na ulinzi ulitokana na makubaliano kati yao na wafanyabiashara.

" Ndiyo haipo kwenye mkataba lakini tulikubaliana na wafanyabiashara ili wachangie huduma,"amesema

Wafugaji Watatu Wauwawa kwa Kupigwa na Wakulima Mkoani Morogoro

$
0
0
Wafugaji Watatu Wauwawa kwa Kupigwa na Wakulima Mkoani Morogoro
Wakulima watatu wakazi wa Kata ya Kolero wilayani Morogoro wameuawa kwa kupigwa walipokamata mifugo iliyokuwa inalishwa kwenye mazao yao.

Diwani wa Kata ya Kolero, Eligius Mbena amesema Alhamisi Septemba 28 ng’ombe zaidi ya 140 waliingizwa kwenye mashamba ya wakulima katika Kijiji cha Kidodi na kula mazao.

Ng’ombe hao ambao inadaiwa ni mali ya mfugaji mmoja inaelezwa wameharibu zaidi ya eka tano za mazao ya mahindi, kunde na mbogamboga yaliyokuwa yakikaribia kukomaa.

Diwani huyo amesema baada ya wakulima kuona kundi la ng’ombe waliamua kuwasiliana na mtendaji wa kata ambaye alituma mgambo na kwa kushirikiana na wananchi waliondoa mifugo hiyo na kuipeleka ofisi ya kata.

“Baada ya mgambo kufika wale vijana waliokuwa wakilinda ng’ombe walikimbia ndipo wananchi na mgambo walipowaswaga ng’ombe hadi ofisi ya Kata ya Kolero kwa hatua zaidi,” amesema.

Amesema kwa utaratibu waliojiwekea, ng’ombe wanapokamatwa kwenye mashamba hutozwa faini ya Sh10,000 kwa kila mmoja. Mbena amesema mtendaji ndivyo alivyofanya kwa mifugo hiyo iliyokamatwa.

Amesema baada ya mhusika kulipa faini na kukabidhiwa ng’ombe wake, wananchi waliondoka na wakiwa njiani walishambuliwa.

Amewataja waliouawa kuwa ni Richard Edward, Riziki Juma na Antoni Matei ambao ni wakulima na wakazi wa Kata ya Kolero.

“Ninachosikitika ni kwamba, taarifa za mauaji haya tumezitoa katika mamlaka zote za wilaya na mkoa tangu Alhamisi Septemba 28 lakini hadi leo Jumamosi hakuna hatua iliyochukuliwa japo mwenye mifugo tunamjua na tumewatajia polisi,” amesema Mbena.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo alisema hawezi kuzungumzia lolote kwa kuwa masuala ya mauaji yanahusu Jeshi la Polisi na si ofisi yake.

“Msemaji wa matukio yote ya mauaji ni RPC si mimi,” alisema Chonjo.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leons Rwegasira alisema wamepata taarifa hizo na wametuma timu kufuatilia.

“Tuna taarifa kwamba kuna watu wameuawa Kolero lakini bado hatujapata kwa usahihi kwa kuwa timu yetu ndiyo imekwenda huko,” amesema.

Ndege ya Kijeshi Yaanguka DR Congo

$
0
0
Ndege ya Kijeshi Yaanguka DR Congo
Ndege ya kijeshi imeanguka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuwaua abiria wote.
Maafisa wa maswala ya angani wamesema kuwa ndege hiyo ilifeli kupaa vizuri kutoka uwanja wa ndege wa N'djili katika mji mkuu wa Kinshasa na kuanguka katika makaazi ya Nsele.
Haijabainika iwapo kuna watu wowote waliouawa ama kujeruhiwa ardhini.
Mkurugenzi wa uwanja wa ndege wa Kinshasa amesema kuwa ndehe hiyo ilikuwa ikibeba mizigo na kwamba haikuwa na abiria wowote.
Ripoti nyengine zinasema kuwa baadhi ya wanajeshi waliuawa.

Uturuki Yafungua Kambi kubwa ya Kijeshi Somalia

$
0
0
Uturuki Yafungua Kambi kubwa ya Kijeshi Somalia
Uturuki imefungua kambi kubwa ya kijeshi mjini Mogadishu, Somalia.
Hii itakuwa kambi yake kubwa kabisa ya mafunzo ya kijeshi nje ya nchi.
Kambi hiyo itayokuwa kando ya bahari, ina uwezo wa kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Somalia, zaidi ya 1500 kwa wakati mmoja
Lengo ni kulipa nguvu jeshi la Somalia, kupambana na kundi la wapiganaji wa Kiislamu, Al Shabaab.

Wanajeshi zaidi ya 20,000 wa Umoja wa Afrika na wengine wa kigeni, wanapigana na Al Shabaab hivi sasa.
Kuna kambi kadhaa za majeshi ya kigeni nchini Somali.

ZARI: “Siji Kwa Magoti madale”

$
0
0
Zari azidi kupost picha kwenye kurasa yake ya instaggram na leo september 30 kapost picha tatu na moja kati ya post alizopost kutia gumzo ni hiyo picha ya kusema kwamba hawezi kwenda kwa magoti madale. VIDEO:

Hivi Kwanini Baadhi ya Watanzania Wanataka Diamond Aanguke Kimuziki?

$
0
0
Diamond Platnumz ni mwanadamu ana madhaifu yake kama alivyo binadamu yeyote yule. Lakini katika picha kubwa na kimuziki huyu ndugu yetu anaiwakilisha nchi vyema sana huko nje.

Nadhani hili ndilo la Msingi na tungebaki kuliangalia wote kama Watanzania. Kuwa na timu siyo makosa hata Yanga na Simba ni Wapinzani wakubwa lakini tukija kwenye Taifa Stars hizo timu tunazivua na tunavaa Utaifa. (Huu ndiyo Uzalendo jamani)

Utaifa ukiisha tunarudi kwenye timu zetu na kuanza kung'oa viti pale uwanja wa taifa. Hivyo basi kwenye kujenga sifa za wasanii wetu awe Ali Kiba, Diamond au Vanessa Mdee tushindane humu ndani lakini tusifanye chuki kiasi cha kutaka kuchafua sia zao. Hao ni watoto wetu kabisa,watoto wa nchi hii: Hakuna mzazi anayetup watoto jamani.

Tumtie moyo Alikiba na tumtie Moyo Diamond: Pia tuwakosoe pale wanapofanya vibaya hali tukiwa na dhamira safi kabiaa ya kutaka kuwajenga kimuziki. Tuepukane na fitna,majungu na uzandiki l: haya mambo hayajengi kabisa.

Ray C Amuomba Msamaha Zamaradi Mketema Kisa Ruge

$
0
0
Ray Ameamua kufunguka na Kusema Haya: "Kiukweli huwa naumia sana ninapoona mastaa tunatumia muda mwingi kulumbana na kugombana kwa mambo ya kipuuzi sana,mastaa wenzetu wa Nigeria wanatushinda kwa mambo mengi sana sababu wao wanashirikiana na kusapotiana katika mambo mengi sana na hata ukiskia wamepishana basi ujue ni kwa ajili ya biashara tu na si vinginevyo!

Nilichogundua Mimi ni kwamba kumekuwa na makundi mbalimbali mitandaoni yanayokuza mambo na kusapoti wasanii kulumbana Mara team simba Mara team nyani!naingea kutoka.

Moyoni kuwa watanzania tunasifika kwa kuwa na amani na upendo!sasa iweje tena tuishi maisha ya kuchukiana na ugomvi badala ya kuishi kwa amani?najua sisi wasanii tuna mashabiki wengi.

Na tunapenda na nnyie mnatupenda kwahiyo mnatakiwa kutupatanisha tunapogombana na si kutushabikia coz mnaposhabikia ugomvvi ndio mnapotufanya tupoteze muda kulumbana badala ya kutumia huo muda kufanya kazi zetu za sanaa kwa bidii tutangaze nchi yetu tunapoteza muda kulumbana,wenzetu wanaigeria wako mbali sana kwa sababu wanasapotiana sana!

Wasanii tuache bifu za kijinga na tutumie muda mchache tuliopewa na mola kufanya kazi zetu kwa bidii tutangaze nchi yetu ili vizazi vijavyo virithi bidii zetu,na naomba sana mashabiki wote msapoti mazuri tuyafanyayo" Ray C ameendelea kusema na kumwomba msamaha Zamaradi Mketema kama ifuatavyo : "Love u zama n sorry for everything keep doing wat u do best Zamaradimketema n hey dogo langu wemasepetu and my friend @new_kajala tusameheane na tupendane na tupige kazi Africa watutambue bana!!

Baraka Da Prince Awaporomoshea Mitusi Wanaomponda Kwa Kuusapoti Wimbo Mpya wa Diamond

$
0
0
Kama kawaida yake Baraka Da Prince Awaporomoshea Mitusi Wanaomponda Kwa Kuusapoti Wimbo Mpya wa Diamond...Amepost picha hii hapa na kuandika haya:

Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images